Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ratiba Ya Kuaga Mwili wa Akwilina Akwiline Leo NIT


Viongozi wa Dini, Wanasiasa Wakutana Kujadili Hali ya Usalama Nchini

$
0
0
Viongozi  wa madhehebu ya dini walikutana jijini Dar es Salaam jana pamoja na wanasiasa kujadili "hofu iliyotawala" miogoni mwa wananchi inayosababishwa na kutokea kwa matukio ya mauaji na watu kutekwa nchini.

Viongozi hao pia walijadili uimara wa taasisi za madhehebu ya dini, uimara wa mfumo wa serikali, pamoja na uimara wa taasisi za vyama vya siasa tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.

Katika siku za karibuni, mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Maftah (22) alifariki kwa kupigwa risasi na polisi akiwa kwenye daladala jijini Dar es Salaam Ijumaa iliyopita.

Rais John Magufuli alisema katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii ya Twitter Jumapili "Nimeviagiza vyombo vya dola kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria waliosababisha tukio hili."

Rais Magufuli pia alielezea kusikitishwa sana na kifo cha Akwilina, na kutoa pole kwa familia, ndugu, wanafunzi wa NIT na wote walioguswa na msiba huo.

Aidha, kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ambaye pia alikuwa katibu wa Chadema kata ya Hananasif, Daniel John, alikutwa ameuawa na mwili wake kutupwa katika ufukwe wa Coco jijini Dar es Salama pia wiki iliyopita baada ya kutekwa mwanzoni mwa mwezi na watu wasiojulikana.

Akizungumza katika kikao hicho, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Dayosisi ya Karagwe mkoani Kagera, Benson Bagonza alisema hofu nchini bado ipo baada ya kuwapo kwa matukio ya watu kupigwa risasi na kutekwa.

"Sijawahi kuona risasi za moto zikirushwa kwa raia, watu wanapigwa risasi mchana kweupe, sasa inatakiwa tufike mahali tuseme basi," alisema Askofu Bagonza.

Alisema viongozi wa dini wataendelea kuonya matukio kama hayo pindi yatakapotokea bila ya kujali nani yupo madarakani.

Naye Amiri Mkuu wa Baraza Kuu na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Mussa Yusuph Kundecha alisema ni kweli hofu miongoni mwa wananchi ipo baada ya kuwapo kwa matukio ambayo hawajawahi kuyaona miaka ya nyuma.

Alisema hofu hiyo inatokana na baadhi ya matamshi ya viongozi wanayoyatoa kwa wananchi na viongozi wa vyama vya siasa.

Akizufungua kikao hicho, Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia (TCD), James Mbatia alisema:"Tanzania bado kuna hofu, vipo viashiria ambavyo siyo vizuri.

"Kuna Watanzania wamepoteza maisha kwa kupigwa risasi, akiwamo binti Akwilina. Wengine wamepotea, wengine wametekwa na kuuwawa.

"Bado kuna manung'uniko, malalamiko miongoni mwa wananchi, mauaji yanatokea, Watanzania wana hofu juu ya matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu."

Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha NCCR-Mageuzi, alisema lengo kuu la mkutano huo lilikuwa kujadili lengo la 16 katika 17 ya malengo ya millennia, ambalo linahusu amani, haki na taasisi imara.

Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alisema Watanzania siyo kwamba wana hofu tu, bali hata hali ya kuishi haipo.

Mwenyekiti wa Chama cha UDP, John Cheyo alisema kongamano hilo limejikita katika kuwa na mazungumzo ya kujenga amani.

Alisema Watanzania wanahitaji kuishi kwa amani na kwamba watu wanapoandamana, kuuawa, kukaidi amri ya polisi maana yake hakuna amani nchini.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (Nec), Kilumbe Ng'enda alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye amani kati ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, na Nchi za Maziwa makuu.

"Kwenye nchi hamuwezi kukaa kama mpo peponi, lazima mtatofautiana," alisema Ng'enda, "(lakini) Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye amani."

Viongozi wengine wa dini waliohudhuria ni Askofu Dk. Alinikisa Cheyo ambaye ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristu nchini, Mkuu wa Kanisa la KKKT, Dk. Fredrick Shoo, Askofu Moses Matonya, Askofu Stephen Munga na Askofu Ebem Mshiu.

Pia Sheikh Hassan Kebeke ambaye ni mwenyekiti mwenza wa kamati ya viongozi wa amani Mwanza alikuwepo.

TANGA RAHA- Sehemu ya Kumi na Moja ( 11 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

   Recho akaongeza sauti ya redio hadi mwisho na kuipunguza haraka haraka na kunitazama usoni.Sikujua na jinsi kwani tayari pombe za mchana zimewachanganya.Recho akaendelea kucheza taarabu nayoimba ‘JAMANI NINA MWAGA RADHI’ huku wengine wakiitikia ‘MWAGAAAA’
Zena akawa anafungua taulo na kulifunaga.Mlango ukagongwa tane nikajua bibi amerudi tena,nikasimama na kwenda kufungua mlango.Moyo ukanistuka baada ya kumkuta ni Mama Fety amesimama huku akihitaji kuingia ndani kwangu

ENDELEA
   Tukatazamana na Mama Fety kwa sekunde kadhaa huku kila mmoja akiwa kimya ikanibidi niuvunje ukimya
“Vipi mbona unakuja bila taarifa?”
“Eddy akuomba unipishe niingie ndani?”
Mama Fatuma alizungumza huku akinisukuma akitaka kupita ndani kwangu kilazima ila hakunishinda nguvu nikamzuia na akabakia amesimama huku sura akiwa ameikunja
“Eddy nataka niingie huko ndani nikamkomeshe huyo Malaya wako”
“Kwani huku ndani ni kwako wewe vipi?”
“Eddy kama unataka nikujazie watu sema sishindwi mimi nakusemesha kiustaraabu unajifanya kuweka kibesi”
Mama Fety akausukuma mkono wangu uliokuwa umemzuai mlangoni na kuingia ndani kwa hasira.
“Mwangalie lilivyo mshuka”
Mwalimu Zena alizungumza huku akimtazama Mama Fety na kumfanya aanze kuangua kicheko huku akikaa kwenye sofa
“Shosti zangu jamani nisameheni kwa kuwatukana jamani”
“Mimi nilivyo isikia sauti yako wala sikujisumbua kunyanyuka kwani tumesha kuzoea”

Madam Recho alizungumza na kunifanya nishangae hapo ndipo nikagundua wanajuana ila sikujua wamejuana juana vipi
“Eddy huyu Asha umejuana naye vipi?”
“Heee Zena hadi kujuana na Eddy unataka kujua hembu acha ushapkuna”
“Sio ushapkuna kwa maana Eddy wa watu hapa Tanga hana hata mwezi bibi wewe umesha anza  kumuwekea wivu”
Wakaachia kicheko kikali huku kikisindikizwa na maneno ya kimbea ‘KANITANGAZE USIPO NITANGAZA NITAKUTANGAZA MIMI’ huku wakigongeana mikono na kunifanya nikae kimya
“Eddy usitushangae huyu Asha sisi tumemjua kutokana na mwanaye anasoma kidato cha pili basi huyo mtoto wake mcharuko kama mama yake haipiti mwezi bila shost huyu kutinga shule kusikiliza kesi ya mwanaye”

“Eddy wala mwanagu si mcharuko wanamsingizia tu ndio maana siku nyingine huwa ninawachambaga waalimu”
“Unatuchamba au tunakuchamba na safari hii  mwanao akileta tu mapepe mapepe tunamtimua”
“Mtimueni kwani shule ni moja nitampeleka ulaya akasome”
“Teeee ulaya kwenyewe unapasikia ndio embuse mwanao apeleke kiuno chake huku kufanya nini”
“Si kusoma”

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Mwili wa Akwilina ulivyochukuliwa Muhimbili kupelekwa NIT kuagwa

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa aliongoza msafara wa magari, likiwemo lililobeba mwili wa  mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kuelekea katika viwanja vya chuo hicho kwa ajili ya kuagwa.

Jeneza lenye mwili wa mwanafunzi lilikuwa  katika gari maalumu la kubebea maiti.

Baada ya kuaga mwili wa mwanafunzi huyo, saa 10 jioni safari kuelekea wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro kwa mazishi itaanza. Akwilina atazikwa kesho

Wanafunzi Wazimia na Kupoteza Fahamu Baada ya Kumuona Akwilina ndani ya Jeneza

$
0
0
Vilio, simanzi na kupoteza fahamu kwa baadhi ya wanafunzi ni baadhi ya matukio ya huzuni yanayojitokeza katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), baada ya kuwasili mwili wa aliyekuwa mwanafunzi wa chuo hicho, Akwilina Akwiline.

Mwili wa mwanafunzi huyo unaagwa leo, Februari 22, 2018 katika viwanja vya chuo hicho.

Wanafunzi zaidi ya wanne aliokuwa akisoma nao Akwilina chuoni hapo ni kama hawaamini baada ya kushuhudia jeneza lenye mwili wake, huku wengine wakipoteza fahamu na kupewa huduma ya kwanza na Shirika la Msalaba Mwekundu.

Viongozi waliofika mpaka sasa katika viwanja vya NIT ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi; Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako; Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni; Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa na Mbunge wa Kibamba (Chadema), John Mnyika.

Tayari ibada ya kuaga mwili wa mwanafunzi huyo imeanza.

Wafuasi 28 wa CHADEMA Waliokamatwa Wakiandamana Kinondoni Wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Watu 28 wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Chadema wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakituhumiwa kufanya mkusanyiko usio halali na kinyume na sheria.

Washtakiwa hao wamefikishwa mahakamani hapo mbele ya hakimu mkazi, Godfrey Mwambapa na kusomewa shtaka la kufanya mkusanyiko usiyo halali na Wakili wa serikali, Faraji Nguka

Wakili Faraji Nguka, amedai kosa hilo wamelitenda February 16, 2018 barabara ya Kawawa maeneo ya Kinondoni Mkwajuni ambapo walifanya mkusanyiko usio halali wakiwa na nia ya kusababisha uvunjifu wa amani.

Baada ya kusomewa kosa hilo washtakiwa walikana ambapo Wakili Nguka ameeleza kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Hata hivyo, Hakimu Mwambapa alitoa masharti ya dhamana kwa washtakiwa ambapo wametakiwa kuwa na mdhamini mmoja atakayesaini Bondi ya Sh.Milioni 1.5

Washitakiwa hao wamerudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 3, 2018 itakapotajwa.

Baadhi ya mabango kwenye msimba wa Akwilina Akwlini yakiwashinikiza Mwigulu Nchemba na IGP Sirro Wajiuzulu

$
0
0
Baadhi ya waombolezaji katika ibada ya kuaga mwili wa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali, yakiwamo ya kumtaka waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba na mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro kujiuzulu.

Ibada hiyo imefanyika leo Februari 22, 2018 katika viwanja vya NIT, Mabibo na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu, wakiwamo viongozi mbalimbali wa Serikali.

Waombolezaji hao walinyanyua mabango hayo baada ya waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako aliponyanyuka kutoa salamu kwa wafiwa kama walivyofanya viongozi wengine, akiwamo mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Baadhi ya ujumbe katika mabango hayo ni; “muuaji hawezi kujichunguza na Mwigulu, Sirro kwa mauaji haya bado mko ofisini.”

Juhudi za kuwataka waombolezaji hao kushusha mabango ziligonga mwamba kutokana na baadhi ya watu waliokuwa karibu yao kuja juu, wakitaka waachwe kwa maelezo kuwa wana haki ya kufanya hivyo.

Katika salamu zake za rambirambi, Profesa Ndalichako alisema: “Rais Magufuli ameshaagiza uchunguzi ufanyike na mimi kama waziri nasisitiza vyombo vinavyohusika vifanye uchunguzi haraka.

“Matukio ya aina hii hayapaswi kuendelea, nimehuzunika kwa msiba huu na naomba Watanzania waungane kuiombea familia.”

Father Raymond: Aliyetekeleza Mauaji ya Mwanafunzi Akwilina Awekwe Hadharani na Aombe Msamaha..... Vinginevyo Hatutafika Mbali

$
0
0
Padri Raymond Mayanga wa Parokia ya Yohane Mbatizaji Luhanga amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kumsaka mtu aliyempiga risasi mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafishaji (NIT), Akwilina Akwilini, kumweka wazi ili awaombe radhi Watanzania.

Akizungumza katika ibada ya kuaga mwili wa mwanafunzi huyo inayofanyika katika viwanja vya NIT, Mabibo, Padri Mayanga amesema mtu huyo hata akifungwa miaka 30 hadi 40, Akwilina hatarudi.

“Awe amefanya kwa nia nzuri au mbaya vyombo vinavyohusika vikimaliza taratibu zake kama ni kupitia televisheni ama nini huyu mtu aombe msamaha, vinginevyo hatutafika mbali. Leo kwa Akwilina huenda kesho kwa mwingine,” amesema.

Naye mwakilishi wa familia ya Akwilina, Aloyce Shirima amesema, “Tunaomba mtufikishie salamu kwa Rais John Magufuli  kuwa wale wote waliofanya kitendo hicho wachukuliwe hatua stahiki. Taifa haliwezi kuendelea kwa kuondokewa na wasomi kizembe.”

“Akwilina ni mtoto wa sita katika familia ya watoto nane wa mzee Akwilini na ni mtoto  pekee aliyependa elimu katika familia hiyo.”

Rais wa Serikali ya wanafunzi NIT, Mchunja Othman amesema, “Alikuwa mcheshi asiyejua kununa. Tunaiomba Wizara ya Mambo ya Ndani kuhakikisha inalisimamia hili ili haki itendeke. Hii inatupa fursa ya kujifunza sisi kama binadamu maisha yetu siyo ya kudumu hivyo tutende mema.”

Mpenzi Wangu Ibilisi ( Simulizi ya Kweli) Sehemu ya 01

$
0
0
Mwandishi: Grace Godfrey Rweyemam
“Habari dada Grace! Ninaweza kuonana na wewe tuongee?”
Nilipata ujumbe huo mfupi wa simu kutoka kwa namba nisiyo ifahamu nikiwa katikati ya shughuli zangu.

Nilisoma nikajiambia kuwa ningempigia baadaye kujua ni nani na ni sababu gani hasa inamtaka aniombe tuonane. Simu yangu ya awali ilikuwa imeharibika hivyo kunifanya nipoteze baadhi ya namba, hivyo sikuwa na ujasiri sana wa kumuuliza mtu ni nani endapo ametumia namba nisiyoifahamu na hajajitambulisha.

Niliendelea na kazi zangu, nikarudi kwangu na kuwa bize na shughuli za ndani, nikaja kukumbuka ule ujumbe nikiwa kitandani tayari kwa kulala. Mara nyingi huwa sipendi kupiga simu ikishafika saa nne usiku, nikaamua kwamba ningempigia yule mtu kesho yake.

Asubuhi sana nikiwa ndio naamka uliingia ujumbe mwingine kwenye simu yangu, “Dada Grace, naitwa Jovina, hunifahamu ila mimi nakufahamu kwa kusikia habari zako. Nahitaji sana kuongea na wewe, najua utanisaidia.”

Nilimpigia muda huo na kumwambia juu ya ratiba yangu ya siku hiyo. Nilikuwa na muda kuanzia mchana na ingebidi anifate maeneo ambayo ningekuwa, kwa bahati akawa tayari kunifuata popote.

Alidai maongezi yetu yangechukua muda mrefu kidogo na yangehitaji sehemu tulivu. Nilimuomba tukutane maeneo ya chuo  kikuu cha mlimanii kwani huko tungepata sehemu tulivu bila kuingia gharama yoyote, na pia nilikuwa na kazi kadhaa za kufanya nikiwa huko chuo. Dakika kumi kabla ya muda niliopanga tuonane alinipigia, tukakutana.

Kwa muonekano huyu ni binti umri wa kati, siyo mdogo sana lakini sikudhani kama huenda akawa mwanamke mwenye watoto. Ni mzuri wa sura na rangi, mrefu kiasi na siyo mnene.

Hakuna mtu ambaye angemtazama na kuhisi mzigo alioubeba, kwani uso wake una tabasamu muda wote na ana muonekano wa kujiamini. Nilipoanza kumsikiliza ndipo niligundua kuwa alichobeba moyoni hakiwezii kuonekana kwa macho.

“Kuna siku nikiwa na mawazo mengi mno kuhusiana na hali ambazo nimekuwa nikipitia, niliamua kupitia mtandaoni, nikakutana na post yako ya ushuhuda ambayo rafiki yangu wa fesibuku alikuwa ameshea kwenye kurasa yake. Nilitazama picha yako ile uliyolala kitandani unaumwa kabla sijasoma, nikajikuta natoa machozi (mimi ni mtu wa machozi ya karibu sana).

Nilianza kusoma nikahisi ni hadithi au habari ya mtu mwingine kwani sikuamini kuwa mwenye hiyo picha inayoonekana ndiye aliyeandika hayo yote, kwani ulionyesha ni mwaka tu umepita.

Kuanzia hapo nilifuatilia huo ushuhuda wako mpaka mwisho na hakuna simulizi ya mtu imewahi kuniliza kiasi kile. Baada ya kukufuatilia kwenye kurasa yako, na ule ushuhuda wako, niliiambia nafsi yangu kuwa huenda wewe ukawa mtu sahihi kuongea naye.

Najua ninachokwambia huenda hakitahusiana sana na ushuhuda wako, lakini ndani ya nafsi yangu nimeona ni vema niongee na wewe, na nashukuru sana umekubali kunisikiliza.

Nina miaka 26, na nina mume na watoto wawili. Niliolewa nikiwa na miaka ishirini lakini ilikuwa kwa shinikizo la wazazi wangu. Mume wangu ana pesa nyingi mno, yaani ni Tajiri sana, lakini hutaweza kuamini maisha ambayo mimi na watoto wangu tunaishi.

Tunaishi maisha ya kawaida kabisa, usafiri tunaotumia ni daladala mara zote isipokuwa siku ambazo tunatoka na mume wangu. Yeye ana gari nzuri, za kifahari na siyo moja wala mbili lakini siruhusiwi hata kupewa dereva aniendeshe.

Ananipa mahitaji yangu yote lakini sina akaunti ya binafsi wala siwezi kupewa kiwango kikubwa cha pes hata siku moja. Wakati naolewa nilikuwa ndio nimemaliza diplopa ya mambo ya hoteli lakini sikuwahi kuruhusiwa kufanya kazi, ingawa niliona ni kawaida sababu mume ana pesa na hata kazi ambayo ningepata ingekuwa ya kipato kidogo tu, lakini nilipoingia kwenye ndoa niliona bora ningefanya hata kazi ndogo. Kwa sasa kiukweli hayo maisha nimeyazoea na najionea sawa tu.

Mume wangu aliwashawishi wazazi wangu kwa pesa zake kunioa, wakidhani wananipeleka kwenye mikono salama, lakini kumbe walikuwa wananipeleka kwenye uangamivu mkubwa.

Ndani ya miaka sita ya ndoa yangu nimekuwa mtumwa mkubwa Grace, nilikuja kugundua miezi michache tu baada ya kuolewa kuwa mume wangu ni mchawi na sharti kubwa la pesa zake ni mke wake asionekane hata siku moja kama mke wa tajiri. 

==>Endelea Nayo <<Kwa Kubofya Hapa>>

Msajili wa Vyama vya Siasa Aiweka Kitanzini CHADEMA.....Awaandikia Barua Kuwata Wajieleze Kwa Kufanya Vurugu na Maandamano

$
0
0
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amekiandikia barua Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akitaka kijieleza kwa nini asikichukulie hatua kwa kufanya maandamano Februari 16, 2018.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema amesema barua hiyo ya msajili waliipokea jana na wanapaswa kuijibu kabla ya Februari 25, 2018.

Chadema waliandamana Februari 16 mwaka huu wakishinikiza kupewa viapo vya mawakala wao kabla ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kinondoni.

Serikali Yaagiza Viwanda Nchini Kutumia Barcodes Za GS1

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza kila kiwanda kilichopo nchini kihakikishe kinatumia alama za utambuzi za GS1 Tanzania simbomilia (barcodes).

Ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Februari 22, 2018) wakati akifungua Mkutano wa Sita wa Wamiliki wa Viwanda na Watumiaji wa simbomilia (barcodes). Hadi sasa GS1 ina wanachama 2000.

“Natoa wito kwa wenye viwanda kutumia GS1 Tanzania kutangaza na kuuza bidhaa zenye ubora katika maduka ya kimataifa, ambapo pia bidhaa zao zitachangia katika ulipaji wa kodi kwa usahihi”.

Amesema matumizi ya alama hiyo, iwe ndio chanzo cha kulipeleka Taifa kwenye kampeni ya kuhamasisha jamii kununua bidhaa zilizotengenezwa nchini. Hadi sasa

Waziri Mkuu amesema kama kila bidhaa itakuwa na utambuzi wa Taifa kiambishi “620”, wataweza kuwa na takwimu sahihi za wazalishaji ambao wanatambulika.

Pia Waziri Mkuu amesema utambuzi wa bidhaa zinazozalishwa nchini ukifanyika kwa kutumia GS1 kila duka litalipa kodi kwa kila bidhaa inayouzwa.

Hata hivyo Waziri Mkuu amesema barcodes ni muhimu kwa sababu zinawawezesha wajasiriamali kuuza bidhaa zao katika maduka rasmi ya nje na ndani ya Tanzania.

Amesema miaka ya nyuma kabla ya kuanzishwa kwa GS1 Tanzania, wazalishaji wa bidhaa za Tanzania walilazimika kwenda nje ya nchi yetu kutafuta barcodes ili waweze kuuza bidhaa zao.

Waziri Mkuu amesema hali hiyo iliifanya Tanzania kuwa wategemezi na kuchangia kuzalisha ajira kwa ajili ya nchi nyingine kwa kununua barcodes zao. “Tangu kuanzishwa kwa chombo chetu, tumejinasua kutoka katika utegemezi huo.

Pia Waziri Mkuu amesema amefurahishwa na mipango iliyowekwa na GS1 Tanzania ya kuhakikisha kwamba mazao ya kilimo yanapatiwa barcodes na kuwaelimisha wananchi kuhusu alama hizo.

Mkutano huo umehudhuriwa na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stella Manyanya, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara SMZ, Balozi Amina Salum Ally,  Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Elisante Ole Gabriel.

Wengine ni Mwenyekiti wa Bodi ya GS1 Tanzania Dkt. Gidion Mazara, Wakuu wa Taasisi na Wadau wa GS1 kutoka Tanzania Bara na Visiwani (TBS, BRELA, TANTRADE, ZNCIAAL, COSTECH na Mtendaji Mkuu wa GS1 Tanzania Bi. Fatuma Kange.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, FEBRUARI 22, 2018.

Taarifa Muhimu Toka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais IKULU

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa wito kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kusimamia vizuri rasilimali walizonazo na kukusanya kodi vizuri ili waweze kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi wa miundombinu na kuimarisha huduma za afya kwa wananchi.

Mhe. Rais Magufuli ametoa wito huo leo tarehe 22 Februari, 2018 mjini Kampala nchini Uganda wakati akichangia katika mkutano wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaojadili maendeleo na upatikanaji wa fedha kwa ajili ya miradi ya sekta ya miundombinu na afya.

Kabla ya Mhe. Rais Magufuli kutoa mchango wake, Marais walioshiriki mkutano huo wamepokea taarifa ya mkutano wa majadiliano ya kisekta (Round Table) kuhusu mahitaji ya fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya sekta ya miundombinu na afya ambapo imeelezwa kuwa katika miaka 10 ijayo nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zitahitaji Dola za Marekani Bilioni 78 kutekeleza miradi ya miundombinu inayopendekezwa.

Taarifa hiyo imechangiwa na wadau mbalimbali wakiwemo Marais, wawakilishi wa sekta binafsi na washirika wa maendeleo ambao wameelezea njia mbalimbali za kupata fedha za kutekeleza miradi hiyo ikiwemo kutumia mfumo wa ushirikiano kati ya Serikali na Sekta binafsi (PPP).

Katika mchango wake Mhe. Rais Magufuli amesema pamoja na kutumia mfumo wa PPP ni muhimu kwa Serikali za kila nchi kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato ya kodi na rasilimali nyingine ili kutekeleza miradi ya miundombinu, afya na sekta nyingine.

Ametahadharisha kuwa japo kuwa mfumo wa PPP ni mzuri, ni vyema wataalamu wakachukua tahadhali za kutosha ili kuepusha Serikali kuingia katika mikataba isiyokuwa na maslahi kwa nchi zao kutokana na baadhi ya wadau wa sekta binafsi kutaka kutengeneza faida kubwa kwa kupandisha gharama za miradi.

Mhe. Rais Magufuli ametolea mfano wa miradi mikubwa iliyoanza kutekelezwa nchini Tanzania ukiwemo ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) na ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stieglers’ Gorge), kuwa Serikali ya Tanzania imeamua kuanza kutekeleza miradi hiyo kwa kutumia fedha zake baada ya kufanikiwa kusimamia vizuri rasilimali zake na kubana matumizi.

“Mimi naamini tukiamua tunaweza, nchi zetu zina rasilimali nyingi za kuweza kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo, mathalani tafiti zinaonesha kuwa kama nchi zetu zitaweza kukusanya vizuri mapato ya kodi, zinaweza kutekeleza nusu ya miradi yake ya maendeleo.

“Lakini ukiachilia mbali mapato ya kodi, tunapoteza fedha nyingi kupitia utoroshaji wa rasilimali zetu, ripoti ya jopo la Umoja wa Afrika lililoongozwa na Rais Mstaafu wa Afrika Kusini Mhe. Thabo Mbeki imeeleza kuwa nchi za Afrika zinapoteza Dola za Marekani Bilioni 150 kila mwaka kutokana na utoroshaji wa rasilimali” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Marais waliohudhuria mkutano huo ni Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Muigai Kenyatta, Rais wa Sudan Kusini Mhe. Salva Kiir Mayardit na Marais wa Rwanda na Burundi wamewakilishwa.

Kesho tarehe 23 Februari, 2018 Mhe. Rais Magufuli atahudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Kampala
22 Februari, 2018

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya February 23

Tanzania, Rwanda Zang’ara Vita ya Rushwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)

$
0
0
Misimamo thabiti ya Rais John Pombe Magufuli katika masuala mbalimbali ya maendeleo ya Taifa imezidi kuleta mafanikio ambapo ripoti mpya katika mapambano dhidi ya rushwa imeonesha Rwanda na Tanzania kuongoza katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika mapambano dhidi ya rushwa kwa mwaka 2017.

Kwa mujibu wa Ripoti ya Tathmini ya Hali ya Rushwa (Corruption Perception Index) iliyotolewa  Februari 21, 2018 na Taasisi ya Transparency International, juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano Tanzania chini ya Dkt. John Pombe Magufuli katika kupambana na rushwa zimezidi kuzaa matunda katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Taarifa hiyo iliyokusanya takwimu za mwaka mzima wa 2017 zinaonesha kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi chache zilizopanda kwa kiasi kikubwa katika kupambana na rushwa huku nyingi  zikishuka au kubaki pale pale.

Wakati mwaka 2016 Tanzania ilikuwa ya 116 duniani, katika ripoti hiyo mpya Tanzania imepanda kwa nafasi 13 na kuwa ya 103 huku ikizizidi kwa mbali nchi kadhaa kubwa duniani katika utafiti huo uliohusisha mataifa 180.

Aidha, kwa eneo la Afrika Mashariki, Tanzania imekuwa nchini ya pili baada ya Rwanda iliyoongoza kwa kupunguza rushwa ambapo katika alama za mtazamo wa rushwa Tanzania imepata 36, alama ambazo ni nyingi kuwahi kufikiwa na nchi katika kipindi cha miaka 10 iliyopita.

Takwimu hizo zinaonesha kuwa Tanzania, kufikia nafasi hiyo ya juu, imeonesha kufanikiwa katika kufanyiakazi mianya mingi ya rushwa, kwa mujibu wa vigezo vya rushwa kupungua katika taasisi mbalimbali za Serikali na kwa mujibu pia wa mtazamo wa wafanyabiashara na wawekezaji.   

Ripoti hii inakuja ikiwa ni hivi karibuni tu Tanzania chini ya juhudi kubwa za Serikali ya Awamu ya Tano ilitajwa na ripoti ya jarida la The Economist kuongoza katika EAC kwa utawala bora na demokrasia (Democracy Index).

Akizungumzia ripoti hii jijini Dar es Salaam jana, Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, alisema ripoti hiyo ni sehemu tu ya kuonesha kuwa vita dhidi ya rushwa na ufisadi nchini inafanikiwa.

“Unaweza kuyapima mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna nyingi katika kupambana na rushwa, ripoti hii kuonesha tumepanda kwa kuzipita nchi 13 katika mwaka mmoja ni moja tu ya ishara kuwa vita yetu hii ya haki ni ya haki kweli na inapaswa kuendelea,” alisema.

Dkt. Abbasi aliongeza,“Kama nchi tutaendelea kutekeleza. Tutaendelea kuhakikisha kile kidogo wanachokichangia wananchi kinatumika kwa maendeleo ya Taifa kama mnavyoona namna tunavyotekeleza miradi mikubwa na ya kihistoria karibu katika kila sekta.”

Hivi karibuni Ripoti nyingine ya Taasisi ya Kiuchumi Duniani (World Economic Forum) iliitaja Tanzania kuwa ya pili Afrika na ya kwanza katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika nyanja za uchumi jumuishi.

Mafanikio yote haya yanakuja wakati ambapo Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais aliyeahidi na anayetekeleza mageuzi, Dkt. John Pombe Magufuli, ikiwa inaendelea kwa kasi kusimamia maendeleo ya Taifa.

Zitto Kabwe akamatwa Morogoro, Polisi watuhumu ziara yake

$
0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amechukuliwa maelezo katika Kituo Kituo cha Polisi cha Mkoa wa Morogoro, baada ya kukamatwa  jana kwa tuhuma za kufanya mikutano kinyume na sheria.

Wakili wa Zitto Emmanuel Lazarus Mvula, amesema Polisi inatuhumu ziara ya ACT ya kutembelea madiwani wa chama hicho katika kata mbalimbali kwenye mikoa nane kwamba ni kosa kisheria.

“Ndugu Zitto ametuhumiwa kufanya Unlawful Assembly S. 74 cap 16 ya sheria ya kanuni ya adhabu, lakini kosa hilo amefunguliwa peke yake tu. Baada ya kuandika maelezo tokea saa 4:42 usiku wa jana mpaka 5:40 usiku, Jeshi la Polisi wamekataa kumpa dhamana kwa maelezo wanasubiri maelekezo kutoka juu,” amesema.

Wakili Mvula ameeleza kuwa, Zitto amewekwa mahabusu katika kituo kikuu cha polisi Morogoro.

“Polisi imekataa kusema kama dhamana ipo wazi ama la, na kama ipo wazi masharti yake ni yapi, na wamekataa kusema iwapo leo watampeleka mahakamani kwa mujibu wa sheria au la,” amesema.  

Mwandishi Mariam Mziwanda wa Gazeti la Uhuru anusurika kifo katika Ajali ya malori na gari ndogo

$
0
0
Mwandishi wa habari wa Gazeti la Uhuru,  Mariam Mziwanda, amejeruhiwa katika ajali iliyohusisha magari matatu, eneo la Tabata TOT jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo baada ya gari dogo alilokuwa akiliendesha lenye namba za usajili T222 DJX kugongana na lori la mizigo lenye namba za usajili T 495 na kisha kuingia katikati na kubanwa na lori la mafuta lenye namba za usajili T 748 BMT.

Kwa mujibu wa dereva wa lori la mafuta lililohusika katika ajali, William Colonel, chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa lori la mzigo ambalo liliacha njia na kupanda  kingo za katikati ya barabara, kisha kupinduka na kuangukia lori la mafuta na gari lililokuwa likiendeshwa na Mziwanda.

Lori la mafuta na gari dogo yote yalikuwa  upande wa kushoto wa barabara. Imeelezwa lori hilo baada ya kuanguka lililibana gari dogo lililokuwa katikati.

Shuhuda wa ajali hiyo, Adeodatus Sylivester Charles "Nilimtambua majeruhi kwani namfahamu tangu akiwa mtoto na sasa ni mwandishi wa habari wa Gazeti la Uhuru" amesema shuhuda Huyo.

Anasema baada ya ajali kutokea alikuta wasamaria wema tayari wanamtoa majeruhi kwenye gari akiwa ameumia sana.

“Nilikuta ametolewa kwenye gari yake akiwa ameumia sana, nikamsaidia kuvitoa vitu vyake kama simu na pochi na kumpelekea maana alikua analalamika simu yangu simu yangu, na watu walikua tayari wameshasogea eneo la ajali wanagombania vitu hivyo.

Madereva wote wa malori walitoka salama bila majeraha ya aina yoyote.
Credit: Mwananchi

Naibu Waziri wa madini akerwa na usiri wa mapato ya mwekezaji

$
0
0
Na Mathias Canal, Mbeya
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko amekerwa na usiri wa mapato na matumizi ya muwekezaji wa mgodi wa uchimbaji madini ya dhahabu wa Sunshine uliopo Wilayani Chunya Mkoani Mbeya.

Mhe Biteko ameonyesha masikitiko makubwa wakati akizungumza na uongozi wa mgodi huo mara baada ya uongozi wa mgodi huo kushindwa kumpatia taarifa ya mapato na matumizi wakati akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani humo kukagua shughuli za uchimbaji Madini.

Kumbukumbu hizo zimekosekana kufuatia viongozi wa ngazi ya juu ya mgodi kutokuwepo kwenye kikao hicho pamoja na kukiri kupokea taarifa ya ujio wake kupitia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chunya.

Alisema kuwa viongozi hao kukosekana pamoja na kuwa na taarifa ya muda mrefu juu ya ziara hiyo ni utovu mkubwa na nidhamu kwa serikali ya awamu tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli.

Alisema kuwa pamoja na kutokuwepo kwao lakini taarifa zilitakiwa kuwepo ofisini kwani ni kosa kisheria kukosekana kwa taarifa za mgodi ilihali sheria ya Madini ya mwaka 2010 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2017 inaeleza vyema kuwa mmiliki wa leseni ya Madini anatakiwa kutunza kumbukumbu za mapato na matumizi kwa miaka mitano.

“Endapo atashindwa kufanya hivyo serikali itamchukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kifungo cha mwaka mmoja jela ama faini ya shilingi Milioni 50 mpaka milioni 150,” alisema Naibu Waziri huyo

Mhe Biteko akizungumza huku akionyesha kukerwa na baadhi ya viongozi ambao walikuwepo katika eneo la ofisi ya mgodi huo huku wakishindwa kuhudhuria katika kikao hicho cha kazi alisisitiza kuwa muwekezaji wa mgodi huo anapaswa kuzingatia na kufuata sheria, taratibu na kanuni za nchi.

Sambamba na hayo pia Mhe Biteko aliutaka uongozi wa mgodi huo kutoa taarifa sahihi za uwepo wa mashapu katika mgodi waliyokuwa wakichimba au kama mashapu katika mgodi huo yameisha wafuate taratibu za kisheria za ufungaji wa mgodi ikiwemo kuyarudisha mazingira katika halo take ya kawaida.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images