Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Watu wawili watiwa mbaroni kwa kuhusika na mauaji ya kiongozi wa CHADEMA Kinondoni

0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Slaam linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya aliyekuwa Kiongozi wa chama cha Chadema Kata ya Hananasifu, Marehemu Daniel John.

Akizungumza na wanahabari  jana  jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Lazaro Mambosasa alisema watu hao walikamatwa majira ya saa nne usiku, Februari 23 mwaka huu maeneo ya Hananasifu Kinondoni.

“Kufuatia uchunguzi unaoendelea juu ya mauaji hayo, walikamatwa watu wawili mmoja jinsia ya kike na mwingine wa kiume,” alisema.

Mwili wa marehemu Daniel John uliokotwa maeneo ya Coco Beach jijini Dar es Salaam, ambapo kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni, ilisema mwili wa John ulikutwa na majeraha sehemu za mikono, miguu na kichwani yanayoashiria kwamba alijeruhiwa na kitu chenye ncha kali.

MamboSasa: Ole Wenu Mtakao Andamana....Kitakachotokea Tusilaumiane

0
0
KAMANDA wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amesema ni marufuku kwa mwanachi yoyote kushiriki kwenye maandamano kwani hawapo tayari kuona watu wakiandamana na kusababisa uvunjifu wa amani iliyopo.

Mambosasa ametoa kauli hiyo jana  jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia mambo mbalimbali na ametumia nafasi hiyo kutoa rai kwa wananchi kutojihusisha na maandamano.

Alifafanua kwenye mitandao ya kijamii kuna baadhi ya watu wanaitumia vibaya na sasa wameanza kuhamasisha maandamano kwa kupanga tarehe ambayo itakuwa Aprili 26 mwaka huu.

“Kwenye mitandao ya kijamii tumeona watu wanahamasisha maandamano.Tunawaambia Polisi hatutakaa kimya na wale ambao wataandamana kitakachotokea wasitulaumu.

“Polisi tumejipanga kwa ajili ya kuhakikisha wananchi wanakuwa salama na wanafurahia hali ya ulitulivu iliyopo.

"Wale ambao wanataka kufanya maandano wahesabu hawana bahati na ndio maana tunaomba wananchi wasishiriki kwenye maandamano ambayo yameanza kuhamasishwa kupitia mitandao ya kijamii,”alisema Mambosasa.

Alifafanua Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linataka kuona wananchi wakiendelea na shughuli zao za kimaendeleo na wachache wenye kutaka kuvuruga amani iliyopo haitawavumilia.

Hivi karibuni kumekuwa na vuguvugu la kufanyika maandamano  Aprili 26 huku Mwanaharakati wa mitandaoni Mange Kimambi akionekana kuwa mstari wa mbele katika uhamasishaji.

Tundu Lissu Afunguka Mambo 6 Kuhusu Kifungo cha Sugu

0
0
Mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Lissu amefunguka kuhusu adhabu ya kifungo cha miezi mitano kwa Mbunge wa Mbeya Mjini na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa Emmanuel Masonga.

Tundu Lissu kwanza alianza kwa kutoa pole kwa yaliyowakuta viongozi hao wa CHADEMA lakini baadaye ametoa ufafanuzi kuhusu hukumu hiyo na kudai hukumu hiyo siyo mwisho wa mjadala mahakamani.  

==>Hili ni Tamko lake
"Waheshimiwa wangu salaam kutoka Ubelgiji. Nawapeni pole nyingi kwa yaliyomkuta Mh. Sugu na Goddie Masonga siku ya leo.
.
Naomba kuzungumzia suala hili kwa kirefu kidogo. .

Kwanza, hukumu ya leo sio mwisho wa mjadala mahakamani. Bado kuna fursa, nay haki, ya rufaa High Court na, ikibidi, Court of Appeal.
.
Pili, hukumu ya leo haina maana Sugu atakaa gerezani muda wote huo. Kuna haki ya dhamana pending appeal. Ndivyo ambavyo tumefanya kwa viongozi na wanachama wetu wengi in the past. .

Tatu, hukumu ya leo haina athari yoyote kwa ubunge wa Sugu. Katiba inaweka masharti ya kifungo cha miezi sita au zaidi, na kwa makosa ya 'utovu wa uaminifu.' Uchochezi au kutoa lugha ya matusi sio makosa ya utovu wa uaminifu. .

Nne, pamoja na kwamba sijaona nakala ya hukumu, adhabu ya kifungo bila faini kwa kosa la kwanza ni kinyume na sentencing principles. Hii ni mojawapo ya hoja zetu zilizoshinda katika kesi ya Mh. Juakali High Court mwaka jana. .

Tano, hata kama atakaa gerezani muda wote huo, hukumu za kesi za kisiasa kama hii hazijawahi kuwapunguzia heshima wapigania haki popote pale duniani. .

On the contrary, kifungo cha aina hii ni beji ya heshima kwa kila mpigania haki na uhuru. Orodha ya mifano ni ndefu sana: Nyerere (ijapokuwa yeye alilipa faini), Kenyatta, Mandela, Mugabe, Fidel Castro, etc. .

Alichokifanya hakimu leo ni kuwaongeza Sugu na Masonga kwenye orodha hii ya heshima. They'll come out even bigger and stronger than when they went in. .

Sita, naunga mkono pendekezo la Mh. Zitto kwamba wabunge wetu wote warekodi maneno aliyofungiwa nayo Sugu .

Nawatakieni kila la kheri katika hii safari ndefu ya kuelekea kwenye haki."

Mchungaji Mwingira Ashinda Kesi ya Kuzaa na Mke wa Mtu

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeitupilia mbali kesi ya madai iliyofunguliwa na Dk William Morris, raia wa Marekani dhidi ya mkewe Dk Phills Nyimbi na Mchungaji Josephat Mwingira.

Akisoma hukumu hiyo jana Februari 26, 2018,  Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba alisema Dk Morris katika kesi hiyo ameshindwa kuthibitisha uhusiano wa kimapenzi  kati ya Dk Phills na Mchungaji Mwingira.

Pia, ameshindwa kuthibitisha kuwa mtoto aliyezaliwa ni matokeo ya uhusiano wa kimapenzi kati ya Dh Phills na Mchungaji Mwingira.

Hivyo, mahakama imeitupilia mbali kesi hiyo ya madai na kusema mdai ameshindwa kuthibitisha katika kiwango kinachotakiwa kwa kesi za madai na kumtaka  alipe gharama za kesi na gharama walizotumia wadaiwa.

Baada ya kutolewa kwa hukumu huyo Wakili Respicius Ishengoma alisema watakata rufaa kwa sababu hawajaridhika na hukumu hiyo.

Hukumu hiyo yenye kurasa 54 ilisomwa jana saa nane mchana iliandaliwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mhini na kusomwa na Hakimu Simba.

Awali katika utetezi wa Dk Phills Nyimbi, aliieleza mahakama hiyo kuwa hajawahi kuwa na uhusiano na Mchungaji Josephat Mwingira.

Akiongozwa na Wakili Peter Swai kutoa ushahidi katika kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyekuwa mumewe ambaye ni raia wa Marekani, Dk William Morris, Dk Nyimbi aliomba mwanaume huyo asilipwe kiasi cha fedha cha Sh7.5 bilioni anazodai kwa sababu hakuwa na uhusiano na Mchungaji Mwingira.

Dk Nyimbi kupitia wakili Swai aliomba Dk Morris asilipwe kiasi hicho cha fedha kwa sababu hajawahi kuwa na uhusiano na Mchungaji Mwingira na kwamba  hicho anachodai si madai halali.

Desemba 28, 2011,  Dk Morris na Dk Phills walifunga ndoa ya Kanisani na wakati wa uhusiano wao, Dk Phillis na Mchungaji Mwingira wanadaiwa  kuingia katika uhusiano wa mapenzi na kubahatika kupata  mtoto wa kiume ambaye kwa sasa ana umri wa miaka tisa.

Mlalamikaji huyo alidai kuwa alitoa taarifa katika kituo cha polisi Kibamba ambapo walimueleza kuwa suala hilo ni la uzinzi ama udhalilishaji na haliwezi kuwa la kijinai na kushauriwa kufungua kesi ya madai.

Pia, alidai kwamba, kitendo cha mke wake kuwa na uhusiano na Mwingira ni kwenda kinyume  na ndoa yao halali  na kwamba kitendo hicho kimeharibu mipango yake ya siku za usoni kiasi cha kumfanya  apoteze hata matumaini ya kuendelea kuishi.

Vilevile, alidai kimemuaibisha na kushusha hadhi yake si tu Tanzania bali na duniani, hivyo kumsababisha ateseke kiakili na kiuchumi.

IGP Sirro Atoa ONYO Kali Waliopanga Kuandamana Nchi Nzima

0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro ametoa onyo akisema wamejiweka tayari kukabiliana na watu, wakiwemo wanasiasa wanaohamasishana kuandamana nchi nzima kinyume cha sheria.

Sirro alisema hayo jana mjini Bariadi baada ya kukutana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Simiyu alikokuwa ziarani kukagua utayari wa askari wa jeshi hilo.

“Kuna makundi ya vijana wanaojiita wana mapinduzi wanahamasishana na kupanga kuandamana nchi nzima wakiratibiwa na chama kimoja cha siasa, tumejipanga kuwadhibiti na tutawakamata wote bila kujali vyeo na madaraka yao,” alisema.

Sirro aliwataka wazazi na walezi kuwaonya na kuwazuia vijana wao kushiriki maandamano yasiyo na kibali kwa sababu hakuna atakayevunja sheria atakayesalimika bila kuchukuliwa hatua stahiki.

“Kuvunja sheria ni jambo rahisi lakini madhara yake ni makubwa. Wananchi wasijiingize kwenye mambo yakiwemo uhalifu ambayo mwishowe huwagharimu,” alisema.

==>Msikilize hapo chini

Waziri Mkuu: Viongozi Waliokula Fedha Za Wakulima Wa Korosho Warudishe

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema viongozi wa Vyama vya Ushirika waliokula fedha za wakulima wa korosho wilayani Masasi wazirudishe na wakishindwa mali zao zikiwemo nyumba zitauzwa ili kufidia.

Pia Waziri Mkuu amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bw. Gelasius Byakanwa ahakikishe anawasaka viongozi wa chama Ushirika cha Msingi cha Nanyindwa wilayani Masasi ambao wamekula fedha za wakulima na kisha kutoroka.

Amesema viongozi wa vyama vya Ushirika katika wilaya hiyo si waaminifu, ambapo mwaka wa fedha 2016/2017 jumla ya sh. bilioni 2.3 za wakulima ziliibiwa na viongozi hao, ambapo mwaka 2017/2018 sh. bilioni 1.7 zimeibiwa.

Waziri Mkuu alitoa maagizo hayo jana (Jumatatu, Februari 2018) alipozungumza kwa nyakati tofauti na wananchi pamoja na watumishi wa wilaya akiwa kwenye ziara yake ya kikazi mkoani Mtwara.

Alisema viongozi wa Ushirika wa Nanyindwa ambao wametoroka ni Michael Mkali, Yusuph Mataula, ambapo alimuagiza Bw. Byakanwa kuwasaka na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola ili waweze kuchukuliwa hatua zinazostahili.

Pia Waziri Mkuu aliwaagiza Wakuu wa wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri nchini kuvichunguza vyama vya Msingi katika maeneo na wakikuta kuna kiongozi amekula fedha za wakulima wamkamate na kumchukulia hatua za kisheria.

Alisema wakati wa watu kuomba kuchaguliwa kuongoza vyama vya Ushirika kwa lengo la kujitajirisha umepita na Serikali imedhamilia inawasimamia wakulima wa mazao mbalimbali nchini wakiwemo wa korosho ili kuhakikisha nao wananufaika.

Waziri Mkuu alisema vyama vya Ushirika wilaya hiyo vinaongoza kwa ubadhilifu wa fedha za wakulima ambapo wiki iliyopita Bw. Byakanwa aliwakamata viongozi 36 wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) wilayani Masasi.

Viongozi hao ambao ni wenyeviti na makatibu wanakabiliwa na tuhuma za ubadhirifu wa fedha za wakulima wa korosho ambazo ni zaidi ya sh bilioni 2.3, ambazo ni malipo ya zao hilo kwa msimu wa ununuzi 2016/2017 na 2017/18.

Alisema mbali na wafanyabiasharahao, pia Meneja wa benki ya NMB tawi la Masasi, Aidan Msuya anaye alikamatwa kwa tuhuma za kufanya muamala wa fedha za malipo ya wakulima sh milioni 45 kwa zaidi ya mara 11 kwa siku moja.

Waziri Mkuu alimpongeza  Bw. Byakanwa kwa hatua alizozichukua dhidi ya viongozi hao na kumuagiza ahakikishe viongozi wote waliosababisha ubadhirifu huo wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, FEBRUARI 27, 2018.

Waziri Mkuu: Wahudumieni Wananchi Bila Ubaguzi wa Kidini, Kiitikadi

0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa umma wawatumikie wananchi kwa uweledi na ustadi bila ya ubaguzi wa aina yoyote.

Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo jana (Jumatatu, Februari 26, 2018) wakati akizungumza na watumishi wa wilaya za Masasi na Nanyumbu kwa nyakati tofauti.

Waziri Mkuu ambaye yuko mkoani Mtwara kwa ziara ya kikazi aliwasisitiza watumishi wa umma kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Alisema Rais Dkt. John Magufuli amesisitiza watumishi wa umma wawatumikie wananchi bila ya ubaguzi wowote pamoja na kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

“Watumishi wa umma lazima mtambue kwamba msimamo wa Serikali ni kuwahudumia wananchi bila ya ubaguzi wa kidini, kiitikadi na kipato.”

Waziri Mkuu alisema ni vyema watumishi hao kuanza kujitathmini kwa sababu Serikali haitowavumilia watumishi watakaoshindwa kuwajibika kwa wananchi.

Pia aliwataka watendaji hao kuacha urasimu na wahakikishe kila fedha iliyotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inatumika kama zilivyoelekezwa.

Waziri Mkuu aliwaagiza watendaji hao wawe na mpango wa kuwatembelea wananchi kwa ajili ya kusikiliza kero zinazowakabili na kuzipatia ufumbuzi.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, FEBRUARI 27, 2018.

Waziri Mkuu: Tukikukuta na Binti wa Shule tutakukamata na kukutupa miaka 30 Jela......Ole Wenu Vijana!

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuwalinda watoto wa kike na ndiyo maana tunawataka watoe taarifa za watu wanaotaka kuwakwamisha kimasomo kwa watendaji wa vijiji kwenye maeneo yao.

Alitoa agizo hilo jana (Jumatatu, Februari 26, 2018) wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wakazi wa wilaya ya Masasi akiwa katika siku ya kwanza ya  ziara yake ya kikazi mkoani Mtwara.

Waziri Mkuu alisema watoto wa kike wanatakiwa kuheshimiwa katika jamii kwa kuachwa waendelee na masomo yao bila ya usumbufu wa aina yoyote na atakayebainika kukatisha masomo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Alisema Serikali  itatoa adhabu kali ya kifungo cha miaka 30 jela kwa mtu atakayekatisha elimu ya mtoto wa kike iwe kwa kumuoa, kumpa ujauzo na hata ukikutwa naye nyumbani kwako, katika nyumba ya wageni.

“Tukikukuta na binti wa shule katika kona isiyoeleweka tunakukamata na kukuchukulia hatua za kisheria. Ole wenu vijana, mkibainika mmewapa mimba mabinti wanaosoma, adhabu yake ni miaka 30 jela.”

Waziri Mkuu alisema kwa wazazi au walezi watakaowaozesha watoto kike ambao bado wanafunzi na kwa upande wa wazazi watakaomsindikiza mtoto kwenda kuoa mwanafunzi wote watachukuliwa hatua za kisheria.

Pia Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwataka wanafunzi wote kusoma kwa bidii ili watimize ndoto zao na wasikubali kushawishika kwa sababu watashindwa kufikia masomo yao.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, FEBRUARI 27, 2018.


Diamond Akabidhiwa Rasmi Leseni ya Wasafi TV na Wasafi Redio

0
0
Hatimaye Bosi wa Wasafi Classic Baby (WCB) Diamond Platinumz amepata leseni ya kuziweka hewani redio na televisheni za Wasafi zilizobatizwa jina la ‘Wasafi Radio na Wasafi TV’.

Diamond amevuka maji na kuzipata leseni zake visiwani Zanzibar ambapo alikabidhiwa na Wizara ya Habari, Tamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar, Rashid Ali Juma.

Mkali huyo wa ‘Sikomi’ jana aliwashirikisha mashabiki wake habari hiyo njema iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu, siku chache baada ya kuonesha picha akiwa anajaribu mitambo ya mradi huo mpya.

Kupitia Instagram, ameandika ujumbe akiambatanisha na picha za leseni hizo, akiishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

==>Diamond ameandika:
(Leo tulikabidhiwa Rasmi Leseni ya @wasafitv na @wasafifm na Mh Waziri wa Habari, Tamaduni , Utalii na Michezo Zanzibar mh Rashid Ali Juma…..Shukran Nyingi ziifikie Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Jamuhuri nzima ya Muungano wa Tanzania… Ma raisi wetu pendwa Dr John Pombe Magufuli & Dr Ali Mohammed Shein pamoja na Mawaziri wa Habari Tamaduni na Michezo Mh Rashid Ali Juma & Harrison Mwakiyembe….

Tamanio letu ni kutengeneza nyanja za Ajira kwa nduguzetu wenye Taaluma za Habari na Utangazaji ambao pengine hawajapata nafasi bado….kwa kuthamini kuwa, bila wao leo hii sisi tusingekuwepo….lakini pia Pamoja kushirikiana na Media zetu nchi Kuendeleza kunyanyua Vipaji toka mitaani na Tasnia nzima ya Sanaa, Michezo na Tamaduni…. ) #HiiNiYetuSote.

Ni dhahiri kuwa Wasafi TV na Redio zitagusa anga la Tanzania Bara na Visiwani.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Freeman Mbowe na vigogo wengine wa Chadema waripoti polisi

0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wengine wa chama hicho wamekwenda kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mchana Jumatatu Februari 27, 2018 Mbowe amesema wamekwenda kuripoti kuitikia wito wa Polisi.

Amesema katibu mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji hatakwenda kwa kuwa yupo nje ya nchi na atakaporejea atakwenda kwa kuwa hawana sababu ya kugoma.

Februari 20,2018 Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam iliagiza kukamatwa viongozi saba waandamizi wa Chadema akiwamo Mbowe.

Wito huo ulikuja siku chache baada ya tukio la kuuawa kwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini.

Akwilina aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya daladala eneo la Mkwajuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakienda ofisi za mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni kudai viapo vya mawakala wao.

Mbowe akizungumza na waandishi wa habari amesema wana taarifa kuwa watakamatwa na kwamba kuna mpango wa kubambikiziwa kesi.

TANGA RAHA- Sehemu ya Kumi na Sita ( 16 )

0
0
 AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA  

“NAHITAJI SIRI HII UITUNZE NA USIMWAMBIE BINADAMU WA AINA YOYOTE NA LAITI UKIDHUBUTU KUMWAMBIA MWANADAMU KUWA UMEKUTANA NA MIMI NITAITOA ROHO YAKO UMENIELEWA……?”
“Ndi….ooo”
“Na kingine nitahitaji uwe rafiki yangu”
“Siwez….”
Kabla hata sijaimaliza sentensi yangu nikajikuta akinisukuma na kunikandamiza ukutani huku mkono wake akiwa umenikaba kwenye koo lango na nikaanza kuhisi roho yangu ikitaka kunitoka kwani ananguvu nyingi na kingine kinachozidi kuniogopesha ni macho yake kaunza kuwaka moto huku akitokwa na machozi ya damu

ENDELEA
      “Katika maisha yangu haijawahi binadamu wa aina yoyote kunikataa”
Olvia Hitler alizungumza na sauti nzinto iliyo nifanya nizidi kuogopa,kisha akaniachia na nibaki nikiwa nina elea elea angani.Sura yake ikarudi katika hali yake ya kawaida huku akiwa ananitazama kwa tabasamu zuri
“Eddy narudia tena kuzungumza mimi sio kiumbe mbaya wa kuwadhuru wanadamu ila ninauwezo wa kumdhuru yule tu anaye hitaji mimi nimfanyie hivyo……Nahitaji kukufanya kuwa mtu maarufu na anaye fahamika sana Tanzania na Duniani kwa ujumla”
“Ki…v…ipi?”
“Sawali zuri,kwanza unatakiwa usiniogope.Pili unatakiwa kufwata zile amri zangu nitakazo kupa na nilizo kupa……Natambua sana moyo wako unampenda Rahma japo huyo mwnamke mchafu anakufanya ummsaliti…..Kutokana hukuwa unajua ni kitu gani kinachoendelea kwa leo nitakusamehe ila kwa sharti moja tu nahitaji ummuamshe huyo mwanamke na aende zake kwake wakati huu kisha ndio nitaendelea na mazungumzo na wewe”

“Sa..sawaa”
     Nilizungumza kwa kigugumizi kisha taratibu akanirudisha kitandani na gafla akapotea na hali ya chumba ikarudi kama kawaida na nikajikuta nimekaa kitandani huku shuka likiwa limenifunika kuanzia miguuni hadi kwenye kiunoni,Nikamtazama Halda mwenzangu hana hata analo lijua ndio kwanza ananazidi kukoroma kiasi kwamba nikaanza kujipa moyo labda  inaweza ikawa ndoto.Nikaanza kumtingisha Halda huku nikiliita jina lake hadi akaamka  na kukaa kama nilivyo kaa mimi huku akipiga miyayo ya usingizi
“Nakuomba uvae uende kwako”
“Eddy”
“Wewe ninakuomba uvae uende kwako sasa hivi”
“Eddy umechanganyikiwa?”
“Sijachanganyikiwa nina akili zangu ni nzima kama unavyo niona ila nakuomba tuu uvae na uenda kwako kama kulala tutalala siku nyingine”
“Eddy kama unaota nakuomba uniache mimi nilale shughuli uliyo nipa ni kubwa sawa mpenzi wangu”
Halda alizungumza huku ikijilaza tena kitandani na kunifanya nimuamshe kwa nguvu hadi akaanza kukasirika
“Eddy saa tisa yote hii unataka mimi niende wapi mwanaume gai huna huruma au unataka usiku huu nikabakwe huko barabarani?”

“Kama utabakwa ukiwa ndani ya gari basi ila ninacho taka mimi vaa nguo zako uende zako kwako sitaki matatizo na mpenzi wangu”
“Eddy siondoki”
“Kumbuka upo kwangu?”
“Hata kama ila siondoki lije WINCHI,TREKTA au KATAPILA haliwezi kuning’oa hapa kitandani na wala siondoki”
“Hilda unanijua tena vizuri? Sihitaji nikubamize ndio uondoke”
“Eddy nipige,nikate kate,nivunje vunje,nisage sage ila mimi siondoki NG’OO”
 Nikazidi kuchanganyikiwa kwani Halda hakutaka kabisa kusikia kitu kinacho itwa kuondoka ikanilazimu kushuka kitandani na kujifaunga taulo langu na kumbukumbu ya maji aliypo nipa bibi ikanijia kichwani nikakaumbuka nimeyaweka jikoni
“Unakwenda wapi sasa?”
“Wewe lala kama hutaki kuondoka niache”
“Sasa Eddy huko nje usiku huu unapo kwenda untaka kwenda kufanyaje?”
“Kwani nimekuambia ninakwenda nje hembu lala huko”
“Nakufwata”

Halda akanyanyuka kitandani huku akiwa ameijifunga shuka na kuanza kunifwata jikoni ninapo elekea,Nikaikuta chupa ya maji katika sehemu niliyo iweka kaisha taratibu nikayatoa kwenye kifuko cheusi nilipo kuwa nimeyaweka
“Sasa hayo maji ni ya kazi gani?’
“Hilda hembu niache wewe rudi chumbani kalale”
“Mmmm haya mwaya kama ndio uchawi wa kwenu kunywa maji ya Dasani usiku wa manae”
  Halda alizungumza huku akirudi zake chumbani kwangu,nikamchungulia na kuona tayari ameingia ndani kwangu na kuufunga mlango.Nikapiga hatua za kwenda nje nikashika kitasa cha mlango na kufungua.Moyo ukanipasuka kiasi kwamba nikajikuta natamani kuzirai kwanik eneo zima la nje ya nyumba yangu nikakuta ni bahari tena yenye maji mengi huku Olvian Hitler akiwa amekaa kwenye kiti cha dhahabu huku pembeni yake kukiwa na wasichana wawili wanao mpepea kwa mikia ya Simba iliyo tengenezwa vizuri huku wakiwa juu ya maji
“Eddy nashindwa kuamini kama mwanamke huyo umeshindwa kumtoa ndani kwako”

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 13 na 14)

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA 

Kuingia ndani kwangu nikakuta simu yangu ikiita na kukuta ni Hassani akinipigia, nikaipokea akanijulisha yupo njiani anakuja, kwa haraka haraka nikajiandaa, nilipo maliza tu akanipigia simu tena na kunifahamisha kwamba yupo nje. Nikabeba begi langu, nikatoka na kufunga chumba changu, nikiwa kwenye kordo nikakutana na Mariam akitoka kuamka huku akiwa amejifunga, tenge moja. Alipo niona kwa haraka akaja kunikumbatia, joto lake likapenya kwenye mwili wangu na kujikuta nikisisimka. Tukiwa bado tumekumbatiana nikasikia mlango wa chumba cha mama Mariam ukifunguliwa, ikionyesha kwamba ndio anatoka chumbani kwake.

ENDELEA
Nikamuachia Mariam kwa haraka na kwaishara nikamonyeshea kwamba nitampigia simu, na asiwe na wasiwasi. Mama Marim alipo fungua mlango, macho yetu yakakutana.
“Mama mimi ndio ninakwenda”
“Ahaaa sawa Dany nakutakia safari njema na ugua pole”
“Sawa mama”
Tulizungumza mazungumzo ya mafumbo, kamba vile ni watu tunao heshimiana kumbe ni masaa machache tu yamepita tumetoka kuburudishana. Nikawaaga wote kwa pamoja yeye na mwanaye kisha mimi nikatoka nje na kumkuta Hassani akiwa ananisubiria nje ya gari. Akanipokea begi langu na kuliweka siti za nyuma. Kutokna gari yenyewe ni VX V8, hakuona haja ya kuliweka begi langu hilo nyuma kabisa kwenye buti. Nikapanda kwenye gari na Hassani naye akaingia, taratibu safari ikaanza. Tukiwa kwenye mataa ya Ubungo, simu yangu ikaita, nikaitoa mfukoni na kukuta ni K2 ndio anaye piga.

“Ndio bosi”
“Mumefika wapi?”
“Ndio kwanza tupo foleni hapa Ubungo mataa”
“Ahhaa sawa, nilitaka kulifahamu hilo tu”
“Usijali”
“Basi safari njema mukifika Tanga utanijulisha”
“Sawa”
Nikakata simu na kuirudisha mufukoni. Magari ya upande wetu yakaanza kuruhusiwa na trafki anaye yaongoza magari sehemu hii. Safari ikaendelea huku kwenye gari tukisikiliza msiki wa taratbu. Kutokana na mikiki mikiki niliyo ipata jana usiku na mama Mariam, nikajikuta nikipitiwa na usingizi na kumuacha Hassani akifanya kazi yake ya uendeshaji, sikuwa na wasiwasi naye kwa maana Hassani ni dereva mmoja mzuri, hadi amepewa jukumu la kumuendesha bosi wa kitengo chetu basi aliweza kufudhu majaribio mengi aliyo pewa kabla ya kuajiriwa.

Kwa mbali nikiasikia sauti ya Hassani akiwa anazungumza na mtu, taratibu nikajikuta nikifungua macho, nikakuta simu yake akiwa ameiweka sikioni. Nikataza nje ya kioo na kukuta tupo Chalinze, kwenye foleni kidogo ya mabasi yaendayo Morogoro na mikoa ya Tanga na Arusha.
“Sawa honey”
Hassani akakata simu, na kuiweka mfukoni mwake.
“Kaka umetembea?”
“Yaaa nimetumia lisaa kama na dakika tano hivi, ingekuwa hii asubuhi hakuna foleni foleni ya mabasi, basi sasa hivi tungekuwa mbali sana”
“Sawa sawa, tukifika pale Lugoba naomba tuingie tupate kifungua kinywa”
“Sawa sawa”
Safari ikazidi kusonga mbele muda huu tukiwa tunazungumza mambo mengi na Hassani. Tukafika maeneo ya Lugoba na kuingia kwenye shele hiyo ambo watu hapa wanajipatia vyakula mbalimbali. Hassani akasimamisha gari pembeni, kisha tukashuka wote wawili, akalifunga  na kuelekea katika sehemu yenye mgahawa.
“Hassani zungumza tu unakula nini?”
“Kaka labda chai ya maziwa na sambusa”
“Kula ndugu yangu”
“Ahaa huwa nikiwa ninasafiri tena nikiwa ninaendesha huwa sipendi kula sana, huwa tumbo linamtindo wa kunisumbua sumbua”
“Sawa”

Nikaagizia sambusa tano na supu. Vikaeletwa vyakula hivyo na muhudumu tuliye muagiza na kuanza kula msosi huo taratibu taratibu. Tukiwa hapo mabasi kadhaa yakaingia, huku basi moja linalo kwenda Tanga niliweza kulifahamu, linaitwa Ratco. Wakashuka abiria wake, kwa ajili ya kuweza kujipatia vyakula na kunyoosha viungo.
“Hili gari linakwenda Tanga”  
“Ahaaa”
“Yaa kampuni yake ipo maeneo ya uwanja mmoja Tanga uitwa Mkwakwani”
“Ahaa sawa, alafu hizi gari zipo nyingi sana”
“Yaa zipo nyingi”
Tukaendelea kula taratibu huku tukiwatazama abiri wanao zunguka zunguka kwenye sehemu hii, huku wengine wakionekana kuwa na haraka haraka. Gari ambalo tunalizungumzia, likaanza kuondoka eneo hili na kuelekea Tanga. Ila tukiwa hapo, tukamuona dada mmoja, akihaha huku baadhi ya wauza miskaji wakimuuliza ana tatizo gani.
“Ratco imeniacha”
Dada huyo alizungumza huku machozi yakinilenga lenga.
“Ratco si hili basi lililo ondoka muda huu?”
Hassani aliniuliza huku akimtazama dada huyo mwenye asili ya kiarabu.
“Ndio hilo”  
“Kama linaelekea Tanga, basi tuondoke naye, tulifukuzie gari hilo”
“Hembu ngoja”
Nikanyanyuka kwenye kiti na kumfwata dada huyo sehemu alipo simama na wauza miskaki hao, wanao onyesha kufanya juhudi za kutaka kumsaidia.

“Samahani dada umechwa na basi hillo linalo elekea Tanga?”
“Ndio kaka yangu naomba munisaidie jamani”
“Mimi nipo na gari binafsi tunaelekea Tanga, tunaweza kulifukuzia gari hilo na kulipata”
“Kaka anga tafadhali nakuomba sana”
Dada huyu aliye valia baibui jeusi, alizungumza kwa kubabaika sana.
“Naomba unisubiri hapa”
Nikarudi hadi kwenye kiti alicho kaa Hassani, nikamuita muhudumu, nikampatia pesa anayo tudai, kisha Hassani akanyanyuka na kuelekea alipo lisimamisha gari. Nikamfwata dada huyo alipo, tukaelekea sehemu gari lilopo, yeye akapanda siti ya nyuma na mimi nikaka siti ya mbele ambapo ndipo kuna nilipo kuwa nikekaa.
“Dada yangu funga mkanda tafahali”
Dada huyo akatii alicho eleza na Hassani, na hapo safari ikaanza. Hassani ikamlazimu kutumia ujuzi wake wote katika kuhakikisha kwamba analifukuzia basi hilo na kulipata. Mara kwa mara nikawa ninayatupia macho yangu kwenye dasbod ya gari hili na kuona jinsi mshale wa spidi unavyo panda taratibu hadi kwenye spidi mia na thelathini. Nilijikuta nikiguna kimoyo moyo kwa maana gari kusema kweli, linakwenda mwendo mkubwa, sikuweza kumuambia Hassani apunguze kwa maana lengo la kufanya hivyo ni kulipata basi hilo.

“Dada usiwe na wasiwasi tutalipata basi hilo”
Nilizungumza huku nikigeuka nyuma na kumtazama dada huyo, anaye onekana kujawa na wasiwasi mwingi sana. Hassani hakuishia hapo akazidi kuongeza mwendo kasi, hadi mapigo ya moyo yakawa yananienda mbio kwani tayari mstari huo ulisha gonga kwenye spidi mia na sabini.
“Hapa tukikutana na askari wakitupiga tochi imekula kwetu”
Hassani alizungumza, huku akilipita gari kubwa, semitrela ambalo nalo lipo kwenye mwendo wa kasi. Hadi tunafika maeneo ya daraja la Wami, kidogo Hassani akapunguza mwendo, kwenye matuta hayo, ila basi hilo hatukuweza kulikuta.
“Ina maana Ratco inakimbia kiasi cha kutowea kulikuta?”
Hassani alizungumza na kumfanya dada huyo ambaye hadi sasa hivi hatulifahamu jina lake.
“Ndio, dereva wa leo anakwenda kasi kama nini?”
“Aahaaa anataka kugeuza tena?”
“Ndi akifika tena Tanga anageuza na kurudi nalo Dar”
“Basi hakuna tabu, hadi tunafika Segere na kuhakikishia Dany, tutakuwa tumesha likuta”


Riwaya: SIKU YANGU- Sehemu ya 05 na 06

0
0
 Mtunzi: YOZZ PIANO MAYA
***ilipoishia***

akanyanyuka haraka akaanza kumkagua kulwa kwa kugisi huenda damu hizo zinamtoka mwanae....alistahajabu kumkuta kulwa hana jeraha lolote.....Rose akaamua kuzipiga hatua za taratibu huku hofu kubwa imetanda juu yake....macho ya Rose yalionekana kutazama kwa tahadhari kubwa.....wakati huo bi'chenda macho yalimtoka akawa na wasiwasi....jasho lilimtoka mfululizo hata hakusikia maumivu ya lile jeraha alilochomwa na kipande cha chupa..
Rose alipokaribia kuifikia kabati,,,ghafla ikasikika Honi ya pikipiki......upande wa nje ya Geti...

***Endelea***
Rose akastuka.....akazipiga hatua za harakaharaka mpaka dirishani, alipochungulia aliona pikipiki nje ya uzio..kutokana geti lilikuwa na uwazi kuanzia katikati mpaka upande wa juu..akamuina Mumewe Seba amerudi...Rose akaamua kutoka chumbani na kuelekea upande wa nje ili akafungue geti....
Bi'chenda akaona hiyo ndio nafasi pekee ya kutoka chumbani humo......akatoka haraka kule nyuma ya kabati,huku akichechemea akazifuta yale matine ya damu iliyokuwa kwenye sakafu.......kisha akafungua mlango alipotoka nje,,,akakutana uso kwa uso na Rose huku akiwa Seba kwenye korido....Bi'chenda alistuka sana..hakutarajia kukutana na Rose akimshuhudia akitokea chumbani kwake..wakati tangu asubuhi alionekana kuwa hayupo ndani ya nyumba hiyo...Rose alistahajabu kumuona mama mke wake akiwa ameva kaniki nyeusi kwa kujifunga rubega.....Seba hakushangaa,, hakujua kilichokuwa kinaendelea ndani ya nyumba hiyo...

Rise akauliza kwa mshangao....Mama ulikuwapi nimekutafuta tangu asubuhi haukuwepo ndani!!!....Bi'Chenda akajibu kwa kudanganya,,huku akitabasamu akasema,,"mimi nilikuwemo chumbani kwangu nimelala najisikia homa,,,nimeamka baada ya kumsikia kulwa akilia...ndio nikawa nimeingia humu chumbani kuona kapatwa na nini,,,sijakukuta..
nimembembeleza amekwisha nyamaza...Rose hakujali akajisemea moyoni,,"kumbe alikuwemo chumbani kwake...mmh!!!niliogopa...
Rose na Seba wakaingia chumbani....

Polisi yawashikilia watu 10 kwa mauaji diwani wa Chadema Morogoro

0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linawashikiliwa watuhumiwa zaidi ya 10 wa mauaji ya aliyekuwa diwani wa Chadema, Kata ya Namwawala Wilaya ya Kilombero, Godfrey Lwena.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Ulrich Matei amesema watuhumiwa hao wanashikiliwa kwa uchunguzi na upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani.

Lwena aliuawa na watu wasiojulikana kwa kukatwa na mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake akiwa nyumbani kwake Februari 22, 2018.

Matei amesema kwa sasa majina ya watuhumiwa hayo yanahifadhiwa ili kutoharibu uchunguzi, na kwamba yatawekwa wazi baada ya upepelezi kukamilika.

Awali, katika taarifa yake kwa nyombo vya habari kamanda Matei amesema mauaji hayo yanatokana na kisasi kufuatia kifo cha mkazi wa kata hiyo, Kennan Haule aliyeuawa na watu wasiojulikana mwanzoni mwa mwaka 2016.

Amesema mtu huyo ameuawa kufuatia mgogoro wa shamba uliopo kati ya wananchi na Bodi ya Sukari ambapo Lwena alinukuliwa akiwaambia wananchi kuwa Haule asipokufa hawatapata haki yao na baada ya siku kadhaa aliuawa.

Amebainisha kuwa eneo hilo lina migogoro ya muda mrefu ya mashamba na watu wengi wameuawa katika mazingira yanayofanana.

 “Tunaendelea na uchunguzi wa kina katika eneo lile la Namwawala na kata za jirani ili kubaini hao wanaoendesha haya mauaji na wote watachukuliwa hatua za kisheria,” amesema  Matei.

DPP akata rufaa hati ya kuzuia dhamana kukataliwa

0
0
Mkurugenzi wa Mashtaka DPP amekata rufaa kupinga uamuzi wa Jaji wa Mahakama Kuu, Firmin Matogoro wa kukataa hati ya kuzuia dhamana ya washtakiwa Antonia Zakaria na Timoth Kilumile wanaokabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi.

Kwa mara ya kwanza, washtakiwa katika shauri hilo la uhujumu uchumi namba 3/2018 walifikishwa mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza Januari 17 mwaka huu.

Washtakiwa hao walikuwa  wakikabiliwa na mashtaka matatu ya kula njama na kujimilikisha mali Chama cha Ushirika cha Nyanza (NCU) na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh10 bilioni.

Baada ya kusomewa mashtaka, wakili wa upande wa mashtaka Seth Mkemwa anayesadiana na Shadrack Kimaro aliwasilisha hati ya kiapo ya DPP kuzuia dhamana kwa kile alichoeleza ni kulinda maslahi ya Taifa na usalama wa washtakiwa.

Baada ya kusikiliza hoja za upande wa utetezi unaowakilishwa na wakili Deocles Rutahindurwa, Jaji Matogoro uliitupilia mbali hati hiyo akisema haina uhalali mbele ya macho ya sheria kwa sababu imetoa hoja za jumla bila kueleza maslahi ya Taifa inayolindwa wala watakaowadhuru washtakiwa wakiachiwa kwa dhamana.

Katika uamuzi wake, Jaji Matogoro alikubaliana na upade wa utetezi kwa kusema DDP ametumia vibaya madaraka yake kuwasilisha hati hiyo kwa sababu kwa sababu anajua haiwezi kuhojiwa mahakamani ndio maana hakubainisha maslahi ya Taifa inayolindwa.

"Haiingii akilini namna gani usalama wa unavyotishiwa wala nani wanaoutishia wakati wameishi mitaani bila kudhurika tangu mwaka 2002 wanapodaiwa kutenda makosa hayo," alisema Jaji Matogoro katika uamuzi wake juzi.

Shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa leo Februari 27 baada ya upande wa mashtaka kuieleza mahakama kuwa upelelezi umekamilika, lakini lilipoitwa ndipo wakili Shadrack alipoieleza mahakama kuwa DPP amekata rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama wa kutupa hati ya kuzuia dhamana.

Jaji Matogoro ameahirisha shauri hilo hadi kesho Februari 28 rufaa hiyo ya DPP itakaposikilizwa.

Mbowe na vigogo Chadema waachiwa baada ya kuhojiwa kwa saa tano

0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wengine wachama hicho wameachiwa kwa dhamana baada ya kuhojiwa Kituo Kikuu cha Polisi tangu saa 6:50 mchana

Viongozi hao walifika kituoni hapo leo Jumanne Februari 27, 2018 na kuachiwa saa 1:02 usiku, kuitikia wito wa polisi.

Walikwenda kituoni hapo baada ya Mbowe kumaliza mkutano wake na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho yaliyopo mtaa wa Ufipa, Kinondoni.

Mmoja wa mawakili wa viongozi hao, Frederick Kihwelo amesema kuwa wote wameachiwa kwa dhamana kwa kutakiwa kuwa na mdhamini mmoja na kutakiwa kuripoti tena kituoni hapo Machi 5, 2018 saa 1 asubuhi.

Amesema viongozi hao walianza kuhojiwa saa 8:30 mchana, baada ya kufanya mazungumzo ya tuhuma zinazowakabili.

Februari 20, 2018 Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam iliagiza kukamatwa viongozi saba waandamizi wa Chadema akiwamo Mbowe.

Wito huo ulikuja siku chache baada ya tukio la kuuawa kwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini.

Akwilina aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya daladala eneo la Mkwajuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakienda ofisi za mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni kudai viapo kwa mawakala wao.

Viongozi wengine waliohojiwa sambamba na Mbowe ni  naibu makatibu wakuu, John Mnyika (Bara) na Salum Mwalimu (Zanzibar).

Pia, wamo mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee; mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti, John Heche na Esther Matiko ambaye ni mweka hazina wa Bawacha.

Mdee, Matiko, Heche na Mnyika walisharipoti awali na walitakiwa kurejea kituoni leo. Viongozi wengine waliwakilishwa na wanasheria.

Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Vicent Mashinji  hakwenda polisi kwa kuwa yupo nje ya nchi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya February 28

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images