Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Picha: Rais Magufuli alivyoondoka kuelekea nchini Uganda

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisindikizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda wakati akielekea kwenye ndege yake tayari kwa safari ya kuelekea nchini Uganda kushiriki Mkutano wa siku mbili wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Kampala

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

TANGA RAHA- Sehemu ya Kumi ( 10 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

 Simu yangu ikaingia meseji na namba iliyoleta meseji hiyo imeandikwa PRIVETE.Taratibu nikaanza kuisoma meseji hiyo
{NIPO NJE NAKUFWATILIA KILA HATUA NA HUYO MALAYA ZENA ULIYE NAYE NDANI KWAKO NITAMUUA UKISHUHUDIA}
Nikatamani ardhi ipasuke nidumbukie.Nikazidi kuchanganyikiwa pale Madam Zena aliponiaga anataka kuondoka ili akawahi kipindi chake cha kufundisha baada ya mapumziko ya saa nne asubuhi

ENDELEA
 “Madam ninakuomba usiondoka please”
“Kwa nini Eddy wakati nimesha kuleta hadi nyumbani?”
“Na penda tu leo unipe  kampan yako ya kukaa hapa kwangu nakuomba”

Madam Zena akajifikiria kwa sekunde kadhaa kisha akatoa simu yake na kupiga kwa mtu ila sikujua ni nani
“Sir Barongo”

“Nakuomba unishikie vipindi vyangu kaka yangu kama huto jali kidogo nimepata dharura”
“Nashukuru kaka yangu haya Mungu akipenda kesho”
Madam Zena akakata simu kisha akairudisha kwenye begi lake na kuniangalia huku aikitabasamu
“Sasaa hapa ninaweza kukaa kwa amani….Ehee mgonjwa una CD gani nzuri nzuri za movie”
“Kwa CD tu hapa utakesha”
Madam Zena akachukua makasha ya CD yaliyopo chini ya meza ya kioo na kuanza kuangalia kasha moja hadi jengine hadi akakuta kasha lililoandikwa PIRATE ON BLACK SEE akaitoa CD yake na kuiweka ndani ya deki kisha akarudi kwenye sofa na kukaa.Madam Zena akaanza kuguna baada ya CD hiyo kuanza kwani imeshamiri mambo ya kikubwa yanayo onyeshwa live bila chenga
“Sir Eddy hivi hizi CD unazitolea wapi?”
“Kwa nini?”
“Huwa ninazitafuta ila sizipati”
“Kuna maeneo ya pale forozi karibu na benki ya NMB kuna jamaa best yangu anaziuza”
“Bei gani?”
“Elfu tatu”
“Basi kuna vijana walinipitishia wakaniuzia kwa elfu ishirini”
“Dooo wamekutapeli hao”

“Tena wamenitapeli sana kwani CD lenyewe lina scratch kama nini”
“Basi nitakutafutia”
Madam Zena akaendelea kutazama CD huku akionekana kunogewa kwa jinsi watekaji wa meli katika CD hiyo wakipeana mambo matamu,Nikatazama Wallet yangu na kukuta  nina pesa ya kutosha.
“Zena ngoja nikanunue chakula cha mchana”
“Haupiki?”
“Sijisikii kupika”
“Lakini mimi si nipo ninaweza kupika”
“Utapika siku nyingine ila nakuomba kama mtu yoyote akigonga usimfungulie hadi usikie sauti yangu”
“Sawa ila ni kwanini?”
“Watu wa mtaa huu ni wasumbufu sana na wamesha anza kunizoea vibaya”
“Sawa au unaogopa vimanzi vyako vitakuja?”
“Sina manzi wala nini wewe fanya kama nilivyo kuambia……………Nikuletee kinywaji gani?”
“Kwanza unakwenda kununua nini….”
“Alafu sikukuuliza nikuchukulie chakula gani?”
“Mimi niletee chipsi yai na kuku nusu nikipata na castel mbili baridi utakuwa umeifanya siku yangu ikawa powaaa”
“Powa nitafanya hivyo ila na wewe fanya kama nilivyo kuagiza usije ukafungua mlango”

“Sawa Eddy nimekuelewa”  
Nikatoka chumbani kwangu na Madam Zena akaufunga mlango wangu kwa ndani lengo langu ni yeye kuweza kuwa katika hali ya usalama kwani kuna watu wameanza kunipa vitisho kwa njia ya meseji.Nikamsalimia bibi kizee mwenye umri kwa makadirio yangu unao fika miaka 70 hivi.Aliyekaa nje ya nyumba ya jirani na ninapo ishi
“Marahaba mjukuu wangu.Hujambo baba”
“Sijambo haya mimi ninapita”
“Sawa…..ila kijana nakuomba mara moja”
Nikamsogelea sehemu aliyokaa na akanionyesha sehemu ya kukaa huku macho yangu yakilichunguza eneo la hapo kwani mtu aliye nitumia meseji alidai yupo maeneo haya huku akijua nipo na nani ndani kwangu
“Kijana unaitwa nani?”
“Ninaitwa Eddy”
“Ahaaa Eddy mjukuu wangu inavyoonekana wewe ni mgeni hapa Tanga?”
‘Ndio”

OFA: Jipatie Riwaya Kali ya Kusisimua ya PRESIDENT WIFE toka kwa Mtunzi makini

$
0
0
OFA OFA OFA OFA
Mara baada ya hadithi ya SORRY MADAM Destination of my enemies kuisha. Je unahitaji kufahamu maisha ya EDDY na RAHAB mara baada ya kumng'oa dikteka MZEE GODWIN, Pata muendelezo wa kisa hicho katika kitabu cha PRESIDENT WIFE. ili uweze kusoma mwisho wa maisha ya EDDY katika mlolongo mzima wa simulizi hizo.

Hadithi ya President wife uta ipata kwa bei ya shilingi 6000 tu kupitia Whatsapp namba 0657072588 au 0768516188. Wanao tumia email, wasiliana nami kwa email eddazariaM@gmail.com
Watumiaji wa facebook book wasiliana nami kwenye akaunti ya @storyzaeddy-tz

Pia nina wakaribisha watumiaji wote wa whatsapp kujiunga na group la hadithi ya TANGA RAHA SEASON TWO. Ada ya mwenzi mzima ni sh 4000. Ukijiunga leo, utapata ofa ya episode 60 Bureeee kabisa. Namba ya kujiunga whatsapp ni 0657072588.

Karibuni sana
By Eddy Msulwa

Kipindupindu chaua 18 Dodoma

$
0
0
Watu 18 wamepoteza maisha kutokana na ugonjwa wa kipindupindu mkoani Dodoma ndani ya miezi minne huku zaidi ya watu 470 wakiugua ndani ya muda huo.

Mganga Mkuu wa Mkoa huo, Dk. James Kiologwe, alisema jana kuwa ugonjwa huo tangu uingie Dodoma Oktoba, mwaka jana, hadi sasa umesababisha vifo hivyo na idadi hiyo ya wagonjwa.

Alisema wagonjwa wengi wanatoka katika  wilaya za Mpwapwa na Chamwino na miongoni mwa sababu za kuenea kwa ugonjwa huo ni unywaji wa maji ya kwenye madimbwi ambayo si safi na salama.

Mganga mkuu huyo alisema ugonjwa huo ulianza  Oktoba, mwaka jana, katika wilaya zote za mkoa wa Dodoma lakini zaidi katika wilaya hizo mbili.

“Kuna wakati ulipungua, lakini umerudi tena na umekuja sana kwa kasi mwezi huu wa pili,” alisema.

Aidha, Dk. Kiologwe alisema hadi juzi kulikuwa na wagonjwa wapya 26 na 22 kati yao  waliruhusiwa kurudi nyumbani na wanatoka Mpwapwa na Chamwino.

Kuhusu hatua zilizochukuliwa, Dk. Kiologwe alisema jitihada zinaendelea kukabiliana na ugonjwa huo kwa kugawa ‘Water Guard’ vidogo 250,000 kwa ajili ya  kusafisha maji na kuweka  katika vyanzo vya maji.

Aliwataka wakazi wa mkoa huo kuhakikisha wanachemsha maji ya kunywa na kuzingatia kanuni zote za usafi, ili kuepukana na ugonjwa huo.

Wanachama 400 wa CHADEMA Wahamia CCM

$
0
0
Wanachama 400 na aliyekuwa Diwani wa Kata ya Bagara na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ngarenaro Mjini Babati mkoani Manyara, Nicodemus Tlaghasi (Chadema) aliyejiuzulu hivi karibuni wamekabidhiwa kadi za CCM.

Katibu wa Uenezi, Siasa, Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga alikabidhi kadi ya CCM kwa wanachama hao wapya na diwani huyo aliyejiuzulu jana mjini Babati.

Akizungumza wakati wa kuwakabidhi kadi hizo mpya, Lubinga amewataka wanachama hao 400 na Tlaghasi, kuwa waaminifu kwenye chama hicho.

Amesema CCM ya hivi sasa inaendana na kasi kulingana na dunia ilivyo, hivyo wajiandae kwenda mwendo kasi ili kufikia maendeleo chanya.

Amesema inapotajwa CCM mpya na Tanzania mpya maana yake ni kuwa Watanzania wa sasa mahitaji yao si ya juzi na jana hivyo viongozi waliopatiwa dhamana ya kuongoza inawabidi watimize wajibu wao ipasavyo.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa kadi ya CCM, Tlaghasi amesema amechoka kuishi maisha ya wasiwasi yasiyo na amani, ambayo alikuwa anayaishi wakati akiwa kiongozi wa jamii kupitia Chadema.

Amesema alikuwa anaishi maisha ya kuvizia ili asionekane na viongozi wa Chadema pindi akitaka kutimiziwa mahitaji ya jamii kwenye Serikali kwani alikuwa anaonekana kama msaliti.

"Ili kuonana na kiongozi wa serikali ilinipasa kuvizia, lengo likiwa nitimize mahitaji ya wapiga kura wangu, nikajiuliza nateseka hivi kwa ajili ya nini?" Alihoji Tlaghasi.

Amesema dhamira yake ikamtuma kuachana na Chadema na kujiunga na CCM ili aungane na Rais John Magufuli na mkuu wa mkoa huo Alexander Mnyeti katika kuwatumikia wananchi.

UPDATES: Rais Magufuli awasili SALAMA Nchini Uganda

$
0
0
Rais John Magufuli leo amewasili nchini Uganda, kuhudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, unaofanyika  mjini Kampala.

Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Entebbe, Rais Magufuli amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda, Sam Kutesa na kisha kuelekea Ikulu ya Entebbe.

Baada ya kuwasili Ikulu amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Uganda  Yoweri  Museveni.

Pia kesho atahudhuria mkutano maalum katika ngazi ya wakuu wa nchi unaohusu masuala ya miundombinu na afya na keshokutwa atahudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 01 na 02)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
Kaubaridi kakali ka asubuhi kananifanya niwe ninabingirika bingirika, kwenye kitanda changu cha sita kwa sita. Sitamani kabisa kunyanyuka kwenye kitanda changu hichi, hii ni kutokana na uchovu unao sababishwa na pirika pirika zangu za siku tano za wiki, na hizi siku mbili za mapumziko muda mwingi ninazitumia kushinda chumbani kwangu. Kiupepo cha feni kinacho nipiga kwa mwendo wa taratibu, kinazidi kuongezeka zaidi na kiupepo cha mvua  inayo nyesha huko nje. Taratibu ninaanza kulipapasa shuka langu sehemu lilipo na kujifunika vizuri mwilini mwangu.

Kabla hata sijaumalizia malizia usingizi wangu vizuri nikashtuliwa na umlio wa mesiji unao ingia kwenye simu yangu, taratibu ninaichukua simu kutoka chini ya mto nilipo iweka na kujilaza chali kisha ninaufungua ujumbe huo unao nifanya nikae kitako kitandani.

(Dany hela ya umeme)      
Nikaurudia kuusoma tena ujumbe huo wa meseji ulio nifanya nipatwe na gadhabu sana, kwani haujaisha hata mwezi mama mwenye nyumba ananitumia meseji hiyo juu ya umeme wa luku tunao changa wapangaji karibia sita tuliopo kwenye hii nyumba ya mama wa kinyaturu. Nikashuka kitandani nikavaa pensi yangu pasipo kuvaa boksa ndani, kisha nikachukua na kaushi yangu na kuivaa haraka haraka na kutoka ndani ya chumba changu huku sura yangu ikiwa imejikunja kwa hasira kali.

Nikatembea kwenye kordo ndefu yenye vyumba vinne kila upande huku chumba viwili vya upande ninao kaa mimi ni vya mama mwenye nyumba anaye ishi na binti wake wa kike. Breki yangu ya kwanza nikasimama nje ya chumba cha mama mwenye nyumba na kugonga mlango wake kwa mara mbili kisha nikasimama kusikilizia majibu. Nilipo ona kimya nikataka kugonga kwa mara ya tatu, ila mama mwenye nyumba akawa tayari ameufungua mlango wa chumba chake akioneona ndio kwanza na yeye ananyanyuka kutoka kitandani, kwani amejifunga na tenge moja tu na macho yake yamejaa malepe ya usingizi.
“Mama nimeipata meseji yako, ila mbona mimi nilisha lipa hela ya umeme?”

“Ulimpa nani hiyo pesa?”
Mama mwenye nyumba anaye julikana kwa jina la mama Mariam, alinijibu huku mkono wake mmoja akishika kingo za mlango kwa upande wa juu.
“Nilimpa Mariam elfu kumi na tano mwanzo wa mwezi”
“Mbona hajanipa sasa?”
“Labda umuulize mwanao ila mimi nilisha toa hiyo pesa”
Mama mwenye nyumba akanikazia macho jinsi ninavyo zungumza kwa kujiamini.
“Sawa, ila usipanic kama umelipa nitamuuliza Mariam”
“Ni lazima nipanic mama, wewe mwenye si unafahamu jinsi hali ya uchumi ilivyo mbaya kwa sasa”
“Ok nisamehe baba yangu”
“Sawa”
Nikaondoka na kurudi chumbani kwangu huku mara kadhaa nikiwa niaachia misu

onyo ya hapa na pale. Usingizi wote nilio kuwa nao ukakata kabisa. Nikatupa kwenye sofa na kutafuta zilipo rimoti zangu za tv pamoja na rimoti za king’amuzi changu cha DST’v. Nikawasha na kuanza kutafuta ni chaneli gani ambayo inaweza kunifaa kwa kuangalia alfajiri hii. Sikuona chaneli inayo nifaa, ikanibidi nisimame na kufungua droo ya dresing table yangu na kutoa CD moja ya ngono iliyo andikwa BIGG BLACK ASS, nikaiweka kwenye deki yangu na kurudi kukaa kwenye sofa langu, nikisubiria kuangalia mkanda huo ambao mara nyingi ninapenda kuutazama kwani unaziamsha hisia zangu za mapenzi.
Mkanda huo ukaanza, ukionyesha wadada wa kimarekani wakitingisha makalio yao makubwa, na kunifanya nijikunje nne kidogo kwani jogoo wangu amesha anza kuwika. Jinsi wadada hao wanavyo zidi kutingisha makalio yao waliyo yapaka mafuta malaini yanayo ng’aa sana, ndivyo nami nilivyo zidi kuanza kupata msukumo wa kuanza kumshika jogoo wangu taratibu na kumtoa kwenye pensi yangu.

Taratibu nikaanza kumsugua sugua jogoo wangu ambaye tayari alisha simama muda mrefu alipo yaona makalio ya wadada hao, na kwa jinsi kaubaridi ka mvua kanavyo ingia dirishani na ukichanganya na kaubariki ka upepo wa feni, basi hisia za kumsugua jogoo wangu zikazidi kunipanda. Nikatema mate kidogo kwenye kiganja cha mkono wangu wa kushoto na kuendela kumpaka jogoo wangu taratibu. Nikiwa katikati ya utamu, mlango wangu ukagongwa na kunifanya niutazame kwa macho ya hasira.
“Dany”
Nikasikia sauti ya mama mwenye nyumba ikiniita, kwa haraka nikamrudisha jogoo wangu ndani ya pensi huku akiwa bado amesimama, kwa kiwewe nikasahau hata kuisimamisha filamu yangu. Nikajifuta kiganja changu kwa taulo na kuufungua mlango. Nikamkuta mama mwenye nyumba akiwa amesimama, akanitazama kuanzia usoni hadi chini pasipo kuzungumza kitu cha aina yoyote.

“Mama zungumza?”
Kwa upenyo wa pazia mama mwenye nyumba nikaona akiyatupia macho yake kwenye Tv yangu aina ya Samsung inch 42, akitizama mikiki mikiki inayo onekana kwenye mkanda hao.
“Mama”
“Ehee…”
Mama mwenye nyumba akastuka, akionekana ametoka kwenye dibwi kubwa alilo zama baada ya kutazama filamu hiyo.
“Nataka niangalie vitu unavyo tumia umeme, kwa maana inaonyesha ukiwepo wewe luku inakwenda haraka kama nini”
Mama mwenye nyumba alizungumza huku akitaka kuingia ndani kwangu, ila ikanibidi kumzuia kwanza kwa maana sikujua utaratibu huo umeanza lini ndani ya nyumba hii.
“Tueleweshane kwanza mama huwezi kuingia ndani kwangu tu, kisa wewe ni mama mwneye nyumba niambie utaratibu wa kuchunguza vitu vya watu umeanza lini?”

“Wenzako nilisha wachunguza wewe tu ndio ulikuwa umebaki, nipishe nikatazame”
“Mama”
Mama mweney nyumba akanisukuma mkono wangu nilio kuwa nimumzuia nao, akaingia ndani kwangu, kitua cha kwanza akasimama na macho yake yote kuyatupia kwenye Tv yangu. Nikamtazama jinsi alivyo duwaa, hapo ndipo nilipo pata nafasi ya kumtazama mama mwenye nyumba kwa nyuma. Ni mwanamke mwenye umbo lililo jazia vizuri na kubarikiwa kupewa kalio kubwa na lenye ujazo wa kuelekeka. Kiuno chake chembamba kama nyigu chenye tumbo kubwa kiasi, kiliweza kugawanyisha kati ya kiwili wili cha juu cha mama huyo na kiwiliwili cha chini chenye miguu minene kiasi.

 “Mama kagua basi na utoke”
Mama mwneye nyumba akawa kama hajanisikia kwani ukimya wake wote niliamini umepumbazwa na wamarekani hao wanao ngonoka kama mashine.
“Mmmm hawa watu jamani, tazama yule anavyo mzamisha mwenzake mb** mku**i hamuonei hata huruma”
Mama mwenye nyumba alijikuta akizungumza huku akinitazama kwa macho ya kuiba iba. Sikumjibu chochote zaidi ya kurudi mlangoni na kuufunga ili hata mtu akipita kwenye kordo hiyo asijue ni nini kinacho endelea ndani ya chumba changu na mama mwenye nyumba.

Mama mwenye nyumba alipo ona nimeufunga mlango, taratibu akaka kwenye kochi, na kuangalia mkanda huo, jambo lililo zidi kuniacha njia panda kwa jinsi mwana mama huyu alivyo na maneno ya kejeli kwa sisi wapangaji wake sikudhani kama anaweza kutazama filamu hizi.
“Njoo tu ukae hapa”
“Hapana hapa kitandani kunanitosha”
Niaamjibu mama mwenye nyumba huku nikiwa nimeketi kitandani, mara kadhaa nikawa ninamtupia jicho na kumuona jinsi anavyo pata pata shida ya kujigeuza geuza kwenye sofa, mara akae hivi, mara akae vile, ilimraidi tu azidi kuitazama filamu hiyo.
“Dany”
Mama mwenye nyumba akaniita kwa sauti ya upole na unyonge, nikamuitikia kwa sauti nzito hadi akanigeukia na kunitazama.
“Mbona sauti nzito hivyo”
“Hapana”


“Ni kosa polisi kujichunguza kwa Matukio yanayowahusu”......Hili ni Tamko la Asasi za Kiraia Kuhusu Hali ya Usalama Nchini

$
0
0
WITO WA ASASI ZA KIRAIA KUHUSU HALI YA USALAMA WA RAIA, HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA WA SHERIA NCHINI

UTANGULIZI
Sisi Asasi za Kiraia tulioweka sahihi katika Waraka huu, kwa umoja wetu tumesikitishwa sana na vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu, utawala wa sheria na usalama wa raia vinavyoendelea hivi sasa hapa nchini. Asasi za Kiraia (Civil Society Organizations) ni taasisi huru zilizoundwa kwa mujibu wa sheria mbalimbali nchini. Taasisi hizi zinatekeleza majukumu mbali mbali hapa nchini katika kuhakikisha ustawi wa taifa letu.

Hivyo tunawaomba viongozi na watanzania kwa ujumla kutambua juhudi zinazofanywa na asasi za kiraia katika kutetea maslahi ya umma, kuleta maendeleo na mabadiliko mengine katika jamii. Katika nchi mbali mbali zilizoendelea, mchango wa asasi za kiraia umesaidia kuleta mabadiliko makubwa ya kimfumo na kimaendeleo na hivyo nchi/mataifa husika kuona umuhimu wa kuheshimu AZAKI na kuweka ushirikiano mzuri wa serikali na asasi za kiraia. 

Pamoja na changamoto changamoto mbalimbali , AZAKI pia zimetambua na kumpongeza Rais wa Jamhuri wa Tanzania kwa kuonyesha juhudi katika kupamnbana na matumizi mabaya ya rasilimai za umma, kuleta nidhamu katika taasisi za umma na usimamizi mzuri wa mali asili za Watanzania. 

AZAKI zitambua kabisa umuhimu wa maendeleo ya kitaifa katika kulinda na kuheshimu haki za binadamu kwa kuwa vitu vyote hivi huenda pamoja na hutegemeana. Kwa maana hiyo tuko bega kwa bega na Rais wetu katika kuhakikisha Tanzania inapata maendeleo makubwa, kwa kuwa maendeleo hayo ndiyo msingi wa haki za binadamu na maisha bora kwa Mtanzania.

TATHMINI YA HALI YA HAKI ZA BINADAMU, UTAWALA WA SHERIA NA USALAMA
Katika utendaji kazi wa asasi za kiraia, huwa zinapata muda wa kukaa na kufanya tathmini ya hali ya mambo mbali mbali ya kitaifa na kuangalia ni namna gani wao kama wadau na washiriki wa kuleta maendeleo na kuhakikisha mustakabali bora wa taifa unalindwa na kutetewa wakati wote. 

Mnamo tarehe 19/02/2017 Jukwaa la Wakurugenzi wa AZAKI (Tanzania CSOs Director’s Forum-CDF) Ililikaa kikao ili kufanya tathmini ya masuala mbalimbali yenye maslahi na mustakabali mzima wa taifa hili na kubaini masuala kadhaa ya ukiukwaji wa haki za binadamu, hali ya taharuki juu ya amani ya nchi, uhuru wa kujieleza, uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa AZAKI, maamuzi yasiyozingatia sheria na taratibu, kuminywa kwa demokrasia ya taifa letu pamoja na chaguzi zisizo na usawa na zenye viashiria za umwagaji damuna kuhatarisha amani ya nchi.
 
Hali hii imetokana na matukio mbali mbali ambayo tumeyashuhudia na kwa kuzingatia historia ya nchi yetu hatukuwahi kuyashuhudia wala kudhani kwamba yangeweza kutokea. Matukio haya yamehusishakuvamiwa (mashambulizi), kuuawawa, kuumizwa, kupotea na kuteswa kwa watetezi wa haki za binadamu, wanahabari, wanasiasa na hata raia wa kawaida. Baadhi ya matukio hayo ni haya yafuatayo;

(i) Mauaji ya Mwanafunzi wa Chuo -Akwlina Baftah
Mnamo tarehe 16/02/2018 taarifa zilisambaa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii juu ya kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Akwilina Baftah ambaye anasadikiwa kuuwawa kikatili akiwa katika daladala na askari polisi waliokuwa wakiwatawanya wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao walikuwa wanakwenda kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoniambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kwa ajili ya kudai fomu za mawakala wa uchaguzi. 

Jeshi la Polisi kupitia kwa Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa, lilithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kukiri kwamba tukio hilo limetokea wakati polisi wakiwa wanafyatua risasi angani kuweza kuwatawanya wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
 
Tukio hili limezua taharuki kubwa kwa taifa na jamii ya kimataifa kwani ni moja kati ya matukio mabaya yanayoendelea kutokea katika Taifa letu. Tukio la kuuwawa kwa mwanafunzi huyu limeleta simanzi kubwa sana kwa taifa kwakuwa limetokea kwa mtu asiyekuwa na hatia yoyote ile. 

Ni moja ya tukio ambalo limewaleta watanzania pamoja bila kujali dini zao, mirengo yao ya kisiasa, vyeo vyao, makabila yao au hali zao. 

Tukio hili limewakumbusha watanzania wengi kwamba kumbe ile amani iliyokuwa ikihubiriwa katika taifa hili inaweza potea ndani ya dakika chache bila kutarajia kama tusipoamka wote kudai Taifa kurudi katika misingi ya demokrasia, usawa, utawala wa sharia na haki za binadamu.

Wana AZAKI tunawashukuru wote wanaoendelea kuifariji familia hiyo hasa Waziri wa Elimu Bi-Joyce Ndalichako alieonyesha ukaribu wa kusimamia msiba huu kama waziri mwenye dhamana ya elimu nchini, lakini pia ushiriki wa Serikali katika kusaidia mazishi ya mwanafunzi huyo. 

Tunaipongeza Serikali kwa kuonyesha kujali na kuwafariji familia ya marehemu kutokana na msaada huo. Sisi kama wana Azaki tunaamini Serikali na wananchi wameguswa sana na msiba huo.
 
(ii) Vitendo vya kutekwa, kuuwa, kuumizwa na kupotea kwa watu mbalimbali
• Matukio ya kutekwa na kuuwa kwa viongozi mbalimbali hapa nchini yalishika kasi pale viongozi wa CCM, askari zaidi ya 10 na wananchi karibu 40 katika eneo la Kibiti walivyoanza kushambuliwa na kuuwawa bila wahusika kukamatwa. Matukio haya yameendelea hadi kwenye vipindi vya uchaguzi ambapo mnamo tarehe 11/02/2018 Kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ndugu Daniel John alitekwa na kishaaliuwawa kikatili wakati wa Kampeni za Uchaguzi mdogo wa jimbo la Kinondoni. Matukio haya ni mengi na yamekuwa yakijirudia kote hadi visiwani Zanzibar.
 
• Tarehe 7/09/2017 Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika na Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu alivamiwa na kupigwa risasi hadharani na watu wasiojulikana katika eneo la area D Mkoani Dodoma ambapo mpaka sasa watu hao hawajaweza kubainika na.
 
• Tarehe 21/11/2017 Mwandishi wa habari wa Mwananchi Communications Limited ndugu Azory Gwanda alipotea katika mazingira ya kutatanisha ambapo mpaka sasa hajapatikana licha ya wana AZAKi na waandishi wa habari kupaza sauti zao juu ya kupotea kwake.
 
• Msaidizi wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Ben Saanane alipotea katika mazingira ya kutatanisha na taarifa za wapi alipo mpaka hazijawahi kutolewa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama wala kuwabaini waliohusika na tukio hilo.
 
• Matukio ya utekaji na uteswaji wa watu yamekithiri katika nchi yetu ambapo hivi karibuni tumeshuhudia matukio kadhaa ya kutekwa na kuteswa kwa wasanii, wanahabari ambao wanaonekana kutoa maoni mbadala juu ya masuala mbali mbali yanayoendelea katika nchi yetu.

(iii) Matumizi ya Sheria Kandamizi na Ukamataji Usiozingatia sheria
• Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 18 inatoa uhuru wa maoni kwa kila Mtanzania ata hivyo kumekuwa na sheria mbali mbali kama vile Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016, Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, Sheria ya Tawala za Mikoa ya mwaka 1997, Sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 pamoja na sheria zingine ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa zikiminya uhuru wa maoni kwa makundi mbali mbali pamoja na watanzania kwa ujumla.
 
• Tumeshuhudia katika kipindi kifupi cha utekelezwaji wa sheria kandamizi, magazeti mengi yamefungiwa, wanahabari wamevamia, kutekwa na kunyanyaswa, watu kufunguliwa mashtaka ya kughushi, kuvamiwa ofisi za mawakili, vyombo vya habari kupigwa faini kwa kurusha taarifa ambazo pengine zinaonyesha kasoro za uongozi. Hali hii imezua taharuki kubwa kwa tasnia ya habari ambapo sasa wanahabari wanafanya kazi katika mazingira magumu sana na ambayo sio salama hivyo kusababisha kuogopa kutoa taarifa juu ya uvunjifu wa haki za binadamu na mwenendo wa demokrasia nchini.
 
• Vyombo vya habari vimepigwa marufuku kutoa taarifa za uchaguzi, haza zile zinazonyesha kasoro katika uchaguzi, wengi tumesikitishwa na kitendo cha ITV kutakiwa kuomba radhi kwa taarifa ya kweli waliyorusha wakati wa upigaji kura kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kinondoni kwa kuonyesha tukio la wizi wa sanduku la kura wakati uchaguzi ukiendelea.
 
• Utawala wa sheria, Demokrasia na haki za kisiasa vimekuwa havisimamiwi vizuri na vyombo husika. Kwa mfano, Jeshi la Polisi nchini limekuwa likishindwa kutokuwa na upande katika mambo yanayowahusu raia na serikali au vyama vya siasa na hivyo kusababisha madhara na maafa kwa wananchi mbali mbali wa taifa hili.Vyombo hivi vya usalama vinalalamikiwa na wananchi kwa kutokufanya kazi zao kwa weledi, uhuru na usawa na kuonekana kama vinaingiliwa na kufanya kazi kwa maagizo mengi toka nje ya mifumo yao na kuondoa dhana ya kuwa vyombo kwa ajili ya ulinzi wa raia na mali zao.
 
• Tume ya taifa ya Uchaguzi nchini imejionyesha wazi kuwa siyo chombo huru kinachofaa kusimamia au kuwa msimamizi wa chaguzi za mfumo wa vyama vingi kutokana na muundo wake au wasimamizi wanaoteuliwa kuwa na uhusiano na vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi. Hili limeonekana dhahiri kwamba kuna mambo ambayo tume imeshindwa kuyasimamia wakati wa uchaguzi uliopita na hivyo kusababisha kutokea kwa vurugu na vifo/athari mbali mbali kwa viongozi wa vyama vya siasa na wananchi kwa ujumla. Kwa mfano, tukio la juzi la kuuwawa kwa mwanafunzi Akwilina Baftah ni matokeo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzina Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni kushindwa kusimamia vizuri zoezi la uchaguzi. 

Taarifa zaidi kuhusu uangalizi wa uchaguzi huo zitaletwa baadaye na muungano wa AZAKI zilizoshirikikufanya uangalizi wa uchaguzi baada ya taarifa hizo kukaguliwa kwanza na Tume kwa Mujibu wa taratibu mpya. Hili nalo ni jambo geni kabisa katika taratibu za uangalizi wa uchaguzi ambapo waangalizi walikuwa huru kutoa taarifa zao za uangalizi bila ya kusubiri taarifa hizo kuhakikiwa na TUME.
 
(iv) Hali ya Watetezi wa Haki za Binadamu na AZAKI
• Watetezi wa Haki za binadamu wameendelea kufanya kazi katika mazingira ambayo sio rafiki na hatarishi huku wengi wao wakifunguliwa kesi, kushambuliwa, kukamatwa na vyombo vya Dola ikiwemo kupewa majina mabaya na hata kuzushiwa kuwa baadhi yao sio raia wa Tanzania.
 
• Makundi mbali mbali na Asasi za kiraia zimeendelea kufanya kazi katika mazingira ambayo sio rafiki huku uhuru wao wa kufanya kazi na kujieleza ukiwa umeminywa kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria zinazoanzisha na/ama kulinda maslahi ya asasi za kiraia.
 
• Tumeshuhudia asasi za kiraia zikitishiwa kufungiwa huku zikiwa zinatekeleza majukumu yao kisheria. Nafasi ya asasi za kiraia imedhoofika kutokana na kauli mbali mbali za viongozi wa serikali pamoja na hatua zinazochukuliwa na serikali hivyo kufanya Asasi za kiraia kushindwa kutimiza majukumu yake kwa ufasaha na kwa wakati katika maeneo mablimbali ya nchi.
 
• Mfano AZAKI nyingi sasa zimekwama kutoa matangazo kwa vyombo vya habari kutokana na kutakiwa kupata kibali kwanza toka TAMISEMI baada ya kuyawasilisha matangazo hayo kwa viongozi kwa ukaguzi. Matangazo kama yale yaliyokuwa yakitolewa na HAKIELIMU kwa utaratibu wa sasa ni lazima kukaguliwa na kupata kibali ndipo chombo cha habari kiweze kuyatoa kwa umma.
 
• AZAKI zinazokwenda Mikoani kufanya kazi zinakumbana na upinzanimkubwa kutokana na maagizo ya kutaka kupata kibali toka Makao Makuu ya TAMISEMI kabla ya kwenda Mikoani
 
• Pia AZAKI zinashindwa kutoa taarifa zauangalizi wa uchaguzi kutokana na kutakiwa kupeleka kwanza taarifa hizo kwa Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi kuzikagua ili kuangalia yaliyomo na kuiridhiwa IKIWAPENDEZA. Changamoto hii imeendana na changamoto ya kupata kibali kwa AZAKI kama waangalizi wa uchaguzi. Mfano yapo Mashirika mengine yalikwenda Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuomba kuwa waangalizi lakini walijibiwa kuwa kuna mashirika mengi yameeomba kufanya uangalizi hivyo nafasi zimejaa.
 
SISI Wana AZAKI tumeona tutumize majukumu yetu kwa kutafuta namna ambayo tunaweza kuijadili kwa pamoja jinsi ya kurekebisha changamoto hizi na kusonga mbele. Tusipofanya hivyo, taifa hili linaweza kuingia katika migogoro ambayo huzaa chuki na hatimaye kupoteza Amani yetu. Kwani kwa sasa kumekuwa na kauli zinazoashiria ubaguzi wa itikadi za kisiasa na kimaendeleo.

WITO WA AZAKI KWA SERIKALI NA TASISI HUSIKA
1. Serikali itazame upya suala la upatikanaji wa Katiba mpya kwani ndiyo suluhisho la matatizo mbali mbali yanayotokea katika jamii kwa sasa, kwani suala la katiba mpya kimekuwa ni kilio kikubwa na hitajio la watanzania wengi ili kutibu hali hii inayojitokeza sasa.Tunashauri Mchakato wa Katiba mpya ufanyike mwaka huu kwa kuwa mawaka 2019 na 2020 Taifa litakuwa bize na mambo ya uchaguzi. Tunamshauri Mhe Rais aitishe kikao cha wadau wote kujadili namna ya kuliweka hili suala kwa maslahi ya Taifa.
 
2. Tunaomba Tume Huru ya Uchaguzi ipatikane kabla ya chaguzi za 2019 na 2020, itakayoweza kusimamia usawa na haki kwa vyama vyote kuepusha madhara ambayo yanaweza kujitokeza kutokana na Tume kushindwa kusimamia misingi ya haki na usawa katika uchaguzi.Tume ya uchaguzi ifungue ofisi zake wilayani na kuajiri wataalam wake kuwa wasimamizi wa uchaguzi na kuachana na mfumo wa sasa unaonekana kuwa na mgonano wa kimaslahi. AZAKI tupo tayari kushirikiana na Serikali na wadau wengine wa maendeleo katika kulifanikisha hili.
 
3. Tunapendekeza iundwe Tume huru ya uchunguzi itakayohusisha AZAKI, Taasisi za Dini, Vyombo vya Habari, Baraza la Vyama vya Siasa, Wanahabari, Majaji/Mahakimu, Polisi, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora kufanya uchunguzi huru juu ya vifo na vitendo vya utekwaji na utesaji vilivyojitokeza wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Kinondoni. Matukio yanayowahusu Polisi kama watuhumiwa ni kosa kubwa kuwaachia wao wenyewe wajichunguze na hili limekuwa sasa chanzo cha matukio kuendelea kutokea na kutochukuliwa hatua.
 
4. Vyombo vya utoaji haki kama Polisi na Mahakama vifanyiwe maboresho na viachweviwe huru katika kutekeleza majukumu yake ili kuepusha wasiwasi na dhana ambayo imeanza kuonekana dhahiri kwamba vyombo vyetu vya utoaji haki haviko huru. Au kuthibitisha ile zana ambayo imeanza kuzoeleka kuwa kuna Mhimili mmoja umejichimbia kwenda chini kuliko mihimili mingine.
 
5. Tunalisihi na kulishauri Jeshi la polisi kutimiza wajibu wake kwa kufanya kazi kwa weledi, taaluma na sheria za nchi pamoja na kuacha kuegemea upande mmoja ili kuepusha lawama chuki na uhasama ambao unajengeka kwa wananchi kwa Jeshi hilo.
 
6. Jeshi la polisi liwe makini katika kutimiza wajibu wake wakati wa kuzuia maandamano, kwani kauli ambazo zimekuwa zikitolewa na viongozi wa Jeshi la Polisi na matumizi ya silaha za moto huonyesha wazi kwamba Polisi inashindwa kutumia njia zilizoanishwa kisheria kukabiliana na waandamanaji wasio na silaha na wasiofanya vurugu. Pia Jeshi la lifanye kazi kwa ushirikiano na wananchi pamoja na Asasi za kiraia na kwa namna yoyote kuepuka kutumia nguvu kubwa ili kuboresha dhana ya ulinzi shirikishi.
 
7. Askari wanaotuhumiwa kuhusika kusababisha kifo cha Mwanafunzi Akwilina wafikishwe katika vyombo vya sheria ili hatua stahiki zichukuliwe kwa aliyehusika na tukio hilo. Taifa liwe na mfumo huru au chombo huru (Oversite body) ya kuchunguza na kusimamia mashtaka yanayohusu vyombo vya usalama badala ya kuwaachia wao kufanya uchunguzi na kuendesha mashtaka.
 
8. Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni ambaye ndiye Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kinondoni ajipime mwenyewe kwa vitendo vyake alivyofanya katika uchaguzi huu kuhusu kuvuruga taratibu za uchaguzi na kuwanyima mawakala wa vyama vingine haki ya kusimamia uchaguzi pamoja na kusababisha uvunjifu wa amani ajipime kama anatsahili kuendelea katika nafasi hizo tena. Viongozi wengine wahusika nao wajitafakari.
 
9. Tume ya Utawala Bora na haki za binadamu nchini iingilie kati vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu nchini kwa kufanya utafiti huru juu ya yale yanayotokea katika jamii na kupendekeza njia sahihi za kushuhulikia ukiukwaji wa haki za binadamuTanzania.
 
10. Tunaziomba asasi za kiraia, asasi za kiserikali, wabunge, wanasiasa, mashirika mengine na wadau mbali mbali wa maendeleo kuendelea kupaza sauti na kuungana kwa pamoja kupigania haki, utawala wa sheria, demokrasia na amani ya nchi hii haswa kipindi hiki ambapo kumekuwepo na uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu.
 
11. Tunashauri kuwepo kwa Mjadala wa kitaifa utakwaowaleta pamoja makundi yote yaliyo kwenye jamii kama viongozi wa dini, taasisi za kitaaluma, vyama vya wafanyakazi, viongozi wa kisiasa, viongozi wa serikali, viongozi wakuu wastaafu na AZAKI ili kujadili amani ya nchi na umoja wetu wa kitaifa ambao uko hatarini kutoweka endapo hatua stahiki hazitachukuliwa.
 
12. Tunawaomba viongozi wa Serikali waone umuhimu kusikia sauti hizi kwa kutoa nafasi ya majadiliano na kundi hili ili kupokea mapendekezo mengi ambayo AZAKIzinawezatoa mapendekezokwa mustakabali wa Taifa letu.
 
13. Tunavishauri Vyama vya siasa kuendelea kutumia njia za amani kudai haki zao pale zinapovunjwa wakati AZAKI zinatafuta njia ya amani na ya mazungumzo na taasisi husika na uongozi kwa ujumla.
 
14. Bunge lirudi katika majukumu yake kama walivyofanya katika matukio ya serikali siku za nyuma kwa kuunda kamati za kibunge kuchunguza hali ya sasa ya utawala wa sheria, haki za binadamu, usalama wa raia na usawa katika jamii.
 
15. Tunaomba viongozi wa serikali (hasa wale wachache wenye mtizamo hasi kuhusu AZAKI) waone Asasi za Kiraia kama wadau wazuri wa maendeleo na hivyo kuondoa vikwazo vya sasa vinazidi kujitokeza wakati AZAKI zinapokuwa katika utekelezaji wa majukumu yao.
 
Mwisho, sisi AZAKI tunatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa Binti Akwilina na wote waliopoteza wapendwa wao Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi. Amina.
 
Imetolewa na Jukwaa la Wakurugenzi wa AZAKI Tanzania leo 21/02/2018

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Serikali Yaridhia Gharama za Mazishi ya Akwilina....Yagoma Kutoa fedha taslim

$
0
0
Familia ya marehemu  Akwilina Akwiline inaendelea na maandalizi ya mazishi, huku ikielezwa kuwa Serikali imekubali kuyagharimia lakini si kutoa fedha.

Serikali imefikia hatua hiyo baada ya jana Februari 20,2018 familia ya Akwilina kueleza kuwa bajeti ya mazishi ni Sh80 milioni.

Katibu wa kamati ya mazishi Moi Kiyeyeu, ambaye ni kaka wa Akwilina amesema Serikali imewajibu kuwa haitawapa fedha taslim bali itagharimia vitu vilioorodheshwa katika bajeti ya mazishi hayo.

"Tulipotoa bajeti hatukuwa na maana kuishinikiza Serikali itoe fedha zote bali ilikuwa mahitaji ya msiba hadi pale utakapoisha. Tunashukuru Mungu kwa Serikali kuridhia kugharimia," amesema Kiyeyeu.

Kuhusu hilo, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia katika taarifa iliyotolewa leo Februari 21,2018  imesema kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Dk Leonard Akwilapo ilipokea makisio ya gharama za mazishi ya Sh80 milioni kutoka kwa msemaji wa familia, Festo Kavishe.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha wizara hiyo, Mwasu Sware alisema baada ya kupokea makisio hayo Dk Akwilapo alitahadharisha kuwa kuna baadhi ya matumizi hayatakubaliwa kwa kuwa kisheria hayagharamiwi na Serikali.

Pia, katika makisio hayo kuna gharama ambazo zilikuwa zimepewa makadirio ya juu.

Alisema katibu mkuu aliagiza kuwe na kikao kati ya wizara na ndugu wa marehemu ili kuweka sawa changamoto hizo na kuwa na bajeti ya pamoja ambacho kilifanyika jana jioni Februari 20,2018 na kufikia muafaka.

“Wizara inapenda kuufahamisha umma kuwa taratibu nyingine za maandalizi ya mazishi zinaendelea vizuri,” amesema.

Wakati huohuo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amefika nyumbani kwa dada wa marehemu Mbezi Luis kuhani msiba.

Dk Mwakyembe amesema tukio la kifo cha Akwilina ni la kusikitisha

Mwenyekiti Wa Halmashauri Ya Misungwi Na Mwanasheria Wakamatwa

$
0
0
JESHI la Polisi mkoani Mwanza kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana  na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) mkoani hapa  imemkamata Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi Bw. Anthony Bahebe.
 
Pia Mwanasheria wa Halmashauri hiyo Bw. Alphonce Sebukoto naye amekamatwa na Jeshi hilo. Viongozi wote hao wanakabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na ubadhilifu wa fedha za umma.
 
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema kukamatwa kwa viongozi hao kunatokana na tuhuma mbalimbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na matumizi mabaya ya madaraka.
 
Kamanda Msangi alisema, Bw. Sebukoto alikamatwa Februari 19, 2017 na Bw. Bahebe amekamatwa leo na wote wanaendelea kuhojiwa na Polisi kwa kushirikiana na TAKUKURU.
 
Naye Kamanda wa TAKUKURU wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Ernest Makale alisema Bw. Sebukoto aliidhinisha malipo ya sh.milioni 278 zilipwe katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw. Bahebe.

Alisema Bw. Sebukoto aliidhinisha malipo hayo kwa Bw. Bahebe Novemba 2017 wakati alipokuwa anakaimu nafasi ya ukurugenzi wa Halmashauri ya Misungwi ambapo jumla sh. milioni 138 ziliingizwa katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti huyo. Alisema kiasi kingine cha fedha kinachunguzwa kubaini kilipo.

Kukamatwa kwa viongozi hao kunatokana na juhudi za Serikali katika mapambado dhidi ya matumizi mabaya ya madaraka pamoja na fedha za umma.
 
Februari 19, 2019 akiwa katika ziara yake wilayani Misungwi Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alimsimamisha kazi Mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi Bw. Sebukoto na kuagiza achungunzwe na vyombo husika.
 
Alichukua hatua hiyo baada Mwanasheria huyo kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo ikiwa ni pamoja na kushindwa kuishauri vyema halmashauri hiyo na kuisababishia hasara ya sh. milioni 278.

Amesema Mwanasheria huyo Novemba 2017 wakati alipokuwa anakaimu nafasi ya ukurugenzi aliidhinisha malipo ya sh.milioni 278 zilipwe katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw. Anthony Bahebe.

Waziri Mkuu alisema Bw. Bahebe aliishtaki halmashauri hiyo akidai kulipwa fedha kwa ajili ya kazi ya ukandarasi wa mradi wa maji Igenge uliojengwa na kampuni ya ukandarasi ya Seekevim.

Alisema mradi huo ulianza 2014 na ulitakiwa ukamilike 2015. Mwanasheria huyo aliidhinisha malipo hayo wakati ambao tayari hati maalumu ya uwakilishi ilikuwa imekwisha tangu Desemba 2015.

Alisema Mwanasheria alimlipa Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kufanya kazi na Halmashauri jambo ambalo ni kinyume na maadili ya utumishi wa umma.

Hivyo alitumia fursa hiyo kuwakumbusha watumishi wa umma kuzingatia maadili ya utumishi na matakwa ya kisheria katika utekelezaji wa majukumu yao.

  (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, FEBRUARI 21, 2018.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhhamisi ya February 22

Serikali Ya Tanzania Yaishukuru Serikali Ya Japani Kwa Ushirikiano

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) akiwa katika kikao na Balozi wa Japani nchini, Mhe. Masaharu Yoshida (wa kwanza kulia) kilichofanyika jana  ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Kubenea amjia juu Mwigulu.....Amtaka Ajiuzulu

$
0
0
Mbunge  wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema), amemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Lameck Nchemba, kujiuzulu mara moja wadhifa wake.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mchana , jijini Dar es Salaam, Kubenea alisema, Mwigulu anapaswa kujiuzulu, kufuatia jeshi la polisi, kutuhumiwa kumminia kwa risasi, Akwilina Akwilini, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza kutoka Chuo cha Usafirishaji (NIT).

Anasema, “naungana na wanafunzi wa NIT na wale wa vyuo vikuu vingine nchini; mashirika ya madhehebu ya kidini, vyama vya hiari, asasi za kiraia na wote wanaolitakia mema taifa hili, kumtaka mheshimiwa Mwigulu Nchemba, kujiuzulu mara moja kufuatia kifo hiki cha Akwilina.”

Alisema, “…utetezi wake kuwa mauaji yale yamefanywa na Chadema, hauna mashiko. Ni utetezi uliosheheni matundu na hivyo hauwezi kukubalika kwenye sura za wananchi. Ni vema akajiuzulu ili kulinda heshima yake.”

Akwilina alipigwa risasi kichwani, February 16, akiwa maeneo ya Kinondoni, Mkwajuni, jijini Dar es Salaam. Alikuwa kwenye basi la daladala linalotokea Mabibo kwenda Makumbusho.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, Akwilina alikuwa ameketi kwenye kiti cha nyuma cha basi alilopanda. Risasi iliyochukua maisha yake, ilitokea nyuma ya alikokuwa.

Kubenea alisema, historia ya Mwigulu inaonyesha kuwa ni mtu wa kukwepa uwajibikaji kwa kutengenezea stori wengine.

Alisema, “Mwigulu amekuwa akikutuhumu Chadema kwenye mikutano ya hadhara na kuihusisha na matukio kadhaa ya uhalifu. Amefanya hivyo, tangu akiwa naibu katibu mkuu wa CCM, Tanzania Bara.”

Tamko la CHADEMA kuhusu Watu 40 waliokamatwa katika Maandamano

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimesema kitalishtaki Jeshi la Polisi na Serikali endapo watashindwa kutoa tamko kuhusu watu 40 waliokamatwa siku ya maandamano katika uchaguzi mdogo wa ubunge Kinondoni.

Akizungumza jana  na waandishi wa habari, Naibu Katibu Mkuu CHADEMA, John Mnyika alisema watu hao 40 walikamatwa February 16, 2018 wakati wakielekea Manispaa ya Kinondoni na miongoni mwao walikuwa ni wapita njia tu na wengine ni watoto waliochini ya miaka 18.

Mnyika alisema hadi sasa Jeshi la Polisi linawashikilia wananchi hao 40, ambapo kisheria lilipaswa kutoa haki kwa wananchi hao kupata dhamana.

“Tunalitaka jeshi la Polisi kupitia IGP kutoa kauli  juu ya watu hao 40 wanaowashikilia na kuwaainisha kwa majina watu hao na kueleza taratibu za kuwapa dhamana ama iwapeleke Mahakamani.”  Alisema John Mnyika

Benki Zawahakikishia Wafanyabiashara Mikopo....Ni Wale Wanaotaka Kununua Pamba

$
0
0
BENKI mbalimbali nchini zimewahakikishia wafanyabiashara wa zao la pamba kuwa zina fedha za kutosha kuweza kuwakopesha ili wanunue pamba yote itakayozalishwa katika msimu wa mwaka huu nchini.
 
Pia viongozi wa benki hizo wamesema wako tayari kusaidia katika uwekezaji wa miundombinu ya aina yeyote ama eneo litakalohitaji mkopo wa fedha ili kufanikisha mchakato wa ununuzi wa pamba katika msimu huu ikiwa ni pamoja na kusaidia ujenzi wa maghala.
 
Hayo yamesemwa jana  (Jumatano, Februari 21, 2018) na viongozi wa benki mbalimbali nchini katika mkutano ulioitishwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa uliowahusisha wafanyabiashara wote wa pamba , Wakuu wa Mikoa ,Viongozi wa Halmashauri na wadau wote.
 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti viongozi wa benki za NMB, CRDB, TIB, EXIM, AZANIA, Mkombozi, Bank of Africa, Equity na Eco waliwahakikishia wafanyabiasha hao mbele ya Waziri Mkuu kwamba wana fedha za kutosha na wako tayari kuwapa mikopo ili wakanunue pamba mara msimu utakapoanza.
 
Akizungumza katika mkutano huo, Waziri Mkuu amewataka wanunuzi wa zao hilo kuandikisha katika ofisi ya Mkurugenzi wa Bodi ya Pamba kiasi cha pamba wanachohitaji kununua pamoja na maeneo ambayo wanatamani kwenda kununua.
 
Waziri Mkuu amesema suala hilo litaiwezesha bodi kufahamu idadi ya wafanyabiashara watakaonunua pamba pamoja na kiasi wanachohitaji na eneo husika. “Serikali itaendelea kusimamia zao hilo kikamilifu.”

Amesema kwa sasa wanauhakika kuwa pamba yote itanunuliwa kwa sababu benki zimewathibitishia kwamba ziko tayari kuwakopesha wafanyabiasha, hivyo wadau wote watambue kuwa Serikali itashirikiana nao hadi katika hatua za mwisho za ununuzi.

Waziri Mkuu aliwahakikishia wafanyabiashara hao kwamba maombi waliyoyatoa kuhusu uboreshaji wa mauzo ya zao hilo yatayafanyiwa kazi na Serikali itaendelea kusimamia zao hilo ili ununuzi wake uwe rahisi.

Kwa upande wake, Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba amesema wamejipanga kikamilifu katika kudhibiti ubora wa pamba, ambapo amewataka viongozi wa maghala wasipokee pamba chafu.

Pia amewataka wakulima wa pamba wasithubutu kuchanganya na maji, mawe au mchanga kwa sababu wataharibu soko. Serikali itapambana na watu wote wakaothubutu kuharibu zao hilo kwa kcuhukua hatua kali za kisheria kwani huo ni uhujumu uchumi.

Aliendelea kusema kuwa uamuzi wa Serikali kusimamia ongezeko la uzalishaji wa zao la pamba unakwenda sambamba na mazao mengine makuu ya biashara ambayo ni korosho, chai, tumbaku, kahawa na mahindi kwa upande wa chakula.

Dkt. Tizeba amesema inatazamiwa kuwa ifikapo 2021 mchango wa mazao katika pato la Taifa unakadiriwa kufikia sh. trilioni 13.6, ambapo yataliwezesha Taifa kuvuka mstari wa kiwango cha umasikini.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango amesema kuwa zao la pamba lina mchango mkubwa katika kukuza uchumi, hivyo watahakikisha zao hilo linaendelea kukua.

Dkt. Mpango amezitaka benki zichukue tahadhari kwa mikopo chechefu  hivyo wajiridhishe kama wakopaji wote wanatumia mikopo hiyo kwa mujibu wa makusudio.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, FEBRUARI 21, 2018.

Tundu Lissu Afunguka Baada ya Kutembelwa na Katani Ahmad Katani, mbunge wa Jimbo la Tandahimba

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya (CHADEMA) Mhe. Tundu Antiphas Lissu amefunguka na kusema amefarijika sana kutembelewa na Mbunge wa Tandahimba (CUF) Katani Ahmad Katani na kudai mbunge huyo alikuwa miongoni mwa watu waliompeleka Nairobi.

Lissu ameeleza hayo kupitia ukurasa wake maalumu wa kijamii na kusema mbali na kumlijua hali lakini waliweza kujadiliana kuhusu mwenendo wa siasa zinazoendelea nchi Tanzania.

"Mheshimiwa Katani amekuja Ubelgiji kunijulia hali pamoja na kuja kujadiliana nami masuala mbali mbali yanayohusu siasa za nchi yetu na mustakbali wa Taifa letu. Katani alikuwa kwenye msafara wa Wabunge walionipeleka Nairobi, Kenya, mara baada ya jaribio la mauaji la September 7, na alikaa Nairobi kwa siku nne. Nimefarijika sana na ugeni huu wa ndugu yangu na kaka yangu Katani", amesema Lissu.

Mbunge Tundu Lissu alishambuliwa na watu wasiojulikana tangu Septemba 7,2017 akiwa mkoani Dodoma, na kisha kupelekwa nchini Nairobi kwa matibabu na baada ya miezi 3 alipelekwa nchini Ubelgiji kwa hatua nyingine ya matibabu.

Mfanyakazi CRDB Atupwa Jela Miaka 93

$
0
0
Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imemhukumu kwenda jela jumla ya miaka 93 aliyekuwa mfanyakazi wa CRDB, Gura baada ya kumkuta na hatia ya makosa 29 ya kughushi na mawili ya wizi wa Sh. milioni 29.8 za benki hiyo.

Aidha, mahakama hiyo imemtia hatiani Gura kwa kosa la kutakatisha Sh. milioni 29.8 na kumwadhibu kulipa faini ya Sh. milioni 100.

Mahakama ilisema akishindwa kulipa faini hiyo atakwenda jela kutumikia kifungo cha miaka mitano na imeamuru arejeshe fedha hizo kwa benki hiyo, na akishindwa kitatolewa kibali cha kifilisiwa mali zake.

Hukumu hiyo ilisomwa jana na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Hakimu Simba alisema mahakama yake imemtia hatiani kwa makosa 32 na kwamba kwa kosa la pili hadi la 30 mshtakiwa atakwenda jela kutumikia kifungo cha miaka mitatu kwa kila kosa.

Pia, alisema Hakimu Simba, mshtakiwa atatumikia kifungo cha miaka mitatu kwa kosa la 31 na 32 ya wizi wa Sh. 29,889,191 mali ya benki ya CRDB.

Kabla ya hukumu hiyo, mshtakiwa Gura alipewa nafasi ya kujitetea, ili apunguziwe adhabu.

Gura alidai kuwa amekaa mahabusu kwa miaka mitatu, ni mwenye familia ya mke na watoto watatu wote wadogo na wenye kumtegemea.

"Mheshimiwa hakimu mimi ni mgonjwa nasumbuliwa na marathi ya mgongo, shinikizo la damu na sukari," alisema Gura. "Maradhi haya yananifanya nisiweze kusimama kwa muda mrefu. Naiomba mahakama iniangalie kwa jicho la huruma."

Hakimu Simba alisema adhabu hizo za kifungo jela zitakwenda sambamba na kwamba mahakama imezingatia maombi ya mshtakiwa.

Katika kesi hiyo Gura anadaiwa kutenda makosa hayo kati ya Agosti,2014 na 2015.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images