Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Dokta Mpango Ateta Na Mkurugenzi Mtendaji Wa Benki Ya Barclays Kuhusu Reli Ya Kisasa Na Mradi Wa Umeme Wa Stiegler's Gorge

$
0
0
Benny Mwaipaja, Dodoma
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, amekutana na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Barclays Kanda ya Afrika, Bw. Peter Matlare na kuiomba Benki hiyo kuangalia uwezekano wa kutoa mkopo nafuu wa ujenzi wa miradi mikubwa inayotekelezwa na Serikali ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati kwa viwango vya kimataifa (SGR) mradi wa miundombinu ya umeme wa Stieglar's Gorge ili kurahakisha maendeleo ya kiuchumi kupitia viwanda.

Amemweleza kiongozi huyo kwamba Serikali imeimarisha uchumi Mkuu kwa kudhibiti mfumuko wa bei ambao uko katika kiwango chatarakimu moja cha wastani wa asilimi 5.3 katika kipindi cha miezi 6 iliyopita.

"Tumewekeza kwenye miundombinu kama vile Elimu, maji, kilimo, afya, madini, na biashara na kwamba katika kipindi kifupi cha miaka 2 zaidi ya viwanda 80 vimejengwa katika eneo la Mkuranga mkoani Pwani, kutokana na fursa za uwepo wa bomba la gesi na eneo hilo kuwa karibu na Bandari ya Dar es Salaam.

Dkt. Mpango ameelezea pia mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (SGR) ambao amesema utarahisisha usafiri na usafirishaji wa abiria na mizigo katika nchi zinazopakana na Tanzania hivyo kukuza biashara kwa kiwango kikubwa.

Akizungumzia kuhusu ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme katika Bonde la mto Rufiji (Stiegler's Gorge), Dkt. Mpango amesema lengo la mradi huo utakao zalisha megawati 2,100 za umeme utakao kuwa wa uhakika na bei nafuu ili kukuza viwanda.

Alisema kuwa mwelekeo wa Serikali kwa sasa ni kuhakikisha kuwa kila biadhaa zinazozalishwa nchini pamoja na madini, vinaongezwa thamani hapa hapa nchini badala ya kuuzwa kama malighafi na kwamba nishati ya umeme ndiyo nguzo kuu ya kufikia malengo hayo.

"Ili tuweze kufikia azma hiyo tunahitaji kuwa na umeme wa uhakika na wa bei nafuu ili viwanda vyetu viweze kuzalisha kwa wingi ndio maana tunaiomba Benki yako iweze kufikiria namna ya kushiriki katika ujenzi wa miradi hii" Alisisitiza Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango ameipongeza Benki ya Barclays ambayo pia ni mwanahisa katika Benki ya NBC kwa ahadi yake ya kutaka kuwekeza kiteknolojia katika sekta ya benki nchini hatua ambayo itasaidia kukuza mitaji na mikopo kwa kundi kubwa la watanzania wakiwemo wajasiriamali wadogo, wa kati na wakubwa.

Alielezea msimamo wake kwamba katika kukuza uchumi, Serikali inathamini mchango mkubwa wa Sekta Binafsi na imeendelea kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na kwamba hivi karibuni alikuta na wadau wa Sekta ya Benki ili kusikiliza changamoto zao na pia kuwaeleza mambo muhimu ambayo ingependa sekta Binafsi ifanye ili kufikia malengo yanayokusudiwa.

Awali, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo ya Barclays anaye hudumia kundi la benki za Barclays Barani Afrika na kwingineko Marekani na Ulaya, Bw. Peter Matlare, ameipongeza Serikali chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa kusimamia kikamilifu uchumi wa nchi unaokua kwa wastani wa asilimia 7.

Alisema hatua hiyo ni ya kupigiwa mfano katika nchi za Kiafrika na Duniani kwa ujumla ambapo amesema Tanzania imekuwa ikifanya vyema katika kukuza uchumi jumuishi unaowafikia watu wengi zaidi wakiwemo waishio mijini na vijijini.

Bw. Peter Matlare amemhakikishia Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, kwamba Benki yake itayafanyia kazi mapendekezo ya kutaka ushiriki wake katika ujenzi wa miradi mikubwa iliyoainishwa na Serikali kuwa kipaumbele chake.

Mwisho

Picha: Ndege yaanguka na kuwaka moto uwanja wa ndege wa Zanzibar

$
0
0
Marubani wawili wamefariki Dunia katika ajali ya ndege wakati wa kurusha ndege baada ya matengezo katika Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani karume.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotekea jana majira ya saa saba Mchana Uwanjani hapo, Muhandisi Mkuu kutoka kampuni ya Tropical Air, David Kisusi  amesema ndege hiyo imeanguka na kuungua na kusababisha vifo kwa marubani hao ambao walikuwa ndani ya ndege hiyo.

Amesema ndege hiyo yenye usajili wa 5H-TDF yenye uwezo wa kubeba abiria wanne ni mali ya Chuo cha Usafirishaji cha Dar-es-Salam (NIT) ambayo ilikuwepo Zanzibar kwa ajili ya matengenezo.

Amesema takriban miezi sita ndege hiyo ipo hapa Zanzibar kwa ajili ya kufanyiwa matengenezo ili iweze kutumika katika chuo cha Usafirishaji .

Daktari Bingwa wa Uchunguzi katika Hospital ya Kuu ya Mnazi mmoja, Msafiri Marijani amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na amesema vifo hivyo vimesababishwa na kukosa hewa safi wakati wa ajali hiyo pamoja na kathirika na moto uliotokea wakati wa kuanguka ndege hiyo.

Amesema uchunguzi ulifanywa katika miili ya maiti hao mnamo majira ya saa 12:45 jioni pia ulitokana na kukosa msaada wa kwa muda mrefu tangu ndege hiyo ianguke na kulipuka.

Wakati huohuo Mkuu wa Chuo cha Usafirishaji wa Anga kutoka Dar es Salaam, Dkt. Bwire Rufunjo alifika Zanzibar kwa ajili ya kufuatilia taarifa za ajali hiyo na amesema wamepokea taarifa hiyo kwa mshtuko mkubwa kutokana na vifo vya wafanyakazi hao muhimu katika sekta ya anga.

Aliwataja  marehemu kuwa ni Injinia Edger Alfred Mecha mwenye Umri wa miaka 26 na mwengine ni Dominic Bomani mwenye umri wa miaka 64 ambao walikuwa wanafanya kazi katika chuo hicho kwa ufanisi mkubwa.

Aidha amewataka wanafamilia wa Marehemu hao kuwa wavumilivu katika kipindi hichi kigumu kufuatia msiba huo pamoja na kutoa wito kwa wanafunzi wa chuo hicho kutokata tamaa wakati wa masomo.

Akizungumzia sababu ya kuanguka kwa ndege hiyo ndogo, amesema uchunguzi bado unaendelea lakini katika uchunguzi wa awali wamebaini kuwa ni hitilafu ya mfumo wa umeme ambao umesababishwa na moto ulilipuka kutokana na ndege kuwa na Mafuta mengi.

Ndege hiyo imenunuliwa kutoka kampuni ya Tropical Air ya Zanzibar kwa ajili ya kufundishia Urubani katika  Chuo cha Usafirishaji lakini kutokana na kutokuwa na hali Nzuri ililazimika kufanyiwa matengenezo na kampuni hiyo kabla kuchukuliwa na chuo.

Rais Magufuli Amlilia Mzee Kingunge Ngombale Mwiru

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa huzuni na masikitiko taarifa za kifo cha mmoja wa waasisi wa Taifa na mwanasiasa mkongwe nchini Mzee Kingunge Ngombale Mwiru kilichotokea leo tarehe 02 Februari, 2018 saa 10:30 alfajiri katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Mzee Kingunge Ngombale Mwiru alikuwa akipatiwa matibabu hospitalini hapo baada ya kushambuliwa na mbwa wake nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Desemba, 2017.

Mhe. Rais Magufuli amesema Taifa limempoteza mtu muhimu ambaye alitoa mchango mkubwa katika juhudi za kupigania uhuru na baada ya kupata uhuru akiwa mtumishi mtiifu wa Chama cha TANU na baadaye Chama Cha Mapinduzi (CCM), na katika nyadhifa mbalimbali za uongozi ndani ya Serikali.

“Mzee Kingunge Ngombale Mwiru ametoa mchango mkubwa sana, sisi kama Taifa hatuwezi kusahau na tutayaenzi mema yote aliyoyafanya wakati wa utumishi wake uliotukuka, ametuachia somo la kupigania maslahi ya nchi wakati wote, kuwa wazalendo wa kweli, kudumisha amani na mshikamano, kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kuwa na nidhamu” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Kufuatia msiba huu, Mhe. Rais Magufuli amewapa pole wanafamilia wote, wanachama wa CCM, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na msiba huu, na amewaombea kuwa na moyo wa subira, uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki cha majonzi.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Kingunge Ngombale Mwiru mahali pema peponi, Amina.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
02 Februari, 2018

Dawa ya Asili ya Vidonda vya Tumbo, Pumu, Nguvu za Kiume, Korodani kuvimba

$
0
0
Super Muhi Mix Power:  Ni dawa ya nguvu za kiume kutoka Congo, inatibu na kuponesha kabisa tatizo la nguvu za kiume, itakufanya uweze kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka. Itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 20- 25, huimaliha misuli iliyolegea na kusinyaa. Dawa hii imechanganywa na mizizi 11.

Sub 3Mix; Hii ni dawa ya mvuto wa mapenzi, huvuta mume, mke, mchumba na atatimiza ahadi zote alizokuahidi. Pia mkufu na pete ya bahati vipo.

Pata pia dawa ya pumu, ngiri, kisukari, kaswende, vidonda vya tumbo na korodani kuvimba

Mawasiliano: 0659874143-Dr. Hussein Omary

Huduma hii utaipata popote ulipo. Tupo Mbagala Dar es Salaam kwa sasa

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Serikali yabanwa madudu mkataba wa Mlimani City

$
0
0
Bunge limeitaka serikali kuhakikisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) anafanya ukaguzi wa kiuchunguzi na kiufanisi katika mikataba yote inayohusu mradi wa Mlimani City na kuwasilisha ripoti bungeni, baada ya kubaini dosari kubwa kwenye uendeshaji wa mradi huo.

Agizo hilo limetolewa ikiwa ni wiki mbili baada ya chombo hicho cha kutunga sheria kuukagua mradi huo jijini Dar es Salaam.

Katika ukaguzi wake, Bunge liligundua mbia wa mradi huo unaokihusisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) amewekeza mtaji wa Dola za Kimarekani 75 (Sh. 150,000) kutoka mfukoni kwake.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Naghenjwa Kaboyoka, ndiye alitoa agizo kwa CAG kukagua mradi huo alipowasilisha bungeni mjini hapa jana taarifa ya shughuli za kamati yake kwa mwaka 2017.

Alisema upungufu uliobainika katika mradi huo unainyima serikali mapato stahiki na hivyo kuwa eneo mojawapo lenye matumizi mabaya ya fedha za umma.

Kaboyoka alisema kamati yake imebaini dosari kutokana na mradi wa ujenzi wa Mlimani City ulioanza Oktoba mosi, 2004 ukitakiwa kukamilika Septemba mosi, 2006 kwa makubaliano ya mkodishwaji na mkodishaji, kwa maana ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Kampuni ya Mlimani Holding Limited (MHL), kutokamilika mpaka sasa.

Alisema uchambuzi wa kamati yake katika ripoti ya CAG pamoja na mahojiano na uongozi wa UDSM, umebaini dosari kubwa katika usimamizi na uendeshaji wa mradi huo, hali ambayo inaipa serikali hasara.

Alizitaja dosari hizo kuwa ni pamoja na Dola 75 ambazo zilionyeshwa kama mtaji wa MHL ambao ni kinyume cha Sheria ya Uwekezaji ya Mwaka 1977 inayoelekeza kwamba, ili kibali cha uwekezaji kitolewe lazima mwekezaji awe na mtaji wa kutosha.

Mbunge huyo wa Same Mashariki (Chadema) alisema kamati yake pia imebaini Turnstar Holding Limited ni miongoni mwa wanahisa wa MHL na anamiliki hisa moja na kwamba kampuni hiyo imetoa mikopo kwa MHL jumla ya Dola za Marekani 49,027,840.

"Kamati ilipata mashaka kuhusu nia hiyo ya mbia huyu kwa kuwa MHL ana hisa 900 ambazo hazijauzwa na hivyo angenunua badala ya kukopesha. Kamati inaona mbia huyu ana lengo lake la kujinufaisha zaidi kwa kutoa mikopo kwa vile riba anayolipwa inatolewa kwenye mapato ghafi kabla ya kugawana faida," alisema.

Kaboyoka pia alibainisha kuwa kwa miaka 13 tangu mkataba huo uingiwe, mradi wa ujenzi wa hoteli ya nyota tatu yenye vyumba 100 bado haujaanza, kinyume cha makubaliano, hivyo kuongeza gharama za kumalizika kwa mradi. Pia mradi wa utengenezaji wa bustani ya wanyama na mimea (Botanical Garden) uliopaswa kwenda sawia na hoteli hiyo haujatekelezwa.

Aliongeza kuwa kumekuwapo ukiukwaji wa malipo ya pango la ardhi ya chuo ambapo vifungu cha 1.1(j) na 10.1 vya mkataba vinaeleza kuwa UDSM itapata asilimia 10 ya pango la mapato ghafi, lakini MHL imekuwa ikifanya malipo ya pango kwa chuo baada ya kutoa gharama za uendeshaji, hivyo kuikosesha serikali mapato stahiki kinyume cha mkataba.

Pia alisema wamebaini kukiukwa kwa kifungu cha 12.2(l) cha hati ya makubaliano ya mpangaji kinachomtaka MHL kutopangisha mtu yeyote ambaye hajathibitishwa na mpangishaji (UDSM).

Alisema ukaguzi wao umethibitisha kuwa MHL amekuwa akipangisha wapangaji wengine bila kupata kibali cha chuo hivyo kusababisha chuo kukosa taarifa sahihi za mapato ya kodi kutoka kwa wapangaji wake.

Kaboyoka alisema kamati hairidhishwi na mazungumzo yanayoendelea kati ya UDSM na MHL kwa kuwa mwekezaji huyo amekuwa akiyakataa mapendekezo yote yenye maslahi kwa pande zote mbili badala yake amekuwa akishikilia mapendekezo yenye maslahi kwake tu.

"Wakati huo MHL ameongeza eneo la maduka na maegesho ya magari ambayo hayakuwamo katika mkataba.

Kama hiyo haitoshi, mwekezaji ameshindwa kuanza utekelezaji wa ujenzi wa hoteli na Botanical Garden ambavyo vipo kwa mujibu wa mkataba," Kaboyoka alisema.

Kigogo wa PAC huyo alisema mapitio ya mkataba yamebainisha kuwa hauelezi hali ya ugawanaji mali pindi mkataba utakapomalizika (miaka 50 au 85) kwa kuwa hakuna makubaliano rasmi yanayoeleza mgawanyo wa mali na miundombinu itakayokuwapo pindi mkataba utakapoisha.

Alibainisha kuwa athari ya jambo hilo ni kuwa kuna uwezekano mkubwa kutokea mvutano wa kisheria pindi mkataba huo utakapofika ukomo.

Kaboyoka alisema dosari nyingine ni kuhusu ushiriki wa serikali kupitia Kituo cha Uwekezaji (TIC) ambapo kituo hicho na MHL wamekuwa wakibadilisha muda wa utekelezaji wa mradi mara kwa mara kwa kumwongeza mwekezaji muda wa kukamilisha mradi bila kukihusisha chuo.

"Kwa mfano, mkataba wa kwanza ulisainiwa Februari 27, 2006 na kumwongeza mwekezaji kipindi cha utekelezaji wa mradi hadi Oktoba 30, 2009. Mkataba wa pili ulisainiwa Julai 13, 2007 kwa kuongeza muda wa utekelezaji hadi Novemba 30, 2013 na mkataba wa tatu ulisainiwa Desemba 10, 2014 ambao uliongeza muda wa utekelezaji wa mradi huo hadi Desemba 31, 2019," alisema.

Kaboyoka pia alisema mkataba unaonyesha kuwa zilitakiwa kujengwa nyumba 50 za kuishi (house estate/villas) lakini kamati yake ilipotembelea mradi huo zilizonekana nyumba 45 na nyumba moja yenye vyumba viwili vilivyotenganishwa na milango miwili.

Kutokana na dosari hizo, Kaboyoka alisema mradi wa Mlimani City unapaswa uangaliwe kwa kina kuanzia mkataba wa kwanza hadi hapo ulipofika sasa.

Kubenea Awaonya CCM....."Litakalotokea Tusilaumiane"

$
0
0

Mbunge wa jimbo la Ubungo Saed Kubenea amevitaka vikundi vinavyodaiwa kuwa vya CCM vinavyozunguka kuandikisha vitambulisho vya watu kuacha mara moja kabla hawajachukua hatua ambazo amezitaka zisilaumiwe.

Akizungumza jana na wanahabari, Kubenea alisema kwamba wamegundua wapo vijana ambao wamekuwa wakilizunguka jimbo la Kinondoni na kuwalaghai wapiga kura kwa kununua vitambulisho, kuchukua shahada pamoja na kununua vitambulisho hivyo ili kupunguza idadi za wapiga kura kwa makusudi.

Kubenea amesema kwamba endapo vikundi hivyo vitakaidi agizo hilo watashughulikiwa kama wahalifu kwani kitend wanachokifanya ni kitendo cha uhalifu.

"Mnyika alituambia  kuwa wanaofanya hivyo ni vibaka kama vibaka wengine, hivyo wanapaswa kushughulikiwa.  Na sisi tunasema kwamba Tutaingiza vijana wetu mitaani ili washughulikiwe na lolote litakalotokea wasituulize." Kubenea

Pamoja na hayo kubenea amesema kwamba tayari wamekwishapeleka malalamiko yao katika vyombo husika.

Kubenea kwa sasa ndiye Kampeni Meneja wa Mgombea Ubunge wa Kinondoni, Salum Mwalimu wa CHADEMA katika uchaguzi mdogo wa marudio unaotarajiwa kufanyika Februari 17

Ijue Afya Yako: Pata Tiba Asili ya Busha, Maumbile Madogo na Nguvu za Kiume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaayhiri watu  wengi sana baada ya kujiona wako tofauti na watu wengine .Kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na maumbile  nchi-6-7 .Matatizo haya yanasababishwa na punyeto) kisukari) presha) naulevi wakupita kiasi pia na msogo wa mawazo, homoni za toka kuzaliwa 

MOMLA ni dawa inayotibu kinacho sababisha tatizo,kama vile sukari, presha, magonjwa ya zinaa, misuli kulegea na kusinyaa kwa kwasababu ya kujichuwa au punyeto na akili kudumaa kwaajili ya tendo bila kushiriki 

MBEPE nikwa wenye maumbile mafupi na membamba kwa matatizo hayo ni dozi ya siku 5 unapona kabisa 

DAGULA hii nikwaajili ya wenye busha iwe ya maji au ya utumbo kushuka inatibu bila opresheni , kuuga mifupa kwwaliopata ajari yoyote inayo sababisha uvujifu wa mifupa inatibu kwa mda wa siku 14 tayali kwa mazoizi 

LUKOMOLO ni dawa ya mvuto wa mpenzi biaashara ata kama mme mke mchumba atakutafuta mwenyewe na kutekeleza yote unayotaka mfanye akutafute mwenyewe pia tunatibu kiuno miguu aina yote tumbo la uzazi kwa kina mama na kina baba nk 

KWA WAKAZI WA DSM TUNAPATIKANA MBANGALA RANGI TATU MKABALA NA KISUMA BAA. 

KWAMIKOA YOTE MTAPATA HUDUMA HILI KWA MAWASILIANO PIGA 0767131395, 0712757594, 0787131395 MUONE DR MWANGARA

Kingunge kuzikwa Jumatatu Katika Makaburi ya Kinondoni

$
0
0
Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale-Mwiru anatarajiwa kuzikwa Jumatatu Februari 5, 2018 katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa kamati ya maziko ya mwanasiasa huyo, Omary Kimbau amesema  Kingunge atazikwa saa tisa alasiri.

Hata hivyo, amesema leo Ijumaa Februari 2,2018 kuwa utaratibu na mipango mingine inaendelea kufanyika.

Kingunge amefariki dunia leo alfajiri akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Alikuwa akiuguza majeraha baada ya kung'atwa na mbwa mwishoni mwa mwaka jana nyumbani kwake.

Mpwa wa Kingunge, Tony Mwiru amesema familia inapitia kipindi kigumu kwa kuwa hivi karibuni wamempoteza mama yao, Peras.

Enock Mwiru ambaye ni mdogo wa marehemu na mtangazaji wa zamani wa iliyokuwa Redio Tanzania (RTD),  amesema  Kingunge alikuwa kiunganishi cha familia.

Mabalozi Juma Mwapachu na Ali Mchumo waliowahi kufanya kazi na Kingunge wamefika nyumbani kwa marehemu Kijitonyama kuhani msiba huo.

Wakili: Afya ya Rugemarila, Seth zinatia mashaka

$
0
0
MAHAKAMA  ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa afya ya mmiliki wa IPTL, Harbinder Singh Sethi na mfanyabiashara James Rugemarila zinaendelea kuwa za mashaka.

Hayo yameelezwa leo mapema na Wakili wa utetezi, Respicius Didas baada ya Mwendesha Mashtaka kutoka Taasisi ya kizuia na kupambana na Rushwa (Takukuru) Leornad Swai kudai kuwa upelelezi katika  kesi hiyo bado haujakamilika.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shahidi Wakili Swai ameomba kesi hiyo iahirishwe na kwamba walienda Magereza kuchukua maelezo ya Seth lakini ilishindika kwa sababu afya yake haikuwa nzuri.

Kutokana na taarifa hiyo, Wakili Didas alidai kuwa wakati afya za washtakiwa zikiendelea kuwa za mashaka wanauomba upande wa mashtaka ukamilishe upelelezi.

Amesema ni vema kila kesi hii inapoahirishwa baada ya siku 14 kuwe na kitu kipya kuhusu hatua zilizochukuliwa, lakini inavyoonekana upande wa mashtaka unachukulia kawaida kuahirishwa kwa kesi hiyo.

"Upande wa mashtaka unacheza na mamlaka, utambue hali za washtakiwa ni mbaya, hivyo ukamilishe upelelezi" amesema Wakili Didas.

Swai alidai, Serikali inajitahidi kuangalia afya za washtakiwa kwani hata mara ya mwisho Serikali ilizungumzia afya ya Seth ambaye alidai anataka madaktari wake wawepo wakati akifanyiwa upasuaji.

Kuhusu upelelezi, Swai amedai ni kweli unachukua muda mrefu ila upo katika hatua za mwisho na kitu kinachochelewesha ni upelelezi mwingine kuwa nje ya nchi (Malysia)

Mshtakiwa Rugemarila aliieleza Mahakama kuwa hajawahi kupelekwa Hospital ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu, pia anahisi ana Cancer kwa sababu ya uvimbe alionao, pia Swai amesema daktari wake alisema hana cancer, "anabahati amefiwa angekuja Mahakamani kusema kwamba nina cancer,"

Hakimu Shaidi amesema Mahakama hiyo haina mamlaka ya kutoa amri wakatibiwe nje ya nchi na alishatoa amri kwamba watibiwe Muhimbili na kama inahitajika wakatibiwe nje ya nchi serikali ndio itasimamia.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 16, mwaka huu

Kwa pamoja washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi, utakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya USD 22, 198,544.60 na Sh.Bil 309.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

SSRA, Nida kushirikiana uandikishaji vitambulisho vya Taifa

$
0
0
Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) wanaendelea na awamu ya pili ya uandikishaji wa vitambulisho vya Taifa kwa wanachama wa mifuko yote ya hifadhi ya jamii.

Awamu hiyo itaanza Februari, 5 hadi 28, 2018 katika wilaya tano za Dar es Salaam.

Akizungumza leo Februari2, 2018 meneja miradi wa SSRA, Sara Kibonde amesema lengo la uandikishaji huo ni kuboresha taarifa za wanachama wa sekta ya mifuko hiyo nchini.

Amesema uandikishaji huo ulianzia mkoani Dodoma, ulikuwa ni mpango maalumu lakini waligundua kuwa asilimia 51.2 ya wachangaji na wanufaika wa mifuko hiyo  hawana vitambulisho vya Taifa .

Amebainisha kuwa mifuko hiyo ina wachangiaji zaidi ya milioni moja na wanufaika zaidi ya milioni mbili, huku asilimia 48.8 pekee ndi wenye  vitambulisho vya Taifa.

“Tunashirikiana na Nida kuhakikisha wachangiaji na wanufaika wa mifuko hii wote wanakuwa na vitambulisho vya Taifa, ”amesema Kibonde.

Meneja wa takwimu wa Nida,  Francis Saliboko amesema  wamejipanga ipasavyo kuhakikisha wanamaliza changamoto zote zilizojitokeza awali katika uandikishaji na utoaji vitambulisho hivyo.

“Hakuna atakayepata namba mbili au vitambulisho viwili, kama alijiandikisha mahali popote na tukachukua alama zake za vidole  akiingiza taarifa nyingine ataonekana,”amesema.

TAKUKURU yawatia mbaroni watu wanne kwa Rushwa

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa wa Temeke imewakamata watu wanne, akiwemo ofisa mtendaji Kata ya Jangwani,  Emanuel Kobelo baada kujifanya maofisa kutoka ofisi ya Rais, kupokea rushwa ya Sh2milioni kutoka kwa mfanyabiashara wa madini.

Mkuu wa Takukuru mkoani humo, Pilly Mwakasege amewataja wengine waliokamatwa kuwa ni ofisa mstaafu wa Jeshi la Magereza, Joseph Chilumba ambaye alijitambulisha kama ofisa Usalama wa Taifa, mfanyabiashara wa kampuni ya Equalmalk, Ally Ally na Doroth Magige.

Amesema Januari 30, 2018 waliwawekea mtego watuhumiwa hao na kuwakamata baada ya kuomba rushwa ya Sh3milioni, kupokea Sh2milioni ili wasimchukulie hatua mfanyabiashara huyo  waliyemtuhumu kushirikiana na raia wa kigeni ambao wanafanya biashara ya madini ya dhahabu na almasi.

“Kutokana na kosa la kushawishi kuomba na kupokea rushwa watuhumiwa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani leo na kufunguliwa mashtaka chini ya kifungu cha 15 cha sheria ya Takukuru namba 11 ya mwaka 2007 katika mahakama ya wilaya ya Temeke,” amesema.

Mwakasege amewatahadhalisha watumishi wa umma na wananchi kutojihusisha na vitendo vya rushwa, atakayebainika atachukuliwa hatua bila kuonewa aibu.

TRA yakanusha kutoa magari kwa Taasisi zinazotoa huduma za kijamii

Basi la abiria lapinduka na kuua

$
0
0
Basi la abiria mali ya kampuni ya Tahmeed coach linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam kwenda nchini Kenya jijini Mombasa limepinduka leo na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi watu wengine zaidi ya 20.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa basi hilo limepinduka katikati ya Msata na Kabuku mkoani katika eneo la Kitumbi Tanga na kudai kuwa mtu mmoja alifariki hapo hapo huku wengine zaidi ya 20 wakijeruhiwa.

"Ni kweli ajali imetokea imesababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine 20, majeruhi wengine walipata majeraha madogo madogo hivyo tayari wamesharuhusiwa lakini majeruhi wengine watano nado wanapata matibabu"

Hii ni ajali ya pili kwa mwaka huu inayohusisha basi za Tahmeed  kutokea katika eneo la Kitumbi, Januari 29, 2018 basi jingine liliwaka na kuteketea kwa moto katika kijiji cha Kitumbi wilayani Handeni mkoani Tanga.

Makamu wa rais apigwa mawe

$
0
0
Makamu wa rais wa zamani nchini Zimbabwe Joice Mujuru ameshambuliwa kwa mawe  wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa siasa.

Chama cha upinzani cha Mama Mujuru cha  National People's Party kimesema Bi Mujuru na wanachama wengine walishambuliwa kwa mawe walipokuwa wakifanya mkutano wa kampeni katika viunga vya mji wa Harare.

Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji BBC limesema kwamba msemaji wa chama hicho ameweka wazi kwamba mama Mujuru amejeruhiwa kidogo huku taarifa kutoka ndani ya chama ikisema watu wanane walijeruhiwa katika shambulio hilo.

Taarifa ya chama hicho imesema shambulio hilo lilikuwa la kisiasa na lilifanywa na wanachama wa chama tawala cha Zanu-PF Party.

Kwa upande mwingine Rais mpya wa nchi hiyo Emmerson Mnangagwa, ameahidi kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini humo baadae mwaka huu na kuuhakikishia umma wa nchi hiyo kwamba uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki.

Ahukumiwa kwa kumtilia mkewe pilipili kwenye chupi

$
0
0
Mtu mmoja nchini Uganda anayejulikana kwa jina la Moses Okello amehukumiwa kifungo cha nje na kufanya kazi za jamii kwa siku 40, baada ya kukutwa na hatia ya kumtilia pilipili mke wake kwenye nguo ya ndani.

Mke wa Okello aliiambia mahakama kuwa mume wake huwa anapenda akiwa amevaa nguo hiyo, na siku hiyo alimlazimisha sana kuivaa na kutekeleza, na baada ya muda mfupi alihisi kuwashwa na kuvimba sehemu za siri na kuamua kwenda kumuona daktari, ndipo walipogundua ilikuwa ni pilipili.

“Aliniambia anavutiwa sana na mimi nikiwa nimevaa hiyo nguo akawa ananilazimisha kuivaa, baada ya kuivaa nikaanza kuhisi muwasho sana, nikaenda kumuona daktari na kugundua ilikuwa pilipili”, amesema Mke wa bwana Okello ambaye jina lake limehifadhiwa.

Moses alikiri kufanya tukio hilo kwa mkewe, na kusema kwamba ulikuwa ni utani ambao amezoea kufanyiana na mke wake huyo kipenzi.

Tundu Lissu Amlilia Mzee Kingunge

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amezungumzia kifo cha Kingunge Ngombale Mwiru akisema historia itamkumbuka.

Akizungumza leo Februari 2, 2018  ameanza kwa kusema “namtakia mapumziko mema.”

Amesema Mzee Kingunge alikuwa miongoni mwa wazee wenye historia kubwa na alionyesha ujasiri mkubwa wa kuhama chama chake cha CCM bila kuhofia kuhudhuriwa kutokana na mazingira yalivyokuwa.

“Ni mmoja wa wazee walioonyesha ujasiri mkubwa katika mazingira ya siasa za Tanzania yalivyokuwa, akahama chama tena CCM bila hofu za kuhudhuriwa  akaeleza madhabi yake kuwa hiki chama (CCM) kinatupeleka kuzimu,” amesema Lissu na kuongeza “historia itamkumbuka.”

Kingunge aliyekuwa kada wa CCM mwenye kadi namba nane, Oktoba 4, 2015 alitangaza kukihama chama hicho na kusema hatojiunga na chama chochote lakini mara kadhaa alionekana akipanda majukwaa ya upinzani kumnadi aliyekuwa mgombea urais wa Chadema/Ukawa, Edward Lowassa kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015..

Rais Magufuli amsaidia mlemavu Bajaji

$
0
0
Rais waJamhuriya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametekeleza ahadi yake ya kumsaidia Bajaj Mlemavu wa viungo Bw. Yusuf Abdulrahaman Ndemanga.

Bw. Ndemanga amekabidhiwa Bajaji hiyo na Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike, Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 02 Februari, 2018.

Mhe. Rais Magufuli alikutanana Bw.Ndemanga tarehe 25 Agosti, 2017 katika sehemu ya abiria wakati akisubiri kupanda kivuko cha MV Magogoni kuelekea Kigamboni Jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya kukutana na Mhe. Rais Magufuli, Bw. Ndemanga alimuomba msaada wakupatiwa Bajaj iliimsadie kupata kipato.

Akikabidhi msaada huo Bw. Ngusa Samike amemtaka Bw. Ndemanga kuitumia Bajaj hiyo vizuri nakujiongezea kipato kitakacho msaidia yeye na familia yake.

“Mhe. Rais amenituma nikukabidhi Bajaj hii mpya kabisa, matarajio yake nikuwa itakusaidia kupiga hatua za kimaendeleo, anatarajia kukuona unaongeza Bajaj nyingine na unaisaidia familia yako kupata nafuu ya maisha na sio kuja kuomba msaada mwingine” amesema Bw. NgusaSamike.

Kwa upande wake Bw. Ndemanga aliyeongozana na Mkewe Bi. Hawa Mohamed amemshukuru Mhe.Rais Magufuli kwa msaada huo na ameahidi kuwa ataitumia Bajaj hiyo vizuri kuzalisha kipato kwa ajili ya familia yake.

Rais Magufuli kuwatunuku kamisheni maafisa wapya wa JWTZ

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, kesho tarehe 03 Februari, 2018 atawatunuku kamisheni maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Watakaotunukiwa kamisheni ni maafisa wapya wa Tanzania na kutoka nchi marafiki waliopata mafunzo katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli Mkoani Arusha.

Tukio la kutunuku kamisheni kwa maafisa hao litarushwa moja kwa moja na vyombo vya habari vya redio, televisheni na tovuti rasmi ya Ikulu ambayo ni www.ikulu.go.tz kuanzia saa 3:00 asubuhi.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
02 Februari, 2018
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images