Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Picha Zaidi za Babu Seya na Mwanae Wakiwa IKULU

$
0
0
Mzee Nguza Vicking(Babu Seya) akiwa na watoto wake Papii Nguza (Papii Kocha),Francis Nguza pamoja na Nguza Mbangu walipomtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Dkt.John Pombe Magufuli kwaajili ya kumshukuru Ikulu jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.

Mzee Nguza Vicking(Babu Seya) akiwa na watoto wake Papii Nguza (Papii Kocha),Francis Nguza pamoja na Nguza Mbangu walipomtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Dkt.John Pombe Magufuli kwaajili ya kumshukuru Ikulu jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.
Mzee Nguza Vicking(Babu Seya) akifurahi na watoto wake Papii Nguza (Papii Kocha),Nguza Mbangu pamoja na Francis Nguza walipomtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Dkt.John Pombe Magufuli kwaajili ya kumshukuru Ikulu jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.
Mzee Nguza Vicking(Babu Seya) akifurahi na watoto wake Papii Nguza (Papii Kocha),Nguza Mbangu pamoja na Francis Nguza walipomtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Dkt.John Pombe Magufuli kwaajili ya kumshukuru Ikulu jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mzee Nguza Vicking(Babu Seya)aliyeambatana na familia yake kwaajili ya kumshukuru Mheshimiwa Rais Ikulu Jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Mzee Nguza Vicking(Babu Seya)pamoja na familia yake walipomtembelea kwaajili ya kumshukuru Mheshimiwa Rais Ikulu Jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Mzee Nguza Vicking(Babu Seya)pamoja na familia yake walipomtembelea kwaajili ya kumshukuru Mheshimiwa Rais Ikulu Jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshikana mikono na Mzee Nguza Vicking(Babu Seya)pamoja na familia yake wakiomba dua walipomtembelea kwaajili ya kumshukuru Mheshimiwa Rais Ikulu Jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshikana mikono na Mzee Nguza Vicking(Babu Seya)pamoja na familia yake wakiomba dua walipomtembelea kwaajili ya kumshukuru Mheshimiwa Rais Ikulu Jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mzee Nguza Vicking(Babu Seya)pamoja na familia yake walipomtembelea kwaajili ya kumshukuru Mheshimiwa Rais Ikulu Jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.
Mzee Nguza Vicking(Babu Seya) akizungumza na wanahabari mara baada ya  kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Dkt.John Pombe Magufuli  walipomtembelea Ikulu jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018.
Papii Nguza (Papii Kocha) akionyesha alama ya mchoro unaosomeka ” JPM “mara baada ya  kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Dkt.John Pombe Magufuli  walipomtembelea Ikulu jijini Dar es Salaam.Januari 2,2018

UGANDA: Rais Museveni aidhinisha sheria kuondoa kikomo cha umri wa rais

$
0
0
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ameidhinisha mswada unaoondoa kikomo cha umri kwa wagombea urais nchini humo, hatua inayompa nafasi ya kuwania tena urais mwaka 2021.

Mswada huo pia unarejesha takwa la rais kuongoza kwa mihula miwili pekee ya miaka mitano.

Kwa kuwa sheria hiyo itaanza kutekelezwa sasa, Bw Museveni anaweza akaongoza taifa hilo hadi 2031.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor la Uganda, katibu wa rais Bi Linda Nabusayi amesema Bw Museveni alitia saini mswada huo kuwa sheria Desemba 27 na kisha akatuma waraka tarehe 29 Desemba.

Sheria ya awali ilikuwa inamzuia mgombea kuwania urais baada ya kutimiza umri wa miaka 75. Bw Museveni kwa sasa ana miaka 73.

Hatua ya rais huyo kuidhinisha mswada huo imetoa wakati ambao amekuwa akihimizwa na viongozi wa kidini na wanaharakati wa kisiasa kutouidhinisha.

Bunge liliidhinisha mswada huo mnamo tarehe 10 Desemba kwa zaidi ya theluthi mbili ya wabunge waliohudhuria kikao, wabunge 317 wakiunga mkono na 97 wakapinga.

Chanzo; BBC

Kamanda Mambosasa awatembelea na kuwafariji askari Walioko Kibiti, Rufiji

$
0
0
Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam imetembelea Mkoa wa Rufiji katika utaratibu wa kawaida wa jeshi hilo wa kuimarisha ujirani mwema na kubadilishana uzoefu.

Makamanda wa polisi wa mikoa inayounda Kanda Maalumu ya Dar es Salaam wakiongozwa na Kamanda wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa walifika Mkoa wa Kipolisi wa Rufiji leo Jumanne Januari 2,2018 na kupokewa na kamanda wa mkoa huo, Onesmo Lyanga.

Msafara wa Kamanda Mambosasa ulibeba zawadi za sikukuu kwa ajili ya askari ambao wapo katika operesheni maalumu katika eneo hilo ambalo siku za nyuma liligubikwa na matukio ya mauaji ya wananchi wasio na hatia na askari.

Akizungumza na baadhi ya askari waliopo Rufiji, Kamanda Mambosasa amewapongeza kwa kufanya kazi kwa uzalendo na kwa kufuata kiapo chao licha ya mazingira ya kazi si rafiki.

"Hakuna asiyejua hali iliyokuwepo Rufiji mpaka wananchi wakakata tamaa na wengine walihama lakini kamanda mwenzangu ameniambia hali sasa ni shwari, Dar es Salaam tuko pamoja na ninyi na tunathamini kazi mnayoifanya. Usalama wa Dar es Salaam unategemea kwa kiasi kikubwa usalama wa hapa pia," amesema Kamanda Mambosasa.

Amesema hali ya usalama Dar es Salaam ni shwari na askari hawajalala wapo imara kama walio kwenye operesheni hiyo kwa kuwa wahalifu wanaobanwa Pwani na kukimbilia Dar es Salaam hawabaki salama.

"Hatukuja Boxing day (siku ya kufungua zawadi) lakini leo tumewaletea ndafu, kidogo, kilo 200 za mchele, sukari, maji na mafuta, ninyi endeleeni kupeperusha bendera ya Jeshi la Polisi na haya mambo yatakwenda lakini baadaye yataisha,” amesema.

Kwa upande wake, Kamanda Lyanga  amesema wamekuwa wakitembelewa na viongozi na watu wengine wengi, hivyo morali ya askari waliopo katika operesheni iko juu na wanafanya kazi kwa weledi na mpaka sasa hakuna malalamiko yoyote ya wananchi jambo ambalo linaashiria kuwa sheria zinafuatwa.

"Baada ya kuwa tumewafikia wahalifu sasa wananchi wanawapenda askari wao, wanatoa taarifa hawaogopi tena kama zamani," amesema Kamanda Lyanga.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Mamlaka Ya Mapato TRA

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imefanya mabadiliko  ya ulipaji kodi kwa wafanyabiashara wadogo ambao watalipa robo ya kwanza ya malipo ndani ya siku 90 badala ya njia ya awali ya kufanyiwa makadirio.

Mabadiliko hayo yatawasaidia wafanyabiashara kuanzia waliposajiliwa tofauti na utaratibu uliokuwepo wa kulipia kodi hiyo hata kabla mfanyabiashara hajaanza kufanya biashara.

Hayo yameelezwa leo Januari 2  na Kamishna wa Kodi za Ndani TRA, Elijah Mwandumbya wakati wa kuzindua kampeni ya usajili wa walipa kodi ambapo amesema wanatarajia kusajili walipakodi  wapya  milioni moja  kwa mwaka 2017/2018.

Mwandumbya amesema TRA hawana wakala yeyote aliyepewa jukumu la kusajili au hata kutoa fomu ya usajili hivyo amewataka wananchi wajihadhari na vishoka ambao watatumia mwanya na kuharibu kampeni hiyo.

"Hatuna mtu yeyote hivyo ni wazi kupitia vyombo vya habari wananchi wanatakiwa kuwa makini kwani usajili utafanyika katika ofisi za TRA na katika vituo maalumu," amesema Mwandumbya.

Amesema kampeni hiyo na mabadiliko hayo yamekuja kwa nia ya kuongeza hamasa kwa wananchi ili wawe na utaratibu wa kulipa kodi.

Mwandumbya ameendelea kusisitiza azma ya serikali kukusanya kodi na kukuza uchumi wa viwanda na kuleta maendeleo kwa Taifa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya January 3

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls 0658316976
0755911233
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Hatua Iliyofikiwa Na Serikali Katika Ununuzi Wa Treni Mpya Za Kisasa

$
0
0
Serikali kupitia Kampuni Hodhi ya Reli (RAHCO) imetangaza mchakato wa awali wa zabuni ya ununuzi wa vichwa na mabehewa kwa ajili ya treni ya umeme itakayotumika katika reli ya kisasa (Standard Gauge) ambayo ujenzi wake unaendelea.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa RAHCO, Masanja Kadogosa ameithibitishia Idara ya Habari (MAELEZO) kuanza kwa mchakato huo ambao unafuata taratibu za kimataifa za ununuzi kwa njia ya ushindani.

Kwa mujibu wa tangazo la zabuni, jumla ya vichwa 14 vya treni ya umeme kwa ajili ya kusafirisha mizigo na vichwa viwili vya treni ya mizigo inayotumia mafuta vinahitajika.

Aidha, RAHCO pia imetoa zabuni ya ununuzi wa vichwa vitano vya treni ya abiria ya kisasa inayotumia umeme (Electric Multiple Units) ambapo kila kimoja kitakuwa na uwezo wa kuvuta mabehewa 60 yenye kuchukua abiria 1,800.

Katika mabehewa hayo ya abiria, mabehewa 15 yatakuwa ni ya kiwango cha daraja la kwanza na mengine 45 ni daraja la pili.

Mbali na mabehewa ya abiria, zabuni hiyo inajumuisha ununuzi wa mabehewa mengine zaidi ya 1,500 yenye muundo tofauti kwa ajili ya kubebea aina mbalimbali za mizigo.

Pamoja na sifa mbalimbali zilizo ainishwa katika tangazo la zabuni, moja ya sifa za reli hiyo ya kisasa ni kuhimili treni ya abiria yenye uwezo wa mwendo kasi wa kilometa 160 na mabaehewa yenye juma ya urefu wa mita 2000, wakati ile ya mizigo yenye uwezo wa kwenda kasi ya kilometa 120 kwa saa.

Kwa mujibu wa tangazo la zabuni, mwisho wa kuwasilisha nyaraka za zabuni ni Januari 30, mwaka huu.

Tayari awamu ya kwanza ya ujenzi wa reli hii kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro inaendelea na wakati huo huo tayari Serikali imesaini mkataba kwa ajili ya awamu ya pili ya ujenzi kutoka Morogoro hadi Makutupola mkoani Dodoma.

Wanyarwanda kutotambulika kama wakimbizi

$
0
0

Mataifa mbalimbali duniani, hayatawatambua tena raia wa Rwanda waliokimbia nchi yao kati ya mwaka 1959 hadi 1988 kama wakimbizi baada ya muda waliopewa kurudi nyumbani kumalizika mwisho wa mwaka 2017.

Hatua hiyo inaamanisha kuwa, raia hao wa Rwanda hawatatambuliwa kama wakimbizi na hawatapa msaada wowote kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa linalowashughulikia wakimbizi UNHCR.

Disemba 31 mwaka jana, ilikubaliwa kati ya serikali ya Rwanda na Shirika la UNHCR pamoja na mataifa mbalimbali ambayo yamekuwa yakiwapa hifadhi wakimbizi hao kutoka Rwanda warejee nyumbani.

Mkataba wa kurejesha nyumbani wa wakimbizi uliokubaliwa mwaka 1951, unawataka wakimbizi kurejea katika nchi zao baada ya kubainika kuwa, hawapo tena katika hatari ya kushambuliwa au kunyanyaswa.

Wanyarwanda wanaoishi nje ya nchi yao ambao wamekuwa wakifahamika kama wakimbizi ni takriban elfu 20 kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa.

Waziri Mwigulu Ataja Matukio Yaliyomuudhi Sana Mwaka 2017

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Mwigulu Nchemba amefunguka na kusema kwamba katika matukio yaliyomuudhi sana mwaka 2017 ni pamoja na kushambuliwa kwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu pamoja na mauaji ya wananchi na Askari huko Kibiti.

Mh. Nchemba amesema hayo jana akiongea na waandishi mkoa wa Dodoma wakati akitoa muelekeo wa wizara yake kwa mwaka mpya wa 2018 nini kama wizara wamejipanga kufanya.

Mh. Nchemba amesema kuwa matukio hayo yalimuudhi sana,  hivyo amewataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika kutoa taarifa na wao kama wizara wapo vitani mda wote kuwasaka wahalifu na kuzuia uhalifu kwa mwaka 2018.

Aidha Waziri Nchemba amewataka wananchi kutokuchukulia kawaida taarifa za kupotea kwa watu zaidi ya wiki bila kutoa taarifa kwa kudhani kuwa atakua mahali fulani, au hakuna ubaya unaoweza kutokea na hata wale wanaopewa vitisho wasichukulie kirahisi mambo hayo bali watoe taarifa polisi.

Akizungumzia kuokotwa kwa miili ya watu katika fukwe za bahari Dk. Nchemba amesema kwamba, miili  hiyo ilikua ya wahamiaji haramu amabao walikuwa wanasafirishwa nje ya nchi na wahamiaji hao walikuwa wanasafirishwa katika magari yasiyo na  hewa na wanabebwa kama mahindi, na kuogeza kuwa wakifa kwa kukosa hewa na chakula basi hutupwa sehemu mbalimbali ili wanaowasafirisha wasikamatwe.

Ray C Atoa Kali Ya Mwaka.....Amuomba Rais Magufuli Awabane Wanaume Wanaowachezea Bila Kuwaoa

$
0
0
Msanii  Ray C amefunguka na kumuomba Rais Magufuli asaidie kupatikana sheria ambayo itaweza kusaidia wanawake na mabinti wa Tanzania kuolewa kwa haraka kwani anadai bila wanaume kulazimishwa wataendelea kuwachezea mabinti tu.

Ray C amedai kuwa endapo kukiwa na sheria ya kuzuia mahusiano ya kimapenzi kati ya mwanaume na mwanamke kabla ya ndoa itasaidia sana wanaume kuoa na kupelekea tatizo la mabinti kutoolewa kupungua.

"Mzee mimi na shida moja, hawa wanaume hapa nchini wanajifanya wajuaji sana! Ombi langu la mwaka huu kwako ni hili. Naomba upitishe sheria hakuna mahusiano ya kimapenzi kati ya mwanamke na mwanaume mpaka wafunge ndoa! Na yeyote atakaekutwa na mwanamke iwe hotelini! Guest house bila cheti cha ndoa wapelekwe wote Segerea. Nadhani itasaidia sana wanawake wengi kuolewa badala ya kuwa manungaembe" alisema Ray C

 Ray C amesema kuwa ameamua kuomba jambo hilo kwa kuwa amekuwa akishuhudia wanawake wengi wakiishia kuchezewa na kuachwa pasipo kuolewa lakini anadai kama kukiwa na sheria hiyo wanaume watakuwa na nidhamu na kunyooka maana watalazika kuoa tu.

Maofisa wa TRA watumia saa sita kumhoji Askofu Kakobe

$
0
0
Watumishi 12 kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) jana walitumia zaidi ya saa sita kumhoji Askofu Mkuuwa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe.

Mwandishi wetu ambaye alipiga kambi nje ya kanisa hilo lililopo Mwenge, Dar es Salaam kuanzia saa tano asubuhi, alishuhudia kuwasili kwa watumishi ambao mara baada ya kushuka katika magari na kutaka kuingia ndani, walizuiwa na wahudumu wa kanisa hilo kwa takribani dakika 15.

Baada ya kuingia ndani, watumishi hao walitoka saa 11:48 jioni kwa staili ya aina yake. Tofauti na walivyowasili kwa magari saba, wakati wa kuondoka walijibana katika magari mawili yaliyoingia ndani ya kanisa hilo kuwachukua, huku mengine yakiondoka tupu.

Tukio la idadi kubwa ya watumishi kuonekana katika kanisa hilo imekuja zikiwa zimepita siku tano tangu Kamishna wa TRA, Charles Kichere kueleza nia ya mamlaka hiyo kuanza mchakato wa kufuatilia ulipaji kodi wa Askofu Kakobe.

Kichere alisema uamuzi huo unatokana na kiongozi huyo wa kiroho kutokuwamo katika kumbukumbu za ulipaji kodi za mamlaka hiyo.

Alitoa kauli hiyo baada ya kusambaa kwa picha za video zikimuonyesha Askofu Kakobe akiwa katika mahubiri kwenye kanisa hilo, akisema kiwango cha fedha alichonacho si tu ni zaidi ya kile cha Serikali, bali pia anaweza kuwakopesha fedha hata mawaziri.

Kiongozi huyo wa kiroho alirejea kauli yake hiyo katika ibada ya Jumapili iliyopita, safari hii akibainisha kuwa ana fedha nyingi kuliko Serikali zote duniani na kuwataka watu wakimsikia anazungumza, watafakari kwanza kabla ya kumkabili.

Mwandishi  alipotaka kupata ufafanuzi kwa Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo kama watumishi hao waliokuwa kwa Askofu Kakobe ni wa mamlaka hiyo, alishindwa kukubali au kukataa.

Alisema ingawa mamlaka hiyo iliahidi kwenda kumhoji hana uhakika kama hao walikuwa maofisa wa TRA au la.

Hata hivyo, mtendakazi wa kanisa hilo, Natus Mwita alipoulizwa kuhusu ujio wa maofisa hao alisema walipokea barua ya TRA tangu Desemba 30, mwaka jana.

“Walileta barua yao kutaka kuonana na Askofu Desemba 30, sasa hatujajua labda leo wamekuja kuchukua mujibu yao, kwa sasa hamuwezi kuingia ndani labda msubiri nje ndiyo mtaweza kuonana nao watakapokuwa wakitoka,” alisema Mwita.

Jitihada za mwandishi wetu kuzungumza na watumishi hao ziligonga mwamba kutokana na kutotoka nje baada ya kumaliza mahojiano hayo kwani waliingia ndani ya magari hayo wakiwa ndani ya kanisa na kutoka katika mwendo wa kasi.

Wakati wakiwa ndani ya kanisa hilo, magari yenye namba za STK na STL yalikuwa yakipita mara kwa mara nje ya kanisa hilo lililopo kando ya Barabara ya Sam Nujoma.

Katikati ya mazungumzo hayo, Askofu Kakobe alitoka kwenye chumba cha mahojiano na kuelekea jengo jingine kanisani hapo. Baada ya kutoka baadhi ya watumishi hao wa TRA nao walitoka kwenye chumba hicho na kuonekana wakizungumza nje. Walirejea ndani baada ya askofu huyo kurudi.

Wakati wote wa mahojiano hayo, shughuli mbalimbali za kanisa zilikuwa zikiendelea huku waumini wakionekana kuingia na kutoka.

Mmoja wa waumini hao, Janet Mathew alisema, “Nimekuja kwa ajili ya huduma ya maombezi na maombi kwa kweli hakuna shida yotote nimepata huduma vizuri.”

Alipoulizwa kama aliona tofauti yoyote na siku nyingine alisema, “Sijui kinachoendelea ni sawa na siku zote sijaona tofauti yoyote.”

Credit: Mwananchi


Ubovu Magari Mapya Ya Polisi Waishitua Wizara Mambo Ya Ndani

$
0
0
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imebaini madudu katika utekelezaji wa mkataba wa uagizaji wa magari 777 kwa ajili ya Jeshi la Polisi yaliyoagizwa kwa gharama za dola za Marekani milioni 29.77 (Sh. bilioni 66.288).

Kutokana na hali hiyo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni, amemwagiza katibu Mkuu wa wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira, kuunda kamati maalum ya kuchunguza mkataba wa uagizaji wa magari hayo.

Vilevile, ameagiza kamati hiyo ambayo itahusisha wataalamu kutoka taasisi mbalimbali, kupitia upya mkataba ulioingiwa mwaka 2013 kati ya serikali na Kampuni ya Ashok Leyland inayoingiza magari hayo nchini.

Masauni aliyabainisha hayo jijini Dar es Salaam jana, muda mfupi baada ya kufanya ziara ya kukagua magari 53 ya jeshi hilo yaliyotolewa bandarini kwa agizo la Rais John Magufuli alilolitoa Novemba 26, mwaka jana, huku naibu waziri huyo akibaini matano yana hitilafu.

Rais Magufuli alifanya ziara bandarini siku hiyo na kukuta magari hayo 53 ya Jeshi la Polisi na magari mengine 50 ya kubebea wagonjwa yakiwa yamekaa hapo tangu Juni, 2016 bila kutoka na kuagiza kutolewa mara moja.

Jana, Masauni alikuta magari hayo yameshatolewa na kuwekwa katika Chuo cha Polisi Kurasini huku Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) wakiyafanyia ukaguzi kabla ya kuyakabidhi kwa Jeshi la Polisi kwa ajili ya ukaguzi zaidi.

Masauni pia alitembelea bandarini na kubaini kuwa magari mengine 119 ya Jeshi la Polisi yameshawasili huku malori yakiwa ni mengi kuliko idadi ya magari madogo ambayo yanahitajika zaidi kwa shughuli za jeshi hilo.

“Tumeamua kuunda hii kamati itueleze kitaalamu kwanini magari haya yanakuja malori zaidi ilhali tuna uhitaji mkubwa wa magari madogo katika vituo vyetu vya polisi nchini na je, mkataba ulielezaje na kama unafuatwa,” alisema Masauni.

Kuhusu hitilafu zilizobainika kwenye baadhi ya magari, Masauni alisema kamati hiyo ichunguze sababu za magari hayo kuharibika ilhali waliagiza magari mapya na siyo yaliyotumika.

Naibu Waziri huyo pia alibainisha kuwa ukaguzi wa awali umebaini moja ya magari kusomeka limeshatembea zaidi ya kilometa 1,000 na kwamba suala hilo pia, litapatiwa ufumbuzi kwa kuwa serikali iliagiza magari mapya na si yaliyotumika.

Masauni alisema kamati itakayoundwa itahusisha pia wataalamu kutoka Chuo cha Usafirishaji (NIT) na Temesa, ili kuchunguza kwa kina magari hayo.

Jeshi la Polisi limekuwa likikumbwa na changamoto za kuwa na utekelezaji wenye utata wa baadhi ya mikataba yake iliyowahi kuingiwa siku za nyuma, huku ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2014/15 ikibainisha kuwa jeshi hilo na Shirika la Umeme (Tanesco) ni miongoni mwa taasisi zinazoongoza kwa madeni na manunuzi makubwa.

Mwakyembe Atoa Maagizo Mazito TFF

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe ameitaka TFF kuyafanyia kazi malalamiko yote yanayohusu michezo ya ligi daraja la kwanza, kati ya Dodoma FC vs Alliance na Pamba vs Biashara.

Sakata la maamuzi yasiyo ya haki katika michezo ya Dodoma FC dhidi Alliance ya Mwanza na Pamba ya Mwanza dhidi Biashara ya Musoma ndio limefanya Waziri mwenye dhamana ya michezo kutoa agizo hilo kwa shirikisho ili kuhakikisha utata huo unamalizika.

Katika taarifa yake  Waziri Mwakyembe ameeleza kusikitishwa na malalamiko ya vitendo vya uonevu na upendeleo katika maamuzi ya mechi hizo huku TFF ikiwa kimya bila kutoa ufafanuzi wa maamuzi hayo.

Mechi hizo zilipigwa Disemba 30 maamuzi yake kugubikwa na utata mkubwa hivyo Waziri amemtaka Rais wa TFF Wallace Karia na viongozi wengine wahusika kuchukua hatua za kuchunguza maamuzi hayo na kuchukua hatua
.

Waliochoma kanisa la EAGT Bukoba wafungwa kifungo cha maisha jela

$
0
0
Mahakama  ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Bukoba, imewahukumu kifungo cha maisha watu watatu, baada ya kuwatia hatiani kwa makosa mawili, likiwamo la kuchoma moto kanisa.

Kanisa lililochomwa moto na watu hao ni la Evangelical Assemblies of God (EAGT) mjini Bukoba mkoani Kagera.

Waliotiwa hatiani na Hakimu wa Mahakama hiyo, Charles Oisso ni Rashid Athuman, Ngesella Ismail na Allyu Dauda Hessein.

Hakimu Oisso alisema kuwa watu hao wametiwa hatiani kwa makosa mawili, la kwanza ni kula njama za kutenda kosa walilohukumiwa kifungo cha miaka saba, na la pili ni kutenda kosa la kuchoma kanisa la Evangelical Assemblies of God (EAGT) lililoko mtaa wa Omukibeta Kata ya Kibeta katika Manispaa ya Bukoba.

Alisema kuwa aliwatia hatiani kutokana na washtakiwa hao kuonyesha vitendo vya chuki dhidi ya dini nyingine.

Hakimu Oisso alisema kuwa maeneo ya ibada inabidi yawe salama, maana siyo sehemu ya kujengea watu hofu.

Kwa upande wake, Mwanasheria wa Serikali, Haruna Shomari, awali aliiomba mahakama hiyo kuwapa adhabu kali washtakiwa hao, ili kukomesha vitendo vya aina hiyo, ambavyo alisema vinajenga hofu kwa jamii.

Mwaka 2015, washtakiwa hao walikamatwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuchoma moto kanisa hilo ambalo liliteketea pamoja na vitu vilivyokuwamo, na kufikishwa mahakamani mwaka huo.

Bodi ya Mikopo (HESLB) Yawageukia Waajiri

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini (HESLB) imesema kuanzia Jumatatu ijayo, Januari 8, 2018 itaanza kukagua taarifa za mishahara za waajiri (payroll) ili kubaini waajiri ambao wanawasilisha kiwango kidogo cha mikopo ya wafanyakazi wao ambao ni wanufaika pamoja na waajiri ambao hawawasilishi kabisa pesa hizo kwenye bodi hiyo kwa mujibu wa sheria ili wachukuliwe hatua stahiki.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo, Abdul-Razaq Badru amesema wanufaika wengi wa mikopo, wakiwemo wadaiwa sugu, wameonesha ushirikiano mkubwa katika kurejesha mikopo yao, hivyo kurahisisha kazi ya kukusanya madeni ya mikopo hiyo.

“Kiasi cha pesa za wadaiwa sugu kilichoiva na kinachotakiwa kuwasilishwa ni Tsh. bilioni 285, hii inajumuisha kuanzia kazi hii ya kukopesha ilipoanza.

“Tangu mwaka jana mpaka sasa tumewapata wadaiwa sugu 26,000, tunashukuru wanufaika hawa wamejitokeza na wanawasilisha mikopo yao. Kuna baadhi ya waajiri wanawasilisha vizuri marejesho ya wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu, wengine hawasilishi na wengine wanawasilisha kiasi kidogo tofauti na asilimia 15 kama sheria inavyotamka.

“Kuanzia Jumatatu, Jan. 8, 2017 tutaanza kukagua taarifa kwenye payroll za waajiri wote waliosajiriwa kubaini waajiriwa wao ambao ni wanufaika wa mikopo wanaodaiwa ili waweze kukatwa.

“Lengo la kufanya ukaguzi kwenye payroll za waajiri ni kubaini iwapo wana waajiriwa wanadaiwa na HESLB, waajiri wanaowasilisha kiwango kinachotakiwa, wanaowasilisha chini ya asilimia 15 na wanaokata pesa na hawaziwasilishi HESLB,” alisema Badru.

Hata hivyo, Badru amesema wamelazimika kufungua ofisi zao nchi nzima kwa ajili kusimamia malipo ya fedha hizo za mikopo, hasa wale waliotajwa kwenye orodha ya wadaiwa sugu ambapo wamewasambaza wakaguzi nchi nzima, kwa ajili ya kufuatilia waajiri wasiotekeleza wajibu wao wa kuwakata asilimia 15 wanufaika hao waliowaajiri.

Bei mpya elekezi za mafuta ya petroli kutoka EWURA

$
0
0
January 3, 2017 Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetoa bei mpya elekezi za Mafuta ya Petrol, Diesel pamoja na mafuta ya Taa kwa Mwaka. Bei hizi zitaanza kutumika kuanzia January 3.
  
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Godwin Samwel, bei zitakazoanza kutumika leo Petroli imezidi kupanda bei kwa shilingi 8/lita, kupanda huku kumetokana na mabadiliko ya bei katika soko la Dunia.
 
Pamoja na kutaja bei kikomo za bidhaa mbalimbali za mafuta nchi nzima, EWURA wametaja mambo muhimu ya kuzingatia   kama ifuatavyo.
  • Bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya aina zote yaliyoingizwa nchini kupitia bandari ya Dar es Salaam, yaani Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa zimeongezeka ikilinganishwa na toleo lililopita la tarehe 6 Disemba 2017. Kwa mwezi Januari 2018, bei za rejareja za Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa zimeongezeka kwa Shilingi 8/lita (sawa na asilimia 0.35), Shilingi 34/lita (sawa na asilimia 1.71) na Shilingi 89/lita (sawa na asilimia 4.57) sawia. Vilevile, kwa kulinganisha na toleo la mwezi uliopita, bei za jumla za Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa zimeongezeka kwa Shilingi 7.56/lita (sawa na asilimia 0.37), Shilingi 33.97/lita (sawa na asilimia 1.81) na Shilingi 88.73/lita (sawa na asilimia 4.85) sawia. Ongezeko la bei za mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa limetokana na ongezeko la bei za mafuta hayo katika soko la dunia na ongezeko la gharama za usafirishaji (BPS Premiums).
  • Bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya Petroli na Dizeli yaliyoingizwa nchini kupitia bandari ya Tanga nazo zimeongezeka ikilinganishwa na toleo lililopita la tarehe 6 Disemba 2017. Bei za Mafuta ya Taa hazijabadilika kwa sababu hakuna Mafuta ya Taa yaliyoingizwa nchini kupitia bandari ya Tanga katika mwezi wa Disemba 2017. Katika toleo hili, bei za rejareja za Petroli na Dizeli kwa Mikoa ya Kaskazini zimeongezeka kwa Shilingi 60/lita (sawa na asilimia 2.78) na Shilingi 69/lita (sawa na asilimia 3.47), sawia. Aidha, kwa kulinganisha na toleo la mwezi uliopita, bei za jumla za Petroli na Dizeli zimeongezeka kwa Shilingi 59.68/lita (sawa na asilimia 2.93) na Shilingi 69.02/lita (sawa na asilimia 3.67). Ongezeko la bei za mafuta ya Petroli na Dizeli katika mkoa wa Tanga linatokana na kuongezeka kwa bei za mafuta hayo katika soko la dunia na kuongezeka kwa gharama za usafirishaji (BPS premiums).
  • Ifahamike kwamba, sehemu kubwa ya shehena za mafuta yaliyopokelewa katika bandari ya Dar es Salaam ni zile zenye bei za soko la dunia za mwezi Oktoba 2017 wakati shehena iliyopokelewa katika bandari ya Tanga ni ya bei za soko la dunia za mwezi Novemba 2017. Bei za mafuta katika soko la dunia kwa mwezi Novemba 2017 ziko juu kwa zaidi ya asilimia 6 ikilinganishwa na bei za mwezi Oktoba 2017.
  • Mamlaka inapenda kuukumbusha umma kwamba bei kikomo za mafuta kwa eneo husika, zinapatikana pia kupitia simu za mkononi kwa kupiga namba *152*00# na kisha kufuata maelekezo. Huduma hii ni bure na inapatikana kupitia mitandao yote ya simu za mkononi hapa nchini.
  • Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya mwaka 2015, bei za bidhaa za mafuta ya petroli zitaendelea kupangwa na soko. EWURA itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta. Taarifa hizi zina lengo la kuwasaidia wadau kufanya maamuzi stahiki kuhusu manunuzi ya bidhaa za mafuta.
  • Kampuni za mafuta ziko huru kuuza bidhaa za mafuta ya petroli kwa bei ya ushindani mradi tu bei hizo zisivuke bei kikomo (price cap) kama ilivyokokotolewa na kanuni (formula) iliyopitishwa na EWURA na ambayo ilichapishwa katika Gazeti la Serikali Na. 216/2017 la mwezi Mei 2017.
  • Vituo vyote vya mafuta vinatakiwa kuchapisha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana na yakionesha bei ya mafuta, punguzo, vivutio vya biashara au promosheni zinazotolewa na kituo husika. Pale ambapo inawezekana kuchagua, wateja wanashauriwa kununua bidhaa za mafuta katika vituo vinavyouza mafuta kwa bei nafuu zaidi ili kushamirisha ushindani. Ni kosa kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja. Adhabu kali itatolewa kwa kituo husika kwa kutotekeleza matakwa ya kisheria kwa mujibu wa kanuni husika.
  • Wauzaji wa mafuta ya petroli wanatakiwa kutoa risiti za mauzo kutoka kwenye mashine za EFPP (Electronic Fiscal Pump Printers) na Wanunuzi wahakikishe wanapata stakabadhi hizo za malipo zinazoonyesha jina la kituo, tarehe, aina ya mafuta yaliyonunuliwa na bei kwa lita. Stakabadhi hizo za malipo zitatumika kama kidhibiti kwa wanunuzi wa mafuta endapo kutajitokeza malalamiko ya aidha kuuziwa mafuta kwa bei ya juu kuliko bei kikomo au kuuziwa mafuta  yasiyo na kiwango cha ubora kinachofaa, na pia, risiti hizo zitasaidia kurahishisha ukusanyaji wa kodi za Serikali zitokanazo na mafuta ya petroli.
A: BEI ZA REJAREJA
Mji
Bei Kikomo
Petroli (Shs/Lita) Dizeli (Shs/Lita) Mafuta Ya Taa (Shs/Lita)
Dar es Salaam                2,167               2,018                    2,031 
Arusha                2,263               2,115                    1,995 
Arumeru (Usa West)                2,263               2,115                    1,995 
Karatu                2,281               2,134                    2,013 
Monduli                2,268               2,121                    2,000 
Monduli-Makuyuni                2,273               2,125                    2,005 
Ngorongoro (Loliondo)                2,347               2,200                    2,079 
Kibaha                2,172               2,023                    2,036 
Bagamoyo                2,178               2,029                    2,042 
Kisarawe                2,175               2,025                    2,038 
Mkuranga                2,177               2,028                    2,041 
Rufiji                2,195               2,046                    2,059 
Dodoma                2,226               2,077                    2,090 
Bahi                2,233               2,084                    2,097 
Chemba                2,252               2,103                    2,116 
Kondoa                2,259               2,109                    2,122 
Kongwa                2,223               2,074                    2,087 
Mpwapwa                2,227               2,078                    2,091 
Iringa                2,231               2,082                    2,095 
Kilolo                2,236               2,087                    2,099 
Mufindi (Mafinga)                2,241               2,092                    2,105 
Njombe                2,259               2,110                    2,123 
Njombe (Kidegembye)                2,280               2,131                    2,144 

Ludewa                2,297               2,148                    2,161 
Makete                2,290               2,141                    2,154 
Wanging’ombe (Igwachanya)                2,257               2,108                    2,121 
Bukoba                2,382               2,233                    2,246 
Biharamulo                2,357               2,207                    2,220 
Karagwe (Kayanga)                2,399               2,249                    2,262 
Kyerwa (Ruberwa)                2,404               2,255                    2,268 
Muleba                2,382               2,233                    2,246 
Ngara                2,348               2,199                    2,211 
Misenyi                2,391               2,241                    2,254 
Geita                2,332               2,183                    2,196 
Bukombe                2,321               2,172                    2,185 
Chato                2,353               2,204                    2,217 
Mbogwe                2,370               2,221                    2,234 
Nyang’hwale                2,347               2,198                    2,211 
Kigoma                2,398               2,249                    2,262 
Uvinza (Lugufu)                2,410               2,261                    2,274 
Buhigwe                2,387               2,238                    2,251 
Kakonko                2,355               2,206                    2,219 
Kasulu                2,384               2,235                    2,248 
Kibondo                2,363               2,213                    2,226 
Moshi                2,253               2,105                    1,984 
Hai (Bomang’ombe)                2,256               2,108                    1,988 
Mwanga                2,246               2,098                    1,977 
Rombo (Mkuu)                2,269               2,122                    2,001 
Same                2,239               2,091                    1,971 
Siha (Sanya Juu)                2,259               2,112                    1,991 
Lindi                2,226               2,077                    2,090 
Lindi-Mtama                2,244               2,095                    2,108 
Kilwa Masoko                2,201               2,052                    2,065 
Liwale                2,247               2,098                    2,111 
Nachingwea                2,255               2,106                    2,119 
Ruangwa                2,257               2,108                    2,121 
Babati                2,297               2,149                    2,029 
Hanang (Katesh)                2,307               2,160                    2,039 
Kiteto (Kibaya)                2,312               2,165                    2,044 
Mbulu                2,310               2,162                    2,041 
Simanjiro (Orkasumet)                2,329               2,181                    2,061 
Musoma                2,346               2,196                    2,209 
Musoma Vijijini (Busekela)                 2,386               2,237                    2,250 
Rorya (Ingirijuu)                2,354               2,205                    2,218 
Rorya (Shirati)                2,389               2,240                    2,253 
Bunda                2,337               2,187                    2,200 
Butiama                2,342               2,193                    2,206 
Serengeti (Mugumu)                2,391               2,242                    2,255 
Tarime                2,357               2,207                    2,220 
Tarime (Kewanja/Nyamongo)                2,361               2,212                    2,225 
Mbeya                2,274               2,125                    2,138 

Chunya                2,284               2,134                    2,147 
Chunya (Makongolosi)                2,298               2,149                    2,162 
Ileje                2,287               2,138                    2,151 
Kyela                2,290               2,141                    2,154 
Mbarali (Rujewa)                2,258               2,109                    2,122 
Mbozi (Vwawa)                2,284               2,134                    2,147 
Momba (Chitete)                2,292               2,143                    2,156 
Rungwe (Tukuyu)                2,283               2,134                    2,147 
Morogoro                2,192               2,043                    2,056 
Mikumi                2,208               2,059                    2,072 
Kilombero (Ifakara)                2,230               2,081                    2,094 
Kilombero (Mlimba)                2,252               2,103                    2,116 
Kilombero (Mngeta)                2,242               2,092                    2,105 
Ulanga (Mahenge)                2,241               2,091                    2,104 
Malinyi                2,251               2,102                    2,115 
Kilosa                2,211               2,061                    2,074 
Gairo                2,211               2,061                    2,074 
Mvomero (Wami Sokoine)                2,203               2,054                    2,066 
Turiani                2,217               2,068                    2,081 
Mtwara                2,240               2,090                    2,103 
Nanyumbu (Mangaka)                2,288               2,139                    2,152 
Masasi                2,265               2,116                    2,129 
Newala                2,272               2,122                    2,135 
Tandahimba                2,265                2,115                    2,128 
Mwanza                2,317               2,168                    2,181 
Kwimba                2,353               2,204                    2,217 
Magu                2,325               2,176                    2,189 
Misungwi                2,323               2,173                    2,186 
Sengerema                2,350               2,200                    2,213 
Ukerewe                2,377               2,227                    2,240 
Sumbawanga                2,340               2,191                    2,203 
Kalambo (Matai)                2,347               2,198                    2,211 
Nkasi (Namanyele)                2,353               2,204                    2,217 
Katavi (Mpanda)                2,375               2,226                    2,238 
Mlele (Inyonga)                2,353               2,204                    2,217 
Songea                2,291               2,141                    2,154 
Mbinga                2,324               2,175                    2,188 
Namtumbo                2,320               2,171                    2,183 
Nyasa (Mbamba Bay)                2,326               2,177                    2,190 
Tunduru                2,349               2,200                    2,213 
Shinyanga                2,296               2,147                    2,160  
Kahama                2,310               2,160                    2,173 
Kishapu                2,324               2,175                    2,188 
Simiyu (Bariadi)                2,337               2,188                    2,201 
Busega (Nyashimo)                2,330               2,181                    2,194 
Itilima (Lagangabilili)                2,340               2,191                    2,204 
Maswa                2,329               2,180                    2,192 
Meatu (Mwanhuzi)                2,336               2,187                    2,199 
Singida                2,258               2,109                    2,121 
Iramba                2,270               2,121                    2,134 
Manyoni                2,242               2,093                    2,106 
Ikungi                2,253               2,104                    2,117 
Mkalama (Nduguti)                2,282               2,133                     2,146 
Tabora                2,321               2,172                    2,185 
Igunga                2,275               2,126                    2,139 
Kaliua                2,339               2,190                    2,203 
Ulyankulu                2,333               2,184                    2,197 
Nzega                2,286               2,137                    2,149 
Sikonge                2,333               2,184                    2,197 
Urambo                2,334               2,185                    2,198 
Tanga                2,206               2,059                    1,938 
Handeni                2,227               2,079                    1,959 
Kilindi                2,242               2,094                    1,974 
Korogwe                2,219               2,071                    1,950 
Lushoto                2,228               2,080                    1,960 
Mkinga (Maramba)                2,213               2,066                    1,945 
Muheza                2,211               2,064                    1,943 
Pangani                2,213               2,066                    1,945 

B: BEI ZA JUMLA 
Bei za Jumla – DSM Petroli (Shs/Lita) Dizeli  (Shs/Lita) Mafuta ya Taa (Shs/Lita)
Bei Kikomo 2,056.41 1,907.12 1,920.00

 

Bei za Jumla – TANGA Petroli (Shs/Lita) Dizeli  (Shs/Lita) Mafuta ya Taa (Shs/Lita)
Bei Kikomo 2,095.46 1,947.93 1,827.17

   Mhandisi Godwin Samwel
KAIMU MKURUGENZI MKUU
  EWURA

Maelekezo ya Bodi ya Mikopo kwa wadaiwa ambao bado hawajaajiriwa

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imewataka wanufaika wote wa mikopo ambao wanadaiwa na hawajaajiriwa bado, wafike katika ofisi za bodi hiyo zilizoko katika maeneo mbalimbali nchini ama kuwasiliana nao, ili wapewe maelekezo na utaratibu maalum wa namna ya kulipa mikopo yao.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Bodi ya Mikopo zilizoko Mwenge, Jijini Dar es Salaam, mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa elimu ya Juu (HESLB), Abdul-Razaq Badru ametoa wito kwa wale ambao bado hawajaanza kurejesha mikopo yao, hata kama bado hawajapata ajira maalumu, wafike katika ofisi za bodi maeneo mbalimbali nchini ili kupewa maelekezo na utaratibu wa namna ya kuanza kurejesja mikopo hiyo.

“Tunatoa wito kwa wale ambao kwa sababu fulani fulani walikuwa hawajaanza kulipa, walipe na wanakaribishwa kwenye ofisi zetu. Hata wale ambao hawako kwenye ajira maalum kuna utaratibu maalum tumewatengenezea. Wanaweza kuwasiliana na sisi katika mawasiliano yetu au wakaja ktika ofisi za Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Arusha, Zanzibar na kwingineko il tuwape maelekezo na utaratibu maalum wa kulipa.” amesema Mkurugenzi Badru

Aidha Mkurugenzi Badru amesisitiza kuwa Bodi itahakikisha kuwa inawashughulikia wale wote ambao bado hawajarejesha mikopo yao ili waweze kuirejesha ikiwemo kuwachukulia hatua za kisheria na kuwafikisha mahakamani.

“Mtu yeyote aliyekopa mkopo kwa ajili ya kusoma, njia pekee ya kisheria inayoweza kumfanya asilipe mkopo huu, ni labda awe amefariki. Lakini kama umekopa, uko hai, uko hapa nchini na hata ukienda nje, sisi ni lazima utalipa huo mkopo kwa gharama yoyote ile,” amesisitiza.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Urejeshaji wa Mikopo, Phidelis Joseph amewataka wale ambao tayari wameshaanza kurejesha madeni katika akaunti za benki za Bodi ya Mikopo, waweke maelezo yote katika ”pay-in-slip’ zao.

“Wale wanufaika ambao wanajitokeza na wanalipa kwenye zile ‘bank accounts’ zetu waweke ‘details’ zote. ‘Unapodeposit’ unatakiwa utoe taarifa kwa Bodi ya Mikopo kwamba nimeweka pesa. Lakini vie vile unapoiandika ile ‘slip’ yako uiandike vizuri..,” amesema Phidelis Joseph.

Vile vile amewataka wanufaika wa mikopo ambao wameshaanza kulipa, wafike katika ofisi za Bodi ya mikopo ama kutumia mitandao ya Bodi, kwaajili ya uhakiki.

LHRC yatoa kauli kuadhibiwa vituo vya televisheni

$
0
0
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeviomba vyombo vya kimataifa vinavyohusika na uangalizi wa haki za binadamu kuingilia kati suala la uhuru wa kujieleza nchini.

LHRC pia imetaka Serikali kuheshimu Katiba kwa kutoingilia uhuru wa kujieleza.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatano Januari 3,2018 siku moja baada ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuvitoza faini vituo vya televisheni vya ITV, Azam Two, Startv, Channel Ten na EATV kwa kukiuka kanuni ya maudhui ya mwaka 2005.

Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Dk Hellen Kijo-Bisimba amesema uamuzi wa kutozwa faini vituo hivyo ni ukandamizaji wa uhuru wa vyombo vya habari wa kutoa taarifa kwa jamii na hasa zinazoikosoa Serikali.

"Serikali ikubali kuyasikiliza mazuri na mabaya na kuyatumia maoni ya wananchi. Vituo hivi vimetozwa faini kwa sababu vimetoa taarifa ya tathmini iliyotolewa na LHRC kuhusu uchaguzi mdogo wa madiwani uliofanyika Novemba mwaka jana,” amesema.

Dk Kijo –Bisimba amesema, "Kwetu  tunaona hili si sawa na tunaona mambo haya yanazidi kuongezeka, Serikali kupitia Jeshi la Polisi wamekuwa wakitumia neno uchochezi kuminya uhuru wa mawazo na kujieleza."

Amesema kutokana na hilo, LHRC ipo tayari kuungana na wadau ambao wako tayari kwenda mahakamani kuomba tafsiri ya neno uchochezi na baadhi ya vifungu vya kanuni ya maudhui.

Dk Kijo -Bisimba amesema LHRC imeanzisha harambee kuchangia gharama kuvisaidia vyombo vya habari vilivyokumbwa na adhabu hiyo.

Rais Magufuli Aagana Na Gavana Wa BOT Anayemaliza Muda Wake

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 03 Januari, 2018 ameagana na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) anayemaliza muda wake Prof. Benno Ndulu Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Baada ya mazungumzo yao, Prof. Ndulu amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumuamini na kufanya nae kazi tangu alipoingia madarakani na amebainisha kuwa anafurahi kumaliza kipindi chake huku uchumi wa nchi ukiwa mzuri.

Prof. Ndulu amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa miongozo muhimu iliyosaidia kuimarisha uchumi ikiwemo kudhibiti mfumuko wa bei ambao mwezi Novemba 2017 ulifikia asilimia 4.4 na kuongezeka kwa akiba ya fedha za kigeni kutoka Dola za Marekani Bilioni 1.8 hadi kufikia Dola za Marekani Bilioni 6 hivi sasa, hali ambayo imeimarisha uwezo wa Serikali kujiendesha na kugharamia miradi mikubwa ya maendeleo.

“Nimekuja kumuaga Mhe. Rais na kumshukuru, nafurahi kuwa naondoka wakati hali ya uchumi ikiwa nzuri, Taifa linakopesheka na kuna mazingira mazuri zaidi ya uchumi kuendelea kukua, nampongeza sana Mhe. Rais kwa kusimamia mambo mbalimbali muhimu ya kuimarisha na kukuza uchumi katika kipindi chote nilichofanya nae kazi” amesema Prof. Ndulu.

Mhe. Rais Magufuli pia amezungumza na Gavana Mteule Prof. Florens Luoga na baada ya mazungumzo hayo, Prof. Luoga amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa uteuzi huo na kumhakikishia kuwa ataisimamia BOT ili iendelee kuwa chombo imara cha kusimamia uchumi wa nchi, kuisimamia fedha ya Tanzania na kuhakikisha nchi inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo kama vile ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge), ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam na mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler’s Gorge).

Prof. Luoga ameungana na Prof. Ndulu kueleza kuwa taarifa zinazotolewa na BOT kuhusu ukuaji wa uchumi zinaandaliwa kitaalamu na kwa kushirikisha vyombo mbalimbali vikiwemo Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na ameonya dhidi ya baadhi ya watu ambao wamekuwa wakipotosha ukweli kuhusu takwimu za uchumi zinazotolewa na BOT.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amempongeza Prof. Ndulu kwa utumishi wake wa miaka 10 na kazi nzuri aliyoifanya kusimamia uchumi ambapo katika kipindi hicho kasi ya ukuaji wa uchumi imeongezeka kutoka wastani wa asilimia 5 hadi kufikia asilimia 7, ameimarisha usimamizi wa benki na maduka ya kubadilishia fedha, amesimamia ongezeko la akiba ya fedha za kigeni inayoiwezesha nchi kumudu kuagiza bidhaa na huduma kwa miezi 6 na kuanza kwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya ujenzi wa reli, umeme, ununuzi wa ndege na mingine.

“Nakushukuru sana Prof. Ndulu, umefanya kazi nzuri ya kusimamia uchumi wa Taifa letu, ndio maana leo unamaliza muda wako lakini tayari Benki ya Dunia na kamisheni ya dunia inayoshughulikia teknolojia na maendeleo shirikishi wanakuhitaji ufanye nao kazi, na mimi nimeidhinisha uende ukatuwakilishe” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amempongeza Gavana Mteule Prof. Luoga kwa kupokea uteuzi wake na amemtaka kufanya kazi ya kusimamia uchumi wa Taifa kwa ufanisi mkubwa zaidi ili nchi ipige hatua za maendeleo kwa kasi zaidi.

Rais Magufuli Aahidi Kulipa Bilioni 200 Madeni Ya Ndani Kuanzia Mwezi Ujao

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameeleza kuwa wezi ujao serikali itaanza kulipa madeni ya ndani yatakayokuwa yamehakikiwa.

Rais Magufuli ameyasema hayo Ikulu, jijini Dar es Salaam, leo baada ya kuagana na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) anayemaliza muda wake, Prof. Benno Ndulu na kueleza kuwa, mwezi ujao Serikali itatoa Shilingi Bilioni 200 kwa ajili ya kulipa madeni ya ndani yatakayokuwa yamehakikiwa, yakiwemo ya wazabuni mbalimbali waliotoa huduma katika taasisi za Serikali, madai ya walimu na madai ya wakandarasi.

“Nasisitiza madeni tutakayolipa ni ya ndani, na tutalipa madeni ambayo yamehakikiwa, kwa hiyo maandalizi ya kutoa fedha hizo yaanze mara moja na ni matarajio yangu fedha hizi zitasaidia kuchochea ukuaji wa uchumi wetu” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images