Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR;Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

Tatizo la Nguvu za Kiume na Chanzo cha Kuwa na Maumbile Madogo

$
0
0
Wataalam katika chuo kikuu cha tiba johns hopkins wanakili kuwa asilimia 75% ya wanaume duniani wamepatwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Tatizo hili linasababishwa na kushuka kwa TESTOSTERON kwenye damu ,kawaida testosteron kwenye damu inatakiwa iwe 400ng/d/hadi 900ng/d/.....chini ya 400ng/d/ mwanaume anapatwa na upungufu wa nguvu za kiume (erectile disfunctioning) kupungua maumbile ya kiume kwa kawaida anatakiwa kutumia dk 20_30 ndipo amalize na umbile lake liwe si chini ya nchi 7.5 .

Sababu zinazoweza kushusha testosterone homoni ya nguvu za kiume ni PUNYETO,SUKARI,BP,MAGONJWA YA FIGO,TUMBO LA CHANGO,ULEVI KUPITA KIASI,MAGONJWA YA ZINAA,U.T.I,KUTOKWA NYAMA SEHEMU ZA HAJA KUBWA,(BAWASIRI).

Wanawake pia wamekumbwa na upungufu wa hamu ya tendo la ndoa kutokana na kushuka kwa homoni estrogen, ambapo mwanamke hupatwa na kuumwa tumbo la chini ya kitovu ,maumivu anapoingiliwa,ukavu mwingi,hata kama ameandaliwa,kuyumba kwa hedhi.

Mtaalam mwingine ambaye ni mkurugenzi wa mradi wa EEP PROF RICHARD SHARP,Anabainisha vyanzo vingine vinavyoondoa mvuto wa mapenzi kuwa aina ya pepo INCUBUS wa kiume hummiliki mwanamke hadi kushindwa kutamani mapenzi na binadamu wa kawaida,mwanamke huota ndoto akifanya mapenzi na watu au wanyama,na mwanaume pia kukosa kuwatamani wanawake naye hujiwa na ndoto akifanya mapenzi nahuamka amelowa.

DR JIDONGEJA  MTAALAM WA TIBA ASILI ANAKUBALIANA NA TAFITI HIZI NA ANAKIRI KUWA WATU WENGI WENYE MATTIZO HAYA ANAWATIBU.

 PIA HUTOA TIBA ZA KISAIKOLOJIA ZA KUKUZA MVUTO KWA MTU KUPENDWA.ANAPATIKANA DAR ES SALAAM NA HUDUMA UNALETEWA POPOTE. SIMU NO 0758078280.

TIC Yakanusha Taarifa Ya Iliyotolewa Na Gazeti Ya Financial Times Kuwa Sera Za Uwekezaji Tanzania Zinakimbiza Wawekezaji

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania Ndg. Geoffrey Mwambe amesema kwamba taarifa zilizotolewa na Mwandishi wa FT. John Aglionby kuhusu mazingira ya Uwekezaji Tanzania kuwa yanatishia wawekezaji si sahihi na yanalenga kupotosha ukweli kuhusu hali halisi kuhusu Uwekezaji Tanzania.

Mwandishi huyo wa Financial Times ametoa maelezo ambayo amesema yametolewa na Muwekezaji Aliko Dangote maelezo ambayo yamelenga kusukuma Agenda yake ambayo haijulikani na yenye lengo la kupotosha sera za uwekezaji na kuwaogopesha wawekezaji ambao wameendelea kuiamini Tanzania na kuwekeza mitaji yao mikubwa hapa nchini.

Hatuamini kuwa Ndugu Dangote anaweza kuwa msemaji wa kuhusiana na sekta ya madini kwa hapa nchini. Amewekeza kwenye sekta ya viwanda na serikali imekuwa mstari wa mbele kusikiliza na kuyafanyia kazi maoni ya mfanyabiashara huyo ili kuweza kuboresha mazingira yetu ya uwekezaji hapa nchini. Serikali yetu imejidhatiti katika kuboresha mazingira ya uwekezaji na imedhamiria kuhakisha uwekezaji huo unakuwa na faida kwa watanzania nan chi kwa ujumla.

Tunaamini kuwa kuna umuhimu wa kuhakikisha maelezo yanakuwa na pande mbili ili kuondoa utata utaojitokeza wa maelezo ambayo yanaweza kuathiri na kusababisha utata kwa wafanyabiashara walioiamini Tanzania kama sehemu yao ya kufanya uwekezaji. Tanzania inathamini na kujali wawekezaji wa aina ya ya Aliko Dangote na mara nyingi tumekuwa tukiwasikiliza na kufanyia kazi maoni yao ili kurekebisha sera ili ziweze kuwa na manufaa kwa wote yaani waTanzania na wawekezaji. Kuna sera pamoja na sheria ambazo tumezifanyia marekebisho ili ziweze kuwa na manufaa kwa wote.

Hivi karibuni ni vizuri kufahamu kwamba DIL ilikuwa na matatizo mbalimbali na serikali iliweza kukaa na Dangote na kusikiliza matatizo yao na kutatua changamoto kadhaa zilizokuwa zinakwamisha uzalishaji katika kiwanda chake cha Saruji na kufikia muafaka wa kutatua matatizo yote ambayo kiwanda ilikuwa ina TIC pia imeanzisha juhudi maalum za kuhakisha kuwa huduma zinotolewa kwa wawekezaji zinaboreshwa ili kuweza kurahisisha utoaji wa huduma kwa ufanisi na kwa haraka. Kituo kimeweza kuanzisha Kamati Maalum ya Kitaifa ya Kuhudumia wawekezaji yaani NIFC ambapo matokeo makubwa yameweza kuonekana kutokana na uboreshwaji wa huduma zetu chini ya mahali pamoja .

Tunamshukuru sana Mh. Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli kwa juhudi zake za dhati za kupambana na rushwa juhudi ambazo zimeweza kuleta mafanikio n ahata kuifanya Tanzania kutajwa na ripoti mbalimbali za dunia kama mahala bora Zaidi pa kuwekeza Afrika. Zaidi ya ripoti tano zimeweza kuitaja Tanzania kwa mwaka huu pekee kama sehemu bora Zaidi ya mazingira ya uwekezaji Afrika. Tunajivunia juhudi kubwa sana alizozionyesha Rais wetu Mh.John Pombe Magufuli katika kuvutia uwekezaji nchini hasahasa katika kutokomeza rushwa, jambo ambalo mwandishi wa makala hiyo kwa sababu zake binafsi ameshindwa kuziweka bayana.

Ni muhimu sana kuelewa kuwa suala la kuwa na sera nzuri za uwekezaji kwa manufaa ya mwekezaji na nchi limepewa kipaumbele kikubwa na Serikali ya Awamu ya Tano. Tunahitaji sekta binafsi kutekeleza majukumu yake kwa kufuata sheria na taratibu, mfano kulipa kodi stahiki wakati Serikali kwa upande wake ikiendelea kuboresha zaidi mazingira ya biashara na uwekezaji nchini. Katika makala yaliyotolewa na FT imejionyesha waziwazi kuwa mwandishi hafahamu vizuri Sheri ya Uwekezaji ya Mwaka 1997.

Sheria za Tanzania zinatambua umiliki binafsi wa mali na kuzuia uwezekano wa kutaifisha mali hizo bila sababu za msingi za kisheria. Vilevile Tanzania ni mjumbe wa Multilateral Investment Guarantee Agency (MIGA) ambapo makubaliano ya wajumbe ni kutoruhusu utaifishwaji wa mali za uwekezaji pamoja na Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICSID).

Tanzania inaendelea kuhamasisha uwekezaji nchini na Kituo cha Uwekezaji kimekuwa mstari wa mbele katika kushawishi wawekezaji na mashirika makubwa ya kimataifa ambayo tayari yana uwekezaji nchini kuongeza mitaji yao. Tanzania imeendelea kupokea wawekezaji wengi ambapo uwekezaji huo umesaidia katika kukuza uchumi katika Nyanja mabilimbali mfano kuzalisha ajira mpya na kuongeza mapato ya kikodi. Matokeo haya chanya yanatokana na juhudi za Serikali kujenga mazingira mazuri ya biashara na uwekezaji nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa TIC amewashukuru wawekezaji waliowekeza mitaji yao Tanzania kwa ushirikiano wao mzuri na kuwaahidi kuwa Serikali itaendelea na juhudi zake za kuboresha mazingira ya uwekezaji ikiwa ni pamoja na kuboresha mfumo mzima wa kuwahudumia wawekezaji.

Ili kuhakikisha kuwa nchi yetu inaendela kuwa na mazingira mazuri ya uwekezaji, Serikali imeipa kipaumbele utekelezaji wa miradi ya miundombinu wezeshi ili kusaidia katika kupunguza gharama za uwekezaji. Baadhi ya miradi hii ni pamoja na Mradi wa kuzalisha umeme wa Stiegler’s Gorge, ujenzi wa barabara, ukarabati wa miundombinu ya Bandari ya Dar es Salaam (Gati 1-7), ujenzi wa Reli ya Kati kwa iwango cha standard gauge. Jitihada nyingine zilizofanyika hivi karibuni ni uanzishwaji wa Mfuko wa Benki ya Ardhi (Land Bank Fund) na kuboresha mfumo wa asajili wa makampuni BRELA.

Tanzania imeendelea kufanya vizuri kwenye kuvutia uwekezaji ukilinganisha na nchi nyingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki. “Tanzania imo katika orodha ya nchi kumi bora Afrika zinazovutia uwekezaji kulingana na ripoti ya Rand Merchant Bank (RMB). Vilevile Tanzania imeendelea kuwa na kiasi kikubwa cha mitaji ya uwekezaji kutoka nje ya nchi (foreign direct investment) ukilinganisha na nchi nyingine za Jumuiya ya Africa Mashariki” amesema Bw.Mwambe

Mvua Zaleta Maafa Tabora, Watano Wapoteza Maisha

$
0
0
Na Tiganya Vincent, RS-Tabora
WATU watano wakazi wa Wilaya ya Igunga wamefariki duniani katika matukio mawili tofauti kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha mkoani Tabora.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora Wilbroad Mtafungwa amesema hayo leo wakati wa mkutano  na waandishi wa habari. 

Alisema kuwa katika tukio la kwanza mnamo tarehe 11 mwezi huu, watu wanne wamefariki dunia baada ya kuangukiwa na ukuta wa nyumba waliyokuwa wakiishi kufuatia mvua zilizonyesha kwa kipindi cha siku mbili.

Kamanda Mtafungwa alisema waliofariki kwa kuangukiwa na ukuta wanatoka kijiji cha Igogo kata ya Nanga na aliwataja kwa majini kuwa ni Kagwa Makenza(80) ambaye pia ni mmiliki wa nyumba iliyosababisha maafa hayo, wengine ni Sande Dule (6), Butonda Shija(3) na Mbula Dule mwenye miezi miwili.

Alisema watoto wote watatu walifariki dunia wakati wakipata matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Igunga.

Katika tukio la Pili , Kamanda Mtafungwa alisema katika kijiji cha Bulyang’ombe kata ya Nanga mtoto Zenga Tano (5) alifariki dunia baada ya kupigwa na radi mnamo tarehe 10 mwezi huu wakati amelala na wazazi wake.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Igunga John Mwaipopo alitoa pole kwa familia za waliopatwa maafa na kuwashauri wakazi wa Igunga kufuata utalaamu wa ujenzi wakati wa ujenzi wa nyumba zao ili kuepuka maafa zaidi.

Alisema kuwa ushauri huo ni pamoja na ujenzi katika sehemu ya miinuko kwa ajili ya kujikinga na maafa zaidi.

Kilichoendelea Leo Mahakamani Katika Kesi ya Agnes Masogange

$
0
0
Upande wa utetezi wa kesi ya kutumia dawa za kulevya inayombili msanii, Agnes Gerald maarufu kama Masogange utaanza kutoa ushahidi Novemba 14, 2017 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Mshtakiwa huyo alipaswa kuanza kujitetea leo Alhamisi lakini Wakili wa Serikali, Adolf Mkini aliomba kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri ipangiwe tarehe nyingine.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Mashauri aliiahirisha kesi hiyo hadi Novemba 14, 2017.

Hatua hiyo imefikiwa mara baada ya Hakimu Mashauri kumuona mshtakiwa huyo kuwa ana kesi ya kujibu na kwamba anapaswa kujitetea na kuwaita mashahidi wake.

Masogane anatetewa na mawakili Nehemia Nkoko na Ruben Simwanza.

Kesi hiyo inaendeshwa na Wakili wa Serikali, Costantine Kakula ambaye kwa upande wao kuwaita mashahidi watatu wa upande wa mashtaka kutoa ushahidi wao na kuufunga.

Masogange anakabiliwa na mashtaka mawili ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Anadaiwa kufanya makosa hayo chini ya kifungu cha 18 (a) cha Sheria ya Kupambana na Dawa za Kulevya namba 5 ya mwaka 2015.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Kilichoendelea Leo Mahakamani Katika Kesi ya Wizi wa Madini ya Almasi

$
0
0
Upande  wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi, inayomkabili Mkurugenzi wa Tathmini, Archard Alphonce Kalugendo (49) na Mthamini wa Madini ya Almas wa Serikali, Edward Joseph Rweyemamu (50) umeileza mahakama kuwa, sehemu kubwa ya upelelezi umekamilika bado maeneo machache.

Wakili wa Serikali, Wankyo Simon alimeeleza hayo leo mbele ya Hakimu Hakimu Mwandamizi, Godfrey Mwambapa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kesi hiyo ilipofika kwa ajili ya kutajwa.

Wakili Wankyo amedai wanakamilisha upelelezi katika sehemu ndogo iliyobakia na  wamewaelekeza polisi kufanya hill na kwamba tarehe ijayo wataieleza mahakama hatua ya upelelezi ilipofikia

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 26, itakapokuja kwa ajili ya kutajwa

Washtakiwa hao wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa  kusababisha hasara ya dola za Kimarekani 1,118,291.43 sawa na Sh 2,486,397,982.54.

Kalugendo ambaye ni Mkazi wa Kinyerezi na Rweyemamu Mkazi wa Mwananyamala wote ni waajiriwa wa Wizara ya Nishati na  Madini.

Wanadaiwa kati ya Agosti 25 na ,31, mwaka huu, katika maeneo mbalimbali kati ya Dar es Salaam na Shinyanga, washtakiwa kwa pamoja na kwa vitendo vyao wakiwa wathamini walioajiliwa na Wizara ya Nishati na Madini walisababisha hasara ya kiasi hicho cha fedha.

Waziri Mkuu: Tutaendelea Kuimarisha Ushirikiano Wetu Na Uganda

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano wake wa kiuchumi na kidiplomasia baina yake na Uganda.

Amesema Tanzania na Uganda zinauhusiano wa muda mrefu na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli inafarijika na ushirikiano huo.Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Alhamisi, Oktoba 12, 2017) alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Bw. Richard Kaonero jijini Dar es Salaam.

“Tunaimani kubwa na ushirikiano wetu na Serikali ya Uganda. Tutaendelea kuimarisha miradi mbalimbali ya maendeleo tunayoitekeleza kwa pamoja ukiwemo ujenzi wa bomba la gesi.”Hivyo ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji kutoka nchini Uganda ili waje kuwekeza kwenye viwanda mbalimbali vikiwemo vya kuchakata mazao ya kilimo.

Pia amewakaribisha raia wa Uganda kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyoko nchini Tanzania kama mlima wa Kilimanjaro, fukwe, mali kale na mbuga za wanyama.Kwa upande wake, Balozi Kaonero ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuwa na dhamira ya dhati ya kuimarisha uchumi wake kupitia sekta ya viwanda.

Pia Balozi huyo ameiomba Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kuanzisha safari ya kwenda Entebe nchini Uganda ili kuimarisha usafiri kati ya nchi hizo mbili.

Akizungumzia kuhusu ushirikiano baina ya nchi hizo mbili, Balozi Kaonero amesema Serikali ya Uganda na Tanzania zinaundugu wa damu na kwamba wataendelea kuudumisha.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, OKTOBA 12, 2017.

Meli ya Kifahali ya Mfalme wa Oman, Shekh Sultan Qabous Bin Said Yawasili Zanzibar na Ujumbe wa Watu 300

$
0
0
Ujumbe wa watu zaidi ya 300 unaomwakilisha Mfalme wa Oman, Shekh Sultan Qabous Bin Said umewasili visiwani Zanzibar leo Alhamisi asubuhi kwa kutumia meli yenye jina la Fulk Al Salamah ambayo hutumiwa na mfalme huyo.

Ujumbe huo wa Serikali ya Oman umewasili katika Bandari Kuu ya Malindi mjini hapa majira ya saa tatu na nusu za asubuhi ikitokea nchini Oman.

Katika mapokezi ya ujumbe huo viongozi wa Serikali ya Zanzibar walihudhuria akiwamo Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo, Rashid Ali Juma, Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud Mohamed, Waziri wa Maji, Nishati, Ardhi na Mazingira, Salama Aboud Talib na Wazir wa Biashara na Masoko, Amina Salum Ali.

Kwa upande wa ujumbe huo wa mfalme uliongozwa na Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman, Mohamed Al-ramh ambapo lengo kuu la kufika Zanzibar ni kusambaza amani na upendo ikiwa ni hatua ya kufikisha ulimwenguni kote.

Akizungumza katika mapokezi hayo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud Mohamed amesema ni faraja kubwa kwa Zanzibar kupata ugeni huo wa heshima.

Amesema ugeni huo ni ishara njema ya kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano baina ya nchi hizo mbili ambazo zinaonekana kuwa na udugu wa kihistoria kwa miaka mingi.

‘’Ishara hii ni njema na tunaifurahia kwa moyo wote na kesho tutakuwa na mazungumzo rasmi na ugeni huo ambapo tunataraji mambo mbalimbali tutayajadili na baadaye kutoa taarifa rasmi ya mazungumzo yetu,” amesema  Aboud.

Hata hivyo amesema ujumbe huo pia utapa nafasi ya kutembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria, ofisi za Serikali lengo ni kubadilishana mawazo juu ya ukuaji wa uchumi.

Waziri Aboud amewataka wananchi wa Zanzibar kuwapokea wageni hao katika maeneo tofauti ili kuonyesha ukarimu wao.

Rais Magufuli awasili Zanzibar kuadhimisha kumbukumbu ya Mwl. Nyerere na kushiriki kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru.

$
0
0
Rais Magufuli leo Oktoba 12, 2017 amekwea pipa na kwenda visiwani Zanzibar akiwa na mkewe Mama kwa ziara ya kikazi ya siku tatu ambapo Rais Magufuli anategemewa kuwa Mgeni Rasmi siku ya kilele cha Mwenge wa Uhuru Oktoba 14, 2017 Uwanja wa Amaan.

Rais Magufuli visiwani Zanzibar amepokelewa na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi mara baada ya kuwasili katika uwanja  wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Grayson Msigwa amesema kuwa Rais Magufuli atakuwepo visiwani Zanzibar kwa siku tatu na kudai pamoja na mambo mengine Rais Magufuli atakuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru na siku ya Mwalimu Nyerere. 

Polisi Waua Watuhumiwa Waliomjeruhi Meja Jenerali Mstaafu

$
0
0
KUUWAWA KWA MAJAMBAZI WAWILI NA KUPATIKANA KWA SILAHA AINA YA SMG RISASI KUMI NA TISA NA MAGANDA MAWILI

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dsm mnamo tarehe 11.10.2017 majira ya saa nne kamili usiku huko maeneo ya Mbezi Mshikamano kwa Mgalula, askari walipata taarifa kutoka kwa FRANCIS MINDE miaka 30, mfanyabiashara ambaye anamiliki duka la vitu mchanganyiko kwamba walifika watu wawili katika duka lake wakitumia pikipiki aina ya Boxer nyeusi ambayo haikusomeka namba na kumuuliza kama kuna huduma ya M-PESA na TIGO-PESA na kuwajibu kuwa hakuna huduma hiyo, aliwatilia mashaka huenda sio watu wazuri hatimaye alitoa taarifa Polisi.

Mara baada ya kupata taarifa hizo askari walikwenda eneo hilo na kuiona pikipiki ikiwa imeegeshwa gizani ikiwa na watu watatu, askari waliwaita watu hao ili kuwahoji lakini watu hao walianza kukimbia huku wakifyatua risasi upande waliopo askari, kuona hivyo askari nao walijibu mashambulizi na kufanikiwa kuwajeruhi majambazi wawili, mmoja kati yao alifanikiwa kukimbia na pikipiki waliyokuwa nayo

Aidha eneo la tukio ilikutwa Silaha aina ya SMG yenye namba UC59821998 ikiwa na magazine mbili, magazine moja ikiwa na risasi kumi na tisa (19) na nyingine ikiwa tupu na maganda kumi na tatu (13) ya risasi aina ya SMG.

Katika ufuatiliaji wa tukio hilo ilibainika kuwa mmoja wa majambazi hao waliouwawa ni miongoni mwa watuhumiwa walioshiriki tukio la kuvamiwa kwa Meja Generali mstaafu wa Jeshi la Wananchi VICENT KARIONGO lililotokea mnamo tarehe 11/09/2017 majira ya saa kumi na moja jioni.

Majeruhi wote wawili walifariki dunia wakiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Mwananyamala. Hakuna askari aliyeumia au kujeruhiwa, miili ya marehemu imehifadhiwa Hospitali ya Mwananyamala. Jitihada za kumtafuta jambazi aliyekimbia zinaendelea.

Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dsm mnamo tarehe 12.10.2017 majira ya saa nane na nusu usiku huko maeneo ya Mbezi Luis, Tegeta “A” askari walipata taarifa kuwa katika Bar iitwayo TUMAINI, kuna majambazi ambao idadi yao haijajulikana wakiwa na gari no. T 563 TAH aina ya Toyota Noah rangi ya Blue ikiwa imetolewa viti vyote vya nyuma na kubaki siti ya dereva na abiria, lengo lao lilikiwa ni kupakia vitu ambavyo wangeiba kwenye Bar hiyo.

Wakati wakiendelea na uvunjaji askari walifika eneo la tukio na baada ya kugundua askari wamefika majambazi hao walifanikiwa kukimbia na kutelekeza gari hilo, majambazi hao hawakufanikiwa kuchukua mali yeyote na gari lipo kituo cha Polisi. Ufuatiliaji unaendelea wa kujua mmiliki wa gari lililotumika katika tukio hilo.

POLISI KANDA MAALUM DSM KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI KUANZIA TAREHE 06.10.2017 HADI TAREHE 11.10.2017 KIMEFANIKIWA KUKUSANYA TSH 466,350,000/= KWA TOZO ZA MAKOSA YA USALAMA BARABARANI

Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es salaam kupitia Kikosi chake cha Usalama barabarani kinaendelea na oparesheni ya ukamataji wa makosa ya Usalama Barabarani kwa kipindi cha kuanzia tarehe 06.10.2017 hadi tarehe 11.10.2017 kama ifuatavyo:-
  1. Idadi ya magari yaliyokamatwa – 14,340
  2.     Idadi ya Pikipiki zilizokamatwa – 413
  3.     Daladala zilizokamatwa -5,024
  4.     Magari mengine (binafsi na malori) -1,205
  5.     Bodaboda waliofikishwa Mahakamani kwa makosa ya kutovaa helmet na kupakia mishikaki -15
  6.     Jumla ya Makosa yaliyokamatwa – 15,545
  7.     Fedha za Tozo zilizopatikana – 466,350,000 /=
  8.     Magari yaliyokamatwa kutokana na Kuchelewa kulipa faini kwa wakati – 2,832 (zaidi ya siku 7)

    Kiasi kilicholipwa – 264, 673,4000/=

L .B.MAMBOSASA – SACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Octoba 13

Jafo aziagiza Halmashauri zinazodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa kurejesha mikopo yao

$
0
0
Na Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo amezitaka Halmashauri zote zinazodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa kurejesha madeni yao kabla ya Desemba 30 mwaka huu.

Jafo ametoa agizo hilo  jana Mjini Dodoma alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu marejesho ya mikopo katika bodi hiyo kutoka kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa.

“Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa imefanikiwa kutoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 9.7 hadi Septemba 30, 2017 kwa Halmashauri 54. Hadi Septemba 30, 2017 jumla ya shilingi 6.57 zilirejeshwa,” alisema Jafo.

Aliendelea kwa kusema kuwa halmashauri nyingi zimejitahidi katika kurejesha mikopo waliyochukua lakini kuna Halmashauri 9 zimeonyesha usugu uliopitiliza katika kurejesha mikopo hiyo, ambapo zaidi ya shilingi bilioni 2 hazijarejeshwa kutoka katika Halmashauri hizo.

Jafo amezitaja Halmashauri zilizoonyesha usugu kuwa ni Halmashauri ya Jiji la Mwanza na Mbeya, Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Singida na Morogoro, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, Karatu, Pangani, Igunga, Mbinga, Mji Mbinga na Kongwa.

Aidha amesema kuwa , kitendo cha usugu katika urejeshaji wa mikopo kinanyima fursa kwa Halmashauri nyingine kupata mikopo kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Hivyo basi, Waziri Jafo amemtaka Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Mikopo kufanya ufuatiliaji ili wadaiwa wote waweze kurejesha mikopo yao na wadaiwa sugu kurejesha mikopo kabla ya Desemba 30, mwaka huu.

Hata hivyo Jafo ameitaka Bodi hiyo kuangalia utaratibu wa kupitisha mikopo inayolenga ujenzi wa viwanda na uwekezaji katika Halmashauri ili kukuza ajira na uchumi wa viwanda.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa Richard Mfugale amesema kuwa bodi itatekeleza agizo la Waziri na tayari imeshafanya mawasiliano na halmashauri zinazodaiwa kuona vyanzo vya mapato watakavyoviachia kwa ajili ya kulipa madeni yao.

Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa ilianzishwa kwa lengo la kuziwezesha Mamlaka za Serikali za Mitaa kupata mikopo ili kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo na utoaji huduma za jamii katika maeneo yao.


Mahakama yaamua aliyekamatwa kwa kudai Mugabe ni ‘Mzee' Apewe Dhamana

$
0
0
Mahakama ya Zimbabwe imeamua kumpa dhamana mfanyabiashara mdogo (machinga) aliyekamatwa kwa tuhuma za kumtukana Rais Robert Mugabe kuwa ‘ni mzee asiye hai na anayeota ndoto za mchana’.

Mahakama hiyo imemuachia mfanyabiashara huyo ambaye ni mwenyekiti wa umoja wa wafanyabiashara wadogo (wamachinga) nchini humo, Sten Zvorwadza kwa dhamana ya $200.

Zvorwadza, alishtakiwa kwa kosa la kumtukana Rais na kudharau Mamlaka halali ya Rais.

Mwenyekiti huyo wa wamachinga alikamatwa baada ya kukaririwa na vyombo vya habari akilaani amri ya Rais Mugabe ya kuwaondoa wamachinga wote kwenye mitaa ya jiji la Harare na kuwahamishia katika maeneo waliyotengewa kwa lengo la kulifanya jiji hilo kuwa safi kuliko majiji yote.

Gazeti la Daily News la Zimbabwe limemkariri Zvorwadza akieleza kuwa, “kama sekta isiyo rasmi hatutasikiliza upuuzi. Mugabe ni mzee na anaota ndoto za mchana.”

“Mugabe anapaswa kuheshimu kazi ya sekta zisizo rasmi. Wazimbabwe wanapaswa kuelewa kuwa Mugabe ni mzee na ni mtu anayetembea lakini ameshakufa,” aliongeza.

Gazeti la Harald la nchi hiyo limeripoti kuwa wamachinga wote wameondolewa mitaani na jeshi la polisi kutekeleza amri ya Rais.

Waziri Kalemani Awapo ONYO Watumishi TANESCO

$
0
0
Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amewatangazia kiama wafanyakazi wa TANESCO nchini watakaoshirikiana na watu kuiba miundo mbinu ya umeme, ili kuhakikisha huduma hiyo haihujumiwi kama zingine.

Dkt. Kalemani ameyasema hayo jana alipokuwa akiongea na maafisa wa TANESCO, na kusema shirika limekuwa likipoteza mapato makubwa kufuatia umeme unaopotea, kutokana na kuhujumiwa miundo mbinu yake, na wizi wa umeme uliokithiri unaofanywa na baadhi ya wateja.

Taarifa hiyo imetolewa  baada ya  TANESCO kugundua wateja zaidi ya mia moja wanatumia umeme bila kulipia hali inayolitia hasara shirika, baada ya kufanya operesheni maalum ya kukagua watu wanaoiba umeme jijini Dar es salaam.

Kufuatia operesheni hiyo, baadhi ya watu wamekuwa wakiyakimbia makazi yao kuogopa kutiwa mikononi mwa polisi, na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Dhahabu ya Mamilioni ya Pesa Yakamatwa Bandarini Ikitoroshwa

$
0
0
Mamlaka ya Bandari Tanzania, TPA, kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi imekamata madini ya dhahabu yenye uzito wa kilogramu 6.2 yenye thamani ya Shilingi milioni 500 katika bandari ya Dar es salaam ndani ya gari aina ya Toyota Noah iliyokuwa na watu wawili.

Noah hiyo ilikuwa imewapeleka watu hao wawili bandarini na walipotaka kushuka, walishtukiwa na askari, lakini dereva alikimbia huku akiliacha gari eneo la tukio.

Watu hao walikuwa wakipeleka mzigo huo unaokisiwa kuwa na thamani ya Sh500.3 milioni visiwani Zanzibar.

Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko alisema dhahabu hiyo iliyokamatwa katika eneo ambalo hutumiwa na wasafiri wanaokwenda Zanzibar ilikuwa katika miche mitano ambayo ilihifadhiwa kwenye begi.

Aliwataja watu hao kuwa ni Akifa Mohamed na Jaffer Hussein.

Kakoko alisema walipohojiwa, mmoja wao alidai kuwa nyaraka za dhahabu hiyo ziko Zanzibar, lakini uchunguzi wao umebaini hakuna nyaraka zozote.

Alisema mtuhumiwa mwingine alidai kuwa alikabidhiwa dhahabu hiyo ili aipeleke Zanzibar.

Kakoko alisema watuhumiwa wote wawili wako kituo cha Polisi cha Bandari ya Dar es Salaam na watafunguliwa shtaka la kupatikana na madini isivyo halali.

Akizungumzia walivyokamatwa, Kakoko alisema tukio hilo lilitokea Oktoba 10, saa 5:20 usiku eneo la Azam Sea Link/DMI, wakati askari wa TPA na wa vyombo vya ulinzi na usalama, walipokuwa katika ukaguzi wa abiria, mizigo na magari yaliyokuwa yakiingia katika meli ya MV Azam Sea Link – I.

Alisema watu hao wawili walikuwa wa mwisho kufika eneo hilo wakiwa na gari hiyo aina ya Toyota Noah.

Alisema begi lililokuwa na dhahabu hiyo lilifichwa kwenye viti vya nyuma vya gari.

Alisema mwanzoni watuhumiwa hao walikataa kukaguliwa, lakini walipobanwa walikubali na ndipo walipoufuma mzigo huo.

Alisema gari hilo linashikiliwa na dereva anaendelea kusakwa.

“Tunaendelea kuimarisha ulinzi na usalama ili kudhibiti uhalifu kwa kufanya ukaguzi wa mizigo yote kabla ya kupakiwa melini,” alisema Kakoko.

Katika siku za karibuni Serikali katika vita yake ya kiuchumi imekuwa ikikamata watu tofauti wanaokutwa na madini na rasilimali nyingine za nchi.

Wabunge CCM Kuisoma Namba.........Ni Baada ya Chama Hicho Kutaka Kila Mgombea Awe Mkazi wa Eneo Analotaka Kugombea

$
0
0
Wanachama wanaotaka kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM, sasa watalazimika kuwa wakazi wa eneo wanalotaka kuliwakilisha, sharti ambalo linaweza kuwaondoa takriban nusu ya wabunge wa sasa.

Kutokana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano kuruhusu mtu kwenda sehemu yoyote apendayo, imekuwa rahisi kwa mtu kuishi mji kama Dar es Salaam na kugombea ubunge wa jimbo lililoko katika mkoa mwingine.

Na uhuru huo umewawezesha watu kama Augustine Mrema, ambaye ni mwenyekiti wa chama cha TLP, kuwa mbunge wa Moshi Vijijini kwa tiketi ya CCM, Temeke (NCCR-Mageuzi) na Vunjo (TLP).

Na ni kutokana na uhuru huo, wabunge wengi wa vyama tofauti, wanaishi Dar es Salaam na kuwakilisha majimbo ya maeneo ya asili yao.

Hata wafanyakazi kutoka serikalini, hasa wakuu wa mikoa na wilaya na sehemu nyingine, huchukua likizo wakati wa uteuzi wa wagombea na kwenda maeneo yao asilia au waliyokulia kuomba wapitishwe na wasipopitishwa hurejea makazini.

Lakini masharti mapya ya CCM yanazuia mwanachama kugombea ubunge, udiwani au nafasi nyingine yoyote bila ya kuwa mkazi wa eneo hilo.

“Shika maneno yangu, mwaka 2020 wagombea ubunge watakuwa ni wale ambao wanatoka kwenye maeneo husika, wanaojua na kushughulika na shida za wananchi,” alisema katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Humphrey Polepole katika mahojiano na kituo cha redio cha Times FM jana.

Alisema hatua hiyo imetokana na chama hicho kujitathmini na kujisahihisha baada ya kugundua watu wanataka viongozi wanaotoka miongoni mwao ambao wanajua kero zao na hivyo wataweza kuzishughulikia.

Polepole, ambaye alipata umaarufu wakati wa Bunge la Katiba akitaka litumie rasimu iliyotokana na maoni ya wananchi, alisema wanachama watakaokuwa wakazi wa maeneo tofauti na wanayotaka kuyaongoza, hawataruhusiwa.

Akihojiwa katika kipindi cha Maisha Mseto, Polepole alisema ili mwanaCCM awe na sifa za kugombea, ni lazima awe mkazi wa eneo husika.

Polepole, ambaye alikuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba, alisema suala hilo lilikuwa sehemu ya maoni ya wananchi wakati wa mchakato wa Katiba Mpya.

Alisema msisitizo mkubwa uliopo ni cheo kimoja kwa mtu mmoja jambo linalofundisha kuwa watu wenye kiasi.

“Haya mambo ndiyo watu wanayoyataka. Rais (John) Magufuli alienda mbele zaidi kwamba utagombea nafasi ya uongozi kwenye eneo ambalo wewe ni mkazi vinginevyo, marufuku kugombea,” alisema Polepole.

“Mwaka 2020 unakuja, si mtu upo zako Times FM unapiga kazi, halafu ikifika mwishoni unaenda Ileje eti unaenda kuchukua jimbo.”

Akizungumzia uamuzi huo, katibu wa wabunge wa CCM, Jason Rweikiza alisema sharti hilo litakomesha tabia iliyojengeka kwa baadhi ya wanachama wa chama hicho kwenda kugombea ubunge maeneo ambayo hawajui yana matatizo gani.

“Unakuta wananchi wana shida ya maji, umeme na barabara anakuja mgombea kipindi cha uchaguzi na ahadi kemkem, kumbe yote ni kuwavutia wampigie kura na akishajihakikishia ushindi humumuoni tena,” alisema Rweikiza.

Rweikiza alisema hatua hiyo itasababisha watu wathamini kwao na kuelewa matatizo ya maeneo waliyotoka na uchaguzi utakuwa huru bila ya rushwa.

Credit: Mwananchi

Kwa Mara Ya Kwannza Katika Historia Wizara Ya Madini Kufanya Mnada Wa Tanzanite Mirerani

$
0
0
Wizara ya Madini kwa mara ya kwanza itafanya mnada wa madini ya Tanzanite kutoka kampuni nne za uchimbaji na biashara ya madini eneo la Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara.

Kaimu Kamishna Msaidizi (Uchumi na Biashara ya Madini), Godleader Shoo amesema mnada huo utafanyika Oktoba 15.

Shoo amesema utaratibu wa kufanya mnada huo ni jitihada za Serikali za kudhibiti utoroshwaji wa madini hayo nje ya nchi na pia kuwasaidia wachimbaji kuuza madini yao kwa bei ya ushindani inayoendana na soko la dunia.

Taarifa ya Wizara ya Nishati na Madini imemkariri Shoo akisema mnada huo utashirikisha wanunuzi kutoka ndani na nje ya nchi.

Amesema atakayenunua madini hayo katika mnada ni atakayeshinda bei iliyowekwa.

Amezitaja kampuni zitakazouza madini katika mnada huo kuwa ni TanzaniteOne, Franone, Glitter Germs na Classic Gems. Amesema zitauza madini ghafi na yaliyokatwa.

Shoo amesema mnada utafanyika kwa uwazi kwa kushirikisha wachimbaji, wanunuzi, Shirika la Madini la Taifa (Stamico), vikosi vya ulinzi na usalama, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro na Wizara ya Madini.

“Mnada huu utaendeshwa kwa usalama mkubwa kwa kuwa madini ya Tanzanite yana thamani kubwa. Serikali imeimarisha ulinzi ili kujihadhari na watu wasio waaminifu,” amesema Shoo.

Amesema mnada utaiwezesha Serikali kupata mrabaha stahiki na kodi kwa uwazi ili kuchangia pato la Taifa na kuimarisha ulinzi na usalama kwa wauzaji, wanunuzi na mali zao.

Shoo amesema minada kama hiyo pia hufanyika kwa nchi za Afrika zenye madini ya vito kama vile Zambia (emerald), Zimbabwe (almasi) na Afrika Kusini (almasi).

Mama Maria Nyerere Atoa Ushauri Kwa Vijana

$
0
0
Mama Maria Nyerere, amewaasa vijana kuzingatia utamaduni na michezo ili kuweka sawa akili zao.

Amesema michezo hukutanisha watu wengi na kuwawezesha kubadilishana mawazo yenye kujenga katika maisha.

Mama Maria amesema hayo jana Alhamisi alipozungumza na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Dk Hassan Abbasi nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.

Taarifa ya Maelezo imesema Mama Maria amesema michezo ni hatua muhimu ya ukombozi wa fikra kwa vijana kwa kuwa wakiizingatia wataweza kufanya kazi na kujipatia mahitaji muhimu kama vile chakula na kuondokana na dhana ya utegemezi.

“Vijana wamejikita katika mambo maovu, sasa kitakachoweza kusaidia ni michezo kwa kuwa inawachangamsha, kuwakutanisha na kubadilishana mawazo mazuri na kwa sasa wanaendelea vyema na masuala haya ya michezo ambayo yanadumisha pia utamaduni,” amesema.

Mama Maria, ambaye ni mjane wa Baba wa Taifa, Julius Nyerere amesema kwa sasa vijana wameanza kujirudi katika kudumisha utamaduni kwa kuwa walitaka kupotoka na kuacha utamaduni wao.

Amesema watoto wanazaliwa bila ukomavu wa akili katika utamaduni, lakini pia hawapati elimu ya kutosha kutoka kwa wazazi kuhusu utamaduni, hivyo matokeo yake ni kuishia kuwa na watu wenye tabia za ajabu.

Mama Maria amesema jukumu la ukombozi wa vijana kutoka katika vitendo vibovu ni la Watanzania wote kuwaelimisha vijana kuhusu michezo ili kuweka akili zao sawa.

Amesema kujitegemea kwa vijana na hasa katika kufanya kazi kutawawezesha kutimiza ndoto zao na za Taifa lenye kipato cha kati kwa kutegemea uchumi wa viwanda.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls 0658316976
0755911233
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images