Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Benki Yaamua Kuuza Shamba Lake Kujinasua kufungiwa na Benki Kuu (BoT)

$
0
0
Chama Kikuu cha Ushirika mkoani Kilimanjaro (KNCU), kimejitwisha jukumu la kuinusuru Benki ya Ushirika ya KCBL isinyang'anywe leseni na kufungiwa na Benki Kuu (BoT), kwa kuamua kuuza ekari 581 za Shamba la Lerongo.

KCBL inakabiliwa na upungufu wa mtaji, tatizo ambalo hualika BoT kunyang'anya leseni na kufungia benki husika, ikiwamo tano kwa pamoja mwanzoni mwa mwezi huu.

Aidha, benki hiyo ambayo inamilikiwa na KNCU kwa asilimia 69, inahitaji kiasi cha Sh. bilioni tano ili kufikisha mtaji wa Sh. bilioni 6.5 ulioelekezwa na BoT uwe umefikiwa hadi ifikapo Juni, mwaka huu.

Uamuzi wa kuuza shamba hilo ulitangazwa jana na Mwenyekiti wa KNCU, Aloyce Kitau, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mkakati wa kuinusuru benki hiyo isifutiwe leseni.

“Baada ya kupokea taarifa juu ya upungufu wa mtaji wa kuendesha benki yetu ya ushirika, wanachama wa KNCU (1984) Ltd, waliridhia kuuza moja ya mali zake na fedha itakayopatikana iongezwe kwenye mtaji wa benki hiyo ili ifikie kiasi hitajika cha mtaji kama ilivyoelekezwa na Benki Kuu,” alisema Kitau.

Shamba la Lerongo lililowekwa sokoni kwa sasa na ambalo bado zabuni yake haijatangazwa hata hivyo, lipo katika wilaya ya Siha.

Kitau aliwasihi wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro kuendelea kutumia benki hiyo kwani hadi kufikia jana michakato yote na kibali cha kuuza shamba hilo ilikua imekamilika, na kwamba KCBL itafikia mtaji husika kama inavyotakiwa kisheria mapema iwezekanavyo.

Wakati huo huo, taarifa iliyotolewa kwa umma jana na makamu mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya KCBL, Tumaini Yarumba ilisema benki hiyo itatimiza vigezo vyote vya kuwa na mtaji hitajika kufikia Juni.Kwa mujibu wa Yarumba, Benki Kuu iliitaka KCBL kuhakikisha inaendelea kutoa huduma kwa wananchi wote wa mkoa wa Kilimanjaro.

Taarifa hiyo inakwenda sambamba na tangazo la BoT la Januari 9, mwaka huu linalotaka wananchi kuwa na imani kwa sekta ya kibenki nchini kuwa iko imara na tayari kuwahudumia Watanzania wote kwa ukaribu.

Akitoa ufafanuzi kuhusu umiliki wa benki hiyo, Meneja wa KCBL, Joseph Kingazi alisema benki hiyo ya ushirika ina wanahisa 245 ambao ni Vyama vya Ushirika wa Mazao (Amcos), Vyama vya Ushirika vya Akiba na Mikopo (Saccos) pamoja na watu binafsi.

KCBL iliyoanzishwa miaka 20 iliyopita, ndiyo benki ya kwanza ya ushirika nchini kufunguliwa na Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na ndio waanzilishi wa mfumo wa stakabadhi ghalani.


Rais Magufuli Akutana na Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo Na Kupiga Marufuku Michango Yote Shuleni

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Januari 17, 2018 amepiga marufuku aina yoyote ya michango katika shule za Serikali za msingi na Sekondari na kuwaagiza Mawaziri Jafo na Ndalichako kusimamia hilo.

Magufuli amepiga marufuku hiyo hiyo leo alipokutana na Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani S. Jafo na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce L. Ndalichako Ikulu jijini Dar es salaam na kuwataka mawaziri hao kwenda kusimamia jambo hilo na kuhakikisha hakuna michango yoyote wanafunzi au wazazi wanachangishwa kwenye shule za sekondari. 

"Tumesema elimu bure,  haiwezi ikaja kwa mgongo mwingine ikawa elimu pesa . Tumeweka utaratibu kwamba kuanzia shule ya msingi mpka sekondari form four hakuna kulipa ada yoyote lakini sasa hivi michango ya kila aina, nimewapa maelekezo kwamba kuanzia leo iwe ni marufuku na wakalisimamie hili sitaki kusikia mwanachi yoyote mahali popote akilalamika kwamba mtoto wake amerudishwa shule kwa sababu ya michango na walimu wote popote walipo wasishike mchango wowote wa mwanafunzi" amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amesema kuwa kama kutakuwepo na mchango wowote wa mzazi ambaye atajisikia kuchangia jambo lolote kuhusu masuala ya shule basi pesa hizo zipelekwe kwa Mkurugenzi na si kushikwa na mwalimu yoyote yule 

VIDEO: Msikilize Rais Magufuli Akipiga Marufuku Michango Yote Shuleni

$
0
0
Rais Dkt. John Magufuli leo Januari 17, 2018 amepiga marufuku aina yoyote ya michango katika shule za Serikali za msingi na Sekondari na kuwaagiza waziri Suleiman Jaffo na Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako kusimamia hilo.

==Msikilize hapo chini

Kiongozi wa CCM achomewa nyumba

$
0
0
Nyumba ya Katibu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wa Mkoa wa Iringa, Alphonce Muyinga iliyopo maeneo ya Kihesa njiapanda ya Kwabeda imechomwa moto na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo.

Ambapo kikosi cha Zima Moto kilifanikiwa kufika katika nyumba hiyo na kujaribu kuzima moto huo ambao tayari ulikuwa umeshaleta athari ndani ya nyumba hiyo kwa mali mbalimbali zilizokuwepo ndani.

Pia aliyekuwa Diwani wa kata ya Mwangata, Iringa kwa tiketi ya Chadema na baadaye kujiuzulu nafasi yake hiyo, Anjelus Mbogo naye amefanyiwa uharibifu katika nyumba ambayo alikuwa akijenga baada ya watu wasiojulikana kuibomoa nyumba hiyo.

Anjelus amedai kuwa tukio hilo linawezekana kuwa limetokea kutokana na matamko ya uchochezi yaliyotolewa na Mbunge kwa wananchi.

“Kauli ya Mbunge ndiyo inaweza kuwa chanzo cha uchochezi kwa wananchi kuja kubomoa nyumba hizi kwa sababu yeye aliwaambia wananchi kama atajiuzulu wabomoe nyumba yake hata gari yake ichomwe moto nadhani wananchi wakachukua hilo kwani wananchi unapowashawishi ndivyo unavyomuaminisha kuja kufanya hivi huo ndiyo ukweli. Na mimi sisemi mambo mengi kwa kuwa jambo hilo bado linaendelea na upelelezi lakini naamini wameniaminisha kuwa hatabaki mtu” amesema Anjelus Mbogo

Aidha amesema hawezi kuongea mengi zaidi kwani swala hilo linafanyiwa upelelezi kubaini watu hao wasiojulikana.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhhamisi ya January 18

Serikali yaanza mazungumzo na kampuni ya Tanzanite One

$
0
0
Kamati iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuchunguza biashara ya madini ya Tanzanite imeanza kufanya mazungumzo na kampuni ya Tanzanite One.

Tiba Asili ya Kuondoa Michirizi,Tumbo Kujaa Gesi, Maumivu ya Mgongo na Nguvu za Kiume

$
0
0
JE, UNA DALILI HIZI? (Kushindwa kurudia tendo la ndoa)
(Kutojiskia hamu ya tendo la ndoa)
(Maumivu ya kiuno mgongo)
(Tumbo kuunguruma na kujaa ges)
(Uume kusinyaa na kuingia ndan na kuwa mdogo au mfupi)
(Korodani moja kuvimba)
Kama dalili hizi unazo upo kwenye hatari ya kuishiwa nguvu za kiume kabisa,kwa matibabu tumia OZYMIX POWER dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikal ambayo itakuwezesha kurudia tendo LA ndo zaidi ya Mara tatu bila hamu kuisha
PIA KUNA DAWA YA KUNENEPESHA NA KUREFUSHA MAUMBILE YA KIUME

DAWA ZA KIKE ZA KUTENGENEZA SHEPU
(Kusimamisha maziwa yaliyolala)
(Kuongeza makalio)
(Kuondoa michirizi)
(Kumrudisha mwanaume aliekuacha au Asie kupa hela)
KWA MAWASILIANO ZAIDI
0716096205 au FIKA OFISIN au piga simu utaletewa dawa popote ulipo daresalam KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI

Rais Magufuli ateua Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

Finland yaonesha nia kuwekeza sekta ya nishati nchini

$
0
0
Ujumbe kutoka Kampuni ya Fortum ya Finland umemtembelea Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani na kueleza nia yao kuwekeza kwenye sekta ya nishati nchini.

Ujumbe huo ukiongozwa na Balozi wa Finland nchini Tanzania, Pekka Hukka, ulimtembelea Waziri ofisini kwake mjini Dodoma, Januari 16 mwaka huu.

Akiwatambulisha maafisa aliombatana nao, Balozi Hukka alisema ni wawakilishi kutoka Kampuni ya Fortum inayotoa huduma za nishati ya umeme nchini Finland, ambayo hisa zake nyingi zinamilikiwa na Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi yenye hisa chache.

“Tunatambua umuhimu wa sekta ya nishati katika kuleta maendeleo hususan katika kuwezesha uchumi wa viwanda, ndiyo maana tungependa kuwekeza katika sekta hii,” alisema Balozi Hukka.

Kwa upande wake, Waziri Kalemani aliueleza Ujumbe huo kuwa Serikali ingali inahitaji wawekezaji makini katika sekta ya nishati hususan katika uzalishaji na usambazaji wa umeme.

“Kiasi cha umeme tulichonacho kwa sasa kinaweza kuonekana kutosheleza mahitaji yetu lakini tunajipanga kuzalisha umeme zaidi kwani mahitaji yanazidi kuongezeka siku hadi siku.”

Waziri aliongeza kufafanua kuwa, umeme mwingi zaidi unahitajika hususan kipindi hiki ambapo Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuhakikisha nchi inaingia kwenye uchumi wa viwanda.

Aliwataka wawekezaji hao kukutana na wataalam kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ili kujadiliana na kuainisha maeneo mahsusi yanayohitaji uwekezaji.

Hata hivyo, Waziri aliainisha baadhi ya maeneo muhimu ya sekta ya nishati ambayo yanahitaji uwekezaji kwa sasa ambayo alisema ni pamoja na njia ya kusafirisha umeme wa kilovolti 400 kutoka SomangaFungu hadi Dar es Salaam.

Nyingine ni uzalishaji wa umeme kwa kutumia makaa ya mawe. “Tunayo hazina ya kutosha ya makaa ya mawe huko Magharibi mwa nchi yetu. Hii pia ni fursa nyingine nzuri ya uwekezaji,” alisisitiza.

Serikali kupitia Wizara ya Nishati imeendelea kuweka mikakati madhubuti inayolenga kuongeza uzalishaji wa umeme na usambazaji katika maeneo yote nchini.

CCM Yazidi Kuwasomba Wapiinzani....Yazoa Wengine 36

$
0
0
Viongozi 17 wa ACT- WAZALENDO na 19 wa CHADEMA wa ngazi mbalimbali wakiwemo wajumbe wa Kamati kuu, Wenyeviti  na Makatibu wa mikoa, wilaya na kata kutoka mikoa mbalimbali wamevihama vyama vyao na kujiunga na CCM  tarehe 17 Januari 2018 katika  Mkutano wa Halmashauri  Kuu ya CCM Mkoa wa Kilimanjaro. Viongozi hao wamepokelewa na Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi wa CCM Ndugu Humphrey Polepole.

Maamuzi ya viongozi hao yametokana na kile wanachodai kuwa vyama vyao vimehama kutoka kuwa taasisi za umma na kuwa kampuni za watu binafsi na wapambe wao, aidha, viongozi hao wamekiri kuridhishwa na kazi nzuri inayofanywa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Awamu ya Tano na wameguswa na Mageuzi makubwa yanayofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kipindi hiki.

Mmoja wa viongozi hao, aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha ACT Wazalendo, Ndugu Kansa Mohammed Mbaruku amefafanua kuwa maamuzi hayo ya kukihama chama cha ACT na kujiunga na CCM ni kutokana kuwepo na  ugonjwa mkubwa sana uliyopo kwenye vyama vya upinzani, wa kutokutembea kwenye maneno na misingi yake, vinasema ni vyama vya kidemokrasia ila havina demokrasia kabisa na mambo mengi yanakwenda kinyume na misingi ya uanzishwaji wa vyama hivi na jambo hili linawakatisha tamaa wanachama wengi wa vyama hivi

Akizungumza kwa niaba ya wanachama wa Chadema waliohamia CCM, aliyekuwa Katibu Mwenezi wa Wilaya ya Siha, Ndg. Daniel Nkini amesema wamegundua Chama cha Mapinduzi katika masuala ya maendeleo hakibagui wananchi tofauti na ambavyo vyama vingine vimekuwa vikitenda.

Katibu wa Itikadi na Uenezi ambaye ndio alikuwa mgeni rasmi amewapokea viongozi hao waliokuwa wa vyama vya upinzani, amewahakikishia wamefanya uamuzi sahihi, wamechagua upande mzuri na washirikiane na wanachama wengine wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukijenga chama na nchi ya Tanzania.

Ndugu Polepole amewaapisha wanachama hao, Katika kiapo cha Imani na Ahadi za mwanachama wa CCM na akisisitiza umuhimu wa wanachama wapya na wale wazamani kujengeka kiitikadi na kiimani ya Chama na kuishi sawasawa na Imani, Itikadi na Ahadi za mwana CCM huku akinukuu usemi maarufu wa “Imani bila matendo imekufa”.

Huu ni muendelezo wa mamilioni ya watanzania wanaojiunga na CCM na mamia ya viongozi wa vyama vya upinzani kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika awamu hii ya tano chini ya uongozi wa Ndugu John Pombe Joseph Magufuli Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Imetolewa na,
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
MOSHI, KILIMANJARO

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Katibu UVCCM Iringa Mjini Asimulia Alivyonusurika Kufa Baada ya Nyumba Yake Kulipuliwa na Watu Wasiojulikana

$
0
0
KATIBU wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM), Alophance Myunga amenusurika kifo baada ya kitu chenye mlipuko kurushwa dirishani kwake na kufikia kitandani huku yeye akiwa amelela na kisha kusababisha moto ulioteketeza nyumba anayoishi yote.

Amesema kutokana na kurushwa kwa kitu hicho ambacho kilisababisha mlipuko mkubwa chumbani kwake na kisha moto kuanza kuwaka alichofanikiwa ni kuchukua simu yake ya mkononi tu huku vitu vingine vyote vikiteketea kwa moto.

 Myunga amesema yeye ni moja kati ya wapangaji saba wanaoishi kwenye nyumba ambayo wanaishi na chumba ambacho kilianza kuwaka moto ni cha kwake.

Katibu huyo wa UVCCM Wilaya ya Iringa amesema kuwa kwenye mida ya saa saba usiku akiwa amelala chumbani kwake alisikia dirisha lililopo chumbani kwake likivunjwa.Hata hivyo aliogopa kuchungulia kwani hakujua wanaofanya hivyo wanalengo gani dhidi yake.

Ameongeza wakati anaendelea kutafakari huku akiwa bado yupo kwenye kitanda chake alishangaa kuona amerushiwa kitu ambacho hawezi kukielezea ni cha aina gani lakini ghafla kikaangukia chini na kusababisha kulipuka na moto kuanza kuwaka.

“Naogopa kusema ni kitu aina ya bomu au laa.Maana si mtaalamu wa kutambua aina ya kitu ambacho kimerushwa chumbani.Niseme tu baada ya kitu hicho kurushwa kitandani na kudondokea chini, moto ukaanza kufuka na kisha kulipuka.Nilichofanikiwa ni kuchukua simu na Kompyuta mpakato na kisha kukimbilia nje.

“Nilipotoka nje na wapangaji wenzangu nao wakatoka na kuanza kuulizana nani amefanya tukio hilo.Tayari tumetoa taarifa Polisi jana(juzi) usiku baada ya nyumba kuungua na hivyo tunasubiri watakachobaini kilichosababisha nyumba kuchomwa na waliohusika kufanya tukio hilo,”amesema.

Alipoulizwa anahisi nini baada ya tukio hilo, Myunga alijibu kuwa anachoamini sababu kubwa itakuwa ni mambo ya siasa kwani yeye si mfanyabashara na hana kazi nyingine zaidi ya siasa na siku za karibuni kuna moja ya kiongozi wa kisiasa wa upande wa upinzani alimtishia kwa bastola.

“Mbali ya kunitisha kwa bastola aliniambia kuwa nitakiona na lazima atanihamisha Iringa kwani najifanya mjanja kwa kuwa nimetoka Dar es salaam.Huyu kiongozi(jina tunalo) ndio atakuwa adui yangu namba moja na ndio namhisi atakuwa kafanya tukio hilo.

“Inaonesha kabisa walikuwa wamedhamiria kuniuua mimi na ndio maana walivunja dirisha la chumbani kwangu na kurusha kitu hicho ambacho kilisaabisha mlipuko uliofanya moto kuanza kuwaka.Hata hivyo acha Jeshi la Polisi Iringa nalo lifanye kazi yake ya kuchunguza na ukweli utapatikana,”amesema.

Waliopeperusha Bendera Ya Tanzania Bila Kibali Wapandishwa Kizimbani

$
0
0
WAKURUGENZI wawili wa Kampuni za Saha Limited  na Lucky Shipping Co.Ltd, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashitaka mawili ya uhujumu uchumi ikiwemo kupeperusha bendera ya Tanzania bila kibali.

Washitakiwa hao ni Issa Haji au Salum (39) ambaye ni baharia na Mkurugenzi wa Kampuni ya Lucky Shipping pamoja na Abdullah Hanga (73) mfanyabiashara na Mkurugenzi wa Kampuni ya Saha ambaye ni mkazi wa Mbezi Beach.

Akisoma  mashitaka hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa, Wakili wa Serikali, Wankyo Saimon alidai washitakiwa walijihusisha na mtandao wa uhalifu kinyume na aya 4(1) C, jedwali la kwanza na kifungu cha 57(1) na 60 (2) cha Sheria ya Uhujumu uchumi.

Saimon alidai kuwa Julai 19, mwaka jana na Januari 16, mwaka huu jijini Dar es Salaam, walitoa ushauri, msaada na maelekezo katika kutenda kosa la jinai la mtandao wa uhalifu ambalo ni kupeperusha bendera ya Tanzania kwenye meli iitwayo Huihang 68 zamani ilijulikana kama Greko 02, bila kuwa na hati ya usajili kutoka kwa msajili wa meli nchini kwa lengo la kujipatia faida kutoka katika shughuli za uvuvi haramu.

Pia alidai kuwa Julai 19, mwaka jana na Januari 16, mwaka huu, katika jiji la Dar es Salaam washitakiwa hao huku wakifahamu kuwa ni kosa kisheria waliruhusu upeperushwaji wa bendera katika meli hiyo ya Huihang 68 au zamani ilijulikana kama Greko 02 bila kuwa na leseni kutoka kwa msajili wa meli kwa lengo la kuifanya ionekane kuwa ya Tanzania wakati sio kweli.

Hakimu Nongwa alisema washitakiwa hao hawatakiwi kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo.

Hata hivyo, Saimon alidai kuwa upelelezi wa shauri hilo upo katika hatua za mwisho kukamilika hivyo wanaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kuieleza mahakama taarifa za upelelezi huo.

Wakili wa utetezi, Dismas Raphael aliiomba mahakama ijielekeze katika Katiba ambayo inawatambua washitakiwa hao kama watuhumiwa na kwamba iwatendee haki kwa kuwapatia dhamana.

Akijibu hoja hiyo, Saimon alidai kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), amewasilisha hati ya kuzuia dhamana kwa washitakiwa hao kwani wakipewa dhamana wataingilia maslahi ya Taifa hivyo mahakama ijielekeze katika suala hilo.

Pia alidai Ibara ya 59 (B) ibara ndogo ya 3 inaainisha mamlaka ya DPP kuhusu masuala yote yanayolenga maslahi ya Taifa kama ilivyoainishwa kwenye Katiba.

“Kama upande wa utetezi wanalenga kuipinga hati ya kuzuia dhamana wanatakiwa wafuate taratibu nyingine katika mahakama za Kikatiba ambapo watakapowasilisha maombi yao, sisi tutayajibu ndipo mahakama itatoa maamuzi,” alidai Saimon.

Hakimu Nongwa alisema upande wa utetezi uwasilishe mapingamizi yao kuhusu hati hiyo na upande wa mashitaka ujibu na kwamba mahakama hiyo itatoa maamuzi kama hati hiyo ni sahihi au la.

Hata hivyo, aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 22, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na kwamba washitakiwa hao wamerudishwa rumande.

Mwisho

NHIF yakanusha taarifa za uongo zilizosambazwa mtandaoni


TCRA CCC Yatoa Onyo Kali kwa Makampuni ya Michezo ya Kubahatisha Yanayotuma Matangazo Kwenye Simu za Watu

$
0
0
BARAZA la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano (TCRA- CCC) limesema asilimia 90 ya malalamiko waliyoyapata, yanatokana na huduma za simu za mkononi ikiwamo wananchi kutuma fedha bila jina kuonekana.
 
Katibu Mtendaji wa TCRA-CCC, Mary Msuya, alisema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu malalamiko waliyoyapata katika kipindi cha Oktoba hadi Desemba mwaka jana.

Alisema katika malalamiko hayo, watu wamekuwa wakilalamikia utumaji wa fedha kwenda mitandao mingine bila jina kuonekana kabla ya kutuma jambo, ambalo linawasababishia usumbufu pale wanapokuwa wamekosea kutuma fedha.

Alisema jambo hilo tayari wameliwasilisha Benki Kuu (BoT) ili ichukue hatua kwa wale ambao wanatuma fedha kupitia simu za mikononi kwa majina kuonekana kabia ya kufanyika kwa miamala.

Alisema mbali na suala hilo, pia kumekuwa na matangazo ya michezo ya kubahatisha ambayo hutumwa kwenye simu kinyume cha utaratibu hali ambayo inawakwaza watumiaji wa mawasiliano.

“Utakuta mtu anasubiri ‘message’ (ujumbe) ya maana labda anategemea kupokea muamala wa fedha. Matokeo yake inakuja ‘message’ ya ‘cheza biko’ au ‘tatu mzuka’. Kama mtu kacheza mara moja basi haina haja ya kuendelea kumtumia ‘message’ kila mara au waweke ‘option’ (nafasi) ya mtu kujitoa au waweke matangazo yao katika magazeti na si kuwasumbua watumiaji wa simu za mikononi. Mbali na matangazo hayo ya kubahatisha yapo mengine yanatumwa kinyume cha utaratibu,” alisema.

Aidha, Msuya alisema kwa upande wa huduma za utangazaji, malalamiko yalihusu kutokupatikana kwa chaneli za bure za kitaifa kupitia huduma ya digitali mpaka mtumiaji alipie kinyume cha kanuni zinazotaka apate huduma hizo bure bila gharama yoyote.

Alisema licha ya serikali na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) kuchukua hatua, bado watumiaji wanapata changamoto ya kutakiwa kuongeza fedha ili kupata king’amuzi kingine ili kuona chaneli za bure tofauti na ilivyokuwa awali.

“Baraza linapenda kutoa rai kwa watoa huduma kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa za kutosha kwa watumiaji ili kuwawezesha watumiaji kufanya maamuzi sahihi na kupata huduma inayostahili.

"Watumiaji wa ving’amuzi vya StarTimes wangepewa taarifa ya kutosha wakati wa kununua ving’amuzi malalamiko yaliyopo sasa yasingekuwepo,” alisema Msuya.

Aidha, Msuya alisema kampuni zinazotoa huduma za mawasiliano zinatakiwa kutoa ushirikiano kwa baraza katika kushughulikia malalamiko ya watumiaji kwa muda muafaka.

Hatima ya waliofukuzwa kwa vyeti feki, Wenye Vyeti vya Darasa la 7 na Kuhhusu Kupandishwa Madaraja

$
0
0
HATIMA ya mafao ya wafanyakazi wa serikali walioondolewa kwenye ajira kutokana na kubainika kuwa na vyeti feki itajulikana kabla ya Bunge la Bajeti, imefahamika.

Hatua hiyo inatokana na serikali kujibu hoja nane za Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta) na kwamba suala la kulipwa au kutolipwa haki zao litafahamika Machi au Aprili, mwaka huu.

Hoja zingine ni ajira ya waliomaliza darasa la saba, kupandishwa madaraja, madeni ya wafanyakazi, nyongeza za mishahara, kutofanyika vikao vya bodi, kujua idadi ya taasisi zilizoundwa na kuunganishwa kwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Katibu Mkuu wa Tucta, Dk. Yahya Msigwa, alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa mamlaka mbalimbali zinamalizia kulifanyia kazi suala la vyeti feki na kwamba kabla ya Mei Mosi, mwaka huu, hatima yao itakuwa imepatikana.

“Unajua kilichofanyika ni kosa la jinai na la kinidhamu, hivyo sisi Tucta tunaendelea kuiomba serikali angalau wapatiwe kifuta machozi,” alisema.

Alisema ajira kwa waliomaliza darasa la saba Serikali ilitoa waraka unaosema watumishi wa umma wanapaswa kumaliza elimu ya kidato cha nne kuanzia Mei, 20, 2004.

Pia alisema baada ya hapo, walitakiwa kujiendeleza ili kuwa na vigezo vya kuendelea kuwa watumishi wa umma iwapo zipo baadhi ya idara zinawahitaji na kujenga hoja.

Kuhusu kupandishwa madaraja,
Dk. Msigwa alisema watumishi wengi hawajapandishwa kutokana na uhakiki wa vyeti, hivyo serikali imetenga fedha kwa ajili ya mpango huo kwa kutegemea bajeti ijayo.

Alisema malipo yataanza tangu siku ya kupata barua ili kupunguza madeni ambayo inadaiwa na kwamba kimsingi katika hilo, yako madeni ya mishahara na isiyo ya mishahara.

Kuhusu madeni, kwa mujibu wa Dk. Msigwa, serikali imesema imemaliza uhakiki na imeanza kulipa lakini itakuwa vigumu kulipa watu wote kwa mkupuo bali watazingatia uhakiki ya madeni yenyewe.

Kwa upande wa nyongeza ya mishahara, alisema Rais John Magufuli hakuahidi wakati wa sherehe za Mei Mosi bali nyongeza hiyo italolewa mwaka huu.

Aidha, Dk. Msigwa alisema hoja ya kuunganishwa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii kuwa na mifuko miwili, mmoja wa binafsi na mwingine wa umma, imetokana kauli za wafanyakazi wenyewe kwenye sherere za Mei Mosi.

Alisema rasimu iliyotegenezwa si mbaya licha upungufu uliopo na wanaendelea kutoa maoni kabla muswada haujawasilishwa Bungeni.

Jeshi la Polisii Lakanusha Habari ya NIPASHE Kuhusu Kuwakama Wavaa Vimini, Milegezo na Wanyoa Viduku

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limekunusha taarifa ya kukamata watu wanaovaa vimini na kunyoa mtindo wa kiduku.

Hatua hiyo inakuja baada ya gazeti la kila siku la Nipashe January 17 (jana) kutoka na kichwa cha habari; Polisi yakamata wavaa vimini, kunyoa viduku.

 
Akizungumza jana Dar es Salaam, Kamanda wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa alisema taarifa hiyo haina ukweli wowote kwani mwandishi ameandika kitu ambacho hakukisema.

“Nilitaka nitoe ufafanuzi nikikanusha haya ambayo yameandikwa hayakusemwa na Jeshi la Polisi, ameyasema mwenyewe mwandishi kwa interest yake na sana alichokuwa anatafuta ni umaarufu wa stori.


Mambosasa alisema hakuna sheria yoyote inayowazuia watu kuvaa nguo fupi na kwamba alichokisema Rais Magufuli ni kwamba anachukizwa na wasanii wanaovaa nusu uchi na kuoneshwa katika vituo vya Runinga,kitu ambacho ni kinyume na maadili yetu.

"Kwa kuwa jambo hilo  ni machukizo na halivunji sheria za nchi ni vigumu  kwa Polisi kuanzisha msako, labda watu hao tuwakute wakifanya biashara ya ukahaba." Alisema Mambosasa na kuongeza;

“Ninamtaka sasa mwandishi arudi kwa watanzania aombe radhi ili kuondosha usumbufu uliojitokeza, nimepigiwa simu kuanzia jana(juzi) toka maeneo mbali mbali kwa jambo ambalo kimsingi halijafanywa na Jeshi la Polisi.”



==>Msikilize hapo chiniakiongea

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Pata Hadithi Kali za Kusisimua Toka kwa Mwandishi Makini

$
0
0
NEW YEAR, NEW GROUPS
BAADA YA KIMYA KIREFU CHA HADITHI YA SORRY MADAM.
Muandishi Eddazaria G.Msulwa(Genius Author ) anawakaribisha wasomaji wote munao tumia mtandao wa Whatsapp 0657072588. Kujiunga kwenye group lake jipya la V.I.P STORIES 2018 lililo anza 13th January 2018.

Hadi kali na za kusisimua SIN na TANGA RAHA Season TWO, zimeanza kupamba moto.

Wahi sasa kwani ada yetu ya group la hadithi ni nafuu kabisa. Sh 4000 tu, utaweza kusoma hadithi kwa mwenzi mzima na hadithi hizo zitaruka kuanzia Jumatatu hadi Jumamosi.

Na ukijiunga kwenye group basi tutakutumia hadithi za nyuma zilizo pita kwenye group bure. Wasiliana na muandishi moja kwa moja kupitia simu namba 0657072588 au 0768516188.

Kama mpenzi msomaji wa hadithi zetu, tunakukaribisha pia kwa maoni yako, kwa kumpigia simu muandishi na moja kwa moja ukazungumza naye.

Karibuni sana whatsapp 0657072588

By. Eddy Msulwa
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images