Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tatizo la Nguvu za Kiume na Chanzo cha Kuwa na Maumbile Madogo

0
0
Wataalam katika chuo kikuu cha tiba johns hopkins wanakili kuwa asilimia 75% ya wanaume duniani wamepatwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Tatizo hili linasababishwa na kushuka kwa TESTOSTERON kwenye damu ,kawaida testosteron kwenye damu inatakiwa iwe 400ng/d/hadi 900ng/d/.....chini ya 400ng/d/ mwanaume anapatwa na upungufu wa nguvu za kiume (erectile disfunctioning) kupungua maumbile ya kiume kwa kawaida anatakiwa kutumia dk 20_30 ndipo amalize na umbile lake liwe si chini ya nchi 7.5 .

Sababu zinazoweza kushusha testosterone homoni ya nguvu za kiume ni PUNYETO,SUKARI,BP,MAGONJWA YA FIGO,TUMBO LA CHANGO,ULEVI KUPITA KIASI,MAGONJWA YA ZINAA,U.T.I,KUTOKWA NYAMA SEHEMU ZA HAJA KUBWA,(BAWASIRI).

Wanawake pia wamekumbwa na upungufu wa hamu ya tendo la ndoa kutokana na kushuka kwa homoni estrogen, ambapo mwanamke hupatwa na kuumwa tumbo la chini ya kitovu ,maumivu anapoingiliwa,ukavu mwingi,hata kama ameandaliwa,kuyumba kwa hedhi.

Mtaalam mwingine ambaye ni mkurugenzi wa mradi wa EEP PROF RICHARD SHARP,Anabainisha vyanzo vingine vinavyoondoa mvuto wa mapenzi kuwa aina ya pepo INCUBUS wa kiume hummiliki mwanamke hadi kushindwa kutamani mapenzi na binadamu wa kawaida,mwanamke huota ndoto akifanya mapenzi na watu au wanyama,na mwanaume pia kukosa kuwatamani wanawake naye hujiwa na ndoto akifanya mapenzi nahuamka amelowa.

DR JIDONGEJA  MTAALAM WA TIBA ASILI ANAKUBALIANA NA TAFITI HIZI NA ANAKIRI KUWA WATU WENGI WENYE MATTIZO HAYA ANAWATIBU.

 PIA HUTOA TIBA ZA KISAIKOLOJIA ZA KUKUZA MVUTO KWA MTU KUPENDWA.ANAPATIKANA DAR ES SALAAM NA HUDUMA UNALETEWA POPOTE. SIMU NO 0758078280.

Rais Magufuli Hatakuwa Mgeni Rasmi Kongamano la Kumbukizi ya Mwl. Nyerere

0
0
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais inapenda kuwajulisha wananchi wote kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli hatakuwa mgeni rasmi katika kongamano la maadhimisho ya kumbukizi ya Mwalimu Nyerere kama inavyotangazwa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Tarehe 11 Oktoba, 2017 ambayo inatangazwa kuwa ndio siku ya kufanyika kwa kongamano hilo, Mhe. Rais atakuwa na majukumu mengine ya Kitaifa kulingana na ratiba yake ya kazi.

Taasisi mbalimbali za umma na zisizo za umma zinazomualika Mhe. Rais katika shughuli zao zinakumbushwa kutokutangaza ushiriki wa Mhe. Rais katika shughuli zao mpaka zipate uthibitisho kutoka ofisi ya Rais.

Tafadhali tuzingatie utaratibu huu.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Godbless Lema Adai Gari lake Limechomolewa nati 13 na Watu Wasiojulikana

0
0
Gari la Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema  limechomoka matairi leo Jumatatu baada kudaiwa kuwa limefunguliwa nati 13 kati ya 20 na watu wasiojulikana.

Lema amesema walikuwa wamepanga na Mbunge wa Arumeru Mashariki(Chadema), Joshua Nassari kuondoka na gari hilo jana usiku kuelekea Dar es Salaam kuwasilisha ushahidi wa tuhuma za rushwa za madiwani waliohama Chadema.

Hata hivyo amesema majira ya mchana alipokuwa na gari alihisi mlio kwenye tairi ndipo alikwenda kuliegesha hoteli ya Equator.

Amesema kutokana na kulitilia shaka gari aliomba lifti kwenye gari la Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli, Isack Joseph kwenda naye Dar es Salaam.

"Asubuhi leo (Jumatatu) nikamtuma dereva wangu akachukue gari Equator hoteli alipeleke gereji na baada ya kutoka mita chache tairi zilichomoka," amesema.

Amesema tayari amemuagiza dereva kwenda kutoa taarifa polisi lakini ameiomba kampuni ya  ulinzi ya inteligence inayolinda nyumba yake kufanya uchunguzi kubaini watu walioingia ndani na kufungua nati.

"Pia nimeomba wataalam kupitia kamera za nyumbani kwangu kuona kilichotokea kwani kuna uwezekano wa watu kuingia ndani kufanya uhalifu huo.”

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Ahukumiwa Miaka 30 Jela Kwa Kumbaka Mwanafunzi

0
0
Mkazi wa Mtaa wa Mitandi Lindi Mjini, Mussa Hassan (35) amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na kulipa fidia ya Sh1 milioni, baada ya kukutwa na makosa ya kubaka na kumpa mimba mwanafunzi wa miaka 13 aliyekuwa anasoma darasa la sita.

Akisoma hukumu hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa, Erasto Philly alisema Mahakama imemtia hatiani mshtakiwa kutokana na ushahidi uliotolewa na shahidi namba moja katika kesi hiyo ambaye ni mwanafunzi.

Hakimu Philly alisema mshtakiwa alitenda makosa hayo Agosti 2017, kwa kumbaka na kumpa mimba mwanafunzi huyo.

Awali, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Emmanuel John aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali kutokana na mshtakiwa kutenda kosa la kinyama tofauti na umri wake ikilinganishwa na wa binti.

RC Gambo Atoa Neno la Faraja kwa Vijana

0
0
Mkuu wa Mkoa Arusha, Mrisho Gambo amefunguka na kuwatia moyo vijana waache tabia ya kuishi katika maisha ya kulia kila siku bali wanapaswa waishi kwa furaha ili waweze kupata baraka za Mungu.

Mrisho Gambo amesema kupitia ukurasa wake maalum wa Facebook baada ya kuwepo na desturi ya watu wengi kuwa na uoga wa maisha huku wengine wakiogopa kusema mbele za watu kwamba huwa wanalia kutokana na kukosa jambo fulani katika maisha yao.

"Usiishi maisha ya kulia kila siku, lazima ifike kipindi useme sasa kulia basi. Kulia kwa uchungu sio maisha, maisha ni kulia kwa furaha, wengi wanaona aibu kusema wamelia sana, mimi nitakuambia ukweli ninalia sana lakini ninamlilia Mungu simlilii binadamu", amesema Mrisho.

Pamoja na hayo, Mrisho ameendelea kwa kusema "Anza kulia na Mungu wako, wanaokucheka waache uchungu ni wao, lia kwa ajili ya watoto wako. Mlilie Mungu kwa ajili ya wazazi, kazi na biashara yako, Mungu akikufuta machozi utaona baraka hata kwa watoto wako, wazazi, kazi hata biashara yako", amesisitiza Mrisho.

TALGWU Kuishitaki Serikali

0
0
Chama  cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) kinatarajia kufungua kesi kuishtaki Serikali kwa madai ya kuwaondoa watumishi 2,115 kinyume na utaratibu.

Kabla ya uamuzi huo, chama hicho kimeiomba Serikali  kuwarejesha kazini watumishi walioajiriwa kupitia cheti cha elimu ya msingi ya darasa la saba.

Katibu Mkuu TALGWU, Rashid Mtima alisema watumishi hao walifukuzwa kazi na kusimamishwa mishahara yao kinyume na tangazo.

Mtima alikuwa akifungua mafunzo ya semina elekezi kwa viongozi wa matawi yote ya Halmashauri Mkoa wa Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.

Alisema chama hicho kinasikitishwa na mwenendo wa Serikali kukaa kimya tangu vilipofanyika vikao vya pamoja vya kuwarudisha watumishi kazini.

Alisema idadi hiyo  ni kubwa na imeathiri  watumishi wa Serikali za Mitaa kwenye  sekta ya afya kwa asilimia 69, watumishi wa afya 27,  maji na asilimia iliyobaki ni kwa watumishi wengine wakiwamo maofisa watendaji wa vijiji.

“Vikao vinne tumefanya nao  sasa inatosha, tayari tunakwenda mahakamani ingawa hatutetei watu wanaoghushi.

“Si kwa kundi hili ambalo Serikali imeliondoa hawakupewa chochote na wala hawaambiwi jambo lolote huku wakibaki kuhangaika jambo ambalo uongozi wa chama umeapa  kutokaa kimya,”alisema Mtima.

Alisema watumishi wanaowapigania kurudi kazini ni wale  walioajiriwa kabla ya Mei 20, mwaka 2004 ili warejeshwe   kazini kwa sababu tayari wamewasilisha vyeti vyao vya kujiendeleza na elimu ya  kidato cha nne.

Serikali ilisimamisha ukaguzi wa watumishi wa umma wenye kiwango cha elimu ya darasa la saba Julai, 11 mwaka huu na watumishi hao walitakiwa kuwasilisha serikalini vyeti vyao vya kujiendeleza.

Alisema   watumishi hao waliweza kuwasilisha vyeti vyao sehemu husika lakini hadi sasa Serikali hawajaweza kuwarudisha katika vituo vyao vya kazi.

Aliwaomba watumishi wa chama hicho waliopata tatizo hilo kuwa na subira wakati suala lao linafanyiwa kazi.

Kuhusu semina hiyo, Mtima alisema itawajengea uwezo na misingi mizuri itakayowasaidia katika utendaji wao wa  kila siku.

Alisema ili kutimiza lengo la kufanya kazi vizuri, ni vema watumishi hao wakafuatilia kwa  makini mafunzo hayo  waweze kuongeza uelewa.

“Usalama wa dawa nchini ni zaidi ya asilimia 95”- TFDA

0
0
Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, kiwango cha ubora na usalama wa dawa nchini kimeongezeka kwa zaidi ya asilimia 95.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Bw. Hiiti Sillo, amemweleza mwandishi wetu hivi karibuni kuwa kwa sasa usalama wa dawa nchini umeongezeka na kwamba Taasisi yake imejizatiti kuongeza weledi wa udhibiti.

“Hivi sasa udhibiti ni mkubwa hivyo dawa zetu ni salama kwa kiwango cha kati ya asilimia 92.5 hadi asilimia 98,” alisema Bw. Sillo.

Aliongeza kuwa hivi sasa hali ya soko la dawa ni salama na taasisi yake inafuatilia kwa karibu ubora na usalama wa dawa kwa kutumia mfumo maalum wa ukaguzi.

Bw. Sillo aliongeza kuwa, mafanikio hayo yanatokana na kuimarika kwa uwezo wa taasisi yake pamoja na ushirikiano mkubwa kati ya taasisi yake na wadau wakiwemo wananchi.

Mkurugenzi Mkuu huyo, alibainisha kuwa taasisi yake imeongeza uwezo wake kwa kuajiri watumishi hadi kufikia zaidi ya 300 kutoka watumishi 53 ilipoanzishwa. Aidha, mbali ya kufungua ofisi za kanda saba (07), TFDA imeongeza uwezo wa maabara zake za uchunguzi na zimepata ithibati za umahiri za kimataifa ikiwa ni pamoja na kutambuliwa na Shirika la Afya la Dunia (WHO).

“Uwezo wetu umekuwa mkubwa na tuko karibu na maeneo yote ya udhibiti. Hivi sasa mbali ya ofisi zetu za kanda, lakini pia tuna wawakilishi katika kila Halmashauri nchini,” alisema.

Alifafanua kuwa Halmashauri zote zina wataalamu ambao wanafanya kazi kwa niaba ya Mamlaka ambapo wanasimamia na kudhibiti ubora na usalama wa dawa kwa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa maelekezo ya TFDA.

Hivi sasa TFDA ina ofisi za kanda saba ambazo ni Kanda ya Ziwa, Kanda ya Kati, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Mashariki, Kanda ya Kusini na ya Nyanda za Juu Kusini.

Mkurugenzi Mkuu huyo aliwapongeza wataalamu wa taasisi yake kwa kazi nzuri wanayoifanya na kuwashukuru wadau mbali mbali kwa ushirikiano wao na hasa wananchi ambao amesema wamekuwa mstari wa mbele kushirikiana na taasisi yake kutoa taarifa zinazohusu uvunjifu wa sheria.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, katika kipindi cha mwaka 2003 hadi Juni, 2017, TFDA imesajili dawa 12,474.

Kwa upande wa dawa zilizoingizwa na kugundulika kuwa hazina ubora, katika kipindi hicho, TFDA iliteketeza dawa zenye jumla ya thamani Shilingi bilioni 11.591.

Na Mwandishi Wetu, MAELEZO

Lema, Nassari, Msigwa Wawasilisha Uhahidi wao TAKUKURU

0
0
Wabunge wa Chadema, Joshua Nassari (Arumeru Mashariki), Godbless Lema ( Arusha Mjini) na Mchungaji Peter Msigwa(Iringa Mjini) wamewasilisha Takukuru ushahidi wanaodai unaonyesha jinsi madiwani wao walivyonunuliwa kwa kupewa rushwa.

Wabunge wao, wamewasilisha ushahidi huo mchana wa leo Jumatatu kwenye ofisi za Makao Makuu ya Takukuru zilizopo Upanga Dar es Salaam.

Wabunge hao wamewasili katika ofisi hizo saa 8.39 mchana na kukutana na waandishi wa habari waliokuwa wakiwasubiri.

Katika kile ambacho waandishi hawakukifikiria, wabunge hao waliwasili kwa miguu na kuelekea moja kwa moja ndani ambapo waandishi walizuiwa kuingia.

Ushahidi huo, wameuwasilisha ikiwa imepita siku moja tangu Lema na Nassari walipofanya mkutano na waandishi wa habari jijini Arusha  kueleza jinsi madiwani wao walivyoshawishiwa na kwa rushwa kuihama Chadema.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Majadiliano kati ya Tanzania na Kampuni ya Barrick Gold Corporation kuhusu Makinikia Bado Yanaendelea

0
0
Wakati majadiliano kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick Gold Corporation kuhusu wizi unaodaiwa kufanywa kwenye uchimbaji na usafirishaji wa mchanga wa madini (makinikia) yakiingia siku ya 64, Ikulu imesema majadiliano hayo yanaendelea.

Majadiliano hayo yanafanyika kipindi ambacho Watanzania wengi wana shauku ya kuona rasilimali za madini zinanufaisha Taifa.

Katika majadiliano hayo yaliyoanza Julai 31, timu ya Tanzania inaongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais- Ikulu, Gerson Msigwa amesema majadiliano yanaendelea na wananchi wasubiri wataelezwa kitakachojiri.

“Majadiliano bado yanaendelea, wakiwa tayari watasema kwani hawawezi kuwa wanajadiliana mara wanakwenda kusema katika media," amesema Msigwa.

Mazungumzo hayo yalianza kufanyika kipindi ambacho Rais John Magufuli alikuwa amekwishapiga marufuku ya kusafirisha nje makinikia hadi mgogoro wa kimaslahi kati ya wawekezaji hao na Serikali utakapomalizika.

Miongoni mwa kinachojadiliwa ni kodi ambayo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeitaka Kampuni ya Acacia kuilipa Serikali ya Tanzania Dola za Marekani Bilioni 190 ambazo ni zaidi ya Sh 434 trilioni zinazodaiwa kutokana na malimbikizo ya kodi na adhabu.

Msingi wa mazungumzo hayo ni baada ya Rais Magufuli kuunda tume mbili kuchunguza madai ya wizi na ufisadi unaodaiwa kufanywa na wawekezaji hao kwa zaidi ya miaka 19 iliyopita tangu walipoanza uzalishaji wa dhahabu.

Hakimu Amtaka RCO Temeke Afike Mahakamani Kujieleza

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesisitiza kuwa Afisa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Temeke, (RCO) lazima afike Mahakamani hapo ili aeleze wamefikia wapi kuhusu upelelezi wa kesi ya mauaji  inayomkabili mke wa marehemu Bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita na mfanyabiashara Revocatus Muyela.

Hatua hiyo inatokana na Wakili wa utetezi Peter Kibatala kumueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kuwa RCO aitwe ili aeleze upelelezi ulipofikia.

Awali, Wakili wa Serikali Estazia Wilson alidai shauri hilo limeitishwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi unaendelea ambapo baada ya kueleza hayo Hakimu Simba alisisitiza RCO aitwe Mahakamani na kuahirisha kesi hiyo hadi October 16, 2017 kwa ajili ya kutajwa.

Washitakiwa hao Februari 23, 2016, waliachiwa huru na Mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa kisha kukakamatwa tena na baadaye kusomewa mashtaka hayo ya mauaji upya.

Katika kesi hiyo namba 5/2017 wanadaiwa kumuua kwa makusudi Dada wa marehemu Bilionea Erasto Msuya, Aneth Msuya tukio linalodaiwa kufanywa May 25, 2016 maeneo ya Kibada, Kigamboni Dar es Salaam.

Watu 50 wauawa kwa risasi kwenye tamasha Marekani

0
0
Zaidi ya watu 50 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 200 wamejeruhiwa baada ya mtu mmoja kufyatua risasi hovyo kwenye tamasha la muziki Las Vegas, Marekani.

Vifo hivyo vimetokea leo baada ya mzee mwenye umri wa miaka 64 kufyatua risasi hovyo kutoka katika ghorofa ya 32 ya hoteli ya Mandalay Bay akizielekeza katika tamasha la wazi la muziki.

Kwa mujibu wa ripoti ya polisi, mshambuliaji huyo aliyetambulika kuwa ni mkazi  wa eneo hilo aliuawa kwa risasi na maafisa wa jeshi la polisi.

Jeshi la polisi linamsaka mtu aliyekuwa na mshambuliaji huyo muda mfupi kabla ya kufanya mauaji hayo.

Mkuu wa Polisi wa eneo hilo, Joe Lombardo ameviambia vyombo vya habari kuwa jeshi hilo pia linamsaka mwanamke mmoja mwenye asili ya bara la Asia anayefahamika kwa jina la Marilou Danely.

Hata hivyo, Lombardo alisema kuwa bado hawajapata idadi kamili ya watu waliopoteza maisha katika tukio hilo.

Msemaji wa hospitali ya eneo hilo ambayo pia ilipokea majeruhi alisema kuwa zaidi ya majeruhi 14 walikuwa katika hali mbaya.

Tamasha hilo la muziki lilikuwa likifanyika katika hoteli kadhaa kwenye eneo la Las Vegas tangu Ijumaa ya wiki iliyopita.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Familia ya Tundu Lissu yafanya kikao na Bunge

0
0
Wakati Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Nairobi, familia yake imefanya kikao cha siri na uongozi ya Bunge kujadili matibabu ya mbunge huyo.

Kikao hicho kimefanyika leo Jumatatu jijini Dar es Salaam na imeelezwa kimehudhuriwa na Spika Job Ndugai, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson, Katibu wa Bunge, Thomas Kashilila, Mbunge wa Vunjo, James Mbatia, Mbunge wa Hanang’, Dk Mary Nagu na ndugu watatu wa Lissu, wanaume wawili na mwanamke mmoja.

Kikao hicho kilianza asubuhi, na ilipofika saa 7:40 mchana, alitoka Mbatia akielekea kwenye gari lake baada ya kumaliza kikao hicho. Mwandishi alimfuata kujua kilichojiri ndani ya kikao hicho, Mbatia alikiri kuwepo kwa kikao hicho lakini hakutaka kuzungumza lolote na kuelekeza aulizwe Spika Ndugai.

“Ni kweli tulikuwa kwenye kikao na familia ya Lissu, lakini siwezi kusema tumezungumzia nini.  Kwa taarifa zaidi nendeni kwa Spika au Katibu wa Bunge, walikuwepo pia ndugu zake watatu, wafuateni wanaweza kuwaeleza,” alisema Mbatia.

Msemaji wa familia ya Lissu, Alute Mughwai alipotafutwa alisema kikao hicho kimefanyika kati ya familia na uongozi wa Bunge kuhusu mambo yanayomhusu Lissu, hata hivyo alisema hakijakamilika kwa sababu ya kukosekana kwa upande wa Chadema.

Mughwai alisema kikao hicho kimeahirishwa mpaka wakati mwingine pande zote zitakapotimia ili kulijadili suala hilo kwa ukamilifu wake. Alisema Chadema kupitia kwa mwenyekiti wake Freeman Mbowe walipewa mwaliko lakini hawakuweza kufika.

“Siwezi kukwambia tumezungumzia nini, moja ya masharti tuliyopeana ni kutokusema hadharani mambo tuliyoyajadili lakini yanamuhusu Lissu. Wote ‘interest’ yetu ni kuona Lissu anapona na kuendelea na majukumu yake kama kawaida,” alisema Mughwai.

Hata hivyo, jitihada za kumtafuta Spika wa Bunge pamoja na Katibu wa Bunge zilishindikana baada ya simu zao kuita bila kupokelewa.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alipoulizwa kuhusu kikao hicho amesema taarifa kuhusu kikao hicho zilipelekwa Ofisi ya Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na siyo kwenye chama.

TRA Yazifunga Ofisi za Yusuf Manji

0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imezifunga ofisi za kampuni ya mfanyabiashara Yusufu Manji kutokana na kudaiwa Sh 12.2 bilioni.
 
 Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi, Richard Kayombo amesema wamekuwa na mawasiliano na kampuni ya Farm Equpment ambayo inamilikiwa na Manji tangu Agosti 15 mwaka huu lakini kulikuwa hakuna mrejesho kuhusu deni hilo.
 
Kutokana na hilo amesema wamefunga ofisi zake kwa sababu kampuni hiyo inadaiwa kiasi cha Sh 12.2 bilioni lakini kampuni hiyo ina nafasi ya kuendelea kuwasiliana na TRA namna ya kulipa deni hilo.
 
Tukio hilo limetokea leo Jumatatu kati ya saa 4 hadi 7 wakati TRA na kampuni ya udalali ya Yono wakiambatana na polisi walipokwenda katika jengo hilo lililopo barabara ya Pugu, wilayani Temeke.
 
Baadhi ya mashuhuda wakiwamo walinzi kwa masharti ya kutotaja majina yao  wamesema kuwa ofisi zilizofungwa ni ya Manji na sehemu yake duka la kuuza pikipiki na matrekta.

Wamesema baada ya kufika watu waliingia moja kwa moja katika ofisi yake kisha kufanya majadiliano na wahusika yaliyodumu zaidi ya saa 2.

"Nadhani hawakufikiana mwafaka kwa sababu walivyotoka wakaamuru wafanyakazi wa ofisi hiyo kutoka nje kisha kuweka utepe wa rangi nyekundu na nyeupe," amesema shuhuda huyo.
 
Hata hivyo, mashuhuda hao wamesema hawajui tatizo ni nini lakini waliwasikia maofisa wa TRA na kampuni hiyo ya udalali wakizungumza kuhusu kodi.

Msigwa: Iringa Tulitumia Vifaa vya Australia Kuwanasa Madiwani Wanaohongwa Wahamie CCM

0
0
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Mchungaji Peter Msigwa amefunguka na kusema kuwa biashara ya kununua madiwani wa CHADEMA pia ilifanyika Iringa na kusema kuwa wao walitumia vifaa kutoka Australia kubaini hilo.

Peter Msigwa amesema hayo leo jijini Dar es Salaam baada ya kutoka Ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambapo walikwenda kuwasilisha ushahidi wa Rushwa dhidi ya kununuliwa kwa madiwani hao na wateule wa Rais John Pombe Magufuli.

"Iringa mjini biashara nayo ilifanyika na nina ujasiri mkubwa kwamba muhusika mkuu wa biashara ya kununua madiwani Iringa Mjini ni ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya pamoja na baadhi ya polisi.

"Hiyo mliona 'Episode' ya Arusha vilitumika vifaa vya Uingereza kule Iringa tulitumia vifaa vya Australia na sisi tutafungua jalada kama ambavyo Mkurugenzi wa TAKUKURU ametushauri kwa hiyo tusubiri sababu tumekabidhi kwenye korido za serikali na tunataka sheria zichukue mkondo wake huu uongo uongo wa kusema watu wanaunga mkono utendaji wa serikali tunataka ufike mwisho ili watu wakae kwenye nafasi zao kwa haki na jinsi ambavyo watu waliamua kuwachagua" alisema Msigwa

Diamond Platnumz Kasimamsha Shughuli Hospitali Ya Amana, Jijini Dar Leo.

0
0
Mwanamuziki wa kizazi kipya Diamond Platnumz amesherehekea siku yake ya kuzaliwa leo kwa kutembelea hospitali ya Amana ambako amesababisha shughuli zisimame kwa muda.

Katika ziara yake hiyo aliyoifanya leo Jumatatu, Diamond ametoa vifaa tiba vyenye thamani ya Sh4 milioni.

Muda wote aliokuwa hospitalini hapo wagonjwa na waliokuwa wakiwahudumia walitoka kwa ajili ya kumuona msanii huyo.

Diamond ambaye sasa anatamba na ngoma yake ya Hallelujah, amesema alifikia uamuzi wa kwenda kwenye hospitali hiyo kwa kuwa ndiyo mahali alipozaliwa.

Amesema anajivunia kuwa na watu wazuri wa karibu ambao wanamshauri kurudisha kwenye jamii inayomzunguka.

"Najua hospitali kuna mahitaji mengi nikaona kwa uwezo wangu mdogo nami nishiriki kusaidia mahali nilipozaliwa siku ya leo ili nipate pia fursa ya kuwaona watoto waliozaliwa tarehe kama yangu,"

"Nafahamu kuna changamoto nyingi, niwasihi watu wengine waangalie ni namna gani wanaweza kusaidia," amesema Diamond.

Kaimu mganga mkuu wa hospitali hiyo, Shaany Mwaruka amempongeza Diamond kwa uamuzi huo na kutaka watu wengine waige mfano huo.

"Ungeweza kusherehekea siku yako ya kuzaliwa kwa kufanya chochote kile, lakini ukakumbuka mahali ulipozaliwa."

Dk Mwaruka amesema hospitali hiyo inakabiliwa na changamoto ya vifaa tiba kutokana na idadi kubwa ya watu wanaowahudumia.

Kwenye ziara hiyo Diamond ameambatana na meneja wake, Said Fella.

Waliokuwa Maofisa Wa Tantrade Wahukumiwa Miaka 3 Jela Au Faini Ya Milioni 20.

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewahukumu kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya Sh5 milioni kwa kila kosa waliokuwa Mkurugenzi wa Utafiti na Mipango wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade) Samweli Mvingira na Naibu Mkurugenzi wa Fedha na Utawala,  Judith Msuya baada ya kupatikana na hatia ya kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia Serikali hasara.

Hata hivyo, mshtakiwa Judith Msuya ambaye alikuwa ni Naibu Mkurugenzi wa Fedha na Utawala kutoka Mamlaka hiyo (Tan Trade) amelipa faini hiyo na kuepuka kifungo cha miaka mitatu jela.

Washtakiwa kwa pamoja wametiwa hatiani katika mashtaka manne kati ya matano walioshtakiwa nayo mahakamani hapo  likiwemo la kutumia madaraka yao vibaya kwa kuagiza gari lililotumika kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma iliyosababisha AL Hamadi Motors FZD kupata faida ya Sh34. 89 milioni.

Katika kesi hiyo, washtakiwa walikuwa watatu akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Tan Trade ambaye alifariki dunia wakati shahidi wa kwanza alipotoa ushahidi wake.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha amesema ameridhishwa na mashahidi wa upande wa Jamhuri ambao wameweza kuthibitisha mashtaka dhidi ya washtakiwa hao.

“Nimewatia hatiani washtakiwa  hawa kwa makosa manne ya kutumia madaraka vibaya, hivyo kosa la kwanza hadi la nne mtalipa faini ya Sh 5milioni kwa kila kosa au kwenda jela miaka mitatu kwa kila kosa na shtaka la tano nawaachia huru kwa sababu Jamhuri imeshindwa kuthibitisha shtaka hili,” amesema Hakimu Mkeha.

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, washtakiwa wanadaiwa kuwa kati ya Septemba 2007 na Julai 2008, Makao Makuu ya TanTrade wilaya ya Temeke walitumia madaraka yao vibaya kwa kuagiza gari lililotumika kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma iliyosababisha AL Hamadi Motors FZD kupata faida ya Sh34.89 milioni.

Katika shtaka la pili, tarehe hiyo na mahali hapo, washtakiwa kwa kutumia madaraka yao vibaya, walinunua gari iliyotumika kwa lengo la kumnufaisha Humer Stars kiasi cha Sh32.77 milioni.

Katika shtaka la tatu, washtakiwa wanadaiwa bila kufuata utaratibu wa kushindanisha zabuni waliagiza gari iliyotumika na kusababisha AL Hamad kupata faida ya Sh34.89 milioni huku shtaka la nne watuhumiwa walinunua gari bila kufuata utaratibu wa zabuni.

Shtaka la tano, ambalo washtakiwa waliachiwa huru baada ya Jamhuri kushindwa kuthibitisha shtaka, washtakiwa walidaiwa kutumia madaraka yao vibaya, uzembe na kumsababishia mwajiri wao hasara ya Sh49.145 milioni.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images