Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Chadema Singida, Wamgeuka Mbowe, Wasimamisha Mgombea

$
0
0
Wakati zikiwa zimebaki siku 25 kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mdogo katika  Jimbo la Singida Kaskazini, kivuli cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Lazaro Nyalandu kimeigawa Chadema katika pande mbili.

Wakati Chadema taifa kikiwa kimeeleza kutoshiriki katika uchaguzi huo Januari 13 mwakani kwa madai ya kutokuridhishwa na uchaguzi wa udiwani wa Kata 43 uliofanyika Novemba 26, uongozi wa Chadema mkoa wa Singida jana umempitisha mgombea atakayepeperusha bendera ya chama hicho.

Uchaguzi wa jimbo hilo unafanyika baada ya Nyalandu kutangaza kujivua uanachama wa CCM Oktoba 30 na kujiunga na Chadema huku mrithi wake akikigawa Chama chake kipya cha Chadema.

Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Singida, Shaban Limu amesema leo Desemba 19  kuwa  wamemteua Djumbe David Joseph kupeperusha bendera ya Chadema na msimamizi wa uchaguzi wilaya ya Singida naye amempitisha.

“Leo tunatarajia kufanya kikao cha kuweka mikakati ya kampeni. Kesho na kesho kutwa, tutaingia kazini kwa kufanya kampeni zitakazokileta chama matokeo tunayoyatarajia ambayo ni kushinda uchanguzi huo mdogo,” alisema Limu

Mbali na Djumbe, wagombea wengine na vyama vyao kwenye mabano ni Dalphina Patrice Mlewa (CUF), Omari Mohammed Sombi (Alliance for Tanzania Farmers Party), Monko Justein Joseph (CCM), Aloyce Mohammed Nduguta (Ada Tadea) na Mchungaji Samwel Libisu (CCK).

Wagombea hao walitangaza jana Desemba 18, 2017 na Msimamizi wa uchaguzi wilaya ya Singida, Rashid Mandoa amesema wamepitisha wagombea hao baada ya kukidhi vigezo vyote vinavyo hitajika.

Mandoa amesema wagombea kutoka vyama vya NRC na UMD wao hawakupitishwa baada ya kushindwa kukidhi vigezo. Pia wagombea kutoka UDP na UDPP hawakurudisha fomu.

Akizungumzia uamuzi huo, Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema amesema; ‘’kwa mjibu wa Katiba ya Chadema, Kamati Kuu ndiyo inayopitisha jina la mgombea na Kamati Kuu haijakutana sasa hilo jina limepatikanaje.”

“Tutashangaa hata NEC (Tume ya Taifa ya Uchaguzi) kama wataendeleza mchakato wa jina hilo na tumeagiza tuletewe taarifa na hatua zitachukuliwa kwa wahusika kwani kilichofanyika ni kosa la jinai, kama barua ya Katibu Mkuu kuthibitisha kupitishwa na Chama haipo wao wameitoa wapi,” amehoji Mrema

Amesema kama kuna watu wametumiwa basi watambue kwamba msimamo wa chama haujabadilika na wanafuatilia suala hilo na hatua zitachukuliwa kwa viongozi waliohusika.

NEC Yatoa Orodha Ya Wanachama 15 Uteuzi Wa Wagombea Ubunge Na Udiwani....CHADEMA Nao Wamo

$
0
0
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa orodha ya wanachama 15 wa vyama vya siasa walioteuliwa kugombea ubunge katika majimbo ya Singida Kaskazini na Longido.

Tume pia imetoa orodha ya majina ya wanachama wengine 15 wa vyama mbalimbali ambao wamejitokeza kugombea udiwani katika uchaguzi mdogo unaofanyika kwenye kata sita.

Walioteuliwa kugombea ubunge katika jimbo la Longido ni Kisiongo Mayasek Olokuya (CUF), Francis Ringo (CCK), Dk Steven KIruswa (CCM), Mgina Mustafa (AFP), Godwin Sarakikya (ADA TADEA), Feruziy Furuziyson (NRA), Ngilisho Paul (Demokrasia Makini), Simon Bayo (SAU) na Robert Lukumy (TLP).

Waliojitokeza kugombea ubunge katika jimbo la Singida Kaskazini ni Omari Sombi (AFP), Dalphina Mlelwa (CUF), Monko Joseph (CCM), David Djumbe (Chadema), Aloyce Nduguta (ADA TADEA) na Mchungaji Yohana Labisu (CCK)

Katika uteuzi huo pia kuna walioteuliwa kugombea udiwani katika kata ya Kimandolu ambako kuna wanachama wa vyama vitano vya Gaudence Lyimo (CCM), |Rashid Nyawaya (CUF), Hamis Mgoya ( NRA), RAmadhani Mcharo (Demokrasia Makini), na  Shafii Kiktunda (SAU).

Katika kata ya KIhesa halmashauri ya Iringa Mjini ameteuliwa Sawani Juli (CCM), Kata ya Keza wilayani  Ngara walioteuliwa ni Eradiu8s Bitemele (NCCR Mageuzi), Bakundukize Gwaibondo (CCM), Philipo Bazubwenge (CUF). Kata ya Kurui wilayani Kisarawe wagombea ni Kunikuni Salumu (CCM) na Kikumbi Mwalimu (CUF),

Kata ya Bukumbi wilaya ya Uyui wagombea ni Kasoga Sizya (CCM), Edward Msigala wa (CUF) wakati kata ya Kwagunda wilaya ya Korogwe walioteuliwa ni Said Shenkawa (CCM) na Yusuf Senkawa wa CUF.

Taarifa ya kuahirishwa kwa kikao cha baraza la vyama vya siasa

Waziri Kigwangalla atengua uteuzi wa wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongro

Taarifa ya CHADEMA kuhusu uteuzi wa mgombea wa ubunge Jimbo la Singida Kaskazini

$
0
0
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) amesikika asubuhi hii wakati akihojiwa na Radio Clouds Fm kwenye kipindi cha Power Breakfast, akisema kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimechukua fomu za kugombea ubunge katika uchaguzi wa marudio Jimbo la Singida Mashariki, mkoani Singida.

Kupitia taarifa hii ya awali, tungependa vyombo vya habari na umma kwa ujumla ujue kuwa;

1. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakijateua mgombea kuwania nafasi ya ubunge katika uchaguzi huo wa marudio, Jimbo la Singida Kaskazini.

2. Mkurugenzi wa NEC, Ndugu Ramadhan Kailima atambue kuwa suala la kugombea nafasi ya ubunge kwa mchakato wa ndani ya CHADEMA linasimamiwa na Kamati Kuu ya Chama na hivyo hivyo yeye hana mamlaka wala hawezi kuwa msemaji wa suala hilo katika hatua ya sasa.

3. Tunafuatilia kupata taarifa za kina kuhusu msingi wa kauli ya Mkurugenzi hiyo, kisha tutatoa taarifa kamili katika hatua ya baadae.

Imetolewa leo Jumanne, Desemba 19, 2017 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano yya Disemba 20

Diwani Mwingine aitosa Chadema na Kujiunga CCM

$
0
0
Diwani wa Chadema wa Donyomurwak wilayani Siha mkoani Kilimanjaro,  Lwite Ndossi maarufu Nsonuu amejivua uanachama wa chama hicho.

Pia, amejiuzuru udiwani na ametangaza kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Taarifa iliyotolewa na idara ya itikadi na uenezi ya CCM  Jumanne Desemba 19,2017 imesema Ndossi ameeleza sababu za kujiunga na CCM ni kuwa kujiunga na watu wanaofanya siasa za kufanya kazi za maendeleo na si kulumbana na maneno matupu.

Rais Magufuli amwaga mabilioni Ruvuma.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kupitia wizara ya Nishati, ametoa kiasi cha shilingi bilioni 210 kwaajili ya ujenzi wa mradi mkubwa wa Umeme unaojengwa mkoani Ruvuma.

Akiongea katika ziara yake ya siku tatu mkoani Ruvuma Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amesema Rais Magufuli ametoa fedha hizo kwa kushirikiana na wahisani wengine.

“Mheshimiwa Rais ndio ametoa fedha hizi bilioni 210 kwa kushirikiana na wahisani ambapo bilioni 104 ni kwaajili ya kusambaza umeme katika wilaya zote za mikoa ya Ruvuma na Songea”, amesema Waziri Kalemani.

Mradi huo wa umeme unatarajiwa kuwafikia wananchi zaidi ya 32,000 katika vijiji 120 vya mikoa hiyo. Waziri ameongeza kuwa mradi huo utawawezesha wananchi kuingiza fedha nyingi kutokana na fursa zitakazojitokeza baada ya kukamilika.

Kalemani amewataka Wakandarasi kumaliza kwa wakati mradi huo kwani tayari wameshapewa fedha zao bila kucheleweshewa. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti 2018.

Wananchi Wampa Makavu Maulid Mtulia Baada ya Kutangaza Kugombea Ubunge Kupitia CCM Baada ya Kuikimbia CUF

$
0
0
Aliyekuwa Mbunge Kinondoni (CUF), Maulid Mtulia ambaye amehamia CCM ametangaza nia ya kugombea tena ubunge katika jimbo hilo kwa tiketi ya chama hicho  tawala.

Desemba 2 Mtulia alijiuzulu nafasi ya ubunge,  huku akisema amefikia uamuzi huo bila kushawishiwa mtu yeyote na amebaini Serikali ya CCM inafanya kazi kubwa ya kutekeleza Ilani na imefanya vizuri katika mambo mengi ambayo upinzani iliahidi kuyatekeleza.

Baada ya hatua hiyo, chama cha CUF upande wa Profesa  Ibrahim Lipumba  kilitangaza  kuwaomba radhi wapiga kura wa Kinondoni kwa Mtulia kujiuzulu uanachama kisha ubunge.

Lakini  jana Jumanne Desemba 19, 2017 kupitia andiko lake mtandaoni, Mtulia amesema atachukua fomu ya kuomba ridhaa  ya kuteuliwa ndani ya CCM ili agombee tena nafasi hiyo.

"Kwaza, nawasalimu wote na khasa wananchi wenzangu wa jimbo la Kinondoni. Nawapa pole sana kwa maumivu makali mliyoyapata kutokana na uamuzi wangu wa kujiuzulu ubunge wa jimbo letu la Kinondoni kupitia chama cha CUF. Nawahakikishia kwamba bado nawapenda sana na niko tayari kuwatumikia tena kwa lengo la kuleta Maendeleo kwenye jimbo letu" aliandika Mtulia

Mtulia alitumia nafasi hiyo kutangaza nia yake kutaka kugombea; "Nichukie fursa hii kutangaza nia kwa wanakinondoni wote na Watanzania kwa ujumla kuwa nitachukua form ya kuomba ridhaa kwenye chama changu cha CCM na endapo chama changu kitaridhia basi nitakuja mbele yenu kuomba ridhaa ya kuwatumikia katika nafasi ya ubunge wa jimbo letu Kinondoni"

Kufuatia ujumbe huo ndipo hapo baadhi ya wananchi walianza kumpa maneno wakionyesha hisia zao juu ya jambo alilofanya na analotaka kulifanya. 

Mkurugenzi wa fedha NHC amrithi Mchechu Aliyetumbuliwa na Waziri Lukuvi

$
0
0
Mkurugenzi wa Fedha wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Felix Maagi ameteuliwa kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Nehemia Mchechu aliyesimamishwa kupisha uchunguzi.

Mchechu alisimamishwa kazi Desemba 16,2017 na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake ambazo hazijawekwa wazi wala mamlaka inayochunguza.

Akizungumza jana  Jumanne Desemba 19,2017 kuhusu mikakati yake baada ya kuteuliwa na Bodi ya NHC kukaimu nafasi hiyo Maagi alisema, ‘’Kwa sasa siwezi kusema kitu kwa kuwa hata ofisi bado sijakabidhiwa.”

“Nikikabidhiwa na nikiingia ofisini nitakuwa na cha kuzungumza lakini kwa sasa sina cha kusema,” alisema.

Maagi ni mhitimu wa Shahada ya Uzamili katika usimamizi wa biashara (MBA) ya Chuo Kikuu cha Esami nchini Uganda na ni mhasibu anayetambulika na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA).

Adam Kimbisa Abwagwa Uspika Bunge la Afrika Mashariki

$
0
0
Bunge la Afrika Mashariki (Eala) limemchagua Spika kutoka Rwanda, Dk Martin Ngoga katika uchaguzi ulioibua mabishano ya kisheria juu ya uhalali wa kufanyika kwake.

Baada ya dua ya kuliombea Bunge, mbunge Dk Ngwaru Maghembe kutoka Tanzania aliomba mwongozo wa kuliahirisha kutokana na akidi kutotimia kutokana na wabunge tisa wa Burundi na saba wa Tanzania kutokuwepo kwa sababu ambazo hazikujulikana.

Mbunge kutoka Uganda, Freddy Mbidde alipinga hoja hiyo akisema kanuni ya 53(1) inayozungumzia akidi inahusu Bunge rasmi ambalo tayari lina Spika lakini kwa kuwa hawakuwa na Spika kanuni hiyo haina nguvu kisheria.

Mbunge mwingine wa Tanzania, Dk Abdullah Makame alisema kutokana na Bunge kuchelewa kuanza kazi kwa kipindi cha miezi sita kutokana na mwanachama wa EAC nchi ya Kenya kuchelewa kuchagua wabunge ni busara uchaguzi usifanyike hadi wabunge wote wawepo.

Hoja hiyo ilipingwa na mbunge kutoka Uganda, Suzane Nakauki aliyedai hoja ya kutokufanya uchaguzi kwa sababu ya wabunge kutokuwepo haina mashiko kisheria na kikanuni kwa sababu wameorodhesha majina yao kwenye kitabu cha mahudhurio na wamepewa posho na wameamua kwa sababu zisizojulikana kugomea uchaguzi.

Alisema haiwezekani wabunge wa Tanzania ambao wapo nchi mwao washindwe kuhudhuria kikao cha Bunge wakati wapo jijini Arusha, huku waliotoka mbali wakiwepo.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Balozi Liberat Mfumukeko alisema kila jambo lenye mgogoro kwenye mihimili ya EAC lina utaratibu wa kulimaliza kwa njia ya kuomba ushauri kwa sekretariati, Mahakama, baraza la mawaziri na kikao cha marais.

Hatua hiyo ilimwinua Waziri wa Afrika Mashariki wa Burundi, Isabella Ndahayo aliyesema wabunge wa Burundi hawakuridhishwa na utaratibu wa uchaguzi licha ya kanuni kutamka wazi nafasi ya Spika ni ya mzunguko kwa nchi wanachama.

"Wabunge wa Burundi hawapo kwa sababu hawaridhiki na kinachoendelea, naomba tupewe tafsiri ya nafasi ya Spika kuwa ni mzunguko kwa nchi wanachama, si kwamba tunapinga juhudi za mshikamano wa jumuiya bali tafsiri halisi," alisema Isabella.

Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Uganda ambayo ni Mwenyekiti wa EAC, Julius Wandera alisema kumekuwa na mashauriano kati ya baraza la mawaziri wa jumuiya hiyo ili kuhakikisha suala hilo linakamilika.

Baada ya mabishano ya kisheria na kanuni, katibu wa bunge aliamua uchaguzi kufanyika na awamu ya kwanza, mgombea kutoka Rwanda, Dk Martin Ngoga alipata kura 35, Leontine Nzeyimana wa Burundi kura moja na Adam Kimbisa wa Tanzania hakupata kura.

Kutokana na kanuni kuhitaji mshindi kupata theluthi mbili ya kura zote 52, uchaguzi ulirudiwa kwa kanuni ya mshindi kupatikana kwa wingi wa kura na Dk Ngoga aliibuka mshindi  kwa kupata kura 33 dhidi kura tatu za Nzeyimana ambaye hakuwepo bungeni.

Baada ya kula kiapo Dk Ngoga ambaye alikuwa mwendesha mashtaka mkuu wa Rwanda alisema anafahamu uchaguzi wowote lazima uache majeraha lakini yupo tayari kushirikiana na kila mbunge kujenga jumuiya hiyo.

Rais Magufuli: "Airtel kwa taarifa tulizo nazo, ni mali ya TTCL......Pamefanyika tu michezo ya hovyo hovyo"

$
0
0
RAIS John Magufuli amesema Serikali imebaini kuwa kampuni ya Mawasiliano ya Bharti Airtel ni mali ya Shirika la Mawasiliani Tanzania (TTCL) na amemwagiza  Waziri wa fedha na mipango kufuatilia suala hilo haraka ili Airtel irudishwe kumilikiwa na serikali.

Rais ameyasema hayo leo Desemba 20 wakati akizungumza kwenye Ofisi za Taifa za Takwimu mjini Dodoma.

“Kampuni ya AIRTEL imethibitika kuwa ni mali ya Shirika la TTCL, lakini kuna mchezo ulifanyika, sasa sitaki kuongea sana. Nataka Waziri wa Fedha ufuatilie suala hili kabla ya mwaka huu kuisha,” amesema Magufuli.

Taarifa na ndani zinabainisha kwamba hisa za Airtel  zinatarajiwa kukabidhiwa kwa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na kuendesha biashara za kampuni hiyo yenye wateja wengi zaidi nchini ikiwa nyuma ya Vodacom na Tigo.

Chanzo cha mpango huo kinatajwa kuwa ni uongozi wa juu wa TTCL uliotaka Serikali kudai haki zake za uwekezaji ndani ya Airtel ambako inaimiliki kwa ubia wa asilimia 40 kwa 60 na mwekezaji.

Taarifa zinaarifu kuwa  TTCL itamiliki hisa zote za Airtel Tanzania Limited ambapo tayari TTCL imewasilisha hoja ya kutaka kufanya hivyo baada ya kubaini kwamba Serikali ilipunjwa kwenye hesabu za uwekezaji.

Hoja ya TTCL inaanzia Novemba 3, 1998 ilipoanzisha kampuni tanzu ya Cellnet ambayo ilifanya kazi mpaka Mei 7, 2001 ilipobadilishwa jina na kuitwa Celtel Tanzania huku umiliki wake ukiendelea kuwa chini ya shirika hilo kwa asilimia zote baada ya kuwekeza Dola milioni tano za Marekani (zaidi ya Sh11 bilioni sasa).

Lakini, Januari 31, 2002, Celtel ikiwa chini ya umiliki wa TTCL ilikopa kiasi cha Dola 82 milioni (zaidi ya Sh180.4 bilioni) ili kukuza mtaji wake.

Kwa kipindi hicho, TTCL iliyokuwa na thamani ya Dola 600 milioni (zaidi ya Sh1.32 trilioni) ilikuwa inamilikiwa kwa ubia kati ya Serikali na Kampuni ya Mobile System International (MSI) ya Uholanzi. Serikali ilikuwa inamiliki asilimia 65 ya hisa zote na mbia huyo asilimia 35 zilizosalia.

Agosti 5, 2005, mabadiliko yalifanywa kwenye bodi ya wakurugenzi wa Celtel kwa lengo la kuunda kampuni mbili tofauti; Celtel ikitenganishwa na TTCL. Kutokana na mabadiliko hayo, Celtel iliwekwa chini ya umiliki wa MSI ambayo Septemba 2007 iliuza hisa zake kwa Zain ambayo nayo ilikuja kuziuza kwa Bharti Airtel, Juni 8, 2010.

Imeelezwa kuwa TTCL inadai uwekezaji wake ilioufanya Celtel baadaye Airtel ambayo thamani yake imeongezeka maradufu sasa haulingani na inachokipata hivyo kutaka kusimamia biashara za kampuni hiyo ya mawasiliano.

Hoja ya madai hayo ni namna umiliki wa hisa ulivyobadilishwa baada ya Celtel kutenganishwa na TTCL ambayo ilipewa hisa chache tofauti na ilivyostahili.

Kwa sasa, Airtel Tanzania inamilikiwa na Serikali yenye asilimia 40 na Celtel Tanzania BV, kampuni tanzu ya Zain Africa BV ambayo ilinunuliwa na Bharti Airtel International, Novemba, 2010 ikiwa na asilimia 60.

Katika mabadiliko yaliyofanywa hivi karibuni, Serikali iliilipa Bharti Airtel Sh14.7 bilioni hivyo kuchukua asilimia 35 ya hisa ilizokuwa inamiliki na kuifanya imiliki asilimia zote za TTCL.

Sheria mpya iliyopitishwa hivi karibuni na Bunge imeibadili TTCL inayohudumia asilimia 0.82 ya soko kuwa shirika la umma la mawasiliano na kulipa jukumu kubwa katika sekta ya mawasiliano nchini.

Bharti Airtel inatakiwa kuorodhesha asilimia 25 ya hisa zake katika Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE) ili kukidhi vigezo vya sheria ya posta na mawasiliano ya mwaka 2010, lakini bado haijafanya hivyo.

Wanaopotosha Takwimu za Taifa Kwa Kisingizio Vyuma Vimekazaka Kufikishwa Mahakamani

$
0
0
Rais  Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa watu ambao wanasema vyuma vimekaza na wale ambao wamekuwa wakisambaza takwimu mbalimbali za kupikwa kukamatwa na kuwekwa ndani na baadaye kupelekwa mahakamani.

Magufuli amesema hayo leo alipokuwa akiweka jiwe la msingi katika jengo la ofisi ya Taifa ya Takwimu Dodoma na kuwataka wananchi kuwa makini na masuala ya takwimu pia amewataka kuwapuuza watu ambao wanasema vyuma vimekaza ili hala watu wa Takwimu wanasema vyuma vimefunguka.

"Ukikosea kutoa takwimu umeichafua nchi, takwimu ni kitu kibaya sana ndiyo maana kuna watu wamebobea kwenye takwimu hivyo wananchi tuwasikilize watu wa takwimu asitokee mtu mwingine akatoa takwimu tofauti na zile walizonazo watu wa takwimu. 

"Mtu anasema vyuma vimekaza wakati watu wa takwimu wanasema vyuma vimefunguka watu hawa wanatakiwa kukamatwa na kuwekwa ndani ili wakajifunze kutoa takwimu huko" alisema Rais Magufuli

Mbali na hilo Rais Magufuli ameagiza watu ambao watatoa taarifa zozote ambazo zipo kinyume na takwimu walizonazo watu wa takwimu wafikishwe mahakamani ....."Mimi ningekuwa hakimu watu wa namna hiyo wangepewa adhabu zote mbili kulipa faini na kufungwa" 

“Ninawaomba Watanzania mpuuze uzushi unaoendelea kwenye mitandao ya kijamii kwamba uchumi umeshuka. 

"wanaosema vyuma vimebana, vitabana tu kwa wale waliokuwa wamezoea fedha za bure bure, na vitaedelea kubana kweli kweli Lakini kwa wale wanaochapa kazi, kwa mfano wakazi wa Lindi na Mtwara, walikuwa wanauza korosho saa nyingine kwa bei ya chini mpaka elfu 2 kwa kilo, sasa elfu 4 kwa kilo. 

"Wale vyuma haviwezi vikabana, wale vyuma vimeachia, nasikia wanaamua hata mbuzi kuzinywesha bia, kule vyuma vimefungua., hivyo wapuuzieni watu wanaowadanganya vyuma vimekaza”, amesema Rais Magufuli.

Mbali na hilo Magufuli amewataka wananchi na taasisi mbalimbali wakitaka takwimu yoyote ile waende ofisi ya Takwimu na wasithubutu kutoa takwimu ambazo zinapingana na zile zilizopo ofisi ya takwimu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Disemba 21

Rais Dkt Magufuli amteua Wakili Albert Msando Katika tume kuchunguza mali za CCM


NEC yawashukia CHADEMA kuhusu mgombea Ubunge Singida Kaskazini

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeeleza kuwa inawashangaa viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wanaosema kuwa hawamtambui mgombea wa ubunge aliyesimamishwa kugombea katika jimbo la Singida Kaskazini.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Ramadhan Kailima ameeleza kuwa CHADEMA kupitia Katibu wa Wilaya wa Singida Vijijini wamekamilisha mchakato wa utambulisho wa mgombea wa Ubunge jimbo la Singida Kaskazini, Joseph Njumbe

“Halmashauri ya Wilaya ya singida wagombea 6 wameteuliwa juzi mmojawapo akiwa bwana Joseph Njumbe wa CHADEAMA. Ameteuliwa kwa sababu amekidhi vigezo vya kikatiba, kisheria na kikanuni yeye na chama chake cha Demokrasia na Maendeleo.”

“Kwa hiyo wanapolalamika kwamba huyu hawamjui nawashangaa sana. Nawashangaa sana kwa saababu Kwa mujibu wa ibara ya 67 ibara ndogo ya 1b ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema Mgombea yeyote wa ubunge lazima awe amependekezwa na chama cha siasa kilichosajiliwa.”

“Kanuni namba 31 kanuni ndogo ya kwanza ya uchaguzi wa Rais na wabunge ya mwaka 2015, inasema mtu akitaka kugombea ubunge atawasilisha barua yake ya utambulisho iliyosainiwa na katibu wa chama au wa wilaya wa chama husika. Barua yake inawasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi.”

“Huyu Bwana David Joseph Njunbe amewasilisha barua hiyo ya utambulisho iliyosainiwa na katibu wa CHADEMA wa Wilaya ya Singida Vijijini, Bwana Amani M mloya,” amesema Kailima.

Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Kailima Ramadhani amesema kuwa kwa kupitia kanuni na vigezo vya sheria ya uchaguzi, Mgombea huyo wa CHADEMA amekidhi vigezo vyote vilivyohitajika ili kupitishwa kugombea Ubunge katika jimbo hilo.

Aidha, Kailima ameeleza kuwa Joseph Njumbe, pamoja na kuwa ameshakamilisha taratibu za kupitishwa kuwa mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CHADEMA, bado ana haki ya kikatiba ya kujiondoa katika kinyang’anyiro hicho pale tu atakapotimiza taratibu zinazotakiwa ili kujiondoa.

Kailima aliongeza kuwa Tume ya Uchaguzi haiangalii

“Sisi hatuangalii muhtasari wa kamati kuu ama hatuangalii katiba iliyosajiliwa na Katibu Mkuu wa chama chochote cha siasa. Tunaangalia barua iliyosainiwa na Katibu wa Chama wa Mkoa ama Katibu wa Chama wa Wilaya  na ni kwa mujibu wa sheria, kanuni na maelekezo,” amesema Kailima.

CHADEMA pamoja na vyama vingine vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) vilitangaza kutokushiriki uchaguzi huo mdogo wa wabunge na madiwani unaotarajiwa kufanyika Januari 18, 2018 ikidai kuwa mwenendo wa hali ya kisiasa nchini siyo shwari na kuitaka Tume ya uchaguzi kuahirisha uchaguzi huo.

Juzi CHADEMA kupitia Mkuu wake wa Idara ya Mawasiliano, Tumaini Makene ilitoa taarifa kuwa hakijateua mgombea wa ubunge katika Jimbo la Singida Kaskazini na kumtaka Ndugu. Ramadhani Kailima kutambua kwamba mchakato wa uteuzi wa mgombea wa ubunge ndani ya CHADEMA linasimamiwa na Kamati kuu ya Chama hicho.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0
Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi apata ajali, avunjika mkono na Kulazwa hospitali ya KCMC

$
0
0
Mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC mjini Moshi baada ya kuvunjika mkono.

Mbatia ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), amevunjika mkono wa kushoto baada ya kuteleza na kuanguka na amelazwa katika wodi za watu mashuhuri (VIP).

Msaidizi wa mbunge huyo, Hamis Hamis alisema jana Jumatano Desemba 20,2017 kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 2:45 usiku wakati akiondoka hotelini kurejea nyumbani.

Hamis alisema Mbatia alikuwa akishuka ngazi katika hoteli ya Uhuru iliyopo eneo la Shanty Town ndipo alipoteleza na kuanguka.
“Bahati nzuri pale kulikuwa na daktari wa KCMC anaitwa Ansbert Sweetbert ndiye alitoa huduma ya kwanza hadi kumpeleka KCMC,” alisema.

Alisema, “Kwa kweli huyo daktari alikuwa msaada mkubwa. Ndiye aliyempeleka KCMC na alikaa naye hadi saa nane usiku. Wauguzi na madaktari KCMC walimpa msaada mkubwa.”

Nape Nnauye Avutiwa ANC Ya Afrika Kusinii Ilivyopata Mwenyekiti Wake, Atupa Jiwe Gizani

$
0
0
Mbunge Nape Nnauye ametoa yake ya moyoni kwa kuhoji vyama vya siasa na wanasiasa Tanzania wanajifunza nini kufuatia mchakato wa uchaguzi ndani ya chama tawala cha (ANC) uliofanyika Afrika Kusini mwanzoni mwa wiki hii kumpata kiongozi wa chama hicho.

Chama tawala cha African National Congress (ANC) kilikuwa na uchaguzi wa ndani kumtafuta kiongozi wa juu ya chama hicho ambapo kulikuwa na zoezi la uchaguzi na nafasi hiyo kugombewa na wananchama wa chama hicho na kupigiwa kura, ambapo mwisho wa siku Cyril Ramaphosa aliibuka mshindi kwa kura nyingi zaidi dhidi ya Nkosazana Dlamini-Zuma hivyo Cyril Ramaphosa kutangazwa Rais wa (ANC).

"Tunajifunza nini kwa mchakato uliopelekea kupatikana kwa Cryll Ramaphosa kama Mwenyekiti wa ANC!? Alihoji Nape Nnauye

Uchaguzi wa Chama tawala nchini Afrika Kusini (ANC) ulitofautiana na uchaguzi wa Chama Tawala nchini Tanzania ambapo Mwenyekiti wake alipatikana kwa kupigiwa kura ya Ndiyo au Hapana wakati Afrika Kusini nafasi hiyo iligombewa na mtu zaidi ya mmoja.

Wabunge wa Tanzania, Burundi Wamkataa Spika wa EALA

$
0
0
Baada ya Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika mashariki kuchaguliwa na wajumbe wa nchi nne za jumuiya badala ya sita wabunge kutoka Burundi na Tanzania na Burundi wamesema uchaguzi huo umekiuka misingi na kanuni za Jumuiya hiyo.

Wakizungumza na waandishi wa habari Jijini Arusha, Mwakilishi wa wabunge hao wamesema hakukuwa na sababu ya kutumia nguvu,jazba na uharaka wa kumchagua Spika kabla ya hoja zao ikiwemo ya kutaka kupata ufafanuzi wa mzunguko wa kumpata spika haujatolewa na kwamba hawakubaliani na  suala hilo na endapo  hali isipodhibitiwa malengo ya kuundwa kwa jumuiya hiyo hayatatimia.

Kwa upande wao Wabunge kutoka Tanzania wamesema hatua ya wabunge wa bunge hilo kuanza kukiuka viapo vyao muda mfupi baada ya kuapishwa ni dalili za kukosa moyo wa uvumilivu, umoja, na ushirikiano wa dhati ambao kwa muda wote ndio umekuwa msingi wa jumuiya hiyo na sio dalili nzuri hasa ikizingatiwa kuwa miongoni mwa malengo ya jumuya ni kudumisha mshikamano na kwamba kilichofanyika ni sio kumchagua Spika bali ni maoni yao kuwa Mh. Martin anafaa kuongoza.

Aidha Wabunge wa Tanzania wamesema kuwa wanaendelea kuziomba ngazi zinazohusika kuangalia upya suala hilo na kutoa nafasi ya majadiliano kwani ndio msingi wa kupata suluhu.

Kufuatia hali hiyo wabunge kutoka Burundi licha ya kudai kuwa hawamtambui Spika aliyechaguliwa wamesema hawawezi kushiriki kikao chochote kitakachoendeshwa na spika huyo.

Wabunge hao wa Jumuiya ya Afrika Mashariki waliapishwa siku ya tarehe 18 /12 /2017 na wakati wa kumchagua spika uliibuka mjadala unaodaiwa kusababishwa na taarifa zilizotolewa na katibu wa Bunge kuwa wabunge wa nchi zote ispokuwa uganda wanaweza kuomba kugombea uspika wakati utaratibu wa awali ulikuwa ni wa kufuata mzunguko.

Wabunge hao wamefafanua kuwa hata kama mzunguko ungezingatiwa bado lingehitaji ufafanuzi ambao ungezihusisha Burundi, Rwanda na Sudani Kusini suala ambalo wanasema licha ya kuliwasilisha lilipuuzwa.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images