Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

SORRY MADAM -Sehemu ya 90 & 91 (Destination of my enemies)

$
0
0

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA  

“Na tambua Eddy nimesha mfahamu, na Eddy huyo huyo ndio atakaye kuja kuja kukuangamiza, na kuanzia hivi sasa usinihusishe na mipango yako ya kikatili”
Manka alizungumza kwa hasira huku akijikongoja kutoka mlangoni ila kabla hajafika mlangoni huku nyuma akasikia bastola  ikikokiwa, taratibu akageuka na kumkuta Mzee Godwin akiwa amemnyooshea bastola ya uso, huku macho yam zee Godwin yakiwa yametawaliwa na ukungu mwekundu wa hasira hadi mkono wake ulio shika bastola ukawa unatetemeka.

ENDELEA
“Na mimi unahitaji kuniua, kama unavyo hitaji kumuua Eddy?”
Manka alizungumza huku machozi yakimwagika, Mzee Godwin akaendelea kumshikilia Manka bastola huku akizidi kutetemeka kwa hasira.
“Kwa nini hukumuua Mery nilipo kuagiza pale Arusha?”
“Damu ni nzito kuliko maji baba, na Mungu aliweza kunipa roho ya ujasiri ya kumuacha akiwa hai, kumbe ni mama yangu mdogo. Nimekua bila ya kuwa na mama, ila wewe hulioni hilo hadi unahitaji nimuue mama yangu mdogo si ndio?”

Hasira ya Manka na kulia kwake kukamfanya aishiwe nguvu, za miguu na kujikuta akianguka chini. Kwa haraka mzee Godwin akairudisha bastola yake mkononi na kumnyanyua Manka na kumuweka kitandani kisha akatoka chumbani humo akiwa na hasira kali.
“Hakikisheni Manka hatoki humu ndani”
“Sawa mkuu”
Mzee Godwin akaondoka huku akiwa na mlinzi wake anaye muamini, moja kwa moja wakarudi ikulu kuendelea na majukumu yao.
                                                                                                               ***
Rahab, Phidaya na Agnes walikesha wakipiga hadithi mbalimbali, kila mmoja akijaribu kusimulia maisha yake ya utotoni na usichana.. Hadi inafika alfajiri hapakuwa na aliye pata hata lepe la usingizi, kila mmoja wao aliweza kufikiria mambo yanayo muhusu kwenye maisha yake hususani kwa wakati huu.
“Yaani Erickson ninampenda sana, na endapo nitakuja kujua ana mwanamke mwengine nitahakikisha nina muua huyo mwanake”
Agnes alizungumza kwa kujiamini na kuwafanya Phidaya na Rahab kutazama, kabla ya Phidaya ajazungumza kitu Rahab akamuwahi.

“Shoga wewe nawe kwa wivu, unamuua mwanamke mwenzako kisa mwanaume?”
“Ahaaa weee Erickson wangu mtamu sana, yaani ni mwanaume shababi, anaye jua kucheza na mwanake sita kwa sita”
“Cha kufanya inabidi ikitimu saa mbili uende ukamuangalie hospitalini”
“Hapo Rahab umezungumza poit huwa ninakupendea hapo tu”
“Ndio hivyo usijikalie hapa kumbe kama ulivyo tuambia mpenzi wako ni mgonjwa”
“Sawa”
Muda wote huo Phidaya alikaa kimya akiyafikiria maneno ya Agnes jinsi yalivyo utibua moyo wake, hata urafiki ambao ulikuwa kwa masaa machache tayari umesha ingia shubiri. Wakaandaa kifungua kinywa, kila mtu akanywa kwa jinsi alivyo weza kunywa chai hiyo yenye itafunwa vingi.

Phidaya akarudi sebleni alipo iacha bahasha yake, akaichukua pamoja na karatasi iliyopo pembeni ambayo hakuiweka kwenye bahasha hiyo. Kabla hajaiingiza karatasi hiyo ndani ya bahasha akaipitishia macho taratibu ili kufahamu ni karatasi za nini. Phidaya hakuamini kitu alicho kiona kimeandikwa kwenye karatasi hiyo, maelezo yanaonyesha uhusiano alio kuwa nao Erickson ambaye ni Eddy pamoja na Manka ambaye ni wifi yake.

‘Imekuwaje hadi ukweli umejulikana?’
Phidaya alijiuliza huku akiketi kwenye sofa, macho yake yakawa na kazi ya kuirudia rudia karatasi hiyo mara kadha.
‘Ila dokta aliye fanya hivi alisha kufa’
Phidaya alizidi kuzungumza mwenyewe huku akiitazama karatasi hiyo, hadi Rahab anafika sebleni hapo, ndipo alipo iingiza karatasi hiyo kwenye bahasha.
“Karatasi za nini?”
Rahab aliuliza huku akijirusha kwenye sofa. Phidaya hakujibu kity chochote zaidi ya kukaa kimya.
“Vipi mbona kimya?”
“Agnes yupo wapi?”
“Nimemuacha akielekea chumbani kwake kuoga”
“Kuna kitu nahisi hakipo sawa”
“Ahaaa kama ni mada hizo tutazizungumza tukiondoka hapa”
Rahab alizunguzma kwa sauti ya chini huku akimtazama Phidaya kwa macho makali. Haukupita muda sana Agnes akatoka akiwa amevalia suti nyeusi. Akamrushia Rahab funguo ya gari moja huku yeye akiwa na funguo ya gari la serikali.
“Mutatumia gari hiyo”

“Una magari mangapi shosti?”
“Mmmm huko uwani yamejazana mengi, sikumbuki kwa haraka nina magari mangapi, si unajua kwamba starehe yangu kubwa ni magari”
“Wewe kiboko”
Wakatoka kwa pamoja na kuelekea eneo la nyuma la nyumba ya Agnes ambapo kuna banda kubwa alilo lijenga lenye magari mengi yaliyo funikwa. Rahab akayahesabu kwa haraka haraka akapata idadi ya magari ishirini na tano.
”Wee mtoto wa kike magari yote haya ni ya nini?”
“Wee acha tu sina mtoto sina ndugu, pesa yangu yote ninayo ipata ni kununua magari. Hapo kuna magari ambayo tangu niyanunue, nimeyaendesha kutoka bandarini hadi hapa”
“Wee kiboko sasa hii funguo uliyo nipa nitafungulia gari lipi?”
“Minya rimoti, litakalo piga alamu ndio hilo hilo”
Rahab akafanya kama alivyo ambia, gari la pembeni lake likaanza kupiga alamu, wakalifunua turubai lililo lifunika gari hilo.

“Hiyo ni Alteza new modern zimetoka mwaka huu”
Agnes alizungumza huku akilitazama gari yake hiyo mpya kabisa. Rahab akaingia na kuliwasha gari hilo.
‘Mamaeee huyu msenge ana hela’
Rahab alijisemea kimoyo moyo, baada ya gari hiyo kumuonyesha tanki lake limejaa mafuta.  Rahab akafungua kioo cha upande wake ili kuzungumza na Agnes.
“Wee mtoto sikuwezi”
“Kwa nini?”
“Gari ipo full tank, nilidhani itakuwa na mafuta ya kulisukumia hadi sheli”
“Nyoo, gari zote hapa unapo ziona zipo full tank. Sasa utawasiliana na mimi ukiwa na simu, au hadi simu nikupe”
“Acha ujinga, nitanunua”
“Haya mwaya, Phidaya karibuni tena jamani”
“Asante”

Phidaya akaingia ndani ya gari, wakaondoka na kumuacha Agnes akiingia kwenye gari lake lenye namba za usajili za wizara yake. Moja kwa moja Agnes akaanzia hospitali ya Agakhan, ambapo akaelekea kwa daktari mkuu wa hospitali hiyo. Akamuuliza kuhusiana na mgonjwa wake ambaye ni Erickson Ford, majibu aliyo kutana nayo yakamshosha sana.
“Ameibiwaje ibibiwaje?”
“Kusmea kweli mimi jana sikuwepo usiku, ila nasikia hata walinzi wa raisi walishindwa kuwazuia hao walio muiba”
“Mungu wangu sasa itakuwaje?”
“Ndio hapo naona muheshimiwa ana lishuhulikia huli, naamini atapatikana tu”
“Sawa nashukuru dokta”
Agnes akaondoka hospitalini hapo huku akiwa amejawa na mawazo chungu nzima, hakujua ni nini anacho weza kukifanya ili kumpata Erickson wake.

TANGA RAHA- Sehemu ya Pili ( 2 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA  

Rahma alizungumza huku akiwa ameishika bastola yangu huku akijipiga piga nayo mashavuni mwake, nakujikuta nikitoa toa miguno
Akautoa ulimi wake na kuanza kuuchezesha juu ya kichwa cha bastola yangu ambayo ina tundu dogo la kutolea risasi zisizo na idadi kamili.Jinsi ulimi wa Rahma unavyo zunguka juu ya kichwa cha bastola yangu kwa ndivyo nilivyo hisi risasi zikitaka kutoka, na kujikuta nikianza kukoroma kama mtu aliye banwa na haja kubwa kwenye choo cha foleni kubwa

ENDELEA
Rahma akazidisha kasi na kunifanya nitoe miguno mizito ya kimapenzi.Gafla raha zikakata, mithili ya umeme wa tanesco unavyo katika. hii ni kutokana na simu ya Rahma kuita kwa mlio mkubwa kiasi, Akanyanyuka na kwenda kuipoke

"Hallow mama"
"Nipo kwa rafiki yangu sinto chelewa kurudi"
Rahma akaendelea kuzungumza kwa lugha ya kiarabu, ambayo sikuielewa hata neno moja analo lizungumza.Akakata simu na kurudi nilipo
"Mama naye"
Rahma alizungumza huku akiwa amenuna
"Ana semaje?"
"Anataka nirudi nyumbani sasa hivi?"
Sikuwa na jibu la kuzungumza zaidi ya kumtazama Rahma na kuendelea kulidhaminisha umbo lake, lilivyo zuri na la kuvutia.Rahma akaishika bastola yangu kisha na kuitumbukiza mdomoni na mara hii akazidisha kuinyonya kwa kasi

Akasimama na kunikalia mapajani huku akiishika bastola yangu na kuiingiza kwenye ikulu yake ambayo ina joto kali.Rahma kama mwanamke aliye pagawa akaendelea kuikalia kwa nguvu huku akiwa anakizungusha kiuno chake, na kunifanya na mimi kutoa vilio vya mfululizo
Bastola yangu ikiwa ndani ya ikulu nikahisi inagusa sehemu ngumu ngumu, ambayo kila inapogusa Rahma akawa anakunja uso kama mtu anayepata maumivu

Rahma akaning'ang'ania shingoni kwa mikono yake huku midomo yetu ikiwa na kazi ya kunyonyana midomo yangu, mipana fulani huku kiuno cha Rahma kikiwa kinazidi kuzunguka
Rahma akajitoa kwenye mapaja yangu akasimama na kunivuta kwenye kochi nami nikawa nimesimama huku nikisubiri maelekezo yake

Serikali Yawatosa Watumishi Wasio na Vyeti vya Kidato cha Nne

$
0
0
Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora imesema watumishi wote waliondolewa katika utumishi wa umma kwa sababu ya kukosa vyeti vya kidato cha nne hawana madai yoyote Serikalini.

Kauli hiyo imetolewa leo, Februari 12, 2018 na Kaimu Katibu Mkuu katika ofisi hiyo,  Mathias Kabunduguru katika kikao cha wakurugenzi wa utawala na rasilimali watu wa wizara zote, makatibu tawala, wasaidizi mkoa na wakuu wa idara za utumishi na utawala.

Amesema zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma lilihitimishwa Oktoba, 2017 na wale wasiokuwa na vyeti vya kidato cha nne waliambiwa waondoke kwa hiari yao.

Hata hivyo, amesema bado watumishi wasio na vyeti hivyo wako kazini kama ilivyobainika katika Wilaya ya Kwimba.

Amewataka maofisa utumishi kuwaondoa wale waliobakia kwa sababu watakapowagundua wataadhibiwa wao na wakurugenzi wao.

"Muwaondoe wote katika orodha ya watumishi wa umma na katika orodha ya mishahara na watakaondolewa wote hawana madai yoyote Serikalini," amesema.

 Amesema watafanya ukaguzi wa kushtukiza kukagua watumishi wasio na vyeti hivyo katika ofisi za umma ili kujiridhisha.

Watumishi hao waliokosa sifa pamoja na wale waliobainika kuwa na vyeti bandia waliagizwa kujiondoa wenyewe kwenye utumishi wa umma mwaka 2016, ambapo Rais John Magufuli alianzisha ‘vita’ dhidi ya wafanyakazi waliokosa sifa ambao walikuwa serikalini.

Msigwa: "Nchi yetu imefika mahali pa hovyo"

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini (CHADEMA), Peter Msigwa amefunguka na kudai nchi ya Tanzania imefika mahali pa hovyo kutokana na watawala kuiendesha nchi kwa mtazamo wao na sio kufuata sheria na kanuni zilizopo.

Msigwa ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa akimuombea ridhaa mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni Salum Mwalimu ili aweze kupata kura za ndio kwa wananchi hao siku ya kupiga kura ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Waziri Mkuu mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA, Mhe. Edward Lowassa , huku akisindikizwa na mameya na Wabunge mbalimbali kutoka UKAWA.

"Watawala wanaendesha nchi kwa 'personality' na badala ya sheria na kanuni. Kwa bahati mbaya sana wale ambao wanategemewa kusema, kukemea pamoja na kuonya wamekaa kimya. Lakini baadhi yetu tumeamua iwe mvua, jua, iwe mabomu ya polisi, vituo vya polisi hata gereza tutazungumza hatutoogopa mtu yeyote", alisema Msigwa.

Pamoja na hayo, Msigwa aliendelea kwa kusema "nchi ya Tanzania imefika mahali ambako kiongozi hawezi kusemwa, Mkuu wa Mkoa hata Spika wa Bunge".

Kwa upande mwingine, Msigwa aliwaambia wananchi wa Jimbo la Kinondoni kwamba wakimuona Mbunge anajikomba komba serikalini basi watambue mtu huyo hatambui wajibu wake anaopaswa kuutekeleza au kuufanya.

RC Mnyeti: Siwezi kutoa msaada kwa diwani wa CHADEMA , Labda Ahamie CCM Ndo Ntamsikiliza

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Manyara,  Alexander Mnyeti amewataka madiwani wa vyama vya upinzani kujiunga na CCM ili waweze kushirikiana naye kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama tawala.

Amesema yupo tayari kupokea simu ya diwani wa CCM hata akipigiwa usiku wa manane, ili kumpa msaada lakini si diwani kutoka vyama  vya upinzani.

Akizungumza jana Februari 11, 2018 katika mkutano wa hadhara kata ya Haydom wilayani Mbulu, Mnyeti amesema ni vyema madiwani wa Chadema wakajiunga na CCM.

Amesema diwani wa Chadema ni ngumu kufanikisha maendeleo ya wananchi kwa madai kuwa, hakuna ambaye atamsikiliza akiwasilisha hoja zake katika vikao vya halmashauri husika.

"Hata hapa Haydom najua ni ngome ya Chadema hata mwenyekiti wa kijiji namuona ana damu ya CCM, sasa ondokeni huko mje huku tutekeleze ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 hadi 2020 kwa kuleta maendeleo," amesema Mnyeti.

Awali, mkazi wa kata ya Hayderer,  John Tluway aliuliza swali kwa mkuu huyo wa mkoa akitaka kujua sababu za mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Chelestino Mofuga kutofika kwenye kata hiyo inayoongozwa na Chadema.

Akijibu swali hilo, Mnyeti amempongeza Mofuga kwa kutokufika kwenye kata hiyo inayoongozwa na Chadema kwa maelezo kuwa diwani wa kata hiyo anapaswa kujiunga na CCM ili kufanikisha maendeleo.

"Mkuu wa wilaya ninakupongeza kwa wewe kutofika kwenye kata hiyo kwani ningepata taarifa umefika mara ya kwanza, mara ya pili na mara ya tatu ningekuwa na mashaka na wewe lakini hongera sana kwa kutokwenda," amesema Mnyeti.

Pia, amewataka watumishi wa halmashauri hiyo kutekeleza na kufanikisha kwa vitendo ilani ya CCM hata kama hawana kadi ya chama hicho kwani ndicho ambacho kipo madarakani.

"Mtekeleze hayo kwa nia safi, hiyo ni sawa na imani kwani hata kanisani huwezi kusikia padri akimsifu Muhammad na pia kule msikitini imamu huwa hamsifu Yesu," amesema Mnyeti.

Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Mbulu, Nasaeli Sulle alimhakikishia Mnyeti kuwa wananchi wa Haydom wamejitambua kuwa walifanya makosa na kuchagua Chadema ila sasa wapo tayari kuwachagua viongozi wanaotokana na CCM.

Rais Mwinyi atengua Rasmi kauli yake

$
0
0
Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi amekiri kufuta kauli yake iliyodumu kwa takribani miaka 30 kuwa Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu na haitakaa ifanye vizuri kwenye michezo.

Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya awali kati ya Simba SC dhidi ya Gendarmerie ya Djibouti, baada ya mchezo alisema kiwango cha mpira nchini kwasasa kimekua hivyo anafuta kauli yake.

''Mchezo umekuwa mzuri na sasa nafuta lile neno (Tanzania ni kichwa cha Mwendawazimu anayejifunza kunyoa atunyoe sisi) lakini sasa sisi ndio vinyozi'', alisema.

Katika mchezo wa jana Simba SC iliibuka na ushindi wa mabao 4-0 hivyo kujiweka vizuri kwenye mchezo wake wa marudiano huko Djibouti. Yanga pia ilishinda dhidi ya St. Louis ya Shelisheli.

Yanga inayocheza klabu bingwa Africa itasafiri kwenda Shelisheli kwaajili ya mchezo wake wa marudiano Februari 20 huku Simba inayoshiriki Kombe la Shirikisho nayo itasafiri kuelekea Djibouti kwaajili ya mchezo wa Februari 20 au 21.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Rais Magufuli amteua Dkt Omari Rashid Nundu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL

$
0
0
China imeridhia kutoa msaada wa Dola za Marekani Milioni 62 sawa na Shilingi Bilioni 138.3 za Tanzania kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Usafirishaji hapa nchini.

Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke amesema hayo leo tarehe 12 Februari, 2018 muda mfupi baada ya kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli na kumkabidhi barua yenye ujumbe wa Rais wa China Mhe. Xi Jinping, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Wang Ke ameeleza kuwa msaada huo ni sehemu ya misaada na miradi mbalimbali ambayo China inaitekeleza hapa nchini Tanzania yenye lengo la kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati yake na Tanzania.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amemuomba Mhe. Wang Ke kumfikishia shukrani zake kwa Rais wa China kwa ujumbe na msaada huo ambao amesema utasaidia kuimarisha huduma za usafirishaji hapa nchini.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amepokea taarifa kutoka kwa viongozi wa Shirika la Simu Tanzania kuhusu mwelekeo wa shirika hilo baada ya kuanza kutumika kwa sheria namba 12 ya mwaka 2017 ya Shirika la Simu Tanzania, iliyolibadili kutoka Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) na kuwa Shirika la Simu Tanzania (TTCL Corporation) kuanzia tarehe 01 Februari, 2018.

Pamoja na kupokea taarifa hiyo Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Omari Rashid Nundu kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL Corp na Bw. Waziri Waziri Kindamba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Corp, na amewataka kuchapa kazi kwa juhudi na kuhakikisha TTCL Corp inaongeza ufanisi, na kutoa gawio kwa Serikali.

Dkt. Omari Rashid Nundu na Bw. Waziri Waziri Kindamba wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa uteuzi huo na wamesema TTCL itaendelea kujiimarisha kwa kupanua huduma za mawasiliano nchini, kuongeza na kuboresha bidhaa ikiwemo TTCL Pesa, kuzalisha faida zaidi na kuusimamia vizuri mkongo wa Taifa kwa maslahi na usalama wa nchi.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
12 Februari, 2018

Makamu Wa Rais Azindua Mradi Wa Kuendeleza Utalii Ukanda Wa Kusini (REGROW)

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imedhamiria kuleta mabadiliko ya dhati katika sekta ya utalii kwa kuhakikisha inatanua mtandao wa barabara na pia kuweka mikakati dhabiti ya kuviendeleza vivutio vya utalii viliovyoko kanda ya Kusini  ili vichangie ukuaji wa uchumi na ustawi wa wananchi.

Makamu wa Rais aliyasema hayo leo kwenye hafla ya uzinduzi wa mradi wa kuendeleza utalii kanda ya kusini mwa Tanzania uliofanyika Kihesa Kilolo mkoani Iringa.

Makamu wa Rais alisema Serikali imeendelea kuandaa na kutekeleza mipango mikakati mabali mbali kwa lengo la kuhakikisha shughuli za utalii zinasambaa nchi nzima .

Makamu wa Rais amasema  katika kuendeleza utalii kanda ya kusini, ambapo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepokea mkopo mwenye masharti nafuu Dola za kimarekani milioni 150 kutoka benki ya Dunia ambapo mradi huo utatekelezwa kwa miaka 6 kuanzia 2017/2018.

Mradi huo wenye lengo kuu la kukuza utalii na kipato kwa wananchi kwa kuboresha miundo mbinu, kujenga uwezo katika usimamizi wa maliasili na kuwawezesha wananchi wanaozunguka hifadhi kuzalisha kwa tija

“Kama nilivyosema hapo awali mradi huu utajulikana  kama Resilient Natural Resource for Tourism and Growth  (REGROW)  na utaanza kutekelezwa katika maeneo ya hifadhi ya Taifa za Ruaha, Mikumi, Udzungwa na Pori la Akiba Selous “

Makamu wa Rais ameiagiza Baraza la Mazingira lililokuwa chini ya Ofisi yake kuharakisha tathmini ya mazingira ya bonde la mto ruaha mkuu ili kuhakikisha kuwa mradi huu unatekelezwa kwa ufanisi bila athari zozote baadaye za mazingira.

Makamu wa Rais alielekeza taasisi zote zinazohusika  zikiwemo Sekretarieti za mikoa, Halmashauri za Wilaya na Vijiji kutoa ushirikiano wa kutosha  wa kufanikisha  utekelezaji wa shughuli za mradi.

“Tuhakikishe sheria zinafuatwa na hakuna uvamizi wala shughuli za binadamu kwenye vyanzo vya maji na hifadhi. Wahenga wanasema tunza mazingira yako yakutunze”.

Makamu wa Rais aliwashukuru benki ya Dunia kwa kukubali kukopesha mkopo wenye masharti nafuu .

Aidha kabla ya Makamu wa Rais kuzungumza, Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla alisema Sekta ya Utalii ni moja ya sekta za kipaumbele katika uchumi wa Tanzania ambapo takribani asilia 20 ya pato la Taifa linatokana na utalii na robo ya fedha za kigeni zinatokana na Utalii.

Watano Wapoteza Maisha, Sita Wajeruhiwa Katika Ajali Kabuku Mkoani Tanga

$
0
0
Watu watano wamefariki dunia papo hapo na wengine sita kujeruhiwa vibaya, baada ya basi kubwa kugongana na hiace katika eneo la Kabuku wilayani Handeni mkoa wa Tanga.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga, Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP)  Leonce Rwegasira alisema ajali hiyo imetokea saa 5:30 asubuhi katika eneo hilo la Kabuku.

Alitaja mabasi hayo kuwa ni basi la kampuni ya AK Safari lililokuwa likitoka Lushoto kwenda Dar es Salaam likiendeshwa na Khalifa Mussa Omary mkazi wa Chamanzi Dar es salaam  lenye namba za usajili T 497 BJB mbalo limegongana na Hiace iliyokuwa ikitoka Mkata kwenda Segera yenye namba T591 AKE.

Alisema waliofariki ambao ni pamoja na Dereva wa hiace aliyefahamika kwa jina moja la Shabaan, wengine majina yao hayajatambulika na maiti zao zimehifadhiwa Kwenye hospitali ya Magunga wilayani Korogwe.

ACP Rwegasira alisema majeruhi ambao hawakuchukua majina yao kutokana na kuwasaidia kuwafikisha katika kituo cha afya Kabuku kwa ajili ya kuendelea na matibabu.

Kaimu Kamanda huyo wa Polisi alisema kuwa chanzo cha ajali ni kutozingatiwa kwa sheria na alama za usalama barabarani kwa madereva hao.

Kamanda huyo wa Polisi alitoa wito kwa watumiaji wa vyombo vya moto kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika.

Aslay, Nandy kuburuzwa mahakamani

$
0
0
Wimbo  wa 'Subalkheri Mpenzi', ulioimbwa na wasanii wa kizazi kipya Aslay Ishack na Nandy, umezidi kuzua utata baada ya mmiliki wa wimbo huo, Kikundi cha Tarab Asilia visiwani Zanzibar (Culture Music Club), .........Kudai kuwa watawaburuza mahakamani kwa kuwa Sh. 800,000 zilizotolewa kama fidia hawazitambui.

Katibu Mtendaji wa kikundi hicho, Taimur Rukuni Twaha, jana alisema wasanii hao kabla ya kuimba tena upya wimbo huo walipaswa kuonana na uongozi huo ili kukubaliana jambo ambalo hawakufanya hivyo.

Kwa mujibu wa katibu huyo, wasanii wa kikundi hicho waliopewa mgawo huo wa fedha ni waimbaji wawili (majina tunayo) ambao mmoja alipewa Sh. 500,000 na mwingine Sh. 300,000.

“Walichokifanya Aslay na Nandy kwenda kwa waimbaji wetu na kuwapa kiwango hicho cha fedha kwetu tunaona hakikubaliki na wametoa kama zawadi tu kwa sababu thamani ya wimbo wetu haulingani na kiwango hicho,” alisema Twaha.

Alisema kwa mujibu wa katiba ya kikundi hicho, ibara ya sita inaeleza nyimbo zote zilizoimbwa na kikundi ni mali ya kikundi na kwamba muimbaji, mtunzi na muweka sauti watakuwa na haki zao kupitia kikundi hicho.

Alisema kimsingi msimamo wao utabaki pale pale wa kuwafikisha mahakamani wasanii hao endapo watashindwa kutimiza masharti waliopewa na uongozi wa kikundi hicho.

Aidha, alisema masharti hayo hayatomhusu Aslay na Nandy peke yao bali na mwanamuziki Hussein Mmanga Faki (maarufu HamaQ) na mwenzake Mosi Suleiman kwa kuimba wimbo wa 'Mke wa Awali ni Wewe Aziza' ambao pia ni mali ya kikundi hicho.

“Tunafahamu kuwa nyimbo zetu wameziimba tena kwa lengo la kibiashara na wamekuwa wakipata fedha kupitia nyimbo hizo,”alisisitiza katibu huyo.

Alisema tayari wameshawaandaa mawakili wao, ambao wataisimamia kesi hiyo mahakamani iwapo wasanii hao watashindwa kutimiza masharti waliyopewa.

Akizungumzia suala hilo, Meneja wa Coconut FM, ambaye ni mwakilishi wa Aslay na Nandy, alisema kuwa wasanii hao watafikishwa katika uongozi wa Kikundi cha Taarab Asilia (Culture) ili kupata suluhu.

Alisema wao hawana makosa kutumia wimbo huo, kwani kabla ya kurudia kuuimba walishakutana na mtunzi wa wimbo huo Bakari Abeid ambaye sasa ni marehemu na kumalizana naye wakati wa uhai wake.

Watumishi 91 Wafukuzwa Kazi Serikalini

$
0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amemwagiza katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia uvuvi Dk. Yohana Budeba pamoja na wakurugenzi wote wa halmashauri za wilaya katika mikoa ya kanda ya ziwa................

Kuwafuta kazi mara moja watumishi 65 na viongozi wa kamati za usimamizi wa raslimali za uvuvi (BMU) 26 baada ya kubainika wanashiriki kufadhili uvuvi haramu ndani ya ziwa Victoria.

Akihitimisha operesheni maalum ya kitaifa ya kupambana na kudhibiti uvuvi na biasahara haramu ya mazao ya uvuvi katika ukanda wa Ziwa Victoria iliyodumu kwa siku 40, katika ukumbi wa chuo cha benki kuu jijini Mwanza, Mpina amesema operesheni hiyo itaendelea hadi disemba mwaka huu ili kuhakikisha uvuvi haramu unatokomezwa huku akidai hatasita kumchukulia hatua za kisheria mtu yeyote atakayebainika kukwamisha juhudi za serikali.

Waziri Mpina pia ameonesha kuchukuzwa na kitendo cha askari wa wanyamapori wa hifadhi ya kisiwa cha Lubodo mkoani geita kuwazuia watendaji wa kikosi cha operesheni hiyo wakati wa msako dhidi ya uvuvi haramu.

Operesheni hiyo ilianza Januari mosi mwaka huu, ambapo jumla ya wadau 1,200 waliopo kwenye sekta ya uvuvi nchini walikutwa na makosa mbalimbali na kutozwa faini ya shilingi Bilioni 4.7, huku tani 73 za samaki wasiokidhi kiwango wakigawiwa kwa wananchi,na tani 173 za mazao ya uvuvi zilitaifishwa,huku mali na zana mbalimbali za uvuvi zenye thamani kubwa ya fedha zikiteketezwa kwa moto.

Heche Akerwa na Kauli za RC Mnyeti....Amtaka Rais Magufuli Atoe Kauli

$
0
0

Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche amedai litakuwa jambo la ajabu kwa Watanzania kunyamazia ubaguzi (wa vyama) unaofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti ikiwa walikuwa mstari wa mbele kupinga ubaguzi wa rangi.

Heche ametoa kauli hiyo mchana wa leo ikiwa ni muda mfupi baada ya habari za Mkuu huyo wa Mkoa kusambaa akiweka wazi wilayani Mbulu  kwamba hayuko tayari kutoa msaada kwa diwani wa chama cha upinzani kwa kuwa yeye anatekeleza ilani ya chama kilichopo madarakani.

Heche amesema kutokana na kauli hiyo iliyotolewa na kiongozi huyo mkubwa wa mkoa anasubiri kusikia kauli ya Chama chake na rais aliyemteua Mnyeti.

Aidha Mbunge huyo amesisitiza kwa kusema kwamba "Ubaguzi ni ubaguzi tu uwe wa rangi, kabila,dini au hata vyama".

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya February 13


Slimming Oil ya Kuondoa Kitambi, Kupunguza Unene na Uzito

$
0
0
Kwa   mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, suala   la  kitambi, unene  na /ama  uzito  ulizo zidi  linasababishwa  na uwepo  kwa  kiasi  kikubwa  cha  mafuta  kwenye  mishipa  ya  damu.

SLIMMING  OIL  ni  dawa  ya  asili  inayo  saidia  kumaliza  tatizo  la  kitambi, unene  na  uzito  ulio zidi kwa  kusafisha  mishipa ya  damu  kwa  kuyeyusha  na   kuondoa  mafuta yasiyo  hitajika  ama  mafuta  ya  ziada  yaliyomo  ndani  ya  mishipa  ya  damu.

VILEVILE :   SLIMMING  OIL  pia  inasaidia  kutibu  na  kumaliza  kabisa  tatizo  la  kutokwa  na  chunusi  za  usoni, vipele  na  majipu mwilini  pamoja  na  tatizo  la  kutokwa  kwa  vipele sugu  katika  eneo  la  chini  ya  kisogo (kichogo )  linalo  tokana  na  kunyolewa  kwa  kutumia  mashine  ambazo  hazijafanyiwa  usafi.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  na  maelezo zaidi  kuhusu  huduma  zetu  nyinginezo,  tutembelee  kupitia :
www.neemaherbalist.blogspot.com

ACT-Wazalendo wapongeza ujumbe wa Maaskofu Katoliki

$
0
0
Chama cha ACT-Wazalendo, kimesema ujumbe wa Kwaresma mwaka 2018 uliotolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kuhusu masuala  ya kisiasa, kichumi na kijamii unaonyesha jinsi demokrasia inavyominywa nchini.

TEC imetoa ujumbe huo Februari, 2018 ulioandikwa na maaskofu wote 35 wa baraza hilo, wakiongozwa na Rais wake, Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa upo katika kitabu cha kurasa 20 ikiwa ni maandalizi ya ibada ya siku 40, kipindi ambacho ni cha mfungo wa kukumbuka siku 40 za Kristo kufunga na kwenda jangwani.

Katibu wa Itikadi na Uenezi na Mawasiliano wa chama hicho, Ado Shaibu amesema, “Tunawapongeza  sana viongozi wetu wa dini kwa kujitokeza waziwazi kuonyesha ugandamizaji wa haki unaoendelea nchini.”

“TEC kutoa waraka wa kiuchungaji ni kurasa mpya katika siasa zetu tangu uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 umalizike.”

Katika ujumbe huo,  TEC wamezungumzia hali ya kisiasa na kusema uamuzi wa Serikali kuzuia, maandamano, mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa ni kwenda kinyume cha Katiba ya nchi.

Shaibu ameitaka Srikali kuondoa zuio batili la vyama vya siasa kutofanya mikutano ya hadhara ya kuzungumza na wananchi.

Mbali na hilo, Shaibu ameiomba Serikali itoe taarifa ya uchunguzi kupotea kwa mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Azory  Gwanda aliyefikisha siku 84 tangu kupotea kwake sanjari na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Kibondo, Simon  Kanguye.

Chama cha Wafanyakazi Champinga Rc Makonda

$
0
0
Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (Talgwu) kimelaani kitendo kikichofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda cha kuwavua madaraka hadharani watumishi wa umma wakisema ni kitendo cha kinyama.

Akizungumza leo Februari 13, 2018 wakati akitoa tamko la chama hicho, Katibu Mkuu, Rashid Mtima amesema chama hicho hakitetei watumishi waovu, bali taratibu zinatakiwa kufuatwa katika kuwawajibisha

Februari 10, 2018  watumishi wa idara za ardhi wa manipaa za Ubungo na Ilala walivuliwa madaraka hadharani hali iliyosababisha mmoja wao, Paul Mbembela (Mkuu wa Idara ya Mipango Miji Ilala) kuzimia kwa muda.

"Tunalaani, tunalaani, tunalaani sana kitendo kilichofanywa na Makonda. Sheria zinataka mtumishi anayekiuka kanuni na sheria za utumishi kushughulikiwa kwa siri hadi uamuzi wa mwisho utakapotolewa,” amesema.

" Jambo baya zaidi tunalolaani hata mtumishi huyo alipozimia Makonda aliendelea kusema Dar es Salaam oyee, huu ni unyama.”

Amesema kibinadamu baada ya Mbembela kuzimia mkutano huo ulipaswa kusimama kwa muda ili kumshughulikia mgonjwa.

Amewaasa wanasiasa na viongozi kufuata sheria wakati wa kushughulikia matatizo ya wafanyakazi.

Serikali Kuondoa Vikwazo Katika Uwekezaji

$
0
0
Jonas Kamaleki- MAELEZO

Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa kushirikiana na wadau wanaohusika na uwezeshaji wa uwekezaji nchini wamejipanga kuondoa ama kupunguza ukiritimba katika utoaji vibali kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Hayo yamebainishwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Geofrey Mwambe katika mahojiano maalum na Idara ya Habari (MAELEZO) jijini Dar es Salaam.

Mwambe amesema kuwa mashirika na taasisi mbali zinazohusika na utoaji vibali kwa wawekezaji ikiwemo, Idara ya Kazi, Uhamiaji, Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Baraza la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na wadau wengine wameazimia kuangalia sheria zao na kuainisha maeneo yanayokwamisha uwekezaji na kuyafanyia kazi mara moja.

“Tutumie Sheria katika kufikia malengo na sio kukwamisha uwekezaji, ili tuweze kufikia uchumi wa kati unaotokana na viwanda,”alisema Mwambe.

Aidha, Mwambe amesema vibali vya uwekezaji vitolewe kwa muda mfupi ili kuvutia wawekezaji wa ndani nan je ya nchi.

Amesema hati ya umiliki wa ardhi kwa ajili ya uwekezaji itolewe kwa wakati ili kumwondelea mwekezaji usumbufu unaoweza kujitokeza, kwa kufanya hivyo wawekezaji wataongezeka na hivyo kujenga viwanda vingi ambavyo vitaongeza ajira hasa kwa vijana.

Katika kuhakikisha uwekezaji nchini unarahisishwa, kimeanzishwa kituo kimoja cha kutolea huduma zinazohusu uwekezaji (One stop Centre) katika ofisi za TIC. Hii inamrahisishia mwekezaji kupata huduma zote sehemu na hivyo kumuondolea bughdha ya kupoteza muda.

Kwa mujibu wa Mwambe, TIC inatafuta pia namna bora ya kulipia vibali mbali mbali vya uwekezaji katika sehemu moja na malipo hayo kupelekwa katika ofisi husika kwa njia ya kielektroniki.

Zipo hatua nyingine nyingi zinazochukuliwa ili kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya uwekezaji. Mpaka sasa TIC kwa kushirikiana na taasisi na mashirika mbali mbali ya Serikali wameshaondoa vikwazo 53 vya uwekezaji.

Ikumbukwe kuwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amekuwa akisema kuwa hataki ukiritimba na zile kauli za “njoo kesho”, “tuko kwenye mchakato” au “tutalishughulikia”. Kwa kuzingatia hilo TIC kwa kiwango kikubwa imeondoa na inaendelea kuondoa ukwamishaji katika eneo la uwekezaji.

Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Wawekezaji inaendelea kutafuta njia ya kuhakikisha inapunguza vikwazo ama urasimu katika uwekezaji nchini ili kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kujenga uchumi wa viwanda.

Msigwa Amvaa Kigwangalla......Asema Yupo Tayari Kujiuzuu Ubunge

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa amefunguka na kuweka wazi kuwa endapo Waziri wa Maliasili na Utalii atatoa ushahidi wowote ambao unaonyesha yeye ana masilahi na makampuni ya uwindaji atajiuzulu nafasi yake ya ubunge.

Mchungaji Msigwa amesema hayo Februari 12, 2018 kupitia moja ya mitandao yake ya kijamii na kudai kuwa Waziri huyo amekuwa ni muongo na ni mtu ambaye hajiamini

"Kigwangalah ni muongo anyependa masifa, ni mtu asiyejiamini. Kama akitoa ushahidi wowote utakaodhihirisha kuwa nina masilahi na makampuni ya uwindaji nitajiuzulu ubunge .Nina wasiwasi na upbringing yake" aliandika Msigwa

Mbunge Msigwa amesema hayo kufuatia kauli ambayo Waziri Kigwangalla aliitoa siku chache zilizopita kupitia mtandao wake wa Twitter kuwa Mbunge huyo wa Iringa Mjini anahusika na ana hisa katika vitalu, jambo ambalo Msigwa mwenyewe amelipinga vikali na kuamua kuweka ubunge wake rehani endapo Waziri huyo atathibitisha hilo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images