Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli atekeleza ahadi yake kwa kampuni ya Bakhresa

0
0
Na Judith Mhina – MAELEZO
 Agizo la Rais John Pombe Magufuli la kuipatia Kampuni ya Said Salim Bakhresa (SSB) Group LTD ardhi yenye ukubwa wa ekari 10,000 kwa ajili ya kuwekeza katika kilimo cha miwa na ujenzi wa kiwanda cha sukari katika Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani limetekelezwa.

Msemaji wa Makampuni ya Said Salim Bakhresa (SSB) Group LTD, Bw Hussein Sufian ameiambia Idara ya Habari (MAELEZO) katika mahojiano maalumu ilipokuwa ikifuatilia utekelezaji wa agizo la Rais Magufuli alilolitoa tarehe 6 Oktoba, 2017 baada ya kufungua kiwanda cha vinywaji baridi cha  Kampuni hiyo kilichopo Mkuranga Mkoani Pwani.

Bw. Sufian amesema, tayari Kampuni yake imetenga takriban Shilingi Milioni 75/- kwa ajili ya kuanza uwekezaji katika shamba hilo kwa shughuli za kilimo cha miwa na kufafanua kuwa, hatua ya awali ya upandaji wa miwa kwenye vitalu imeanza.

 Amesema, maandalizi ya upandaji wa miwa katika Kitalu A chenye ekari 48 umekamilika. Aidha, upandaji wa miwa katika eneo la jumla ya ekari 8 kati ya hizo utaanza tarehe 3 Februali na ekari nyingine 40 utafanyika mwezi Juni na Julai, 2018.

“Baada ya kukamilika kwa upandaji katika Kitalu “A” mwaka huu (2018), tunatarajia ifikapo Januari na Juni 2019 tutaendelea kupanda miwa kwenye kitalu “B” chenye ukubwa wa ekari 300. Mzunguko huo utaendelea hivyo hivyo mpaka kufikia hekari 2030 ambazo tumekusudia kuanza ujenzi wa kiwanda mapema 2019 na uzalishaji wa sukari kiwandani ifikapo Septemba 2020,” alisema Sufian.

Akielelezea zaidi juu ya mradi huo, Bw. Sufian amesema kwamba tayari watu 50 wameajiriwa, kati ya hao 20 ni wa kudumu na 30 vibarua. Watu 5 wanafanya kazi za kiufundi na 45 nguvu kazi. Aidha, Kampuni hiyo imeajiri Wataalamu 2 kutoka nje ambao ni Bw. Abraham Star Mtaalamu wa Umwagiliaji kutoka Israel na Mtaalamu wa Kilimo cha miwa kutoka India, Bw Narayan Krishna, kiwanda kinakusudia kuajiri watu 1000 ifikapo mwaka 2020.

Ili kilimo hicho cha miwa kiwe endelevu,  pamoja na mambo mengine uchimabji wa visima na utengeneaji wa mabwawa matatu umefanyika ambapo maji yanavutwa kutoka mto Wami kilometa 5 mpaka katika bwawa lililotengenezwa la Tambezi 1.

Maji yanapojaa yanavutwa kupelekwa bwawa dogo katika Kitalu A na sehemu ya mitambo ya  kuchuja maji, ambapo kila Kitalu kitakuwa na kituo cha kusukuma maji na kupeleka kwenye mabomba makubwa kisha madogo yanayopita katikati ya mimea iliyopandwa na kufanya umwagiliaji wa matone.

Agizo la Rais Magufuli lilikusudia kuondoa pengo la uzalishaji wa sukari kwa matumizi ya kawaida nchini ambapo katika kipindi cha mwaka 2016/ 2017 mahitaji yalikawa ni tani 590,000 kati ya hizo tani 135,000 ni mahitaji ya kiwandani na 455,000 ni mahitaji ya kawaida ya binadamu.

Uzalishaji wa sukari nchini ulikuwa tani 350,846 na kufanya kuwa na upungufu wa tani 259,156.  Hivyo uzalishaji wa tani elfu 30 mpaka 70 utaondoa pengo la uhaba wa sukari nchini Tanzania.



AG mpya aahidi makubwa sekta ya sheria

0
0
Na Fatma Salum-MAELEZO
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Adelardus Kilangi ameahidi kufanya kazi kwa bidii ili kupunguza changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Sheria hapa nchini.

Akizungumza baada ya kuapishwa katika hafla iliyofanyika jana  ikulu jijini Dar es Salaam, Dkt. Kilangi alisema kuwa changamoto hizo haziishii katika ngazi ya kitaifa tu bali hata kwenye nchi nyingine za Afrika na Jumuiya za Kimataifa.

“Natambua kuwa yapo mambo mengi yanahitaji kufanyiwa kazi na kila nchi katika Afrika ikiwemo Sheria za udhibiti wa rasilimali zetu na mfumo wa Sheria za Kimataifa unaohusu masuala ya uwekezaji,” alisisitiza Kilangi.

Kilangi aliongeza kuwa atahakikisha ofisi yake inazishughulikia kwa karibu changamoto hizo kwa kushirikiana vyema na wadau wengine wa sheria ili kuongeza ufanisi katika Serikali kwa maslahi ya taifa.

“Tunakuahidi Mhe. Rais kwamba tutafanya kazi kwa akili zetu zote, nguvu zetu zote na uwezo wetu wote kwa maslahi ya Watanzania,” alisema Kilangi.

Kwa upande wake Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Juma aliwapongeza majaji wapya walioapishwa katika hafla hiyo na kuwaeleza kuwa nafasi ya Majaji wa Mahakama Kuu ni muhimu sana katika taifa hivyo ni wajibu wao kufanya kazi na kufuata sheria bila upendeleo.

Naye Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi alibainisha kuwa mabadiliko aliyofanya Mhe. Rais ya kuwateua Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Naibu wake ni mwanzo tu wa mabadiliko makubwa ambayo amedhamiria kuyafanya katika Wizara ya Katiba na Sheria, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali.

Alieleza kuwa lengo la mabadiliko hayo yanayotekelezwa na Rais John Magufuli ni kuongeza uwajibikaji na ufanisi katika utendaji kazi.

“Namuomba Mhe. Rais taratibu zifanyike ili wanasheria wote walioko katika wizara zote za Serikali Kuu warudi chini ya usimamizi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili kuimarisha uwezo wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kuongeza ufanisi,” alisema Kabudi.

Akitoa nasaha zake kwa wateule walioapishwa kwenye hafla hiyo, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson aliwaasa kutofanya kazi kwa mazowea kwa kuwa yapo mambo mengi yanahitaji maboresho ikizingatiwa kwamba ulimwengu unabadilika kwa kasi kubwa.

Aidha, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju ambaye uteuzi wake ulitenguliwa katikati ya wiki hii ameapishwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na kuahidi kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano katika kuwatumikia wananchi na taifa kwa ujumla.

Katika hafla hiyo iliyohusisha kiapo cha utii na kiapo cha maadili walioapishwa ni pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Adelardus Kilangi , Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Paul Ngwembe na Majaji wawili wa Mahakama Kuu ambao ni George Masaju na Gerson Mdemu.

Kabla ya uteuzi, Dkt. Adelardus Kilangi alikuwa Mkurugenzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT) kituo cha Arusha na Paul Ngwembe alikuwa Mkurugenzi wa masuala ya Sheria katika Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).


Wafanyakazi waanza kukatwa mishahara kufadhili uchaguzi wa 2020

0
0
Wafanyakazi wa umma nchini Burundi wameanza kukatwa asilimia 10 ya mishahara yao kwaajili ya kufadhili uchaguzi mkuu unaotarajiwa mwaka 2020.

Katika kipindi cha miaka miwili ijayo, raia wote wa Burundi walio na zaidi ya umri wa kupiga kura wa miaka kumi na minane na zaidi, ni sharti wachangie katika hazina hiyo ya kitaifa.

Serikali ya Burundi imesema imechukua uamuzi huo ili kuziba pengo lililosababishwa na uamuzi wa wafadhili wa kuzuia misaada tangu mzozo wa mwaka 2015 wakati rais Pierre Nkurunziza alipowania muhula wa tatu.

Hata hivyo serikali imekariri kuwa hazina hiyo ya uchaguzi ni wazo la raia wa Burundi wenyewe, pendekezo ambalo limepingwa na wakuu wa vyama vya wafanyakazi.

Freeman Mbowe, Polepole wamjibu Zitto Kabwe Kuhusu kusitisha kampeni

0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM), kimesema kipindi hiki cha msiba wa mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru ndicho cha kuvieleza vyama vinavyoshiriki uchaguzi mdogo wa ubunge katika majimbo ya Siha na Kinondoni kufanya kampeni safi.

Wakati chama hicho kikisema hayo kupitia kwa katibu wake wa itikadi na uenezi, Humphrey Polepole, chama kingine kinachoshiriki kampeni hizo, Chadema kimesema kitasimamisha shughuli zote za kampeni Jumatatu siku ambayo mwanasiasa huyo atazikwa katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Kauli ya vyama hivyo imetokana na wito uliotolewa na Kiongozi wa Chama cha ACT – Wazalendo, Zitto Kabwe kwa vyama hivyo kusimamisha kampeni hizo kwa siku tatu kuomboleza kifo cha mwanasiasa huyo mkongwe nchini kutokana na mchango wake katika siasa za nchi na zaidi ndani ya vyama hivyo.

“Kingunge amesaidia kuimarisha CCM na baadaye akasaidia Chadema. Sioni busara vyama kuendelea na kampeni. Nawaomba wasitishe leo (jana), kesho (leo) na Jumatatu mwanasiasa huyu akizikwa wataendelea,” alisema jana nyumbani kwa marehemu, Kijitonyama, Dar es Salaam.

Alipoulizwa kuhusu wito huo, Polepole alisema kwa kuwa mwanasiasa huyo ameishi na kufa akiamini katika siasa za ujamaa na kujitegemea ambazo msingi wake ni kufanya kazi, huu si wakati wa kusimamisha kampeni.

“Ni wakati wa kueleza kuwa vyama vya siasa vina jukumu la kufanya kampeni safi, kujenga misingi imara ya kuwapata makada na wanachama wanaosimamia kwenye imani ya vyama vyao na kuwapata viongozi bora.”

Alisema kazi kubwa aliyoifanya Kingunge tangu kuasisiwa kwa Taifa hadi alipofariki, inapaswa kuendelezwa.

“Nanukuu kifungu cha Biblia ‘mbio amezipiga na mwendo ameumaliza’. Hivyo Kingunge ameumaliza mwendo kazi kubwa ni kuendeleza mema na mazuri aliyotenda,” alisema Polepole.

Mkurugenzi wa itifaki, mawasiliano, uenezi na mambo ya nje wa Chadema, John Mrema alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu ombi hilo la Zitto alisema chama hicho kitasitisha kampeni zake kesho.

“Huu ni ushauri, na mzee wetu amefariki dunia kampeni zikiwa zimeanza na zinafanyika kwa muda mfupi kabla ya uchaguzi. Tuliona Jumatatu (kesho) ndio tushiriki kikamilifu kumuaga mzee wetu na hatutafanya kampeni.”

Hata hivyo, Mrema alisema awali kwamba ni vigumu kutoa uamuzi kuhusu ushauri huo wa Zitto kwa kuwa suala hilo linapaswa kutolewa tamko baada ya vikao kauli inayofanana na ya mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.

“Leo (jana) baada ya kampeni tutafanya kikao cha tathmini lakini ni kwamba sisi tuliona Jumatatu kuwa siku muafaka kutofanya kampeni ili kushiriki shughuli ya kumhifadhi mzee wetu,” alisema Mrema huku Mbowe akisema, “Hili ni swali gumu, lakini nitakwenda kushauriana na viongozi ili tujue cha kufanya.”

Vyama takriban 12 vipo katika kampeni za ubunge jimbo la Kinondoni, Dar es Salaam na Siha, Kilimanjaro zilizoanza Januari 21 zikitarajiwa kumalizika Februari 16 huku uchaguzi katika majimbo hayo na kata 10 ukitarajiwa kufanyika Februari 17.

Kingunge aliyekuwa kada wa CCM mwenye kadi namba nane, alitangaza kukihama chama hicho Oktoba 4, 2015 na kusema hatajiunga na chama chochote lakini mara kadhaa alionekana akipanda majukwaa ya upinzani kumnadi aliyekuwa mgombea urais wa Chadema na Ukawa, Edward Lowassa kwenye Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Mwanasiasa huyo alifariki dunia juzi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), ikiwa ni mwezi mmoja baada ya mkewe, Peras kufariki katika hospitali hiyohiyo.

Rais Magufuli mgeni rasmi misa ya kusimikwa Askofu mteule Jackson kuwa Askofu wa tano wa Kanisa Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Dar es Salaam

0
0
 Rais John Magufuli ni mgeni rasmi katika misa ya kusimikwa Jackson Sosthenes kuwa askofu wa tano wa Kanisa  Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Dar es Salaam.

Misa ya kumsimika Askofu mteule Sosthenes inafanyika asubuhi ya leo Februari 4,2018  ikiongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana Tanzania, Jacob Chimeledya.

Viongozi kadhaa wa Serikali akiwemo Rais Magufuli na mkewe Janeth; Rais mstaafu Benjamin Mkapa, wanasiasa na waumini wa kanisa hilo wamewasili katika Kanisa la Mtakatifu Albano lililoko eneo la Posta jijini Dar es Salaam inakofanyika misa hiyo.

Baadhi ya viongozi waliopo kanisani ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo; Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba; Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi; Kamishna wa Uhamiaji, Dk Anna Makakala; na Waziri Ofisi ya Rais (Utumishi wa Umma na Utawala Bora), George Mkuchika.

Sosthenes anasimikwa kuwa askofu kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Dk Valentino Mokiwa aliyeondolewa madarakani na uongozi wa juu wa kanisa hilo takriban mwaka mmoja uliopita.

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Ijue Afya Yako: Pata Tiba Asili ya Busha, Maumbile Madogo na Nguvu za Kiume

0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaayhiri watu  wengi sana baada ya kujiona wako tofauti na watu wengine .Kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na maumbile  nchi-6-7 .Matatizo haya yanasababishwa na punyeto) kisukari) presha) naulevi wakupita kiasi pia na msogo wa mawazo, homoni za toka kuzaliwa 

MOMLA ni dawa inayotibu kinacho sababisha tatizo,kama vile sukari, presha, magonjwa ya zinaa, misuli kulegea na kusinyaa kwa kwasababu ya kujichuwa au punyeto na akili kudumaa kwaajili ya tendo bila kushiriki 

MBEPE nikwa wenye maumbile mafupi na membamba kwa matatizo hayo ni dozi ya siku 5 unapona kabisa 

DAGULA hii nikwaajili ya wenye busha iwe ya maji au ya utumbo kushuka inatibu bila opresheni , kuuga mifupa kwwaliopata ajari yoyote inayo sababisha uvujifu wa mifupa inatibu kwa mda wa siku 14 tayali kwa mazoizi 

LUKOMOLO ni dawa ya mvuto wa mpenzi biaashara ata kama mme mke mchumba atakutafuta mwenyewe na kutekeleza yote unayotaka mfanye akutafute mwenyewe pia tunatibu kiuno miguu aina yote tumbo la uzazi kwa kina mama na kina baba nk 

KWA WAKAZI WA DSM TUNAPATIKANA MBANGALA RANGI TATU MKABALA NA KISUMA BAA. 

KWAMIKOA YOTE MTAPATA HUDUMA HILI KWA MAWASILIANO PIGA 0767131395, 0712757594, 0787131395 MUONE DR MWANGARA

Ratiba rasmi ya mazishi ya Mzee Kingunge Ngombale Mwiru

0
0
Jumapili tarehe 4/2/2018
- Saa 10:00 jioni mwili kutoka Hospitali kuelekea nyumbani Victoria/Makumbusho Kingunge street, Dar es salaam.

-Saa 11:00 Jioni mwili kuwasili nyumbani na taratibu za ibada mila na desturi kuendelea usiku mzima(mkesha)

******************************
Jumatatu tarehe 5/2/2018
- Saa 1:00 Asubuhi mpaka saa 2:00 asubuhi waombolezaji kuwasili nyumbani Kwa ajili ya kuanza taratibu za mazishi.
- Saa 2:00 Asubuhi mpaka saa 3:30 asubuhi Kupata kifungua kinywa/Chai Kwa waombolezaji wote
- Saa  4:00  Asubuhi mpaka saa 5:00 misa nyumbani Kwa marehemu
- Saa 6:00 Mchana mwili kuwasili Karimjee hall kwa shughuli ya kuagwa
- Saa 6:00 Mchana  9:00 Alasiri kuaga mwili wa marehemu
- Saa 9:00 Alasiri mpaka 9:30 Alasiri msafara wa kuelekea makaburini Kinondoni
- Saa 9:30  Alasiri mpaka 11:30 Jioni maziko
- Saa 11:30 Jioni 12:30 Jioni kuelekea nyumbani kwa marehemu kwa chakula cha jioni kwa waombolezaji wote
1:30 mpaka  2:45  Usiku chakula cha usiku waombolezaji wote
3:00 Usiku-Hitimisho la shughuli ya Mzee wetu kwa waombolezaji wote.

Tunawashukuru sana waombolezaji wote kwa ushiriki wenu wa Hali na mali katika wakati huu mgumu. Mungu awazidishie.

Bwana ametoa, na bwana ametwaa.
Jina lake na lihimidiwe - AMINA

Imetolewa na:
Omary A. Kimbau

Mwenyekiti wa kamati ya mazishi

Waziri Nchemba: Vitambulisho Vya Taifa Vitaondoa Mapingamizi Ya Uraia Katika Chaguzi

0
0
 Na Tiganya Vincent-rs Tabora
Vitambulisho wa uraia vitasaidia kuwa na utambuzi wa wananchi utakao ondoa ile tabia ya baadhi ya watu kutilia mashaka wakati wa shughuli mbalimbali ikiwemo kipindi kushiriki katika zoezi la uchaguzi wote wote.

Kauli hiyo ilitolewa jana mjini Tabora na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt.Mwigulu Nchemba wakati uzinduzi wa zoezi la usajili wananchi kwa ajili ya vitambulisho vya kitaifa mkoani humo.

Alisema kuwa mara nyingi mtu anapogombea nafasi yoyote hapa nchini au kunapokuwepo na migogoro ya kugombania mashamba ndio suala la kusema kuwa huyo sio raia linapojitokeza.

Dkt. Nchemba alisema wananchi wenye sifa kuchangamkia zoezi la usajili na upataji wa vitambulisho vya uraia ili kuepuka matatizo kama vile migogoro ikiwemo ya mapingamizi wakati chaguzi mbalimbali na kuiweza Serikali kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya wananchi wake

Alisema kuwa hata uchumi wa kisasa unaanza na kutambua kwa Serikali kutambua watu iliyonao na ndipo ipange mipango ya maendeleo kwa ajili yao.Waziri huyo aliongeza kuwa hata kwenye vyombo vya fedha kama vile Benki zimekuwa zikiweka riba kubwa katika mikopo kwa sababu ya baadhi wananchi kukosa utambulizi

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Andrew Massawe alisema jitihada hizi zote zimelenga kusaidia Serikali na wananchi kutambulika na hatimaye Mashirika, Taasisi na Makampuni nchini kutumia mfumo huu kutoa huduma zenye ubora na tija kwa Taifa.

Alisema mfumo huu una faida nyingi kwa Taifa na mwananchi mmoja mmoja kama vile kuimarisha Ulinzi na Usalama wa nchi, wananchi kutambulika kwa haraka pindi wanapofika kupata huduma za afya na Elimu.

Massawe alisema kuwa faida nyingine ni kurahisisha utambuzi wa makundi yenye mahitaji maalumu ikiwemo utambuzi wa kaya masikini unaofanywa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) na upatikanaji wa huduma za kifedha na Simu kirahisi.

Kwa upande wa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tabora Queen Mlozi aliwaagiza viongozi wa ngazi zote mkoani humo kuhakikisha kuwa anayesajiliwa na kupata kitambulisho cha uraia ni yule mwenye sifa na sio mgeni.

Alisema Serikali ya Mkoa wa Tabora haitasita kumchukulua mtu yoyote atayeshiriki katika udanganyifu utaosababu watu wasio raia kupata vitambulisho vya uraia.

Queen alisema kuwa kila mmoja ni vema akasimama katika nafasi yake kuhakikisha kuwa anafanya kazi kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu ili kuleta ufanisi.

Alitoa wito kwa jamii kusaidia kuwafichua watu wasio raia wanaotaka kujipenya ili wapate vitambulisho vya uraia

Katambi Ataja Sababu Kuyumba Kwa Upinzani

0
0
 KADA mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Patrobas Katambi ameeleza sababu zinazochangia kudhoofika kwa vyama vya upinzani nchini.

Amesema kuyumba kwa vyama hivyo kunachangiwa na ubinafsi waviongozi wake ambao wengine wamegeuza Chama ni mali yao na kutoa maamuzi ambayo si shirikishi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam January 2,Katambi alisema kuwa tangu ameondoka Chadema ambako alikuwa Mwenyekiti wa Vijana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho amekuwa kimya muda mrefu lakini ameona ni vema akasema mambo kadhaa kuhusu hali ya kisiasa nchini.

Kuhusu vyama vya siasa kuyumba, Katambi alisema zipo sababu ambazo zimekuwa zikichangia vyama hivyo kushindwa kuwa imara na matokeo yake kubaki kulalamikia kila jambo ambalo linafanywa na Serikali hata liwe lenye maslahi kwa nchi.

"Upinzani umeshindwa kujenga chama taasisi kwani hivi sasa kila chama ni cha mtu.Vyama vingi ni vya watu na si taasisi.Dhana ya taasisi ni kwamba sheria ,kanuni na taratibu lazima zifuatwe

"Kama mtu anadharau katiba na misingi iliyowekwa basi huo niudikteta. Wapinzani kabla ya kukimbilia kugombea udiwani na ubunge wajikite kwanza kujenga taasisi, kama wameshindwa kuheshimu katiba za vyama vyao wanapate uhalali wa kudai Katiba,"alisema.

Alisema sababu nyingine vyama vya upinzani vimekosa uamuzi shirikishi."Chadema ambayo inajieleza ni chama cha upinzani chenye nguvu kimeshindwa kuwa na utaratibu wa kuwa na maamuzi shirikishi na hata yanayoamriwa ni maamuzi ya mtu.Na pia kuna ukiukwaji wa uteuzi wa nafasi ikiwamo za ubunge viti maalumu ambao umetawaliwana rushwa  na kupeana nafasi kirafiki.

"Tatizo la upinzani hakuna kuheshimiana na ukosefu wa maadili ya viongozi. Kama Taifa lazima liwe na viongozi wanaozingatia maadili,kwa mfano leo hii Ukawa wakichukua nchi nani anaweza kuwa WaziriMkuu,"amesema.

Kada huyo wa CCM, amesema kuwa vyama vya upinzani adui yaomkubwa ni CCM lakini wameshindwa kuwa na uwazi kwenye mali zaokwani hata Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),akikagua ni lazima atapata hati zenye shaka kwani fedha za ruzukuzinatumika vibaya.

"Wanaosema nimenunuliwa wanajidanganya kwani wakati anakwenda chadema wamemnunua kwa shilingi ngapi. Kuna wabunge zaidi ya 15w ataondoka Chadema na kuna wajumbe wapo ndani ya chama hicho lakini tayari wameshaondoka ila wanaingia kwenye vikao ili kutimiza wajibu tu," alisema Katambi.

Alisema kwa sasa vyama vya upinzani wamekosa ajenda na waliopo huko  wanakwenda tu bora liende na wengine wanajua wakitoka hawataajirika.

"Kukosea ajenda chadema walikuwa wanasema wanapambana na ufisadi na hata Dr. slaa aligeukwa kwa sababu ya masilahi ya watu binafsi.Chadema ya Dk. Slaa kila mtu  anaifahamu ilifika wakati akapelekwa Marekani kwa ajili ya kuandaliwa ili aje kuwa Rais lakini baadaye wakaanza kumtuhumu kwa usaliti," alisema

Kutokana na hali hiyo amesema kuwa sasa umefika mwisho wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwani malengo ya Chadema yametimia kwa kuua nguvu ya kila chama ili wabaki wao katika upinzani.

Chanzo cha Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume na Tiba Yake

0
0

Tendo la ndoa limengawanyika katika makundi matatu baadhi yake makudi hayo niuhanisi, kufanya tendo la ndoa maramoja na kushidwa kurudia tena 

sababu zinazo pelekea ni ugonjwa wa kisukari, kujichuwa, maumivu ya mgongo na kiuno, tumbo kuuguruma na kujaa gesi, msogo wa mawazo, presha, kutokuwa nyama sehemu ya haja kubwa yani mgoro, ulevu wa kupidukia, kuadhilika na madawa ya kulevya 

ARRBERA 1 Ni dawa ya asili ambayo imefanyiwa tafiti kwa hali ya juu isiyo na kemikali yoyote kwa mtumiaji ambayo humfanya mtumiaji kufanya tendo la ndoa maratatu bila kuchoka 

Pia ARRBERA 2 ni dawa asili abayo huimalisha ukuaji wa umbile la kiume lililo sinyaa na kunenepesha saizi upedayo. sihayo tu upade wa wamatatizo kisukari yakushuka na kupada kuna dawa ya kutumia siku saba na kufanya sukari ibaki nomo balasi abayo ni 4-5-6 vilevile kwaupade wa kina mama matatizo ya uzazi na hedhi kuvurugika na kutokwa maji maji sehemu za sili fagasi na kifafa cha mimba kwa kina mama waja wazito na kifafa cha kawaida 

FIKA OFISINI KWETU MBANGALA RAGI TATU ASIYE KUWA NA NAFASI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO KWA KWA KAZI WA DSM muone dr kabero simu 0758078280 au 0713 293 988 wote mnakalibishwa
No automatic alt text available.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Kamishna wa TRA amsimamisha kazi Meneja wa Mara

0
0

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),  Charles Kichere amemsimamisha kazi Meneja wa TRA Mkoa wa Mara  Nicodemus Mwakilembe kwa kushindwa kusimamia vizuri mashine za  Kielektroniki za Kutolea Risiti (EFDs).

Uamuzi huo umetokana na ziara ya kushtukiza ya kukagua matumizi ya EFD aliyoifanya Kamshina Mkuu wa Tra kwenye baadhi ya maduka ya biashara Wilayani Bunda Mkoa wa Mara.

Akizungumza mara baada ya ziara yake, Kamishna Mkuu Kichere alisema kuna wafanyabishara wengi mkoani Mara  ambao walishalipa fedha kwa ajili ya kupata mashine za EFD lakini mpaka sasa hawajapatiwa mashine hizo.

"Katika ziara yangu nimegundua kwamba, wapo wafanyabiashara ambao wameshalipia mashine tangu mwaka 2013, 2014 na 2015 lakini mpaka sasa bado hawajapatiwa mashine za EFD na wamekuwa wakitumia mwanya huo kama kinga ya kutochukuliwa adhabu na TRA wakati Meneja wa Mkoa  yupo na hachukui hatua zozote. Huu ni uzembe uliopitiliza na kamwe siwezi kuuvumilia," amesema  Kichere.

Kichere amewaagiza mameneja wote wa TRA nchi nzima pamoja na majukumu mengine, kuhakikisha wanasimamia kikamilifu matumizi ya mashine za EFD katika mikoa yao na amesema hatasita kumuwajibisha meneja yeyote atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Ziara hiyo ya kushtukiza imewawezesha wafanyabiashara waliokuwa wamelipia mashine za EFD miaka ya nyuma, kupata mashine hizo na kufundishwa jinsi ya kuzitumia ambapo wengine wamejitokeza kununua mashine hizo kwa ajili ya biashara zao.

Kamishna  Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania yuko mkoani Mara kwa ziara ya siku tano  ambapo amepata nafasi ya kutembelea Vituo vya Forodha mipakani na ofisi mbalimbali za mamlaka hiyo pamoja na baadhi ya wafanyabiashara akikagua matumizi ya mashine za EFD.

Rais Magufuli: Tunaposikia Kuna Migogoro Kanisani, Huwa Najiuliza sana Tukimbilie Wapi sasa?

0
0
Rais Dkt. John Magufuli amesema mara zote anaposikia matatizo yametokea eneo fulani fulani huwa anajiuliza akimbilie wapi ili aweze kupata msaada wa utatuzi wa jambo hilo bila ya kuleta athari yeyote katika taifa.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo (Jumapili Februari 04, 2018) wakati alipohudhuria hafla ya kumweka wakfu na kumsimika Mchungaji Jackson Sosthenes kuwa Askofu wa tano wa Kanisa la Anglikana Dayosis ya Dar es Salaam.

"Sisi viongozi wa serikali mara nyingi huwa tunawategemea viongozi wa makanisa na misikiti katika kutuongoza, nafahamu serikali haina dini lakini naheshimu sana dini na kuthamini mawaidha pamoja na mafundisho yanatolewa na viongozi wa dini wawe waislamu, wakristo hata wahindu tunayaheshimu sana", alisema Rais Magufuli.

Pamoja na hayo, Rais Magufuli aliendelea kwa kusema "siku zote sisi viongozi ndani ya serikali huwa tunafurahi sana kuona makanisa na misikiti ikiwa imetulia, unaposikia mahali fulani fulani kuna migogoro sisi viongozi na hasa mimi huwa najiuliza ninapopata matatizo ntakimbilia wapi. Kwa sababu makanisa na misikiti ni sehemu ya uponyaji wa roho zetu. Uponyaji wa roho ni mahali ambako kuna manufaa zaidi kuliko kwenye uponyaji wa mwili".

Kwa upande mwingine, Dkt. Magufuli amedai endapo mahali kwenye uponyaji wa mwili ukisikia kumeanza matatizo basi unapaswa kutazambua jinsi taifa unaloliongoza roho zake zitakavyopotea.

Wabunge Chadema, CUF wamjulia hali Sugu mahabusu

0
0
Wabunge wamefika Gereza Kuu la Ruanda jijini Mbeya kumjulia hali mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi 'Sugu'.

Waliomtembelea Sugu ni mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema na wa Tandahimba (CUF), Katani Katani.

Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wapo mahabusu wakikabiliwa na kesi ya kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Lema na Katani wakiongozwa na mwenyeji wao Mbunge wa  Viti Maalumu, Sophia Mwakagenda pia wamefika nyumbani kwa Desderia Mbilinyi, mama mzazi wa Sugu eneo la Sae jijini Mbeya kwa ajili ya kumfariji na kumtia moyo kutokana na misukosuko anayopitia mtoto wake.

Wakizungumza na familia ya Sugu, wabunge hao wamesema yupo gerezani kwa kuwa anapigania haki za wananchi.

Lema amemtaka mama huyo kuwa na moyo wa uvumilivu.

Serikali Yalikubali Ombi la Reginald Mengi

0
0
Serikali imebariki uanzishwaji wa taasisi ya Dk. Reginald Mengi Disabled Foundation yenye lengo la kusaidia walemavu nchini.

Hilo limesemwa leo Februari 4, na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika hafla ya chakula cha mchana kwa watu wenye ulemavu iliyoandaliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya IPP, Reginald Mengi.

Majaliwa amesema Serikali inatambua mchango wa Mengi katika uthamini wa walemavu ambapo hafla hiyo imefanyika kwa miaka 25 na itaendelea kuwa endelevu hivyo Serikali imeridhia taasisi kuanzishwa.

“Tunataka tufanye uamuzi wa kuungana na wewe, usilifanye jambo hili kama Dk Mengi pekee mimi napendekeza ulifanye kitaasisi, uunde taasisi kwa jina lako ambalo Serikali tumeridhia litumike, Reginald Mengi Disabled Foundation kwa kazi nzuri nataka jina lako liingie kwenye vitabu vya Serikali,” amesema Majaliwa.

Majaliwa ameanza kwa kuichangia Sh10 milioni  ambayo itaingia pindi usajili wa taasisi hiyo utakapokamilika kwa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela).

Majaliwa ameelezea hatua mbalimbali Serikali inazochukua dhidi ya walemavu ikiwa ni kila halmashauri kutenga fedha kwa ajili ya kuwakopesha, kutenga maeneo kwa ajili ya biashara na ujenzi wa majengo utakaowekwa eneo la kupandia walemavu.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu) , Stella Ikupa amesema Serikali inatambua changamoto mbalimbali zinazowakuta walemavu na inahakikisha inazitatua.

Katika hafla hiyo Mkurugenzi wa kampuni ya Kamal Group inayojihusisha na utengenezaji wa nondo walitoa msaada wa miguu bandia kwa baadhi ya walemavu wa miguu.

Mengi amesema amekuwa akifanya hafla hiyo kwa miaka 24 na itakuwa endelevu kila mwaka.

TRA yazifungia hoteli tatu Mtwara kwa Kushindwa Kulipa Kodi

0
0
Mamlaka ya Mapato  TRA  imezifungia hotel tatu mkoani humo pamoja na kituo cha kuuza mafuta kwa kushindwa kulipa kodi .

Hotel zilizofungiwa ni Naf Beach, Naf blue, BNN pamoja na kituo cha Mnarani Petrol Station ambao kwa pamoja wanadaiwa zaidi ya Sh1bilioni ambazo ni malimbikizo ya madeni ya nyuma kwa kipindi cha miaka mitatu.

Ofisa mwandamizi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi mkoa wa Mtwara,  Flavian Byabato amesema zoezi hilo ni endelevu kwa mkoa mzima.

“Ni madeni ambayo yametokana na ukaguzi kwa kipindi cha miaka mitatu nyuma, kikubwa walipe kodi..tunafungia kwa mambo mbalimbali kama malimbikizo ya madeni ya muda mrefu, matumizi sahihi ya mashine za EFD katika kutoa na kudai risiti sahihi inayoakisi gharama halisi ya malipo na kutii sheria  za kodi kama kutunza kumbukumbu,” amesema Byabato

Byabato amesema endapo wadaiwa watashindwa kulipa madeni yao watachukua hatua nyigine kama kukamata mali au kuwapeleka mahakamani kama hawatajitokeza kuomba na kuahidi ni lini watalipa madeni kwani hakuna aliyejitokeza kufanya hivyo.

Aidha amesema pia yapo maduka madogo ambayo yamefungiwa na kwa sasa wako wilayani Masasi wanaendelea na ukaguzi.

Live Ikulu: Rais Magufuli akiwatunuku Kamisheni Maafisa wapya wa JWTZ

0
0
Fuatilia hapa moja kwa moja kutoka katika viwanja wa Ikulu jijini Dar es salaam, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akiwatunuku Kamisheni Maafisa wapya wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ). 

Bofya hapa kutazama

Rosa Ree Afanya Maajabu..Atoa Wimbo Mkali Akimshirikisha Billnass..Unaweza Kusikiliza na Kudownload Hapa

0
0
Msanii wa Hip Hop wa Kike Bongo Aliyewakalisha wengine ameachia wimbo mpya akiwa kamshirikisha mkali mwingine anayeitwa Billnass..Wimbo huo umekuwa gumzo vituo vya radio kila kona ..Unaweza Kuudownload hapa Chini ni bure kabisa

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya January 5

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images