Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mwakyembe Aingilia Kati Sakata la Mzee Majuto Kudhulumiwa Mamilioni ya Pesa

0
0
Waziri wa Habari,  Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amefunguka na kusema kuwa Mzee Majuto amedhurumiwa pesa milioni 25 na kampuni ya filamu ambayo jina lake amelihifadhi na kudai atatumia hata mshahara wake kuhakikisha anawafunga watu hao.

Mwakyembe amesema hayo leo Oktoba 27, 2017 alipokutana na wasanii mbalimbali kujadili changamoto za kazi ya sanaa nchini na kusema katika vitu ambavyo atapambana navyo ni pamoja na watu wanaowadhurumu wasanii haki yao na kuwaibia kazi zao za sanaa.

"Nilipopita Tanga nilikutana msanii nguli wa filamu Mzee Majuto nilikwenda kumjulia hali na bahati nzuri saizi anaendelea vizuri, Mzee Majuto akaniomba kitu kimoja na kuniambia naumwa nahitaji pesa lakini nimeshafanya kazi na kampuni hii akanionyesha na kuwa ameshatengeneza filamu zaidi ya 100 na kampuni hiyo kwa mkataba wa kulipwa fedha ndogo tu shilingi milioni 25 lakini huu ni mwaka wa  pili hajalipwa hata senti tano sasa hayo ndiyo mambo ambayo sifurahii, nimeshapeleka taarifa kwa hiyo kampuni tukutane Dar es Salaam na Dodoma asipokuja tunajua njia za kumsafirisha kwenye kalandinga mpaka Dodoma, huu ni wizi kama wizi wa kwenda kumchomolea mtu mfukoni" alisisitiza Mwakyembe

Waziri Mwakyembe aliendelea kufafanua kuwa kwa sasa yupo tayari kutumia pesa zake mfukoni kuhakikisha Mzee Majuto anapata haki yake kwa kazi mbalimbali alizofanya na kampuni hiyo.

"Mzee Majuto alikwenda Mwanza na familia kupokea ule mzigo, meneja kwa kumuheshimu akamfuata na kumwambia hiyo cheki hata senti tano hakuna na cheki iliyobaundi ni kosa la jinai, tunachezea watu hivi. 

"Mzee Majuto ameacha familia yake, amekaa Mwanza zaidi ya miezi sita anahangaika kuzipata hizo pesa, na mimi niko tayari nitatumia hata mshahara wangu twende mahakamani tufunge watu tumeshachoka huko ni kudharau watu" alisema Mwakyembe

Mwezi Agosti Waziri Mwakyembe alimtembelea msanii nguli na mkongwe wa filamu nchini Mzee Majuto nyumbani kwake ambapo alikwenda kumjulia hali baada ya kupata taarifa kuwa anaumwa.

Mganga Mkuu Akanusha Watoto 9 Kufariki kisa Kukatika kwa Umeme

0
0
Mganga Mkuu Mkoa wa Arusha Dkt. Wonanji Timoth amekanusha taarifa za kufariki kwa watoto 9 waliokuwa kwenye Incubator kutokana na katizo la umeme hapo jana hospitali ya Mt. Meru, na kusema kwamba taarifa hizo hazina ukweli wowote.

Dkt. Timoth amesema kwamba watoto waliofariki walikuwa wanne na sio 9 kama inavyoelezwa kwenye taarifa iliyosambaa mitandaoni, na wamefariki kwa matatizo mengine lakini sio kukatika kwa umeme.

Dkt. Timoth ameendelea kwa kueleza kwamba moja ya sababu iliyofanya watoto hao kufariki ni mama kuchelewa kufika hospitali kujifungua kwa kuwa alijifungulia nyumbani, pamoja na hatari kubwa wanazopata watoto njiti.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Octoba 28

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605   au  0767358654

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Ofisi za Manji zafungwa, kisa kodi ya Sh300 milioni

0
0
Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuf Manji ameendelea kuingia matatani baada ya Kampuni ya Udalali ya Yono kuzifunga ofisi zake zilizopo Barabara ya Pugu.

Yono wamezifunga ofisi na maghala ya Manji ambaye alikuwa Mwenyekiti wa klabu ya Yanga akituhumiwa kudaiwa kodi ya zaidi ya Sh300 milioni na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Yono, Scholastika Kevela jana Ijumaa  alisema, ‘’ni kweli tumezifunga ofisi za Manji zilizopo eneo la Pugu, anadaiwa fedha nyingi za kodi na TRA.”

Alipoulizwa kipi kitafuata baada ya kuzifunga, Kevela alisema, ‘’sisi utaratibu wetu ni kwamba tukizifunga huwa tunatoa siku 14 mhusika akalipe na baada ya hapo sasa tunasubiri maelekezo kutoka kwa TRA.”

Taarifa ya kuomba radhi kutoa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

0
0
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco)  limewaomba radhi wateja wanaokosa huduma ya umeme.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Oktoba 28,2017 na ofisi ya uhusiano Tanesco makao makuu imesema sababu ni kuathirika kwa miundombinu kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Tanesco imesema mvua imesababisha maeneo mengine kuwa vigumu kufikika kwa haraka.

“Mafundi wetu wanaendelea na jitihada usiku na mchana kuhakikisha huduma ya umeme inarejea katika maeneo yote nchini,” imesema taarifa hiyo.

Shirika hilo limesema litaendelea kutoa taarifa na limewaomba radhi wateja kwa usumbufu unaojitokeza.

Tanesco imetoa tahadhari kwa wananchi wasishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka.

Wakati Tanesco likitoa taarifa hiyo, Jumatano Oktoba 25,2017 umeme ulikatika nchini nzima kutokana na hitilafu kwenye gridi ya Taifa.

==>Hapo chini ni taarifa ya TANESCO

Serikali: Ugumu wa Maisha ni wa mpito

0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema maisha magumu wanayopitia wananchi kwa sasa yanatokana na mabadiliko ambayo Serikali inayafanya na hali itakuwa nzuri baadaye.

Mwijage alisema hayo jana Ijumaa Oktoba 27,2017 wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo kwa kampuni 100 za kati zilizofanya vizuri mwaka huu. Shindano hilo huandaliwa na kampuni ya KPMG kwa ushirikiano na kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) kupitia gazeti la The Citizen.

Waziri Mwijage amesema hiki ni kipindi cha mpito ambacho kina mwisho na Serikali inafanya mabadiliko mbalimbali ikitaka kujua matumizi yake halisi.

“Tumekuwa hatuna uhakika wa matumizi yetu au tunachonunua. Msiwe na wasiwasi, ni kipindi cha mpito na kina mwisho wake, tutatoka. Tuwe wavumilivu tu,” alisema Mwijage mbele ya jumuiya ya wafanyabiashara waliohudhuria hafla hiyo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Alisema lengo la kuanzisha mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano ni kujenga uchumi wa viwanda na kuleta maendeleo ya watu.

Waziri Mwijage amesema anaamini mtu mwenye shughuli ya kufanya atapata chochote.

Amesema anatambua kwamba sekta binafsi ni mhimili wa uchumi wa Taifa na kwamba, ukitaka kujenga uchumi shindani lazima uwe na sekta binafsi yenye nguvu na ushindani mkubwa.

“Jukumu langu ni kuhakikisha kwamba sekta binafsi inakuwa na ushindani mkubwa na ili kufanikisha hilo ni lazima niwasikilize ninyi,” amesema.

Waziri Mwijage pia alielezwa na wafanyabiashara hao jinsi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inavyowanyanyasa, kuwabambikia kodi kubwa na jinsi maofisa wake wanavyojipa mamlaka makubwa.Waziri Mwijage alisema anafahamu suala hilo.

“Nalifahamu suala la manyanyaso ndiyo maana nasema tuko kwenye kipindi cha mpito. Kuna watu nawaita ‘wasiojulikana’ kwa sababu wao hawajulikani upande wa polisi wala upande wa TRA,” alisema waziri huyo.

Katika shindano hilo, kampuni 10 zilizofanya vizuri mwaka huu kwa kuanza na nafasi ya kwanza ni Dar Ceramic Centre 2001 Ltd, Songoro Marine Transport, Modern Fitting Mart Ltd, Transit Ltd, Meru Spring Water Ltd, Economic and Business Foundation Ltd, Computer and Network Technology, Premier Agencies Tanzania Ltd, Tanpack Tissue Ltd na Tahafresh Handling Ltd.

Mkurugenzi mtendaji wa Dar Ceramic Centre 2001 Ltd, Hussein Nathoo alisema siri ya mafanikio yao ni kupanua biashara. Mwaka jana ilishika nafasi ya sita katika shindano hilo ikiwa na matawi saba nchi nzima lakini sasa yapo 11.

Mzozo wa fedha za matunzo wasababisha FFU kumuua mzazi mwenzake Kwa Bunduki

0
0
Polisi wilayani Babati mkoani Manyara inamshikilia askari wa jeshi hilo  Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), Cosmas James akituhumiwa kumuua mzazi mwenzake, Regina Daniel (23) kwa kumpiga risasi nne.

Chanzo cha mauaji hayo inadaiwa ni mzozo ulitokea Regina alipomfuata James lindoni kudai fedha za matumizi ya mtoto.

Akithibitisha tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Longinus Tibishubwamu amesema lilitokea mjini Babati Ijumaa Oktoba 27,2017 saa 12:30 jioni.

Amesema askari huyo alikuwa lindoni katika Benki ya NMB tawi la Babati, mtaa wa Usalama, Kata ya Bagara.

Kaimu Kamanda Tibishubwamu amesema Regina ni mkazi wa Mtaa wa Ngarenaro mjini Babati.

Amesema uchunguzi wa awali unaonyesha kabla ya kifo cha mwanamke huyo kulitokea mzozo kati ya wawili hao kuhusu fedha za matumizi ya mtoto.

"Wakati wakiendelea na mzozo, ndipo askari huyo kwa kutumia silaha aliyokuwa nayo alimpiga Regina risasi nne kwenye paji la uso, kifuani na shingoni," amesema.

Amesema askari huyo alitumia silaha aliyokuwa nayo lindoni aina ya SMG mali ya Jeshi la Polisi.

Baada ya tukio, amesema askari huyo aliitelekeza silaha lindoni na kwenda kujisalimisha polisi. Amesema askari waliokwenda eneo la tukio waliokota maganda matatu ya risasi na waliichukua silaha hiyo.

Kaimu Kamanda Tibishubwamu amesema mtuhumiwa yupo mahabusu kwa mahojiano kabla ya hatua nyingine kuchukuliwa na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mji wa Babati ya Mrara.

Askari wa FFU mjini Babati, aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina amesema anashangazwa na tukio hilo kutokana na upole alionao James.

Amesema James ni askari mwenye nidhamu, hivyo hafahamu jambo gani limempata hadi akamuua mzazi mwenzake.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Zitto Kabwe Aikomalia Serikali...... Aomba jumuiya za kimataifa kuchunguza kasi ya ukuaji uchumi nchini

0
0
Chama cha ACT Wazalendo kimeziomba Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Benki ya Dunia (WB) kufanya uchunguzi maalumu wa takwimu za kasi ya ukuaji wa uchumi ya robo ya pili ya mwaka na kuchukua hatua endapo itabainika kile anachodai kuwa Serikali ilipika takwimu.

Kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe ametoa msimamo wake huo leo Jumamosi jijini Dar es Salaam katika mkutano na waandishi wa habari.

Zitto amedai chama hicho kimebaini  takwimu zilizotolewa na Serikali za Aprili hadi Juni haziko sahihi.

Amedai takwimu za Serikali zinaonyesha kasi ya ukuaji wa uchumi katika robo ya pili ya mwaka ni asilimia 5.7, tofauti na za ukokotozi kwa kanuni za kiuchumi anazodai zinaonyesha ni asilimia 0.1.

"Hatujatafuta takwimu nyingine, hizi ni taarifa zilezile zilizotolewa na BoT na NBS lakini ukikokotoa utaona uchumi tulionao unasinyaa badala ya kukua na hali ikiendelea hivi hadi Juni 2018 kutakuwa hakuna uchumi Tanzania," amedai Zitto.

Amedai sababu hiyo inachangia maisha ya Watanzania kuendelea kuwa magumu ilhali Serikali imekuwa ikitoa taarifa za uchumi kukua.

Zitto amegusia pia takwimu za mapato yanayokusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) akidai nazo haziko sahihi.

Amesema ni vyema wakati TRA ikitoa takwimu zake ikaeleza mapato kwa kila idara bila kuchanganya marejesho na madeni ambayo hayajalipwa.

"Taarifa yao ieleze kinagaubaga mapato ya idara ya forodha, walipa kodi wakubwa na walipa kodi za ndani. Wasiishie hapo, kati ya fedha wanazotaja kukusanya iwekwe wazi madeni na marejesho ni yapi tofauti na  inavyofanywa sasa," amesema.

Zitto ametaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi wa mapato ya Serikali ya Julai na Agosti na kuweka wazi taarifa hiyo.

Mbunge akataa milioni 29 alizohongwa na serikali

0
0
Mwanamuziki Uganda, ambaye ni Mbunge Kyadondo East , Bobi Wine amekataa fedha milioni 29 za Uganda alizohongwa na serikali ili aweze kukubaliana na mapendekezo ya kufanyia marekebisho kipengele cha katiba na kuondoa ukomo wa miaka 75 kuongoza nchi.

Bobi Wine ameiamuru benki ambayo amewekewa fedha hizo kuzirudisha kwa watu ambao wameziweka na kusema kutokana na taarifa ya mawasiliano wabunge wote wa Uganda 449 wamepewa fedha hizo ili waweze kukubaliana na hoja hiyo na kuoandoa ukomo wa miaka 75 ili kuweza kumpa nafasi tena  Yoweri Kaguta Museveni (73) kugombea nafasi ya Urais tena kwa awamu ya sita 2021.

"Oktoba 24, 2017 Milioni 29 wa Uganda ziliwekwa kwenye Account yangu ya benki, pesa hizo walipewa wabunge wote wa Uganda kwa mujibu wa taarifa rasmi pesa hizo walizopewa wabunge ni ili kukubaliana na pendekezo la kufanyia marekebisho kipengele cha 102 (b) cha Katiba ya Uganda na kuondoa ukomo wa miaka 75 kama sifa ya kusimama kama Rais wa Uganda" alisema Bobi Wine

Bobi Wine aliwapa taarifa watu wa benki yake kuwa wazirudishe hizo fedha zote zilizotumwa kwa mtu ambaye amezituma kwake na kusema amefanya maamuzi hayo kutokana na ukweli kwamba yeye haungi mkono Katiba yao kuchezewa kwa ajili ya mtu mmoja na kusema hawapo tayari kwa mtu kuwa Rais kwa wakati wote ndiyo maana Katiba iliweka ukomo wa miaka. 

Madiwani Wamfuta Kazi Daktari

0
0
Daktari mmoja wilayani Kisarawe amefutwa kazi baada ya kukutwa na makosa mbalimbali yaliyoonyesha kutia hofu juu ya utendaji kazi kwenye majukumu yake ya kila siku.

Uamzi huo wa kumfuta kazi Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Mtakayo. Emmanuel Shumbusho umefikiwa na  Baraza la Madiwani halmashauri ya Kisarawe mkoani Pwani.

Makosa ambayo baraza hilo la Madiwani limemhukumu nayo Bw. Emmanuel Shumbusho ni pamoja na uzembe, utoro kazini ambapo hajaonekana kazini kwa takaribani siku tisa bila taarifa yoyote kwa mwajiri wake.

Akitoa maamuzi ya kikao cha baraza la madiwani ya kumfukuza kazi mganga huyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Hamis Dikupatile amesema kwamba wamefikia hatua hiyo baada ya kubaini mapungufu mengi kutoka kwa mtumishi huyo.

Madiwani wote kwa pamoja walikubaliana na uamzi huo kutokana na uzembe wa daktari huyo katika suala zima la utoaji wa huduma ya afya kwa wananchi na kusababisha kuibuka kwa usumbufu mkubwa kutokana na kutopatiwa matibabu kwa wakati.

Waziri aahidi kujizulu nafasi yake

0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ameahidi kuwa atajiuzulu nafasi yake endapo tatizo la uvuvi haramu litaendelea kuwa sugu nchini.

Waziri Mpina ameyasema hayo leo walipokuwa akitekeleza lundo la nyavu zinazotumika kwenye uvuvi haramu zenye thamani ya Tsh 30 milioni zilizokamatwa mkoani Kigoma.

Mpina amesema kwamba, endapo atashindwa kutumua dhamana aliyopewa na Rais Dkt John Pombe Magufuli kukomesha uvuvi haramu atajizulu nafasi yake. Lakini alisema kwamba, hadi kufikia wakati huo ambao atakuwa ameamua kujiuzulu, watu wengine ambao ni wasaidizi wake, nao watakuwa wameumia.

Serikali imepiga marufuku matumizi ya nyavu zenye matundu madogo au uvuvi wa kutumia sumu na baruti ambao husababisha samaki wachanga ambao bado hawajafikia wakati wa kuvuliwa kufa jambo linaloharatisha uwepo wa samaki hao katika miaka ya mbeleni.

Rais Dkt Magufuli wakati akiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi amewahi kuendesha zoezi la uchomaji moto nyavu pamoja na samaki wliovuliwa kinyume na sheria ikiwa ni njia ya kutokomeza uvuvi haramu.

Zitto Kabwe Aiomba CHADEMA Imwaachie Uwanja Ajipime na CCM

0
0
Zikiwa zimesalia siku chache kabla ya kufanyika uchaguzi mdogo wa madiwani, Chama cha ACT Wazalendo kimeviomba vyama vingine vya upinzani kukiachia kipambane na CCM katika kata mbili kati ya tatu za Mkoa wa Dar es Salaam ambazo uchaguzi utafanyika.

Uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Novemba 26,2017 utahusisha kata 43 nchini, Dar es Salaam ukihusisha za Saranga, Kijichi na Mbweni.

ACT Wazalendo imesema utafiti iliyoufanya unaonyesha chama hicho kinaweza  kuchukua kata za Kijichi na Saranga endapo vyama vingine vya upinzani vitakiachia kisimamishe wagombea watakaochuana na wa CCM.

Kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi Oktoba 28,2017 jijini Dar es Salaam amesema ACT Wazalendo imeamua kuwasimamisha wagombea wawili na kuiachia kata moja kwa vyama vingine vya upinzani kwa kuwa wamejipima na kuona wanaweza kushinda bila kupingwa Kijichi na Saranga.

“Tumefanya utafiti mdogo kule Mbweni tukaona vyama vikuu vitatu ni ACT, Chadema na CCM tukaona upo uwezekano wa sisi na Chadema kugawana kura, tumeona tuwaachie kata ile,” amesema.

Zitto amesema, “Tumejipima na kuona ACT ikisimama peke yake Kijichi na Saranga tuna uwezo wa kuishinda CCM asubuhi kweupe. Tunachoomba vyama vingine vya upinzani vituachie tusimamishe wagombea halafu tushirikiane nao kuhakikisha tunaiangusha CCM.”

Amesema, “Tunawaambia wenzetu upinzani adui yetu ni mmoja CCM, hivyo tuweke kando tofauti zetu tushirikiane lengo ni kuhakikisha katika kata tatu za Dar es Salaam, CCM haipati hata moja.”

Habari Zilizopo Karika Magazeti ya Leo Jumapili ya Octoba 29


Sababu Zilizowafanya Wazee wa Baraza Wamtie Hatiani Lulu Michael

0
0
Wazee wa baraza wameieleza Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kuwa mwigizaji wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu Lulu amehusika kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, Steven Kanumba.

Wakitoa maoni yao jana baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili, wazee hao walieleza kuwa Lulu ndiye aliyesababisha kifo cha mpenzi wake huyo wakati wa ugomvi baina yao usiku wa Aprili 7, 2012.

Wakizungumza mmoja baada ya mwingine, wazee Omary Panzi, Sarah Lugoma na Rajabu Mlawa, walihusisha tukio la Kanumba kujibamiza kichwa ukutani na kusukumwa na mshtakiwa.

“Kutokana na sababu na uainishi wa kesi (ushahidi) wa pande zote, mimi kwa upande wangu nimeridhika kuwa Elizabeth (Lulu) ameua bila kukusudia,” alisema mzee Mlawa na kuongeza: “Katika ugomvi, inawezekana hekaheka za kujinusuru, alitumia nguvu kumsukuma Kanumba na kuanguka ukutani. Hivyo, kwa maoni yangu kosa la kuua bila kukusudia kwa Elizabeth limethibitika.”

Akitoa maoni yake, Sarah Lugoma alisema Kanumba alifariki dunia kutokana na ugomvi baina yake na mpenzi wake (Lulu) kwa kuwa ndani kulikuwa giza, Kanumba aliteleza wakati wa ugomvi huo akaanguka.

“Hivyo mshtakiwa aliua bila kukusudia,” alisisitiza Lugoma wakati akihitimisha maoni yake.

Mzee mwingine, Panzi alisema Kanumba aliteleza na kuanguka wakati wa ugomvi huo, mshtakiwa ndiye aliyehusika na kifo chake kwa kuua bila kukusudia.

Hata hivyo, maoni ya wazee hao wa baraza siyo hukumu halisi ya Mahakama bali yanayotokana na mtazamo wao tu katika hali ya kawaida nje ya sheria kwa namna walivyousikiliza ushahidi wa pande zote.

Hivyo, kumtia hatiani mshtakiwa huyo hakumaanishi kuwa tayari ana hatia kwa kuwa maoni hayo hayamfungi jaji katika hukumu yake ambaye huongozwa na sheria husika.

Kwa hiyo, hatima ya msanii huyo kama ana hatia au la itabainishwa na Mahakama Novemba 13 wakati Jaji Sam Rumanyika anayesikiliza kesi hiyo atakapotoa hukumu.

Jaji Rumanyika aliwakumbusha wazee hao muhtasari wa ushahidi uliotolewa na pande zote kabla ya kutoa maoni yao.

Jaji Rumanyika akieleza kwa ufupi kilichozungumzwa na kila shahidi wa pande zote, alitoa mwongozo kwa wazee hao pamoja na mambo mengine, kutoa maoni yao bila kuongozwa na huruma wala kuogopa chochote.

“Mnalo jukumu la kutoa maoni yenu bila kuongozwa na huruma wala vitisho. Mnatakiwa kutoa maoni yenu kwa mujibu wa ushahidi mliousikia,” alisema Jaji Rumanyika.

Aliwaeleza kuwa kama walivyosikia ushahidi wa upande wa mashtaka kuwa umejikita kwenye ushahidi wa kimazingira, mshtakiwa ndiye aliyekuwa mtu wa mwisho kuwa na Kanumba.

Alisema ushahidi wa kimazingira lazima uwe ni vipande ambavyo ni mnyororo (muunganiko) unaomhusisha mshtakiwa kuwa ndiye ametenda kosa.

“Kama mkiona kuwa mshtakiwa ametoa maelezo ya kutosheleza basi mnaweza kusema hana hatia, lakini kama mna maoni tofauti pia mtaniambia,” alisema Jaji Rumanyika na kuongeza:

“Mkiona kuwa kifo hicho kilitokana na ugomvi, basi shtaka lake huwa ni la kuua bila kukusudia, mkishawishika kwa vyovyote na kwa namna yoyote ile mshtakiwa hakuhusika na kifo hiki msisite pia kunipa maoni yenu.”

CHADEMA Kukimbilia Mahakamani Kumnasua Mkurugenzi wake Polisi

0
0
Baada ya Polisi kuendelea kumshikilia Mkurugenzi wa Chadema wa Operesheni na Mafunzo, Kigaila Benson chama hicho kimesema kimekwenda Mahakama Kuu kuiomba itoe amri kwa jeshi hilo kumfikisha kortini.

Wakati Chadema ikisema hayo, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa jana  Alhamisi Oktoba 26,2017 alisema, “Upelelezi unaendelea na huenda kesho(Ijumaa hii) akafikishwa mahakamani.”

Kigaila anashikiliwa na polisi tangu Jumatatu Oktoba 23,2017 aliporipoti Kituo Kikuu cha Polisi cha kanda hiyo kuitikia wito wa jeshi hilo.

Taarifa ya Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Chadema, Tumaini Makene iliyotolewa jana Oktoba 26,2017 imesema baada ya kumaliza mahojiano, askari kutoka Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalumu ya Dar es Salaam (ZCO), waliokuwa wakimhoji Kigaila walisema hawana mamlaka ya kumwachia kwa dhamana.

Makene alisema sababu waliyoitoa ni kwamba wakubwa na wenye mamlaka ya kuruhusu dhamana au kutoa dhamana hawakuwepo ofisini.

“Juhudi za mawakili waliokuwepo polisi kumpatia Kigaila msaada wa kisheria, kueleza kuwa dhamana ni haki yake kwa mujibu wa sheria, huku wakihoji ni kwa nini kusifanyike mawasiliano ili hao wakubwa watoe ruhusa hiyo hata kama wako nje ya ofisi, hazikufua dafu!” alisema Makene.

Alisema tuhuma alizohojiwa Kigaila zilihusu kauli za uchochezi anazodaiwa kuzitoa Septemba 12,2017 siku chama hicho kilipotoa tamko la maazimio ya kikao cha dharura cha Kamati Kuu iliyoketi kujadili tukio la kushambuliwa na kujeruhiwa  mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu.

Makene alisema kwa kuitikia wito wa Jeshi la Polisi na kwenda mwenyewe kituoni, ni sababu inayojitosheleza kuonyesha kuwa Kigaila ni mwaminifu na anatoa ushirikiano kwa sheria za nchi.

“Bila kumfikisha mahakamani au kumwachia huru, tafsiri yake ni kwamba Kigaila anashikiliwa na jeshi hilo kinyume cha sheria za nchi,” alisema.

Alisema Chadema imeagiza Kurugenzi ya Katiba na Sheria kuratibu na kusimamia hatua za kisheria ili kuhakikisha Kigaila anapata haki zake za msingi kwa mujibu wa sheria za nchi.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Jafo aagiza kila mkuu wa mkoa kujenga viwanda vipya 100

0
0
Kila mkuu wa mkoa nchini ameagizwa kujenga viwanda vipya 100 katika kipindi cha mwaka mmoja kinachoanzia Desemba 2017.

Akizungumza na wakuu wa mikoa wapya walioapishwa juzi Ikulu jijini Dar es Salaam, waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo aliwataka kuitekeleza ipasavyo sera ya ujenzi wa viwanda.

Jafo alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa ifikapo Desemba 2018 kila mkoa uwe umejenga viwanda vidogo na vya kati visivyopungua 100.

Alisema mikoa 26 ya Tanzania Bara inatakiwa kuwa na viwanda vipya vidogo na vya kati visivyopungua 2,600 ifikapo Desemba 2018. Alisema Serikali imekusudia kufikia nchi ya uchumi wa kati kupitia ujenzi wa viwanda huku akiwataka wakuu hao kuibua viwanda vidogo na vya kati kwa kuhamasisha ushiriki wa viongozi ndani ya mikoa na wananchi katika maeneo yao ya utawala.

Jafo aliongeza kuwa, katika kusimamia utekelezaji wa agizo hilo ofisi yake itaweka utaratibu maalumu wa kupima utendaji kazi wa kila kiongozi wa mkoa kwa kuangalia ushiriki wake wa kuwajengea hamasa viongozi wa chini wakiwamo wakuu wa wilaya na wananchi.

Alisema katika kufanikisha dhana ya ujenzi wa uchumi wa viwanda, Serikali inaendelea kuweka mkazo na kipaumbele katika upatikanaji wa malighafi za kilimo na kuwataka wakuu wa mikoa kuhakikisha kuwa maofisa ugani wanatekeleza vyema majukumu yao ya kazi. 

Pia, aliwataka wakuu hao wa mikoa kusimamia makusanyo ya fedha za ndani katika halmashauri na kutumia vyema asilimia tano zinazotengwa kuwawezesha wananchi kupata mikopo ili washiriki katika ujenzi wa uchumi wa viwanda.

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima alisema ili kufanikisha dhana ya uchumi wa viwanda, Serikali haina budi kuwapa msukumo na ushirikiano wa karibu wanasayansi utakaowezesha kuibua viwanda vingi zaidi pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa malighafi za kilimo nchini.

Mbali na Malima, wakuu wengine wa mikoa waliohudhuria mkutano huo ni Robert Luhumbi (Geita), Joachim Wangabo (Rukwa), Galesius Byakanwa (Mtwara) na Christine Mndeme (Ruvuma).

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605   au  0767358654

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images