Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Dereva wa Dangote na Waethiopia 8 Wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Watanzania  watatu akiwamo dereva wa kampuni ya saruji ya Dangote, Khalid Abdallah na wahamiaji wanane raia wa Ethiopia wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka matano.

Miongoni mwa mashtaka  yanayowakabili ni kusafirisha kwa magendo binadamu na kuingia nchini kinyume cha sheria.

Mwendesha Mashtaka wa Uhamiaji, Novatus Mlay amewasomea mashtaka hayo leo Jumatano mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa.

Baada ya kusomewa mashtaka, raia hao wa kigeni wamekubali makosa yote yanayowakabili, huku Watanzania wakikana.

Raia hao wa Ethiopia, Solomon Ertiso, Gazahegn Tiroro , Haire  Latso, Thadius Lilanso, Dawit Habtam, Deznet Godebo, Feraru Gurana na Elioj Akola wanadaiwa Septemba 20 katika eneo la Kongowe wilayani Temeke walikamatwa wakiingia nchini bila ya kuwa na kibali.

Kwa upande wao, Khalid Abdallah ambaye ni dereva wa kampuni ya Dangote; Hussein Hamad Hassan na Jumanne Mtambo wanadaiwa Septemba 20 eneo la Kongowe wakiwa raia wa Tanzania walikutwa wakiwasafirisha wahamiaji hao haramu kimagendo.

Wanadaiwa waliwasafirisha wahamiaji hao kwa kutumia gari mali ya kampuni ya Dangote kwa kuwatoa Tanzania kwenda nchini Afrika Kusini.

Pia, wanadaiwa kuwaingiza ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania raia hao wa Ethiopia. Washtakiwa wamekana mashtaka.

Hakimu amewataka kuwa na wadhamini wawili kila mmoja ambao watasaini bondi ya Sh50 milioni kila mmoja. Kesi itatajwa Oktoba 10 na upelelezi imeelezwa haujakamilika. Walishindwa kutimiza masharti hayo hivyo wamepelekwa rumande.

Kwa upande wa raia wa Ethiopia, Mahakama imesema watasomewa maelezo ya awali Oktoba 10.

Wakati huohuo, raia 31 wa Ethiopia na wawili wa Tanzania wamepandishwa kizimbani mahakamani hapo wakikabiliwa na mashtaka matano ya kuingia nchini kinyume cha sheria.

Raia hao wa kigeni walikubali mashtaka na  watasomewa maelezo ya awali Oktoba 11.

Watanzania Ibrahim Abdallah ambaye ni dereva wa gari aina ya Nissan Civilian na kondakta Christopher Steven wanadaiwa Septemba 25 eneo la Toangoma wilayani Temeke walikutwa wakiwasafirisha  raia hao wa Ethiopia kimagendo kutoka Tanzania kwenda Afrika Kusini.

Washtakiwa walikana shtaka na upande wa mashtaka ulidai upelelezi haujakamilika. Kesi itatajwa Oktoba 11. Washtakiwa wamepelekwa rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

Maalim Seif Azungumzia Alivyomkuta Tundu Lissu Nairobi

$
0
0
Katibu  Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, ameeleza maendeleo ya afya ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), baada ya kumtembelea hospitalini Nairobi, Kenya.

Akihojiwa na Redio ya Idhaa ya Kiswahili Deutsche Welle (DW) ya Ujerumani jana, Maalim Seif alisema Lissu anaendelea vizuri na hajapoteza mwelekeo.

“Jana (juzi) nilimtembelea Lissu na nilipata moyo sana, kwa kweli anaendelea vizuri ukizingatia mtu ambaye alipigwa risasi zaidi ya 30, anapata nafuu haraka haraka.

“Bado hajapoteza mwelekeo akili yake ipo timamu, ametuhakikishia haya yaliyotokea hayatamrudisha nyuma katika kuwatetea wanyonge.

“Anazungumza vizuri, yuko makini sana anajua anachokisema na mimi nimepata moyo jinsi nilivyomuona,” alisema Maalim Seif.

Alisema kutokana na mambo yanayoendelea nchini, lazima kuwapo na mjadala wa  taifa   kuona tumekosea wapi na kujirekebisha.

“Mambo kama haya kutokea Tanzania ni jambo ambalo kila Mtanzania lazima aingiwe na wasiwasi kwa sababu hakuna hata mmoja na hasa mwanasiasa ambaye ana usalama wa maisha yake.

“Kama taifa tuzungumze kuona tumekosea wapi na kujirekebisha,” alisema.

Kuhusu uchunguzi wa tukio hilo, alisema hata kama vyombo vya dola vya ndani vitafanya  si aibu kwa nchi kutafuta msaada kwa wengine.

“Yako mambo mengine yaliyotokea huko nyuma na bado hatujaaambiwa yalikwenda vipi, tunaambiwa tu uchunguzi unaendelea. Ni vizuri wananchi waone matokeo ya uchunguzi huo…si aibu kwa nchi kutafuta msaada kwa wengine,” alisema.

Lissu alipigwa risasi  zinazokadiriwa kufikia 32, Septemba 7, mwaka huu, alipokuwa akirejea nyumbani kwake Area D mjini Dodoma baada ya kutoka kuhudhuria kikao cha Bunge na kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili wake.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Mwigulu: Aliyemtisha Nape Kwa Bastola Sio Askari Polisi, Uchunguzi Sakata la Beni Saa Nane Bado Unaendelea

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, amesema aliyemtishia bastola aliyekuwa Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, hakuwa askari.

Amesema kijana hiyo alikuwa ni mhalifu aliyetumia nafasi ya mkutano wa Nape na waandishi habari kutaka kutekeleza tukio hilo ambapo aliishia kumtishia bastola.

“Awali tulidhani yule kijana ni polisi lakini hakuwa na sare za polisi, cha kwanza nilimuelekea Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) kufuatilia na akaleta majibu kuwa hakuwa polisi,” amesema Mwigulu akihojiwa na Kituo cha Televisheni cha Clouds leo.

Aidha, amesema suala la aliyekuwa msaidizi wa Mwenyekiti nwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, Ben Sanane ni ngumu kulisemea kwamba amefariki au yuko kwani polisi bado wanaendelea na uchunguzi.

“Kwa aina ya taarifa ninazopata ni kama inaelekea kufikia ukomo ni jambo ambalo tumelipa uzito kulifanyia kazi na Mtanzania yeyote mwenye nia njema anaweza kutusaidia kufuatilia,” amesema.

Moto Wateketeza Nyumba za POLISI Jijini Arusha

$
0
0
Takribani familia 13 zenye jumla ya watu 44 za Polisi zimekosa makazi baada ya nyumba walizokuwa wakiishi kuteketea kwa moto jana usiku majira ya saa moja.

Nyumba hizo wanazoishi polisi zilizopo katika kata ya Sekei Jijini Arusha zimeeketea kwa moto na chanzo cha ajali hiyo kutajwa kuwa ni hitilafu ya umeme.

Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji mkoani Arusha, Andrew Komba alieleza kuwa kama siyo taarifa kuchelewa kulifika jeshi la zima moto, basi huenda wangeweza kuokoa mali nyingi zaidi.

“Tungefika mapema nusu ya nyumba zilizoteketea tungeziokoa,” amesema Komba.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ambaye naye alifika katika eneo la tukio alilipongeza Jeshi la zima moto kwa juhudi kubwa walizozifanya kuuzima moto huo na kuokoa maisha ya watu pamoja na mali.

“Kuna Nyumba za watumishi wetu askari zimepata ajali ya kuungua moto. Nichukue fursa hii kuwapongeza jeshi la zima moto kwa juhudi kubwa ya kuhakikisha kuwa wamezima moto huu. Takribani familia 13 zimeathirika kutokana na ajali hii ambazo zina watu kama 44….. Taarifa za awali zinaeleza kuwa ajali hii imetokana na hitilafu ya umeme..,” alisema RC Gambo.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema kuwa  tukio hilo ni janga, hivyo watakaa kuona ni kwa namna gani watawasaidia walioathiriwa.

Polisi Amuua Mkewe kwa Risasi na Kisha na Yeye Kujitandika Risasi

$
0
0
Askari Polisi Stephen Mungai Kinuthia wa jimbo la Nakuru nchini Kenya, amemuuwa mkewe kwa kumpiga risasi kichwani na kisha kujiua mwenyewe mbele ya mtoto wao ambaye alishuhudia tukio zima.

Kinuthia ambaye alikuwa skari polisi wa kituo cha Molo, amempiga risasi mpenzi wake huyo mara tatu kwa kutumia bunduki ya AK47 wakiwa nyumbani kwao.

Shuhuda wa tukio hilo ambaye ni mlinzi wa eneo hilo amesema walisikia kelele za watu wakilumbana, na walipokuwa wakikimbilia kujua kulikoni walisikia milio ya risasi na kisha kukawa na ukimya.

Majirani wa eneo hilo wamesema walisikia kelele za mtoto akilia kwa sauti huku akisema baba anamuuwa mama.

OCPD wa Nakuru Joshua Omukatta amesema wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo, huku miili ya marehemu wote ikiwa imepelekwa katika hospitali ya serikali ya Nakuru.

Tatizo la Nguvu za Kiume na Chanzo cha Kuwa na Maumbile Madogo

$
0
0
Wataalam katika chuo kikuu cha tiba johns hopkins wanakili kuwa asilimia 75% ya wanaume duniani wamepatwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Tatizo hili linasababishwa na kushuka kwa TESTOSTERON kwenye damu ,kawaida testosteron kwenye damu inatakiwa iwe 400ng/d/hadi 900ng/d/.....chini ya 400ng/d/ mwanaume anapatwa na upungufu wa nguvu za kiume (erectile disfunctioning) kupungua maumbile ya kiume kwa kawaida anatakiwa kutumia dk 20_30 ndipo amalize na umbile lake liwe si chini ya nchi 7.5 .

Sababu zinazoweza kushusha testosterone homoni ya nguvu za kiume ni PUNYETO,SUKARI,BP,MAGONJWA YA FIGO,TUMBO LA CHANGO,ULEVI KUPITA KIASI,MAGONJWA YA ZINAA,U.T.I,KUTOKWA NYAMA SEHEMU ZA HAJA KUBWA,(BAWASIRI).

Wanawake pia wamekumbwa na upungufu wa hamu ya tendo la ndoa kutokana na kushuka kwa homoni estrogen, ambapo mwanamke hupatwa na kuumwa tumbo la chini ya kitovu ,maumivu anapoingiliwa,ukavu mwingi,hata kama ameandaliwa,kuyumba kwa hedhi.

Mtaalam mwingine ambaye ni mkurugenzi wa mradi wa EEP PROF RICHARD SHARP,Anabainisha vyanzo vingine vinavyoondoa mvuto wa mapenzi kuwa aina ya pepo INCUBUS wa kiume hummiliki mwanamke hadi kushindwa kutamani mapenzi na binadamu wa kawaida,mwanamke huota ndoto akifanya mapenzi na watu au wanyama,na mwanaume pia kukosa kuwatamani wanawake naye hujiwa na ndoto akifanya mapenzi nahuamka amelowa.

DR JIDONGEJA  MTAALAM WA TIBA ASILI ANAKUBALIANA NA TAFITI HIZI NA ANAKIRI KUWA WATU WENGI WENYE MATTIZO HAYA ANAWATIBU.

 PIA HUTOA TIBA ZA KISAIKOLOJIA ZA KUKUZA MVUTO KWA MTU KUPENDWA.ANAPATIKANA DAR ES SALAAM NA HUDUMA UNALETEWA POPOTE. SIMU NO 0758078280.

Serikali yawapa msaada askari waliounguliwa nyumba

$
0
0
Serikali kupitia wakala wake wa ujenzi nchini (TBA) imetoa msaada wa nyumba kwa askari polisi waliounguliwa nyumba zao hapo jana, mpaka pale watakapopata makazi rasmi.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo , ambapo amesema  baada ya ajali hiyo askari hao walikosa mahali pakuishi, hivyo wanaishukuru TBA kwa msaada huo.

"Ule moto umeteketeza kila kitu kabisa, hivyo wale askari hawakuwa na sehemu ya kuishi, jana tuliwahifadhi kwenye bwalo letu la polisi, lakini leo wamepatiwa msaada na wakala wa ujenzi wa serikali (TBA ), wamepewa nyumba za kuishi kwa muda hadi pale watakapopatiwa makazi rasmi, tunashukuru kwa hilo", amesema Kamanda Mkumbo.

Tukio la kuteketea kwa nyumba hizo limetokea usiku wa Septemba 27 mwaka huu  majira ya saa mbili na kuteketeza nyumba hizo, lakini jeshi la zimamoto liliwahi eneo la tukio na kutoa msaada kwa wananchi ambao walianza kuzima.

Mwigulu: Tunamsubiri Tundu Lissu Apone ili Atusaidie Kukamilisha Upelelezi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amezungumzia uchunguzi wa tukio la kushambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu akisema anaamini akipona atatoa mchango mkubwa katika upelelezi.

“Lissu tunamuombea akishapona atatupa mchango mkubwa wa kusaidia uchunguzi, mtu akiwa kwenye maumivu makali huwezi kumuuliza lolote,” amesema Mwigulu akizungumza leo Alhamisi katika kipindi cha Clouds 360.

Amesema kutokana na upya wa uhalifu wa aina iliyotokea kwa Lissu, kuna mambo wanaendelea kuyafuatilia ambayo hawezi kuyaeleza kwa sasa.

“Suala la Lissu kutokana na upya wake, kuna vitu tunaendelea kuvifuatilia, hivyo kuna mambo hatuwezi kuyasemea,” amesema.

Amewataka Watanzania waendelee kuwa na subira kwa kuwa kazi inaendelea kufanyika.

Mwigulu amesema baada ya tukio la kushambuliwa Lissu Septemba 7, taarifa kadhaa zilichukuliwa eneo la tukio ambazo zinaendelea kufanyiwa kazi ili kupata undani wake.

“Wahalifu hawajakamatwa wote, ukianza kusema itakuwa ni shida, kuna mambo yanaendelea kufanywa na hayana ukomo. Ukomo utafikiwa endapo wote waliohusika watakamatwa. Nikisema naweza kuvuruga kazi inayoendelea,” amesema.

Akijibu swali la mtangazaji wa kipindi hicho kuwa watu wanahoji kwamba askari wanapouawa wahalifu wanakamatwa mapema Mwigulu amesema, “ Watu wakiwaza hivyo watakuwa wanakosea, hatuweki madaraja, ni mazingira ya tukio tu.”

Akizungumzia uchunguzi unaoendelea kuhusu kuvamiwa kwa Lissu amesema hawezi kueleza waliokamatwa bali tayari kuna magari zaidi ya 10 yanayofanana na lililohusika kwenye tukio yamekamatwa.

Mwigulu amesema alimuona Lissu siku ya tukio Septemba 7 akiwa katika Hospitali ya Rufaa Dodoma na baadaye uwanja wa ndege aliposafirishwa kwa ajili ya matibabu jijini Nairobi nchini Kenya ambako yuko hivi sasa.

Amesema hajafika Nairobi kumjulia hali Lissu bali kwa Mkoa wa Singida, Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu amefika.

“Katika mazingira mengine tunaendelea kupata taarifa, kama Serikali tuna balozi,  kama waziri kwenda kumuona ni jambo jema katika utaratibu wa uchunguzi hata dereva tutazungumza naye,” amesema.

Amesema dereva hivi sasa anapata tiba ya kisaikolojia na anaamini atakapokuwa tayari atazungumza na wanaokusanya taarifa.

Wahadzabe Waiomba Serikali Iwapatie Tani 2 za Bangi

$
0
0
Jamii ya Wahadzabe wanaojishughulisha na uwindaji, kurina asali na kukusanya matunda porini, wameomba kupelekewa msaada wa bangi angalau tani mbili watakayoitumia kwa mwaka mmoja.

Wahadzabe wanaokadiriwa kufikia 500 ni jamii inayoishi porini maeneo ya Endamaghan, Kandeni Tarafa ya Eyasi Wilaya ya Karatu mkoani Arusha.

Jamii hiyo, bado inakabiliwa na umasikini licha ya kuwa kivutio cha watalii katika Ziwa Eyasi.

Ombi hilo walilitoa juzi katika Kijiji cha Endamaghan, wakati walipotembelewa na timu ya wataalamu kutoka serikalini iliyoteuliwa kuandaa mapendekezo ya muundo wa kipindi cha pili cha mpango wa kunusuru kaya masikini unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Akizungumza na Gazeti la Mtanzania  katika eneo la makazi yao yenye nyumba za asili za nyasi zilizoonekana kuwa wazi kutokana na kufunikiwa na nyasi kidogo, Mwenyekiti wa jamii hiyo, Julius Ndaya alizitaja sababu alizodai ni za msingi za kuomba wapelekewe bangi.

Alisema shughuli za kutembea kutafuta wanyama kwa ajili ya kitoweo huwalazimisha kutembea umbali mrefu kiasi cha kilomita 50, kazi ambayo huwa ni sehemu ya majukumu ya mwanamume katika jamii hiyo.

“Kiasi hiki cha tani mbili kinaweza kututosha watu kama 100 au 200  kwa miezi 6, tunavuta bangi si kama ambavyo wengine au Serikali wanafikiria kwamba tunaweza kusababisha vurugu, kuvunja nyumba za watu, kuiba wala kugombana na jamii nyingine, hapana.

“Mmea huu tumeukuta babu zetu wakiwa wanauvuta wameturithisha, tunaendelea kuvuta bila kuwa na madhara yoyote. Hii ni sehemu ya kiburudisho kwetu, huku porini hatunywi pombe hii ndio pombe yetu. “Ikiwezekana turuhusiwe kulima angalau bustani za bangi lakini changamoto kubwa tunayokutana nayo ni pale Serikali inapopiga marufuku zao hili kwa madai kuwa ni sehemu ya dawa za kulevya,” alisema Ndaya.

Kiongozi wa jamii hiyo alikwenda mbali na kueleza pindi wanapovuta bangi huchangamsha akili na miili yao, hivyo hujikuta wakipiga hadithi za matukio ya uwindaji porini au namna walivyokabiliana na au kukurupushana na wanyama wakati wa uwindaji.

Katika eneo la jamii hiyo lenye nyumba za asili za nyasi zikiwa zimezungukwa na mafuvu ya wanyama pori na miti mikubwa, lilikuwa na wanawake watu wazima walionekana wamekaa kwenye makundi pamoja na vijana wa kiume wakiendelea kuvuta bangi.

Akifafanua kuhusu maombi ya Wahadzabe kuomba tani mbili za bangi, Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Theresia Mahongo alisema Serikali haiwezi kukubaliana na maombi hayo.

“Hata sasa walikuwa wakiniomba, majuzi tuliteketeza kiasi kama cha hekari tano za bangi maeneo ya milimani, kwa hiyo kwa sasa hawaipati inawaumiza zaidi.

“Kikubwa tunaendelea kuwapatia elimu kwamba bangi kwao si kitu kizuri, tutatafuta mbadala na kwa vile wameniomba nikutane nao hilo nalo tutaliweka vizuri.

“Naamini vipo vitu mbadala wanavyoweza kutumia badala ya bangi, mnawaona wanalalamika kwa sababu hawaipati. Tunajua ni wawindaji wanakimbia na kupita maeneo magumu ndio maana wanaihitaji ili iwatoe nishai, ukweli ni kwamba jambo hilo hatuwezi kuliruhusu,” alisema.

Wakati watu hao takribani 200 kutoka jamii ya Kihadzabe wakiomba kupelekewa tani mbili za bangi, katika siku za hivi karibuni baadhi ya wabunge waliomba zao hilo liruhusiwe kuwa la kibiashara ili kuwaongezea kipato zaidi wakulima na wauzaji wa bangi.

Chakula kikuu cha jamii hiyo ni mizizi, matunda pori, asali na nyama huku asali ikiwa ni miongoni mwa vitu vinavyopendwa zaidi na jamii hiyo.

Namna wanavyoitumia mizizi hiyo kwa chakula; wanakula kama ilivyo au kuichoma na ladha yake ni kama muhogo au viazi na mizizi hiyo huwa na ukubwa kama wa mguu wa mtu mzima.

Matunda yao makuu ni kwantlanabe, kalahar, kongolobi na ubuyu ambayo husagwa kwenye jiwe na unga wake husongwa kama ugali na kuchanganywa na asali.

Vyakula vyao vinavyotegemea asili yao haviwapi fursa ya kutumia mafuta, nyanya, kitunguu, sukari au kutumia vinywaji vya viwandani, isipokuwa chumvi.

Wanyama wanaopendwa zaidi na Wahadzabe ni pofu, nyani, tumbili, digidigi  na twiga.

Mwigulu Nchemba Aizungumzia Gari Iliyokuwa Ikimfatilia Tund Lissu Jijini Dar

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, amesema gari ndogo ambayo Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, alidai lilikuwa likimfuatilia maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam, iko Arusha na haijawahi kutumika Dar es Salaam.

Mwigulu amesema leo kuwa baada ya polisi kufuatilia gari hiyo wamegundua iliyokuwa inamfuatilia Lissu ilikuwa na namba batili huku gari halisi yenye namba hizo za usajili ikiwa Arusha.

“Utoaji wa taarifa na wenyewe haukuwa rasmi kwa mfano Lissu aliposema kuna gari inamfuatilia nilielekeza polisi wakaifuatilia ikakutwa Arusha kuna gari ndogo ya namba hizo kwa hiyo kuna moja iliweka namba batili.

“Ile gari ilikutwa kule kule na haikuwa na ruti ya huku (Dar es Salaam) huwa iko kule kule, kwa hiyo kwenye mambo haya ndiyo maana tunahitaji sana ushirikiano.

“Natamani watu hawa tungewatia nguvuni pale pale ningepewa ‘tip’ mapema tungefuatilia hili na  kitendawili cha watu wasiojulikana tungekitegua mara moja,” amesema Mwigulu akihojiwa na Kituo cha Televisheni cha Clouds, leo.

Pamoja na mambo mengine amesema Lissu mwenyewe anaweza kusaidia uchunguzi katika tukio hilo ambapo pia ameonya watu watu wanaotengeneza matukio ya aina hiyo kufikiria madhara yanayoweza kutokea baada ya tukio.

Chadema Wampinga Mwigulu Nchemba Kuhusu uchunguzi Dhidi ya Tundu Lissu

$
0
0
Chadema imesema haitabadili msimamo wake wa kutaka wataalamu kutoka nje kuchunguza shambulio dhidi ya mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Juzi, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba alisema hakuna haja ya kuhangaika kutafuta wachunguzi kutoka nje kwa kuwa mazingira watakayofanyia kazi ni yaleyale na hivyo kuitaka Chadema kuviamini vyombo vya ndani vya uchunguzi.

Lakini jana, Chadema imeeleza kuwa haioni kinachoendelea na hata kama ni mazingira yaleyale, wachunguzi kutoka nje ndiyo muafaka.

Lissu, mmoja wa wabunge wa upinzani asiye na woga wa kusema anachokiamini, alishambuliwa kwa risasi mchana wa Septemba 7 akiwa katika gari nje ya makazi yake mjini Dodoma akitokea bungeni.

Pamoja na washambuliaji kufyatua risasi zipatazo 32, Lissu alinusurika kifo na kupelekwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na baadaye alipelekwa Nairobi, Kenya kwa matibabu zaidi, safari ambayo iligubikwa na mabishano baina ya Chadema, uongozi wa Bunge na Serikali, iliyotaka ahamishiwe Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Chadema imekuwa ikihusisha shambulio hilo na tofauti za kisiasa na hivi karibuni ilisema pamoja na kuwa na imani na vyombo vya usalama, inataka wachunguzi kutoka nje kwa kuwa vyombo vya dola vimetuhumiwa.

Mkurugenzi wa itikadi na mambo ya nje wa Chadema, John Mrema alisema jana kuwa ikiwa Serikali haina hofu, iruhusu wachunguzi hao ili yapatikane majibu ya nani alihusika.

Mrema alisema hakuna haja ya kuzuia wachunguzi hao kwa kuwa wana uwezo wa ziada.

“Kwa nini Serikali haitaki wachunguzi huru? Ni kweli kwamba wakija watafanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi, lakini hii haibadili msimamo wetu, hawa wana vifaa na wanaweza kusaidia kupata majibu,” alisema Mrema.

Alisema tangu kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto alipotoa taarifa za awali za tukio hilo, hakuna taarifa nyingine zozote zilizopatikana, jambo ambalo alisema linaendelea kuwatia hofu.

Mrema alisema yapo mauaji mengi kama ya Kibiti ambayo wananchi hawajui matokeo ya uchunguzi wala hakuna waliofikishwa mahakamani.

Kiongozi huyo wa Chadema alisema hata suala la mauaji ya Kibiti halijatolewa taarifa wala watuhumiwa kufikishwa mahakamani, huku kada wa chama hicho, Ben Saanane akiwa hajulikani alipo na mauaji ya mwenyekiti wa Chadema mkoani Geita, Alphonce Mawazo yakiwa hayajatolewa ripoti.

Alisema wataalamu hao kutoka nje wapo tayari kuja kufanya kazi ya kuchunguza tukio hilo na kwamba kitendo cha kuwakataa kinaongeza shaka kwao.

“Tunakaribia mwezi hatujui chochote,” alisema Mrema.

“Kwa hiyo muafaka ni wachunguzi huru. Mtu hawezi kupigwa risasi mchana kweupe tena Dodoma Mjini...” alisema.

Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa alisema kuzuia wachunguzi hao kunawafanya wafikirie kuwa kuna watu ambao hawataki kuumbuka na kuongeza kuwa kama nia ipo, iwaruhusu.

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ????

$
0
0
Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA 
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA 
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI 
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI 
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK 

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO 

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM,NAUTALETEWA POPOTE ULIPO.

 SIMU; NO 0767145357/0629034550.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Mchungaji Msigwa afikishwa mahakamani kwa Matusi na Kutishia Kuua

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amepandishwa kizimbani leo Alhamisi katika Mahakama ya Mwanzo Mjini Iringa kwa madai ya kumtusi na kutishia kumuua aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kitwiru, Baraka Kimata.

Mbali na Msigwa pia Diwani wa Viti Maalum, Selestina Johanes na dereva wa mbunge huyo, Godi Mwaluka wamepandishwa kizimbani kwa kosa hilo.

Akisoma shtaka hilo Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo, Rehema Mayagilo amesema kuwa mbunge huyo na washtakiwa hao wawili wanashtakiwa kwa madai ya kumtusi na kutishia kumuua diwani huyo.

Hakimu Mayagilo amesema kuwa Msigwa na wenzake walitenda kosa hilo jana saa nane mchana katika viunga vya Ofisi za Halimashauri ya Manispaa ya Iringa.

Baada ya kusomewa shtaka hilo Msigwa na wenzake wamepata dhamana na kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktober 9 mwaka huu itakapotajwa tena.

NSSF Kuwaburuza Mahakamani Waahiri 126

$
0
0
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mkoa wa Arusha linatarajia kuwafikisha mahakamani waajiri 126 kwa kutowasilisha michango ya wafanyakazi wake kwa wakati.

Meneja wa NSSF Mkoa wa Arusha, Dk. Frank Maduga amesema  kuwa waajiri hao wameshindwa kuwasilisha michango hiyo kwa zaidi ya miezi sita ambayo ni zaidi ya Sh bilioni moja.

“Kati ya hao waajiri wakubwa ni 14, waajiri wa kati 69 na waajiri wadogo 53, ambapo wote walishapelekewa onyo la mwisho na taratibu za kuwafungulia mashitaka zimeshakamilika na wiki ijayo tunatarajia kuwafikisha mahakamani kwani kutokuwasilishwa kwa michango hiyo kumekuwa na madhara kwa wanachama na wategemezi wao."

Hata hivyo Dk. Maduga alikataa kutaja majina ya mashirika hayo ambapo amesema yatatajwa mahakamani wakati Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaandaa hati za mashtaka.

Pamoja na mambo mengine, meneja huyo amesema kwa sasa shirika hilo limeingia mkataba na hospitali inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ya Selian, ambapo wanawake wajawazito ambao ni wanachama watapatiwa matibabu bure na kuwa wanatarajia kuingia mkataba na hospitali nyingine zaidi.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Mbowe Kanyang'anywa Gari

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kimesikitishwa na hatua ya uongozi wa Bunge la Tanzania ya kulichukua gari la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (KUB), Freeman Mbowe alilokuwa akilitumika kwa shughuli za matibabu ya Tundu Lissu jijini Nairobi .

Chadema imesema Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai, aliamuru gari hilo lipelekwe Nairobi kwa ajili ya kusaidia matibabu ya Lissu ambaye ni mwanasheria mkuu wa chama hicho

Lissu ambaye pia Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), alishambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi Septemba 7 akiwa nyumbani kwake Area D mjini Dodoma na yuko Nairobi kwa matibabu.

Mkuu wa Idara ya Uenezi  Chadema, Hemed Ali  ameeleza hayo leo Alhamisi na kusema kwamba hawana wasiwasi na hatua hiyo kwa kuwa wana marafiki wengi wakiwamo Watanzania waishio nchini humo na Wakenya wenyewe ambao kwa namna moja au nyingine watashirikiana nao.

Akizungumzia suala hilo Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah amedai kuwa hana na taarifa hizo, ndiyo kwanza anazisikia kutoka kwa mwandishi na alimtaka mwandishi amuulize huyo aliyetoa taarifa kama kweli ametumwa na Mbowe.

“Naomba uumulize aliyesema taarifa hizi je ametumwa na Mbowe? Kwa sababu napata shida Mbowe ni kiongozi pale bungeni na ana wasaidizi wake na haya mambo ni ya ndani ndiyo maana nataka kujua huyu aliyetoa taarifa amezungumza kama nani? Alihoji Dk Kashililah.

“Haya mambo yana taratibu zake za kiofisi naomba niishie hapa. Maana tukiendelea nitakuuliza maswali ambayo utashindwa kuyajibu. Pia na utatakakujua mengi ikiwamo hata posho ya dereva wa Mbowe,” amesema.

Rais Magufuli Atpa Milioni 260 kwa Ajili ya Ujenzi wa Nyumba za Polisi Zilizoungua Moo

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amewasili eneo la nyumba za polisi zilizoteketekea kwa moto.Nyumba hizo zilizopo Kata ya Sekei ziliteketea kwa moto jana Jumatano usiku.

IGP Sirro amesema Rais John Magufuli ametoa Sh260 milioni kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za kuishi askari hao.

Amesema Jeshi la Polisi kupitia bajeti yake limetoa Sh40 milioni kwa ajili ya ujenzi huo.

IGP Sirro amesema jeshi hilo pia litatoa Sh1 milioni kwa kila familia iliyoathiriwa na moto huo. Katika nyumba zilizoteketea familia 14 zilikuwa zikiishi.

Kiongozi huyo wa Jeshi la Polisi amesema Rais Magufuli ameagiza Wakala wa Majengo (TBA) kutoa jengo la kuwahifadhi askari hao wakati ujenzi wa nyumba ukifanyika.

Amewataka wananchi wenye nia njema kuzisaidia kwa chochote walichonacho familia za waliounguliwa mali zao.

IGP Sirro na ujumbe wake ameelekea Tengeru kukagua jengo la TBA watakalotumia kwa muda askari hao.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 29

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images