Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Salamu za Shukrani na Pongezi toka CCM kwa Ushindi wa Kishindo katika Majimbo ya Siha, Kinondoni na Kata Kumi


Video: Diamond akionesha vifaa vya gharama vya Wasafi radio na Wasafi TV

0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva nchini, Diamond Platinumz ambaye anafanya vizuri katika sanaa ya muziki, anaendelea kuonesha umahiri katika kazi yake kwa kuendelea kukuza na kutanua soko la ajira Tanzania kwa ujasilia mali.
 
Hivi karibuni ametambulisha ujio wa kituo chake cha radio, Wasafi Fm, na kituo cha TV cha Wasafi TV.
 
Harakati hizo zipo mbioni kukamilika mara baada ya kutumia ukurasa wake wa instagram kuonesha mitambo mbalimbali ambayo tayari imefungwa kuruhusu chaneli hizo kuanza rasmi kurusha vipindi vyake.

==>Tazama kila kitu hapo chini

    Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

    0
    0
    Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

    NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

    MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

    MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

    NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

    Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

    DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

    Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

    0
    0
    TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
     
    FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
     
    NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

     TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

    SORRY MADAM -Sehemu ya 98 & 99 (Destination of my enemies

    0
    0
    MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
    ILIPOISHIA

       Kila mtu moyo wake ulizidi kumuenda mbio akiwa ndani ya gari hilo. Madam Mery taratibu akajikuta akianza kusali sala yake ya mwisho kwa maana wanapo elekea kifo kipo mbele yao.
    “Fanya uwashe gari”
    Manka alizungumza huku machozi yakianza kumwagika, kila jinsi dereva alivyo jaribu kuwasha gari lake, halikuwaka hadi ikafika kipindi akakata tama kabisa. Matairi ya mbele tayari yalisha anza kuelea hewani kwenye korogo hilo linalo endelea kulika taratibu taratibu na matairi ya nyuma pekee ndio yapo kwenye ardhi.
    “Ohoo Mungu wangu tunakufa”
    Manka alizungumza huku akiyafumba macho yake, akisubiria gari hiyo kuangukia kwenye korongo hilo na huo ndio utakuwa ni mwisho wa maisha yao.

    ENDELEA
           Wakiwa katika hali ya sinto fahamu, gafla wakastukia watu wawili wa kiwa nyima yao wakijitahidi kulishika gari hilo kwa nyuma. Walipo geuka wakawaona Shamsa na Eddy ambaye Manka anamtambua kwa jina la Ericksom. Kwa ishara Shamsa akawa anawaomba wateremke.
    Madam Mery akawajibu kwa vitendo kwamba hawawezi kushuka kutokana milango imejifunga na hakuna kitu chochote kinacho weza kufanya kazi ndani ya gari hilo.
    “Tunafanyaje sasa Eddy?”
    “Tafuta jiwe uvunje kioo”
    “Sawa”
    Shamsa akaanza kutafuta jiwe ambalo linaweza kupasua kioo cha gari hilo, kwa bajati nzuri akapata jiwe moja kubwa, kwa haraka akarudi nalo hadi sehemu ilipo gari.
    “Vunja kioo kimoja wapo”

    Eddy alizungumza huku jasho likimwagika, kwa maana shuhuli ya kuizuia gari hilo lisitumbukie kwenye korongo hilo ni kubwa sana kwake. Kila Shamsa alivyo jaribu kupasua kioo cha upande alio kaa madam Mery, hakikupasuka wala kuonyesha dalili ya mpasuko.
    “Mungu wangu gari hii ni bullet proff na haaingia risasi, ndio maana kioo chake hakipasuki.”
    Shamsa alizungumza huku machozi yakimlenga lenga, kwa maana juhudi anazo zifanya zimekuwa ni bura kabisa. Gafla taa za nyuma ya gafi hizo zikaanza kuwaka, dereva kwa haraka akajaribu kuminya kitufe cha kufungua milango hiyo akafanikiwa. Manka akajirusha nje, madam naye akafanya hiyo hivyo, shuhuli ikawa kwa dereva ambaye amekaa siti ya mbele kabisa. Uzito ulizidi kuongezeka pale alipo kuwa kwenye harakati za kutaka kuhamia siti ya nyuma ili atoke kwa maana milango yote ya mbele endapo ataifungua na kujaribu kutoka basi safari yake ni moja kwa moja hadi kwenye korongo hilo.

    “Nisa…..iidi…..eeeni”
    Eddy alizungumza huku akijikaza kadhi ra uwezo wake kuhakikisha kwamba analizuia gari hilo lililo anza kusogea mbele taratibu likelekea kudumbukia kwenye korongo hilo.
    Wote watatu wakaanza kulishika gari hilo kwa nyuma sehemu ambapo Eddy amepashika. Dereva huyo ambaye alisha anza kukinusa kifo kwa haraka haraka akajirusha siti ya nyuma na kujirusha nje. Kitendo cha yeye kutoka Eddy na wezake wakaliachia gari hilo na likadumbukia kwenye korongo hilo refu kwenda chini.
    “Ohooo honey”
    Manka alizungumza huku akimkumbatia Eddy kwa nguvu. Shamsa akataka kuwaachanisha ila madam Mery akamshika mkono na kutingisha kichwa akimuashiria kwamba asifanye chochote. Askar wengine kutoka ikulu nao wakafika eneo hilo wakiwa na bunduki zao mikononi. Shamsa alipo waona askari hao akataka kuondoka ila askari mmoja akamshika bega.

    “Subiri mwaya”
    Kumbe sababu ya askari huyo kumshika Shamsa bega ni kutokana na Manka kumuonyeshea askari huyo kwa ishara amzuie asiondoke eneo hilo. Manka akaachiana na Eddy na kumfwata Shamsa pale alipo simama.
    “Asante kwa kuyasaidia maisha yetu”
    “Usijali ni kitu cha kawaida”
    Manka akampa mkono Shamsa, aliye upokea taratibu. Wakaachiana mikono huku Manka akionekana kumtazama Shamsa usoni. Kumbukumbu zake zikarejea hadi pale hospitalini, alipo weza kumuona Shamsa akiwaangusha walinzi wawili walio pewa kazi ya kumlinda akiwa na Erickson ndani. Kumbukumbu zake hazikuishia hapo akakumbuka jinsi walivyo pambana ndani ya chumba hicho ili asichukuliwe Erickson ila walipo ingia Madam Mery na binti mwengine wa Kijapani hapo ndipo walipo mzidi nguvu na kuondoka naye.

    “Weeee……..”
    Manka hadi anastuka kutoka kwenye dimbwi la mawzo, tayari Shamsa alisha ondoka eneo hiloakijichanganya watu wanao shangaa shangaa kilicho tokea.
    “Mtafuteni yule binti sasa hivi”
    Manka alitoa amri kwa askari wake kutoka ikulu ambao walianza kutawanyika kumfwatilia ni wapi Shamsa alipo elekea huku wengine wanne wakibakia katika eneo hilo wakiimarisha ulinzi dhidi yake.
    Eddy na Madam Mery walibaki kukonyezana kwa maana waliweza kumshuhudia Shamaa akiondoka eneo hilo baada ya Eddy kumpa ishara ya kukimbia huku akimkabidhi funguo za gari la dokta pasipo mlinzi au mtu mwengine yoyote kuweza kuona tukio hilo.

    “Erickson…….!!!”
    Manka alimuita Eddy huku akiwa amemkazia macho na kumtazama kwenye upande wa kushoto wa koti jeupe alilo livaa.
    “Nini?”
    Eddy aliuliza huku akiteremsha macho yake kuangalia ni kitu gani kinacho endelea. Eddy macho yakamtoka, wasiwasi ukamjaa mwingi, hii ni baada ya kuona damu nyingi ikiwa imelowanisha koti hilo alilo vaa ikiashiria kwamba mshono wake umepata tatizo ambalo ni kubwa sana. Kwa haraka walinzi wa Manka wakamchukua Eddy huku wakimsaidia kushika pande zote mbili za mikono yake na kuondoka naye hadi kwenye magari yao yalipo huku Manka na Madam Mery wakimfwata kwa nyuma.
    “Madam tumpeleke hospitali gani?”
    Dereva alizungumza huku wakiwa wote tayari wamesha ingia kwenye gari hilo.
    “Wewe twende tu”
    Manka alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake kila alipo mtazama Erickson wake aliye laza kichwa mapajani mwake na kujikausha kimya asizungumze chochote
                                                                                                                ***
    “Mkuu hatujaweza kumpata kiongozi na hali iliyo jitokeza huku naamni kwa sama ninaamini muna ishuhudia kwneye televishion”

    Mmoja wa vijana wa kikosi maalumu kutoka D.F.E walio tumwa kuweza kumuokoa mzee Godwin alizungumza na simu akiwasiliana na John ambaye yupo kwenye ukumbi wa kutano Serena Hotel akiwa na viongozi wengine wakisuribia kuweza kupata matokeo mazuri kama mzee Godwin amapatikana au laa.
    “Ondokeni eneo hilo, na sura zenu zisionekane kwenye televishion”
    “Sawa mkuu”
    Kijana huyo akakata simu, kwa haraka akelekea kwenye uapende wa pili wa barabara, alipo waacha wezake ndani ya gari, wakiwa wamenuusurika kudumbukia kwenye korongo hilo lisa moja lililo kwisha kupita.
    “Vipi wamesemaje?”
    “Wamesema tuondoke sura zetu zisionekane eneo hili wala kwenye televishion”
    “Poa”
    Dereva akawasha gari na wakaondoka eneo hilo. Mmoja wao aliye kaa siti ya mbele pembeni ya dereva akashusha pumzi kisha akaanza kuzungumza.

    “Jamani hivi munajua laiti tungesubutu kukomaa na wale makachero wa kwanza kuingia ndani mule ya msitu na sisi habari yetu ingekuwa imesha kichwa?”
    “Kweli mwanagu, kwa maana tangu nizaliwe sijawahi kuona bomu la namna hii”
    “Yaani muda ule nilipo anza kuuona ule mpasuko wa ardhi, akili yangu ilinituma kwa haraka kurudisha gari nyuma hadi tukafika barabarani”
    “Nasikia waseng** wote walio kuwemo ndani ya msitu wamedanja”
    “Weee kwa timbwili lile unahisi wasinge danja”
    “Alafu kumbe mtoto wa mzee alikuwepo”
    “Nani?”
    “Manka, naye angeenda na maji”
    “Aisee tuache utani ila lile toto ni lizuri”
    “Anaye lila lile naamini kwamba ana faidi ile mbaya”
    “Kweli, ukishikilia ile mitako na mihispi, mamayeee”
    “Acheni ujinga nyinyi tufikirie ni jinsi gani tunaweza kumpata mzee”
    Mkuu wao alizungumza na kuyakatisha mazungumzo ya vijana wake ambao wote wanamezea mate Manka mtoto wa bosi wao ambaye ni Mzee Godwin.

    Ndugu wagoma kuchukua mwili wa Akwilina

    0
    0
    Ripoti maalum ya uchunguzi kuhusu kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini imezua kizungumkuti katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ulipohifadhiwa baada ya ndugu wa marehemu kuelezwa kuwa majibu ya ripoti hiyo yatatolewa baada ya siku 14 huku baadhi yao wakipinga jambo hilo na kutaka wapewe leo.

    Wakizungumza  leo Februari 19, 2018 baada ya postmortem ya uchunguzi huo, ndugu wa Akwilina waliokuwa wamekusanyika Muhimbili karibu na eneo la chumba cha kuhifadhia maiti wakisubili ripoti, wameeleza kusikitishwa kwao na uamuzi huo huku wakilalamika na kuhoji kwa nini wasipewe ripoti hiyo leo ili wakazike mwili wa ndugu yao.

    “Tumeambiwa na daktari tayari uchunguzi umeshakamilika, tuchukue mwili tukazike, lakini wanasema majibu yatatoka baada ya siku 14. Hivi tukienda tukizika tutawaambiaje waombolezaji na ndugu wengine, kwamba ndugu yetu alikufa je?” alisema ndugu mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake litajwe.

    Kwa upande wa Mkuu wa  NIT, Prof. Zakaria Mganilwa amesema uongozi wa chuo hicho umeungana na familia kuhakikisha wanampumzisha Akwilina huku akifanya jitihada za kuzungumza na madaktari na ndugu wa marehemu kufanikisha zoezi la kuchukua mwili na kwenda kuuzika.

    “Ripoti juu ya kifo chake madaktari wanasema itakuwa tayari baada ya siku 14 hivyo wakawa wamewaruhusu ndugu kuchukua mwili huo ili wakazike lakini ndugu wa marehemu wanasema hawawezi kuchukua mwili mpaka wajue yaani ripoti itoke ndiyo waweze kuchukua mwili kwa hiyo bado wanaendelea kufanya majadiliano na mamlaka husika,” alisema Profesa Zacharia.

     

    Akwilina alifariki dunia Februari 16, 2018 baada ya kupigwa risasi kichwani akiwa kwenye daladala wakati polisi wakiwatawanya waandamanaji ambao ni wafuasi wa Chadema.

    Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

    0
    0
    Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

    Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

    MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

    SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

    KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

    CHADEMA yatoa ratiba ya mazishi ya Kiongozi wao Aliyetekwa na Kuuawa

    0
    0
    Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kinatarajia kuongoza shughuli za utoaji wa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Katibu wa chama hicho Kata ya Hananasif Jimbo la Kinondoni, Daniely John siku ya kesho (Jumanne).

    Hayo yamebainishwa na taarifa zilizotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano, Tumaini Makene jioni ya leo (Jumatatu) na kudai mwili wa marehemu Daniel unatarajiwa kufika nyumbani kwake Hananasif ukiwa unatokea hospitali ya Taifa Muhimbili majira ya saa 4 asubuhi na kisha kupelekwa katika Kanisa la Katoliki kwa ajili ya misa ya kumuombea marehemu itakayoanza saa 5 asubuhi kanisani hapo.

    Baada ya ibada hiyo, waombolezaji watatoa heshima zao za mwisho kwa Daniel kabla ya mwili wake kusafirishwa kwenda mkoani Iringa ambako atazikwa siku ya Jumatano, katika kijiji cha Chikelewatu wilayani Mafinga.

    Kwa taarifa kamili soma hapo chini.

    Waziri Mkuu amsimamisha kazi Mwanasheria........Ni baada ya kuisababishia halmashauri hasara ya sh. milioni 279

    0
    0
    WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi Bw. Alphonce Sebukoto na kuagiza achungunzwe na vyombo husika.
     
    Amechukua hatua hiyo baada Mwanasheria huyo kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo ikiwa ni pamoja na kushindwa kuishauri vema halmashauri hiyo na kuisababishia hasara ya sh. milioni 279.

    Waziri Mkuu amemsimamisha kazi Bw. Sebukoto leo (Jumatatu, Februari 19, 2018) wakati akizungumza na watumishi na madiwani wa halmashauri hiyo akiwa katika siku ya tano ya ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza.

    “Mwanasheria utasimama kazi kuanzia leo na tuhuma zako zitachunguzwa kikamilifu na vyombo husika na uchunguzi ukibaini kama huna kosa utarudi kazini. Hatuta kuonea lakini hatuwezi kukuvumilia kwa utaratibu huo ulioufanya.”

    Amesema mwanasheria huyo Novemba 2017 wakati alipokuwa anakaimu nafasi ya ukurugenzi aliidhinisha malipo ya sh.milioni 279 zilipwe katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw. Anthony Bahebe.

    Waziri Mkuu amesema Bw. Bahebe aliishtaki halmashauri hiyo akidai kulipwa fedha kwa ajili ya kazi ya ukandarasi wa mradi wa maji Igenge uliojengwa na kampuni ya ukandarasi ya Seekevim.

    Amesema mradi huo ulianza 2014 na ulitakiwa ukamilike 2015. Mwanasheria huyo aliidhinisha malipo hayo wakati ambao tayari hati maalumu ya uwakilishi ilikuwa imekwisha tangu Desemba 2015.

    “Mwanasheria amemlipa Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kufanya kazi na Halmashauri baada ya kuifikisha Halmashauri yake Mahakamani. Amemlipa fedha wakati kazi yenyewe ilikuwa haijaisha na aliharakisha malipo hayo kipindi ambacho Mkurugenzi hayupo.”

    Waziri Mkuu amewakumbusha watumishi wa umma kuzingatia maadili ya utumishi na matakwa ya kisheria katika utekelezaji wa majukumu yao. Amesema fedha alizolipwa Bw. Bahebe zingeweza kutumika katika ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika halmashauri hiyo.

    Awali, Waziri Mkuu alifungua mabweni ya watoto wenye mahitaji maalumu katika shule ya msingi Mitindo iliyoko wilayani Misungwi na kisha alikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa.

    (mwisho)
    IMETOLEWA NA:
    OFISI YA WAZIRI MKUU,
    JUMATATU, FEBRUARI 19, 2018.

    Taarifa Toka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais IKULU

    0
    0
    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Makenya Abraham Honoratus Maboko kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH).

    Uteuzi wa Prof. Maboko unaanza leo tarehe 19 Februari, 2018.

    Pro. Maboko ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

    Gerson Msigwa
    Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
    Dar es Salaam
    19 Februari, 2018

    Hatimaye Ndugu Wamekubali Kuuchukua Mwili wa Mwanafunzi Aliyepigwa Risasi

    0
    0
    Ndugu wa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline aliyepigwa risasi na Polisi Februari 16, 2018 wameeleza ndugu yao alifariki dunia baada ya kupigwa risasi kichwani.

    Wametoa ufafanuzi huo leo Februari 19, 2018 muda mfupi baada ya kususa kupokea mwili wa mwanafunzi huyo uliokuwa ukifanyiwa uchunguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) bila kuelezwa nini kilichomuua.

    Wakizungumza mara baada ya maafikiano baina yao na madaktari, wamesema wamepewa sehemu ya ripoti ya uchunguzi ambayo wameridhika nayo na sasa wanakwenda kufanya kikao cha ndugu kujadili namna gani watampumzisha Akwilina.

    Shemeji wa mwanafunzi huyo, Festo Kavishe amesema uchunguzi wa mwili huo, umeonyesha kwamba Akwilina alijeruhiwa vibaya kichwani.

    "Ripoti ambayo tumepewa imeonyesha kwamba kichwa cha marehemu kilipasuliwa vibaya na risasi ambayo iliingilia upande wa kushoto kwa kichwa chake na kutokea upande wa kulia  ambao umefumuka vibaya," amesema.

    Kwa mujibu wa Kavishe, iwapo madaktari wasingewapatia majibu hayo wasingethubutu kuuchukua mwili huo kwa mazishi, kwa sababu walihitaji kupata picha kamili ya nini kilimuua Akwilina.

    "Sasa tumeshafahamu nini hasa kimemuua ndugu yetu kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na madaktari baada ya uchunguzi, hivi sasa tunakwenda kujadiliana kuhusu mazishi yake," amesema Kavishe.

    Akwilina alifariki dunia Februari 16, 2018 baada ya kupigwa risasi kichwani akiwa kwenye daladala wakati polisi wakiwatawanya waandamanaji ambao ni wafuasi wa Chadema.

    Baba wa Akwilina atamani kukutana na Polisi Aliyempiga Risasi Mwanaye ili Amng'ate hata Meno Tu

    0
    0

     Akwilini Shirima ambaye ni baba mzazi wa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline aliyepigwa risasi na polisi Februari 16, 2018 amesema siku akikutana na askari aliyemuua mwanaye atapambana naye hadi kifo.

    Akizungumza leo Februari 19, 2018 nyumbani kwake Kijiji cha Olele, Shirima alisema endapo muuaji atakuwa ni kijana mwenye nguvu kumzidi, atapambana naye hata kwa kumuuma kwa meno.

    "Najua ni ngumu kukutana na aliyempiga mwanangu risasi, lakini laiti ningekutana naye kama ni kijana mwenye nguvu kunizidi nitapambana naye hata kumuuma kwa meno,” amesema.

    “Kama ni mzee mwenzangu nitapambana naye hadi kifo ila kwa bahati mbaya siwezi kumpata, hivyo sina namna. Kwa kweli hiki kifo kimezima ndoto ya familia ya kuondokana na umasikini.”

    Shirima ameiomba Serikali kuliangalia suala hilo kwa kina na kuona namna ya kumsaidia kwa kuwa tegemeo lake limeondoka na wao kwa sasa hawana msaada wowote na wanachosubiri ni kifo.

    "Jamani hii ni taa yangu imezimika na kuniacha gizani kwani toka nimepata taarifa za kifo chake sijaweza kula chochote. Nimekuwa kama nguruwe aliyetelekezwa porini bila msaada," amesema.

    "Nilipopata taarifa za kifo cha mwanangu nilishtuka sana na kuhoji ni mwizi au nini kimetokea, lakini baadaye nikaambiwa ni Serikali imefanya mambo hayo. Imenitia uchungu sana na siwezi hata kula"

    Shirima amesema ni afadhali mwanaye angeugua akamuuguza kuliko kifo cha ghafla alichokipata ambacho kimewaacha kwenye hali ambayo haitafutika mioyoni mwao katika maisha yao yote.

    Mama wa marehemu, Costanzia Akwilini amesema mauaji ya mwanaye ni ya kinyama na bora angekuwa mbuzi angekula nyama kujifariji kuliko kwa mwanaye ambaye hakuna anayeweza kumfuta machozi.

    "Mwanangu hakuwa mwanasiasa ameuawa akiwa kwenye gari akielekea kwenye shughuli zake, familia tulijinyima tukajichanga kwa kushirikiana na majirani ili asome aje atukomboe,” amesema.

    “Leo nasubiria niletewe maiti kwenye jeneza. Kwa kweli imeniuma sana na kunikatisha tamaa. Naomba Serikali itende haki katika tukio hili," amesema mama wa marehemu katika mahojiano hayo.

    Akwilina alifariki dunia Februari 16, 2018 baada ya kupigwa risasi kichwani akiwa kwenye daladala wakati polisi wakiwatawanya waandamanaji ambao ni wafuasi wa Chadema.
     
    Credit: Mwananchi

    Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya February 20

    Viongozi wa CHADEMA Akiwemo Mbowe na Katibu Mkuu waitwa Polisi Kwa Mahojiano

    0
    0
    Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe pamoja na viongozi wengine sita wa chama hicho wameitwa na Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum Dar kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu tuhuma zinazowakabili za kufanya maandamano kinyume cha sheria.

    Bariadi Wampa Heshima Makamu Wa Rais...... Barabara Yapewa Jina La Samia

    0
    0
    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akishuhudia barabara iliyopewa jina lake Bariadi mjini ikiwa siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Simiyu. 
    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akishuhudia barabara iliyopewa jina lake Bariadi mjini ikiwa siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Simiyu.
    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka pamoja na Watoto wa Mji wa Bariadi mara baada ya hafla fupi ya Barabara kupewa jina la Samia Suluhu Avenue. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

    Makamu Wa Rais Awahakikishia Wananchi Upatikanaji Wa Dawa Za Kuuwa Wadudu Waharibifu Wa Pamba

    0
    0
    Na Stella Kalinga, Simiyu
    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Simiyu kuwa Serikali itamaliza kabisa tatizo la uhaba wa dawa za kuuwa wadudu waharibifu wa zao la pamba.
     
    Mhe. Makamu wa Rais ameyasema hayo jana wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Busega kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Lamadi wakati akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake Mkoani Simiyu.
     
    Amesema awamu ya kwanza ya dawa zimeshafika Simiyu kwa ajili ya kuwagawia wakulima wa pamba na akaahidi kuwa awamu ya pili ya kuleta dawa hizo inamalizika katika wiki iliyoanza jana tarehe 19/02/2018, hivyo tatizo hilo litakuwa limekwisha.
     
    “Ninajua kuna kiasi kikubwa cha dawa kinakuja Simiyu dawa itakuwa nyingi na wakulima wote watapata, hatuwezi kuacha nguvu zenu zipotee bure na kwa kuwa Simiyu ni mkoa wa Viwanda na ndiyo unazalisha pamba kwa wingi tutajenga viwanda vinavyotumia pamba, kwa maana hiyo hatuwezi kuiacha pamba iharibike” alisema.
     
    Katika hatua nyingine Mhe.Makamu wa Rais wakati akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Masanzakona baada kuweka  jiwe la msingi mradi wa maji wa Kiloleli amewahimiza wananchi kuchangia huduma za maji ili miradi ya maji iwe endelevu.
     
    Alisema Serikali imedhamiria kumaliza kabisa tatizo la maji hapa nchini kwa kujenga miradi ya maji  hivyo ni vema wananchi wakaunga mkono juhudi za Serikali kwa kuchangia huduma za maji ili kusaidia miradi hiyo kujiendesha. 
     
    Akiwasilisha taarifa ya mradi wa Kiloleli kwa Makamu wa Rais, Mhandisi wa Maji Wilaya ya Busega, Mohammed Said alisema mradi huo utagharimu jumla ya shilingi bilioni 1.6 mpaka kukamilika kwake mwezi Machi 2018  na utawahudumia wananchi wa vijiji vitatu vya Yitwimila B, Ihale na Ijitu.
     
     Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Busega, Mbunge wa Busega Mhe. Raphael Chegeni alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli kwa kutekeleza ahadi aliyoitoa kwa wananchi wakati wa kampeni ya kuwapelekea mradi wa Maji wananchi wa kata ya Kiloleli.
     
    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameanza ziara ya kikazi ya siku nne(04) mkoani Simiyu, ambapo amepata fursa ya kuzungumza na wananchi pamoja na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Wilaya ya Busega na Bariadi.

    MWISHO

    TRA Yataifisha Tena Gari Na Bidhaa Mpakani Namanga

    0
    0
    Na: Veronica Kazimoto ,Arusha
    Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kwa mara nyingine ndani ya wiki mbili imekamata na kutaifisha tani moja ya sukari, mafuta ya kupikia katoni 10 na gari lililotumika kusafirisha bidhaa hizo kutoka nchini Kenya kupitia njia za magendo mpakani Namanga mkoa wa Arusha.

    Meneja Msaidizi wa Forodha mkoani hapo Edwin Iwato alisema bidhaa hizo zimekamatwa usiku wa kuamkia jana  na ni mali ya mfanyabiashara Paul Swai, ambaye alitumia gari namba T 496 AFE Nissan Carravan mali ya Christian Nko ambalo limetaifishwa pamoja na bidhaa husika.

    "Tumemkamata mfanyabiashara mwingine aitwae Paul Swai akiwa anaingiza nchini bidhaa kutoka Kenya kuelekea mkoani Arusha kupitia njia za magendo bila kibali wala kulipa ushuru wa Serikali", alisema Iwato.

    Iwato amefafanua kuwa tani moja iliyokamatwa ambayo ni mifuko 20 ya sukari ina thamani ya shilingi 2,200,000 na mafuta ya kupikia ambayo ni kilogramu 12 yana thamani ya shilingi 520,000.

    Mfanyabiashara huyo pamoja na dereva wa gari lililotaifishwa watachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria ya Forodha na bidhaa  hizo baada ya kukaguliwa na kugundulika kuwa zinafaa kwa matumizi ya binadamu zitagawiwa kwa taasisi mbalimbali za Serikali zenye uhitaji kwa mujibu na taratibu zilizowekwa na TRA.

    Hii ni mara pili katika mwezi huu ambapo Mamlaka ya Mapato Tanzania imekamata na kutaifisha bidhaa mbalimbali zikitokea nchini Kenya kupitia njia za magendo mpakani Namanga mkoa wa Arusha.

    MWISHO.

    Waziri Mkuu: Vijiji Vyote Kupatiwa Maji Safi Na Salama

    0
    0
    WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewahakikishia wananchi wa wilaya ya Misungwi kuwa vijiji vyote vitapatiwa huduma ya maji safi kupitia miradi inayotekelezwa katika wilaya hiyo ukiwemo wa Mbarika-Misasi utakaogharimu sh. bilioni 12.4.
     
    Alitoa kauli hiyo  jana (Jumatatu, Februari 19, 2018) wakati akizungumza na wananchi mara baada ya kuweka jiwe la ujenzi wa mradi huo akiwa katika siku ya tano ya ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza. Mradi huo unatarajiwa kuhudumia vijiji 12.

    Vijiji hivyo ni Igenge, Lutalutale, Bugisha, Ngaya, Ikula, Sumbugu, Matale, Kasololo, Isuka, Nduha, Manawa na Misasi ambapo jumla ya wakazi 47,011 wanatarajiwa kunufaika na mradi huo.

    Alisema Serikali ya Awamu ya Tano ina mikakati mizuri inayolenga kumaliza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo mbalimbali nchini vikiwemo vijiji vya wilaya ya Misungwi ili kuwawezesha wananchi hasa wanawake kushiriki katika shughuli za maendeleo kuliko kutafuta maji.

    Waziri Mkuu alisema Serikali kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo, itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini wanapata huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao.

    Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Misungwi, Bw. Eliud Mwaiteleke alisema mradi huo umegawanyika katika miradi midogo minne ambayo ni Igenge, Mbarika-Ngaya, Ngaya-Matale na Matale-Manawa-Misasi.

    Alisema shughulli zilizokamilika ni pamoja na ujenzi wa vituo 48 vya kuchotea maji, matanki mapya manne na moja limekarabatiwa pamoja na mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilomita 73,087.

    Awali, Waziri Mkuu aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kata ya Gulumungu katika kijiji cha Nyamayinza, ambapo aliwapongeza wakazi wa kata hiyo kwa uamuzi wa kujenga shule, ambayo itawawezesha watoto wao kupata elimu.

    (mwisho)
    IMETOLEWA NA:
    OFISI YA WAZIRI MKUU,
    JUMANNE, FEBRUARI 20, 2018.

    Waziri Mkuu Atembelea Kiwanda Cha Nyama Misungwi.....Kina Uwezo Wa Kuchinja Ng’ombe 600 na kondoo 900 Kwa Siku

    0
    0
    WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea na kukagua kiwanda cha kusindika nyama cha Kampuni ya Chobo Investment kilichpo wilayani Misungwi chenye uwezo wa kuchinja ng’ombe 600 mbuzi na kondoo 920 kwa siku.
     
    Alitembelea kiwanda hicho kinachomilikiwa na wazawa jana (Jumatatu, Februari 19, 2018) wakati akiwa katika siku ya tano ya ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza. Alisema amefarijika na uwekezaji huo.

    Alisema uwekezaji wa aina hiyo ulikuwa unasubiriwa sana nchini kwa sababu unakwenda kupunguza tatizo la wafugaji kutokuwa na soko la uhakika wa mifugo yao, hivyo Serikali itamuunga mkono ili kiwanda hicho kiwe endelevu.

    Waziri Mkuu alisema Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza sera ya uchumi wa viwanda na inahamasisha wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza katika viwanda mbalimbali, ambapo aliipongeza kampuni hiyo kwa kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano za kukuza uchumi kupitia sekta ya viwanda

    Akizungumzia kuhusu changamoto ya kutokuwa na maeneo ya kunenepeshea na kulisha mifugo yao, Waziri Mkuu alisema tayari alishamuagiza Waziri wa Mifugo Bw. Luhaga Mpina kushughulikia suala hilo na kwamba litapatiwa ufumbuzi.

    Pia Waziri Mkuu aliwataka watumishi waliojiriwa katika kiwanda hicho wafanye kazi kwa bidii, wawe waaminifu na waadilifu.

    Awali, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Bw. John Chobo alisema kiwanda hicho kinakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji, hivyo kinategemea maji ya kisima au ya kuletwa na boza kutoka Mwanza mjini jambo ambalo linachangia katika kuongeza gharama za uzalishaji.

    Baada ya kutoa malalamiko hayo Waziri Mkuu alimuagiza Mkurugenzi wa MWAUWASA, Mhandisi Anthony Sanga  kushughulikia suala hilo na ahakikishe kiwanda hicho kinapata maji. Kiwanda hicho kipo umbali wa kilomita nne kutoka Ziwa Victoria.

    Akizungumzia kuhusu changamoto ya eneo la kulishia na kunenepeshea ng’ombe Bw. Chobo alisema kampuni yake iliomba kupatiwa eneo kutoka kwa Serikali tangu mwaka 2014 karibu na kiwanda hicho lakini hadi sasa hawajapatiwa.

    Kiwanda hicho kinauza bidhaa zake ndani na nje ya nchi. Nchi hizo ni Oman, China, Canada na Misri. Baadhi ya wanunuzi hao kutoka Omani ni Bw. Tahir Al Hashim na kutoka China ni Bw. Kingsong Shao walisema nyama inayochakatwa kiwandani hapo ni nzuri na ina ubora wa kimataifa.

    Pia kiwanda hicho kinasambaza nyama katika migodi yote mikubwa nchini ambayo awali ilikuwa inaagiza nyama kutoka nje ya nchi, hivyo, Mkurugenzi wa kiwanda hicho aliiomba Serikali kuwasaidia katika kulinda soko la ndani.

     (mwisho)
    IMETOLEWA NA:
    OFISI YA WAZIRI MKUU,
    JUMANNE, FEBRUARI 20, 2018.

    Makamu Wa Rais Aagiza Kila Shule Ya Sekondari Kuwa Na Maabara

    0
    0
    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka Viongozi wa mkoa wa Simiyu kuhakikisha kila shule ya sekondari inayojengwa inajengwa ikiwa na maabara.

    Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati akiwahutubia wananchi Lamadi wilaya ya Busega mkoani Simiyu ikiwa siku yake ya kwanza ya ziara ya siku tano mkoani humo.

    Makamu wa Rais ambaye alianza ziara yake kwa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa maji uliopo Kiloleli ambapo mradi huo ukikamilika utasaidia kupatikana kwa maji safi na salama kwa vijiji vitatu na utagharimu shilingi za kitanzania bilioni 1.6 ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 80%.

    Makamu wa Rais aliwapongeza wananchi kwa kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano katika uwekezaji na uendelezaji wa viwanda ambapo mpaka sasa kuna viwanda 14 vya usindikaji wa pamba na viwanda vidogo vidogo vya usindikaji mazao 1,035.

    “Nawapongeza kwa mkakati wa kuzalisha bidhaa za afya zinazotokana na pamba na maji ya drip”

    Makamu wa Rais aliwaambia wananchi hao kuwa hadi mwisho wa mwezi huu chupa milioni 2 za dawa za kuuwa wadudu wanaoshambulia pamba zitakuwa zimesambazwa.

    Mwisho Makamu wa Rais aliwataka Viongozi na Watendaji kushirikiana na wananchi. Katiak Ziara hiyo Makamu wa Rais aliweka pia jiwe la msingi la ujenzi wa Nyumba za Viongozi wa Serikali zilizopo Nyaumata.
    Viewing all 45270 articles
    Browse latest View live




    Latest Images