Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kamishna wa Maadili Awataka Viongozi Kutoa Ushirikiano Wakitakiwa Kuwasilisha Benk Statement

0
0
Kamishna wa Maadili Jaji (Mst) Harold Nsekela amewataka viongozi wa umma kutoa ushirikiano kwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi pindi watakapotakiwa kuwasilisha pamoja na nyaraka nyingine “bank statement zao” kama sehemu ya tamko la raslimali na madeni.

Akizungumza na waandishi wa habari jana (11/1/2018) ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Kamishna Nsekela alisema Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na 13 ya mwaka 1995 inampa mamlaka ya kumuagiza kiongozi kuwasilisha nyaraka za mali anazomiliki zikiwemo hati za mashamba, viwanja, kadi za magali na benk statement kama sehemu ya tamko la raslimali na madeni ya kiongozi.

“Nikiwaandikia barua viongozi kuwataka kuwasilisha benk statement na nyaraka nyingine za mali wanazomiliki watoe ushirikiano kwasababu ni matakwa ya kisheria,” alisema.

Kamishn Nsekela alieleza kuwa baada ya zoezi la kupokea tamko kukamilika tarehe 31 Desemba, 2017, zoezi linaloendelea kwa sasa ni kuchambua matamko hayo ili kuona ni viongozi wapi wataanza kuhakikiwa mali zao.

“Tukifikia wakati wa kuhakiki mali za viongozi baada ya uchambuzi wa matamko yao, watatakiwa kutoa ushirikiano. Tutataka wathibitishe mali hizo walizipataje?,” alisema na kuongeza kuwa viongozi hawatakiwi kuwa na hofu pindi wanapotakiwa kuhakikiwa mali zao kwasababu sheria ya maadili haiwazuii kumiliki mali, isipokuwa wathibitishe walivyozipata.

Kwa mujibu wa Kamhsina Nsekela, Sekretarieti ya Maadili haipokei tamko kuwatunzia viongozi bila kulifanyia kazi ndio maana, lazima zoezi la uhakiki lifanyike.

“Hatupokei matamko ya viongozi kuwatunzia, lazima tuthibitishe waliyoandika ndani vinginevyo hatuna sababu ya kuwepo,” alisema.

“Viongozi wa Umma lazima waelewe kuwa tukienda kuhakiki mali zao, lengo ni kutaka kuthibitisha mali walizonazo nan ni jukumu letu kufanya hivyo sio kuwatuhumu.”

Live Zanzibar: Sherehe za miaka 54 ya Mapinduzi Zanzibar

0
0
Tazama hapa moja kwa moja kutoka Zanzibar, kufuatilia maadhimisho ya sherehe za miaka 54 ya Mapinduzi ya Serikali ya Zanzibar. 

Mgeni rasmi wa sherehe hizo ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, pia katika sherehe hizo wapo viongozi mbali mbali wa kitaifa wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. John Pombe Magufuli

TLS yakusanya mamilioni kugharamia matibabu ya Tundu Lissu

0
0
Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kimesema kimefanikiwa kukusanya Sh138 milioni kugharamia matibabu ya Rais wa Chama hicho, Tundu Lissu aliyelazwa Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven nchini Ubelgiji.

Taarifa iliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa TLS, Godwin Ngwilimi amesema kiasi hicho wamekipata kutoka kwa watu mbalimbali walijiotolea kuchangia wa ndani na nje ya nchi wakiwemo wanachama wa chama hicho.

Kuhusu mchanganuo wa fedha hizo, Ngwilimi amesema kimetumika kulipa gharama za matibabu ya Lissu katika Hospitali ya Nairobi, Leuven na visa kwa watu watatu wakiwa nchini Ubelgiji.

Ngwilimi ametoa shukuran kwa wale wote waliojitokeza kuchangia matibabu ya Lissu ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki na mwanasheria mkuu wa Chadema.

Lissu aliyeshambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa katika makazi yake mjini Dodoma ambapo alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na usiku wa siku hiyo alihamishiwa Hospitali ya Nairobi alikolazwa hadi Januari 6 baada ya kahamishiwa Leaven, Ubelgiji kwa mazoezi ya viungo na saikolojia.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Hapa ndio itakapokuwa Radio na TV Station ya Diamond Ambayo Itaanza Kuruka Mwezi wa Pili

0
0
Kampuni ya Wasafi Classic (WCB), inayomilikiwa na msanii maarufu wa muziki wa Bongofleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’ wanatarajia kufungua televisheni na redio Februari mwaka huu.

Haya yamebainika ikiwa ni saa chache tangu Diamond na viongozi wa kampuni hiyo watupie jumba la kifahari  ambalo linaelezwa  litakuwa ndiyo  makao makuu ya WCB ambapo mbali ya kuwa na studio za kurekodia muziki pia litakuwa na Redio na TV.

Katika mahojiano hayo, Fela amesema hatua waliofikia ni katika harakati za kampuni hiyo kuendelea kujitanua na kutoa fursa kwa vijana wengi zaidi.

Meneja wa Diamond, Said Fela  amesema pamoja na kwamba wao ni watu wanaojishughulisha na kazi za burudani, lakini TV yao na redio zitakuwa zinarusha vipindi vya aina zote vikiwemo vya kuelimisha na habari kama vilivyo vituo vingine.

“Kwetu sisi hii tunaona ni hatua nzuri kwa kuwa tunajua tukifungua vituo hivi ndivyo kadri tunavyozidi kuzalisha ajira na tumeamua kutumia wataalam ambao walikuwa kwenye fani hiyo ikiwemo wazee waliostaafu katika Shirika la Utangazaji(TBC) enzi hizo TVT kwa ajili ya kutuongoza kwa kuwa sisi wenyewe hatuwezi,”amesema Fela.

Hata hivyo, alipoulizwa kama wamejenga wenyewe mjengo huo au Fela amesema wamekodisha kama walivyokuwa wamekodisha ile ya Sinza huku sababu za kuhama akieleza ni kutokana na kuongeza huduma na pia sehemu waliyokuwepo kulikuwa na taabu ya maegesho ya magari na kujaa maji hasa mvua zinaponyesha.

Mjengo huo wa wasafi wa ghorofa moja ambao upo maeneo ya Mbezi umeonekana kuwa gumzo  katika mitandao ya kijamii na watu wengi wamempongeza Diomond na uongozi wake kwa hatua aliofikia.

Mbali na redio, tayari Diamond ameshajiingiza katika biashara nyingine ikiwemo ya manukato yanayoitwa 'Chibu', na 'Diamond karanga'

Jalada Kesi Ya Malinzi Larudi Takukuru

0
0
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) amewarejeshea TAKUKURU jalada la kesi ya utakatishaji wa fedha inayomkabili aliyekuwa rais wa (TFF), Jamal Malinzi na wenzake ili warekebishe vitu vichache vya kiuchunguzi.

Mbali ya Malinzi, wengine ni Katibu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mhasibu wa shirikisho hilo, Msiande Mwanga.

Hayo yameelezwa jana na Wakili wa TAKUKURU, Leornad Swai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, wakati shauri hilo lilipoitishwa kwa ajili ya kutajwa.

Swai amedai jalada la kesi hiyo limesharudi TAKUKURU likitokea kwa DPP, hivyo wamepewa maelekezo ya kukamilisha baadhi ya uchunguzi.

Baada ya kueleza hayo, wakili wa Utetezi Nehemia Nkonko aliomba upelelezi wa shauri hilo ukamilike kwa haraka kwa sababu washtakiwa wapo ndani.

Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi January 25, 2018 kwa ajili ya kutajwa.

Mahakama yawahukumu waliokutwa na dhahabu ya mamilioni

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewahukumu kifungo cha miaka mitano jela  au kulipa faini ya  Sh6 milioni, wafanyabiashara wawili, Naushad Mohammed Suleiman (63) na Ali Makame Juma (36) baada ya kupatikana na hatia ya kusafirisha vipande saba vya madini ya dhahabu  vyenye thamani ya Sh 989.7 milioni bila kuwa na leseni.

Pia, mahakama hiyo imetaifisha dhahabu yote iliyokamatwa pamoja na mabegi mawili ya fedha mbalimbali kutoka nchi 15 duniani, walizokamatwa nazo, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aman Karume uliopo Zanzibar.

Hukumu hiyo imetolewa jana Alhamisi, Januari 11 na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri baada ya washtakiwa hao kukiri mashtaka yanayowakabili.

“Ili iwe fundisho kwa watu wengine, katika kosa la kwanza mahakama inawahukumu kulipa faini ya Sh.milioni 2 ama jela miaka 2, pia kosa la pili faini Sh.mil 4 ama jela miaka 3, mkishindwa mtaenda jela na kutumikia vifungo hivyo sambamba,” Alisema Hakimu Mashauri

Wafanyabiashara hao maarufu  ambao ni wakazi wa Zanzibar, walikuwa wanakabiliwa na makosa mawili, ambayo ni kula njama na  kusafirisha madini nje ya nchi kinyume cha sheria na bila kuwa na leseni kutoka mamlaka husika.

Washtakiwa wanadaiwa kukamatwa Novemba 29, 2017,  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aman Karume,  wakisafirisha madini hayo kwenda Dubai katika Falme za Kiarabu.

Hata hivyo, wafanyabiashara hao walilipa faini na kuepuka kifungo hicho.

Steve Nyerere: Naumwa Sana, Aliyeniroga Anisamehe

0
0
Msanii wa filamu, Steve Nyerere amefunguka na kusema kuwa kutokana na matatizo ambayo anapitia ikiwa pamoja na maradhi yake kuna watu wengi wamekuwa wakisema kuwa ameathirika na virusi vya Ukimwi.

Muigizaji huyo amekiambia kipindi cha Enewz ya EATV kuwa anashangaa kwanini kila mtu anaongea lake kuhusu kuumwa kwake huku wengine wakifika mbali zaidi kwa kudai kwamba ameathirika.

“Watu wananifuatilia kutaka kujua hali yangu kwa sababu mimi ni mtu maarufu, ni jambo jema lakini kama kuna watu wamenitupia vitu vya ajabu naomba wanisamehe, mimi ni binadamu labda kuna namna watu nimewakosea,” alisema Steve. 

“Lakini nashangaa kuna watu wanadai imeathirika mmenipima, yaani kila mtu anaongea lake,”

Steve amedai kwa sasa anasumbuliwa na mbavu, miguu na tayari ameanza kupatiwa matibabu.

ACT – Wazalendo watoa neno Maadhimisho ya Mapinduzi ya Zanzibar

0
0
Chama cha ACT Wazalendo kinawatakia Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla maadhimisho mema ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Taarifa kutoka kwa Chama hicho imeeleza kuwa maadhimisho haya ya Mapinduzi ya Zanzibar yawe kichocheo cha kuimarisha misingi ya undugu.

==>Soma taarifa kamili;
SALAMU ZA MAPINDUZI KUTOKA ACT WAZALENDO

Chama cha ACT Wazalendo kinawatakia Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla maadhimisho mema ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Maadhimisho haya ya Mapinduzi ya Zanzibar yawe kichocheo cha kuimarisha misingi ya undugu, umoja na mshikamano miongoni mwa Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla.

Kwa Wazazibari, Miaka 54 ya Mapinduzi iwe fursa maridhawa ya kufanya tafakari na tathmini ya kina. Ni kipindi cha kujiuliza maswali. Je malengo ya Mapinduzi ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuleta haki na usawa yamefikiwa? Vipi kuhusu ustawi wa Zanzibar? Ni kwa kiwango gani Mapinduzi ya Zanzibar yameleta maendeleo yaliyokusudiwa ya kiuchumi na kijamii kwa Wazanzibari Wote?

Ujumbe wa Chama chetu kwa Wazanzibar ni kuwa ustawi wa Zanzibar unahitaji jitihada za Wazanziabari Wote bila kujali tofauti za kisiasa. Maadhimisho ya 54 ya Mapinduzi yawakumbushe Wazanzibari umuhimu wa maridhiano ya kisiasa na kuimarisha undugu kwa ajili ya ustawi wa Zanzibar.

Juma Said Sanani, Makamo Mwenyekiti, ACT Wazalendo, Zanzibar.

12 Januari 2018

Kauli ya Zari kuhusu Diamond Kufungua Kituo cha Redio na TV

0
0
Mama watoto  wa Diamond Platnumz, Zari The Boss Lady amempongeza muimbaji huyo mara baada ya kuweka wazi ujio wa kituo chake cha redio na runinga.

Katika pongezi hizo Zari amemtaja Diamond kama mtu anayejituma zaidi katika kile anachokifanya. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Zari ameandika;

Hongera Damond Patnumz sana kwa juhudi na bidii uliyonayo Allaah akujalie kwa mengine mazuri zaidi. Siku zote umekuwa mpiganaji wa kazi zako, kwa kuwa njia pekee ya kuijenga familia ni kupiga KAZI najua malengo yako Alhamdulillah! #wcbTV #wcbFILMSTUDIO #wcbMUSICSTUDIO #wcbRADIO #wcbHEADQUATERS.

Bila kusahau #DiamondKaranga na chibuperfume #ChibuPerfume 2018 looking good👌🙏

Hapo jana Diamond aliachia video mtandaoni ikionyesha mjengo mpya wa WCB ambao utatumika kama makao makuu ya kampuni hiyo pamoja na studio za Wasafi TV na Wasafi Redio. 

Pia utakumbuka hii si biashara ya kwanza kwa Diamond kwani ameshaingiza sokoni manukato yake ‘Chibu Perfume’ pamoja na Karanga.

Kamati Kuu Chadema kukutana Jumamosi

0
0
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kesho inakutana katika kikao cha ‘dharura’ jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema-Zanzibar, Salum Mwalimu amesema lengo la kikao hicho ni kufanya tathmini ya hali ya kisiasa nchini.

Alipotakiwa kueleza kama lengo la kikao hicho ni kujadili ziara ya waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa kwenda Ikulu, Mwalimu amesema kikao hicho si cha dharura kwani kilipangwa kufanyika Desemba mwaka jana lakini kiliahirishwa kutokana na sikukuu za mwisho wa mwaka.

Amesema ajenda za kikao hicho zilipangwa kabla Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema hajaenda Ikulu hivyo hakina uhusiano na ziara hiyo ila huenda jambo hilo likajitokeza.

“Suala hilo halipo kwenye ajenda ila linaweza kujitokeza na likijitokeza litazungumziwa lisipojitokeza basi,” amesema Mwalimu na kuongeza;

“Hata hivyo kwa upande wake inaweza kuwa fursa nzuri kuielezea Kamati Kuu na viongozi wenzake nini kilitokea.”

Rais Kagame kufanya ziara nchini tarehe 14 Januari

0
0
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda amefunguka na kusema uwezo mkubwa wa Rais Magufuli na Demokrasia ya kweli ni jambo ambalo linawavutia wageni kuja Tanzania akiwepo Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame anayetarajiwa kuwasili nchini Jumapili.

Makonda amesema hayo leo akiwa katika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam baada ya kuagana na Rais Magufuli ambaye ameelekea visiwani Zanzibar kushiriki sherehe za maadhimisho ya Miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

“Amani Demokrasia ya kweli, upendo na uwezo wa mkubwa wa Rais Magufuli ndiyo msingi wa kuwavuta wageni kuja kutembelea hakuna mgeni ambaye anaweza kutembelea nchi ambayo haina upendo, amani na mshikamano. Tanzania chini ya uongozi wa Rais Magufuli inaendelea kuchanja mbuga katika nyanja za kidemokrasia hasa pia katika uwanja mwingine wa kidiplomasia na kuwafanya wageni waone sehemu nzuri ya kuja kutembelea,” alisema Makonda.

Mbali na hilo Makonda amesema kuwa Rais Paul Kagame atawasili nchini Tanzania siku ya Jumapili ya tarehe 14 ambapo atakuwa nchini kwa ziara ya siku moja na kufanya mazungumzo na Rais John Pombe Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Mrema atoa taarifa polisi za kuzushiwa kifo

0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Parole Tanzania, Augustino Mrema amelitaka Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kumchukulia hatua aliyezusha taarifa za kifo chake Januari 9 mwaka huu.

Mrema ambaye ni Mwenyekiti wa TLP Taifa ameyasema hayo mapema leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari nje ya Kituo cha Polisi jijini Dar es Salaam alipokwenda kuripoti tukio hilo.

Amesema, aliyezusha taarifa hiyo alifahamu kwamba Lowassa amekwenda Ikulu kuonana na Rais Dkt Magufuli, hivyo akazusha uongo ili watu wasiwe makini kuhusu kilichojadiliwa Ikulu.

Mrema amesema wapinzani wa Rais ndio walizusha taarifa hizo za uongo na kuzua taharuki kwa sababu yeye ni mtu maarufu na wanajua kwamba kwa kufanya hivyo wangesababisha watu kutofautilia kilichozungumza Ikulu.

Baada ya kusema hayo, Mrema ameweka wazi kwamba anataka kulipwa fidia ya TZS 20 bilioni kutokana na kuzushiwa kifo na kwamba fedha hiyo haitapungua hata shilingi mia.

Serikali Yazipiga Marufuku Shule binafsi kukaririsha darasa au kufukuza Mwanafunzi kwa kutofikia wastani wa shule

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya January 13

Majina ya wafungwa 12 waliopewa msamaha na Rais Dkt Shein

0
0
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Rais wa Zanzibar, Dkt Ali Mohamed Shein, ametoa msamaha kwa wafungwa 12 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe za miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Rais Dkt Shein ametoa msahama kwa wafungwa hao ambao walikuwa wamehukumiwa kwa makosa mbalimbali.

Msamaha huo umetolewa kwa mujibu wa ibara ya 59 ya Katiba ya Zanzibari ya mwaka 1984 ambayo imempa Rais mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa. 

Msamaha huo unatolewa kwa wafungwa kama nafasi ya wao kuanza kuishi maisha mapya na kuachana na vitendo vya kihalifu.

Wafungwa waliopewa msamaha huo ni;
  1.    Abdul-Aziz Abdalla
  2.     Omar Abdalla Nuhu
  3.     Ali Khamis Mrau
  4.     Mussa Ali Vuai
  5.     Hassan Seif Khamis
  6.     Nassor Abeid Issa
  7.     Jihadi Jalala Jihadi
  8.     Edward Jemeria Magaja
  9.     Sleiman Abdalla Amir
  10.     Mtumwa Khamis
  11.     Said Seif Omar
  12.     Masoud Seif Nassor
Katika hatua nyingine, raia wengi 74 wa Zanzibar (baadhi yao wamefariki) wametunukiwa medali na Rais Dkt Shein kutokana na mchango wao mkubwa katika mapinduzi na pia kuleta maendeleo katika visiwa hivyo.

Miongoni mwao, raia 43 wamepewe medali za mapinduzi huku wengine 31 wakipewa medali za mfano kwa utumishi wao uliotukuta kwa wananchi.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls 0658316976
0755911233
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Kingunge arejeshwa Tena Muhimbili

0
0
Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombare Mwiru amerejeshwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili kuendelea na matibabu.

Kingunge aliruhusiwa kutoka hospitalini hapo Januri 10, 2018 ili kwenda kushiriki tukio la mazishi ya mkewe ,Peras Ngombare Mwiru yaliyofanyika jana katika makaburi ya Kinondonbi jijini Dar es Salaam.

Pares alifariki dunia Januari 4, katika hospitali ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa ugonjwa wa kupooza huku Kingunge naye akilazwa hospitalini hapo akiuguza majeraha ya kushambuliwa na mbwa nyumbani kwake, Victoria jijini humo hivi karibuni.

Mtoto wa Kingunge, Kinje Ngombare Mwiru  jana alisema baada ya baba yake kupata kumzika mkewe amerejea hospitalini ili kuendelea na matibabu kama alivyotakiwa na madaktari wake.

“Leo (jana) Mzee (Kingunge)  amerudishwa hospitalini tayari kwa ajili ya kuendelea na matibabu na amelazwa ICU (chumba cha wagonjwa mahututi) cha Mwaisela na hali yake inaendelea vizuri,” alisema Kinje.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images