Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Sumaye asema kuzuiwa mikutano ya hadhara ni uonevu kwa wananchi

$
0
0
Waziri Mkuu wa mstaafu, Frederick Sumaye amesema zuio la kufanya mikutano ya hadhara hadi mwaka 2020, linaminya uhuru wa wananchi wenye nia ya kuanzisha vyama vipya ya siasa.

Sumaye ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini ametoa kauli hiyo jana Januari 14, 2018 katika mahojiano na kituo cha Televisheni cha Azam.

Amesema zuio la kufanya mikutano liko kinyume na sheria iliyoanzisha vyama vya siasa.

“Jambo jingine ambalo ni gumu zaidi, nikisema leo si mwana CCM sitaki kwenda CCM, CUF wala Chadema, kwa utaratibu ulipo sasa siwezi kuanzisha chama kwani huwezi kufanya mkutano wowote kwa sababu tunafunga kabisa mtu kuanzisha chama,” amesema Sumaye na kuongeza,

 “…, CCM wao wanaonekana hawana wa kuwazuia, Mwenyekiti wao (Rais John Magufuli) anakwenda popote, wakati wowote ingawa unashindwa kumtofautisha na ziara za kiserikali.”

Kuhusu hamahama ya wanachama amesema, “ “Wanacheza na fedha za wananchi,  mfano mbunge wa Kinondoni (Maulid Mtulia aliyehamia CCM) alikuwa CUF, anakwenda CCM halafu wanamrudisha tena kugombea.”

“Sawa na yule wa Siha (Dk Godwin Mollel amehamia CCM) naye karejeshwa kugombea. Hii ni sawa na kuwatukana watu.”

Jeshi la Polisi Tanzania na Msumbiji watiliana saini ya makubaliano Kuzuia Uharibifu

$
0
0
Jeshi la Polisi nchini limetiliana saini mkataba wa makubaliano na Jeshi la Polisi la Msumbiji kushirikiana kupambana na uhalifu katika nchi hizo mbili, hasa maeneo ya mpakani.

Mkataba huo utahusisha kubadilishana taarifa, mbinu na uzoefu katika kupambana na ugaidi na dawa za kulevya ambazo zinaathiri nguvu kazi kwenye mataifa yao.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Januari 15, 2015 kabla ya kusaini makubaliano hayo, Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP,  Simon  Sirro amesema wahalifu waliodhibitiwa katika maeneo ya Kibiti, Mkuranga na Rufiji sasa wamekimbilia Msumbiji.

Hata hivyo, amewaonya wahalifu hao kwamba hata huko hawatakuwa salama kwa sababu Jeshi la Polisi Tanzania linashirikiana na Msumbuji katika kupambana na uhalifu kwa kubadilishana taarifa.

"Wale wahalifu waliokimbilia Msumbiji au Congo hawako salama. Majeshi yetu ya polisi yanashirikiana, ndiyo maana leo tunatiliana saini makubaliano ya ushirikiano," ameaema Sirro.

Amewataka wahalifu hao waliokimbilia Msumbiji kuachana na uhalifu kwa sababu wakiendelea watakamatwa kwa ushirikiano wa majeshi hayo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Jeshi la Polisi la Msumbiji, Bernardino Rafael amesema nchi yake inakabiliwa na wahalifu kutoka nchi nyingine, hivyo makubaliano hayo yatasaidia kupunguza uhalifu.

Amesema wanataka kudhibiti mipaka yao dhidi ya wahalifu hao ambao wanahatarisha amani katika nchi hiyo pamoja na nchi za jirani.

"Watu wenye ualbino wanauawa kwa imani za kishirikina na taarifa zinaonyesha wahalifu hao wanatoka mataifa mbalimbali. Tutashirikiana na Polisi  Tanzania katika kubadilishana taarifa ili kukomesha mauaji hayo," amesema Rafael.

BREAKING: Lowassa afunguka kilichompeleka Ikulu

$
0
0
Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Edward Lowassa ametoa ufafanuzi kuhusu mazungumzo yake na Rais John Magufuli yaliyofanyika Ikulu Dar es Salaam siku sita zilizopita. 

Kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa leo Januari 15, 2015, Lowassa amesema alimueleza masuala mbalimbali yanayowakumba wananchi na wanasiasa tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani.

“Nilijadiliana naye kuhusu masuala mbalimbali ya msingi kuhusu nchi yetu ikiwemo kutoheshimiwa kwa Katiba na sheria, uminywaji wa demokrasia, ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu,” amesema na kuongeza,

“Unaohusisha kupotea kwa watu, kuvamiwa, kutishwa na kushambuliwa kwa viongozi wa kisiasa wa upinzani na hali ngumu ya uchumi kwa wananchi wetu. Ni imani yangu kwamba Rais atayazingatia na kufanyia kazi masuala haya kwa masilahi yetu.”

Kupitia barua hiyo, Lowassa amesema yupo madhubuti kuliko wakati mwingine wowote ule.

Cyprian Musiba atangaza kumshitaki Tundu Lissu

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa CZ Information & Media Consultant LTD, Cyprian Majura Nyamagambile leo January 15, 2018 amezungumza na waandishi wa habari na kueleza kuwa yeye na baadhi ya Wanasheria nchini katika siku mbili zijazo watamfungulia mashtaka Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

Ameeleza kuwa wamefikia uamuzi huo kutokana na maneno aliyoyatoa Lissu kabla ya kwenda nchini Ubelgiji kwaajili ya matibabu, kwa kutoa kauli nzito kuwa Tanzania kwasasa sio mahali salama pa kuishi na eneo hatarishi kwa maisha ya binadamu.

Musiba ameeleza kuwa kauli hizo zililenga kuidhalilisha nchi, kuwapa hofu wageni wanaokuja nchini kwa ajili ya kutalii lakini pia kuwaogopesha wananchi washindwe kufanya kazi zao kwa amani na hivyo wanahitaji aisaidie nchi kutoa uthibitisho wa kauli zake hizo katika vyombo vya sheria.

“Tunampa siku mbili atoe uthibitisho wa kauli zake vinginevyo tutampeleka mahakamani, na japokuwa tutampeleka katika mahakama za ndani, nakala yake itapelekwa The Hague Uholanzi kwenye Mahakama ya Kimataifa.” Amesema Cyprian Musiba

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya January 16

Uamuzi wa serikali dhidi ya gazeti la Nipashe kwa taarifa ya kupotosha kuhusu Rais

Waziri Mkuu: “Tutakamilisha ujenzi wa hospitali ya rufaa ya Musoma”

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali itahakikisha inakamilisha ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mara iliyoanza kujengwa mwaka 1980.

Alitoa kauli hiyo wakati alipokagua ujenzi wa hospitali hiyo baada ya kuwasili mkoani Mara kwa ajili ya ziara yake ya kikazi.

Waziri Mkuu amesema Serikali itakamilisha ujenzi wa jengo hilo kwa awamu, ambapo wataanza na eneo la mapokezi na vyumba vya madaktari.

Amesema Serikali imedhamiria kuboresha huduma za afya nchini, hivyo amewaomba wananchi waendelee kuiamini na kushirikiana nayo.

Waziri Mkuu amesema tayari Serikali imetoa sh. bilioni 1.4 ili ujenzi uendelee. Ujenzi huo ulianza mwaka 1980, ulisimama mwaka 1987 kuanza tena 2010.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amekagua uwanja wa ndege wa Musoma mkoani Mara ambao unatarajiwa kukarabatiwa na kuwekwa lami.

Amesema kukamilika kwa ukarabati huo wa kiwanja hicho kutafungua fursa za utalii ndani ya mkoa huo ambao umezungukwa na vivutio vingi.

Amesema Serikali imedhamilria kukarabati viwanja mbalimbali vya ndege nchini kikiwemo cha Musoma ili kuboresha huduma za usafiri wa anga.

Viwanja vingine vinavyotarajiwa kukarabatiwa ni Iringa, Kilwa Masoko, Lake Manyara, Lindi, Moshi, Njombe, Tanga, Simiyu, Singida na Songea.

Waziri Mkuu amesema viwanja hivyo kwa sasa vinakarabatiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), ambao wanajenga kwa gharama nafuu na kwa viwango vinavyostahili.

Awali, Meneja wa TANROADS, mkoa wa Mara Mhandisi Mlima Ngaila alisema ukarabati huo utafanyika kwa awamu tatu ambapo ya kwanza itahusisha upanuzi wa uwanja na ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege.

Alisema barabara ya kuruka na kutua ndege ina urefu wa km. 1.6 na upana wa mita 33 ni ya changarawe, hivyo kusababisha baadhi ya ndege kushindwa kutua.

Pia, Waziri Mkuu alikagua ukarabati wa Shule ya Sekondari ya Ufundi ya Musoma na kwamba ameridhishwa na ukarabati wa miundombinu ya shule hiyo.

“Shule hii ilipewa sh bilioni 1.28 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu. Nimekagua jengo la utawala, madarasa, mabweni, jiko, maabara na bwalo, nimeridhika na kazi iliyofanyika.”

Shule hiyo ni miongoni mwa shule 10 kongwe ambazo Serikali iliamua kuzikarabati ili ziweze kurudi kama zamani na kuendelea kutumika.

Hata hivyo Waziri Mkuu aliuagiza uongozi wa Manispaa ya Musoma kushirikiana na uongozi wa shule hiyo katika kutatua baadhi ya changamoto zinazoikabili.

Miongoni mwa changamoto hizo ni malipo ya watumishi wasaidizi wakiwemo wapishi, walinzi na madereva, ambapo aliitaka kuchukua jukumu la kuwalipa watumishi hao badala ya kuacha jukumu hilo kwa Mkuu wa Shule.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

RC Makonda amfuta machozi mjane ambaye nyumba yake iliuzwa na matapeli

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amemsaidia mama mjane Benadetha Rwendela aliedhulumiwa nyumba yake Plot No. 239 Block B Kunduchi Beach kwa kupigwa mnada na madalali kutoka kampuni ya Nkanya Ltd kinyume na taratibu kisha kuamrishwa kuondoka ndani ya siku 30.

Baada ya RC Makonda kuona taarifa hizo kwenye baadhi ya vyombo vya vabari na mitandao alimuita mjane huyo ofisini kwake kisha kumkutanisha na wanasheria wa mkoa na kubaini utapeli mkubwa uliotumika kuuza nyumba hiyo kutokana na watu kufoji nyaraka ikiwemo sahihi ya mwenyekiti wa mtaa huku nyumba hiyo ikiwa na zuio la Mahakama.

Aidha imebainika kuwa hati za nyumba hiyo zilifojiwa kisha kutumika kuchukuwa mkopo wa shilingi bilioni moja pasipo mmiliki wa nyumba kujua kinachoendelea.

Kutokana na hilo RC Makonda ameagiza Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa kuwakamata matapeli waliohusika pamoja na kuagiza kusimamishwa mnada huo kwakuwa ni batili huku akimsihi mama mjane kuishi kwa amani kwenye nyumba yake.

Aidha RC Makonda amesema Jumatatu ya wiki ijayo atakutana na Bank ya KCB kwa ajili ya mazungumzo huku akiwaagiza madalali wote wanaotaka kufanya minada kwenye mkoa huu kuhakikisha wanapata ruhusa kutoka kwa wakuu wa wilaya.

Kwa upande wake mjane huyo Benadetha Rwendela ameishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kuwajali wananchi wake na kuwasaidia pale wanapopata matatizo huku akimpongeza Rais Magufuli kwa kumteua RC Makonda.

Jinsi Kitambi Kinavyopatikana na Jinsi Kinavyoondolewa na Dawa ya Mkataa Kitambi

$
0
0

Kitambi  ni  ile  hali  ya  tumbo  kuwa kubwa  na  kuchomoza  kwa  mbele  na  wakati mwingine  kufikia  hatua  ya  kunin’ginia.

JINSI  KITAMBI  KINAVYO  PATIKANA
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, mwili wa binadamu una seli kati  ya bilioni 50  hadi 200 za mafuta zilizogawanyika katika  sehemu  mbalimbali  za  mwili wa binadamu.

 Kwa wanawake  seli hizo  zipo sana katika maeneo ya matiti, kwenye  nyonga, kiunoni na kwenye makalio.

Kwa upande  wa  wanaume seli  hizo zinapatikana  sana kwenye kifua, tumboni na kwenye makalio pia.

Mafuta ya tumbo yanayofanya kitambi hukusanywa kwa njia kuu mbili:

i.Njia  ya kwanza ni mafuta kutoka kwenye tishu zilizo chini ya ngozi

ii.Na  njia  ya pili ni kutoka kwenye ogani za ndani kama moyo, kongosho n.k

SABABU ZA KUPATA KITAMBI
Sababu kubwa ya kitambi ni kukosekana ulingano wa nguvu(kalori) katika  mwili  wa  mwanadamu, hali  inayo  sababishwa  na  mtu  kula vyakula vinavyotia nguvu sana kuliko jinsi anavyoweza kutumia na kutoa kama taka mwili.

VYAKULA  VINAVYO  CHANGIA KULETA  KITAMBI

Vyakula vinavyochangia  kuleta  kitambi ni  pamoja  na :
i.Vyakula  vyenye  mafuta  mengi  kama  vile  nyama nyekundu  (iwe ni ya kuchemsha, kukaanga au kuchoma), nyama  ya  kuku  wa  kizungu  ( iwe  ya  kuchemsha, kukaanga  ama  kuchoma ), mafuta ya kupikia, (hasa yale yatokanayo na bidhaa za wanyama, kama siagi, na jibini), viazi ya kukaanga kwa  mafuta  (chips) pamoja  na  pizza.

ii.Vyakula vyenye wanga mwingi kama  vile ugali wa mahindi, mihogo, wali, mkate  mweupe.

iii. Vyakula  na  vinywaji  vyenye  sukari  nyingi  iliyo  ongezwa( added  sugar ), kama  vile  soda  na  keki.

iv. Vyakula  vilivyo  tengenezwa  kwa  ngano  na  sukari kama  vile  keki, skonzi, chapatti, maandazi, mkate  mweupe  nakadhalika

v. Pamoja  na  vinywaji  vilivyo  tengenezwa  kwa  kutumia  ngano  kama  vile  bia  za  aina  mbalimbali  na  kadhalika.

Vyakula  vilivyo  tajwa  hapo  juu, vikitumiwa  bila  kuzingatia  kanuni  za  mlo  kamili, huchangia  kuleta  tatizo  la  kitambi.

vi. Sababu nyingine ni  kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na  viungo(  physical  exercises  )  kwa  muda  mrefu.

JINSI YA KUJUA KAMA UNA KITAMBI
Kitambi kinaweza kuonekana kirahisi kwa macho. Ila kujua ni kwa kiwango gani kitambi chako kipo inabidi kufanya vipimo vya kiuno(waist) na nyonga (hips).

Mzingo wa kiuno ukiwa >102 cm au 40  kwa wanaume na >88 cm au 35  kwa wanawake, na uwiano wa kiuno na hips(Waist-Hip Ratio) ikiwa >0.9 kwa wanaume na >0.85 kwa wanawake.

BMI ya 30 au zaidi inaashiria 'Obese' uzito kuzidi kiasi. Kuwa na mzingo uliozidi kawaida ni kiashiria hatari cha matatizo ya kimetaboliki, kuliko hata cha BMI.

Kipimo kingine cha kitambi ambacho kimeonyesha uwezo zaidi kuliko BMI katika kutabiri uwezekano mkubwa wa magonjwa ya moyo ni Index Of Central Obesity(Waist-To-Height Ratio-WHtR) ambapo uwiano ukiwa sawa na 0.5 au zaidi, hii ikimaanisha mzingo wa kiuno angalau ni nusu ya kimo cha mtu.

Kipimo kingine ni Body Volume Index, kinachopima kitambi kwa kupima umbo la mtu na mgawanyo wa uzito wake.

MAMBO  YANAYO  MUWEKA  MTU  KATIKA  HATARI  YA  KUPATWA  NA  KITAMBI
Tumekwisha  ona  hapo  juu jinsi  kitambi  kinavyo  patikana  na  vyakula  pamoja  na  sababu  nyinginezo  zinazo  sababisha  kutokea  kwa  kitambi, sasa  tutazame  mambo  yatakayo  kufanya  uwe  katika  hatari  ya  kupatwa  na  kitambi.

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za kitaalamu, mambo  yafuatayo  huwaweka  watu  katika  hatari  kubwa   ya  kupatwa  na  kitambi :

1. Ulaji  mbovu  wa  chakula; Ulaji  mbovu  wa  chakula  ni  ulaji  usio  zingatia  kanuni  za  mlo  kamili. Hapa  mtu  hufululiza  kutumia  chakula  cha  aina  fulani  pekee  bila  kuzingatia  aina  nyinginezo  za  chakula.  Mfano; mtu  anaweza  kuwa  anakula  mlo  ufuatao :

Asubuhi :  Mchemsho  ama    supu  ya  ng’ombe , chapatti  tatu  na  soda  moja.  Mchana :   Ugali  nyama  choma anashushia  kwa  maji  na  soda.

Jioni :  Mchemsho  wa  kuku  na  bia  mbili  nakuendelea.

Usiku  :  Chips  mayai  au  chips  kuku  au  chips  mishikaki  na  bia.

Mtu  huyu  akiendelea  na  utaratibu  huu  kwa  muda  mrefu, ni  lazima  atapatwa  na  kitambi.

2. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  mafuta  mengi

3. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye wanga  mwingi  

4.Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  sukari  iliyo  ongezwa ( added  sugar  ).

5.Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vya  ngano.

6.Ulaji  mfululizo  wa   vinywaji  vyenye ngano  na  sukari.

7.Kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na viungo  ( physical  exercises  ).

Mhusika  anapokuwa  katika  makundi  yote  yali yotajwa  hapo  juu, hali  huwa  mbaya  zaidi. 

NJIA ZA KUONDOA KITAMBI
Kuwa  na  kitambi  ni  lugha  ya  mwili  ( body-language )  inayo  leta  ujumbe  kwako  kwamba  “ Mwili    wako  haupo  salama  tena “

Kama  una  kitambi   maana  yake  una  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini, mwili  wako  unatumika  kuhifadhi  mafuta  usiyo  yahitaji.

Hali  hii  kitabibu  imaanisha  kwamba, ogani  nyinginezo  zilizomo  ndani  ya  mwili  wako  zinao gelea  kwenye  mafuta( fats  )  yasihotika  yaliyomo ndani  ya  mwili  wako,  jambo  linalo  kuweka  katika  hatari  kubwa  sana  ya  kushambuliwa  na  magonjwa  hatari  kama  vile  shinikizo  kubwa  la  damu, kiharusi  na kisukari  na  kwa kutaja  machache.

Hivyo  basi  ili  kuondokana  na  hatari  hiyo, yakupasa   kupambana  kuondoa  hayo  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini  mwako.

NJIA  ZA  KUONDOA  KITAMBI.
Unaweza  kuondokana  na  kitambi  kwa  kufanya  diet  pamoja  na  mazoezi ya  mwili  na  viungo.

Vilevile  unaweza  kuondoa  kitambi  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  dawa  asilia  ya  kuondoa  kitambi  na  kuondoa  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

DAWA   ASILIA  YA  KUONDOA  KIAMBI  NA  MAFUTA  MWILINI.
Hii  ni  njia  ya  uhakika  kabisa  ya  kuondoa  tatizo  la  kitambi  pamoja  na  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

 Unaweza  kuondoa  tatizo  la  kitambi  pamoja  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  DAWA  ASILIA   IITWAYO YA  MKATAA  KITAMBI.

 Dawa   hii  ni  ya asili  kabisa
“  Pure  Herbal “, ambayo  haijachanganywa  na  kemikali  yoyote, haina  side  effect kwa  mtumiaji  na  inaondoa  kabisa  tatizo  la  kitambi  ndani  ya  siku  kumi  na  nne.

JINSI  DAWA  YA  MKATAA  KITAMBI  INAVYO  FANYA  KAZI.
1.Huyeyusha  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

2.Husaidia  kupunguza  hamu  ya  chakula.

3.Inazuia  kutengenezwa  kwa  seli  za  mafuta  ( fat cells  ) katika  mwili  wa  mwanadamu. Unapokula  chakula  chenye  mafuta  mengi, dawa  hii asilia  hupambana  kuyafanya  mafuta  hayo  yasitengeneze  seli  za  mafuta  mwilini  mwako. Hali  hii  huuepusha  mwili  wako  kuhifadhi  mafuta   yasiyo  hitajika  mwilini.

4. Husaidia  kupunguza  uzito wa mwili  kwa  haraka  sana  endapo  itatumika  pamoja  na  diet  ya  kabechi.

UFANISI  WA  DAWA.
Ufanisi  wa  dawa  hii  ni  wa  asilimia  mia  moja. Dozi  ya  dawa  hii  hutumika  kwa  muda  wa  siki  ishirini  na  moja.

MATOKEO  YA  DAWA:
Dawa  hii  huondoa  kabisa  kitambi  ndani  ya  siku  kumi  na  nne.

BEI  YA  DAWA :
Dawa  hii  inaoatikana  kwa  kiasi  cha  SHILINGI  ELFU  HAMSINI  TU  (Tshs. 50,000/=)

MAHALI  TUNAPO  PATIKANA.
Tunapatikana  jijini  DAR  ES  SALAAM, katika  eneo  la  UBUNGO  karibu  na  SHULE  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

KWA  WATEJA  WASIO  WEZA  KUFIKA  OFISINI  KWETU.
Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu  Tabata, tunao  utaratibu  wa  kuwafikishia  dawa  mahali  popote  walipo  ndani  ya  jiji  la  Dar  Es  salaam.

KWA  WATEJA  WA  NJE  YA  DAR  ES  SALAAM.
Kwa  wateja  waliopo  nje  ya  Dar  Es  salaam, tunawatumia  dawa  kwa  njia  ya  MABASI.

Kwa  wateja  wa  ZANZIBAR  tunawatumia  dawa  kwa njia  ya  boti.

KWA  WATEJA  WA  NJE  YA  NCHI:
Kwa  wateja  wa  nje  ya  nchi, tunatumia  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA : 0766  53 83 84

TUTEMBELEE:

UDSM Wampongeza Rais Magufuli Kwa Misimamo Thabiti Isiyoyumba

$
0
0
Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es salaam (DARUSO) ni serikali ya wanafunzi inayoamini katika sheria, kanuni na taratibu. Lakini pia, ni serikali inayoamini katika kushauri, kuhamasisha na kupongeza kila jambo jema linapotendwa na mtu au kikundi cha watu kwa manufaa ya taifa letu. 

Kwa kutumia misingi hii, DARUSO inatumia wasaa huu kutoa pongezi za dhati kwa Mhe. Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuonesha kwake kusikitishwa na baadhi ya watanzania wasiokuwa na nia njema na taifa letu kwa kufikiria kukiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuanzisha mjadala wa kuongeza muda wa Rais kukaa madarakani kitu ambacho hakijawahi kuzungumziwa kwenye kikao chochote halali cha Serikali ya Jamhuri kama hitaji la muhimu kwa taifa letu. 

Katika hili, ni wazi kwamba Rais wetu ameonesha mfano wa kuigwa si tu kwa Tanzania bali Afrika na duniani kwa ujumla katika kuheshimu katiba yetu kwa kuwataka wanaoendeleza mjadala huo kusitisha mara moja kwani hauna tija katika nchi yetu.

DARUSO, tukiamini pia wanazuoni wengi na waumini wa demokrasia kote duniani wanaungana nasi, tumefurahishwa sana na uamuzi wa Mhe. Rais kwa kukemea vikali suala hili kwani ni uamuzi wa kizalendo katika nchi yetu. 

Ipo mifano ya marais wenye uchu wa madaraka na kuamua kujiongezea muda wa kuendelea kukaa madarakani hata kwa kubadili katiba bila ya kujali hali mbaya za taharuki na sintofahamu wanazozisababisha kwenye nchi zao kwa sababu ya kujali maslahi yao binafsi. Ila Rais wetu kalikataa hili kwa manufaa ya taifa. 

Mwisho kabisa, rai yetu kwa watanzania wote kwa ujumla ni kwamba kulinda katiba si tu  jukumu la Rais pekee bali sote tunalo jukumu la kuiheshimu, kuilinda na kuisimamia katiba yetu ya nchi kwa gharama yoyote na wivu wa hali ya juu. 

Kwa moyo mkunjufu tunawatakia watanzania nyote utekelezaji mwema wa majukumu yenu ya kila siku. Ahsanten,

 Imetolewa na DARUSO kupitia Ofisi ya Rais Ndugu John Jeremiah Jilili -14.01. 2018

Naibu Waziri Dotto Biteko Akerwa na Mchango Mdogo wa Sekta ya Madini Katika Pato la Taifa

$
0
0
Na Mathias Canal, Dodoma
Sekta ya Madini inachangia kati ya asilimia 3.5 mpaka 4 katika Pato la Taifa ukilinganisha na sekta zingine ambazo zimejitutumua kwa kiasi kikubwa katika mchango mahususi wa pato la Taifa nchini Tanzania.

Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko amebainisha kuwa kiasi cha kati ya asilimia 3.5 mpaka 4 ni kidogo sana ukilinganisha na umuhimu wa sekta hiyo nchini hivyo Wizara ya Madini imekusudia kuongeza tija katika mchango wa pato la Taifa kupitia sekta hiyo muhimu ya Madini.

Mhe Biteko amebainisha hayo jana Januari 15, 2018 wakati akizungumza na wakuu wa idara na vitengo pamoja na watumishi wa Wizara ya Madini ofisi Kuu Mjini Dodoma huku akiwataka watumishi wote kufanya kazi kwa bidii, nidhamu na uzalendo mkubwa kwa manufaa ya Taifa.

Alisema kuwa sekta ya Madini ni muhimu nchini kutokana na rasilimali Madini ilizonazo hivyo watumishi wote wanapaswa kufikiria namna ya kufanya kazi kwa tija ili kuwa na ongezeko la mchango mkubwa katika pato la Taifa.

“Natamani nione kwenye taarifa ya robo mwaka ya BOT ikisoma kwamba sekta ya madini inachangia angalau asilimia 10 ya Pato la Taifa kuliko ilivyo hivi sasa na hilo naamini linawezekana kwa ushirikiano wa pamoja” Alisisitiza Mhe Biteko

Mhe Biteko alisema kuwa hakuna mtu yeyote ambaye atatutumua mabega kwamba ni mkubwa katika Wizara badala yake ukubwa wa cheo na umri utaonekana katika matokeo muhimu na makubwa katika utendaji kazi.

“Mimi kuwa Naibu Waziri hapa So What… kama sitofanya kazi yenye matokeo makubwa kutokana na imani niliyopewa na Rais nitakuwa si lolote, hivyo kwa ushirikiano wenu pekee tutaweza kutimiza utendaji uliotukuka na wenye manufaa makubwa” Alikaririwa Mhe Biteko wakati akizungumza na watumishi wa Wizara ya Madini

Mhe Biteko alisema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli anafanya kazi nzuri kwa manufaa makubwa ya watanzania wote hivyo watumishi mbalimbali wa serikali, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla wanapaswa kuunga mkono jitihada hizo pasina kurudisha nyuma makusudi na matakwa ya utekelezaji wa ilani ya ushindi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mwaka 2015-2020.

Asubuhi siku ya Jumatatu Januari 8, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli alimuapisha Mhe Dotto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri wa madini, Ikulu Jijini Dar es salaam.

MWISHO

Naibu Waziri Wa Madini Mhe Biteko Autaka Uongozi Wa Chuo Cha Madini Dodoma Kujitathimini

$
0
0
Na Mathias Canal, Dodoma
Uongozi wa Chuo cha Madini Dodoma kilichopewa ithibati kamili ya kutoa mafunzo ya umahiri yaani Competence Based Education and Training System (CBET) umetakiwa kujitathmini ikiwemo kutatua changamoto zinazokikabili chuo hicho ndani ya wiki mbili.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko jana 15 Januari 2018 alipotembelea chuoni hapo na kujionea hali ya ufanisi wa chuo hicho huku akikerwa na uduni wa utunzaji wa vifaa katika chumba cha maabara ya uchenjuaji wa madini.

Mhe Biteko alisema kuwa pamoja na changamoto lukuki walizoainisha katika taarifa ya chuo iliyosomwa na Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Ndg Vincent Willium Pazzia ikiwa ni pamoja na uchache wa bajeti, uhaba wa wakufunzi katika fani za uhandisi na usimamizi wa mazingira migodini na upungufu wa ofisi za watumishi, wanatakiwa kuwa na mikakati ya kukabiliana nazo ndani ya wiki mbili zitakazofika ukomo mwishoni mwa mwezi huu.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli haitatoa fedha mahali ambapo hakuna matokeo ili ziliwe na watu wasiokuwa na matakwa mema na Taifa.

Aliongeza kuwa katika Wizara ya madini kumekuwa na malalmiko mengi kuliko utendaji jambo ambalo lisipotafutiwa ufumbuzi wa kudumu haraka litabakisha usugu na uvivu wa kufikiri kwa baadhi ya watendaji na kusalia kufanya kazi kwa mazoea pasina kuwa na ubunifu.

Naibu Waziri wa Madini Mhe Biteko alisema kuwa wakati Taifa likiwa linaelekea kuwa katika uchumi wa kati na mapinduzi ya viwanda huku rasilimali za madini zikipewa umuhimu mkubwa ni lazima watendaji wakubali kukabiliana na changamoto mbalimbali kwani tiba ya changamoto hizo ni pamoja na kuzikabili na kuzipatia ufumbuzi wa haraka.

Aidha, ameutaka uongozi wa chuo hicho cha madini kuhakikisha kuwa kinazalisha wataalamu wengi katika sekta ya madini ambao watalisaidia Taifa kutekeleza majukumu muhimu ya serikali ikiwemo uzalendo na ulinzi wa mali za umma.

Alisema kuwa watendaji wote serikalini wanapaswa kutambua kuwa wana jukumu kubwa moja la kuhakikisha kuwa wanatekeleza kwa ubora na umakini mkubwa maelekezo rasmi ya serikali ambayo yamebainishwa katika ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi katika kipindi cha mwaka 2015-2020.

MWISHO

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls 0658316976
0755911233
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Dr Mashinji (Katibu Mkuu) Azungumzia Nafasi ya Uenyekiiti Ndani ya CHADEMA

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Vicent Mashinji amefunguka kuhusu nafasi ya uenyekiti ndani ya chama hicho.

Mwanasiasa huyo amesema mwanachana yeyote wa Chadema anaweza kuwa Mwenyekiti ila kwa sasa ni wakati wa Freeman Mbowe ambaye ndiye anashikilia nafasi hiyo.

“Chadema ni chama ambacho kina fursa na kila mtu na mwanachama yeyote anaweza kuwa Mwenyekiti lakini watu waelewe huu si wakati wake ni zamu ya Mhe. Freeman Mbowe ukifika wakati wa uchaguzi atakuja mtu mwingine,” amesema Dkt. Mashinji.

“Mfumo wetu ni tofauti na CCM, chama kinaongozwa na Mwenyekiti ambaye ni Rais amevaa kofia mbili kwa utawala bora hili haliwezekani sababu chama kinatakiwa kuongozwa na Mwenyekiti ambaye anatakiwa pia kuisimamia Serikali,” ameongeza.

Pia amesema toka miaka ya 90 Mhe. Mbowe alikuwa Mwenyekiti wa vijana lakini watu wanasahau kuwa bado hiki ni kipindi cha uongozi wake na bado haujamalizika.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Katibu Mkuu CHADEMA Awajibu Wanaodai Ameshindwa Kuimudu Nafasi Hiyo

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Vincent Mashinji amesema kuwa yeye yuko tofauti na makatibu wengine wa vyama.

Ameyasema hayo Jijini Dar es salaam wakati akifanya mahojiano na kituo kimoja cha Televisheni, ambapo amesema kila kiongozi huwa na mikakati yake ya kiutendaji.

Amesema kuwa wapo baadhi ya watu wanaosema amepooza, mkimya, hana mikiki mikiki kama walivyo viongozi wengine.

“Ukichanganya majukumu yangu ya kikazi na yale aliyokuwa akifanya Dkt. Slaa unaweza kuharibu mipango ya kitaasisi,” amesema Dkt. Mashinji.

Hata hivyo, amezitaja baadhi ya kazi alizozifanya akiwa Katibu Mkuu kuwa ni pamoja na uandaaji wa Katiba ya Chadema pamoja na miongozo mbalimbali.

Waziri Mkuu Asema Serikali Haitasubiri Kuwaundia Tume Wezi na Mafisadi......Asisitiza kwamba atakayebainika atashughulikiwa hapo hapo

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa umma nchini wasijihusishe na vitendo vya wizi, ufisadi kwani Serikali haitosubiri kuwaundia tume za kuwachunguza bali itawashughulikia hapo hapo.

Amesema Serikali haikotayari kuwavumilia watumishi wanaojihusisha na wizi, ubadhilifu, rushwa na uzembe, hivyo ni vema viongozi waliopewa dhamana wahakikishe wanatekeleza majukumu yao kwa uadilifu.

Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo jana jioni (Jumatatu, Januari 15, 2018) wakati akizungumza na watumishi wa wilaya ya Musoma mkoani Mara akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi ya siku sita mkoani hapa.

“Fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo zinalenga kutatua kero za wananchi na si kuwanufaisha wachache wenye tamaa. Kama ni za ujenzi wa zahanati ijengwe na atakayezitafuna Serikali haitosita kumchukulia hatua.”

Waziri Mkuu asiwasisitiza watumishi wa umma kufanya kazi kwa mujibu wa sharia kwa sababu vitendo vya wizi, uzembe vinachangia kupunguza kasi ya kuwaletea maendelea maendeleo Watanzania.

Alisema lengo ni kuhakikisha azma ya Serikali ya kuwaletea maendeleo wananchi hususan ni wale wa hali ya chini inatimia, hivyo aliwaagiza viongozi wa halmashauri wakiwemo Madiwani kusimamia vizuri miradi ya maendeleo.

Pia Waziri Mkuu aliwataka wakuu wa idara na watendaji wengine wa halmashauri kuacha tabia ya kukaa ofisini na dabala yake waende vijijini kwa ajili ya kuwafuata wananchi na kushirikiana nao katika kutatua kero mbalimbali zinazowakabili.

Waziri Mkuu alisema watendaji hao wanatakiwa waachane na tabia ya kuwasubiri wananchi wawapelekee malalamiko yao kwa sababu baadhi yao hawana uwezo wa kufika katika ofisi zao.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Atiwa Mbaroni Kwa Kubaka Mbuzi Wawili wa Jirani Yake

$
0
0
Mtu mmoja nchini Kenya mwenye umri wa miaka 35 amefikishwa mahakamani akituhumiwa kubaka mbuzi wawili wa jirani yake, na kisha kuwaua.

Tukio hilo limetokea Januari 13 mwaka huu, baada ya watu kumuona akiwaburuza mbuzi hao kutoka porini ambako anahisiwa kufanya tukio hilo, katika eneo la  Kangundo

Waendesha mashtaka wametaka mbuzi hao wapelekwe kufanyiwa vipimo ili kubaini kama kweli wamefanyiwa kitendo hicho, na kutaka mshtakiwa kupatiwa matibabu baada ya kulalamika alipigwa vibaya na polisi walipoenda kumkamata.

Kesi hiyo imehairishwa mpaka Januari 29, na mshtakiwa kupewa dhamana ya shilingi 100,000 za Kenya.

Sheria za Kenya zinamtaka mtu atakayekutwa na hatia ya kufanya ukatili kama huo kwa wanyama kwenda jela kwa miaka 14.

Babu Tale Amfunda Shilole na Mumewe

$
0
0
Meneja wa WCB na Tip Top Connection, Babu Tale ambaye alikuwa msimamizi wa ndoa kati ya Shilole na Uchebe, amewataka pindi wanapopishana katika ndoa yao kutopeleka mambo hayo katika mitandao ya kijamii.

Tale amesema endapo watafanya hivyo wasifike kwake ila kama ugomvi utakuwa wa ndani kwa ndani wasisite kufika wake.

“Kama unampenda usigombane naye kwenye mitandao, kwa hiyo kama mnagombana na mpenzi wako mnaenda kugombania Instagram, mtaachana na kwangu usije,” Tale amemueleza Uchebe.

“Kama mkigombania chumbani njoo kwangu any time tutayamaliza, kama mnagombania kwenye mitandao hayo si mapenzi,” amesisitiza.

Hata hivyo amesema si kwamba anamkataza kujidai na mkewe katika mitandao ila anapaswa kutambua kuwa amezungukwa na mbwa mwitu ambao kazi yao ni kuharibu maendeleo ya ndoa za watu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images