Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Zitto akubali kushindwa uchaguzi wa udiwani....Ni Baada ya Chama Chake Kuamulia Patupu

$
0
0
Kiongozi  wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, leo Jumatatu, Novemba 27, 2017 amefunguka kuwa, chama chao wameshapata matokeo ya kata zote walizoshiriki uchaguzi mdogo wa madiwani ulifanyika jana Jumapili huku akisema hawajashinda hata kata moja.

Adiha kiongozi huyo amelaani vitendo vya vurugunna fujo vilivyofanywa katika baadhi ya vituo vya kupigia kura na kusababisha taharuki miongopnmi mwa wapiga kura.

“Uchaguzi wa Madiwani Umekwisha, ACT Wazalendo, tunalaani vurugu na Kuwashukuru Watanzania. Jana tumemaliza Uchaguzi mdogo wa madiwani nchi nzima. Katika kata zote 43 nchini zilizogombewa, Sisi ACT Wazalendo tuliweka wagombea kwenye kata 17 tu.

“Tumepata matokeo ya kata zote na hakuna kata tuliyoshinda. Wapiga kura wameamua na sisi tumekubali. Tunafanya tathmini ya matokeo nchi nzima na tutazungumza na Wananchi. Tunawashukuru sana kwa kura tulizopata. Tutazienzi kwani ndio haki yetu.

“Tunajiandaa na chaguzi ndogo zinazokuja ikiwemo za Ubunge kwenye majimbo yaliyowazi. Tutatumia mafunzo tuliyoyapata kwenye chaguzi ndogo hizi kujipanga na chaguzi zinazokuja.

“Kwetu sisi Chama cha Wazalendo, Uchaguzi ulikuwa fursa ya kuzungumza na Wananchi na kufikisha ujumbe wetu kwani kuzuiwa kwa mikutano ya hadhara kunatunyima fursa hiyo. Hatutachoka kuendelea kusambaza sera zetu kwani tunaamini ni bora zaidi na zinazoweza kuleta unafuu kwa wananchi

“Mwezi mmoja huu wa kampeni, tumepita sehemu mbalimbali za nchi na kuzungumza na Wananchi, kusikiliza matumaini na changamoto zao na kuwaeleza hali ya nchi kisiasa na kiuchumi. Tumeweza kufikisha ujumbe wetu wa kampeni za mwaka huu zilizojikita kwenye masuala ya Haki na Uchumi

“Tumewaeleza namna haki za raia zinavyominywa na namna Uendeshaji mbovu wa uchumi unavyowaweka kwenye dimbwi la umasikini. Tumewaeleza namna uhuru wa mawazo unaminywa, vyama kuzuiwa kufanya mikutano kueneza sera zetu.

“Bunge kuzuiwa kuonyeshwa moja kwa moja ili Wananchi kufuatilia namna wanavyowakilishwa na magazeti kufungiwa ili kudhibiti uhuru wa Habari.

“Tumewaeleza kuhusu vitendo vya kinyama vya kushambulia wawakilishi wa Wananchi kwa lengo la kuua na kufungulia kesi wanasiasa wanaoikosoa Serikali na kutoa mawazo mbadala.

“Yote haya yanafanywa kwa lengo la mtu mmoja kudhibiti mamlaka ya nchi na kufanya ukiritimba wa Uendeshaji wa nchi yetu jambo ambalo ni hatari kwa Demokrasia yetu.” amesema Zitto Kabwe.

Hatimiliki Za Ardhi Kutolewa Ndani Ya Wiki Moja....Wenye Hati za Zamani Watatakiwa Kuzibadili

$
0
0
Serikali itaanza kutoa hatimiliki za viwanja kati ya siku moja na siku saba kwa kutumia mfumo wa kielektroniki ifikapo Juni 1, 2018.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendelo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi wakati wa ziara ya kutembelea ofisi za Mfumo Unganishi wa Taarifa za Ardhi.

“Tunataka kupunguza urasimu na kuongeza ufanisi katika kutoa hati kutoka ilivyo sasa ambapo hati hutolewa kati ya mwezi mmoja hadi miezi mitatu”, alisema Lukuvi.

Ameongeza kuwa mfumo huo utaondoa udanganyifu katika kutoa hati kwa watu wawili au zaidi katika kiwanja kimoja na kuondoa migogoro ya viwanja ambayo imekuwa kero kwa wananchi.

Lukuvi amesema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuondoa utapeli uliokuwa ukifanyika kuhusu ardhi na ndio maana imeanzisha mfumo huo ambao ameuita muarobaini wa migogoro ya ardhi.

Aidha, Waziri Lukuvi alisema kuwa hati ya kisasa itakuwa na ukurasa mmoja badala ya zamani ambayo ilikuwa na kurasa zaidi ya ishirini.

Kwa mfumo huo, maafisa ardhi hawatatumia tena karatasi bali watakuwa na kompyuta ambamo taarifa zote zitahifadhiwa, aliongeza Lukuvi.

Lukuvi amesema kuwa mfumo utaiwezesha Serikali kuwafahamu wamiliki wote wa viwanja na kuwakumbusha muda wa kulipia viwanja vyao, hivyo mapato ya Serikali yataongezeka.

Kwa mujibu wa Waziri Lukuvi, Mfumo huo utatumika kutunza taarifa za ardhi za nchi nzima na hauwezi kuchezewa na mtu yeyote kwani kutakuwepo na nywila (password) ya kuingia kwenye mfumo ambayo itatolewa kwa maafisa wachache na hivyo kupunguza uwezekano wa kutoa hati zaidi ya moja kwa kiwanja kimoja.

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kushirikiana na wataalam kutoka Kampuni ya IGN FI wanatekeleza, uundaji, usambazaji, usimikaji na uendeshajiwa mradi wa mfumo unganishi wa taarifa za ardhi unaodhaminiwa na Benki ya Dunia.

Dhumuni la mradi huo ni kuimarisha usalama katika umiliki wa ardhi kwa kuboresha usalama na usahihi katika manunuzi ya ardhi pamoja na kuanzisha mfumo sahihi na imara wa taarifa za ardhi.

Mfumo huo utakamilika ifikapo Juni 1 mwakani (2018) na hati ya kwanza ya kielektroniki ndipo itatolewa rasmi. Na wenye hati za zamani watatakiwa kubadilisha hati zao na kupewa za kielektroniki.

Japan Yaonesha Nia Kuijenga Dodoma Kwa Miundombinu Ya Kisasa

$
0
0
Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
SHIRIKA la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) limesema liko tayari kushirikiana na Serikali kujenga miundombinu ya kisasa ya usafiri, Nishati ya umeme, maji na usafi wa mazingira katika Makao Makuu ya nchi, Dodoma.

Ahadi hiyo imetolewa na Makamu wa Rais wa Shirika hilo Bw. Hiroshi Kato wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Jijini Dar es Salaam.

Bw. Kato alisema kuwa mradi mwingine wanaotaka kuutekeleza katika mji wa Dodoma ni udhibiti wa taka ngumu na kwamba wanachosubiri ni Serikali kuainisha maeneo ya vipaumbele vilivyoko katika mpango mji wa Dodoma.

Aidha Makamu huyo wa Rais wa JICA alisema kuwa Shirika lake litaendelea kusaidia eneo la kilimo hususan kilimo cha mpunga ili kuongeza thamani ya zao hilo na kuwakomboa wakulima.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango amelishukuru Shirika hilo kwa kuonesha nia ya kusaidia ujenzi wa mji wa Dodoma ambao ndio Makao Makuu ya nchi.

Alisema kuwa mradi huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kuupanga mji wa Dodoma mapema ili kuondoa changamoto za msongamano wa huduma za jamii kwenye eneo moja kama ilivyo Jijini Dar es Salaam.

“Pamoja na umuhimu wa miundombinu ya maji, umeme, usafiri wa mjini, lakini pia tunataka tujenge mapema njia za juu (ring roads) ili kudhibiti msongamano wa magari” alisema Dkt. Mpango.

Aliongeza kuwa mradi mwingine wa kipaumbele katika mji huo ni ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa katika eneo la Msalato, karibu kilometa 20 kutoka katikati ya mji huo ili kurahisisha usafiri kwa njia ya anga.

Polepole: Matokeo Yanaonyesha CCM Inaongoza Kata 42 Kati ya 43 (VIDEO)

$
0
0
Polepole atoa kauli ya CCM kuhusu uchaguzi mdogo wa madiwani uliofanyika jana

==>Msikilize hapo chini

Taarifa Kutoka Wizara Ya Afya Kuhusu Matapeli

$
0
0
Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto inapenda kuutahadharisha Umma dhidi ya matapeli wanaopita maeneo mbali mbali wakiwaeleza watu kwamba wanauwezo wa kuwapatia Ajira za Afya, huku wakiwataka kutoa rushwa, kitu ambacho si kweli na ni kinyume na sheria na taratibu za nchi. 

Katika watu hao kuna mtu anayetumia jina la Godfrey Nyami  anaejifanya ni mtumishi wa Idara ya Utawala Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na huchukua fedha kiasi cha shilingi 100,000/ kwa ahadi ya kuwapatia kazi.

Kama kuna mtu yoyote anafanya hivyo na unamfahamu tafadhari  toa taarifa katika vyombo vya dola, kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria na hatua kali zitachukuliwa.

Imetolewa na ,
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Afya
27/11/2017.

Wabunge wa CUF waliovuliwa Ubunge wazungumza baada ya kushinda kesi

$
0
0
WANACHAMA wanane wa CUF waliovuliwa ubunge wamemwandika barua Katibu wa Bunge ili amjulishe Spika Job Ndugai kuhusu uamuzi wa Mahakama Kuu ili achukue hatua stahiki ikiwamo kuwafahamisha utaratibu utakaotumika kuwarejesha kwenye nafasi zao.

Wanachama hao ni Miza Haji, Saverina Mwijage, Salma Mwasa, Raisa Mussa, Riziki Mngwali, Hadija Al-Qassmy, Saumu Sakala na Halima Mohamed.

Taarifa iliyotolewa na wabunge wao wa CUF waliovuliwa uanachama na chama hao hii hapa:-

WABUNGE CUF WAMUANDIKIA BARUA SPIKA KUTAKA UTEKELEZWAJI WA MAAMUZI YA MAHAKAMA KUU:-
THE CIVIC UNITED FRONT (CUF-CHAMA CHA WANANCHI)

TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU MAAMUZI YA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA KANDA YA DAR ES SALAAM KUREJESHWA KATIKA NAFASI YA UBUNGE WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

1. Ndugu Waandishi wa Habari; Awali ya yote hatuna budi kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kutujaalia Uzima na Afya njema ya kuweza kukutana hapa leo kuweza kuzungumza nanyi na kupitia nyinyi kufikisha ujumbe wetu kwa Watanzania wote.
 
2. Mtakumbuka kuwa Tarehe 25 Julai, 2017 Spika wa Bunge wa Jamhuri ya Muunagano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Ndugai, alitangaza kutuvua Ubunge Wabunge [8] wa CUF Viti Maalum kwa kasi tuliyoiita (supersonic speed) na baadaye haraka haraka Tume ya Taifa ya Uchaguzi [NEC] kuwatangaza wafuasi wa Lipumba kuchukua nafasi hizo bila ya kufuata utaratibu huku wakijua kuwa kuna Shauri Mahakamani linalosubiri kusikilizwa na kufanyiwa maamuzi.
 
3. Tulifungua Shauri la Madai Mahakama Kuu ya Tanzania (Civil Case No. 143/2017) na Shauri dogo la Madai (Miscellaneous Civil Case No. 479/2017). Hata hivyo, kutokana na michakato ya kisheria Mahakama Kuu haikuweza kutoa maamuzi ya Zuio [Temporary Injunction and Maintenance of Status Quo] tuliloomba kwa wakati huo ndani ya muda muafaka. Baadaye Tarehe 5 Septemba, 2017 Wafuasi 8 wa Lipumba waliotangazwa kuwa wameteuliwa na NEC kuwa Wabunge waliapishwa na Bunge kuchukua nafasi zetu.
 
4. Tarehe 10 Novemba, 2017 Mahakama Kuu baada ya kusikiliza maombi yetu na kuzipitia hoja za pande zote imetoa maamuzi ya kuizuia CUF kujadili kwa namna yoyote ile Uanachama wetu na imetengua utekelezwaji wa kufukuzwa kwetu Uanachama (suspend implementation), kisheria ikiwa na maana kwamba sisi sote bado ni Wanachama halali wa CUF na pia bado tuna sifa za kuendelea kuwa Wabunge.
 
Sehemu ya Maamuzi ya Mahakama Kuu inasomeka kama ifuatavyo, ninanukuu:
“…The object of the temporary injunction is to protect the plaintiff against injury by violation of his right for which he could not adequately be compensated in damages recoverable in the action if the uncertainty were resolved in his favour on the trial…”
 
To the extent it relates to the 1st, 2nd, and 3rd Respondents, it can hardly be argued in this application that a loss shutting down the Applicants political carrier can be easily atoned by award of damages and I would not hesitate upholding the submission on the second principle.
 
Lastly, on balance of convenience. Under this condition, the court has to assess in whose favour the balance lies by the grant or refusal of the order sought. Again I am Satisfied that the Applicants have met this condition. The Applicants have averred that have appealed to the MKUTANO MKUU against their expulsion from CUF and that pending the determination of their appeals, the 1st, 2nd, and 3rd Respondents should be restrained from implementing their impugned decision.
 
“….IN ZITTO ZUBEIR KABWE V. BOARD OF TRUSTEES OF CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO & ANOTHER, CIVIL CASE NO. 270 OF 2013 (unreported) this Court speaking through Utamwa, J considered an application in more or less similar circumstances involving an elected member of parliament whose membership in the sponsoring party was about to be terminated which could have culminated into loss of his seat. Discussing the last condition, Court said:
 
“….I agree …that the balance of convenience is in favour of the Applicant in this matter for, in case temporary injunction order is not issued, the feared irreparable loss will become real, the main suit will become nugatory and thus the Applicant will face more inconvenience than the Respondents and the party generally will not suffer more inconvenience than the Applicant because,… the order is not intended to restrain the Respondents from their other functions generally….” (at page 45).
 
I am inclined to agree with my brother in his reasoning and that disposes the third condition in favour of the Applicants.
In the upshot, the application against the 1st, 2nd, and 3rd Respondents [Board of Trustees – CUF, Lipumba na Magdalena Sakaya] is hereby granted and the Court makes the following temporary orders of Injunction as Follows:
 
1. Suspension of the implementation of the expulsion Order issued against the Applicants from the Civic United Front (CUF) Political Party pending the hearing and final determination of Civil Case No. 143 of 2017 or any other order from the Court.
 
2. The 1st, 2nd and 3rd respondents, their agents, assignees or anybody acting under their authority are restrained from in any shape or form discussing the membership of the Applicants herein pending the hearing and final determination of Civil Case 143 of 2017 or any other order from the Court.
 
L. J. S. Mwandambo
JUDGE
 
Nakala ya Maamuzi haya tumeambatanisha na Taarifa hii
5. Ni kwa msingi huu Tarehe 20 Novemba, 2017 tulimuandikia Katibu wa Bunge na ili amjulishe Mheshimiwa Spika Job Ndugai kuhusu Maamuzi haya ya Mahakama Kuu ili naye achukue hatua stahiki ikiwemo kutufahamisha utaratibu atakaoutumia kuturejesha katika nafasi zetu za Ubunge kama ilivyokuwa awali ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
6. Tumeonelea ni vyema kuwajulisha wanaCUF na Watanzania kwa ujumla hatua tulizozichukua baada ya Maamuzi ya Mahakama Kuu, na ni matarajio yetu kuwa Mheshimiwa Spika na Mamlaka zake zote zitaheshimu Maamuzi ya Mahakama Kuu.

HAKI SAWA KWA WOTE
Imetolewa Leo Tarehe 27 Novemba 2017
Dar-es-Salaam.
………………………………………………….
RIZIKI SHAHARI MNGWALI
Kwa niaba ya:
1) MHE. SEVERINA SILVANUS MWIJAGE,
2) MHE. SAUMU HERI SAKALA,
3) MHE. SALMA MOHAMED MWASSA,
4) MHE. RAISA ABDALLAH MUSSA,
5) MHE. MIZA BAKARI HAJI,
6) MHE. KHADIJA SALUM ALLY AL-QASSMY, NA
7) MHE. HALIMA ALI MOHAMED

Majengo Ya Wizara ya Maji Yaanza Kubomolewa Kutekeleza Agizo la Rais Magufuli

$
0
0
TINGATINGA limeanza kubomoa majengo ya Wizara ya Maji yaliyopo eneo la Ubungo jijini Dar es Salaam kufuatia amri ya Rais John Magufuli aliyoitoa hivi karibuni.

Jengo lingine ambalo lkinatarajia kubomolewa na tingatinga ni la Shirika la Umeme Nchini (Tanesco), ambalo linatazamana na wizara ya maji eneo la Ubungo.

Majengo hayo yanatakiwa kubomolewa ili kupisha ujenzi wa barabara itakayoanzia Ubungo hadi Chalinze mkoani Pwani kwa njia sita.

Leo asubuhi majengo hayo ya wizara yameanza ‘kupigwa nyundo’ ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli ambaye aliagiza majengo ya wizara hiyo na ghorofa la Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuwekwa alama ya X kwa ajili ya kubomolewa.

Novemba 15,2017 akitokea Chato alipokwenda kwa mapumziko baada ya ziara ya Uganda, Rais Magufuli aliagiza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kuweka alama ya X katika jengo la Tanesco na Wizara ya Maji, sehemu zilizo katika hifadhi ya barabara.

Katika majengo ya Wizara ya Maji, tingatinga limevunja ukuta, huku watu wengine wakiendelea na kazi ya kuondoa madirisha na milango kwenye majengo. Jengo lililoanza kubomolewa ni la ofisi ya Waziri wa Maji.

Wafanyakazi wa wizara hiyo wanaendelea kutoa mali ndani ya majengo waliyokuwa wakiyatumia kwa ofisi.

Mbali ya majengo hayo, Tanraods inaendelea kuweka alama ya X kwenye nyumba za wananchi zilizo katika hifadhi ya barabara ikiwa ni pamoja na kupisha ujenzi wa barabara za juu eneo la Ubungo.

Tayari nyumba takriban 1,200 zikiwamo tano za ibada, vituo vya mafuta na baa katika eneo la Ubungo hadi Kimara mwisho zimewekwa alama kwa ajili ya ubomoaji.

Kwa mujibu wa Tanroads, ubomoaji katika eneo la Ubungo hadi Kimara mwisho unahusisha nyumba zilizo mita 91.7 katika hifadhi ya barabara ikiwa ni utekelezaji wa Sheria ya Hifadhi ya Barabara ya mwaka 1932.

Magdalena Sakaya: Sipo Tayari Kuhama CUF na Kama Kitafutwa Basi Ntastaafu Siasa

$
0
0
Naibu Katibu wa CUF Tanzania Bara, Magdalena Sakaya  amedai hayuko tayari kuondoka Chama cha Wananchi CUF na kwenda katika vyama vingine hata kama chama chake kina mgogoro na iwapo na ikitokea Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ikiamua kukifuta chama hicho yeye atastafu siasa

Akifanya mahojiano maalumu na Nipashe, Sakaya amesema kwamba Mgogoro unaoendelea ndani ya chama chao ni wa Kikatiba na unafahamika kwa msajili wa vyama na kuongeza kama ikitokea kwamba CUF inafutwa basi yeye atastaafu siasa na siyo kuhama chama.

"Kwanza naamini CUF haiwezi kufutwa. Yaani hilo halipo pamoja na changamoto ya mgogoro iliyopo. CUF ina misingi yake na mgogoro uliopo ndani yake ni wa kikatiba. Kwa hiyo, mimi nikiamua kwamba sasa sitaki kuendelea kuwapo CUF, ninaacha siasa. Ninaendelea na mambo yangu mengine, eeeh" Sakaya

"Kwanza mimi sijawahi kuwa na kadi ya CUF pekee. Nakumbuka wakati tunaripoti Shule yaSekondari ya Wasichana Kibosho (mwaka 1986) tuligawiwa kadi za kijani (CCM) wakati ule nchini kulikuwa na chama kimoja. Baadaye nikiwa na akili yangu timamu kadi niliyoichukua ni ya CUF ambayo niliichukua mwaka 1995 na ninayo mpaka leo na nitaendelea kuwa nayo. .

Serikali kununua kondomu milioni 500 ......Zitasambazwa Bure Nchi Nzima

$
0
0
Serikali inatarajia kununua kondomu milioni 500 zitakazosambazwa nchi nzima bure kwa lengo la kupunguza maambukizi ya Ukimwi ifikapo mwaka 2030.

Kondomu hizo zitasambazwa bila malipo ambapo kutakuwa na mashine maalumu zitakazofungwa kwenye maeneo ya baa, nyumba za kulala wageni, migodini na katika kumbi za burudani.

Akizungumza leo wakati wa uzinduzi wa mkakati wa kitaifa wa kondomu, Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Neema Rusibamaila, amesema kondomu hizo zitanunuliwa kupitia fedha za Global Fund.

“Takwimu za mwaka 2011/12 zinaonyesha asilimia 69 ya wanawake na asilimia 77 ya wanaume wanafahamu kwamba kondomu inaweza kuzuia VVU lakini ni asilimia 27 tu ya watu wenye wenza zaidi ya mmoja walitumia kondomu walipofanya ngono mara ya mwisho,” amesema.

Credit:Mtanzania

TANESCO yatekeleza agizo la Rais Magufuli..... Yaanza kubomoa jengo lake kwa Hiari

$
0
0
Uongozi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) umesema umeanza utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kubomoa jengo lake lililo ndani ya hifadhi ya barabara eneo la Ubungo jijini Dar es Salaam.

Kazi hiyo iliyoanza leo Jumatatu Novemba 27,2017 ni utekelezaji wa agizo la Rais Magufuli aliyeagiza majengo ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji na ghorofa la Tanesco kuwekwa alama ya X kwa ajili ya kubomolewa.

Novemba 15,2017 akitokea Chato alipokwenda kwa mapumziko baada ya ziara ya Uganda, Rais Magufuli aliagiza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kuweka alama ya X katika majengo hayo sehemu zilizo katika hifadhi ya barabara.

Taarifa ya Tanesco kwa umma imesema kuanzia leo Jumatatu Novemba 27,2017 wameanza kubomoa ukuta wa mbele ya jengo.

Tanesco imesema baadhi ya watumishi wa shirika hilo wameanza kuhamishiwa katika ofisi nyingine za shirika zilizopo jijini Dar es Salaam ili kupisha shughuli za ubomoaji kufanyika kwa usalama.

Uongozi wa shirika hilo na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) unaendelea kufanya utaratibu utakaowezesha ubomoaji wa jengo hilo la ghorofa kufanyika bila kuathiri huduma kwa wateja wa Tanesco.

“Katika kipindi hiki cha utekelezaji wa agizo la Rais. Tunapenda kuwahakikishia wateja  na Watanzania kwa jumla kuwa, huduma za umeme zitaendelea kupatikana kama kawaida ikiwemo huduma ya ununuzi wa Luku,” imesema taarifa hiyo.

Uongozi wa shirika hilo umesema utaendelea kutoa taarifa kwa kadri kazi hiyo itakavyokuwa ikiendelea. 


==>Soma taarifa iliyotolewa na Tanesco kwa Vyombo vya Habari leo Novemba 27, 2017.


Mbunge wa CHADEMA Susan Kiwanga Atiwa Mbaroni......Polisi Waendelea Kumsaka Mbunge Lijualikali

$
0
0

Polisi mkoani Morogoro inawashikilia watu 41 akiwemo mbunge wa Mlimba (Chadema), Susan Kiwanga.

Pia inawashikilia madiwani wawili, huku mbunge wa Kilombero (Chadema), Peter Lijualikali akitafutwa na jeshi hilo wakidaiwa kufanya fujo na kuchoma moto ofisi ya mtendaji baada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata ya Sofi wilayani Malinyi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Urlich Matei katika taarifa leo Jumatatu Novemba 27,2017 amesema tukio hilo lilitokea jana Jumapili Novemba 26,2017 saa tano usiku ambako walikwenda kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa udiwani.

Kamanda Matei amesema wabunge hao na madiwani wawili wa Chadema kutoka Ifakara walionekana kuhamasisha baadhi ya wafuasi wao kufanya vurugu.

Amesema watuhumiwa wanadaiwa kuchoma majengo ya umma ambayo ni ofisi shule ya msingi Sofi, nyumba ya walimu wa shule hiyo na ofisi ya mtendaji kata.

Kamanda Matei amesema fujo na uharibu huo ulitokea baada ya msimamizi wa uchaguzi kutangaza matokeo kuwa mgombea wa CCM ndiye alishinda kwa kupata kura 2,099.

Mgombea wa chadema alipata kura 1,684 jambo lililopingwa na wafuasi wa chama hicho na kuanza  vurugu.

Amesema baada ya kuchoma majengo hayo kwa kutumia petroli, walidhamiria pia kwenda katika zahanati lakini askari waliwakamata.

Kamanda Matei amesema polisi inaendelea kuwatafuta watu wengine waliohusika na vurugu hizo, akiwemo mbunge Lijualikali.

Amesema watuhumiwa 41 wamepelekwa wilayani Ulanga kwa ajili ya kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Mbunge Lijualikali amesema wakati matokeo yakitangazwa alikuwa Ifakara.

 “Baada ya kumalizika kampeni Jumamosi nilirejea Ifakara kwa hiyo sijui chochote kuhusu hizo vurugu na nashangazwa kuhusishwa na tuhuma hizo, lakini kama kweli natafutwa nitakwenda kujisalimisha polisi,” amesema Lijualikali.

Kajala Aonyesha Umahiri Wake wa Kumtega Shemeji Yake

$
0
0
Video mpya ya 'Omulilo' ambayo ni kazi yake mwanamama Saida Karoli imeachiwa rasmi, huku Kajala akiigiza muhusika aliyeimbwa kwenye wimbo huo.

Video hiyo inamuonyesha Kajala akiwa anaishi kwa shoga yake kipenzi, lakini licha ya kumsitiri anafanya kitendo kibaya cha kumtaka shemeji yake kimapenzi kwa kumtega kwa kumvalia mavazi ya kumshawishi.
 
Kazi hiyo ambayo imefanywa na mikono ya Hanscana, ni moja ya kazi zilizoachiwa hivi karibuni na Saida karoli tangu arudi rasmi kwenye game, baada ya kishindo cha wimbo wa 'Orugambo'. 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Novemba 28

Agizo la Rais kuhusu hospitali nchini latekelezwa ndani ya saa 48

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo amekabidhi rasmi Hospitali za Rufaa za Mikoa kwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Hatua hiyo imekuja kufuatia pendekezo lililotolewa na Rais John Magufuli Novemba 25 aliyetaka hospitali hizo zitolewe TAMISEMI ziwe chini ya Wizara ya Afya ili kuweza kuwapo kwa mfanano wa sera lakini pia ugawaji wa rasilimali watu katika hospitali hizo.

Rais aliyasema hayo alipokuwa akizindua Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Kampasi ya Mloganzila na kueleza kuwa kumekuwa na utofati mkubwa wa ugawaji wa madaktari katika hospitali za rufaa kutokana na mgawanyo huo kufanywa na wizara mbili tofauti.

Mbali na Rais kuagiza hospitali hizo ziwe chini ya Wizara ya Afya ili zisimamiwe vizuri na wataalamu na pia ameiagiza wizara hiyo kurekebisha mgawanyo wa madaktari katika hospitali zote nchini ili kuepuka uwepo madaktari wengi katika sehemu moja, huku maeneo mengine yakiwa na uhaba mkubwa.

“Kuanzia leo (Novemba 27) hospitali zote za rufaa zitakuwa chini ya Wizara ya Afya na kwetu sisi (TAMISEMI) tutabaki na hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati pekee,” amesema Waziri Jafo.

Kuhusu madaraka ya Waganga Wakuu wa Mikoa amesema wataendelea kuwa chini ya TAMISEMI lakini Waganga Wafawidhi wa Hospitali watapelekwa Wizara ya Afya.

IGP Sirro Atembelea Bandarini Kufanya Ukaguzi wa Magari ya Polisi Yaliyoibuliwa na Rais Magufuli

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, amefanya ziara katika bandari ya Dar es salaam, ili kufanya ukaguzi wa magari 31 ya Jeshi hilo ambayo Mhe. John Pombe Magufuli, alielekeza kukabidhiwa kwa Jeshi hilo ili kurahisisha utendaji kazi

Akiwa Bandarini IGP Sirro amekutana na kufanya mazungumzo na askari wa Jeshi hilo Kikosi cha Bandari ambapo amewataka kuhakikisha wanatimiza majukumu yao ipasavyo pamoja na kutenda haki ikiwa ni pamoja na kutoa huduma bora kwa wateja.

Hata hivyo IGP amewataka Polisi wasaidizi wanaofanya kazi bandarini hapo kushirikiana na Jeshi la Polisi ili kuendelea kudhibiti vitendo vya kihalifu vinavyofanywa na baadhi ya watu wasio waaminifu.


Serikali ya Zimbabwe Yatangaza siku ya kuzaliwa Rais Mugabe, Februari 21 kuwa ni Siku ya Taifa na Itakuwa ni Mapumziko

$
0
0
Serikali ya Zimbabwe imetangaza siku kuu mpya ya kukumbuka mchango wa Robert Mugabe ambaye aliondolewa madarakani wiki iliyopita.

Gazeti la serikali la Herald limesema sikukuu hiyo itakuwa ikiadhimishwa siku ya kuzaliwa kwa Bw Mugabe kila mwaka.

Uamuzi wa kusherehekea Siku ya Taifa ya Vijana ya Robert Gabriel Mugabe kila 21 Februari ulifanywa rasmi kupitia tangazo rasmi kwenye gazeti la serikali.

Tangazo hilo lilichapishwa Ijumaa – siku ambayo Rais Emmerson Mnangagwa aliapishwa kuwa rais, na kufikisha kikomo uongozi wa Mugabe wa miaka 37.

Serikali ya Bw Mugabe ilikuwa imeamua kutangaza siku ya kuzaliwa kwake kuwa sikukuu ya taifa mwezi Agosti, baada ya kampeni kutoka kwa mrengo wa vijana katika chama cha Zanu-PF.

Bw Mugabe aliondolewa mamlakani wiki iliyopita kutokana na shinikizo kutoka kwa wanajeshi waliokuwa wamechukua udhibiti wa serikali wiki iliyotangulia.
 
Credit:BBC

Mabasi ya Mwendokasi Dar Yageuka shule kwa nchi za Afrika.....Dart Yapanga kuongeza mabasi Mengine 165

$
0
0
Tangu kuanza rasmi Mei 10, 2016 kwa mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, zaidi ya nchi tano za Afrika zimetuma viongozi wake kujifunza namna ya uendeshaji wake.

Mfumo huo wa usafiri unalenga kupunguza foleni katika barabara, tangu uzinduliwe na Rais John Magufuli nchi za Ethiopia, Malawi, Uganda na Kenya zimetuma viongozi kuja kujifunza.

Pia, ugeni kutoka Rwanda jana uliongeza idadi ya viongozi wanaoendelea kuja mahsusi kwa ajili ya mradi huo huku kukiwa na taarifa za ujio mwingine Desemba kutoka nchini Senegal.

Akielezea utekelezaji wa mradi huo kwa wageni hao, mtendaji mkuu wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart), Ronald Lwakatare kuwa wanatarajia kuongeza mabasi kutoka 140 yaliyopo sasa hadi 305 katika awamu ya kwanza ya mfumo huo itakapokamilika Juni mwakani.

Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na Lwakatare, inasema wageni hao sita kutoka Serikali ya Rwanda wana ziara ya siku tano kujifunza namna wakala huo unavyotoa huduma.

Lwakatare alisema ongezeko la mabasi kutasaidia kuongeza idadi ya abiria kutoka 200,000 wanaohudumiwa sasa kwa siku hadi kati ya 400,000 na 500,000. 

“Licha ya hilo, tutaongeza njia za mlisho kutoka mbili zilizopo sasa hadi tisa zitakazokuwa zikienda Masaki, Sinza, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na maeneo mengine ambayo yapo jirani ili kupanua huduma ya usafiri kwa maeneo yaliyomo ndani ya mfumo wa mabasi yaendayo haraka katika awamu ya kwanza ya mradi,” alisema.

Kuhusu athari zilizotokana na mvua iliyonyesha Oktoba 26, Lwakatare alisema mabasi 20 yaliharibika zaidi lakini yameshatengezwa na yanatoa huduma.

Alisema Dart imejipanga kuhakikisha mitaro yote inayozunguka karakana ya Jangwani inasafishwa, ili kuepuka eneo hilo kukumbwa tena na mafuriko.

Naye kiongozi wa ujumbe huo kutoka Mamlaka ya Halmashauri ya Jiji la Kigali, Rwagatore Etienne alisema wamechagua kutembelea wakala huo kwa sababu ndiyo mradi uliofanikiwa barani Afrika na upo karibu na Rwanda.

Katika msafara huo, Etienne ameambatana na wataalamu washauri ambao waliopewa kazi ya usanifu wa Jiji la Kigali ili liweze kuwa na mfumo wa mabasi yaendayo haraka.    

Nape Nnauye Atoa Neno Kwa Vyama vya Upinzani Baada ya Uchaguzi wa Madiwani

$
0
0
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, amekiri kuwepo na vitendo ambavyo siyo sahihi ambavyo vilivyojitokeza katika Uchaguzi wa marudio katika baadhi ya kata  na kutaka hatua za kisheria zichukuliwe.

Nape amefafanua hayo  baada ya kuwepo na malalamiko hayo kutoka upande wa upinzani ambapo amesema  kwamba vitendo hivyo vinapaswa kushughulikiwa kisheria kama wahalifu na siyo kushughulikiwa kisiasa  na kwamba kufanya matendo hayo kisiasa ni njia za kuficha uovu.

Pamoja na hayo Nape ameongeza kwamba hajawahi kuwa muumini wa matumizi ya nguvu kwenye siasa na wala hajawahi kushiriki mipango ya kutumia nguvu bali anaamini katika matumizi zaidi ya nguvu.

Aidha Nape ameongeza kwamba sehemu zote alizofanya kampeni na wala hakubariki matumizi ya nguvu hivyo kuwashauri vyama vya upinzani wafanye tathmini ya kweli kisha kuchukua hatua pale walipoteleza katika uchaguzi.

"Rafiki zangu Upinzani fanyeni tathmini ya kweli halafu chukueni hatua pale mlipoteleza. Hichi kinachoendelea cha kutoa visingizio vya jumla. Sikatai kuwa kulikuwa na baadhi ya maeneo kumekuwa na vitendo si vya kibinadamu  lakini si kwa kata zote. Vitendo hivyo vishughulikiwe specific kisheria kama wahalifu na si kushughulikiwa kisiasa".Amesema Nape

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0
Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

LIVE: Sherehe za kuapishwa Uhuru Kenyatta

$
0
0
Ni siku nyingine ambayo Taifa la Kenya leo linatekeleza shughuli muhimu ya kikatiba ya kumuapisha kiongozi wa taifa hilo kufuatia ushindi wake wa marudio ya uchaguzi wa Oktoba 26 uliosusiwa na upinzani.

Uhuru Kenyatta leo anaapishwa rasmi kuwa rais wa nchi hiyo kwa muhula wa pili baada ya kuibuka mshindi kwenye uchaguzi mkuu.

Wageni mbalimbali wanatarajiwa kushuhudia sherehe za kuapishwa kwa kiongozi huyo wa Kenya huku ulinzi ukiimarishwa kila kona

Uchaguzi wa  uliofanyika Agosti ulifutwa  na mahakama kutokana na kile kilichotajwa kuwa uchaguzi usio huru na haki.

Marudio ya uchaguzi wa Oktoba 26 ulimpatia Uhuru Kenyatta asilimia 98 ya kura huku waliojitokeza kushiriki katika shughuli hiyo wakiwa  na asilimia 39.

==>Tazama tukio hilo hapo chini
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images