Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Yawaandikiia Barua Wabunge Kutaka Miamala Yao

$
0
0
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imewaandikia barua baadhi ya wabunge, ikiwataka kuwasilisha taarifa za miamala ya benki za kuanzia Januari hadi Desemba 2017.

Sekretarieti hiyo imetaka taarifa hizo ziwe zimeifikia ndani ya siku 30 kuanzia Januari 15, 2018.

Barua hiyo  inawataka wabunge hao  kutekeleza agizo hilo ili kuthibitisha taarifa zilizomo kwenye tamko lake  alilowasilisha.

Ofisa mmoja wa taasisi hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe, alithibitisha kuwepo kwa barua hizo, akisema si wote walioandikiwa barua za kutakiwa kutoa taarifa hizo.

Hata hivyo, alisema wabunge walioandikiwa ni wale ambao fomu zao zinaonyesha haja ya uhakiki zaidi wa taarifa zao.

Rais wa John Pombe Magufuli ndiye alikuwa wa kwanza kuwasilisha fomu yake ya tamko kuhusu rasilimali na madeni katika ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliyopo Mtaa wa Ohio, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam Desemba 28, 2017.

Baada ya kuwasilisha fomu hiyo, Rais aliipongeza sekretarieti hiyo kwa kazi inazofanya na kumtaka Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu, Harold Nsekela kutopokea fomu ya kiongozi yeyote ambaye angeshindwa kuwasilisha tamko la kabla ya Desemba31, 2017.

Kauli hiyo ya Rais iliwaamsha viongozi mbalimbali wakiwemo wabunge na viongozi wengine wa Serikali kufurika kwenye ofisi hiyo kuwasilisha matamko yao ya mali walizonazo.

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ????

$
0
0
Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA 
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA 
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI 
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI 
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK 

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO 

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM,NAUTALETEWA POPOTE ULIPO.

 SIMU; NO 0767145357/0629034550.

Msimamo mpya wa Rais kuhusu kunyonga watu

$
0
0
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema anatafakari uwezekano wa kuanza tena kuwanyonga wahalifu nchini humo.

Rais Museveni amesema licha ya kwamba yeye ni "Mkristo" kuwa dini yake imemzuia kutekeleza hukumu ya kifo dhidi ya wale ambao wamehukumiwa kunyongwa, hata hivyo amesema, hali hiyo imekuwa ikiwatia moyo wahalifu.

Kiongozi huyo ametoa kauli hiyo wakati wa sherehe za kuhitimu kwa askari wa idara ya magereza, katika gereza la Luzira jijini Kampala ambapo ni miaka 13 sasa tangu Uganda ilipotekeleza hukumu ya kifo dhidi ya wahalifu.

Watetezi wa haki za kibinadamu wameshutumu tamko hilo la Rais Museveni na kusema adhabu ya kifo haikomeshi uhalifu.

Mara ya mwisho kwa Rais Museveni kuidhinisha hukumu ya kifo itekelezwe ilikuwa katika gereza la Luzira mwaka 1999 na mwaka 2005 aliidhinisha mahakama ya kijeshi kutekeleza hukumu ya kifo

Tahadhari Kuhusu Homa ya Chikungunya, Hakuna Tiba Mahusi Wala Kinga

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya Afya imeutahadharisha umma kuhusu ugonjwa wa Homa ya Chikungunya ambao huambukizwa na mbu aina ya aedes na hauna tiba mahsusi wala kinga. Isome taarifa hii kuelewa zaidi kuhusu ugonjwa huo.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Itazame Hapa Video Mpya Ya Mpenzi wa Wolper

$
0
0
Mpenzi mpya  wa Staa wa sinema za Kibongo na Malkia wa Mavazi, Jacqueline Wolper, Sadiki Athanasy Sanga ‘Engine’, ametoa video yake ya wimbo wa Ulingo. 

==>Itazame Hapo Chini

Wastara Awachana Bongo Movie...."Sitazikwa na Wasanii Pekee"

$
0
0
Msanii wa filamu nchini Wastara Juma amesema hatokuja kumladhimisha mtu yeyote katika tasnia ya 'bongo movie' kuwa yeye hana pesa ya kujitibia ugonjwa wake unaomsumbua kwa madai hata siku ikitokea akifa hawezi kuzikwa na hao pekee yao.

Wastara ametoa kauli hiyo wakati akiongea na kituo cha EATV baaada ya kuwepo kwa baadhi ya watu kutomuamini kwa kile kinachomsumbua huku wengine wakidiriki hata kujaribu kumwambia anatafuta kiki kupitia tatizo hilo linalomsumbua la mguu wake.

"Yani hapa mtu anaweza akaniumiza kwa maneno au vitendo kwa sababu yeye anaamini kwa mawazo yake na kichwa chake kwamba, mimi nimekaa kitandani siumwi au pengine nimejiona nimepotea katika ulimwengu hivyo natafuta kiki yaani nijifunue nguo niupige picha mguu wangu uliyochanika kisha niuweke kwenye gazeti ama kwenye runinga (Tv) ?", alihoji Wastara.

Hata hivyo Wastara amesema hawezi kubadilisha fikra za watu wanavyofikilia kwa kuwa hayo ndiyo maisha yao ya kutoamini jambo lolote lile.

"Na kama kuna wasanii ambao wanaamini mimi siumwi siwezi kumladhimisha hata siku moja na ambaye atasema hatokuja kumtembelea Wastara kwa sababu haumwi au hana shida pesa, mimi siwezi kumfanya aniamini kwamba sina pesa. Sitoweza kufanya hicho kitu kwa sababu maelezo ninayoyaeleza katika runinga ndiyo yaleyale hayotokuja kubadilika. Kwa hiyo ninachoongea hapa ni ukweli hautokuja kubadilika miaka yote hata nikifa", alisisitiza Wastara.

Pamoja na hayo Wastara aliendelea kwa kusema "wapo watu wa kweli wanaoamini na wengine wasioamini ambao huwezi kuwafanya waniamini. Watanzania wanaoniamini mimi wanatosha kwa sababu mwisho wa siku sitokuja kujizika mwenyewe au kuzikwa na wasanii pekee yake", alisema Wastara.

Mkurugenzi Muwasa aingia matatizoni....Ni Baada ya Waziri Mkuu Kumtupa TAKUKURU

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameamuru Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Mara kumkamata na kumuhoji Mkurugenzi Mtendani wa Mamlaka ya Maji Musoma (Muwasa) Gantala Said kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za mradi wa maji Bunda.

Mbali na mkurugenzi huyo pia ameiagiza Takukuru imuhoji mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi ya Nyakirang'anyi, Mahuza Mumay ambaye ndiye mkandarasi anajenga mradi huo unaotoa maji kutoka Ziwa Victoria kwenye eneo la Nyabehu hadi Bunda mjini.

Waziri Mkuu amefikia uamuzi huo jana Ijumaa jioni baada ya mkurugenzi huyo kushindwa kueleza kitu kilichosababisha mradi wa maji Bunda kutokamilika  pamoja na Serikali kutoa fedha nyingi.

Akizungumza katika kikao maalumu cha kujadili changamoto za utekelezaji wa miradi ya maji mkoani Mara, alichokiitisha mjini Bunda, Waziri Mkuu alisema alimua kuitisha kikao hicho baada ya kutoridhishwa na utekelezwaji wa miradi hiyo hususan inayosimamiwa na Muwasa.

Alisema kwa sasa Serikali inatekeleza kampeni ya Rais John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani. Kampeni hiyo  inayolenga kuwaondolea wananchi tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama, hivyo itawachukulia hatua wote watakaokwamisha miradi ya maji.

Waziri Mkuu alisema malengo ya kampeni hiyo ni kuwafikishia wananchi huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao.

Pia Majaliwa aliagiza kupitiwa upya kwa mradi huo   kwa sababu hafurahishwi na ujenzi wake.

“Kama mkurugenzi wa Muwasa anasema mradi umekamilika kwa asilimia 98 sasa kwa nini wananchi walalamikie kukosa huduma hiyo.”

Alisema mkurugenzi huyo amekuwa akimlipa mkandarasi fedha kabla ya kufanya kazi ambapo hadi sasa tayari mkandarasi anayenga mradi huo ameshalipwa zaidi ya Sh 7 bilioni na mradi haujakamilika na wananchi wanaendelea kutumia maji ambayo siyo salama.

Waziri Mkuu alisema viongozi hao wahojiwe na wakibainika kuhusika na ubadhilifuu wa fedha za mradi huo, wachukuliwe hatua kali za kisheria.

“Serikali imedhamiria kuimarisha huduma za maji, hivyo hatuhitaji mtu atakayeenda kinyume na mpango huo.”

Mradi wa kupeleka maji kwenye mji wa Bunda maji kutoka Ziwa Victoria katika eneo la Nyabeho ulisanifiwa mwaka 2006 na ulikuwa unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha za maendeleo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima aliagiza kufungwa na ofisi za Muwasa na kuwataka wafanyakazi wa mamlaka hiyo kutoruhusiwa kuingia ofisini hadi hapo uchunguzi utakapokamilika.

Waziri Mkuu: Watumishi Na Madiwani Shirikianeni

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa Halmashauri na Mji wa Bunda pamoja na Madiwani washirikiane katika utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya maendeleo.

Pia amewaagiza watumishi wa umma katika halmashauri ya wilaya na mji wa Bunda wafanye kazi kwa bidii na wawahudumie wananchi bila ya ubaguzi wa aina yoyote.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana (Ijumaa, Januari 19, 2018) wakati akizungumza na watumishi na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya na wa Halmashauri Mji wa Bunda, katika ukumbi wa Halmashauri ya Bunda.

“Watumishi wa umma  acheni kukaa sana maofisini tengeni muda wa kuwatembelea wananchi katika maeneo yao na shirikianneni nao katika kutatua kero zinazowakabili. Madiwani na watumishi lazima mshirikiane ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Alisema watumishi na madiwani wakishirikiana katika usimamizi wa utekelezaji wa miradi mbalimbali  ya maendeleo, wilaya itafanikiwa katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Pia Waziri Mkuu aliwasisitiza watumishi hao kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu za utumishi  na wajiepushe na vitendo vya rushwa, wizi , ufisadi na uzembe kwa sababu vinarudisha nyuma maendeleo ya wananchi.

Awali, Waziri Mkuu alikagua mradi wa maji wa Bunda na baadae alizindua kikundi cha Ushirika cha Igembe Sabo na kukagua skimu ya umwagiliaji wa zao la mpunga ya Nyatwali wilayani Bunda.

Waziri Mkuu alihitimisha ziara yake wilayani Bunda kwa kuhutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Stendi Mpya katika mji mdogo wa Bunda.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri arudi CCM atwae jimbo 2020

$
0
0
Mwanasiasa  wa upinzani na aliyekuwa Naibu Waziri katika serikali ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Goodluck Ole Medeye, ametangaza kurejea Chama Cha Mapinduzi huku akidai kuwa ameamua kufanya hivyo kwa kuwa vitendo vya rushwa,-Hususan nyakati za uchaguzi, vimemalizwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Dk. John Magufuli.

 Ole Medeye juzi alisema kilichomkimbiza CCM mwaka 2015 na kujiunga na Chadema ni vitendo vya rushwa katika mchakato wa kupata wagombea wa chama hicho tawala.

Alisema anafurahi kuona sasa vitendo hivyo havipo ndani ya CCM baada ya kudhibitiwa na Rais Magufuli.Ole Medeye alikuwa mmoja wa wabunge watano wa CCM waliojiunga na Chadema Agosti 12, 2015 wakiongozwa na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (Monduli). 

Ole Medeye aliteuliwa na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuwania nafasi ya Uspika wa Bunge baada ya Uchaguzi Mkuu.

Wengine waliohama pamoja na Lowassa ni Makongoro Mahanga (Segerea), James Lembeli (Kahama) na mbunge wa viti maalum, Esther Bulaya ambaye sasa ni mwakilishi wa wananchi wa Bunda Mjini (Chadema).

Hata hivyo, Ole Medeye alihama Chadema kabla ya mwaka kumalizika na kujiunga na UDP kinachoongozwa na John Cheyo Juni 12, 2016.

Medeye alisema alihamia UDP kwa kuwa inasimamia haki na demokrasia na kwamba yeye alikuwa akitaka demokrasia ya kweli na jukwaa la haki katika kuleta haki na maendeleo kwa Watanzania.

Alisema  kuwa alikaa chama hicho cha 'Bwana Mapesa' kwa miezi mitatu tu hata hivyo, kwa kuwa "nilikwenda kufanya kazi maalum."

Na sasa, Ole Medeye amesema ameamua kurejea CCM kwa kuwa kila mwanachama anayo fursa kushiriki uchaguzi, ikiwamo kugombea nafasi yoyote bila kutoa rushwa na akashinda.

"Mimi sijawahi kuwahonga watu ili wanichague," alisema Ole Mideye na "wakati huo CCM kulikuwa na rushwa sana; ndiyo maana nikaamua kukimbia.

"Lakini kwa sasa hakuna tena kitu kama hicho, hivyo nimeamua kurejea CCM."

Ole Medeye alisema katika Uchaguzi Mkuu ujao, mwaka 2020, anataka kurudi na kuwatumikia wananchi kupitia nafasi ya ubunge.

Waziri Ndalichako: Ninawapa wiki moja la sivyo tutavunja mkataba na TBA

$
0
0
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amechukizwa na hali ya ujenzi katika Hosteli za Chuo Kikuu cha Taaluma na Tiba cha Mloganzila na kuipatia wiki moja Wakala wa Ujenzi Tanzania (TBA) kuhakikisha inarekebisha mapungufu yote.

Profesa Ndalichako ameyasema hayo leo Jumamosi wakati wa ziara ya kukagua hali ya ujenzi Mloganzila, ambapo alishuhudia  ujenzi huo ukiwa umesimama huku kukiwa na uchimbaji wa msingi pekee katika majengo manne.

Amesema hajaridhishwa na maendeleo ya ujenzi huo, licha ya yeye kutoa kiasi cha Sh3.9 bilioni Agosti mwaka jana kwa ajili ya ujenzi huo wa majengo saba ambayo yangehusisha mabweni mawili ya wanafunzi, jengo la kufundishia, jengo la maktaba, bwalo la chakula, jengo la maabara, jengo la maabara maalum na jengo la kazi za nje.

"Hamko makini na kazi yenu, niwahakikishie ikifika Jumamosi sijaona kinachoendelea nawachukulia hatua haiwezekani nimewapa fedha tangu Agosti mwaka jana mpaka leo mmenichimbia msingi pekee, nahangaika ujenzi ukamilike madaktari wakae hapa watoe huduma kwa wagonjwa ninyi mnaleta mchezo, nipo kazini lazima mtii ninachokiagiza," aling'aka Profesa Ndalichako.

Meneja wa TBA Kanda ya Dar es Salaam, Manasseh Shekalaghe amesema kilichokwamisha ujenzi huo ni mvua zilizonyesha ambazo zilileta changamoto na hivyo msingi ulifukiwa na udongo.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Waziri wa Maji aagiza kaimu mkurugenzi wa maji mijini kutumbuliwa

$
0
0
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Kitila Mkumbo kumsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi wa Maji Mijini, Clement Kivegalo.

Pia, Kamwelwe amemwagiza mkurugenzi wa utawala wa wizara hiyo, Barnabas Ndunguru  kuwahamishia Dodoma watumishi 178 wa wizara ifikapo Januari 30, 2018 la sivyo atamchukulia hatua.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 20, 2018 jijini Dar es Salaam, Waziri Kamwelwe amesema jana Januari 19, alizivunja bodi  za maji safi za Mkoa wa Arusha na Musoma baada ya kujiridhisha kuwa utendaji wao si mzuri.

“Juzi tu niliuondoa utendaji wa Lindi, kuna tatizo la utendaji wa wakandarasi hapa Dar es Salaam, Chalinze na tuna tatizo Kigoma, mamlaka za maji za miji ya mikoa  zinasimamiwa na mkurugenzi wa maji mijini, hapa tuna idara kama tatu au nne zinasimamia utekelezaji wa miradi hiyo,” amesema Mhandisi Kamwelwe na kuongeza,

“Idara ya maji mijini inaongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mhandisi Clement Kivegalo wakati haya yote yanatokea Kivegalo yupo lakini matatizo yanatokea yanabainiwa na waziri, naibu waziri au katibu mkuu, leo Januari 20, 2018 namwagiza Katibu Mkuu atengue uteuzi wake atafute mtu mwingine.”

Waziri Kamwelwe amesema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyeko ziara mkoa wa Mara amebaini kasoro za utendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Musoma (Muwasa) na kuagiza hatua zichukuliwe ikiwamo kuchunguzwa watendaji wote.

“Kupitia ziara ya Waziri Mkuu imebainika yapo matatizo yanayomhusu mkurugenzi wa Muwasa, Gantara Said na wahusika wote ameeleza wafanyiwe uchunguzi, hivyo kuanza leo Januari 20, natengua uteuzi wake na nafasi yake itakaimiwa na Petro Muhoja wa Mamalaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza, namwagiza mkurugenzi wa mamalaka ya maji Mwanza, asaidie mamlaka ya maji Musoma ili waweze kufanya kazi,” amesema.

Mgombea Wa Ubunge Chadema Atoa Neno Zito Akirudisha Fomu Leo

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, Salum Mwalimu amefanikiwa kurudisha fomu ya kugombea Ubunge jimbo la Kinondoni huku akiwataka wanachama wa chama hicho kuwa wavumilivu katika kipindi hiki cha muda mfupi.

Mhe. Salum ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari vilivyoweza kujitokeza katika ofisi za Tume ya Uchaguzi Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo alasiri(Jumamosi).

"Nimefarijika kwamba fomu imepokelewa na haina mapungufu yeyote yale, kwa hiyo hatuna shaka lolote katika fomu yetu kwa maana tumeikagua na kuuliza maswali katika kipengele jinsi tulivyojaza na wakatujibu tupo sahihi. Imani yangu ni kwamba hawajaona kosa ambalo wanaweza kulikalia kimya walisubiri ili lilete matatizo baadae", alisema Mhe. Salum Mwalimu.

Aidha, Mhe. Salum aliendelea kufafanua baadhi ya mambo kwa kusema hatoweza kutangaza siku ya kuanza kampeni rasmi mpaka itakapofika alasiri ya kesho (Jumapili) kwa maana muda huu wa katikati ameuacha ili kama kutakuwa na watu waweze kuweka mapingamizi yao.

"Kwa hiyo baada ya muda huo kupita siku ya kesho bila ya shaka nitakuwa mgombea rasmi wa jimbo la Kinondoni ambaye nisiyekuwa na doa kwa ajili ya mapambano hayo", alisistiza Mhe. Salum Mwalimu.

Pamoja na hayo, Mhe. Salum aliendelea kwa kusema "kikubwa labda niwaambie hatukuja ku-beep wala hatu-beep kamwe haitakuja kutokea ku-beep katika jimbo la Kinondoni. Tunamaanisha na tunaamini kabisa kama nidhamu ya siasa waliyoikataa, hapa watairudisha na wasipoikubali kuirudisha Kinondoni maana yake ustaarabu katika siasa tunaamini utakuwa umekwishamalizika. Hatutokuwa wa kulia, safarii hii ikibidi tutawasababisha wale waliosababisha sisi tunalialia wao ndio walie".

Kwa upande mwingine Mhe. Salum Mwalimu amesema amedhamilia na amejitoa kusimamia haki ya wananchi wa Jimbo la Kinondoni na kuahidi hatoweza kuyumba katika hilo.

Agizo la Waziri Mwigulu kwa Polisi kuhusu kukamata wazururaji

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dr. Mwigulu Nchemba leo January 20, 2018  amelitaka Jeshi la Polisi nchini kutafuta namna ya kupunguza wahalifu wanaokamatwa kwa makosa kama uzururaji ili kupunguza mrundikano kwenye mahabusu.

Ameeleza kuwa suala hili pia litaepusha watuhumiwa wanaopelekwa mahabusu kwa makosa ya uzururaji kupata nafasi ya kuzungumzia masuala ya uhalifu na watuhumiwa waliozoea.

Kwa upande mwingine Dr. Mwigulu ameagiza wananchi kushirikiana na serikali katika ujenzi wa vituo vya polisi kwa kuwa suala la ulinzi ni ajenda ya kila Mtanzania na linapaswa kupewa kipaumbele.

Akizungumza na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Dr. Mwigulu amesema kuwa mkakati wa Halmashauri hiyo kujenga kituo cha kisasa cha polisi ni kitendo cha kupongezwa kwani wanalenga kukomesha uhalifu wa aina zote.

Binti mwenye uvimbe begani afariki dunia....Waziri Ummy Amlilia

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema amesikitishwa na kifo cha msichana Marim Sandalu (17) aliyekuwa na uvimbe begani.

Mariam ambaye ni mkazi wa Masasi mkoani Mtwara, amefariki dunia leo alfajiri akipatiwa matibabu katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI).
 
Binti huyo ambaye alitakiwa kufanyiwa upasuaji Muhimbili mwaka mmoja uliopita wakati huo uvimbe ukiwa bado mdogo, alitoweka baada ya kwenda katika tiba za asili kabla ya kurejea hospitalini hapo Januari 3 mwaka huu, baadaye kuhamishiwa katika taasisi hiyo.

Waziri Ummy amesema inasikitisha kwani msaada wa Watanzania haukuweza kuokoa maisha yake.

“Tutaongeza jitihada zaidi kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kuwahi hospitalini kufanyiwa uchunguzi na kuzingatia maelekezo ya madaktari wanayopewa ikiwamo kuanza matibabu mara moja na si kwenda kukaa nyumbani na mgonjwa,” amesema Waziri Ummy ambaye hivi karibuni alimtembelea Mariam hospitalini kumjulia hali.

Mgombea Ubunge CHADEMA Jimbo la Siha Naye Kajiapiza Kuichapa CCM

$
0
0
Mgombea ubunge wa Jimbo la Siha, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Elvis Mosi, amesema atashinda ubunge wa jimbo hilo mapema asubuhi kutokana na mgombea aliyepitishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Godwin Mollel, kutokuwa na nguvu ya kushinda kwani amekosa sifa za kuwa kiongozi kwa madai kuwa ni mtu mwenye tamaa na asiyekuwa na msimamo.

Mgombea huyo amesema chama chake kimemuamini na kumpitisha baada ya kumpima na kuona anao uwezo wa kukabiliana na Dk. Mollel na kwamba ushindi wake utapatikana asubuhi.

“Mgombea wa CCM hawezi kamwe kushindana na mimi yaani ni ardhi na mbingu na sifa ya kumshinda tunayo, kwanza ni mtu aliye na tamaa na asiyekuwa na msimamo wananchi hawawezi kumchagua mtu wa namna hiyo kwani walimuamini lakini amewasaliti,” amesema.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya January 21

Mkuu Wa Majeshi Ya Ulinzi Jenerali Mabeyo Akagua Uharibifu Wa Miundombinu Ya Reli Kilosa Mkoani Morogoro

$
0
0
Na. Andrew Chimesela – Morogoro
Hali  mbaya ya mafuriko yanayoendela kuathiri wananchi wa Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro yamemfanya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Generali Venance Mabeyo kufika Kilosa na kutembelea baadhi ya maeneo yaliyoathirika ili kutafuta ufumbuzi wa pamoja wa kuokoa maisha ya wananchi wa maeneo hayo na mali zao.

Generali Mabeyo aliwasili Kilosa Jan.19, 2018 majira ya jioni na kuungana na mwenyeji wake Dkt. Kebwe Stephen Kebwe Mkuu wa Mkoa wa Morogoro aliyepiga kambi Wilayani humo kwa ajili ya mafuriko hayo kisha bila kujali mvua iliyokuwa inaendelea kunyesha muda wote wakatembelea baadhi ya  maeneo yaliyoakuwa yamethiriwa ili kuona hali halisi ya mafuriko hayo.

Kwenye kikao cha majumuisho Mkuu huyo wa Majeshi nchini alishauri kuwa ili kutatua changamoto hiyo inatakiwa nguvu ya ziada na ya pamoja kwa taasisi zote kuungana, Ikiwa ni pamoja na taasisi mbali ili kuweza kuokoa maisha ya watu, mali zao pamoja na miundombinu iliyoathiriwa.

Hata hivyo alisema changamoto hiyo inatakiwa kuwe na mpango wa muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu. Amesema suluhisho la mpango wa mda mfupi ni kuwa na kazi ya dharura, na kazi hiyo ya dharura inahitajika kuwepo na mpango wa dharura ambao ni kuokoa maisha ya watu waliozingirwa na maji ili wasiendelee kukosa huduma za kijamii na pia kuathiri afya zao kwa kunywa maji ambayo si salama.

Pamoja na kuwepo kwa wazo la kurekebisha tuta la mto Mkondoa ikiwa ni mpango wa muda wa kati ili maji hayo yafuate mkondo wake lakini pia Generali Mabeyo ameshauri kuangalia namna ya kupunguza kasi ya maji hayo kuanzia yanakotoka kwa kujenga mabwawa ikiwa ni mpango wa muda mrefu.

“Maji haya yanakuja huku ni kama sisi ni waathirika zaidi lakini yanakoanzia hatujui hali iko namna gani, pengine katika mpango wa muda mrefu ingetazamwa namna ya kuyapunguza haya maji kasi yake.Sasa katika kuyapunguza, taasisi mablimbali zina wataalamu ambao wanaweza kusaidia kuweza kujenga mabwawa makubwa huko yanakoanzia ili haya maji  kupunguza kasi yake kabla hayajafika huku” alisema Generali Mabeyo.

Akitoa maelezo ya awali Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Stephen Kebwe amesema tuta hilo la mto Mkondoa lilijengwa enzi za Mkoloni kama kinga kwa  mji wa Kilosa na kwa mara ya kwanza lilipasuka mwaka 2010. Ujenzi  wake kuanzia hapo haukukamilika vizuri kutokan na hali ya kifedha na sasa limepasuka baada ya Mvua nyingi kunyesha kuamkia Jan,11 mwaka huu.

Hata hivyo Dkt. Kebwe ametoa Ombi kwa Mkuu huyo wa Majeshi, kupata nguvu kazi ya wananjeshi, vifaa na utaalamu wao ili baada ya mvua hizi kupungua waendelee na kutafuta mbinu ya kuuongoza mto Mkondoa uweze kupita katika sehemu yake ya awali na hivyo kutoathiri wananchi, mali zao na miundombinu iliyopo eneo hilo .

Zitto Kabwe aweka wazi uwekezaji mzito Kigoma

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT- Wazalendo),  Zitto Kabwe amesema amepatikana mwekezaji wa kujenga maduka makubwa la biashara (malls) mkoani humo kama yale ya  Mlimani City ya jijini Dar es Salaam.
 
Akihutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Community Center, Mwanga jana Januari 20, 2018,  Zitto amesema haiwezekani mkoa wa Kigoma ukaendelea kubaki nyuma kimaendeleo.
 
Zitto ambaye pia ni Kiongozi wa ACT- Wazalendo amesema inapofika jioni mji wa Kigoma unakuwa kimya jambo alilodai kuwa haliwezi kuleta mabadiliko na kukuza mzunguko wa fedha.

 “Tumepata mwekezaji wa kujenga mall kubwa kama ya Mlimani City ili ikifika usiku kuwe kumechangamka. Hatuwezi kuendelea kuwa mkoa au mji wa mwisho,”  amesema Zitto na kuongeza,

“Haina maana sisi watoto wenu kusomeshwa na kuuacha mji huu ukaendelea kuwa hivi. Tunahangaika, mtuache tufanye kazi na mwaka 2020 mtaniuliza kupitia kile nilichoahidi na mtaninyonga kwa nilichowaahidi.”

Kuhusu mapato ya halmashauri ya Kigoma Ujiji, Zitto amesema kitendo cha Serikali kuu kuchukua vyanzo vya mapato vilivyokuwa vikiiingizia mapato halmashauri hiyo na kutekeleza mipango yake,  imewalazimu kuongeza kodi kwa wafanyabishara.

“Tukiwaumiza kidogo katika kodi tuvumiliane na mimi sitawaangusha lakini huwezi kwenda peponi bila kufa, kwa hiyo lazima tuumie kidogo na nitakuwa kiongozi mwongo nikija hapa na kusema kila kitu mtapata ni uongo,” amesema Zitto na kuongeza,

“Sisi hatuna wa kutubeba. Lazima tupambane wenyewe na tutiane moyo. Hakuna jambo baya tunapopambana kuleta maendeleo lakini wengine wanaturudisha nyuma, haipendezi, tutiane moyo jamani.”
 
Amesema lengo ni kuubadili mji wa Kigoma kwa kuwa umekuwa nyuma kwa muda mrefu.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images