Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

NEC yavionya vyama vya siasa katika uchaguzi mdogo

$
0
0
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Kailima Ramadhani amevitaka vyama vya siasa na wagombea wanaoshiriki uchaguzi mdogo wa madiwani kutekeleza na kuheshimu maadili ya Uchaguzi na kuonya kuwa chama au mgombea atakayekiuka maadili hayo atachukuliwa hatua kama ilivyoanishwa chini ya Kifungu cha 124A cha Sheria ya Uchaguzi Na.1 ya mwaka 1985.

Akitoa taarifa kuhusu maandalizi ya Uchaguzi huo Madiwani utakaofanyika Novemba 26 mwaka huu amevitaka vyama vya siasa kuhakikisha kuwa vinawaelemisha wafuasi wao juu ya kutekeleza maadili hayo katika kipindi chote cha kampeni.

Amesema iwapo wafuasi wa vyama vya siasa watavunja maadili hayo, chama husika pamoja na mgombea wake kitachukuliwa hatua za kinidhamu.

Mkurugenzi Kailima amevitaja vitendo vinavyokiuka maadili ya uchaguzi kuwa ni pamoja na wagombea au wafuasi wa vyama hivyo kuchana mabango ya wagombea wengine, kutoa lugha chafu wakati wa mikutano ya kampeni pamoja na kupitisha muda wa kufanya mikutano ya kampeni.

Amezitaka kamati za maadili za kata na jimbo kuchukua hatua kali kwa chama au mgombea ambaye atavunja maadili hayo. Amesema kamati hizo zinatakiwa kuchukua hatua ndani ya saa 48 mara chama au mgombea anapovunja maadili.

Amesema kuwa miongoni mwa adhabu zinazowakabili wagombea au chama ambacho kitakiuka maadili ya uchaguzi ni kuomba radhi wananchi hadharani, kutotumia vyombo vyha habari kwa muda fulani, onyo la maandishi kusimamishwa kufanya kampeni, mgombea kutangaza mbele ya vyombo vya habari kuwa yeye ni bingwa wa kuvunja maadili ya uchaguzi au kutozwa faini Sh 100,000.

Kailima pia amesema chama cha siasa ambacho kinataka kufanya mabadiliko ya ratiba ya mikutano ya kampeni, lazima kimfahamishe msimamizi wa uchaguzi wa kata na ombi hilo lazima lijadiliwe na vyama vyote vinavyoshiriki kwenye uchaguzi.

Kuhusu vitambulisho mbadala vitakavyotumika wakati kupigia kura kwa wale ambao wamepoteza kadi ya mpiga kura ambavyo ni vitambulisho vya taifa, leseni ya udereva na hati ya kusafirisha; Kailima amesema vitambulisho hivyho vitatumika tu kwa watu ambao wameandikishwa katika kituo husika mwaka 2015, lakini pia bado wana sifa za kupiga kura.

Amesema vitambulisho hivyo vitatu hata kama vimeisha muda wake, mhusika anaruhusiwa kupiga kura. “Pale tunachoangalia ni uthibitisho wa mtu sio kwamba anasafiri au anaendesha gari, pia tunaamini kuwa vimetolewa na mamlaka husika.

Kailima ametoa mwito kwa vyama vya siasa kutambua kwamba tume ya taifa ya uchaguzi imeruhusu mikutano ya kampeni na sio mikutano ya vyama vya siasa. Amesema mtu anayeruhusiwa kwenye mikutano ya kampeni ni mgombea mwenyewe, chama chake au mtu yeyote ambaye anaona anaweza kumfanyia kampeni ndani ya katiba iliyopitishwa.

Amesema tume imepokea rufaa 14 kutoka kwa wagombea ambao hawakuridhika na maamuzi yaliyotolewa na wasimamizi wa uchaguzi wa majimbo. Amesema wataanza kusikiliza rufaa hizo Ijumaa na Jumatatu ijayo watakuwa wameshatoa uamuzi.

Wakati huo huo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa katika uchaguzi mdogo wa madiwani utakaofanyika Novemba 26, 2017 katika kata 43 utagharimu kiasi cha Sh bilioni 2.5.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Ramadhani Kailima, amesema msingi wa bajeti ya uchaguzi unategemea idadi ya vituo vya kupigia kura na idadi ya wapiga kura waliokuwepo katika kata husika. Amesema idadi ya watu ndio inatoa bajeti ya karatasi za kupigia kura pamoja na vituo ambavyo vinakuwa na watumishi wasiopungua wanne.

Amesema katika kituo cha kupigia kura kina watumishi msimamizi wa kituo, msaididzi, karani mwongozaji na mlinzi wa kituo “lakini pia kuna watu wa ziada wako ngazi ya kata na jimbo ambao wanaweza kutumika iwapo msimamizi wa kituo na msaidizi wake wameapata dharura.

Kailima amesema kwamba kata yenye vituo 40 ina bajeti kubwa kuliko kata yenye vituo vichache. Amesema bajeti hiyo pia inategemea askari wanaosimamia uchaguzi na umbali ambako uchaguzi huo unafanyika.

Amefafanua kuwa gharama zingine za uchaguzi ziko kwenye usafirishaji wa vifaa kwenda kwenye kata ambako uchaguzi unafanyika pamoja na machapisho mbalimbali yatakayotumika kwa ajili ya kutoa elimu ya mpiga kura.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Mkurugenzi Mkuu Wa Kampuni ya Acacia AJIUZULU

$
0
0
Wakati utekelezaji wa makubalino baina ya Serikali na Barrick ukisubiriwa, Ofisa Mtendaji Mkuu na Ofisa Mkuu wa Fedha wa Kampuni ya Acacia, wametangaza kujiuzulu kuanzia leo Alhamisi.

Kwenye barua yake, Ofisa Mtendaji Mkuu, Brad Gordon amesema anataka kurudi nyumbani Australia kusimamia masuala ya familia yake wakati Ofisa Mkuu wa Fedha, Andrew Wray akisema amepata fursa nzuri zaidi sehemu nyingine.

“Pamoja na uamuzi huo, wote wataendelea kuhudumu kwenye nafasi hizo wakati wakikabidhi majukumu ya ofisi kwa warithi wao,” imesema taarifa ya Acacia iliyotolewa leo Alhamisi asubuhi.

Kuziba nafasi hizo, Bodi ya Wakurugenzi wa Acacia imemtangaza Peter Geleta kuchukua majukumu ya ofisa mtendaji mkuu baada ya Gordon na Jaco Maritz kusimamia masuala yote ya fedha za kampuni hiyo.

Wote wawili walikuwa watendaji wa Acacia kwa muda mrefu. Geleta alikuwa mkuu wa oganaizesheni wakati Maritz alikuwa meneja mkuu wa idara ya fedha.

“Licha ya majukumu ya uendeshaji, Geleta atahudhuria vikao vya bodi vitakavyofanyika mwishoni mwa mwaka huu badala ya Gordon na kuifanya idadi ya wajumbe kuendele akubaki saba,” imesema taarifa hiyo.

Kwa miezi miwili iliyobaki, makabidhiano ya ofisi yataendelea kufanyika mpaka Januari Mosi, mwakani yatakapohitimishwa na uongozi mpya kuendelea kutekeleza majukumu yake.

Oktoba 19, Serikali na Kampuni ya Barrick Gold Mine inayomiliki asilimia 63.9 ya hisa za Acacia ilitangaza makubaliano yaliyoafikiwa baada ya majadiliano ya takriban miezi mitatu ambapo kampuni hiyo ilikubali kutekeleza masharti yote ya sheria mpya za madini pamoja na kulipa Dola 300 milioni za Marekani wakati majadiliano kuhusu kodi yakiendelea.

Oktoba 20, Wray aliwaambia waandishi wa habari kwamba Acacia haina uwezo wa kulipa kiasi hicho kwa mkupuo.

Mahakama Yamwachia Huru Mtuhuiwa wa ESCROW

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru aliyekuwa Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Rugonzibwa Mujunangoma aliyekuwa akikabiliwa na shtaka la kupokea rushwa ya Sh 323 milioni toka kwa James Rugemalira fedha ambazo ni sehemu ya zilizotoka kwenye Akaunti ya Tegeta Esrow.

Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa amemuachia huru Rugonzibwa leo Alhamisi baada ya Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Takukuru, Leonard Swai kuomba kesi hiyo iondolewe mahakamani hapo chini ya kifungu cha 98 (a) cha Sheria ya Makosa ya Jinai (CPA) na Mahakama kuridhia.

Rugonzibwa alifikishwa na Takukuru mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Januari 14, 2015 akikabiliwa na shtaka la kupokea rushwa ya Sh 323 milioni toka kwa Rugemalira fedha ambazo ni sehemu ya zile Akaunti ya Tegeta Esrow.

Hata hivyo baadaye alibadilishiwa hati ya Mashtaka na kusomewa upya  ambayo hayakuonyesha tena kuwa fedha zilizopokelewa na Mujunangoma toka kwa Rugemalira ni sehemu ya fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow.

Kupitia hati hiyo mpya,  Rugonzibwa alikuwa akidaiwa kuwa Februari 5, 2014  akiwa mtumishi wa Serikali kama Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, alipokea rushwa ya Sh Sh323 milioni kupitia akaunti yake namba 00120102602001 iliyopo kwenye  Benki ya  Mkombozi .

Alidaiwa kuwa alipokea kiasi hicho cha fedha kutoka kwa Rugemalira, ambaye ni mshauri huru wa kitaalamu, mkurugenzi wa VIP na mkurugenzi wa zamani wa Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL kama tuzo kwa kushughulikia mambo ya ufilisi wa muda wa kampuni hiyo.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, alikana na upelelezi  wa kesi hiyo ulikuwa umekwisha  kamilika.

Nyalandu: Sikupata barua yoyote kutoka CCM yakunifukuza

$
0
0
Aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu amesema kuwa hajawahi kupata barua yoyote kutoka CCM inayomfukuza unanacha kama inavyodai.

Mh. Nyalandu ameiambia Bongo5 kuwa ndani ya chama hicho huwa kuna utaratibu na hawamfukuzi mtu kwa barua bali kuna kuwa na vikao vinavyohusiana na maadili hivyo basi amesema tangu awe ndani ya chama hicho hakuna kikao kilichowahi muita kuhusiana na masuala ya maadili.

“Wakati najiuzulu tarehe 30 mwezi Oktoba, nilifanya hivyo kwa nia yangu mwenyewe na kwa uamuzi wangu mwenyewe, sikuwa nimepata barua yoyote kutoka CCM inayonifukuza, kwahiyo dhana ya kwamba kulikuwa na barua yakunifukuza uanachama sio kweli lakini vilevile ikumbukwe kwamba mimi sikuwa mwananchama wa kawaida mimi nilikuwa ni mbunge ana jimbo pili nilikuwa ni mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM na utaratibu wa chama chetu haufukuzwi tu kwa barua huwa kuna vikao vinavyohusiana na maadili huwa vinakaa,” amesema Nyalandu.

“Hakuna kikao chochote tangu niwe mwananchama ambacho kiliwashawahi kuniita kuhusiana na masuala yanayohusiana na maadili, kwahiyo mimi naona tungejikita tu kufanya muktabari wa nchi yetu tufanye siasa za ushindani na turuhusu watu wawe huru na tusisababishe malumbano ambayo hayana sababu yoyote,”ameongeza.

Nyalandu Jumatatu hii ya tarehe 30 Oktoba mwaka huu aliamua kukihama chama cha Mapinduzi (CCM) na kujivua ubunge wa jimbo la Singida Kaskazini.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Octoba 3

Zitto awaomba Watanzania waichangie ACT- Wazalendo

$
0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe amewaomba Watanzania kukichangia Chama hicho ili kiweze kuwafikia na kuwaeleza mambo makuu mawili wakati wa mikutano ya kampeni ya udiwani.

ACT- Wazalendo imesimamisha wagombea 28 kati ya 43 katika uchaguzi mdogo wa udiwani utakaofanyika Novemba 26 ambapo kampeni zake zimeanza Oktoba 29.

“Nachukua fursa hii kuwaomba Watanzania wenye uchungu na nchi yetu kuchangia kampeni zetu. Tunataka kufika kila ya kona ya nchi yetu na wewe ndio utatuwezesha kufika,” amesema Zitto

“Chochote ulicho nacho tunaomba utuchangie kwa kutumia namba hizi hapa. Tigo pesa 0713957977 na M-Pesa 0744959112,  Asante Sana,” ameongeza

Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini Chama hicho kitatumia kampeni hizo kuwaeleza  Watanzania mambo makuu mawili ambayo ameyataja kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za wananchi na hali ngumu ya maisha ya wananchi.

“Lengo kubwa ni kuwaamsha Watanzania kukataa ubinywaji wa haki za binaadamu na kutaka mabadiliko ya sera za uchumi ili kuongeza ajira na kuondoa umasikini,” amesema Zitto

Amesema watatumia mifano halisi kwenye kata husika na kutoa sera mbadala kwa misingi ya Azimio la Tabora.

Tundu Lissu Amkaribisha Nyalandu......Asema Hatua Aliyoichukua Kujiondoa CCM ni ya Kijasiri

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki(Chadema), Tundu Lissu amempongeza aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki(CCM), Lazaro Nyalandu kwa kupata ujasiri wa kuchukua hatua kubwa ambayo hata wabunge wengi waliopo ndani ya CCM wanashindwa kuichukua.

Lissu ambaye yuko kwenye matibabu jijini Nairobi  amempongeza Nyalandu kwa kuwa ni alikuwa mbunge jirani yake na kwa ujasiri wa kufanya hivyo.

Mbali na kumpongeza Nyalandu pia Lissu amezungumzia  uchaguzi wa madiwani katika kata 43 akieleza kuwa kuwapa CCM kura katika kata hizo ni sawa na kukubaliana na yanayoendelea nchini.

“Kuwapa CCM kura sasa hivi ni sawa na kuwapa CCM mamlaka ya kutapanya mali zetu kama wanavyotaka,”amesema Lissu leo Jumanne akiwa jijini Nairobi.

Malima Afutiwa Kesi.....Ni Siku 6 Baada ya Kuteuliwa Kuwa Mkuu wa Mkoa

$
0
0

Siku sita baada ya Adam Malima kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mahakama imemfutia kesi ya shambulio iliyokuwa ikimkabili.

Rais John Magufuli, Alhamisi Oktoba 26,2017 alifanya uteuzi mbalimbali ukiwemo wa wakuu wa mikoa.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Jumatano Novemba 1,2017 imeifuta kesi dhidi ya Malima na mwenzake.

Malima ambaye amesharipoti mkoani Mara hakuwepo mahakamani wakati uamuzi huo ukitolewa.

Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage ameifuta kesi hiyo na kuwaachia huru washtakiwa baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa kuomba ifutwe.

Chini ya kifungu cha 91 (1) cha Mwenendo wa Mashauri ya Jinai, Mutalemwa ameomba shauri lifutwe kwa sababu Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hana nia ya kuendeleza mashtaka dhidi ya washtakiwa.

Baada ya ombi hilo kuwasilishwa, Hakimu Mwijage alimuhoji Mutalemwa iwapo kuna sababu ya kuifuta kesi hiyo na kama hana hataifuta.

Wakili Mutalemwa alisoma kifungu hicho akisema kinampa mamlaka DPP kuiondoa kesi mahakamani wakati wowote anapoona inafaa na pia, kinamruhusu kuirudisha mahakamani.

Baada ya maelezo hayo, Hakimu Mwijage alikubali kuwaachia huru washtakiwa.

Shauri hilo lilikuwa katika hatua ya usikilizwaji wa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka.

Waliposomewa maelezo ya awali, Malima na mshtakiwa mwenzake Ramadhani Kigwande walikubali maelezo yao binafsi, siku ya tukio walikuwepo Masaki, walikamatwa na kushtakiwa.

Walikana maelezo mengine kuhusu mashtaka yanayowakabili.

Katika kesi hiyo, Malima aliyewahi kuwa naibu waziri katika Serikali ya Awamu ya Nne na mbunge wa zamani wa Mkuranga alidaiwa Mei 15,2017 katika eneo la Masaki kwa makusudi alimzuia ofisa wa polisi Konstebo Abdu kufanya kazi yake halali.

Malima alidaiwa kumzuia askari huyo kumkamata Ramadhani Kigwande kwa kosa la kumshambulia Mwita Joseph.

Kigwande alidaiwa Mei 15,2017 eneo la Masaki wilayani Kinondoni akiwa na nia ya kumzuia Mwita Joseph, ambaye ni ofisa operesheni wa kampuni ya Priscane Business Enterprises alipokuwa akimkamata kwa kupaki vibaya gari alimshambulia na kumsababishia maumivu.

Waliposomewa mashtaka, washtakiwa walikana na walikuwa nje kwa dhamana  kwa kila mmoja kuwa na mdhamini mmoja ambaye alisaini bondi ya Sh5 milioni.

Nape Ampuuza Nyalandu

$
0
0
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amembeza aliyekuwa mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu kwa kujivua uanachama wa chama hicho na kuonyesha dhamira ya kujiunga na Chadema.
 
Nape aliyewahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amekuwa mbunge wa pili wa CCM kuzungumzia uamuzi wa Nyalandu akitanguliwa na mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde ‘Kibajaji.’
 
Kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Twitter, Nape ameandika ujumbe ukiambatana na picha inayowaonyesha yeye, Nyalandu na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakiwa na nyuso za tabasamu.
 
Ujumbe huo ulisomeka “Chama cha siasa ni itikadi, itikadi ni imani, siamini sana katika kubadili imani kienyeji. Nitashughulikia mapungufu nikiwa ndani sio nje!”

Diamond Adai Hana Uwezo wa Kumlipa Hamisa Mobeto Milioni 5 kwa Mwezi za Matunzo ya Mtoto

$
0
0
Msanii Nasib Abdul maarufu Diamond Platinumz, amedai mahakamani kuwa hana uwezo wa kumlipa Mwanamitindo Hamisa Mobeto, Sh milioni tano kama gharama za matunzo ya mtoto kwa mwezi.

Diamond amewasilisha majibu hayo katika Mahakama ya Watoto Kisutu, mbele ya Hakimu Mkazi Devotha Kisoka baada ya Mobeto kumfungulia kesi ya madai katika Mahakama hiyo ya watoto akidai mambo mbalimbali ikiwamo matunzo ya mtoto.

Katika majibu yake Diamond amedai fedha hizo anazodai Hamisa kulipwa kwa mwezi kwa ajili ya matunzo ya mtoto ni kubwa hawezi kuzimudu.

Mobeto katika maombi yake kupitia mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Godluck wa Kampuni ya Uwakili ya Century Attorneys, anaiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto kila mwezi, mtoto huyo wa kiume aliyezaa na msanii huyo na kumuomba msamaha kwa umma kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake.

Baada ya kupokea majibu hayo mahakama iliahirisha kesi hiyo ya madai hadi Novemba 8, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa. Mobeto kupitia wakili wake walimpa notisi Diamond ya kutaka amwombe radhi na kupeleka matunzo ya mtoto ndani ya siku saba lakini notisi hiyo haikutekelezeka hivyo aliamua kulifikisha suala hilo mahakamani.

Barua ya Spika wa Bunge kuhusu lililokuwa Jimbo la Nyalandu

$
0
0
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai leo Novemba 3, 2017 amemuandikia barua Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC) kumtaarifu kuwa jimbo la Singida Kaskazini lipo wazi kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Taarifa ya Bunge iliyotolewa leo inasema kuwa jimbo hilo lipo wazi kutokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumfuta Uanachama Lazaro Nyalandu toka Oktoba 30, 2017 siku ambayo Mbunge huyo alitangaza mwenyewe kupitia vyombo vya habari kujivua nafasi zake ndani ya chama hicho na kusema kuwa ameandika barua kwa Spika kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge kupitia CCM.


Halmashauri yasimamisha mishahara ya walimu 15

$
0
0
Halmshauri ya wilaya ya Kilosa Morogoro imesimamisha mishahara ya walimu 15 waliohamishwa mwezi Machi bila kulipwa stahiki zao za uhamisho na kupelekea walimu hao kugoma hatua inayodaiwa ni kushindwa kufuata sheria za utumishi wa umma katika kudai.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti walimu wa shule tofauti, Rehema Mkway mwalimu shule ya sekondari Masanze, Isaya Milimi mwalimu shule ya msingi Msimba Kilosa, wamesema walimu wamekuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya kuhamishwa bila kulipa stahiki zao na kuleta usumbufu na kuvunja morali ya utendaji kazi na kuisababishia serikali madeni yasiyo na msingi.

Akizungumza kwenye mkutano wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Kilosa  Katibu wa Chama hicho Flora Malomele amesema pamoja na kupatikana mafanikio kadhaa lakini walimu wanakabiliwa na changamoto ikiwemo kutolipwa stahiki zao kwa wakati huku katibu wa tume ya walimu (TSC) Daudi Mchilu akasisitizia watumishi kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.

Kwa upande wake Afisa utumishi wa halmashauri ya wilaya ya Kilosa Noel Abeid akijibu madai ya walimu hao  ameahidi kushughulikia suala hilo kwani halmashauri inatafuta fedha na kuwaonya watumishi wa umma kutojichukuliwa sheria mkononi pale wanapoona mwajiri ameenda kinyume cha sheria badala yake wafuate sheria zilizopo.

Katibu Mkuu CHADEMA Atoa Neno Uchaguzi Mdogo wa Madiwani.....Azungumzia Sakata la Wanaohamia CHADEMA

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Vincent Mashinji amesema kuwa baadhi ya wasimamizi wa Uchaguzi mdogo wa udiwani ambao unatarajiwa kufanyika karibuni katika Kata 48 katika mikoa 18 nchini wamepewa maelekezo kutowatangaza Madiwani CHADEMA wakishinda.

Ameyasema hayo leo kupitia mtandao wake wa Twitter na kudai kuwa hiyo itakuwa ni fursa kwao wao CHADEMA kuwaonyesha na kuwafundisha ustaarabu mpya ambao wameuanzisha.

“Wasimamizi wa uchaguzi wana maagizo ya kutowatangaza madiwani wa CHADEMA watakao shinda. Hii ni fursa kwetu kuwafundisha ustaarabu mpya. Na imani maneno haya utayakumbuka nikupe mshahara, nyumba na gari halafu umtangaze mpinzani kashinda,”amesema Mashinji

Aidha, mbali na hilo Mashinji amejibu hoja ya Rais ambayo aliitoa akiwa Mwanza kuwa wezi ambao walikuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walikimbilia CHADEMA na kudai kuwa watu hao ambao wanatoka CCM na kwenda CHADEMA wameamua kuokoka.

Hata hivyo, ameongeza kuwa kuhama kwa wanachama kutoka Chama cha Mapinduzi CCM kwenda Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwa wameokoka hivyo wameenda sehemu sahihi.


Bodi ya mikopo Yawatoa Hofu Wanafunzi

$
0
0

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu nchini (HESLB) imewatoa hofu wanafunzi waliokosa mikopo kwakuwa ipo katika hatua za mwisho kutoa majina ya awamu ya tatu.

Kauli hiyo imekuja ikiwa leo   ni siku ya mwisho iliyotolewa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha ya kuitaka bodi hiyo kuhakikisha kila mwanafunzi mwenye sifa anapewa mkopo.

Akizungumza leo Novemba 3,Meneja Mawasiliano wa bodi hiyo, Omega Ngole amesema agizo hilo linaendelea kutekelezwa na kwamba hadi kufikia kesho  kila mwanafunzi mwenye sifa atapata mkopo.

Amesema kwa wale watakaokosa mkopo wanaweza kukata rufaa kupitia bodi hiyo ili kupitia upya taarifa zao.

“Maelekezo hayo yote yanatekelezwa na tutakamilisha leo na tutatoa taarifa ya kuhusu utekelezaji wake wiki ijayo,” amesema

Katika mwaka wa masomo wa 2017/18 Serikali imetenga bajeti ya Sh427 bilioni kwaajili ya mikopo ambapo wanafunzi 30,000 wa mwaka wa kwanza watanufaika na fungu hilo.

Hadi sasa Jumla ya wanafunzi 21,677 maombi yao yamekubaliwa ikiwa ni awamu mbili zilizotolewa na bodi hiyo ambapo awamu ya kwanza ilitoa majina 10,196 na ya pili 11,481.

Meneja huyo amesema kwa wale waliodahiliwa kwenye vyuo walivyothibitisha kupitia Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) tayari fedha zimeanza kutumwa kwenye vyuo husika.

“Mwanafunzi akipangiwa mkopo halafu asipoliridhika, akaona uhitaji wake ni mkubwa kuliko kiwango alichokipata kuna nafasi ya kukata rufaa ambayo itaanza wiki ijayo,”amesema.

Waziri Apiga Marufuku Biashara ya Damu

$
0
0
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  ameendelea kusisitiza kuwa wananchi hawapaswi kununua damu kwani huduma hiyo ni bure kwa watanzania wote katika hospitali zote.

Hayo amezungumza leo jijini Dar es salaam  wakati wa  uzinduzi wa Benki ya damu iliyodhaminiwa na Ubalozi wa Kuwait katika Taasisi ya Mifupa MOI ambapo uliuzuliwa na Balozi wa Kuwait nchini Tanzania.

“Watanzania wanahoitaji huduma ya kuongezewa damu wapewe bure marufuku kwa watoa huduma za vituo vya afya pamoja na hospitali zote kuuza damu hiyo kwani inatoka kwa wananchi wenyewe” alisisitiza Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa wananchi wanatakiwa kujitokeza katika kuchangia damu ili kuweza kuwa na hifadhi ya kutosha na kufanya kazi kwa wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo kwa wakati sahihi bila ya usumbufu wowote katika kuokoa maisha ya watanzania.

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema  kuwa anayo furaha kutimiza miaka miwili tangu kuingia kwa Serikali ya awamu ya tano kwa kupiga hatua katika sekta ya afya hasa katika kupunguza rufaa za nje na kuwa na utaalamu wa matibabu ya kibingwa kama vile upandikizaji wa figo, vifaa vya usikivu( Coclea Impant) na kutibu magonjwa ya moyo.

Kwa upande wake Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Bw. Jasem Ibrahim Al-Najem amesema kuwa  wameamua kuchangia kiasi cha fedha cha shilingi Milioni 200 katika kutengeneza Benki hiyo ya damu MOI ili kuweza kusaidia kuboresha sekta ya afya nchini.

“Mbali na kiasi hicho cha fedha pia tumetoa Dola za Kimarekani 500 ili kuweza kusaidia  walemavu mbalimbali katika kulejesha hali zao za kawaida hapa nchini” alisema Bw. Al-Najem.

Aidha katika uzinduzi huo wa Benki ya damu Balozi Al-Najem alijitolea damu unit moja ili kuweza kuchangia benki hiyo ya taasisi ya Mifupa MOI ili kuweza kuhamasisjha na wananchi wengine waweze kuchangia damu kwa msaada wa wagonjwa wengine.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Lwezimula alisema kuwa katika kuhakikisha Matibabu ya kibingwa yanapiga hatua nchini waliamu kuanzisha kambi za matibabu kuanzia mwaka 2000 na kufanya taasisi zingine za afya kuiga mfano huo.

“Tunataka kuhamasisha matibabu ya kibingwa kufanyika nchini pamoja na uchangiaji damu kwani damu hiyo haitatumika MOI peke yake bali hata kwenye Taasisi zingne na vituo vya Afya nchini kote” alisema Dkt. Lwezimula.

Sambamba na tukio hilo Kikundi cha Kutayarisha Madereva wa Magari Makubwa  Wanawake (WOW) Afrika Mashariki walijitolea kuchangia damu ili kuweza kusapoti benki hiyo kwa ajili ya wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo ya damu.

“Tumehamasika kuja kuchangia damu ili kuweza kutoa mfano kwa wanachi wengie waweze kujitolea katika uchangiaji huu wa damu ili kujenga taifa lenye watu wenye afya bora” alisema Mkurugenzi wa WOW Bw. Martin Gabone.

Mohammed Dewji apongeza jitihada za Rais Magufuli kufufua viwanda

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mohammed Enterprises (MeTL Group), Mohammed Dewji amepongeza uamuzi wa Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda kwa kufufua viwanda ambavyo vilikuwa havifanyi kazi.

Dewji ametoa pongezi hizo wakati akizungumza katika mkutano wa siku mbili wa Global Business Forum 2017 (GBF) kuhusu Viwanda kwa Nchi za Afrika uliofanyika Dubai, Falme za Kiarabu (UAE).

Mfanyabiashara huyo ambaye anamiliki viwanda 41 alisema uamuzi aliochukua Rais Magufuli ni mzuri hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania inaelekea katika uchumi wa kati.

Dewji alisema kampuni yake ya MeTL Group itaendelea kushirikiana na serikali na katika kipindi cha miaka kadhaa ijayo amejipanga kuhakikisha anatoa ajira kwa Watanzania 100,000 jambo ambalo litasaidia kukuza uchumi wa nchi na kwa wananchi..

 “Nianze kwa kumpongeza Mhe. Rais John Pombe Magufuli kwa shabaha yake ya viwanda, ni nzuri sababu kuna ongezeko la thamani lakini pia watu wanaweza kupata ajira na pia hizi biashara zitalipa kodi ambazo zitaisaidia serikali kuwekeza kwenye mambo ya afya na maji na huduma za jamii. Mimi shabaha yangu kwenye miaka saba au nane ijayo MeTL Group tunataka tuajiri watu 100,000,” alisema Dewji.

Dewji ambaye kwa mujibu wa jarida la Forbes ni tajiri namba moja nchini aliongeza kuwa utendaji wa Rais Magufuli ni wa kasi hivyo anategemea kuwa katika kipindi cha miaka michache ijayo uchumi wa Tanzania utakuwa umekuwa  sana.

“Mimi naona kwa kasi ya Mhe. Rais kwenye miaka miwili au mitatu ijayo tutakuwa tumefika mbali sana, uchumi wetu kwasasa ni asilimia sita au saba lakini kama tukitaka kuondoa umaskini lazima nchi yetu ukuaji wa uchumi uanze kukua kwa zaidi ya asimilia 10, mimi nina muamini sana Mhe. Rais na shabaha yake kwahiyo Mungu atutangulie na sisi tupo nyuma yake tutafika hivi karibuni,” alisema Dewji.

Pia Dewji alizungumzia umuhimu wa mkutano wa GBF ambao umekutanisha watu kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika wakiwepo viongozi wa serikali za nchi za Afrika na wawekezaji alisema ni nafasi ya kipekee kwani pamoja na kujadili viwanda pia amepata nafasi ya kuwaelezea washiriki wa mkutano fursa za uwekezaji zilizopo hapa nchini.

“Umuhimu ni mkubwa sana nakuja hapa kama MO lakini pia nawakilisha nchi yangu Tanzania, nimeitangaza nchi yangu ili watu waje na wawekeze, nimewaeleza mazingira yetu ya uwekezaji ni mazuri, tuna malighafi na tunahitaji viwanda angalau watu wetu wa Tanzania wapate ajira na serikali ipate kodi,” aliongeza Dewji.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images