Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Profesa Lipumba Atema Cheche Pemba...... Mazrui Azipangua

0
0
Profesa Ibrahim Lipumba, mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa amesema chama hicho hakina nguvu visiwani Zanzibar kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma kwa sababu ya uamuzi mbaya kiliouchukua wa kususia uchaguzi wa marudio.

Akizungumza katika mkutano wa ndani wa chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa Makonyo Chake Chake Pemba, Profesa Lipumba alisema nguvu ya CUF haipo tena kwa sababu hakipo katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK).

Alimtuhumu Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kuwa chanzo kwa uamuzi wake wa kubariki kutoshiriki uchaguzi huo, jambo lililokifanya kikose sifa za kuwamo katika serikali hiyo.

Wakati Profesa Lipumba akieleza hayo, Nassor Ahmed Mazrui ambaye ni naibu katibu mkuu wa CUF Zanzibar upande unaomuunga mkono Maalim Seif, alisema hawatambui ziara hiyo kwa maelezo kuwa mwenyekiti huyo si kiongozi wao.

“Chama kinawataka wanachama, viongozi na wapenzi wa CUF waliopo Pemba na Unguja kuwa watulivu na kuendelea na shughuli zao za maisha ya kawaida na kupuuza kabisa ujio huo wa Profesa Lipumba,” alisema Mazrui.

Mazrui alisema CUF kipo imara na hakijaishiwa nguvu kama Profesa Lipumba anavyodai.

“Mimi ndiyo mtendaji wa shughuli za chama, mwezi uliopita nilifanya tathmini inayoonyesha CUF ina nguvu na bado ipo imara. Pia wanachama na wafuasi wake wanakikubali na wana morali,” alisema Mazrui.

Januari 28, 2016 Baraza Kuu la Uongozi la CUF lilitangaza kutoshiriki uchaguzi wa marudio visiwani Zanzibar uliotangazwa na Tume ya Uchaguzi (ZEC), likitoa hoja 12 za uamuzi huo.

Uchaguzi huo wa marudio wa rais wa Zanzibar, wawakilishi na madiwani ulifanyika Machi 20, 2016.

Uamuzi huo wa CUF kutoshiriki uchaguzi huo ulitokana na mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha kufuta matokeo ya uchaguzi wa rais, wawakilishi na madiwani uliofanyika Oktoba 25, 2015 kwa maelezo kuwa sheria na kanuni zilikiukwa na baadaye kutangaza kurudiwa upya.

Kususia kwake kushiriki, kulikipa fursa CCM kushinda kwa kishindo uchaguzi huo huku Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein akiwateua wanachama wa vyama vingine vya upinzani katika baraza lake la mawaziri, akiwamo, mlezi wa chama cha ADC Hamad Rashid Mohamed ambaye pia aliwania urais kupitia chama hicho aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi.

Katika mkutano wake wa jana, Profesa Lipumba alisema CUF kuwapo ndani ya SUK ilikuwa ni fursa kubwa kwake kupiga hatua za maendeleo kwa jamii na Taifa kwa ujumla na kwamba kukosekana kwake kumewanyima haki wananchi wanaokiunga mkono.

“Wawakilishi wangapi tumekosa kwa kugomea uchaguzi? Nataka ieleweke kuwa mtu akifanya jambo lazima aangalie masilahi ya mbali badala ya kuangalia masilahi ya karibu,” alisema Profesa Lipumba.

Alisema hatua hiyo inaweza kutoa mwanya kwa chama tawala kubadilisha Katiba kwa urahisi kwa sababu SUK haipo.

Pia Profesa Lipumba alisema matukio mengi yakiwamo ya kupigwa kwa wafuasi wa CUF hasa katika maandamano yaliyofanyika miaka ya nyuma yanatokana na Maalim Seif kutofuata maelekezo ya viongozi wenzake wa juu wa chama hicho.

Mbali na hilo, Profesa Lipumba aliwakumbusha wanachama na wafuasi wa chama hicho waliohudhuria mkutano huo namna aliyojiuzulu Agosti, 2015 na kurejea katika nafasi hiyo mwaka mmoja baadaye.

Profesa Lipumba ambaye pia mtaalamu wa uchumi, aliwasomea wajumbe hao barua yake ya kujiuzulu wadhifa huo na ile ya kutengua uamuzi wake huo.

Aliwaambia wana CUF hao kuwa hivi sasa si wakati wa kulumbana, bali ni wa kuunganisha nguvu ili chama hicho kiendelee kudumu na kutetea haki za wanachama na wananchi.

Akijibu hoja kususia uchaguzi, Mazrui alisema mazingira yaliyojitokeza katika Uchaguzi wa Mkuu 2015, chama hicho kisingiweza kushiriki uchaguzi wa marudio.

“Hatuyumbishwi, hatujutii kutoshiriki uchaguzi ule, bali tunasonga mbele ya kudai haki yetu ya Oktoba 25, 2015,” alisema.

Mazrui alisema hawakushangaa kusikia Profesa Lipumba akitoa kauli hiyo dhidi ya CUF upande wa Zanzibar na kusisitiza kwamba uamuzi wa kutoshiriki uchaguzi uliamuliwa na Baraza Kuu la Uongozi Taifa la chama hicho.

“Tunawajua watu waliopo nyuma ya ziara hii ya Profesa Lipumba na waliofanikisha mpango huu.Ndio maana hatutambui ujio wake na hatuna shida wala hatuhitaji kusikia maneno yake,” alisema Mazrui.

Mmoja wa viongozi waliokuwamo katika kikao hicho cha Lipumba ni mbunge wa zamani wa Gando, Khalifa Suleiman Khalifa ambaye aliwataka wanachama wa CUF kuamka na kuachana na tabia ya kumfanya Maalim Seif kama mfalme katika chama hicho.

“Licha ya upendo mlionao kwa Maalim Seif, lakini mtambue wakati wa kufanya hivyo umepita hasa kwa sababu ameshawambia uongo na anaendelea kuwadanganya,” alisema.

Akizungumzia ziara ya Profesa Lipumba juzi, kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Shekhan Mohamed Shekhan alisema anayo taarifa,
 
“Ni kweli tumepokea taarifa ya ujio wake na tutatoa ulinzi kwa maana anatambuliwa na vyombo husika kama kiongozi ukizingatia zaidi mazingira walionayo kwenye chama chao.”

Mgogoro CUF ulianza mwaka 2016 baada ya Lipumba aliyekuwa amejiuzulu kutengua uamuzi huo. Alitangaza kujiuzulu uenyekiti, Agosti 5, 2015 lakini baada ya mwaka mmoja alitengua uamuzi huo na kurejea katika wadhifa huo jambo ambalo lilipingwa na baadhi ya wananchama.

Mgogoro huo umezaa makundi mawili ya wanachama, moja linaloongozwa na Profesa Lipumba na jingine, Maalim Seif. Mgogoro huo umesababisha pande hizo mbili kuburuzana mahakamani.

Zitto Kabwe asimulia kuhusu Mtu Aliyevunjwa Mbavu Mahabusu

0
0
Mbunge wa jimbo la Kigoma Mjini , Mhe. Zitto Kabwe amefunguka na kudai kuwa jeshi la polisi nchini limekuwa likikiuka utaratibu na kuvunja sheria na kusema akiwa rumande amemshuhudia kijana ambaye amevunjwa mbavu kituoni na hajapelekwa kutibiwa.

Zitto Kabwe amesema hayo juzi Februari 23, 2018 akiongea na waandishi wa habari na kusema kuwa kitendo cha yeye kukamatwa na kulazwa ndani kwa siku moja kumemfanya agundue kuwa kuna Watanzania wengi wanateseka na kupata shida kwenye vituo vya polisi nchini.

"Watanzania wanateseka sana chini ya mikono ya polisi, sheria inataka ndani ya masaa 48 polisi wame wamewafikisha mahakamani watuhumiwa lakini tumekutana na watu wamekaa ndani siku 3 hata maelezo tu hawajaandika, wengine wana siku 20 wapo ndani hawajafikishwa mahakamani" alisema Zitto Kabwe

Kiongozi huyo aliendelea kudai kuwa polisi wamekuwa wakiwatesa wananchi ndani ya vituo hivyo vya polisi na kusababisha majeraha kwa baadhi ya watuhumiwa bila kuwapeleka hospitali kwa matibabu.

"Tumekuta watu ambao wanateswa, kijana mmoja mpaka mbavu zimevunjika na zaidi ya siku saba hajapelekwa hospitali kwa matibabu, mpaka  tunaondoka hajapelekwa hospitali, tulipozungumza na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro tulimweleza hilo, kuna watu ni wagonjwa hawajapelekwa hospitali akasema atashughulikia sasa sijui kama yeye alikuwa hajui hilo" alisema Zitto Kabwe

Mbali na hilo Zitto Kabwe amesema hali kiujumla ya nchi yetu kwa sasa ni tata kwa kuwa suala la mauaji yameendelea kutokea kinyume na mazoea yaliyokuwepo kipindi cha nyuma na kudai kuwa kuna kila sababu ya uchunguzi wa mauaji hayo kuanzia yale ya Kibiti mpaka haya ambayo yanaendelea sasa kuchunguzwa na vyombo huru na si jeshi la polisi kwa kuwa jeshi hilo nalo linatuhumiwa.

CHADEMA Yataka Wafuasi Wake Waliko Polisi Ambao Wanamajeraha ya Risasi Wakatibiwe

0
0
Siku 10 baada ya wanachama wa Chadema kukamatwa na polisi eneo la Mkwajuni wilayani Kinondoni jijini Dar, chama hicho kimelalamika baadhi yao kuendelea kushikiliwa na polisi katika kituo cha Oysterbay wakiwa na majeraha ya risasi bila kupatiwa matibabu, wala kufikishwa mahakamani.

Wakati chama hicho kikuu cha upinzani nchini kikieleza hayo, Polisi Mkoa wa Kinondoni wamesema hakuna mahabusu mgonjwa anayeshikiliwa bila kutibiwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Jumanne Murilo alisema  jana kwamba, polisi wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mahabusu wagonjwa wanatibiwa katika hospitali za Serikali bila malipo yoyote.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema jana  alisema wanachama wao watatu walishambuliwa kwa risasi Februari 16.

Mrema alibainisha kuwa wanachama hao walishambuliwa kwa risasi wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakielekea ofisi ya msimamizi wa uchaguzi wa ubunge Jimbo la Kinondoni kudai barua za viapo vya mawakala wao.

Aliwataja wanachama hao kuwa ni Isaack Ngaga, Erick John na Aida Oromi.

 “John na Ngaga wao walikamatwa wakiwa majumbani mwao baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali. Hawa hawakukamatiwa kwenye vurugu,” alisema Mrema. 

“Mmoja kati yao (John) alikamatwa na watu waliojifanya watumishi wa haki za binadamu na kudai wanataka kwenda kumhoji, alipokataa ndipo walitoa vitambulisho vyao vinavyoonyesha wao ni Polisi.”

Alisema hatua iliyochukuliwa hadi sasa ni kuwaelekeza wanasheria wa Chadema kufungua kesi Mahakama Kuu kumshtaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali na polisi, kuwataka wawafikishe mahakamani wanachama hao. 

“Tumemwelekeza mwanasheria wetu kufungua kesi ili wanachama wetu hao watatu wapelekwe mahakamani na kupatiwa matibabu,” alisema Mrema.

Alisema kuendelea kushikiliwa bila kupelekwa hospitali wakati wana majeraha ni hatari kwa maisha yao, kwa kuwa vidonda hivyo vitaoza.

“Wanakaa nao kinyume na sheria, mpaka sasa walipaswa wawe wameshawapeleka mahakamani,” alisema.

Kwa upande wake, Murilo alisema sheria ipo wazi inawaelekeza mahabusu wote wanapougua kutibiwa.

“Si hao mahabusu wa Chadema pekee, mahabusu yeyote anapougua hupelekwa hospitali za Serikali ambako hutibiwa bure kwa mujibu wa sheria,” alisema.

“Kama wanaolalamika wangekuwa mahabusu ningekuwa na cha kuzungumza, lakini kama wapo nje waache waendelee kusema, ninachojua hakuna mahabusu ambaye hajatibiwa.”

Mmoja wa ndugu wa Aida, Hilda Sigala alisema, “Jana (juzi) nilikwenda kumtembela ndugu yangu kituoni. Amenieleza kuwa mpaka sasa hajapelekwa hospitali na wanampaka dawa tu ya kukausha kidonda wakati ana jeraha la risasi. Yupo kituoni tangu Februari 16.”

Alisema hali hiyo si sahihi kwa sababu kidonda alichonacho Aida kinazidi kuwa kikubwa jambo ambalo ni hatari kwa afya yake.

Wahamiaji Haramu 83 Wakamatwa Iringa

0
0
Zikiwa zimepita siku tatu tangu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam iwahukumu kifungo cha mwaka mmoja jela wahamiaji haramu 77 kutoka Ethiopia, wengine 83 wamedakwa mkoani Iringa huku dereva aliyekuwa akiwasafirisha akifanikiwa kutoroka.

Wahamiaji hao walikamatwa wilayani Kilolo mkoani hapa wakiwa safarini kupelekwa Malawi kisha Afrika Kusini.

Hata hivyo katika harakati za kukamatwa kwao, dereva wa lori mali ya mkazi wa Tukuyu mkoani Mbeya alitoroka.

Raia hao wa Ethiopia walikamatiwa katika Kijiji cha Mbigili ambapo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji Mkoa wa Iringa, Hope Kawawa alisema walikamatwa juzi saa kumi na moja jioni karibu na bomba la mafuta la Tazama.

Alisema wahamiaji hao walipelekwa kituo cha polisi cha Lugalo na kwamba, kukamatwa kwao kunatokana na taarifa iliyofikishwa Uhamiaji na wananchi.

Alisema maofisa wa Uhamiaji kwa kushirikiana na polisi walipowakamata baadhi yao waliwakuta hali zao ni mbaya kutokana na kukosa chakula kwa siku tatu na pia kuathiriwa na joto kutokana na bodi la lori walilokuwa wakisafiria kuwa la bati. 

“Wahamiaji hawa walikuwa wanasafiri kwenye lori mali ya mkazi wa Tukuyu mkoani Mbeya, dereva alikimbia na hajapatikana lakini uchunguzi unaendelea,” alisema.

Aliongeza kuwa wahamiaji hao watafikishwa mahakamani kesho kujibu mashtaka yanayowakabili.

“Naomba niwaambie madalali wanaosafirisha hawa wahamiaji kuwa mkoa wa Iringa si mahala salama kuwapitisha kwa kuwa tuko makini saa 24 na tukiwabaini hatua kali zitachukuliwa dhidi yao,” alisema.

Alitoa wito kwa wananchi kutoa taarifa pindi wanapohisi baadhi ya watu si raia wa Tanzania na wanapowaona watu wasiowatambua. Mtanzania aliyekamatwa akihusishwa na usafirishaji wa wahamiaji hao, Hassan Mwalusanjo alisema hana anachofahamu.

Alisema aliomba lifti katika gari hilo kutoka Tukuyu kwenda Dar es Salaam kununua vifaa vya gari wakati gari hilo lilipokuwa likisafirisha ndizi. Mwalusajo alisema baada ya kushusha ndizi eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam, dereva aliondoka na aliporeja alipanda kurejea Tukuyu.

Alisema walipofika Ilula alishuka kula ndipo dereva alipoondoka na gari na aliporejea alimuomba amsaidie kusafisha gari.

“Sielewi chochote nilishangaa kuwekwa chini ya ulinzi baada ya dereva kuniambia nimsaidie kusafisha gari ambako nilikuta makopo ya maji na mifuko ya mikate,” alisema akiwa chini ya ulinzi.’’

Mpenzi Wangu Ibilisi ( Simulizi ya Kweli) Sehemu ya 04

0
0
Mwandishi: Grace Godfrey Rweyemam

Baadaye mchungaji alianza kuyakemea na kuyawashia moto hayo mapepo, yakapiga kelele sana huku yakidai kuwa akiyafukuza yakaondoka mume wake hataweza tena kuishi. Yalidai kuwa kwa yeye kufanya maamuzi ya kwenda kuombewa ni kama kusababisha fedheha kubwa kwa mume wake na hivyo wakuu wake watamuua.

 Yalipiga kelele kwa nguvu yakidai kuungua kisha yakamtoka, nadhani wenye uzoefu wa kukemea mapepo mnanielewa. Nilizungumza na kaka yangu huyu mchungaji akanieleza baadhi ya vitu ambavyo Jovina hakuwa amenieleza kabla.

Baada ya kufunguliwa alimwambia ukweli kuwa mara kadhaa amekuwa akiota kama katika kitanda chao wamelala yeye na mumewe na wanawake hata watatu au wane.

 Alidai hiyo hutokea mara nyingi sana, lakini pia alikiri kuwa licha ya kuwa yeye hufanya tendo la ndoa na mumewe kila siku, lakini siku zote amekuwa ni kama mtu ambaye ana muda mrefu sana hajakutana na mwanaume na hicho kitu kimemsumbua kwa muda mrefu sana. Yaani hali ya mwili wake kutamani mwanaume siku zote iko juu sana.

Siku hiyo baada ya kuombewa alidai hataki tena kwenda nyumbani kwake. “Sitaki tena kumuona mume wangu, simuhitaji tena, sijisikii kuwa naye na hii ni ajabu sana kwani mimi muda wote huwa najihisi kumtamani mume wangu.

Hapa ninawawazia watoto wangu tu, lakini siko tayari tena kuishi nyumba moja na yule shetani tena. Hisia za mapenzi nilizokuwa nazo juu yake hazipo tena na simuoni tena kama mume wangu bali kama adui mkubwa,” Alieleza Jovina huku akisisitiza kutorudi tena nyumbani kwake. Niliwaza ni namna gani kaka yangu huyo mchungaji alitatua hilo, kwani alikuwa bado ni mke wa mtu na ana familia. Pia hapo akili ikaanza kujiuliza ni jinsi gani angerudi nyumbani kwake baada ya kumshambulia mume wake kiasi hicho katika ulimwengu wa roho.

TANGA RAHA- Sehemu ya Kumi na Nne ( 14 )

0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Mama Fetry akamrukia Madam Fety na kumlaza kwenye kochi na wakaanza kuminyana na kumfanya madam Zena kutoka bafuni uchi huku akiwa ana mapovu kwenye baadhi ya sehemu za mwili wake”
“Jamani shost zangu mbona munakuwa kama watoto wadogo kupigana pigana.Hilo swala si tu-shalizungumza kuwa Eddy akija atachagua nani amtakaye.Na wewe Eddy mwanaume mzima wezako wanapigana wewe umesimama unawaangalia”
“Tena koma wewe manamke usen*** wenu kaufanyieni kwenu musitake niwazabe amkofi hapa”
“Msen*** mwenyewe wewe na wazazi wako walio kuzaa”
“Zena unasemaje wewe”
“Kama ulivyo nisikia”
Nikamsogelea Madam Zena kwa hasira na kumkaba koo na kuwafanya Mama Fety na Recho kuacha kupigana kuja kuingilia ugomvi huku wakianza kunipiga makofi ya mgongoni baada ya kumsikia mwenzao akiomba msaada anakufa

ENDELEA
Nikamuachia Madam Zena na kuwageukia Mama Fety na Madam Recho na kuwafanya warudi nyuma kwani sura yangu imetawaliwa na asira kiasi kwamba kila mmoja akaniona ni mtu watofauti
“Changanyeni mbaliga zenu na mtoke ndani kwangu kabla sijafanya kitu kitakacho wapotezea maisha”
Kwa jinsi sauti yangu ilivyo badilika na kuwa ya kutisha masikioni mwao kila mmoja akaanza kuvaa kilicho chake na kutoka ndani ya chumba changu na nikaufunga mlango,baada ya dakika kadhaa mlango ukagongwa nikapiga hatua za taratibu kwenda kuufungua na kukuta na madam Zena
“Samahani Eddy niimesahau funguo za gari langu hapo juu ya meza”
Nikazichukua funguo zake kisha nikampatia na kaondoka zake,nikabadilisha nguo na kuvaa nyinine na kisha safari ya kuelekea kwenye hoteli ikaanza huku nikipita ile njia ya vichpochoro hadi nikafika Hotelini,Nikapiga hatua mpaka ninafika usawa wa chumba nikamuona muhudumu akigonga mlango ikanibidi kuongeza hatua za kwenda sehemu alipo
“Samahani dada nikusaidie nini?”
Nilizungumza huku nikishika kitasa cha mlango na kumfany muhudumu kusogea kando kidogo na kunipisha mimi nisimame usawa wa mlangoni

“Nyinyi si ndio mulio kuja na ile gari aina ya Spacio?”
“Ndio”
“Basi nilikuwa ninawomba mukaisogeze pale mlangoni kwani sio sehemu za parking za magari”
“Sawa dada nimekuelewa….Je maegesho ya magari yapo wapi?”
“Upande wa kushoto wa hoteli kuna geti amapo humo ndani ndio maegesho yapo”
“Asante:
Nikamuacha aondoke usawa wa mlango na mimi nikafungua mlango na kukaa ndani nikastuka kuto kumkuata shem Halda kitandani,Nikapiga hatua hadi bafuni na kumkuta akiwa amesimama kwenye huku ameegemea ukutani huku akiwa analia
“Halda nakuomba twende nyumbani”
Halda hakuzungumza kitu zaidi ya kukaa kimy huku akinitazama kwa macho ya hasira kiasi kwamba mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio
“Halda nakuomba twende nyumbani kwani usiku umesha ingia”
“Niache wewe ndenda zako”
“Hapana tumakuja pamoja kwanini unahitaji kubaki peke yako”
“Eddy niche peke yangu hunijui sikujui kwahiyo usiwe mtu wa kunisumbu hembu nenda kwako au nimwambie Rahma kuwa unanisumbua?”

“Hapana shemeji utakuwa hujatenda haki kwani hembu basi jaribu kulifikiria swala la mimi ku-fanya mapenzi na wewe endepo Rahma siku atafahamu wewe unahisi itakuwaje?”
“Wewe ni mtoto hadi mwambie kuwa umefanya mapenzi na mimi?”
“Hapana ilAa….”
“Eddy hakuna cha ila.Nakuomba utoke ndani ya chumba changu nitalala mwenyewe sawa”
Halda alizungumza kwa hasira na kunifanya nianze kupiga harua za kuelekea mlangoni taratibu kabla sijaufikia nikaisikia sauti yake kwa nyuma
“Eddy ndio unaondoka?”
“Halda ni bora niondoke kuliko kumsaliti mpenzi wangu”
“Eddy nakuomba usimwambie Rahma kuwa nilikufanyia hivi”
“Snto mwambia endapo wewe huto endelea kunisumbua”
“Sawa Eddy mimi sinto kusumbua ila nakuomba unifikirie japo kwa siku moja na mimi niweze kupata kile unacho mpa Rahma”
“Sawa”
“Basi ngoja nivae nguo zangu nikurudishe nyumbani kwako”
Halda akavaa nguo zake kisha tukaondoka na safari ya kuelekea kwangu ikaanza,njia nzima ha-kuana aliye msemesha mwenzake zaidi ya ukimya kutawala ndani ya gari
“Ingia barabara ya mtaa huo”

Rais Magufuli Ashiriki Ibada Ya Misa Takatifu Iliyofanyika Katika Kanisa La Kigango Cha Mlimani Chato

0
0
Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akishiriki Ibada ya misa Takatifu katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25,2018.


Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akishiriki Ibada ya misa Takatifu katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25,2018


Walichojadili Waziri Mwakyembe, Rais wa FIFA na CAF kuhusu uanachama wa Zanzibar

0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM,Dar es Salaam
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) Gianni Infantino na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) Ahmad Ahmad wamekiri kuielewa hali ya Zanzibar pamoja na kuzingatia Sheria wamesema wanaona mazingira Maalum ya Zanzibar.

Kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mambo mbalimbali serikali iliyozungumza na Marais hao wa mashirikisho ya mpira wa miguu kwa ngazi ya bara la Afrika na Dunia walipofika nchini hivi karibuni kwa ajili ya kufanya mkutano wao wa kuandaa ajenda za mkutano mkuu wa dunia.

‘’Marais hao walisema kuondolewa kwa Zanzibar katika uanachama wa CAF kulizingatia sheria zinazosimamia Shirikisho hilo lakini pamoja na hayo waliamua kuiachia  Zanzibar kuendelea kufaidika na  fursa zote wanazopatiwa wanachama wa CAF  isipokuwa kuwaruhusu kupiga kura, pia wanasema wataangalia zaidi ya hilo maeneo mengine namna ya kuisaidia Zanzibar,”Dkt.Harrison Mwakyembe.

Akiendelea kuzungumza katika Mkutano huo Mheshimiwa Mwakyembe alisisitiza kuwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa alieleza kwa ufasaha mgogoro huu wa soka kwa viongozi hao wenye dhamana na mashirikisho hayo nao kumuelewa ambapo walisisitiza kuhitaji serikali kuendelea kushauriana nao katika suala hilo.

Pamoja na hayo nae Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia aliwasihi wapenzi wa soka nchini kuendelea kuwa watulivu kwani suala hilo linashughulikiwa na viongozi wa ngazi za juu nao wanalifahamu

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 09 na 10)

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA      

Lucy alizungumza mara baada ya kuniona nikiwa ninashangaa shangaa. Tukaingia kwenye lifti japo ni nyumba ya gorofa moja ila ina lifti yake. Tukafika juu, nikakuta seble nyingine hii ikiwa imeizidi seble ya chini mara dufu.
“Hichi ndio chumba utakacho kuwa unakitumia kwa maagizo ya baba kama jinsi alivyo sema”
Nikaingia kwenye chumba hicho, kwa jinsi kilivyo kikubwa kikanifanya nibaki nimeduwaa.
“Njoo nikuonyeshe kitu”
Lucy alizungumza huku akielekea kwenye mlango mmoja ulipo ndani ya chumba hicho, akaufugua na kuingia ndani na mimi name nikaingia ndani.
“Hili ni bafu, sinki hilo la kuogea lote limetengenezwa na dhahabu hata hayo mabomba unayo yaona hapo pembeni yametengenezwa na dhahabu”
Lucy alizungumza, kitendo cha yeye kugeuka na kunitazama, usoni tukagonda vifua na kujikuta chocho zake zilizo simama vizuri zikigusana na kifua change kilicho jengeka vizuri kwa mazoezi.

ENDELEA
“Ahaa am sorry”
Lucy alizungumza huku akitazama chini kwa aibu, akataka kusogea pembeni ila nikamuwahi kumshika kiuno. Tukatazama usoni kwa dakika kadhaa, nikamuona jinsi Lucy anavyo tetemeka kwa woga kwenye midomo yake inayo chezacheza.
“Dany”
“Mmmm”
Lucy akaka kimya baada ya mimi kuitikia hakujibu kitu chochote, nikamsogeza karibu kabisa na mwili wangu, miili yetu ikagusana kabisa. Lucy akazidi kutetemeka na kujikuta akifumba macho na kushindwa kunitazama kabisa usoni mwangu.

Nikasogeza lipsi zangu taratibu hadi zikagusana na lipsi zake. Lucy akakunja kabisa sura yake na kuyapandisha mabega yake juu kidogo akionekana kuogopa sana kwa kitu ambacho ninataka kukifanya. Nikameza mate kidogo  kisha nikarudisha kichwa changu nyuma na kumuachia mkono.
Nikaendelea kutazama bafu hilo lililo tengenezwa vizuri sana, akilini mwangu ninakwaza juu ya utajiri wa mzee Jongo, akiwa kama mtumishi wa serikali japo yupo ngazi ya juu, ila pesa zote hizi amezitolea wapi. Lucy akatoka bafunu humo pasipo kunisemesha kitu cha aina yoyote. Ikanibidi na mimi kutoka, sikumkuta pia katika chumba hichi.

“Amekwenda wapi huyu?”
Nilizungumza huku nikielekea mlangoni, nikafungua na kumuona akiingia kwenye moja ya chumba kilichomo huku juu gorofani.
“Anatatizo gani huyu?”
Nilijiuliza huku nikielekea kwenye chumba hicho, nikakuta mlango ameurudishia tu na kuna kijiupenyo kidogo ambacho unaweza kuona ndani. Nikausukuma taratibu na kuchungulia ndani. Nikamuona Lucy akiwa amekaa kitandani huku akimwagikwa na machozi usoni mwake.
‘Ina maana amechukizwa na kumkiss?’
 Ikanibidi kuingia chumbani humo, Lucy akanyanyua kichwa chake. Kwa ishara ya mkono akanionyesha ishara ya kutoka chumbani humo.

“Lucy kuna tatizo lolote jamani?”
“Nimesema ondoka chumbani kwangu”
Hapo Lucy alizungumza kwa hasira hadi nikabaki nikiwa nimemkodolea macho kwa maana sikutarajia msicha mzuri kama huyu anaweza kukasirika kwa namna hii.
“Lakini Lucy si…..”
“Koma kuniita jina langu, sitaki mazoea na wewe, hata kama umeniokoa na moto ila masikini kama wewe huwezi kuwa na mimi”
Maneno ya Lucy yakapenya moja kwa moja kwenye moyo wangu. Nikamtazama Lucy kwa macho yaliyo jaa uchungu, nikajikuta nikianza kujutia moyoni mwangu ni kwa nini nimejitia kwenye majaribu ya kumsaidia hadi leo sehemu ya mgongo wangu imepatwa na majeraha.

“Look at yourself. Do you think unaweza kuwa na msichana kama mimi ehee”
Lucy alizidi kuzungumza kwa dharau huku akinitazama usoni mwangu. Akanipandisha kwa macho na kunishusha kisha akaachia msunyo mkali ulio anza kunipandisha hasira.
“Let me tell you this. Wewe sio level yangu, na siwezi kuwa na wanaume wa Sinza kama wewe. Toka chumbani kwangu kabla sijakufanya kitu mbaya”
“Asante”
Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga. Nikatoka chumbani kwake, sikuona hata haja ya kurudi katika chumba nilicho ambiwa nitakaa humo. Sikutumia lifti iliyopo ndani humo, nikaanza kushuka kwenye ngazi za chumba hicho kwa haraka, nikatoka nje ya nyumba hicho. Nikafika getini mlinzi akanifungulia huku akinitazama usoni kwa kunishangaa kwa maana machozi yalisha anza kunilenge lenga. Ubaya wa huku Masaki, pikipiki wala bajaji hazipiti piti mitaani, ikanibidi kuanza kutembea hadi kwenye kituo cha dalala, nikakodi pikipiki, dereva akanipeleka hadi Sinza ninapo ishi.

“Nisubiri nikuletee pesa yako”
“Sawa bosi”
Nikaingia ndani, moja kwa moja nikaelekea chumbani kwangu, kitu kilicho nistua kidogo ni kuukuta mlango wangu upo wazi kidogo. Nikakumbuka kwamba jana sikuweza kuufunga na funguo ila niliuurudishia tu.
Nikaingia kwa kuusukuma taratibu. Macho yakanitoka baada ya kumkuta K2 akiwa amelala kitandani huku amejifunga taulo kiunoni mwake na amelala kifudi fudi.
Sikumstua chochote zaidi ya kuchukua pesa kwenye waleti yangu iliyokuwa kwenye sofa, nikatoka nje na kumlipa dereva bodaboda na kurudi chumbani kwangu.
   Nikamtazama jinsi K2 alivyo lala kitandani na makalio yake yalivyo ju. Nikatamani hata kuchukua mkanda na kuyacharaza pasipo uruma ila heshima ya kazi nikajikuta ikinivaa taratibu nikajikuta nikimgusa mgongoni na kumtingisha.
“Bosi, Bosi”
“Mmmmm”
K2 alizungumza huku akijigeuza taratibu. Akanitazama usoni mwangu, akaachia tabasamu pana kidogo.
“Umerudi?”
“Ndio, umekuja kufanyaje chumbani kwangu?”
“Kwani kuna ubaya wa mpenzi kuja nyumbani kwa mpenzi wake”
K2 alizungumza huku akikaa kitako kitandani, kwa jinsi ninavyo mtazama usoni mwake nikatamani kumtandika kofi kama alili nipiga jana asubihi, ila nikajikuta nikibaki nimemkazia macho. K2 akanitazama mikononi na kuishika kwa haraka na kuitazama.

Ahadi ya FIFA kwa Tanzania baada ya Rais Gianni Infantino kufika Nchini

0
0
Na Anitha Jonas –WHUSM , Dar es Salaam.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeahidi kuendeleza viwanja tisa nchini kufuatia kuongezeka kwa dau la pesa za Maendeleo na Kujiendesha zinazotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA kuanzia mwaka 2019 .

Kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari kuhusu mambo mbalimbali serikali iliyojadili na Rais wa FIFA Gianni Infantino alipokuwa nchini kwa mkutano wake hivi karibuni.

‘’Rais wa FIFA alieleza kuongeza mara nne ya kiwango cha pesa za maendeleo na kujiendesha walizokuwa wanatoa kwa mashirikisho kama TFF mpaka kufikia Dola Milioni Moja na Laki Mbili na Nusu kwa mwaka na kusema pesa hizo ndiyo zitumike kuendeleza viwanja vya michezo kwani uwepo wa viwanja ndio unaosaidia kukuza vipaji vya soka,’’alisema Dkt.Mwakyembe.

Akiendelea kuzungumza katika mkutano huo na waandishi wa habari Waziri Mwakyembe alisisitiza kuwa Rais huyo wa FIFA ametoa msisitizo wa kutokuwa na huruma kwa kiongozi yoyote wa shirikisho atakayekuwa na matumizi mabaya ya pesa pamoja na kufanya udanganyifu kwani yeye yuko mstari wa mbele kupinga ufisadi katika sekta ya maendeleo ya Soka duniani.

Pamoja na hayo nae Rais wa TFF  Bw. Wallace Karia alitoa ufafanuzi wa hali ya kifedha kwa shirikisho na kueleza kufuatia kuwepo na matatizo katika shirikisho hilo .FIFA ilikuwa imesitisha kuwapatia fedha hizo za maendeleo za kujiendesha tangu mwaka 2015 lakini baada ya kuingia uongozi mpya FIFA wameridhika nao na wameshaupa utaratibu wa kufuatilia fedha hizo.

‘’Rais wa FIFA alitueleza kuwa fedha hizo ziko salama nchini Zurich ni kwamba tu hazikuwa zimeruhusiwa kuingia nchini na kwa sasa tumeshaanza mchakato wa kufuatilia fedha hizo kwa kuzingatia maelekezo ya FIFA hivyo basi tutakapo pata fedha hizo Shirikisho  litaendeleza baadhi ya miradi ambayo tumekwisha iandaa,’’alisema Bw. Karia.

Pamoja na hayo rais huyo alitoa wito wa wakazi wa jiji la Tanga waliovamia eneo linalotarajia kujengwa Technical Center  ya mchezo wa soka  waondoke mara moja kabla hawajachukuliwa hatua.

Hukumu ya Sugu Kusomwa Kesho February 26

0
0
Hatima ya mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu Sugu anayeshtakiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli itajulikana kesho.

Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wanakabiliwa na kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya ambayo kesho Februari 26,2018 itatoa hukumu.

Washtakiwa wanadaiwa kutenda kosa hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Desemba 30,2017 eneo la Uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.

Hakimu Mkazi Mfawidhi, Michael Mteite anatarajiwa kutoa hukumu baada ya upande wa mashtaka na ule wa utetezi kukamilisha ushahidi Februari 9,2018.

Jamhuri iliwasilisha mashahidi watano na kielelezo kimoja cha sauti iliyodaiwa kurekodiwa na shahidi wa tano, Inspekta Joram Magova.

Upande wa utetezi uliwasilisha mashahidi sita wakiwamo Sugu na Masonga waliokana kutamka maneno wanayoshtakiwa kuyatoa.

Washtakiwa walitetewa na mawakili Sabina Yongo, Boniface Mwabukusi na Hekima Mwasipu kabla ya kujitoa na sasa wanawakilishwa na Peter Kibatala.

Kwa mara ya kwanza, Sugu na Masonga  walifikishwa mahakamani Januari 16 na kusomewa mashtaka na Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Pande aliyeeleza upelelezi ulikuwa umekamilika na walikuwa tayari kuendelea na usikilizaji.

Riwaya: SIKU YANGU- Sehemu ya 01 na 02

0
0
  Mtunzi: YOZZ PIANO MAYA
Ilisikika sauti ya mwanamke akilia kwa sauti kali sana ndani ya sekunde chache.....kisha sauti hiyo ikatulia kimya....baada ya sekunde kumi ikasikika sauti ya mtoto mchanga akilia.....baada ya dakika kumi kupita,,zikasikika sauti zikisikika zikisema"sukuma kwa nguvu....usibane mapaja utamuuwa mtoto...ghafla ikasikika sauti ikisema ""mama weee...

baada ya sekunde tatu hivi ikasikika sauti tena ya mtotochanga akilia....mwanamke huyo aitwae Rose alijifungua watoto mapacha wote wa kiume.walipishana dakika kumi za kuzaliwa...Rose alifurahi sana..Akamshukuru Mungu kwa kujifungua salama...baada ya masaa mawili kupita alikuja mumewe aitwae SEBA....alifurahi sana akasema,nitakupa zawadi mke wangu..nakuahidi nitakununulia gari...Rose alifurahi sana kusikia kauli hiyo ya mumewe..

***************
kesho yake majira ya saa nne za asubuhi.. madaktari walimruhusu Rose kwenda nyumbani..kutokana Rose alikuwa na nyonga pana sana hivyo haikuwa vigumu yeye kuzaa.. alijifungua salama bila kufanyiwa upasuaji wala kuongezewa njia kwa kuchanwa ukeni.
Seba alimchukua mkewe pamoja na mama yake mzazi ambayae ni mama mkwe wake Rose wakatoka nje ya hospital,,waliingia ndani ya gari na kuianza safari ya kuelekea nyumbani.

*************
ilipofika majira ya saa saba za usiku....mama yake na Rose aliamka....akanyanyuka kutoka kitandani akafungua begi lake na akatoa kaniki nyeusi akajifunga rubega...kisha akatoa mkoba mdogo uliokuwa umetengenezwa kwa ngozi ya Nyumbu.. akaufungua na kutoa irizi mbili zilizokuwa zimefungwa kamba nyeusi nyemba....akazivaa irizi hizo.....akazipiga hatua mpaka kwenye kona ya chumba akasimama wima. huku makalio kayageuzia ukitani......akatoweka kichawi....akajitokeza ndani ya chumba cha mwanae.....Rose alikuwa kalala fofofo pamoja na mumewe Seba...Mama huyo aitwae Bi'CHENDA  akavua irizi moja yenye rangi nyekundu..akaitemea mate kisha akazipiga hatua kukifuata kitanda...alipofika karibu sana...akaanza kukizunguka kitanda mara tatu..kisha akamgusa pacha mmjoja kichwani kwa kutumia irizi hiyo...akazioiga hatua na kueleke kwenye kona ya chumba hicho akageuka na makalio yakageukia ukutani kisha akatoweka kichawi....

Kakobe akana kukwepa kodi,asema taarifa za TRA ni za Kisiasa

0
0
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Followship (FGBF), Zachary Kakobe amekanusha taarifa za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwamba kanisa lake linakwepa kodi.

Akizungumza leo Jumapili Februari 25, 2015 katika kanisa hilo lililopo Mwenge, jijini Dar es Salaam Kakobe amewataka waumini wa kanisa hilo kuzikataa taarifa hizo na kwamba zimejaa siasa,ni za kishilawadu

Kakobe ametoa ufafanuzi huo zikiwa zimepita siku nne tangu TRA kutoa taarifa ya uchunguzi katika kanisa hilo na kubaini mambo saba.

Polisi wamtia mbaroni Mama anayetuhumiwa kumuua Mwanae na kumzika

0
0
Msichana mwenye umri wa miaka 25, Anastazia Elias, mkazi wa Kata ya Kipindu wilayani Nkasi mkoani Rukwa, amenusurika kifo baada ya kuokolewa na polisi akituhumiwa kumuua mtoto wake baada ya kujifungua.
 
Wananchi wakiwa na silaha za jadi yakiwemo mawe walianza kumshambulia mwanamke huyo wakimtuhumu kumuua mwanawe wa kiume baada ya kujifungua ambapo alimviringisha na vipande vya khanga na kumuweka kwenye kikapu alichokificha chini ya uvungu wa kitanda chake.
 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, George Kyando amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea juzi saa nane mchana katika Kijiji cha Kipundu kilichopo mjini Namanyere.
 
Kamanda Kyando amesema mtuhumiwa huyo anashikiliwa na Polisi wilaya Nkasi na kwamba atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi wa tukio kukamilika. Wakizungumza baadhi ya wanawake  wamedai mtoto huyo alizikwa juzi usiku katika kaburi lililochimbwa ndani ya nyumba ambayo mama yake mzazi anaishi na bibi yake.
 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya February 26

Mwijage azindua kiwanda cha kwanza cha mita za luku Dar

0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amezindua kiwanda cha Inhemeter ambacho kitakuwa kinazalisha mita za luku na kuziuza kwa mashirika ya ugavi wa umeme nchini.

Kiwanda hicho ambacho ni cha kwanza kujengwa hapa nchini na cha nne Afrika kina soko la uhakika la kuuza mita 500,000 kwa mwaka kwa Shirika la Umeme nchini (Tanesco), Wakala wa Umeme Vijijini (Rea) na Shirika la Umeme Zanzibar (Zeco).

Mwijage aliyataka mashirika hayo kutumia fursa ya kuwepo kwa kiwanda hicho kuboresha huduma zao huku akisisitiza kwamba kitakuwa na manufaa mengi ikiwemo ajira kwa vijana 100 na mashirika kutotumia fedha za kigeni kuagiza mita nje ya nchi.

“Ninamuomba mwekezaji kuzalisha bidhaa nyingi zenye ubora wa kimataifa na bei nafuu sokoni,” alisema Mwijage wakati akizindua kiwanda hicho jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Alisema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kujenga uchumi wa kati na viwanda ifikapo 2025 na kuzinduliwa kwa kiwanda cha Inhemeter ni uthibitisho kuwa azma hiyo imeshaanza kutekelezwa kwa vitendo.

“Tunahitaji viwanda vitakavyo mpunguzia gharama mlaji au mtuamijia pamoja na kuzalisha ajira kwa vijana wetu,” alisema huku akitaka aliye tayari kuanzisha kiwanda ofisi yake iko wazi kumsaidia.

Waziri Mwijage alimpongeza mwekezaji huyo kwa uamuzi wake wa kuja Tanzania.

“Wakati umefika wa kuondokana na uchuuzi. Tunataka tuzalishe wenyewe hapa nchini na tuuze nje, simaanishi kuwa hatuhitaji bidhaa za nje, zije zile tu zenye ubora stahili,” alisema.

Pia alisema anayo furaha kushuhudia uzinduzi wa kiwanda kipya cha 3,307 katika kipindi kifupi.

Awali, akizungumza kwenye hafla hiyo, Mshauri Mkuu wa kiwanda hicho ambaye pia ni katibu mkuu mstaafu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dk Adelhem Meru alivishauri vitengo vya manunuzi nchini kusaidia ujenzi wa viwanda.

“Ningependa kutoa wito kwa vitengo vya manunuzi kuunga mkono kwa dhati azma hii ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kujenga uchumi wa kati na viwanda. Ninafahamu vitengo hivi vina nafasi nzuri sana,” alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho, Abraham Rajakili alisema Inhemeter ni kampuni yenye uzoefu wa miaka 20 katika tafiti, uzalishaji na usambazaji wa mita za luku na tayari wameshasambaza katika zaidi ya nchini 60 dunia.

“Kiwanda hiki kitakuwa na uwezo wa kuzalisha mita za luku milioni moja kwa mwaka na pia kuajiri mafundi mia moja Watanzania,” alisema.

PICHA: Sugu amefika Mahakamani tayari kusikiliza Hukumu ya Kesi yake

0
0
Ulinzi umeimarishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya ambako itatolewa hukumu ya kesi inayomkabili mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga.

Katika eneo la mahakama wapo askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiimarisha ulinzi nje ya jengo. Tayari washtakiwa wameshafika mahakamani.

Mahakama leo Februari 26,2018 inatoa hukumu ya kesi ambayo Sugu na Masonga wanashtakiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Wawili hao wanadaiwa kutenda kosa hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Desemba 30,2017 eneo la Uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.

Hukumu inatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Michael Mteite aliyesikiliza kesi hiyo. Upande wa mashtaka na wa utetezi ulikamilisha ushahidi Februari 9,2018.

Jamhuri iliwasilisha mashahidi watano na kielelezo kimoja cha sauti iliyodaiwa kurekodiwa na shahidi wa tano, Inspekta Joram Magova.

Upande wa utetezi uliwasilisha mashahidi sita wakiwamo Sugu na Masonga waliokana kutamka maneno wanayoshtakiwa kuyatoa.

Washtakiwa walitetewa na mawakili Sabina Yongo, Boniface Mwabukusi na Hekima Mwasipu kabla ya kujitoa, hivyo sasa wanawakilishwa na Peter Kibatala.

Kwa mara ya kwanza, Sugu na Masonga  walifikishwa mahakamani Januari 16 na kusomewa mashtaka na Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Pande aliyeeleza upelelezi ulikuwa umekamilika na walikuwa tayari kuendelea na usikilizaji

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Serikali Kuweka Alama za Kimataifa Mipaka ya Kenya na Uganda

0
0
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula amesema serikali itaanza kuweka alama za mipaka ya kimataifa katika mipaka yake na nchi jirani za Kenya na Uganda kuanzia mwezi ujao.

Hatua hiyo inatokana na baadhi ya alama za mipaka yake na nchi jirani katika maeneo mbalimbali kuharibika ama kuchezewa na hivyo kuleta mkanganyiko na nchi hizo.

Akizungumza katika ziara yake mkoani Mara mwishoni mwa wiki, Mabula alisema kwa sasa fedha kwa ajili ya kazi hiyo imeshatengwa na kinachosubiriwa ni kuanza rasmi kwa kazi hiyo mwezi ujao.

"Katika zoezi la kuweka alama za mipaka vitawekwa vigingi kila baada ya umbali wa mita mia moja sambamba na kubainishwa eneo la ardhi huru," alisema Mabula.

Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa serikali, tayari timu ya wataalamu kutoka nchi za Kenya, Uganda na Tanzania zimeshakutana na kukubaliana kuhusiana na uainishaji mipaka ya nchi hizo.

Mabula alisema kwa kuanzia alama zitawekwa katika mipaka iliyopo mikoa ya Mara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga na baadaye zoezi litaendelea katika maeneo mengine ya mipaka ya nchi.

Alisema ni imani yake kuwa baada ya kukamilika kwa zoezi la kuweka alama za kimataifa za mipaka, migogoro kuhusiana na mipaka itakwisha.

Mara ya mwisho Tanzania kuweka alama za mipaka ya kimataifa kati yake na nchi jirani ilikuwa mwaka 1975, ikiwa ni utekelezaji wa Tangazo la Serikali (GN) mwaka 1965 kuhusiana na mipaka.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Grorious Luoga, alimweleza naibu waziri huyo kuwa, mbali na suala la mipaka ya kimataifa, wilaya yake inakabiliwa na changamoto ya mipaka baina ya hifadhi ya Serengeti na wananchi wanaoizunguka kwa kuwa wamekuwa wakivamia na kujenga ndani ya hifadhi na wakati mwingine kuingiza mifugo.

Katika ziara yake hiyo ya kukagua mpaka wa Tanzania na Kenya katika eneo la Serengeti, Mabula alifuatana na Mkuu huyo wa Wilaya ya Tarime pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Upimaji Vijijini kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Huruma Lugalla ambao kwa pamoja walijionea hali halisi ya mpaka wa Tanzania na Kenya na baadhi ya alama za mipaka zilizoharibika.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images