Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kwa Nini Wanaume Wengi Wana Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Asilimia 85 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vema wake au wapenzi wao na kuwasababishia waweze kuwasaliti na kutoka nnje ya ndoa 

NI NINI CHAZO CHAKE ; upiga punyeto, ngiri, vidonda vya tumbo, magonjwa ya moyo, presha, kisukari, korodani moja kuvimba, utumiaji hovyo madawa ya kizungu, msongo wa mawazo, kufanyiwa tohara ukubwani nk 

DOKTA HAMISI SASA KAPATA TIBA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO :

MAPRO POWER  ndio dawa tosha kwa sasa. Hutibu na kuponesha kabisa tatizo la NGUVU za kiume, utarudisha heshima ya ndoa yako 

1 itakufanya uchelewe kufika kileleni 
2 itakupa hamu ya kurudia tendo 
3 Huhimalisha moduli iliyoregea na kusinyaa

 OKOA NDOA YAKO SASA : MANGUNGU MIX ni tiba kwa wanaume wenye uume mfupi kwa msemo wa Dada zetu wanaita vibamia. Dawa hiyo huboresha uume saizi upendayo ich 1-8 na unene cm 1-5.

Dawa zipo za kupaka na kunywa na ni tofauti na ulizowai kutumia na hazina madhara.

Pia tunato Pete, mkufu au saa kwa mfanya biashara,mkulima mchimba madini 

Pete ya mapenzi nayo IPO NATOA GARANTII YA MIEZI SITA kama umepata tiba na ukafanikiwa na tatizo kujirudi utakuja kupewa bure tiba yako OFISI IPO MBAGALA ZAKHEMU UKISHUKA TU SITENDI . Pia utaipata popote huduma kama hauna nafasi ya kuja ofisini 

Mawasiliano; 0686980006

TAKUKURU Wampa ONYO Kali Joshua Nassari

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Valentino Mlowola amemtahadharisha Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari kuacha kugeuza taarifa anazoziwasilisha kwenye taasisi hiyo kuwa ni za kisiasa.

Mlowola ametoa tahadhari hiyo kwa Nassari leo Jumanne, Oktoba 17, 2017 alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Amesema endapo Nassari ataendelea kuingiza siasa kwenye suala hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Mlowola amesema kitendo cha mwanasiasa huyo kuweka hadharani taarifa za uchunguzi ni kinyume cha sheria kwa kuwa kazi hiyo inatakiwa kufanyika kwa siri na Mahakama ndiyo yenye jukumu la kuchukua hatua.

Amesema Takukuru ina wajibu wa kumlinda mtoa taarifa lakini jukumu hilo linakuwa tofauti kwa Nassari ambaye ameamua kujitokeza hadharani.

"Alicholeta Nassari kwetu ni taarifa si ushahidi. Ameleta tumezipokea na tunazifanyia kazi, inashangaza anapozungumza na vyombo vya habari na kutuelekeza namna ya kufanya kazi," amesema.

Mlowola amesema, "Tulishampa angalizo kuwa mambo tunayoongea ni siri lakini mwenzetu inaonekana anafanya siasa kama anavyosema mwenyewe kuwa ataendelea kuleta ushahidi kama series ya Isidingo."

Mkurugenzi mkuu huyo amemtaka Nassari kuacha kukiingiza chombo hicho kwenye siasa ili kifanye kazi kwa uhuru kama sheria inavyoelekeza.

"Nitoe rai kwa Nassari na wengine wote, ukishaleta taarifa kwenye chombo husika kama hiki kiache kifanye kazi. Hakuna sababu ya kukishinikiza au kukiingiza kwenye malumbano ya kisiasa. Ukweli wa mambo utajulikana mahakamani," amesema.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Lissu atoka ICU aona jua kwa mara ya kwanza tangu apigwe risasi .......Mbowe Asema Atasafirishwa Nje ya Nchi

$
0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema kuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ametoka ICU na sasa anaweza kukaa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne, Mbowe amesema afya ya Lissu inaimarika kwa kuwa alihitaji upasuaji mwingi sana kutokana na risasi zilizoingia kwenye mwili wake.

“Amefanyiwa upasuaji mkubwa mara 17 mpaka sasa. Ameongezewa damu nyingi kuliko mtu yeyote miaka 20 iliyopita ametoka ICU wiki iliyopita,” amesema Mbowe.

Amesema Lissu hatumii oxygen tena wala mirija na kwamba anakula chakula anachokitaka.

“Juzi kwa mara ya kwanza alikaa, anatembea Wheel Chair na aliliona jua kwa mara ya kwanza,” amesema Mbowe.

“Tunawashukuru madaktari wa Dodoma na Nairobi. Hospitali ya Nairobi imefikisha awamu ya pili ya kutibu. Tunavyozungumza baada ya wiki moja kadri madaktari watakavyoshauri atamaliza matibabu ya pili,”

“Ataanza awamu ya tatu nje ya Nairobi yatakayokuwa ya muda mrefu. Kwa usalama wake hatutataja wapi anakwenda. Siyo Tanzania na sio jirani. Hiyo ndio hali halisi ya mgonjwa.”

Milioni 412 zatumika kumtibu Tundu Lissu

$
0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema gharama za matibabu ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyelazwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya zimefikia Sh412.7 milioni.

Lissu ambaye ni mwanasheria wa chama hicho, amelazwa hospitalini hapo tangu Septemba 7 aliposhambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi akiwa maeneo ya nyumbani kwake Area D mjini Dodoma.

Mbowe akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne, Oktoba 17, 2017 jijini Dar es Salaam, Tanzania amesema gharama ni kubwa, ila anawaomba Watanzania wasichoke kuchangia kwa kuwa Lissu atarudi barabarani.

“Tunaishukuru sana familia ya Lissu, imekuwa na msimamo kama Lissu mwenyewe. Tumefanya kazi na familia na tutaendelea kufanya kazi na familia. Tutakapokwenda katika matibabu ya tatu, tutaiacha kwa familia iwe msemaji wa kwanza, mgonjwa anaweza kuongea na kujitambua,” amesema.

Kuhusu mchanganuo wa michango, Mbowe amesema wabunge wa Chadema wamechanga Sh48.4 milioni.

Amesema wananchi wamechangia Sh24.2 milioni kupitia simu ya Mbunge wa Tarime Mjini (Chadema), Esther Matiko.

“Watu mbalimbali wakiwemo wanachama wa Chadema wamechanga Sh90 milioni kupitia akaunti iliyofunguliwa katika Benki ya CRDB,” amesema.

Mbowe amesema wabunge wote wakiwemo wa Chadema wamechanga Sh43 milioni na kwamba, Watanzania walio nje ya nchi wamechanga kupitia Go fund me Dola 29,000 za Marekani.

Kiongozi huyo wa Chadema amemshukuru Mange Kimambi kwa kufanya kazi kubwa ya kuhamasisha michango.

Mbowe amesema wafanyabiashara wakihamasishwa na Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema wamechanga Dola 18,000.

Amesema wana orodha nzima ya wote waliochangia na amewaomba Watanzania waendelee kuwapigania.

Nassari Awajibu TAKUKURU......"Sitakaa Kimya"

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari amesema kuwa hatokaa kimya endapo haoni hatua zinazochukuliwa.

Nassari amesema hayo leo Jumanne muda mchache baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Valentino Mlowola kumtaadharisha Nassari kuacha kugeuza taarifa anazoziwasilisha kwenye taasisi hiyo kuwa ni za kisiasa.

Hata hivyo Nassari amesema, “Mlowola inabidi asome sheria ya ‘Whistle blower’ ili nikae kimya lazima nione jitihada zinazofanyika kama hakuna nitaendelea kuongea. Sitokubali kutishwa ili nisiendelee kupeleka ushahidi ninachotaka kuona ni wahusika wanachukuliwa hatua sio madiwani, wahusika wakuu ni mkuu wa wilaya na mkurugenzi,”

Awali akizungumza leo Jumanne asubuhi, Mlowola ametoa tahadhari hiyo kwa Nassari leo Jumanne, Oktoba 17, 2017 alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Amesema endapo Nassari ataendelea kuingiza siasa kwenye suala hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Mlowola amesema kitendo cha mwanasiasa huyo kuweka hadharani taarifa za uchunguzi ni kinyume cha sheria kwa kuwa kazi hiyo inatakiwa kufanyika kwa siri na Mahakama ndiyo yenye jukumu la kuchukua hatua.

Amesema Takukuru ina wajibu wa kumlinda mtoa taarifa lakini jukumu hilo linakuwa tofauti kwa Nassari ambaye ameamua kujitokeza hadharani.

"Alicholeta Nassari kwetu ni taarifa si ushahidi. Ameleta tumezipokea na tunazifanyia kazi, inashangaza anapozungumza na vyombo vya habari na kutuelekeza namna ya kufanya kazi," amesema.

Mlowola amesema, "Tulishampa angalizo kuwa mambo tunayoongea ni siri lakini mwenzetu inaonekana anafanya siasa kama anavyosema mwenyewe kuwa ataendelea kuleta ushahidi kama series ya Isidingo."

Mkurugenzi mkuu huyo amemtaka Nassari kuacha kukiingiza chombo hicho kwenye siasa ili kifanye kazi kwa uhuru kama sheria inavyoelekeza.

"Nitoe rai kwa Nassari na wengine wote, ukishaleta taarifa kwenye chombo husika kama hiki kiache kifanye kazi. Hakuna sababu ya kukishinikiza au kukiingiza kwenye malumbano ya kisiasa. Ukweli wa mambo utajulikana mahakamani," amesema.

Mawaziri watakiwa kueleza mafanikio ya wizara zao tangu Rais aingie madarakani

Mahakama Kuu Kenya yaondoa zuio la maandamano

$
0
0
Mahakama Kuu nchini Kenya imeondoa kwa muda zuio la maandamano ya muungano wa vyama vya upinzani nchini humo (NASA) katika miji ya Nairobi, Mombasa na Kisumu lililowekwa na Serikali.

Zuio hilo la kufanya maandamano katika miji hiyo ya kibiashara ilitolewa wiki iliyopita na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Kenya, Fredi Matiangi ili kuweza kuondokana na uharibifu ambao ungeweza kujitokeza, lakini zuio hilo limeondolewa baada ofisa mtendaji mkuu wa Nasa, Norman Magaya kufungua kesi mahakamani.

Aidha, Jaji John Mativo ametoa zuio la kukamatwa kwa Magaya kutokana na maandamano ya Nasa hadi kesi yake itakaposikilizwa na kutolewa hukumu.

Hata hivyo, Katika kesi hiyo, Magaya amemfungulia kesi Inspekta Jenerali wa Polisi, Joseph Boinnet, Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka, Keriako Tobiko na Kaimu  Waziri wa Mambo ya Ndani Fred Matiang’i kwa kuzuia maandamano dhidi ya tume huru ya uchaguzi IEBC.

Whatsapp Yamponza Mbunge

$
0
0
Mbunge mmoja nchini Kenya ametakiwa kuomba radhi mara baada ya kutuma ujumbe wa kimapenzi kwenye group la Whatsapp la wabunge.

Anthony Kiai alituma ujumbe wa kimapenzi kwenye group na kuwaomba wabunge wenzake kutoutilia maanani kwani amekosea lakini wabunge wenzie katika group hilo walimtaka kuomba radhi.

Aidha, Admin wa group hilo, Bernad Chege, alimuomba mbunge huyo kuomba radhi, na badala yake msaidizi wa Mbunge huyo ndio akaomba radhi kwa kitendo hicho cha bosi wake kutuma ujumbe wa mapenzi katika group hilo

Ujumbe huo ulioandikwa kwa lugha ya Gikuyu ambayo inaongelewa na Wakikuyu nchini Kenya, ilikuwa ikitoa maelezo jinsi ya kumridhisha mwanamke chumbani, huku baadhi ya wabunge wengine walionekana kumtetea wakisema ngono sio dhambi.

Hata hivyo, Mbunge Kiai amekuwa mbunge wa jimbo la Mukurweini kufuatia ushindi alioupata kwenye uchaguzi wa Agosti 8, 2017

Akari Aliyekuwa Akifanya Mapenzi na Mfungwa Ajinyonga

$
0
0
Askari mmoja  wa Chuo cha Mafunzo ya Wafungwa cha Losperfontein, nchini Afrika Kusini amejinyonga hadi kufa mara baada ya kuzagaa kwa picha zilizomwonyesha akimpiga busu mfungwa kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii .

Taarifa iliyotolewa na Idara ya Magereza nchini humo imesema kuwa ilifahamishwa kuhusu picha zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na kwamba wakati wanafanya uchunguzi wa tukio hilo, tayari ofisa huyo alikuwa ameshajinyonga.

Aidha, Kamishna wa Magereza wa Limpopo‚ Mandla Mkabela amesema  katika taarifa yao kwamba wameshtushwa sana na wamehuzunishwa mno na tukio hilo la kujinyonga kwa Askari huyo.

“Tumetuma timu ya mameneja waandamizi na wataalamu wa mpango wa ushauri kwa wafanyakazi kwa ajili ya kutoa msaada wowote muhimu,” amesema Mkabela.

Hata hivyo, Mkabela amelaani tukio la usambazaji wa picha zinazodaiwa kuwa ni za ofisa huyo ambazo zimeweza kumsababishia kuchukua maamuzi ya kujinyonga.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls 0658316976
0755911233
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Habari Zilizopo katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Octoba 18

Kamishna wa Tume Huru ya Uchaguzi Kenya Ang'atuka

$
0
0
Kamishna wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) nchini Kenya, Dk Roselyn Akombe ametangaza kujiuzulu nafasi yake katika tume hiyo.

Dk Akombe ametuma taarifa ya kujiuzulu akiwa mjini New York nchini Marekani  anakoishi ambapo alikuwa akiufanyia kazi Umoja wa Mataifa kabla ya kujiunga na tume ya IEBC.

Katika taarifa yake, Akombe amesema kwamba  uchaguzi wa marudio wa uraisi uliopangwa kufanyika Oktoba 26 mwaka huu haujafikia vigezo vya kuwa uchaguzi huru na wa haki.

Akombe anajiondoa kwenye tume hiyo ya IEBC ikiwa imebaki wiki moja uchaguzi wa urais kurudiwa kutokana na matokeo ya awali kufutwa na mahakama kuu na kuamuru uchaguzi mpya ufanyike.

Agosti Akombe alizuiliwa kwenye uwanja wa ndege wa JKIA akielekea nchini Marekani.

Dk Roselyn Akombe Kwamboka alizaliwa 1976 katika kaunti ya Nyamira , na kusomea katika chuo kikuu cha Nairobi kabla ya kuelekea nchini Marekani kwa masomo zaidi.

Ana shahada ya uzamifu katika masuala ya sayansi na kimataifa mbali na shahada nyengine kama hiyo katika somo hilo kutoka chuo kikuu cha Rutgers .

Hadi uteuzi wake katika tume hiyo alifanya kazi kama katibu katika Umoja wa Mataifa mjini New York, wadhfa ambao anasema ulimwezesha kuwa na uzoefu katika maswala

Uwezo wake mkuu amesema mbele ya kamati ya bunge nchini Kenya, ni kutatua migogoro na kwamba ameishi ng'ambo kwa takriban miaka 15, hatua iliomwezesha kuelewa zaidi mahitaji ya watu wanaoishi ughaibuni wakati wa uchaguzi.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) yahadharisha Uwepo wa Mvua Kubwa

$
0
0
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imewataka wachimbaji wa madini katika migodi midogo midogo kuwa makini kwani ongezeko la maji katika udongo linaweza kusababisha mmomonyoko wa ardhi na maporomoko migodini katika kipindi hiki cha mvua za msimu.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk Agnes Kijazi alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utabiri wa mvua za msimu wa Novemba mwaka huu hadi Aprili mwakani.

Pia imezitaka mamlaka za miji pamoja na wananchi, kuchukua tahadhari kwa kuhakikisha mifumo na njia za kupitisha maji zinafanya kazi katika kiwango cha kutosha ili kuepusha maji kutuama na kusababisha mafuriko na uharibifu wa miundombinu pamoja na upotevu wa maisha na mali.

Akizungumzia mwelekeo wa mvua za msimu, Dk Kijazi alisema kutakuwa na mvua za wastani hadi juu ya wastani katika maeneo mengi yanayopata msimu moja wa mvua kwa mwaka, na kwamba mvua kubwa inatarajiwa Januari mwakani.

“Msimu huu ni mahususi katika maeneo ya magharibi mwa nchi, kanda ya kati, nyanda za juu Kusini Magharibi, kusini mwa nchi, maeneo ya kusini mwa mkoa wa Morogoro pamoja na Ukanda wa Pwani ya Kusini.

Mvua inatarajiwa kuanza wiki ya kwanza ya Novemba na kuisha wiki ya nne ya Aprili, 2018,” alieleza Dk Kijazi. Alisema Kanda ya Kati kwenye mikoa ya Singida na Dodoma, mvua zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya kwanza na ya pili ya Desemba mwaka huu, zinatarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya wastani katika maeneo mengi.

Kwa Nyanda za Juu Kusini Magharibi na maeneo ya Kusini mwa nchi, mvua zinatarajiwa kuanza wiki ya nne ya Novemba na wiki ya kwanza ya Desemba. Alisema Pwani ya Kusini kwenye mikoa ya Lindi na Mtwara mvua zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya nne ya Novemba na wiki ya kwanza ya Desemba.

Dk Kijazi aliwataka watumiaji wa taarifa za hali ya hewa ambao ni wakulima, wafugaji, mamlaka za wanyama pori, mamlaka za maji na afya waendelee kutafuta, kupata na kufuata ushauri wa wataalamu katika sekta husika.

Waziri Mkuchika Atoa Maagizo Mazito Kwa Waajiri Serikalini

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofi si ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amewaagiza waajiri wote wa serikali kuhakikisha wanatoa vielelezo vinavyotakiwa vya watumishi wao ndani ya siku 14 pale wanapoagizwa kufanya hivyo na Tume ya Utumishi wa Umma, kinyume cha hapo watawajibishwa.

Mkuchika alitoa agizo hilo jana alipotembelea Tume hiyo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujionea shughuli zinazofanywa. 

Aliwataka waajiri hao kuzingatia sheria kwa kuwa imeelezwa kuwa wamekuwa ndio chanzo cha kuchelewesha kesi za waajiriwa kwa kutokutoa ushirikiano kwa haraka.

“Waajiri zingatieni sheria, pale tume inapotaka kupata vielelezo inataka ijiridhishe. Kesi zinachukua muda mrefu kama hakuna vielelezo lazima zichelewe,” alisema Mkuchika. 

Kwa upande mwingine, aliwataka wafanyakazi wa tume hiyo kutekeleza majukumu yao ya kazi, huku wakijiepusha na rushwa kwa kuwa eneo wanalofanyia kazi lina ushawishi mkubwa.

Pia aliahidi kushughulikia changamoto mbalimbali zinazokabili tume hiyo zikiwemo za rasilimali fedha, watu na usafiri. 

Naye Kaimu Naibu Katibu wa Tume hiyo, Richard Odongo alisema tume hiyo inapokea na kushughulikia rufaa na malalamiko ya watumishi wa umma ambao hawajaridhika na mamlaka zao za nidhamu.

Waziri Mwigulu atembelea ujenzi wa nyumba za Polisi Arusha

$
0
0
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Mwigulu Nchemba leo mchana (Oktoba 17) amekagua eneo la ujenzi wa nyumba za Polisi jijini Arusha zinazoendelea kujengwa baada ya ajali ya moto iliyotokea mwishoni mwa mwezi Septemba ambayo ilisababisha familia za askari 13 kuunguliwa vitu mbalimbali na kukosa makazi.

Mwigulu alitumia fursa hiyo kwa kuishukuru kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa ambayo inaoongozwa na Mkuu wa mkoa Mh. Mrisho Gambo lakini pia aliwashukuru wadau ambao wote kwa pamoja walichukua hatua za haraka za kurejesha makazi ya askari ambao walikumbwa na janga la moto huku akisisitiza kwa kusema kwamba hali ilioonyeshwa na wadau hao ni mfano mzuri wa kuigwa na mikoa mingine waone nchi inajengwa na wananchi.

Alisema kwamba suala la makazi ya askari lipo katika kipaumbele cha serikali na Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameonyesha kwa vitendo katika maeneo tofauti ikiwemo hapa Arusha.

Alisema Serikali ikishamaliza hilo itaendelea na utaratibu mwingine wa kujenga majengo ya kisasa ili askari wapate makazi bora huku akimuagiza Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha awafikishie salamu askari wa Arusha kwamba, Mh. Rais yupo pamoja nao na Wizara ipo pamoja nao.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo mbali na kuendelea kuwashukuru wadau hao kwa kujitolea na kumuunga mkono Mh. Rais ambaye alionyesha njia siku hiyo hiyo usiku kabla hakujapambazuka kwa kutoa mchango wake kama Serikali, lakini pia alisema bado milango ipo wazi kwa watu wengine ambao hawakuwa na taarifa juu ya tukio hilo ili kulisaidia Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha liweze kufanikisha ujenzi wa makazi ya askari hao.

Kamanda Mkumbo aliongeza kwa kusema ujenzi wa makazi bora ya askari mkoani hapa utasaidia kuwaongezea morali zaidi wa kazi askari hao hali ambayo itazidi kuimarisha usalama na shughuli za maendeleo kusonga mbele.

Jumla ya nyumba 29 za askari katika moja ya kambi iliyoathirika na ajali ya moto zilianzwa kujengwa toka tarehe 2 mwezi huu jijini hapa na saba ambazo zipo katika ngazi ya msingi zinatarajiwa kujengwa katika kituo kidogo cha Polisi Morombo kata ya Murieti.

Waziri wa Maliasili Dkt. Kigwangalla atembelea meli ya Mfalme wa Oman, Dar leo

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dkt.Hamisi Kigwangalla amesema  Tanzania na Nchi ya Oman wamefanya mazungumzo ya pamoja ya namna ya kukuza sekta ya Utalii baina ya nchi hizo mbili ambapo watashirikiana katika muingiliano wa Watalii watakaokuwa wakitokea moja kwa moja Oman na kuja Tanzania.

“Tumeweza kuzungumzia ushirikiano wa sekta ya Utalii. Hii ni pamoja na kuanzisha soko la pamoja  kati ya Oman na Tanzania. Watalii wanaokwenda Oman wanaotaka kuja nchi za Afrika basi waunganishwe moja kwa moja kutoka Oman na kuja Tanzania kwani wenzetu wana watalii wengi kuliko sisi. Hivyo ujio wao hapa nchini ni faida kubwa kabisa na tumejifunza mengi katika sekta hii.

"Pia tumeweza kujifunza namna wenzetu wanavyoitangaza nchi yao  na sisi tutatumia uzoefu huo kuboresha sekta hii ya Utalii kama dhamana tuliyopewa” alieleza Dk. Kigwangalla.

Awali Dk. Kigwangalla aliweza kutembelea meli hiyo ya kifahari ya Mfalme wa Oman Mhe. Qaboos bin Said ‘Fulk Al Salamah’ iliyofika mapema jana Jijini Dar e Salaam ikiwa katika msafara wa kitaifa kati ya Serikali ya Oman na Tanzania.

Aidha, katika tukio hilo Mh. Waziri DK. Kigwangalla aliweza kuungana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Mama Samia Suluhu Hassan katika chakula cha mchana ndani ya Meli hiyo ya Mfalme wa Oman Mhe. Qaboos bin Said  ijulinakanyo kama ‘Fulk Al Salamah’.

Meli hiyo ya kifahari ya Mfalme wa Oman Mhe. Qaboos bin Said ‘Fulk Al Salamah’ ipo nchini hadi Oktoba 21.2017. ambapo ipo nchini kusambaza ujumbe wa ‘Amani na upendo’ duniani ambapo  ikitoka Tanzania  inatarajia kuelekea Mombasa Kenya kwa madhumuni hayo hayo.
Moja ya alama za kuvutia za Taifa la Oman
Moja ya usafiri unatumika katika nyanja za Utalii nchini Oman

TAKUKURU Yawahoji Madiwani Waliojiuzulu CHADEMA

$
0
0
Maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kutoka makao makuu jijini Dar es Salaam, wamewahoji kwa zaidi ya saa sita, madiwani waliojiuzulu Chadema wanaotuhumiwa na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari kuwa walipewa rushwa.

Waliofika Takukuru ni Catherine Mtui, aliyekuwa diwani wa viti maalumu, Japhet Jackson (aliyekuwa diwani wa Ambuleni) na Bryson Isangya (aliyekuwa diwani wa Maroroni). Baada ya kuhojiwa hawakutaka kuzungumza chochote wakisema wanaacha uchunguzi uendelee.

Pamoja nao, diwani wa Mbuguni, Ahimidiwe Rico anayedaiwa kuwa ndiye alirekodi sauti na picha wakati akishawishiwa na viongozi wa Serikali na wa Halmashauri ya Meru amehojiwa kwa zaidi ya saa tatu jana Jumanne Oktoba 17, 2017.

Rico amesema amewaeleza Takukuru kila kitu ambacho anakifahamu katika sakata hilo, ikiwemo kuwarekodi viongozi ambao walimshawishi kujiuzuru udiwani.

"Msimamo wangu ni kwamba, nachukia rushwa. Nimewaeleza kila kitu na wao waliniuliza kuhusu vifaa nilivyotumia kuwarekodi nikawaambia ni mali ya mbunge, alivitoa nchini Uingereza," alisema.

Rico aliyesindikizwa na diwani wa  Nkwanankore, Wilson Nanyaro amesema  ana imani na Takukuru kwamba watafanya uchunguzi wa kina na kuchukua hatua.

"Nimewaeleza wazi kuwa hata shauri hili likienda mahakamani nipo tayari kwenda kutoa ushahidi na kuthibitisha sauti za watu ambao niliwarekodi," alisema.

Alisema baada ya mahojiano yaliyoanza saa tatu hadi saa sita mchana, maofisa wa Takukuru walimwambia aondoke na watamuita watakapomuhitaji.

Hakuna ofisa wa Takukuru aliyekuwa tayari kuzungumzia mahojiano hao wakisema wasemaji ni makao makuu ya ofisi hiyo Dar yaliyoko jijini Dar es Salaam.

Orodha ya majina ya wanafunzi watakaopata mikopo ya HESLB Yakamilika

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imesema baada ya uchambuzi wa maombi ya mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2017/2018, orodha ya awamu ya kwanza yenye wanafunzi 10,196 wa mwaka wa kwanza waliopangiwa mikopo imekamilika.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Jumatano Oktoba 18,2017 amesema Sh34.6 bilioni zimetengwa kwa ajili ya wanafunzi hao 10,196.

Amesema kwa jumla Sh108.8 bilioni zitatolewa kwa wanafunzi 30,000 wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2017/2018.

Badru amesema orodha ya awamu ya kwanza inapatikana kwenye tovuti ya Bodi ya Mikopo http://www.heslb.go.tz/ na itatumwa kwa vyuo husika.

Amesema orodha nyingine (batches) zitafuata kwa kadri utaratibu wa udahili na uchambuzi unavyokamilika.

“Lengo ni kutoa majina ya wote waliofanikiwa kupata mkopo kabla ya vyuo kufunguliwa mwishoni mwa mwezi huu wa Oktoba, 2017,” amesema.

Mkurugenzi mtendaji huyo amesema orodha hiyo ya wanafunzi 10,196 imepatikana baada ya kupokea na kuchambua awamu ya kwanza ya majina ya wanafunzi 32,495 waliopata udahili katika chuo kimoja.

“Itakumbukwa kuwa moja ya sifa kuu za kupata mkopo ni mwombaji kupata udahili katika taasisi ya elimu ya juu inayotambuliwa na Serikali,” amesema.

Amesema wanafunzi waliopata udahili katika chuo zaidi ya kimoja na ambao wana sifa za kupata mikopo, watapangiwa mikopo baada ya kuchagua na kuthibitisha chuo watakachojiunga kwa ajili ya masomo.

Wakati huohuo, Badru amesema wanatarajia kuanza kutuma vyuoni fedha za mikopo ya wanafunzi wanaoendelea na masomo ambao wamefaulu mitihani yao kuanzia leo Jumatano, Oktoba 18, 2017.

Amesema Sh318.6 bilioni zitatolewa kwa wanafunzi 93,295 wanaoendelea na masomo kwa mwaka 2017/2018.

“Tayari Serikali imeshatoa fedha hizo na lengo la Bodi ni kuhakikisha zinafika vyuoni kabla ya kufunguliwa kwa vyuo ili kuwaondolea wanafunzi usumbufu,” amesema.

Bodi imewasihi waombaji wa mikopo kuwa na subira wakati ikiendelea kukamilisha maandalizi ya orodha zinazofuata za wanafunzi waliopata mikopo.

Rais Magufuli amtumia ujumbe mfalme wa Oman

$
0
0
Rais John Magufuli leo Oktoba 18, 2017 amemtumia ujumbe Mfalme wa Oman Mtukufu Sayyid Qaboos bin Said Al Said na wawekezaji wengine wa Oman kuwa atafurahi kuona wanakuja kuwezeka nchini tena kwa haraka na kudai serikali itatoa ushirikiano.

Rais ametuma ujumbe huo kwa mfalme wa Oman kupitia kwa Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman Mhe. Dkt. Mohammed Hamad Al Rumhy aliyeongozana na Waziri wa Uwekezaji wa Oman Mhe. Salem Ben Nasser Al Ismaily na Naibu Waziri wa Utalii Mhe. Maitha Saif Majid, ambao walikua Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Mfalme wa Oman Mtukufu Sayyid Qaboos bin Said Al Said amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuwa nchi hiyo ipo tayari kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuongeza uwekezaji katika viwanda, uzalishaji wa nishati, kuongeza thamani ya madini, kuendeleza sekta ya gesi na mafuta na kuendeleza ukanda wa uwekezaji wa Bagamoyo ili kukuza uchumi kwa kasi zaidi.

“Mhe. Dkt. Mohamed naomba ukamwambie Mfalme kuwa namshukuru kwa ujumbe huu na namkaribisha sana Tanzania, nimefurahi kuona mpo tayari kushirikiana nasi kujenga viwanda, kuzalisha mazao na kuendeleza ukanda wa uwekezaji wa Bagamoyo, sisi tupo tayari hata leo, njooni tushirikiane kwa sababu nyinyi ni ndugu zetu na tutafanya uwekezaji kwa faida yetu sote” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ametaka Oman iongeze ushirikiano na Tanzania katika masuala ya utalii na usafiri wa anga, kuwekeza katika usindikaji wa nyama na uvuvi na ushirikiano katika kubadilishana wataalamu wa nyanja mbalimbali wakiwemo walimu wa lugha ya Kiswahili na Kiarabu.

Mbali na hilo Rais Magufuli amemshukuru Mfalme wa Oman kwa msaada kujenga visima vya maji 100 hapa nchini na amemuomba kuungana na Serikali katika safari yake ya kuhamia Dodoma kwa kujenga miundombinu itakayoweka kumbukumbu ya ushirikiano wa kidugu na kihistoria kati ya nchi hizi mbili.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images