Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Trump amjibu Jay Z kuhusu Afrika na ‘Wamarekani Weusi’

$
0
0
Rais wa Marekani, Donald Trump amemjibu rapa Jay Z kwa kile alichokisema kwenye mahojiano na CNN kuhusu matamshi ya kibaguzi yanayodaiwa kutolewa na kiongozi huyo.

Akizungumza katika mahojiano maalum kwenye kipindi cha The Van Jones Show wiki hii, rapa huyo nguli ambaye jina lake halisi ni Shawn Carter alikosoa vikali matamshi yanayodaiwa kuwa ya Trump akiizita nchi za afrika kuwa ni nchi chafu (nchi za shimo la choo).

“Ndiyo, inaumiza sana na inatuangusha. Kila mtu alisikia hasira. Baada ya hasira inaumiza kweli kama mtu anawadharau watu wote,” alisema na kuongeza kuwa ingawa amekanusha matamshi hayo, hivyo ndivyo watu humzungumzia.

Rapa huyo alienda mbali akimkosoa Trump kwa vitendo vya kibaguzi na kumuita kuwa ni mdudu aliyeshindikana kwa dawa (superbug).

Alipinga kauli kuwa Marekani sasa imeongeza idadi ya ajira hasa kwa nchi za Afrika kama inavyodaiwa na Serikali ya Trump.

Leo, Trump ametumia mtandao wa Twitter kama ilivyo kawaida yake na kumjibu Jay-Z akimtaja jina, akisisitiza kuwa tangu aingie madarakani idadi ya Wamarekani Weusi wasio na ajira imeshuka.

“Mtu mmoja amtaarifu Jay –Z tafadhali kwamba kwa sababu ya sera zangu, idadi ya watu weusi wasio na ajira wameripotiwa kuwa katika KIWANGO CHA CHINI KUWAHI KUTOKEA,” inasomeka tweet ya Trump.

Simba Mwendo Wa 4G.....,Okwi Mbili,Bocco Mbili

$
0
0
Timu ya Simba imezidi kujichimbia kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kupata ushindi wa magoli 4-0 dhidi ya Majimaji kutoka Songea mkoani Ruvuma Mchezo uliopigwa katika uwanja wa Taifa na kuhitimisha Mzunguko wa Kwanza.

Simba walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa John Bocco dakika ya 17 akimalizia mpira uliorudi baada ya kugonga mwamba kufuatia beki Mghana, Asante Kwasi kupiga tik tak kuunganisha kona ya winga Shiza Ramadhani Kichuya.

Bocco aliye katika msimu wake wa kwanza Msimbazi tangu asajiliwe kutoka Azam FC , aliwainua vitini wapenzi wa Simba kwa kufunga bao la pili dakika ya 26 kwa kichwa akimalizia ‘majaro’ ya kiungo Said Hamisi Ndemla.

Hadi timu zinakwenda mapumziko Simba walikuwa mbele kwa magoli hayo mawili dhidi ya Majimaji kipindi cha pili kilianza kwa mabenchi yote ya ufundi kufanya mabadiliko hata hivyo yaliwanufaisha wenyeji zaidi.

Mnamo dakika ya 52 na 68 Simba walipata magoli hayo mawili kupitia kwa Mshambuliaji hatari Raia wa Uganda Emanuel Okwi na kuendelea kukalia usukani wa wafungaji akiwa na jumla ya magoli 12.

Kwa Matokeo hayo Simba wamefikisha Jumla ya pointi 35 huku wakifuatiwa na Azama 30 na mahasimu wao wakubwa wa jadi Yanga wakiwa kwenye nafasi ya tatu kwa pointi 28 na Mchezo mwingine ulipigwa katika dimba la Namfua ambapo wenyeji Singida United wamefanikiwa kupata pointi tatu baada ya kuwafunga Tanzania Prinsons goli 1-0.

UVCCM Wakamata Gari la Meya wa Jiji Likiwa na Dereva......CHADEMA Wadai Alitekwa

$
0
0
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Kinondoni, Lilian Rwebangira amesema wamelikamata gari la meya wa jiji wa Dar es Salaam kwenye ofisi za CCM Wilaya ya Kinondoni likiwa na vijana wawili waliovaa sare za chama hicho tawala.

Rwebangira alidai kwamba kuonekana kwa gari hilo ni njama za Chadema kutaka kuvuruga uchaguzi wa Februari 17 na kwamba tayari wamefikisha suala hilo katika Kituo cha Polisi Magomeni ambako dereva wake anashikiliwa pamoja na gari hilo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Jumanne Murilo alithibitisha kukamatwa kwa gari hilo na kusema, “Gari lilikuwa linachunguzwa tangu jana, sasa muda mrefu umepita, sijui wamefikia wapi katika uchunguzi huo.”

Hata hivyo, uongozi wa Chadema umekanusha kula njama dhidi ya CCM na kusema kwamba hiyo ni mbinu za chama hicho tawala kutaka kuvuruga uchaguzi.

Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita hakupatikana mara moja kuzungumzia tukio hilo lakini Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Patrick Ole Sosopi alisema kwamba jana usiku baada ya kikao cha tathmini Mwita alilalamika kwamba dereva wake haonekani.

Ole Sosopi alidai kwamba CCM wanataka kutengeneza mazingira ya kuvuruga uchaguzi huo kwa kisingizio kwamba Chadema ndiyo wameanzisha.

“Inawezekanaje dereva wa Chadema akaenda CCM! Kufanya nini? Wanajaribu ku pre-empty ili zikitokea fujo waseme ni sisi. Ninaomba jeshi la polisi wachukue hatua, kwa sababu hali hii haikubaliki,” alisema Sosopi.

Alidai kwamba dereva huyo alitekwa na watu wa CCM kuanzia saa tisa alasiri na akaachiwa saa kumi na moja alfajiri baada ya kumtesa.

Akizungumzia tukio hilo jana, mwenyekiti huyo wa UVCCM, alisema dereva huyo wa meya alikamatwa jana saa 2:30 usiku katika ofisi za CCM Kinondoni na alipoulizwa alitoa sababu tofautitofauti kwamba alikwenda kuegesha na sababu nyingine kuwa alimpeleka meya Mwita kwenye mkutano maeneo ya jirani.

“Tulipekua simu ya dereva na kubaini mawasiliano kati yake na meya wa jiji akimuuliza “Uko na nani hapo?”, “Mpango unakwendaje?”. Zote hizo ni njama za wenzetu kutaka kuvuruga uchaguzi, sasa tunaliomba jeshi la polisi lifanye kazi yake kwa haki,” alisema Rwebangira.

Alidai kwamba vijana wawili waliokuwa kwenye gari hilo walitoroka lakini walitambuliwa kwa jina moja moja la Godfrey na Alex na kwamba watalisaidia jeshi la polisi kuwapata kwa sababu wanafahamika kwa vurugu huko Kigamboni.

“Tumekuwa tukipokea taarifa kwamba ofisi ya meya inatumika vibaya. Hatuwezi kuacha mambo haya yakaendelea, lazima vyombo vyetu vya dola vichukue hatua,” alisema mwenyekiti huyo. 

Tazama Hapa Msimamo Wa Ligi Kuu Vodacom Bara Mzunguko Wa Kwanza 2017-18

VIDEO: Diamond Na Wema Walivyowapagawisha Mashabiki Ndani Ya Maisha Basement

$
0
0
Suprise ya nguvu imefanyika usiku wa kuamkia leo pale Hyatt Regency Hotel baada ya Malkia wa Bongo Movies, Wema Seetu kumpandisha mkali wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz ukumbuni kwa ajili ya ufanya makamuzi.

Tukio hilo limetokea wakati wa hafla ya kumtambulisha msanii mpya wa Lebo ya WCB Wasafi, Mbosso ambaye amejiunga na lebo hiyo baada ya kundi lake la awali la Yamoto band kuvunjika.

Wakati sherehe ikiendelea, Rayvanny alikuwa akikamua, wakati akimalizia shoo alimuita Wema Sepetu ambaye aliibuka jukwaani kisha zikaanza kusikika kelele za mashabiki wakiimba …Wema…. Wema….Wema… ambaye baada tu ya kupanda na kuwasabahi mashabiki alimuita mpenzi wake wa zamani, Diamond Platinumz naye apande jukwaani.

Kelele ziliongezeka …Diamond… Diamond… Diamond…., haikuchukua muda Diamond akaibuka jukwaani na kukumbatiana na Wema kwa sekunde takribani 20 kabla ya kuanza kukamua.

Wakati Mond akikamua jukwaani na wasanii wengine wa WCB, Wema alikuwa akikata mauno jukwaani hapo jambo ambalo liliamsha msisimuko na shangwe miongoni mwa mwashabiki na kelele nyingi za kuwashangilia zikitawala.

Ikumbukwe kuwa Wema na Diamond waliwahi kuwa wapenzi miaka kadhaa iliyoita kabla ya kuachana na kila mtu kuingia kwenye mahusiano mengine.

Credit:GlobalPublisher

WCB wamtambulisha msanii mpya. Itazame video yake ya kwanza chini ya WCB

$
0
0
Lebo ya muziki ya WCB jana usiku ilitambulisha msanii mwingine ambaye kazi zake zitakuwa zikisimamiwa na lebo hiyo, ambapo mbali na kumtambulisha, msanii huyo aliachia ngoma yake ya kwanza akiwa chini ya WCB.

Msanii huyo ni Mbosso ambapo awali alikuwa mmoja kati ya wasanii wanne waliokuwa wakiunda kundi la Ya Moto Band ambalo limesambaratika.

Kabla ya kujiunga na WCB, Mbosso alikuwa akitumia jina la Marombosso.

Hapa chini ni video yake mpya aliyoiachia jana mara baada ya kutambulishwa.

Ijue Afya Yako: Pata Tiba Asili ya Busha, Maumbile Madogo na Nguvu za Kiume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaayhiri watu  wengi sana baada ya kujiona wako tofauti na watu wengine .Kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na maumbile  nchi-6-7 .Matatizo haya yanasababishwa na punyeto) kisukari) presha) naulevi wakupita kiasi pia na msogo wa mawazo, homoni za toka kuzaliwa 

MOMLA ni dawa inayotibu kinacho sababisha tatizo,kama vile sukari, presha, magonjwa ya zinaa, misuli kulegea na kusinyaa kwa kwasababu ya kujichuwa au punyeto na akili kudumaa kwaajili ya tendo bila kushiriki 

MBEPE nikwa wenye maumbile mafupi na membamba kwa matatizo hayo ni dozi ya siku 5 unapona kabisa 

DAGULA hii nikwaajili ya wenye busha iwe ya maji au ya utumbo kushuka inatibu bila opresheni , kuuga mifupa kwwaliopata ajari yoyote inayo sababisha uvujifu wa mifupa inatibu kwa mda wa siku 14 tayali kwa mazoizi 

LUKOMOLO ni dawa ya mvuto wa mpenzi biaashara ata kama mme mke mchumba atakutafuta mwenyewe na kutekeleza yote unayotaka mfanye akutafute mwenyewe pia tunatibu kiuno miguu aina yote tumbo la uzazi kwa kina mama na kina baba nk 

KWA WAKAZI WA DSM TUNAPATIKANA MBANGALA RANGI TATU MKABALA NA KISUMA BAA. 

KWAMIKOA YOTE MTAPATA HUDUMA HILI KWA MAWASILIANO PIGA 0767131395, 0712757594, 0787131395 MUONE DR MWANGARA

Chanzo cha Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume na Tiba Yake

$
0
0

Tendo la ndoa limengawanyika katika makundi matatu baadhi yake makudi hayo niuhanisi, kufanya tendo la ndoa maramoja na kushidwa kurudia tena 

sababu zinazo pelekea ni ugonjwa wa kisukari, kujichuwa, maumivu ya mgongo na kiuno, tumbo kuuguruma na kujaa gesi, msogo wa mawazo, presha, kutokuwa nyama sehemu ya haja kubwa yani mgoro, ulevu wa kupidukia, kuadhilika na madawa ya kulevya 

ARRBERA 1 Ni dawa ya asili ambayo imefanyiwa tafiti kwa hali ya juu isiyo na kemikali yoyote kwa mtumiaji ambayo humfanya mtumiaji kufanya tendo la ndoa maratatu bila kuchoka 

Pia ARRBERA 2 ni dawa asili abayo huimalisha ukuaji wa umbile la kiume lililo sinyaa na kunenepesha saizi upedayo. sihayo tu upade wa wamatatizo kisukari yakushuka na kupada kuna dawa ya kutumia siku saba na kufanya sukari ibaki nomo balasi abayo ni 4-5-6 vilevile kwaupade wa kina mama matatizo ya uzazi na hedhi kuvurugika na kutokwa maji maji sehemu za sili fagasi na kifafa cha mimba kwa kina mama waja wazito na kifafa cha kawaida 

FIKA OFISINI KWETU MBANGALA RAGI TATU ASIYE KUWA NA NAFASI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO KWA KWA KAZI WA DSM muone dr kabero simu 0758078280 au 0713 293 988 wote mnakalibishwa
No automatic alt text available.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Waziri Jafo ashangazwa siri za Serikali kuwekwa WhatsApp

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo amewaagiza wakuu wa wilaya na wakurugenzi watendaji wa halmashauri (DED) kutunza siri za Serikali.

Jafo ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Januari 29,2018 mjini Dodoma alipofungua mafunzo ya uongozi kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa mikoa sita.

Mafunzo hayo ni mwendelezo wa ambayo yanatolewa kwa viongozi wa kada hiyo.

Waziri Jafo amesema ujenzi wa Serikali utakuwa mzuri iwapo viongozi hao watakuwa makini na kutunza siri.

"Hivi unakuwaje wewe mkurugenzi au mkuu wa wilaya unapeleka siri za Serikali kwenye mitandao ya kijamii na nyingi unaziona kwenye WhatsApp, inatia aibu sana," amesema Jafo.

Amewataka wakurugenzi kujipambanua na kusimamia miradi ya maendeleo katika kukusanya mapato na kuyatumia vyema na hasa ya ndani.

Jafo amesema tatizo kubwa kwa wakurugenzi ni kutofanya uamuzi kwa haraka.

Mtulia : Nilifanya Maamuzi Ya Kiume Kuhama CUF....Hivi Sasa Hadi Namba ya Rais Ninayo

$
0
0
Mgombea wa Jimbo la Kinondoni kupitia CCM, Maulid Said Mtulia amesema amefanya maamuzi ya kiume ya yeye kuhamia chama hicho kwa sasa kwa maana wapo wengi wanataka kufanya hivyo lakini wameshindwa kwa madai wanasubiri kulipwa kiiunua mgongo.

Mtulia ameeleza hayo wakati alipokuwa anaendelea kujinadi kwa wananchi wa jimbo la Kinondoni ambalo hapo awali alikuwa analishikilia yeye kupitia chama chake cha CUF kabla ya kujivua uanachama wake na kuenda kumuunga mkono Rais Magufuli katika jitihada zake za kuijenga nchi.

"Kujiuzulu Ubunge sio mchezo, nimefanya maamuzi ya kiume maana kuna wenzangu wengine mpaka sasa hawawezi kutoka kwa sababu wanasubiri kiiunua mgongo. Sasa kijana kama mimi nikae pale nisubirie kiunua mgongo hivi kweli ntaweza kuishi kwa kusubiri kiiunua mgongo", alisema Mtulia.

Aidha, Mtulia amesema amejinusuru kwa mengi kukihama chama chake cha awali ili aweze kuwapigania wananchi wa jimbo hilo kwa maana hapo awali alikuwa anashindwa kuyafanya majukumu yake vizuri kutokana na mgawanyiko ndani ya chama chao.

"Wenzangu Wabunge 10 walifukuzwa uanachama CUF hamkujua, mlisubiri nifukuzwe au mna roho mbaya na mimi. Hivi nilipo hapa nimeruka kwa kujinusuru nashukuru nipo salama na nimesimama tena kwa wana kinondoni ninaomba kugombea Ubunge nyie mnanuna kitu gani au huo ndio usaliti. Lakini jambo jingine mimi nimekuja CCM kwa sababu nampenda Magufuli balaah", aliuliza Mtulia.

Pamoja na hayo, Mtulia aliwashangaza baadhi ya watu kwa kusema ametumikia Ubunge ndani ya miaka miwili na kushiriki vikao vyote vya Bunge lakini hakuweza kuwa na namba ya Rais Magufuli.

"Leo ninawaambia siri yangu, nilivyokuwa Mbunge miaka miwili namba ya Rais Magufuli sikuwa nayo lakini sasa namba ninayo. Hivyo wanakinondoni mnataka nini kama mnataka maendeleo ndio haya", alisisitiza Mtulia.

Kwa upande mwingine, Mtulia amewaambia wananchi wa Jimbo la Kinondoni endapo watamchagua yeye katika chaguzi hizo za marudio zilizopangwa kufanyika mapema Februari 17 mwaka 2018 basi watakuwa wametengeneza daraja la kujipatia maendeleo.

Sumaye Ampa Makavu Mtulia.....Awataka Wananchi Wampuuze

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu , Frederick Sumaye amefunguka na kusema kuwa kazi ya Mbunge ni kutetea wananchi wa jimbo lake na si kwenda kumsifia Rais na kudai wabunge waliojizulu nafasi zao kwa kigezo cha kumuunga mkono Rais hawakutambua majukumu yao.

Sumaye amesema hayo kwenye kampeni za Ubunge wa marudio katika jimbo la Kinondoni zinazoendelea na kusema kuwa kwa Wabunge ambao wamejiuzulu nafasi zao na kwenda chama kingine kugombea tena hawafai kabisa kuwa wabunge kwa kuwa hawatambui maana ya Ubunge.

"Kazi ya Mbunge si kwenda kumtetea Rais bali ni kutetea wananchi waliompa kura, kama Mtulia yeye anasema ameondoka na kudharau kura za watu wa Kinondoni kwa sababu amependezeshwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania basi akateuliwe na Rais kuwa Mbunge maana kazi yake ndiyo itakuwa kwenda kumtetea na kumsifia Rais. 

"Watu ambao wanahama chama eti kwa sababu Rais ametenda mambo mema pamoja na ukweli kwamba mimi naweza kubishana sana maana hatujaona hayo mambo wewe kama umehama maana yake ulikuwa huelewi maana ya kuwa Mbunge" alisisitiza Sumaye

Mbali na hilo Sumaye alidai kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa sasa hakijali tena maslahi ya wananchi wake kwa kuwa kimeshika madaraka kwa muda mrefu ndiyo maana wameweza kumrudisha Mtulia kugombea kwenye jimbo la Kinondoni bila kujali mtu huyo amesababisha fedha za wananchi zaidi ya bilioni moja ziteketee kwenye uchaguzi wa marudio wakati fedha hizo zingeweza kutumika katika kufanya mambo ya maendeleo kwa wananchi.

Necta yatangaza tarehe ya mtihani kidato cha sita

$
0
0
Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) limesema mitihani ya kuhitimu kidato cha sita itaanza Mei 7 hadi 24, 2018.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Necta Januari 26, 2018 inaonyesha somo la kwanza litakuwa ni masomo ya jumla ‘General Studies’ na somo la mwisho litakalofanyika Mei 24 litakuwa ni Baiolojia 3C (kwa vitendo).

Msemaji wa Necta, John Nchimbi amesema “lengo la kutoa ratiba ni kuwafanya wanafunzi na walimu wao kujiandaa kwa ajili ya mitihani yao.”

“Ratiba inawasaidia wao kuweza kufanya maandalizi lakini kuwaweka sawa kisaikolojia  na kujua mitihani ipo, itakuwa lini hadi lini na muda gani,” ameongeza

Dawa Bora Ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE YA UMME MDOGO "Arrabela" FIKA NJOMBE MJINI, TUPO MTAA WA MPECHI KWA TABIBU MABULA HERBAL CLINIC.                                                    

 75%Ya Wanaume hukabiliwa na upungufu wa Nguvu za Kiume kwa sababu mbalimbali za matatizo ya Kiafya na Kibailojia hasa MTU ambaye anakuwa na Matatizo ya Ugonjwa wa KISUKARI, Zinaa, maumivu ya mgongo na kiuno, Tumbo kajaa gesi na kuunguruma, mshipa wa ngiri, Bawasiri au Mgoro, Au ugonjwa wowote unaochukua muda mrefu bila kupona hufanya kupungua kwa hormones za kichocheo kwa tendo la ndoa. 

Pia Matumizi ya dawa za kulevya ,Pombe,na utafunaji wa milungi.lakini wakati mwingine hutokana na sababu za Kimfumo wa kimwili na kuasilika kisaikolojia kwa kuwa na msongo wa Mawazo.

Lishe duni,upungufu wa protini mwilini na Madini.Kwa Huduma Bora za Matibabu ya KISUKARI, Nguvu za Kiume, maumbile ya umme MDOGO ,Matatizo ya kimaisha,muwasho sehemu za siri, Uzazi, Vidonda vya Tumbo,kikohozi kigumu,Magonjwa nyemelezi, mahusianona Tambazi

 FIKA KWENYE KITUO CHETU CHA TABIBU MABULA HERBAL CLINIC NJOMBE MJINI MTAA WA MPECHI

 KWA WALIOPO NJE NA MKOA WA NJOMBE HUDUMA YA DAWA ITAWAFIKIA KWA KUTUMIWA KWA MABASI ,SIMU 0768351097/0767488895 NYOTE MNAKARIBISHWA

BREAKING: Dk Wilbrod Slaa Akutana na Rais Magufuli leo Ikulu Jijini Dar

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Januari, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi Mteule Mhe. Dkt. Wilbrod Peter Slaa, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Baada ya Mazungumzo hayo Balozi Mteule Mhe. Dkt. Slaa amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumuamini na kumteua kuwa Balozi na ameahidi kuwa yupo tayari kutekeleza majukumu atakayopangiwa kwa kutanguliza maslahi ya Taifa.

Mhe. Dkt. Slaa amempongeza Mhe. Rais Magufuli na Serikali yake ya Awamu ya Tano kwa uongozi bora wenye maono na uthubutu wa kutekeleza mambo makubwa yenye maslahi kwa nchi ikiwemo miradi mikubwa kama vile ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge), ujenzi wa daraja la juu (Flyover) katika makutano ya barabara ya Nyerere na Mandela (Tazara), mradi wa uzalishaji umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stieglers’ Gorge) na mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi.

“Kwa kweli naona faraja, ninafurahi Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza hatua kwa hatua karibu yote tuliyokuwa tunayapigania kwa miaka takribani 20 ya huko nyuma, na mimi Dkt. Slaa nilikuwa napiga kelele kwa sababu nilikuwa naona kuna upungufu.

“Leo ninasema ninafurahi yale niliyokuwa napigia kelele yanatekelezwa kwa sababu nimeyaona, sasa kitu kikubwa ni macho, ushabiki katika maendeleo hauna tija, ushabiki katika siasa nao hauna tija, kama nilivyowahi kueleza huko nyuma siasa ni sayansi, wapo wanaofikiri siasa ni upotoshaji na siasa ni udanganyifu lakini siasa ni sayansi, na siasa kama ni sayansi ina misingi yake inayohitaji kusimamiwa, na misingi yake ni nini kilikuwa ni tatizo na tatizo hilo linatatuliwa kwa misingi ipi, sasa haya tunayoyasema ni hivi, tulikuwa na tatizo la umeme, Stieglers’ Gorge inaanza kujengwa, na miradi mingine mikubwa inatekelezwa, haya ndio mambo ya msingi” amesema Mhe. Dkt. Slaa.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amempongeza Mhe. Dkt. Slaa kwa moyo wake wa kizalendo na amesema aliamua kumteua kuwa Balozi kwa kuwa anatambua kuwa ataweza kupigania maslahi ya Tanzania popote atakapopangiwa kuiwakilisha.

“Dkt. Slaa alinijulisha kuwa anakuja na akaomba akija angependa kuja kuniona na nikampangia leo, tumezungumza mambo mengi na ameniahidi kuwa atakwenda kufanya kazi yake vizuri kwenye nchi atakayokwenda kuwa Balozi.

“Mhe. Dkt. Wilbrod Slaa ni mtu safi, anazungumza kutoka moyoni na anaipenda Tanzania na mimi kutokana na moyo wake wa kuchukia ufisadi na kuchukia wizi nikaamua kumteua kuwa Balozi” Amesema Mhe. Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameagana na maafisa wakuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambao wanastaafu baada ya kutimiza umri.

Walioagana na Mhe. Rais Magufuli ni Luteni Jenerali James Mwakibolwa aliyekuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ na Meja Jenerali Michael Isamuhyo aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

Wengine ni Brigedia Jenerali Aron Lukyaa, Brigedia Jenerali William Kivuyo, Brigedia Jenerali Elizaphani Marembo na Kanali Peter Samegi.

Akizungumza baada ya kuagana, Luteni Jenerali Mwakibolwa amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumteua kuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ na amesema anaondoka na kuliacha jeshi likiwa na nidhamu, utii, uzalendo na weledi.

Nae Meja Jenerali Isamuhyo pamoja na kumshukuru Mhe. Rais Magufuli  amesema anafurahi kuiacha JKT ikiwa imeimarika katika majukumu yake yakiwemo ujenzi wa viwanda, kilimo na kuimarisha mafunzo kwa vijana wazalendo.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
29 Januari, 2018

Zari amwambia Mama Diamond “Tuhame Guest House tumwachie mwanao”

$
0
0
Bado inaonekana swala la Diamond Platnumz kudaiwa kulala na wasichana wengine nyumbani kwake Madale, mama watoto wake Zari The Boss Lady hajaichukulia poa na inadaiwa kuwa amekasirishwa na tuhuma hizo zilizosambaa katika mitandao ya kijamii.

Diamond siku kadhaa zilizopita alidaiwa kupeleka msichana mwingine na kulala nae nyumbani kwake Madale, ila baada ya kuenea kwa video clip ikimuonesha msichana huyo akiwa Madale, Zari alionesha kukasirishwa na kuandika snapchat “Ati Madale State lodge au Madale Guest house?”
Baada ya siku kadhaa kupita baadhi ya mashabiki waliamini inawezekana swala hilo limepita ila comment ya Zari katika post ya instagram ya mama Diamond inaonesha amekasirika bado, hiyo ni baada ya ku-coment katika picha ya Mama Diamond aliyopost na kuandika “Kubwa la maadui” ikimuonesha Mama Diamond akiwa Madale lakini Zari akacomment “Fanya tuhame Guest House tumuachie mwanao”

Mnigeria akamatwa JNIA kwa kupatikana na cocaine

$
0
0
Polisi Kikosi cha Viwanja vya Ndege jijini Dar es Salaam linamshikilia raia wa Nigeria akituhumiwa kupatikana na dawa za kulevya aina ya Cocaine.

Christian Ugbechi (26), anadaiwa kukamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa kwa Julius Nyerere (JNIA) akiwa na pipi 59 zenye uzito wa zaidi gramu 800.

Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, Matanga Mbushi amesema leo Jumatatu Januari 29,2018 kuwa mtuhumiwa anaishi na kufanya kazi nchini Ufaransa.

Amesema alikuwa akisafirisha dawa hizo za kulevya kwenda nchini Ufaransa.

"Tumemkamata mtuhumiwa akiwa na pipi 59, kati ya hizo 56 alizificha kwenye soksi na tatu amezitoa leo kwa njia ya haja kubwa. Yupo chini ya uangalizi maalumu,” amesema Mbushi.

Basi la Tahmeed lawaka moto Tanga

$
0
0
Basi kampuni ya Tahmeed  lililokuwa likitoka jijini Dar es Salaam kwenda Mombasa, Kenya limeteketea kwa moto leo Januari 29, mwaka 2018  katika kijiji cha Kitumbi wilayani Handeni mkoani Tanga.

Mkuu wa Jeshi la Polisi wilayani Handeni, William Nyero amesema polisi wapo eneo la tukio na hakuna madhara yoyote kwa abiria waliokuwa kwenye basi hilo.

Amesema dereva wa basi hilo baada ya kubaini kasoro aliliegesha pembeni na abiria kuteremka, kushusha mizigo yao.

"Abiria wote waliokuwa wakisafiri na basi hilo wapo salama. Baada ya abiria kushuka na kushusha mizigo yao basi liliwaka moto,” amesema.

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari

$
0
0

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni 3Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

FINA Power Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR SHEIKH OMARY
Anapatikana dar magomeni moroco hotel
SIMU NO 0767 14 53 57/0629 03 45 50.

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images