Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kagame awasili na kupokelewa na Rais Magufuli

$
0
0
Rais wa Rwanda, Paul Kagame amewasili nchini leo Januari 14 kwa ziara ya siku moja na kupokelewa na mwenyeji wake, Rais John Magufuli.

Baada ya kuwasili katika uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA), Rais Kagame alielekea katika chumba maalumu na kukaa hapo kwa takribani dakika 30.

Aliondoka uwanjani hapo saa 4:45 na kuelekea Ikulu ambapo atafanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Magufuli.

Hii ni mara ya pili kwa Kagame kuwasili nchini na kufanya mazungumzo na Rais Magufuli tangu mwaka 2015. Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2016 ambapo alifanya ziara na kushiriki maonesho ya 40 ya biashara (Sabasaba).

Yaliyojiri wakati wa mazungumzo kati ya Rais Dkt Magufuli na Rais Kagame

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Rwanda Mhe. Paul Kagame leo tarehe 14 Januari, 2018 amefanya ziara ya kikazi ya siku moja hapa nchini kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Mhe. Rais Kagame amewasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam na kupokelewa na mwenyeji wake Mhe. Rais Magufuli na kisha kulakiwa na viongozi mbalimbali wakiongozwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, na baadaye akaelekea Ikulu ambako pamoja na kufanya mazungumzo ya faragha, viongozi hao wamezungumza na wananchi kupitia vyombo vya habari.

Mhe. Rais Magufuli amesema katika mazungumzo yao wamekubaliana ujenzi wa reli kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) kati ya Isaka nchini Tanzania na Kigali nchini Rwanda yenye urefu wa takribani kilometa 400 uanze mwaka huu (2018), na wamewaagiza Mawaziri wanaohusika na miundombinu kukutana ndani ya kipindi cha wiki mbili kuanza sasa ili kuweka mipango ya utekelezaji ikiwemo upatikanaji wa fedha.

Mhe. Rais Magufuli ameongeza kuwa wakati uamuzi huo ukifikiwa, Tanzania ambayo tayari imeanza ujenzi wa reli ya kati (Standard Gauge) kuanzia Dar es Salaam – Morogoro hadi Dodoma yenye urefu wa kilometa 726 na itakayogharimu Shilingi Trilioni 7.6, itaanza mchakato wa kuunganisha sehemu iliyobaki ya kutoka Dodoma – Isaka yenye urefu wa takribani kilometa 400 ili mizigo iweze kusafirishwa moja kwa moja kutoka bandari ya Dar es Salaam hadi Kigali nchini Rwanda.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amebainisha kuwa japo kuwa kumekuwa na ongezeko la mizigo ya Rwanda inayosafirishwa kupitia Tanzania iliyofikia tani 950,000 kwa mwaka, biashara kati ya nchi hizi mbili sio ya kuridhisha na hivyo amesema wamekubaliana kuboresha zaidi mazingira ya biashara ikiwemo kuimarisha miundombinu ya reli na barabara na kuwahamasisha wafanyabiashara wa Tanzania na Rwanda kufanya biashara zaidi.

“Tukijenga reli kutoka Isaka hadi Kigali, na sisi huku tunajenga kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma na tukaunganisha Dodoma hadi Isaka, mizigo mingi ya Rwanda itasafirishwa kupitia bandari ya Dar es Salaam, biashara itakua zaidi na ajira zitaongezeka, kule Lulenge Ngara, Burundi na Rwanda kote kuna madini ya Nickel, tukijenga miundombinu yetu tutasafirisha madini haya na tutaongeza biashara.

“Na reli hii itatumiwa na nchi nyingine za Burundi, DRC na Uganda, kwa hiyo ni jambo muhimu sana kwa uchumi wetu na majirani” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amemhakikishia Mhe. Rais Kagame kuwa Tanzania itaendeleza na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wake na Rwanda kwa manufaa ya wananchi, na kwamba ipo tayari kumuunga mkono atakapochaguliwa kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) katika kikao cha wakuu wa nchi na Serikali kinachotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu wa Januari, 2018 Mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.

“Mhe. Rais Kagame nakupongeza sana, unafanya kazi kubwa ya kuwapigania wananchi wako, Watanzania tunajua ulikoitoa Rwanda na tunajua ulipoifikisha, nakuhakikishia tutaendelea kushirikiana katika jukumu la kuwaletea wananchi maendeleo” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Kwa upande wake Mhe. Rais Kagame amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa mwaliko wake na amempongeza kwa kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya nchi yake na Tanzania.

Mhe. Rais Kagame amesema yeye na Mhe. Rais Magufuli wameamua kufanya kazi ya kuwaletea wananchi maendeleo na ameahidi kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano na Mhe. Rais Magufuli ili mipango yote waliyojiwekea itekelezwe ikiwemo kuinua biashara na kuongeza ajira, na pia ameshukuru kwa Tanzania kuwa tayari kumuunga mkono atakapochaguliwa kuwa Mwenyekiti wa AU.

Mhe. Rais Kagame amemaliza ziara yake ya kikazi ya siku moja hapa nchini na amerejea nchini kwake Rwanda.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

14 Januari, 2018

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya January 15

Serikali yasitisha uchimbaji madini mgodi wa ZEM

$
0
0
Serikali imesitisha kwa muda usiojulikana shughuli za uchimbaji wa madini katika mgodi wa dhahabu wa ZEM uliopo kijiji cha Nyasirori wilaya ya Butiama mkoa wa Mara.

Imesema imechukua uamuzi huo baada ya uongozi wa mgodi huo kushindwa kutekeleza maagizo ya Serikali, ikiwa ni pamoja na kuboresha maslahi ya wafanyakazi.

Uamuzi wa kusitisha uchimbaji wa dhahabu katika mgodi huo umetolewa  Januari 13, mwaka 2018 na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo baada ya kufanya ziara mgodini hapo.

Akiwa mgodini hapo, Nyongo aliutaka uongozi wa mgodi kumkutanisha na wafanyakazi, hasa wachimbaji jambo ambalo lilishindikana baada ya kuzungushwa maeneo mbalimbali bila kuona mfanyakazi yoyote.

 “Mbona muda unazidi kwenda hao wachimbaji hawafiki, hebu twendeni huko huko (chini ya ardhi) nataka niongee nao nione kama mmetimiza maagizo ya Serikali mliyopewa wiki mbili zilizopita," amesema Nyongo.

Baada ya kufika eneo la uchimbaji, naibu waziri huyo aliombwa asubiri kwa maelezo kuwa wachimbaji hao wameitwa, kujikuta akiganda kwa zaidi ya saa moja.

Kufuatia hali hiyo aliutaka uongozi wa mgodi kusitisha shughuli za uchimbaji hadi hapo utakapotekeleza maagizo waliyopewa, kubainisha kuwa ingawa Serikali inasisitiza uwekezaji haipo tayari kuona wananchi wake wakinyanyasika.

Wakati Nyongo akisema kwa mujibu wa taratibu na sheria, wachimbaji hao wanapaswa kulipwa mshahara usiopungua Sh400,000, meneja rasilimali watu wa mgodi huo, Luo Giriquam amesema hawakuwaficha wafanyakazi hao.

“Hatukuwaficha, uongozi uliwatafuta bila mafanikio kwa vile walikuwa ndani ya shimo wakiendelea na shughuli zao,” amesema na kuahidi kutekeleza maagizo ya Serikali.

Waziri Mkuu Auvunja Mfuko Wa Kuendeleza Kahawa.....Amuagiza CAG Kufanya Uchunguzi Tangu Kuanzishwa Kwake

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameuvunja Mfuko wa Wakfu wa Kuendeleza zao la Kahawa (CDTF) na amemuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuchunguza mwenendo wa mfuko huo tangu ulipoanzishwa.

Ametoa agizo hilo jana (Jumapili, Januari 14, 2018) wakati akizungumza na wadau wa zao hilo kwenye kikao cha kujadili maendeleo ya zao la kahawa alichokiitisha, mjini Dodoma.

Waziri Mkuu amechukua hatua hiyo baada ya kubaini kwamba uundwaji wa mfuko huo si wa kisheria bali ni wadau wa zao hilo kwa kushirikiana na Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB).

“Wakati Serikali inapambana kupunguza makato ya hovyo kwa wakulima, kumbe huku kuna chombo cha kuwachukulia fedha wakulima hii haikubaliki.”

Pia aliagiza kufungwa kwa ofisi za CDTF ili kupisha uchunguzi na baada ya CAG kukamilisha uchunguzi na kukabidhi ripoti, kazi zote zilizokuwa zinafanywa na mfuko huo zitafanywa na Bodi ya Kahawa.

Hata hivyo, Waziri Mkuu ameongeza kuwa  majukumu ya kuundwa kwa mfuko huo yanaingiliana na yale ya Bodi ya Kahawa, ambayo ni pamoja na kufuatilia maendeleo ya zao hilo, hivyo hakuna haja ya kuwa vyombo viwili vinavyofanya kazi moja.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amepiga marufuku wanunuzi wa kahawa kwenda kununua kwa wanavijiji na badala yake kahawa yote itauzwa kwa njia ya minada.

“Kahawa itauzwa katika minada tu na utaratibu wa kutoa vibali kwa wanunuzi wa kahawa kwenda kununua kwa wananchi vijijini marufuku kuanzia sasa, kama kuna watu wamepeleka fedha zao wazirudishe kwani hazitafanya kazi.”

Amesema Wakuu wa Mikoa na Wilaya wasimamie uuzwaji wa zao hilo na kuwachukulia hatua wote watakaokutwa wananunua kahawa kwa wakulima. “Anayetaka kahawa akanunue mnadani na si kwa wanavijiji lengo ni kuhakikisha mkulima anapata tija.”

Pia ameziagiza halmashauri zote zinazolima kahawa nchini kuanzisha vitalu vya miche ya kahawa na kisha kuigawa bure kwa wakulima, pia Maofiza Kilimo wawaelimishe walkulima wote wenye miti mikongwe waanzisha mashamba mapya.

Kuhusu suala la utafiti wa zao hilo, Waziri Mkuu ameiagiza Wizara ya Kilimo itumie vyuo vyake vya kilimo ianzishe vituo vyake vya utafiti vitakavyofanya kazi ya utafiti wa zao hilo.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bw. Joseph Kakunda amesema watahakikisha maagizo hayo yanafanyiwa kazi, ambapo aliwaagiza Wakuu wa mikoa yote 16 inayolima kahawa pamoja na wakuu wa wilaya wake 52 wahakikishe wanafuta mara moja vibali vya ununuzi wa kahawa katika vyanzo vyao vya mapato.

Kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Hazina mjini Dodoma kilihudhuliwa na Waziri wa Kilimo Dkt. Chales Tizeba, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bw. Kakunda.

Wengine ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu,, Bibi Maimuna Tarishi, Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Mhandisi Mathew Mtigumwe, Wakuu wa mikoa 16 wanaolima kahawa na wakuu wa wilaya,Mrajis wa Vyama vya Ushirika Nchini, Dkt. Tito Haule, Makatibu tawala wa mikoa inayolima kahawa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Kahawa na wajumbe wa bodi hiyo,,Mkurugenzi wa bodi ya Kahawa Tanzania, Wakurugenzi wa Halmashauri,

 IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Serikali yaufungua mgodi wa Buhemba

$
0
0
Hatimaye Serikali imefungua Migodi ya Dhahabu ya Wachimbaji Wadogo iliyopo katika eneo la Buhemba Wilaya ya Butiama Mkoani Mara baada ya kujiridhisha hali ya usalama katika migodi hiyo.

Migodi hiyo imefunguliwa rasmi na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo Januari 13, 2018 na kushuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Annarose Nyamubi.

Akizungumza katika tukio hilo, Nyongo alisema jumla ya migodi 10 imefunguliwa kati ya 16 baada ya kujiridhisha usalama wake.

Alifafanua kwamba eneo la Buhemba lina jumla ya Migodi ya Dhahabu 16 ambayo inamilikiwa na Wachimbaji Wadogo hata hivyo iliyokidhi vigezo vya kiusalama ni Migodi 10 pekee ambayo imeruhusiwa kuendeleza shughuli za uchimbaji.

Alisema Serikali ilisitisha shughuli za uchimbaji Madini kwenye eneo hilo la Buhemba Februari 2017 baada ya kutokea vifo vya Wachimbaji Saba na wengine wapatao 15 kujeruhiwa kutokana na kufanya shughuli zao bila kuzingatia taratibu na kanuni za uchimbaji salama.

Alibainisha kuwa Mwezi Desemba mwaka jana alifanya ziara kwenye eneo hilo ili kujionea hali halisi ya machimbo husika pamoja na kuzungumza na wachimbaji waliosimamishwa kuendeleza shughuli zao ambapo aliagiza shughuli za ukaguzi zikamilike ifikapo Mwezi huu wa Januari ili migodi ifunguliwe.

"Kama mtakumbuka nilifanya ziara hapa na niliagiza kufikia Januari 10, 2018 Ukaguzi wa Usalama kwenye eneo la Machimbo ya Dhahabu ya Buhemba uwe umekamilika ili shughuli za uchimbaji zilizokuwa zimesimamishwa ziruhusiwe; tumejiridhisha mashimo kumi ni salama na sasa tunafungua rasmi," alisema Naibu Waziri Nyongo.

Alisema shughuli hiyo ya Ukaguzi kama alivyokua ameagiza ilifanyika kwa umakini na kwamba maduara Kumi (Migodi Kumi) yameruhusiwa na mengine Sita hayatoruhusiwa kuendeleza shughuli za uchimbaji.

Aliongeza kuwa baada ya kufika kwenye eneo hilo kwa mara ya kwanza alisikitishwa kuona wananchi wengi wakiwa wamekosa shughuli za kufanya kutokana na migodi hiyo kufungwa na ndiyo sababu ya kuagiza ukaguzi wake ukamilike haraka.

“Nilivyotembelea hapa Mwezi Desemba mwaka jana nilisikitishwa kuona shughuli za uchumi kwenye eneo hili la Buhemba zimesimama kutokana na shughuli za uchimbaji kusimamishwa baada ya kutokea ajali,” alisema.

Aidha, Naibu Waziri Nyongo aliwaagiza Wakaguzi wa Migodi kuhakikisha wanatembelea mara kwa mara maeneo ya migodi ili kukagua hali ya usalama pamoja na kutoa mafunzo ya uchimbaji salama kwa wachimbaji hususan wadogo lengo likiwa ni kuepusha ajali.

“Ninawaagiza kwa mara nyingine Wakaguzi wa Migodi kuhakikisha mnatembelea maeneo ya migodi mara kwa mara ili kuepusha ajali,” aliagiza Naibu Waziri.

Naibu Waziri Nyongo vilevile aliwaagiza wachimbaji madini kuhakikisha wanafuata sheria, kanuni na taratibu za uchimbaji ili kuepusha ajali migodini na wakati huohuo kunufaika ipasavyo na shughuli zao bila kupata usumbufu.

Aidha, Naibu Waziri alizungumzia ulipaji wa kodi na tozo mbalimbali ambapo aliwaagiza wachimbaji hao kuhakikisha wanalipa kwa mujibu wa sheria na alionya kwamba mgodi utakaoshindwa kulipa inavyostahili, utafungiwa.

"Tumewafungulieni migodi yenu tukiamini kwamba nanyi mtatimiza wajibu wenu wa kulipa kodi kwa mujibu wa sheria. Mkishindwa kulipa, hatutosita kuifungia," alibainisha Nyongo.

Naibu Waziri Nyongo yupo Mkoani Mara kwa ajili ya shughuli za ukaguzi wa migodi na kuzungumza na wachimbaji wadogo.

PICHA: Akamatwa uwanja wa ndege Dar akiwa ameficha dola 83,000

$
0
0
Mwezi mmoja baada ya kumnasa Mganda akiwa anasafirisha kwa ndege Dola za Marekani milioni moja, Jeshi la Polisi limedai kunasa mfanyabiashara wa vipuri vya magari akiwa na Dola za Marekani 123,000 (Sh. milioni 274.4) dakika chache kabla hajaingia kwenye ndege iliyokuwa inakwenda Dubai.

Kamanda wa Viwanja vya Ndege, Matanga Mbushi, jana alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi saa 9:30 alasiri kwenye eneo la kuondokea 'Terminal II' la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam.

Akieleza zaidi kuhusu tukio hilo, Mbushi alisema polisi kwa kushirikiana na maofisa wa usalama na Mamlaka ya Mapato (TRA) walimkamata abiria huyo, aitwaye Boniface Mbilinyi (32) mwenye hati ya kusafiria AB 757247.

Alisema kuwa mfanyabiashara huyo ambaye ni mkazi wa Tabata Segerea jijini alikuwa anasafiri kwa ndege ya Shirika la Emirates kuelekea Dubai kwa shughuli za kibiashara.

“Baada ya kupita kwenye mashine, alionekana ana fedha nyingi, akaenda kutoa taarifa ya kiasi cha Dola 40,000 badala ya fedha zote na hivyo kiasi cha Dola 83,000 hakukitolea taarifa,” Mbushi alisema.

Aliongeza: "Tunaendelea na mahojiano na iwapo yatakamilika leo (jana), faili litapelekwa kwa mwanasheria kwa ajili ya kufikishwa mahakamani. Kosa lake ni kushindwa kutoa taarifa ya fedha anazosafiri nazo.”

Alipoulizwa kama wameshabaini sababu za mfanyabiashara huyo kushindwa kutolea maelezo fedha hizo, Mushi alisema: "Ni kutokujua sheria. Sheria bado inawasumbua watu, inahitajika elimu watu waelewe kuwa unapokuwa unasafiri kwenda nje ya nchi na fedha nyingi, lazima utoe maelezo ya fedha husika kwa TRA."

Kamanda Mushi alibainisha kuwa mfanyabiashara huyo ni muuzaji wa vipuri vya magari, hivyo alikuwa anakwenda Dubai kununua vifaa hivyo.

Alisema kiasi hicho cha fedha kimehifadhiwa kwenye akaunti ya Dola ya FIU yenye namba 20110028135.

Tukio hilo ni la pili kwa uwanja huo ndani ya kipindi cha takribani mwezi mmoja baada ya Desemba 11 Mganda Winfrida Vusinge kukamatwa na Dola za Marekani milioni moja (Sh. bilioni 2.23) alizokuwa anazileta Tanzania kwa lengo la kuziweka kwenye Benki ya Stanbic.

Kwa mujibu wa Kamanda Mushi, raia huyo wa Uganda tayari alishafikishwa mahakamani kwa kukiuka sheria za nchi.


Mbunge CHADEMA Awataka Wananchi Wachome Moto Nyumba Yake

$
0
0
Mbunge  wa Jimbo la Mbozi (Chadema), mkoani Songwe, Pascal Haonga, amejitabiria mabaya baada ya kuwataka wananchi kuchoma nyumba yake iwapo atahamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Haonge amewataka wananchi hao kufanya hivyo kutokana na baadhi ya viongozi wa upinzani hususan madiwani na wabunge kujiuzulu na kuhama vyama vyao.

Idadi kubwa ya madiwani wa upinzani wamejiuzulu na kuhama vyama vyao na kujiunga na CCM wakati wabunge watatu hadi sasa wamejiuzulu na kuhama vyama vyao ambao ni Godwin Mollel (Siha-Chadema) aliyehamia CCM, Lazaro Nyalandu (Singida Kaskazini-CCM) aliyehamia Chadema na Maulid Mtulia (Kinondoni-CUF) aliyejiuzulu na kujiunga na CCM.

Haonga alitoa maelekezo hayo Jumamosi alipowahutubia wananchi wa Mji wa Mlowo wilayani Mbozi, ambapo alisema hawezi kuwasaliti wananchi waliosimama kidete kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa 2015 kuhakikisha anapata ushindi.

Alisema wakati wa uchaguzi kulikuwa na matukio ya vurugu katika jimbo hilo huku baadhi ya watu wakipoteza biashara zao, kujeruhiwa na wengine waliwekwa ndani kwa ajili ya kupigania ushindi wake na wa Chadema, hivyo hawezi kuwasailiti.

Aliwaponda baadhi ya wabunge na madiwani wa chama hicho na vyama vingine vya upinzani wanaohamia CCM kwa madai ya kuunga mkono Serikali ya awamu ya tano kuwa hawatumii akili bali wanatumia matope.

“Najua baada ya baadhi ya wasio na msimamo kuanza kuhamia CCM, mmepata hofu kuwa hata kwangu itakuwa hivyo, niwahakikishie mimi siwezi kulamba matapishi yangu, kuna watu mlipigwa mabomu ya machozi, kuna watu walifungwa na kuna wengine walijeruhiwa kuhakikisha tunashinda, ikitokea hivyo kateketezeni nyumba yangu,” alisema Haonga.

Aidha Mbunge huyo alisema kuna baadhi ya viongozi wa CCM wanajinadi wanataka kulirejesha jimbo hilo mikononi mwao na kwamba hawataweza kwa kuwa chama hicho hakiaminiki tena na wananchi.

Alisema kwa sasa wanajipanga kuhakikisha wanapata ushindi mkubwa kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani, ili kujihakikishia ushindi zaidi kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Aidha, alisema anaendelea kuzitumia fedha za Mfuko wa Jimbo kuboresha miundombinu zikiwamo zahanati, vyumba vya madarasa kwenye shule za msingi na sekondari pamoja na barabara ili kuwapunguzia wananchi mzigo wa kuchangia.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mafunzo Chadema Kanda ya Nyasa, Mdude Nyagali, alisema madiwani na wabunge wanaohamia CCM wakidai wanaunga mkono Serikali ya awamu ya tano ‘wananunuliwa’.

Alisema mbwembwe za viongozi wa CCM katika Mkoa huo kutaka kurejesha majimbo yote ya upinzani kwenye uchaguzi Mkuu wa 2020 ni ndoto na haitatokea.

Vilevile alisema baadhi ya viongozi na wanachama wa CCM wanaodai Chadema kinaelekea kufa, watakufa wao na sio chama hicho ambacho alidai kinakubalika kila eneo kwa sasa tofauti na miaka iliyopita.

Alidai uchaguzi wowote kura za CCM hazipo maeneo ya vijijini wala mjini bali zipo kwenye vyombo vya Dola likiwemo Jeshi la Polisi.

“Watawezaje kurejesha majimbo yetu wakati waliahidi milioni 50 kila kijiji, zahanati kila kijiji na kuboresha miundombinu ya barabara ambayo mpaka sasa hawajatekeleza?” Alihoji.

Diwani wa Kata ya Mlowo, Sebastian Kilindu, aliwataka wananchi wa kata hiyo kumkatakata mapanga endapo ‘atanunuliwa’ na CCM.

Alisema kwa sasa ana misukosuko mingi ya kisiasa katika wilaya hiyo, hasa kwenye vikao vya Baraza la Madiwani kwa madai baadhi ya viongozi wa Halmashauri wanaongoza kimabavu.

Wizara Nne Zakutana Kushughulikia Changamoto Za Uwanja Wa Ndege JNIA

$
0
0
Na John Bukuku
SERIKALI kupitia wizara zake nne tofauti zimeamua kufanya jitihada za kuondoa changamoto ya  msongamano wa wageni wanaiongia na kutoka nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere(JNIA) jijijini Dar es Salaam.

Pia kuondoa changamoto ya joto katika eneo la kuchukulia mizigo pamoja na kushughulikia hati za kusafiria kwa wageni wanaoingia nchini pamoja na changamoto ya ufinyu wa eneo la kusubiri huduma uwanjani.

Wizara hizo zimekutana jana katika uwanja huo na kufanya ziara ya kukagua shughuli za utoaji huduma kwa wageni na kubaini mambo kadhaa.

Mawaziri hao ni Wizara ya Maliasili na Utalii Dk.Hamis Kigwangala, Wizara ya Mambo ya Ndani Dk.Mwigulu Nchemba, Wizara ya Mambo ya Nje kupitia Naibu Waziri Dk.Susan Kolimba na Naibu Waziri wa Ujenzi na Mawasiliano Atashasta Nditiye.

Akizungumza uwanjani hapo baada ya kufanyika ziara hiyo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Dk. Susan Kolimba alisema  wanaridhishwa na hatua zinazochukuliwa za kuondoa changamoto zinazoelezwa kuwepo katika uwanja huo.

 Alisema baada ya kufanya ziara na kuona namna ambavyo huduma zinatolewa kwa wageni mbalimbali wanaoingia nchini ameridhishwa na hatua ambazo zinachukuliwa ni hakika zitaondoa kero hizo haraka.

“Awali mgeni alikuwa anahudumiwa kwa saa tatu lakini hivi saa mgeni anahudumiwa kwa saa moja,”alisema Dk.Kolimba.

Kwa upande wa Waziri wa Mambo ya Ndani Dk.Mwigulu Nchemba alisema jitihada zinafanywa kutatua changamoto hizo na kuna matumaini makubwa ya kuzipatia ufumbuzi kwa haraka.

“Hatua ambazo wizara yetu inachukua ni kuharakisha utoaji huduma wa hati ya kusafiria kwa njia ya kieletroniki badala ya mfumo wa sasa na  siku za karibuni mchakato utakamilika.

“Pia wizara yetu itaongeza idadi ya madawati ya kutolea huduma kwa wageni ikiwa sambamba na kuongeza watoaji huduma uwanjani hapo,”alisema.

Alifafanua kuwa taarifa zinaonesha kwa sasa kuna unafuu mkubwa wa kutoa huduma kwani badala ya saa tatu ambazo zilikuwa zinatumia awali hivi sasa muda wa utoaji huduma umeshuka hadi saa moja.

“Mbali ya kuboresha huduma kwa nafasi yetu tutahakikisha pia tunaongeza ulinzi na usalama katika viwanja vyetu vyote nchini ili kudhibiti wageni wenye nia ovu na nchi yetu,”alisema.

Akizungumza changamoto zilizopo uwanjani hapo Waziri wa Maliasili na Utalii Dk.Kigwangala alisema wamefikia hatua hiyo baada ya baadhi ya wageni na hasa watalii wanaiongia nchini kulalamika.

Alitaja baadhi ya malalamiko ni kwamba wanatumia zaidi ya saa tatu kupata huduma wakiwa uwanjani hapo.Pia joto kali na ufinyu wa eneo katika eneo ambalo wageni wanasubiri kuhudumiwa.

Hivyo Dkt.Kigwangala alisema kutokana na malalamiko hayo na mengine kadhaa hatua mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa na kueleza Agosti 8 mwaka 2017 manaibu waziri wa wizara hizo nne walikutana kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi.

Alisisitiza ukarimu kwa wageni ni muhimu katika maeneo mbalimbali ya utoaji huduma, akitoa mfano  kuwa hata polisi uwanjani hapo katika kutekeleza majukumu yao ni vema wakawa wakarimu licha ya kwamba wakati mwingine wamedaiwa kutumia nguvu.

 “Ni vema sasa wakawa na ukarimu ndani yake ili mgeni adhibitiwe kistaarabu kwa yule ambaye atakuwa ameshikiliwa kutokana na sababu yoyote akiwa uwanjani hapo”.

Alisema anatamani kuona kuanzia uwanja huo wa ndege hadi hotelini ambako mgeni anakwenda anatumia muda mchache, anapata nafasi ya kuona picha za viongozi mbalimbali ambazo zitakuwa uwanjani , picha za wanyama na video zinaonesha utalii wa Tanzania.

“Kumpokea mgeni jambo moja lakini namna ya kumhudumia ni jambo jingine na ndilo muhimu zaidi.Tunataka mgeni afurahie kuwa Tanzania,”amesema.

Wakati huo huo  Naibu Waziri wa Ujenzi na Mawasiliano, Nditiye alisema wizara yao tayari imechukua hatua za kuondoa changamoto zilizopo ikiwamo ya kufunga viyoyozi(AC) kwa ajili ya kuondoa hali ya joto.

Alisema AC zilizopo ni za muda mrefu kwani ziliwekwa tangu majengo ya uwanja huo yalipojengwa.Pia unafanyika ukarabati wa kuongeza eneo kwa ajili ya wageni wanaosubiri kuhudumiwa.

Aliongeza kuna jitihada ambazo Serikali inafanya za kuondoa msongamano wa wageni ikiwamo ya kuharakisha ujenzi wa jengo jipya la kusafiria wageni la Terminal III litakalohudumia watu milioni sita badala ya jengo la sasa ambalo lengo lake lilikuwa kuhudumia watu milioni moja.

“Ujenzi wa jengo jipya umekamilika kwa asilimia 70 na litakapokuwa tayari kwa asilimia 100 litaanza kutumika kwani kasi ya ujenzi inakwenda vizuri,’alisema.

Askofu Kakobe aelezea alivyohojiwa na TRA

$
0
0
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe amewaelezea waumini wake jinsi alivyohojiwa na timu mbili zilizoundwa kwa nyakati tofauti na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Askofu Kakobe, ambaye ameingia kwenye mgogoro na mamlaka za nchi tangu aeleze kuwa ana utajiri mkubwa, alisema hayo wakati wa ibada iliyofanyika katika kanisa lake lililopo Mwenge jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mara ya pili kuzungumzia sakata hilo kwa waumini wake tangu Desemba 31 mwaka jana.

Hata hivyo, Kakobe alisema kutoa mrejesho huo hakuwazuii TRA kueleza waliyobaini, lakini amesema ameona azungumze mapema na waumini wake kwa kuwa ndio watoa sadaka na wana haki kwa asilimia 100 kujua kinachoendelea kanisani kwao.

“Baada ya kuleta barua, Januari 2, kiongozi wa tume iliyoundwa awali na kikosi chake walifika na tuliwapa ushirikiano. Nilikuwa nao katika ofisi ya kiuchungaji kwa mahojiano, walikuwa na karatasi za maswali na majibu waliyaandika,” alisema.

“Waliuliza kuhusu utajiri wangu, niliwaambia nina nyumba moja tu duniani ipo Kijitonyama niliijenga kwa gharama ya Sh2 milioni na kiwanja nilinunua Sh30,000. Ni nyumba ya kawaida na ipo katika mtaa wa kawaida uitwao kwa Kakobe. Utafuteni mtaiona nyumba yangu.”

Askofu Kakobe alisema aliwaeleza wazi kuwa ana waumini wake ambao hawakuridhishwa na anapoishi, hivyo walitamani awe na sehemu nzuri itakayoweza kufaa kwa ajili ya wageni wa kimataifa wanaoweza kuwatembelea. Alisema walimshirikisha hilo na walijenga eneo jingine kwa michango yao miaka 10 iliyopita.

Alisema suala la akaunti za kanisa aliliweka wazi na kuwaambia kuwa kuna akaunti benki ya NBC na akaunti ya mfuko wa kitaifa wa FGBF iliyopo pia NBC Meru, Arusha.

“Niliwaambia wazi mimi wala mke wangu hatuna akaunti benki. Binafsi sina mradi wowote, sina shamba, sina kuku hata mmoja, paka na wala panya niliyefuga. Niliwaambia hata kanisa hatuna mradi wowote wa kiuchumi na hivi ndivyo tunavyoishi,” alisema.

“Mmoja akaniuliza kwa nini hamna mradi wa kiuchumi, nilimweleza huo ni wito wetu. Wakatoa karatasi moja ya kumbukumbu za TRA wakasema kuna shule moja inaitwa Full Gospel si yenu? Nikasema hatuijui ila ni neno ambalo linatumika kote duniani. Mkifuatilia vizuri mtajua wenye shule ni ya kina nani.”

Alisema walimuuliza iwapo ameajiri watu kanisani, akasema kuna watumishi zaidi ya 1,000 ambao hawalipwi wanafanya kazi ya Mungu na huo ndiyo mfumo wa kanisa.

Alisema walimuuliza kuhusu ukusanyaji wa sadaka, maisha yake bila ya kuwa na mradi wowote na baadaye waliitwa wakusanyaji sadaka kwa mahojiano zaidi.

“Wakauliza kutoka kwa hicho kikosi ‘bahasha za maombi maalumu ambazo huelekezwa kwa mchungaji zinakuwa nzito sana’, wakasema zinakuwa za kawaida tu. Wakaniambia kwa uzoefu wako kiasi gani huwa kinapatikana kwa mwezi, nikawaambia hufika hata Sh5 milioni lakini wakati mwingine kinaweza kwenda chini.”

Alisema baada ya hapo walihojiwa watoto na mke wake na kijana wake mmoja na majibu yakawa yaleyale. Alisema walichukua baadhi ya kompyuta na nyaraka muhimu kwa ajili ya uchunguzi na baadaye walitoa maoni yao.

“Kilichofuatia ndicho kilichonifanya nitoe mrejesho kabla ya TRA. Yule kiongozi niliyekabidhiwa na TRA alitoa ripoti inayoonyesha sina miradi wala vyanzo vya fedha, kinachosalia ni sadaka na wao hawahusiki nazo,” alisema Kakobe.

“Baada ya kiongozi huyo kutoa ripoti hiyo, aliondolewa katika hiyo kazi na hivi tunavyozungumza amepelekwa mkoani. Nikasema sasa nitamwaga mboga leo, nikasema hapa kuna hila, nitaitungua ndege kabla haijapaa.”

Askofu Kakobe alisema baada ya kiongozi huyo kutimuliwa ameletwa kiongozi mwingine na kazi imeanza upya, “Wamekwenda nyumbani kwangu wamekagua chumba kwa chumba, vyumba vyote nguo za wanangu, mke wangu; wanachambua nguo mojamoja yaani wanasagula kama mtumbani. Wamekuja ofisini hivyohivyo. Wameenda kwa viongozi wangu wamefanya hivyohivyo,” alisema.

Alisema wamehoji wapi anapeleka fedha na kuwapa mrejesho kuhusu safari zake za ndani na nje ya nchi lakini hawajaridhika.

“TRA sasa ipo ndani ya sadaka. Hii ni TRA kweli? au kuna jambo? Mimi leo nimemwaga mboga, hata (Askofu Josephat) Gwajima aliwahi kutoa mrejesho. Sasa Gwajima na Kakobe ni mapacha. Walikuja ofisini wanakagua chumba kimoja mara kingine nikasema watumishi tuwe macho wasijekutuwekea bangi,” alisema.

Aidha katika hatua nyingine, Askofu Kakobe aliwataka watumishi wa TRA kufuata utaratibu na ikiwa wataanza kukusanya sadaka basi wakusanye makanisa yote.

Alitoa onyo kwa watumishi hao na kusema wanamchonganisha Rais John Magufuli na wananchi wake kwa kuwa haamini kama wametumwa.

“Ninavyomjua Rais John Magufuli ana hofu ya Mungu. Nalikumbuka neno lake la ‘mniombee nisiwe na kiburi’ na sijayasahau. Leo kama anatuma TRA wachunguze sadaka sina imani hiyo. Tunajua kuna watu siku hizi wanatafuta kiki, wanatafuta kupanda vyeo, nakushauri Rais wanaotafuta vyeo kwa staili hii wageukie na uwatumbue,” alisema.

Serikali yataka makanisa yatangaze mapato

$
0
0
Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amewataka viongozi wa dini nchini kutimiza wajibu wao na kuhakikisha wanahifadhi vyema mapato ya fedha na kuyaweka wazi kwa waumini ili kuondokana na migogoro isiyokuwa ya lazima kwenye nyumba za ibada.

Aliyasema hayo jana alipokuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Shinyanga kwenye ibada ya kumuweka wakfu na kitini askofu wa pili wa dayosisi hiyo Johnson Chinyong’ole ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa Kanisa la Angilikana nchini kisha mwaka jana kupendekezwa kuwa askofu.

Kabudi aliwataka viongozi wa dini kutimiza wajibu wao na kuhakikisha wanahifadhi vizuri mapato ya fedha kwa kuhakikisha yanaonekana kwa waumini ili kuondokana na migogoro inayoibuliwa ndani ya nyumba za ibada ikihusishwa na vitendo vya rushwa na ufisadi.

“Tunatambua Kanisa la Angilikana limekuwa mstari wa mbele katika kutoa huduma za kijamii kama maji, elimu na afya pale ambapo serikali imekwama kupafikia. Dayosisi hii ni yenu wala siyo ya wazungu hivyo ni wajibu kwenu kuhakikisha mapato ya fedha anaonekana ili kuondoa migogoro isiyokuwa ya lazima kati ya viongozi na waumini,” alisema Waziri Kabudi.

Aliongeza: “Serikali haina dini lakini ni wajibu wa kila Mtanzania kuwa na dini yake hivyo viongozi wa dini wanatakiwa kuwa kiungo kati ya waumini na askofu ikiwa kuwakumbusha kupiga vita rushwa, vitendo vya kishirikina na ufisadi ambao serikali ya Rais Dk John Magufuli imekuwa ikipiga vita kila siku”.

Pia alitoa rai kwa askofu aliyewekwa wakfu na kitini, Chinyong’ole kuwa awakumbushe waumini maadili ya kanisa katika kuwajenga kiroho na kiuchumi lakini pia kutumia uongozi wake kuwajenga waamini ili waweze kushirikiana kwenye mipango mbalimbali ya maendeleo.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika ambaye ni mlezi wa kanisa hilo alisema kuwa kanisa hilo limepitia wakati mgumu kwani kulikuwa na vuguvugu la migogoro kwa baadhi ya waumini kujidai wanazishika nyadhifa ambazo kuzipata zimeonekana kumbe kunautaratibu wake hivyo kushikamana na kwa umoja na kuepuka migogoro.

Askofu Mkuu wa kanisa hilo nchini, Jacob Chimeledya alisema kuwa kuna kazi kubwa na kwamba hali iliyopo ni mapito hivyo aliiomba serikali kulisimamia kanisa hilo kiuchumi kwani tayari limeanza mchakato wa kuanzisha chombo chake cha kusimamia na kuliangalia mali zake.

Tiba Asili ya Kuondoa Michirizi,Tumbo Kujaa Gesi, Maumivu ya Mgongo na Nguvu za Kiume

$
0
0
JE, UNA DALILI HIZI? (Kushindwa kurudia tendo la ndoa)
(Kutojiskia hamu ya tendo la ndoa)
(Maumivu ya kiuno mgongo)
(Tumbo kuunguruma na kujaa ges)
(Uume kusinyaa na kuingia ndan na kuwa mdogo au mfupi)
(Korodani moja kuvimba)
Kama dalili hizi unazo upo kwenye hatari ya kuishiwa nguvu za kiume kabisa,kwa matibabu tumia OZYMIX POWER dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikal ambayo itakuwezesha kurudia tendo LA ndo zaidi ya Mara tatu bila hamu kuisha
PIA KUNA DAWA YA KUNENEPESHA NA KUREFUSHA MAUMBILE YA KIUME

DAWA ZA KIKE ZA KUTENGENEZA SHEPU
(Kusimamisha maziwa yaliyolala)
(Kuongeza makalio)
(Kuondoa michirizi)
(Kumrudisha mwanaume aliekuacha au Asie kupa hela)
KWA MAWASILIANO ZAIDI
0716096205 au FIKA OFISIN au piga simu utaletewa dawa popote ulipo daresalam KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Rais Magufuli ataja sababu za kumuunga mkono Kagame kuongoza Umoja wa Afrika (AU)

$
0
0
Rais John Magufuli amesema Rais Paul Kagame wa Rwanda anafaa kuongoza Umoja wa Afrika (AU) kwa sababu ya historia yake na hivyo anazifahamu changamoto zinazolikabili bara hili.

Rais Magufuli alisema hayo jana Ikulu wakati Kagame alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja, ikiwa ni mara yake ya pili kufanya ziara tangu Rais Magufuli alipoapishwa. Alifanya ziara kwa mara ya kwanza Julai Mosi, 2016.

Magufuli alimwaga sifa hizo akianzia matatizo yaliyoibuka nchini Libya baada ya kiongozi wake wa kijeshi, Muamar Gadaffi kuondolewa madarakani kwa vurugu licha ya kuliongoza taifa hilo vizuri kiuchumi.

“Baada ya kiongozi wa Libya kuondoka, na nyinyi nyote mnajua, matokeo yake ni haya. Na haya ndiyo ya ukweli na utabaki kuwa ukweli,” alisema Rais Magufuli katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jana.

“Nina uhakika Mheshimiwa Kagame atakapokuwa mwenyekiti wetu Afrika, atayaadress (atayashughulikia haya), atayaadress vizuri masuala ya migogoro miongoni mwa nchi za Afrika, atayaaddress vizuri masuala ya ukoloni mamboleo unaoweza kuletwa na mtu yeyote kutoka nje akasababisha matatizo kwa Waafrika.

“Mheshimiwa Kagame hadi kufikia urais anafahamu shida za wananchi wa Rwanda; anajua historia ya Rwanda ilitokotoka hadi ikatokea genocide (mauaji ya watu wengi). Anafahamu mateso ya Wanyarwanda; anafahamu mateso yanayoweza kuletwa na mtu hata mmoja tu, inawezekana ikawa ni media kwa kutangaza au kuandika kitu cha ovyo kikaleta multiplying effect.”

Alisema ndio maana anaamini kutokana na mchango wake kwa Afrika na kwa sababu ni mwanamapinduzi mzuri, uzoefu wake utasaidia maendeleo ya Afrika.

“Rais Kagame ni mwanamapinduzi wa kweli wa Afrika, ameishi maisha ya Kiafrika, maisha ya mateso tangu akiwa kijana; ameishi kwenye nchi za ugenini kama mkimbizi, anayafahamu mateso ya kijana,” alisema.

“Kwa hiyo kwa yale maisha aliyoyaishi kama mkimbizi, kama kijana, nina uhakika ataleta mageuzi makubwa Rwanda ambayo ameshaanza kuyaleta, lakini ataleta mageuzi makubwa Afrika.”

Alisema Tanzania inamuunga mkono Rais Kagame kwa nguvu zote ili kuwepo kwa mabadiliko ya kiuchumi kwa Waafrika wote hasa kwa vijana ambao ndiyo nguvu kazi kubwa katika bara hili.

Makala: Yanayojiri CHADEMA Ndo Hali Halisi Au Kuna Kitu Kingine

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo-Chadema kiko kwenye matatizo. Matatizo yanayotishia uhai wake na uwepo wake kama chama cha siasa nchini. 

Kuna uwezekano mkubwa kwamba hadi hivi sasa siyo viongozi wala wanachama wa chama hicho ambao wametumia muda wa kutosha kuweza kuangalia ni tatizo gani linawakabili.

Tatizo hili ukiwasikiliza wana Chadema na hasa viongozi wao linahusishwa moja kwa moja na utendaji, sera na mwelekeo wa Rais John Magufuli kisiasa nchini. Wapinzani wanamlaumu  Rais Magufuli  kwa kudumaza upinzani  na kutaka  kuua kabisa upinzani nchini.

Kuzuiwa kwa mikutano ya kisiasa kwa vyama vya upinzani, na kuzuiwa kwa wanasiasa kufanya siasa nje za majimbo yao kunatajwa kama  ushahidi wa sababu zinatolewa na wapinzani.

Zaidi pia tuhuma za wanasiasa wa upinzani hasa kwenye maeneo ambayo upinzani umejijenga 'kununuliwa' na hatimaye kuachia nafasi zao za kuchaguliwa kunatajwa kama mkakati wa wazi wa Chama cha Mapinduzi-CCM, kuiua Chadema.

Miezi kadhaa sasa viongozi mbalimbali wa Chadema hasa madiwani wamekuwa wakiachia nafasi zao ambazo walizigombea miaka miwili tu nyuma na kukimbilia CCM wakidai kuwa wanaunga mkono Serikali ya Rais Magufuli.

Matukio mengine ambayo yametishia upinzani na ambayo wapinzani hasa Chadema wanayatumia kuonyesha lengo, nia na dhamira ya Serikali kuumaliza upinzani ni pamoja na mauaji ya nyota iliyokuwa imeanza kung’ara ya kiongozi wa chama hicho kanda ya magharibi aliyekuwa anaibuka kwa umaarufu Alphonce Mawazo. Tukio la mauaji ya Mawazo lilihusishwa na siasa ambalo upinzani umeendelea kudai kuwa uchunguzi wa kina haujafanyika.

Hata hivyo, tukio kubwa zaidi ambalo limewafanya wapinzani waone kuwa wamelengwa  ni jaribio la mauaji dhidi ya Mbunge Singida Mashariki na Mnadhimu Mkuu wa upinzani bungeni Tundu Lissu ambaye alishambuliwa na wale walioitwa “watu wasiojulikana” ndani ya makazi ya wabunge mjini Dodoma mchana wa jua kali.

Swali kubwa ambalo linapaswa kuulizwa; je kununuliwa kwa madiwani na wabunge peke yake kunatosha kuelezea kinachoendelea Chadema? 

Je, kuna uwezekano kuna jambo jingine ambalo linaendelea ndani ya chama hicho ambalo viongozi wake ama kwa hofu ya kufungua sanduku la pandora wanaogopa kuona kilichomo kwani hawataweza tena kulifunga? 

Je, inawezekana kuna vitu vingine ambavyo wanachama wa kawaida hawajaambiwa na kinasumbua ndani ya Chadema?

Tukio la aliyekuwa mgombea wa Chadema kwenye Urais na Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kwenda kukutana na Rais hivi juzi kimewaumiza wanachama wengi na baadhi ya viongozi walikutwa hawakujiandaa na taarifa hizo.

 Baadhi ya wanachama na hata viongozi wameanza mara moja kutaka Lowassa aondolewe au aondoke huku wengi wakionekana sasa hivi hawamtaki tena. 

Kwa baadhi yetu hii inashangaza kwani miaka miwili tu nyuma viongozi na wanachama wale wale ambao walikubali kubadili gia angani walizungusha mikono na kuimba “mabadiliko-Lowassa, Lowassa – Mabadiliko”. Kwa Lowassa kwenda kukutana na Magufuli amekuwa tena si nuru, kimbilio, tumaini na nyota ya mabadiliko?

Tayari tumemsikia Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye akianza kumtaja hadharani Tundu Lissu aliyeko kwenye matibabu Ubelgiji kama mtu ambaye anapaswa kubeba bendera ya Urais mwaka 2020. 

Hii itakuwa kinyume kwani tayari Chadema walishaanza kumtaja Lowassa kama mgombea wao tena? Je, watambadilishia gia Lowassa na kumchukua Lissu ambaye anaonekana kama anaweza kweli kupambana na umaarufu wa Rais Magufuli? 

Na swali jingine ambalo wapo wanaoweza kuliuliza ni je; Lissu atakuwa na tofauti ya kiutawala kumlinganisha na Rais Magufuli? Watatofautiana nini hasa? wengine wanaweza kuhoji.

Licha ya hilo, Lissu pia anatajwa kama mtu sahihi wa kurithi mikoba ya Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe ambaye ndani ya uongozi wake Chadema inajikuta mara nyingi kwenye mgogoro mkubwa wa kisiasa. 

Swali linaloweza kuwagawa tena Chadema ni je, wale wanaomuunga mkono Mbowe watakuwa tayari kuhamisha utii wao kwenda kwa Lissu? 

Je, inawezekana tena ukatokea mgogoro kama ule uliotokea wakati aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe alipotaka kugombea nafasi ya uenyekiti ndani ya chama na kukutana ugumu ambao uliacha doa kubwa ambalo hatimaye lilimlazimisha kujiondoa na chama hicho na kwenda kuanzisha ACT-Wazalendo.

Zitto sasa ni mbunge wa Kigoma Mjini na yeye kama ilivyo Chadema anakabiliwa na kukimbiwa na viongozi wa chama chake ambao wamechukuliwa na Serikali akiwemo aliyekuwa mgombea wake wa Urais Anna Mghwira, ambaye amepewa Ukuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. 

Alifuatiwa na mmoja wa waanzilishi wa ACT ambaye walitoka na Zitto Chadema Dk. Kitila Mkumbo ambaye aliitwa na serikali na kupewa nafasi ya Ukatibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji. 

Kijana mwingine wa chama hicho ni Mwanasheria anayepanda kila kukicha Albert Msando. Mara baada ya kujiunga na CCM Msando aliingizwa kwenye kamati ya Mwenyekiti Magufuli ambayo ameiunda ndani ya chama kwenda kufuatilia mali za CCM nchi nzima.

Ni wazi kuwa pamoja na zile zinazoonekana juhudi na mkakati wa dhati wa Serikali kudhoofisha upinzani – kitu ambacho si kigeni mahali popote duniani , Inawezekana kuna mambo mengine ambayo hayajafunguliwa vizuri na ambayo yanachangia viongozi wa upinzani walioonekana ni wapinzani kweli kujiondoa kwenye vyama vya upinzani. 

Ni mambo gani haya? Je, viongozi wa upinzani wanaweza kukaa chini na kuangalia wao wenyewe wanaongozaje, na wanafanya nini ndani ya vyama vyao kufanya wazidi kuaminiwa na wanachama na viongozi wenzao?

Je, upinzani ambao haujawa na uthubutu wa wazi wa kujitokeza kuendesha upinzani wa kweli bado unasubiria huruma na hisani ya serikali kufanya upinzani bado utaweza kuhimili mitikisiko ya miaka mitatu ijayo? 

Je, viongozi wa Chadema watakaobakia wataweza kweli kusimama na kufanya upinzani? 

Je, hawana mbinu nyingine au wamekubali masharti ya wao kufanya siasa nje ya yale yaliyowekwa na sheria na Katiba?

Au yawezekana viongozi wetu wa upinzani walichimba shimo ambalo sasa wao wenyewe hawawezi kutoka; shimo la kuvunja uaminifu na sasa wanapata shida ya kuaminiwa tena? Au kuna jingine?

Yaliyojiri kwenye sherehe ya harusi ya Shilole jana

$
0
0
Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva na Mjasiriamali, Shilole ‘Shishi Baby” jana amefanya sherehe ya harusi yake aliyofunga na mumewe Uchebe katika ukumbi ulioko Mikocheni, jijini Dar es Salaam.

Sherehe hiyo ilipambwa na burudani mbalimbali na ilihudhuriwa na mastaa mbalimbali wa filamu na muziki wa Bongo Fleva.

Wasanii mbalimbali waliohudhuria katika sherehe hizo walijaribu kumfurahisha bibi harusi pamoja na mumewe kwa staili tofauti tofauti huku zikiambatana na zawadi kem kem.

Rais wa WCB, Diamond Platnumz alitoa kali ya mwaka katika sherehe ya harusi ya Shilole na Uchebe baada ya kumtaka bibi harusi huyo kuchagua zawadi ambayo anaitaka kutoka kwake. Baada ya Diamond kusema hivyo, Shishi alimuomba Diamondi kumsaidia kuitangaza biashara yake mpya ya Shishi Chili, ambapo Diamond alikubali ombi hilo.

Naye msanii ambaye yuko chini ya lebo ya WCB, Harmonise hakuacha kuonyesha makali yake baada ya kumtaka Shilole atafute gari aina ya Toyota Noah, yenye thamani ya shilingi za kitanzania, milioni 9 ambayo yeye (Harmonise) atailipia na itatumika katika kurahisisha biashara za Shishi.

Kwa upande wao Jux na Vanessa nao hawakubaki nyuma, ambapo Jux aliahidi kumlipiaa ada ya mwaka mzima mtoto wa Shilole katika shule anayosoma, huku mpenzi wake Vanessa akijitolea kuwalipia Hoteli ya Nyota tano ya kilimanjaro, Shilole na mumewe Uchebe.

Msanii Shilole ambaye pia ni muigizaji wa filamu hapa nchini, amejikita kwenye ujasiriamali ambapo kwa sasa anamiliki mghahawa pamoja na bidhaa ya ‘shishi chili’.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Rais Magufuli aomboleza vifo vya watu 11 Kagera

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu kufuatia watu 11 kupoteza maisha katika ajali ya gari iliyotokea katika Kijiji cha Nyangozi, Wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera.

Ajali hii imetokea jana tarehe 14 Januari, 2018 majira ya saa 11 jioni baada ya basi dogo la abiria aina ya Nissan Caravan lililokuwa likitoka Kakonko Mkoani Kigoma kuelekea Kahama Mkoani Shinyanga kuligonga ubavuni lori la mizigo kisha kugongana uso kwa uso na lori jingine na kusababisha vifo vya watu 11 na wengine 6 kujeruhiwa.

Mhe. Rais Magufuli amepokea kwa huzuni na masikitiko makubwa taarifa za vifo vya Watanzania hao na amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu kumfikishia pole kwa familia za Marehemu wote, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na vifo hivyo.

“Nimehuzunishwa na kusikitishwa sana na vifo hivi, nawapa pole wafiwa wote, ninawaombea marehemu wapumzike mahali pema na majeruhi wapone haraka ili waweze kuungana na familia zao na kuendelea na shughuli zao za kila siku”  amesema Mhe. Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewakumbusha watumiaji wa barabara hasa madereva kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabarani na ameviagiza vyombo vinavyohusika kuongeza jitihada za kukabiliana na ajali za barabarani ili kuokoa maisha ya watu na mali zinazopotea kutokana na ajali.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
15 Januari, 2018

Serikali yatoa ufafanuzi Kuzuia matumizi fedha za kigeni

$
0
0
Serikali imesema haijazuia matumizi ya fedha za kigeni nchini bali imechukua hatua ya kudhibiti matumizi ya fedha hizo kulinda thamani ya shilingi ya Tanzania.

Kauli hiyo imetolewa leo Januari 15, 2018 na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji alipokutana na wawakilishi wa wafanyabiashara mkoani Arusha kujadiliana mambo mbalimbali kwa ajili ya kukuza sekta ya biashara nchini.

Amesema sheria haijazuia matumizi ya fedha hizo nchini, inasisitiza kuwa watu wanapaswa kutambua kuwa sarafu ndiyo fedha halali kwa malipo ndani ya nchi.

“Tatizo kubwa tunalokumbana nalo ni uhuru ulioachiwa unaosababisha kushuka kwa thamani ya shilingi yetu. Kila mmoja anaweza kutumia fedha za kigeni, pia watumiaji wa fedha za kigeni hawafuati thamani ya fedha iliyoko sokoni. Kila mmoja anakuwa na kiwango tofauti cha thamani ya kubadili fedha,” amesema Dk Kijaji.

Amebainisha kuwa ili kuondoa changamoto hizo Serikali imeamua kurekebisha sheria ya matumizi ya fedha za kigeni na sheria ya Benki Kuu (BoT) ambayo inazitaka bei zote nchini zitangazwe kwa shilingi ya Tanzania.

Amesema bei hizo zinajumuisha kodi za nyumba za kuishi na ofisi, bei za ardhi, gharama za elimu na afya, bei za vyombo vya usafiri na vifaa vya kielektroniki.

“Bei ambazo walengwa wake wakuu ni watalii au wateja ambao sio wakazi zinaweza kutangazwa kwa fedha za kigeni na malipo yake yanaweza kufanyika kwa fedha za kigeni,” amesema na kuongeza,

“Hata hivyo kama mlengwa akitaka kulipa kwa shilingi ya Tanzania asilazimishwe kulipa kwa fedha za kigeni.”

Amezitaka vyombo vya dola kuchukua hatua za kisheria kwa wote watakaokiuka maagizo hayo yaliyotolewa na Serikali.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images