Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Wema Sepetu: Sina Mpango wa Kurudi CCM

$
0
0
Mrembo wa Tanzania na Muigizaji Wema Sepetu amemfunga mdomo muigizaji mwenzake Steve Nyerere kwa kumwambia hana mawazo ya kurudi CCM kama jinsi ambavyo wengine wanavyofanya.

Wema amefanya tendo hilo kwa kujibu ujumbe wa Steve Nyerere aliokuwa ameuandika kupitia ukurasa wake wa Instagram akimkaribisha ndani ya CCM, Wakili Alberto Msando ambaye mapema jana alitangaza kujiunga na CCM.

Steve aliandika "Sasa utakuwa mzalendo wa kweli , Msando naheshimu maamuzi yako maana ni maamuzi sahihi, kwako pamoja na family yako , rafiki zako nasi tupo pamoja nawe, soon na yuleeeeeeeee rafiki yetu , dada yetu , msanii mwenzetu , naye yupo njiani kurudi nyumbani"

Hata hivyo Wema Sepepetu baada ya kuona ujumbe huo ambao alihisi kama inamlenga yeye, alijibu chini ya ujumbe huo kwa kuandika "I hope hauniongelei mimi... Maana mawazo hayo sina"

Muigizaji Wema Sepetu alihama ndani ya chama cha mapinduzi Februari mwaka huu kwa madai kuwa ameamua kujiunga na Chadema kupigania demokrasia ya kweli.


Mwigulu Nchemba Awachana CHADEMA Kumtumia Tundu Lissu Kama Mtaji

$
0
0
Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt Mwigulu Nchemba amewakosoa upinzani kutumia tukio la kushambuliwa kwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kama ajenda katika kampeni za uchaguzi wa marudio na kusema kwamba chama hicho kimefilisika.

Akiwa Masasi katika kampeni za kumnadi mgombea wa udiwani wa tiketi ya CCM, Dkt Nchemba amesema kwamba kitendo hicho cha Chadema kufanya kila mahali tukio la Lissu kama ndiyo ajenda atakwenda kuwaambia wakazi wa Singida wawaangalie vizuri watu hao.

"Mimi nitaenda kuwaambia wana Singida kwamba tuwaangalie vizuri hawa watu. Wao  ni mwenzao kwenye Chama sisi ni ndugu yetu na tunatoka sehemu moja. Inawezekanaje wawe wanafurahia tukio hilo? Kama kuna kitu walikuwa wanataka kitokee ili warushe maneno kwa serikali" amesema Dkt Nchemba.

Aidha akiendelea Nchemba amesema Chadema wanamuona kama Lissu mtaji ndiyo maana hata polisi walipomtaka dereva wake ili kuweza kumhoji wameamua kukaa naye huko.

Pamoja na hayo Nchemba amewata watu wakapige kura bila kuhofia fujo zinazoweza kufanywa na wanachadema kwani serikali ipo kwa ajili ya kusimamia sheria.

 "Wamezoea kufanya fujo. Nendeni mkapige kura akitokea mtu atakayethubutu kukughasi wewe mkariri sura alafu sisi tutamfundisha ustaarabu wa vyama vingi. Anayefanya fujo atakutana na mkono wa sheria. Na uzuri vijana wangu wapo hapa atakayethubutu kufanya fujo, Muwaonyeshe kwamba mmepitia mafunzo" Nchemba

Hata hivyo Nchemba amewataka wananchi hao kuichagua CCM kwa kazi nzuri inayofanya na kuwaamba kuuchagua upinzani wakitegemea itashinda ni sawa na kujeruhi nafsi.

RC Makonda Atembelea Ofisi Za Clouds Media Group Na Kutoa Pole

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Paul Makonda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Dar es Salaam mapema leo ametembelea Ofisi za Clouds Media Group kutoa pole ikiwa ni siku moja baada ya ofisi hizo kukumbwa na janga la moto uliotokea hapo jana majira ya saa nne asubuhi.

Viongozi wengine wa serikali waliofika ofisini hapo ni Mkuu wa Wilaya wa Kinondoni, Ally Hapi na Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta.

Hata hivyo, tayari matangazo ya vituo vya Clouds FM na Clouds TV yamerejea hewani baada ya kupotea siku nzima  jana kutokana na hitilafu iliyosababishwa na moto huo ambao chanzo chake hadi sasa hakijajulikana.

Waziri Mwakyembe Awapa Pole Clouds Media Group Baada Ya Ofisi Zao Kupata Ajali Ya Moto

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amepokea kwa mshtuko na masikitiko taarifa za ajali ya moto kwenye ofisi za  kituo cha Redio na Televisheni cha Clouds Media cha Jijini Dar es Salaam hapo jana.

Waziri huyo ambaye yuko mkoani Iringa kwa ziara fupi ya kikazi, ametoa pole kwa viongozi na wafanyakazi wa kituo hicho cha redio na televisheni kwa kuunguliwa na baadhi ya vifaa vya kazi vya chombo hicho cha habari na kuzitaka Taasisi husika kufanya uchunguzi wa kina kujua chanzo cha moto huo.

Aidha, Dkt. Mwakyembe amelipongeza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini kwa kuitikia wito na kufika kwa haraka sehemu husika na hivyo kudhibiti moto huo usilete madhara makubwa zaidi.

Imetolewa na:
Lorietha Laurence
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo.
22/11/2017.

Rais Magufuli Akutana Na Rais Wa Zanzibar Dkt. Shein Ikulu Jijini Dar Es Salaam Leo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein walipokutana na kufanya mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 22, 2017-PICHA NA IKULU

David Kafulila Aitosa CHADEMA Na Kuhamia CCM

$
0
0
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Kigoma Kusini mwaka 2010-2015 David Kafulila amejivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Taarifa ya Kafulila kuondoka CHADEMA imetolewa leo kwa vyombo vya habari, na kueleza kwamba hana imani tena na vyama vya upinzani katika kupambana na ufisadi.

David Kafulila anafahamika zaidi kwa kuibua mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa kwa kuibua bungeni suala la Escrow.


Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0
Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Novemba 23

Mhasibu feki atiwa mbaroni kwa wizi wa Tsh. 873,000

$
0
0
Na Nathaniel Limu, Singida
 Mhasibu wa hospitali ya mkoa mjini Singida aliyeachishwa kazi kwa kosa la kumiliki vyeti feki, Edith Talasi (49) mkazi wa Minga,anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma ya kuvunja milango ya ofisi yake ya zamani na kuiba shilingi 873,000 taslimu, kwa kutumia funguo bandia.

Talasi  ambaye imelelezwa kwamba alifanya kazi hospitalini hapo kwa  muda na baadaye alirejeshwa kwenye kituo chake cha kazi manispaa ya Singida,kwenye wizi huo, alimshirikisha mlinzi wake wa nyumba ya kulala wageni Nandau, Antony Felix (51).Mlinzi huyo naye anashikiliwa na polisi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa, ACP Debora Magiligimba, alisema tukio hilo limetendeka Novemba, 21 saa 6.30 usiku huko katika hospitali ya mkoa mjini hapa.

Alisema siku ya tukio muuguzi wa zamu Shamir Omari (27) akitokea maeneo ya mapokezi akielekea wodini, alimwona mtu akiwa amesimama karibu na ofisi ya mhasibu, alisimama akamsalimia na mtu huyo aliondoka.

“Muuguzi huyo aliamini kuwa mtu aliyemwona,huenda alikuwa  mgonjwa au mtu aliyeleta mgonjwa hospitalini.Lakini aliporudi,alimwona mtu yule yule amerudi eneo lile lile, kitendo kilichopelekea amshuku kuwa sio mtu mzuri,” alisema kamanda huyo.

Alisema muuguzi huyo baada ya kumtilia shaka mtu huyo, alitoa taarifa kwa mlinzi wa zamu wa hospitali hiyo, Abubakari Jumanne,ambaye alimweka chini ya ulinzi mtu huyo.

ACP Magiligimba alisema hata hivyo mtu huyo alijitetea kuwa amefika hospitalini hapo, kwa ajili kuchoma sindano na kuonyesha dawa ya unga na kichanganyio chake.

“Wakati wanaendelea na mahojiano hayo,waliona makufuli  mawili ya mlango wa nje/grili yapo chini na mlango huo wa chuma upo wazi. Mtuhumiwa mlinzi Antony alieleza kuwa bosi wake (mtuhumiwa Edith) kwa wakati huo,alikuwa ndani ya ofisi ya mhasibu amejifungia ndani,” alisema.

 Akifafanua  alisema  jeshi la polisi baada ya kupata taarifa ya wizi huo, liliweza kufika eneo la tukio na kukuta mlango wa ndani ukiwa umefungwa kwa ndani.

“Walipoamuru mhasibu afungue mlango huo kwa kutumia funguo zake,walimkuta mtuhumiwa (Edith) akiwa amejibanza kwenye kona ya mlango na watumishi wa hospitali hiyo, waliweza kumtambua. Alipohojiwa ameingiaje humo ndani,alionyesha funguo saba (07) na zilipojaribiwa ziliweza kufungua milango yote ya ofisi ya mhasibu,” alisema Magiligimba.

Alisema pamoja na wizi huo wa shilingi 873,000,imeelezwa kwamba aprili mwaka huu,wahasibu wa hospitali hiyo,walibaini upotevu wa shilingi 1,800,000.Oktoba mwaka huu,pia walibaini upotevu wa shilingi 3,600,000.

Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. David Mwasita,amekiri kutokea upotevu huo lakini wahasibu katika wakati huo,waliweza kuziba upotevu huo, kwa fedha zao za mishahara.

Ameeleza kuwa wahasibu hao walilazimika kutoa fedha zao binafsi, na wasingeweza kutoa taarifa ya upotevu huo, kwa vile milango na kasiki, ilikuwa imefungwa kama kawaida.

ACP Magiligimba amesema kwa sasa wanaendelea kuwahoji watuhumiwa hao na baada ya kumalizika kwa mahojiano hayo,watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayowakabili.

GodBless Lema Amtaka Kafulila Amshauri Mkewe Naye Ajiondoe CHADEMA

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini kupitia CHADEMA Godbless Lema, amefunguka kuhusu kitendo cha David Kafulila kuhama CHADEMA na kusema ana amini atamshauri mke wake naye afuate nyayo zake.

Kwenye ukurasa wake wa twiter Godbless Lema ameandika ujumbe akisema Kafulila ni rafiki yake wa karibu, lakini kwa namna alivyoamua hana shaka atamshauri mke wake ambaye ni mbunge kupitia chama cha CHADEMA, kufanya kama yale aliyoyafanya.

"David Kafulila ni rafiki yangu, nafikiri kwa namna hii alivyoamua ataweza bila shaka kumshauri Mbunge wa Chadema, Jesca Kishoa (mke wake) kufikiri kama yeye, hii inaweza kusaidia maoni yake juu ya uamuzi aliouchukua leo na kuthibitisha ukweli huu kama hupo", ameandika Godbless Lema.

Jana David Kafulila ametangaza kukihama chama cha CHADEMA akidai vyama vya upinzani havina nia ya kupambana dhidi ya ufisadi, lakini mke wake Jesca Kishoa ambaye ni mbunge wa viti maalum kupitia CHADEMA bado hajazungumza chochote.

Waziri Mkuu Kufanya Ziara Ya Kikazi Mkoani Ruvuma

$
0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa (Mb) anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku tatu katika Mkoa wa Ruvuma kuanzia tarehe 23 - 25 Novemba, 2017.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana tarehe 22 Novemba 2017 na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema Mheshimiwa Waziri Mkuu atawasili mjini Songea siku ya Alhamisi tarehe 23 Novemba, 2017 na kupokelewa na viongozi wa Chama na Serikali katika Uwanja wa ndege Songea majira ya 7.00 mchana.

Baada ya kuwasili atapokea taarifa ya maendeleo ya Mkoa na ile ya Chama Tawala Uwanja wa Ndege Songea. Kisha ataelekea Wilaya ya Namtumbo ambapo atafungua ghala la MIVARF, kuongea na Madiwani na watumishi wa Umma na baadaye ataongea na wananchi wa Namtumbo kwenye mkutano wa hadhara. 

Ijumaa tarehe 24 Novemba, 2017 Mheshimiwa Waziri Mkuu ataendelea na ziara yake kwa kuongea na wananchi wa kijiji cha Mchomoro kisha ataelekea Wilaya ya Tunduru ambapo atasalimia na wananchi wa vijiji vya Rahaleo,Milonde na Matemanga akiwa njiani kuelekea mjini Tunduru.

Aidha, Mheshimiwa Waziri Mkuu atatembelea kituo cha Afya cha Nakayaya, ghala la kuhifadhia Korosho na kupata taarifa ya Chama Kikuu Cha Ushirika TAMCU. Jioni Mheshimiwa Waziri Mkuu ataongea na wananchi kwenye mkutano wa hadhara utakaofanyika mjini Tunduru katika uwanja wa michezo. Jumamosi tarehe 25 Novemba, 2017 Mheshimiwa Waziri Mkuu atahitimisha ziara yake mkoani Ruvuma na kurejea Dar es Salaam

Mkuu wa Mkoa Mndeme ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Ruvuma kujitokeza kwa wingi katika mapokezi kuanzia uwanja wa Ndege Songea atakapowasili Aidha amewaomba wananchi kujitokeza kwenye maeneo yote ambayo Waziri Mkuu atapita na kwenye mikutano ya hadhara ili wapate fursa nzuri ya kumsikiliza Mheshimiwa Waziri Mkuu na kupokea maelekezo atakayoyatoa.

Serikali yawafuata Marekani wanaoshikilia Bombardier

$
0
0

Tanzania imeiomba Mahakama ya Jimbo la Columbia kutupilia mbali ombi la Stirling Civil Engineering la kutaka kusajili hukumu mbili za Mahakama ya Kimataifa Usuluhishi ili kampuni hiyo ya Uingereza ikamate mali nyingine za Serikali zilizopo nchini Marekani.

Stirling, ambayo ni kampuni ya ujenzi iliyokatishwa zabuni ya kujenga Barabara ya Bagamoyo kutoka eneo la Wazo Hill kutokana na kutekeleza mradi huo chini ya kiwango, ilishinda ksi iliyofungua kupinga kitendo hicho msuluhishi akaagiza ilipwe dola 38 milioni za Kimarekani.

Kampuni hiyo ilisajili uamuzi huo wa msuluhishi nchini Uingereza na Uholanzi na kufanikiwa kushikilia ndege aina ya Bombardier Q400 iliyonunuliwa na Serikali na sasa inataka mahakama isajili hukumu mbili za mwaka 2015 na 2016 zisajiliwe Marekani ili ipate nguvu ya kushikilia mali nyingine.

Lakini Serikali ya Tanzania imeamua kupambana na kampuni hiyo mahakamani kuizuia isiendelee kukamata mali zake.

Kwa mujibu wa tovuti ya Law360, ambayo ni maalum kwa ajili ya habari za kisheria, Tanzania imewasilisha pingamizi, ikitaka mahakama hiyo isisajili hukumu hiyo ya Mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi.

Katika hoja yake, Tanzania imesema mahakama hiyo haina mamlaka ya kisheria ya kushughulikia ombi hilo la Stirling.

Serikali inasema ina kinga dhidi ya hukumu mbili zilizotolewa na mahakamani nchini Uingereza na Uholanzi ambazo kampuni hiyo inaomba zitambuliwe pia Marekani, ikisema kuwa ondoleo hilo la kinga linalotolewa na Sheria ya Kinga ya Mataifa ya Kigeni, haiwezi kutumika.

Kwa mujibu wa tovuti hiyo, Sheria ya Kinga ya Mataifa ya Kigeni inasema taifa la kigeni halitakuwa na kinga dhidi ya mamlaka ya mahakama ya Marekani katika mashauri yanayowasilishwa kwa ajili ya kuthibitisha tuzo za mahakama ya usuluhishi zinazoongozwa na makubaliano yaliyoidhinishwa na nchi yanayotambuliwa nchini Marekani.

Serikaloi inasema Stirling inataka kutambuliwa kwa hukumu za mahakama ya nje ili ziwe na nguvu, badala ya kuomba kutekelezwa kwa hukumu hizo.

“Kuna tofauti inayotambulika vizuri kati ya kuthibitisha tuzo ya msuluhishi, kwa upande mmoja, na kutambua hukumu ya mahakama ya nje, kwa upande mwingine,” tovuti hiyo inakariri hoja hizo za Serikali.

“ingawa tuzo ya msuluhishi na hukumu ya mahakama zinalingana kwa kiasi kikubwa, hata hivyo zina tofautiana.”

Kwa hiyo, Serikali inasema Stirling haiwezi kutumia mwanya huo, kuomba utekelezaji wa hukumu hizo.

Kampuni hiyo inadai kuwa kitendo cha Serikali ya Tanzania kukubali kwenda kwenye Mahakama ya Usuluhishi, kiliondoa kinga hiyo na kuipa yenyewe haki ya kulipwa fidia hiyo.

Mwaka 1999 Serikali iliipa kandarasi kampuni ya Impresa Ing. Fortunato Federici SpA (IFF) ambayo baadaye ilinunuliwa na Stirling, kukarabati barabara ya Wazo Hill-Bagamoyo, lakini baadaye ikatimuliwa.

Mwaka 2004 kampuni hiyo ilifungua kesi Mahakama ya Usuluhishi wa Kimataifa na hukumu ilitolewa mwaka 2009 na 2010, lakini Serikali haikulipa fidia iliyopendekezwa na kuilazimu kukazia hukumu Uingereza na Uholanzi.

Novemba 2015, mahakama nchini Uingereza iliridhia utekelezaji wa hukumu hiyo na Uholanzi ilifanya hivyo Desemba 2016.

VideoMPYA: Roma na Stamina Ft. Maua Sama........ Dr. Shika ( 900 Itapendeza ) Naye Kapewa Nafasi ya Kuuza Sura

$
0
0
Roma na Stamina wametoa ngoma mpya ambapo  wamemshirikisha Mwimbaji Staa Maua Sama, 

Ndani ya ngoma hiyo, Dr Shika aliyejizolea umaarufu wa 900 itapendeza nae kaonekana.


Masharti Magumu ya mnada yaliyowekwa na Yono Aution Mart

$
0
0
Kampuni ya Udalali ya Yono imetangaza kuwa kesho, Novemba 24, 2017 itarudia upya mnada wa nyumba mbili za kifahari za mfanyabiashara Said Lugumi zilizoshindikana kuuzwa baada ya Dr. Louis Shika kuzinunua na kushindwa kuzilipia.

Nyumba zilizotajwa kurudiwa kuuzwa katika mnada ni Plot. No 47, iliyopo Mbweni JKT,  na nyingine iliyopo Upanga

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Yono Auction Mart, Scholastica Kevela ameeeleza kuwa kwa sasa kampuni ya Yono imeweka masharti magumu ili kuhakikisha kwamba hakuna atakayeibuka kuuharibu mnada huo.

“Niwakaribishe wateja ndani na nje ya nchi kuja kujinunulia nyumba zile kwa maana ujenzi ni mgumu..” amesema.

Aidha Bi Scholastica Kevela amewaonya wale wote wenye nia ya kuuharibu mnada huo kutofanya hivyo kwani hawatavumiliwa na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

“Niseme kwamba mchezo ule tuliochezewa mara ya mwisho hautarudiwa tena. Kwa sasa hivi tumekuja na masharti magumu kwamba washiriki wote wawe aware na wanielewe,” amesema Bi. Kevela.

Masharti yaliyowekwa katika minada hiyo ni kwamba mshiriki atapaswa kujiandikisha kwenye kitabu maalum cha washiriki wa minada, baada yahapo atajaziwa ‘commitment form’ (fomu maalumu ya kushiriki mnada).

Baada ya hayo, vitambulisho vya mshiriki ikiwemo hati ya kusafiria (passport), leseni ya udereva na kitambulisho cha mpiga kura vitachukuliwa na kampuni.

Kila mshiriki halali atapaswa kulipa kiasi cha shilingi milioni 2 kupitia akaunti ya Yono ili kuthibitisha kuwa ana lengo la kushiriki. Kwa atakayeshinda mnada, fedha hizo (sh. 2 milioni) zitatumika kama sehemu ya malipo. Kwa ambao watakosa basi fedha zao zitarudishwa hapo hapo.

Kwa watakaoshiriki kuharibu mnada, hawatorudishiwa fedha hizo na watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Kwa mshindi atakayepata nyumba atatakiwa kulipa hapohapo 25% ya gharama yote ya nyumba na 75% ya gharama inayobaki atapaswa kulipa ndani ya muda wa siku 14.

Yono Auction Mart wametoa onyo kubwa kwa watakaohusika kwa namna yoyote kuharibu minada hiyo kuwa watakamatwa na kufunguliwa kesi mahakamani kwa kuwa na nia ovu ya kukwamiha ukusanyaji wa kodi ya serikali.

Kuweni Makini Na Mchanga Wa Kaburini

$
0
0
KUWENI  MAKINI  NA  MCHANGA  WA  KABURINI
IMESIMULIWA  NA.DOKTA  MUNGWA  KABILI…0744 000 473.

 Kuna  watu  wamepata  nuksi, mikosi  na mabalaa  makubwa katika  maisha  yao  kwa  sababu  ya  matumizi  ya  mchanga  wa  makurini  bila  kuzingatia  au  kufuata  maelekezo.

Unapokuwa  unafanya  kitu chochote  kile  kinacho  husiana ama  kuyahusisha  makaburi  kwa  namna  moja  au  nyingine  iwe  ni  kutumia  mchanga , kuzika  vitu, kuoga, kuchoma  ama kutambika, unatakiwa  kuwa makini  sana  na  kufuata  na  kuzingatia  kanuni  na  taratibu  zake  kwa  sababu  usipo  zingatia  hayo  yatakupata  makubwa.

Kwa  bahati  mbaya  sana  watu  wengi  wamekuwa  wakitumia  mchanga  wa  makaburini  bila  kufuata    taratibu  na  matokeo  yake  wamevaa nuksi,mikosi  na  mabalaa  makubwa  ya maisha.

Sio  makaburini  tu, bali  hata  katika maeneo  mengine ambako  mchanga  umekuwa  ukitumika katika  shughuli  za  uganga  na  utabibu  watu  wamekuwa  wakitumia  ndivyo  sivyo  na  matokeo  yake  wamekuwa  wahanga  na  nuksi, mikosi na  mabalaa.

Mfano mzuri  na  rahisi  wa  sehemu  hizo  ni  NJIA  PANDA.  Watu  wengi  huwa  wana  enda kutupa, kuzika, kufukia, kuchoma  vitu  au  kuoga  njia  panda  bila  kuzingatia   taratibu  sahihi.

Huwa  nasikitika  sana  ninapokutana  na  vitu  vimetupwa  au  kuchomwa  NJIA  PANDA  DUME  wakati  vilitakiwa  vifanyike   NJIA  PANDA  JIKE.

Kwa  wasio  fahamu  , njia  panda  huwa   zipo   za  aina  kuu  mbili  ; Njia  panda  inayo  unganisha  njia  tatu  na  nyingine  ni  njia  panda  inayo  unganisha  njia  nne. Kati  ya  aina  hizo  mbili  za  njia  panda, moja  huwa  ni  njia  panda  dume  na  nyingine  ni  njia  panda  jike.  Kwa sababu za  msingi  sitaweka  wazi  ipi  ni  njia  panda  jike  na  ipi  ni  njia  dume.   Aina hizi kuu  mbili  zap  njia  panda nazo  zimegawanyika  katika  aina  mbalimbali.

Njia  panda  hizo  kila  moja  ina  matumizi  yake  ambayo  yapo  tofauti  na  aina  nyingine. Kufanya  kitu  ulicho  takiwa  kukifanya  kwenye  njia  panda  dume  wewe  ukaenda  kukifanya  kwenye  njia  panda jike  ni  makosa  makubwa  sana  na  madhara  yake  yaweza  kuwa  nuksi, mikosi,mabalaa  na  hata  kifo  cha  ghafla.

 Nirudi  kwenye  mchanga  wa  kaburini.   Toka  enzi  za  mabibi  na  mababu  vitu  vinavyo  tokana  na  kuhusiana  na  maeneo  ya  kaburini  vimekuwa  vikitumika  katika    uganga  na  uchawi  yaani  wachawi  wamekuwa wakivitumia  kwa  ajili  ya  kuwatengenezea  watu  matatizo  ilihali  waganga  wamekuwa  wakivitumia  kuwakinga  na  kuwaondolea  watu matatizo.

Moja  kati  ya  vitu  vinavyo  tumika  sana  katika  uganga  na  uchawi  ni  mchanga  wa  kaburini.

Watu  wengi  wamekuwa  wakitumia  mchanga  wa  kaburini  ndivyo  sivyo  na  badala  yake  wameishia  kupata  nuksi,  mikosi  na  mabalaa  makubwa  katika  maisha  yao.

Mchanga  wa  kaburini una  matumizi  mengine  sana  kuanzia   kuwatia  watu  nuksi, mikosi  na  mabalaa  hadi  kuwafungua  watu  kutoka  kwenye  vifungo  vibaya  na  kuwaletea  bahati.

Mchanga  wa  kaburini  una  matumizi  mengi  mazuri  kwa  mabaya  lakini  mazuri  ni mengi  kuliko  mabaya.

Wachawi  wanau  tumia  kuwafisadi  watu  na  waganga  wanautumia  kuwakinga  watu  dhidi  ya  shari  za  wachawi  na  majini  wabaya.

Kama  nilivyo dokeza  hapo  juu  mchanga  wa  kaburini  unatofautiana  matumizi.  Aina  ya  matumizi  ya  mchanga  wa  kaburini  hutegemeana  na mchanga  huo  umechukuliwa  kutoka  kwenye  kaburi  la  aina  gani  na  lenye  asili  gani.

Katika  ulimwengu  usio onekana  zipo  aina  za  makaburi  zaidi  ya  sabini  na  kila  aina  ina  matumizi  yake.  Sitazitaja  aina  hizo  za  makaburi  na  matumizi  ya  kila  aina  kwa  sababu  najua  wapo  wachawi  watatumia  maarifa  hayo  kuwafanyia  ubaya  watu  wengine.

Matumizi  ya  mchanga  wa  kwenye  kaburi  la  kale  ambalo  limeshasahaulika  hayawezi  kuwa  sawa  sawa  na  matumizi  ya  mchanga  wa  kaburi  la mtoto  alie zaliwa  akiwa  amekufa.

Matumizi  ya  mchanga  wa  kaburi  lililozama  na  kutitia  hayawezi  kuwa  sawa sawa  na  matumizi  ya mchanga ulio chukuliwa kutoka  kwenye  kichuguu  kilicho  mea  kwenye  kaburi. Hivi  ni  vichuguu  vidogo  ambavyo  humea  kwenye makaburi  na  husababishwa  na  wadudu  fulani  wa  porini  wanao  fanana  sana  na  panya.

Mchanga  kutoka  kwenye  kaburi  la  aina  fulani  unaweza  kuwa  na  matumizi zaidi  ya  kumi, yote  yanaweza  kuwa  mabaya  au  mazuri  au  mchanganyiko   wa mabaya  kwa  mazuri. Kinacho  takiwa  kuzingatiwa  hapo  ni  elimu  na  maarifa  aliyo  nayo  muhusika  kuhusu  mchanga  wa  kaburini. Kwa  sababu  sio  rahisi  kwa  mtu  asie  na  maarifa  haya  kujua  ni  mchanga  upi  wa  kaburi  unatumika  katika  mambo  yepi.

Mchanga  ulio  patikana  kwa  kufagia  makaburi  hauwezi  kuwa  na  matumizi  sawa  na  mchanga  ulio  chukuliwa  kutoka  kwenye  kaburi  lililo  lala  wazi, au  kaburi  ambalo lilichimbwa  tu  halafu hakuzikwamo  mtu  au  kaburi  ambalo  mchanga  ulichukuliwa  wakati  maiti  inazikwa  au kabla  maiti  haijshushwa  kaburini.

Wakati  mwingine  mchanga  wa  kaburini  unaweza  kuwa  umechukuliwa  kwenye  kaburi  moja  na  ukawa  na  matumizi  tofauti  kabisa  tena  yanayo  kinzana.

Kwa  mfano  kuna  aina  fulani  ya  kaburi, ukichukua  mchanga  kwenye  sehemu  ya  moyo  ya  kaburi  hilo  matumizi  yake  huwa  tofauti  na  kinyume  kabisa  na  mchanga  ulio  chukuliwa  kwenye  sehemu  ya  kichwa  cha  kaburi  hilo.

Wakati  mchanga  ulio  chukuliwa  kutoka  kwenye  sehemu ya  moyo  ya  aina ya  kaburi  nililo  litaja  hapo  juu  ukitumiwa   na  baadhi  ya  watu  kuoshea  vyombo  kwa  ajili  ya  kuvuta  wateja  kwenye  biashara  ya  chakula   au  kuwatuliza  wafanyakazi  wasiondoke , wachawi  wanatumia  mchanga  ulio  chotwa  kutoka  kwenye  miguu  ya  kwenye  kaburi  hilo  hilo kupima  nguvu ya  kinga  kwenye  nyumba  ambayo  wanataka  kwenda  kuiwangia.

Wachawi  wanapoenda  kuroga  kwenye  nyumba  wasio  ifahamu  vizuri  ili kujua  nguvu  ya kinga  iliyopo   katika  nyumba  hiyo  huwa  wanatumia  mchanga  huo  wa  kaburini . Wanacho  kifanya  husubiri  hadi giza  lizame  majira  ya  saa  moja  za  usiku, mchanga  utarushwa  kwenye  paa  la  nyumba. Ukisikia  paa  lenu  la  nyumba  limetupiwa  mchanga  mida  ya  saa  moja  za  usiku  basi  jua  wanga  walikuwa  wanapima  nguvu  ya  kinga  ya  nyumba  yenu  na  kama  wakijiridhisha  ninyi  ni  wepesi  basi  usiku  wa siku  hiyo  watakuja  kuwanga na  kuroga .

Katika  kupima  nguvu ya  kinga  ya  mji, kuna  vitu  huwa  wanavitazama  baada  ya  kutupa  mchanga  huo. Wakitupa  mchanga  halafu  zikatokea  cheche  za  moto  juu   ya  bati  basi  siku  hiyo  hawatokuja, watarudi  kujipanga  na  kuja  na  nguvu  zaidi, na  zisipo tokea  cheche  za  moto  basi  wanajua  mji  huo  ni  mwepesi, usiku  wa  siku  hiyo  watakuja  kuwanga.

Katika  uganga  na  uchawi, mchanga  wa  kaburini  huangaliwa  na  kutazamwa  katika  uwanja  wake  mpana. Haungaliwi  tu  mchanga  ambao  umechotwa, umechukuliwa, au  umeombwa  kutoka  kaburini, bali  hata  mchanga  uliokuja  ( ulio lazimisha ) wenyewe nyumbani  kutoka  kaburini

Ngoja  nifafanue  kidogo  hapo, ninaposema  mchanga  uliokuja  wenyewe  nyumbani  kutoka  kaburini  ninamaanisha  mchanga  ulio fika  kwenye  mji  wako  kutoka  kaburini  bila  wewe  mwenyewe  kujua wala  kupenda.Hapa  ni pale  unapokuwa  umeenda  kaburini eidha  kushiriki  katika  uchimbaji  wa  kaburi  au  kusafisha  kaburi  halafu  mchanga  ukabaki  kwenye  viatu  vyako  na  wewe  bila  kujua  ukarejea  nao  nyumbani  kwako  na  hatimaye  mchanga  ukabaki  kwenye  viatu  vyako.  Katika  uganga  na  uchawi  hicho  ni  kizimba  cha  hatari  sana. Mtu akichukua  mchanga  huo  anaweza  kufanya  kitu  kibaya  sana  dhidi  yako. Ndio  maana  mnashauriwa  unapoenda  makaburini  nenda  na  ndala  na  ukitoka  unawe  vizuri.  Kikubwa  usitengeneze  mazingira yatakayo  kufanya uingia  nyumbani  kwenu/kwako  na  mchanga  wa  kaburini.

Vile  vile  ipo  aina  moja  ya  mchanga  wa  kaburini  ambayo  nayo  ina  matumizi mengi  sana  makubwa  kwa  madogo  mazuri  kwa  mabaya . Huu  ni  mchanga  uliopo  katika  eneo  linalo  tumiwa  na  wafu  na  watu  walio  hai  kwa  wakati  mmoja.  Kama  hujaelewa  nazungumzia  kitu  gani, nazungumzia  Mchanga  uliopo  kwenye  daraja  linalo  tumika  kuwavusha  wafu  na  walio  hai  kwa  pamoja.  Hapa  nazungumzia  madaraja  yaliyo karibu  na  makaburi  ambayo  watu  wakiwa  wanawapeleka  marehemu  wao  kuwazika  lazima  wayavuke.     Huu  ndio  aina  ya  mchanga  ninao  uzungumzia. Katika kuonyesha  kuwa  mchanga   wa  aina  hii  una  nguvu  sana, hata  yale  maji  yanayo  patikana  chini  ya  daraja  hili, nayo huwa  na  nguvu  ileile  ya  mchanga  na  huwa  na  matumizi mengi mabaya kwa  mazuri.

Kwa ufupi  mchanga  wa  kaburini  una  matumizi  mengi  sana  kuanzia  kuvuta  heri  na  bahati, kuongeza  mvuto  wa  mapenzi,  kufungua  vifungo  vibaya  hadi  kuwatia  watu  nuksi, mikosi  na  mabalaa.

MAMBO  YA  KUZINGATIA  KABLA  YA  KUTUMIA  MCHANGA  WA  KABURI  AU  KUFANYA  TAMBIKO  LOLOTE  KABURINI.

1. Kwanza  lazima  ujue aina  ya  kaburi  ambalo mchanga  wake unaendana na  tatizo lako  au jambo  unalo  litaka.

2. Pili  lazima  ulijue  lango  kuu  la  kiroho  la kuingia  kwenye  eneo  la  makaburi  husika. Lango  kuu  la kiroho la  kuingia  kwenye  makaburi  husika  huwa   lipo katikati  ya  makaburi. ( Usichanganye  na  mlango  unao  onekana  kwa  macho  hususani  kwenye  makaburi  yaliyo jengewa  uzio na  kuwekewa  mageti )

3. Pili  unapoingia  kaburini  lazima  uanze  kwa  kumlipa   mlinzi  wa  lango  kuu  la  kaburi. Ninaposema  mlinzi  wa  lango  kuu  la  kaburi  simaanishi  mtu  anaelinda    geti  kwenye eneo  la  makaburi  hususani  yale  makaburi  yaliyo  jengwa  kisasa  .HAPANA   simaaninishi  hivyo. Nina  maanisha  “mlinzi  wa  kiroho “  wa  makaburi.   Kwa wasio fahamu  ni  kwamba  katika  kila  eneo  la  makaburi  huwa  kuna  jinni /malaika  mwenye  dhamana  ya  kulinda makaburi  hayo. Ili uweze  kuchukua au kufanya  chochote  chenye  manufaa  kutoka  ndani  ya  eneo  hilo  la  makaburi  ni  lazima  kwanza  upate  ridhaa  yake. Unapata  ridhaa  yake  kwa  kumlipa.  Walinzi  wa  makaburi  huwa  wanalipwa  kwa  sadaka  maalumu ambayo  hulingana  na siku  na  muda  ulioenda  lakini  katika  vitu  vyote  hivyo  lazima  kuwepo  na  mvinyo.

4. Unapoenda  kuchota  mchanga  wa  kaburi  husika  kwenye eneo  husika hakikisha  kwanza  unamuomba  alie  lala  kwenye  hilo  kaburi  na  KUMLIPA!  Hawa huwa  wanalipwa  kama  wanavyo  lipwa  walinzi  wa  makaburi.  KAMWE  USICHUKUE  MCHANGA  BILA  KUWEKA  SADAKA   KWENYE  KABURI  HILO KWA  SABABU  HUO  MZIMU  UNAO  ENDA  KUUTUMIA  KWENYE MAMBO  YAKO  HAU UTEKI  NA  KUULAZIMISHA  KUFANYA  UNACHOKITAKA  WEWE  BALI  UNAUOMBA  NA  KUUPA  ZAWADI  MAALUMU. MIZIMU  NI  TOFAUTI  SANA  NA  MAJINI.USIPOWEKA  SADAKA  MZIMU  HUO  UTAKURUDIA  WEWE  NA  KUKUDHURU  AU  UTAFANYA  KINYUME  CHA  KILE  ULICHO KUSUDIA  UKUFANYIE.

5. Hakikisha  unachota  mchanga  wako  katika  eneo  husika  unalo  takiwa  kuchota. Kamwe  usichote  katika  eneo  ambalo  halihusiani.

6. Kitu kingine  lazima  uzingatie  muda  wa  kwenda  kuchukua  mchanga  wa  kaburi. Kila aina ya mchanga  wa  kaburi  una  muda  na  wakati  wake  maalumu  wa  kwenda  kuuchukua. Hivyo  unatakiwa  kuzingatia  hilo  pia  kabla  ya  kwenda  kuchukua  mchanga  wa  kaburi.

KITU  CHA  MSINGI  UNATAKIWA  KUWA  NA HESHIMA  YA  HALI  YA  JUU MNO, KUWA  MSAFI  WA  MWILI NA  KULIPA SADAKA  STAHIKI  PINDI  UNAPOENDA  KUCHUKUA  MCHANGA  WA  KABURI.



 DOKTA. MUNGWA  KABILI  ANAPATIKANA  KWA   SIMU  NAMBA  0744 000 473.

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kifo cha Mzee Kleist Sykes

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia kifo cha Mzee Kleist Sykes kilichotokea jana tarehe 22 Novemba, 2017 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Rais Magufuli amesema amepokea taarifa za kifo cha Mzee Kleist Sykes kwa majonzi na huzuni hasa akikumbuka mchango mkubwa alioutoa katika ujenzi wa Taifa akiwa mmoja wa viongozi waliokuwa mstari wa mbele katika kupiga vita umasikini, kuilinda misingi ya uhuru na kujenga uzalendo kwa Watanzania.

Ameongeza kuwa Mzee Kleist Sykes na familia yake walijitoa kwa hali na mali kukijenga chama tangu TAA, TANU na baadaye Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kushiriki katika harakati kubwa za uhuru, kwa kuweka mbele maslahi ya Taifa licha ya changamoto mbalimbali walizokabilina nazo.

“Mchango wa Mzee Kleist Sykes na familia yake katika nchi yetu hautasahaulika, uzalendo wake utakumbukwa na kudumishwa na hakika kifo chake kimetuachia majonzi na huzuni hasa kwa kuwa kimetokea wakati ambapo busara zake bado zinahitajika”

“Nawapo pole wanafamilia, ndugu, jamaa, wana CCM, marafiki na wote walioguswa na kifo hiki, naungana nao katika majonzi na sala za kumuombea Mzee Kleist Sykes apumzike mahali pepo, Amina”

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

23 Novemba, 2017

Isaya Mwita: Sina Mpango wa Kuhamia CCM na Hakunaga Mkurya Msaliti

$
0
0
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amekanusha uvumi unaomhusisha na mipango ya kujiondoa katika Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM).

Mwita amesema lengo la uzushi huo ni kumchafua hasa kutokana na staili yake ya kazi ya kushirikiana na serikali badala ya kupambana katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali za kimeya.

Akisisitiza historia na utamaduni wa Mkurya ni kukataa kuwa msaliti akasema: “Naomba ifahamike kuwa hakuna Mkurya ambaye aliwahi kuwa msaliti katika nafasi yoyote ambayo aliwahi kuwa nayo. Kutokana na historia hiyo, naomba niaminike na wanachama na wananchi wote kuwa haitakuja kutokea Mkurya mimi nikakisaliti chama changu.

“Na kama itakuja kutokea nikafanya hivyo ninaweza kuhatarisha maisha yangu, familia yangu, na hivyo kujikuta nikiingia kwenye matatizo makubwa ambayo kimsingi siyo mazuri. Mama yangu ni mjane, kama itafanya hivyo Chadema wote Mkoa wa Mara hawawezi kuwaacha ndugu zangu salama”.

Meya huyo amesema hajawahi kudhani wala kufikiria kuhama Chadema na kwenda kwenye chama chochote cha siasa kwani ametoka nacho mbali tangu mwaka 2004 kwa kukijenga chama hicho kwa gharama zake mwenyewe ambapo anatambua kuwa chama kimemheshimu kwa kumpa nafasi ya umeya hivyo haoni sababu ya kuondoka kwani ana nia ya kuwatumikia wananchi.

“Kukaa kwangu kimya, kutofanya siasa za kiharakati ndani ya Jiji la Dar es Salaam haimanishi kwamba niko upande wowote ama kukihujumu chama changu. Ila huu ni mfumo ambao nimeuchagua na kujijengea kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na si kufanya harakati za kisiasa kwa kuwa nina nia ya kufanya maendeleo ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Katibu Mkuu CHADEMA: Sina Mpango wa Kuhamia CCM

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  Dkt. Vicent Mashinji amekanusha habari za kwamba anahamia Chama cha Mapinduzi na kusema kwamba yeye siyo mtu wa kuamini kwenye zidumu fikra za Mwenyekiti bali nguvu ya mamlaka ya umma.

Mashinji amesema kwamba yeye siyo mjamaa bali ni mlengo wa kipepari hivyo amewataka wananchi wawe na amani kuhusu hizo taarifa za yeye kuhamia CCM si za ukweli.

"Napokea simu nyingi eti nahamia CCM, mi si Mjamaa. Mi ni mlengo wa kibepari. Siamini kwenye “zidumu fikra za mwenyekiti” Ninaamini katika “nguvu na mamlaka ya umma”. Naomba ndugu zangu muwe na amani kabisa" Mashinji.

Dkt Mashinji ameongza kwamba "Nitaendelea kutumikia CHADEMA kwa makini na kutimiza ndoto za watanzania".
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images