Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Atoa Maagizo Mazito kwa Kamishina wq Uhamiaji

$
0
0
 Rais John Magufuli ameitaka Idara ya Uhamiaji kuhakikisha inapambana na wahamiaji haramu pasipo kumwogopa mtu.

Amemwagiza Kamishna wa Uhamiaji, Dk Anna Makakala kuwachukulia hatua kali watumishi wake watakaoshindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo.

Dk Magufuli akizungumza leo Jumatano Januari 31,2018 akizindua hati ya kusafiria ya kielektroniki jijini Dar es Salaam, amesema utambuzi wa wananchi wanaoishi bila vibali na wenye vibali vilivyoisha ni muhimu.

Amesema uhamiaji ina jukumu kubwa katika kutekeleza hayo.

"Haiwezekani wahamiaji haramu wanakamatwa Mbeya halafu wamepita Kilimanjaro, Manyara. Kamishna (Dk Makakala) ifike mahali unapoona hili washushe vyeo, mwondoe nyota moja ili wajue wajibu wao," ameagiza Rais Magufuli.

Amesema awali Uhamiaji iligubikwa na matatizo yakiwamo ya utoaji hovyo wa vibali vya uraia, hata kwa watu ambao walikuwa hawana sifa.

"Kuna raia wengi walipata uraia bila sifa na wapo waliopata uraia na vyeo vya juu kabisa serikalini wakati  si raia," amesema.

Dk Magufuli amesema hiyo ndiyo sababu iliyofanya akamteua Dk Makakala kuwa Kamishna. "Wanawake ni waaminifu sana na ameanza kutatua matatizo haya."

Baadhi ya viongozi waliohudhuria uzinduzi huo ni Rais wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein; Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan;  na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Wengine ni marais wastaafu Amani Abeid Karume na Ali Hassan Mwinyi; Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma; na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Ali Iddi.

Pia, viongozi wa Serikali, Bunge, Baraza la Wawakilishi, wa dini, wanasiasa, na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Serikali Kuzifikia Kaya Zote Masikini Nchini

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akijibu swali kuhusu utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini nchini Bungeni leo.



Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari: Dk. Kigwangalla Aeleza Hatma Ya Wavamizi Katika Hifadhi Ya Bonde La Mto Kilombero

Rais Magufuli Amjulia Hali Mzee Majuto Hospitalini, Afunguka Alivyomtabiria Makubwa

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemtembelea muigizaji mkongwe, Mzee Majuto katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam ambako amelazwa akitibiwa.

Akizungumza mara baada ya kutembelewa na Rais, Mzee Majuto amefunguka na kudai yeye ndio mtu wa kwanza kutabiri ujio wa Rais Magufuli katika kuongoza nchi ya Tanzania huku akisisitiza kwamba anajisikia faraja kuona ana misimamo iliyokuwa imara.

“Mimi ndiyo mtu wa kwanza kumtabiri kwamba akiwa Rais itakuwa shughuli. Nilishukuru sana kuchaguliwa huyu bwana, tumepata Rais sio masihara watu wote sasa hivi wana adabu zao wanajua nini maana ya kazi”, alisema Majuto.

Pamoja na hayo, Mzee Majuto aliendelea kwa kusema ;“sisi wazee tunafarijika sasa hivi, viwanda kila kona vimetapakaa na leo amekuja kutembea hospitalini hapa sijui kama wengine hawajikojolea huko kwa uoga maana hataki masihara. Hii ndio raha ya kupata viongozi wenye msimamo”.

Kwa upande mwingine, Mzee Majuto amesema sio rahisi kupata Rais mwenye misimamo na asiyekuwa na masihara kama Dkt. John Magufuli.

Nape Nnauye aipa changamoto Serikali

$
0
0
Mbunge Nape Nnauye leo Bungeni ameipa changamoto Serikali juu ya gharama za kuunganisha umeme na kuishauri kuendelea kuchaji elfu 27,000 hata baada ya mradi wa REA kupita ambapo wataanza kuchaji 177,000 kuunganisha umeme.

Nape Nnauye ametoa ushauri huo alipopata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza Bungeni kwenda kwenye Wizara ya Nishati

"Kwanza niipongeze Serikali chini ya Wizara ya Nishati kwa kazi nzuri wanayofanya ya usambazaji mzuri wa umeme vijijini hasa REA awamu ya 3, kwa kuwa gharama za kuunganisha umeme wakati mradi unaendelea ni elfu 27,000 na mradi ukipita ni 177,000 na kwa kuwa idadi kubwa na nzuri ya watumiaji wa umeme ni biashara nzuri kwa TANESCO kwanini bei hii isiwe moja ya elfu 27" alisema Nape Nnauye

Hata hivyo Nape Nnauye aliendelea kusisitiza kuwa kama jambo hilo halitawezekana basi REA waendelee na uwekaji wa nguzo na miundombinu na TANESCO wafanye kazi moja ya kupeleka umeme na kukusanya kodi baada ya kupeleka umeme.

Naibu Waziri Wizara ya Nishati alijibu hoja hiyo na kudai kuwa amepokea ushauri huo wa Mbunge wa Mtama na kuwa atapeleka katika ngazi zingine na kuona Serikali nini itafanya

"Wazo alilosema Kaka yangu Nape Nnauye linapokelewa na litafanyiwa kazi kwani ni la msingi kwa sababu Wizara yetu na shirika letu la TANESCO na wadau wengine wa nishati tunauza bidhaa hii hivyo ni vema tunapouza tupate wateja wengi ili tupate mapato na kuendesha shughuli mbalimbali na uwekezaji mpya wa maeneoya nishati"

TAMISEMI yaagiza Shule ya Sekondari Njombe kuchunguzwa baada ya wanafunzi wote kupata 0

$
0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Rais –Tamisemi, Joseph Kakunda ameagiza mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Njombe kufanya uchunguzi wa matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Viziwi Njombe.

Katika matokeo yaliyotangazwa jana Jumanne Januari 30,2018 na Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), shule hiyo katika matokeo ya mtihani uliofanyika Oktoba na Novemba mwaka jana watahiniwa wote 21 wamepata daraja sifuri (0).

Naibu Waziri Kakunda ametoa agizo la kufanyika uchunguzi leo Jumatano Januari 31,2018 bungeni alipojibu swali la mbunge wa Buyungu (Chadema), Samson Bilago.

Bilago alitaka kujua ni kwa nini shule za wanafunzi wenye mahitaji maalumu zinafanya vibaya kwenye mitihani.

Akizungumzia hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema walimu waliosoma elimu maalumu watapata ajira bila kikwazo cha kusubiri.

Mkuchika amesema wanasubiri kupelekewa orodha ya walimu hao.

Alikuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini aliyetoa mfano wa shule ya Viziwi Njombe ya wanafunzi wa mahitaji maalumu iliyofanya vibaya katika matokeo ya mitihani ya kidato cha nne akisema ni kutokana na kukosa walimu hao.

Mbunge aliyesimamia kiapo cha Raila Odinga Akamatwa

$
0
0
Mbunge wa Ruaraka Tom J Kajwang’, ambaye alisimamia “kuapishwa” kwa kiongozi wa muungano wa Nasa Raila Odinga kwenye viwanja vya Uhuru Park Jumanne amekamatwa.

Mbunge huyo amekamatwa leo Jumatano mchana na maofisa wa polisi ambao hawakuwa wamevalia sare nje ya Mahakama ya Milimani jijini Nairobi.

Alikamatwa muda mfupi baada ya kuhudhuria katika Mahakama Kuu mbele ya Jaji George Odunga kusikiliza uamuzi wa kesi aliyowawakilisha wabunge wanaopinga kukatwa mishahara yao na posho.

Kajwang’ na mwanasheria mwingine Miguna Miguna, ndio walikuwa wasimamizi wakuu wa matukio ya kwenye viwanja vya Uhuru Park yaliyomalizikia kwa “kuapishwa” Odinga kama ‘rais wa watu’.

Wakati wa sherehe za kiapo Kajwang’ alikuwa amevaa vazi na wigi na alishangiliwa sana na wafuasi wa Nasa.

Odinga alikula “kiapo” huku Kajwang’ akiwa amesimama nyuma yake japokuwa wajibu wake katika tukio hilo bado haujafahamika.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya February 1

ILANI Aliyosaini Dk. Kigwangalla Leo Kuhusu Waliovamia kiwanja cha Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kilichopo Njiro, Jijini Arusha

Naibu Waziri Wa Elimu Afafanua Utaratibu Wa Kupata Cheti Mbadala/ Uthibitisho Kwa Mtu Aliyepoteza

$
0
0
NAIBU Waziri wa Elimu ,Sayansi na Teknolojia,William OleNasha,amefafanua utaratibu wa kupata cheti mbadala/uthibitisho kwa mtu aliyepoteza cheti ambapo ameeleza kuwa Baraza la Mitihani litafanya kazi hiyo kwa muda usiozidi siku 30.

Ole Nasha aliyasema hayo jana bungeni mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini,Cosato Chumi (CCM) lililokuwa likihoji ‘’Je ni utaratibu gani unaotumika pale mtu anapopoteza cheti ili aweze kupata cheti kingine’’?,Je ni unapata cheti halisi au nakala? na ni taratibu gani anatakiwa kuzifuata  mtu ili ombi lake lifanyiwe kazi ipasavyo na bila kucheleweshwa?.

Katika majibu yake Naibu Waziri huyo alieleza kuwa mhitimu aliyepoteza cheti hupatiwa cheti mbadala/uthibitisho wa matokeo kwa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi kuhusu upotevu wa cheti na kupata hati ya upotevu.

Pia  mtu aliyepotelewa na cheti atatakiwa kutangaza gazetini kuhusu upotevu huo  kwa lengo la kuutaarifu umma ili kusaidia kukipata na endapo cheti hakitapatikana hata baada ya kufuata utaratibu huo ,mhitimu atajaza fomu ya ombi la cheti mbadala /uthibitisho wa matokeo na kuiwakilisha Baraza la Mitihani.

‘’Baada ya mhitimu kujaza fomu hiyo Baraza la Mitihani hufanya uchunguzi wa uhalali wa umiliki wa cheti husika na kutoa huduma stahiki ,wahitimu waliofanya mtihani kuanzia Mwaka 2008 ambao vyeti vyao vina picha hupatiwa vyeti mbadala ‘’alisema na kuongeza kuwa

“Na waliofanya mtihani kabla ya Mwaka 2008 hupatiwa uthibitisho wa matokeo ambao hutumwa kwa waajiri wao au mahali pengine kwa mahitaji yaliyotolewa na mwombaji na kundi hilo halipewi cheti mbadala’’

Alisema cheti mbadala kinachotolewa ni cheti halisi ambacho huongezwa maandishi yanayosomeka ’DUBLICATE’ kuonyesha kuwa cheti hicho kimetolewa mara ya pili.

LIVE: Rais Magufuli Katika Maadhimisho ya Wiki ya Sheria

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo ni  mgeni rasimi katika maadhimisho ya wiki ya sheria.

==>Tazama tukio zima hapo chini

Mhagama atoa ufafanuzi muungano wa mifuko ya pensheni

$
0
0
Waziri wa nchi Nchi, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemevu, Jenista Mhagama  jana bungeni amewasilisha muswada  wa sheria ya mfuko wa hifadhi ya jamii kwa watumishi wa Umma wa mwaka 2018 na kupendekeza kuunganishwa mifuko ya pensheni ya PSPF, LAPF, GEPF na PPF ili kuanzisha mfuko mmoja wa hifadhi ya jamii.

#Muswada huu unapendekeza kuunganishwa mifuko ya Pensheni ya PSPF, LAPF, GEPF na PPF ili kuanzisha Mfuko mmoja wa Hifadhi ya Jamii.

#Hatua ya kuunganisha mifuko ya Pensheni inalenga kukidhi kilio cha muda mrefu cha wafanyakazi kuhusu kuunganisha mifuko hiyo ili kupunguza gharama za luendeshaji.

#Sheria inayopendekezwa itaweka mfumo madhubuti utakaomhakikishia mwanachama kulipwa mafao ya msingi kama inavyoeleza Katiba ya Jamuhuri ya Muungano Tanzania ya 1977 Ibara ya 11 (1).

#Sheria inayopendekezwa inabainisha kwa uwazi Jumla ya mafao 7 yatayolipwa na mfuko huu ikiwamo *Fao la Pensheni, Fao la warithi, Fao la Ulemavu, Fao la Uzazi, Fao la Ukosefu wa Ajira, Fao la Ugonjwa na Fao la Kufiwa.*

#Sheria inaweka utaratibu bora na ulio rahisi wa wanachama wa mifuko inayounganishwa kuhamia kwenye mfuko mpya pasipo kuathiri mafao yao na uendelevu wa mfuko mpya.

#Kuweka bayana kwamba mafao na michango ya wanachama haitatozwa kodi kama ilivyokwisha bainishwa katika sheria ya kodi.

#Kiwango cha Uchangiaji kitakuwa ni asilimia 20 ambapo mwajiri atachangia asilimia 15 na mwajiriwa atachangia asilimia 5 ya mshahara wake.

#Kuweka mfumo madhubuti utakaohakikisha mwanachama anapata mafao kwa wakati ikiwamo kwa kuutaka mfuko kumlipa mwanachama aliyekidhi vigezo mafao yake hata kama mwajiri hajawasilisha na baadae mfuko utafuatilia michango ambayo haijawasilishwa kutoka kwa mwajiri.

#Kuainisha adhabu ya tozo ya Asilimia 5 kwa mfuko utakaochelewesha mafao ya wanachama.

#Kuainisha adhabu ya tozo ya Asilimia 5 kwa mfuko utakaochelewesha mafao ya wanachama.

#Sheria hii itamwezesha mwanachama kutumia mafao yake kujipatia mikopo ya nyumba na shughuli nyingine za kiuchumi kwa riba nafuu.

#Sheria hii inaainisha kwa uwazi haki na stahili za warithi pale mwanachama au mstaafu anapofariki.

#Sheria inaondoa kilio cha muda mrefu cha wastaafu katika utumishi wa umma kuhusu kukoma kwa mafao/pensheni pale mstaafu anapofariki dunia, sheria hii inaruhusu wategemezi kuendelea kupokea mafao kwa kipindi cha miezi 36.

#Sheria inapendekeza kuboresha masharti kuhusu fao la uzazi ambapo pamoja na kupata fedha taslimu baada ya kujifungua, mwanachama pia atapata huduma za matibabu kabla na baada ya kujifungua endapo huduma hizo hazilipwi na NHIF.

#Mwanachama atakuwa na fursa ya kupata fao la uzazi mara nne katika kipindi chote cha ajira.

#Sheria inapendekeza kuanzisha kwa Fao la Upotevu wa Ajira ili kuondoa changamoto ya muda mrefu ya wanachama kujitoa kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

#Mwanachama atakuwa na fursa ya kupata Fao la Upotevu wa Ajira baada ya kukidhi vigezo vilivyoainishwa ndani ya sheria.

#Vigezo ni Awe amechangia kwa kipindi kisichopungua miezi 18, awe Mtanzania, awe hajaacha kazi kwa matakwa yake mwenyewe, awe hajafika umri wa kupata pensheni, uthibitisho wa Mkurugenzi Mkuu kuwa hajaweza kupata kazi nyingine, awe hajafika umri wa miaka 55.

#Sheria hii inatoa fursa kwa mwanachama anayetumikia kifungo jela kushirikishwa juu ya namna bora ya mafao yake yatakavyotumika ikiwa ni pamoja na kutunza familia yake akiwa anaendelea na kifungo.

*Imeandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO*

Zitto Kabwe: "Hili ni jambo la hatari, kama Serikali isipofanya marekebisho wabunge tusipitishe sheria hii

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Kigoma , Zitto Kabwe amefunguka na kusema jambo ambalo Serikali inataka kufanya kuhusu fao la matibabu litapelekea watu zaidi ya laki sita katika mfuko wa NSSF kukosa fao hilo jambo ambalo litaongeza shida kwa watumishi.

Zitto Kabwe amesema hayo jana Januari 31, 2018 wakati akichangia Bungeni juu ya mswada wa mfuko wa hifadhi ya jamii wa watumishi wa sekta ya Umma na kuwataka wabunge kutoipitisha sheria hiyo kama Serikali haitaifanyia marekebisho kwani kufanya hivyo ni kuwakosesha haki za kimsingi wanachana zaidi ya laki sita wa NSSF.

"Serikali inafanya marekebisho ya sheria ya NSSF, Sheria ya NSSF inatoa 'Health Insurance Benifit' kwa wanachama wa NSSF lakini sheria hii ambayo serikali inaileta hapa inaondoa 'Health Insurance Benefit' kwa wanachama wa NSSF. Hili ni jambo la hatari, sasa hivi NSSF wanazaidi ya wanachama laki sita kwa hiyo Serikali hii inakwenda kutunga sheria kuwaondoa watu laki sita kwenye takwa la kisheria la Health Insurance" alisema Zitto Kabwe

Mbali na hilo Zitto Kabwe aliweza kutoa ushauri ambao Serikali inaweza kuufuata ili mwisho wa siku wanachama wa NSSF waweze kupata haki yao ya msingi ya matibabu pindi mifuko hiyo itakapounganishwa.

"Serikali inataka 'Health Insurance' zote ziwe zinatolewa na NHIF inaeleweka tunachopaswa kukifanya kwenye sheria ni kuweka provision inayosema kwamba fao hilo la Health Insuarance litatolewa na NHIF kwa NSSF kuchukua ile michango inayolipia Health Insurance na kuipeleka NHIF. Hivyo ukiwa na kadi ya NSSF na mwanachama wa NSSF moja kwa moja unakuwa mwanachama wa NHIF, hii ndiyo njia bora kabisa ambayo Serikali inapaswa kufanya na nawashauru ndugu wabunge kama marekebisho haya hayatafanywa tusiipitishe sheria hii kwa sababu tunakwenda kuwaondoa watu laki sita kutoka kwenye 'Health Insurance'" alisisitiza Zitto Kabwe

Msanii Radio afariki dunia

$
0
0
Msanii wa muziki kutoka nchini Uganda, Radio amefariki dunia.

Msanii huyo ambaye alikuwa akifanya vizuri na mwenzie Weasel,  tangu January 23 mwaka huu hali yake ilikuwa ikiripotiwa kuwa mbaya kufuatia majereha aliyoyapata kutokana na ugomvi wa klabu.

Hapo jana Rais wa Uganda, Yoweri Museven alitoa Milioni 30 kwa ajili ya  matibabu ya msanii huyo, pia kulikuwa na maombi maalumu yalikuwa yameandaliwa kwa ajili ya kumuombea ambayo yalitarajiwa kufanyika February 4 mwaka huu katika kanisa la Light the World.

Dawa ya Asili ya Vidonda vya Tumbo, Pumu, Nguvu za Kiume, Korodani kuvimba

$
0
0
Super Muhi Mix Power:  Ni dawa ya nguvu za kiume kutoka Congo, inatibu na kuponesha kabisa tatizo la nguvu za kiume, itakufanya uweze kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka. Itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 20- 25, huimaliha misuli iliyolegea na kusinyaa. Dawa hii imechanganywa na mizizi 11.

Sub 3Mix; Hii ni dawa ya mvuto wa mapenzi, huvuta mume, mke, mchumba na atatimiza ahadi zote alizokuahidi. Pia mkufu na pete ya bahati vipo.

Pata pia dawa ya pumu, ngiri, kisukari, kaswende, vidonda vya tumbo na korodani kuvimba

Mawasiliano: 0659874143-Dr. Hussein Omary

Huduma hii utaipata popote ulipo. Tupo Mbagala Dar es Salaam kwa sasa

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Mtanzania ahukumiwa kunyongwa Uganda

$
0
0
Mahakama Kuu nchini Uganda imemuhukumu raia mmoja wa Tanzania kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya mauaji.

Mtanzania huyo aliyetambulika kwa jina la Matule Chresporeto Coleheri mkazi wa Bukoba anadaiwa kumuua mfanyakazi mwenzake katika shamba moja lililoko eneo la Wakyuto wilayani Nakaseke.

Akisoma hukumu hiyo, Jaji Steven Mubiru amesema baada ya kusikiliza ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka, mahakama imejiridhisha kuwa Matule ndiye alitenda kosa hilo.

Amesema  mashahidi watatu walioshuhudia tukio hilo wameiridhisha mahakama kuwa Thomas Kamuhebwa aliuawa na mtuhumiwa huyo. Mwili wa Kamuhebwa ulikutwa ukiwa umetupwa katika shimo moja na kufungwa katika begi. Mwili uliokotwa  karibu na makazi ya mshtakiwa.

Hata hivyo, mbele ya mahakama hiyo Matule alijitetea kutohusika katika mauaji hayo na kudai tuhuma hizo zilitengenezwa na watu waliotaka kuiba magogo yake aliyoyaandaa kwa ajili ya kuzalisha mkaa.

Awali, ilielezwa mahakamani hao kuwa Matule ni mhamiaji kutoka Tanzania aliyekuwa akifanya kazi za vibarua na kwamba Februari 6, 2014 alimuua Kamuhebwa kwa sababu zisizo julikana na kufukia mwili wake katika shimo.

Kutana na Mtaalam wa Kutafsri Ndoto Yoyote...Anasafisha Nyota na Kutoa Mikosi

$
0
0
SHEIKH SHARIF OMARY
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
SHEIKH SHARIF ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)
 
SHEIKH SHARIF ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)
Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
 
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
 
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
 
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone SHEIKH SHARIF Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
SHEIKH SHARIF Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
 
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.
 
ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
 
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..
 
Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..
Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
 
Mawasiliano ..+255 743 203 171

Jaji Mutungi avionya CCM, Chadema

$
0
0
MSAJILI wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mtungi, amevikumbusha vyama vinavyoshiriki uchaguzi mdogo kuhakikisha vinatii sheria zake, sheria za gharama za uchaguzi na kanuni zake katika kipindi hiki cha uchaguzi mdogo katika Majimbo ya Siha na Kinondoni.

Jaji Mtungi aliyasema hayo kupitia barua aliyoiandikia vyama hivyo juzi kuhusu wajibu wao wa kutii sheria wakati wa uchaguzi huo.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Monica Laurent, alisema vyama hivyo vimetakiwa kutii sheria hasa kwa kuepuka vitendo vya fujo, lugha za uchochezi na matusi.

“Natambua kuwa vyama vyenu vinashiriki katika kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge na udiwani zinazoendelea katika majimbo na kata, hivyo natumia fursa hii pia kuvipongeza vyama vyote vinavyoshiriki katika uchaguzi huo katika tukio hilo muhimu la kidemokrasia,” ulisomeka ujumbe wa barua hiyo kwa vyama vya siasa.

“Aidha, naviasa vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo, kuheshimu na kufuata sheria za nchi, hasa sheria ya vyama vya siasa, sheria ya gharama za uchaguzi na kanuni zake, kwa kuepuka vitendo vya fujo na lugha za matusi na uchochezi,” aliongeza.

Pia Jaji Mtungi alitoa wito kwa wanachama wa vyama vya siasa kutoa taarifa katika mamlaka husika endapo wanashuhudia viashiria vya uvunjifu wa sheria katika kampeni na uchaguzi badala ya kujichukulia sheria mkononi.

Uchaguzi katika majimbo ya Kinondoni na Siha unafanyika baada ya wabunge waliokuwapo kuhama wakitokea vyama vya upinzani vya CUF na Chadema na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katika jimbo la Kinondoni, Maulid Mtulia anagombea kupitia CCM baada ya kujiengua kutoka CUF ilhali Siha, Dk. Godwin Mollel, ambaye naye alihama Chadema na kuhamia CCM, anagombea kupitia chama hicho.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images