Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Awabana Wakurugenzi Bukoba......Washindwa Kujibu Maswali Mbele ya Wananchi

$
0
0
Rais John Magufuli amewabana wakurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya na Manispaa ya Bukoba akitaka kujua matumizi ya fedha za mfuko wa barabara zilizopelekwa huku baadhi ya viongozi wakishindwa kutoa majibu.

Akizungumza leo  Novemba 6 ,2017 wakati wa uzinduzi wa mradi wa upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba, Mkoani Kagera Rais Magufuli amesema anashangazwa kuona viongozi aliowateua wanakosa majibu juu ya fedha za Serikali.

Kama ilivyo ada, Rais Magufuli ameanza kwa kuwaeleza wananchi juu ya mabadiliko aliyoyafanya tangu aingie madarakani ikiwamo udhibiti wa watumishi hewa na vyeti feki akisema mambo hayo yameigharimu nchi.

Baada ya kuzungumza masuala hayo aliwaita viongozi wa halmashauri ya Bukoba kwenye mkoa huo akitaka kueleza ni kiasi gani cha fedha za mfuko wa barabara walizopokea pamoja na matumizi yake.

“Serikali huwa inaleta fedha kwaajili ya maendeleo ya kila manispaa na hata hapa tumeshaleta,”

“Mkurugenzi wa Manispaa,tumeleta kiasi gani hapa? bajeti ya manispaa ya Bukoba ni kiasi gani?amehoji na kwamba anataka watu wajue matumizi yake.

Mkurugenzi wa manispaa hiyo Erasto Mfugale , amemueleza kuwa hadi sasa amepokea Sh33 bilioni ikiwa ni bajeti ya jumla huku akishindwa kutolea majibu fedha za mfuko wa barabara.

 “Katika fedha hizo kuna fedha ambazo ni mishahara ambazo ni mishahara Sh19 bilioni kwa mwaka,”amesema

Kabla hajamaliza, Rais alimuuliza “fedha za road fund (mfuko wa barabara)ni kiasi gani, nasema hivi kwasababu zinapoteaga poteaga tu nataka uziseme hapahapa,”amesisitiza

Mkurugenzi huyo ameshindwa kutoa majibu suala ambalo rais ameliita ni kucheza na fedha za Serikali.

Naye Mkurugenzi wa halmashauri, Mwantum Dau alivyosimama kutoa majibu alisema hakumbuki ni kiasi gani suala ambalo limeonekana kumkasirisha rais.

“Hapana mheshimiwa Rais labda aje mtunza hazina, mimi nina idara nyingi siwezi kukumbuka,” alisema

Rais amesema anashangaa kuona viongozi aliwateua hawajui kuhusu fedha za Serikali.

“Nani anafahamu hela za mfuko wa barabara manispaa ya Bukoba kwa sababu viongozi niliowateua hawajui,pengine naweza nikateua Mkurugenzi sasa hivi,”amesema

Meya wa Manispaa hiyo  Jerry Silaa  ndiye aliyewanasua viongozi hao baada ya kueleza jumla ya fedha Shmilioni700 za ujenzi wa barabara pamoja na Sh120 kwaajili ya maboresho.

Breaking News: Rais Magufuli Awatumbua Wakurugenzi Wawili Walioshindwa Kujibu Maswali Yake Bukoba

Serikali Yatangaza Kuongeza Mihahara ya Wafanyakazi na Kuwapandisha Madaraja Mwezi Huu

$
0
0
Serikali imesema itaongeza mishahara ya watumishi wake mwishoni mwa mwezi huu, sambamba na kuwapandisha madaraja kuanzia mwezi huu pia.

Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (Maelezo) na Msemaji wa Serikali, Dk. Hassan Abbasi, ndiye aliyetangaza neema hiyo kwa watumishi jijini Dar es Salaam jana alipokuwa akieleza mafaniko ya serikali ya awamu ya tano kwa kipindi chake cha miaka miwili.

Dk. Abbasi alisema mwishoni mwa mwezi huu, serikali itawaongeza mishahara watumishi wake pamoja na kuwapandisha madaraja.

"Mwezi huu tutawaongezea mishahara wafanyakazi na watumishi wa serikali watapanda madaraja na watalipwa stahiki zao," alisema Dk. Abbasi.

Kupandishwa mishahara na madaraja kwa watumishi wa umma kulisitishwa na serikali Machi mwaka jana ili kupisha uhakiki wa watumishi hewa na wafanyakazi wenye vyeti feki.

Oktoba 14, mwaka huu visiwani Zanzibar, wakati wa kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru na maadhimisho ya miaka 18 ya kifo cha Mwalimu Nyerere, Rais John Magufuli alisema serikali yake itawapandisha vyeo na kurekebisha mishahara ya watumishi 59,967 baada ya kumalizika kwa uhakiki wa vyeti feki na watumishi hewa.

Rais Magufuli katika hotuba hiyo siku hiyo, alitolea mfano uzalendo wa Baba wa Taifa ambaye wakati wa uhai wake aliamua kupunguza mshahara wake na kukataa kuongeza mishahara ya watumishi wachache huku walio wengi wakipata shida.

“Ninaposema hivyo simaanishi kuwa mishahara isiongezwe. La hasha! Ninachosema ni kwamba kabla ya kudai nyongeza ya mishahara ni lazima kwanza kufahamu uwezo wa serikali, lakini pia tutambue kuwa kuna Watanzania wenzetu wengi tu wanaohitaji kuboreshewa huduma," alisema.

Rais Magufuli aliongeza: "Baada ya kukamilisha zoezi la uhakiki wa watumishi hewa na vyeti feki, Serikali imewapandisha vyeo na kuwarekebishia mishahara watumishi 59,967 ambapo kiasi cha Sh. bilioni 159.33 zimetengwa kwenye bajeti ya mwaka huu na mishahara mipya itaanza kulipwa kuanzia mwaka huu."

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatibu Tatizo la Kutohika Mimba, Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Pete za Bahati

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Novemba 7

Dk Kigwangalla afuta vibali vipya vya uwindaji vilivyokuwa vianze Januari 2018

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla Oktoba 22,2017 alitoa kauli ya kufuta vibali vyote vya uwindaji kwa kampuni na kutoa siku 60 kwa watendaji ili waratibu mchakato upya utakaowezesha vitalu kugawiwa kwa mnada.


Jana Jumatatu Novemba 6,2017 kupitia mitandao ya kijamii Dk Kigwangalla ametoa andiko linalosomeka ifuatavyo:

KWA UFUPI: Kuhusu Vitalu vya Uwindaji

Na Dkt. Hamisi Kigwangalla

Nimefuta vibali vipya vya uwindaji vilivyokuwa vianze Januari 2018. Nitatangaza upya mchakato mpya wa ugawaji vitalu kwa njia ya mnada - sasa hivi wataalamu wetu wanatengeneza utaratibu utakaotumika kuuza vitalu kwa njia ya mnada wa wazi. Pia, tunarekebisha sheria na kanuni kabla ya kuanza mchakato mpya. Hivyo waliokuwa na vibali vya zamani, uhai wake unaisha Disemba 31.

Kimsingi mchakato wa vibali nilivyovifuta haukuwa halali kisheria, ulijaa rushwa na upendeleo na haukuwa wa kimkakati, sababu Mpango wa Taifa wa miaka mitano (2016 - 2021) unaelekeza twende kwenye njia ya mnada, BRN inaelekeza twende kwenye njia ya mnada!

Wataalamu walifaidika na utaratibu wa zamani - hawa walifanya tathmini ya nani 'ameendesha kitalu vizuri, nani ameendesha vibaya, hivyo wapendekeze kwa waziri nani apate nani akose' (hapa kulikuwa na watu walitoa rushwa mapema kabisa ili kujihakikishia wanapata vitalu; wanasiasa hususan Mawaziri waliokalia hiki kiti zamani nao walifaidika na utaratibu huu wa zamani (uliweka mazingira rahisi ya kuamua nani apate nani akose, na maamuzi haya yalikuwa kwenye kichwa cha Waziri pekee - hapo mazingira ya rushwa na upendeleo yalikuwa rahisi kabisa), wafanyabiashara na wawekezaji kwenye sekta hii ya utalii wa uwindaji walikuwa wafaidika wakubwa sababu walitupunja mapato ya ushuru (nchi zingine kitalu kidogo tu kiliuzwa mpaka Dola 2,000,000, sisi tuliambulia Dola 60,000 tu.

Wanasiasa na watu wajanja wanaojiita wazawa, ambao hata hawana weledi wala uwezo wa kuwinda, walikuwa wakichukua vitalu (kwa ushawishi wao kwa Waziri) kisha wanakikodisha kwa waendeshaji wa nje. Wengi walidai pango la hadi Dola 300,000 kwa mwaka, huku wao wakilipa serikalini Dola 60,000 tu.

Utaratibu huu wa zamani uko kinyume kabisa na tafiti mbalimbali zilizofanyika miaka ya mwishoni mwa tisini na mwanzoni mwa miaka ya 2000. Leo zaidi ya miaka 20 hakuna aliyethubutu kubadilisha utaratibu. Sababu kubwa ni syndicate ya wanufaika, tena wachache wale wale tu. Ikawa maeneo haya wamejimilikisha kama yao milele.

Uamuzi wangu kuufuta utaratibu huu ni dhahiri umewaudhi wengi na najua watanishambulia sana. Naombeni dua zenu. Tanzania ilihitaji mmoja wetu afike mahali aseme 'sasa basi' na tutake tusitake iwe hivyo, Rais Magufuli amejitoa, Mimi namuunga mkono kwa 'vitendo', nasema sasa basi! Nitamsaidia kazi hii kwa uaminifu, uadilifu, uzalendo na weledi wa hali ya juu. Si amenipa kazi, kazi nitafanya! Dua zenu tu.

Nape: CCM ikikataa kuambiwa ukweli ndiyo mwanzo wa kuanguka

$
0
0
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye ameonya kuwa endapo chama hicho hakitataka kuambiwa ukweli na kukosolewa, utakuwa mwanzo wa kuanguka kwake.

Nape aliyewahi kuwa katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho, amesema endapo CCM itaua utamaduni wa kukosoana kupitia vikao itapoteza mwelekeo.

“Hiki chama tukifika mahali tukaanza kufanyiana unafiki kwamba hatutaki kuambiana ukweli tunapokosea utakuwa ndiyo mwanzo wa kuanguka kwa CCM.”

Amesema hayo juzi nyumbani kwake eneo la Kisasa mjini Dodoma katika mazungumzo maalumu na Mwananchi.

Nape ambaye leo anatimiza miaka 40 ya kuzaliwa, ameeleza kusikitishwa na namna ya baadhi ya watu aliowaita “vijana wa CCM”, kupotosha kwa makusudi kauli na ujumbe wake anaoutuma kupitia mitandao ya Twitter na Instagram.

“Kuna ambao wanamchukia tu Nape kwa sababu wanadhani alishiriki kuzuia wagombea wao na hasa hawa vijana wafuasi wa Edward Lowassa ambao bahati mbaya alipohama hawakuhama naye,” alisema.

“Hawa nao wako wanapitia humo kusema hasira zao. Mara Nape huyu anamsema Rais. Unamuona Nape huyu anaisema Serikali. Hawa nao tuwapuuze. Wakikua wataacha.

“Wanaona Nape ni beki mzuri wa kufanyia mazoezi au ya kuonekana wapo ili tu wapewe vyeo. Bahati nzuri mimi nimekulia ndani ya CCM najua lipi zuri na lipi baya kwa CCM,” alisema.

Mbunge huyo alisema husikitika anaposoma namna kauli zake zinavyopotoshwa, huku wengine wakidai anatumia maneno makali kwa vile ameondolewa kwenye uwaziri alikokuwa waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Nape alisema, “Hakuna jambo ambalo nimelisema kwenye Twitter na Instagram ambalo halifai kusemwa. Wakati mwingine nina maneno magumu kwenye vikao. Ninaamini kwenye hayo maneno magumu ndiko ambako tutakijenga chama chetu,” alisema.

Alisema akiwa katibu wa itikadi na uenezi kuna vikao vilifanyika mpaka saa sita usiku na alikuwa mkorofi kidogo kwa sababu maneno yake wakati mwingine yalikuwa magumu.

“Namshukuru sana Kikwete (Rais mstaafu Jakaya) amenilea na amenivumilia wakati mwingine, maana sarakasi nyingine na ujana huu amenivumilia sana,” alisema.

Alisema, “Katika watu wenye moyo wa ajabu sana ni Rais Kikwete (mstaafu). Katibu mkuu wetu (Abdulrahman) Kinana naye ameni shape (nijenga) sana kunivusha kutoka ujana hadi kukomaa.

“Lakini nasema lazima CCM ijenge utamaduni wa kukosoana na kujikosoa ili tuende mbele. Tukiua huo utamaduni tutakifanya hiki chama kitapoteza mwelekeo. Tuujenge kwa nguvu kubwa.”

Akizungumzia aina ya maneno anayoyatumia kufikisha ujumbe kupitia Tweeter, Nape alisema ujumbe mzuri ni ule ambao ukiwekwa unafikirisha na unamfanya mtu kueleza namna alivyouelewa.

“Tweet nzuri ni ile ambayo ukiiweka inafikirisha. Tweet nzuri ya mtu aliyetumia akili, ya mtu msomi huweki tweet ambayo kila mtu akisoma umeandika shikamoo baba. Inatakiwa iwe ambayo mtu akisoma anafikiria na anapata hamu ya kuitafakari. Nafurahi sana kwa sababu Tweet zangu zinasumbua akili wakati mwingine wanapata majibu tofauti tofauti.

“Wengine wananitukana wengine wananituhumu. Kwenye Tweet zangu hizi kwa sehemu kubwa watu wanapotosha na wanaopotosha wamegawanyika katika makundi mawili. Kuna ambao hawamjui Nape na hao ndiyo wale wanaosema Nape toka (tangu) ametoka uwaziri ana tweet hivi lakini nimekuwa nikiwauliza kwani kabla sijawa waziri, sijawa katibu mwenezi sikuwa nasema?”

“Wanasahau mimi niliwahi kumnyoonyeshea kidole waziri mkuu wa Tanzania hadharani nikasema wewe fisadi. Leo wanasema Nape anasema maneno makali sana! Hivi kuna maneno makali zaidi ya kumnyooshea waziri mkuu wa nchi ukasema hapa kwenye mradi huu umefanya ufisadi?

“Hawajui mimi ndiye niliyesimama Songea nikasema Kikwete kuna mawaziri wako hapa ni mizigo. Hivi kuna kauli kubwa ya kufikia hapo?

“Mtakumbuka niliwahi kusimama kwenye mkutano wa hadhara lakini mtakumbuka nilikwenda Arusha nikamwambia Lazaro (Nyalandu) nenda katimize wajibu wako acha kuweka watetezi”.

Afikiria kujitoa mitandao ya kijamii
Akizungumzia mkanganyiko wa namna watu wanavyopotosha ujumbe mbalimbali, Nape alisema, “Pengine nitoke kwenye social media (mitandao ya kijamii) sababu unaona kila mara uki-post (kutuma) jambo ooh linakuwa kubwa sana.

“Tena wakati mwingine ni jambo la utani sana. Kwa mfano siku moja nimeangalia kipindi kwenye televisheni wanasema mara paap na mimi nikaweka mara paap.

“Nilipoweka mara paap, wakaanza mara paap kahama CCM mara paap kafanya hivi, unakaa unasema kwa nini wanafikiria negative (mabaya) kwa nini hawafikirii positive (mazuri)?”

“Kwa nini hawasemi mara paap ameimarisha chama... Ukiyaona haya naanza kutafakari seriously (makini) umefika wakati nisimame kidogo hii social media.”

Hata hivyo alisema anaona akifanya hivyo atawapoteza wafuasi wake zaidi ya 200,000 walioko Tweeter na maelfu walioko Instagram na ndiyo maana anajiuliza kwa nini atoke kwa sababu ya wapuuzi wachache?

Mbunge huyo wa Mtama alisema pamoja na watu kutafsiri tofauti na kupotosha maana halisi ya ujumbe wake, hajawahi kuitwa na chama chake kuhojiwa.

“CCM ni chama kikubwa sana na mimi nimekaa humu zaidi ya miaka 10 nikiwa mtumishi ukiacha miaka 20 nikiwa mwanachama. CCM ninaijua. Ninajua jambo gani baya na jambo gani zuri.

Hata Nyerere aliiokosoa CCM
Alisema si dhambi kuikosoa CCM ikiwa tu dhamira inakuwa ni kuijenga na kuiimarisha na kwamba hata Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere alikuwa akiikosoa.

“Mwaka 1995 wakati mwalimu anazunguka kumnadi (Benjamin) Mkapa alikuwa anasema CCM kokoro hili limebeba watu wote kuna wengine humu nikijiuliza inakuwaje tuko chama kimoja nao. Yalikuwa maneno makali. Alienda Musoma pale akasema nyie CCM mmesimamisha mgombea wenu pale mla rushwa. Huyu mimi sitampigia kura nitampigia yule wa NCCR-Mageuzi.”

“Hivi kuna maneno makali nimeyasema kuliko haya? Mwalimu alisema maneno makali sana, lakini akasema kuna maneno ya uongo? Ni lazima tujenge utamaduni wa kukosoana ili kujenga”

Mbunge huyo alitumia mahojiano hayo kumpongeza Rais Magufuli kwa kutimiza miaka miwili madarakani, lakini akasema upo mjadala wa namna anavyotekeleza ilani ya CCM.

Nape alisema yote yaliyoingizwa katika ilani ambayo Rais Magufuli anaitekeleza kwa mafanikio, yalitokana na ziara yake yeye na Kinana iliyowachukua miezi 36 ya kukiimarisha CCM.

“Tulipokuwa tunazunguka yapo mambo mengi tuliyasema. Yale ndiyo yalikuja kuzaa ilani ya uchaguzi ya CCM (2015-2020). Yale ndio yalikuja kuzaa mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Tano.

“Sasa hapa tunapotimiza miaka miwili, ukifanya tathmini mambo mengi anayoyafanya Rais Magufuli pamoja na kumpongeza kwa kufikisha miaka miwili, ni yale ambayo tuliyaweka kwenye ilani.”

Alisema walipozunguka mikoani, wananchi walilalamikia kuhusu kuporomoka kwa nidhamu ya utumishi wa umma, wingi wa sherehe za kitaifa, mikataba mibovu ya madini na rushwa.

“Shida ya nidhamu katika utumishi wa umma ilikuwa kubwa. Tuliikuta kila mahali. Hili ni jambo moja Rais Magufuli amelisimamia vizuri,”alisema.

Aliyataja maeneo mengine ambayo alisema Rais ameyasimamia vizuri kuwa ni kudhibiti matumizi ya Serikali, kusimamia sera ya uchumi wa viwanda na kushughulikia migogoro ya ardhi.

Maeneo mengine ambayo alisema Rais amewafurahisha Watanzania ni kuondoa utitiri wa kodi kwa wakulima, kudhibiti rasilimali ya madini na kusimamia masilahi ya watumishi wa umma.

“Kwa hiyo amefanikiwa kugusa kila mahali lakini mjadala uliopo ni namna anavyoyatekeleza haya mambo. Hapa ndipo palipo na mjadala na watu wengi wanazungumza hapo.

“Hili mimi sitegemei watu wote watakubaliana. Wako wanaodhani angeenda taratibu kidogo, wapo wanaodhani akaze zaidi, wapo wanaodhani afinye zaidi na wako wanaodhani aende mdogomdogo.”

Nape alisema hakuna ubishi nchi ilikuwa katika matatizo makubwa ya rushwa na watu walitamani kupata kiongozi ambaye hataona aibu hata akimkuta rafiki yake anafanya ufisadi amshughulikie.

“Tunadhani Magufuli ameanza vizuri. Mjadala utakuja tu hivi katika utekelezaji pengine tupunguze mwendo, twende kasi zaidi, tutumie busara zaidi, tutumie upole fulani hivi. “Huu ndiyo mjadala ambao upo ambao nadhani si mbaya lakini sio ambao unapaswa kumrudisha nyuma. Kwa tathmini yangu mimi amefanikiwa kwa miaka hii miwili kutengeneza mwelekeo fulani.”

“Kitakachofuata sasa hapa ni namna ya kuboresha utekelezaji wa yale tulioyaweka kwenye ilani ya uchaguzi, yale ambayo ni matumaini ya Watanzania na yale ambayo tuliwaahidi,” alisema.

Ajibu kauli ya Nyalandu CCM kupoteza mwelekeo
Akizungumzia kauli ya Nyalandu kuwa CCM imepoteza mwelekeo, Nape alisema kwake anadhani huo ni mtizamo wake na wala hataki kupuuza mtizamo wake huo wala kuubeza.

“Na mimi naamini CCM haijapoteza mwelekeo na mtakumbuka haya maneno Nyalandu sio wa kwanza kuyasema. Aliwahi kuyasema Horace Kolimba miaka hiyo na bado iko madarakani”

“Aliwai kusema Kingunge Ngombale Mwiru kuwa CCM imeishiwa pumzi na bado inapumua. Haya maneno ni mitizamo ya watu na Nyalandu anayo haki ya kuwa na mtizamo wake,”alisema.

“Alipotoka nilisema hivi kwamba aliibua hoja sita ukiacha hiyo ya kupoteza mwelekeo. Nikasema hizi hoja zote alizoziibua zinazungumzika ndani ya chama chetu. Angeweza tu kuzileta tukajadiliana”.

Kwa sababu ukisema CCM imepoteza mwelekeo ukaandika paper (mada) ukaja nayo ndani vikao uka justify (ukaitetea) ndio njia bora ya kurekebisha chama na sio kuondoka,”alisema na kuongeza;-

“Ndio maana alipoondoka mimi nika tweet nikasema kama yapo mapungufu ndani ya CCM nitayashughulikia nikiwa ndani ya CCM”

“Mimi katika utumishi wangu ndani ya CCM yako mengi sana ambayo nimeyasukuma ndani ya chama na yametokea ikiwamo kuibadili kabisa ile idara ya itikadi na uenezi”.

“Ninaamini katika kuleta mabadiliko. Kila mmoja kwenye nafasi aliyopewa akijitahidi kuleta mabadiliko fulani CCM itabadilika. CCM ya leo sio CCM ya jana”.

“Ndio maana kuna kauli mbiu CCM Mpya, Tanzania Mpya. Tunapotaka kuijenga Tanzania mpya ni pamoja na fikra na mawazo. CCM mpaka leo haina mbadala kwababu ya mfumo wake”.

Nape alisema Chadema wamejitahidi kujenga msingi chini lakini wameshindwa na chama chao kimebaki ngazi ya kitaifa zaidi lakini CCM ina uongozi hadi chini ngazi ya balozi na shina.

“Lakini CCM balozi wa nyumba kumi anajijua ni CCM na ndio nguvu ya CCM ilipo. Hata uwezo wa kupanga. Ukitaka kuiua CCM lazima uue mfumo wake jambo ambalo haliwezekaniki,”alisema.

“Kusema CCM inapoteza mwelekeo ghafla sio sawa lakini kusema hakuna mapungufu nayo sio sawa. Yapo mapungufu yanashughulikiwa na yanaweza kumalizwa na vikao na mfumo wa chama”

“Haya mapungufu ambayo pengine Lazaro aliyaona au wengine wanayaona dawa sio kuyakimbia. Dawa ni kukaa kuyashughulikia. Wewe mwenzetu unayeona yanakukera sana lete hoja”

Nape alitolea mfano walipoingia kuwa Katibu Mwenezi, kulikuwa na kitengo cha propaganda kilichokuwa kikiongozwa na watu waliotoka upinzani ambacho alitoa hoja kikabadilishwa.

“Hiki kitengo kilikuwa kinaongozwa na Tambwe Hiza. Moja ya jambo ambalo lilikuwa linanikera sana ni kitengo hiki kuwa na historia ya kuongozwa na watu waliotoka upinzani”

“Hili lilikuwa moja ya jambo lilikuwa linapeleka sura mbaya kule nje. Nilipoenda nikasema lazima tutoe hii. Tukaondoa propaganda tukatengeneza mawasiliano na umma”

“Tukaweka mawasiliano sio propaganda tu, kikaongozwa na Daniel Chongolo kwa muda mrefu tu na akakijengea heshima kubwa sana na ndio hapo tukarudisha mahusiano na vyombo vya habari”.

Nape alisisitiza kuwa endapo kuna mwana CCM anayeamini katika itikadi yake anayaona mapungufu fulani, ongeza nguvu ya kuleta hoja za mabadiliko ndani ya chama na sio kukimbia.

Chanzo: Mwananchi

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Shughuli Za Mkutano Wa Tisa Wa Bunge


Tiba ya Asili ya Pumu, Vidonda vya Tumbo, Busha na Nguvu za Kiume

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wangu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Ile Tiba Sahihi Ya Matatizo Haya 

CHAZO CHAKE NA VISABABISHO VYAKE:
DALILI:-Mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata Choo vizuri hata ukipata Choo kinakuwa kigumu Kama cha mbuzi ,Misuri  kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. Miguu kuuma na kuwaka au kufa ganzi

TIBA YAKE:
RADI-90-POWER---Ni dawa ya vidonge asilia iliyo tengenezwa kutokana na miti shamba yenye uwezo mkubwa kabisa ktk kutibu matatizo (4) Kwa wakati ==>(1)Huongeza nguvu za kiume maradufu (2)kati ya umri (15-90)(3)hurefusha na kunenepesha uume mdogo kadrii upendavyo inch (6-8)kwa dakika (15)tu.(4)kuchelewa kufika kileleni (5)kuimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa. 

Nini huchangia kuwa na matatizo Kama haha? Kisukari,Presha,Ngiri,Zinaa,Kiuno kuuma, Tumbo kuunguruma na kujaa gesi,kutopata Choo vizuri, Mgongo kuuma. 

RADI-90-POWER:-Hutibu na kumaliza matatizo haya kwa mda mfupi tu na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika(45)kwa tendo(1) na utarudia Mara (5)na zaidi bila kuchoka huanza kazi baada ya dakika( 30)tu.Pia huongeza Hamu ya kufanya tendo la ndoa maradufu(2),Kumbuka tatizo hili si geni, kigeni ni tiba sahihi ya kutibu matatizo haya na pia ina guarantee ya miaka(65)na zaidi. 

Tunatibu :---Kisukari, Presha, uzazi, Ngiri, Pumu, maralia sugu, vidonda vya tumbo, chango aina zote, kifua kikuu na busha bila upasuaji. 

ITUJA NO2:--Nidawa ya mvuto wa biashara, kazi, kupandishwa cheo, kupendwa na mwajiri, kumvuta mme/mke,mpenzi, hawara, mchumba unaye muhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zake kwa dhati utampata kwa lisaa limoja (1)tu na atatulia daima na kumfunga asitoke nje ya ndoa.

BOMBA2:--Ni dawa ya kupunguza matiti makubwa, unene turbo, kitambi,mafuta mwilini,uzito,toa fangasi makovu, chunusi, nyama zembe, michirizi, kwa siku tatu (3)tu.NO7:--Inaongeza makalio, Hips, miguu kwa saizi uipendayo kwa siku (2)tu.

HUDUMA HIZI Na zingine nyingi UTAZIPATA popote TANZANIA Name NJE YA NCHI:--MUONE DR SHARIF AU PIGA SIMU NO:-0659347707, 0763483813 ,0688991509,0659347707.  DR SHARIF

Janeth Masaburi Aapishwa Rasmi Kuwa Mbunge

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amemuapisha  Janeth Masaburi kuwa mbunge. Janeth aliingia bungeni akisindikizwa na wabunge wanawake wa CCM.

Rais John Magufuli, Oktoba 21,2017 alimteua Janeth kushika wadhifa huo.

Janeth ni mke wa marehemu Dk Didas Masaburi aliyewahi kuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam.

Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Dk Masaburi aligombea ubunge wa Ubungo na kushindwa na Saed Kubenea wa Chadema.

Uteuzi wa Janeth umefanywa na Rais Magufuli kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1)(e) ya Katiba ya Tanzania inayompa mamlaka ya kuteua wabunge 10 na ulihitimisha nafasi hizo.

Wateule hao ambao ni mawaziri ni; Dk Philip Mpango (Fedha na Mipango), Profesa Palamagamba Kabudi (Katiba na Sheria), Profesa Joyce Ndalichako (Elimu, Sayansi na Teknolojia), Profesa Makame Mbarawa (Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano) na Dk. Augustine Mahiga (Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa).

Wengine walioteuliwa na Rais Magufuli ni Dk Tulia Ackson ambaye ni Naibu Spika wa Bunge, Salima Kikwete, Anne Kilango na Abdallah Bulembo.

Jeshi la Polisi Laichukua Simu ya Zitto Kabwe

$
0
0
Simu ya mkononi ya Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe imechukuliwa na vyombo vya dola kwa uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili.

Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini, anatuhumiwa kwa makosa ya sheria ya mitandao na takwimu.

Mbunge huyo leo Jumanne Novemba 7,2017 amefika kitengo cha uhalifu wa makosa ya kifedha kilichopo Kamata, Kariakoo jijini Dar es Salaam kujua hatima yake.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ofisi hizo, Zitto amesema, ''Nimeambiwa nirudi hapa Novemba 21,2017 lakini wamechukua simu yangu wanadai niliitumia kusambaza taarifa za takwimu nami nimewaachia kwa kuwa wana haki hiyo."

Amesema, "Kwa sasa sitapatikana, watu waliokuwa wananitafuta hawatanipata, kwa hiyo ndio hivyo wameamua wao lakini niwahakikishie tu kuwa mawasiliano niliyokuwa nayafanya yanalinda uhuru wangu wa Kikatiba."

Zitto amesema kabla ya kuwapatia simu walijadiliana kuhusu uamuzi huo lakini mwisho akaona awaachie wafanye wanavyotaka wao.

Amesema upekuzi pia utafanyika katika ofisi za ACT-Wazalendo na haijajulikana utafanyika lini.

Waliokosa mikopo watakiwa kukata rufaa

$
0
0
Mkurugenzi wa Bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HESLB), Abdul Razaq Badru amesema kuwa bodi hiyo itafungua dirisha la kukata rufaa kwa wanafunzi waliokosa mikopo ili waweze kupata haki yao.

Ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam wakati akifafanua vigezo na sifa za mwanafunzi kupata mkopo baada ya kuwepo kwa kasoro kadhaa kwa baadhi ya waombaji katika awamu ya kwanza ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza.

“Kwa wale wenye changamoto ndogo ndogo labda walikosea, tutatangaza dirisha la kukata rufaa mapema wiki ijayo na tutashughulikia watakaokamilisha vigezo watapata mkopo lakini wanatakiwa kuzingatia maelekezo tutakayoyatoa,” amesema Badru

Hata hivyo, mkurugenzi amesema katika majina ya waombaji waliyoyapokea na kuthibitishwa na TCU kwamba yamepata vyuo na wakayapitia wakajiridhisha hayana kasoro kwenye uombaji, tayari wanafunzi 29,578 wameshapata mkopo na wameanza masomo ambapo kiasi cha shilingi bilioni 96 zimetumwa vyuoni

Waziri Wa Afya Azungumzia Upungufu wa Dawa Nchini

$
0
0

Waziri wa Afya, Jinsia, watoto na wanawake Mheshimiwa Ummy Mwalimu, amesema kwa sasa nchi haina tatizo la upungufu wa madawa, kama ambavyo wengi wanadai.

Akijibu swali la Waziri Kivuli wa Afya, Mhe Dr Godwin Mollel Bungeni mjini Dodoma, na kusema kwamba serikali ya awamu ya tano chini ya Dk. John Pombe Magufui, imehakikisha imeongeza bajeti ya dawa ili kuinua sekta ya afya nchini.

“Kwanza nataka kumsahihisha waziri kivuli jambo moja, hakuna upungufu mkubwa wa dawa Tanzania, na kati ya jambo kubwa ambalo Rais amelifanya ni kuongeza bajeti ya dawa, tusikariri taarifa zilizopitwa na wakati, kama mnataka kumtendea haki Rais Magufuli, mtendeeni kwa kumpima ni kiasi gani amewekeza katika upatikanaji wa dawa”, amesema Waziri Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy ameendelea kwa kusema kwamba sasa hivi serikali imejidhatiti katika kuhakikisha inakabiliana na kutoingiza dawa ambazo zinakaribia kuharibika, na kuingia hasara kuziteteketeza huku ikisema changamoto kubwa huwa inajitokeza kwa dawa za misaada, kitu ambacho wameshaacha kufanya hivyo.

“Tanzania dawa zinazochina ni1.8% tuko chini ya kiwango cha kimataifa cha 5%, kuna tatizo kubwa la maoteo, watu hawaleti mahitaji halisi ya dawa, dawa nyingi zinazochina ni za misaada, unakuta tumenunua dawa za kutibu malaria, unaletewa tena dawa za misaada, tumechukua miongozo sasa hivi hatuchukui dawa za misaada ambazo zimekaribia kuharibika au tayari tunayo kwenye bohari yetu ya dawa”, amesema Waziri Ummy Mwalimu.

Majibu hayo yalikuja mara baada ya Mbunge Godwin Mollel kuuliza swali la nyongeza linalosema “katika nchi ambayo kuna upunufu wa dawa na kuna dawa zinaharibika huku tukitumia mabilioni kuteketeza, haoni kama kuna ufisadi unaofanyika?”.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Hotuba Ya Waziri Wa Fedha Na Mipango, Dkt. Philip Mpango , Akiwasilisha Bungeni Mapendekezo Ya Mpango Wa Maendeleo Wa Taifa Kwa Mwaka 2018/19

$
0
0
UTANGULIZI
1.    Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba, Bunge lako Tukufu likae kama Kamati ya Mipango ili kupokea na kujadili Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka 2018/19 na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka 2018/19.

2.    Mheshimiwa Spika, awali ya yote, naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima na afya. Aidha, tunamshukuru sana kwa kuendelea kulijalia Taifa letu amani na utulivu na kutuwezesha kukutana katika mkutano huu wa tisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kujadili namna ya kuharakisha maendeleo ya nchi yetu.

3.    Mheshimiwa Spika, kipekee napenda kumshukuru Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuniamini kuongoza Wizara ya Fedha na Mipango kufuatia mabadiliko aliyoyafanya hivi karibuni katika Baraza lake la Mawaziri na safu ya uongozi wa Mikoa. Aidha, ninawapongeza Waheshimiwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Wakuu wa Mikoa waliobakia katika nafsi zao na wale waliobadilishwa vituo vya kazi. Vile vile, ninawapongeza kwa dhati wote walioteuliwa kuwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Wakuu wa Mikoa wapya.

4.    Mheshimiwa Spika, naomba pia nitumie fursa hii adhimu kutambua na kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uongozi wake mahiri na makini katika kusimamia rasilimali za Taifa, kupambana na rushwa, kuimarisha nidhamu na uwajibikaji katika utumishi wa umma na zaidi ya yote, kwa moyo wake adili katika kupatia majibu kero za wanyonge. Hakika uongozi wake umezidi kuijengea heshima kubwa nchi yetu.

5.    Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii kumpongeza Mhe. Janeth Masaburi (Mb) aliyeteuliwa na Mheshimiwa Rais kuwa Mbunge katika Bunge lako Tukufu hivi karibuni kutoka Chama Tawala cha CCM. Aidha, nawapongeza kwa pamoja Waheshimiwa Alfredina Apolinary Kahigi, Kiza Hussein Mayeye, Nuru Awadh Bafadhili, Rukia Ahmed Kassim, Shamsia Aziz Mtamba, Sonia Jumaa Magogo, Rehema Juma Migilla na Zainab Mndolwa Amir walioteuliwa na Chama cha Wananchi - CUF kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ninapenda kuwakaribisha na kuwashauri watumie jukwaa hili kikamilifu katika kuishauri Serikali na kuwatumikia wananchi. Napenda pia kumpongeza Bw. Stephen Kagaigai kwa kuteuliwa na Mheshimiwa Rais kuwa Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

6.    Mheshimiwa Spika, ninawiwa pia kutoa shukrani za dhati kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji (Mb) na watendaji wote wa Wizara ya Fedha na Mipango wakiongozwa na Katibu Mkuu, Bw. Doto Mgosha James kwa ushirikiano walionipa katika maandalizi ya hotuba hii na vitabu vya Mapendekezo ya Mpango na Mwongozo. Aidha, ninawashukuru sana Wizara, Taasisi, Idara za Serikali, Sekta Binafsi na wadau mbalimbali waliotoa maoni na michango yao katika kukamilisha Mapendekezo ya Mpango na Mwongozo.


Malkia wa Tembo : “Kauli ya JPM ya ‘Hapa Kazi Tu’ haitekelezwi Mahakamani”

$
0
0
Raia wa China anayedaiwa kuwa malkia wa pembe za ndovu, Yang Feng Glan ameilalamika Mahakama kuhusu mashahidi wa upande wa mashtaka kutofika mahakamani licha ya kesi kupangwa kusikilizwa mfululizo.

Katika kuwasilisha malalamiko yake, amekariri kauli za Jaji Mkuu na Rais John Magufuli.

Yang ametoa malalamiko hayo leo Jumanne Novemba 7,2017 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Akizungumza lugha ya Kiswahili, amedai alisikia Jaji Mkuu akisema kesi za muda mrefu lazima zimalizwe mwaka huu. Yang amesema kesi yake huwa inapangwa kusikilizwa mfululizo lakini hilo halijawahi kufanyika hata mara moja.

"Rais John Magufuli anasema hapa kazi tu, nikasema sasa Mahakama ile kazi haipo kwa haraka, nipo mahabusu naumwa moyo najitahidi nakuja," amesema Yang.

Ameomba kesi ikipangwa mashahidi wafike mahakamani akihoji iwapo shahidi mmoja anaumwa, na wengine wote wanaumwa?.

Yang ameeleza hayo baada ya Wakili wa Serikali, Wankyo Simon kudai kuwa shahidi waliyemtarajia kutoka ushahidi bado anaumwa. Ameomba shauri hilo lipangiwe tarehe nyingine na wanaamini siku hiyo atakuwa vizuri.

Wakili wa utetezi, Nehemiah Nkoko ameiomba Mahakama waendelee na mashahidi wengine wa upande wa mashtaka ili kuokoa muda.

Wakili Wankyo alidai katika hali ya kawaida ni lazima shahidi huyo amalizie kutoa ushahidi wake kwanza ndipo wengine waendelee.

Hakimu Shaidi ameutaka upande wa mashtaka kupeleka mashahidi wengine kama huyo hatakuwa ametengemaa kiafya.

Kesi hiyo imepangwa kuendelea kusikilizwa Novemba 21, 24, 27 hadi 30 na Desemba Mosi, 2017.

Washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Salvius Matembo na Philemon Manase ambao kwa pamoja, wanadaiwa kati ya Januari Mosi, 2000 na Mei 22,2014  walijihusisha na biashara ya nyara za Serikali kinyume cha sheria.

Wanadaiwa kufanya biashara ya vipande 706 vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilogramu 1,889 zenye thamani ya Sh13 bilioni bila ya kuwa na leseni iliyotolewa na Mkurugenzi wa Wanyamapori.

ACT Wazalendo wagoma kupekuliwa, Polisi wamfuata Katibu Mkuu nyumbani

$
0
0
Polisi wamefika Makao Makuu ya ACT, wamekutana na Katibu wa Uenezi, Itikadi na Mawasiliano ya Umma, Ado Shaibu, ambaye baada ya kuwapokea amewaeleza kuwa mwenye Ofisi ni Katibu Mkuu ambaye hayupo ofisini.

Amewaeleza pia kuwa kama Jeshi la Polisi lilitaka kufanya Upekuzi kwenye Ofisi za ACT Wazalendo, nafasi nzuri kwao ilikuwa ni jana kwa kuwa walimhoji Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo kwa Masaa 7.

Polisi wamesisitiza kufanya upekuzi leo, hivyo wameamua kumfuata Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Ndugu Dorothy Semu, nyumbani kwake ili awepo wakati wa upekuzi husika.

Dawa ya Asili ya Tatizo Sugu la Nguvu za Kiume.

$
0
0
MAPRO POWER NO 3; NI DAWA YA NGUVU ZA KIUME KWA WANAOSHINDWA KURUDIA TENDO NA KUKOJOA HARAKA :

Tatizo LA kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na matatizo yafuatayo;
 1 kupiga punyeto au kujichua
 2 kufanyiwa tohara ukubwani 
3 utumiaji usio na mpangilio madawa ya ospitalini au ya kizungu 
4 usongo wa mawazo 
5 magonjwa ya moyo, PRESHA, kisukari, kuvimba kwa korodoni, vidonda vya tumbo, tumbo kujaa gesi au kuunguruma, unene kupita kiasi nk

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha kutofanyika vema kwa tendo la  ndoa na kutojiamini na hivyo husababisa ndoa au mahusiano mengi kuvunjika 

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI 
1 KUWAHI KUJOA HALAKA 
2. KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA 
3. KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA 
4 UUME KUSIMAMA UKIWA LEGELEGE NK 

TUMIA MANGUNGU MIX kwa wale wenye uume mdogo,na mwembamba utapata saiz upendayo urefu inchi 1-8 na unene sentimita 1-5. Dawa hizi ni za mitishamba na HAZINA MADHARA YOYOTE 

KUNA DAWA ZA KUMRUDISHA mpenzi kwa mda mfupi tu, kupata kazi haraka, kurudishwa kazini.Je unakesi au umedhurumiwa au unadaiwa 

JE HUJAPATA MTOTO, MPENZI WAKO HAKUTIMIZII MAITAJI YAKO>>???? NJOO SASA UJACHELEWA 

FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU NYUMA YA HOSPITALI 

SIMU NA 0743362017,  0686980006 -DR AGU 

KAMA HUNA NAFASI YA KUFIKA OFISINI UTALETEWA POPOTE

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu,vidonda Vya Tumbo,busha,nguvu Za Kiume

$
0
0
MTALAAM NA BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU NAYALIYOSHINDIKANA KAMA VILE PUMU,VIDONDA VYA TUMBO,BUSHA,NGUVU ZA KIUME,KISUKARI,MIVUTO YOTE,KUSAFISHA NYOTA,KURUDISHA MALI,NK.
 
Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani
 
Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI,KIUNO KUUMA,MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA,KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO,NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni SUPER SAYI 3,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu 

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

SUPER SAYI 4 Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI,PRESHA,UZAZI,NGIRI,PUMU,MALARIA SUGU,VIDONDA VYA TUMBO,CHANGO AINA ZOTE,BP,BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR UPENDO ANAPATIKA KADA YA ZIWA KWA WAKAZI WA DAR ES SALAAM HUDUMA HIZI UTAZIPATA MAGOMENI 

SIMU NO 0753 15 30 26, 0715 26 85 10 

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Trilioni 32.4 kukusanywa bajeti ijayo......Trilioni 7.6 kutumika kulipa mishahara

$
0
0
 Serikali inatarajia kukusanya na kutumia Sh 32.4 trilioni katika bajeti ya mwaka 2018/19.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema leo wakati akiwasilisha Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2018/19 na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti kwa mwaka 2018/19 bungeni mjini hapa.

Mpango amesema mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa zaidi ya Sh 22 trilioni sawa na asilimia 68 ya mahitaji yote.

"Washirika wa maendeleo wanatarajia kuchangia Sh 3.7 trilioni katika bajeti," amesema Dk Mpango.

Amesema Sh 20.2 trilioni ni fedha za matumizi ya kawaida wakati maendeleo ni Sh 12.2 trilioni.

Amesema Sh  7.6 trilioni zitatumika kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wa Serikali na taasisi za umma katika mwaka huo.

Amesema vipaumbele vya serikali ni vinne vya mpango wa maendeleo wa Taifa wa mwaka wa fedha 2018/ 19.

Amesema Sh 9.7 trilioni kutumika kulipa deni la Taifa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/19.

Amevitaja vipaumbele hivyo kuwa ni kukuza uchumi na ujenzi wa msingi wa uchumi wa viwanda, kugungamanisha uchumi na maendeleo ya watu, ujenzi wa mazingira wezeshi kwa uendeshaji biashara na uwekezaji na kuimarisha usimamizi na utekelezaji wa mpango.

Dk Mpango amesema deni la Taifa limeongezeka kufikia dola 26,115.2 Juni mwaka huu ikiwa ni ongezeko la asilimia 17 ikilinganishwa na dola 22,320.76 za kimarekani Juni mwaka jana.

Dk Mpango amesema msukumo mkubwa utaweka katika mikakati ya kuongeza mapato, kupunguza gharama na matumizi ya uendeshaji wa Serikali na kudhibiti ulimbikizaji wa madeni- Waziri wa Fedha na Mipango Dk Philip Mpango

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images