Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Zungu: Bunge Halitatunga heria ya Kuzuia Mimba Shuleni, Hilo ni Jukumu la Wazazi

$
0
0
Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu amesema hakuna sheria itakayotungwa na chombo hicho itakayozuia mimba shuleni na kuwataka wazazi kuwajibika kutoa malezi bora kwa watoto wao ili wasipate ujauzito.

Zungu aliyasema hayo jana kwenye mahafali ya 15 ya kidato cha nne katika Sekondari ya Wasichana ya Barbro Johansson akimwakilisha Spika Job Ndugai.

Alisema jukumu la kudhibiti mimba halipaswi kutegemee sheria pekee na kwamba, wazazi wanawajibika kuhakikisha wanatoa malezi bora kwa kuwa baadhi ya tabia zao zinaendana na watoto wao.

“Ukiona mtoto ni mhuni ujue na mzazi wake ni mhuni, mtoto akiwa na nidhamu na mzazi wake ana nidhamu,” alisema Zungu na kuibua gumzo miongoni mwa wazazi waliofika shuleni hapo.

“Ni jukumu la wazazi kuwalea vizuri watoto wenu na kuhakikisha hawajiingizi katika makundi hatarishi.”

Zungu ambaye pia ni mbunge wa Ilala aliwataka wanafunzi kutojihusisha na masuala ya kisiasa shuleni, bali wajikite katika masomo kwa manufaa yao.

“Kilimo ni njia ya kujikwamua kiuchumi, lakini najua vijana wengi hampendi kilimo. Niwaambieni jishughulisheni na kilimo kama sehemu ya ajira,” aliwaambia wahitimu 116 watakaohitimu.

Mbunge wa Muleba Kusini, Anna Tibaijuka alisema ni lazima jamii ikubaliane na agizo la Rais John Magufuli la kuwataka wanafunzi wanaopata mimba kutoendelea na masomo.

Tibaijuka ambaye pia ni mwenyekiti mwanzilishi wa taasisi hiyo, alisema kuwaruhusu wanafunzi wanaopata mimba kuendelea na masomo ni kuongeza tatizo .

Mkuu wa shule hiyo, Halima Kamote alisema licha ya kuwa na wanafunzi wa kike zaidi ya 600, hakuna aliyepata mimba akiwa shuleni kutokana na malezi mazuri kwa kushirikiana na wazazi.

Nape Nnauye Anasema Wananchi Wake Wanahoji Hizo Ndege za Bombardier Zina Faida Gani Kwao Kijijini

$
0
0
Wananchi wa jimbo la Mtama mkoani Lindi wamemhoji mbunge wao, Nape Nnauye kuhusu ndege aina ya Bombardier, wakitaka kujua inawasaidiaje.

Ndege mbili aina ya Bombardier Dash 8 Q400 zilinunuliwa na Serikali kwa ajili ya kulifufua shirika la usafiri wa anga la Air Tanzania (ATCL), ambalo lilikuwa limezorota na kutishia uhai wake.

Ndege hizo zilizinduliwa na Rais John Magufuli Septemba 28, 2016 jijini Dar es Salaam.

Lakini wananchi wa Mtama bado hawajaona umuhimu wake na walimuhoji Nape, ambaye alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Jana Nape aliandika katika akaunti yake ya Twitter kuhusu utashi huo wa wananchi wake kuhusu Bombardier.

“Watu hawa wanapambana na hali zao! Waliniuliza bombardier ndiyo nini” na sie wa vijijini tutafaidikaje au ni kwenu mjini tu!?” ameandika Nape katika akaunti hiyo.

Alipoulizwa , Nape aliyewahi kuwa katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, alithibitisha kutuma ujumbe huo, akisema ni swali aliloulizwa na wanakijiji.

“Mimi sijui kwa nini mnauliza sana hicho kitu.Mimi nilikuwa jimboni kwangu nazungumza na wananchi kuhusu korosho, mwanakijiji mmoja akauliza kwamba hiyo Bombardier ina faida gani? Na mimi nimeripoti maneno yake. Si maneno yangu.

“Suala si mimi kuwa na cheo, mimi ni mbunge wa wananchi. Hilo swali hata wewe ukiliuliza hapo mtaani utapata majibu matano tofauti.

“Nilikuwa nazungumza na wanavijiji kuhusu fedha zinazotolewa na Serikali kuhusu korosho, mbaazi na mazao mengine, ndipo nikaulizwa na mimi nimeripoti kwa rafiki zangu nilivyoulizwa.”

Lindi na Mtwara ni kati ya mikoa iliyokuwa inafikika kwa shida kabla ya Serikali kujenga barabara zilizorahisisha usafiri. Pamoja na usafiri wa barabara, Air Tanzania imeanzisha usafiri wa anga kwa ajili ya kuhudumia wasafiri wengine kwenda na kutoka mikoa hiyo ambayo hivi sasa inachangamshwa na uwekezaji katika gesi na viwanda vya saruji.

Faida Nyingine Za Mti Mvunge Mbali Na Kurefusha, Kunenepesha Uume Na Kuongeza Ukubwa Wa Makalio.

$
0
0
 Watu  wengi  wanaufahamu  mti  wa  mvunge  kama  mti unaotumika  katika  tiba  ya  kurefusha  na  kunenepesha  maumbile  ya  kiume  pamoja  na kuongeza  ukubwa  wa  makalio  kwa  wanawake.

Hii  ni  kwa  sababu, mti  wa  mvunge  umekuwa  ukitumika  katika  tiba  ya  kurefusha  na  kunenepesha  maumbile  ya  kiume  pamoja  na  kuongeza  ukubwa  wa  makalio  tangu  enzi   za  mabibi  na  mababu.
 
Vile  vile, mti wa  mvunge  tayari umethibitishwa  kitaalamu  kuwa  na  uwezo  wa  kitabibu  katika  kurefusha  na  kunenepesha   maumbile  ya  kiume  pamoja  na  kuongeza  ukubwa  wa  makalio.
 
Taarifa  ya  kuthibitishwa  kwa  mti  wa mvunge, imeripotiwa  katika  gazeti  la  Mwananchi  la  tarehe  26, Januari  2013.
 

Hata  hivyo, mbali  na  kuwa na  uwezo wa  kurefusha  na  kunenepesha maumbile  ya  kiume  pamoja na kunenepesha makalio, mmea  wa  Mvunge unazo faida  nyingine  lukuki  kwa afya  ya  mwanadamu.
 
Baadhi  ya  faida hizo  ni kama  ifuatavyo ;

FAIDA   NYINGINEZO   ZA   KITABIBU ZA   MTI  WA  MVUNGE

1.    Mti  wa  mvunge  una  uwezo wa  kutibu majeraha ya vidonda
2.   Mti wa  mvunge  hutibu  vidonda  visivyo pona ‘ Vidonda  Ndugu ‘
3.   Mti  wa  mvunge  hutumika  kutibu  vidonda  vya  tumbo
4.   Majani  ya  mti  wa  mvunge  hutumika  kutibu  magonjwa mbalimbali ya  zinaa  kama  vile  kaswende  na  kisonono.
5.   Unga  wa  tunda  la  mvunge hutumika  katika  tiba  dhidi ya magonjwa  mbalimbali  ya  ngozi.
6.   Unga wa  tunda  la  mvunge  hutumika  kutibu chunusi za  usoni  na  mwilini
7.   Mti wa  mvunge  hutumika katika  kutibu bacteria  na  maambukizi  ya  bacteria
8.   Mti  wa  mvunge  hutumika kuongeza  ukubwa wa  matiti na kuyasimamisha
9.   Mti  wa  mvunge  unatumika  kutibu  ukurutu
10.   Mti  wa  mvunge  ni  tiba  nzuri  sana  dhidi ya majipu au  upele  wenye  kutoa  usaha.
11.  Mti  wa  mvunge  unatumika  kutibu maumivu ya  chini  ya  mgongo
12.   Mti  wa  mvunge  hutibu  maradhi  ya  maumivu  kwenye  magoti
13.  Mti wa  mvunge  ni  tiba  nzuri  sana  ya  tatizo la  baridi yabisi.
14.  Mti  wa mvunge  unasaidia  kutibu  maumivu ya  tumbo
15.  Mti  wa  mvunge  husaidia kutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo la maumivu  ya  kwenye  meno.
16.  Mti  wa  mvunge  hutumika  katika  tiba  dhidi ya  Homa  ya  mapafu
17.  Mti  wa  mvunge  husaidia  kutibu  tatizo  la  kukosa  choo
18.  Mti  wa  mvunge  husaidia kuupa  mwili  nguvu na  joto
19.  Mti  wa  Mvunge  hutumika  kutibu  bawaziri
20.  Mti  wa  Mvunge  hutumika  kuondosha  minyoo  wa  tumboni
21.  Mvunge  unapochemshwa  kitaalamu  kwa  pamoja  na  asali  mbichi  ya  nyuki wadogo, husaidia  sana  kuondoa  lehemu( Cholestrol ) isiyo  hitajika  mwilini.
22.  Mti  wa  Mvunge  husaidia  kuongeza  maziwa  kwa  mama  anaye nyonyesha

Tunachukua   fursa hii kuonya kuwa wasomaji wasijiamini sana katika kutengeneza dawa na kuzitumia mara baada ya kusoma makala haya. 

Unashauriwa upate ushauri wa kutosha kutoka  kwetu  au kwa  wataalam waliobobea katika tiba asili
zinazohusu mti  huu  wa  mvunge.

Na  kwa  mahitaji  ya  bidhaa  mbalimbali  zitokanazo  na  mti   wa  Mvunge  kwa  ajili  ya  matumizi  mbalimbali  ya  kitabibu, fika  katika  duka  la  NEEMA  HERBALIST.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM, karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING, nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

Kwa  wateja  waliopo  nje  ya  Dar  Es  Salaam, tunawatumia bidhaa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  mabus  mbalimbali.

WASILIANA NASI KWA  SIMU  NAMBA  0766  53 83 84.

Na  kwa taarifa  zaidi kuhusu huduma zetu, tutembelee kupitia :

Nyalandu Alivyojitoa Muhanga Sakata la Tundu Lissu

$
0
0
Mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu amesema kitendo cha Tundu Lissu kusalimika kifo kwenye tukio la kupigwa risasi ni Mungu tu ndiye aliandika, lakini kinamuumiza zaidi huku akilaumu ameikosea nini nchi mpaka kufanyiwa hivyo.

Kupigwa risasi kwa Lissu, ambaye alikuwa Dodoma kutekeleza majukumu yake ya kibunge, kuliwaibua wabunge walioliomba Bunge kuunda timu ya kwenda jijini Nairobi kumjulia hali mwenzao, lakini kiti cha spika kilikataa hoja hiyo kwa maelezo kuwa tayari baadhi yao walishaenda kuwawakilisha.

Wabunge ambao wakati huo walikuwa Nairobi ni Freeman Mbowe, ambaye ni mwenyekiti wa Chadema na mbunge wa Hai, na Mchjungaji Peter Msigwa, ambaye ni mbunge wa Iringa Mjini wa chama hicho.

Wakati wabunge wakilalamika kukosa ruhusa ya Bunge, kulikuwa na malumbano kuhusu ushiriki duni wa Serikali na Bunge katika kumuuguza Lissu aliyepigwa risasi katika kipindi ambacho alishatoa malalamiko kuwa kulikuwa na watu asiowafahamu waliokuwa wanamfuatilia.

Lakini, Nyalandu alijitokeza na kwenda Nairobi kumuona Lissu, akiandika katika akaunti zake za mitandao ya kijamii kuhusu safari hiyo na maendeeleo ya ziara yake, huku akituma picha zinazomuonyesha akiwa hospitalini.

Mbali na kumjulia hali na kuhimiza wananchi wamuombee, harakati za Nyalandu zimekuwa zikiambatana na ujumbe unaonekana kuwa na utata, ambao umemfanya atafsiriwe tofauti, akihimiza wananchi upendo, amani, kuvumiliana na haki kushinda dhuluma.

Pia, Nyalandu, ambaye amekuwa mbunge tangu mwaka 2000, amelielezea tukio la kushambuliwa kwa Lissu kuwa ni kurudi nyuma kidemokrasia huku akiwaita waliomshambulia kuwa ni waonevu na kutaka Serikali ifanye jitihada kuwasaka na kuwafikisha mbele ya vyombo vya haki.

“Sote tuungane katika kufanya maombi maalumu kwa ajili ya #TunduLissu, na kwa wale walio karibu na mji wa Mbeya, naomba muungane nami katika Kanisa la Ebenezer,” ameandika Nyalandu katika ukurasa wake wa Instagram.

Katika video aliyotuma kwenye ukurasa huo, Nyalandu anasema: “Nimekuja Mbeya kulikumbusha Taifa kuwa kupigwa kwa mmoja wetu ni kupigwa kwetu sote, kuumizwa kwake ni kuumizwa kwetu sote, na kudhulumiwa kwake huyo mmoja ni dhuluma dhidi ya kila Mtanzania.

“Tundu Lissu amepona kwa kuwa imeandikwa (katiba Biblia) ‘hatasinzia yeye akulindaye’, na kwetu kama Taifa, tukasimama naye wakati huu wa kujaribiwa kwake. Naamini ndani ya moyo wake akiwa katika maumivu lukuki aliyonayo, #TunduLissu atakuwa anajiuliza nimekukosea nini Taifa.”

Wakati katika baadhi ya maeneo, watu walizuiwa kukusanyika kufanya maombi kwa ajili ya mwanasiasa huyo, Nyalandu anahimiza katika ujumbe wake kuwa Lissu aombewe “kimya, na tumwombee kwa sauti, tuombe mahali pa sirini, na tuombe hadharani”, akisema kuwa wameagizwa “kulia na wanaolia, kwenda kuwaona wagonjwa na waliofungwa, na tuwatangazie kufunguliwa kwao”.

“Naaam, hii ndiyo siasa sahihi ya utu kabla ya itikadi, upendo kabla ya visasi; heshima kabla ya husuda,” anasema Nyalandu.

“Watanzania wote tusimame, miguu yetu ikatiwe utayari, roho ya mapenzi na ujasiri ikatamalaki na kuondoa roho ya hofu na ganzi (spirit of indifference), tukaipandishe tena bendera yetu pale kileleni Kilimanjaro.

“Yamkini kwamba haki iishinde dhuluma; umoja wetu, ushinde roho ya matengano; na sauti za walioteswa na kuonewa zisikike na kuleta tena tumaini jipya la amani, haki, upendo, na mshikamano.”
Nimekuja MBEYA kulikumbusha TAIFA kuwa KUPIGWA kwa mmoja wetu ni kupigwa kwetu SOTE, kuumizwa kwake ni KUUMIZWA kwetu sote, na KUDHULUMIWA kwake huyo mmoja ni dhuluma dhidi ya kila Mtanzania. #TunduLissu amepona kwa kuwa imeandikwa, 'hatasinzia yeye akulindaye', na kwetu kama TAIFA, tukasimame naye wakati huu wa KUJARIBIWA kwake. Naamini, ndani ya moyo wake akiwa katika maumivu lukuki aliyonayo, #TunduLissu atakuwa anajiuliza nimekukosea nini TAIFA. Sasa basi, TUKAOMBE kwa ajili yake, tumwombee kimya kimya, na tumwombee kwa sauti, tuombe mahali pa sirini, na tuombe hadharani. Kwa kuwa Katika ukiri wa imani yetu, tumeagizwa kulia na wanaolia, kwenda kuwaona wagonjwa na waliofungwa, na tuwatangazie kufunguliwa kwao. #TunduLissu tumtangazie KUPONA na KUFUNGULIWA KWAKE katika jina la YESU KRISTO wa Nazareth. Naam, hii ndiyo DINI iliyobora, na hii ndiyo SIASA sahihi ya utu kabla ya itikadi, upendo badala ya visasi, heshima badala ya husuda. Tunaomba IKAWE heri kwake, na kwamba maadui zake wakawe maadui wa MUNGU, na akawatendee alivyoahidi katika maandiko aliposema 'KISASI ni juu yangu, asema Bwana'. Watanzania WOTE tusimame, miguu yetu ikatiwe utayari, roho ya mapenzi na ujasiri ikatamalaki na kuondoa roho ya hofu na ganzi (spirit of indifference), tukaipandishe tena bendera ya yetu pale kileleni Kilimanjaro, yamukini kwamba HAKI iishinde DHULUMA, UMOJA wetu ushinde roho ya matengano, na sauti za walioteswa na kuonewa zisikike na kuleta tena tumaini jipya la amani, haki, upendo, na mshikamano. Amen.
A post shared by LazaroNyalandu (@lazaronyalandu) on

Korea Kaskazini yadai Marekani imetangaza vita......Yaapa Kutungua Ndege za Marekani Hata Nje ya Anga Lake

$
0
0
Waziri wa mambo ya nje wa Korea Kaskazini amedai kwamba rais wa Marekani Donald Trump ametangaza vita dhidi ya taifa hilo.

Ri Yong-ho aliwaambia waandishi wa habari kuwa Korea Kaskazini ina haki ya kudungua ndege za vita za Marekani  hata zile ambazo hazipo katika Anga ya Korea Kaskazini.

"Dunia ni lazima ikumbuke kuwa Marekani ndiyo ilikuwa ya kwanza kutangaza vita,"  Anasema  Bwana Ri alisema.

Pande hizo mbili zimekuwa zikitupiana maneno makali. Licha ya majuma kadhaa ya misukusuko, wataalamu wanasema kuwa hakuna uwezekano wa makabiliano ya moja kwa moja kati ya Marekani na Korea Kaskazini.

Baada ya Bw Ri kuhutubia Umoja wa Mataifa siku ya Jumamosi, Rais Trump alijibu kupitia mtandao wa twitter, akisema kuwa Bw. Ri na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un hawatakuwepo kwa muda ikiwa wataendelea na maneno yao.

Jibu la Bwana Ri lilikuja wakati akiondoka New York baada mkutano wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa.

Korea Kaskazini imeendelea na majaribioya makombora ya nyuklia na ya masafa marefu siku za hivi karibuni licha ya vikwazo vya Umoja wa Mataifa.

Viongozi wa nchi hiyo wanasema kuwa uwezo wake wa zana za nyulia ndiyo njia pekee dhidi ya mataifa yanayotishia kuiharibu.

Baada ya jaribio la hivi majuzi na kubwa zaidi la nyulia mapema mwiezi huu, baraza la usalama la Umoja wa Mataifa, liliidhinisha vikwazo vipya dhidi ya nchi hiyo.

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ????

$
0
0
Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA 
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA 
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI 
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI 
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK 

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO 

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM,NAUTALETEWA POPOTE ULIPO.

 SIMU; NO 0767145357/0629034550.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Mwigulu Nchemba Akataa Wazungu Kuja Kuchunguza Sakata la Tundu Lissu

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amesema hakuna haja ya kuanza kuhangaika kutafuta wachunguzi kutoka nje kwa ajili ya kufuatilia wahusika wa shambulizi la Mbunge wa Singida Mashariki(Chadema), Tundu Lissu kwa vile vyombo vya ulinzi na usalama nchini vinajitosheleza na vina weledi na kazi hiyo.

Waziri huyo amesema haoni kwa nini baadhi ya watu wanasisitiza kuletwa kwa wataalamu wa nje kwani hata kama wataletwa bado watalazimika kufanya kazi kwa mazingira ya Kitanzania wakitumia wataalamu waliopo na hata ikiwekezana watahukumiwa kwa kutumia sheria za nchini.

“Nchi yetu inajitegemea hakuna haja ya kuleta vyombo vya nje kufanya uchunguzi...upelelezi utafanywa na vyombo vyetu, watafikishwa katika vyombo vya muhumu na watahukumiwa na watoto wetu,” alisema.

Hivi karibuni Chadema ilitaka wachunguzi nje kuendesha upelelezi kuhusiana na tukio la kushambuliwa kwa Lissu ikidai kuwa hatua yake hiyo haimaanishi kuwa vyombo vya ulinzi na usalama havina uwezo bali vimetuhumiwa katika tukio hilo.

Hata hivyo, Waziri Nchemba alisisitiza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama daima viko macho na vinaendelea na kazi ya kuwasaka wale wote wanaojihusisha na matukio ya kushambulia watu.

Amesema suala la uchunguzi haliwezi kukamilika kwa siku moja akitolea mfano jinsi Marekani ilivyotumia muda mwingi kumsaka mtuhumiwa wa ugaidi, Osama bin Laden aliyekuwa kiongozi wa kundi la Al Qaida.

“Uchunguzi hauna ukomo...unaisha pale tu wanapokamatwa wahusika wote lakini vinginevyo uchunguzi hauishi maana hata Marekani walimtafuta Osama kwa muda mrefu sana hawakusema sasa tumesitisha kumsaka,” amesema.

Kiongozi huyo wa Al Qaida aliuawa Mei 2, 2011 na vikosi vya Marekani vilivyoendesha operesheni maalumu iliyoratibiwa kutoka Pentagon na kufuatiliwa kwa karibu na Rais Barack Obama ambaye hivi sasa amestaafu.

Osama alikuwa amejichimbia katika maficho yake nchini Pakistan katika eneo lililojulikana Abbottabad.

Waziri Nchemba aliwatumia salamu wale wanaojulikana kama ‘watu wasiojulikana’ akisema kasumba ya wahalifu wachache kufanya mauaji na kisha kujinadi kwa jina la watu wasiojulikana inaelekea ukingoni.

Ameeleza kuwa dakika za wale wanaojihusisha na uhalifu huo kufikishwa kwenye mkono wa sheria zinahesabika

Inspekta Ambaye ni Daktari Gereza la Keko aeleza jinsi Manji alivyoumwa gerezani

$
0
0
Daktari Mfawidhi wa Gereza la Keko, Inspekta Eliud Mwakawanga ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jinsi maisha ya mfanyabiashara Yusufu Manji yalivyokuwa gerezani kwamba alikuwa akitumia vidonge kati ya 25 mpaka 30 kwa siku.
 
Ameeleza kuwa walikuwa wakipatia dawa hizo alipokuwa akisikia aumivu hasa ya mgongo na kwamba kuna kipindi alikuwa anaamka akiwa na hali ya kutetemeka au kuchanganyikiwa.
 
Pia ameeleza kuna wakati Manji alikuwa anaamka anashindwa hata kutembea na wakati mwingine alikuwa akitumia mkanda kufunga mgongo.
 
Shahidi huyo wa sita wa upande wa mashtaka ametoa ushahidi huo leo Jumanne katika kesi ya  kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin inayomkabili Manji.
 
Ameeleza kuwa Julai 6, 2017 walimpokea Manji akitokea Hospitali ya Muhimbili Kitengo cha Moyo cha JKCI ambapo waliambiwa ni mshtakiwa lakini ni mgonjwa.
 
“Nilienda kumuona, tukazungumza naye na tulikaa naye gerezani hadi alipokuja kuachiwa,”
 
"Tangu nimempokea hali yake kiafya haikuwa nzuri na alikuwa mtu anayetumia dawa wakati wote na alikuja na dawa zake za aina sita kutoka Muhimbili ambazo alikuwa akizitumia, pia kulingana na hali yake na mazingira anayokuwa anajisikia, tulikuwa tukimpatia dawa gerezani mbali na hizo."
 
Ameeleza kuwa utaratibu wa kuwapatia dawa mahabusu na wafungwa huwa wanakaa nazo wao wataalam na wanawapa kutokana na maelezo ya daktari yaliyopo kwenye cheti ambapo Manji kuna dawa alikuwa anakunywa asubuhi na jioni na nyingine kulingana na hali yake ya siku hiyo.
 
Shahidi huyo ameeleza kuwa wao huwa hawatoi dawa za kulevya kwa mgonjwa ila wanatoa dawa.
 
Alisema hivyo baada ya kuulizwa na Wakili Hajra Mungula kuwa dawa walizompatia Manji zinahusiana vipi na dawa za kulevya.
 
"Sijachunguza sana kuona zina uhusiano gani na dawa za kulevya,” ameeleza na kusisitiza wao hawatoi dawa za kulevya kwa mgonjwa wanatoa dawa.

Polisi watumia mabomu ya machozi kuwatawanya Wafuasi wa Raila Odinga na Uhuru Kenyatta

$
0
0
Polisi wamelazimika kuwatawanya kwa mabomu ya machozi wafuasi wa vyama vya Jubilee na muungano wa upinzani wa Nasa baada ya kuzua vurugu katika ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC) zilizoko jengo la Anniversary Towers.

Wafuasi wa Nasa waliokuwa wakiimba nyimbo “Chiloba lazima ang’oke” walikabiliwa na wafuasi wa Jubilee waliokuwa wakiimba “Tunataka amani”. Makundi yote mawili yalitimua mbio baada ya polisi wa kuzuia ghasia kuwarushia mabomu ya kutoa machozi.

Huku wakikohoa na wakitafuta mahali salama, wote walikimbia kukwepa kukamatwa.

Maandamano hayo yamefanyika kuitikia wito uliotolewa jana na kiongozi mkuu wa Nasa Raila Odinga kwamba wafuasi wake wajitokeze kwa wingi kuandamana hadi kwenye makao makuu ya IEBC lengo likiwa kumtoa kwa nguvu Ofisa Mtendaji Mkuu wa IEBC Ezra Chiloba kwa madai ya kuhusika kuvuruga uchaguzi mkuu uliofanyika Agosti 8.

Maandamano hayo yanafanyika siku chache baada ya Mahakama ya Juu kufuta ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta.

Katika mji wa Kisumu, ambao unatajwa kuwa moja ya ngome za Nasa baadhi ya wakazi waliandamana hadi ofisi za IEBC na baada ya kufika walitoa wito maofisa wa ngazi za juu akiwemo Ezra Chiloba wajiuzulu.

Walimshutumu Chiloba na kikundi chake kwa kufanya njama za kuingilia mchakato wa uchaguzi mkuu ambao matokeo yaliyompa ushindi Uhuru Kenyatta yalifutwa na Mahakama ya Juu.

Waandamanao waliokuwa wamebeba matawi ya miti, mabango huku wakipiga yowe na honi za pikipiki walianzia barabara ya Obote wakaenda mtaa wa Oginga Odinga kabla ya kuchukua Barabara Kuu ya Kenyatta na baadaye Mtaa wa Ang’awa katikati ya jiji.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Hukumu ya Yuuf Manji Kutolewa Octoba 6

$
0
0
Mahakama ya Hakimu ya Mkazi Kisutu, imepanga Oktoba 6, mwaka huu kutoa  hukumu katika kesi ya dawa za kulevya inayomkabili Yusuf Manji(41).

Uamuzi huo umetolewa leo na Hakimu Mkazi Mfawidhi , Cyprian Mkeha, baada ya wakili wa utetezi Hajra Mungula kusema kuwa ameshafunga ushahidi wa mashahidi saba.

Mashahidi watatu wa upande wa mashtaka wametoa ushahidi wao dhidi ya mshtakiwa Daktari Mfawidhi wa Gereza la Keko, Inspekta Eliud Mwakawanga ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jinsi maisha ya mfanyabiashara Yusufu Manji yalivyo kuwa gerezani kwamba alikuwa akitumia vidonge kati ya 25 mpaka 30 kwasiku.

Ameeleza kwamba  walikuwa wakimpatia dawa hizo alipokuwa akisikia maumivu hasa ya mgongo na kwamba kuna kipindi alikuwa anaamka akiwa na hali ya kutetemeka au kuchanganyikiwa.

Ameeleza kuwa Julai 6, 2017 walimpokea Manjia kitokea Hospitali ya Muhimbili Kitengo cha Moyo cha JKCI ambapo waliambiwa ni mshtakiwa lakini ni mgonjwa.

“Nilienda kumuona, tukazungumza naye na tulikaa naye gerezani hadi alipokuja kuachiwa,”

Maalim Seif Amtembelea Tundu Lissu Nairobi Kenya

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Mhe. Seif Sharif Hamad leo Septemba 26, 2017 ameingia jijini Nairobi Kenya kwenda kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu ambaye alipigwa risasi.

Mwenyekiti wa kamati ya muda ya uongozi CUF, Julius Mtatiro amethibitisha hilo na kusema kuwa kiongozi huyo na baadhi ya viongozi wa CUF wamewasili nchini Kenya kwa ajili ya kwenda kumuona Tundu Lissu.

"Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Mhe. Seif Sharif Hamad ameingia jijini Nairobi kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika Mhe. Tundu Antipas Lisu (leo) ambaye amelazwa Hospitali ya Nairobi" alisema Julius Mtatiro

Mhe. Shariff Hamad ameongozana na Mhe. Juma Duni Haji Nairobi kumjulia hali, Mhe Tundu Lissu.

Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 mjini Dodoma na kisha baadaye kupelekwa nchini Kenya kwa matibabu zaidi.

Uganda Nako Hali si Shwari.....Kiongozi wa Upiinzani Naye Kakamatwa kwa Kuhamasiha Wananchi Kupinga Kufutwa kwa Ukomo wa Rais

$
0
0
Kiongozi mkuu wa chama cha Former Forum for Democratic Change (FDC) Dk Kizza Besigye amekamatwa leo saa moja kabla ya Bunge kuanza kujadili pendekezo la kuondoa ukomo wa umri wa rais.

Besigye, aliyewahi kugombea urais mara nne na akishindwa kwa Rais Yoweri Museveni alikamatwa mjini hapa alipokwenda kuwahamasisha wafuasi wake kupinga kufutwa Ibara ya 102 (b) kwenye Katiba iliyoweka ukomo wa kugombea urais kuwa miaka 75.

Besigye alikataa kushuka kutoka kwenye gari lake hali iliyowalazimisha maofisa wa Kituo Kikuu cha Polisi cha Kampala (DPC) wakiongozwa na Joseph Bakaleke kulivuta gari lake hadi kituoni hapo.

Vilevile Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Fred Mukasa Mbidde alikamatwa kuhusiana na suala hilo hilo. Zilikuwepo taarifa za kukamatwa vijana wengi katika maeneo mbalimbali yalikofanyika maandamano ya kupinga pendekezo hilo. Maeneo mengine yalikofanyika maandamano ni Mbale, Arua, Mbarara, Masaka na Pader

Katika hatua nyingine, maofisa polisi walisambazwa katika maeneo mengi muhimu katika jiji la Kampala ulinzi unaohusiana na pendekezo la kufutwa Ibara ya 102 (b) ya Katiba likilenga kuondoa ukomo wa umri wa rais.

Makao makuu ya ofisi za chama cha FDC yalizingirwa na polisi wa kawaida, wa kuzuia ghasia na wa kupambana na ugaidi. Ofisi hizo zilizopo Najjanankumbi katika barabara ya Kampala-Entebbe zimezungukwa na polisi wenye silaha.

Msemaji wa Polisi Asan Kasingye alisema juzi kwamba maofisa hao wamesambazwa kwa ajili ya kukabiliana na kitisho cha aina yoyote. Kadhalika maeneo mengi nyeti, eneo lililojaa shughuli za kibiashara na Bunge yote yanalindwa.

Polisi wa kijeshi pia wamesambazwa maeneo ya Constitution Square ambako wameweka mahema sawa na bungeni, eneo muhimu kwa ajili ya mjadala uliotarajiwa kuwasilishwa jana kuhusu kuondolewa ukomo wa umri.

Kusambazwa kwa wingi kwa askari hao kumefanyika katikati ya kampeni zinazofanywa na za vikundi vya kisiasa na sasi za kiraia kupinga marekebisho ya katiba yanayolenga kufuta ukomo wa umri wa rais wa miaka 75. Hoja ya marekebisho hayo ilitarajiwa kuwasilishwa jana baada ya kushindikana Alhamisi iliyopita.

Mjadala ni mkali ndani ya bunge na chama tawala cha NRM wakiwemo baadhi ya wenyeviti wa majimbo ambao wamepinga pendekezo la kufuta Ibara ya 102 (b) ya Katiba wakisema ni jaribio la kupindua sheria mama.

Baraza la Viongozi wa Dini nchini limeongeza uzito kwa kutoa wito kwa serikali kuruhusu hoja ya ukomo wa umri wa rais iamuliwe na wananchi wote kwa kupiga Kura ya Maoni.

Baraza hilo linalojumuisha wakuu saba wa madhehebu makubwa ya dini nchini limesema katika taarifa yao ya pamoja wiki iliyopita kwamba watu waruhusiwe kuamua hatima yao.

“Mjadala kuhusu kuondolewa kwa ukomo wa umri wa rais si suala la upande mmoja ambalo linahodhiwa na wanasiasa na au wabunge...wananchi wana maoni tofauti kuhusu sauala hilo, hivyo kuna haja ya kusikiliza kwa utulivu pande zote bila ya kuegemea upande mmoja na kuutisha mwingine.

Hivi karibuni wabunge wa chama tawala cha National Resistance Movement (NRM) na wa kujitegemea walipitisha uamuzi wa kuondolewa ukomo wa umri wa miaka 75 uliowekwa katika Katiba.

Ikiwa marekebisho hayo yatapitishwa bungeni, itakuwa na maana kwamba Rais Museveni mwenye umri wa miaka 73 sasa ataweza kugombea uchaguzi ujao mwaka 2021 akiwa na umri wa miaka 77. Mwaka 2005, katiba ilifanyiwa marekebisho ukaondolewa ukomo wa mihula miwili ya miaka mitano kila mmoja

Mambosasa afunguka maiti kuokotwa baharini....Ataka Uthibitisho ili Atoe Ufafanuzi

$
0
0
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amesema hajapelekewa uthibitisho kuhusiana na maiti za wanaume watatu waliokutwa pembezoni mwa Bahari ya Hindi eneo la Coco Beach.

Amesema kwamba iwapo atapelekewa udhibitisho huo ni lazima atatolea ufafanuzi suala hilo kiundani zaidi.

Maiti za watu hao zilikutwa juzi Septemba 24 ambapo mbili zilifungwa kwenye viroba huku nyingine zikiwa ikiwa imekutwa na jiwe kubwa lililofungwa na kamba.

“Sijaletewa ‘fact’ nikiletewa nitalitolea ufafanuzi,”amesema Mambosasa.

Wafanyabiashara wa mihogo wa eneo hilo wamesema  wakiwa kwenye biashara zao asubuhi ghafla waliona maiti moja ikielea karibu na miti aina ya mikoko ikiwa na jiwe lililofungwa kifuani huku mikono yake ikifungwa na kamba.

Mmoja wa wafanyabiashara, Aziza Ally amesema baada ya kuona maiti hiyo walitoa taarifa polisi ambapo walifika saa 4 asubuhi na kuichukua kwenye gari lao.

 Amesema ilipofika saa 8 mchana waliona maiti mbili kila moja ikiwa kwenye kiroba zikielea ndipo mmoja wao alipoamua kutoa  taarifa polisi baadaye zikachukuliwa.

"Polisi walipokuja kuchukua hizi maiti hakuna hata mtu mmoja aliyeruhusiwa kusogelea na kupiga picha tulishangaa sana kuona  ulinzi mkali tofauti na siku zote na aliyebainika amepiga alipokonywa simu yake," amesema Ally.

Mfanyabiashara mwingine Issa Isaya amesema cha kushangaza maiti zinazookotwa ni za kiume pekee.

Amesema  wanaishi kwa wasiwasi kwasababu  kila wiki wanakuta maiti zikiwa zinaelea kwenye maeneo hayo.

Basi La Tashriff Lililokuwa Likitoka Tanga kwenda Dar Laungua Kwa Moto

$
0
0
Abiria waliokuwa wakisafiri kutoka Tanga kuelekea Jijini Dar es salaam wamenusurika kufa baada ya basi walilokuwa wamepanda la  kampuni ya Tashriff kuteketea kwa moto.

Kwa mujibu habari ambazo zimepatikana na kuthibitishwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Tanga,Benedict Wakulyamba zimedai kwamba ajali hiyo imetokea saa nane machana katika eneo la Pongwe nje kidogo ya jiji la Tanga.

Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema wameona moshi ukitoka chini ya basi hilo ndipo wakapiga kelele na kusababisha dereva kusimama dakika chache baada ya hapo likaanza kuwaka moto.

"Tumesikia kelele kutoka kwa watu waliokuwa nje tukaona dereva kasimamisha basi muda si mrefu moshi ulianza kutoka mara moto ukalipuka"amesema Bahati Mussa abiria wa basi hilo.

Kamanda Wakulyamba amesema basi hilo ambalo lilikuwa likiendeshwa na Hemed Ali (35) lilikuwa na abiria 29 ambapo hakuna aliyejeruhiwa wala kupoteza maisha.

"Hakuna aliyejeuhiwa wala kupoteza maisha imeteketea kwa moto"amesema Wakulyamba na kusisitiza kwamba jeshi la polisi linafanya uchunguzi kujua chanzo cha moto huo

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Septemba 27

Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR;Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

Ndugu 6 wa Familia Moja Wahukumiwa Kunyongwa Hadi Kufa

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga mkoani Rukwa imewahukumu adhabu ya kifo watu sita ambao ni ndugu wakazi wa Kalambo baada ya kupatikana hatia ya kumuua ndugu yao.

Ndugu hao wamedaiwa kwamba walifikia uamuzi wa kumuua ndugu yao huyo kwa madai ya kwamba anajihusisha vitendo vya kishirikiana.

Hukumu hiyo imetolewa jana Jumanne na Jaji Mahakama hiyo, Dk Adam Mambi baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashitaka uliopeleka mashahidi sita ili kuthibitisha mashitaka hayo.

Waliokutwa na hatia katika shauri hilo ni Ferdinand Kamande, Peter Mpandisharo, Edes Kamande, Stephen Sikanda, Henrick Nguvumali na Anatory Kamande huku Alistid Kamande na Will broad Kamande wakiachiwa huru kwa kutokutwa na hatia.

Katika shauri hilo upande wa mashitaka uliongozwa na mawakili wa serikali ambao ni Scolastica Lugongo na Adolf Lema huku upande wa utetezi ukiwakilishwa na wakili Mathias Budodi, ambapo ilidaiwa kwamba washitakiwa walitenda kosa hilo Septemba 27, mwaka 2014.

Ilielezwa mahakamani hapo kuwa siku ya tukio nyakati za usiku washitakiwa wakiwa na silaha za jadi kama vile mapanga, nondo, mawe, majembe walivamia nyumba ya Kamande na kugonga dirisha kisha kuvunja mlango ambapo Kamande alikimbia kuelekea kusikojulikana.

Ilielezwa kwamba baada ya hapo waliichoma moto nyumba hiyo na kuteketeza kila kitu kilichokuwemo ndani kisha kuondoka zao.

Wakati nyumba hiyo ikiteketea kwa moto Kamande aliyekuwa amekimbia ili kunusuru maisha yake, alikamatwa na watu hao na kuanza kupigwa huku wakimtuhumu kuwa ni mchawi na baada ya kumpiga sehemu mbalimbali za mwili wake walimchoma moto na kufariki papo hapo.

Ilidaiwa kwamba  washitakiwa hao walikamatwa na polisi Oktoba 10, 2014 na baada ya kuhojiwa na polisi walikana shitaka hilo.

Awali kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mawakili wa Serikali waliiomba mahakama kutoa adhabu kali iwe fundisho kwani watu wamekuwa wakichukulia sheria mkononi na kuua watu kinyume cha sheria wakiwatuhumu kuwa ni washirikina.

Akitoa adhabu hiyo Jaji wa Mahakama hiyo, Dk Mambi amesema ameridhishwa ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashitaka hivyo kwa kutumia Kifungu cha Sheria ya Makosa ya Jinai Namba 196 Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo 2002 anawahukumu watu hao sita kifo kwa kunyongwa.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images