Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mwalimu wa Madrasa jela kwa kulawiti

$
0
0
Mwalimu wa madrasa, Abdillah Sharifu, amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela baada ya kutiwa hatiani kwa kumlawiti mtoto wa kiume wa miaka 11.

Mshtakiwa anadaiwa kumlawiti mtoto huyo na pia kumtishia kuwa angemroga endapo angetoa taarifa kwa wazazi wake kuwa anamfanyia kitendo hicho.

Akisoma hukumu, Hakimu Mkazi Mwandamizi, Juma Hassan amesema ameridhishwa na ushahidi wa mashahidi wanne akiwemo daktari.

“Mshtakiwa nimekutia hatiani kama ulivyoshtakiwa, ninakuhukumu kifungo cha miaka 30 jela ili iwe fundisho kwako na watu wengine wenye tabia mbaya kama hii,” amesema.

Hakimu Hassan amesema kitendo kilichofanywa na mshtakiwa ambaye ni mwalimu wa dini ni cha kikatili.

Shahidi huyo aliieleza Mahakama kuwa mshtakiwa alimfanyia ukatili huo, huku akimtishia kuwa iwapo angethubutu kutoa siri hiyo angemroga.

“Mara kwa mara alikuwa akinifanyia mchezo huu hadi nilipomwambia mama na kisha kwenda kufungua kesi katika kituo cha polisi Mazizini,” alisema mtoto huyo katika ushahidi alioutoa mahakamani.

Katika ushahidi wa mama mzazi wa mtoto huyo, alidai baada ya kuripoti polisi walikwenda hospitali ambako kwa mujibu wa vipimo vya daktari licha ya kutokuwa na michubuko ilionekana aliingiliwa.

Mshtakiwa alidai ana mke kipofu na kwamba, hafanyi vitendo hivyo isipokuwa alikuwa na ugomvi na mama wa mtoto huyo na ndiyo sababu ya kumfungulia kesi.

Hata hivyo, mshtakiwa alishindwa kuifafanulia Mahakama chanzo cha ugomvi hivyo ilitupilia mbali utetezi wake na kumtia hatiani.

Mshtakiwa alitenda kosa hilo, Februari 25 katika eneo la Moshi Bar, Gongo la Mboto.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Tatizo La Kudumaa, Kusinyaa, Kunywea Na Kurudi Ndani Kwa Maumbile Ya Kiume Pamoja Na Tiba Yake

$
0
0
Kudumaa , kusinyaa  na  kunywea  au kurudi ndani  kwa  uume  ni tatizo  linalo  wakabili wanaume  wengi  duniani.
Dalili  za  tatizo  hili  ni  pamoja  na  kuwa na  maumbile madogo sana yaliyo dumaa, sinyaa  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuyafanya  yaonekane  kama  ya  mtoto  mdogo.

VYANZO  VYA  TATIZO  LA  KUDUMAA  NA  KUSINYAA  KWA  MAUMBILE  YA  KIUME.
Kwa  mujibu wa  tafiti  mbalimbali  za  kisayansi, tatizo la  kudumaa  na  kusinyaa  kwa  maumbile  ya kiume  huchangiwa na  mambo mengi. 
 
Baadhi  ya  mambo  hayo  ni  pamoja na  kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu,  kuugua  chango  la  kiume,  kuugua  ngiri,  kuwa  na  uzito & unene  ulio pitiliza, kufanyiwa  upasuaji  wa  tezi  dume , uzee  na  kuugua  maradhi  yasababishayo  kupinda  kwa  uume.
Katika  makala  haya , tutaangazia  namna  suala  la  upigaji  punyeto  linavyo  sababisha  kudumaa  na  kusinyaa  kwa  maumbile  ya  kiume.



NINI  HUSABABISHA  UUME  KUSINYAA,KUDUMAA, KUNYWEA  NA  KURUDI  NDANI KIASI CHA  KUUFANYA  UONEKANE  KAMA  WA  MTOTO ?

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali za kisayansi, Sababu  kubwa   inayo  sababisha  kudumaa, kusinyaa  na  kurudi  ndani    kwa  uume  ni kupungua  ama  kukosekana kabisa   kwa  homoni  zijulikanazo  kitaalamu  kama  HGH  ambazo  pamoja  na  mambo mengine , zina  husika  na  kuchochea  ukuaji  wa  seli zinazo  husika na  ukuaji  wa  misuli ya  uume na  uume  kwa ujumla.

MAMBO  YANAYO  SABABISHA  KUPUNGUA  AMA  KUKOSEKANA  KWA  HOMONI  ZINAZO  SAIDIA  KUCHOCHEA  UKUAJI  WA  MISULI  YA  UUME.

Kwa  mujibu  wa  tafiti za  kitaalamu, mambo  yanayo  sababisha  kupungua  na/ ama  kukosekana  kwa  homoni zinazo  saidia kuchochea  ukuaji  wa  misuli ya  uume ni  pamoja  na :
1.   Kujengeka kwa  mafuta kwenye  mishipa  ya ateri ipitishayo  damu kwenda  kwenye  misuli ya  uume  na  hivyo  kuzuia kutiririka  kwa  damu kwenda  kwenye  misuli  ya  uume.
2.    Kujengeka  kwa  tishu zisizo  vutika ndani ya  mishipa  ya  ateri. Tishu  hizi  huzuia  mishipa ya  ateri kupanuka  na hivyo  kushindwa kuongezeka ukubwa.

KWANINI  PUNYETO HUSABABISHA  UUME KUSINYAA, KUNYWEA  NA  KURUDI  NDANI KIASI CHA  KUONEKANA  KAMA  UUME  WA  MTOTO  MDOGO ?

Kwa mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  huathiri  na  kuharibu  mishipa  na  misuli  ya  uume na  hivyo kusababisha  kujengeka  kwa  mafuta na  tishu  zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri na  hivyo  kuzuia  mishipa ya  ateri  kupanuka na  kuongezeka  pamoja  na  damu  kutiririka  kwenda  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili yanapotokea  huathiri  uzalishaji  wa homoni muhimu  zinazo  husika  na ukuaji wa misuli ya  uume, na hatimaye  hufanya  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa, kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama wa  mtoto.
 Homoni  hizo hujulikana  kama  HGH  na  huzalishwa  kwenye  ini.

Sababu nyingine   inayo  tajwa  na  wataalamu  ni kwamba, mtu  anaye fanya punyeto   hutumia  akili,  nguvu na  nishati  nyingi sana, jambo ambalo  huathiri utendaji  wa  ogani  nyingine  muhimu  katika  mwili , likiwemo  ini.
 
Ini  linapo kosa  nishati   ya kutosha  hushindwa  kufanya kazi  zake  vizuri  na  moja  kati  ya  kazi kubwa  za  ini  ni  pamoja  na  uzalishaji  wa  homoni  zijulikanazo  kitaalamu kama  HGH  ambazo  kama  ilivyo andikwa  hapo juu, zinahusika na  kuchochea  ukuaji  wa  sehemu mbalimbali  katika  mwili  wa  mwanadamu  ikiwemo   misuli  ya  uume.
 
Mbali na  kuathiri  utendaji  wa  ogani  nyingine  mwilini, upigaji  punyeto  husababisha  athari nyingine  kwenye  mwili wa  mwanadamu  kama  vile uchovu  sugu  wa mwili  pamoja na kunyonyoka kwa  nywele.
 
Athari nyingine  za  upigaji punyeto  ni  pamoja  na  kupoteza  kumbukumbu, kuwahi  kufika  kileleni  ambako  husababishwa  na  kulegea  kwa  mishipa  ya  ateri, kushindwa  kurudia  tendo  la  ndoa, kukosa  hamu  ya  tendo  la  ndoa, uume  kusimama  katika  hali  ya  ulegelege,   maumivu  wakati  wa  tendo  la  ndoa  husuani  wakati  wa  kurudia  tendo  la pili na    mara  baada  ya  tendo  la  ndoa  la  kwanza.

KWANINI   WATU WENGI  WANAO  JIHUSISHA  NA  UPIGAJI  PUNYETO  WANA  MAUMBILE  MADOGO  YA  KIUME YALIYO  DUMAA, SINYAA  NA  KURUDI NDANI.
Uzeofu  unaonyesha  kuwa,  asilimia  kubwa  ya  wanaume  ambao  wamewahi  kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu, wanakabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  maumbile  ya  kiume yaliyo dumaa, sinyaa  na  kurudi ndani.

SABABU  KUBWA   NI  HII  HAPA
Sababu  kubwa  ni kwamba   vijana wengi  wa  kiume, huanza  kujihusisha  na  punyeto   wakiwa  na  miaka  kumi  na sita , kumi na  saba  au  chini  ya  hapo.
Hiki ni  kipindi  ambacho  vijana  hawa  ndio  wanakuwa  wamebalehe.
 
Na kwa mujibu  wa  tafiti  za kisayansi, katika  kipindi  hiki cha  balehe  ndio  kipindi  ambacho  homoni za  HGH  ambazo huhusika   ukuaji  wa  sehemu  mbalimbali  za  mwili  ikiwemo  maumbile ya  kiume, huzalishwa  kwa wingi.
Kama  tulivyo ona  hapo  juu, upigaji  punyeto  huathiri  uzalishwaji  wa   homoni  hizo.
 
Mwisho wa  siku  maumbile  ya  kiume  ya  wahusika, hushinda  kukua  na  kuishia  kudumaa na  kusinyaa.
Na  hii ndio  sababu  kubwa  wanaume  wanao  kabiliwa  na  tatizo  hili  husalia  kuwa  na  maumbile yenye  ukubwa  ule  ule  wakati wa  kubalehe.

NINI  TIBA  ASILIA  YA  TATIZO  LA  KUDUMAA, KUSINYAA  NA  KURUDI NDANI KWA  MAUMBILE  YA  KIUME.

Kama uume wako  umedumaa, umesinyaa, umelegea, umenywea  na  kurudi ndani  kwa  sababu  ulifanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  na  unataka  kuondokana  na  hali  hiyo.
HII  NI HABARI NJEMA  SANA  KWAKO! 

Yapo  MAFUTA  YA  ASILI  ambayo  HUTIBU  na  KUPONYESHA  KABISA  tatizo la  KUDUMAA, KUSINYAA, KUNYWEA  NA  KURUDI NDANI  KWA MAUMBILE  YA  KIUME.
Ni  mafuta  ya  asili  kabisa  yasiyo  na  kemikali  yoyote ya  kiwandani  ambayo  hutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la kudumaa  na  kusinyaa  kwa  uume  ndani ya siku thelathini.

JINSI   YANAVYO   TUMIKA
Mafuta  haya  hutumika  kwa  kuchua  uume. Na hutumika  mara  mbili  kwa  siku  asubuhi  na  jioni kwa  muda  wa  siku  thelathini.
MAMBO   YANAYO FANYWA  NA  MAFUTA  HAYA
Mafuta  haya  husaidia  katika  mambo  yafuatayo :
1.    Kuimarisha  na  kuipa  nguvu mishipa  iliyo legea kwa  sababu  ya  punyeto
2.   Hunenepesha  uume  ulio sinyaa  kwa  sababu  ya  punyeto
3.   Hurefusha  uume  ulio dumaa  na  kurudi ndani  kwa  sababu  ya  punyeto.
4.   Huimarisha  na  kuongeza  nguvu  za  kiume
5.   Hukupa  uwezo wa  kurudia tendo  bila  kuchoka
6.   Hukupa  uwezo  wa  kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  muda  mrefu.
7.   Husaidia  kuongeza  na  kuimarisha  nguvu  na  nishati ya  misuli ya  uume.

JINSI YA  KUYAP ATA
Kuyapata  mafuta  haya, fika  katika  duka  la  kuuza  dawa  za  asili  la  NEEMA  HERBALIST  lililopo  UBUNGO  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  PLAZA  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.
 
Kwa  wateja  wetu  waliopo  jijini Dar  Es  Salaam, ambao  hawana  muda  wa  kufika  ofisini kwetu, tunayo huduma  ya  kuwapelekea  dawa  mahali  walipo  ndani ya  jiji la  Dar  Es Salaam  ( HOME & OFFICE  DELIVERY )
Kwa wateja  wetu waliopo  nje  ya mkoa  wa Dar  Es  Salaam na  Zanzibar, tunawatumia  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  mabus  na boti.
 
WASILIANA NASI  KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84
Na kufahamu  kuhusu  tiba  asilia ya  magonjwa  na  matatizo mbalimbali  ya  kiafya, tutembelee  kila  siku :
 

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Kauli ya Paul Makonda Baada ya Rais Magufuli Kudai ni Mfano wa Kuigwa

$
0
0
Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kutaka Wakuu wa mikoa wengine kuiga utendaji kazi wa Paul Makonda ambaye ni Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam,  Mkuu wa mkoa huyo amemshukuru Rais Magufuli na wananchi wa Dar es salaam kwa kumpa ushirikiano.

RC Makonda ametoa shukrani hizo  kupitia ukurasa wake wa instagram huku akitaka pongezi za Rais Magufuli ziwaendee wale wote waliomuunga mkono.

"Utukufu na heshima apewe Mungu aketie mahali patakatifu.Asante sana Mh Rais asante watumishi wa Mkoa wa Dar es salaam. 

"Asante sana wadau na Wananchi wote wa mkoa wa Dar es saalam kwa mshikamano wenu,Upendo wenu na Umoja wenu katika kuleta maendeleo ya mkoa wa Dar es salaam.

"Pongezi za Mh Rais ziende kwenu nyote mnaoendelea kuunga mkono Kwa hali na mali maendeleo ya Mkoa wa Dar es salaam."

Rais Magufuli Ataja Mshahara wake kwa Mwezi

$
0
0
Rais  Dk. John Magufuli amesema tangu alipoingia madarakani hajapandisha mishahara ya watumishi wa umma na  hatapandisha kwa sababu  anawatumikia Watanzania kwanza.

Kauli hiyo aliitoa   Dar es Salaam jana alipofungua Mkutano Mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) ambao uliwakutanisha mameya na wenyeviti wa halmashauri nchini.

Rais Magufuli alieleza umuhimu wa ALAT katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM na mikakati yake kwa Watanzania.

Aliahidi kushughulikia changamoto za uhaba wa watumishi katika halmashauri na ucheleweshwaji wa ruzuku ya miradi ya maendeleo.

Aweka wazi mshahara wake
Katika mkutano huo, Rais Magufuli pia alitaja mshahara wake anaolipwa kuwa ni Sh milioni tisa kwa mwezi.

“Watu walikuwa wanafanya ‘board meeting’ Dubai na wakienda kule wanapandisha mshahara mpaka Sh milioni 40, mimi mshahara wangu ni Sh milioni tisa. Naeleza ukweli. Watu walikuwa wanafanya kufuru,” alisema.

Akihutubia kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika mkoani Kilimanjaro, Mei Mosi mwaka huu, Rais Magufuli aliahidi nyongeza ya kawaida ya mishahara na kuwapandishia madaraja wafanyakazi wanaostahili.

“Watumishi 9,932 walikuwa na vyeti feki, watumishi hewa walikuwa 19706, hivyo kama Serikali ingeongeza mishahara ina maana watumishi hawa pia wangefaidika na fedha ambazo hawakustahili kuzipata,”  alisema Rais Magufuli.

Pia alisema wafanyakazi 12,000 ‘waliotumbuliwa’ kwa vyeti feki hawawezi kumpenda na ndiyo maana wanapiga kelele kupitia mitandao ya  jamii kwa sababu  naye hahitaji kupendwa nao.

“Watu 12,000 waliotumbuliwa kwa vyeti feki hawawezi kunipenda na hao ndiyo wanaopiga kelele kwenye mitandao huko. Tanzania ina watu milioni 52 sasa hawa (12,000) hata hawanisumbui, nikiwaona ‘I just enjoy them’ hata sishtushwi na wanaolalamika.

“Ukimtumbua mtu jipu hawezi kufurahi akipona ndiyo ataanza kuelewa,”alisema.

Pensheni za watumishi hewa
Rais Magufuli aliagiza Sh bilioni 38 zilitokana na waliokuwa watumishi hewa zirudishwe serikalini.

“Zile pensheni zote za watumishi hewa zirudishwe serikalini, Sh bilioni 38 zirudishwe serikalini. Likizo hewa, likizo za uzazi hewa. Tunachukua hatua lakini ni kwa Taifa la Watanzania. Tulikuwa tunaenda kubaya, kuzimu,” alisema.

Benki Ufisadi
Pamoja na mambo mengine, Rais Magufuli alisema kulikuwa na benki moja   nchini ambayo ilipata hasara ya asilimia sita na hata ilipoongezewa fedha ilipata hasara zaidi.

“Ikapata hasara zaidi ikaongezewa hela sasa ikapata hasara ya asilimia 11 ikaongezewa hela ikapata hasara zaidi asilimia 22. Sasa tumeifunga.

“Watu kama hawa hawawezi kutupenda na mimi sitaki wanipende ilimradi napendwa na watanzania. Sikuja kuuza sura, nimependwa na mke wangu inatosha,”alisema.

Alisema kuna  benki makao makuu yake yalionekana Dar es Salaam lakini imefunguliwa Marekani na   hata wataalamu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) hawakuligundua hilo.

“Kuna benki makao makuu yake yako Dar es Salaam lakini ikafunguliwa kule Marekani. Wataalamu wa BoT hawakugundua haya na fedha ambayo ipo kwenye hiyo benki haizidi asilimia tano,” alisema Rais Magufuli.

Pembejeo hewa
Alisema kwenye halmashauri 140, kulikutwa na pembejeo hewa za kilimo zenye thamani ya Sh bilioni 57.9.

“Hata Chato kwetu kulikuwa na huu uozo pembejeo hewa za thamani ya Sh bilioni 1.5.

“Wanafunzi hewa 65,000 kutoka elimu ya msingi mpaka chuoni. Wanafunzi hewa wanaopokea mikopo walikuwa 8500.

“Ungekuwa mimi umekuta li-Tanzania liko hivi, uozo kila kona ungefanyaje? Ningekuwa Mhehe ningejinyonga, ningesema “Swela,”  alisema.

Alisema wakati anaingia madarakani alikuta mikoa mingi inasumbuliwa na kipindupindu lakini baadaye yalipelekwa madawa.

Pia alisema   bei ya mbolea ya kupandia imeweza kushuka, mathalani katika Mkoa wa Lindi kutoka Sh 100,00 hadi  Sh 51,000.

Alisema wapo watu ambao wanalalamika fedha imepotea na kwamba wanaolalamika ni wale ambao walizoea vya bure.

“Apartment zilikuwa zimepangishwa mtu ana washikaji 10 na wote anawatunza, wengine hadi baa walikuwa wanalipia viti kwamba kila siku lazima akae hapo. Watumishi wengine walikuwa wanasafiri kila wiki, wanabadilishana mabegi pale airport,”alisema Magufuli.

Video Mpya ya Lady Jaydee – I Miss You

$
0
0
Lady Jaydee ameachia video mpya ya wimbo wake uitwao ‘I Miss You’. Wimbo umetayarishwa na Man Walter wakati video imefanyika Afrika Kusini na imeongozwa na Justin Campos pamoja na Icandi.

Nay wa Mitego Azungumzia Athari za Ugomvi wa Diamond na Ali Kiba

$
0
0
Msanii Nay wa Mitego amesema ugomvi wa Diamond ana Alikiba haujaathiri wimbo wake hata mmoja.

Nay ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma Makuzi ameiambia Dj Show ya Radio One kuwa kipimo cha ngoma zake kufika mbali ni pale anapokuwa kwenye show au mapokezi ya watu mtaani ila mambo ya mtandaoni hayaathiri chochote.

“Ni wimbo wangu gani umeathiriwa na ugomvi na Diamond na Alikiba?” alihoji Nay wa Mitego.

“Majibu ya wimbo unayapata kwenye show, majibu ya wimbo unayapata mtaani, mimi nafanya muziki kwa ajili ya watu wangu wa mtaani siyo watu wa kwenye mitandao” amesema.

Ameongeza kuwa nguvu yake ya mtandaoni anaijua na nguvu yake ya mtaani anaijua, hivyo majibu sahihi yanayothibitisha ukubwa wa wimbo wake ni pale anapokuwa kwenye show jinsi watu wanakuwa wanaimba na kupokea.

Waziri Ndalichako Aanika MADUDU Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB)

$
0
0
Serikali  imeeleza kwamba matatizo ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ni kulipwa kwa wanafunzi hewa, ubadhirifu wa fedha na kuwepo kwa watendaji wanaohusika kuweka fedha za wanafunzi wanne kwa mwanafunzi mmoja.

Kadhalika imeeleza tabia ya HESLB kujiona ‘Mungumtu’, kuwaona watoto wa Watanzania kama ni shida kwao na wasiostahili kupewa mikopo na hata kuwa na majibu ya mkato yasiyokuwa na chembe ya kazi ya utoaji huduma. 

Waziri wa Elimu, Sayansi ya Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako  alisema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizindua Bodi mpya ya HESLB na kuitaka kujitenga na menejimenti wakati wa utekelezaji wa majukumu yake na kuhakikisha matatizo hayo yote ambayo yapo katika taarifa aliyowakabidhi, yanakaguliwa upya, kuhakikiwa na kufanyiwa kazi.

Pia alisema taarifa hiyo imeambatanisha taarifa ya fedha za HESLB zilizochezewa. 

Alikabidhi taarifa hiyo kwa Makamu Mwenyekiti wa bodi mpya, Madina Mwinyi akiagiza ifanyiwe kazi kuhakikisha na kujiridhisha pamoja na kuwajua wadeni wa HESLB huku ikiepuka kuiamini menejimenti kama ilivyokuwa kwa bodi ya awali badala yake kuisimamia. 

“Ninakabidhi taarifa yenye changamoto za Bodi ya Mikopo kwenu Bodi ya Wakurugenzi ambayo inaainisha uwepo wa wanafunzi hewa na ambao wanalipwa mikopo wakiwemo waliomaliza au kuacha chuo,” alisema.

Pia alisema taarifa hiyo inahusisha kuwepo kwa watendaji wanaohitajika kujieleza ambao walikuwa wakiweka fedha za wanafunzi wanne kwa mwanafunzi mmoja ambapo ushahidi upo na eneo hilo bado kuna shida. 

Kadhalika, aliiagiza Bodi mpya kutazama upya na kujiridhisha kuhusu vigezo vya utoaji mikopo kwani kumekuwa na matatizo, na hata kutizama utoaji wa mikopo kama taratibu na sheria zinazingatiwa. 

“Malalamiko ya Bodi ya Mikopo yapunguzwe ama kuondolewa kabisa ili kukidhi matarajio ya wadau wa elimu nchini, endeleeni kukagua na hata majina ya wanaohitajika kupata mikopo kabla ya kutolewa rasmi,” alisema Profesa Ndalichako.

Kuhusu Bodi mpya aliitaka isimamie zaidi urejeshwaji wa mikopo kwani hadi sasa serikali imetoa Sh trilioni 3.1 tangu kuanzishwa kwa bodi, lakini ni Sh milioni 217 pekee zilizorejeshwa huku Sh bilioni 588 zikiwa zimefikia muda wake zikitakiwa kulipwa.

 Akizungumza baada ya bodi hiyo kuzinduliwa, Makamu Mwenyekiti, Madina Mwinyi alisema katika kufanyia kazi changamoto za HESLB wataanza kwa kujipanga wao wenyewe katika taasisi wanamotoka ili kila mmoja kujua ni kiwango gani cha mikopo kinachotakiwa kurejeshwa.

Kadhalika alisema bodi hiyo itahuisha taswira ya HESLB pamoja na kuiaminisha jamii kuwa suala la mkopo wa elimu ya juu ni lazima kurejeshwa kwa wakati. 

Wajumbe wa bodi hiyo na taasisi wanazotoka katika mabano ni Profesa Caroline Nondo (Mwakilishi kutoka Tume ya Vyuo Vikuu), Susan Urio (Mwakilishi wa Wanafunzi), Madina Mwinyi ambaye ni Makamu Mwenyekiti (Mwakilishi wa Wizara ya Elimu Zanzibar).

Wengine ni pamoja na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Gerson Mdemu (Mwakilishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali), Dk Dalmas Nyaoro (Mwakilishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia), Frank Mgeta (Mwakilishi wa Wizara ya Fedha na Mipango), Dk Francis Masika (Mwakilishi wa Baraza la Elimu ya Ufundi) na Mjumbe mmoja ambaye ni Mwakilishi wa Wizara ya Fedha Zanzibar hajateuliwa.

Mahakama Yakwama Kutoa Uamuzi Kesi ya Wema Sepetu

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imekwama kutoa uamuzi wa ama kupokea au kutopokea kielelezo cha hati ya ukamataji mali nyumbani kwa Wema Sepetu katika kesi ya kutumia dawa za kulevya kwa sababu Hakimu hajamaliza kuandaa uamuzi huo.

Uamuzi huo ulitarajiwa utolewe leo October 4, 2017 na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, lakini amesema bado hajamaliza kuandaa uamuzi huo ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi November 1, 2017.

Awali, Wakili wa Wema, Peter Kibatala aliiomba Mahakama isipokee hati hiyo kwa kuwa haikukidhi vigezo.

Mbali ya Wema, washtakiwa wengine ni Angelina Msigwa na Matrida Abbas ambao wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.

Kilichoendelea Leo Mahakamani Kuhusu Kesi ya Rais wa Simba, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirisha kesi ya utakatishaji fedha na kugushi inayowakabili Rais wa Simba, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ hadi October 11, 2017 kwa sababu upelelezi haujakamilika.

Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leornad Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa kuwa shauri hilo limeitishwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi haujakamilika, hivyo anaomba ipangiwe tarehe nyingine ambapo baada ya kueleza hayo Hakimu Mwambapa aliahirisha kesi hiyo hadi October 11, 2017.

Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha Dola za kimarekani 300,000.

Katika shtaka la kwanza, washtakiwa hao wanadaiwa kuwa walikula njama ya kughushi fomu ya maombi ya kuhamisha fedha ya March 15, 2016 wakionesha Klabu ya Simba inalipa mkopo wa Dola za kimarekani 300,000 kwa Evans Aveva wakati si kweli.

Katika shtaka la pili alidai kuwa March 15, 2016 katika benki ya CRDB tawi la Azikiwe Ilala, Aveva akijua alitoa nyaraka ya uongo ambayo ni fomu ya maombi ya kuhamisha fedha ya March 15, 2016 wakati akijua ni kosa.

Katika la tatu la kutakatisha fedha, Aveva na Nyange wanadaiwa kuwa kati ya March 15 na June 29, 2016 Dar es Salaam  kwa pamoja walikula njama ya kutakatisha fedha kwa kupata Dola za kimarekani 300,000 wakati wakijua ni zao la uhalifu.

Kwa upande wa shtaka la nne la kutakatisha fedha, Aveva anadaiwa kuwa kati ya March 15, 2016 katika benki ya Barclays Mikocheni alijipatia Dola za kimarekani 300,000 wakati akijua zimetokana na kughushi.

Katika shtaka la tano la kutakatisha fedha, mshtakiwa Nyange anadaiwa kuwa March 15, 2016 katika benki ya Barclays tawi la Mikocheni alimsaidia Aveva kujipatia Dola za kimarekani 300,000 wakati akijua fedha hizo zimetokana na kughushi.

Washtakiwa wapo rumande kwa sababu shtaka la kutakatisha fedha linalowakabili halina dhamana.

Tatizo la Nguvu za Kiume na Chanzo cha Kuwa na Maumbile Madogo

$
0
0
Wataalam katika chuo kikuu cha tiba johns hopkins wanakili kuwa asilimia 75% ya wanaume duniani wamepatwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Tatizo hili linasababishwa na kushuka kwa TESTOSTERON kwenye damu ,kawaida testosteron kwenye damu inatakiwa iwe 400ng/d/hadi 900ng/d/.....chini ya 400ng/d/ mwanaume anapatwa na upungufu wa nguvu za kiume (erectile disfunctioning) kupungua maumbile ya kiume kwa kawaida anatakiwa kutumia dk 20_30 ndipo amalize na umbile lake liwe si chini ya nchi 7.5 .

Sababu zinazoweza kushusha testosterone homoni ya nguvu za kiume ni PUNYETO,SUKARI,BP,MAGONJWA YA FIGO,TUMBO LA CHANGO,ULEVI KUPITA KIASI,MAGONJWA YA ZINAA,U.T.I,KUTOKWA NYAMA SEHEMU ZA HAJA KUBWA,(BAWASIRI).

Wanawake pia wamekumbwa na upungufu wa hamu ya tendo la ndoa kutokana na kushuka kwa homoni estrogen, ambapo mwanamke hupatwa na kuumwa tumbo la chini ya kitovu ,maumivu anapoingiliwa,ukavu mwingi,hata kama ameandaliwa,kuyumba kwa hedhi.

Mtaalam mwingine ambaye ni mkurugenzi wa mradi wa EEP PROF RICHARD SHARP,Anabainisha vyanzo vingine vinavyoondoa mvuto wa mapenzi kuwa aina ya pepo INCUBUS wa kiume hummiliki mwanamke hadi kushindwa kutamani mapenzi na binadamu wa kawaida,mwanamke huota ndoto akifanya mapenzi na watu au wanyama,na mwanaume pia kukosa kuwatamani wanawake naye hujiwa na ndoto akifanya mapenzi nahuamka amelowa.

DR JIDONGEJA  MTAALAM WA TIBA ASILI ANAKUBALIANA NA TAFITI HIZI NA ANAKIRI KUWA WATU WENGI WENYE MATTIZO HAYA ANAWATIBU.

 PIA HUTOA TIBA ZA KISAIKOLOJIA ZA KUKUZA MVUTO KWA MTU KUPENDWA.ANAPATIKANA DAR ES SALAAM NA HUDUMA UNALETEWA POPOTE. SIMU NO 0758078280.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Ajali ya lori yaua watu 15 Sumbawanga.......Rai Magufuli Atuma Salamu za Rambi rambi

$
0
0
Watu 15 wamefariki dunia na wengine tisa kujeruhiwa baada ya lori walilokuwa wakisafiria kupinduka eneo la Ntembwa ndani ya Hifadhi ya Lwafi wilayani Nkasi mkoani Rukwa.

Ajali hiyo imetokea jana Jumanne saa mbili usiku baada ya lori aina ya Fuso lililokuwa likitoka Kijiji cha Mvimwa kuelekea Kijiji cha Wampembe kupinduka. Lori hilo lilikuwa limebeba mahindi na abiria.

Kutokana na ajali hiyo, Rais John Magufuli amemtumia rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Stephen, familia za marehemu, ndugu, jamaa na marafiki  walioguswa na vifo hivyo.

Katika taarifa ya Ikulu, Rais Magufuli amewaombea majeruhi wa ajali hii wapone haraka ili warejee katika afya njema na kuungana na familia zao katika maisha yao ya kila siku.

Rais Magufuli amezitaka mamlaka zinazohusika na usalama barabarani kuongeza juhudi zitakazowezesha kukabiliana na matukio ya ajali ili kuokoa maisha ya watu na mali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando katika taarifa amesema lori hilo  liligonga mwamba kabla ya kupinduka.

Kyando amesema watu 12 walikufa papo hapo na wengine watatu walifariki baada ya kufikishwa katika Hospitali ya Mkoa wa Rukwa. Amesema dereva wa lori hilo alikimbia baada ya ajali kutokea.

Serikali Yapiga Marufuku watumishi Kukamatwa na kuwekwa ndani

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepiga marufuku tabia ya baadhi ya viongozi  katika maeneo mbalimbali nchini kuwakamata na kuwaweka ndani watumishi wakiwemo wauguzi bila ya kufuata taratibu.

Pia amewataka wauguzi nchini kufanya kazi kwa weledi, uaminifu pamoja na kufuata maadili ya taaluma yao kwa kuwa maisha ya wagonjwa yako chini yao.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Oktoba 04, 2017) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa 45 wa Chama cha Wauguzi Tanzania, mkoani Lindi.

“Naagiza viongozi wote kufuata na kuzingatia sheria. Kama kuna makosa ya kitaaluma, Mabaraza husika yashughulikie jambo hilo na ni marufuku kuwaweka ndani watumishi kwa tuhuma za kitaaluma.”

Amesema kwamba katika sekta ya afya bila wauguzi ambao ni kundi kubwa kati ya Wanataaluma wa Afya, Serikali haitaweza kutekeleza ipasavyo mikakati mbalimbali iliyopangwa kwa ajili ya kuboresha sekta hiyo.

Katia hatua nyingine Waziri Mkuu amewaasa wauguzi wote nchini kuhakikisha wanazingatia kiapo cha maadili ya kazi yao na kwamba Serikali haitamvumilia yeyote atakae bainika kwenda kinyume.

“Nanyi Wauguzi mnao wajibu wa kutoa huduma kwa wananchi kwa kuzingatia kiapo na miiko ya taaluma yenu. Tunazo taarifa kuhusu baadhi ya Wauguzi kutoa lugha chafu kwa wagonjwa, kuomba rushwa na wengine kujihusisha na vitendo vya wizi wa dawa.”

Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha afya za Watanzania wote zinaimarika ili kuendana na kasi ya utendaji kazi wa Serikali ya kuinua uchumi na kufikia wa kiwango cha kati, hivyo ni lazima watoe huduma bora kwa wananchi.

Pia amewaomba waunge mkono kwa nguvu zote jitihada za Serikali katika kuhakikisha miundombinu na vifaa vyote havihujumiwi na watu wachache ili viwe msaada mkubwa hususani kwa akina mama wajawazito ili wajifungue salama.

Akizungumzia kuhusu upungufu wa wauguzi nchini, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa kada mbalimbali wakiwemo Wauguzi na Wakunga na kuwapanga katika maeneo yenye upungufu zaidi.

Awali, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Khamis Kigwangalla alisema baadhi ya viongozi katika maeneo mbalimbali wamekuwa wakiwakamata na kuwachukulia hatua watumishi wa Sekta ya Afya bila ya kufuata taratibu, jambo ambalo si sahihi.

Mkutano huo umehudhuriwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Kigwangalla,  Rais wa Chama cha Wauguzi Tanzania Bw. Paul Magesa, Mbunge wa Lindi Mjini Bw. Hassan Kaunje, Mbunge wa Kuteuliwa  Mama Salma Kikwete(MB) Viti maalum.

Wengine ni Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Gustav Moyo, Mwenyekiti wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania Bw. Stewart Mbelwa.

Wengine ni Mbunge wa Viti Maalumu, Hamida Abdallah, Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo ya Uuguzi Bw. Ndementria Vermund, Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania Dkt. Obadia Nyongole na wawakilishi wa wauguzi kutoka mikoa yote nchini.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, OKTOBA 04, 2017.

TUCTA kukaa vikao kumjibu Rai Magufuli

$
0
0
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), limesema linatarajia kutoa msimamo wao hivi karibuni kufuatia kauli ya Rais Magufuli ya kutoongeza mshahara, mara baada ya vikao vyao na serikali kufanyika.

Katibu Mkuu wa TUCTA, Yahya Msigwa amesema wanakusudia kuonana na uongozi wa serikali ili kujadili suala hilo, na ndipo watatoa msimamo wao kama hawatafikia makubaliano mazuri.

“Tunahitaji kuonana na uongozi wa serikali tujadili, kuna mambo mengi ya kujadili sio la mishahara tu, kwa muda mrefu vikao vimekuwa havikaliwi, hata vikikaliwa havina majibu, sasa hivi lazima tulitafutie ufumbuzi kwa sababu changamoto ni nyingi, wafanyakazi hawana hali nzuri kabisa, malalamiko ni mengi mno”, amesema Yahya Msigwa.

Hapo jana Rais Magufuli ametoa kauli ambayo imeibua sintofahamu nyingi kwa wananchi, baada ya kusema hajaongeza mishahara na hatoongoze mishahara kwa wafanyakazi kwa kipindi chote atakachokuwepo madarakani.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Octoba 5

Dereva wa Tundu Lissu Amtesa IGP Sirro ........Amtaka Afike Polisi Kuhojiwa

$
0
0
Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro amesema wanaendelea na upelelezi wa tukio la kushambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu.

IGP Sirro akizungumza  Jumatano akiwa ziarani mkoani Mtwara amemtaka dereva wa Lissu kulisaidia jeshi hilo katika kukamilisha upelelezi.

Lissu ambaye anapata matibabu katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya, alishambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi Septemba 7 nyumbani kwake Area D mjini Dodoma na watu wasiojulikana.

Alisema miongoni mwa wanaohitajika kwa kuhojiwa ni dereva wa Lissu ambaye inaelezwa yuko Nairobi anakopatiwa matibabu ya kisaikolojia.

“Yule kijana kwenye picha ukimwona yuko vizuri tu, sasa wanaposema anapata huduma ya kisaikolojia wakati kwenye magazeti anaonekana hii inatupa changamoto. Ndugu zangu, mheshimiwa Lissu amepigwa risasi na watu tunaowatafuta, huyo kijana aje. Kuja kwake kutatusaidia kupata majibu ya mambo mengi,” alisema IGP Sirro.

Alisema, “Mtu anasema anatibiwa kisaikolojia lakini kila siku nikiona magazeti anaonekana anawaka, inanipa tabu.”

IGP Sirro aliwataka waandishi wa habari kuwasilisha taarifa hiyo kwa umma akisema, “Kimsingi waandishi wa habari naomba mlipeleke hili sisi tuna uchungu sana na mheshimiwa Tundu Lissu, tunamheshimu ni mtu muhimu kwa Watanzania na sisi tunataka tuwapate waliofanya lile tukio lakini ushirikiano ni mzuri ili  kufanikiwa,” 

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Kauli ya IGP irro Kuhusu Miili Iliyookotwa Bahahiri

$
0
0
Inspekta Jenerali wa Polisi, Simon Sirro amesema wameunda timu ya wataalamu kuchunguza miili iliyookotwa na sampuli kutoka miili hiyo zimechukuliwa.

Amesema iwapo kuna watu ambao ndugu zao wamepotea ni vyema wakafika katika ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kwa ajili ya vipimo na kufanyika upelelezi.

“Bahari ni kubwa inapita katika nchi nyingi na inachukua kila kitu, haya mambo yanapotokea hata nchi nyingine yanatokea, kwa hiyo kimsingi tumeunda timu ya wataalamu ya kupeleleza kuhusu miili hii, wamechukua majimaji kutoka mwilini,” alisema.

IGP Sirro alisema, “Kama kuna mtu ambaye ndugu yake amepotea afike makao makuu ya Polisi upande wa DCI tuweze kufanya uchunguzi kuona kama ni ndugu yake.”

Alisema miili hiyo haijabainika kuwa ni ya watu wa Taifa gani.

“Tatizo letu Watanzania ni kwamba moja kwa moja wanaanza kuhisi, sijui kwa nini tunakuwa tunaishi kwa hisia na hii hisia hisia si nzuri, tuseme kitu tukiwa na uhakika. Ikitokea jambo utasema ni Sirro, utasema ni nani, hii si nzuri na niwaambie tumwogope Mungu pia,” alisema IGP Sirro.

Viongozi wa dini nchini waeleza wasiwasi wao juu ya hali inayoendelea

$
0
0
Matukio ya uhalifu yanayoendelea nchini yamewaibua viongozi wa dini ambao licha ya kuelezea wasiwasi wao kutokana na kuongezeka, wameitaka Serikali ibuni mikakati ambayo itamhakikishia kila raia usalama wake.

Wamesema kuna haja kwa wananchi kuhakikishiwa usalama kwani woga na hali ya kutokuaminiana iliyoanza kujitokeza miongoni mwao inaweza kusababisha hali kuwa mbaya baadaye.

Viongozi hao wamesema hayo jana walipokutana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba katika kikao kilichofanyika jijini Dar  na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), James Mbatia.

Ingawa kikao hicho kilikuwa sehemu ya utamaduni wa viongozi wa dini zote kukutana na kujadiliana kuhusu mambo yanayohusu nchi, lakini kwa sehemu kubwa kilitawaliwa na matukio yaliyoanza kuibuka katika siku za hivi karibuni.

Matukio hayo ni pamoja na kushambuliwa kwa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, vitisho vinavyotolewa kwa baadhi ya makundi ya watu pamoja na tukio la kukutwa kwa miili katika eneo la Coco Beach jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Askofu Alinikisa Cheyo alisema katika majadiliano hayo wamekubaliana kwamba suala la ulinzi wa raia linapaswa kuwa ajenda ya kudumu kwa Serikali bila kujali itikadi.

“Ni muhimu mwanachi ahakikishiwe usalama wake popote pale alipo… potelea yukoje, yuko wapi lakini ahakikishiwe ya kwamba yupo salama,” alisema.

Hii ni mara ya kwanza kwa viongozi hao wa dini kukutana na waziri Mwigulu tangu kuibuka kwa matukio hayo na walitumia fursa hiyo kufanya maombi ya pamoja kumuombea Lissu ambaye anaendelea na matibabu jijini Nairobi.

Sheikh Hassan Said Chizenga kutoka Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata) alisema mikutano ya namna hiyo inawapa fursa waumini wa pande zote kubadilishana mawazo na kisha kukubaliana njia bora zaidi ya kulinda amani ya nchi.

“Huku kukutana tu kwenyewe pia kunasaidia kufuta tofauti zilizopo baina yetu na kuweza kutupa moyo wa kushirikiana sisi kwa sisi na kujua mambo mengine ambayo tulikuwa hatujui,” alisema.

Baadaye waziri Nchemba alisema  kuwa ingawa Serikali inaendelea kuchukua jukumu la kuimarisha ulinzi na usalama, wananchi nao wanapaswa kuchukua tahadhari.

“Wananchi lazima wawe makini maana unaweza ukamkuta mtu anamtuma mtoto kwenda dukani nyakati za usiku wakati sasa kuna haya matukio ya utekaji watoto, kwa hiyo wananchi lazima wazingatie hilo,” alisema.

Alisema Serikali imezipokea hoja zilizotolewa na viongozi wa dini na kwa kuzitilia maanani, inaanza kuangalia namna ya kufanikisha ulinzi wa nyumba kumi.

“Wametupa changamoto na sisi tunazifanyia kazi na tunaangalia uwezekano wa kuanzisha ulinzi wa nyumba kumi,” alisema.    
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images