Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu: Wanaume Wa Tarime Acheni Ukatili Kwa Wanawake Na Watoto

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaasa wanaume wa wilaya ya Tarime kujiepusha na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto pamoja na kuachana na kilimo cha bangi.

Alitoa kauli hiyo jana jioni (Jumatano, Januari 17, 2018) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Serengeti, wilayani Tarime.

Waziri Mkuu alisema vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto pamoja na kilimo cha bangi vinaitia doa wilaya hiyo, hivyo hawana budi wakaepukana navyo.

“Serikali inakemea vitendo vya ukatili, achaneni navyo. Mtu unamchapa mtoto makofi hadi anazimia, kitendo hicho hakiwezi kuvumilika na pia kinaitia doa wilaya yenu.”

Wakati Huo huo, Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa wilaya hiyo, Bw. Glorious Luoga kuendelea na msako wa mashamba ya bangi na mirungi na kuchukua hatua kwa watakaobainika kuendesha kilimo hicho.

Alisema ardhi ya wilaya hiyo ni nzuri na inahimili kilimo cha mazao mbalimbali ya chakula na biashara kama mahindi, mihogo, ndizi, kahawa, pamba, ni marufuku kulima bangi.

Pia Waziri Mkuu aliagiza kuchukuliwa hatua kwa wakandarasi waliotekeleza ujenzi wa maji mkoani Mara kwa sababu miradi hiyo wameijenga chini ya kiwango.

Waziri Mkuu aliyasema hayo baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kupitia mabango wakidai kutonufaika na miradi ya maji katika maeneo yao licha ya Serikali kutoa fedha.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu Asimamisha Uuzaji Wa Mali Za KNCU......Walitangaza Kuuza Shamba ili Benki Yao Isifungwe na Beki Kuu-BoT

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bibi Anna Mghwira asitishe uuzwaji wa mali za Chama cha Ushirika cha Kilimanjaro (KNCU).

Ametoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Januari 17, 2018) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Serengeti, wilayani Tarime.

Hatua hiyo imekuja baada ya KNCU kutangaza kuuza shamba lake kwa ajili ya kuiwezesha benki yake ya KCBL  kutimiza sharti la mtaji la Benku Kuu ya Tanzania (BoT).

Benki hiyo ya KCBL inatakiwa kutimiza sharti la kuwa na mtaji kamili unaotosha wa shilingi bilioni  tano (5) katika kipindi cha miezi sita tangu kutolewa kwa tangazo hilo.

Waziri Mkuu alisema ni marufuku kuuza mali za Ushirika huo, hususan katika kipindi hiki ambacho Serikali inafanya uhakiki wa mali za vyama mbalimbali vya Ushirika nchini.

Alisema Serikali imedhamiria kuimarisha Ushirika nchini na sasa inafanya uhakiki wa mali za vyama vya Ushirika na watakaobainika kuhusika na ubadhilifu watachukuliwa hatua.

Januari 4, 2018 BoT ilizipa miezi sita benki tatu ili ziweze kuongeza kiwango cha mtaji unaohitajika kutokana na matakwa ya kisheria ya kuwa na mtaji kamili wa kutosha.

Benki hizo ni Kilimanjaro Co-Operative Bank Limited, Tanzania Women Banki Plc na Tandahimba Community Bank Limited, zitakaposhindwa kutekeleza agizo zitachukuliwa hatua.

BoT ni itazifutia leseni na kusimamisha shughuli za kibenki chini ya ufilisi, iwapo benki hizo zitashindwa kutekeleza agizo hilo ihadi kufikia Juni 30, 2018.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ????

$
0
0
Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA 
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA 
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI 
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI 
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK 

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO 

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM,NAUTALETEWA POPOTE ULIPO.

 SIMU; NO 0767145357/0629034550.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Polisi yasema askari wa pikipiki marufuku kutoza faini

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema askari wanaotembea na pikipiki maarufu kama ‘tigo’ hawana mamlaka ya kutoza faini kwa mtu aliyevunja sheria za barabarani.

Amesema jukumu lao ni kumkamata aliyevunja sheria na kumpeleka kwa askari wa usalama barabarani.

“Niwasihi wananchi,  msikubali kutoa hela kwa hao askari hiyo itakuwa ni rushwa. Fedha unayompa inamfaidisha askari husika na familia yake. Jambo hili tunalipinga mno,” amesema Mambosasa leo Januari 18, 2018 katika kipindi cha 360 kinachorushwa na Redio Clouds.

Amesema kikosi hicho cha pikipiki hakikuanzishwa kwa ajili ya kukamata wanaovunja sheria barabarani na kuwatoza faini, kwamba askari wa usalama barabarani ndio wenye jukumu la kutoza faini na kutoa risiti.

“Kikosi cha pikipiki kilianzishwa kwa ajili ya kuangalia usalama na inapotokea kosa wanawajibika kumfikisha mhusika kwenye mamlaka inayosimamia usalama barabarani,” amesema.

Ametoa wito kwa askari wa usalama barabarani kutumia busara wakati wa kuteleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria.

“Tunaelekeza polisi asitafute makosa, asikusimamishe bila kujua kwanini amekusimamisha halafu anaanza kuhangaika kutafuta kosa. Tunaendelea kuwaeleza wenzetu kuwa busara inahitajika wakati wa kusimamia sheria,” amesema na kuongeza,

“Hawapaswi kuwaumiza watu. Askari unatakiwa kufikiria tu unamtoza faini mtu mchana kwa kuwa taa zake haziwaki sasa hapo anakuwa amefanya kosa gani maana ametembea mchana, labda ingekuwa usiku halafu taa haziwaki hapo sawa.

Mtu Mmoja Afarikii Dunia Baada ya Kuigonga Ndege ya Fastjet Jijini Mwanza

$
0
0
Mkazi mmoja wa mkoa wa Mwanza amefariki dunia baada ya kuigonga ndege ya Fastjet iliyokuwa ikiruka katika Uwanja wa Ndege Mwanza kuelelea jijini Dar es Salaam.

Kaimu MKurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Richard Mayongela amesema tukio hilo la aina yake limetokea jana usiku.

Amesema ndege hiyo ilikuwa njia moja kuelekea jijini Dar es Salaam, kubainisha kuwa mtu huyo ndiye aliyeigonga ndege hiyo.

“Ingawa ndege ndio ilimgonga mtu huyo ambaye jina lake hatulifahamu, kisheria mtu au kitu chochote kinachokuwa kwenye njia ya kurukia  na kutua ndege ndiyo kinahesabiwa kuigonga ndege. Ni kama ilivyo kwa treni,” amesema Mayongela.

Amesema kabla ya ndege hiyo kuruka,  taratibu zote za kiusalama zilifuatwa ikiwemo kukagua njia kujiridhisha hakuna kitu chochote.

“Haijulikani mtu huyo alitokea wapi. Vyombo vya ulinzi na usalama vipo eneo la tukio kuchunguza tukio hilo kwa kina na tutatoa taarifa kamili uchunguzi utakapokamilika,” amesema kaimu mkurugenzi huyo.

Amesema kitendo cha mtu huyo kuwepo katika njia ya kurukia ndege licha ya ukaguzi kufanyika kinawaumiza vichwa viongozi na wataalam wa usalama uwanjani hapo.

 “Pengine tatizo la muda mrefu la kukosa uzio tunaloanza kukabiliana nalo kwa ujenzi na upanuzi wa uwanja linaweza kuwa chanzo cha mtu huyo kuingia katika njia ya kurukia ndege,” amesema.

Ili kukabiliana na matukio ya aina hiyo, amesema wataimarisha mifumo ya usalama kwenye viwanja vya ndege nchini.

Dr. Mashinji Akanusha Kuugua Ghafla na Kupelekwa Amana

$
0
0
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk. Vincent Mashinji  amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa, ni mgonjwa na amelazwa katika Hospitali ya Amana.

Mashinji amesema taarifa hizo hazina ukweli wowote, yupo mzima wa afya na anaendelea na kikao cha Kamati Kuu katika Hoteli ya Bahari Beach. Amesema huenda kuna makosa kwa aliyemhusisha na kikao.

Taarifa hiyo ya uzushi iliyokuwa ikisambaa ilisema;
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk. Vincent Mashinji, ameugua ghafla na kukimbizwa katika Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk. Shani Mwaruka amethibitisha kumpokea Dk. Mashinji leo saa tano asubuhi akiwa mahututi ingawa amesema ni mapema mno kujua kinachomsumbua hadi hapo madaktari watakapotoa ripoti baada ya kumfanyia uchunguzi.

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amefika hospitalini hapo kumjulia hali Dk. Mashinji ambaye amelazwa katika chumba cha dharura.

Polisi Shinyanga wakamata bunduki aina ya AK47 yenye skafu ya CHADEMA

$
0
0
Na Kadama Malunde
Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata silaha ya kivita aina ya AK-47 iliyotupwa na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi waliokuwa wanataka kuvamia kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd kilichopo Nhelegani katika kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Alhamis Januari 18,2018 Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule amesema walikamata silaha hiyo usiku wa kuamkia leo majira ya saa tano eneo la Tinde wakati majambazi hao wanafuatiliwa na polisi ndipo wakaamua kutupa bunduki hiyo.

“Silaha hii aina ya AK-47 yenye namba 18116428 ilikuwa imefungwa kwenye skafu yenye rangi ya nembo ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ikiwa na risasi 25 ndani ya magazine yake na risasi zingine 8,zikiwa kwenye mfuko mdogo wa nailoni,” alieleza Kamanda Haule.

“Majambazi wawili pia walitelekeza pikipiki aina ya SANLG yenye namba za usajili MC 856 BPF,mafuta ya cherehani ya kulainishia silaha,tochi mbili na koti zito,” aliongeza.

Alisema jeshi la polisi lilipata taarifa za majambazi hao kutaka kuvamia kiwanda hicho kinachomilikiwa na raia wa China tangu tarehe 6.01.2018 kisha kuanza kuwafuatilia na kubaini kuwa baadhi yao ni wakazi wa Kahama na Ushirombo ambapo amewataka kujisalimisha polisi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha silaha aina ya AK-47 yenye namba 18116428 na mafuta ya kulainishia silaha yaliyotupwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Jielong
Bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428 iliyokuwa imefungwa kwenye skafu yenye rangi ya nembo ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) iliyotelekezwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Wachina mjini Shinyanga
Silaha na vifaa vilivyotelekezwa na majambazi 
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha skafu iliyotumika kufunga bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha bunduki aina ya AK-47 yenye namba 18116428 iliyotupwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Jielong
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha risasi zilizotelekezwa na majambazi
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha pikipiki aina ya SANLG yenye namba za usajili MC 856 BPF iliyotelekezwa na majambazi

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Novemba 19

Serikali Yafutia Usajili Meli Zilizokamatwa na Dawa za Kulevya......Makamu wa Rais Aagiza Kupitiwa Upya Usajili wa Meli Zote

$
0
0
Na: Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa agizo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba kuunda Kamati ya pamoja ya wataalam kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ili kupitia upya usajili wa meli nchini.

Makamu wa Rais ametoa agizo hilo mbele ya Waandishi wa Habari jana Jijini Dar es Salaam, alipokuwa akitoa ufafanuzi juu ya meli zilizokamatwa zikiwa na Bendera ya Tanzania.

Mhe. Samia amesema kuwa suala la usajili wa meli za nje ni la kawaida na linafanywa na nchi nyingi duniani hivyo Serikali inaendelea kushughulikia taarifa juu ya meli za nje zilizosajiliwa Tanzania zenye tuhuma za kusafirisha silaha na dawa za kulevya kwa sababu ni kinyume cha sheria za usajili wake.

“Kwa kuwa uendeshaji wa biashara hii unaonekana kuleta utata na kutia dosari kubwa kwa Taifa letu na kuharibu sifa njema kwa nchi yetu, tumeona ipo haja ya kuunda kamati ya pamoja ya wataalam kutoka Tanzania Bara na Zanzibar itakayoshirikisha vyombo vya ulinzi na usalama kwa ajili ya kupitia upya usajili uliokwishafanyika na kuzihakiki taarifa za meli zote zilizosajiliwa nchini mwetu, kuangalia mwenendo mzima wa usajili na hatimaye kutoa mapendekezo na ushauri kwa Serikali”, alielezaa Makamu wa Rais.

Kamati itakaundwa pia itapitia sheria za usajili wa meli ili kuzipa nguvu zaidi taasisi zinazosimamia usajili huo hivyo kamati itaangalia kwa makini kodi zinazotozwa na mchango wake nchini ili zisiwe kivutio kwa meli zisizokidhi viwango kuomba usajili Tanzania.

Aidha, Mhe. Samia amsema agizo lakupitiwa upya sharia za usajili wa meli baada ya kubainika kuwa wamiliki wa meli wanapenda kusajili meli zao nje ya nchi zao kukimbia ukubwa wa kodi na sheria zinazobana pia wakala aliyekuwa akifanya kazi hizo kwa niaba ya taasisi ya Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibar (ZMA) alishavunjiwa mkataba lakini bado anaendelea kufanya usajili kwa kuiba bendera ya Tanzania.

Amefafanua kuwa Sheria na Kanuni zote za usajili zinamlazimu mimiliki wa meli kujaza fomu ya kiapo cha kutovusha biashara za dawa za kulevya wala silaha kinyume na utaratibu hivyo Watanzania wanatakiwa kuelewa kuwa kukamatwa kwa meli hizo sio makosa ya Tanzania ila nchi inahusishwa kwa kuwa usajili wa meli hizo umefanyika Tanzania.

Meli mbili, Kaluba yenye namba za usajili IMO 6828753 na Andromeda yenye namba za usajili IMO 7614666 zilizosajiliwa Tanzania kupitia taasisi ya Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibar (ZMA) zilikamatwa kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya na silaha ambapo hadi sasa tayari zimeshachukuliwa hatua ya kufutiwa usajili.

Tanzania ina aina mbili za usajili wa meli ambao ni usajili wa meli zenye asili ya Tanzania na zisizo asili ya Tanzania, usajili huo ni kwa mujibu wa mkataba wa UNCLOS wa mwaka 1982 ambapo kila nchi imepewa haki ya kufanya usajili wa meli kwa kuzingatia mikataba ya kimataifa na sheria za nchi husika.

SUMATRA inaruhusu usajili wa meli zinazomilikiwa na Watanzania au kwa ubia kati ya Mtanzania na raia wa nchi nyingine ambapo jumla ya meli 88 zimesajiliwa wakati meli za kimataifa zinasajiliwa Tanzania kupitia Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibar (ZMA) ambazo hadi Disemba 31, 2017 jumla ya meli 457 za nje zimesajiliwa.

Waliosaini Mkataba Mbovu Mlimani City Kuhojiwa na Bunge ....Inadaiiwa Mwekezaji Alikuja na Sh. 150,000 tu

$
0
0
Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeutaka uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kurekebisha mkataba kati yake na kampuni ya Mlimani Holding Ltd kutokana na upungufu uliojitokeza, huku ikihoji sababu ya mwekezaji huyo kuja na mtaji wa Sh150,000 tu.

Wakizungumza katika kikao cha kamati hiyo kilichoketi eneo la Mlimani City jijinj Dar es Salaam leo Januari 18 wajumbe wa PAC walikosoa pia gawio la asilimia 10 la mapato yote kwa mwaka ambapo Mlimani  City wamekuwa wakikata gharama zao kabla ya kulipa.

Jambo la tatu lililolalamikiwa ni umri wa mkataba ambapo UDSM imetaka upunguzwe kutoka miaka 50 hadi miaka 35.

Mbunge wa Magomeni (CCM) Zanzibar, Jamal Kassim amehoji sababu za chuo hicho kumpokea mwekezaji akiwa na mtaji wa Sh150,000.

"Ukisoma mkataba huu utaona mtaji wa mwekezaji ni Sh150,000 yaani Dola 75. Maana yake mwekezaji hakuja na pesa bali alichukua pesa za upangishaji na kuzifanya kuwa mkopo na anajilipa riba ya mabilioni ya fedha," amesema Kassim.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Naghenjwa Kaboyoka amehoji: "Je, Chuo kikuu cha Dar es Salaam kilimkubalije mwekezaji mwenye mtaji wa Dola 75 tu? Dhamana ilikuwa nini?"

Hoja hiyo ilimwibua Mbunge wa CCM (Vijana)  , Khadija Naasir akihoji sababu ya mwekezaji huyo kutuma barua pepe kila anapotakiwa kutoa maelezo na UDSM.

Mbunge wa Ulanga Magharibi Dk Haji Mponda amesema mkataba huo ni mbovu kwa sababu umeshindwa kuna ardhi iliyopangishwa bila kutumika kwa muda mrefu.

Baada ya hoja za wabunge hao, Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo, Hilal Aeshi ameitaka kamati kuwaita watumishi wa UDSM walioshiriki kusaini mkataba huo ili wahojiwe na kuchukulia hatua.

"Kwa kuwa waliotia saini mkataba huo wapo, tuwaite Dodoma, wajieleze ili wachukuliwe hatua na Rais. Mimi nilikuwa mjumbe wa kamati ya madini ya Spika, tuliwaita waliohusika wakajieleza," amesema Aeshi.

Hata hivyo baadhi ya wabunge walitaka viongozi wa sasa wa UDSM  wajieleze kabla ya kuwaita wa zamani.

Tofauti na mtazamo wa wabunge hao, Naibu Makamu mkuu wa chuo hicho anayeshughulikia utawala, Profesa David Mfinanga amekiri kuwa mkataba huo una mapungufu na kwamba wana mgogoro na Mlimani Holding.

Mwanasheria wa Chuo hicho, Profesa Bonaventure Rutinwa amesema tangu alipoteuliwa alianza kuupitia mkataba huo.

"Tangu nilipoteuliwa mwaka jana nilifika ofisini kwa Profesa Rwekaza Mukandala nikamuomba vipaumbele vitano vya kisheria, mojawapo akaniambia ni kuupitia mkataba wa Mlimani," amesema Profesa Rutinwa.

Akifafanua zaidi, Kaimu Katibu wa Baraza la Chuo hicho, Dr Saudin Mwakaje alikiri kuwepo tatizo la mtaji na kwamba walishaiambia kamati hiyo.

Awali Mkurugenzi wa mipango na maendeleo wa chuo hicho, Pancras Pujuru amesema Mlimani Holding iliingia mkataba huo mwaka 2004 ukiwa katika sehemu mbili ambapo sehemu ya kwanza ulihusu kati yake na UDSM na sehemu ya pili ilikuwa kati yake na Serikali kupitia kituo cha

Vigogo KNCU Wahaha Kuikoa Benki Yao Isifungwe na BoT

$
0
0
SAA chache baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuagiza kusitishwa kwa mpango wa uuzaji shamba la Lerongo linalomilikiwa na Chama Kikuu cha Ushirika mkoani Kilimanjaro (KNCU), ili kuokoa benki yake isinyang'anywe leseni na kufungwa, vigogo wa chama hicho wanaumiza vichwa kutafuta njia mbadala.

Sasa bodi ya wakurugenzi ya KNCU inakutana leo kujadili katazo hilo na kutafuta mbinu mpya ya kuiwezesha Benki ya Ushirika Kilimanjaro (KCBL) kukidhi masharti ya hitaji la kisheria ya kufikisha mtaji wa Sh. bilioni tano.

Mwenyekiti wa KNCU, Aloyce Kitau alithibitisha jana kwamba tayari ameitisha kikao cha bodi ya wakurugenzi kujadili hatima ya KCBL baada ya Waziri Mkuu kusitisha mchakato wa kuuza ekari 581 za shamba la Lerongo lililopo Wilaya ya Siha.

"Kwa ujumla tume-paralize (tumepooza) baaada ya amri hiyo ya PM (Waziri Mkuu)," alisema Kitau kwa njia ya simu jana.

"Kwa jinsi hali ilivyo na masharti yaliyowekwa na Benki Kuu, nimeitisha kikao cha bodi ya wakurugenzi kesho (leo) kutafuta mbinu mpya za kuinusuru benki yetu ya KCBL kabla ya deadline (muda wa ukomo) haijapita.

"Unajua serikali ndio Mungu wa duniani kwa hiyo hatuwezi kubishana nayo, tumepokea taarifa hiyo na tunatafuta sasa plan B (namna nyingine) kukidhi takwa la kufikisha mtaji wa Sh.bilioni tano."

KCBL inakabiliwa na upungufu wa mtaji, tatizo ambalo hualika BoT kunyang'anya leseni na kufungia benki husika, ikiwamo tano kwa pamoja mwanzoni mwa mwezi huu.

Aidha, benki hiyo ambayo inamilikiwa na KNCU kwa asilimia 69, inahitaji kiasi cha Sh. bilioni tano, ili kufikisha mtaji wa Sh. bilioni 6.5 ulioelekezwa na BoT uwe umefikiwa hadi ifikapo Juni, mwaka huu.

Uamuzi wa kuuza shamba hilo ulitangazwa Jumanne na Mwenyekiti Kitau wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mkakati wa kuinusuru benki hiyo isifutiwe leseni.

Kitau aliwasihi wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro kuendelea kutumia benki hiyo kwani hadi kufikia Jumanne michakato yote na kibali cha kuuza shamba hilo ilikuwa imekamilika, na kwamba KCBL ingefikia mtaji husika kama inavyotakiwa kisheria mapema iwezekanavyo.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Tunde Lissu Sasa Anaweza Kutembea Mwenyewe, Kuoga

$
0
0
Afya ya Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, ambaye anaendelea na matibabu nchini Ubelgiji, inazidi kuimarika na sasa anaweza kufanya mambo mengi mwenyewe ikiwamo kwenda kuoga na kutembea kwa kutumia magongo.

Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), alipelekwa Ubelgiji Januari 7, mwaka huu, akitokea Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alipokuwa akipatiwa matibabu tangu Septemba 7, mwaka jana.

Mbunge huyo aliumia vibaya baada ya kushambuliwa kwa risasi 32 na watu wasiojulikana nyumbani kwake mjini Dodoma Septemba 7, mwaka jana, tano kati ya hizo zikimpata katika maeneo mbalimbali ya mwili.

Vinceti Mghwai, ambaye ni mdogo wa Lissu, alisema  jana kuwa Lissu ameanza kutembea mwenyewe kwa kutumia magongo na kujipatia huduma mbalimbali ikiwemo kwenda kuoga bila msaada wa mtu mwingine.

"Tunamshukuru Mungu sana, Lissu anaendelea vizuri... tangu ameanza kupatiwa matibabu na mazoezi ya viungo tunaona mabadiliko makubwa mno," alisema na kueleza zaidi:

"Maendeleo ni makubwa sana, kuna vitu alikuwa hawezi kuvifanya lakini sasa anaweza kuvifanya mwenyewe kama kuoga. Siku za nyuma alikuwa akipelekwa maliwatoni lakini sasa hivi anatembea na magongo mwenyewe kwa kukanyagia mguu chini.

"Anakula mwenyewe.Tunaamini atatengamaa mapema zaidi, (na) haya kwetu ni maendeleo makubwa."

Mghwai alisema Lissu anapata muda mwingi wa kupumzika na huenda hiyo ndiyo ikawa sababu kubwa ya yeye kuendelea kupona haraka kutokana na kupatiwa matibabu na bila usumbufu wowote.

Alisema Lissu anapata matibabu katika mazingira tulivu tofauti na alipokuwa Hospitali ya Nairobi ambako alikuwa akisumbuliwa na makundi ya watu waliokuwa wakienda kumjulia hali.

"Kwa sasa ana muda wa kutosha kufanyiwa matibabu ya mazoezi, madaktari wanamfanyia mazoezi muda wote kwa sababu hakuna watu wanaokwenda kumuona na ndiyo sababu anaendelea kupona haraka," alisema Mghwai.

"Ubelgiji muda wote yuko na madaktari akipatiwa matibabu hasa mazoezi ya viungo... huku ni kazi kazi tu. Na madaktari waliahidi kufanya kazi.

"Kule Nairobi wakati mwingine alikuwa akiwaambia madaktari wamuache pale anaposikia maumivu wakati wa mazoezi lakini sasa hakuna kitu kama hicho na wamemwambia avumilie apone."

Kuhusu risasi iliyobakia kwenye nyonga, Mghwai alisema madaktari wa Ubelgiji hawataitoa na wataiacha kwa sababu walishaeleza kuwa haiwezi kuwa na madhara kwake kiafya.

"Kule Ubelgiji kazi kubwa ni kumfanyisha mazoezi ili sasa aweze kurejea katika hali yake na ndicho ambacho wanaendelea nacho na kwa kweli tumeanza kuona maendeleo makubwa."

Kuhusu gharama za matibabu, Mghwai alisema, zaidi ya Sh. milioni 100 zinatumika kila mwezi kwa ajili ya kumtibu na kwamba hadi sasa Bunge halijatoa fedha na familia inafuatilia lakini wamekuwa wakizungushwa huku na kule.

Alisema fedha zinazotumika kwa ajili ya matibabu yake ni zile zilizochangwa na wadau mbalimbali na wamekuwa wakifanya harambee kadhaa za kuchangia.

"Gharama ni kubwa sana kwa mwezi analipia zaidi ya milioni 100 katika hospitali hiyo na kama atakaa miezi miwili tutatumia zaidi ya milioni 200 na hizi ni fedha za matibabu pekee," alisema Mghwai.

Alieleza zaidi kuwa fedha zilizochangwa hazitoshi kumtibu Lissu na kwamba kwa sasa wadau wamesitisha kutoa michango baada ya tetesi kuwa serikali inagharamia matibabu yake.

Alisema familia inaendelea na juhudi za kuchangisha fedha zaidi ili kukamilisha matibabu yake.

"Tunaamini hakuna kitakachoharibika kwa sababu tumeshaweza kumponya tunaamini atakuwa mzima."

Alisema gharama kamili za matibabu na fedha zilizopatikana kwa ajili ya matibabu ya Lissu zinaweza kuzungumzwa katika vikao vya makubaliano na si yeye peke yake kuzungumzia.

Lissu ambaye Januari 6 alizungumza na waandishi wa habari akiwa nje ya Hospitali ya Nairobi, ikiwa ni siku moja kabla ya kusafiri kuelekea nchini Ubelgiji, alieleza kuwa alishambuliwa kwa risasi zaidi ya 20 na 16 zilimjeruhi maeneo mbalimbali ya miguu, mikononi na kwenye nyonga.

Lissu alisema kutokana na shambulio hilo alifanyiwa operesheni 17 zilizofanikisha kuondoa risasi saba zilizoingia mwilini huku risasi moja ikisalia.

Wataalam wa afya walimshauri kuiacha risasi hiyo iliyopo kwenye nyonga wakisema kuwa inaweza kuleta madhara zaidi kama watajaribu kuitoa.

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kutoa Michirizi, Kuondoa Chunusi, Kuongeza Maumbilie na Nguvu za Kiume

$
0
0
BIDHAA MPYA 2018
  Ktk kusajiliwa kwa kampuni ya  @natural_beauty_prod
     Bidhaa hizi MPYA zimefanyiwa maboresho makubwa zaidi hivyo zina matokeo ya haraka kuliko ilivyokua awali. 
    Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda hazina kemiko wala madhara kwa mtumiaji mtumiaji yoyote.
        🍇Zimethibitishwa kiafya🍇
               NI PAMOJA NA  HIZI👇
1.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaj) @200,000/=
2.Kurefusha nywele @130,000/=
3.Kuongeza urefu na upana wa uume kwa size uipendayo @230,000/=
4.Kung'arisha mwili mzima na kuondoa sugu @150,000/=
5.punguza unene na manyama uzembe @180,000/=
6.Kuongeza nguvu za kiume  hata kwa mwenye kisukari (diabetic) @180,000/=
7.Kuondoa mvi moja kwa moja na zisiludi tena milele @150,000/=
8.Kuongeza unene, uzito na hamu ya kula @150,000/=
9.Kutengeneza miguu (Chupa ya bia) na kuondoa kigimbi @150,000/=
10.Kubana uke na kuondoa uchafu @150,000/=
11.Kuongeza au Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @140,000/=
12.Kuondoa michirizi ya uzazi  au unene @130,000/=
N.K 
    NB: MATOKEO NI UHAKIKA NA GARANTII NA HAKIKISHA UNAPATA RISITI YENYE MUHURI HALISI WA NATURAL BEAUTY
    Wasiliana nasi kwa no
         (+255) 0759029968
                0659618585
  Popote ulipo utapata huduma
   Follow us on
GOOGLE👉 natural beauty
INSTAGRAM@natural_beauty_prod
YOU TUBE 👉natural beauty
          <<WELCOME ALL>>

Mtoto wa miaka 11 Ajinyonga

$
0
0
Mtoto mwenye umri wa miaka kumi na moja amekutwa akiwa amejinyonga katika eneo la Ongata Rongai  Kenya katika mazingira ya kutatanisha.

Mtoto huyo wa kiume ambaye alikuwa akiishi na mama yake pamoja na mdogo wake wa kike alikutwa juzi jioni akiwa ananing’inia kwenye kamba.

Tukio hilo lilibainika baada ya mdogo wake huyo mwenye umri wa miaka sita kurejea nyumbani na kukuta mlango ukiwa umefungwa kwa ndani na jitihada zake za kujaribu kufungua na kuita hazikufanikiwa kwani hapakuwa na mtu aliyeitikia.

Kutokana na kugonga mlango na kuita kwa muda mrefu, majirani akiwamo mwenye nyumba walikwenda kumsaidia na walikubaliana kwamba waondoe chuma kilichokuwa katika mlango ili kumwezesha binti kuingia ndani na kumkuta kaka yake akiwa ananing’inia kwenye kamba.

Majirani hao walitoa taarifa katika kituo cha Polisi Rongai ambao walifika na kuchukua mwili wa marehemu na kuuhifadhi katika chumba cha kuhifadhia maiti cha jiji huku wakiendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Waziri Mkuu Aubeba Mgogoro wa Nyamongo

$
0
0
Mapokezi ya mabango yaliyobebwa na wananchi wa eneo la Nyamongo wilayani hapa, yamesababisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kujitwisha mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 15 kati ya wakazi hao na Mgodi wa Dhahabu Acacia North Mara.

Serikali imeahidi kutatua mgogoro huo kati ya mgodi na wananchi wanaozunguka eneo hilo, ili kumaliza uhasama na kurejesha amani kati ya makundi hayo mawili yanayohasimiana kwa kipindi kirefu.

Ahadi hiyo ilitolewa jana na Majaliwa alipotembelea eneo la Nyamongo wilayani Tarime katika ziara yake ya siku saba inayoendelea mkoani Mara.

Hiyo ni baada ya kupokewa na mabango aliyosema hayapungui 400 alipofika eneo la Nyamongo, jambo alilosema ni ishara tosha ya kuwapo tatizo linalowachukiza wananchi linalohitaji ufumbuzi wa Serikali na viongozi wa ngazi zote.

Kikao cha kwanza cha kujadili na kutafutia ufumbuzi mgogoro huo kitakachohusisha wajumbe watano wa watakaowakilisha wananchi, uongozi wa mgodi, mbunge wa Tarime vijijini (John Heche) na wataalami wa Wizara ya Madini kitanatarajiwa kufanyika mjini Dodoma Januari 27.

Mambo muhimu yatakayojadiliwa na kupatiwa ufumbuzi kwa mujibu wa Waziri Mkuu ni malipo ya fidia kwa mali ya wananchi, maeneo ya uchimbaji kwa wachimbaji wadogo, upatikanaji wa mawe (mabaki) ya dhahabu maarufu kama magwangala.

Mengine ni upatikanaji wa maji safi na salama eneo la Nyamongo (vyanzo vya maji vya asili vinadaiwa kuchafuliwa na kemikali), na udhibiti wa matumizi ya nguvu kupita kiasi, ikiwamo kupiga mabomu ya machozi na risasi panapotokea mgogoro au vurugu kati ya wananchi na mwekezaji.

“Nimepokewa na mabango tangu nianze ziara mkoani Mara Januari 15; lakini mabango ya Nyamongo yametisha. Hayapungui 400 na yote yanaonyesha uhusiano mbaya kati yenu (wananchi) na mwekezaji. Nitalibeba hili na kulimaliza,” alisema Majaliwa akiamsha shangwe na nderemo kutoka kwa wananchi.

Licha ya amani na utulivu eneo la Nyamongo, uamuzi huo wa Serikali pia unalenga kuondoa kuviziana kati ya wananchi na vyombo vya dola vinavyotumika kudhibiti na kurejesha amani na utulivu nyakati za uvamizi unaofanywa na makundi ya watu, hasa vijana wanaoingia eneo la mgodi kuchukua mawe au mchanga wa dhahabu.

“Mgogoro huu unakwamisha juhudi za wananchi, Serikali na wawekezaji katika kujiletea maendeleo kupitia rasilimali ya madini yanayopatikana Nyamongo, lazima tuutafutie ufumbuzi wa kudumu kwa faida na masilahi ya pande zote,” alisema Majaliwa.

Alisema yeye binafsi ataongoza mazungumzo ya kutatua mgogoro huo hadi mwafaka utakapopatikana na kuagiza pande zote kuunga mkono juhudi hizo kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu huku maslahi na maendeleo ya wananchi yakipewa kipaumbele.

Awali, mbunge wa Tarime vijijini, John Heche alimweleza Majaliwa kuwa uhasama kati ya wananchi na wawekezaji, kukosekana kwa huduma bora za kijamii kulinganisha na ya utajiri wa madini eneo hilo na matumizi ya nguvu ya vyombo vya dola dhidi ya wakazi kwa faida ya mwekezaji bila kujali uhalali wa madai ya wenyeji ni miongoni mwa changamoto zinazowakabiliwa wakazi wa Nyamongo.

Ajali ya gari la Polisi (FFU) Yaua Polisi Wawili na Kujeruhi 9

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kukabiliana na vitendo vya uhalifu pamoja na ajali za barabarani ili kuhakikisha kuwa wakazi wa Mkoa huu wanaendelea kuwa salama na mali zao. Hata hivyo kwa siku ya jana kumekuwa na ajali 01 ya barabarani kama ifuatavyo:-

Mnamo tarehe 18.01.2018 majira ya saa 16:45 jioni huko eneo la Iwambi, Kata ya Iwambi, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya katika barabara kuu ya Mbeya kwenda Tunduma, Gari yenye namba za usajili PT 2079 Toyota Land Rover mali ya Jeshi la Polisi Kikosi cha FFU – Mbeya  ikiendeshwa na askari namba G. 3452 PC ADAM [30] Mkazi wa Iganzo ikitokea Mbeya Mjini kuelekea Mbalizi iliacha njia na kupinduka kisha kusababisha vifo kwa askari wawili ambao ni 1. H. 4335 PC MATHEW JAILOS MPOGOLE [26] na 2. H. 1215 PC PROSPER JORDAN CHALAMILA [29].

Aidha katika ajali hiyo, askari 09 walijeruhiwa ambapo kati yao majeruhi wawili wamelazwa Hospitali ya Rufaa Mbeya na majeruhi saba wametibiwa na kuruhusiwa. Waliolazwa ni 1. H. 6952 PC KELVIN MARTIN [28] Mkazi wa forest ameumia kichwani na 2. G. 3452 PC ADAM [30] Mkazi wa Iganzo, Dereva.

Aidha majeruhi wengine waliotibiwa na kuruhusiwa ni 1. H. 3929 PC LEONARD MICHAEL [26] ambaye ameumia mkono wa kushoto, 2. H. 469 PC FREDY MBANDE [28] ambaye ameumia mgongoni, 3. H. 948 PC DAVID IBRAHIM [27] ambaye amepata maumivu mwilini, 4. G. 9588 PC MARWA [29] ambaye amepata maumivu mwilini, 5. H. 1325 PC CHRISTOPHER DANIEL MSANGI [26] ambaye ameumia mbavu, 6. H. 6789 PC LUCAS ANDREA MASHALA, [24] ambaye ameumia kichwani na mbavu upande wa kulia na 7. G. 6849 PC HAMIS ALLY [32] ambaye amevunjika mkono wa kulia.

Chanzo cha ajali ni mwendokasi akijaribu kuyapita magari mengine pamoja na utelezi katika barabara. Upelelezi unaendelea. Miili ya marehemu imehifadhiwa Hospitali ya Rufaa Mbeya na majeruhi wamelazwa Hospitalini hapo. Taratibu za kusafirisha miili ya marehemu kwenda nyumbani kwao Iringa zinafanyika.

WITO:
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi MOHAMMED R. MPINGA anatoa wito kuwa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha madereva kuzingatia udereva wa kujihami hasa kutokana na utelezi na kujiepusha na uendeshaji wa mwendo kasi. Aidha Kamanda MPINGA anatoa rai kwa madereva  kuzingatia sheria na kanuni zote za usalama barabarani.

        Imesainiwa na:        
[MOHAMMED R. MPINGA – DCP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA

Simba Yamtambulisha kocha mpya

$
0
0
Kocha Mkuu mpya wa Simba, Mfaransa Pierre Lechantre, amekishuhudia kikosi chake kikiibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Singida United katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana.

Katika ushindi huo uliochangiwa na Mganda Emmanuel Okwi aliyetokea benchi na kutupia mawili katika kipindi cha pili, Simba ilicheza kwa kujiamini zaidi ya wageni hao.

Lechantre, ambaye alitangazwa rasmi jana kuwa Kocha Mkuu wa Simba, ni wa kiwango cha juu, na haijawahi kutokea kwa klabu za hapa nchini kunasa kocha wa kiwango hicho katika kipindi cha hivi karibuni, imefahamika.

Lechantre ambaye aliwasili nchini juzi usiku na kuanza mazungumzo na viongozi wa klabu hiyo ambayo jana mchana yalifikia tamati baada ya kukubaliana, sasa anazima tetesi za majina kibao ya makocha waliokuwa wakihusishwa kupewa mikoba ya Mcameroon Joseph Omog.

Moja ya sifa kubwa ya kocha huyo katika kipindi cha hivi karibuni ni pamoja na kuinoa timu ya Taifa ya Congo mwaka 2016, ambayo imekata tiketi ya kushiriki fainali zijazo za Kombe la Dunia zitakazofanyika Urusi baadaye mwaka huu, na sasa amepewa mikoba ya kuiongoza Simba baada ya viongozi wa klabu hiyo kuamua kuachana na Mbrazil Fabio Lopez, aliyeko nchini tangu Jumanne.

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara, jana alisema Lechantre atasaidiwa na Mrundi Masoud Djuma, ambaye alikuwa akikaimu nafasi hiyo baada ya kuondoka kwa Omog.

Manara alisema Lechantre amefuatana na kocha wa viungo, Mohammed Aymen, raia wa Morocco na baada ya kufikia makubaliano, wanatarajia kukamilisha taratibu za kupata kibali na hatimaye Mfaransa huyo aweze kuanza kazi yake mapema.

Sifa nyingine ya Lechantre, ni kwamba analifahamu vema soka la Afrika, kwani aliwahi kuiongoza Cameroon kuchukua ubingwa wa Afrika mwaka 2000 huku klabu alizowahi kuzifundisha ni pamoja na Al Ittihad ya Libya, Al Arabi (Qatar), CS Sfaxien na Club Africaine zote za Tunisia.

Mbali na kuiongoza Simba kuwania taji la Ligi Kuu Tanzania Bara ambalo linashikiliwa na Yanga, Mfaransa huyo atatakiwa kuhakikisha ‘Wekundu wa Msimbazi’ hao wanaodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, wanafanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho Afrika yatakayoanza mapema mwezi ujao.

Mpango mkakati wa kuiokoa Dar na mafuriko waja

$
0
0
Makamu wa Rais, Samia Suluhu amewataka viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam kuanzia ngazi za wilaya, halmashauri kuwa na mpango mmoja wa kuboresha mazingira ili kujikinga na maafa yatakayotokana na mvua hasa mafuriko.

Mama Samia amesema hayo leo Ijumaa wakati akifungua mkutano unaokutanisha wadau wa mazingira wa jiji hili ambao una lengo la kuja na mpango kazi wa kuondoa majanga hasa mafuriko.

Mkutano huo ambao umeudhuriwa na viongozi na mawaziri mbalimbali akiwamo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na wakuu wa wilaya.

Samia amesema katika maafa yanayotokea katika jiji la Dar es Salaam kumekuwa na mipango tofauti katika wilaya zote jambo ambalo sio sawa kwani lazima kuwe na mkakati wa kunusuru jiji zima.

"Lazima tuwe na mkakati kabambe wa kufanya usafi wa mifereji na hatuwezi kusubiri maafa ndio tuanze kufanya kazi ya uokoaji sio sawa kabisa," amesema Samia.

Katika mkutano huo ambao mwenyekiti wake ni Makamba amesema kikao hicho kitatoka na azimio moja katika kukabiliana na majanga hayo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images