WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutoruhusu mtu yeyote kununua urais kama njugu.
Alitahadharisha kuwa kama itatokea kada yeyote wa CCM amepata urais kwa kununua kama njugu, waandishi wa habari nchini watakuwa wa kwanza kulaumiwa kwa kuwasaidia kuwaingiza madarakani watu wa aina hiyo.
Ingawa Waziri Membe hakutaja
Benard Membe amchokonoa Edward Lowassa kiaina ....Adai kuwa ikitokea kada yeyote wa CCM mwenye PESA akawa Rais, lawama zote zitaelekezwa kwa waandishi wa habari
↧
↧
Lulu Michael ayakumbuka mapenzi ya Steven Kanumba katika "siku ya wapendanao"
WAKATI kesi yake juu ya kifo cha aliyekuwa nyota wa filamu Bongo,
Steven Kanumba ikianza kurindima leo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es
Salaam, mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ ametoa la moyoni akikumbuka
mapenzi ya jamaa huyo aliyetangulia mbele za haki.
Lulu alifunguka hayo mwishoni mwa wiki iliyopita, Siku ya Wapendanao
(Valentine’s Day) iliyosherehekewa duniani kote Ijumaa
↧
Kodi ya ving`amuzi kushuka......Lengo ni kuhamasisha kampuni nyingi zaidi kujitokeza kuuza vifaa hivyo kwa wananchi
Serikali
imesema inatarajia kuwa kodi ya ving'amuzi itashuka ili kuhamasisha
kampuni nyingi zaidi kujitokeza kuuza vifaa hivyo kwa wananchi, tofauti
na sasa.
Hayo yalisemwa mjini hapa mwishoni mwa wiki na Naibu Waziri wa
Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba, wakati akifunga
mkutano wa jukwaa la kujadili mchakato wa kuhama kutoka mfumo wa
analojia kwenda digitali,
↧
Hamisa Mobeto alikana penzi la Diamond...“Kamwe siwezi kutembea na Diamond na haitatokea kwani jamii nzima inajua yupo na Wema Sepetu"
Mrembo aliyewahi kushiriki miss Tanzania Hamisa Mobeto a.k.a Hamisa
kadomo amekanusha tetesi za kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii
kipenzi cha kinadada Naseeb Abdul a.k.a Daimond Platnumz na kusema kuwa
anamuheshimu kama shemeji yake.
Hamisa ambaye pia amewahi kuonekana katika video ya msanii Quick
Rocka ‘My baby’, ameiambia Global Publishers kuwa maneno yanayosemwa si
↧
Ndege ya Ethiopian Airlines yatekwa na Rubani wake, Abadili uelekeo na kutua Uswis ili kuomba hifadhi ya kisiasa
Rubani msaidizi wa ndege ya Ethiopian Airlines iliyokuwa ikienda
Roma toka Addis Ababa ameteka ndege hiyo mapema leo na kuilazimisha
itue Geneva, Uswisi, polisi wameieleza AFP.
Rubabi huyo alitenda kitendo hicho cha ajabu kama
njia ya kujaribu kuomba hifadhi ya kisiasa nchini Uswisi. “Anadai
anaishi kwa hofu nchini kwake mwenyewe, hivyo anataka hifadhi
↧
↧
Picha za kikao Cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kilichofanyika jana ikiwa ni siku yake ya pili chini ya mwenyekiti wake, Rais Kikwete
Mwenyekiti
wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa
Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana
baada ya kuwasili ukumbini kuendesha Kikao Maalum Cha Halmashauri Kuu ya
Taifa ya CCM, mjini Dodoma jana, Feb 16, 2014.
Wajumbe
wa NEC, na Kamati Kuu ya CCM, Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib
Bilal, Waziri Mkuu Mizengo Pinda
↧
Daladala zagoma jijini Mwanza zikidai nauli IPANDE.... Abiria nao waamua kutumia Malori, baiskeli, Toyo Kilimo na pikipiki kusafiria
Madereva wa daladala jijini Mwanza leo wameamua kugoma kutoa huduma hiyo muhimu kwa jamii wakiishinikiza serikali kupandisha nauli na kupunguza faini pindi wanapokamatwa na askari wa usalama barabarani....
Baada ya mgomo huo kuanza, abiria walimua kutumia Malori, baiskeli, Toyo Kilimo na pikipiki kama njia mbadala ya kusafiria.
↧
Mkutano mkuu wa maofisa waandamizi wa jeshi la polisi waanza leo mjini Moshi.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akisalimiana na makamishna
wa Jeshi la Polisi baada ya kuwasili kwa ajili ya kumpokea mgeni rasmi
Naibu Waziri wa Mambo ya ndani kwenye ufunguzi wa mkutano Mkuu wa
Maofisa wakuu waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika katika chuo cha
taaluma ya Polisi Moshi.
Naibu
waziri wa Mambo ya Ndani Mh, Pereira Ame Silima akisalimiana na
↧
Mahabusu afariki dunia baada ya KUJINYONGA kwa kutumia tambala la kupigia deki ndani ya choo cha mahabusu ya Kituo cha Polisi
MAHABUSU, Vumi Elias (30), amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa
kutumia tambala la kupigia deki ndani ya choo cha mahabusu ya Kituo cha
Polisi Tunduma.
Elias, mkazi wa Maporomoko-Tunduma, aliyetuhumiwa kwa unyang’anyi wa
kutumia nguvu katika eneo la Tunduma wilayani Momba, alifariki dunia
jana, saa 12 asubuhi muda mfupi baada ya kufikishwa katika Kituo cha
Afya Tunduma
↧
↧
Godbless Lema anusurika kukamatwa na jeshi la Polisi kutokana na WARAKA wake unaomhusu Rais Kikwete aliouposti kwenye mtandao wa kijamii
Mbunge wa Jimbo la Arusha, Godbless Lema jana alinusurika
kukamatwa na makachero wa Jeshi la Polisi ili kuhojiwa kutokana na
ujumbe wake aliouposti kwenye mtandao wa kijamii akiandika: “Rais
Kikwete mbona umeamua kuliangamiza taifa.”
Akizungumza na gazeti la Mwananchi jana akiwa njiani
kuelekea Dodoma kushiriki Kikao cha Bunge la Katiba, Lema
↧
Naibu Mwanasheria mkuu wa serikali aiomba mahakama kuu iitupilie mbali kesi ya kikatiba inayomkabili waziri mkuu, Mizengo Pinda
NAIBU Mwanasheria Mkuu, Mhe George
Masaju (pichani) amedai mahakamani katika kesi ya kikatiba
iliyofunguliwa na Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha
Wanasheria Tanganyika (TLS) dhidi ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwamba kwa
mujibu wa katiba mamlaka ya mahakama kuingilia mwenendo wa bunge
yameondolewa.
Pia,
Mhe Masaju amedai kuwa kwa mujibu wa Katiba ya nchi
↧
Lulu Michael akiri mahakamani kuwa alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Kanumba, akana mashitaka ya kuua bila kukusudia na kueleza kilichotokea
Mwigizaji maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Michael Kimemeta,
amekiri mahakamani kuwa na uhusiano wa kimapenzi na aliyekuwa mwigizaji
mwenzake, Steven Kanumba na pia kuwa ugomvi na Kanumba siku ya tukio la
kifo cha mwigizaji huyo, lakini akakana mashtaka ya kumuua bila
kukusudia.
Lulu ambaye yuko nje kwa dhamana anakabiliwa na
kesi hiyo katika
↧
"Fedha chafu zinachochea uhalifu nchini "...Hii ni kauli ya naibu waziri wa mambo ya ndani wakati akifungua mkutano wa maofisa wakuu waandamizi wa Jeshi la Polisi
NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani, Perreira Ame Silima, amesema uwepo wa fedha chafu nchini umechangia kuendelea kukua kwa uhalifu.
Kwa mujibu wa naibu waziri huyo, matendo hayo ya uhalifu ni
usafirishaji wa dawa za kulevya, biashara ya binadamu na mitandao ya
kigaidi nchini.
Akifungua mkutano wa siku sita wa wakuu na maofisa wakuu waandamizi
wa Jeshi la Polisi kwenye ukumbi wa
↧
↧
Mchawi wa ungo adondoka jijini Arusha ....Baada ya watu kujaa, abadilika ghafla na kuwa kuku mweupe
HALI ya taharuki iliyoambatana na imani za kishirikina iligubika Jiji
la Arusha kufuatia mwanamke ambaye hakufahamika jina kudondoka na ungo
wa kishirikina asubuhi ya Ijumaa iliyopita kisha ghafla kubadilika kuwa
kuku mweupe mwenye mayai ndani ya ungo....
Mamia ya wananchi katika eneo la Kimandolu kando ya Barabara ya
Arusha- Moshi walimiminika kushuhudia tukio hilo lililojiri saa tatu
↧
Rais wa Rwanda, Paul Kagame aifanyia ukachero Tanzania....Jeuri yake yadaiwa kujengwa na ushirika wake wa kiintelijensia alioupandikiza ndani ya mfumo wa serikali ya Tanzania
JEURI ya wazi inayoonekana kuwemo ndani ya taarifa ambazo zimekuwa zikichapishwa mara kwa mara na vyombo vya habari vya serikali ya Rais Paul Kagame wa Rwanda dhidi ya Rais Jakaya Kikwete na serikali yake, inaelezwa kujengwa na ushirika wake wa kiintelijensia alioupandikiza ndani ya mfumo wa serikali na taasisi mbalimbali hapa nchini,MTANZANIA limedokezwa.
Taarifa zilizolifikia gazeti
↧
Mwanamke atiwa mbaroni baada ya kumfunga MINYORORO mtoto wa kaka yake na kuanza kumtumia KISHIRIKINA
KATIKA hali ya kushangaza, mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la
Dorah Joseph (34) anashikiliwa na jeshi la polisi baada ya kutuhumiwa
kumfunga mnyororo mtoto wa kaka yake aitwaye Happy Joseph (13) na
kumtelekeza bila kumpatia huduma muhimu, ikiwemo chakula.
Kwa mujibu wa majirani na mashuhuda, kisa cha mwanamke huyo kufanya
kitendo hicho cha kikatili, ni katika harakati zake za
↧
Vigogo sita wa CCM waliohojiwa na kamati ya maadili ya chama hicho wapewa adhabu ya ONYO KALI
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kati ya tarehe 13/02/2014 na tarehe 18/02/2014 kumekuwa na mfululizo wa
vikao kadhaa vya Chama kitaifa vilivyoshughulikia suala la maadili
ndani ya Chama.
Vikao hivyo ni pamoja na Kamati Ndogo ya Udhibiti tarehe 13-14/02/2014,
Tume ya Udhibiti na Nidhamu 18/02/2014 na Kamati Kuu tarehe 18/02/2013.
Waliohojiwa katika mfululizo wa vikao hivi ni
↧
↧
Mheshimiwa Pandu Amir Kificho ashinda nafasi ya Mwenyekiti wa Muda wa Bunge la Katiba
Spika wa Bunge la Wawakilishi Zanzibar na Mbunge wa Bunge
maalum la Katiba, Pandu Amir Kificho amechaguliwa na wajumbe wa Bunge
hilo kuwa Mwenyekiti wa muda.
Kutokana na ushindi huo Kificho sasa atakuwa na
kazi kuandaa kanuni ambazo zitatumika kwa ajili ya kumchagua mwenyekiti
wa kudumu wa bunge hilo na kusimamia vikao vyake.
Muda wa mwenyekiti
↧
Habari njema kwa akina dada: Mchumba mwaminifu anahitajika haraka sana. Vigezo na masharti ya huyo muoaji, bofya hapa
Mimi ni kijana wa kitanzania ambaye nimekulia katika maadili ya kidini na malezi mazuri ya kifamia, napenda nichukue fursa hii nitangaze nafasi ya mchumba ambaye kama ata kidhi vigezo vyangu atakuwa ndio mke wangu wa ndoa. Kifupi mi ni mtaalam wa IT naishi Dar es salaam.Mchumba ninaye mtaka ni vema awe amekulia malezi ya kidini kwa sababu mimi ni mcha Mungu na napenda kusali kwa hiyo napenda
↧
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Jumbe Mangu aongoza mkutano mkuu wa maafisa wakuu wa jeshi la polisi mjini Moshi leo
Mkuu
wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Jumbe Mangu akisisitiza jambo
kwenye mkutano Mkuu wa Maofisa Wakuu Waandamizi wa Jeshi la Polisi
unaofanyika katika Chuo cha Taluma ya Polisi Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Mkutano huo umebebwa na kauli mbiu isemayo “Zingatia Weledi katika Kutoa
Huduma Bora Kwa Jamii”.
Kamishna
wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi (CP) Paul Chagonja
↧
More Pages to Explore .....