Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli awatembelea hospitalini mapacha walioungana, Maria na Consolata

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 06 Januari, 2018 amewajulia hali baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Jijini Dar es Salaam wakiwemo Mzee Kingunge Ngombale Mwiru na Mapacha walioungana Maria na Consolata Mwakikuti.

Katika wodi ya Mwaisela, Mhe. Rais Magufuli amemjulia hali Mzee Kingunge Ngombale Mwiru ambaye anatibiwa majeraha baada ya kushambuliwa na mbwa wake, nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Ibrahim Mkoma wa hospitali hiyo amemueleza Mhe. Rais Magufuli kuwa hali ya Mzee Kingunge inaendelea vizuri.

Mzee Kingunge amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kwenda kumuona hospitalini hapo na amemueleza kuwa sasa anajisikia nafuu baada ya kupata matibabu.

Pamoja na kumpa pole na kumuombea apone haraka Mhe. Rais Magufuli amesema anatambua mchango mkubwa wa Mzee Kingunge katika siasa na maendeleo ya nchi.

Katika wodi ya Sewahaji, Mhe. Rais Magufuli amemjulia hali Bw. Richard Kajumulo ambaye ni Kaka wa Mbunge wa Muleba Kusini Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka, Bw. Said Abeid Salim, Bi. Amina Ismail Shirwa, Mzee Hamad Lila na amempa pole Naibu Katibu Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Dkt. Zainab Chaula aliyefiwa na Mama yake mzazi wakati Mhe. Rais akiwa wodini humo.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amewajulia hali mapacha walioungana Maria na Consolata Mwakikuti ambao wamelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa matibabu ya moyo.

Maria na Consolata wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kwenda kuwaona na kuwapa pole na pia wameongoza sala ya kumuombea Mhe. Rais Magufuli na nchi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Prof. Mohamed Janabi amesema matibabu kwa Maria na Consolata ambao ni wanafunzi mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Kanisa Katoliki Ruaha (RUCU) yanakwenda vizuri.

Aidha, Prof. Janabi amesema taasisi hiyo imefanikiwa kutoa matibabu kwa wagonjwa wa moyo 1,400 katika mwaka uliopita na kwamba inashika nafasi ya tatu barani Afrika kwa utoaji wa huduma bora za matibabu ya moyo.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewashukuru na kuwapongeza madaktari wa hospitali ya Taifa Muhimbili na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa wanayofanya kutibu wagonjwa na amesema Serikali itaendelea kutatua changamoto zinazowakabili ili kuboresha huduma zaidi.

“Nawashukuru sana madaktari na wafanyakazi wote, mnafanya kazi kubwa ya kuwatibu wagonjwa, pia mmeboresha hospitali na inaonekana ni safi, mimi niwaahidi kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira yenu ya kazi ili muendelee kutoa huduma nzuri” amesema Mhe. Rais Magufuli.


CCM 'yawarudisha ulingoni' wabunge wa upinzani waliojiuzulu

$
0
0
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinapenda kuujulisha umma wa wanachama wa CCM kuwa kimepokea taarifa kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwa kutakuwa na uchaguzi wa marudio katika Kata na Majimbo yaliyotajwa hapo juu.

Wanachama wote wenye sifa za msingi kwa mujibu wa Katiba ya Nchi na waliokidhi vigezo vya uanachama kwa mujibu wa Katiba ya CCM na Kanuni zake wanahamasishwa kujitokeza ili kuomba ridhaa ya Chama kupeperusha bendera ya CCM katika Uchaguzi huu wa marudio isipokuwa na kama inakavyoelekezwa na taarifa hii.

Aidha Chama kimejipanga kufanya kampeni za kistaarabu na kisayansi, na zilizosheheni siasa za hoja na zinazojikita katika kushughulika na shida za wananchi na hatimaye kushinda kwa kishindo katika uchaguzi huu wa marudio. Kwa maana hii, msisitizo unawekwa kwa wanao omba ridhaa ya kugombea, vikao vya uchujaji na mapendekezo, na vikao vya uteuzi kuzingatia Misingi ya Maadili na kuhakikisha waombaji wana akisi uaminifu, uadilifu, uchapakazi, heshima kwa watu, ukubalifu wa imani, siasa na itikadi ya CCM, nidhamu kwa chama na wawe watu ambao umma wa wananchi unawatambua kwa nafasi yao katika jamii inapokuja katika kushughulika na shida zao.

KWA WAOMBA DHAMANA YA UDIWANI
Wana CCM ambao wamejipima na kujitafakari na kuona wanatosha, wanakumbushwa kwamba kuchukua fomu ya ugombea udiwani katika Ofisi za Kata tajwa hapo juu ni tarehe 8-11 Januari 2018. Mwisho wa kurudisha fomu ni tarehe 11 Januari 2018 saa 10:00 jioni. Gharama ya fomu ni Shilingi 10,000/- tu za Kitanzania.

Wajumbe wa Mikutano Mikuu ya Kata watapiga kura za maoni tarehe 12 Januari 2018. Kamati za Siasa za Kata zitajadili na kutoa mapendekezo kwa Kamati za Siasa za Wilaya tarehe 13 Januari 2018.

Kamati za Siasa za Wilaya zitajadili na kutoa mapendekezo yake kwa Kamati za Siasa za Mkoa tarehe 14 Januari 2018. Kamati za Siasa za Mikoa zitajadili na kutoa mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu za Mikoa tarehe 16 Januari 2018. Halmashauri Kuu za Mikoa zitajadili na kufanya uteuzi wa mwisho tarehe 17 Januari 2018

Wagombea walioteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kushiriki katika uchaguzi wa Udiwani katika Kata nne watachukua fomu kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata katika kata husika tarehe 18-19 Januari 2018 na zoezi hili litafanyika chini ya usimamizi wa Katibu wa CCM wa Wilaya.

UCHAGUZI WA MARUDIO KWA MAJIMBO YA SIHA NA KINONDONI
Baada ya tafakuri na tathimini ya kina, Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kwa mamlaka iliyokasimiwa kwake na Kikao cha Halmshauri Kuu ya Taifa (NEC) imemteua Ndg. Dkt. Godwin Mollel kusimama na kugombea Jimbo la Siha, Mkoa wa Kilimanjaro na Ndg. Maulid Mtulia kusimama na kugombea Jimbo la Kinondoni, Mkoa wa Dar es Salaam.

Aidha wagombea wa Ubunge wanaelekezwa kufika katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Mikoa husika na kupokea maelekezo yahusuyo Uchaguzi kutoka kwa Makatibu wa CCM wa Mikoa hiyo siku ya Jumanne, tarehe 9 Januari 2018 bila kukosa.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Imetolewa na,
HUMPHREY POLEPOLE
KATIBU WA NEC – ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
06 Januari 2018

VIDEO: Mzee Kingune Amwambia Rais Magufuli CCM Ni Chama Chake

$
0
0
Leo Rais  Magufuli amemjulia hali Mzee Kingunge Ngombale Mwiru aliyelazwa katika wodi ya Mwaisela, Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Mzee Kingunge anatibiwa majeraha baada ya kushambuliwa na mbwa. Akiwa katika kitanda cha hospitali amemwambia  Rais Magufuli  kuwa CCM ni chama chake na amekiunda yeye.

“CCM ni chama changu nimetoka tu, tumeachana lakini nimefanya kazi zote, nimekiunda mimi, hakiwezi kuwa kinyume changu,”– Mzee Kingunge 

==>Msikilize Hapo Chini

Kingunge apokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mkewe

$
0
0
Mwanasiasa mkongwe nchini Kingunge Ngombale Mwiru leo Jumamosi amepewa taarifa za kifo cha mke wake Pares Mwiru ambazo imeelezwa kuwa amezipokea kwa mshtuko mkubwa.

Kingunge aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wodi ya Mwaisela akipatiwa matibabu baada ya kushambuliwa na mbwa nyumbani kwake Kijitonyama, alifanyiwa upasuaji Januari 4 mwaka huu.

Leo Januari 6, mtoto wa mwanasiasa huyo Kinje Mwiru amesema wamempa taarifa baba yao saa tano asubuhi leo.

“Tumemfahamisha leo saa tano, ilikuwa ni vigumu sana wakati tunamfikishia taarifa hizo na amezipokea kwa ugumu sana. Haikuwa rahisi kwa yeye kupokea taarifa wakati tunamweleza,” amesema.

Kinje amesema kwa sasa wamemuacha apumzike ili aweze kuwapatia mwongozo nini kifanyike baada ya kifo cha mke wake.

Pares alifariki Januari 4 saa nane mchana katika wodi ya Sewahaji alikokuwa amelazwa, tangu alipofikishwa Muhimbili Oktoba 3, mwaka jana.

Ofisa Uhusiano wa MNH John Stephen amesema kwa sasa afya yake imeimarika.

 "Anaendelea vizuri na afya yake imetengamaa, bado yupo chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari, baada ya upasuaji aliofanyiwa," amesema.

Kauli ya CUF baada ya CCM kumteua Mtulia kuwa mgombea Ubunge Kinondoni

$
0
0
Waheshimiwa Watanzania, tumepigiwa simu na Wanahabari kutaka kujua msimamo wa CUF kuhusu uteuzi uliofanywa na CCM dhidi ya Maulidi Saidi Mtulia kugombea Jimbo la Kinondoni. 

Kwanza tunapenda Watanzania watambue kua Mtulia si Mwanachama wa CUF na katika hali hiyo, Cuf hawezi kua na sababu yoyote ya kushangazwa na uteuzi huo.

Pili Watanzania wanapaswa kutambua kwamba CCM kama Chama wanayohaki ya kumsimamisha Mtulia kua ni Mgombea wao japo Uamuzi huo unaweza kua na mtimanyongo kwa wanaccm na hata wasiokua wanaccm kutokana na tamaduni za CCM au historia ya Mtulia mwenyewe kwakua kabla hajajiuzulu alishakua Mbunge.

CUF – Chama cha Wananchi kinamtazama Mtulia kama CHAMBO KWENYE NDOANO YA KUVULIA SAMAKI, Mtulia ni kivutio cha Utalii, ili Mbuga ya Wanyama itembelewe na Watalii wengi lazima pawepo na kivutio. 

Uteuzi wa Mtulia utawavuta wengi kwenye CCM wakiwa na Mategemeo kua na wao wakifanya kama alichofanya Mtulia basi watateuliwa kua Wagombea kwenye Majimbo yao ya awali. 

Lakini Chambo kwenye NDOANO ni ngumu kumpata ila anarahisisha kuvuliwa au kupatikana kwa Samaki wengi. CUF – Chama cha Wananchi kitawashinda Wagombea wa Vyama vingine wataoshiriki kwenye Uchaguzi huo. Tumeshaanza maandalizi muda mrefu na tuna Mgombea mzuri, tuna uhakika wa kushinda kwenye Jimbo hilo la Kinondoni.

Wito wetu kwa Watanzania wajitokeze Kwa wingi kupiga Kura za kukataa Matumizi mabaya ya Fedha za Umma yanayofanywa na Maulidi Mtulia kwa kutuingiza kwenye Uchaguzi usiokua wa lazima na CCM nayo kuridhia Matumizi hayo kwa kurejesha jina la Mtulia kugombea nafasi ambayo alikua nayo hapo awali. Haya ni matumizi mabaya yalioridhiwa na CCM kwa kumrejesha Mtulia kama Mgombea wa Jimbo la Kinondoni kupitia CCM.

Watanzania bado tunachangamoto nyingi katika sekta mbali mbali kama vile Elimu, Afya na Miundombinu duni ndani ya Nchi yetu ambapo Fedha hizi za Uchaguzi zingeweza kuelekezwa huko. Kataaeni Matumizi haya kwa kushiriki kikamilifu kwenye Marejeo ya Uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Mwezi February

HAKI SAWA KWA WOTE

Abdul Kambaya 
Mkurugenzi wa Habari Uenezi CUF

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya January 7

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls 0658316976
0755911233
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Waziri Mkuu Aagiza Maafisa Kilimo Wasambazwe.......Ataka takwimu za kahawa ziwe tayari ifikapo Feb. 28

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Mji na Wilaya za Mbinga wahakikishe kuwa wanaunda kanda za kilimo na kuwasambaza maafisa kilimo wao badala ya kuwaacha wakae maofisini.

Ametoa agizo hilo Ijumaa, Januari 5, 2018 wakati akizungumza na watumishi na madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga pamoja na Halmashauri ya Mji wa Mbinga, kwenye ukumbi wa Jumba la Maendeleo, mjini Mbinga.

“Mkurugenzi wa TC na DC chuja maafisa kilimo ulionao na uhakikishe wanabakia watatu tu. Abaki DALDO, mtu wa horticulture na mthamini, wengine wote wasambaze kwenye kanda ili wasimamie wakulima wakiwa huko huko. Hili litekelezwe na Mkuu wa Wilaya ulisimamie” alisema.

Aliwataka maafisa kilimo wa zao la kahawa waende vijijini na kufanya sensa ili waweze kubaini wana wakulima wangapi wanaozalisha kahawa. “Afisa kilimo wa wilaya lazima ujue kijiji kina wakulima wangapi wa kahawa, na wana ekari ngapi? Na katika ekari hizo, ana miche mingapi? Hii itaisaidia Serikali ijue inahitaji dawa za aina gani, mbolea kiasi gani na miche mingapi kwa wakulima wake,” alisema.

“Ninataka hizi takwimu ziwe zimekamilika ifikapo tarehe 28 Februari, mwaka huu,” alisisitiza.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka maafisa ushirika wa wilaya hiyo wakasimamie uundwaji wa AMCOS mpya na kuimarisha zile za zamani ambazo zinafanya kazi vizuri.

“Maafisa ushirika ninataka nipate takwimu ya AMCOS very strong (ambazo ziko imara) kwenye wilaya yako. Iifikapo tarehe 28 Febriari, takwimu hizi ziwe zimekamilika. Kama kuna AMCOS nzuri ziimarisheni, itisha uchaguzi ili uanze na uongozi mpya,” alisisitiza.

Aliwaeleza watumishi na madiwani kwamba Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kurudisha heshima ya zao hilo ambapo zamani iliweza kusomesha watoto kadhaa kwenda sekondari kutokana na mfuko wa kahawa.

“Zamani zao la kahawa lilikuwa likisomesha watoto wa wakulima, sasa hivi hakuna hata anayefaidika na zao hili. Tunataka zao hili liwanufainishe wakulima, iinue uchumi wa wanaMbinga, isomeshe watoto na iwezeshe wakulima kujenga majumba,” alisema.

Alisema kuanzia msimu ujao wa Mei, Juni na Julai 2018, ununuzi wa kahawa utafanywa na vyama vya msingi vinavyotambulika kwa maafisa ushirika.

Aliwaonya watumishi wa Halmashauri hizo waache kutoa vibali vya ununuzi wa kahawa kwa watu binafsi wanaomiliki kampuni za kununua kahawa. “Halmashauri ndiyo mnatoa vibali vya kampuni kununua kahawa. Huu ni mwisho sasa. Hatuna mnunuzi binafsi wala hatuna kampuni binafsi, hawa wote tukutane kwenye mnada,” alisema.

Alisema hataki kuona watumishi wa Halmashauri wakionesha vibali vya kununua kahawa kama moja ya chanzo cha mapato kwenye Halmashauri hizo. “Ni marufuku kuingiza vibali kwenye mapato ya Halmashauri,” alisema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Abaini Madudu Ushirika Mbinga.....Aagiza uchunguzi ufanyike Haraka, maafisa wa MBICU, MBIFACU kikaangoni

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amebaini madudu kwenye Vyama Vikuu vya Ushirika vya Mbinga (MBICU na MBIFACU) na kuagiza uchunguzi ufanyike kuanzia leo.

“Nikiondoka hapa jukwaani, viongozi wote wa zamani na wa sasa waripoti kwa Mkuu wa Wilaya, na OCD hakikisha ofisi za chama hazifunguliwi hadi kesho asubuhi (leo) kazi itakapoanza, ili wasije kubadilisha nyaraka kwenye ofisi yao. Timu yangu ya uchunguzi iko hapa Mbinga, kesho waende wote kwenye ofisi hizo,” alisema huku akishangiliwa na wananchi.

Ametoa agizo hilo Ijumaa, Januari 5, 2018 wakati akiwahutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Mbinga, kwenye viwanja vya CCM, mjini Mbinga.

“Natambua kuwa MBICU ilishakufa ikiwa na madeni makubwa na mkaunda tena MBIFACU, ambayo nayo inasuasua, lakini viongozi wote hawa watafutwe, waje waonane wa timu  yangu na waeleze fedha za chama zimeenda wapi na kama walizikopea zilifanya nini,” alisisitiza.

Alisema timu hiyo ya uchunguzi itakiangalia chama hicho na kukifumua chote, na wote wakaobainika kuhusika watachukuliwa hatua za kinidhamu. “Tunataka MBICU na madeni yenu yaliyoko kwa Msajili wa HAZINA yajulikane, tunataka turudishe hoteli yetu, mashamba yetu na majengo yetu,” alisema.

Waziri Mkuu aliwaeleza wananchi hao kuwa Serikali imeamua kuboresha ufanisi katika mazao matano ya biashara ambayo ni pamba, kahawa, chai, korosho na tumbaku kwa sababu yanaliingizia Taifa fedha za kigeni.

“Mazao haya tutayasimamia kuanzia kilimo hadi uvunaji na utafutaji wa masoko. Nimeshafuatilia mazao ya korosho, tumbaku na pamba. Na sasa nimeanza na zao la kahawa na nimeamua kuanzia huku Mbinga,” alisema.

Alisema Serikali imedhamiria kuimarisha zao la kahawa katika mikoa yote inayolima zao ikiwemo Ruvuma, Mbeya, Kagera, Kigoma na maeneo mengine.

“Na nikimaliza ziara hii, nimeitisha kikao cha wadau wa zao la kahawa mjini Dodoma ifikapo Januari 14, 2018. Nimewaita Wakuu wa Mikoa, wakuu wa wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa ushirika, Maafisa kilimo na wadau wote kutoka mikoa yote inayolima kahawa hapa nchini, tukutane na kupeana maelekezo juu ya usimamizi wa zao hili,” alisema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameagiza kwamba kuanzia msimu ujao, zao la kahawa litauzwa kwa mnada chini ya mfumo wa ushirika. “Kuanzia msimu ujao, kahwa yote utauzwa kwa mnada, mnunuzi yeyote akitaka kununua kahawa aende kwenye mnada, tukikukuta mtu ananua kahawa kwa mkulima tutamkamata,” alisema na kuamsha shangwe kwa wananchi hao.

Alisema kuna watu wamekuwa wanapita na kununua kahawa kwa mfumo wa ‘magoma’ ambapo huwalaghai wakulima kwa kuwapa noti chache za sh. 10,000. “Huu mfumo wa magoma ni wa kuwaibia wananchi, hatutaki tena kuuona. Hakuna tena magoma hapa Mbinga,” alisisitiza.

“Bei ya mnada ndiyo fedha ya mkulima na sasa, Serikali tumeondoa tozo 17 kwenye zao hili kwa sababu tunataka tuone mkulima afaidike na zao hili,” alisema.

Waziri Mkuu anaendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Ruvuma kwa kutembelea wilaya ya Nyasa ambako atazungumza na watumishi na madiwani, ataweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, atakuwa mgeni rasmi kwenye tamasha la utalii na pia kuhutubia mkutano wa hadhara.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Serikali yapinga utaratibu wa ajira za mikataba

$
0
0
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema kuwa, ofisi yake haiungi mkono mfumo wa kazi kwa mikataba.

Waziri Mkuchika ameongeza kuwa, mfumo huo ni gharama kubwa ukilinganisha na kuajiri mfanyakazi kwa ajira ya kudumu na kwamba wizara yake inashughulikia suala hilo na kwamba hivi karibuni taasisi za umma hazitaruhusiwa kuajiri wafanyakazi wapya kwa mfumo wa mikataba.

“Tunataka kila ofisi kuajiri kwa mujibu wa mahitaji, hatutaruhusu mfumo huu wa mikataba kuendelea kwa sababu ni gharama kubwa mno kwa serikali,” alisema.

Kuhusu wafanyakazi wanaokwenda likizo maalum,  waziri alisema yeyote atakayekwenda katika likizo ya namna hiyo atatakiwa kuwasilisha nyaraka zake wizarani lini anarudi na wale watakaowasilisha barua kuwa wamerudi wanatakiwa kusubiri jibu la serikali.

“Kama ulikuwa nje ya nchi au ofisi mfano miaka mitano, ni dhahiri kuna mtu alijaza nafasi yako, hivyo unaporudi, unatakiwa kuwasilisha barua na kuipa nafasi serikali kujibu,” alifafanua Waziri Mkuchika.

Ameeleza kwamba, suala la likizo  maalum sio jambo jipya katika mfumo wa utumishi wa umma na umekuwa ukitumika katika nchi nyingi duniani

“Hatuna shida nayo, lakini tunataka wafuate taratibu sahihi wanaporudi.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuchika amesema kuwa, Bodi ya Mishahara na Maslahi (HSRB) iko katika hatua za mwisho za kurekebisha mfumo mzima wa mishahara, utakaondoa tofauti ya uwiano wa mishahara katika taasisi za umma kwa wafanyakazi wenye ujuzi, sifa na uzoefu.

Wanafunzi watano wakamatwa kwa kupata mimba

$
0
0
Jumla ya wanafunzi watano wa kike wa shule za sekondari Tandahimba waliopata mimba mwaka 2017 wamekamatwa pamoja na wazazi watano baada ya kufanyika msako na kufanikiwa kukamatwa kwa watu hao.

Katibu Tawala wa wilaya ya Tandahimba, Mohamed Azizi amesema hayo jana Jumamosi kwa niaba ya mkuu wa wilaya hiyo, Sebastian Waryuba baada ya kufanikiwa kuwakamata wanafunzi hao wakiwa na watoto wao huku wahusika ambao wamewasababishia kukatiza masomo yao kutokomea kusikojulikana.

“Tumefanikiwa kuwakamata wazazi na wanafunzi watano wakiwa wamejifungua kati yao  mmoja ameacha shule akiwa kidato cha nne, huku mwingine tatu na kidato cha pili baada ya kuzungumza nao wote wamesema hakuna hata mmoja ambaye anapata huduma kutoka kwa wahusika ambao wamewapa mimba hali ambayo inawapa shida wazazi wao kuwahudumia,” alisema Azizi

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji wa Kata ya Mkolea, Selemani Abduli amesema baada ya kupata taarifa kutoka kwa mkuu wa shule hatua ambazo amezichukua ni kuwakamata wahusika wote wawili na kuwapeleka katika kituo cha polisi kilichopo wilayani humo.

 “Hatua ambayo nilichukua baada ya kupata taarifa kwa wakuu wa shule ni kuwatafuta wanafunzi ambao wamepata ujauzito pamoja na wahusika kuwapeleka kituo cha polisi lakini wahusika wakifika kituo cha polisi waliachiwa,” alisema  Abdul

Akizungumzia tukio hilo mmoja wa mzazi ambaye mwanaye amekatiza masomo yake kutokana na kupata ujuzito Hassan Mfaume amesema amesikitishwa baada ya kusikia mwanaye amepata ujauzito hali ambayo imepelekea kukatiza masomo yake.

Sekondari za Azania, Jangwani, Milambo Zapigwa STOP Kufunguliwa Kesho

$
0
0
Serikali imelazimika kusogeza mbele tarehe ya kufungua shule kwa shule za Azania, Jangwani na Milambo kutokana na Wakala wa Majengo(TBA), kushindwa kumaliza ukarabati huo kwa muda uliotakiwa.

Uamuzi huo ulifikiwa jana  Jumamosi jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Leonard Akwilapo alipokutana na walimu wa shule hizo na viongozi wa Manispaa ya Ilala.

Akwilapo alisema kitendo hicho hakijamfurahisha na kuahidi kufuatilia kwa mara nyingine mkataba wa namna ya utekelezaji wa ukarabati huo walioingia Wizara na TBA.

"TBA mnapaswa kujua mmepewa jukumu hili kwa kuwa Serikali imewaamini, lakini hii isiwe kisingizio cha nyie kuvurunda kwa kisingizio tu ni taasisi ya Serikali nitapitia tena upya na mwanasheria wetu mkataba tulioingia kuona ni wapi watu hawakutekeleza wajibu wao na hatutasita kuchukua hatua tutakapobaini kuna tatizo," alisema.

Hata hivyo, alisema pamoja na kuongeza siku hizo ambapo sasa badala ya kufungua shule kesho Jumatatu, watafungua Januari 22, hataongeza siku zaidi na kuwahakikishia walimu kwamba muda walioupoteza wa ratiba za kufundisha zitafidiwa katika likizo ya Aprili na ile ya Juni.

Akijibu sababu zilizowachelewesha kumaliza ukarabati huo kwa muda, Kaimu Meneja wa TBA Mkoa wa Dar es Salaam,  Manasseh Shekalaghe alisema zipo sababu nyingi zilizochelewesha ikiwemo gharama kuongezeka tofauti na ilivyodhaniwa awali.

Tazama Hapa Picha za Tundu Lissu Alivyowasili na Kupokelewa Ubelgiji

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu amewasili katika uwanja wa ndege jijini Brussels, nchini Ubelgiji ambapo amepelekwa kwa ajili ya awamu ya tatu ya matibabu yake yatakayohusisha mazoezi ya viungo.

Tundu Lissu amewasili jijini hapo akitokea katika Hospitali ya Nairobi, nchini Kenya alikokuwa anapatiwa matibabu kwa muda wa takribani miezi minne sasa, kutokana na kushambuliwa kwa risasi.

Mbunge Tundu Lissu, ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa kambi ya Upinzani Bungeni, alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana, alipokuwa akitokea Bungeni, majira ya saa 7 mchana, karibu na nyumbani kwake Area D, Mjini Dodoma.

Kwa Mujibu wa taarifa ya madaktari waliokuwa wanamtibu, walieleza kuwa jumla ya risasi 16 zilimpata Tundu Lissu mwilini mwake, na wamefanikiwa kuzitoa, isipokuwa moja ambayo iko nyuma ya uti wa mgongo wake.

Tundu Lissu alieleza kuwa wataalamu na madaktari wake walishauri kuwa risasi hiyo ni hatari zaidi kama ikitolewa kuliko ikibaki ndani ya mwili wake, kutokana na eneo ilipokwama.

==>Picha za Mbunge Tundu lissu alipowasili jijini Brussels kwa ajili ya matibabu zaidi.

ACT Wazalendo Wataja Uelekeo Wa Chama Chao Mwaka 2018

$
0
0
Chama cha ACT-Wazalendo kimetangaza mikakati minne ya kipaumbele itakayoitumia kufanya siasa mwaka huu, ikiwemo kuimarisha ushirikiano na vyama vya wafanyakazi.

Akizungumza leo Jumapili, Januari 7, 2018, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano ya Umma ya chama hicho, Ado Shaibu amesema wanatambua kwamba wafanyakazi wanakabiliana na changamoto mbalimbali.

Amesema chama hicho kitawasemea wafanyakazi wanaolipwa mishahara duni, mazingira duni ya kufanyia kazi na uonevu unaofanywa na waajiri.

Shaibu amesema jambo jingine litakalofanywa mwaka huu ni kuimarisha ushirikiano na vyama vya siasa hasa katika kudai demokrasia na Katiba Mpya.

“Tutaongeza ushirikiano na vyama vingine vya upinzani katika kudai Katiba Mpya, tunahitaji kushirikiano ili kufanikisha hili,” amesema.

Amesema mwaka huu chama hicho kitafanya uchaguzi wa ndani ya chama kuanzia ngazi ya shina hadi taifa.

“Demokrasia inatakiwa ianzie ndani ya chama, tunawaomba wanachama wetu wajitokeze kugombea nafasi mbalimbali za uongozi,” amesema.

Shaibu amesema chama hicho kitaongeza juhudi katika kupambana na haki za kijamii hasa katika kuwapigania wastaafu na bima ya afya kwa watu walio nje ya mfumo rasmi wa ajira.

“Mwaka 2018 utakuwa wa kuimarisha ushirikiano wetu na wanyonge katika kupigania haki za kijamii na kurejesha misingi ya utu na heshima,”amesema.

Waziri Mkuu awataka mawaziri kutoa taarifa za fedha za miradi ya maendeleo

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka mawaziri, naibu mawaziri, makatibu wakuu, wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi kujenga utamaduni wa kutoa taarifa za fedha  za miradi ya maendeleo kwa wananchi badala ya kusubiri kufanya hivyo katika ziara za viongozi wakuu.

Majaliwa ametoa agizo hilo jana Jumamosi Januari 6,   wakati akizungumza na watumishi na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Nyasa kwenye kikao kilichofanyika mjini Mbamba Bay, wilayani Nyasa mkoani Ruvuma.

“Kuanzia sasa ninaagiza, viongozi wote wa ngazi za juu wakiwemo mawaziri hadi wakurugenzi na hata ninyi wakuu wa idara mnawajibika kutoa taarifa za fedha tunazopeleka kwenye miradi kwa sababu wananchi wana haki ya kujua utekelezaji wa ahadi za Serikali,” amesema.

Amewataka kila wanapoenda kwenye ziara ya kikazi vijijini, waelezee thamani za kazi zilizofanyika na waeleze ni lini miradi hiyo itakamilika.

“Mnapopata fursa ya kupanda jukwaani, tumieni wasaa huo kueleza kazi kubwa ambazo zimefanywa na Serikali,” amesema na kuongeza,

“Elezeni Serikali imeleta fedha kiasi gani, kwa ajili ya kitu gani na kwa kufanya hivyo, mtasaidia kutoa taarifa za utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na Rais John Magufuli wakati wa kampeni.”

Amesema wananchi wana haki ya kupatiwa taarifa za utendaji wa Serikali yao na akawataka viongozi hao wasisubiri ziara za viongozi wa kitaifa.

 “Nendeni mkaongee na wananchi, msiwaachie wakuu wa wilaya au wabunge peke yao ndiyo waseme na wananchi,” amesema.

Saa zahesabika msako wa mtuhumiwa kifo cha mke

$
0
0
Jeshi la Polisi limesema msako dhidi ya Mhasibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, Ami Lukule, ambaye anatuhumiwa kwa mauaji ya mkewe, kichanga chake na shemejiye wa kike, unaendelea vizuri na wanaamini kuwa watamtia mbaroni wakati wowote.

Lukule anadaiwa kutekeleza mauaji hayo kwa kutumia jembe la kulimia Jumatano iliyopita, katika eneo la Masota Darajani, Goba jijini Dar es Salaam. Waliofariki kutokana na tukio hilo ni Pendo Lukule, kichanga chake cha umri wa miezi minne, Joshua na shemeji wa kike wa mtuhumiwa ambaye ni ndugu wa mkewe, Magreth Samwel.

Inadaiwa kuwa Lukule alikimbilia kusikojulikana mara tu baada ya kufanikisha mauaji hayo, huku akiacha ujumbe unaowataka polisi kutohangaika kwa sababu ni yeye aliyetekeleza mauaji kutokana na kitendo cha mkewe kutokuwa mwaminifu na kwamba hata mtoto aliyemuua siyo wa kwake bali mkewe amezaa na watu wengine.

Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Benedict Kitalika, amesema kuwa hadi sasa, wanaendelea vizuri na msako dhidi ya mtuhumiwa kwa sababu wameshapata taarifa muhimu za kumtia mbaroni wakati wowote kuanzia sasa.

“Tumeshapokea taarifa na tunaamini zitatusaidia kumpata… yupo hapa nchini. Jeshi letu lipo vizuri, tutamkamata na kumchukulia hatua dhidi ya mauaji aliyoyafanya,” amesema Kitalika.

Katika hatua nyingine, taarifa zilidai jana kuwa miili ya marehemu inatarajiwa kuzikwa leo katika makaburi ya Kinondoni.

Serikali Yaanza Kuwashughulikia Wasanii Wanaovaa Nusu UCHI....Tazama Majina ya Baadhi Yao

$
0
0
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza amesema kuwa, serikali inafuatilia kwa karibu wasanii wote wanaoweka picha za kukosa maadili kwenye mitandao na kuwachukulia hatua.

Shonza ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaama alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari. Agizo hilo la Naibu Waziri ni matokeo ya kauli iliyotolewa na Rais Dkt Magufuli aliyoitoa mjini Dodoma wakati akizungumza na Jumuiya ya Wazazi ya CCM. 

Rais Magufuli alivitaka vyombo husika kuwachukulia hatua wasanii hasa wa kike ambao wamekuwa wakivaa nguo zinazopelekea kumomonyoka kwa maadili.

Wakati akizungumza hayo Naibu Waziri alitaja majina ya wasanii ambao wameanza kuwachukulia hatua ambapo baadhi wametakiwa kufika ofisini kwake huku mwingine akifungiwa kujihusisha na masuala ya sanaa kwa muda wa miezi sita.

Shonza amemtaka msanii, Jane Rimoy maarufu kwa jina la Sanchi kufika ofisini kwake mara moja kutokana na kuchapisha mitandaoni picha zisizo na maadili.

Mbali na Sanchi, Shonza ametoa maagizo, ”Ninamtaka Msanii wa Bongo Fleva, Gift Stanford maarufu kama Gigy Money kufika ofisini kwangu mara moja sababu alitumiwa ujumbe lakini hakujibu, hivyo ajue kuwa hawezi kushindana na serikali.”

Pia, Naibu Waziri wa Habari, Juliana Shonza amemfungia msanii wa filamu na muziki, Suzan Michael maarufu Pretty Kind kujihusisha na shughuli zote za sanaa kwa muda wa miezi sita, kutokana na kuweka picha za utupu katika mtandao ya kijamii.

Wakati huo huo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Godfrey Mngereza amewasisitiza wamiliki wa studio za kutayarisha kazi za sanaa na waandaji wa kazi za sanaa (Producers) kujisajili katika ofisi za Baraza hilo. Asisitiza, kufanya kazi bila kusajiliwa ni kinyume na sheria.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya January 8

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kutoa Michirizi, Kuondoa Chunusi, Kuongeza Maumbilie na Nguvu za Kiume

$
0
0

🎁OFFER SPECIAL MWAKA MPYA🎁
    PENDEZA SASA KWA PUNGUZO KUBWA LA BEI. 
       KATIKA KUSHEREHEKEA MSIMU WA SIKUKUU  @natural2162 TUNA  PUNGUZO LA 20% KWA BIDHAA ZETU ZOTE, IKIWA NI SHUKRANI KWA KUTUUNGA MKONO.

        BIDHAA ZETU ZOTE ZIMETENGENEZWA KWA MIMEA NA MATUNDA HAZINA KEMIKALI WALA MADHARA.
    KWA WANAUME TUNATIBU👇👇
☆Kukosa hamu ya tendo.
☆Kuwahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo.
☆Maumbile madogo ya uume.
☆Kuchoka sana wakati wa tendo na uume kusinyaa  nk.
      @natural2162 tumeandaa tiba bora kabisa kama ifuatavyo:-
 
1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @220,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @130,000/=
3VigRX  CREAM_ Inaongeza uume inch 6.5 hadi 8 (wiki 2-3) @170,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @140,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @220,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @140,000/= 
 
     PIA KWA WANAWAKE WANAOPENDA KUWA NA MUONEKANO MZURI ZIPO ZA👇👇👇
1.Kuongeza hips, makalio na mapaja @180,000/=
2.Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @130,000/=
3.Kuwa mweupe bila sugu kwa:-
(a)mafuta @130,000/=
(b) Vidonge @150,000
4.Kurefusha nywele na kutokukatika ovyo @130,000/=
5.Kuongeza hips, makalio na mapaja kwa vidonge (YODI PILLS ORIGINAL) @200,000/=
6Kupunguza au kuongeza maziwa kuyasimamisha @130,000/=
7.Kubana uke na kuondoa uchafu ukeni @120,000/=
8.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
        NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri na garantii ili kukuhakikishia ubora na usalama wa bidhaa za NATURAL BEAUTY CO

    Wasiliana nasi Popote
  ulipo duniani kwa (+255)
           0659618585 na
           0759029968
        UTAPATA HUDUMA.
👉🏻OUR WEBSITE:- www.naturalworldbeauty.og
👉🏻INSTAGRAM PAGE:-
@natural2162
@natural2162
@natural2162

         < WELCOME ALL>

Msanii aliyesambaza picha za uchi aomba radhi baada kufungiwa

$
0
0
Msanii filamu na video vixen, Suzan Michael maarufu kama Pretty Kind amefunguka na kuomba radhi kwa Serikali na Watanzania kwa ujumla kutokana na vitendo vyake vya kupiga na kuweka picha mitandaoni za nusu uchi.

Akiongea jana na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kufungiwa na serikali kujihusisha kufanya kazi zozote za sanaa kwa miezi sita, Pretty Kind alisema kuwa amejifunza na kugundua kuwa alikuwa anafanya makosa hivyo sasa hataweza kurudi tena kufanya mambo hayo.

“Naomba niombe radhi kwa Watanzania wote kwa hiki nilichokifanya natambua nimefanya kosa naomba msamaha aweze kunisamehe, pia naomba msamaha kwa mashabiki zangu kwa hiki kilichotokea nimejifunza hivyo nitakuwa Pretty Kind mwingine mpya na kufanya yale yanayotakiwa katika jamii” alisema

Pretty Kind amefungiwa kujihusisha na sanaa kwa takribani miezi sita baada ya kuposti picha katika mtandao wake wa Instagram ikimuonyesha akiwa nusu utupu jambo ambalo ni kinyume na maadili ya Kitanzania na kwenda kinyume na maagizo ya Rais John Pombe Magufuli ambayo aliyatoa hivi karibuni kuwataka wasanii wa kike kuvaa kwa staha.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images