Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tume Ya Uchaguzi (NEC) Yajibu Upotoshwaji Wa CHADEMA Kuhusu Kuhamisha Vituo Jimbo La Kinondoni

$
0
0
Hussein Makame, NEC
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imesema uamuzi wa kuhamisha vituo 46 vya kupigia kura katika jimbo la Kinondoni umezingatia matakwa ya kanuni za Uchaguzi kwa kuvishirikisha vyama vyote vya siasa ikiwemo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani jijini Dar es Salaam, kufuatia taarifa za upotoshaji zilizotolewa na baadhi ya magazeti zinazodai kuwa Chadema hakikushirikishwa katika uamuzi wa kuhamisha vituo hivyo.

Alisema kabla ya uamuzi wa kubadilisha vituo hivyo, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kinondoni iliitisha mkutano na vyama vya siasa tarehe 30 Januari, 2018 na wawakilishi 26 walishiriki kwenye mkutano huo wakiwemo wawakilishi wa Chadema.

“Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kushirikiana na vyama vya siasa katika kikao kilichofanyika tarehe 30 mwezi Januari mwaka huu walikubaliana kuhamisha vituo 46 na katika vituo hivyo vituo 16 viko kata ya Kigogo, vituo 8 viko kwenye kata ya  Mwananyamala na vituo 22 viko kwenye kata ya Kijitonyama” alisema Kailima.

Alifafanua kuwa kwa mujibu wa kifunga cha 21 (1) cha kanuni za Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, vituo vya kupigia kura havitakiwa kuwa kwenye maeneo ya watu binafsi, nyumba za mashabiki wa vyama vya siasa au maeneo ya majeshi na ibada.

“Nimesikitishwa na kauli ya Chadema eti hawakushirikishwa, nimesikitishwa kwa sababu kumbukumbu za mikutano zilizopo tarehe 30 Januari mwaka huu, chama cha Chadema kiliwakilishwa na Mwenyekiti wa Wilaya Bw. Mustafa Muro pamoja na Katibu wa Wilaya Bw. Shabani Kirita” alibainisha Kailima.

Alifafanua kuwa wawakilishi hao walihudhuria mkutano wa msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Kinondoni na vyama vya siasa na katika mkutano huo kulikuwa na ajenda moja tu kuhusu kuhamisha vituo vya kupigia kura na vyama vyote kwa pamoja vilikubaliana kikiwemo Chadema.

“Unaposema chama cha Chadema hakikuhusishwa ninapata masikitiko makubwa sana.Tume ya Taifa ya Uchaguzi haiwezi kuingilia mawasiliana ya ndani ya chama husika, kwa hiyo kama hakuna mawasiliano kati ya makao makuu na ngazi ya Wilaya hilo sio tatizo la Tume” alisema Kailima.

Alifafanua kuwa katika kata ya Kigogo kuna baadhi ya vituo vya kupigia kura vilikuwa ndani ya msikiti wa Kigogo na vingine vilikuwa ndani ya eneo la Zahanati eneo ambalo lilikuwa dogo kutosha kwa ajili vituo vya kupigia kura.

Kailima aliongeza kuwa, vituo 8 vya Mwananyamala vilikuwa kwenye eneo ambalo wananchi walikuwa wanalilalamikia, vyama vya siasa vikaridhia kwamba vituo hivyo vihamishwe na vituo 6 vikapelekwa kwenye kata inayohusika na vituo 2 vikapelekwa uwanja wa Kopa.

Akizungumzia vituo 22 kwenye kata ya Kijitonyama, Kailima alisema vyama vyote vilikubaliana kuvihamisha, hivyo Chadema kikisema havikukubaliana ndipo inapoleta shida.

Alisema Maelekezo kwa Wasimamizi wa Uchaguzi kipengele cha 9 (2) (C) kinasema kabla vituo vya kupigia kura havijahamishwa ni lazima Tume ishirikiane na vyama vya siasa na Tume imetimiza takwa hilo la kikanuni na vyama viliitwa vikakubali.

“Ukisema huwezi kuhamisha vituo kabla hujafanya Uboreshaji, huwezi kuacha makosa yakaendelea kuwa makosa.Hatujahamisha kutoa mkoa mmoja kwenda mwingine, bali tumehamisha kwa ridhaa na vyama vikaridhia.

“Kwa hiyo niwasihi chama cha Chadema kabla hakijaanza kulaumu wawasiliane na wenzao kwenye ngazi husika.” Alisema Kailima.

Katika hatua nyingine, Kailima amelisihi gazeti la Mwananchi, litoe habari sahihi kuhusu Tume na kuacha kuandika habari zinazoihusu Tume bila ya kuwasiliana nayo ‘kubalance’ kuhusu habari husika.

“Nalisihi gazeti la Mwananchi, tunaliheshimi ni gazeti bora na gazeti linaloheshimika, lakini nilisihi kabla halijatoa habari lazima lifanye balance ya habari” alisema Kailima na kuongeza kuwa:

“Wenyewe walipowauliza Chadema wakasema hawakushirikishwa walitatakiwa kuchukua fursa ya kuwauliza Tume kama hawakushirikishwa.

“Kwa hiyo nilisihi kwa sababu si mara moja wala mara mbili wamekuwa wakitoa taarifa ambazo si sahihi kuhusu Tume, tunawasihi na kuwaomba wanapotaka kutoa habari za Tume watoe habari za Tume zikiwa sahihi”

Alifafanua kuwa kulitaka gazeti hilo kwamba hata linapotaka kukosoa ni  lazima likosoe kwa habari sahihi na sio kwa habari za upotoshaji na za upande mmoja.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0
Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Bashe Aichambua Serikali

$
0
0
Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM) amefunguka na kusema kuwa kwa twakimu mbalimbali ambazo zinatolewa na BoT zinaonyesha mambo hayapo sawa hivyo kuna haja kubwa kwa Serikali kupitia Waziri wa Fedha kubadili sera zake za kibajeti.

Bashe alisema hayo akiwa Bungeni na kudai takwimu mbalimbali kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT) mwaka 2011 mpaka Disemba 2017 zinaonyesha kuwa kuna mabadiliko makubwa na vitu kushuka kwa kasi kubwa.

"Umefika wakati kama nchi hasa Wizara yetu ya Fedha kukubali kubadili sera zake za kibajeti, nitatoa takwimu chache ambazo ukitazama takwimu hizi zinazoonekana kwenye taarifa za BoT kuanzia mwaka 2011 mpaka 2017, mzunguko wa fedha umeshuka kutoka asilimia 22% ya mwaka 211 mpaka asilimia 1.8% ya sasa hivi, ukiangalia export hasa ya mazao ya kilimo ambayo ndiyo yameajiri asilimia 70 Tanzania, ukichukua zao la Kahawa mwaka 2011 gross late yake ilikuwa asilimia 55% lakini sasa hivi ni asilimia -5.4, Cotton mwaka 2012 ilikuwa kwa asilimia 16% saizi imekuwa kwa asilimia - 3.8%, Sisal ndiyo imekuwa na ongezeko la asilimia 2.9 iliyokuwa mwaka 2012 saizi ipo kwa asilimia 4% .

"Manufacturing mwaka 2011 ilikuwa kwa asilimia 96% gross late sasa hivi imekuwa kwa asilimia -244, tafsiri yake ni ndogo tu sera zetu hazichochei ukuaji wa biashara na uchumi katika nchi. 

"Takwimu zinaonyesha Watanzania tunakuwa kwa wastani wa asilimia 2% na kitu lakini ukuajia wetu wa kilimo ni asilimia 0.4% hakuna uwiano hapa hili ni jambo ambalo hata tukasema humu dani ya Bunge lisifurahishe upande wa Serikali kwa kauli zetu lakini tunajukumu la kusema ukweli na ni muhimu kabisa Wizara ya Fedha ikakubali kwamba sera za kibajeti za Wizara ya Fedha siyo rafiki katika kuchochea kukuza uchumi wetu"  alisema Bashe

Mgombea CHADEMA Atoweka

$
0
0
WAKATI kampeni za ubunge na udiwani zikiendelea, mgombea udiwani (Chadema) Kata ya Buhangaza wilayani Muleba amepotea katika mazingira ya kutatanisha.

Imeelezwa alipotea Februari 2,2018 alipokuwa akitokea Bukoba mjini kwenda nyumbani kwake Kijiji cha Buhangaza ikidaiwa ametekwa.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Isack Msangi amethibitisha kupokea taarifa za kupotea kwa mgombea huyo.

Amesema kuwa hawana madai kuwa ametekwa bali aliondoka nyumbani na hajarejea.

Msangi amesema polisi inawaomba wananchi kutoa ushirikiano bila kupotosha au kuegemea upande mmoja wa kisiasa kwa kutuhumu upande mwingine bali waungane kufanikisha kupatikana kwake.

Katibu wa uenezi wa Chadema jimbo la Muleba Kusini na mratibu wa chama hicho jimbo la Muleba Kaskazini, Hamisi Yusufu alisema jana  Februari 4,2018 kuwa mgombea huyo ni Athanasio Makoti (28).

Yusufu alisema Makoti ambaye ni Mchungaji wa Kanisa la AGT anashiriki uchaguzi mdogo wa udiwani utakaofanyika Februari 17. Anachuana na mgombea wa CCM, Jenitha Tibeyenda na wa NCCR -Mageuzi, Grason Anaseti.

Alisema Februari 2,2018 saa 12:00 jioni akitumia simu yake ya mkononi aliwajulisha viongozi wa Chadema ngazi ya wilaya kuwa alipanda gari lenye watu wanne kutoka Kijiji cha Mafumbo njia panda ya kwenda Kamachumu akielekea Kijiji cha Buhangaza.

Yusufu alisema baadaye ujumbe mfupi wa maneno (sms) ulitumwa kwa Advera Kalikwela, diwani wa viti maalumu (Chadema) Kata ya Ijumbi ukieleza, “Nimeteremka hapa Mafumbo kabla ya kufuatwa na bodaboda wangu nimezingirwa na gari lenye watu wanne mmoja mwanamke, mbele dereva wa kiume na vijana wengine wawili ni kama nimetekwa.”

Alisema baada ya ujumbe huo, simu ya Makoti iliita bila kupokewa na hadi sasa hakuna taarifa za kuonekana kwake na kwamba familia ilitoa taarifa polisi.

Egbert Makoti ambaye ni mdogo wa mgombea huyo amesema baada ya kuchukua fomu, ndugu yake aliwaeleza kuna watu ambao hakuwataja waliomtaka aachane na kata hiyo wakimtaka apokee Sh8 milioni lakini alikataa.

Katibu wa Baraza la Wazee la Chadema, Rodrick Lutembeka amesema chama hicho kitaendelea kumnadi katika kampeni zinazoendelea katika Kata ya Buhangaza.

Kata hiyo ina vijiji vitatu vya Buhangaza, Kashenge na Buyaga ikiwa na vitongoji 13 ikikadiriwa kuwa na zaidi ya wapiga kura waliojiandikisha 2,500.

Wastara amwaga chozi akiaga kwenda kutibiwa

$
0
0
Muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Wastara ameondoka nchini kuelekea India kwa ajili ya matibabu ya mguu wake ulioanza kumsumbua mwishoni mwa mwaka jana huku akiwashukuru watanazania na Vyombo vya Habari kwa kuwa pamoja naye kipindi alivyokuwa akihitaji msaada wa fedha.

Wastara akiongea na waandishi wa Habari jana Jumapili Februari 4, 2018 katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam, alisema “nina washukuru sana vyombo vya habari wote kwa moyo wa upendo walionesha kwa sababu bila ya wao hata mimi nisingekuwa Wastara. 

"Napenda kuwaambia watanzania kwamba tuamini sana maneno anayosema mtu kuliko neno analosema mtu mwingine kwa hiyo naamini kuna wengine watakuja na matatizo tujaribu kuwaangalia nawao pia”.

Na alipoulizwa kuhusu tuhuma za kutumia fedha za matibabu kwa starehe kama alivyowahi kuchangiwa kipindi cha nyuma na kwenda Dubai, Wastara alisema hajawahi kuchangiwa na Watanzania bali alisaidiwa na Makamu wa Rais na hakutumia kwa matumizi mengine.

“Kwanza niseme sijawahi kuchangiwa na Watanzania mimi kama mimi, mara ya kwanza nilipoumwa aliyenichangia asilimia kubwa alikuwa ni Makamu wa Rais, na uzuri ni kwamba mpaka nafika hospitalini nilikuwa nampigia simu. Kilichosababisha watu waseme baada ya kufika hospitali kama hivi ninavyokwambia wiki tatu linapotokea tatizo kama umefanyiwa Oparesheni au upasuaji wowote niliambiwa unauwezo wa kukaa au kuishi kwenye hoteli karibu na hospitali..Ndipo watu wa karibu yangu wa Oman wakawa wamenipa Visa nikaenda kukaa huko kwa muda.“alisema Wastara.

Mahakama ya Rufaa yamwondolea DPP mamlaka ya kuzuia dhamana za Washitakiwa

$
0
0
Mahakama ya Rufaa imemwondolea Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) mamlaka ya kuzuia dhamana ya mshtakiwa bila hata kulazimika kutoa sababu, baada ya kubatilisha kifungu cha 148 (4) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai, kinachompa mamlaka hayo.

Kifungu hicho kinampa DPP mamlaka ya kuizuia Mahakama au ofisa wa polisi kutoa dhamana kwa mshtakiwa au mtuhumiwa baada ya kuwasilisha hati ya maandishi, kwa maelezo kuwa usalama au masilahi ya Jamhuri yataathirika.

Mahakama hiyo katika hukumu ya rufaa ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya mwanaharakati wa haki za binadamu, Jeremia Mtobesya imesema kifungu hicho ni kinyume cha Katiba na ni batili.

Hukumu iliyotolewa na jopo la majaji watano wa Mahakama ya Rufaa imekubaliana na ya awali iliyotolewa na Mahakama Kuu.

Majaji waliosikiliza na kutoa hukumu ya rufaa hiyo ni Bernard Luanda (kiongozi wa jopo), Kipenka Mussa, Bethuel Mmila, Stellah Mugasha na Jacob Mwambegele.

Hukumu hiyo ilisomwa Ijumaa iliyopita na Msajili wa Mahakama ya Rufaa, John Kahyoza aliyesema kifungu hicho kwa jinsi kilivyo, Mahakama au ofisa wa Polisi anakuwa hana uchaguzi zaidi ya kumnyima dhamana mshtakiwa au mtuhumiwa.

Alisema kifungu hicho hakikidhi matakwa ya kisheria kwa kuwa haipaswi kuwa ya maelezo ya jumla na kinaweza kutoa mwanya wa matumizi mabaya ya mamlaka kwa DPP.

Baada ya kufanya rejea ya sheria na uamuzi wa kesi kadhaa za ndani na nje ya nchi, Kahyoza alisema Mahakama imejiridhisha kuwa masharti ya kifungu hicho ni kinyume cha Katiba na hivyo ni batili.

Akizungumzia  jana kuhusu hukumu hiyo, Mtobesya alisema Mahakama imeitoa kwa misingi ya kikatiba.

“Katiba ndivyo inavyoelekeza kuwa mtu yeyote ana haki ya kusikilizwa na kila mtu ana haki ya kuwa huru. Sasa iwapo hizo haki zinaweza zikaondolewa, kuna utaratibu ambao unawekwa kisheria,” alisema.

Mtobesya alisema, “Kwenye ngazi zote, Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa zimeangalia na kujiridhisha kwamba sawa hizo haki zinaweza kuwa si absolute (kamilifu) lakini je misingi ya kunyimwa hizo haki imefuatwa?”

Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikata rufaa akipinga hukumu ya Mahakama Kuu ya Desemba 22,2015 iliyotolewa na jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Kiongozi, wakati huo, Shaban Lila. Majaji wengine walikuwa Sekieti Kihiyo na Profesa Eudes Ruhangisa. Katika shauri la msingi la madai namba 29 la mwaka 2015, Mtobesya ambaye ni wakili wa kujitegemea alidai kifungu hicho kwa jinsi kilivyo kinamnyima mshtakiwa aliye mahakamani au mtuhumiwa aliye polisi haki ya kusikilizwa.

Katika hoja za maandishi, alidai kila kesi inaangaliwa kwa mazingira yake na kwamba, kitendo cha DPP kuzuia tu dhamana kwa madai kwamba itaathiri masilahi ya umma bila kutoa sababu kinamnyima haki mhusika.

Alidai maelezo hayo tu ya kuathiri masilahi ya umma hayatoshi bali anapaswa kwenda mbali zaidi na kutoa sababu na kisha mshtakiwa au mtuhumiwa naye apewe nafasi ya kusikilizwa ndipo Mahakama ipime na kutoa uamuzi kwa sababu hizo.

Mahakama Kuu katika hukumu yake ilikubaliana na hoja za Mtobesya, ikisema kifungu hicho kinamnyima mtu haki ya kusikilizwa na ni kinyume cha Ibara ya 13 (6) ya Katiba ya nchi.

Mahakama ilisema kifungu hicho kinaenda kinyume cha misingi ya kidemokrasia.

Hukumu hiyo katika kesi ya jinai, DPP na mshtakiwa wote wanakuwa na haki sawa lakini kifungu hicho kinaupa upande mmoja mamlaka zaidi na kuufanya mwingine kuwa dhaifu, hivyo kutokuwa na usawa.

Mahakama Kuu ilisema kifungu hicho kinaondoa mamlaka ya Mahakama kuwasikiliza wadaiwa.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali hakukubaliana na uamuzi huo, hivyo alikata rufaa Mahakama ya Rufaa akiwasilisha hoja tano za kuipinga. Wakati wa usikilizwaji aliondoa hoja tatu zikabaki mbili.

Pamoja na mambo mengine, AG aliipinga hukumu hiyo akidai kifungu hicho kiko sawa kwa kuwa kuna ibara za Katiba ambazo zinakifanya kiwe hivyo kilivyo, sawa na ibara ya 30 (2) (a) ya Katiba.

Mtobesya kupitia kwa wakili wake Mpale Mpoki alipinga hoja zilizotolewa na AG kupitia Wakili wa Serikali Mkuu, Vitalis Timon akidai kifungu hicho kwa namna kilivyo hakimpi fursa mshtakiwa kusikilizwa kabla ya kuzuiwa dhamana kwa hati ya DPP.

Wakili Mpoki alidai kifungu hicho kinakiuka ibara ya 13 (6) ya Katiba ya nchi, huku akiungwa mkono na Profesa Gamaliel Mgongo Fimbo aliyealikwa na Mahakama kutoa maoni ya kitaalamu.

Profesa Mgongo Fimbo pamoja na mambo mengine alisema kifungu kinachomzuia mshtakiwa kusikilizwa maombi yake ya dhamana au kupinga hati ya DPP, hakiweki usawa wa usikilizwaji, hivyo kinakiuka ibara ya 13 (6) (a) ya Katiba.

Tiba Asili ya Kuondoa Chunusi, Kupunguza Tumbo, Maziwa Makubwa na Nguvu za Kiume

$
0
0
Asilimia 90 ya wanaume hushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kiafya  kama vile kisukari, punyeto ambayo huathiri mfumo mzima wa wa misuli inayozalisha vichocheo ashiki , kutopata choo vizuri hali ambayo huchakiwa na kula chakula kisicho na asili,tumbo kuunguruma, kujaa gesi,kiuno kuuma, mgongo na miguu kufa ganzi

SUPER HOLO; Ni dawa itokanayo na miti shamba, ipo katika mfumo wa vidonge na unga. Hutibu na kumaliza tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa muda mfupi tu.,SUPER HOLO hurudisha heshima ya ndoa, itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-30. Itakupa hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3. Pia itaimarisha misuli iliyosinyaa na kulegea. Dawa hii hutumiwa kwa watu wa umrii wa miaka 20- 80

NZOGIWE ni dawaya maumbile.Hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo urefu wa nchi 4-8 na unene wa sentimita 2-4 za upenyo

NZOGOMA ni dawa asili ya miti shamba, huboresha mbegu za uzazi...huzibua mirija na kusafiisha ili kuweza kushika mimba au kutia mimba.

Pia tunayo dawa ya kupunguza tumbo, unene, maziwa makubwa, kuongeza hips, makalio na kutoa chunusi

TUNAPATIKANA MTONI MTONGANI. KANA HAUNA NAFASI YA KUFIKA UTALETEWA ULIPO. WASILIIANA NA DR. MBUSI.  PIGA SIMU NAMBA:   0718 431222

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Mgombea udiwani Chadema apatikana akiwa hajitambui

$
0
0
Mgombea udiwani (Chadema) Kata ya Buhangaza, Mchungaji Athanasio Makoti (28) aliyepotea Februari 2,2018 katika mazingira ya kutatanisha amepatikana akiwa hajitambui.

Makoti amepatikana leo Februari 5,2018 saa moja asubuhi, Katibu wa Chadema wilayani Muleba, Elisha Kabombo alisema alitelekezwa na watu wasiojulikana jirani na Hospitali ya Kagondo.

Amesema wananchi waliokuwa wakipita eneo hilo usiku wa kuamkia leo walimuona akiwa kando mwa  barabara ya kuelekea Bukoba, hivyo kumpeleka hospitali.

“Hali yake si nzuri kwa sababu hawezi kuzungumza vyema wala kuketi. Kawekewa dripu za maji. Tuzidi kumuombea,” amesema.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Isack Msangi amethibitisha kupokea taarifa za kupatikana mgombea huyo. Amesema vyombo vya dola vinamhoji ili kuendelea na uchunguzi.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Kagondo, Dk Humphrey Batungi alipoulizwa afya ya mgombea huyo amesema ni mapema kuzungumza.

“Ninaelekea kwenye kikao nitafute mchana baada ya dawa anazotumia mgonjwa kufanya kazi na huenda akawa na mabadiliko,” amesema Dk Batungi.

Katibu wa uenezi wa Chadema jimbo la Muleba Kusini na mratibu wa chama hicho jimbo la Muleba Kaskazini, Hamisi Yusufu amesema baada ya kufikishwa hospitali alikutwa na majeraha, huku akizungumza kwa shida.

Amesema mgombea huyo wa udiwani aliwaeleza amenyang’anywa fedha, waliomteka walimfunga kitambaa cheusi usoni na kumtaka asigombee uchaguzi utakaofanyika Februari 17,2018 na amekiri  kuwafahamu baadhi ya waliomteka.

Katika uchaguzi huo anachuana na mgombea wa CCM, Jenitha Tibeyenda na wa NCCR-Mageuzi, Grason Anaseti.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Aapishwa Rasmi Bungeni

$
0
0
Naibu Spika wa Bunge, Dkt.  Tulia Ackson amemwapisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Dkt. Adelardus Kilangi bungeni na kumkabidhi vitendea kazi kabla ya kuanza kwa Kikao cha Tano cha Mkutano wa 11 wa Bunge, Mjini Dodoma, leo Feb 5, 2018.
 
Dkt. Kilangi ambaye amekula kiapo cha uaminifu, aliteuliwa na Rais Dkt. John Pombe Mgufuli,  Februari Mosi, 2018 na Paul Ngwembe aliteuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Katika hatua nyingine,Magufuli alimtea aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju na naibu wake, Gerson Mdemu kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania ambao waliapishwa juzi Jumamosi, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Watumishi Wasiyoiunga Mkono CCM Kufukuzwa Kazi

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti amefunguka na kuwataka watumishi mbalimbali mkoani kwake ambao hawaiungi mkono Serikali ya awamu ya tano iliyopo chini ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuondoka mapema katika nafasi zao hizo.

Mnyeti amesema kuwa siku zote Chama Cha Mapinduzi ndiyo kimekuwa kikihangaika kuomba kura majukwaani huku viongozi mbalimbali wa chama hicho wakiwa si wanufaika wakubwa kulinganisha na watumishi, hivyo watumishi wanapaswa kutambua na kuiunga mkono Serikali ya CCM na kama hataki waondoke kwenye nafasi hizo.

"Wanaoumia kuomba kura majukwaani ni CCM anayekuja kula ugali na familia yake ni wewe mtumishi, unanufaika wewe na familia yako. Sasa tumejipanga vizuri wale wote ambao siyo wenzetu watupishe mapema kabla ya uchaguzi, mimi ndiyo Mkuu wa Mkoa huu wa Manyara nasema hivi kama wewe huungi mkono Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ondoka mapema" alisisitiza Mnyeti

Serikali Kuboresha Mafunzo Kwa Watu Wenye Ulemavu

$
0
0
Na Beatrice Lyimo- MAELEZO, DODOMA
Serikali kwa kushirikiana na wadau imeendelea kuboresha Vyuo vya Mafunzo ya Ufundi vya Watu wenye Ulemavu ili kuwawezesha kuajiriwa na kujiajiri na kupata ujuzi mbadala wa kumudu maisha yao.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Walemavu) Stella Ikupa jana Mjini Dodoma  wakati akijibu swali la Mbunge wa Biharamulo Magharibi Mhe. Oscar Mukasa lililohusu umuhimu wa kuwatazama vijana wenye ulemavu mbalimbali kwa namna ya kipekee.

Mhe. Ikupa amesema kuwa Serikali inatambua Vijana wenye ulemavu kuwa ni kundi mojawapo miongoni mwa watanzania wenye ulemavu ambalo linakabiliwa na changamoto mbalimbali.

“Kwa kutambua umuhimu wa kundi hili la watu wenye ulemavu wakiwemo vijana, Serikali iliunda Baraza la Taifa la watu wenye ulemavu ambalo kazi yake kubwa ni kutoa ushauri kwa Serikali na wadau mbalimbali wanaohusika na masuala ya watu wenye ulemavu juu ya namna bora ya kushughulika na changamoto zao zikihusisha zile za kundi la vijana wenye ulemavu,” alifafanua Naibu Waziri Ikupa.

Aidha, Mhe. ikupa alisema kuwa  Serikali imeendelea kuunda kamati za watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya Mkoa, Halmashauri ya Wilaya, Kata na Mtaa kwa lengo la kuhakikisha masuala ya watu wenye ulemavu yanazingatiwa ili kuondokana na kero mbalimbali wanazokumbana nazo ikiwa ni pamoja na masuala yanayohusu Elimu, Afya, Ajira na Mikopo ya Uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Hata hivyo, Naibu Waziri Stella Ikupa amewahimiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kusimamia ipasavyo utekelezaji wa suala hilo ambalo liko kisheria na pia ametoa wito kwa Wakurugenzi hao kuhamasisha walemavu kujiunga kwenye vikundi mbalimbali ikiwemo vikundi vya vijana.

Wananchi Watakiwa Kutoa Taarifa Hospitali Zinazotoza Mama Wajawazito

$
0
0
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO, DODOMA
Serikali imewataka wananchi kutoa taarifa kuhusu hospitali zinazotoza fedha kwa ajili ya matibabu kwa akina mama wajawazito ili kuweza kuchukua hatua muhimu kukomesha hali hiyo.

Kauli hiyo imetolewa jana Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu  Hawa Chakoma lililohusu matibabu bure kwa mama wajawazito.

Dkt. Ngugulile alisema kuwa mama wajawazito ni moja ya makundi maalumu wanaostahili kupata huduma za matibabu bure kama ilivyooneshwa katika mwongozo na uchangiaji wa huduma za afya wa mwaka 1997.

“Mwongozo umeweka bayana kuwa kina mama wajawazito ni haki yao kupewa huduma zote bila malipo na sio zile tuu zinazohusu huduma za ujauzito katika mwongozo uliopitiwa mwaka 2009/2010 imetamkwa bayana kuwa huduma za afya kwa mama wajawazito ni bure, ikiwa na maana kwamba mara tu mwanamke anapokuwa na ujauzito huduma zote kuanzia kliniki ya wajawazito, pale anapogundulika maradhi yoyote, pamoja na huduma ya kujifungua sanjali na kumuona daktari, kupatiwa vipimo, kupewa dawa na kufanyiwa upasuaji pale inapohitajika kufanya hivyo” alifafanua Dkt. Ndugulile.

Aidha, Dkt. Ndugulile alisema kuwa Wizara imeanzisha utaratibu wa kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vinavyohitajika wakati wa kujifungua ambapo watapewa akina mama wajawazito wanapokaribia kujifungua.

Hata hivyo, Dkt Ndugulile alisema kuwa kwa sasa kumekuwa na mwitikio mkubwa kwa akina mama kujifungua katika vituo vya afya ambapo zaidi ya asilimia 60 ya akinamama wanajifungulia kwenye vituo vya afya.

Mbali na hayo, Serikali imezitaka Halmashauri zote nchini kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sera hiyo ili akina mama wajawazito wapate huduma za matibabu bure kama Mwongozo wa Uchangiaji wa mwaka 1997 na Sera ya Afya ya mwaka 2007 inavyoelekeza.

Viwanja Vya Ndege 11 Nchini Kufanyiwa Upanuzi Na Ukarabati

$
0
0
Na Beatrice Lyimo- MAELEZO, DODOMA
Serikali imeanza majadiliano na Benki ya Dunia ili kupata mkopo wa kugharamia ukarabati na upanuzi wa Viwanja vya Ndege 11 kwa kuzingatia mapendekezo ya ripoti ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambao ulizingatia mambo mbalimbali  ikiwa ni pamoja na ukuaji wa shughuli za kiuchumi, utalii na mahitaji ya usafiri wa anga.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  Mhandisi Atashasta Ndikiye jana  Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Tanga Mhe. Mussa Mbarouk lililohusu Ujenzi wa Uwanja wa Ndege mkubwa na wa kisasa katika jiji la Tanga.

Mhandisi Ndikiye alisema kuwa kiwanja cha ndege cha Tanga ni miongoni mwa viwanja hivyo 11 vilivyofanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa kugharamiwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa Transport Sector Support Project (TSSP).

“Katika upembuzi huo kiwanja cha ndege cha Tanga ni miongoni mwa viwanja vilivyopewa kipaumbele kwa mahitaji ya ukaribu hivyo katika majadiliano ya awali Benki ya Dunia imeonesha nia ya kugharamia ukarabati wake.”

“Kwa sasa majadiliano kati ya Serikali na Benki ya Dunia yanaendelea yakiwemo mapitio ya awali ya ripoti za miradi iliyopendekezwa pamoja na maandalizi ya taarifa mbalimbali zinazohitajika kabla ya mkataba wa mkopo kusainiwa na baadaye kutangaza zabuni,” alifafanua Mhandisi Ndikiye.

Hata hivyo, Mhandisi Ndikiye alivitaja viwanja vingine vilivyofanyiwa upembuzi yakinifu  ikiwemo Lake Manyara, Musoma, Iringa, Songea, Kilwa Masoko, Lindi, Moshi, Njombe, Simiyu na Singida ambapo usanifu huo ulimalizika mwezi June 2017 kwa kuhusisha usanifu wa miundombinu ya viwanja  hivyo kwa ajili ya upanuzi na ukarabati ili kukidhi mahitaji ya sasa.

Serikali Kuendelea Kuvifungia Vyuo Vinavyovunja Sheria

$
0
0
SERIKALI imeendelea kudhibiti ubora wa elimu nchini kwa kuvichukulia hatua vyuo na shule zinazobainika kukiuka taratibu za utoaji wa elimu ikiwa ni pamoja na kusitisha udahili wa wanafunzi,kusitisha program zitolewazo,kupunguza idadi ya wanafunzi waliozidi na kufuta usajili wa taasisi husika.

Aidha katika Mwaka 2017/18 ulifanyika uhakiki katika vyuo na taasisi 458 za elimu ya ufundi ambapo jumla ya vyuo na taasisi 59 zilibainika kuwa na mapungufu na hivyo walitakiwa kurekebisha mapungufu hayo ndani ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia Februari 1 Mwaka 2018,chuo kitakachoshindwa kurekebisha mapungufu hayo kitafutiwa usajili.

Kauli hiyo imetolewa jana  bungeni na Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,William OleNasha alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum,Zubeda Sakuru (Chadema),lililoulizwa kwa niaba yake  na Mbunge wa Viti Maalum,Susan Lymo,.

Katika swali hilo ambalo lilihoji “Baadhi ya shule na vyuo nchini vinaendelea kudahili wanafunzi pamoja na kutokidhi matakwa ya sheria mbalimbali,Je serikali inachukua hatua gani kudhibiti vyuo na shule zinazoendelea kudahili wanafunzi huku zikiwa na mapungufu,Je hadi sasa ni vyuo na shule ngapi zilizofutiwa usajili kwa kutokidhi matakwa ya kisheria?”

Akifafanua katika majibu yake OleNasha alisema kwa upande wa vyuo vikuu serikali kupitia TCU ilifanya uhakiki wa Vyuo vyote vya Elimu ya juu  nchini kati ya Ocktoba 2016 na Januari 2017 ili kuhakiki ubora wa elimu inayotolewa vyuoni .

“Taarifa ya uhakiki inaonesha mapungufu katika baadhi ya vyuo ,kufuatia programu hiyo TCU kwa Mwaka wa masomo 2017/18 ilisitisha udahili wa wanafunzi wa programu za Afya na uhandisi kwenye vyuo vitano’’alisema OleNasha na kuongeza kuwa

“Vilevile,TCU ilisitisha udahili katika program zote kwa Mwaka wa kwanza wa vyuo 14 ,katika Mwaka huo huo wa masomo TCU imedhibiti na kuzuia vyuo vikuu kudahili wanafunzi katika program ambazo hazijapata ithibati zipatazo 75 katika vyuo vikuu 22’’

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya February 6

Chanzo cha Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume na Tiba Yake

$
0
0

Tendo la ndoa limengawanyika katika makundi matatu baadhi yake makudi hayo niuhanisi, kufanya tendo la ndoa maramoja na kushidwa kurudia tena 

sababu zinazo pelekea ni ugonjwa wa kisukari, kujichuwa, maumivu ya mgongo na kiuno, tumbo kuuguruma na kujaa gesi, msogo wa mawazo, presha, kutokuwa nyama sehemu ya haja kubwa yani mgoro, ulevu wa kupidukia, kuadhilika na madawa ya kulevya 

ARRBERA 1 Ni dawa ya asili ambayo imefanyiwa tafiti kwa hali ya juu isiyo na kemikali yoyote kwa mtumiaji ambayo humfanya mtumiaji kufanya tendo la ndoa maratatu bila kuchoka 

Pia ARRBERA 2 ni dawa asili abayo huimalisha ukuaji wa umbile la kiume lililo sinyaa na kunenepesha saizi upedayo. sihayo tu upade wa wamatatizo kisukari yakushuka na kupada kuna dawa ya kutumia siku saba na kufanya sukari ibaki nomo balasi abayo ni 4-5-6 vilevile kwaupade wa kina mama matatizo ya uzazi na hedhi kuvurugika na kutokwa maji maji sehemu za sili fagasi na kifafa cha mimba kwa kina mama waja wazito na kifafa cha kawaida 

FIKA OFISINI KWETU MBANGALA RAGI TATU ASIYE KUWA NA NAFASI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO KWA KWA KAZI WA DSM muone dr kabero simu 0758078280 au 0713 293 988 wote mnakalibishwa
No automatic alt text available.

Ijue Afya Yako: Pata Tiba Asili ya Busha, Maumbile Madogo na Nguvu za Kiume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaayhiri watu  wengi sana baada ya kujiona wako tofauti na watu wengine .Kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na maumbile  nchi-6-7 .Matatizo haya yanasababishwa na punyeto) kisukari) presha) naulevi wakupita kiasi pia na msogo wa mawazo, homoni za toka kuzaliwa 

MOMLA ni dawa inayotibu kinacho sababisha tatizo,kama vile sukari, presha, magonjwa ya zinaa, misuli kulegea na kusinyaa kwa kwasababu ya kujichuwa au punyeto na akili kudumaa kwaajili ya tendo bila kushiriki 

MBEPE nikwa wenye maumbile mafupi na membamba kwa matatizo hayo ni dozi ya siku 5 unapona kabisa 

DAGULA hii nikwaajili ya wenye busha iwe ya maji au ya utumbo kushuka inatibu bila opresheni , kuuga mifupa kwwaliopata ajari yoyote inayo sababisha uvujifu wa mifupa inatibu kwa mda wa siku 14 tayali kwa mazoizi 

LUKOMOLO ni dawa ya mvuto wa mpenzi biaashara ata kama mme mke mchumba atakutafuta mwenyewe na kutekeleza yote unayotaka mfanye akutafute mwenyewe pia tunatibu kiuno miguu aina yote tumbo la uzazi kwa kina mama na kina baba nk 

KWA WAKAZI WA DSM TUNAPATIKANA MBANGALA RANGI TATU MKABALA NA KISUMA BAA. 

KWAMIKOA YOTE MTAPATA HUDUMA HILI KWA MAWASILIANO PIGA 0767131395, 0712757594, 0787131395 MUONE DR MWANGARA

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Wabunge wajadili miradi ya umeme wa Rufiji na Bomba la Mafuta

$
0
0
Na Veronica Simba, Dodoma
Wabunge walio katika Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini pamoja na wale wa Mikoa ya Morogoro, Iringa na Pwani, wamejadili Mradi wa kuzalisha umeme wa Rufiji pamoja na wa Bomba la kusafirisha mafuta ghafi la Afrika Mashariki.

Walipata fursa ya kujadili Miradi hiyo mikubwa wakati wa Semina iliyoandaaliwa kwa ajili yao na Wizara ya Nishati, mwishoni mwa Juma, Februari 3 mwaka huu mjini Dodoma, kwa ajili ya kuwaongezea uelewa kuhusu utekelezaji wake.

Akiwakaribisha wabunge katika Semina hiyo, Waziri mwenye dhamana, Dkt. Medard Kalemani alisema kuwa ili kuhakikisha Miradi hiyo inatekelezwa kwa ufanisi, ni lazima wananchi pamoja na viongozi mbalimbali washirikishwe ili waielewe vema na ndiyo azma ya kuandaa semina husika.

“Kama Wizara tumeshakutana na kuwajengea uelewa kuhusu Miradi hii Viongozi wa Mikoa inayohusika. Sasa hivi tunaendelea kujenga uelewa kwa ngazi ya vijiji ili wananchi nao waweze kuwa na ufahamu,” alifafanua Waziri.

Akizungumzia kuhusu Mradi wa kuzalisha umeme kutokana na maporomoko ya maji ya Mto Rufiji, Waziri Kalemani alisema kuwa ni Mradi mkubwa na muhimu sana kwa Taifa kwani utakuwa kichocheo kikubwa kwa uchumi wa nchi na hivyo Serikali imedhamiria kuutekeleza kwa kasi kubwa.

Alisema kuwa, Mradi huo unatarajiwa kuzalisha megawati 2100 za umeme ambacho ni kiasi kikubwa kitakachotosheleza matumizi mbalimbali ikiwemo Mradi wa ujenzi wa Reli ya kisasa (standard gauge) uliopangwa kutekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano.

“Kwa sasa tuna jumla ya megawati 1451 za umeme ambazo tumeingiza kwenye Gridi ya Taifa. Kwa hiyo, kujenga Mradi huu wa megawati 2100, kutatupatia umeme mwingi zaidi kwa matumizi makubwa zaidi ya kimaendeleo.” alisema Skt. Kalemani.

Vilevile, alisema kuwa Fedha za kutekeleza Mradi zitatoka ndani ya nchi na kwamba unatarajiwa kuanza kujengwa ifikapo Machi mwaka huu na kukamilika ndani ya kipindi cha miezi 36.

Aliendelea kueleza kuwa, sambamba na Mradi huo, Serikali inatarajia kujenga njia ya kuusafirisha umeme utakaokuwa ukizalishwa Rufiji na kuupeleka Chalinze, na kuutoa Chalinze hadi Dodoma. “Njia hiyo itasafirisha umeme wa kilovoti 400.”

Kwa upande wa faida za Mradi husika, Waziri Kalemani alizitaja kuwa ni pamoja na kupatikana kwa umeme wa kutosha, kuvutia utalii pamoja na kuwezesha kilimo cha umwagiliaji, ambavyo vyote hivyo vitasaidia kujenga uchumi wa viwanda.

Aidha, akifafanua zaidi kuhusu faida za Mradi, alisema kuwa, watanzania wasiopungua 200 watapata ajira hivyo kuinua vipato vyao.

Kuhusu Mradi wa kusafirisha mafuta ghafi kutoka Uganda hadi Tanga Tanzania, Dkt. Kalemani alieleza kuwa utakuwa na manufaa makubwa kwa Taifa kutokana na fursa zitakazopatikana ikiwemo kuajiri watanzania zaidi ya elfu 10.

“Bomba lina urefu wa kilomita 1445 kuanzia Hoima Uganda hadi Tanga Tanzania, lakini kwa Tanzania pekee linapita umbali wa kilomita 1115 ambayo ni takribani asilimia 90 ya urefu wake wote. Hii ni fursa kubwa kwa watanzania.”

Akifafanua zaidi, alisema kuwa Bomba litapita katika Mikoa Nane ya Tanzania ambayo ni Kagera, Geita, Shinyanga, Singida, Tabora, Dodoma, Manyara na hatimaye Tanga.

“Katika Mikoa hiyo, Bomba litapita katika Wilaya 24, Vijiji takribani 138 na Vitongoji 287, hivyo kwa kiasi kikubwa linagusa sana maisha ya watanzania walio wengi.”

Alisema kuwa inatarajiwa utekelezaji wa Mradi huo uanze rasmi ifikapo mwezi Mei mwaka huu, baada ya shughuli za maandalizi zinazoendelea sasa kukamilika.

Akifunga Semina hiyo, Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenister Mhagama aliwataka wabunge kusahau tofauti zao za kisiasa na kuunga mkono miradi hiyo mikubwa kwani italeta faida kubwa kwa wananchi wote pasipo kujali itikadi na tofauti zao.

Ujumbe huo wa Waziri Mhagama uliungwa mkono na Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu aliyewasihi wabunge wote waliopata fursa ya kuelimishwa kuhusu utekelezwaji wa miradi hiyo, kupeleka elimu hiyo kwa wananchi katika maeneo yao na kushirikiana kwa pamoja kuhakikisha inatekelezwa bila vikwazo.

Kwa upande wao, Wabunge mbalimbali waliopata fursa ya kujadili miradi hiyo, walisisitiza suala la ushirikishwaji wananchi lizingatiwe ili kuhakikisha inakuwa na tija stahiki.


Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images