Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Yafanikiwa Kurejesha Mali Za NCU, SHIRECU

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imefanikiwa kurejesha mali tisa kati ya 10 za Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza (NCU) ambazo zilichukuliwa kinyume cha taratibu na kuagiza watuhumiwa wachukuliwe hatua za kisheria.

Amesema mali moja iliyobakia bado inafanyiwa uchunguzi na mali mbili za Chama Kikuu cha Ushirika cha Shinyanga (SHIRECU) nazo pia zimepatikana lakini bado ziko kwenye hatua ya makabidhiano.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Februari 9, 2018) bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa 10 wa Bunge la 11. Bunge limeahirishwa hadi Aprili 3, mwaka huu.

Waziri Mkuu amezitaja mali za Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza (NCU) zilizorejeshwa kuwa jengo la Nyanza Cooperative Union (1984) Ltd. maarufu kwa jina la “Transport House” au KAUMA House, lililopo katika kiwanja namba 242, Kitalu T, Mtaa wa Stesheni; kiwanda cha kusindika mafuta cha New Era Oil Mill, kilichopo katika eneo la Igogo; na jengo na viwanja vya Ashock Industries vilivyopo eneo la viwanda Igogo.

Nyingine ni majengo ya kilichokuwa kiwanda cha mkonge na dengu kilichopo eneo la Igogo kwenye kiwanja namba 41 na 79; jengo lililopo katika kiwanja kilichopo Isamilo namba 80, kitalu “D”; jengo lililopo katika kiwanja kilichopo Isamilo namba 110, kitalu “D” na ghala moja katika kiwanja namba 104, kitalu “A” kilichopo eneo la Igogo.

“Mali nyingine zilizorejeshwa ni jengo moja lililopo mjini Geita katika kiwanja namba 8 Kitalu “K”; jengo moja lililopo mjini Geita, katika kiwanja namba 24, Kitalu “K” na jengo lililopo Isamilo katika kiwanja namba 89 Kitalu “D”,” amesema Waziri Mkuu.

Kwa upande wa mali za SHIRECU, Waziri Mkuu amezitaja mali zilizopo kwenye hatua ya makabidhiano kuwa ni ghala lililopo Kurasini, Dar es Salaam na nyumba ya ghorofa tatu iliyopo kiwanja namba 1001 “BB” Ilala, jijini Dar es Salaam.

“Katika kusimamia misingi ya utawala bora na uwajibikaji wa watendaji wa vyama vya ushirika, Serikali inaendelea kufanya uchunguzi maalum kuhusu mikataba mibovu ya Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza (NCU), Chama Kikuu cha Ushirika cha Shinyanga (SHIRECU), Chama Kikuu cha Ushirika cha Kagera (KCU) na Chama Kikuu cha Ushirika cha Kilimanjaro (KNCU). Vilevile, tunachunguza kushikiliwa kwa mali za ushirika bila kufuata utaratibu,” amesema.

Amesema Serikali itaendelea kuviamsha vyama vya ushirika vya msingi na vyama vikuu vilivyosinzia katika mikoa yote ili kujenga ushirika imara na kwamba juhudi na hatua hizo zinazochukuliwa na Serikali, zinalenga kuongeza imani, hamasa na uzalishaji wa mazao na kusimamia masoko yake, na hivyo, kuinua kipato cha wakulima sambamba na kuwapatia fursa ya kujiajiri wenyewe katika sekta ya kilimo.

Waziri Mkuu: Akiba ya Fedha za Kigeni Imeongezeka na Kufikia dola 5.91 bilioni za Marekani

0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema akiba ya fedha za kigeni imeongezeka na kufikia dola 5.91 bilioni za Marekani kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa kwa takriban miaka minne kuanzia mwaka 2013 hadi 2016.

Ameyasema hayo leo Februari 9, 2018  bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa 10 wa Bunge la 11. Bunge limeahirishwa hadi Aprili 3, mwaka huu.

Amesema mbali na kuongezeka kwa akiba ya fedha za kigeni, pia thamani ya mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi imekuwa takriban dola 8.695 bilioni za Marekani ikilinganishwa na wastani wa dola 8.828 bilioni za Marekani kwa miaka mitatu iliyopita.

Hata hivyo, amesema utekelezaji wa bajeti kwa kipindi cha nusu mwaka ni wa kuridhisha ambapo ukusanyaji wa mapato ulifikia Sh12.95trilioni sawa na asilimia 82.8 ya lengo lililopangwa katika kipindi hicho.

Amesema matumizi ya fedha hizo yameelekezwa katika kugharamia shughuli mbalimbali za Serikali za kuhudumia wananchi na miradi ya kipaumbele ambayo ni kuanza kwa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa.

Pia kugharamia mpango wa elimumsingi bila malipo, kugharamia mpango wa ununuzi wa dawa, vifaatiba na vitendanishi na utekelezaji wa miradi ya usambazaji maji vijijini na mijini na usambazaji wa umeme vijijini kupitia REA.

Miradi mingine ni ununuzi wa meli za abiria na mizigo katika maziwa, ukarabati na ujenzi wa baadhi ya viwanja vya ndege na kujenga na kuendeleza maeneo ya uwekezaji wa viwanda katika mikoa mbalimbali nchini.

“Hakika kwa mafanikio haya tuna kila sababu ya kumpongeza Rais John Magufuli kwa uongozi wake mahiri na juhudi anazofanya za kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma muhimu na maendeleo ya haraka,” amesema.

Waziri Mkuu amesema Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha kuwa inatekeleza ahadi zake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba malengo yaliyowekwa kwa mwaka 2017/2018 yanafikiwa kwa kiwango kikubwa.

Amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha na kujenga misingi na mifumo imara ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa lengo la kuwa na mapato endelevu kwa ajili ya kugharamia matumizi yake.

Vilevile, kuwa na usimamizi madhubuti wa ukusanyaji wa mapato ambao utasaidia kupanua wigo na kudhibiti ukwepaji wa kodi kupitia urasimishaji wa shughuli za uchumi kwa kuwezesha ukuaji wa biashara katika sekta ndogo na za kati ambazo ndiyo mihimili ya kuzalisha ajira na kukuza uchumi.

Akizungumzia kuhusu viashiria mbalimbali vya kiuchumi, Waziri Mkuu amesema vinaonyesha kwamba hali ya uchumi ni nzuri na pato la Taifa katika kipindi cha Julai hadi Desemba, 2017 lilikua kwa wastani wa asilimia 6.8.

“Hali hii inaashiria kwamba tuna matarajio makubwa ya kufikia lengo la mwaka la ukuaji wa asilimia 7.0. Sekta zilizochangia kwa kiwango kikubwa katika ukuaji huo ni habari na mawasiliano, uchimbaji madini, biashara, ujenzi na uzalishaji viwandani,” amesema.

Msigwa apelekwa Kamati ya Maadili

0
0
Dk Tulia Ackson Mwansasu amempeleka Mbunge wa Iringa  Mch Peter Msigwa kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ili akatoe ushahidi wake wa namna ufisadi ulivyofanyika kwenye mradi wa mfumo wa uhamiaji mtandao (E-Immigration)

Tulia Ackson amesema hayo baada ya Msigwa kudai kuwa ana taarifa za kutosha juu ya ufisadi uliofanyika katika mradi uliozinduliwa na Rais Magufuli hivi karibuni na kudai kuwa Kambi ya Upinzani bungeni wanazo nyaraka za kutosha ambazo hazina mashaka kuhusu namna ufisadi ulivyofanyika katika mradi huo chini ya Serikali ambayo inajipambanua kupambana na ufisadi. Kufuatia kauli hiyo ndipo hapo Naibu Spika aliagiza Mbunge huyo kwenda kutoa taarifa hizo kwa Kamati ya maadili. 

"Mhe. Msigwa taarifa ulizonazo kuhusu ufisadi uliofanyika kwenye hili zoezi zipelekwe kwenye hii kamati, Kamati itakuja kulishauri bunge tufanye nini na huo ufisadi unaoendelea hayo maeneo kwa hiyo naiagiza kamati imuite Mhe. Peter Msigwa na yeye namuagiza Mhe. Msigwa apeleke huko hizo nyaraka ili bunge liweze kushauriwa na kuchukua hatua mahususi" alisema Tulia Ackson.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. John Pombe Magufuli  Januari 31, 2018  alizindua Pasipoti Mpya ya Tanzania ya kielektroniki jijini Dar es Salaam.

Tangazo la Majina ya Watumishi wa Umma wanaostahili kulipwa madai ya malimbikizo ya Mishahara baada ya Uhakiki

0
0
Tangazo la Majina ya Watumishi wa Umma wanaostahili kulipwa madai ya malimbikizo ya Mishahara baada ya Uhakiki

Waziri Mkuu Azungumzia Suala la Elimu BURE Shule za Serikali....Asisitiza Watoto Kurudishwa Nyumbani ni kinyume na maelekezo ya Serikali

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kitendo cha watoto kurudishwa nyumbani kwa sababu ya mzazi au mlezi kuto changia michango shuleni ni kinyume na maelekezo ya Serikali.

Amesema Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ilitoa Waraka wa Elimu Namba 3 wa mwaka 2016 ambao pamoja na mambo mengine, ulipiga marufuku michango ya aina yoyote isiyo ya lazima katika Elimumsingi.

Waraka huo ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 sambamba na maelekezo ya Ibara ya 52(a) ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015-2020 inayosisitiza utoaji wa Elimumsingi bila malipo.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Februari 9, 2018) bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa 10 wa Bunge la 11. Bunge limeahirishwa hadi Aprili 3, mwaka huu.

Amesema katika siku za hivi karibuni kumejitokeza malalamiko kuhusu baadhi ya shule kuchangisha michango mbalimbali kutoka kwa wazazi na walezi na kusababisha watoto kurudishwa nyumbani kwa sababu ya mzazi au mlezi kuto changia michango shuleni.

“Napenda kutumia fursa hii kutoa wito kwa watendaji wa elimu kuanzia Wakurungezi wa Halmashauri pamoja na wadau wote wa elimu kuzingatia maelekezo ya Waraka uliotolewa na Serikali, ambapo majukumu ya kila mdau katika kutekeleza Mpango wa Elimumsingi Bila Malipo yamefafanuliwa.”

Akizungumzia fedha zilizotolewa katika utekelezaji wa mpango huo, Waziri Mkuu amesema katika kipindi cha mwezi Julai hadi Desemba, 2017, Serikali imetuma moja kwa moja shuleni jumla ya sh. bilioni 124.8.

“Fedha zinazopelekwa moja kwa moja shuleni kwa mwezi ni shilingi bilioni 20.8 na shilingi bilioni 3.06 hupelekwa Baraza la Mitihani kwa ajili ya fidia ya gharama za mitihani kwa wanafunzi wa shule za Serikali. “

“Ruhusa ya michango shuleni ipo, kutoka mtu mmoja mmoja, vikundi au Taasisi. Hata hivyo, michango yote sasa itafikishwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ili ashirikishe Kamati ya Shule za Msingi na Bodi kwa Shule za Sekondari. Walimu wasisumbuliwe na michango ili wajikite na taaluma.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kukusanya taarifa kutoka shule mbalimbali za Sekondari za Serikali kwa lengo la kujua hali ya umiliki wa ardhi katika shule hizo.

Hatua hiyo imekuja kufuatia kuwepo kwa changamoto ya umiliki wa ardhi kutokana na baadhi ya shule kutokuwa na hati miliki, ambapo inatarajia   kuhusisha shule za Sekondari Kongwe zipatazo 89.

Amesema zoezi hilo litakapokamilika litawezesha Serikali kuandaa hati miliki kwa shule zenye umiliki wa Serikali na pia kufanya maamuzi kwa shule ambazo umiliki wake uko chini ya taasisi za dini.

Waziri Mkuu amesema kupitia zoezi hilo maeneo ya mipaka ya shule ikiwemo viwanja vya michezo vitatambuliwa na kujumuishwa kwenye ramani za shule. “Zoezi la ufuatiliaji wa umiliki wa ardhi kwa shule za msingi na shule za Sekondari zilizobaki za Serikali litaendelea kufanyika ili kuondoa changamoto za migogoro ya ardhi.”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Rais Magufuli Ahutubia Mabalozi Katika Sherehe Za Mwaka Mpya Kwa Mabalozi Wanaowakilisha Nchi Zao Hapa Nchini

Sugu, Masonga waachiwa kwa dhamana

0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi-Mbeya imewaachia kwa dhamana washtakiwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga katika kesi inayowakabili ya kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Sugu na Masonga wamekaa mahabusu kwa muda wa siku 24 baada ya kunyimwa dhamana na mahakama hiyo kutokana na hoja za upande wa  Jamhuri.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Michael Mteite amewaachia kwa dhamana wawili baada ya Wakili upande wa utetezi, Peter Kibatala kuiambia mahakama hiyo kwamba imeshafunga ushahidi wake ambapo mashahidi sita walitoa ushahidi wao.

Mawakili wa pande zote mbili walikubaliana kwamba Februari 19 watawasilisha majumuisho ya shauri hilo mahakamani hapo.

Hakimu Mteite amekubaliana  na hoja hiyo ya mawakili na kusema hukumu ya kesi hiyo itatolewa Februari26 mwaka huu.

"Washtakiwa wote wanaachiwa kwa dhamana, na kila mmoja atajidhamini mwenyewe kwa hati ya dhamana ya maneno ya Sh5 milioni kwa kila mmoja.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya February 10


Wabunge Wataka Wapewe Ulinzi, Serikali Yagoma

0
0
Bunge limeagiza Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge ifanyiwe marekebisho ili kuweka sharti la wabunge kupatiwa ulinzi, hususan katika makazi yao wanapokuwa katika utekelezaji wa majukumu ya kibunge mjini Dodoma na katika maeneo yao ya uwakilishi.

Chombo hicho cha kutunga sheria pia kimeagiza kuweka utaratibu wa kutoa namba maalum za usajili wa magari ya wabunge huku kikiitaka serikali iboreshe na kuimarisha ulinzi katika maegesho ya magari bungeni.

Hayo yalisema na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu, alipowasilisha taarifa ya mwaka ya shughuli za kamati kwa kipindi cha Februari, 2017 hadi Januari, 2018.

Agizo hilo limetoka ikiwa ni takribani miezi minane tangu kushambuliwa kwa kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema).

Rais huyo wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) alipigwa risasi akiwa anajiandaa kushuka kwenye gari lake nyumbani kwake Area D mjini hapa Septemba 7, mwaka jana.

Mpaka sasa, hakuna taarifa ya kukamatwa kwa wahusika wa tukio hilo na Lissu anaendelea na awamu ya tatu ya matibabu yake ya kibingwa nchini Ubelgiji.

Baada ya kutokea kwa tukio hilo, Spika Job Ndugai aliiagiza kamati hiyo kulifanyia kazi na kulitolea taarifa bungeni.

Balozi Adadi alisema katika kipindi cha Novemba mwaka jana, kamati yake ilipokea na kujadili taarifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuhusu udhibiti wa usalama wa viongozi wakiwamo wabunge.

Alisema uchambuzi wao ulibaini viongozi wanaolindwa na Jeshi la Polisi kwa mujibu wa sheria ni viongozi wakuu wa nchi ambao ni Rais na Makamu wa Rais wa Tanzania, Rais wa Zanzibar, Waziri Mkuu na viongozi wakuu wastaafu.

Alisema wengine ni viongozi waandamizi wa serikali ambao ni mawaziri na manaibu mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya pamoja na Spika na Naibu Spika wa Bunge.

"Kwa mujibu wa Sheria ya Jeshi la Polisi na Polisi Wasaidizi Sura ya 322, wabunge na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi hupewa ulinzi wa jumla wanapokuwa katika shughuli za bungeni au kwenye safari zao za kikazi," Balozi Adadi alisema na kuongeza:

"Utaratibu huu unaliacha suala la ulinzi na usalama wa wabunge katika makazi yao wakiwa kwenye shughuli za Bunge na kwenye maeneo yao ya uwakilishi kuwa jukumu la mbunge mwenyewe."

Balozi Adadi alisema kazi za wabunge katika kuisimamia serikali zinagusa maslahi ya watu au makundi binafsi ambayo yanaweza kujenga chuki dhidi yao.

Majibu ya Serikali
Katika majibu yake, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Mwigulu Nchemba, alisema wazo hilo ni zuri lakini nchi inatakiwa kuwekeza kwanza katika kuimarisha miundombinu kabla ya kutoa ulinzi kwa mbunge mmoja mmoja.

Aliongeza kuwa bila kuwa na miundimbinu mizuri, askari watakaopewa jukumu la kuwalinda watunga sheria hao watakuwa kwenye hatari kubwa ya kudhurika na hata kushambuliwa.

Mauaji Kibiti
Alisema kamati yake ilikutana na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Septemba na Januari na ikaridhishwa na juhudi za serikali katika kushughulikia matukio mbalimbali ya uhalifu hususani matukio ya Kibiti, Mkuranga na Rufiji yaliyohusisha mauaji ya viongozi, askari polisi, na raia.

"Nafurahi kutoa taarifa kuwa, kwa kazi nzuri iliyofanywa na vyombo vya ulinzi na usalama katika maeneo hayo, hali ya usalama sasa ni shwari.

Lakini kamati inasisitiza kuwa ni wajibu wa serikali kuhakikisha kiini cha mauaji hayo kinajulikana na kudhibitiwa ili mauaji ya aina hiyo yasijirudie tena nchini," alisema.

Msongamano wa Wafungwa
Balozi Adadi pia alisema kamati yake imebaini kuna msongamano wa wafungwa na mahabusu magerezani nchini kutokana na kile ilichoona matumizi hafifu ya sheria zinazoruhusu adhabu mbadala kwa wafungwa kama vile kifungo cha nje na mahabusu kutopelekwa mahakamani kwa muda uliopangwa.

Pia kutotumika ipasavyo kwa mpango wa Parole, kasi ndogo ya kusikiliza mashauri yanayohusu mauaji na dawa za kulevya pamoja na kutokutekelezwa kwa adhabu iliyotolewa dhidi ya wafungwa waliohukumiwa kunyongwa.

"Hali hiyo inaathiri afya za wafungwa na mahabusu. Vilevile, kuiongezea serikali gharama za kuwatunza," alisema.

Ajali
Alibainisha kuwa katika kipindi cha kuanzia Oktoba hadi Desemba, jumla ya ajali 1,428 ziliripotiwa na kati yake, ajali 562 zilisababisha vifo.

Alisema idadi hiyo ya vifo ni pungufu kwa vifo 91 kulinganishwa na idadi ya vifo vya aina hiyo katika kipindi kama hicho mwaka 2016.

Alisema vifo vingi vya ajali vinachangiwa hasa na mwendokasi, kutovaa kofia ngumu, kutofunga mikanda, matumizi ya vilezi, matumizi ya simu za mikononi na matumizi ya vizuizi vya watoto.

Balozi
Mkurugenzi huyo wa zamani wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) pia alisema kamati yake imebaini uchakavu wa majengo ya balozi za Tanzania kutokana na kutofanyiwa ukarabati kwa muda mrefu.

Pia alizungumzia changamoyo ya meli zenye usajili Tanzania kukamatwa nje ya nchi kwa makosa ya kihalifu ambayo ni pamoja na kubeba dawa za kulevya na vifaa vya kutengenezea silaha kali za kivita.

Alisema kamati yake inaishauri serikali kuchukua hatua za haraka kama ilivyoahidi mbele bungeni Mei 2, mwaka jana.

Utekaji na Amri za Wakuu wa Wilaya
Balozi Adadi pia alisema kamati yake ilibaini kumekuwa na ucheleweshaji wa kutoa taarifa rasmi kwa umma kuhusu hatua zilizofikiwa katika upelelezi wa matukio ya muda mrefu na yanayovuta hisia za jamii kama vile matukio ya mauaji, kutekwa na kupotea kwa viongozi na wananchi mbalimbali, unyang'anyi wa kutumia silaha na makosa makubwa ya uhujumu uchumi.

"Kamati pia ilibaini kuwa baadhi ya wakuu wa wilaya wanawaweka mahabusu wananchi na watumishi wa umma kinyume cha matakwa ya kifungu cha 15 cha Sheria ya Tawala za Mikoa ya Mwaka 1997," alisema.

"Ni wajibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa kushirikiana na Tamisemi kuendelea kuwaelimisha wakuu wa wilaya kuhusu matumizi sahihi ya sheria hiyo ingawa kwa sasa vitendo hivyo vimepungua."

Credit: Nipasher

Serikali kuwashughulikia Polisi wanaotesa raia wakiwa kizuizini

0
0
Serikali imeahidi kuwashughulikia Askari Polisi watakao bainika kutesa na kuwapiga raia wakiwa kizuizini, kwa kuwa vitendo hivyo ni kinyume na sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20 kifungu cha 11.

Kauli hiyo imetolewa jana Februari 10, 2018 Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Eng. Hamad Masauni wakati akijibu swali la Mbunge Viti Maalum Rungwe (Chadema) Sofia Mwakagenda lilohoji kama kuna sheria inayomruhusu Askari Polisi kumkamata mtuhumiwa na kumpiga na kumtesa kabla ya kufikisha kituo cha polisi.

Eng. Masauni alisema serikali kupitia wizara yake imekuwa ikiwachukulia hatua Askari Polisi wanaofanya makosa mbalimbali, ambapo  katika kipindi cha mwezi Januari hadi Disemba mwaka 2017, jumla ya askari polisi 105 waliotenda makosa mbalimbali wamechukuliwa hatua za kinidhamu ikiwa pamoja na kufukuzwa kazi.

“Kwa mujibu wa sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura 20 kifungu 11 kinaeleza namna ya ukamataji, aidha kifungu hiki mahsusi cha ukamataji hakimruhusu askari kumpiga na kumtesa raia akiwa kizuizuni, kwa mujibu wa kanuni za utendaji wa jeshi la polisi askari yeyote atakayebainika kutesa, kupiga raia akiwa kizuizini huchukuliwa hatua za kinidhamu ikiwemo kufukuzwa kazi au kufikishwa mahakamani,” alisema.

Dawa ya Asili ya Vidonda vya Tumbo, Pumu, Nguvu za Kiume, Korodani kuvimba

0
0
Super Muhi Mix Power:  Ni dawa ya nguvu za kiume kutoka Congo, inatibu na kuponesha kabisa tatizo la nguvu za kiume, itakufanya uweze kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka. Itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 20- 25, huimaliha misuli iliyolegea na kusinyaa. Dawa hii imechanganywa na mizizi 11.

Sub 3Mix; Hii ni dawa ya mvuto wa mapenzi, huvuta mume, mke, mchumba na atatimiza ahadi zote alizokuahidi. Pia mkufu na pete ya bahati vipo.

Pata pia dawa ya pumu, ngiri, kisukari, kaswende, vidonda vya tumbo na korodani kuvimba

Mawasiliano: 0659874143-Dr. Hussein Omary

Huduma hii utaipata popote ulipo. Tupo Mbagala Dar es Salaam kwa sasa

Hatma ya Zitto mikononi mwa Spika

0
0
Kuadhibiwa  ama kutoadhibiwa na Bunge kwa Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo) kuko chini ya Spika Job Ndugai baada ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kukamilisha uchunguzi wa shauri lake.

Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo anakabiliwa na tuhuma za kudharau mamlaka ya Spika kutokana na kauli yake kwamba, "Bunge limewekwa mfukoni na serikali."

Akiwasilisha bungeni mjini hapa jana taarifa ya shughuli za Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kipindi cha kuanzia Januari 2017 hadi Januari 2018, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Almas Maige, alisema tayari wameshakamilisha uchunguzi wa shauri hilo.

Pia alisema kamati yake imeshamshauri Spika hatua za kuchukua kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge toleo la Januari 2016.

Maige ambaye pia ni Mbunge wa Tabora Kaskazini (CCM), alisema kuwa katika mkutano wa nane wa Bunge, baada ya Spika kupokea na kuikabidhi serikali taarifa za kamati mbili alizoziunda Julai tano kwa ajili ya kufanya uchunguzi katika sekta ya madini, Zitto aliandika kwenye mtandao wa Twitter maneno ya dharau dhidi ya Spika.

Spika aliunda kamati mbili za kuchunguza na kuishauri serikali kuhusu mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa biashara ya madini ya Tanzanite na almasi.

"Kamati ilifanya uchunguzi wa shauri hili na kukamilisha kisha kumshauri Spika kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge," Maige alisema.

Spika Ndugai hakuongoza kikao hata kimoja katika mkutano wa wiki mbili uliomalizika jana.

Waziri Mkuu: Usalama Wa Chakula Umeimarika Nchini

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema hali ya usalama wa chakula nchini imeimarika kutokana na uzalishaji mzuri wa mazao ya chakula.

Aliyasema hayo jana (Ijumaa, Februari 9, 2018) bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa 10 wa Bunge la 11. Bunge limeahirishwa hadi Aprili 3, mwaka huu.

Waziri Mkuu alitaja mazao hayo kuwa  ni pamoja na mahindi yaliyovunwa katika mikoa ya Ruvuma, Njombe, Iringa, Katavi, Kigoma, Mbeya, Songwe na Rukwa.

“Matarajio yetu kuwa hali ya mavuno msimu huu itakuwa nzuri kwa sababu mwenendo wa unyeshaji wa mvua za vuli ulikuwa wa kuridhisha katika maeneo mengi nchini.”

Alisema Serikali inaendelea kusimamia na kuhakikisha kuwa hali ya utengamano na usalama wa chakula unaendelea kuwa imara kwa wananchi wote na kwa wakati wote.

Waziri Mkuu alisema Serikali inawezesha wafanyabiashara wa mazao ya chakula kuendelea kusafirisha na kuuza mazao ya chakula nje na ndani ya nchi.

Hivyo, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa wakulima waendelee kuzitumia vizuri mvua zinazoendelea kunyesha kwa kupanda mazao stahiki na kutumia chakula walichonacho kwa uangalifu hadi msimu mwingine wa mavuno.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alisema upatikanaji na usambazaji wa pembejeo kwa wakulima umeimarika, ambapo takwimu zinaonesha kwamba hadi kufikia Februari Mosi, 2018 upatikanaji wa mbolea nchini kwa ajili ya mahindi na tumbaku ulifikia tani 250,376 sawa na asilimia 51.6 ya wastani wa mahitaji ya tani 485,000 kwa mwaka.

“Katika kipindi hicho hicho, mbolea za kupandia na kukuzia zipatazo tani 229,839 ziliingizwa nchini na kusambazwa mikoani. Upatikanaji wa dawa za maji na unga (Salfa) kwa ajili ya mazao ya pamba na korosho unaendelea.”

Waziri Mkuu alisema hadi kufikia Februari Mosi, 2018 upatikanaji wa mbegu bora nchini ulifikia tani 51,700, sawa na asilimia 86.2 ya mahitaji halisi ya tani 60,000 kwa mwaka. Katika kipindi hicho jumla ya tani 22,357 za mbegu bora zilisambazwa nchini.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Serikali yawasha moto Bungeni kuhusu madanguro, biashara ya ngono

0
0
Serikali imesema ina andaa mikakati itakayowezesha kudhibiti biashara ya ngono na uwepo madanguro nchini, hasa kwenye maeneo ya mijini.

Hayo yamesemwa jana Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile wakati akijibu swali la Mbunge wa Mtambwe, Khalifa Mohammed Issa aliyehoji juu mpango serikali katika kudhibiti biashara ya ngono na madanguro ili kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (VVU) nchini.

Akijibu swali la Issa, Dkt. Ndugulile alisema Serikali inaandaa mikakati mbalimbali ikiwemo utoaji wa elimu kuhusu madhara ya biashara ya ngono kwa jamii pamoja na kuchukua hatua za kisheria kwa wanaojihusisha na baishara hiyo, pamoja na kudhibiti uwepo wa madanguro.

Katika hatua nyingine, Dkt. Ndugulile alisema serikali inaendelea kuchukua hatua katika kudhibiti mila na desturi potofu zinazochangia maambukizi mapya ya VVU, ikiwemo ukeketaji na urithishaji wa wajane kwa ndugu wa mume, kwa kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara ya mila potofu pamoja na kutoa hamasa kwa wakunga wa jadi wanaojihusisha na ukeketaji.

SORRY MADAM -Sehemu ya 86 & 87 (Destination of my enemies)

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Agnes mwili mzima akaijikuta ukimtetemeka kwa hasira kali huku akiendela kuitazama picha ya Eddy.
“Huyo ni mtu aliye weza kutambua mpango wenu wa nyinyi kumtafuta. Na kitu alichokuwa anapanga kukifanya ni kuhakikisha anaanza kuwatanguliza nyinyi kuzimu, kisha anawafwatia wale walio wapa kazi ya kumfwalia. Ameona akimuua Erickson basi wewe utateteraka na itakuwa ni rahisi kwa wewe kuweza kufa”
Uongo wa John ukazidi kumuingia Agnes akilini kisawasawa, kila jinsi alivyo zidi kuitazama picha ya Eddy ndivyo jinsi hasira ilivyo zidi kumpanda hadi akajikuta akitamani kuivunja simu hiyo aliyo ishika.
“Kumbuka mtu anye fata katika kuuawa ni wewe Agnes, Eddy amemteka Erickson kuwa makini”
Kwa hasira Agnes akaitupa chini simu ya John, huku akihema kwa hasira kama Simba jike aliye uliwa watoto wake alio wazaa muda mchache ulio pita.

ENDELEA
   John akabaki akishangaa jinsi simu yake ilivyo gawanyika vipande vipande chini. Hakuzungumza chochote zaidi ya kumeza mate tu. Agnes kwa haraka akrudi kwenye kiti chake na kukaa.
“Nitampata vipi huyo Eddy?”
Agnes alizungumza huku sura yake ikiwa imejikunja ndita zilizo upoteza uzuri wak wote ambao, John muda mchache alivyo ingia ofisini hapo alikuwa akiufurahia sana.
“Ungana na mimi, na utaweza kumpata Eddy”
Kabla Agnes hajazungumza kitu cha aina yoyote, simu ya Agnes ikaita na kumfanya kuitazama kwa haraka, kitu kilicho mshangaza ni kuona jina la Erickson likijitokeza kwenye simu yake, kabla hajaipokea akamtazama John kwa macho makali kisha akaipokea.
                                                                                                                       ***
   Eddy taratibu akajikuta akipunguza mwendo kasi wa gari lake, baada kwa mbali kidogo kuona msusuru wa magari ukiwa umesimama. Hakujua ni kitu gani kilicho polekea gari hizo kusimama. Taratibu akalisimamisha garni lake nyuma ya gari lililpo mbele yake. 
 
“Kuna nini?”
Eddy alizungumza mwenyewe huku akiitooa simu yake mfukoni. Akakuta ikiwa imezima kutokana na kuisha kwa chaji, na siku mbili hizi hakuitumia kabisa kutokana na matatizo yaliyo weza kujitokea. Akachukua waya wa chaji na kuuchomeka katika sehemu ya USB, iliyo kwenye gari lake, taratibu chaji ikaanza kuingia. Pasipo kujua ni kitu gani kipo mbele yake, akazidi kusogeza gari lake taratibu kuifwata foleni hiyo. Hadi zimebaki gari mbili mbele yake ndipo Eddy anagundua foleni hiyo imesababishwa na ukaguzi mkali wa jeshi la polisi wakisaidiana na jeshi la kujenga taifa wakikagua magari yote yanayo ingia na kutoka katika mkoa wa Dar es Salaam.
 
“Shitii”
Eddy akajikuta akitoa macho na kuanza cha kufikiria ni nini cha kufanya kwa maana askari hao wanakagua gari zima hadi kwenye buti. Bahati mbaya ni kwamba kwenye buti ya gari lake amebeba silaha anazo zimiliki kinyume na sheria. Kitu kingine kinacho zidi kumpagawisha nyuma yake kuna magari mengi ambayo nayo yapo kwenye msururu huo wa kukaguliwa. 
 
“Agnes Agnes”
Eddy alizungumza huku kwa haraka akijitahidi kuiwasha simu yake, kwa bahati nzuri akaiwasha japo ina asilimia tano za chaji, ila akajitahidi hivyo hivyo kumpigia Agnes akiamini anaweza kuapata msaada kwake. Tayari gari la mbele yake lilisha anza kukaguliwa, huku askari wengine wawili walio shikilia mbwa wawili wakubwa, wakilisogelea gari lake huku bunduki zao zikiwa begani. Kitendo cha Agnes kupokea simu, simu ya Eddy ikazima chaji tena.
 
“Fu*k”
Eddy akajikuta akiachia tusi zito huku akiitazama simu hiyo, kwa haraka akakumbuka anasimu ambazo ni mpya ameziweka siti ya nyuma, akageuka kwa haraka na kuichukua moja, akatoa chip kwenye simu yake na kuiweka kwenye simu moya. Kwa haraka akaiwasha, simu ikiendelea kuwaka tayari askari wa mbele alisha anza kumpa isha ya kulisogeza gari lake kwenye sehemu yanapo kaguliwa. Ikambidi taratibu kulizogeza gari lake, mbaya zaidi mbele kuna geti la chuma pamoja na miba mirefu iliyo kaa mfumo wa chuma iliyo tandazwa barabarani endapo utajaribu kukimbia na kuikanyaga miba hiyo basi tairi za gari lako zote zitapata pancha. 

Kitu kingine ambacho ni ngumu kuweza kuwakimbia askari hao, ni magari makubwa ya jeshi yaliyo katika pande zote mbili za barabara yakiwa  yamefungwa mitutu mikubwa ya bunduki, zenye uwezo wa kulichakaza gari lako vibaya ndani ya dakika moja pale tu utakiuka sheria na kuwakimbia. Mbwa hao wakubwa, walio fundishwa mbinu za kunusa kitu chochote ambacho si cha usalama, wakanza kulizunguka gari la Eddy hususani sehemu ya buti, ambapo ndipo zilipo bunduki, mabomu pamoja na vibunda vya pesa za kigeni. Askari mmoja akagonga kioo cha upande wa Eddy alipo kaa kwa ishara akimuomba kushuka haraka. 
 
Eddy akamtazama askari huyo, aliye anza kuishika bunduki yake vizuri huku akiwa amemkazia macho, taratibu akashuka kwenye gari huku akiwa ameshika simu yake mkononi.
“Muheshimiwa fungua buti, tunahitaji kukagua”
Askari mmoja alizungumza huku akimtazama Eddy kwa umakini.
“Munataka kukagua nini?”
“Hilo wewe halikuuhusu fungua buti tukague usitupotezee muda bwana”
“Siwezi kukagua gari kwa maana mzigo ulio kuwemo humo ni wa muheshimiwa waziri Agnes”
“Bwana wewe, sisi hatujali kama ni mzigo wa waziri au laa. Tutancho hitaji fungua buti tuangalie ni kitu gani ulicho bebe. Utakuta nyinyi ndio munao lipua lipua raia wema”

===>Endelea Nayo Kwa Kubofya <<HAPA>>

Tiba Asili ya Kuondoa Chunusi, Kupunguza Tumbo, Maziwa Makubwa na Nguvu za Kiume

0
0
Asilimia 90 ya wanaume hushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kiafya  kama vile kisukari, punyeto ambayo huathiri mfumo mzima wa wa misuli inayozalisha vichocheo ashiki , kutopata choo vizuri hali ambayo huchakiwa na kula chakula kisicho na asili,tumbo kuunguruma, kujaa gesi,kiuno kuuma, mgongo na miguu kufa ganzi

SUPER HOLO; Ni dawa itokanayo na miti shamba, ipo katika mfumo wa vidonge na unga. Hutibu na kumaliza tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa muda mfupi tu.,SUPER HOLO hurudisha heshima ya ndoa, itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-30. Itakupa hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3. Pia itaimarisha misuli iliyosinyaa na kulegea. Dawa hii hutumiwa kwa watu wa umrii wa miaka 20- 80

NZOGIWE ni dawaya maumbile.Hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo urefu wa nchi 4-8 na unene wa sentimita 2-4 za upenyo

NZOGOMA ni dawa asili ya miti shamba, huboresha mbegu za uzazi...huzibua mirija na kusafiisha ili kuweza kushika mimba au kutia mimba.

Pia tunayo dawa ya kupunguza tumbo, unene, maziwa makubwa, kuongeza hips, makalio na kutoa chunusi

TUNAPATIKANA MTONI MTONGANI. KANA HAUNA NAFASI YA KUFIKA UTALETEWA ULIPO. WASILIIANA NA DR. MBUSI.  PIGA SIMU NAMBA:   0718 431222

Nape Awamwagia Lawama Usalama wa Taifa

0
0
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye ameibuka na kuituhumu Idara ya Usalama wa Taifa nchini haifanyi kazi zake ipasavyo inavyohitajika na badala yake wamekalia kusikiliza simu za watu wanavyoongea pamoja na kufanya mambo ambayo hayalindi uchumi wa Tanzania.

Nnape ametoa kauli hiyo  jana wakati alipokuwa akichangia bungeni taarifa ya Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama katika mkutano wa 10 kikao cha nane cha Bunge mjini Dodoma na kuishauri kamati hiyo ipeleke mapendekezo ili waweze kupitia upya sheria ya Usalama wa Taifa na kuiwezesha mikono yao iende mbali, kukumbuka jukumu lao la kuhakikisha wanalinda uchumi wa nchi katika kipindi hichi, ambacho demokrasia ya siasa inahama na kuelekea kwenye demokrasia ya uchumi ambapo muda mwingi wanapaswa kuutumia huko na sio pengine.

Kutoka na hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Kapteni George Mkuchika alimjibu Nape na wabunge wengine kwamba kazi ya Idara ya Usalama wa Taifa sio kutafuta watu waliopotea au kuumizwa kama wanavyodai na laiti wangelifahamu wanachokifanya wangekaa kimya.

"Kazi ya usalama wa Taifa nchi yeyote ni kutafuta habari na kuishauri serikali. Kwa kifupi tu mimi nasema hoja mlizozitoa kuhusu idara kwamba haishauri serikali mambo ya uchumi na mambo mengine hamna ushahidi", alisema Kapteni Mkuchika.

Pamoja na hayo, Kapteni Mkuchika aliendelea kwa kusema "sheria ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1996, kazi zilizopitishwa kwa mujibu wa Bunge kuna shughuli nne za idara kwamba ni kukusanya na kutafuta habari pamoja na kuzifanyia tathmini na wanapoyafanya hayo hawayafanyi katika mkutano wa hadhra, kushirikiana na vyombo vya idara nyingine vinashughulikana na usalama wa nchi, kuwashauri Mawaziri ili waishauri serikali na mambo yote ya kuhujumu uchumi na vingine wanayafanya kimya kimya".

Shughuli za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Taifa zimehairishwa jana jioni (Ijumaa) mpaka Aprili 03 mwaka 2018.

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Serikali Yawasimamisha Kazi Maafisa Utumishi Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Kwimba Kwa Kutowajibika

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images