Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Ataka Wanaopika Data za Uongo Wahughulikiwe

$
0
0
Rais John Pombe Magufuli amefunguka na kuvitaka vyombo vya dola nchini viwashungulikiwe watu ambao wamekuwa wakipika data za uongo za serikali na kuzichapisha sehemu mbalimbali na kusema watu hao wanapaswa kufikishwa mahakamani.

Rais Magufuli amesema hayo leo katika hafla ya kuwatunuku vyeti vya pongezi maaalum kwa wajumbe waliohusika kuchunguza kiwango, aina ya madini katika mchanga wa madini ambao ni makinikia. Rais Magufuli amesema kuwa kuna haja Waziri wa Sheria na vyombo vya dola kuangalia namna inavyowezekana kuwashughulikia watu ambao wanapika data.

"Niwaombe Watanzania wengi tofauti na wale wachache wanaopiga kelele muwapuuze, mtu ambaye anabadili data za serikali na kusema kuwa uchumi umeshuka nadhani wanapaswa kuchukuliwa hatua vyombo vya dola na wewe Profesa Kabudi ni Waziri wa Sheria muanze kuangalia watu wa namna hii ambao kwao kubadili Takwimu wanaona kitu kidogo.

"Nafikiri kuna sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 na kunakifungu kinasema mtu anayebadilisha Takwimu za serikali anaweza kufungwa hata miaka 2 jela, kwanini hatuvitumii hivi? Unakuta mtu anazungumza makusanyo ya serikali yameshuka wakati anajua kabisa si kweli" alisema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli aliendelea kusisitiza kuwa mapato ya nchi hayajashuka ndiyo maana Serikali imeweza kununua ndege zaidi ya sita kwa mpigo, serikali imeweza kujenga barabara kwa fedha za ndani, na kusema serikali imeweza kujenga reli kwa kuwa uchumi wake ni mzuri.

Mahakama Kuu Yasema Lulu Michael Ana Kesi ya Kujibu

$
0
0
Mahakama Kuu imesema msanii wa kike katika fani ya uigizaji wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu Lulu anayekabiliwa na kesi ya kuua bila ya kukusudia ana kesi ya kujibu.

Lulu ambaye yupo nje kwa dhamana anakabiliwa na kesi ya kumuua bila ya kukusudia msanii wa fani hiyo, Steven Kanumba.

Anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 7, 2012, nyumbani kwa marehemu Kanumba, Sinza Vatican jijini Dar es Salaam.

Jaji wa Mahakama Kuu, Samu Rumanyika amesema baada ya upande wa Jamhuri kufunga ushahidi kwa kuita mashahidi wanne amejiridhisha kuwa mshtakiwa ana kesi ya kujibu.

Wakili Peter Kibatala anayemwakilisha Lulu ameieleza Mahakama kuwa mshtakiwa atajitetea chini ya kiapo na ameomba muda kwa ajili ya kufanya maandalizi.

Tiba ya Asili ya Pumu, Vidonda vya Tumbo, Busha na Nguvu za Kiume

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wangu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Ile Tiba Sahihi Ya Matatizo Haya 

CHAZO CHAKE NA VISABABISHO VYAKE:
DALILI:-Mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata Choo vizuri hata ukipata Choo kinakuwa kigumu Kama cha mbuzi ,Misuri  kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. Miguu kuuma na kuwaka au kufa ganzi

TIBA YAKE:
RADI-90-POWER---Ni dawa ya vidonge asilia iliyo tengenezwa kutokana na miti shamba yenye uwezo mkubwa kabisa ktk kutibu matatizo (4) Kwa wakati ==>(1)Huongeza nguvu za kiume maradufu (2)kati ya umri (15-90)(3)hurefusha na kunenepesha uume mdogo kadrii upendavyo inch (6-8)kwa dakika (15)tu.(4)kuchelewa kufika kileleni (5)kuimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa. 

Nini huchangia kuwa na matatizo Kama haha? Kisukari,Presha,Ngiri,Zinaa,Kiuno kuuma, Tumbo kuunguruma na kujaa gesi,kutopata Choo vizuri, Mgongo kuuma. 

RADI-90-POWER:-Hutibu na kumaliza matatizo haya kwa mda mfupi tu na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika(45)kwa tendo(1) na utarudia Mara (5)na zaidi bila kuchoka huanza kazi baada ya dakika( 30)tu.Pia huongeza Hamu ya kufanya tendo la ndoa maradufu(2),Kumbuka tatizo hili si geni, kigeni ni tiba sahihi ya kutibu matatizo haya na pia ina guarantee ya miaka(65)na zaidi. 

Tunatibu :---Kisukari, Presha, uzazi, Ngiri, Pumu, maralia sugu, vidonda vya tumbo, chango aina zote, kifua kikuu na busha bila upasuaji. 

ITUJA NO2:--Nidawa ya mvuto wa biashara, kazi, kupandishwa cheo, kupendwa na mwajiri, kumvuta mme/mke,mpenzi, hawara, mchumba unaye muhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zake kwa dhati utampata kwa lisaa limoja (1)tu na atatulia daima na kumfunga asitoke nje ya ndoa.

BOMBA2:--Ni dawa ya kupunguza matiti makubwa, unene turbo, kitambi,mafuta mwilini,uzito,toa fangasi makovu, chunusi, nyama zembe, michirizi, kwa siku tatu (3)tu.NO7:--Inaongeza makalio, Hips, miguu kwa saizi uipendayo kwa siku (2)tu.

HUDUMA HIZI Na zingine nyingi UTAZIPATA popote TANZANIA Name NJE YA NCHI:--MUONE DR SHARIF AU PIGA SIMU NO:-0659347707, 0763483813 ,0688991509,0659347707.  DR SHARIF

Rais Magufuli amemteua Profesa Luoga kuwa Gavana mpya wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT).

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli, amemteua mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Makinikia, Profesa Florens Luoga kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kuchukua nafasi ya Prof. Benno Ndulu aliyekuwa akiushikilia wadhifa huo.

Rais Dk. Magufuli ametangaza uteuzi huo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam katika hafla ya kuwatunuku vyeti wajumbe wa Kamati ya Makinikia iliyofanikisha kufikiwa makubaliano ya kihistoria baina ya serikali na kampuni ya Barrick Gold yaliyofungua ukurasa mpya kwa Tanzania kunufaika zaidi na madini ya dhahabu.

Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wenyeviti wa kamati za bunge za madini ya Almasi na Tanzanite, baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani.

Rais Dk. Magufuli alimshukuru Spika wa Bunge na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupitisha hati ya dharura sheria ya madini.

Kwa upande wake Gavana mteule Profesa Florens Luoga amesema atafanya kazi kwa uweledi kama sheria za nchi zinavyoelekeza na kuomba ushirikiano kwa wataalamu wengine wa mambo ya fedha ili kuinua uchumi wa taifa.

Aidha, Dk. Magufuli alitumia fursa hiyo kuwashangaa watu wanaozusha kuwa mapato ya nchi yamepungua na kusema kuwa huo ni uongo kwani haiwezekani serikali ikafanya miradi mikubwa ya ununuzi wa ndege kujenga reli ya kisasa, kujenga mradi wa umeme wa Stiegler Gorge kama mapato ya nchi yangekuwa yameshuka.

Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema, Kigaila Benson Atupwa Rumande

$
0
0

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam 'limemtupa' rumande Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema, Kigaila Benson.

Kigaila anayetuhumiwa kutoa lugha za kichochezi Oktoba 12 katika mkutano wake na waandishi wa habari, alikutana na kadhia hiyo jana aliporipoti kituoni kituo kikuu cha kanda hiyo.

Mwanasheria wa Kigaila, Frederick Kihwelo akizungumza na waandishi wa habari nje ya kituo hicho leo Jumatatu amesema hatima ya dhamana ya mkurugenzi huyo itaamuliwa kesho Jumanne.

''Amehojiwa kwa masaa 3 kuanzia saa 7 hadi saa 10  na amehojiwa kwa makosa aliyoyafanya katika mkutano wake wa Oktoba 12 na wamekataa kutoa dhamana labda hadi kesho,'' amesema Kihwelo.

''Lakini makosa yake yana dhamana ila wametueleza wanaoweza kuamua ama kupata dhamana au kukosa hawapo ofisini,"

Mwanasheria huyo amesema katika mkutano huo alizungumza mambo mengi ikiwamo kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na kutekwa kwa Ben Saanane ambaye ni msaidizi wa mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.

Kauli ya Profesa Luoga Baada ya Kuteuliwa Kuwa Gawana wa BoT

$
0
0
Gavana mteule wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Florens Luoga amesema amepokea kwa heshima kubwa dhamana aliyopewa na Rais John Magufuli na anatambua changamoto za nafasi hiyo.

Profesa Luoga ambaye ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) - Taaluma, amesema leo Jumatatu Oktoba 23,2017 kuwa atatumia wataalamu wa BoT kufanya kazi.

Amesema anahitaji ushirikiano wa kila mtu katika kufanikisha kazi aliyopewa.

“Nimepokea kwa heshima dhamana niliyopewa nikitambua kwamba zipo changamoto. Nitakwenda kujifunza zaidi kwa sababu sijawahi kuwa Gavana, nitatumia wataalamu waliopo katika kutekeleza majukumu yangu,” amesema Profesa Luoga.

Rais Magufuli Julai 11,2017 alimteua Profesa Luoga kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), akichukua nafasi ya Bernard Mchomvu ambaye uteuzi wake ulitenguliwa Novemba mwaka jana na bodi hiyo kuvunjwa.

Profesa Luoga ni mtaalamu katika masuala ya sheria za kodi na amefundisha katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tangu mwaka 1986 kabla ya kupandishwa cheo na kuwa profesa mshiriki (Associate Professor) mwaka 2005.

Ameshika nafasi mbalimbali chuoni hapo ikiwa ni pamoja na mwenyekiti wa kamati ya misaada ya kisheria katika kitivo cha sheria mwaka 1993 - 1995, mkurugenzi wa masomo ya shahada za awali (2005 - 2009), katibu wa baraza la chuo kikuu (2009 - 2013) na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo – Taaluma (2013 hadi sasa).

Profesa Luoga aliyezaliwa mwaka 1958 ni wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Alihitimu shahada ya kwanza ya sheria UDSM mwaka 1985. Baadaye alikwenda kusoma Shahada ya Uzamili (LLM) katika chuo cha Queen’s University cha Canada (1988).

Mwaka 1988 alihitimu Shahada ya Uzamili ya Sheria za Kimataifa (MIL) katika Chuo cha Lund University cha Sweden (1991) na Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Warwick cha Uingereza mwaka 2003.

Rais Magufuli aliponda gazeti la TanzaniaDaima

$
0
0
Jana nilikuwa nasoma gazeti moja, katika ukurasa wa mbele wameandika “Asilimia 67 ya Watanzania wanatumia ARVs,” nilipo liona nikajua wamekosea bahati mbaya nikaamua kufungua ndani nione kama walirekebisha.

Nilipofungua ndani, nilikuta kichwa cha habari kile kile, nikasema ngoja nisome, labda watakuwa wamerekebisha humu ndani, lakini habari ikawa vile vle kuwa watanzania 67% wanatumia dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI.

Hayo yamesemwa leo na Rais Magufuli alipokuwa anatoa wito wake kwa waandishi wa habari nchini kuwa wazalendo na kuandika habari za kujenga kwani akiandika habari za kupotosha, wanaichafua Tanzania.

Rais alisema hayo kwenye hafla ya kutoa vyeti kwa wajumbe wa kamati mbalimbali zilizohusika katika mchakato mzima wa madini, na kufanikisha kufikiwa kwa makubaliano ambayo yameweka mwanzo mzuri wa serikali kuanza kunufaika na rasilimali zake.

Rais alisema baada ya kusoma hiyo habari alishtuka, na kuamua kumpigia simu Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ili apate ufafanuzi, na ndipo waziri akasema taarifa hiyo si ya kweli.

Waziri Mwalimu alisema kuwa, alichokisema wakati wa Tsh 860 milioni kwa ajili ya kununua dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI ni kwamba, jumla ya watanzania milioni 1.4 wameathirika na virusi vya UKIMWI na kwamba miongoni mwao (walioathirika), ni asilimia 67% pekee wanaotumia ARVs na kwamba lengo la serikali ni kufika asilimia 90% ifikapo mwaka 2020.

Taarifa hiyo iliandikwa kwatika gazeti la kila siku la TanzaniaDaima ambalo hutolewa na Kampuni ya Free Media inayomilikiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Freeman Mbowe.

Rais Magufuli alisema kwamba, taarifa kama hiyo inapoandikwa, inamadhara makubwa kwa nchi kwani hata wawekezaji hawawezi kuja kwenye nchi ambayo inaelezwa asilimia 67 ya watu wake wameathirika na UKIMWI kwa sababu anajua hata akija hatopata nguvu kazi ya kutosha kufanyakazi kwenye kiwanda/kampuni yake.

Lakini pia alisema, taarifa hiyo inaweza kutishia hata watalii waliopanga kuja kutembelea vivutio mbalimbali vya kitalii vilivyopo nchini Tanzania.

Katika hatua nyingine, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amelazimika kutolea ufafanuzi kauli yake aliyoitoa akiwa Sumbawanga mkoani Rukwa kuwa wale wote waliojenga katika maeneo ambayo wamevamia au wamewadhulumu watu wengine, serikali itabomoa nyumba zao.

Waziri amelazimika kutolea ufafanuzi kauli hiyo kutokana na magazeti ya leo Oktoba 23 kuripoti taarifa hiyo kwa namna ya kuogofya, huku baadhi ya vichwa vya habari vikisomeka, Bomoa Bomoa kubwa yaja (Nipashe), Bomoa Bomoa ya karne yaja (Mtanzania).

Akiongezea kwenye taarifa hiyo ya bomoa bomoa, Rais alisema kuwa waandishi hao wangeweza wakaandika Waliojenga bila vibali kukiona cha moto na watu wakasoma badala ya kuandika vitu ambavyo vinapotosha na kuwatia hofu wananchi.

Mwigamba Amjibu Zitto Kabwe

$
0
0
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa ACT -Wazalendo, Samson Mwigamba ametaja sababu mbili zilizomfanya kukataa wito wa kikao cha Kamati ya Uongozi ya chama hicho kwa ajili ya mahojiano.

Jumamosi Oktoba 21,2017 Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe aliwaeleza waandishi wa habari kwamba Kamati ya Uongozi ya chama hicho, ilimwita Mwigamba ili atoe maelezo baada ya kukituhumu chama hicho kukiuka misingi yake lakini hakufika.

Zitto alisema kamati hiyo baada ya kukutana na kujadiliana ilibaini hakuna misingi iliyokiukwa.

Mwigamba aliyekihama chama hicho na kujiunga na CCM, leo Jumatatu Oktoba 23,2017 amesema hakuona jambo jipya litakalojadiliwa dhidi yake katika kikao cha Kamati ya Uongozi kwa kuwa mengi aliyoyalalamikia alishayatolea ufafanuzi kwenye barua yake ya kujiuzulu.

Amesema jambo lingine lililomfanya kutohudhuria kikao hicho ni Kamati ya Uongozi kuwa na wajumbe 12 badala ya watano waliopo kwa mujibu wa Katiba ya ACT-Wazalendo.

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa chama hicho, Ado Shaibu amesema hawana muda wa kulumbana na Mwigamba na wanaheshimu uamuzi wake wa kujiuzulu, hivyo wanamtakia kila la kheri kwenye safari yake ya kisiasa.

Lulu Michael Aieleza Mahakama Jinsi Alivyogombana na Kanumba na Jinsi Alivyofariki

$
0
0
Kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili muigizaji wa filamu Tanzania, Elizabeth Michael (Lulu), imeendelea leo ambapo upande wa mshtakiwa umeanza kutoa utetezi wake.

Akisimulia jinsi ilivyokuwa siku ya tukio, Lulu amesema marehemu alikuwa akimpiga na panga baada ya kutokea ugomvi uliotokana na wivu wa mapenzi, alipomuona akiongea na simu.

"Nilikuwa nataka kutoka ila marehemu 'Kanumba' alinikataza, alikuwa hataki nitoke, nilipomwambia natoka na marafiki zangu alinikimbiza na taulo na mimi nilikuwa naogopa kupigwa, mara nyingi alikuwa ananipiga kila akilewa na sio kwa akili zake, alipoona simu yangu inaita akahisi ni simu ya mwanaume akasema kwanini naongea na simu ya mwanaume mbele yake? Marehemu akaingia uvunguni akatoa panga akasema leo nakuua huku akinipiga na panga kwenye mapaja", ameelezea Lulu.

Lulu ameendelea kusimulia...."Marehemu alianguka mwenyewe na kujigonga kwa nguvu na kuinuka sehemu nyingine alikuwa kama anatapatapa, nilimwambia Seth kuwa Kanumba amedondoka na akajaribu kumuamsha hakuamka akasema anaenda kumuita daktari, alivyosema anaenda kumuita daktari na mimi nikaondoka nikiogopa anaweza akaamka akaanza kunipiga, niliondoka nikawasha gari kuelekea Coco Beach kutuliza akili".

Muigizaji huyo ameendelea kusimulia kwamba ..."Nilivyofika Coco beach meseji zilianza kusambaa kuniuliza kuwa nasikia Kanumba amefariki, nikampigia 'Kidume'  ambaye ni rafiki yake Kanumba kumuuliza Kanumba yupo hospitali gani niende kumuona, akaniambia wewe usije hospitali, niambie uko wapi, tukakubaliana tuonane Bamaga, tulivyokutana Bamaga alikuwa kama anataka kuongea na mimi ghafla wakaja askari kunikamata".

Pamoja na hayo muigizaji huyo ameithibitishia mahakama kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na marehemu (Steven Kanumba) kwa muda wa miezi minne kabla ya kukutwa na mauti.

Mahakama Kuu imeghailisha kesi hiyo mpaka siku ya kesho Oktoba 24, ambapo itasikilizwa tena

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Octoba 24

Waziri Mwakyembe mgeni rasmi mkutano wa viongozi wa dini

$
0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe atakuwa mgeni rasmi katika mkutano wa viongozi wa madhehebu ya dini wenye lengo la kubadilishana mawazo kuhusu mambo mbalimbali yakiwamo masuala ya kiimani, kijamii na kiuchumi.

Taarifa hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Msaidizi Lugha kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi Hajjat Shani Kitogo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mkutano huo.

“Sera ya Utamaduni ya Mwaka 1999 Sura ya Nane inazungumzia Malezi na inasema mafunzo ya dini yatakuwa sehemu ya malezi ya watoto ili kusisitiza Maadili,Malezi Mema, Kazi, Kustahiana na Kuvumiliana,” alisema Hajjat Kitogo.

Akiendela kuzungumza katika mkutano huo Mkurugenzi Msaidizi huyo alisema serikali inatambua umuhimu wa Viongozi wa Dini katika ulezi wa jamii na maendeleo ya Taifa na ndiyo maana imeona ni vyema kukutana nao na kujadili ni namna gani itaweza kulisimamia taifa katika kufikia malengo.

Naye mmoja wa washiriki wa mkutano huo Bi Hadija Kisubi alitoa maoni yake na kusema anaamini viongozi wa dini wanamchango mkubwa katika kujenga nidhamu ya kwa taifa sababu ya neema ya mungu iliyondani ya viongozi hao pale wanatoa maelekezo kwa umma.

Pamoja na hayo mkutano huo umebeba Kauli Mbiu inayosema “Imani na Uzalendo Kuelekea Uchumi wa Viwanda” na utafanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) tarehe 25/10/2017.


Tuzo za Mawaziri na Wabunge watakaofanya vizuri zazinduliwa

$
0
0
Kamati ya utawala ya shindano la tuzo za utekelezaji maendeleo kwa kasi ya juu kwa Wabunge na Mawaziri (THSDA) imezindua shindano la kutoa tuzo kwa Wabunge na Mawaziri watakaofanya vizuri katika kutekeleza majukumu ya kuwaletea Wananchi maendeleo.

Hayo yamesemwa Jijini Dar es Salaam na Katibu wa Kamati hiyo Bw. Wilson Maage alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, juu ya uzinduzi wa shindano hilo ambalo litafanyika kwa muda wa miezi miwili.

“Tuzo hizo zimetokana na kuwepo wazo bunifu (intellectual property) ambalo azma yake ni kuhamasisha utekelezaji wa shughuli za huduma na maendeleo kwa wananchi wa Tanzania na kupima kasi ya utekelezaji wa shughuli hizo kwa viongozi wa ngazi mbalimbali katika sekta na taasisi za kiserikali hapa nchini,” alifafanua Maage.

Aliendelea kusema kuwa, vigezo vitakavyotumiwa katika kuteua viongozi hao ambao ni wabunge pamoja na Mawaziri ni pamoja na kuwa mtetezi wa Wananchi wake bila uoga akiwa ndani au nje ya Bunge, mtendaji bora wa maendeleo yenye kuonekana, sifa ya kutoa hoja zenye tija kwa kutumia lugha ya staha bila matusi, sifa ya utekelezaji wa haraka apatapo matatizo ya Wananchi wake pamoja na sifa ya kutetea demokrasia, uhuru na kutetea wanyonge.

“Faida za shindano la tuzo hizi ni kwamba zinaweka Wananchi karibu na viongozi, kuchochea utekelezaji huduma na maendeleo kwa kasi ya juu, utawla bora na uwajibikaji wa viongozi kwa Wananchi, uhusiano mzuri kati ya serikali na Wananchi na kuimarisha furaha, utulivu na amani,” alieleza Maage.

Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa Kamati hiyo, Herman Mnenuka alisema kuwa Wananchi ndiyo nguzo kuu ya kupata kiongozi atakayepata tuzo hiyo kwani wao ndio watakaopendekeza majina ya wabunge pamoja na mawaziri wanaofaa kuwania tuzo hiyo.

Katika tuzo hiyo, hatua ya kwanza, wananchi wanapaswa kupendekeza wabunge 15 kwa kila kigezo shindanishi, pia Wananchi watawateua Mawaziri 5 kwa kila kipengele shindanishi kwaajili ya kuingia kwenye ushindani wa tuzo hiyo na wabunge watano na Mawaziri watatu watakaopata kura nyingi kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS) kutoka kwa wananchi wataingia katika fainali ya king’anyiro kuwania tuzo hiyo.

Aidha aliongeza kuwa, katika hatua nyingine, wananchi kupitia simu watawachuja washiriki waliofika hatua ya fainali kwa kutuma SMS na mbunge pamoja na waziri atakayepata kura nyingi ndiye atakaye kuwa mshindi katika kilele cha tuzo hiyo kitakachofanyika tarehe 23 Desemba Mwaka huu.

“Niwaombe wananchi washiriki kikamilifu ili kuweza kupata kiongozi anayejishughulisha na anayechapa kazi kupitia tuzo hii na mwisho wa kilele tutapata mshindi wa kila kipengele kilichowekwa ambacho kina tija muhimu katika taifa kupitia waheshimiwa wabunge na mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alieleza Mnenuka.

Aidha aliongeza kuwa, Wananchi watapendekeza majina kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu kupitia namba 15555 kwa mitandao ya Tigo, Airtel, Vodacom, Halotel Smart na Zantel na kila SMS itatozwa gharama ya shilingi 500 vilevile kutakuwa na vipindi vya radio runinga na magazeti ili kuwakumbusha mwenendo na hatua za shindano la tuzo za THSDA hadi siku ya kilele.

Hizi ni tuzo za kwanza kuandaliwa hapa nchini na kamati hiyo ambazo zitafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha.

Jinsi Supu Ya Ulimi Wa N’gombe Inavyo Tumika Katika Tiba Ya Kunenepesha Mwili Ulio Konda Na Kudhoofu Kwa Sababu Ya Maradhi Mbalimbali

$
0
0
Kwa  watu  ambao  wamekonda  na  kudhoofu  mwili  kwa sababu  ya  maradhi  mbalimbali  na wanataka  kurejesha  afya  zao  katika  hali ya  kawaida, wanashauriwa  kutumia dawa za  asili  na  vyakula  mbalimbali  ambavyo  husaidia  kuurejesha  mwili  katika  hali  yake  ya  kawaida.

Dawa-lishe  ya  kuongeza, kurutubisha  na  kunenepesha  mwili, ni  dawa  maalumu  kwa  watu  wenye  uzito  wa  chini  (  Under weight ) ambao  wanataka  kuongeza  mwili  na  uzito.
 
Dawa  hii  huwasaidia  watu  ambao  miili  yao  imedhoofu  kutokana  na  sababu  mbalimbali  kama  vile  kuugua  magonjwa  na  maradhi  mbalimbali.

Na  kwa  wale  watu  wembamba  ambao  wanataka  kuongeza  miili  yao, dawa  hii  huwasaidia  vizuri  sana.
MAHITAJI   YA  DAWA –LISHE
 i. Dawa –lishe vijiko  viwili vikubwa.
ii.Asali  ya  tende  vijiko  vitano  vikubwa.
iii. Tangawizi  ya  unga  vijiko  vikubwa  viwili
iv. Unga  wa ufuta
v.Maziwa  fresh nusu  lita
vi.Maji  ya  moto  kiasi  cha  milimita  mia  mbili  na  hamsini  ( 250 mills  )

MATAYARISHO
 i. Chukua  vijiko  vinne  vyenye  dawa  lishe  yako  kisha  chemsha  na  nusu  lita  ya  maji  hadi  mchanganyiko  wako  utokote  halafu  ipua, chuja , makapi  weka  pembeni  kisha  hifadhi  juisi  yako.
ii.Tayarisha  uji kwa  kutumia  unga  wa  ufuta  na maziwa  fresh
iii.Chukua  vijiko  viwili  vikubwa  vya tangawizi  ya  unga  kisha  changanya  kwenye  kikombe  cha  maji  ya  moto  chenye  ujazo  wa  milimita  mia  mbili  hamsini  (  250  mills )

MATUMIZI:
i.Tumia  kunywa  nusu  lita  ya  dawa –lishe  yako  kisha
ii.Tumia kula  vijiko  vinne  vikubwa  vya  asali  ya  tende
iii.Kisha tumia  kunywa  vikombe  vinne  vya  uji  wa  ufuta  ulio changanywa  na  maziwa  fresh
iv.Halafu  kunywa  glasi  moja  ya  moto  iliyo  changanywa  na  vijiko  viwili  vikubwa vya tangawizi  ya  unga.
 
UTAFANYA  HIVYO  MARA  MBILI  KWA  SIKU  KWA  MUDA  WA  SIKU  THELATHINI  MFULULIZO.
Baada  ya  siku  thelathini, utaangalia  na  kujitathmini  kiasi  ulicho  ongezeka. Kama  utataka  kuendelea  kuongezeka  zaidi, utaendelea  kutumia  dozi  hii  hadi hapo utakapo fikia kiwango  utakacho  rizika  nacho.
 
SUPU  YA  ULIMI  WA  N'GOMBE. N.B : KAMA  UTAWEZA  UNASHAURIWA PIA, KUWA  UNATUMIA  SUPU  YA  ULIMI  WA  N'GOMBE  MARA  KWA  SIKU KWA  KADRI UTAKAVYO WEZA. HII KWA  SABABU  ULIMI  WA N'GOMBE UNATAJWA  KUWA  NA  KIASI  KIKUBWA  CHA PROTINI  ITOKANAYO  NA  WANYAMA  AMBAYO INATAJWA  KUWA  MUHIMU  SANA  KATIKA  UKUAJI WA  MISULI  YA  SEHEMU MBALIMBALI  ZA  MWILI.

JINSI  YA KUTUMIA  SUPU YA  ULIMI  WA  N'GOMBE  KATIKA LISHE  YA  KUNENEPESHA  MWILI
Muhitaji  anashauriwa kutumia  walau robo kilo  au  nusu kilo  ya  supu ya  ulimi  wa  n'gombe kwa siku. Ni nzuri  sana  kwa  mtu  anae  tumia  dawa lishe  ya  kunenepesha  mwili. Hata  hivyo  unashauriwa  kutokutumia  supu  hii  kwa wingi  kwani  inaweza  kuzidisha  kiwango  cha  lehemu (cholestrol)  mwilini. Unashauriwa  kutumia  kwa  busara  pamoja na  vitu vilivyo orodheshwa  hapo juu, yaani  Dawa Lishe, Asali  ya  Tende  na  Uji  wa  Ufuta.

=======================================

JINSI YA  KUIPATA  DAWA  LISHE:
 Dawa  hii  inapatikana  katiuka  duka  la dawa  asilia  la  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAN  katika  eneo  la  TABATA  MAKOKA  karibu  na  SHULE  YA  SEKONDARI  YA  MT. ANNUARITE.
 
 Unaweza  kufika  moja  kwa  moja  katika  ofisi  zetu  AU  unaweza  kuletewa  mahali popote  ulipo  jijini  Dar   Es  salaam.
 
Kwa  wakaazi  wa  ZANZIBAR  watatumiwa dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti  na  kwa  wateja  wetu  wa  ughaibuni watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.
 
Kwa  mawasiliano  zaidi  wasiliana  nasi  kwa  simu
0766  53  83   84

Pata Tiba Asili ya Fangasi, Harufu Mbaya, Vidonda vya Tumbo na Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume wengi Wanasumbuliwa na tatizo la kushidwa kushiliki vyema tendo hilo na kuwapelekea kuwa na mawazo mengi ambayo hayana majibu. Usikate tamaa MKWASHA POWER Ndio suluisho lako ina uwezo wakutibu na kumaliza tatizo hilo kwa mda mfupi sana 
 
(1)Huimarisha misuli ilio legea nakukufa uume usimame vizuri 
(2)Huongeza ham ya tendo la ndoa na itakufanya uweze kuludia tendo hilo zaidi ya Mala Tatu bila kuchoka 
(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa Dk10-25 kwa tendo moja. Itamfanya mwenzi wako kufurahia  tendo hilo zaidi .Huongeza saizi ya maumbili madogo na kulefisha saizi uipendayo 

NINI CHANZO CHA TATIZO HILO;  Tatizo hili husababishwa na msongo wa mawazo, ugongwa wa kisukari, presha, utumiaji wa pombe kali kupita kisa, utumiaji wa dawa za kulevya, tumbo kujaa gesi, NK 

Kutana na DR.ATHUMANI ndio bingwa wa matatizo hayo pia ana tibu matatizo ya uzazi kushidwa kupata mimba mimba karibia, kupunguza unene (kitambi) vuidonda vya tumbo, fangasi sugu, maumivu wakati wa tendo la ndoa, kukosa ham ya tendo, kuondo harufu mbaya ukeni, Anatikana mbagala 

==>Piga simu;  0676969816- DR. ATHUMANI

Kenyatta akutana na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, IEBC

$
0
0

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, amekutana na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, IEBC, kabla ya uchaguzi mpya uliopangwa kufanyika siku ya Alhamisi Oktoba 26.

Wiki iliyopita Mwenyekiti huyo Wafula Chebukati alikutana na kiongozi wa Muungano wa Upinzani, Nasa, Raila Odinga.

Mapema wiki iliyopita Bw. Chebukati aliomba mazungumzo ya moja kwa moja kati ya rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga. Mazungumzo ambayo yalipuuziwa na rais Kenyatta.

Raila Odinga alitangaza kutoshiriki uchaguzi wa Oktoba 26. Lakini baada ya kukutana na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, alilegeza msimamo na kusema anaweza kubadilisha mawazo na kurejea kwenye kinyang'anyiro hicho iwapo kutakuwa na mazungumzo na kufanyika kwa mageuzi ndani ya Tume ye Uchaguzi.

Bw. Chebukati ameviambia vyombo vya habari kwamba anapanga kuwakutanisha Raila Odinga na Uhuru Kenyatta kabla ya uchaguzi mpya wa urais Alhamisi wiki hii.

Waziri Mkuchika atangaza kiama kwa watumishi wala rushwa

$
0
0
Serikali imesema mtumishi anayefanya kazi katika Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (Mkurabita) akibainika kushiriki vitendo vya rushwa atachukuliwa hatua mara moja.

Mkurabita ilianzishwa kwa lengo la kumsaidia anayemiliki ardhi kimila atambulike kisheria na apewe hati itakayomwezesha kupata mkopo ili aendeleze biashara.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Kapteni mstaafu George Mkuchika alitoa onyo hilo alipotembelea taasisi hiyo. Alisema asingependa kusikia kuna mwananchi anatafuta hati au wanataka eneo lake lipimwe lakini mtumishi wa Mkurabita anamweleza kuwa ili kazi yako iende haraka lazima ‘waonane’ jambo ambalo si sawa.

“Naomba muelewe, anayepambana na rushwa ni Rais mwenyewe kwa sababu Takukuru (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa) ipo chini yake. Pia, Mkurabita ipo chini ya Ofisi ya Rais Ikulu. 

“Maana yake Waziri wa Mkurabita ni Rais John Magufuli, mimi namsaidia kwa hiyo mnapofanya kazi hapa mjue mkuu wa nchi ndiyo mwenye wizara,” alisema Kapteni Mkuchika ambaye pia ni Mbunge wa Newala Mjini (CCM).

Mratibu wa Mkurabita, Seraphia Mgembe alisema licha ya mafanikio walionayo kuna changamoto ya kutopata fedha za kutosha ili kujiendesha. Alisema mwaka 2009 Mkurabita iliomba Sh43 bilioni kwa ajili kufanya shughuli zake kulingana na mpango kazi wao, lakini fedha walizopata hadi sasa ni asilimia 55 sawa na Sh23 bilioni.

Mahakama Kuu Yamtaka Josephine Mushumbusi Katika Kesi ya Lulu Michael

$
0
0
Kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili msanii wa fani ya uigizaji filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu Lulu imeahirishwa hadi kesho Jumatano Oktoba 25,2017.

Kuahirishwa kwa kesi hiyo leo Jumanne Oktoba 24,2017 kunatokana na Jaji Sam Rumanyika kuamuru polisi aliyechukua maelezo ya shahidi Josephine Mushumbusi kufika mahakamani.

Awali, Wakili Peter Kibatala anayemwakilisha Lulu katika kesi hiyo aliieleza Mahakama Kuu kuwa shahidi huyo hapatikani kwa kuwa yuko nchini Canada.

Kibatala aliiomba Mahakama iyapokee maelezo yake kama sehemu ya ushahidi.

Wakili wa Serikali, Faraja George alisema hapingi kuwasilishwa maelezo hayo mahakamani, bali anapinga kuwasilishwa na wakili Kibatala kwa kuwa yeye si aliyeyaandika.
 
Shahidi huyo ni wa pili wa upande wa utetezi baada ya Lulu kujitetea jana Jumatatu Oktoba 23,2017. Alijitetea  baada ya Jaji Rumanyika kusema ana kesi ya kujibu.

Lulu ambaye yupo nje kwa dhamana anakabiliwa na kesi ya kumuua bila ya kukusudia msanii wa filamu, Steven Kanumba.

Anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 7, 2012, nyumbani kwa marehemu Kanumba, Sinza Vatican jijini Dar es Salaam.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605   au  0767358654

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Mkuu wa Wilaya Aingilia Kati Ugomvi wa FFU na Wananchi wa Ukonga Dar

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amewapiga marufuku askari wa kikosi cha FFU na kusema hataki kuwaona wakisumbua wananchi katika eneo la Ukonga Dar es Salaam na kutaka waliohusika wachukuliwe hatua kwa kitendo walichofanya kuwapiga wananchi.

Sophia Mjema amesema hayo alipowatembelea wananchi hao ambao wamelalamika kufanyiwa fujo na kupigwa na askari hao kwa siku mbili kutokana na askari mmoja kuuwawa na watu wasiojulikana.

 Mkuu wa Wilaya anasema kuwa askari hao walipaswa kufanya uchunguzi kujua ni watu gani walihusika kufanya mauaji ya askari huyo na si kwenda kufanya fujo na kuwapiga wananchi pasipokuwa na sababu.

"Kama kuna askari alipatikana ameshafariki utaratibu ulikuwa uchunguzi ufanyike ili waweze kujiridhisha baada ya hapo wale ambao wangetambulika ndiyo wangechukuliwa hatua lakini kwa hili halikubaliki, kwa hiyo nasema hivi askari wote waliohusika kufanya fujo na vurugu wachukuliwe hatua za kinidhamu na huku barabarani sitaki kuona FFU yoyote anasumbua wananchi" alisema Mjema

Aidha Mkuu wa Wilaya huyo ametaka wananchi ambao wameumizwa na askari hao kwa vipigo kwa siku mbili mfululizo waweze kujiorodhesha kwa majina ili wapatiwe matibabu na kusema wale ambao wamepoteza mali zao utaratibu utafanyika kuona nini kifanyike

FFU waingilia kati kuwatuliza abiria wa FastJet Mwanza

$
0
0
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia(FFU) leo wamelazimika kuingilia kati kutuliza vurugu zilizoazishwa na abiria 75 waliokosa usafiri wa ndege ya kampuni ya FastJet kutoka Mwanza kwenda Dar es Salaam kutokana na hitilafu za kiufundi.

Abiria hao waliokaa uwanjani hapo kwa zaidi ya saa nne kuanzia saa 3:00 asubuhi walipotakiwa kusafiri hadi saa 7:00 mchana, walianzisha vurugu kushinikiza kupatiwa usafiri.

Akizungumzia kadhia hiyo, Meneja wa FastJet Mkoa wa Mwanza, Ezekiel Manyiga amesema ndege iliyotakiwa kusafirisha abiria hao haikufika kutoka jijini Dar es Salaam kutokana na kupata hitilafu ya kiufundi.

“Hata abiria waliotakiwa kusafiri kutoka Dar es Salaam kuja Mwanza hawajafika hadi sasa; tunafanya kila lililo ndani ya uwezo wetu kutatua tatizo hili,” amesema Manyiga

Ilipofika saa 7:00 mchana jana, uongozi wa kampuni hiyo ulifikia uamuzi wa kuwarejeshea nauli abiria waliokuwa tayari kupokea fedha zao ili kutafuta usafiri mwingine pamoja na Sh30, 000 ya kujikimu kwa kila abiria aliyekosa usafiri.

“Watakaokuwa tayari kusubiri ndege yetu watalazimika kusafiri kesho (Jumatano)  kwa sababu ndege tayari imejaa,” amesema Manyiga
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images