Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tundu Lissu Asimulia Alivyonusurika Kupigwa Risasi ya Fuvu la Kichwa

0
0
Kwa mara ya kwanza, Tundu Lissu amezungumzia shambulio la kinyama alilofanyiwa na watu wasiojulikana kwa kueleza kuwa, alinusurika kufumuliwa fuvu la kichwa kwa risasi.

Lissu, Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), aliyasema hayo jana, jijini Nairobi anakotibiwa wakati akihojiwa na Jarida la Financial Times  la Uingereza.

Yakiwa ni mahojiano yake ya kwanza tangu aliposhambuliwa nje ya makazi yake yaliyoko Area D, mjini Dodoma Septemba mwaka huu, Lissu mmoja wa wakosoaji wakubwa wa serikali alisema anaamini alikuwa mlengwa wa jaribio la mauaji.

Akizungumzia shambulio hilo dhidi yake, alisema sekunde chache baada ya watu wawili wenye silaha kushuka katika gari lililokuwa likimfuatilia kwa wiki tatu, derava wake alimsukuma chini ya sakafu ya gari lake wakati wakihangaika kukwepa risasi nyingi zilizoelekezwa kwenye gari lake, nyingi zilimpiga mgongoni na nyingine kwenye bega lakini risasi moja ilikosakosa kufumua fuvu lake la kichwa.

“Hali ikawa mbaya sana kwa sababu sikuweza kuhesabu risasi, naambiwa kwamba risasi 38 zilipiga gari langu na 16 zilinipata na moja iliyokuwa imelengwa kunifumua fuvu la kichwa ilinipiga begeni karibu na shingo,” alikaririwa Lissu.

Mwanasiasa huyo ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu wa kambi ya upinzani alikakririwa akieleza zaidi kuwa kilichotokea ni ushahidi wa kile ambacho amekuwa akikizungumzia mara nyingi kuhusu uwepo wa watu waovu wanaotekeleza kampeni ovu ya kuipeleka nchi pabaya.

Wakati Lissu akikutwa na mkasa huo mbaya, historia yake ya kisiasa inaonyesha kuwa amekwishtakiwa mara sita, mwaka huu kwa makosa mbalimbali yakiwemo ya uchochezi.

Wachambuzi na wafuatiliaji wa mambo wamekuwa wakieleza kuwa shambulio hilo linaweza kuwa moja ya mikakati ya magenge ya wapinzani wa serikali waliobanwa na dola ambao sasa wanajaribu kutumia kila aina ya mbinu kuifarakanisha jamii hususan wanasiasa.

Tayari Jeshi la Polisi limekwishaanzisha uchunguzi wa tukio hilo na Inspekta Jenerali (IGP), Simon Sirro amekwitoa wito kwa mtu yeyote mwenye taarifa zinazoweza kusaidia uchunguzi huo kuzitoa kwa makachero wa polisi.

Sambamba na hilo, Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbas naye alikutana na waandishi wa habari kuzungumzia tukio hilo ambapo alitoa rai kuwa shambulio hilo lisichukuliwe kisiasa kwa sababu ni uhalifu wenye sura za ile ile ya matukio ya kihalifu ambayo yamekuwa yakitokea nchini.

Katika mkutano wake na wanahabari alioufanya siku chache baada ya Lissu kushambuliwa, Dk. Abbas alionya kuhusu upotoshaji uliokuwa ukifanywa na baadhi ya watu waliokuwa wakijaribu kuipata matope serikali kwa kuihusisha na shambulio na aliwataka wote wenye taarifa zinazoweza kusaidia uchunguzi, akiwemo Lissu kutoa ushirikiano kwa polisi.

TANESCO Wataja Chanzo cha Kukatika kwa Umeme Dar, Pwani

0
0
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limetoa taarifa kwa wateja katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kuwa baadhi ya maeneo hayana umeme kutokana na hitilafu iliyojitokeza.

Taarifa ya Tanesco imesema baadhi ya maeneo ya mikoa hiyo hayana umeme kuanzia saa 3:20 asubuhi ya leo Jumatano Novemba 29,2017 kutokana na mashine namba tatu ya kuzalisha umeme kwa njia ya gesi asilia kituo cha Ubungo II kupata hitilafu.

“Mafundi wa shirika wanaendelea na jitihada za kutatua hitilafu hiyo kwa haraka ili kurejesha umeme katika hali yake ya kawaida,” imesema taarifa ya Tanesco.

Shirika hilo limesema litaendelea kutoa taarifa za maendeleo ya kazi hiyo.

Pia, Tanesco imetoa tahadhari kwa wananchi kutosogelea, kushika wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka.

Uongozi wa shirika hilo umewaomba radhi wateja kwa usumbufu uliojitokeza.

Zitto Kabwe Apigilia Msumari Mapambano Dhidi ya Rushwa

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT Wazalendo), Zitto Kabwe amesema licha ya Serikali kuonyesha juhudi za kukabiliana na rushwa, jitihada hizo hazitakuwa endelevu endapo taasisi za uwajibikaji hazitaachwa zifanye kazi kwa uhuru na uwazi.

Akizungumza katika mjadala ulioandaliwa na taasisi ya Twaweza leo Jumatano Novemba 29,2017, Zitto amesema taasisi kama Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG); Mamlaka ya Ununuzi wa Umma (PPRA); kamati za Bunge za hesabu na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) zinapaswa kuachwa huru ili zifanye kazi kwa ufanisi.

Mjadala huo umelenga kuangalia ni namna gani ufa uliopo kati ya nia ya Serikali ya kupambana na rushwa kwa uwazi dhidi ya utamaduni wa usiri na porojo za kisiasa zinazoonekana kushamiri serikalini.

Zitto amesema kuendelea kuingiliwa kwa taasisi hizo kunasababisha mambo kufanyika ndivyo sivyo.

Ametoa mfano wa ujenzi wa uwanja wa ndege wa Chato akisema haieleweki mradi huo umeendeshwaje.

"Hatukatai Chato kuwa na uwanja wa ndege kwa sababu ni sehemu ya Tanzania; kinachoibua maswali ni namna mradi ulivyotekelezwa,” amesema.

Zitto amesema, "Hakukuwa na bajeti, zabuni hazikuwekwa wazi; aliyeshinda haijulikani ameshindaje na tunasikia hajawahi kujenga uwanja wowote."

Amesema taasisi za Serikali ikiwemo ofisi ya CAG na PPRA zilitakiwa zitoe taarifa ya kina kuhusu ujenzi huo.

Akizungumza katika mjadala huo, mwanzilishi wa mtandao wa JamiiForums, Maxence Mello amesema kuna haja ya Serikali kuongeza uwazi katika uendeshaji wa shughuli zake.

"Kuendelea kuweka mambo siri kunawafanya watu waibue vitu vingine ambavyo vingezuilika endapo wangekuwa wanafahamu kinachoendelea," amesema.

Mello amesema, "Kuficha mambo haisaidii na itasababisha Serikali iliyopo ikiondoka madarakani nyingine itakayochukua hatamu itaibua mambo ya ajabu."

Waziri Mkuu Abaini Semi Trela 44 Zikitaka Kutolewa Bandarini Bila Yakufuata Utaratibu....Amtaka IGP Sirro Awakamate Wahusika

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemtaka Inspekta Jenerali wa Polisi, Simon Sirro kuwakamata, Bw. Bahman wa kampuni ya NAS na Wakala wa Kampuni ya Wallmark Bw. Samwel kwa kutaka kutoa bandarini magari makubwa aina ya semi tela 44 bila ya kulipa kodi kwa kutumia jina la Waziri Mkuu.

Pia Waziri Mkuu ameitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na kutowasikiliza wafanyabiashara wanaotaka kukwepa kodi kwa madai ya kupewa vibali vya msamaha wa kodi kutoka kwa viongozi wa juu Serikalini.

“Mtu asije hapa aseme amepewa kibali na Rais Dkt. John Magufuli, Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan au Waziri Mkuu cha kutaka kutoa mzigo wake bila ya kufuata taratibu. Akija mtu na taarifa hizo akamatwe mara moja na achukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.”

Ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Novemba 29, 2017) alipofanya ziara ya ghafla bandarini baada ya kupata taarifa za mfanyabiashara huyo aliyetaka kuutapeli uongozi wa TPA kutaka kutoa magari hayo yaliyoingizwa nchini mwaka 2015 kutoka nchini Uturuki.

Hatua hiyo imekuja baada ya Bw. Bahman wa kampuni ya NAS kutaka kupata msamaha wa  kodi kwa kuidanganya TPA kwa madai kwamba wamewasiliana na Waziri Mkuu na wasipotekeleza jambo hilo watapata matatizo.

Amesema Serikali inasisitiza watu kufuata sheria na taratibu za nchi ikiwa ni pamoja na kulipakodi  ipasavyo na inataka watendaji wake wafanye kazi bila ya kubugudhiwa, hivyo amewataka wafanyabiashara kufuata sharia za nchi na kwamba Serikali haina ugomvi nao.

Waziri Mkuu amefafanua kuwa mfanyabiashara huyo alitaka kuyatoa magari hayo bila ya kukamilisha malipo ya ununuzi kutoka kwenye kampuni Serin ya nchini Uturuki.

“Magari haya aliyalipia asilimia 30 tu kwa makubaliano ya kumaliza asilimia 70 iliyobaki baada ya kufika Tanzania na atakapokamilisha ndipo angepewa nyaraka ambayo inaonyesha jina la mwenye mzigo, aina ya mzigo na thamani  (bill of lading) inasaidia mteja kufanyiwa tathmini ya gharama za kulipia ushuru, lakin huyu bwana hajafanya hivyo”

Waziri Mkuu amesema kitendo cha kuyasajili magari hayo bila ya kuwa na nyaraka hizo ni kinyume cha sheria na pia kinaweza kusababisha kampuni iliyouza magari hayo ya Serin kutolipwa malipo yaliyobaki. 

Amesema jambo hilo halikubaliki kwa sababu linaweza kudhohofisha mahusiano mazuri iliyopo kati ya Tanzania na Uturuki kwani tayari kampuni hiyo imeshawasilisha malalamiko hayo katika ofisi za Ubalozi wa Uturuki nchini Tanzania.

“Uturuki wanawaamini sana wafanyabiashara wa Tanzania sasa huu ujanjaunja uliotumika katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kuyasajili magari haya bila ya kuwa na bill of lading halisi unajenga sura mbaya kwa wafanyabiashara wengine waaminifu na watiifu wa sheria nawaagiza TRA kuchukua hatua kwa wahusika, hatuwezi kupoteza mahusiano na nchi kwa sababu ya utapeli wa mfanyabiashara mmoja.”

Pia Waziri Mkuu ametoa wito kwa Mawakala wa Forodha kuhakikisha wanakuwa makini katika kazi zao na Serikali haitawavumilia wababaishaji kwani inasisitiza wafanyabiashara kulipa kodi kwa mujibu wa sheria na si vinginevyo.

Awali, Mkurugenzi wa Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko alimueleza Waziri Mkuu kuwa pamoja na vitisho vya mfanyabiashara huyo kuwa wasipotekeleza matakwa yake watapata matatizo, lakini waliendelea kusimamia sheria na taratibu.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMATANO, NOVEMBA 29, 2017

IGP Sirro Asema mtandao Wa Kiuhalifu Kibiti Umesambaratishwa Kwa Kiasi Kikubwa....Ataka Watoto 13000 Wapatikane Haraka

0
0
MKUU wa jeshi la polisi nchini (IGP)Simon Sirro amewahakikishia wananchi mkoani Pwani kuwa silaha zote zilizochukuliwa na wahalifu wa ovyo ovyo huko Kibiti na Mkuranga zimerudi zote mkononi mwa dola na kusambaratisha mtandao wa kiuhalifu .

Aidha ametoa rai kwa wazazi na walimu kutoa taarifa kwenye vituo vya polisi mara watakapobaini kuna mwanafunzi mtoro ama hajaripoti shule kwa miezi kadhaa kwani wapo baadhi ya watoto wanaotumika kufundishwa uhalifu hata wakutumia silaha na watu wasiowema.
 
Pamoja na hayo IGP Sirro ,amesema vyombo vya ulinzi na usalama nchini vinashirikiana na nchi ya Msumbiji kupambana na wahalifu waliobainika kukimbilia nchini  humo wakitokea Tanzania.
 
Aliyasema hayo wilayani Kibaha ,mkoani Pwani ,katika ziara yake ya kikazi ya siku moja ambapo pia alizungumza na viongozi wa mashirika ya umma,wazee maarufu ,wastaafu mbalimbali na kamati ya ulinzi na usalama mkoani hapo.
 
IGP Sirro alieleza kuwa ,vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kupambana na yeyote atakaekuja kwa moto nae wataenda nae kwa moto na atakaekuja baridi wataenda nae baridi.
 
Alisema serikali imeshinda kwa hilo na hali kwa sasa ni shwari katika wilaya hizo.
 
IGP Sirro alieleza amepatiwa taarifa ya wanafunzi zaidi ya 1,300 mkoani hapo kuwa ni watoro na hawajulikani walipo hivyo wazazi washirikiane kusaidia jeshi la polisi kujua walipo.
 
“Kuna baadhi misikiti,makanisa yanadaiwa yanayotumia watoto hawa katika masuala ya kiuhalifu hivyo kuna kila sababu ya kuingia ndani kutafuta suluhu “
 
“Ni kazi yetu wazazi jamii na walimu kushirikiana ,na hapa ni muhimu wazazi wasaidie kusema watoto wao walipo ili kuwa na usalama” alisema .
 
Katika hatua nyingine IGP Sirro alielezea viongozi wa dini wana nafasi ya kuhakikisha wanatumia eneo lao kuhubiri amani .
 
“Tusidharau taarifa hata kama ni ndogo ,tusibweteke umoja ni nguvu tusaidiane kukomesha vitendo vya uvunjifu wa amani ” alifafanua IGP Sirro.
 
Akizungumzia changamoto ya wahamiaji haramu alisema wanashirikiana na uhamiaji kuusaka mtandao unaohusika kufanya biashara ya kusafirisha wahamiaji haramu .
 
IGP Sirro alisema hawatamvumilia yeyote anaekumbatia wahamiaji haramu kwani ni chanzo cha kusababisha kuleta magaidi  na kusafirisha bidhaa za haramu .
 
Alisema kwasasa wamejipanga kutaifisha mali za wafanyabiashara hao wa wahamiaji haramu na usafiri utaotumika kuwasafirisha.
 
Nae mkuu Wa Mkoa Wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo ,ameshukuru kuwepo Kwa kanda maalum kwani imeweza kuleta mafanikio makubwa .
 
Alisema kipindi cha nyuma kulikuwa na hali ya sintofahamu ,watu walisitiza shughuli zao za maendeleo ,biashara zilikwama,watu na baadhi ya viongozi walihama nyumba zao na wengine kulala saa 12 jioni kwa kuhofia mauaji.
 
Mhandisi Ndikilo alieleza sasa Kibiti na Rufiji hali ni shwarii kutokana na kuimarishwa ulinzi.
 
Aliwataka pia wawekezaji na wadau mbalimbali mkoani Pwani ,kujitokeza kushirikiana kusaidia kutatua changamoto zinazolikabili jeshi la polisi ikiwemo uhaba wa vitendea kazi ,usafiri na kujenga vituo vya polisi .
 
Mhandisi Ndikilo, alisema kuwa Mkoa huo umesheheni viwanda vya kutosha hivyo ni vyema kusaidia mambo hayo kwa manufaa ya wote wakati kukitokea uhalifu.
 
“Tukikumbwa na uhalifu tunapigia simu polisi, tusiwe Wa kwanza kulaumu wakati wa matatizo ,tukumbuke na kuwasaidia ili kufanikisha kazi zao kifanisi.;:” alisema mkuu huyo wa mkoa .
 
Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoani Pwani ,(ACP)Jonathan Shanna alisema ziara hiyo ni neema kwao na wamepewa maagizo mbalimbali ambayo watayafanyia kazi.
 
Kamanda Shanna alisema wamemfikishia kero IGP zinazowagusa askari polisi ikiwemo upungufu wa makazi .

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Novemba 30

Taarifa kutoka Ofisi ya Bunge kuhusu Wabunge wa CUF wanaodai kurudishiwa ubunge wao

0
0
Ofisi ya Bunge imesema hakuna sehemu katika uamuzi wa Mahakama Kuu dhidi ya wabunge wanane wa viti maalumu CUF waliofukuzwa uanachama na chama hicho inayosema  wanatakiwa kurudishwa bungeni.

Uamuzi wa Mahakama Kuu ulitolewa Novemba 10,2017 katika Kanda ya Dar es Salaam umeizuia CUF kujadili na kuwafukuza uanachama wabunge hao na madiwani wawili wa viti maalumu.

Hata hivyo, Mahakama ilitoa uamuzi huo huku tayari chama hicho kikiwa kimeshawavua uanachama na baadaye kupoteza nafasi zao za ubunge.

Wabunge hao ni Miza Bakari Haji, Saverina Mwijage, Salma Mwasa, Raisa Mussa, Riziki Mngwali, Hadija Salum Al-Qassmy, Saumu Sakala na  Halima Mohamed.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 30,2017, Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai amesema shauri lililofunguliwa ni kupinga uamuzi wa CUF kuwafukuza uanachama na kwa mujibu wa kumbukumbu za Mahakama bado uamuzi wa mwisho haujatolewa.

"Uamuzi uliotolewa na Mahakama ni wa awali kuhusu pingamizi na uliwalenga walalamikiwa ambao ni baraza la wadhamini wa CUF na uongozi wake ambao uliamuru walalamikiwa wasitishe utekelezaji wa uamuzi wa kuwafukuza uanachama na vilevile, kutojadili suala lolote kuhusu uanachama  wa walalamikaji hao hadi Mahakama itakapokamilisha shauri la msingi," amesema.

Amesema ifahamike vyema kuwa hakuna sehemu yoyote katika uamuzi huo wa Mahakama inapoelekezwa wabunge hao wanatakiwa kurudishiwa ubunge.

Kagaigai amesema kumekuwapo tafsiri isiyo sahihi ya uamuzi huo wa Mahakama inayotolewa na baadhi ya watu na vyombo vya habari ikiwemo mitandao ya jamii kusambaza taarifa potofu kuwa wabunge hao wamerejeshwa bungeni kwa uamuzi huo wa Mahakama  baada ya kurejeshewa uanachama wa CUF.

Amesema wabunge hao waliiandikia ofisi ya Bunge barua wakiomba kufahamishwa utaratibu utakaotumika kuwarejesha bungeni.

"Tunapenda umma uelewe kwamba, nafasi za ubunge zilizoachwa wazi baada wabunge husika kufukuzwa uanachama zilijazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa mujibu wa sheria na wabunge waliopatikana kujaza nafasi hizo wanaendelea kutekeleza majukumu yao ya kibunge ipasavyo," amesema.

Rais wa Nigeria atoa neno kuhusu soko la watumwa Libya

0
0
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ameingilia kati suala ambalo sasa limeigusa dunia nzima kwa kitendo cha raia wa Libya kuwauza kama watumwa wahamiaji wanaoingia nchini humo.

Kwenye ukurasa wake wa twitter Rais Buhari amesema vitendo hivyo havikubaliki, na kwamba wako tayari kufanya lolote kuwalinda raia wake ambao pia ni miongoni mwa wahanga wa biashara hiyo, yenye ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

“Hali ya Libya ya watu kuuzwa ni ya kutisha na haikubaliki, tutafanya kila kitu kuwalinda raia wetu popote walipo, na pia tumeshaanza kuwarudisha nyumbani wanigeria wote waliopo Libya na sehemu nyingine, tutahakikisha wote wanarejea nyumbani salama na kuhudumiwa”, ameandika Rais Buhari.

Kitendo cha raia wa Libya kuwauza wahamiaji wanaoingia nchini humo ambao wengi wao ni raia wa mataifa ya Afrika Magharibi, kimeishtua dunia nzima ambapo mpaka watu maarufu mbali mbali duniani, wamekuwa wakipost kwenye mitandao ya kijamii kukemea vitendo hivyo.


Zitto Kabwe Akerwa na Biashara ya Watumwa Inayoendelea Libya.....Aitaka Tanzania isiingie Uwanjani dhidi ya Libya Jumapili

0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Kabwe ameitaka timu ya taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) kutoshuka dimbani kuikabili Libya siku ya Jumapili katika michuano ya CECAFA ikiwa ni hatua ya kuonyesha kuchukizwa na vitendo vya biashara ya utumwa vinavyoendelea katika nchi hiyo.

Zitto ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Twitter ikiwa zimesalia siku chache  kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania Bara kucheza mchezo wake wa kwanza siku ya Jumapili ya Desemba 3 dhidi ya Libya katika michuano ya Afrika Mashariki na Kati inayofanyika huko nchini Kenya.

    Leo @masoudkipanya ameshauri Tanzania isusie mechi yake dhidi ya Libya siku ya Jumapili kuonyesha kuchukizwa na Biashara ya Utumwa. Ninaunga mkono. Tanzania isiingie Uwanjani kucheza na Libya. @SADC_News iagize nchi zake zote zirudishe mabalozi wake kutoka Libya.

Kilimanjaro Stars itacheza mchezo huo wa kundi A, katika kuwania kombe la michuano ya Afrika Mashariki na Kati CECAFA ambayo inatarajiwa kuchezwa nchini Kenya kuanzia Desembe 3 hadi 17 mwaka huu.

Mataifa 10 yanatarajiwa kushiriki katika michuano hiyo mikubwa kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki huku droo ya hatua ya makundi ikionyesha mwenyeji Kenya itacheza mchezo wa ufunguzi dhidi ya Rwanda huku Tanzania ikiikabili Libya siku hiyo.

Mbunge wa CUF Ashinda Pingamizi la Serikali Mahakamani

0
0
Mbunge wa Malindi (CUF), Ally Saleh ameruka kihunzi cha Serikali mahakamani, baada ya kushinda pingamizi la awali lililowekwa na Serikali katika kesi ya kuhoji uhalali wa wajumbe wapya wa bodi ya wadhamini wa chama hicho.

Saleh ambaye pia ni mwanasheria amefungua kesi Mahakama Kuu akihoji uhalali wa wajumbe wapya wa bodi waliosajiliwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita).

CUF imegawanyika pande mbili; inayomuunga mkono Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad na inayomuunga  Mwenyekiti, Profesa Ibrahim Lipumba anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, ambaye ndiye aliunda bodi inayopingwa.

Wadaiwa katika kesi hiyo ni Ofisa Mtendaji wa Rita, anayewakilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kupitia jopo la mawakili wa Serikali linaloongozwa na Gabriel Malata.

Wengine ni bodi ya wadhamini (mpya) ya CUF, mwenyekiti wa bodi hiyo, Peter Malebo, wanaowakilishwa na wakili Majura Magafu na wajumbe wapya wa  bodi hiyo wanaowakilishwa na wakili Mashaka Ngole.

Wadaiwa wengine ni wajumbe wa bodi waliomaliza muda wao na ambao wengine walipendekezwa tena na upande wa Maalim Seif ambao hata hivyo hawakuidhinishwa na Rita, wanaowakilishwa na mawakili Juma Nassoro, Daimu Halfan na Hashim Mziray.

Serikali kwa niaba ya mdaiwa wa kwanza (Mtendaji wa Rita), iliweka pingamizi la awali ikiiomba Mahakama iitupilie mbali kesi, ikitoa hoja kuwa imefunguliwa kabla ya wakati bila kufuata utaratibu wa kuishtaki Serikali na kwamba mdai amemshtaki mtu asiyestahili.

Saleh anayewakilishwa na mawakili Mpale Mpoki na Fatma Karume, ameshinda pingamizi hilo katika uamuzi uliotolewa na Jaji Wilfred Dyansobera alioutoa jana Jumatano, Novemba 29,2017.

Jaji Dyansobera ametupilia mbali pingamizi hilo la Serikali baada ya kuridhika kuwa hoja za pingamizi hilo hazikuwa na mashiko.

Wakati wa usikilizwaji wa pingamizi hilo, wakili Malata alidai mdai amemshtaki mtu asiye sahihi; akidai Rita ni wakala ndani ya ofisi ya Kabidhi Wasihi Mkuu ambaye ndiye aliyestahili kushtakiwa na si mtendaji wa Rita.

Pia, alidai kesi ilifunguliwa kabla ya wakati kwa kuwa ilifunguliwa kabla ya kutoa taarifa ya kusudio kwa Serikali ya siku 90, kama inavyoelekezwa katika sheria ya mashauri dhidi ya Serikali.

Wakili Mpoki alipinga hoja hizo akidai mtu waliyemshtaki ni sahihi na kwamba, kwa aina ya kesi hiyo hapakuwa na haja ya kutoa taarifa ya siku 90 kwa Serikali kwa kuwa hawaishtaki Serikali.

Jaji Dyansobera katika uamuzi wake amekubali hoja za upande wa mdai, kuwa suala la nani ashtakiwe na nani asishtakiwe ni jukumu la mdai kwa kuwa ndiye anaona kuwa nafuu anazoziomba atazipata kwa nani.

Amesema kesi hiyo haikuhitaji kutoa taarifa ya siku 90 kwa Serikali kwa kuwa si Serikali inayoshtakiwa bali kesi hiyo inahusu mgogoro wa ndani ya chama cha siasa, ambako Serikali haipaswi kujiingiza wala kuwa na upande.

Jaji Dyansobera amepanga kuendelea na usikilizwaji wa kesi hiyo Desemba 8,2017 kwa kusikiliza hoja za msingi za mbunge Saleh na majibu ya wadaiwa na kisha atapanga tarehe ya kutoa uamuzi.

Waziri Mkuu aruhusu kozi za 'Foundation' Chuo Kikuu Huria

0
0
Chuo Kikuu Huria pekee kimepewa ruhusa ya kuendelea kutoa kozi ya Foundation iliyokuwa imesitishwa na serikali kwa wanafunzi ambao wamekosa vigezo vya kujiunga na elimu ya Chuo Kikuu baada ya mtaala wake kuboreshwa na kupitishwa na Wizara ya Elimu.

Ruhusa hiyo imetolewa na Waziri Mkuu, Mh. Kassim Majaliwa leo akiwa mkoani Singida yanapofanyika Mahafali ya chuo hicho.

Ikumbukwe kuwa Mwaka 2016 Naibu Waziri wa Elimu, Mhandisi Stella Manyanya alitoa katazo hilo na kusema utaratibu wa kozi ya Foundation umefanywa na  vyuo  vyenyewe hivyo serikali haiwezi kuukubali mfumo wa  elimu hiyo na kwamba kama mtu anasoma kozi ya Foundation apewe cheti na kama atahitaji  kujiendeleza asafishe cheti au asome mfumo ambao utamfikisha katika shahada.

Mbali na hayo katika Mahafali hayo ambayo Waziri Mkuu ndiye Mgeni rasmi atamtunuuku mkewe Bi Mery Shahada ya Uzamiri ya Elimu.

"Wakati najiandaa kuja kwenye sherehe mwenzangu naye kumbe anajiandaa,  nashukuru amemaliza sasa mambo nahisi yataenda vizuri maana wakati mambo ya masomo yalipokuwa busy hata tulikuwa hatuonani...Leo pia naona familia yangu nayo itakuwa inasherehekea" Majaliwa

Pamoja na hayo Waziri Mkuu amejipigia debe sherehe ya mahafali yajayo yakafanyike mkoani Lindi pia kwani wamejiandaa vyema

Alikiba awapa zawadi mashabiki Kwa Kuachia Video Mpya.....Itazame Hapa

0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Seduce me' Alikiba ameamua kuachia video ya wimbo wake wa zamani ambao ulivuja kama zawadi kwa mashabiki wake katika siku yake ya kuzaliwa.

Alikiba ambaye jana alikuwa anasherehekea kumbukumbu ya mwaka wa kuzaliwa aliamua kuachia video ya wimbo wa 'Maumivu Per Day' kama njia ya kusherekea siku hiyo na mashabiki zake.

"Nashukuru sana watu ambao wamenitakia kheri katika siku yangu ya kuzaliwa, nimejaliwa, kupendelewa na kupendwa pia nashukuru sana kwa jambo hilo, nawapenda wote na nitafanya kazi kwa nguvu zote kuwafanya mjivunie uwepo wangu. 

"Maumivu Per Day ni kati ya nyimbo zangu za zamani zinazopendwa nimeamua kuitoa japo siyo rasmi ili kusherehekea kumbukumbu ya siku yangu ya kuzaliwa na mashabiki zangu" alisema Alikiba

Wema Sepetu achoshwa....Atamani Kifo

0
0
Muigizaji mwenye nyota yake bongo na Afrika Mashariki Wema Sepetu, amesema kuna muda anatamani Mungu amchukue afe ili aweze kupumzika na mambo ya dunia ambayo yanamnyima raha.

Wema Sepetu ameyasema hayo kwa kuandika ujumbe kwenye ukurasa wake wa instagram, akisema ingawa anajua ipo siku atakufa, lakini anatamani ingetokea sasa ili aweze kupumzika na mambo yanayomuumiza nafsi yake ikiwemo kutukanwa bila sababu za msingi kwenye mitandao ya kijamii.

Wema Sepetu amendeelea kusema kuwa kutokana na mambo ambayo anayapitia anatamani hata asingetokea duniani, na kuamua kukaa nje ya mitandao ya kijamii kwa muda.

"Ipo siku nitakufa, hakuna anaeishi milele... Sijui mtaendelea kunisema kwa kejeli na kunitukana matusi ya nguoni au ndo itakuwa, “Maskini ya Mungu, Dada wa watu alikuwa hivi na vile, Mungu ailaze Roho yake mahali pema...” Kuna muda mwingine huwa natamani Allah Subhannah wata’allah anichukue tu... Ya Duniya ni mengi sana", ameandika Wema Sepetu.

Wema ameendelea kuandika akisema.." Kuna muda mwingine nakufuru mwenyezi Mungu na kutamani labda hata nisinge exist... Ila acha niendelee kumtegemea yeye... Kila jambo hutokea kwa sababu.... Hili nalo litapita... I think I need a Time Off Social Media... Kwa mara nyingine Tena.... Siwezi jamani".

Licha ya hayo Wema Sepetu hajaweka wazi moja kwa moja ni jambo gani ambalo limemkwaza zaidi, kwani kitendo cha kutukanwa na kusemwa vibaya kwake sio jambo geni. 

Rais Magufuli Ateua Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amteua Bi. Stella Tullo Chagi kuwa Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba wa Wilaya.

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Eng. John Kijazi ametangaza kuwa uteuzi huo Bi. Stella Tullo umeanza rasmi toka Novemba 25, 2017. 

Wabunge CHADEMA Wanyimwa Dhamana na Kupelekwa Mahabusu

0
0
 Wabunge wawili wa Mkoa wa Morogoro kupitia Chadema pamoja na washtakia wengine 34 wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro kujibu mashtaka nane yanayowakabili likiwemo la kuchoma moto ofisi ya Kata ya Sofi iliyopo wilayani Malinyi.

Wabunge hao ni Susan Kiwanga(Mlimba) na Peter Lijualikali(Kilombero) na baada ya kusomewa mashataka hayo upande wa mashtaka uliwasilisha mahakamani hapo hati ya kiapo cha kupinga dhamana yao kwa madai kuwa wataharibu upelelezi wa kesi hiyo.

Kesi hiyo ya jinai namba 296 iliyovuta hisia za wakazi wengi wa manispaa ya Morogoro ilisomwa mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Ivan Msack ambapo upande wa mashtaka ulikuwa ukiongozwa na wakili wa Serikali, Edga Bantulaki na Sunday Hyera huku washtakiwa hao wakitetewa na wakili Bartalomew Tarimo.

Akisoma mashtaka hayo leo Alhamisi huku ulinzi mkali ukiwa umeimarishwa ndani na nje ya mahakama Wakili Bantulaki alidai kuwa washtakiwa hao kwa pamoja walitenda makosa hayo Novemba 26 mwaka huu katika Kata ya Sofi wilayani Malinyi.

Alidai kuwa bila uhalali huku wakijua kufanya hivyo ni kosa washtakiwa hao walikula njama na kuchoma moto ofisi ya kata hiyo sambamba na kufanya uharibifu wa mali mbalimbali za ofisi hiyo.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo washtakiwa wote walikana kuhusika na hivyo mahakama kuaihisha kesi hiyo hadi Desemba 5 mwaka huu kwa ajili ya kutolewa maamuzi ya dhamana.

Kabla ya kufikishwa mahakamani hapo Lijualikali alijisalimisha katika kituo cha polisi Morogoro majira ya saa nne asubuhi baada ya jeshi la polisi kutangaza kumtafuta.

Waziri Mkuu Ataka Udahili Elimu Ya Juu Uongezwe....Ashuhudia Mkewe Akitunikiwa Shahada Ya Uzamili OUT

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema uchumi wa kati na wa viwanda hauwezi kufikiwa au kuwa endelevu pasipo kuwa na kiwango cha udahili katika elimu ya juu cha angalau asilimia 23.

“Hivi sasa, kiwango cha Tanzania cha udahili katika elimu ya juu ni asilimia nne. Kiwango hiki ni kidogo hata kuliko nchi kama Jamhuri ya Kidemorasia ya Kongo, ambao licha ya hali ya vita nchini mwao kwa muda mrefu, wamefikia asilimia saba,” amesema.

Ametoa kauli hiyo leo mchana (Alhamisi, Novemba 30, 2017) wakati akiwahutubia mamia ya wakazi wa mji wa Singida na mikoa jirani waliohudhuria mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) yaliyofanyika kwenye viwanja vya Kanisa Katoliki mjini Singida,

Waziri Mkuu amesema takwimu zinaonyesha kwamba karibu nchi zote washirika katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, ukiacha Burundi, zina viwango vya juu zaidi vya udahili katika elimu ya juu na kwa maana hiyo zimeizidi Tanzania.

Amesema, Chuo Kikuu pekee chenye kanuni za udahili (open entry), chenye kufundisha, kujisomea na hata kutathmini maendeleo ya wanafunzi (assessment on demand) ni Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

“Naungana na Mheshimiwa Rais kuwaomba mtumie fursa hiyo, kuisaidia nchi yetu kuongeza kiwango cha udahili wa wananchi wake katika elimu ya juu, kwa haraka na kasi itakayotuwezesha kufikia lengo la kuwa nchi ya uchumi wa kati na wa viwanda, ifikapo 2025.”

“Kwa kushirikiana na Baraza la Elimu Masafa Afrika (African Council for Distance Education (ACDE), Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Baraza la Elimu ya Ufundi (NACTE) na hata vyuo vikuu vingine ndani na nje ya nchi yetu, ongezeni ubora na panueni wigo wa udahili, kwenye programu za sasa na zingine mtakazoziongeza,” alisisitiza.

Aliwataka wahakikishe kuwa siku zote, mfumo wao wa utoaji elimu, yaani elimu huria na masafa (Open and Distance Learning (ODL) unajitanabaisha kama mfumo wa kisasa na mahiri katika kutoa elimu na mafunzo yenye ubora unaokubalika na kutambulika kitaifa, kikanda na kimataifa.

“Kwa kuzingatia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendelelo na mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Tano, napenda nisisitize kuwa dira ya utendaji wenu, ijikite katika maeneo yaliyoainishwa, chini ya mwanvuli wa kaulimbiu ya Chuo “elimu bora na nafuu kwa wote.”

Waziri Mkuu amesema katika kutambua umuhimu wa elimu huria na masafa kwa maendeleo ya elimu hapa nchini, Serikali inaunga mkono azma ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ya kuanzisha dawati maalumu kwa ajili ya kuimarisha Mfumo wa Elimu Huria na Masafa.

“Kupitia hafla hii, ninaagiza dawati kama hilo lianzishwe pia katika Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) na Baraza la Elimu ya Ufundi (NACTE) kwa lengo la kuhakikisha kuwa taratibu zao za ithibati zinazingatia na kukidhi matakwa ya viwango vya mfumo wa Elimu Huria na Masafa,” alisema Waziri Mkuu.

“Ninaungana na Waziri mwenye dhamana kuagiza kuwa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) washirikiane na TCU na NACTE kuhakikisha kuwa taratibu za ithibati zinatekeleza azma ya Serikali kama ilivyoainishwa kwenye Sera ya Elimu ya Mafunzo 2014, hususan juu ya suala la kuwatambua watu waliopata ujuzi bila kupitia mfumo (rasmi) wa elimu na mafunzo,” alisisitiza.

Waziri Mkuu pia alishuhudia mke wake, Mary Majaliwa akitunukiwa Shahada ya Uzamili katika Elimu ya Utawala, Mipango na Sera (Masters’ of Education in Administration, Planning and Policy Studies) na Mkuu wa Chuo hicho ambaye pia ni Waziri Mstaafu, Mizengo P. Pinda.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Finland Yaipiga Jeki Tanzania Shiingi Bilioni 75 Kuendeleza Ubunifu, Misitu Na Uongozi Bora

0
0
Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
Serikali ya Tanzania na Finland zimetiliana saini mikataba mitatu yenye thamani ya Euro milioni 28.8 sawa na Shilingi bilioni 75 kwa ajili ya kuendeleza misitu, ubunifu na masuala ya uongozi.

Akizungumza wakati wa utiaji saini wa mikataba hiyo, Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James amesema, msaada huo kutoka Finland umetolewa ili kuendeleza  uwezo wa viongozi na kufanya maamuzi sahihi yenye tija kwa ukuaji wa uchumi wa Taifa, mradi ambao unasimamiwa na Taasisi ya Uongozi, ambapo kiasi cha Euro milioni 9.90 zimetolewa kuendeleza mradi huo.

Aidha Serikali ya Finland imetoa kiasi cha Euro milioni 8.95 kwa mradi wa  kuiimarisha mfumo wa ubunifu nchini kwa kutengeneza mazingira rafiki kwa wabunifu ili kuweza kubuni na kuendeleza ubunifu wao na kuchochea ukuaji wa viwanda.

Bw. James alisema fedha hizo zitatumika kuwasaidia wabunifu kwa kuwapatia vifaa na msaada wa kitaalamu ili kuyaendeleza mawazo yao na kuyafanya yawe ya kibiashara na kuweza kusaidia kubadili mawazo hayo kuwa viwanda.

“Fedha hizi zitasaidia kutatua changamoto katika viwanda vilivyopo nchini ili vifanye kazi kwa ufanisi kwa kuwaunganisha wanataaluma mbalimbali nchini, ikiwa ni pamoja na wabunifu wachanga, wataalamu kutoka vyuoni, wataalamu kutoka Serikalini na Sekta binafsi” Alisema Bw. Doto James

Eneo lingine lililonufaika na msaada huo ni programu ya misitu, ambayo imepatiwa Euro milioni 9.95 kwa lengo la utuzaji wa misitu na uongezaji thamani ya mazao yatokanayo na misitu ili kuongeza kipato kwa Wananchi, kupunguza umasikini na kulinda mazingira.

Katibu Mkuu amemshukuru balozi wa Finland Nchini, Mhe. Pekka Hukka kwa msaada walioutoa na kwa kuunga mkono shughuli za maendeleo za Serikali, na kuongeza kuwa Finland wamekuwa wakifadhili miradi mbalimbali nchini, ukiwemo mradi wa kilimo biashara Mkoani Lindi na Mtwara (LIMAS), uliogharimu Euro milioni 9, Mradi wa kuimarisha usambazaji na upatikanaji wa umeme wa uhakika Jijini Dar es Salaam, uliogharimu Euro milioni 25, na Programu ya maboresho ya Serikali za Mitaa, Euro milioni 10.5

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja aliiishukuru Serikali ya Finland kwa kuendelea kuisaidia Taasisi hiyo.

‘Hii ni mara ya tatu Finland wamekuwa wakitusaidia kuendeleza jitihada zilizoanzishwa na Serikali yetu ambapo awamu ya kwanza ilikuwa ni mwaka 2012 ambapo walitupatia Euro milioni 7, mwaka 2014 Euro milioni 12 na sasa wametupatia Euro milioni 9.90 huu ni msaada mkubwa’ alisema Profesa Semboja.

Aidha kwa upande wake Balozi wa Finland Bw. Pekka Hukka, aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuendeleza ushirikiano na Serikali yake, na kuongeza kuwa msaada huo ni muhimu sana katika kutimiza malengo ya maendeleo ya nchi.

Amesema msaada huo ukitumika ipasavyo hasa katika kuendeleza mnyororo wa thamani wa mazao ya misitu utasadia kuongeza ajira na kuongeza pato la Taifa.

Ameitaka Serikali kupitia Wizara ya nishati,  kushirikiana na sekta binafsi na kuitumia fursa hiyo ya kuboresha misitu ili kuiongezea nchi mapato zaidi yatakayotokana na makusanyo ya kodi.

Waziri Mbarawa Atoa Maagizo Mazito Bodi na Menejimenti ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)

0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, amesema anasikitishwa na utendaji wa Bodi na Menejimenti ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kutofanya maamuzi kwa wakati hali ambayo inachangia malalamiko kuongezeka Bandarini hapo.

Aidha, Mbarawa amesema Serikali inapeleka Naibu Mtendaji Mkuu mpya wa shughuli za Uendeshaji Bandarini hapo kutokana na aliyekuwepo kushindwa kusimamia majukumu yake ipasavyo.

Profesa Mbarawa amesema hayo leo wakati wa ziara ya kushtukiza aliyoifanya bandarini ikiwa ni siku chache baada ya Rais John Magufuli, na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, kufanya ziara ya kustukiza na kubaini madudu bandarini hapo.

Ziara ya Waziri Mbarawa ni mwendelezo wa ziara mbalimbali bandarini hapo  kubaini uendeshaji na utendaji wa shughuli zinazotolewa na Mamlaka hiyo.

“Nimelazimika leo kuwaita Watendaji na Bodi ya TPA ili kuwaeleza kasoro zenu  ambapo inaonesha wazi kuwa  asilimia kubwa ya mambo yanayotokea humu  ni  kuwa mnakuwa wazito katika kutoa  maamuzi”, amesema Profesa Mbarawa.

Amesema katika bandari hiyo ipo mizigo ya kahawa ambayo imefika bandarini tangu mwaka 2014 huku kukiwa hakuna sababu za kueleweka za wenye mali kutochukuwa mizigo yao.

Profesa Mbarawa amesema hahitaji wasaidizi ambao wanakaa katika vikao na kulipana posho ila wanapaswa kufanya kazi ya kuangalia shughuli zote za bandari.

“Kama hamtabadilika nitaendelea kuja katika bandari hii ili kuchukua hatua pale ambapo inaonekana kwani haipendezi kila kukicha malalamiko kutokea,” amesisitiza Waziri Mbarawa.

Aidha, Waziri Mbarawa ameitka bodi na menejimenti kuhakikisha kuwa inatatua changamoto iliyopo katika bandari ya kushusha na kupakia mizigo kutoka Zanzibar na kuingia Tanzania Bara ambapo wafanyabiashara wanalalamikia utaratibu unaotumika kuwahudumia.

Amesema haingii akilini kuona mizigo inayotoka au kwenda Zanzibar kutozwa kodi baada ya masaa huku inayotoka nje ya Tanzania ikitozwa baada ya siku saba.

Kuhusu ujio wa Naibu mtendaji Mkuu mpya Mbarawa aliitaka Bodi na menejimenti kumpa ushirikiano ili aweze kutoa matokeo chanya kwenye bandari.

“Tunaleta Naibu Mtendaji Mkuu mpya ambaye atasimamia operesheni, naomba apewe ushirikiano ili kusaidia Serikali huyu ambaye anakaimu tunamuondoa ameshindwa kwenda na kasi yetu,” amefafanua Profesa Mbarawa.

Akizungumza baada ya ziara hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya TPA Ignas Rugaratuka, amesema wamejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa wanaitendea haki nafasi waliyopewa kwa kusimamia mabadiliko ndani ya bandari.
 
Amesema tangu waingie wamekuwa wakipambana kuhakikisha kuwa mapungufu ya TPA yanaisha ambapo wamefanikiwa kurekebisha kwenye utawala kwa kutoa mafunzo kwa watumishi na kuzuia wizi ambao ulikuwa umekithiri.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko, amesema kuwa tangu aingie katika mamlaka hiyo wamekuwa wakifanya jitihada za kurekebisha mapungufu na kumuahidi waziri kuwa ataongeza jitihada zaidi.

“Kama ni mabadiliko tumefanya makubwa sana hasa katika utawala na uongozi ila kila anayehusika katika sekta hiyo anapaswa kutoa msaada,” amesema Mkurugenzi Mkuu.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Decemba 1

Ufafanuzi kuhusu mwekezaji aliyekwamishwa na TRA na Wizara ya Viwanda

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images