Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Uteuzi wa Rais Robert Mugabe watenguliwa

0
0
Shirika la Afya Dunia (WHO) limetengua uteuzi wa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe kuwa Balozi Mwema wa Magonjwa Yasiyoambukiza (NCDs) barani Afrika kutokana na malalamiko ya watu mbalimbali wakielezea kutoridhishwa na uteuzi huo.

Katika taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti ya shirika hilo, Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Tedros Adhano amesema kuwa, kwa siku chache zilizopita, nimefiriki kuhusu uteuzi wangu wa Mhe. Mugabe kama balozi mwema, na baada ya kutafakari kwa kina, nimeamua kutengua uteuzi huo.

"Nimesikiliza kwa kina mawazo ya wote walioeleza kuhusu kutoridhishwa kwao na uteuzi huo, na nimesikiliza madai mbalimbali yaliyoibuliwa. Pia nimewasiliana na serikali ya Zimbabwe, na tukafikia kwenye hitimisho kuwa uamuzi huu ni bora kwa manufaa ya shirika letu, "aliandika Tedros Adhano.

Baadhi ya watu waliokosoa uteuzi huo wa Rais Mugabe walisema kuwa, katika kipindi cha miaka 30 cha uongozi wa Rais Mugabe, mfumo wa afya wa taifa hilo umeporomoka pakubwa.

Wakosoaji walisema kuwa hospitali hazina dawa, watumishi wa afya wakati mwingine hawalipwi stahiki zao, na kiongozi huyo aliyekaa madarakani tangu uhuru, husafiri nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

Licha ya kutengua uteuzi huo, Tedros amesema kuwa, bado yupo kwenye nafasi ya kufanya kazi na nchi yeyote na kwamba wapo tayari kushirikiana na mtu yeyote katika kujenga mfumo wa afya ulio imara.

Aidha, amewashukuru wote waliotoa mawazo yao kuhusu uteuzi huo na kusema kuwa, anategemea ana mijadala ya kujenga ili kuweza kutekeleza majukumu aliyochaguliwa kuyafanya.

Jinsi Mbuzi Anavyo Tumika Katika Tiba Dhidi Ya Tatizo La Nguvu Za Kiume.

0
0

Wanyama  na  ndege  au bidhaa ama  vitu  vitokanavyo nao  huweza  kutumika  katika  tiba dhidi  ya magonjwa  na  matatizo  mbalimbali  ya  kifaa.

Mbuzi  Dume  aliye  komaa.  Nyama, korodani  na  dhakari  zinazo  faa  kutumika  kama  lishe  maalumnu  kwa  wanaume  wenye  tatizo  la  ukosefu na  upungufu  za  kiume vinatakiwa  kutokana  na  mbuzi  beberu  aliye  komaa 
 
Katika   makala  ya  leo  tutatazama  namna  mnyama mbuzi  anavyo  tumika  katika  tiba  asilia  ya  tatizo  la  ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume.

Mbuzi  jike  na dume  kwa pamoja  wanaweza  kutumika  katika  tiba  dhidi  ya  tatizo  la  ukosefu  na  upungufu  wa  nguvu  za  kiume kwa  namna  tofauti  tofauti.

Wanyama  hawa  hawatumiki kama  tiba  persee  ila  wanatumika  kama  lishe  maalumu  kwa   watu wanao  tumia  tiba  asilia za  tatizo  la  nguvu  za  kiume .
 
Matumizi  ya  mnyama  huyu  si  tu  kwa  wanaume  wenye  tatizo  la  ukosefu  na  ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, bali  hata  kwa  wanaume  ambao  hawana  tatizo  hilo  lakini  wanataka  kuzitunza,kuzilinda  na / ama  kuziimarisha  nguvu  zao.
 
JINSI  MBUZI  WANAVYO  TUMIKA  KATIKA  TIBA  YA  TATIZO  LA  UKOSEFU  NA/ AMA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mbuzi  anaweza   kutumika  kama  sehemu  ya  tiba  -lishe  ama  lishe  maalumu  kwa  wanaume  wanao  sumbuliwa  na  tatizo  la  ukosefu  na  /ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  kufuata  utaratibu  ufuatao

A.   MBUZI  JIKE

Mahitaji
1.    Lita moja  ya maziwa  ya  mbuzi
2.     Punje kumi  na nne  za  tende  au vijiko  vikubwa  vinne  vya  asali  ya  tende
3.    Kijiko  kimoja  kikubwa  cha unga  wa  hiriki (Unga  wa  hiriki  unapatikana  kwa  kusaga  hiriki. Kwa  lugha  nyingine, unga wa  hiriki  ni  hiriki  iliyo  sagwa )
4.      Vijiko  viwili  vidogo  vya  dawa  asilia  ya  Jiko.
5.    Kikombe  cha  maji ya  moto au vuguvugu  chenye  ujazo  wa  mills  250.

Matayarisho
1.     Changanya  lita  moja  ya  maziwa fresh ya  mbuzi  na  punje  kumi na  nne  za  tende au  changanya  hiyo lita  moja  ya  maziwa  fresh  ya  mbuzi  na vijiko  vikubwa  vinne  vya  asali  ya  tende.  Tia  kwenye  chupa  au chombo  chochote  kisafi na  salama  na  ambacho  unaweza  kukitumia  kuhifadhia, kisha  koroga  na  uhifadhi  ndani  ya  friji  halafu  acha  mchanganyiko  wako usiku kucha.

2.    Ikifika  asubuhi, changanya  mchanganyiko huu na  kijiko kimoja  kikubwa  cha  hiriki  iliyo  sagwa, vijiko  vitatu  vya  dawa  ya  jiko  iliyo  katika  mfumo  wa  unga unga  kisha  koroga  halafu  gawanya  dawa yako katika   portion mbili  zenye  ujazo  sawa.

MATUMIZI
Tumia  kunywa  lishe hii  mara  mbili kwa  siku  asubuhi  na  usiku na utafanya  hivyo  mara  moja  kwa  wiki  kwa  wiki  nne  mfululizo. Hapa  maana  yake  ndani  ya mwezi mmoja, utatakiwa  kuwa umetumia  lishe  hii  mara  nne  tu.

JAMBO  LA  KUZINGATIA
 Lishe  hii  inaenda  sambamba na  matumizi  ya  dawa  asilia  ya  jiko.  Unashauriwa  kutumia  lishe  hii katika  kipindi  ambacho  unatumia  jiko  pia. Ingawa  lishe  hii  utakuwa ukiitumia  mara  moja kwa  wiki kwa muda  wa  wiki  nne, dawa  ya  jiko  utatakiwa  kuitumia  mara  mbili  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku thelathini.
 
B: MBUZI  DUME
Sehemu  ya  mbuzi  dume  inayo  tumika  katika  tiba  dhidi  ya  tatizo  la  ukosefu  na  upungufu  wa  nguvu  za  kiume  ni  KORODANI, NYAMA (HUSUSANI NYAMA  YA MBAVU  AU SHINGO )  pamoja na  DHAKARI.

MAHITAJI
i.   Korodani  za  mbuzi zilizo
ii.  Pink  salt  ( Chumvi  ya  pink  ) kijiko kidogo kimoja
iii. Dawa  ya  jiko ( Eidha  iliyo  sagwa  katika  unga  au  iliyo katika  mfumo  wa  mizizi  )
iv.  Sufuria  lenye  uwezo  wa kubeba  kuanzia  lita tatu  za  maji  na  kuendelea
v.  Maji  lita  moja  na  nusu

MATAYARISHO
i.  Chukua  korodani  za  mbuzi kisha  tia  kwenye  sufuria
ii. Ongeza  maji  lita  moja  na  nusu
iii.Ongeza  pink salt  kijiko  kidogo kimoja
iv.Ongeza  vijiko  vitatu  vidogo vya  dawa  ya  jiko  iliyo katika  mfumo  wa  unga  au  kipande  kimoja cha mzizi  wa  jiko.
v.Chemsha  mchanganyiko  wako  hadi  utokote.
vi.Ipua, chuja  makapi  weka  pembeni  ubaki  na  supu  yako.
 
MATUMIZI  
Tumia  kunywa  supu  yako  hii  mara  moja tu.
JAMBO  LA  KUZINGATIA
 Lishe  hii  inaenda  sambamba na  matumizi  ya  dawa  asilia  ya  jiko.  Unashauriwa  kutumia  lishe  hii katika  kipindi  ambacho  unatumia  jiko  pia. Ingawa  lishe  hii  utakuwa ukiitumia  mara  moja kwa  wiki kwa muda  wa  wiki  nne, dawa  ya  jiko  utatakiwa  kuitumia  mara  mbili  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku thelathini.
 
Ama  kwa  upande  wa  DHAKARI  ya mbuzi, jinsi  inavyo  tumika  kama  lishe  maalumu  kwa  wanaume  wenye  tatizo  la  ukosefu  na upungufu  wa  nguvu  za  kiume , matayarisho  yake  yapo  kama  ifuatavyo :

i. Dhakari  za  mbuzi  kuanzia  tatu hadi  tano  ambazo  zimenyonyolewa  tayari( Hizi  unaweza  kuzipata  ukienda  machinjioni )
ii. Pink  salt  nusu kijiko  kidogo
iii.Vijiko  vudogo  viwili  vya  dawa  ya  jiko  iliyo katika  unga.
 
JINSI   YA  KUTAYARISHA
Kausha  dhakari  zako  kwenye mwanga  wa  jua.  Zikisha  kauka, zisage  hadi zisagike  kisha  changanya  na  nusu kijiko  cha  pink salt,  na  vijiko  viwili  vidogo  vya  daw  ya jiko  iliyo  katika  ungaunga  kisha  tumia  kulamba  mchanganyiko  wako . Utakuwa  unafanya  hivyo  mara  mbili  kwa  siku  asubuhi  na  jioni. Utafanya  hivyo  hadi  mchanganyiko  wako  utakapo kamilika.

NYAMA  YA  BEBERU ( NYAMA  YA  MBUZI  DUME )  KAMA  LISHE  MAALUMU KWA  WANAUME  WENYE  TATIZO  LA  UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
 Jinsi  ya  kutumia  nyama  ya  beberu la  mbuzi  kama  lishe  maalumu  kwa  mwanaume  mwenye  tatizo  la  ukosefu na / ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, fuata  maelekezo  yafuatayo :
 
Mahitaji
i. Nyama  ya  beberu  iliyo chomwa, kiasi  cha  nusu  kilo au  kilo moja  kulingana  na  uwezo  wako  wa  kula.
ii.  Nusu  lita  ya  asali ya  tende  au  robo kilo  ya  tende
iii.Pink salt  kijiko  kidogo kimoja
iv. Vijiko  vidogo  vitatu  vya  dawa  ya  jiko.
 
MATAYARISHO
Changanya  kijiko kimoja  kidogo  cha  pink salt kwenye nusu lita  ya asali ya  tende kisha  ongeza  ndani  yake  vijiko vidogo  vitatu  vya  dawa  ya  jiko  halafu koroga  hadi  vichangamane.

MATUMIZI
Chukua  kipande  cha  nyama  yako  ya  mbuzi, chovya  kwenye  mchanganyiko  wako  kisha  kula  hadi  utakapo  maliza  vipande  vyako  vyote  vya  nyama. Utafanya  hivyo mara  moja  tu inatosha  sana.

AU  KAMA  HAUNA  ASALI YA  TENDE
Changanya  pink  salt  na  dawa  ya  jiko, halafu  chukua  kipande  chako cha  nyama, chovya  kwenye  mchanganyiko  wa  jiko  na  pink  salt halafu  kula  pamoja  na punje moja ya tende(Naposema  punje  simaanishi  mbegu, namaanisha ile sehemu ya tende  inayo  faa kuliwa  )
 
Utafanya  hivyo  hadi kiasi chote  cha  tende  kitakapo  isha. Na  utafanya  hivyo  mara  moja tu.

JIANDAE  KUSOMA  MAKALA  NYINGINGE  KUHUSU  AINA  MBALIMBALI  ZA  LISHE  MAALUMU  KWA  WANAUME  WENYE  TATIZO LA  UKOSEFU  NA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

MAKALA  HAYA  YAMEANDALIWA  NA  DUKA  LA  NEEMA HERBALIST LILILOPO  UBUNGO  JIJINI  DAR  ES  SALAAM, JIRANI  NA  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  NYUMA  YA  JENGO  LA  UBUNGO  PLAZA.

WASILIANA   NASI  KWA  SIMU  NAMBA  0766  53 83 84.

NA  KWA  HABARI  NA  MAKALA  MBALIMBALI  KUHUSU  TIBA  ASILIA. TUTEMBELEE  KILA  SIKU  KUPITIA  BLOGU YETU : www.neemaherbalist.blogspot.com

Serikali kuvunja nyumba zilizojengwa bila kibali

0
0
Serikali imewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji kuweka alama za X na kuvunja majengo yote yanayojengwa katika miji yao bila kibali na yale yanayojengwa katika viwanja vya watu wengine walio na hati

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ameyasema hayo alipofanya ziara wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa alpoenda kutatua mgogoro wa ardhi ambapo ameagiza eneo ya lililokuwa shamba la mifugo la Malonje wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa lenye ukubwa wa ekari 12,750, lirejeshwe serikalini kwa vile utaratibu wa kuligawa umekiukwa kwa kiwango kikubwa, na masharti ya uendeshaji hayajazingatiwa kabisa.

Waziri Lukuvi amesema tatizo la ujenzi holela lianaanza pale ambapo Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji wanaacha majengo yanaibuka katika miji yao bila kujua ujenzi huo una kibali au unajengwa katika kiwanja chenye hati na muhusika wa hati hiyo ndio anayejenga.

“Hatuwezi kuendelea na zoezi la kufanya urasimishaji wa makazi kila siku wakati chanzo cha tatizo hilo kinajulikana, kwa hiyo naagiza Wakurugenzi, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji kuweka x katika majengo yote yanayojengwa bila vibali na ujenzi unaofanywa kwenye viwanja vya watu masikini kwa dhuruma” amesema Lukuvi.

Lukuvi amesema atapambana na viongozi hao pale ambapo atakuta majengo yamekithiri katika miji yao na hayana vibali vya ujenzi na baya zaidi majengo hayo yamejengwa katika maeneo ambayo hayaruhusiwi kujenga au yamejengwa katika kiwanja cha mtu mwingine na viongozi hao wameshindwa kufuatilia kwa kuyavunja au kuyaweka alama ya x majengo hayo, kwa kuwa huu ni uzembe unaotokea nchi nzima.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amemhakikishia Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi kuwa atayafanyia kazi mapendekezo yake kikamilifu na kwa haraka ili kuondoa migogoro na kero zinazoukabili mkoa wake katika masuala yote ya ardhi.

Maagizo Aliyopewa Sugu na Tundu Lissu

0
0
Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mh. Joseph Mbilinyi amefunguka na kusema ameagizwa na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kuwaambia wana Mbeya pamoja na Watanzania kiujumla kuwa wajiandae.

Joseph Mbilinyi amesema hayo baada ya kumtembelea Tundu Lissu jijini Nairobi nchini Kenya na kusema kutokana na uimara ambao Tundu Lissu anao amewataka Watanzania kujianda.

"Nimemtembelea 'Big hommie', Nairobi hospital. Ameniambia nikawaambie wana Mbeya kuwa alisikia mwitikio wao wa kishindo nilipomtaja kwenye jukwaa la muziki na kuwa mwili wake 'uliovunjwa vunjwa' kwa risasi unazidi kuimarika na atasimama tena. Ameniagiza niwaambie wana Mbeya na Watanzania wote wajiandae, wajiandae, wajiandae" alisema Sugu.

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini,Mh. Joseph Mbilinyi pamoja na Mbunge wa Iringa Mjini juzi walimtembelea Tundu Lissu jijini Nairobi Kenya anapopatiwa matibabu kufuatia kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma Septemba 7, 2017. 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Octoba 23

Kigwangallah Afuta Vibali Vyote Vitalu vya Uwindaji

0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kigwangalla amefuta vibali vyote vya uwindaji kwa kampuni kuanzia  Oktoba 22,2017 na kutoa siku 60 kwa watendaji ili waratibu mchakato upya utakaowezesha vitalu kugawiwa kwa mnada.

Dk Kigwangalla pia amemwagiza katibu mkuu wa wizara hiyo, ndani ya muda mfupi kuwaandikia Hazina ili kuzichukua hoteli 10 kati ya 17 zilizobinafsishwa ambazo zimeshindwa kutimiza masharti.

Ametoa maagizo hayo jana alipohitimisha mazungumzo na wadau wa sekta ya utalii na maliasili aliokutana nao mjini  Dodoma.

“Kwa mamlaka niliyonayo katika sheria, natamka kwamba, nafuta rasmi vibali vyote vya uwindaji kwa kampuni vilivyotolewa na wizara yangu kwa mwaka huu. Pia, naagiza watendaji wote wanaosimamia hili wahakikishe wanaandaa mchakato ndani ya siku 60 ili mnada ufanyike na uwe wa uwazi,” aliagiza Dk Kigwangalla.

Kuhusu vitalu vyenye migogoro vikiwemo vya Loliondo na Natroni, ameagiza visigawiwe hadi migogoro itakapokwisha.

"Kwenye hili la hoteli, nataka katibu uwasiliane na mamlaka husika, ikiwemo Msajili wa Hazina ili ndani ya siku 60 uje na majibu tutangaze kwa wawekezaji watakaokwenda na masharti," amesema.

RC Makonda alikabidhi Jeshi la Polisi magari 18 ya kisasa yaliyokuwa mabovu

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda jana Oktoba 22 amekabidhi Magari ya kisasa 18 kati ya 26 yaliyopelekwa Mkoani Kilimanjaro yakiwa Mabovu (Mkweche) kwaajili ya kufufuliwa upya.

Magari hayo yalipelekwa Kilimanjaro yakiwa yamebebwa kutokana na ubovu lakini sasa yanarejea Dar es Salaam yakiwa Mazima na Mwonekano kama Magari ya UN ambapo yatakuwa na uwezo wa kubeba Askari 11 wakiwa wamekaa na silaha zao.

Akikabidhi Magari hayo kwa Jeshi la Polisi leo RC Makonda amesema yataenda kuhudumia Wananchi kwa kuimarisha Ulinzi na Usalama jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa kilichomgusa kuboresha Jeshi la Polisi ni Baada ya kuona Askari wakifanya kazi katika mazingira magumu na wakati mwingine kuvamiwa na majambazi kisha kuuawa na kuporwa Silaha.

Aidha RC Makonda ameishukuru kampuni ya Rajinder Motors Ltd (RSA) kwa kumuahidi kutengeneza Magari 56 ya Polisi Dar es Salaam bila kutumia fedha za serikali (Bure).

Makonda ametumia Makabidhiano hayo kutuma salamu kwa Majambazi, Vibaka na wale wenye nia ya kuvuruga Amani na Usalama kuwa kiama chao kimefika.

Amesema alipotangaza mpango wa kufufua Magari yaliyokufa wapo waliombeza lakini sasa wanajionea Magari yakiwa Mapya.

Makabidhiano hayo yameshuhudiwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira, Kamanda wa Polisi kanda Maalumu ya Dar ea Salaam Lazaro Mambosasa na viongozi wengine wa vyombo vya Ulinzi na Usalama ambapo wamempongeza RC Makonda kwa ubunifu mkubwa alionao.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Makamu wa pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd Aishauri Serikali Ifute VAT

0
0
Makamu wa pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi amesema ipo haja kwa Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuangalia uwezekano wa kuondoa kodi ya ongezeko la thamani (Vat) kwa wawekezaji wa makazi nchini ili kuharakisha upatikanaji wa makazi bora kwa wananchi.

Balozi Iddi alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam wakati akizindua mradi wa nyumba za makazi unaofahamika kama Hamidu City Park uliopo wilayani Kigamboni. Mradi huo unatekelezwa na Kampuni ya Orange Tanzania Limited unalenga kujenga nyumba za kisasa zaidi 1,560.

“Makazi bora ni haki ya kila Mtanzania hivyo sisi kama Serikali ni wajibu wetu kila siku kufikiria sera bora zitakazo wawezesha wananchi kufanikisha hilo,’’ alisema.

Alisema kuna haja ya Taifa kuwekeza zaidi kwenye mipango miji inayowaunganisha Watanzania, badala ya ile inayowatenganisha kulingana na vipato.

“Sifa ya miji mizuri ni pamoja mwingiliano wa makazi kati ya watu wenye vipato tofauti, hatuhitaji kuwa na miji inayowatenganisha watu,’’ alisisitiza.

Akizindua nyumba 20 za awali, Balozi Iddi aliipongeza kampuni hiyo kupitia Mkurugenzi wake mkuu, Hamidu Mvungi kwa uzalendo wake wa kuwekeza katika taifa lake huku akiahidi kumuunga mkono kwa kununua nyumba moja.

Akizungumzia mradi huo uliopo kilomita 16 tu kutoka eneo la Feri na kilomita 12 kutoka Daraja la Nyerere, Hamidu alisema unahusisha eneo la zaidi ya eka 130 na utatekelezwa kwa awamu tano tofauti.

“ Awamu ya kwanza itahusisha ujenzi wa nyumba zaidi ya 150 ambazo zitauzwa kati ya mil 120 hadi mil 370 ,’’ alitaja huku akisifia ubora, usalama na baadhi ya huduma za kisasa ikiwemo viwanja vya michezo vitakavyohusishwa katika mradi huo.

Hata hivyo, aliiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kupunguza kama siyo kuondoa kabisa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) ambayo imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la bei kwenye nyumba za makazi.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Hashim Mgandilwa.

TanzaniteOne : Tupo Tayari Kuipitia Mikataba Upya

0
0
Uongozi  wa Kampuni ya uchimbaji madini aina ya tanzanite ya TanzaniteOne Mining Limited, umejitokeza na kutangaza wazi kuwa wako tayari kushirikiana na serikali katika kupitia upya makubaliano ya mkataba wa uchimbaji na kuhakikisha kuwa taifa linanufaika na vito hivyo.

“Wakati tunasubiri taratibu za serikali kukamilika kabla ya kuanza majadiliano, tunapenda kumhakikishia Mheshimiwa Rais John Magufuli na Watanzania kwa ujumla kwamba sisi kama TanzaniteOne tutatoa ushirikiano utakaowezesha kuwa na hitimisho lenye tija kwa taifa letu,” ilisema taarifa kutoka kwenye uongozi wa kampuni hiyo.

Taarifa hiyo rasmi kutoka Bodi ya Uongozi wa TanzaniteOne Limited iliyosainiwa na Katibu wa Kampuni, Kisaka Mnzava, inasema kuwa viongozi wake wako tayari kufuata maelekezo yoyote yatakayotolewa na serikali baada ya mazungumzo yanayotarajiwa kufanyika baina ya kampuni hiyo na serikali.

“TanzaniteOne iko tayari kuingia kwenye majadiliano na serikali kwa ajili ya kufanya mapitio ya mkataba husika pamoja na kurekebisha taratibu zote za uchimbaji na biashara ya madini nchini kwa manufaa ya Watanzania wote,” alifafanua Mnzava.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo rasmi, TanzaniteOne itashirikiana bega kwa bega na timu ya serikali itakayoundwa kwa ajili ya kutekeleza wajibu huo, lengo likiwa ni kuwezesha madini ya tanzanite yanayopatikana Tanzania peke yake, kuwa yenye manufaa kwa taifa.

“Tunafanya hivyo kwa sababu mbili: Kwanza ni kutambua juhudi zinazofanywa na Rais John Magufuli na hatua anazochukua kulinda rasilimali za taifa na kuhakikisha kuwa madini yanawanufaisha Watanzania wote kwa ujumla.”

“Pili tunaamini kuwa wabia wa kampuni ya TanzaniteOne, mbao ni Watanzania wazawa wana wajibu wa kushiriki katika mchakato mzima wa kuliwezesha taifa kunufaika na rasilimali za madini nchini,” waliongeza viongozi wa TanzaniteOne katika taarifa yao kutoka Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara.

TanzaniteOne Mining Limited ni kampuni ya ubia baina ya wafanyabiashara wa jijini Arusha, Hussein Gonga na Faisal Shahbhat kupitia Sky Associate wanaomiliki asilimia 50 za hisa na serikali kupitia Shirika la Madini la Taifa (Stamico) lenye hisa 50 pia.

Wakati wa ziara yake ya uzinduzi wa Barabara ya KIA-Mirerani, Septemba 27, mwaka huu, Rais Magufuli aliagiza kupitiwa upya mkataba wa uchimbaji na biashara ya madini hayo ya vito baina ya Sky Associate na Stamico.

Oktoba 19, mwaka huu, baada ya kushuhudia kutiwa saini makubaliano baada ya mazungumzo baina ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya uchimbaji dhahabu ya Barrick Gold Corporation, Rais Magufuli alimuagiza Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi kwamba timu ya serikali ianze kufanyia kazi madini ya tanzanite na almasi.

Gazeti La Tanzania Daima Laomba Radhi

0
0
Gazeti la Tanzania Daima limeandikia barua ya kuomba radhi kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Dkt. Hassan Abbas baada ya gazeti hilo kutoa taarifa yenye kichwa cha habari ‘Asilimia 67 ya Watanzania wanatumia Dawa za kufubaza Virusi vya Ukimwi’.

ACACIA Watemwa.....Barrick Kuunda Kampuni Mpya ya Kusimamia Shughuli za Uchimbaji Madini Tanzania

0
0
Barrick Gold Corporation yenye makao yake jijini Toronto, Canada, litaunda kampuni mpya (sio Acacia) kuendesha migodi yake ya Bulyanhuru, Buzwagi na North Mara nchini Tanzania.

Katika taarifa yake juu ya makubaliano na serikali ya Tanzania yaliyofikiwa juzi jijini Dar es salaam, Shirika hilo limesema msimamo wa uwazi ulioafikiwa baina ya washirika (Tanzania na Barrick) ndio utaoainisha namna kampuni hiyo mpya itafanya shughuli zake.

"Kwa mfano Serikali ya Tanzania itashiriki katika maamuzi yahusuyo shughuli, uwekezaji, mipango, manunuzi na masoko (ya kampuni hiyo mpya itapoanzishwa)", sehemu ya taarifa hiyo iliyosainiwa na Makamu wa Rais Mwandamizi  wa Barrick Gold anayeshughulikia Shughuli za Uwekezaji na utawala Bw. Daniel Oh na Makamu wa Rais Mwandamizi wa Barrick anayeshughulikia Mawasiliano Bw. Andy Lloyd.

Taarifa imesema kampuni hiyo mpya itaajili Watanzania, itawajengea uwezo wazawa  katika ngazi zote, kuanzia uanachama wa bodi hadi shughuli zote, na kwamba itaongeza ununuzi wa bidhaa na huduma ndani ya Tanzania katika kuhakikisha faida  ya dhahabu inaifaidisha nchi.

Taarifa hiyo imethibitisha kwamba faida ya kiuchumi kutoka katika migodi hiyo mitatu itagawanwa nusu-kwa-nusu ama 50-kwa-50 baina ya kampuni hiyo mpya na serikali ya Tanzania,  faida yake  ya kiuchumi ikitokana na mirahaba na kodi huku asilimia 16 ikibakia pale pale.


Makubaliano Barrick: Rais Magufuli awa gumzo duniani......Mining Quartz Wasema Ana msimamo usioyumba, New York Times wasema ni mageuzi tupu

0
0
SIKU chache tu baada ya Rais John Pombe Magufuli kufanikisha kukamilika kwa ufanisi sehemu ya kwanza majadiliano na kampuni ya Barrick Gold kuhusu biashara ya madini hayo nchini, majarida na magazeti mbalimbali maarufu duniani yamemzungia kwa staili tofauti.

Katika makubaliano hayo, huku Mwenyekiti wa Barrick Gold, Prof. John Thornton, akilazimika kusafiri kwa ndege binafsi kuja mara 2 nchini Tanzania, Tanzania imefikia kile ambacho nchi chache sana duniani zimeweza kufanikisha katika kunufaika na sekta ya madini.

Pamoja na kupewa hisa zinazofikia asilimia 16 katika migodi yote ya Barrick nchini, makubaliano hayo pia yanaruhusu Tanzania kuchukua madini yote yanayopatikana baada ya makinikia kuuzwa na itapata faida ya nusu kwa nusu na Barrick baada ya dhahabu ya kawaida kuuzwa.

Aidha, kampuni ya Barrick itaweka ofisi zake mpya katika jiji la Mwanza Tanzania na kwamba idadi ya watanzania wanaoshiriki katika Bodi na menejimenti ya Shirika hilo itaongezeka ili kulinda maslahi ya pande zote mbili.

Ndio maana katika makala yake iliyoitwa “Tanzania’s squeeze on mining firms seems to be working as it gets $300 million in back taxes” Jarida mashuhuri la masuala ya madini Quartz lilimueleza Rais Magufuli kama kiongozi aliyefanikiwa kuyabana makampuni makubwa kwa maslahi ya wananchi wake na hayumbishwi.

“Rais wa Tanzania mwenye msimamo usioyumba katika madini, Dkt. John Pombe Magufuli anaongoza vita inayohakikisha kuwa makampuni makubwa yanapata haki yao lakini wananchi wa Tanzania nao wanapata faida katika sekta ya madini,” anaandika Abdi Latif Dadir mwandishi wa jarida hilo lenye makao yake makuu Marekani.

Kwa upande wake mtandao wa habari za uchumi na biashara wa Bloomberg ulisema kuwa Rais Magufuli ni kiongozi ambaye “anaifanyia mageuzi makubwa sekta ya madini ili kuwafaidisha wananchi.”

Mtandao huo pia umeongeza kuwa licha ya azma hiyo, Serikali ya Magufuli pia ina mikakati mipana zaidi katika “kutekeleza sera ya viwanda na miradi ya kiuchumi katika nchi ya Tanzania ambayo ni ya sita kuwa na uchumi mkubwa katika Ukanda wa Afrika Kusini mwa Sahara.”

Gazeti mashuhuri la New York Times lilianza kwa kusema Serikali nyingi katika nchi za Afrika na Asia-kutoka Afrika Kusini hadi Indonesia zimeanzisha harakati za kuhakikisha zinafaidika zaidi na madai yao.

Gazeti hilo limeeleza hatua mbalimbali alizozichua Rais Magufuli ikiwemo kuzuia usafirishaji wa mchango wa madini maarufu kama makinikia. “Rais wa Tanzania hata hivyo hakusema iwapo uuzaji nje wa madini hayo utaruhusiwa tena ama la,” limeripoti New York Times.

Rais Magufuli leo anatarajia kuwatunuku vyeti wote waliofanikisha kufikiwa makubaliano kati ya serikali na Kampuni ya Madini ya Barrick

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 23 Oktoba, 2017 atawatunuku vyeti wajumbe wa kamati zilizofanya uchunguzi wa kiwango, aina na thamani ya madini katika makinikia na baadaye kufanya mazungumzo na kampuni ya Barrick Gold.

Tanzania na Barrick Gold Corporation zilifikia makubaliano tarehe 19 Oktoba, 2017 na kutiliana saini mkataba wa kutekeleza mwelekeo mpya wa namna kampuni hiyo itakavyoendesha biashara ya madini ya dhahabu yanayochimbwa katika migodi yake hapa nchini, pamoja na kulipa Dola za Marekani Milioni 300 za kuonesha nia njema ya kufidia madai ya upotevu wa mapato yaliyotokana na biashara hiyo.

Tukio hili litafanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam kuanzia saa 5:00 asubuhi na kurushwa moja kwa moja na vyombo vya habari vya redio, televisheni na mitandao mbalimbali.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

23 Oktoba, 2017

Kigwangallah: Sihongeki na Wala Sipo Tayari Kuuza Utu Wangu Kisa Umasikini na Tamaa

0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kigwangalla amesema ataendelea kuwepo ndani ya wizara hiyo kama kilichowafanya watangulizi wake kuondoka ni masilahi binafsi, kwa kuwa hahongeki, hashawishiki na aliyemteua analifahamu hilo.

 “Sitakuwa tayari kupoteza heshima yangu, aliyeniteua anajua kuwa mimi ni muarobaini wa hayo yote, hata nilipoteuliwa walianza kunidhihaki kupitia mitandao ya kijamii kuwa ninakwenda kuharibikiwa huko, eti kwa sababu mawaziri hawadumu, haipo hiyo,” alisema Dk Kigwangalla jana Jumapili Oktoba 22,2017 mjini Dodoma.

Alisema hayo akijibu kauli ya Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro aliyemtahadharisha kuwa mawaziri wamekuwa hawadumu ndani ya wizara hiyo kutokana na kununulika na wadau kwa kuwa kuna ushawishi mwingi.

Hayo yameibuka kwenye mkutano wa wadau wa sekta mbalimbali zinazofanya kazi na Wizara ya Maliasili na Utalii ambao Dk Kigwangalla alikutana nao akiwa na Naibu Waziri wake, Japhet Hasunga.

Katika mchango wake, Meya Lazaro alisema, “Niliwahi kumtahadharisha waziri mwenzako Hamisi Kagasheki kuwa hatadumu katika wizara hiyo kutokana na wadau kuwa na vishawishi vingi, leo hii naomba kukuambia kuwa sheria hizo mnazosema kuwa ni mbovu si kweli bali zinakosa usimamizi wa kutosha kwa sababu ya masilahi ya watu.”

Meya Lazaro alimtaka waziri kukutana na kila sekta ili kusikiliza kilio chao akisema ndani ya wizara hiyo kama atapatikana mtu wa kuisimamia vizuri inaweza kutoa mchango mkubwa ambao haujapata kutokea lakini akaahidi kuwa watamsaidia ili adumu kuliko mawaziri wengine.

Alisema “Napenda uendelee kubaki katika wizara hii, wewe ni kijana mdogo nisingependa uwe geti la kutokea.”

Mawaziri waliowahi kuiongoza wizara hiyo ni Anthony Diallo (2005-2006), Profesa Jumanne Maghembe (2007-2008; 2016-2017), Shamsa Mwangunga (2008-2010), Ezekiel Maige (2010-2012), Balozi Hamis Kagasheki (2012-2013) na Lazaro Nyalandu (2014-2015).

Meya Lazaro alisema baadhi ya mawaziri wamekuwa wakiitwa na makundi mbalimbali akitoa mfano wa wawindaji na kuzungumza nao lakini hushawishika kuegemea huko na wakiitwa na watu wengine huegemea huko, hivyo kushindwa kubaki katikati ya sekta zote.

Akijibu hoja hiyo, Dk Kigwangalla alisema hana shaka ya aina yoyote kuhusu kupewa wizara hiyo.

Dk Kigwangalla aliwatahadharisha wadau akisema wanapofika ofisini kwake wajiandae vyema, vinginevyo anaweza kusimama na kumuacha mtu kama atagusa suala la rushwa.

“Mimi sihongeki, kwa hivyo siko tayari kung’oka kwa sababu yoyote ile, kama ni umasikini ni bora kufa njaa, kwangu fedha haiwezi kunitolea heshima licha ya kuwa wote tunazitaka,’’ alisema.

Waziri huyo amejisifu kuwa hata aliyemteua anajua yeye ni muarobaini, hivyo imani yake ni kubwa kwake na kwa upande wake hatakuwa tayari kuona akiharibikiwa njiani.

Tatizo la Nguvu za Kiume na Chanzo cha Kuwa na Maumbile Madogo

0
0
Wataalam katika chuo kikuu cha tiba johns hopkins wanakili kuwa asilimia 75% ya wanaume duniani wamepatwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Tatizo hili linasababishwa na kushuka kwa TESTOSTERON kwenye damu ,kawaida testosteron kwenye damu inatakiwa iwe 400ng/d/hadi 900ng/d/.....chini ya 400ng/d/ mwanaume anapatwa na upungufu wa nguvu za kiume (erectile disfunctioning) kupungua maumbile ya kiume kwa kawaida anatakiwa kutumia dk 20_30 ndipo amalize na umbile lake liwe si chini ya nchi 7.5 .

Sababu zinazoweza kushusha testosterone homoni ya nguvu za kiume ni PUNYETO,SUKARI,BP,MAGONJWA YA FIGO,TUMBO LA CHANGO,ULEVI KUPITA KIASI,MAGONJWA YA ZINAA,U.T.I,KUTOKWA NYAMA SEHEMU ZA HAJA KUBWA,(BAWASIRI).

Wanawake pia wamekumbwa na upungufu wa hamu ya tendo la ndoa kutokana na kushuka kwa homoni estrogen, ambapo mwanamke hupatwa na kuumwa tumbo la chini ya kitovu ,maumivu anapoingiliwa,ukavu mwingi,hata kama ameandaliwa,kuyumba kwa hedhi.

Mtaalam mwingine ambaye ni mkurugenzi wa mradi wa EEP PROF RICHARD SHARP,Anabainisha vyanzo vingine vinavyoondoa mvuto wa mapenzi kuwa aina ya pepo INCUBUS wa kiume hummiliki mwanamke hadi kushindwa kutamani mapenzi na binadamu wa kawaida,mwanamke huota ndoto akifanya mapenzi na watu au wanyama,na mwanaume pia kukosa kuwatamani wanawake naye hujiwa na ndoto akifanya mapenzi nahuamka amelowa.

DR JIDONGEJA  MTAALAM WA TIBA ASILI ANAKUBALIANA NA TAFITI HIZI NA ANAKIRI KUWA WATU WENGI WENYE MATTIZO HAYA ANAWATIBU.

 PIA HUTOA TIBA ZA KISAIKOLOJIA ZA KUKUZA MVUTO KWA MTU KUPENDWA.ANAPATIKANA DAR ES SALAAM NA HUDUMA UNALETEWA POPOTE. SIMU NO 0758078280.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Kwa Nini Wanaume Wengi Wana Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

0
0
Asilimia 85 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vema wake au wapenzi wao na kuwasababishia waweze kuwasaliti na kutoka nnje ya ndoa 

NI NINI CHAZO CHAKE ; upiga punyeto, ngiri, vidonda vya tumbo, magonjwa ya moyo, presha, kisukari, korodani moja kuvimba, utumiaji hovyo madawa ya kizungu, msongo wa mawazo, kufanyiwa tohara ukubwani nk 

DOKTA HAMISI SASA KAPATA TIBA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO :

MAPRO POWER  ndio dawa tosha kwa sasa. Hutibu na kuponesha kabisa tatizo la NGUVU za kiume, utarudisha heshima ya ndoa yako 

1 itakufanya uchelewe kufika kileleni 
2 itakupa hamu ya kurudia tendo 
3 Huhimalisha moduli iliyoregea na kusinyaa

 OKOA NDOA YAKO SASA : MANGUNGU MIX ni tiba kwa wanaume wenye uume mfupi kwa msemo wa Dada zetu wanaita vibamia. Dawa hiyo huboresha uume saizi upendayo ich 1-8 na unene cm 1-5.

Dawa zipo za kupaka na kunywa na ni tofauti na ulizowai kutumia na hazina madhara.

Pia tunato Pete, mkufu au saa kwa mfanya biashara,mkulima mchimba madini 

Pete ya mapenzi nayo IPO NATOA GARANTII YA MIEZI SITA kama umepata tiba na ukafanikiwa na tatizo kujirudi utakuja kupewa bure tiba yako OFISI IPO MBAGALA ZAKHEMU UKISHUKA TU SITENDI . Pia utaipata popote huduma kama hauna nafasi ya kuja ofisini 

Mawasiliano; 0686980006

Daktari aeleza Kanumba alikuwa na uvimbe sehemu ya nyuma kwenye ubongo

0
0
Daktari bingwa wa uchunguzi wa magonjwa ya binadamu na vifo vyenye kutia shaka, Innocent Mosha kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili ameieleza Mahakama Kuu alichobaini baada ya kuufanyia uchunguzi mwili wa msanii wa fani ya uigizaji wa filamu nchini, Steven Kanumba.

Dk Mosha ambaye ni shahidi wa nne wa upande wa mashtaka katika kesi ya kuua bila ya kukusudia inayomkabili msanii wa fani hiyo, Elizabeth Michael maarufu Lulu amesema walipofungua fuvu walibaini ubongo wa Kanumba ulikuwa umevimba.

Lulu anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 7, 2012, nyumbani kwa marehemu Kanumba, Sinza Vatican jijini Dar es Salaam.

Katika ushahidi wake leo Jumatatu Oktoba 23,2017, Dk Mosha akiongozwa na Wakili wa Serikali, Faraja George mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu, Samu Rumanyika ameeleza akiwa kazini alipewa maagizo kuwa anatakiwa kuufanyia uchunguzi mwili uliokuwa umehifadhiwa katika Hospitali ya Muhimbili.

Shahidi huyo amesema katika uchunguzi wa mwili wa Kanumba alibaini kuwepo uvimbe sehemu ya nyuma kwenye ubongo na walipofungua fuvu walibaini ubongo ulikuwa umevimba.

Dk Mosha alipoulizwa na wakili wa mshtakiwa Peter Kibatala juu ya sampuli walizopeleka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kuhusu hali ya kilevi katika mwili wa Kanumba, amesema hakuwahi kufahamu matokeo ya uchunguzi.

Pia, amesema hafahamu kama Kanumba alijigonga ukutani kwa kuwa hakuwepo eneo la tukio.

Wizara ya Ardhi yatoa Ufafanuzi Kuhusu Kubomoa Nyumba Zote Zilizojengwa Bila Kibali

0
0
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetoa ufafanuzi kuhusu uwekaji wa alama za X na kuvunja majengo yanayojengwa katika miji bila kibali na katika viwanja vya watu wengine walio na hati miliki za ardhi kwa dhuluma.

Taarifa ya wizara iliyotolewa leo Jumatatu Oktoba 23,2017 imesema kwa wale waliojenga kwenye viwanja vyenye hati za watu wengine kwa nguvu na kuwadhulumu wenye hati miliki haki yao ya kisheria, hatua zitachukuliwa ili kuwarudishia haki wanaostahili.

“Hatutabomoa nyumba ya mtu bali tutaendelea na urasimishaji wa makazi kwa maeneo yaliyojengwa holela ili yawe makazi rasmi na wananchi wapelekewe huduma muhimu kama vile barabara, umeme na maji,” imesema taarifa hiyo.

Wizara imesema, “Muhimu wapewe hati miliki ili ziwasaidie kiuchumi na waweze kulipa kodi ya ardhi... lakini tutazuia ujenzi mpya holela katika miji yetu kwa mujibu wa sheria.”

Taarifa imesema viongozi wote wa wilaya na mitaa wahamasishe wananchi kushiriki kikamilifu katika urasimishaji wa makazi yao kwa faida yao na Taifa kwa jumla.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images