Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Muafaka wa mtoto aliyerudishwa Tanzania Baada ya Wazazi wake Kukamatwa na Madawa ya Kulevya China

$
0
0
Hatimaye  pande mbili za familia ya mtoto ambaye wazazi wake walikamatwa na dawa za kulevya hivi karibuni nchini China, zimekubaliana alelewe na upande wa bibi mzaa mama yake.

Familia hizo zilikutana jana kwenye ofisi za Ustawi wa Jamii Makao Makuu jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo yaliyofikia mwafaka huo.

Wazazi hao, Baraka Malali na Ashura Mussa, walikamatwa Januari 19 mwaka huu kwenye uwanja wa ndege wa Baiyun, Guangzhou nchini China wakiwa wamemeza pipi 129 za dawa za kulevya.

Mtoto huyo alirejeshwa nchini Alhamisi iliyopita katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), majira ya saa 7:42 mchana akiwa ameambatana na Ofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Akizungumzia uamuzi uliofikiwa kuhusiana na familia ambayo itamchukua mtoto huyo, Kamishna wa Sheria wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Edwin Kakolaki, alisema familia hizo zilikubaliana mtoto alelewe na upande wa bibi mzaa mama ingawa watashirikiana katika matunzo yake.

“Upande wa mama yake mzazi ndiko atakakolelewa kwa sababu alishawahi kukaa huko kwa muda kwa hiyo upande wa baba yake wameridhia mtoto aendelee kukaa huko.

Lakini makubaliano ni kwamba mtoto ni wa familia zote mbili na wataendelea kumlea kwa pamoja,” alisema.

”Hayo ndiyo waliyokubaliana kwa pamoja hapakuwa na ubishani na sisi tulikuwa tunashuhudia makubaliano yao.”

Wazazi hao baada ya kukamatwa Januari 19, mwaka huu, walipimwa na kubainika kuwa wamemeza dawa za kulevya na kuwekwa katika chumba maalumu. Malali alitoa pipi 47 na Ashura alitoa pipi 82.

Wakati wazazi hao wakiwa mahabusu, serikali ya China iliwasiliana na Tanzania na kufanya utaratibu wa kumrudisha mtoto nchini huku wazazi hao wakisubiri hatima yao mahakamani.

Watu wanaopatikana na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya nchini China huhukumiwa adhabu ya kunyongwa.

Kwa Tanzania hufungwa kifungo cha maisha kwa yeyote atakayekamatwa na ‘unga’ kuanzia gramu 20.

Kakolaki alisema bado hawajajua mzigo wa dawa za kulevya walikozichukulia kwa sababu safari yao ya kwenda China waliianzia Zanzibar.

“Walianzia safari yao Zanzibar na baadaye walikwenda hadi Nairobi wakatoka hapo na kuanza safari yao moja kwa moja hadi Guangzhou, China. Sasa kujua mzigo walichukulia wapi bado hatujajua, lakini si kwamba walipita katika uwanja wetu wa Dar es Salaam,” alisema Kakolaki.


Mkurugenzi Kituo cha Sheria (LHRC) Alivyofika Katika Msiba wa Akwilina Kutoa Mkono wa Pole

$
0
0
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Dk.Helen Kijo-Bisimba  jana alifika Msibani kwa mwanafunzi Akwilina, Mbezi mwisho katika Wilaya ya Ubungo kwa ajili ya kuwapa pole wafiwa.

Akwilina alifariki dunia Februari 16, 2018 baada ya kupigwa risasi akiwa kwenye daladala wakati polisi wakiwatawanya waandamanaji ambao ni wafuasi wa Chadema

Waziri Kigwangalla Aitembelea Familia Ya Akwilina na Kutoa Ubani Wa Pole

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla jana ali tembelea nyumbani kwa familia ya Akwilina na kutoa ubani wa pole kwa msiba huo.

“Nimefika hapa kama Raia mwema tu ambaye nimeguswa na msiba huu na nimetafakari kwani na mimi kipindi fulani nilipitia chuo hasa kutoka familia zetu hizi masikini kwa hiyo inapotokea tukio kama ili unaona ni pigo kwa familia, pigo kwa jamii, pigo kwa wanafunzi wenzake na pigo kwa Taifa kwa ujumla wake” alieleza Dkt. Kigwangalla wakati akizungumza na vyombo vya Habari msibani hapo.

“Ndoto za binti huyu zimezimika ghafla, nimesikitika sana, nimekuja kujumuika na Watanzania wenzangu kumlilia Akwilina, nmeguswa na msiba tuendelee kumlilia ....sidhani kama ni wakati muafaka kuanza kunyoosheana vidole nani kafanya nini, hili halina umuhimu kwa sasa,”  Aliongeza Kigwangalla

Dkt.Kigwanalla ambaye alifika msibani hapo majira ya saa saba mchana, aliweza kuungana pamoja na ndugu na jamaa wa wafiwa ambapo pia alipata chakula cha mchana pamoja na waombolezaji wengine sambamba na kutoa ubani wake kama mwananchi mwingine.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Makoli ambaye yupo hapo kwa ajili ya kusimamia shughuli  kwa upande wa Serikali, alibainisha kuwa wataendelea kuratibu baadhi ya mambo yanayoendelea hapo kwani msiba huo kwa namna moja Serikali imeguswa nao.

Mbali na Mkuu wa Wilaya hiyo, Wengine waliofika hapo ni pamoja na Mkurugenzi wa Ubungo, John Kayombo ambapo kwa pamoja na watendaji wengine wa Kiserikali wameweza kusaidiana na familia ya marehemu katika shughuli mbalimbali zinazoendelea msibani hapo.

Akwilina kabla ya kifo chake alikuwa Mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji(NIT) amepoteza maisha baada ya kupigwa risasi Februari 16 mwaka huu eneo la Mkwajuni jijini Dar es Salaam wakati Polisi walipokuwa wakizuia maandamano ya chama cha siasa cha CHADEMA.

Dawa Asilia Inayo Saidia Kushusha Sukari Iliyopanda.

$
0
0
Je ! Sukari  yako  ipo  juu ? Unatafuta tiba  asilia  ya  kushusha  sukari ?
Kama jibu  lako  ni NDIO basi  hii  ni HABARI NJEMA  SANA  KWAKO.
Ipo tiba  asilia  inayo  saidia  kushusha  sukari iliyo  panda.

JINSI  INAVYO  TUMIKA :  Dawa  hii  huchemshwa  na  kuachwa  ipoe  kabisa  kisha  mhusika  anatumia  kunywa  nusu  glasi  yenye ujazo wa  milimita mia mbili  na  hamsini ( 250 mills ) .

Asubuhi  atakunywa  nusu  glasi  na  usiku  atakunywa  nusu  glasi. Atafanya  hivyo  kwa  muda  wa  wiki mbili  hadi  tatu.

BAADA  YA  KUMALIZA  DOZI : Baada ya  kumaliza  dozi  mhusika anashauriwa  kwenda  hospitali  kupima  ili  kuona  sukari  yake  imepungua  kwa  kiasi  gani na  kupata  ushauri  wa  kitaalamu  kutoka  kwa  Daktari.

Tiba  hii  pia  inasaidia  kuimarisha  afya  ya  mwili  kwa  ujumla.
N.B : Tiba hii  haiwafai  watu wenye  sukari  ya  kushuka  ama  sukari  iliyo  chini  kwa  sababu inashusha  sana  sukari mwilini.

Kwa  watu wenye  sukari  ya kushuka  ambao  wanatafuta  tiba  ya  kupandisha  sukari, bado  hatujapata  dawa  ya  uhakika  inayo  weza  kusaidia  kupadisha  sukari.

Jaribu  kutumia  tiba  hii  uone  namna inavyo weza  kukusaidia  kudhibiti  kiwango  cha sukari kwenye  damu.

Kwa wewe  ambae  sukari  yako  ipo  juu  na  unataka  kutumia  tiba  asilia  ya kushusha  sukari  yako, jaribu  kutumia  tiba  hii  ili  badae  uweze  kutoa  ushuhuda wa  namna  tiba  hii  ilivyo  kusaidia.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma ya jengo  la  UBUNGO PLAZA.

Wasiliana nasi kwa  simu  namba  0766 53 83 84.

Kwa  Makala  mbalimbali kuhusu  tiba  asilia  za  magonjwa  na  matatizo  mbalimbali  yanayo  msumbua  mwanadamu, tutembelee  kila  siku  kupitia  blogu yetu : wwww.neemaherbalist.blogspot.com 

Picha: John Mnyika Alivyofika Msiba wa Akwilina Kutoa Pole

$
0
0
JANA  February 19, 2018 Mbunge wa Jimbo la  Kibamba na  Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA -Bara John Mnyika akiwa ameongozana na Afisa Habari wa CHADEMA  Tumaini Makene walifika kwenye msiba wa Mwanafunzi aliyepigwa risas, Akwilina Akwilini akiwa kwenye daladala wakati Polisi wakitawanya waandamanaji wa CHADEMA.

SORRY MADAM -Sehemu ya 100 na ya MWISHO (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA  

“Shitiii”
Agnes akaikoki bunduki yake na kumuelekezea mtu huyo na kumpima maeneo ya kichwa. Mzee Godwin hadi anakaribiana na Erickson akaweza kuona alama nyekundu ya buduki ikiwa imemlenga Erickson kifuani. Kwa haraka Mzee Godwin akamuwahi Erickson ambaye anatambua ni mkwe kwa mwanaye Manka, akamsukuma na risasi ambayo ilipangwa kumpiga Erickson ikapiga mzee Godwin mgongoni na kumuangusha chini na kumfanya Eddy kushangaa na kwaharaka akaipiga magoti chini na kumgeuza Mzee Godwin na kumkuta akimwagikwa na damu mdomoni.
“BABABAAAAAAAAAA”
Eddy alipiga kelele humu machozi yakianza kumwagika usoni mwake na kumfanya Mzee Godwin kutabasamu na kumshika mkono wa kulia Eddy na kuuweka kifuani mwake.

ENDELEA
“Eddy”
Mzee Godwin aliweza kuitambua sauti ya Eddy na kulia kwake. Eddy kwa hasira akaanza kuivua sura yake ya bandia, japo imeshikana sana na ngozi ya uso wake, ila hakujali hayo maumivu.  Mzee Godwin akaendelea kumuangalia Eddy kitu anacho kifanya hafi ikafikia hatua akamaliza kabisa kuivua sura yake na kubaki na sura alisi.
“Baba fungua macho please”
Eddy alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Japo baba yake huyo ameweza kumfanyia mambo mengi mauvu katika maisha yake yote ila damu ni nzito kuliko maji.
“Ku….uu…wa…..jasiri D.F.E1993”

Mzee Godwin alizungumza maneno hayo kwa shida kidogo na hapo hapo akakata roho. Kitendo cha mzee Godwin kuanguka chini na kunyanyuliwa na Erickson, kiliweza kumstua Manka aliye anza kushuka kwenye gari kwa garaka, na kuanza kukimbilia eneo alipo kaa Mzee Godwin na Erickson. Agnes hakutaka kumpa nafasi nyingine mlinzi wa John ambaye alikuwa akihangaika kuikoki bunduki yake. Akamtandika riasi moja ya kicha na kumchangua hapo hapo. Makachero wengine walipo ona makubaliano yameingia dosari wakaanza kufaya mashambulizi kwa kina Rahab na Fetty, ambao nao waliweza kuyajibu mashambulizi hayo huku wakiwa amejificha pembeni ya gari lao.
Agnes akashusha pumzi huku akimtazama Manka kwa kutumia lenzi ya bunduki yake, akikimbilia eneo alipo Erickso.

“Mpumbavu wewe”
Agnes alizungumza huku akiikoki bunduki, yake. Alipo hakikisha Manka amekaribia kufika karibu kabisa na walipo Eddy na mzee Erickson, akaivuta traiga ya bunduki hiyo na kuiruhusu risasi moja kutoka kwa kasi. Kitendo cha Manka kumtazama Erickson na kukuta akiwa ni Eddy, alistukia akianguka chini na hapo hapo akakata roho, risasi aliyo ifyatua Agnes iliweza kutua kichwani mwa Manka ndio iliyo yakatisha maisha ya msichana huyo.

Eddy alihisi kuchanganyikiwa, baada ya kumuona Manka akiwa amelala chini, damu nyingi zikiwa zimesambaa kwenye  lami. Halima na Anna wakiwa chini ya maji, waliweza kupambana na makachero wengine ambao walitumwa kuimarisha ulinzi chini ya daraja hilo. Mapambano yao yakawa ni kufa na kupona. Halima akajitahidi kupambana kadri ya uwezo wake, ila kwa leo bahati haikuwa kwake kwani kachero aliye kutana naye aliweza kumzidi kwa kila kitu na kujikuta akifia kwenye mikono ya kachero hiyo kwa kuchomwa kisu cha shingoni.

Kifo cha Halima, kilimshangaza sana Anna, aliye jikuta akiivunja shingo ya kachero aliye kuwa akipambana naye na kuimtoa mtungi wa gesi alio jifunga nao mgongoni. Akamfwata kachero aliye muua Halima, akaanza kuparanganaye, mapigano kati yao yaliweza kumpa ushindi Anna japo naye aliweza kujeruhiwa na kisu cha kachero hiyo ila akafanikiwa kummaliza maisha yake.

Taratibu Anna akaanza kuufwata mwili wa Halima sehemu unapo elea elea. Akaushika, na kujikuta akianza kulia kwa uchungu, kwa maana hakutarajia kama rafiki yake huyo anaweza kukutwa na mauti. Agnes kazi yake ikawa ni kuwaua makachero wote ambao wanapambana na kina Fetty na Halima. Haikuwa kazi ngumu kwake kwa maana sehemu alipo jificha ni si rahisi kwa mtu kuweza kumuona ila yeye aliweza kuona eneo zima.
                                                                                                       ***
    Wanajeshi na walinzi walio weza kubaki ikulu kwa ajili ya kuimarisha ulinzi kwa siku hiyo hawakuwa na bahati, kwa maana waliweza kushambuliwa na wanajeshi ambao wamevalia kombati za jeshi la taifa, ila utoafuti ni kwamba karibia wote wamejifunga vitambaa vyekundu katika mikono yao ya kushoto. Walijitahidi kuilinda Ikulu ila hawakuweza kwa maana shambulizi hilo ni kubwa na la kustukiza. Meja Paul Msuya aliweza kuwaongoza vijana wake katika kufanya mapinduzi hayo ya kuing’oa serikali yam zee Godwin madarakani.

   Zoezi lao halikuchukua muda mrefu sana, wakawa wamesha maliza kazi yao na kuiwek aikulu chini ya ulinzi wao. Meja Msuya akatuma wanajeshi wengine kwenda katika daraja la kigamboni kumsaidia mkuu wao ambaye ni Rahab. Milio ya risasi, iliwafanya wakazi wa maeno ya Posta na Kigamboni kuingiwa na hofu kubwa sana, kwa maana sio hali ya kawaida na hawakujua ni kitu gani kinacho endelea. Wananchi wengi walio ingiwa na woga, kila mmoja aliweza kujificha sehemu ambayo alihisi anaweza kuokoa maisha yao.

Wapo ambao waliweza kujificha chini ya vungu za vitanda vyao, wengine walijificha kwenye makabati, wengine waliamua kujifuanika mashuka gubigubi na kujinyoosha vitandani mwao na kuigiza kama wamekufa. Ukawa ni usiku mgumu sana kwao. Wanajeshi wanao muunga mkono Rahab, wakafika katika dareja la Kigamboni na kukuta mambo ndio yanamalizikia malizikia, huku walinzi wengi wa raisi Godwin wakiwa wamesha potea maisha yao. Wakaweza kuuona mwili wa mzee Godwin na mwanaye Manka wakiwa tayari wamesha teketea kwa kupigwa risasi.

TANGA RAHA- Sehemu ya Tisa ( 9 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Rahma akiwa anaendelea kuzungumza na simu kwa mbali nikamuona Mama Fety(Fatuma) akija katika eneo la ninapoishi huku akiwa ameongozana na mwanamke mwengine ambaye sikuweza kumtambua mara moja kwani bado wapo mbali kidogo na nilipo simama mimi
 
ENDELEA
Rahma akamaliza kuzungumza na simu akashush kiio cha gari katika upande nilio simama mimi
“Baby wala siingii ndani hapa baba amenifokea kama nini kwa jinsi nilivyo chelewa”
“Sawa tutaonana kesho shule?”
“Powa.Nakupenda Sir Eddy”
“Hata mimi ninakupenda pia”
Rahma akawasha gari na kuondoka.Nikabaki nimesimama huku nikiwaona Mama Fety na mwenzake wakija nilipo simama
“Mambo Eddy?”
“Powa vipi?”
“Safi mida ya mchana nilikuja sikukuta ulikwenda wapi?”
“Kuna sehemu nilikwenda kufwatilia mambo yangu ndio ninarudhi hivi”
 
“Ahaa vipi chai ulikunywa”
“Ohhh yaani mwanao alipokuwa anaileta yaani nilikuwa ndio naondoka ikanibidi niiweke ndani na sasa hivi kama unavyo niona ndio ninarudi”
Nikamuona rafiki wa Mama Fety akimminya Mama Fety kiunoni kama anapeana ishara ila sikujua ni ishara ya nini
“Karibuni ndani”
Tukaingia chumbani kwangu nikawakaribisha na kuwawashia video waangalie wanachopenda kuangali.
“Baby huyu ni rafiki yangu anaitwa Saumu…..Saumu huyu kama nilivyo kuadisia anaitwa Eddy ndio mahabuba wangu”
Utambulisho alio ufanya Mama Fety haukunifurahisha hata kidogo japo ninajitahidi kuweka sura ya furaha usoni kwangu
“Nashukuru kukufahamu Eddy”
 
“Na mimi pia nasg=hukuru kukufahamu”
Nikachukua Laptop yangu na kuanza kupangilia mada nitakazo fundisha shuleni siki itakayo fwata.Wakaendelea kutazama Video baada ya muda Mama Fety akanyanyuka kutoka katika sofa alilo kaa hadi kwenye sofa nililo kaa mimi.
“Baby”
“Mmmmm”
“Mbona upo kimya jamani hata huzungumzi na sisi?”
“Kuna kazi hapa nina ifanya si unajua kesho ni Jumatatu inanibidi kupangilia kila kitu cha kufundisha mapema ili kesho nisipate tabu”
“Utamaliza saa ngapi?”
“Kwani munataka kuondoka?”
“Hapana ila nilitaka kujua ni saa ngapi utamaliza kwani mimi na rafiki yangu tunataka tukupeleke ukashangae shangae mji”
 
“Kwa hili best itakuwa ngumu”
“Kwa nini jamani?”
“Hap nilipo nimechoka kiasi kwamba nikimaliza tu hii kazi nalala ili kesho nisichelewe kazini”
“Jamani Baby si tunakwenda mara moja mida ya saa tano tano tunarudi”
“Yaani kweli kwa hapo nisamehe baby hembu tufanye siku nyingie”
“Mama Fatuma kweli shemeji Eddy anaonekana amechoka muache apuumzike kwani si yupo kila siku”
“Shemeji umeona eheeee”
“Haya bwana mumeamua kunishambulia watu wawili basi sina jinsi inabindi nikubaliane na nyini”
 
Nikashukuru Mola kwa shemeji Saumu kunitetea.Mama Fety akarudi alipokuwa amekaa awali na kuendelea kutazama video,baada ya dakika kumi wakaaga na kuondoka mimi nikashukuru Mungu.Nikamaliza kufanya kazi zangu nikaingia bafuni nikaoga na kupanda kitandani na kuaanza kuulazimisha usingizi huku kumbukumbu za maisha yangu ya nyuma zikianza kunijia akilini.

==>Endelea Nayo <<kwa Kubofya Hapa>>

Matokeo Ya Uchunguzi Kuhusu Kauli Ya Askofu Zachary Kakobe kwamba ‘ana pesa nyingi kuliko Serikali’.

$
0
0
Kufuatia kauliiliyotolewa na Askofu Zachary Kakobe wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship katika mahubiri ya Ibada ambayo alisema kuwa “Yeye ana pesa kuliko Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilifanya uchunguzi ili kubaini usahihi wa kauli hiyo.

Yafuatayo ni mambo ambayo yalibainika baada ya kufanyika uchunguzi kuhusu kauli ya Askofu Zachary Kakobe;

1.Askofu Zachary Kakobe hana akaunti wala fedha katika taasisi yoyote ya fedha hapa nchini. Aidha uchunguzi ulibaini kuwa Askofu Kakobe ni mmoja wa wasimamizi wakuu wa akaunti za kanisa (signatories) zilizopo katika benki ya NBC zenye jumla ya kiasi cha shilingi 8,132,100,819.00, kiasi hiki cha fedha kimetokana na sadaka, zaka na changizo ambazo zinatolewa na waumini wa kanisa tajwa hapo juu, hivyo kwa mujibu wa Sheria hakitozwi kodi.

2.Kanisa lilikwepa kulipa kodi kiasi cha shilingi 20,834,843.00 ambazo zilitokana na uwekezaji katika makampuni ya kukuza mitaji.Kodi hiyo imelipwa baada ya uchunguzi.

3.Kampuni inayomilikiwa na watoto wa Askofu Zachary Kakobe ilikwepa kulipa kodi kiasi cha shilingi 37,280,030.00 ambazo zimelipwa baada ya uchunguzi. Kwa ujumla, kiasi cha kodi kilicholipwa kutokana na uchunguzi huu ni shilingi 58,114,873.00.

4. Kanisa linatunza kiasi kikubwa cha fedha kwenye ndoo na ‘majaba’ kinyume na taratibu za utunzaji wa fedha, lakini pia uwekaji na utoaji wa fedha nyingi kutoka benki haushirikishi vyombo vya ulinzi na usalama kwa ajili ya usalama wa fedha zenyewe na wahusika.

5.Pia ilibainika kwamba Kanisa halitengenezi hesabu za Mapato na Matumizi ya Fedha kitu ambacho ni kinyume na Katiba ya Kanisa pamoja na sheria za usimamizi wafedha ambayo imepelekea matumizi mabaya ya fedha za waumini kama vile safari za nje ya nchi ambazo zimedhaminiwa na Kanisa lakini wanaosafiri ni Askofu na familia yake.  Vile vile fedha za Kanisa zinatumika kujenga nyumba ya mke wa Askofu, kwa jina lake na wala si kwa jina la Kanisa, kitu ambacho ni kinyume na taratibu za Kanisa.

Aidha, wakati uchunguzi huo ukiendelea,mnamo tarehe 24.01.2018 Askofu Kakobe aliandika barua kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuomba radhi kutokana na kauli yake ya kebehi pamoja na matamshi yake ya dharau kwamba ana pesa nyingi kuliko Serikali.

WITO:
•  Mamlaka ya Mapato Tanzaniainatoa wito kwa Taasisi zote za dini ambazo zinajihusisha na shughuli zozote za kiuchumi kulipa kodi stahiki na kwa wakati kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za kodi.

• Mamlaka ya Mapato Tanzania inazitaka Taasisi zote za kidini kufuata katiba zao ikiwa ni pamoja na kutengeneza hesabu za mapato na matumizi.

Charles E. Kichere
KAMISHNA MKUU 
MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA

“Pamoja Tunajenga Taifa Letu”

Viongozi Watano wa CHADEMA Waripoti Polisi na kuachiwa kwa Dhamana

$
0
0
Viongozi watano wa Chadema kati ya saba waliokwenda Kituo Kikuu cha Polisi kuitikia wito wa kamanda  wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, wameachiwa kwa dhamana.

Walifika kituoni hapo leo Februari 20, 2018 saa 6: 10 mchana na kuachiwa saa 7:45 mchana.

Viongozi walioitwa na Mambosasa ni mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, katibu mkuu wa chama hicho, Dk Vincent Mashinji, naibu makatibu wakuu John Mnyika (bara) na Salum Mwalimu (Zanzibar).

Pia wamo, mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee; mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti, John Heche na Esther Matiko ambaye ni mweka hazina wa Bawacha.

Waliofika leo kituoni hapo na kuachiwa ni Bulaya, Mdee, Matiko, Heche na Mnyika.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Mnyika amesema kupitia wakili wao, Peter Kibatala  wamepewa dhamana na kutakiwa kuripoti tena kituoni hapo, Februari 27, 2018.

Amedai kuwa fununu zilizopo ni kwamba wanaweza kufunguliwa shataka la kuandamana bila kuwa na kibali.

"Tumefika hapa lakini hatujahojiwa hivyo tumepewa dhamana na tutaripoti siku ya Jumanne wiki ijayo,” amesema.

Wito wa viongozi hao polisi umekuja siku siku nne tangu kutokea kwa kifo cha Akwilina Akwiline, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo cha Taifa cha Usfairishaji (NIT).

Akwilina aliuawa kwa kupigwa risasi Februari 16, 2018 akiwa ndani ya daladala eneo la Mkwajuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakienda ofisi za mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni kudai viapo vya mawakala wao.

Mazishi ya Akwilina kugharimu sh milioni 80

$
0
0
Familia ya mwanafunzi wa  mwaka wa kwanza katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), anayedaiwa kuuawa na polisi wiki iliyopita, Aquilina Akwilini imeikabidhi  serikali bajeti ya maziko ya zaidi ya Sh milioni 80.

Msemaji wa Familia, Festo Kavishe amekabidhi bajeti hiyo leo Jumanne Februari 20, kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Leonard Akwipalo na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisali Makori leo.

 "Hayo ndiyo makubaliano ya familia, tumewakabidhi wataenda na kujadiliana kisha tutakutana nao saa 10 jioni leo, kisha watatueleza ya kwao pia, tunachohitaji ndugu yetu apumzike kwa amani," amesema Kavishe.

Marehemu Aquilina ambaye aliuawa kwa risasi Ijumaa iliyopita akiwa katika basi baada ya polisi kuwatawanya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), waliokuwa wakiandamana kwenda kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Wilaya ya Kinondoni kudai viapo vya mawakala wao, anatarajiwa kuagwa Alhamisi wiki hii katika viwanja vya NIT na kusafirishwa Rombo mkoani Kilimanjaro, Ijumaa.

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Waziri Mkuu: Shida Ya Maji Jiji La Mwanza Kuwa Historia....Ni Baada Ya Serikali Kuanza Ujenzi Wa Miradi Ya Sh. Bil. 112

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akipokea mabomba ya maji yenye urefu wa kilomita tano kutoka kwa  Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Mwanza Plastics, Joel Makanyaga wakati alipotembelea kiwanda hicho jijini Mwanza , Februari 20, 2018. Kulia ni Mbunge wa Ilemela na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina mabulla. Mabomba hayo yatatumika kupeleka maji katika Kituo cha Afya cha Karume kilichopo kata ya Bugogwa wilayani Ilemela.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


CCHANGAMOTO ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika Jiji la Mwanza kuwa historia baada ya Serikali kuanza utekelezaji wa ujenzi wa miradi mikubwa miwili ya maji yenye thamani ya sh. bilioni 112.

Hayo yamesemwa leo na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (Jumanne, Februari 20, 2018) wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa Halmashauri za Jiji la Mwanza, Ilemela na Nyamagana akiwa katika siku ya sita  ya ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza.

Waziri Mkuu amesema miradi hiyo inahusisha kuboresha upatikanaji wa maji katika maeneo ya pembezoni wenye thamani ya sh. bilioni 75 ambao utahusisha ujenzi wa chanzo kipya cha maji kwenye eneo la Butimba chenye uwezo wa kutoa lita milioni 40 kwa siku.

Ametaja maeneo yatakayonufaika na mradi huo kuwa ni Butimba, Nyegezi, Mkolani, Buhongwa, Sawa, Lwanhima, Kishiri, Nyahingi, Luchelele, Malimbe, Bulale, Fumagila, Usagara, Kisesa, Buswelu, Nyamwilolelwa, Kahama, Nyamadoke, Nyamhongolo, Mondo, Kiseke, Kangae, Meko, Nsumba na Bulola.

Waziri Mkuu amesema mradi mwingine ni wa kuboresha upatikanaji wa maji katika maeneo ya milimani wenye thamani ya sh. bilioni 37 ambao ulianza kutekelezwa Februari, 2017 na unatarajiwa kukamilika Agosti 2018.

Amesema wakazi 105,649 wanaoishi katika maeneo ya milimani hususan yaliyo juu ya matenki ya maji ambayo hayapati huduma kwa sasa watanufaika. Maeneo hayo ni Nyasaka, Bugarika, Nyegezi, Capripoint, Mjimwema, Nyakabungo na Kitangiri.

Amesema Serikali kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo, itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini watapata huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka viongozi na watendaji wa Jiji la Mwanza kuhakikisha wanashirikiana katika kuwatumikia wananchi bila ya ubaguzi wa dini, kabila wala kipato. Pia amewataka watambue miiko na ukomo wa madaraka yao.

Amesema watumishi hao wanatakiwa wawe waaminifu na wasimamie vizuri matumizi ya fedha za uetekelezaji wa miradi mbalimbali kwenye maeneo yao na wahakikishe zinatumika katika miradi husika kama ilivyoelekezwa na Serikali.

Pia Waziri Mkuu alimuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Bw. Kiomoni Kibamba kuifuta Taasisi ya Bunge la Jamii kwa sababu inakiuka sharia na kazi inazofanya zinalingana na za bunge. Taasisi hiyo ilisajiliwa na ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, FEBRUARI 20, 2018.

Serikali yatoa tamko walimu wa sekondari kufundisha Shule za msingi

$
0
0
Serikali imesema mwalimu wa sekondari kufundisha shule ya msingi si kushushwa cheo na wala si jambo la ajabu.

Taarifa ya mkuu wa kitengo cha mawasiliano Ofisi ya Rais (Utumishi), Florence Lawrence imesema Serikali kuwapangia baadhi ya walimu wa sekondari kufundisha shule za msingi ni moja ya hatua za kuongeza ufanisi na kuleta mgawanyo sawa wa walimu katika shule hizo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk Laurean Ndumbaro amekaririwa katika taarifa hiyo iliyotolewa leo Februari 20,2018 akisema hatua hiyo haimaanishi kuwa walimu wanaotoka katika shule ya sekondari kwenda kufundisha msingi wameshushwa cheo.

Dk Ndumbaro ametoa ufafanuzi huo katika kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Makambako.

Amesema lengo la Serikali ni kuondoa upungufu wa walimu katika shule za msingi na kuimarisha utoaji wa elimu.

Katibu mkuu ameainisha kuwa sifa za kufundisha na kiwango cha elimu zinaendana na mabadiliko yanayotokea duniani, hivyo mwalimu mwenye elimu ya kiwango cha Shahada ya kwanza kufundisha shule ya msingi isionekane ni jambo la ajabu.

Dk Ndumbaro amewaambia watumishi wa umma kuwa, maendeleo katika sekta yoyote, ikiwamo ya elimu yanakuja na mabadiliko hivyo wayapokee na kufanya kazi ili kufikia lengo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya February 21


Rais Magufuli atoa mil.10/- kwa wananchi Handeni

$
0
0
Rais John Magufuli ametekeleza ahadi yake ya kuwapatia Sh milioni 10 wananchi wa kijiji cha Kwamkonga wilayani Handeni, mkoani Tanga walizoomba Agosti 3 mwaka jana.

Waliomba fedha hizo kwa ajili ya kuboreshewa huduma za afya katika zahanati ya kijiji hicho iliyokuwa na uhaba wa vifaa tiba.

Rais Magufuli alipita katika kijiji hicho kilichopo pembezoni mwa barabara ya Chalinze-Segera na kuzungumza na wananchi hao wakati akielekea mjini Tanga kwa ajili ya uzinduzi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Chongoleani mkoani Tanga hadi Hoima nchini Uganda.

Wananchi hao walimweleza Rais matatizo mbalimbali inayoikabli zahanati yao hasa suala la maabara ambayo walikuwa wakikosa huduma hizo hadi wazifuate katika kituo cha afya Mkata au kwenda katika hospitali ya wilaya Handeni.

Akikabidhi kwa niaba ya Rais, Mkuu wa mkoa wa Tanga, Martine Shigela, alisema Rais alipopewa malalamiko na wananchi kuhusu kuboreshwa zahanati hiyo, ameleta kiasi cha milioni 10 ambacho kimetumika kununua vifaa mbalimbali vinavyopaswa kuwekwa kwenye maabara.

Shigela alisema Rais anajali wananchi wake waliomchagua ndiyo maana ameweza kuleta fedha hizo ili wapatae huduma karibu na vijiji vyao kwa lengo la kupunguza safari za kwenda umbali mrefu kufuata huduma za maabara.

Mganga Mkuu wa wilaya ya Handeni, Dk Credianus Mgimba alisema walipopokea fedha hizo kutoka katika ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Tanga, waliziweka katika akiba ya zahanati ya kijiji hicho ambapo walifanya manunuzi ya vifaa hivyo.

Akitoa shukrani Mkuu wa wilaya hiyo, Godwin Gondwe alimshukuru Rais kwa kutekeleza ahadi hiyo ambayo itawawezesha wananchi wa kijiji hicho na vijiji jirani kupata huduma bora za afya hasa za maabara na kupunguza msongamano katika vituo vya afya na hospitali ya wilaya.

Simanzi Yatawala Mwili wa Kada wa CHADEMA Aliyetekwa na Kuuawa Ukiagwa

$
0
0
Simanzi na vilio vilitawala wakati wa ibada ya kuuaga mwili wa aliyekuwa kada wa Chama cha maendeleo na Demokrasia (Chadema), Daniel John, aliyeuawa na watu wasiojulikana.

John aliuawa wiki iliyopita katika ufukwe wa Bahari ya Hindi, eneo la Coco wakati akitokea katika kampeni za uchaguzi mdogo wa marudio jimbo la Kinondoni na mwili wake uliokotwa katika ufukwe wa Coco.

Wakati mambo yakiwa hivyo katika ibada hiyo iliyofanyika kwenye Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Anna Hananasif, Kinondoni jijini Dar es Salaam, Jeshi la Polisi liliwazuia wafuasi wa Chadema waliotaka kuusindikiza mwili kwa kuusukuma hadi barabara ya Kawawa Kinondoni.

Ibada ya kuuaga mwili wa John, aliyekuwa Katibu wa chama hicho kata ya Hananasif, ikongozwa na Paroko Alistadius Kibangula, viongozi mbalimbali wa Chadema wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, walihudhuria.

Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Makamu Mwenyekiti Chadema Taifa, Prof. Abdalah Safari, Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob.

Akizungumza baada ya ibada, Sumaye alisema chama kimesikitika kwa yote yaliyotokea dhidi ya John.

"Daniel hakufariki (dunia) kwa sababu ya kupigania Chadema, bali alifariki kwa kupigania haki ya Watanzania. Wapo wengi ndani ya Chadema waliofariki dunia kwa kupigania haki,” alisema Sumaye.

Alisema anaamini serikali itafanya uchunguzi pamoja na kutenda haki kwa wote waliohusika na kifo cha Daniel.Naye, Meya Jacob alisema Daniel alikuwa mtaalamu wa siasa za mtaani, na aliishi na watu vizuri.

“Marehemu ndiye aliyechangia ushindi wa Chadema katika uchaguzi wa mwaka 2015 kwa kupata Diwani na Mbunge. Yeye pia ndiye aliyeisambaratisha CCM kata ya Hananasif iliyokuwa inaongozwa na Tarimba,” alisema Jacob.

Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi lililazimika kuwazuia wafuasi wa Chadema, waliotaka kuusindikiza mwili wa John.

Baada ya ibada ya kuaga mwili katika Kanisa hilo, wafuasi wa Chadema walijipanga kwa ajili ya kulisindikiza kwa kulisukuma gari lililobeba mwili wa marehemu John lakini walipofika mtaa wa Tarimba eneo la Kinondoni Muslim, walizuiwa na askari waliokuwa kwenye magari mawili ya wazi.

Askari hao walikuwa katika magari yenye namba PT 3675, pamoja na PT 1686 yote aina ya Toyota Land Cruizer. Polisi hao waliwazuia wafuasi hao na gari lililobeba mwili kuendelea na safari.

Serikali Yatoa Sh. Bil. 2.6 Kuboresha Vituo Vya Afya Jijini Mwanza

$
0
0
SERIKALI imepeleka sh. bilioni 2.6 katika Jiji la Mwanza kwa ajili ya kugharamia uboreshaji wa vituo vya afya ili kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Hayo yalibainika jana (Jumanne, Februari 20, 2018) wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipokagua na kuweka jiwe la msingi la kituo cha afya cha Karume.

Waziri Mkuu alikagua ukarabati wa kituo hicho kilichopo kwenye kata ya Bugogwa wilayani Ilemela akiwa katika siku ya sita  ya ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza.

Alisema uboreshaji huo ulihusisha ujenzi wa chumba cha upasuaji, maabara, chumba cha kujifungulia, jengo la mama na mtoto na wodi ya wanawake na wanaume.

Waziri Mkuu alisema ameridhishwa na uboreshaji wa kituo hicho, ambapo Serikali inatarajia kupeleka sh. milioni 200 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa mbalimbali.

Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha inasogeza huduma za afya karibu na wananchi. Uboreshaji wa kituo cha afya cha Karume umegharimu takriban sh. milioni 497 hadi hivi sasa.

Waziri Mkuu aliongeza kuwa  mkakati wa Rais Dkt. John Magufuli ni kuimarisha sekta ya afya ili kuhakikisha  wananchi wanapata matibabu karibu na maeneo yao ya makazi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndungulile alisema Serikali imetoa sh. bilioni 2.6 kwa ajili ya uboreshaji wa vituo vya afya jijini Mwanza.

Alisema fedha hizo zinalenga kuboresha vituo hivyo ili kuviwezesha kutoa huduma bora kwa wananchi wa jiji zikiwemo huduma za afya ya mama na mtoto, upasuaji na maabara.

Awali, Waziri Mkuu alifungua zahanati ya Bulale iliyopo katika kata ya Buhongwa wilayani Nyamagana na kisha alitoa vitambulisho vya matibabu kwa wazee 250. Jumla ya wazee 5,398 wilayani humo wamepatiwa vitambulisho vya matibabu.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, FEBRUARI 21, 2018.

Waziri Mkuu Awataka Watanzania Kujiepusha Na Dawa Za Kulevya

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania wakiwemo wakazi wa mkoa wa Mwanza kuachana na biashara ya dawa za kulevya.

Pia Waziri Mkuu amegiza vijana nchini waelimishwe madhara mbalimbali yanayosababishwa na matumizi ya dawa za kulevya ili wajiepushe nazo.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana (Jumanne, Februari 20, 2018) alipozindua kliniki ya methadone kwa ajili ya waathirika wa dawa za kulevya.

Alizindua kliniki hiyo iliyopo kwenye hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mwanza ya Sekou Toure akiwa katika siku ya sita  ya ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza.

“Serikali imejizatiti katika vita dhidi ya biashara ya dawa za kulevya, hivyo nawataka wananchi wasijishughulishe nayo. waache kutumia, kusambaza na kuuza.”

Pia aliwaomba wananchi washirikiane na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa kutoa taarifa za watu wanaojihusisha na dawa hizo.

Kwa upande wake, Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Bw. Rogers Siyanga  aliishukuru Serikali kwa kutambua madhara ya dawa za kulevya na kuchukua hatua.

Bw. Siyanga alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa waathirika wa dawa za kulevya kwenda katika kliniki za methadone ili wapatiwe matibabu yatakayowafanya kuachana na matumizi ya dawa hizo.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw. John Mongella alisema kuwa, mkoa huo ni miongoni mwa waathirika wakubwa wa biashara ya dawa za kulevya. Aidha, aliongeza kuwa bado kuna watu wanaoendeea kujishughulisha na biashara hiyo na kwamba Mkoa unaendelea kupambana nao.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndungulile alisema dawa za kulevya zinasababisha madhara makubwa katika sekta ya afya kwa kuwa yanachangia kusambaa kwa magonjwa mbalimbali yakiwemo ukimwi na kifua kikuu.

Pia alisema kwa sasa dawa za methadone zinazotolewa kwa waathirika wa dawa za kulevya wanazipata kutoka kwa wahisani mbalimbali. Hata hivyo, Serikali imepanga kuingiza suala hilo katika bajeti ijayo ili ianze kuagiza yenyewe.

Baadhi ya vijana waliokuwa wanatumia dawa za kulevya mkoani Mwanza akiwemo, Nyamizi Sospeter na Abdul Abdallah, waliishukuru Serikali kwa kuanzisha vituo vya methadone.

Nyamizi alitumia dawa za kulevya kwa muda wa miaka saba na muda wote huo alikuwa akiisumbua familia yake kutokana na matukio mbalimbali ya kihalifu aliyokuwa akiyafanya ili apate fedha za kununulia dawa hizo.

Naye Abdul Abdallah alisema alitumia dawa za kulevya aina ya heroine kwa takribani miaka 20 na muda wote huo alikuwa anakaba watu ili apate fedha za kununulia dawa hizo.

“Naishukuru Serikali kwa kuanzisha kliniki ya methadone na sasa nimeacha mimi pamoja na mke wangu. Najiona binadamu maana nilikuwa mwizi, mchafu kwani nilikuwa nakaa mwezi bila kuoga na hata kutengwa na jamii.”

Kwa pamoja waathirika hao wa dawa za kulevya waliiomba Serikali kuwasaidia kwa kuwapa elimu ya ujasiriamali ili waweze kupata ujuzi utakaowawezesha kufanya kazi na kupata kipato kitakachowasaidia kuendesha maisha yao.

Awali, Waziri Mkuu alizindua muongozo wa uendeshaji wa nyumba za waathirika wa dawa za kulevya (Soba Houses) ambao unalenga kuwawezesha wamiliki wa nyumba hizo kuziendesha vizuri na kuwasaidia ipasavyo.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, FEBRUARI 21, 2018.

Meya wa Ubungo aishambulia Serikali....."Wanaenda tu kupiga picha kwa Akwilina hawaji kwenye msiba wa CHADEMA "

$
0
0
Meya wa Ubungo, Boniphace Jacob amesema kuwa viongozi wengi wa serikali wanapendelea upande mmoja wa msiba wa Akwilina kwani hata wao chadema wamekuwa wakipata misiba lakini serikali haitoi pole wala kuwafariji wafiwa.

Ameyasema hayo jijini Dar es salaam  jana wakati wa kuaga mwili wa kada wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA), Daniel John.

Alisema kuwa kitendo cha viongozi wa serikali kutoenda kutoa pole katika familia ya Daniel John na kuegemea upande mmoja wa msiba wa familia ya Akwilina ni fedhea kubwa.

“Kwakweli hii ni fedhea kubwa sana kwa viongozi wa serikali kuegemea upande mmoja kwenye msiba wa Akwilina, hii si haki kwani wangekuja hata huku kutoa angalau salamu za pole na kuwafariji wafiwa, kwani kifo cha Daniel kinasikitisha sana,”alisema Jacob 

==>Msikilize hapo chini
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images