Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

LIVE UPDTES: Hali Ilivyo Kenya, 'Raila Odinga Akijiapisha Kuwa Rais'....Matangazo ya TV Yamezimwa

0
0
Hali ya wasiwasi imetanda nchini Kenya baada ya kiongozi mkuu wa upinzani nchini humo Bwana Raila Odinga, kushikilia kuwa ataapishwa leo kama rais wa nchi hiyo.

Muungano wa upinzani National Super Alliance (Nasa) umesema hafla hiyo itafanyika katika uwanja wa Uhuru Park, Nairobi.

Baada ya sherehe hizo kuahirishwa mwezi uliopita, muungano mkuu wa upinzani nchini humo-NASA, bado unaendelea na msimamo wake wa kuwaapisha viongozi wake Raila Odinga na Stephen Kalonzo Musyoka, kama Rais na Makamu wa rais wa Jamhuri ya Kenya.

Maafisa wa polisi walifika asubuhi na mapema katika uwanja wa Uhuru Park, Nairobi unaopanga kutumiwa na muungano wa Nasa kwa shughuli ya kumuapisha Bw Odinga.

Kituo cha habari cha kibinafsi cha Citizen kimeripoti kuwa maafisa wa polisi wameamrishwa kuondoka katika uwanja wa Uhuru Park.

==>Mabasi ya wafuasi wa upinzani yazuiwa Voi
Mabasi matatu yaliyokuwa yanawasafirisha wafuasi wa upinzani waliokuwa wanaelekea Nairobi kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa kiongozi wao Raila Odinga yamekamatwa na maafisa wa polisi katika mji wa Voi, katika barabara ya kutoka Mombasa kwenda Nairobi.

Mji wa Voi unapatikana takriban kilomita 330 mashariki mwa mji huo mkuu wa Kenya.

Afisa wa polisi amewaambia wanahabari kwamba madereva wa mabasi hayo walikuwa wamevunja sheria kadha za barabarani.

Wafuasi wa upinzani nchini Kenya wameanza kuingia uwanja wa Uhuru Park baada ya polisi kuondoka.Baadhi wanazunguka uwanja huo wakiimba ‘Uhuru Must Go’.
 
==>Wafuasi wa upinzani waliozuiliwa Voi waachiliwa
Wafuasi wa upinzani waliokuwa wanasafiri kuelekea Nairobi ambao walizuiliwa awali mjini Voi baadae wameachiliwa na kuruhusiwa kuendelea na safari.

==>Vituo vya habari vyafungiwa matangazo Kenya
Baadhi ya vituo vya redio na televisheni vya Royal Media Services (RMS), vikiwemo runinga ya Citizen TV, vimefungiwa matangazo pamoja na kituo cha televisheni cha NTV kinachomilikiwa na kampuni ya Nation Media Group (NMG) katika baadhi ya maeneo.

Vituo hivyo vimekuwa vikipeperusha matangazo kuhusu sherehe iliyopangiwa kufanyika leo ya kuapishwa kwa kiongozi wa upinzani Kenya Raila Odinga.

Serikali ilikuwa imetahadharisha vituo vya habari Kenya dhidi ya kupeperusha moja kwa moja hafla hiyo.

Mmoja wa wahariri wakuu wa Citizen Peter Opondo amesema  kwamba maafisa wa Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (CA)  wakiandamana na polisi walivamia vituo vya kupeperushia matangazo na kuzima matangazo.

Citizen TV ndicho kituo cha runinga kinachoongoza Kenya. Matangazo ya kituo cha NTV yanapatikana pekee kupitia ving’amuzi vya kulipia. Kituo kingine kikubwa KTN bado kinarusha matangazo.

Shule 10 BORA na Shule 10 za Mwisho Matokeo ya Kidato cha Nne 2017

0
0
Baraza la mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne kwenye mtihani ambao ulifanyika October 2017 ambapo Shule  iliyoshika namba moja inatoka Mbeya.

TOP 10 YA SHULE BORA.

1. St. Francis Girls ya Mbeya

2. Feza Boys ya Dar es salaam

3. Kemebos ya Kagera 

4. Bethel Sabs Girls ya Iringa 

5. Anwarite Girls ya Kilimanjaro 

6. Marian Girls Pwani 

7. Canossa ya Dar es salaam 

8. Feza Girls ya Dar es salaam 

9. Marian Boys ya Pwani 

10. Shamsiye Boys ya Dar es salaam 

TOP 10 YA SHULE ZA MWISHO KITAIFA
10. Mtule ya Kusini Unguja

9. Nyeburu ya Dar es salaam

8. Chokocho ya Kusini Pemba

7. Kabugaro ya Kagera

6. Mbesa ya Ruvuma

5. Furaha ya Dar es salaam

4. Langoni ya Mjini Magharibi

3. Mwenge S.M.Z ya Mjini Magharibi

2. Pwani Mchangani ya Kaskazini Unguja

1. Kusini ya Kusini Unguja

Breaking News: NECTA Watangaza Matokeo ya Kidato Cha Nne 2017....Bofya Hapa Kuyatazama

0
0
Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) limetangaza matokeo ya kidato nne ambapo ufaulu umeongezeka kwa asilimia saba.

Jumla ya watahiniwa  385, 767 walisailiwa kufanya mtihani kidato cha nne mwaka 2017, kati yao 287,713 sawa na asilimia 77.09 ndio wamefaulu ambapo wasichana ni  143,728 sawa na asilimia 75.21 na wavulana 143,985 sawa na asilimia 79.06.

Akitangaza matokeo hayo leo Januari 30, 2018 Katibu Mtendaji wa Necta,  Dk Charles Msonde amesema mwaka 2016 watahiniwa waliofaulu walikuwa 277,283 sawa na asilimia 70.09.

Amesema matokeo ya watahiniwa 50 wa shule ambao walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya baadhi ya masomo ya mitihani hiyo, watapata fursa hiyo mwaka huu.

"Watahiniwa 77 wa shule ambao walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mtihani watapata fursa mwaka 2018," amesema Dk Msonde.

Dk Msonde amesema watahiniwa 265 waliobainika kufanya udanganyifu katika mitihani  matokeo yao yamefutwa huku mtahiniwa mmoja akiandika matusi katika karatasi yake ya majibu.

==>Yatazame Matokeo hapo chini



Matokeo Kidato cha Nne 2017: Wanafunzi 10 BORA waliofanya vizuri na shule wanazotoka

0
0
Baraza la mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne kwenye mtihani ambao ulifanyika October 2017.

==>Watahiniwa 10 waliofanya vizuri na shule wanazotoka ni kama ifuatavyo;

1.Felison Mdee -Marian boys
2.Elizabeth Mango -Marian girls
3.Anna Benjamin Mshana - Marian girls
4.Emanuel Lameck Makoye -Ilboru
5.Lukelo Thadeo Luoga-Ilboru
6.Fuadi Padic -Feza Boys
7.Godfrey Mwakatage -Uwata
8.Baraka Mohammed -Angels
9.Lilian Moses Katabaro -Marian girls
10.Everlyn Moses Mlowe -St. Fransis Mbeya

Wabunge wa Upinzani Wasusa Kutoa Maoni Yao Bungeni

0
0
Msemaji wa upinzani wa Wizara ya Katiba na Sheria, Ally Salehe amesusa kusoma maoni ya upinzani ya Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kukataa kusomwa kwa baadhi ya maneno yaliyomo katika maoni hayo.

Salehe alikuwa akisoma maoni hayo leo Januari 30 mwaka 2018 kwa niaba ya msemaji wa Wizara ya Katiba na Sheria, Tundu Lissu aliyeko nchini Ubelgiji kwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi Novemba 7 mwaka jana.

Maneno yaliyozuiwa na Chenge kusomwa na upinzani ni kuhusu matukio ya uhalifu nchini, likiwemo la kushambuliwa kwa Lissu.

Salehe alianza kusoma maneno hayo lakini alipofika aya ya nne alikatizwa na Chenge akimtaka asubiri, baadaye kumueleza kuwa lugha iliyotumika katika ukurasa kwa kwanza na pili wa hotuba hiyo si ya kibunge.

Baada ya kauli hiyo, Salehe amesema upinzani unaiamini na unaisimamia hotuba hiyo kwa kuwa wabunge wote wanayo nakala yake, akaomba kuiwasilisha na kurejea kuketi.

Wabunge wapya wala kiapo bungeni

0
0
Mkutano wa 10 wa Bunge umeanza leo Januari 30 mwaka 2018 mjini Dodoma kwa wabunge wapya watatu wa CCM kula kiapo cha uaminifu mbele ya Naibu Spika, Dk Tulia Ackson.

Wakati wabunge hao wakila kiapo, takribani wabunge 50 wa upinzani walikuwa nje ya ukumbi wa chombo hicho cha kutunga sheria.

Walioapishwa ni Dk Damas Ndumbaro (Songea Mjini), Justin Monko (Singida Kaskazini)  na Dk Stephen Kisurwa wa Longido.

Pia, Dk Tulia aliomba wabunge kusimama kwa dakika moja kumkumbuka aliyekuwa mbunge wa Songea Mjini, Leonidas Gama ambaye alifariki dunia Novemba mwaka jana.

Ijue Afya Yako: Pata Tiba Asili ya Busha, Maumbile Madogo na Nguvu za Kiume

0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaayhiri watu  wengi sana baada ya kujiona wako tofauti na watu wengine .Kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na maumbile  nchi-6-7 .Matatizo haya yanasababishwa na punyeto) kisukari) presha) naulevi wakupita kiasi pia na msogo wa mawazo, homoni za toka kuzaliwa 

MOMLA ni dawa inayotibu kinacho sababisha tatizo,kama vile sukari, presha, magonjwa ya zinaa, misuli kulegea na kusinyaa kwa kwasababu ya kujichuwa au punyeto na akili kudumaa kwaajili ya tendo bila kushiriki 

MBEPE nikwa wenye maumbile mafupi na membamba kwa matatizo hayo ni dozi ya siku 5 unapona kabisa 

DAGULA hii nikwaajili ya wenye busha iwe ya maji au ya utumbo kushuka inatibu bila opresheni , kuuga mifupa kwwaliopata ajari yoyote inayo sababisha uvujifu wa mifupa inatibu kwa mda wa siku 14 tayali kwa mazoizi 

LUKOMOLO ni dawa ya mvuto wa mpenzi biaashara ata kama mme mke mchumba atakutafuta mwenyewe na kutekeleza yote unayotaka mfanye akutafute mwenyewe pia tunatibu kiuno miguu aina yote tumbo la uzazi kwa kina mama na kina baba nk 

KWA WAKAZI WA DSM TUNAPATIKANA MBANGALA RANGI TATU MKABALA NA KISUMA BAA. 

KWAMIKOA YOTE MTAPATA HUDUMA HILI KWA MAWASILIANO PIGA 0767131395, 0712757594, 0787131395 MUONE DR MWANGARA

Chanzo cha Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume na Tiba Yake

0
0

Tendo la ndoa limengawanyika katika makundi matatu baadhi yake makudi hayo niuhanisi, kufanya tendo la ndoa maramoja na kushidwa kurudia tena 

sababu zinazo pelekea ni ugonjwa wa kisukari, kujichuwa, maumivu ya mgongo na kiuno, tumbo kuuguruma na kujaa gesi, msogo wa mawazo, presha, kutokuwa nyama sehemu ya haja kubwa yani mgoro, ulevu wa kupidukia, kuadhilika na madawa ya kulevya 

ARRBERA 1 Ni dawa ya asili ambayo imefanyiwa tafiti kwa hali ya juu isiyo na kemikali yoyote kwa mtumiaji ambayo humfanya mtumiaji kufanya tendo la ndoa maratatu bila kuchoka 

Pia ARRBERA 2 ni dawa asili abayo huimalisha ukuaji wa umbile la kiume lililo sinyaa na kunenepesha saizi upedayo. sihayo tu upade wa wamatatizo kisukari yakushuka na kupada kuna dawa ya kutumia siku saba na kufanya sukari ibaki nomo balasi abayo ni 4-5-6 vilevile kwaupade wa kina mama matatizo ya uzazi na hedhi kuvurugika na kutokwa maji maji sehemu za sili fagasi na kifafa cha mimba kwa kina mama waja wazito na kifafa cha kawaida 

FIKA OFISINI KWETU MBANGALA RAGI TATU ASIYE KUWA NA NAFASI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO KWA KWA KAZI WA DSM muone dr kabero simu 0758078280 au 0713 293 988 wote mnakalibishwa
No automatic alt text available.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

BREAKING: Raila Odinga Ajiapisha Kuwa ‘Rais wa Wananchi wa Kenya’

0
0
Kiongozi  wa upinzani Raila Odinga (NASA) ameapishwa kuwa ‘Rais wa Wananchi’ wa Kenya licha ya kugomea uchaguzi mkuu wa marudio nchini humo.

Raila Odinga amefika  leo katika Uwanja wa Uhuru Park pamoja na viongozi wengine wakuu wa NASA akiwemo Moses Wetangula na Musalia Mudavadi na kujiapisha akishika Biblia.

Aidha, mgombea mwenza wake Kalonzo Musyoka wa Chama Cha Wiper hakuwepo wakati wa kuapishwa kutokana na kuhofia kukamatwa, ambapo Odinga amesema ataapishwa baadaye.

“Odinga amesema leo ni siku ya kihistoria kwa Kenya, hatua ya leo ni kuelekea kutoa udikteta na kuleta demokrasia Kenya, maelekezo mengine mtayapata baadae,” alisema Odinga baada ya kuapishwa. Awali Raila Odinga aliiambia kituo cha habari cha KTN kwamba shughuli hio ‘ si mapinduzi ya serikali’

Raila aligomea uchaguzi huo kwa sababu za kusema kuwa tume ya Uchaguzi nchini humo si ya Uhuru na haki. Uchaguzi huo wa marudio ulikuja baada ya Mahakama ikiongozwa na Jaji Maraga kutengua Uchaguzi wa awali uliofanyika 8 Agosti.

Katika uchaguzi huo wa Oktoba, Rais Kenyatta alitangazwa mshindi akiwa na kura 7.5 milioni ambazo ni sawa na asilimia 98 ya kura zilizokuwa zimepigwa.

Waliojitokeza kushiriki uchaguzi huo walikuwa 39% kati ya waliojiandikisha kupiga kura. Kenyatta aliapishwa kuwa Rais wa Kenya baada ya uchaguzi wa marudio mnamo tarehe 28/11/2017

Umri wa Kustaafu Kwa Madaktari Bingwa, Wahadhiri Waandamizi na Maprofesa Sasa miaka 65.

0
0
Frank Mvungi- Maelezo, Dodoma.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha muswaada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali ikiwemo sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298  (The Public Service Act) itakayowezesha muda wa kustaafu kwa  Wahadhiri waandamizi, Maprofesa na Madaktari Bingwa kuwa miaka 60 kwa hiari na lazima miaka 65.

Akizungumza wakati akiwasilisha muswaada huo  Mwanasheria  Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju amesema kuwa marekebisho katika jedwali yanapendekeza kuongezwa kwa kifungu kipya cha 25A ambacho kinaainisha kuhusu umri wa kustaafu ambapo kwa sasa sheria ilivyo  haina masharti hayo isipokuwa umri wa kustaafu umetajwa katika sheria zinazoanzisha mifuko ya hifadhi za jamii.

Aliongeza kuwa, uzoefu umeonyesha kuwamba Maprofesa na Wahadhiri waandamizi wa vyuo  Vikuu  vya Umma pamoja na madaktari Bingwa wa Binadamu wa Hospitali za Umma wamekuwa wakihitajika kuendelea kutoa huduma, utaalamu na uzoefu wao licha yakufikisha umri wa miaka 60 kwa sasa ya kustaafu na hivyo kulazimika kuajiriwa na Serikali kwa mikataba.

Hatua yakuwaajiri wataalamu hao kwa mikataba baada ya kustaafu imetajwa kuongeza gharama kubwa kwa Serikali ambapo muswaada ulipitishwa  unawezesha Serikali kuokoa Kiwango kikubwa cha fedha zilizokuwa zikitumika katika kuwalipa wataalamu wao mara baada ya kustaafu ili waweze kufanya kazi kwa mikataba.

Kwa upande wake Waziri  wa Elimu Sayansi na Teknplojia mhe. Profesa Joyce Ndalichako alisema kuwa anaunga mkono hoja  yakuongeza umri wa kustaafu kutoka miaka 60 kwa lazima hadi 65 na kutoka miaka 55 kwa hiari hadi miaka 60.

Aliongeza kuwa Serikali inayo mikakati ya makusudi yakuwaendeleza wataalamu wa kada zenye uhaba  wataalamu wabobezi ili kuziba pengo  lililopo.

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano wake wa 10 kikao cha 1 limepitisha muswaada wa marekebisho ya sheria mbalimbali nne ambazo ni Sheria ya Ufilisi, sura ya 25, Sheria ya Bajeti, sura ya 439, Sheria ya Ardhi, sura ya 113 na Sheria ya Utumishi wa Umma, sura ya 238.

Waziri Jafo: Madarasa Ya Nyasi, Tembe, Udongo Yasitumike Katika Shule Zote Nchini

0
0
Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amewaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi ambao kwenye maeneo yao bado kuna wanafunzi wanasomea katika madarasa ya Tembe ama yalioezekwa Nyasi au kujengwa kwa Udongo kuhakikisha wanaacha mara moja kutumia madarsa hayo na kujenga madarasa bora.

Waziri Jafo ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya nne ya Uongozi wa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi yanayotolewa kupitia ofisi ya Rais Tamisemi kwa kushirikiana na Taasisi ya Uongozi yenye lengo la kujenga uwezo wa viongozi kuweza kutawala kwa ufanisi.

“Viongozi wangu nataka Mkakusanye mapato ya ndani kwa nguvu zote na Fedha hizo mzitumie kwenye miradi ya maendeleo na kwa wale ambao mpaka leo wanafunzi wanasomea kwenye mazingira duni hawana madarasa bora watoto wanasomea kwenye madarsa ya Tembe, mengine yameezekwa kwa Nyasi nahitaji muelekeze Nguvu katika ujenzi wa madarasa bora na hayo ya Tembe yotoweke kabisa; Mjenge madarasa ambayo wanafunzi watajiskia fahari kusoma”Alisema Waziri Jafo.

Waziri Jafo hakusita kuwakumbusha Viongozi  kuhusu Usimamizi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Afya 212 vinavyoendelea kujengwa hivi sasa katika ameneo yote yote Nchini.

Niwapongeze baadhi ya Wakurugenzi ambao mpaka sasa wamefanya kazi nzuri sana ya Usimamizi wa ujenzi wa Miundombinu hiyo ya Afya wameshakamilisha ujenzi na wamejenga mpaka Njia za kutembelea(Walk Way) katika vituo hivyo na nataka mpaka Tarehe 30 April 2018 Kila Halmashauri iliyopokea Fedha za ujenzi wa Miundombinu ya Afya iwe imekamilika.

Waziri Jafo alitumia nafasi hiyo pia kuwakumbusha viongozi mara wapatapo mafunzo haya kuheshimu  mipaka yao ya kazi, kuboresha mahusiano kazini, kutunza Siri za Serikali na kusimamia Maadili katika maeneo ya kazi.

Awali akizungumza katika Ufunguzi wa  Mafunzo ya Uongozi Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Prof. Joseph Semboja amesema kuwa mafunzo haya yanakamilisha mtiririko wa mafunzo yaliyofunguliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania Mhe. Majaliwa K. Majaliwa miezi nane iliyopita na baada ya mafunzo haya yanayoanza leo tutakuwa tumewafikia   Viongozi 324.

Prof.Semboja aliongeza kuwa Lengo la mafunzo haya ni yale yale ambayo ambayo yamelengwa tangu Kikao cha Mwanzo cha Mafunzo haya ambayo ni kuimarisha uwezo wa kufanya maamuzi wa Kimkakati  kwa kuzingatia mahitaji ya jamii kwa manufaa mapana ya sasa nay a baade ya Jamii Tunayoihudumia.

Sambamba na hilo Mkutano huu pia unalenga kuongeza uwezo wa Viongozi wetu katika kuongoza watu na rasillimali zingine zilizoko kwenye maeneo yetu ili kwa pamoja tuweze kufikia malengo ya pamoja.

Alisisitiza kuwa Mafunzo haya yatajielekeza katika Kuimarisha Sifa Binafsi za Viongozi  kwa sababu Viongozi ndio wanaowasimamia wananchi katika kiLA Eneo hivyo ni lazima kila kiongozi aweze kujitenegenezea Sifa binafsi ili akubalike na kuhesimika katika Jamii husika.

“Sifa hizi binafsi tunazozizungumzia ni Ushawishi, Kuaminika, Uadilifu, Mtenda Haki, Muumini wa Utawala bora na Utawala wa Sheria na zaidi kuwa mchahapa kazi na awe na weledi wa hali ya juu sasa haya yote yatafundishwa kupitia mafunzo haya ya namna gani Kiongozi anaweza Kujijengea Sifa Binafsi katika Jamii tunazoziongoza.

Akitoa Neno la Shukrani kwa niaba ya viongozi walioshiriki katika Mafunzo haya Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mhe. Joseph Mkirikiti ameshukuru OR-TAMISEMI na Taasisi ya Uongozi kwa kuandaa mafunzo haya na zaidi ameahidi Umakini wa washiriki kwa siku zote za mafunzo.

Mafunzo haya ya awamu ya Nne na ya mwisho kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa imegususa Viongozi kutoka katika Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Tanga, Kilimanjaro na Arusha.

Kutana na Mtaalam wa Kutafsri Ndoto Yoyote...Anasafisha Nyota na Kutoa Mikosi

0
0
SHEIKH SHARIF OMARY
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
SHEIKH SHARIF ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)
 
SHEIKH SHARIF ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)
Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
 
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
 
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
 
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone SHEIKH SHARIF Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
SHEIKH SHARIF Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
 
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.
 
ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
 
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..
 
Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..
Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
 
Mawasiliano ..+255 743 203 171

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya January 31


Serikali Yasisitiza Uwazi Shughuli Za Madini

0
0
Kampuni za Madini nchini zimetakiwa kufanya shughuli zake kwa uwazi sambamba na kufuata Sheria za nchi ili kuepuka migongano.

Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam Januari 29, 2018 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila kwenye mkutano na Balozi wa Canada nchini, Ian Myles aliyeambatana na Mshauri masuala ya Uwajibikaji kwa Jamii kwenye Tasnia ya Uziduaji kutoka Serikali ya Canada, Jeffrey Davidson.

Ujumbe huo ulimtembelea Katibu Mkuu Msanjila kwa lengo la kujadiliana masuala mbalimbali kwenye Sekta ya Madini ikiwemo suala la Sheria ya Madini, masuala ya uwajibikaji kwa jamii (CSR) yanayofanywa na kampuni mbalimbali zikiwemo za kutoka nchini Canada na matarajio ya Serikali kwa kampuni (wawekezaji).

Profesa Msanjila alisisitiza kuwa kampuni zinazofanya shughuli zake nchini zinalazimika kufuata taratibu na sheria za nchi ili kujijengea mazingira rafiki ya utekelezaji wa shughuli husika.

Alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha Sekta ya Madini inanufaisha Taifa kwa ujumla sambamba na wawekezaji na alibainisha kwamba lengo hilo litafikiwa ikiwa kampuni husika zitatekeleza wajibu wake kwa uwazi kulingana na matakwa ya sheria.

“Kampuni zinazojihusisha na shuguli za madini zinapaswa kufanya shughuli zake kwa usahihi na uwazi,” alisisitiza Profesa Msanjila.

Aidha, Profesa Msanjila alisisitiza kuwa kampuni zinazojihusisha na shughuli za madini nchini, zinapaswa kupata taarifa sahihi kutoka kwa Wataalam waliopo Serikalini ili kupata mwelekeo sahihi wa dhamira ya Serikali.

“Kampuni zinatakiwa kupata taarifa sahihi kutoka kwa vyanzo sahihi ili kufanya shughuli zake kwa usahihi,” alisisitiza Profesa Msanjila.

Profesa Msanjila vilevile alizungumzia dhamira ya Serikali ya kuhakikisha madini yanayochimbwa nchini yanaongezwa thamani kabla hayajasafirishwa nje ili kukuza uchumi wa Taifa.

“Madini yakiongezwa thamani hapa nchini, faida ni nyingi ikiwemo ajira na pia mapato yataongezeka kwani tutakuwa tumeelewa thamani halisi ya madini husika, kabla hayajasafirishwa,” alisema.

Ili kufikia dhamira hiyo, Profesa Msanjila alisema Serikali ipo kwenye mazungumzo na kampuni zilizoonyesha nia ya kujenga viwanda vya kuyeyusha na kusafisha madini (smelting and refining).

Mbali na hilo, Profesa Msanjila alizungumzia suala la uwezeshaji wachimbaji wadogo wa madini ambapo alisema Serikali imedhamiria kuhakikisha kwamba wananufaika ipasavyo na shughuli zao sambamba na mchango wao kwenye pato la Taifa kuonekana.

Alielezea jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika kuwawezesha wachimbaji wadogo ikiwemo uanzishaji wa vituo vya mafunzo vya mfano (centre of excellence) ambavyo alivitaja baadhi yake kuwa ni Kituo cha Tanga, Geita na Mtwara.

Kwa upande wake Balozi Myles alisema ni muhimu Serikali, Wawekezaji na Jamii kwa ujumla kushirikiana na pia kuwa na lengo la wazi la namna ya kunufaika kutokana na Sekta ya Madini.

Naye Davidson aliahidi kuzungumza na kampuni za Canada kuelezea matarajio ya Serikali kwao kwa namna mbalimbali ikiwemo suala la sheria, uwajibikaji kwa jamii, mazingira na michango mbalimbali ya kampuni kwa maendeleo ya jamii.

“Nitawakumbusha kwamba wanawajibika si kwa wanahisa wao peke yake bali pia kwa jamii wanapofanyia shughuli zao,” alisema Davidson.

Mkutano wa Katibu Mkuu wa Madini na Balozi wa Canada nchini ulihudhuriwa na watendaji mbalimbali kutoka Wizara ya Madini akiwemo Kamishna wa Madini ambaye pia ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Kamisheni ya Madini, Profesa Shukrani Manya.

Wanne wafariki kwa kufukiwa na kifusi Arusha

0
0
 Wachimbaji wanne wamefariki na  mmoja yupo mahututi baada ya kuangukiwa na Ngema  walipokuwa wakipakiza  changarawe kwenye gari katika machimbo ya changarawe yaliyopo katika mlima Murieti katika jiji la Arusha.

Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha jana Januari 30 kuhusu  kutokea tukio hilo  mchana, katika eneo ambalo ni machimbo ya muda mrefu ya changarawe.

Miili ya watu watatu tayari imetambulika ambao ni Yusuph Mohamed Kamwende(35) Athuman Hussein  umri wake haujatambulika na Richard Kishimbo(57).

"Bado  mwili wa marehemu mmoja haijafahamika na tunaomba watu kufika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya mkoa Mount Meru kutambua ndugu zao" alisema  Kamanda.

Hata hivyo, alitoa  wito kwa maafisa madini kwenda mara kwa mara kwenye maeneo ya machimbo ili kutazama usalama wa maeneo hayo ili kuondoa majanga.

"Pale inaonekana ngema moja ilikuwa imelegea sasa wao wakiwa wanachimba changarawe ndipo iliwadondokea na kuwafukia" alisema

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, John Lemanya amesema  wakati watu hao wakichimba, ilisikika mlio wa kuanguka  ngema na waliona wakiangukiwa.

"Wao walikuwa wameingia chini ya ngema na kuanza kukata miamba na ndipo mtikisiko ulitokea na kufanya kumeguka kwa ngema na kuwaangukia"Amesema

Hata hivyo hili ni tukio la pili ndani ya miaka mitatu kutokea ambapo mwaka juzi pia machimbo hayo yalifungwa baada ya kusababisha vifo kutokana na wachimbaji kuangukiwa na ngema.

Rais Magufuli Kuzindua Pasipoti ya Kielektroniki

0
0
Jonas Kamaleki- MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. John Pombe Magufuli leo  atazindua Pasipoti Mpya ya Tanzania ya kielektroniki jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi huo utafanyika Jumatano, Januari 31, 2018 kuanzia saa moja na nusu asubuhi, Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini Dar es salaam.

Hayo yalisemwa na Mrakibu wa Uhamiaji ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Ali Mtanda katika mahojiano maalum na Idara ya Habari (MAELEZO).

Mtanda alisema kuwa Pasipoti Mpya ya Tanzania ya kielektroniki ni sehemu ya Mfumo wa Uhamiaji Mtandao ambao utakuwa na visa, vibali mbali mbali na manejimenti mipakani.

Kwa kuwa teknolojia inazidi kukua, Tanzania haiwezi kubaki nyuma ndiyo maana imeamua kuingia katika masuala ya digiti.

Uzinduzi huu utahudhuriwa pia na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein.

Marais wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, waheshimiwa, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin William Mkapa na Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wengine wa Serikali wanatarajiwa kuhudhuria uzinduzi huo kwa mujibu wa Mtanda.

Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati katika kutoa huduma zake kwa wananchi kwa njia ya mtandao. Ikumbukwe kuwa usajili wa makampuni chini ya Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) wamezindua usajili wa makampuni kwa njia ya mtandao, miamala ya pesa inafanyika kwa kiwango kikubwa kwa njia ya mtandao na kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi ikiwepo kulipa kodi mbali mbali.

Familia Yahofia Tundu Lissu Kufukuzwa Hospitali

0
0
Familia ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), imelitaka Bunge kutoa fedha za matibabu yake kama halitaki mtunga sheria wake huyo akafukuzwe hospitalini alikolazwa.

Lissu amelazwa katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Luvein nchini Ubelgiji tangu mapema mwezi huu baada ya kutibiwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya kwa miezi minne.

Msemaji wa familia ya Lissu, wakili Alute Mughwai, aliwaeleza waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa miezi ni mitano sasa Lissu hajapata stahiki zake kimatibabu kama Mbunge.

“Tumemaliza miezi mitano tangu kutokea kwa tukio la kushambuliwa kwa Lissu na Bunge kama taasisi limeshindwa kutoa fedha za matibabu kwa mwenzao," alisema Mughwai.

“Sasa Lissu atalaumiwaje? Akilia Mungu wangu mbona umeniacha, Bunge langu mbona limeniacha... au wanataka afukuzwe hapo hospitalini kwa kukosa fedha za matibabu?

“Mpaka sasa hatujui kinachoendelea. Tunaweza kusema ni siasa au kwa namna nyingine tunaweza kutafsiri kuwa sababu Lissu ni mkosoaji mzuri wa serikali bungeni.

“Waheshimiwa hawa wanataka mwenzao kuwa kilema au kupoteza maisha? Cha msingi wanapaswa kutoa haki za msingi ambazo sisi tumeona zinacheleweshwa kwa makusudi.”

Bunge lilishasema hata hivyo kwamba Lissu alifuata matibabu nje ya nchi kinyume na utaratibu wa bima ya afya ya wabunge, hivyo kuwa kikwazo cha kuhudumiwa kwake.

Lissu (49) alipigwa risasi tano na watu wasiojulikana akiwa kwenye gari nyumbani kwake Area D mjini Dodoma Septemba 7, mwaka jana. Jumla ya risasi 32 zilirushwa na watu hao kwa mujibu wa taarifa za Bunge.

Akizungumzia mawasiliano ya familia na ofisi ya Bunge, alisema Desemba 15, mwaka jana, alitoa mrejesho kwa vyombo vya habari kuhusu barua waliyoandikiwa na Katibu wa Bunge ikiwataka familia hiyo kutoa ufafanuzi wa haki zipi ambazo Lissu anatakiwa kupewa na Bunge.

Alisema waliandika barua ya kuomba ufafanuzi huo, Desemba 13, mwaka jana, na barua hiyo ilipokelewa na Ofisi ya Bunge Desemba 18, mwaka jana na ilipokelewa kwa njia ya barua za haraka ya DHL.

“Tulichoomba ufafanuzi ni kuhusu fedha za matibabu, stahiki za usafiri wa kwenda nje ya nchi pamoja na posho ya kujikimu kwa yule anayemuangalia hospitalini," alisema.

“Bunge ilitoa majibu Desemba 10, mwaka jana, kupitia kwa Katibu wa Bunge ambapo alidai kuwa barua hiyo iliwaelekeza kurudia utaratibu wa kufuata utaratibu ambao bunge linatumia kwa ajili ya matibabu ya wabunge pindi wabunge wanapokwenda kupewa matibabu,” alisema.

Aidha alisema baada ya kurudia kufanya marekebisho ya barua hiyo, Katibu wa Bunge aliwajibu Januari 10, mwaka huu, kuwa Wizara ya Afya imeunda timu ya madaktari bingwa kwenda Nairobi kumuangalia Lissu wakati wakitambua kuwa mbunge huyo Januari 6, mwaka huu, alishasafirishwa kwenda nje ya Afrika kwa ajili ya matibabu.

Akizungumzia afya ya Lissu, Mughwai alisema kwa sasa anaendelea vizuri na mazoezi ya viungo, ili kuimarisha afya yake.

Alisema aliwasiliana na Lissu Jumapili ambapo alimweleza anaendelea vizuri na mazoezi akiwa anafanya mara tatu kwa siku.

Alisema mazoezi anayofanyishwa kwa sasa ni kupanda ngazi sita na kuvuta vitu vizito.

Aidha alidai kwa mguu ambao ulipata majeraha makubwa unaweza kustahimili kusukuma kitu chenye uzito kwa kilo 25 na kwamba mazoezi yataendelea hadi hapo atakapo kuwa vyema kiafya.

Raila Odinga hatarini kushtakiwa kwa uhaini

0
0
MAMLAKA za Kenya, jana zilizima vituo vya televisheni kuzuia matangazo 'live' ya sherehe za kuapishwa kwa kiongozi wa upinzani, Raila Odinga, ambaye alisusia uchaguzi wa marudio wa mwaka jana uliobishaniwa.

Alijitangaza kuwa "rais wa watu" mbele ya maelfu ya wafuasi wake katika mji mkuu wa Nairobi.

Matokeo ya uchaguzi mkuu wa Agosti, mwaka jana, yalibatilishwa kutokana na  madai ya ukiukwaji wa kanuni.

Uhuru Kenyatta alishinda uchaguzi wa marudio Oktoba, lakini Odinga hakushiriki, hivyo Kenyatta aliapishwa kuongoza muhula wa pili Novemba, mwaka jana.

Alivionya vyombo vya habari kutotangaza shughuli ya jana na mwanasheria wa serikali alisema kufanya hafla hiyo ni kosa la uhaini.

Hata hivyo, vituo vikuu vya TV vilionyesha tukio hilo kupitia mitandao yake ya kompyuta, kwenye YouTube na Facebook.

Akiwa ameshika Biblia mkono wake wa kulia katika bustani ya jijini Nairobi, Odinga alitangaza kuwa anajibu "wito wa ngazi ya juu kuchukua ofisi ya rais wa watu wa Jamhuri ya Kenya."

Watu wamechoshwa na wizi wa kura katika uchaguzi na tukio hilo lilikuwa hatua kuelekea ujenzi wa demokrasia sahihi katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki, Odinga aliuambia umati uliokuwa ukishangilia.

Aliyekuwa mgombea mwenza wake, Kalonzo Musyoka, hakuwapo kwenye hafla hiyo. Odinga alisema ataapishwa siku nyingine.

Akizungumza awali na televisheni ya Kenya ya KTN, Odinga alisema kufungwa kwa vyombo vya habari "kumethibitisha kuwa tumeporomoka kufikia kiwango cha Uganda", ambayo ilisimamisha matangazo ya vyombo vya habari wakati wa uchaguzi mwaka 2016.

"Kuapishwa kwake" kulikuwa na lengo la "kuonyesha dunia kuwa tunachofanya ni halali kisheria, kikatiba na kitu ambacho huwezi kukielezea hata kidogo kuwa mapinduzi", alisema zaidi.

Vituo vitatu binafsi vya televisheni - NTV, KTN na Citizen TV - vilizima matangazo kuanzia saa 3:10 asubuhi.

Citizen TV iliiambia BBC kuwa mamlaka za serikali ziliwalazimisha kuzima matangazo kutokana na mipango ya kuonyesha mkusanyiko huo.

Watazamaji wa KTN walishuhudia vioo vya luninga zao vikishika rangi nyeusi wakati mtangazaji akisoma taarifa kutihibitisha kuwa mamlaka ya mawasiliano ilikuwa ikizima matangazo.

Kuzimwa kwa 'signo' ya matangazo ya vyombo vya habari si jambo la kawaida hapa Kenya.

Palikuwa na wasiwasi jana huku baadhi ya shule katika mji mkuu wa Kenya zikifungwa kwa sababu ya tukio hilo, na watu kutojua nini kingetokea.

Polisi awali walizingira viwanja hivyo, lakini baadaye wakaondoka.

Chanzo: BBC
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images