Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mwigulu Nchemba Atoa Suluhu ya "Watu Wasiojulikana"

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu  Nchemba amesema kutengeneza mioyo yenye maadili  mema kwa wazazi, watoto na jamii kwa ujumla ni miongoni mwa suluhisho la kudumu la jamii kutokuwa na watu wasiojulikana.

Nchemba ameitoa  kauli hiyo jana  wakati wa maadhimisho ya miaka 57 ya Ushirika wa Wanafunzi wa Kiinjili wa Tanzania (Tafes) yaliyokwenda sambamba na kusherehekea miaka 27 ya uwepo wao hapa nchini.

Tafes ni taasisi isiyo kiserikali inayojishughulisha na kuwajengea uwezo wa kiroho wanafunzi wa vyuo vikuu ili wawe na misingi bora ya uongozi katika ngazi mbalimbali.

Amesema maandalizi ya maadili mema yaanza katika ngazi ya familia na taasisi za kiroho na kwamba, Serikali inawaandaa watu kwa shule, kiafya, lakini afya na uaminifu wa kiroho utatoka kwenye taasisi hizo.

Nchemba ambaye pia Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), amesema uhalifu wa kikatili ni zao la kutokuwapo kwa hofu ya Mungu kwenye mioyo ya watekelezaji wa matukio ya aina hiyo.

"Labda niwaambieni kuna watu wana roho mbaya na wengi wana uwezo kufanya vitu vibaya. Wakati Serikali tunashughulikia jambo hilo, tunazipongeza jitihada kama hizi zinazolenga kubadilisha jamii nzima inayofanywa na Tafes," amesema  Nchemba.

Alisema watu wa vyuo vikuu wana famalia zao na kwamba wakiwa maadili mema itawasaidia kuwaelimisha jamii zinazowazunguka kuhusu misingi bora  ya maadili.

"Tukiwa na watu waliolelewa katika misingi ya imani ya aina hii, hatuwezi tukapata watu wasiojulikana na jambo hili linaniudhi sana. Hatuwezi tukawa na watu wasiojulikana, wanaotenda uhalifu  na kukimbia kusikojulikana na tutashughulika na nguvu ya dola," amesema  Nchemba.

Mbali na hilo, Mwigulu ameongeza kwamba  Tafes kwa kazi wanayoifanya huku akitumia msemo wa nahau ya' Usione vyaelea ujue vimeundwa'.

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Bodi ya Tafes, Profesa Lazaro Busagala amesema  lengo la taasisi hiyo ni kuwatengeneza na kuwajengea uwezo wanafunzi wa vyuo vikuu wa kuwa na maadili mema.

Alisema wametumia nafasi ya maadhimisho hayo kupeana moyo namna ya kuwasaidia  kiroho na kimaadili wanafunzi wa vyuo vikuu ili baadaye wasiwe viongozi wazembe na wala rushwa.

"Hadi sasa Tafes imeweza kuwafikia wanafunzi 5000 wa vyuo vikuu mbalimbali," amesema Profesa Busagala.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya hafla hiyo, Dk Grace Kazoba amesema walitumia maadhimisho hayo kuweka msisitizo wa misingi bora itakayowasaidia wanafunzi hao.

Tatizo la Nguvu za Kiume na Chanzo cha Kuwa na Maumbile Madogo

$
0
0
Wataalam katika chuo kikuu cha tiba johns hopkins wanakili kuwa asilimia 75% ya wanaume duniani wamepatwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Tatizo hili linasababishwa na kushuka kwa TESTOSTERON kwenye damu ,kawaida testosteron kwenye damu inatakiwa iwe 400ng/d/hadi 900ng/d/.....chini ya 400ng/d/ mwanaume anapatwa na upungufu wa nguvu za kiume (erectile disfunctioning) kupungua maumbile ya kiume kwa kawaida anatakiwa kutumia dk 20_30 ndipo amalize na umbile lake liwe si chini ya nchi 7.5 .

Sababu zinazoweza kushusha testosterone homoni ya nguvu za kiume ni PUNYETO,SUKARI,BP,MAGONJWA YA FIGO,TUMBO LA CHANGO,ULEVI KUPITA KIASI,MAGONJWA YA ZINAA,U.T.I,KUTOKWA NYAMA SEHEMU ZA HAJA KUBWA,(BAWASIRI).

Wanawake pia wamekumbwa na upungufu wa hamu ya tendo la ndoa kutokana na kushuka kwa homoni estrogen, ambapo mwanamke hupatwa na kuumwa tumbo la chini ya kitovu ,maumivu anapoingiliwa,ukavu mwingi,hata kama ameandaliwa,kuyumba kwa hedhi.

Mtaalam mwingine ambaye ni mkurugenzi wa mradi wa EEP PROF RICHARD SHARP,Anabainisha vyanzo vingine vinavyoondoa mvuto wa mapenzi kuwa aina ya pepo INCUBUS wa kiume hummiliki mwanamke hadi kushindwa kutamani mapenzi na binadamu wa kawaida,mwanamke huota ndoto akifanya mapenzi na watu au wanyama,na mwanaume pia kukosa kuwatamani wanawake naye hujiwa na ndoto akifanya mapenzi nahuamka amelowa.

DR JIDONGEJA  MTAALAM WA TIBA ASILI ANAKUBALIANA NA TAFITI HIZI NA ANAKIRI KUWA WATU WENGI WENYE MATTIZO HAYA ANAWATIBU.

 PIA HUTOA TIBA ZA KISAIKOLOJIA ZA KUKUZA MVUTO KWA MTU KUPENDWA.ANAPATIKANA DAR ES SALAAM NA HUDUMA UNALETEWA POPOTE. SIMU NO 0758078280.

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ????

$
0
0
Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA 
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA 
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI 
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI 
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK 

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO 

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM,NAUTALETEWA POPOTE ULIPO.

 SIMU; NO 0767145357/0629034550.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Diamond aeleza sababu za Kutumia Youtube Badala ya VEVO

$
0
0
Mwanamuziki Diamond Platnumz amelitolea ufafanuzi suala la mtandao wa YouTube na Vevo baada ya kuzuka sintofahamu kuhusiana na chaneli hizo mbili za kurushia nyimbo za wasanii.

Katika maelezo yake pia ametoa sababu za kuuita wimbo Hallelujah alioutoa juzi usiku. Wimbo huo uliowekwa saa 38 zilizopita umetazamwa na watu milioni1.6 katika mtandao wa YouTube.

Diamond amesema licha ya kujiunga na mtandao wa Vevo, aliamua kuachana nao kutokana na masuala ya maslahi kutomridhisha.

Amesema kulinganisha YouTube na Vevo kwa mtu anayejua masuala ya mitandao ni sawa na kulinganisha baba na mtoto.

“Vevo wanauza Youtube hivyo moja kwa moja mtandao ninaoutumia kuweka kazi zangu ndiyo ambao unanilipa zaidi na ndiyo mtandao mama, ni kweli niliingia Vevo hapo awali lakini kutokana na kushidwana kwenye maslahi niliamua kuachana nao,” amesema mwanamuziki huyo.

 Kwanini  Hallelujah?
Meneja wa mwanamuziki huyo, Salaam Sharaf amesema jina la wimbo huo limetumika kama kionjo cha kusifu uumbaji wa Mungu na si kama wengi wanavyotafsiri.

Salaam hakuishia hapo alitolea mifano ya baadhi ya wasanii hapa nchini ambao wamewahi kuweka neno Mashaalah katika nyimbo zao, huku wengine wakitumia neno Halelluya maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi akiwemo mwanamuziki Nameless katika wimbo wake “Nasinzia”.

“Wakati anatunga mashairi yake lengo lilikuwa kusifia uumbaji, mbona wapo wasanii wengi hapa nchini wametumia neno Mashaallah, Hallelujah maana yake ni kumtukuza na kumsifu Mungu lina tofauti gani na Mashaalah?” amehoji Salaam.

Hata hivyo amesema watu wanaozungumzia suala hilo wanatafuta namna ya kuonekana wanaongea na iwapo wanaona kuna mahali mambo hayajakaa sawa ni vema wakaenda kwenye vyombo vya sheria, “Nafikiri hawana jipya wameshindwa watasema nini kuhusu wimbo huu, hawana sababu ya msingi.”

LIVE: Polepole akitangaza maamuzi ya kikao cha NEC ya CCM kilichokaa leo

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) anazungumza na waandishi wa habari muda huu katika Ofisi Ndogo za CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.

Katika mkutano huo na wanahabari, Polepole anaeleza maamuzi yaliyofikiwa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) iliyokutana leo katika kikao chake.

Fautilia matangazo hayo moja kwa moja hapa chini;

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Tanzania yaeleza sababu za kujitoa Mpango wa Uwazi Serikalini

$
0
0
Wakati Tanzania imejitoa katika Mpango wa Uendeshaji Shughuli za Serikali kwa Uwazi (OGP), sababu za kufanya hivyo zimebainika.

Barua ya Tanzania kujitoa katika mpango huo iliyoandikwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa, Balozi Augustine Mahiga ya Juni 29 iliyowekwa kwenye tovuti ya OGP imeeleza sababu ni kutokana na kuwepo kwa Sheria ya Upatikanaji wa Habari ya mwaka 2016.

Amesema sheria hiyo inalenga kuongeza haki ya upataji wa taarifa na uwazi wa shughuli za Serikali.

Sababu nyingine amesema ni Serikali kuanzisha Tovuti Kuu ya Takwimu Huria (www.opendata.go.tz) kuchapisha data ili zitumiwe na mtu yeyote na hasa kutoka sekta za kipaumbele za elimu, maji na afya.

Pia, amesema Tanzania ni mwanachama wa Mpango wa Afrika wa Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM) wenye malengo sawa na OGP.

Kutokana na hilo, amesema Tanzania inaamini uanachama katika mpango mwingine wenye malengo sawa unaweza kuathiri ushiriki wake.

Tanzania ilikuwa mwanachama wa OGP tangu Septemba 2011. Dhamira ya Serikali kujiunga na OGP ilikuwa  kufanya shughuli zake kuwa wazi zaidi kwa wananchi kwa manufaa ya uboreshaji wa utoaji wa huduma kwa umma katika kupambana na rushwa na kujenga uaminifu zaidi.

Kupitia mpango kazi wa nchi wa OGP wa 2012-2013 na  wa pili wa 2014-2016, Serikali ilitoa ahadi ya kuendeleza ufikiwaji wa taarifa kuhusu utekelezaji wa Serikali na kuchapisha takwimu huria kwenye sekta za kipaumbele za afya, elimu na maji.

CCM yafuta uchaguzi wilaya nne

$
0
0
Mkutano Mkuu wa Halmashauri  Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa (NEC), umefuta uchaguzi wa wenyeviti katika wilaya nne baada ya kubaini wagombea waliojitokeza hawakua na sifa.

Akitangaza uamuzi huo leo , Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole, amezitaja wilaya hizo zilizofutiwa uchaguzi kwamba ni Moshi Mjini,  Siha, Hai,  pamoja na Makete.

Amesema sababu ya kufuta matokeo hayo ni kubainika kwamba  wagombea waliojitokea hawakuwa na  sifa, pamoja na kubainika kuwepo na viashiria hatarishi kwa chama.

Hivyo kutokana na uamuzi huo  Polepole amesema kwamba  wilaya hizo zitaanza upya mchakato wa uchaguzi huo.

CCM Yafichua Alipo Kinana, Yatoa Onyo Kali Kwa Makada Wake

$
0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM), kimesema Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana hajahudhuria vikao vya kamati kuu na halmashauri kuu kwa kuwa aliomba udhuru wa kihali kwa kuwa anauguza ndugu yake wa karibu wa familia.

"Ndugu yetu Kinana anauguza ndugu yake wa karibu, tumwombee apone lakini Kinana alishiriki vyema kikao cha Sekretarieti. Kinana hajajiuzulu au kuandika barua ya kujiuzulu," amesema Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole.

Chama hicho pia kimetangaza kuwachukulia hatua kali makada wake watakaobainika kukiuka utaratibu wa uchaguzi wa ndani wa chama hicho.

Polepole amesema hayo leo Jumamosi alipozungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za chama hicho Lumumba jijini hapa akitoa taarifa ya vikao vya juu vilivyoanza juzi Ikulu ya Dar es Salaam. Amesema Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli amesema vikao hivyo vimepitisha majina ya wagombea wa uenyekiti ngazi ya wilaya.

Amesema kati ya wilaya 161 za kiserikali ambazo ni sawa na za kichama, kikao cha Kamati Kuu na Halmashauri Kuu iliyoketi leo Jumamosi  imezuia uchaguzi katika wilaya sita.

Amezitaja wilaya hizo kuwa Moshi Mjini, Siha, Hai na Makete kwa sababu waliojitokeza kugombea wameonekana kuwa watu hatarishi kwa chama hicho na uchaguzi utatangazwa baadaye.

Wilaya za Musoma Mjini na Musoma Vijijini zitarudia baada ya kutenganishwa kutoka wilaya moja na kuwa mbili.

"Chama hakitasita kuwachukulia hatua kali ikiwemo kufuta uchaguzi au kuwafukuza uanachama wale wote watakaobainika kutozingatia maadili na kanuni za chama chetu," amesema Polepole.

Amesema Halmashauri Kuu imetoa onyo kali kwa wanachama wa Zanzibar walioanza kampeni za uchaguzi mkuu ikisema muda bado na wakiendelea watachukuliwa hatua.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya October 1

Nyumba ya Professor Jay yabomolewa, aeleza jinsi sheria ilivyokiukwa

$
0
0
Mbunge wa Mikumi Mjini, Joseph Haule maarufu kama Professor Jay amekumbwa na zoezi la bomoa bomoa linaloendelea maeneo ya Kimara, jijini Dar es salaam kwa kuvunjiwa nyumba yake huku akieleza kuwa uvunjaji huo haukufuata sheria.

Professor Jay akithibitisha taarifa hizo kupitia kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii amesema zoezi hilo limefanyika wakati yeye akiwa jimboni kwake na mbaya zaidi hakupewa taarifa na zoezi hilo limeendeshwa jioni ambapo sio muda wa kazi kiserikali.

“Jana nikiwa katika majukumu jimboni Mikumi Majira ya saa kumi mbili hivi jioni, nilitaarifiwa kwamba, watu wa Tanroads wakiwa wameambatana na grader mbili na magari mawili ya polisi (defenders) yenye askari waliokuwa na silaha mbalimbali za moto walikuwa wanabomoa nyumba yangu. Sijawahi kuumia kiasi hiki, nimesikitishwa sana jinsi Tanroads wanavyoweza kujichukulia maamuzi bila ya kujali mhimili muhimu wa Mahakama wametoa maagizo gani.“ameandika Professor Jay huku akiwalaumu Tanroads kwa kutotoa taarifa mapema kabla ya kubomoa nyumba yake.

“Taratibu zilizotumiwa kubomoa nyumba yangu bila ya mimi na Tanesco kupewa taarifa saa kumi na mbili jioni (haukuwa muda wa kazi) na kubomoa huku Umeme ukiwa unawaka ni kitendo ambacho kwanza kina hatarisha maisha ya wabomoaji wenyewe, maisha ya familia yangu pamoja na majirani zangu. Tanesco wamenipigia simu baada ya masaa 24 au zaidi baada ya zoezi la kubomoa nyumba kufanyika kunitaarifu kuja kukata Umeme kabla ya ubomoaji huo, pindi nilipo waambia kwamba mbona nyumba imeshabomolewa kabisa na sijaweza kuokoa kitu chochote na hata hiyo meter yenu mnayoiulizia mkaitafute kwenye kile kifusi cha nyumba yangu kilichokusanywa kwa pamoja na watu wa Tanroads. Tanesco walishangazwa sana kuvunjwa nyumba yangu kwa taratibu hizo.“ameandika Professor Jay.

Hata hivyo, Professor Jay amesema tukio hilo ni changamoto tu ya maisha hapa duniani na amelipokea kwa mikono yote miwili kwani kila jambo hutokea kwa sababu maalumu.

“Nimejifunza kumtegemea Na kumshukuru Mungu kwa kila jambo. Na hili ni moja ya mitihani ya hapa duniani. Nimepokea na kumsikiliza Mungu ana mipango gani juu yetu katika familia yangu mbeleni. Tumelipokea na Naamini tutashinda“

Katibu Mwenezi CCM ahamia Chadema

$
0
0
Aliyekuwa Katibu  Mwenezi wa CCM Wilaya ya Nyasa, Staniford Emmanuel amehamia Chadema kwa maelezo kuwa wakati wa ukombozi umefika.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi kadi hiyo kwa viongozi wa Chadema, Emmanuel amesema wakati wa ukombozi umefika hivyo hana budi kuhama CCM ili aweze kutendea haki nchi yake.

“Kuna wanaCCM wenzangu bado hawajafanya maamuzi kama niliyoyafanya mimi kujiondoa na kuhamia chama cha ukombozi ambacho mimi nimekiona ni Chadema,”amesema Emmanuel.

Wazee Chadema wamwomba Rais Magufuli akutane nao

$
0
0
Wakati leo Jumapili dunia ikiadhimisha siku ya wazee, Baraza la Wazee wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) limemwomba Rais John Magufuli kukutana na wazee nchini ili kujadiliana na kupata ufumbuzi wa masuala mbalimbali.

Wito huo umetolewa leo na katibu mkuu wa baraza hilo, Roderick Lutembeka wakati akizungumza na waandishi wa habari makao mkuu wa Chadema jijini Dar es Salaam kuhusu siku ya wazee duniani.

"Wazee ambao tunashauri Rais Magufuli akutane nao ni wazee kutoka vyama vya siasa, viongozi wastaafu wa dini, wastaafu serikalini na awe tayari kupokea ukosoaji wao na kuufanyia kazi," amesema Lutembeka.

Amesema mchakato wa Katiba uliokwama unapaswa kupatiwa ufumbuzi ili kuleta tija kwa Taifa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

"Umuhimu wa Taifa kuwa na Katiba mpya unazidi kuonekana kila siku...Watanzania wanataka Katiba mpya kwa ajili ya kutibu majeraha ya Taifa hili," amesema.

Kuhusu wazee, Lutembeka amesema wamekuwa hawathaminiwi na kutambulika katika ngazi za uamuzi, afya na ndani ya jamii.

Amesema ni wakati sasa kwa Serikali kupeleka muswada wa sheria ya wazee bungeni ili kutekeleza Sera ya Taifa ya Wazee ya Mwaka 2003.

Lutembeka amesema kama Serikali haitafanya hivyo, wawakilishi wa wananchi ambao ni wabunge watumie kanuni ya Bunge kuwasilisha muswada binafsi kuhusu sheria ya wazee nchini.

Mwinyi Ataja Sababu Zilizomfanya Ajiuzulu Uwaziri

$
0
0
Rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi ametaja sababu za kujiuzulu kwake nafasi ya Waziri wa Mambo ya Ndani kuwa kulitokana na kulinda heshima ya Taifa na ya Rais wa awamu ya kwanza.

Hata hivyo amesema anasikitika kuona chanzo cha kujiuzulu kwake bado hadi sasa kipo ambacho ni mauaji ya vikongwe jambo ni fedhea kubwa kwa Taifa kama Tanzania.

Akizungumza katika hafla ya siku ya wazee duniani leo Jumapili ambayo alikuwa mgeni rasmi, Mzee Mwinyi amesema hakuna haja kwa sasa kiongozi kujiuzulu kutokana na mauaji bali Serikali inapaswa kupambana na wauaji wote ili kutoruhusu hali hiyo kuendelea.

Mwaka 1976 akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwinyi alilazimika kujiuzulu nafasi yake baada ya kutokea mauaji katika Mkoa wa Shinyanga lakini miaka tisa baadaye akawa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha miaka kumi.

"Hali ya kuongezeka kwa wazee ni jambo jema linaloonyesha Taifa linapata maendeleo lakini hili kuwaua vikongwe ni aibu na fedheha kubwa sana, naomba likomeshwe," amesema Mwinyi

Kutokana na hali hiyo Mzee Mwinyi amevitwika jukumu kubwa vyombo vya habari akisema wakati wote atalia navyo kwa kuwa ndivyo vyenye jukumu la kutoa elimu kwa watu wenye tabia ya kuwaua vikongwe.

Awali Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema Serikali imetoa kipaumbele kwa wazee na haitasita kuwahudumia kila inapobidi.

Amesema Serikali inapeleka kila mwezi fedha katika kambi 17 za wazee huku ikiwa imeshanunua bajaji 10 kwa ajili ya kuwahudumia ikiwemo majiko matano ya kutumia.

Nassari, Lema waanika ushahidi wa rushwa Dhidi ya Madiwani Waliohamia CCM

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari ameweka hadharani ushahidi wa rushwa na waliopewa madiwani ambao wamejiuzulu Chadema kwa madai ya kumuunga mkono Rais Magufuli.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Nassari ambaye ameambatana na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema walitoa ushahidi huo na kueleza wataukabidhi Takukuru na katika taasisi nyingine.

Katika ushahidi wa video  uliorekodiwa viongozi kadhaa wakiwema Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Alexander Mnyeti pamoja Mkurugenzi Mtendaji wa (H) Meru Christopher Kazeri wamesikika wakiwashawishi madiwani kuhama na baadhi waliahidiwa wangelipwa posho za vikao vyao vilivyobaki hadi 2020 na kukamilishwa miradi yao.

Miongoni mwa makubaliano hayo ni kuwa wapewe fedha na kupata ajira na kukamilishwa miradi yote ya maendeleo waliyoahidi ikiwa ni pamoja na wengine kubadilishiwa makazi pamoja na diwani mmoja kusaidiwa gharama za kufanikisha harusi.

Hata hivyo Mbunge Nassari pamoja na Godbless Lema wameahidi kesho watadfika katika ofisi za TAKUKURU Dar es salaam kwa ajili ya kuukabidhi ushahidi huo wa rushwa kwa Mkurugenzi  Valentino Mlowola

Pamoja na hayo wakati Nassari akiutoa ushahidi huo hadharani leo tayari madiwani 10 wa Chama chake wameshapokelewa ndani ya CCM huku wengie wakiwa wamepinga vikali kuhama chama hicho kwa sababu ya rushwa.

Aidha Nassari amesema ameamua kutoa ushahidi huo sasa kwa sababu alikuwa akiendelea kukusanya ushahidi wa kutosha.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya October 2

Nyimbo za Bob Wine Zapigwa Marufuku

$
0
0
Tume ya mawasiliano nchini Uganda (UCC) imepiga marufuku kwa vyombo vya habari nchini humo kufanya 'interview' na mwanamuziki Bobi Wine, baada ya kuonekana kinara kwenye suala la kupinga ukomo wa urais nchini humo.



Taarifa hiyo imetolewa na mwenyewe Bobi Wine ambaye pia ni mbunge wa upinzani nchini humo kwenye ukurasa wake wa instagram akisema kuwa amepigiwa simu na baadhi ya vyombo vya habari nchini humo na kuthibitisha suala hilo, kuwa wamepigwa marufuku kufanya naye mahojiano yoyote.
 

"Hii asubuhi nilitakiwa kufanya mahojiano na Capital FM, baadaye nikataarifiwa kuwa wamepewa agizo na UCC na kupigiwa simu na watu wa usalama kwamba wasiwe na mimi, nikapigiwa simu na vituo vingine vya redio na runinga na kunithibitishia wamepewa agizo hilo hilo na kwa vitisho, na iwapo watakuwa na mimi watakuwa katika hatari ya kufungiwa", ameandika Bobi Wine. 
 

Bobi Wine ameendelea kuandika akisema kwamba.. "Iwapo unaangalia dalili za kuanguka kwa serikali usiendelee tena, huu ni upumbavu na haukubaliki, serikali inadhani inaweza kutuzuia kufikia watu wetu, wanafanya vitu ambavyo havina tofauti na vile wanavyohubiri kuvipinga",
 

Bobi WIne amekuwa miongoni mwa viongozi maarufu ambao wanapinga vikali suala la kutaka kupitishwa kwa katiba ambayo itongeza muda wa ukomo wa urais, kitendo ambacho kitamruhusu Rais Yoweri Museveni wa nchi hiyo, kugombea tena awamu ijayo.

Viongozi wa dini watakiwa kuwapiga vita wanaotaka kuvuruga amani nchini

$
0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewaomba Viongozi wa Jumuiya na Taasisi zote za kidini nchini wahakikishe wanawapiga vita watu wote wanaopanga na kutaka kuvuruga amani na utulivu uliopo nchini kwa sababu watakwamisha maenendeleo.

Amesema Serikali inaelewa kwamba dini ni miongoni mwa vyanzo muhimu vya maendeleo ya ustaarabu wa mwanadamu kwani inatoa elimu ya maadili mema yenye kuwafanya waumini waepukane na maovu mbalimbali.

Majaliwa ametoa kauli hiyo  Oktoka 01, 2017 wakati akifungua mkutano Mkuu wa mwaka wa 48 wa Jumuiya ya Waislamu Waahmadiyya uliofanyika katika eneo la Kitonga kata ya Msongola wilayani Ilala, Dar es Salaam.

Amesema kila Mtanzania anatakiwa ahakikishe anadhibiti matukio yote yenye viashiria vya uvunjifu wa amani kwa kutoa taarifa katika mamlaka husika.”Tanzania ni nchi salama na yenye utulivu, hivyo ni lazima wote tushirikiane kuitunza.”

“Napenda niwahakikishieni kuwa Serikali inaunga mkono juhudi za Jumuiya za kidini katika kupiga vita maovu ya kila aina; mathalan utumiaji wa dawa za kulevya, wizi, rushwa, uzinzi ambao husababisha madhara mengi ukiwemo ugonjwa wa UKIMWI.”

Amesema iwapo dini zetu zitatumika vizuri tutaweza kwa haraka sana kutekeleza agizo la Rais Dkt. John Magufuli  la ‘Hapa kazi tu’ kwani kila mtu ataepuka uzembe na kuwajibika ipasavyo.

Majaliwa amesema ana imani kwamba jumuiya hiyo kama zilivyo taasisi zingine za kidini itaendeleza kazi kubwa ya kupambana na maovu katika jamii yetu kwa kuwapatia waumini wao na wananchi kwa ujumla elimu na maarifa ya kuboresha tabia zao na maadili yao kiroho.

Amesema amani na utulivu uliopo nchini unatokana na mambo mengi ikiwemo na wananchi kupata ustawi, kuweza kufanya shughuli zao vizuri na kuwa na imani na Serikali yao, ambayo imejiwekea mikakati ya kuhakikisha wananchi hususan wanyonge wanapata faraja ndani ya nchi yao.

Amesema mambo yameweza kupatikana baada ya Serikali kupambana na rushwa na ufisadi pamoja na kuimarisha maadili ya watumishi wa umma, ambayo vimekuwa ni vyanzo vya kupotea kwa amani na utulivu katika baadhi ya nchi.

“Serikali imeweka mikakati madhubuti ya kupambana na ufisadi, kupitia mikataba mibovu na kuimarisha maadili ili kujenga imani kwa wananchi, kuondoa migongano na tofauti ya kipato, kuwa na matumizi mazuri ya rasilimali za umma, kuleta tija kwa kuongeza thamani ya huduma na kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato.”

Kabla, Amir na Mbashiri Mkuu wa Jumuiya ya Waislamu Waahmadiyya Tanzania, Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry  amesema Jumuiya hiyo imekuwa ikifanya mikutano kila mwaka kwa lengo la kukumbushana misingi sahihi ya dini tukufu ya kiislam pamoja na kukuza undugu wao.

Sheikh Chaudhry amesema mkutano wa mwaka huu umejumisha watu zaidi ya 4,000 kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani pamoja na wageni kutoka nchi za Uingereza, Canada, Rwanda, Uganda, Ujerumani, Kenya, Burundi, Malawi na Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).

Amesema Jumuiya hiyo mbali na masuala ya kidini pia inatoa huduma mbalimbali za kijamii kama elimu, maji na afya kwenye mikoa tofauti tofauti nchini.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images