Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Baada ya Polisi kumkamata ‘Nabii Tito’, Waziri Mwigulu Kayasema Haya

$
0
0
Leo Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limemkamata  Tito Machibya maarufu kama Nabii Tito, ambaye amekuwa akionekana mitaani kuhubiri huku akiwa anakunywa pombe na kuwabusu wanawake huku akiwashauri  watu kufanya mapenzi na wafanyakazi wao wa ndani 

Kupitia ukurasa wake wa instagram Waziri wa Mambo ya Ndani Dr. Mwigulu Nchemba amesema  mtu huyo amekamatwa  kwa tuhuma za udhalilishaji.

“Udhalilishaji wa aina yoyote ile haukubaliki(Kijinsia,Dini n.k)”- Ameandika waziri Mwigulu
A post shared by Dr. Mwigulu Lameck Nchemba (@mwigulunchemba) on

Jaji Mkuu awaonya viongoz wa serikali na wanasiasa

$
0
0
Jaji Mkuu wa Tananzania, Profesa Ibrahimu Juma amewataka viongozi wa serikali na vyama vya siasa kuacha mara moja vitendo vya kuingilia mhimili wa Mahakama na kuvunja amri zake.

Jaji Profesa Juma ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wiki ya Sheria inayotarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi ujao (Februari mosi), siku ambayo ndio itakayoashiria kuanza rasmi kwa shughuli za Mahakama kwa mwaka huu 2018 yatakayofanyika katika viwanja vya Mahakama vilivyopo mtaa wa Chimala jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi atakuwa Rais John Magufuli.

"Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania mamlaka ya utoaji haki ni ya Mahakama tu, nawasihi viongozi wote wa serikali wenye mamlaka za kikatiba na kisheria wabaki ndani ya maeneo yao ya Kikatiba na wajiepushe kuingilia maeneo yaliyo ndani ya haki, hadhi na Mamlaka ya Kikatiba ya Mahakama", alisema Jaji Profesa Juma.

Kwa upande mwingine, Jaji Profesa Juma ametoa rai kwa wananchi na wadau wote wa sheria kutembelea Mnazi Mmoja kwa ajili ya kujifunza na kupata huduma mbalimbali za Kisheria kutoka kwa Majaji, Mahakimu, Wasajili, Watendaji, Mawakili wa serikali na Mawakili wanaojitegemea ambao watakuwa tayari kuwasikiliza na kuwahudumia ipasavyo.

Mapingamizi yatupiliwa mbali Kinondoni....Mtulia na Mwalimu Rasmi Ulingoni

$
0
0
Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Kinondoni ambaye pia mkurugenzi wa manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli ameyatupilia mbali mapingamizi matatu yaliyowasilishwa na wagombea wa vyama vya Chadema, CCM na CUF.

Mapingamizi hayo ni kwa mgombea wa CUF, Rajab Juma kumwekea mgombea wa Chadema, Salumu Mwalimu, wakati Mwalimu yeye alimwekea Maulid Mtulia wa CCM na mgombea huyo wa chama tawala alimwekea mgombea wa SAU, Johnson Mwangosi.

Baada ya jana ofisi ya msimamizi wa uchaguzi kutoa barua ya utetezi kwa wagombea waliowekewa mapingamizi leo Jumanne imetoa majibu ya kuyatupilia mbali mapingamizi hayo.

“Tumeyatupilia mbali mapingamizi yao kwa sababu hayana mashiko, kilichobaki ni wagombea kwenda uwanjani wakapambane,” amesema msimamizi huyo.

Polisi Waeleza Sababu za Kumkamata Nabii Titto

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Dodoma, linamshikilia Onesmo Machibya maarufu Nabii Tito mwenye miaka 44 ambaye ni mkazi wa kijiji cha Ng’ong’ona Manispaa ya Dodoma, kwa kosa la kueneza chuki ya kidini dhidi ya watu wengine.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto, amesema Nabii Tito amekamatwa baada ya kurekodi vipande vifupi vya video na picha vyenye maudhui ya kukashifu dini nyingine, na kuleta chuki dhidi ya watu wengine na kurusha mitandao ya kijamii, kinyume na kifungu cha sheria namba 129 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 na marekebisho yake ya 2002.

Aidha, kamanda Muroto amesema mtuhumiwa huyo amesambaza vipeperushi mbalimbali katika maeneo ya starehe akitangaza imani ya kidini inayokiuka maadili ya nchi na kufanya hadharini vitendo visivyofaa, akitumia kitabu kitakatifu cha Biblia.

Nabii huyo amekamatwa akiwa na majoho (kanzu) yakiwa na misalaba miwili, vipeperushi 80, Biblia moja ambayo anatangazia imani inayokwenda kinyume na maadili mema ya taifa.

Nabii Tito kwenye mahubiri yake amekuwa akiwahamasisha watu kutumia vilevi, kufanya maasi, kuoa wanwake zaidi ya mmoja akiwemo msaidizi wa kazi, kitendo ambacho ni kinyume naa maagizo ya kitabu hicho kitakatifu na imani anayoihubiri.

Walichokibaini Polisi baada ya kumhoji ‘Nabii’ Tito

$
0
0
JESHI la Polisi mkoani Dodoma,  baada ya kumkamata na kumfanyia mahojiano Onesmo Machija (44) anayejiita ‘nabii’ Tito, kutokana na mahubiri ya kidini anayoyafanya, limesema mtu huyo ana  matatizo ya akili.

Akizungumza na wanahabari mjini Dodoma leo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gillesi Muroto, amesema mnamo Juni 23, 2014, mtu huyo aliwahi kulazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu ya akili chini ya daktari aliyejulikana kwa jina moja la William ambapo aliporuhusiwa alitakiwa kurejea hospitalini hapo Julai 9 mwaka huohuo lakini hakurejea.

Kamanda Muroto aliendelea kusema kwamba baada ya hapo, Machija ambaye kanisa lake halijasajiliwa popote,  aliibukia mkoani Dodoma katika kijiji cha Nong’ona kilicho karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) akifanya  mahubiri ya kidini yaliyodaiwa kuwa hayakuwa na maadili ya kidini.

Kwa msingi huo, alisema jeshi la polisi limempeleka Hospitali ya Rufaa ya Mirembe iliyoko mkoani Dodoma  kwa ajili ya kumpima tena matatizo hayo ya akili na baada ya majibu kutolewa,  Dkt. Dixon Philipo aliyemshughulikia alithibitisha kwamba bado ana matatizo hayo.

Pamoja na hayo, Muroto alisema jeshi la polisi mkoani humo  bado linaendelea kumshikilia kutokana na matendo yake aliyoyafanya ili kufanya uchunguzi zaidi.

Wagombea 27 wa Ubunge na Udiwani wateuliwa kugombea katika uchaguzi mdogo

$
0
0
Wagombea 27 wa ubunge na udiwani wameteuliwa kugombea nafasi hizo katika uchaguzi mdogo utakaofanyika Februari 17, mwaka huu katika majimbo mawili ya ubunge na kata nne.

Katika uteuzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki,  mgombea udiwani kupitita CCM katika kata ya Kimagai iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya  Mpwapwa mkoani Dodoma, amepita bila kupingwa.

Mbali na uteuzi huo, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi katika kata sita za Tanzania Bara wanatarajia kuteua wagombea wa udiwani wa kata hizo siku ya Jumatano ya tarehe 24 Januari, 2018 kukamilisha kata 10 zilizopangwa kushiriki Uchaguzi Mdogo wa Februari 17, 2018.

Akizungumzi uteuzi huo, Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Hamis Mkunga amesema mgombea huyo wa CCMa amepita bila kupingwa baada ya mgombea wa CHADEMA kushindwa kurejesha fomu za uteuzi.

Amesema katika uteuzi wa wagombea Jimbo la Kinondoni, msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo amewateua wagombea 12 ambao ni ambao ni Godfrey Maliza  kutoka chama cha TLP, Johnson Mwangosya  (SAU) na  Mwajuma Milambo kutoka UMD.

Mkunga amewataja wagombea wengine walioteuliwa kuwa ni John January Mboya  (Demokrasia Makini), Maulidi Mtulia (CCM), na Mary Mpangala wa DP.

Wengine ni Salim Mwalimu  (CHADEMA), Rajabu Salum (CUF), Mohamed Majaliwa (NRA), George Christian (CCK),  Ally Omari Abdallah (ADA THADEA) na Ashiri Kiwendu wa AFP

Kuhusu uteuzi wa wagombea ubunge katika Jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro, Mkunga amewataja wagombea wanne walioteuliwa kuwa ni Dk Godwin Mollel (CCM) Mdoe Azania Yambazi (SAU), Tumsifuheri Mwanry (CUF) naElvis Christopher MosiwaCHADEMA.

Katika kata tatu zilizobaki, Mkunga amevitaja vyama vya siasa vilivyopitisha wagombea ambao waliteuliwa katika kata ya Isamilo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Nyamagana mkoa wa Mwanza kuwa ni Chama cha CUF, DP, UDP, CCM, na CHADEMA.

Amevikumbusha vyama na wagombea kuheshimu maadili ya uchaguzi katika kipindi hiki cha kampeni kwani vyama vyote vimekubaliana kuheshimu maadili hayo na kuwaomba wananchi wajitokeze kwa wingisiku ya kupiga tarehe 17 Februari mwaka 2018.

Na Hussein Makame-NEC

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya January 24

Kamati ya Bunge yatoa agizo mifuko ya plastiki Ipigwe Marufuku

$
0
0
Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira imeiagiza Serikali kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki kutoka nje ya nchi ili kulinusuru Taifa na madhara yanayotokana na mifuko hiyo.

Maagizo hayo yalitolewa baada ya kamati hiyo jana kukutana na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Akizungumza jana, mwenyekiti wa kamati hiyo, Sadiq Murad alisema walipata maelezo kutoka serikalini kuwa uzalishaji katika viwanda 41 vya plastiki nchini ulikuwa ni tani 73 katika mwaka 2016.

Hata hivyo, alisema mifuko iliyoingia nchini kupitia bandarini na mipakani ilikuwa tani 1,375.

“Kamati ilishauri ipigwe marufuku mifuko ya plastiki kutoka nje ya nchi na iwekwe tahadhari katika mipaka yetu,” alisema.

Alisema kamati inaitaka Serikali kufanya uhakiki wa uzalishaji katika viwanda vya nchini ambavyo vimepunguza uzalishaji ili waweze kukaa chini na kuzalisha mifuko ambayo itakayokidhi mahitaji na vigezo.

“Na hii itakuwa ni ya muda kuzalisha mifuko hiyo kwa masharti ya vigezo baadaye Tanzania isiwe na uzalishaji wa mifuko hii tena inayoharibu mazingira,” alisema.

Murad alisema zipo nchi nyingine kama Kenya, Rwanda, Uganda na Zanzibar ambazo zimepiga marufuku uzalishaji na uingizaji wa mifuko hiyo na kutafuta mifuko mingine inayotengenezwa na nguo, karatasi na majani.

Alisema mfano mzuri ni Zanzibar ambayo imepiga marufuku mifuko hiyo tangu mwaka 2016 na mtu anapoingia na mifuko hiyo bandarini hunyang’anywa na kupewa mingine.

“Tueleweke kabisa sisi kama kamati hatutaki kiwanda chochote kifungwe, tunataka uzalishaji kwa kufuata masharti na vigezo. Tunaunga mkono juhudi za Rais John Magufuli za kuipeleka nchi katika uchumi wa viwanda lakini vigezo na masharti lazima yazingatiwe,” alisema.

Akizungumzia agizo hilo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba alisema hawaja japelekewa rasmi hayo mapendekezo. Hata hivyo alisema watapiga marufuku mifuko yote ya ndani na nje. “Wenye viwanda wajiandae maana yake dhamira ya Serikali wanaijua tangu mwaka 2016,” alisema

Shahidi aeleza alivyomrekodi Sugu

$
0
0
Mvutano wa kisheria katika kesi inayowakabili mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga umeibuka kwa mawakili wa pande mbili kuhusiana na ushahidi wa sauti iliyorekodiwa kwa kinasa sauti ambao upande wa Jamhuri uliiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi-Mbeya kuusikiliza na upande wa utetezi kuupinga.

Mvutano huo umeibuka baada ya shahidi wa tano upande wa Jamhuri, Inspekta Joram Magova akiongozwa na wakili wa Serikali mkuu, Joseph Pande kudai kwamba ndiye aliyefanya kazi ya kurekodi sauti za Sugu na Masonga kwenye mkutano wao wa Desemba 30 mwaka jana hivyo kuiomba Mahakama kupokea kifaa kilichotumika kurekodia kama kielelezo cha pili kilichowasilishwa na shahidi wa wanne, askari Daniel Masanja katika ushahidi unaondelea kutolewa mahakamani hapo.

Upande wa utetezi ukiongozwa na mawakili Boniface Mwabukusi na Hekima Mwasipu waliupinga ushahidi huo wakiiomba Mahakama kutoupokea wala kusikiliza wakidai shahidi aliyetoa kifaa hicho ana masilahi na kesi hiyo hivyo wanaona ushahidi huo haujakidhi matakwa kisheria.

Hata hivyo, mawakili wa Serikali, Pande na Baraka Mgaya kwa nyakati tofauti, waliinuka na kupinga hoja zilizotolewa na mawakili wa utetezi kwa hoja kwamba walichoiomba mahakama hiyo ni kusikiliza maudhui yaliyomo kwenye kifaa hicho ambacho kimewasilishwa kama kielelezo na kimepokewa.

“Shahidi anapaswa kuwa yule aliyeona, kushuhudia na aliyefanya na kusikia. Sasa hawa wenzetu wanataka kutuaminisha kwamba shahidi siyo yule aliyeona, aliyesikia na kufanya na kushuhudia, kitu ambacho sicho. Kama kielelezo kimepokewa na Mahakama hivyo hoja kwamba kisisikilizwe kilichomo ndani yake, itakuwa imepokea ya nini wakati hatujui kilichomo? Hivyo mheshimiwa hakimu naomba hoja hii itupiliwe mbali.”

Kifaa hicho kilitolewa na shahidi wa wanne Masanja ambaye alidai ndiye aliyekipokea na kukihifadhi katika chumba cha kuhifadhia vielelezo vyote vinavyotakiwa kutolewa ushahidi mahakamani katika Ofisi ya Upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO).

Shahidi huyo aliongozwa na wakili wa Mgaya na mahojiano yalikuwa:

Wakili: Shahidi hebu tueleze wewe ni nani na unafanya kazi ofisi gani.

Shahidi: Ni askari polisi nafanyia Ofisi ya Upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) lakini vilevile ni mtunza vielelezo katika ofisi hiyo.

Wakili: Tangu lini unafanya kazi hiyo?

Shahidi: Tangu mwaka 2004.

Wakili: Vielelezo gani unavyotunza?

Shahidi: Vielelezo vya kesi inayopelelezwa na kuna aina mbili, kwanza vielelezo ambavyo vimeshafunguliwa kesi na pili vielelezo ambavyo kesi yake inakuwa haijafunguliwa mahakamani.

Wakili: Ieleze Mahakama Desemba 30 mwaka jana ulikuwa wapi na ulikuwa unafanya nini?

Shahidi: Siku hiyo majira ya saa 12 jioni nilikuwa nyumbani lakini nikapigiwa simu na Inspekta Joram akinihitaji ofisini niweze kupokea vielelezo.

Wakili: Ulifanyeje baada ya hapo?

Shahidi: Ilinibidi niende na baada ya kufika ofisini nilimkuta Inspekta Joram akanieleza kuna vielelezo vya kuhifadhi, ametoka kwenye mkutano.

Wakili: Mkutano gani?

Shahidi: Mkutano wa Chadema.

Wakili: Ulifanyika wapi?

Shahidi: Ulifanyika maeneo ya Ruanda Nzovwe.

Wakili: Kielelezo gani ulichopokea?

Shahidi: Ni tape recorder.

Wakili: Baada ya kukueleza hivyo ulifanya nini?

Shahidi: Baada ya kuelezwa hivyo, nikavihifadhi kwa kuvifungia kwenye kasiki ofisini.

Wakili: Hebu ieleze Mahakama, Januari 2 mwaka huu ulikuwa wapi na kufanya nini?

Shahidi: Nilikuwa ofisini kwangu nikiendelea na majukumu yangu na akaja Inspekta Joram akihitaji tape recorder ile kwa ajili ya kwenda kuwasikilizishia viongozi wa Chadema akiwamo mbunge (Sugu).

Wakili: Baada ya hapo nini kiliendelea?

Shahidi: Inspekta Joram aliendelea na mahojiano na viongozi hao hadi saa nane mchana akanirudishia kifaa hicho nami nikakihifadhi kwenye kasiki.

Wakili: Tokea siku hiyo ulipokabidhiwa hadi leo (jana) hii nini kiliendelea?

Shahidi: Niliendelea kuhifadhi hadi leo (jana) nilioambiwa vinahitajika mahakamani.

Wakili: Ukiviona unaweza kuvitambua?

Shahidi: Ndiyo.

Wakili: Unahitaji Mahakama ifanyie nini vielelezo hivi?

Shahidi: Naomba Mahakama ivipokee kama vielelezo vya ushahidi katika kesi hii.

Wakili: Mheshimiwa Hakimu, shahidi wetu anaomba vidhibiti hivi vyote vipokewe na Mahakama yako kama vielelezo katika kesi hii.

Baada ya wakili kumuongoza shahidi huyo, Wakili Mwabukusi wa utetezi alisimama na kuweka pingamizi juu ya kielelezo hicho akipinga kisipokewe kwa madai kwamba hakijakidhi matakwa ya kisheria na hakina ubora unaotakiwa.

“Kifaa kinachotaka kuwa kielelezo mahakamani hapa ni kifaa ambacho kinasemekana kina maelezo yaliyorekodiwa na mtu mwingine na huyu aliyerekodi hatujaambiwa alirekodi kwa maudhui gani,” Mahakama haijaelezwa kwa namna gani ‘data massage’ zilizomo katika kifaa hiki hazijawa ‘tempered’ na haziwezi kuwa ‘tempered’ kwa namna gani. Tunapinga kifaa hiki kisipokewe kwa vile hakijakidhi matakwa na hakina ubora unaotakiwa kisheria.

Baada ya hoja hizo za Wakili Mwabukusi, Wakili wa Jamhuri, Pande aliinuka na kusema msingi wa hoja hizo unapinga kutolewa kwa kifaa hicho kama ushahidi kwa madai kwamba shahidi aliyewasilisha si aliyerekodi kwamba hawana pingamizi ikiwa kitatolewa na shahidi anayefuata ambaye kimsingi atakitambua.

Hata hivyo, mawakili wa utetezi walipinga hoja za wakili huyo na kutaka visipokewe vyote

Mabishano hayo yalidumu kwa takriban nusu saa kabla ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Michael Mteite kuahirisha kesi hiyo kwa nusu saa ndipo atoe uamuzi juu ya kinachobishaniwa.

Baada ya kurejea, Hakimu Mteite alisema Mahakama imejiridhisha kwamba vielelezo hivyo vinaonekana katika muonekano wake halisi, hivyo inavipokea kama vidhibiti na itatoa ufafanuzi wa kwa nini iliamua kuvipokea siku ya hukumu ya kesi yenyewe. Kesi hiyo inaendelea leo.

Mwanakwaya Afariki Kanisani Baada ya Kutoa Sadaka

$
0
0
Mwanakwaya wa kwaya ya Kanisa Katoliki la Mtakatifu Secilia, Kigango cha Muze Parokia ya Zimba Jimbo la Sumbawanga, Flora Nandi (25), ameanguka na kufariki dunia muda mfupi baada ya kutoa sadaka ya shukrani akiwa kanisani.

Tukio hilo la kifo cha mwanakwaya huyo wa kwaya ya Mtakatifu Secilia lilitokea Jumapili saa 4 asubuhi wakati wa idada ya kwanza.

Akisimulia tukio hilo Katekista wa kanisa aliyekuwa akiongoza ibada hiyo, Philipo Lupadasi, alisema kuwa wanakwaya wakiwa wanaimba na marehemu muda mfupi baada ya Lupadasi kutoka kutoa sadaka ya shukrani na kuendelea kuimba.

Alisema ghafla aliangua chini hali iliyozua mtafaruku na kusababisha ibada kusimama kwa muda mfupi, hali iliyowafanya wanakwaya wenzake kumnyanyua na kumtoa nje ya kanisa, ili pate hewa wakiamini kuwa amepoteza fahamu.

Katekista huyo alisema baada ya kumpepea kwa muda wanakwaya wenzake waliona Flora hapati fahamu, hali iliyowalazimu kumkimbiza katika zahanati ya kijiji cha Muze kwa ajili ya matibabu.

Alisema baada ya kufikishwa katika zahanati hiyo alipokewa na wahudumu wa afya na baada ya kufanyiwa uchunguzi ilibainika kuwa walimpeleka katika zahanati akiwa ameshafariki dunia.

Baada ya kupewa taarifa ya kifo hicho wanakwaya hao waliangua vilio hali iliyosababisha washindwe kurudi kanisani kuimba katika ibada ya pili, hivyo kuuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka nyumbani kwake.

Katekista huyo alifafanua kuwa Flora wakati anafariki dunia alikuwa na ujauzito wa miezi mitano.

Kwa upande wake mwalimu wa kwaya ya Mtakatifu Cecilia, Aloyce Mwandanje, alisema kuwa kifo cha mwanakwaya mwenzao kimewaachia majonzi makubwa, ingawa ni mapenzi ya Mungu.

Alisema mwili wa marehemu ulizikwa Jumatatu katika makaburi ya Kijiji cha Muze.

Jaji mstaafu Robert Kisanga afariki dunia

$
0
0
Jaji Mstaafu Robert Kisanga amefariki dunia  katika Hospitali ya Regence ya Jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na Msajili wa Mahakama ya Rufaa, John Kahyoza.

Mbali na Mahakama ya Rufaa, Marehemu Jaji Robert Kisanga alifanya kazi Baraza la Habari Tanzania (MCT).

Pia amewahi kuwa mwenyekiti wa kwanza wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini ambapo alistaafu mwaka 2008.

Idris Sultan atoa neno kuhusu tuzo za Oscar, Awamwagia Sifa Wakenya

$
0
0
Muigizaji wa filamu ambaye siku  zijazo anatarajia kwenda kuigiza katika filamu ya ‘The Blue Maurtius’ Idris Sultan, ametoa neno kwa Watanzania kuhusiana na majirani zetu Kenya kupata nafasi katika tuzo za filamu za Oscar.

Idris ametoa maneno katika mtandao wa Twitter na huku akionyeshwa kukerwa na baadhi ya watu wanaopenda umbea kuliko kazi.

“Kenya imepata Oscar award moja ya Lupita, imekua nominated Oscar award nyingine movie ya WATU WOTE na sasa wamefanikiwa kutengeneza satellite yao ya kwanza. Kwa kifupi watafanya yote ila hawatakaa watukute kwa instagram followers, sisi ndio noma. Satellite ndo nini ? Ina umbea ?,” ameandika Idris.

Washiriki wa tuzo za Oscar mwaka 2018 walitajwa hapo jana huku upande wa Afrika Mashariki imetoa filamu moja iitwayo iiywayo ‘Watu Wote/All of Us’ kutoka Kenya ambayo inazungumzia shambulizi la kigaidi la Al-shabaab lililotokea nchini Kenya mwaka 2014 katika eneo la Mandera ambapo watu 28 waliuawa kwenye tukio hilo.

Ashtakiwa kwa Kutoa Taarifa za Uongo

$
0
0
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO, DODOMA
Serikali imemshtaki John Hima (29) kwa kosa la kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu Namba 9 ya mwaka 2015.

Akisoma kesi hiyo namba 9 ya mwaka 2018 katika Mahakama ya Wilaya ya Bahi mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Suniva Mwajumbe, Inspekta Msaidizi Amani amesema kuwa mshtakiwa ametenda kosa hilo Januari 7 mwaka huu katika kijiji cha Nghulukano, Kata ya Chikola, Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma.

Ilielezwa mahakamani hapo kuwa mshitakiwa ni mwajiriwa wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) akiwa ni mkusanya taarifa (mdadisi) katika Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2017/2018 kwa Tanzania Bara.

Hata hivyo baada ya kusomewa mashtaka hayo, Mdadisi Hima alikana mashitaka na kesi hiyo itasomwa tena tarehe 7 Februari, 2018 ambapo amerudishwa rumande baada ya kukosa wadhamini.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya Mahakama, Mwanasheria wa NBS Oscar Mangula amesema kuwa, mtuhumiwa Hima aliingia mkataba na NBS kuwa mmoja wa wadadisi wa Utafiti huo unaoendelea hivi sasa ambao ulianza Desemba mwaka jana.

“Kwa mujibu wa sheria akiwa kama mdadisi majukumu yake alitakiwa kuwa katika eneo la kazi kulingana na mkataba na kiapo alichopata  ambapo yeye kwa makusudi aliamua kutelekeza majukumu hayo na kuwa nje ya kituo cha kazi hivyo kwa mujibu wa sheria ya Takwimu ametenda kosa la kijinai” amesema Mwanasheria Mangula.

Mwanasheria Mangula ameongeza kuwa, “Mkataba wa kazi ni wa miezi 12 ambapo ulianzia Desemba 2017 hadi Novemba 2018 lakini mdadisi huyu aliacha kutimiza majukumu yake kuanzia tarehe 7 Januari ambapo sisi tulifika pale tarehe 13 na 14 Januari mwaka huu ila hakuweza kufanya kazi yake kama ilivyotakiwa”.

Mwanasheria Mangula alieleza kuwa kesi hiyo inawakumbusha wadadisi waliopewa jukumu la kukusanya taarifa za kitakwimu kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa mikataba yao ya ajira, kiapo na mafunzo waliyopewa ili kuepuka kutenda makossa ya kijinai kama analodaiwa kutenda na mtuhumiwa.

Aidha, inawakumbusha wananchi umuhimu wa kuendelea kutoa ushirikiano kwa wadadisi mbalimbali wanaopewa jukumu la kukusanya taarifa za kitakwimu kwani kufanya hivyo ni kutekeleza matakwa ya Sheria ya Takwimu ya mwaka 2015.

Rais Magufuli aomboleza kifo cha Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma kufuatia kifo cha Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga kilichotokea jana tarehe 23 Januari, 2018 katika hospitali ya Regency Jijini Dar es Salaam.

Katika salamu hizo Mhe. Rais Magufuli amesema Jaji Mstaafu Robert Kisanga atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa alioutoa kwa Taifa wakati wote wa utumishi wake uliojaa umakini, uchapakazi, uzalendo na ushirikiano na wengine, mambo ambayo yalimwezesha kupata mafanikio makubwa.

“Sote tunafahamu kazi nzuri alizofanya akiwa katika majukumu mbalimbali ya kitaifa, mchango wake katika kuijenga taaluma ya uanasheria baada ya uhuru na uanzishaji wa Mahakama ya Rufani baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977, kwa hakika mchango wake hautasahaulika.

“Nakuomba Mhe. Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma unifikishie salamu zangu za pole kwa familia ya Marehemu Jaji Mstaafu Kisanga, Majaji na wanasheria wote, ndugu, jamaa na marafiki wote walioguswa na msiba huu” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amewaombea wafiwa wote wawe na moyo wa subira, uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na amemuombea Marehemu Jaji Mstaafu Kisanga apumzishwe mahali pema peponi, Amina.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
24 Januari, 2018

Mwanafunzi SUA asakwa kwa tuhuma za kumnyonga mpenzi wake

$
0
0
 Jeshi la polisi mkoani Morogoro linamsaka mwanafunzi wa mwaka wa tatu Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Mwita Marwa (30) kwa tuhuma za kumuua kwa kumnyonga mpenzi wake Kibua Adam (39) baada ya kutokea kutokuelewana kati yao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amesema tukio hilo lilitokea Januari 22 mwaka huu katika eneo la Modeco Manispaa ya Morogoro ambapo mwanafunzi huyo alitoweka baada ya tukio hilo.

Amesema siku ya tukio mwanafunzi huyo na mpenzi wake ambaye ni mhudumu wa baa walichukua chumba katika nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kama Aluta ambapo walilala lakini baadaye mwili wa marehemu ulikutwa chumbani.

“Dada huyu mkazi wa Kihonda alikutwa ameachwa chumbani akiwa ameshafariki na baada ya uchunguzi ilionekana kwamba marehemu alinyongwa shingo kabla ya kifo chake,” amesema Kamanda Matei.

Hata hivyo, kamanda huyo amesema baada ya tukio hilo mtuhumiwa alimwandikia ujumbe wa simu dada wa marehemu aitwaye Happiness Adamu ujumbe akisema kwamba tayari marehemu keshatangulia na yeye mtuhumiwa atafuata.

“Nasikitika sana hamtatuona hapa duniani Mwita na Kibua, mimi ninayeandika meseji hii ni Mwita, nikimaliza nakunywa sumu au vidonge nife na mimi nimechoka na dunia na Kibua yeye keshatangulia, njooni hapa Aluta Bar mtutoe chumbani tulipolala,” ulisomeka ujumbe huo.

Hata hivyo, watu wa karibu wa marehemu ambao hawakutaka kutaja majina yao walisema marehemu alikuwa na mpenzi mwingine kabla ya Mwita na walipokorofishana ndipo alipoamua kuwa na Mwita lakini siku chache kabla ya tukio alimwambia Mwita kwamba mpenzi wake wa awali amejirekebisha hivyo anataka kurejeana naye jambo ambalo mtuhumiwa alikuwa analipinga.

Kamanda Matei amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa ya Morogoro na jeshi hilo bado linaendelea na jitihada za kumsaka mtuhumiwa.   

Mkuu wa Wilaya Aamuru Aliyemkashifu Rais Magufuli Atupwe Ndani Masaa 48

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara, Chelestino Mofuga amemuagiza Mkuu wa Polisi wilayani humo kumkamata Eliud Petro (50) akituhumiwa kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais.

Mofuga ametoa kauli hiyo jana Jumanne Januari 23,2018 akitaka Petro akamatwe na kuwekwa ndani kwa saa 48 na baadaye kufikishwa mahakamani.

Amesema mtuhumiwa alitumia lugha hiyo baada ya kukamatwa na polisi kwa kosa la kuvamia eneo la Shule ya Msingi Endamasak na kulima.

Mofuga amesema wakati polisi wakiendelea kuwakamata wenzake wanne, Petro alitamka kuwa Rais John Magufuli naye ni mtuhumiwa bila kufafanua anatuhumiwa kwa kosa gani.

Amebainisha kuwa Petro na wenzake walikamatwa kwa kosa la kuvamia na kulima eneo la shule hiyo.

Amewataja watuhumiwa wengine kuwa ni Yohana Baida, Boay Nonash, Paulo Gutii na Martin Joseph.

Mofuga amesema kwa mamlaka aliyonayo amemuagiza mkuu wa polisi wa wilaya  kumweka rumande kwa saa 48 mtuhumiwa na kumfikisha mahakamani.

JKCI yaokoa milioni 800 kwa kufanyia upasuaji moyo watoto 20

$
0
0
Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto ya nchini Israel na Kituo cha Moyo cha Berlin kutoka nchini Ujerumani wamefanya upasuaji wa moyo bila kufungua kwa watoto 15 kati ya watoto 20 wenye matatizo ya moyo waliopangwa kufanyiwa matibabu hayo.

Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Tiba JKCI, Dkt. Peter Kisenge amesema upasuaji huo unaotumia mtambo wa Cathlab umefanyika katika kambi maalumu ya matibabu iliyoanza Januari 20 ambayo inatarajiwa kumalizika kesho Januari 25, 2018, ambapo watoto 32 walifanyiwa uchunguzi wa moyo.

Amesema upasuaji wa watoto hao katika taasisi ya JKCI umeokoa zaidi ya milioni 800 ambazo zingetumika kuwasafirisha na kuwatibia wagonjwa nje ya nchi.

Dkt. Kisenge amesema matibabu mengine yaliyofanyika ni pamoja na kuzibua matundu kwenye moyo, kutanua mishipa ya moyo kwa watoto wenye umri kuanzia mwezi mmoja hadi miaka 18.

Matibabu hayo yamefanywa na Timu ya madaktari bingwa wa moyo kutoka taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto iliongozwa na Dkt. Sagi Assa na wa kituo cha Moyo cha Berlin kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa JKCI.

Gesi ya Helium ya futi za ujazo bilioni 98.9 yagunduliwa mkoani Rukwa

$
0
0
Kampuni ya uchunguzi na utafiti wa madini, Helium One, ambayo kwa sasa inafanya utafiti wa gesi ya heliamu mkoa wa Rukwa imegundua kuwapo kwa futi za ujazo bilioni 98.9 za gesi hiyo katika maeneo iliyokwishafanyia uchunguzi.

Hayo yalielezwa katika warsha ya siku moja iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es salaam, na kuratibiwa na Idara ya Jiolojia ya chuo hicho, Helium One na Chuo Kikuu cha Oxford.

Akizungumza katika warsha hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Helium One, Thomas Abraham-James, alisema kwamba kampuni yao imetafuta leseni 23 za uchunguzi na kwamba nyingine tatu zimeombwa.

Alisema kwamba leseni hizo zote zinamilikiwa na kampuni hiyo kwa asilimia 100 na kwamba ina haki za kipekee za gesi hiyo ya heliamu .

Pamoja na kutoa taarifa hiyo,alisema lengo la kuwa na warsha ni kuwaita wataalamu na wadau mbalimbali wa hapa nchini na kimataifa kubadilishana uzoefu na taarifa zilizopo kuhusu gesi hiyo na kuangalia fursa zinazoambatana na uwapo wa gesi hiyo katika harakati za kitaifa za kuwa na taifa la viwanda.

“Helium One inaamini kwamba kuna fursa kupitia utafiti huu kuweza kutengeneza utaalamu wa kiwango cha juu na utaalamu wa hapa nchini juu ya uendelezaji wa gesi hiyo. Tutaendelea kujenga uhusiano na Chuo Kikuu cha Dar es salaam kuweza kubadilishana elimu, kutoa mafunzo kwa wanafunzi na maofisa wizara ya madini na kutengeneza mpango wa ufadhili wa masomo,” alisema.

Kwa mujibu wa Abraham-James, warsha hiyo ilihudhuriwa na wanasayansi waandamizi wa gesi kutoka Chuo Kikuu cha Oxford cha Uingereza na Idara ya Jiolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam,UDSM, watu wenye mamlaka na maamuzi, wadau wa maendeleo, watengeneza sera kutoka serikalini, watafiti na sekta binafsi.

Aidha kampuni hiyo imetoa ufadhili wa masomo ngazi ya shahada ya uzamili kwa wanafunzi wawili wa UDSM kusoma katika Chuo Kikuu cha Oxford , ikiwa ni sehemu ya kuingiza utaalamu wa hali ya juu wa kisayansi kwa watanzania na pia kuendeleza uhusiano mzuri kati ya Helium One na UDSM.

Wakati wa warsha hiyo, Profesa John Machiwa, akimwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo, Prof Cuthbert Kimambo, alisema kwamba jukwaa hilo ni jema kwa wanafunzi, wakufunzi na Chuo kizima kutafuta njia ya kuona namna ya kushirikiana na Helium One.

“Tunaweza kufanyakazi pamoja na kunoa taaluma na pia kupata utaalamu katika utafiti wa heliamu uzalishaji na usafirishaji wake,” alisema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images