Msanii
wa filamu Elizabeth Michael Kimemeta (18), maarufu kama Lulu (pichani)
anayekabiliwa na kesi ya mauaji ya bila kukusudia ya msanii mwenzake
Steven Kanumba (28), anatarajia kujibu mashitaka yake kwa mara ya
kwanza Februari 17, mwaka huu katika Mahakakama Kuu Tanzania, Kanda ya
Dar es Salaam.
Kwa
mujibu wa ratiba ya vikao vya kesi za mauaji na bila kukusudia,
iliyotolewa
Lulu Michael kusomewa mashitaka ya kuua bila kukusudia tarehe 17 ya mwezi huu
↧
↧
Mtu mmoja akutwa amejinyonga maeneo ya ufukwe wa spice motel beach huko Kagera
Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Bahati maarufu kwa uuzaji wa
mifuko ya plastiki maeneo ya stand kuu ya mabasi Bukoba amekutwa
kajinyonga juu ya mti maeneo ya ufukwe wa Spice Motel
majira ya saa nane mchana ..
Taarifa za awali kutoka kwa watu
waliokuwa katika tukio hilo zinasema kuwa , kabla ya kifo cha, marehemu alionekana akiwa na mafurushi ya vitu na
alikuwa akifua
↧
Vijana wanaswa wakijisaidia katika masinki ya kunawia ndani ya uwanja wetu wa taifa wa mpira.
Pichani
juu ni baadhi ya wadau wa Soka waliokutwa hivi karibuni wakijisaidia
kwenye masinki ya kunawia mikono kama waonekanavyo pichani.
Hapa
baada ya kumaliza shughuli yao haoo wakaondoka,je wahusika
wanalichukuliaje jambo hili lisilo la kiungwana kabisa ndani ya uwanja
wa wetu wa mpira,ambao umejengwa kwa gharama kubwa,lakini kuna baadhi ya
watu kama hawa wamekuwa wakiharibu
↧
Rais Atangaza majina ya wajumbe wa bunge la katiba ....Bofya hapa kuyaona
UTANGULIZI
1. Uteuzi wa Wajumbe wa Bunge la Katiba Unatawaliwa na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura, 83 (The Constitutional Review Act, Cap 83).
Sheria hii inaweka mamlaka ya uteuzi, masharti, taratibu, vigezo na
mambo mengine yote yanayopaswa kuzingatiwa katika uteuzi wa Wajumbe wa
Bunge la Katiba. Kwa mujibu wa Kifungu cha 22 (2A) na (2B) vigezo hivi
vinajumuisha umri, jinsia,
↧
Taarifa ya Ofisi ya Lowassa kuhusu kurasa zenye jina lake facebook, twitter na instagram
Kumekuwa na kurasa (accounts) mbalimbali zenye jina la Mhe. Edward
Lowassa katika mitandao ya kijamii kama vile Facebook, Twitter,
Instagram n.k. zinaonekana mmiliki wake ni Mhe. Edward Lowassa.
Ukweli ni kwamba hizo zote hazimilikiwi na Mhe. Lowassa.
Kwa maana hiyo chochote kinachoandikwa au kuchapishwa kwenye kurasa hizo hazihusiani kwa namna yoyote na Mhe Lowassa.
↧
↧
Mshahara kima cha chini ni 720,000/-
SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), limependekeza mshahara wa kima cha chini uwe sh 720,000.
TUCTA imekuja na pendekezo hilo huku kukiwa na taarifa kwamba
serikali imepandisha kiinua mgongo kwa wabunge kutoka sh milioni 43 za
awali hadi sh milioni 160, pamoja na nyongeza ya mishahara na posho zao.
Pendekezo hilo la TUCTA lilitangazwa jana na Katibu Mkuu wa
↧
"Wanaohoji Lowassa kutengenezewa fulana zenye picha yake na ujumbe wa ‘Friends of Lowassa’ (Marafiki wa Lowassa) ni washamba".. Talib Ali Talib
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Talib Ali
Talib, amesema wanachama na viongozi wanaohoji Waziri Mkuu mstaafu
Edward Lowassa kutengenezewa fulana zenye picha yake na ujumbe wa
‘Friends of Lowassa’ (Marafiki wa Lowassa) ni washamba.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, mjumbe huyo alisema
haikuwa sahihi kwa Waziri Mkuu mstaafu John Samuel Malecela kushangaa
↧
Mwalimu wa Shule ya Msingi ajinyonga chooni kwa madai ya msongo wa mawazo.
MWALIMU wa Shule ya Msingi Mwang’osha Kata ya Nyamalongo wilayani Shinyanga, Christipian Mafuru (24) amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa madai ya msongo wa mawazo.
Mafuru ambaye alitumia kamba ya katani na kujinyonga kwenye choo chake. Ameacha ujumbe uliosomeka ‘Msongo wa mawazo umenilazimu nifanye hivi, poleni sana walimu wenzangu, samahani wazazi wangu, kwa heri mwanangu Ray.’
↧
Shule Dar taabani, walimu wakalia khanga chini ya miti
Shule
ya Msingi Mtambani iliyoko Kinondoni jijini Dar es Saalam, haina
samani hali inayosababisha wanafunzi kukaa chini, wakati walimu
wanalazimika kutandaza khanga wanazokalia chini ya miti.
“Shule hii ina upungufu wa madawati, nusu ya wanafunzi wanakaa chini,
hatuna ofisi za kutosha za walimu wale wasio na nafasi wanakaa chini
ya miti”, alisema Mwalimu Mkuu Emmanuel Munisi.
↧
↧
Watu tisa watiwa mbaroni kwa tuhuma za mauaji ya wanawake wawili wanaodaiwa kuzuia mvua kunyesha mkoani Simiyu
Na Chibura Makorongo, Simiyu.
Jeshi la polisi mkoani Simiyu
linawashikilia watu tisa wakiwemo wanawake wawili wa kijiji cha
Mwabulimbu wilayani Maswa kwa tuhuma za mauaji ya kikatili ya kina mama
wawili kuuawa na kuchomwa moto kwa kudaiwa kuzuia mvua kunyesha.
Mbali na wanawake hao polisi pia inawashikilia viongozi wakuu wa jeshi la
ulinzi wa jadi "Sungusungu" akiwemo Mtemi na
↧
Jambazi mkuu aliyekuwa anasakwa na jeshi la polisi kwa mauaji ya watu 8 huko Tarime akamatwa mkoani Tanga
Mkuu wa jeshi la polisi nchini
**
via Imma Matukio — Jambazi mkuu anayetuhumiwa kujihusisha na matukio
ya mauaji na unyang'anyi wa kutumia silaha yaliyo tokea Wilayani Tarime
kuanzia 26 hadi 28.01.2014 amekamatwa na jeshi la polisi jioni ya Tarehe
06.02.2014 mkoani Tanga.
Akisimulia kukamatwa kwa jambazi huyo
Kamanda wa mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya Justus Kamugisha amesema kuwa
↧
Nape alaani vitendo vya kikatili na kinyama vinavyofaywa na CHADEMA.....
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari
katika ofisi za CCM Mkoa wa Mwanza.Nape alisema kitendo cha wana CCM
kushambuliwa ni kitendo cha kinyama na kinatakiwa kikemewe na kila
mtu,pia alisisitiza Vijana wa CCM kuwalinda wapigaji kura wao siku ya
kupiga kura.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisisitiza jambo wakati wa
mkutano
↧
Shilole ayazungumzia MADONGO aliyorushiwa na Baby Madaha, "najua kuna vitu vingi nimekuzidi.." .. ampa ushauri
Baada ya msanii wa Candy n Candy, Baby Madaha kufunguka
akimchana wazi msanii mwenzake wa kike, Shilole kwa
kudai kuwa nyimbo zake haziwezi kulinganishwa na nyimbo anazofanya
Shilole, Shilole nae kakikalia kiti kile kile na kuyajibu makavu hayo.
Shilole amedai kuwa hawezi kupoteza muda kumzungumzia Baby Madaha, na
kwamba yeye anaamini hana tatizo naye lakini anashangaa kuona
↧
↧
Jose Chameleone amuonesha mkewe 'Danniella' anavyompenda kwa kuchora tattoo ya jina lake shingoni
Wakati tunaelekea katika ile siku inayoaminika kuwa siku ya
wapendanao ‘Valentine’s Day’, mkali wa Valuvalu Jose Mayanja Chameleone
ameamua kumuonesha mkewe Daniella na dunia nzima jinsi anavyompenda, kwa
kujichora tattoo yenye jina lake shingoni.
Chameleone ambaye yuko nchini Afrika Kusini kwa shughuli za kimuziki,
alipost picha hizo kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook, picha
↧
DK Cheni adai filamu yake ya 'Nimekubali Kuolewa' haichochei USHOGA kama bodi ya filamu ilivyoichukulia na kuamua kuizuia
Uamuzi wa bodi ya Filamu Tanzania (TFB) kuizuia filamu ya
muigizaji wa kiume na mkongwe, Dk Cheni ‘Nimekubali Kuolewa’, kwa madai
ya kukiuka maadili na kuchochea tabia za ushoga, umepingwa na msanii
huyo ambaye anaamini kabisa kuwa maudhui ya filamu hiyo yangeelimisha
jamii zaidi ya picha katika cover yake.
Dk Cheni ameiambia Global Publishers kuwa picha iliyoko kwenye bango
la
↧
Video ya wimbo wa Shakira na Rihanna yadaiwa kuchochea USAGAJI na uvutaji sigara, Colombia yaombwa kuipiga marufuku
Video ya wimbo wa Shakira ‘Cant Remember to Forget You’ aliyompa
shavu mwimbaji mwenzake wa Caribbean, Rihanna imekosolewa vikali na
mwanasiasa mmoja nchini Colombia anayefahamika kwa jina la Marco Fidel
Ramirez, akidai kuwa kinyume cha maadili na hivyo kuwaharibu watoto
wadogo.
Marco Fidel, ameiomba serikali ya Colombia kuipiga marufuku video
hiyo ama vipande vya video hiyo
↧
Askari wa usalama barabarani ajikuta katika wakati mgumu baada ya kulipiga mkono na kulizuia gari alilokuwa amepanda mheshimiwa Rais.
Tukio hili limetokea kwenye mji mkuu wa Kenya ambao ni Nairobi pale Rais Uhuru
Kenyatta wa nchi hiyo alipotumia gari moja tu bila msafara akitokea Ikulu kwenda
kwenye hoteli moja kwa ajili ya kukutana na Wanafamilia.
Toka amechukua madaraka, Rais Uhuru Kenyatta amekuwa na tabia ya kutumia gari moja tu bila msafara, tofauti na Rais Kibaki ambaye kila sehemu aliyotia mguu
↧
↧
Maaskofu, Masheikh waeleza uhusiano wao na wanaowania urais 2015
VIONGOZI wa dini nchini wamesema kuwa uhusiano wao na watu wanaoutaka
urais mwaka 2015 si wa kisiasa, bali ni wa kiimani zaidi. Kauli hiyo ya
viongozi wa dini imekuja wakati ambao baadhi ya wanasiasa wamewaelekezea
lawama kuwa wanatumiwa vibaya na watu wanaoutaka urais mwaka 2015.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti la Mtanzania viongozi hao walisema
uhusiano wao na wanasiasa,
↧
CHADEMA na CCM kupambana leo katika uchaguzi wa madiwani
Uchaguzi wa madiwani katika Kata za Malindo wilayani Rungwe na Santiliya katika Wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani Mbeya , unafanyika leo.
Msimamizi wa Uchaguzi wa Kata ya Malindo, Stephen Mwakingwe alisema maandalizi yote muhimu yamekamilika.
Mwakingwe alisema “CCM imesimamisha Nelson
Mwaitembo, wakati Chadema mgombea
↧
Mtoto wa aliyekuwa waziri wa fedha ( marehemu Dr. Mgimwa ) ashinda kura za maoni kugombea ubunge wa jimbo hilo la Kalenga
Godfrey
Mgimwa, mmoja wa watoto wa Marehemu Dkt William Mgimwa, akiongea kwa
niaba ya familia wakati wa mazishi ya baba yake kijijini Magunga jimbo
la Kalenga mkoani Iringa.
--
Na Francis Godwin, Iringa
**
Mtokeo
ya kura za maoni ndani ya CCM yametangazwa usiku wa kuamkia leo
huku mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Godfrey Mgimwa akishinda
kwa kishindo katika
↧
More Pages to Explore .....