Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kitwanga aikosoa Serikali ujenzi wa Reli

$
0
0
Mbunge wa Misungwi (CCM), Charles Kitwanga ameikosoa Serikali ya awamu ya tano na kuitaka iwe na mipango inayoeleweka na si kufanya maamuzi au mipango ya zimamoto.

Kitwanga amesema hayo bungeni na kudai kuwa Serikali haina haja ya kujenga reli nusu nusu ikiwa inaona haina mpango endelevu wenye tija na kuleta matumaini kwa wafanyabiashara na watu wa viwanda.

"Tunahangaika kutengeneza reli na reli inajengwa kutoka Dar es Salaam kuja Morogoro inawekwa reli ya umeme ila ukishafika Morogoro kuja Dodoma utofauti wa reli kati ya hiyo standard gauge na ya kawaida unatofautiana, sijui sasa unaanza kupakua hiyo mizigo uanze kupakua kwenye ile reli nyingine ya zamani? Mimi nadhani kuwe na mipango ambao unakuwa ni wa jumla utachukua muda lakini unajua tunajenga reli kutoka Dar es Salaam mpaka Kigoma au Dar es Salaam mpaka Mwanza" alisema Kitwanga

Kitwanga aliendelea kusema kuwa; "Lazima kuwa na mipango thabiti tunasema kwamba hicho ni kipindi cha mpito ambacho kitakuwa kinaeleweka kwa wafanyabiashara na watu wenye viwanda nchini ambapo watakuwa na matarajio yanaoeleweka na mipango hii ifuatwe 

"Hakuna sababu ya kuanza kujenga nusu nusu wakati hujui kinachofuatia na huna mpango wa kupata hela, ni vyema ukawa umejipanga kwamba nikitoka Dar es Salaam kufika Morogoro nitakuwa nimepata fedha kutoka Morogoro kwenda Dodoma, Tabora tusiwe na mipango ya zima moto" alisisitiza Kitwanga

Tiba Asili ya Kuondoa Chunusi, Kupunguza Tumbo, Maziwa Makubwa na Nguvu za Kiume

$
0
0
Asilimia 90 ya wanaume hushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kiafya  kama vile kisukari, punyeto ambayo huathiri mfumo mzima wa wa misuli inayozalisha vichocheo ashiki , kutopata choo vizuri hali ambayo huchakiwa na kula chakula kisicho na asili,tumbo kuunguruma, kujaa gesi,kiuno kuuma, mgongo na miguu kufa ganzi

SUPER HOLO; Ni dawa itokanayo na miti shamba, ipo katika mfumo wa vidonge na unga. Hutibu na kumaliza tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa muda mfupi tu.,SUPER HOLO hurudisha heshima ya ndoa, itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-30. Itakupa hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3. Pia itaimarisha misuli iliyosinyaa na kulegea. Dawa hii hutumiwa kwa watu wa umrii wa miaka 20- 80

NZOGIWE ni dawaya maumbile.Hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo urefu wa nchi 4-8 na unene wa sentimita 2-4 za upenyo

NZOGOMA ni dawa asili ya miti shamba, huboresha mbegu za uzazi...huzibua mirija na kusafiisha ili kuweza kushika mimba au kutia mimba.

Pia tunayo dawa ya kupunguza tumbo, unene, maziwa makubwa, kuongeza hips, makalio na kutoa chunusi

TUNAPATIKANA MTONI MTONGANI. KANA HAUNA NAFASI YA KUFIKA UTALETEWA ULIPO. WASILIIANA NA DR. MBUSI.  PIGA SIMU NAMBA:   0718 431222

Rais Magufuli, Kikwete, na Lowassa walivyomzika Mzee Kingunge Kinondoni

$
0
0
Viongozi mbalimbali wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli jana February 5, 2018 wamemzika Mwanasiasa Mkongwe Mzee Kingunge Ngombale Mwiru katika makaburi ya Kinondoni Jijini DSM shughuli iliyotanguliwa na ibada iliyofanyika nyumbani kwake

Kingunge alifariki Siku ya Ijumaa akiwa anapatiwa matibabu katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili baada ya kushambiliwa na mbwa nyumbani kwake Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamini Wiliam Mkapa pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakiwa katika ibada ya mwisho ya marehemu Mzee Kingunge Ngombale Mwiru katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiweka mchanga kwenye Kaburi la marehemu Mzee Kingunge Ngombale Mwiru katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akijiandaa kuweka Shada la Maua kwenye Kaburi la Marehemu Mzee Kingunge Ngombale Mwiru katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Al Haji Mussa Salimu Ampa ONYO Kali Mange Kimambi

$
0
0
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Al Haji Mussa Salimu amemjibu mwanadada mkosoaji wa mtandaoni Mange Kimambi kwa kudai kuwa huu ndiyo mwaka wake wa mwisho kutumia mikono pamoja na ulimi wake kutukana watu.

Sheikh huyo amesema kwamba kutokana na kitendo hicho cha Mwanadada huyo kumuanika mtandaoni na kumtolea maneno machafu yeye kama kiongozi wa dini atarudi kwenda kushtaki katika mahakama ya mbinguni ambayo haina rushwa.

Kauli hiyo ya Sheikh Mkuu imekuja ikiwa ni siku moja tangu ianze kusambaa picha yake mitandaoni na kuanza kutuhumiwa kuwa anashiriki katika kampeni za uchaguzi mdogo kukisaidia Chama Cha Mapinduzi

"Tutarejea katika mahakama ya mbinguni kwani mahakama ya Mwenyezi Mungu haina rushwa na tutamuuliza  Mwenyezi Mungu kama alimpa Huyu Mange Kimambi mikono kwa ajilli ya kudhalilisha na kuvunja heshma za watu. Amekuwa akiwatukana viongozi wa serikali lakini kwa hekima zao wamemnyamazia kimya.

"Tunamuonya acheze na namba nyingine lakini siyo viongozi wa dini kwani wao wana mahakama ya kushatakia. Huu utakuwa mwaka wake wa mwisho kutumia ulimi au mikono yake kudhalilisha watu".-Al Haji Mussa Salimu .

Hata hivyo Sheikh huyo amesema kwamba wapo watu wengi waliompa rai ya kutomjibu Mange Kimambi  na kwamba kumjibu kwake kutamfanya atukanwe sana lakini amesema kwamba mwanadada huyo aendelee kutukana kwani dua ya mwenye kudhulumiwa haina kizuizi na kama anaishi hapa duniani basi afahamu kwamba hataendelea kuwa salama na amejihalalishia mwenyewe kwa ulimi wake na mikono yake.

Waziri Mwigulu: “Mikoa ya Kaskazini inaongoza kwa wahamiaji haramu”

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Mwigulu Nchemba amelitaka jeshi la polisi kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa na kwamba taasisi hiyo ndiyo inayoshughulika na haki za watu na wasipofanya kwa uadilifu yapo madhara makubwa kwa jamii na kutoka kwa wahalifu.

Akizungumza  katika uzinduzi wa ujenzi wa Kituo cha polisi Wilaya ya Pangani jana, Dk Mwigulu alisema kuwa wilaya ya Pangani ni lango ambalo wahalifu hasa wahamiaji haramu hupitia kwenda kusini mwa Tanzania.

‘’Kamateni wahalifu wote wanaoingia kimagendo au wanaoingiza mizigo kimagendo hakuna mjadala kamateni na wafikisheni katika vyombo vya sheria ,’’alisema Dk Mwigulu.

Kwa mujibu wa Dk Mwigulu, Mikoa ya kaskazini mwa Tanzania inaongoza kwa kuingiza wahamiaji haramu na bidhaa kwa magendo kwasababu ipo mipakani hivyo kuamua kuchangia vifaa vya ujenzi ili kuunga mkono juhudi hizo.

‘’Ujenzi huu wa kituo cha polisi utasaidia kuimarisha ulinzi na usalama zaidi hivyo mimi nitachangia nondo 150 baada ya mifuko 450 ya cement kupatikana basi ujenzi uanze haraka iwezekanavyo na kituo kiwe cha hali ya juu kikubwa.’’ alisisitiza

Kwa upande wake, Mkuu wa Polisi wilaya hiyo, Mrakibu Mwandamizi wa polisi Christina Musyani amesema kuwa wilaya hiyo ina vituo vitatu pekee vya polisi ambavyo havitoshi na mazingira yake hayaridhishi.

Alisema wameamua kuanza ujenzi wa kituo hicho ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wakazi wa eneo hilo ambao kwa sasa hulazimika kusafiri umbali mrefu kutafuta vituo vya polisi.

"Kwa kushirikiana na wananchi, Mbunge na halmashauri tumeamua kuanza ujenzi wa kituo cha kisasa ,’’ alisema Christina.

Maofisa wa Jumuiya ya Ulaya (EU) Wamtembelea Tundu Lissu Kumjulia Hali

$
0
0
Maofisa watatu wa Jumuiya ya Ulaya (EU) jana  Februari 5,2018 wamemtembelea Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu anayeendelea na matibabu nchini Ubelgiji.

Lissu alishambuliwa kwa zaidi ya risasi 30, Septemba 7 mwaka jana na kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na siku hiyohiyo alihamishiwa Hospitali ya Nairobi alilazwa hadi Januari 6,2018  alipohamishiwa Ubelgiji katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven, anakoendelea na matibabu.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa jana Februari 5,2018 Lissu amewataja maofisa hao kuwa ni Mkuu wa Idara ya Pembe ya Afrika na Afrika Mashariki katika Wizara ya Nje ya EU, Patrick Simonnet.

Wengine ni Mkuu wa Dawati la Tanzania katika EU, Marta Szilagyi, Vania Bonalbert ambaye ni ofisa wa ubalozi wa EU Tanzania anayeshughulikia masuala ya utawala bora na haki za binadamu na Hortensia May Lyatuu.

Amesema ujumbe wa maofisa hao mbali ya kumjulia hali walifanya mazungumzo ya masuala mbali mbali yanayohusu Tanzania.

Bombardier Nyingine na Boeing 787 Kutua Nchini Julai Mwaka Huu

$
0
0
Ndege mbili; moja aina ya Bombardier na nyingine kubwa Boeing 787 yenye uwezo wa kubeba abiria 262 zilizonunuliwa na serikali, zinatarajiwa kuwasili nchini Julai mwaka huu.

Serikali imenunua ndege hizo ikiwa ni mkakati wa kuimarisha Shirika la Ndege (ATCL) ili limudu ushindani kwenye biashara ya kusafirisha abiria na kujiendesha kwa faida.

Akiwasilisha taarifa ya shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwa kipindi cha Januari 2017 hadi, jana, mjini hapa, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Prof. Norman Sigalla, alisema wamejulishwa kuwa pamoja na ndege mbili mpya aina ya Dash 8 Q400, Julai serikali inategemea kupokea ndege zingine mbili ambapo moja ni Dash 8 Q400 na nyingine aina ya Boeing 787 yenye uwezo wa kubeba abiria 262.

Alisema kwa sasa ATCL ina ndege tatu zinazofanya safari ndani na nje ya nchi, lakini akasisitiza kuwa biashara ya ndege inahitaji mikakati mikubwa ya kibiashara kuweza kuingia katika soko la ushindani.

"ATCL iangaliwe kama kampuni ya kibiashara na siyo kutoa huduma na ijitangaze kwenye vyombo rasmi vya kimataifa ambavyo huonyesha safari za ndege duniani," alisema.

"Kampuni ijipange kuingia katika soko kwa kujitangaza kwenye vyombo vya habari, majarida, vipeperushi, kujali wateja, kuwa na bei nafuu ili kuhakikisha abiria wengi wanatumia ndege hizo."

Prof. Sigalla pia alisema Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) inashauriwa kuhakikisha viwanja vya ndege visivyokuwa na hati vinapimwa kisha kupatiwa hati miliki.

Alisema viwanja hivyo pia vinapaswa kuwekewa uzio kuepusha uvamizi wa maeneo jambo ambalo huleta migogoro na wananchi.

"Ili kuongeza udhibiti na ulinzi katika viwanja vya ndege vilivyopo mipakani kama vile Mtwara, Kigoma na Kagera kuepusha viwanja hivyo kupitishwa biashara haramu," alisema.

Mahakama yaagiza Nabii Titto apime upya akili

$
0
0
MAHAKAMA ya Wilaya ya Dodoma imeagiza mkazi wa mtaa wa Ng’ong’ona Manispaa ya Dodoma Tito Machibya, maarufu kama ‘Nabii Tito’ (45) kupimwa akili upya katika Taasisi ya Afya ya Akili ya Mirembe Isanga mkoani Dodoma ili kujiridhisha kama ana matatizo ya akili.

Licha ya kuagizwa mtuhumiwa huyo kufanyiwa vipimo upya, mahakama pia imetaka kuwasilishwa kwa vielelezo kama kweli ana tatizo hilo kama alivyoieleza mahakama.

Nabii Tito anashtakiwa kwa kosa la kujaribu kujiua kwa kutumia wembe.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, James Karayemaha, alisema jana kuwa kutokana na mshtakiwa kuieleza mahakama kuwa ana matatizo ya akili na alifanya tukio hilo kutokana na kusikia vitu ambavyo vilikuwa vinamwamuru akate, mahakama itabidi ipate vielelezo ambavyo vitathibitisha anachokisema.

Karayemaha alisema kutokana na kifungu namba 219 (2) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai, kama mshtakiwa atabainika kweli ana matatizo ya afya ya akili, mahakama itaamua kuwa alivyofanya tukio hilo hakuwa na akili timamu, hivyo hana hatia.

“Mshitakiwa anadai kuwa ana matatizo ya akili na amekuwa akitibiwa katika hospitali mbalimbli ikiwemo ya Maweni. Mahakama hii inaagiza vielelezo vyake vyote viletwe hapa lakini pia apelekwe kwenda kufanyiwa uchunguzi wa afya ya akili Mirembe Isanga,” alisema Karayemaha.

Pia alisema kama mshtakiwa atabainika kuwa hana tatizo lolote la afya ya akili kwa mujibu wa vielelezo vyake pamoja na vipimo atakavyofanyiwa, atakuwa na kesi ya kujibu.

“Kutokana na hili aliloiambia mahakama kuwa ana matatizo ya akili hata suala la dhamana tunaliweka pembeni kwanza kwa sababu hawezi kujieleza lakini kama itabainika kuwa hana matatizo ya akili kutokana na vielelezo vitakavyoletwa pamoja na vipimo vitakavyofanyika, suala la dhamana litafanyiwa kazi,"alisema.

Hata hivyo alisema mshtakiwa huyo anarudi rumande hadi kesi hiyo itakapotajwa Februari 19, mwaka huu.

Wakati kesi itakapotajwa vielelezo vyote pamoja na vipimo vinatakiwa kuwa tayari vimeshawasilishwa mbele ya mahakama hiyo.

Nabii Tito anashtakiwa kwa tuhuma za kutaka kujiua kwa kujikata


CHADEMA Yapata Pigo Tena....Ni Baada ya Mgombea Wake Kuhamia CCM Siku Tatu Baada ya Kuzindua Kampeni

$
0
0
Chadema kimepata pigo baada ya mgombea wake wa udiwani Kata ya Manzase wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma, Mashaka Chalo kujiunga na CCM pamoja na wanachama wengine 131.

Chalo amehama Chadema siku ya tatu tangu chama hicho kikuu cha upinzani nchini kuzindua kampeni katika Kata hiyo na kunadiwa jukwaani na mbunge wa viti maalum, Kunti Majala.

Uchaguzi wa ubunge jimbo la Siha, Kinondoni na katika Kata 10 nchini utafanyika Februari 17, 2018. Uchaguzi katika Kata hiyo unafanyika baada ya aliyekuwa diwani, Peter Madanya (CCM), kufariki dunia mwishoni mwa mwaka jana.

Mgombea huyo amehamia CCM  Februari 4, 2018 katika kijiji cha Manzase wakati wa uzinduzi wa kampeni za chama hicho na kupokewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Rodrick Mpogolo.

Mbunge wa Mtera (CCM),  Livingstone Lusinde amesema uamuzi wa Chalo kujiuzulu ni ushindi kwa chama tawala.

“Mpogolo unaweza kufungua kampeni hizi na kisha kuzifunga maana kazi imekwisha. Tulikuwa na  wagombea watatu, lakini kuondoka kwa huyu,  CCM tunaona kazi imekwisha. Wagombea wengine waliobaki  hata tukilala usingizi hakuna kitu ushindi ni wetu,” amesema.

Mgombea wa CCM katika Kata hiyo ni Amosi Mloha.

Lusinde amesema Chadema walimpitisha Chalo dakika za mwisho kuwania udiwani bila kujua kuwa alikuwa pandikizi la CCM.

Akizungumza katika mkutano huo Chalo amesema amerejea CCM kwa sababu ni chama chake na kimemlea.

Baunsa Anayedaiwa Kumuua Mowzey Radio Atiwa Mbaroni

$
0
0
Mtuhumiwa namba moja ambaye anayedaiwa kuhusika na kifo cha msanii muziki nchini Uganda, Mowzey Radio amekamtwa na Jeshi la Polisi nchini humo.

Kijana Wamala Godfrey mwenye umri wa miaka 28 ndiye alikuwa akisakwa na jeshi la polisi kama mtuhumiwa mkuu mara baada ya mmiliki wa bar, Egesa George na Meneja wake kilipotokea kifo cha Radio kushikiliwa na Polisi.

Wamala alikamatwa katika eneo la Kyengera alipokuwa amejificha kwa siku kadhaa nyumbani kwa rafiki yake. Wamala amehamishiwa mjini Entebbe.

Mwimbaji Mowzey Radio alifariki dunia Februari Mosi mwaka huu kutokana na majeraha ambayo aliyapata kichwani kufuatia ugomvi katika bar hiyo.

Kamanda wa Polisi Kampala, CP. Frank Mwesigwa amethibitisha kushikiliwa kwa Wamala Godfrey na kueleza kuwa kwa sasa wanaandaa majalada ili kuweza kumfikisha mahakamani.

Dk Slaa: Sijaja Tanzania kuapishwa kuwa balozi

$
0
0
Balozi mteule, Dk Willibrod Slaa  amesema amekuja nchini kwa ajili ya kushughulikia usajili wa Hospitali ya CCBRT.

Katibu mkuu huyo wa zamani wa Chadema, ametoa kauli hiyo leo Februari 6, 2018 wakati akihojiwa katika kipindi cha 360 kinachorushwa na Kituo cha Televisheni ya Clouds.

“Familia yangu nimeiacha Canada, wengine wanajua, sikuja kwa sababu ya ubalozi. Mimi ni mwenyekiti wa CCBRT ndicho kimenileta na wengine mnafahamu katika nchi yetu mengi yanafanyika,” amesema.

Novemba 23 mwaka jana, Rais John Magufuli alimteua Dk Slaa kuwa balozi, lakini mpaka sasa hajaapishwa na kupangiwa kituo cha kazi.

Dk Slaa ambaye kwa sasa anaishi Canada alitangaza kuachana na siasa kutokana na kutofautiana na chama chake katika kumpokea Edward Lowassa aliyehama kutoka CCM na baadaye kupitishwa kuwa mgombea urais kupitia muungano wa Ukawa.

Alisema chama chake hakikutekeleza makubaliano waliyoafikiana ya kuwapokea baadhi ya makada wa CCM akiwamo Lowassa.

Januari 29, 2018, Dk Slaa alikutana na kufanya mazungumzo na Rais Magufuli, Ikulu Dar es Salaam na kumshukuru kwa kumteua kuwa Balozi na kuahidi kuwa yupo tayari kutekeleza majukumu atakayopangiwa kwa kutanguliza maslahi ya Taifa.

Katika kipindi hicho, Dk Slaa ameulizwa kama amekuja kula kiapo na kupangiwa kituo cha kazi, lakini amepinga jambo hilo na kubainisha kuwa amekuja kushughulikia usajili wa hospitali hiyo kwa kuwa yeye ni mwenyekiti wa bodi.

Amesema kwa mujibu wa mabadiliko ya sheria, CCBRT inatakiwa kujiandikisha upya vinginevyo itafutwa.

Kuhusu taarifa kuwa ameajiriwa katika duka kubwa la bidhaa za nyumbani (Supermarket) la Costco lililopo Oakville, Toronto nchini Canada, amesema: “Hizo ni propanganda nisingependa kuzizungumza lakini Supermarket inayozungumzwa si kama mnavyofikiri ni kubwa.

“Kitu kikubwa tunatofautiana katika mtazamo, fikra  tunavyofanya vitu vyetu. Canada haina mwenyewe kuna raia wa kutoka kila nchi. Sisi hapa tunasema hapa kazi tu lakini kule ni maisha. Unakuta waziri anatoka ofisini kwake anakwenda kufanya kazi nyingine, baadaye anatoka na kwenda kufanya nyingine. Kufanya kazi tatu ni kawaida.”

Ametolea mfano ufanyaji kazi wa Canada na Tanzania amesema baadhi ya Watanzania huingia ofisini na kusoma magazeti, au kutumia simu kufanya biashara zao.

“Canada utaingia ofisini na simu au ipad lakini utaiacha getini na matokeo yake nchi ile ni matajiri. Watu ni matajiri kila mtu ana utambuliso wa maisha mazuri ni kwa sababu wanafanya kazi na huduma zote ziko vizuri,” amesema.

Kuhusu kufunga ndoa amesema: “Siasa za Tanzania zilichangia mimi kutokufunga ndoa kwa kipindi chote lakini Februari 2016 kule Canada nilifunga ndoa (na Josephine Mushumbusi), ile si ndoa kwani tulishakaa, kanisa ilichokuja kufanya ni kuhalalisha tu.”

Nassari afikishwa mahakamani Arumeru

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru akisubiri kusomewa shitaka linalomkabili.

Nasari amesema jana alikwenda Kituo cha Polisi Usa River kufuatilia silaha yake iliyochukuliwa na askari wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2014.

Nassari amesema alipofika polisi alielezwa kuwa ana kesi ya kumshambulia mtendaji kosa analodaiwa kutenda mwaka 2014 .

Sheki Mfinanga ambaye ni wakili wa Nassari amesema hajui mteja wake anakabiliwa na shtaka gani.

"Jana walisema alishambulia lakini hatujui leo anashitakiwa kwa kosa gani ndiyo tunasubiri," amesema.

Chadema Hawamwamini Msimamizi Uchaguzi Kinondoni

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemkataa msimamizi wa uchaguzi wa ubunge jimbo la Kinondoni kwa madai kuwa ameshindwa kusimamia taratibu za uchaguzi.

Pia, chama hicho kikuu cha upinzani nchini kimemwandikia barua Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Simon Sirro na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wakikituhumu CCM  kuandaa mikakati ya kufanya vurugu siku ya uchaguzi huo, Februari 17.

Hayo yameelezwa leo Februari 6, 2018 na Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema, Benson Kigaila katika mkutano wake na waandishi wa habari.

Kigaila amesema mwenendo wa uchaguzi, hasa kamati ya maadili ya Kinondoni inayoongozwa na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli inasimamia mambo isiyoyahusu.

Amesema malalamiko yanayotolewa ni ya kijinai na hayawezi kufanyiwa kazi na kamati ya maadili, “Kimsingi kamati ya maadili haina uwezo nayo, yanapaswa kupelekwa polisi yenye jukumu ya kufanya uchunguzi.”

"Kamati ya maadili haishughulikii masuala ya jinai, watu wakipiga, wakipigwa wanashughulikiwa na polisi. Mkurugenzi ni msimamizi wa uchaguzi lakini amekuwa akiyashughulikia kinyume cha kanuni," amesema.

Amesema katika barua hiyo wameeleza mienendo ya mkurugenzi huyo wakidai kuwa si mizuri, “Hatumkubali, hatumtaki, aondolewe na tunapinga kwani hawezi kutenda haki.”

Amesema suala la jinai ambalo Kagurumjuli  analishughulikia ni la madai ya mwanachama wa CCM kupigwa na vijana wa Chadema, “Hatujajua hao vijana wanaotuhumiwa ni wa Chadema au la lakini hata kama ni kweli, mwanachama mmoja huwezi kuiwajibisha Chadema."

Katika mkutano huo, Kigaila amedai CCM wameanza  kuandaa vijana kufanya vurugu katika uchaguzi huo na  kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua hatua.

"Tumeandika barua kwa IGP na NEC. Tumesema yeyote atakayejeruhiwa CCM iwajibike kwani imeanza kusambaza silaha, mashoka, nondo na mapanga," amedai Kigaila na kwamba barua hizo wanazipeleka leo katika taasisi hizo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Operesheni ya Kampeni Kinondoni, Frederick Sumaye amesema tuhuma hizo ana imani zitafanyiwa kazi.

Waziri Mkuu huyo wa zamani amesema jitihada kubwa zinapaswa kufanyika nchini ili nchi kutoondolewa katika mfumo wa vyama vingi kwa madai kuwa vyombo vinavyosimamia uchaguzi vinahakikisha wapinzani hawashindi.

"Tunaitaka NEC katika chaguzi hizi itende haki, Polisi wanaosimamia amani wote watende haki ili uchaguzi ufanyike kwa amani. Wasimamizi wa uchaguzi watende haki," amesema Sumaye.

UPDATES: Nassari ashtakiwa kwa kesi ya shambulio

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru kujibu shtaka la shambulio.

Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Fortunatus Muhalila mbele ya hakimu Jasmine Abdul amedai Desemba 14,2014 Nassari alimshambulia Neeman Ngudu.

Anadaiwa kutenda kosa hilo eneo la Makiba kwa kumpiga mateke Ngudu na kumsababishia maumivu akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

Muhalila amedai upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na ameiomba Mahakama kupanga siku nyingine ya kutajwa shtaka hilo.

Nassari anayetetewa na wakili Sheki Mfinanga alikana kutenda kosa hilo.

Hakimu Abdul aliahirisha kesi hadi Machi 6,2018 itakapotajwa.

Nassari alidhaminiwa na diwani Gabriel Mwanda wa Kata ya Ambuseri aliyesaini bondi ya Sh5 milioni.

Jaji Mkuu akamatwa na Polisi.

$
0
0
Polisi nchini Maldives imemkamata Jaji Mkuu wa Mahakama ya Juu nchini humo huku mgogoro wa kisiasa ukiendelea kuwa katika hali mbaya kwenye nchi hiyo iliyoko katika bahari ta Hindi.

Jaji Mkuu Abdulla Saeed na Jaji Ali Hameed, walikamatwa na polisi baada ya nchi hiyo kutangaza hali ya hatari huku kukiwa hakuna maelezo yaliyotolewa na uchunguzi au mabadiliko juu ya mtafaruku huo ulipata kasi baada ya rais wa nchi hiyo Abdulla Yameen alipokataa kutii amri ya Mahakama ya kuwaachilia wafungwa wote wa kisiasa.

Maldives ni taifa dogo katika bahari ya Hindi likiviunganisha visiwa vidogo 1,192 na utalii ndiyo chanzo kikubwa cha mapato ya nchi hiyo. Wiki iliyopita Mahakama ya juu nchini humo iliamuru kuachiwa kwa wanasiasa wa upinzani na pia Mahakama hiyo iliamua kwamba mashitaka ya rais wa zamani wa nchi hiyo Mohamed Nasheed ya mwaka 2005 ambaye yuko uhamishoni yalikuwa kinyume na katiba.

Hatua hiyo ya Mahakama ya juu ilifuatiwa na tamko la Kamishna Mkuu wa Jeshi la Polisi ambaye alisema kuwa atatekekeleza amri ya Mahakama na mara baada ya kauli hiyo kamishna huyo alifukuzwa kazi na Rais Adulla Yameen huku jeshi la nchi hiyo likiamuriwa kukataa kumuondoa Rais Yameen madarakani.

Prof. Palamagamba ataja mamlaka ya Rais Magufuli Kuhusu Zanzibar

$
0
0
Waziri wa katiba na sheria Profesa. Palamagamba Kabudi amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli ana mamlaka yote ya kutoa maagizo kwa Mawaziri ambao wapo ndani ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Waziri Kabudi ametoa ufafanuzi huo leo (Jumanne) katika mkutano wa 10 kikao cha sita cha Bunge kinachoendelea mjini Dodoma wakati alipokuwa akijibu swali la nyongeza kutoka kwa Mbunge Juma kombo Hamadi alipotaka kufahamu Rais Magufuli ana mamlaka gani kikatiba ya kutoa maagizo kwa Waziri aliyepo katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

"Rais wa Muungano wa Tanzania anayo mamlaka ya mambo yote yanayohusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama nchi huru", amesema Prof. Palamagamba.

Pamoja na hayo,  Prof. Palamagamba ameendelea kufafanua baadhi ya mambo kuwa "katika masuala yote yanayohusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mkuu wa nchi ni mmoja tu tena ambaye ni Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na yeye peke yake ndio Amri Jeshi. Hakuna mtu mwingine yeyote wa kuyaamuru majeshi ya Tanzania isipokuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu yeye ndio kiongozi mkuu wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania".

Kwa upande mwingine, Prof. Palamagamba amesema Rais wa Zanzibar ni wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mwenye heshima na hadhi ya urais kwa mambo yote yasiyokuwa ya Muungano yanayohusu Zanzibar ambapo pia ni Mjumbe wa Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nafasi yake hiyo.

CCM yazungumzia kutekwa diwani wa CHADEMA

$
0
0
Mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Prof. Anna Tibaijuka amefunguka na kusema kuwa CCM hakihusiki kivyovyote vile na kutekwa kwa mgombea wa Udiwani wa CHADEMA Kata ya Buhaganza , Nelson Athanas ambaye alipatikana Februari 5, 2018 akiwa hajitambui.

Tibaijuka amedai kuwa kuwekuwepo na tetesi kuwa chama chake kimehusika na kitendo hicho cha kinyama na kudai kuwa hilo ni lengo la kutaka kuvuruga uchaguzi huo hivyo amesisitiza kuwa chama chake hakihusiki na unyama huo.

"Kamati ya siasa ya wilaya ya Muleba imeamua kuwajulisha wananchi rasmi na wapiga kura wa Kata ya Buhaganza na Umma wa Watanzania kiumjula kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakiusiki kwa lolote lile na tuhuma hizo zinazoongozwa kwake na viongozi wake kwa nia mbaya ya kuwachafua na kukichafua chama na kuvuruga uchaguzi baada ya kuzidiwa.

"CCM kimejitayarisha vyema kwa ushindani na kinaamini mgombea wake Bi. Jenitha Tibihenda anatosha hivyo hakuna haja ya kumteka mshindani wake yoyote yule tupo imara" alisema Tibaijuka

Aidha Tibaijuka alivitaka vyombo vya usalama kufanya uchunguzi wa tukio hilo kwa haraka ili watu waliotenda tukio hilo ovu waweze kupatikana kwa haraka na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Mgombea wa udiwani Kata ya Buhangaza, Muleba (CHADEMA), Athanasio Makoti aliyekuwa amepotea tangu Februari 2, 2018 alipatikana Februari 5, 2018 akiwa hajitambui, CHADEMA imesema alitupwa barabarani maeneo ya Hospitali ya Kagondo na sasa aendelea kupatiwa matibabu. 

Habari Ziliizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya February 7

Rais Magufuli azindua Kituo cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli  tarehe 06 Februari, 2018 amezindua Kituo cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi (Comprehensive Training Center – CTC) kilichopo Mapinga katika Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.

Kituo hicho kimejengwa kwa msaada kutoka Jeshi la Ukombozi la Watu wa China kwa gharama ya Shilingi Bilioni 67.87 na kitatumika kutoa mafunzo ya kijeshi ya kisasa yatakayowawezesha askari kukabiliana na vitisho vya kisasa vya kiusalama.

Kabla ya kuzindua kituo hicho Mhe. Rais Magufuli na Balozi wa China hapa nchini Mhe.  Wang Ke wameshuhudia makabidhiano ya kituo hicho kutoka Jeshi la Ukombozi la Wananchi wa China lililowakilishwa na Naibu Mkuu wa Idara ya Mafunzo na Utawala ya Kamisheni Kuu ya Jeshi hilo Jenerali Yang Jian kwenda kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lililowakilishwa na Meja Jenerali Yakub Hassan Mohamed.

Mhe. Rais Magufuli pia ameshuhudia mazoezi ya kijeshi yaliyofanywa katika kituo hicho yakiwemo shambulizi la kutokea baharini (amphibian landing), makomandoo kukabiliana na magaidi na kupiga shabaha kwa kutumia miundombinu ya kisasa.

Akizungumza na Maafisa, Askari na wananchi waliojitokeza kushuhudia tukio la makabidhiano ya kituo hicho Mhe. Rais Magufuli amelishukuru Jeshi la Ukombozi la Watu wa China na Serikali ya China kwa kutoa msaada wa kujengwa kwa kituo hicho na amesema Serikali ya Awamu ya Tano inathamini na kutambua mchango wa China katika Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania.

Mhe. Rais Magufuli amesema China imeendelea kudhihirisha urafiki na udugu wake na Tanzania kwani licha ya kujenga kituo hicho pia imetoa msaada wa kujenga kituo cha mafunzo ya kijeshi ya anga cha Ngerengere Mkoani Morogoro na miradi mingine ya maendeleo ya jamii na hivyo amemuomba Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke kufikisha shukrani zake kwa Rais wa China Mhe. Xi Jinping.

Mhe. Wang Ke na Jen. Yang Jian wamesema China imejenga kituo hicho cha mafunzo maalum ya kijeshi ambacho ni alama nyingine ya uhusiano na ushirikiano wa kirafiki na kidugu kati yake na Tanzania na wameipongeza JWTZ kwa kupata kituo ambacho wanaamini kitatumika kuimarisha ulinzi na usalama wa Tanzania na nchi nyingine za Afrika.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Venance Salvatory Mabeyo amesema miundo ya kituo hicho inakifanya kuwa kituo cha kimataifa kilicho bora zaidi Afrika Mashariki na Kati kitakachoweza kutoa mafunzo ya kisasa kwa askari wengi na amemuomba Mhe. Rais Magufuli kusaidia ujenzi wa daraja la mto Mpigi litakalokiunganisha na barabara ya kwenda Dar es Salaam.

Pamoja na kukubali ombi hilo Mhe. Rais Magufuli pia amekubali maombi ya Jen. Mabeyo ya kupeleka maji, umeme na barabara katika eneo ambalo China imekubali kutoa msaada wa kujenga makao makuu ya JWTZ Mkoani Dodoma na ameahidi kuziagiza wizara husika kutekeleza maombi hayo haraka.

Tukio la kukabidhiwa kwa kituo cha mafunzo maalum ya kijeshi limehudhuriwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amezungumza na wananchi wa Mapinga waliosimamisha msafara wake na kumuomba awasaidie kulipwa fidia kufuatia maeneo yao kuchukuliwa kwa ajili ya miradi ukiwemo mradi wa ujenzi wa kituo hicho cha mafunzo cha jeshi na kuvunjiwa nyumba zao katika eneo la Makurunge.

Katika majibu yake Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali haiwezi kurudia kuwalipa watu ambao tayari walishalipwa fidia na hawezi kuwatetea watu ambao wamevunja sheria kwa kuvamia maeneo yasiyokuwa yao.

Mhe. Rais Magufuli pia amesema Serikali ina dhamira ya dhati ya kutekeleza  mradi wa bandari na eneo la uwekezaji la Bagamoyo na amewataka watu wote waliolipwa fidia wakati hawakuwa na maeneo warejeshe fedha za Serikali, waliolipwa fidia kuondoka katika maeneo yaliyolipiwa, na kwa wale ambao hawajalipwa fidia waendelee kutumia maeneo yao kwa shughuli zao mbalimbali.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
06 Februari, 2018

Prof. Kabudi: “Hakuna mgongano wa kimamlaka katika katiba ya Tanzania na Zanzibar”

$
0
0
Na Beatrice Lyimo- MAELEZO, DODOMA
Serikali imesema Kikatiba hakuna mgongano wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar unaosababisha ongezeko kubwa la kero za Muungano na mgongano wa kimamlaka baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi bungeni jana mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Wingi Mhe. Juma Kombo lililohusu mgongano wa Katiba hizo.

Prof Kabudi alisema kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka utaratibu mahususi wa kushughulikia tafsiri ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano na utekelezaji wake inayobishaniwa kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

“Hadi sasa hakuna upande wowote baina ya Serikali hizi mbili ambao unatafsiri tofauti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano au utekelezaji wake”

“Hivyo kwa kuzingatia kuwa hakuna mgongano wa Katiba kati ya  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Serikali haina sababu ya kuleta mapendekezo ya mabadiliko ya Katiba ili kuondoa changamoto hiyo ambayo haipo.” alifafanua Prof Kabudi.

Akizunguzmzia kuhusu mgongano wa kimamlaka Prof. Kabudi alisema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anamamlaka yote katika masuala yanayohusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, akijibu swali la Mbunge wa Korogwe Mjini Mary Chandanda kuhusu upandishwaji vyeo kwa Mahakimu na Watumishi wa Mahakama, Prof Kabudi alisema kuwa suala la kupandisha vyeo watumishi wenye sifa stahiki ni wajibu endelevu kwa Serikali.

“Mahakama ya Tanzania imekuwa ikichukua hatua kuwapandisha Mahakimu na Watumishi wa ngazi mbalimbali vyeo kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa kisheria ikiwa ni pamoja na muda wa utumishi kazini, utendaji kazi, weledi na maadili pamoja na upatikanaj wa vibali kutoka Idara Kuu ya Utumishi,” alisema Prof Kabudi.

Hata hivyo, Prof. Kabudi alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2012/2013 jumla ya Mahakimu na Wasaidizi wa Sheria wa Majaji 52 walipandishwa vyeo, mwaka 2013/2014 jumla ya watumishi 200 walipandishwa vyeo, mwaka 2014/2015 Mahakimu na Wasaidizi wa Sheria wa Majaji 22 na watumishi 686 walipandishwa vyeo na mwaka 2015/2016 Mahakimu na Wasaidizi wa Sheria 59 na watumishi 447 walipandishwa vyeo.


Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images