Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Rais Museveni aagiza uchunguzi Ufanyike Kubaini chanzo cha ajali iliyoua Watanzania 13

0
0
Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema upelelezi kubaini sababu za ajali iliyosababisha vifo vya Watanzania 13 waliokuwa wakitoka harusini nchini humo unaendelea.

Waziri wa Ofisi ya Rais anayeshughulikia Jiji la Kampala, Bety Kamya akisoma salamu za rambirambi kutoka kwa Rais Museveni amesema licha ya kutoa pole kwa familia, kiongozi huyo ameagiza uchunguzi wa sababu za ajali ufanyike.

Amesema pia amewapongeza maharusi, Dk Aneth na Dk Trease Ibingira na amewatakiwa maisha mema ya ndoa.

Mbali ya hilo, amesema anawaombea ili kukabiliana na kipindi kigumu walichonacho.

Amesema Rais anawashukuru Watanzania kwa kuwa wavumilivu katika kipindi kigumu cha kupoteza wapendwa wao.

"Nakabidhi vyeti hivi vya vifo vya ndugu zetu 13 nawapa pole sana," amesema Waziri Kamya akimkabidhi vyeti hivyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki.

Waziri Kairuki amesema Rais John Magufuli amepokea taarifa ya vifo hivyo kwa mshtuko na alitoa maelekezo ya kupokewa miili hiyo, kuhifadhiwa kwenye Hospitali ya Jeshi Lugalo, kuagiwa hapo na kusafirishwa kwa maziko.

Amesema maagizo hayo wanaendelea kuyatekeleza ikiwa ni pamoja na kutoa magari kwa ajili ya kusafirisha miili hiyo.

Waziri Kairuki amesema kwa namna isiyo katika wakati wa kawaida, anawapongeza maharusi na kuwatakia maisha mema.

"Haya ni mapenzi ya Mungu, hili lisiwanyong'onyeshe maharusi," amesema Kairuki.

Ameishukuru Serikali ya Uganda kwa kukodi ndege kuirudisha nyumbani miili hiyo.

Rais Magufuli aagiza ukuta mkubwa kujengwa migodi ya Tanzanite

0
0
Rais John Magufuli ameagiza kujengwa uzio katika eneo linalozunguka machimbo ya Tanzanite liliko Simanjiro ikiwa ni hatua yake ya kutaka kukabiliana na utoroshwaji wa rasilimali hiyo.

Amelisisitiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuanza kazi hiyo haraka iwezekanavyo.

Rais Magufuli ambaye yuko ziarani mkoani Manyara amesema vikosi vya ulinzi na usalama vinapaswa kushirikiana kujenga ukuta huo ambao utaanzia eneo la block A hadi D la machimbo hayo.

Baada ya ujenzi huo kukamilika ametaka kufungwa mitambo maalumu ikiwamo kamera zitakazokuwa na uwezo kutambua na kubaini matukio yoyote yanayotendeka katika eneo hilo.

“Nataka ukuta huu uanze mara moja tena JWTZ kupitia Suma JKT waanze kazi hii mara moja na baada ya kukamilika eneo hili liwe na mlango mmoja tu ambao utaweka mtambo wa ukaguzi... wewe ukiweka Tanzanite tumboni tutakubaini, ukiweka kwenye kiatu uonekane pia,” amesema Rais Magufuli.

Amesema lengo la Serikali kufanya hivyo ni kuhakikisha inapata sehemu ya mapato yake na wawekezaji waondoke na haki yao bila kupunjwa upande wowote.

Amesema hataki kuona rasilimali za Taifa zinatoroshwa kienyeji na kwenda kuwafaidisha wajanja wachache walioko nje ya nchi hivyo ili kudhibiti hali hiyo ameamua kuchukua hatua madhubuti.

“Hapa adui yetu siyo CCM au Chadema ama mwingine yeyote, adui yetu ni yule anayopora mali zetu, hatupaswi kugombana sisi wenyewe na kumuacha adui yetu yuko pembeni, naomba tushikamane katika hili maana hii vita ya uchumi siyo lelemama lazima tuwe wamoja,” amesema.

Pia, amesema ndoto yake ni kuona soko la Tanzanite linakuwa Simanjiro ili wafanyabiashara kutoka ng’ambo kama Marekani, India na Ulaya wanafika kwenye eneo hilo kufanya biashara.

“Tunataka soko la Tanzanite linakuwa hapa Simanjiro ili hawa wafanyabiashara wafunge safari waje kununulia hapa na hiyo itakuwa na manufaa pia kwa wafanyabiashara wa eneo hilo maana hata yule mchinja mbuzi ama mwenye gesti atafaidika na ujio huo,” amesema.

Rais Magufuli amesema hayo leo Jumatano wakati akizindua barabara ya kiwango cha lami ya Mererani yenye urefu wa kilometa 26 ambayo imegharimu kiasi cha Sh 32.5 bilioni.  Rais ameahidi kuendelea na kipande kilichobakia ili lami hiyo ifike makao makuu ya Mkoa wa Manyara ambayo ni Babati.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Waasi wa CONGO Waua Askari Mmoja wa JWTZ

0
0
Askari wa jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) aliyefahamika kwa jina la Praivate Mussa Jumanne Muryery ameuawa kwa kupigwa risasi na kundi la waasi akiwa kwenye ulinzi wa Amani nchini DRC Congo.

Kwa mujibu wa taarifa ya (JWTZ) inasema kuwa askari wake huyo alifariki Septemba 17, 2017 na kufuatia shambulio hilo Umoja wa Mataifa umeunda bodi ya uchunguzi kuchunguza tukio hilo

Bunge LAKANUSHA Kuendeshwa Kibabe wala Kuendeshwa na Serikali

0
0
Bunge la Tanzania limetoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali na kusema Spika wa Bunge, Ndugai haendeshwi na serikali kama ambavyo wanasiasa wamekuwa wakisema na kudai watu hao wanalenga kumchafua, kumshambulia Spika wa Bunge na kumkosanisha na wananchi.

Katika taarifa iliyotolewa Septemba 20, 2017 na Bunge imesema kuwa kitendo cha viongozi hao kusema bunge la kumi na moja halina meno, halitekelezi wajibu wake na kudai kuwa bunge hilo na Spika wa Bunge wanaendeshwa na serikali si kweli kwani ni uongo na uzushi wenye lengo la kulichafua bunge pamoja na Spika wa Bunge Job Ndugai.

Mbali na hilo taarifa ya bunge imeweza kutolea ufafanuzi wa mambo mbalimbali ikiwepo kauli ya kusema bunge la sasa linaendeshwa kibabe, limetolewa ufafanuzi kuhusu sakata la matibabu ya Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu pamoja na baadhi ya viongozi kufikishwa kwenye Kamati mbalimbali za Bunge kwa ajili ya mahojiano. 

Kamati ya Bunge yashindwa kumhoji Kubenea, alazwa kliniki ya Bunge

0
0
Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, imeahirisha kumuhoji Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea kutokana na kufika mbele yake akiwa mgonjwa.

Kubenea amefika mbele ya kamati leo Jumatano saa nne asubuhi akiwa katika baiskeli ya wagonjwa (Wheel chair) chini ya ulinzi wa askari wa Jeshi la Polisi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Kapteni mstaafu George Mkuchika amesema  walikutana kutokana na kupelekewa shauri na Spika la kumuita Kubenea akidaiwa kudharau mamlaka ya Spika kwa kauli alizozitoa katika kanisa moja jijini Dar es Salaam.

“Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge inakutana pale inapoletewa shauri na Spika, tumeletwa mashauri ya Kubenea ya kudharau mamlaka ya Spika kwa kauli ambazo amezitoa katika kanisa huko Dar es Salaam,” amekaririwa Mkuchika katika taarifa iliyotolewa na Bunge.

Amesema utaratibu unamtaka mtu anayetakiwa kufika mbele ya kamati hiyo kupelekewa hati ya kuitwa na kwamba alishapelekewa.

Mkuchika amesema Kubenea amepelekwa akiwa katika baiskeli ya wagonjwa na kuiomba kamati impangie siku nyingine kwa hiyo wameridhia ombi lake.

“Kamati baada ya kumsikiliza Kubenea imeridhia ombi lake la kumpangia tarehe nyingine kwa kumpa muda wa kuangalia afya yake mpaka atakapopona,”
 amesema.

Mkuchika aliagiza Kubenea apelekwe katika Zahanati ya Bunge ili apewe huduma ya kwanza.

Awali, Kubenea baada ya kuhojiwa na kamati kama ataweza kuzungumza katika kikao hicho aliiomba kamati kumpangia siku nyingine kwa kuwa asingeweza kuzungumza kwa wakati huo kutokana na kuwa katika maumivu makali.

Septemba 12, Spika wa Bunge, Job Ndugai aliagiza mbunge huyo kufika mbele ya kamati hiyo kuhojiwa kuhusu tuhuma alizozitoa wakati wa ibada Septemba 10  kwamba Spika alisema uongo bungeni wakati akitangaza idadi ya risasi zilizopigwa kwenye gari la Mbunge wa Singida Mashariki,  Tundu  Lissu.

Zitto Kabwe akamatwa na polisi Akiwa Uwanja wa Ndege Dar

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe amekamatwa na jeshi la polisi usiku huu katika uwanja wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam akitokea Kigoma.

Afisa Habari wa Chama Cha ACT Wazalendo, Abdallah Khamis amethibitisha kukamatwa kwa kiongozi huyo wa chama chake na kusema kuwa kwa sasa wanasheria wa chama hicho wanafuatilia kujua sababu ya kiongozi wa chama chao kukamatwa na jeshi la polisi.

"Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, ndugu Zitto Kabwe amekamatwa na Polisi muda huu uwanja wa ndege wa JNIA, Dar es salaam wakati akitoka Kigoma. Kwa sasa wanasheria wa chama wanafuatilia kujua sababu za kukamatwa kwake" alisema Abdallah Khamis

Asubuhi ya leo kulikuwa na taarifa kuwa Katibu wa Bunge Dkt. Thomas kashililah alitoa amri kwa jeshi la polisi kumkamata Mbunge huyo wa Kigoma Mjini na kutakiwa kumfikisha mjini Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa kutokana na kauli ambazo amewahi kuzitoa juu ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu Job Ndugai pamoja na Bunge lenyewe.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamii ya Septemba 21

Serikali yatangaza nafasi za kazi ya ualimu wa Shule ya Msingi

0
0
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetangaza ajira za walimu wa shule za msingi kwa walimu ambao wamemaliza masomo yao mwaka 2014/2015 katika ngazi ya cheti (III A).

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na kuthibitishwa na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbas imesema kuwa walimu ambao wamemaliza mwaka 2014/2015 na walituma maombi yao kwenye tangazo la kazi ya Agust 10, 2017 hawatakiwa kuomba upya kwani barua zao zinafanyiwa kazi.

Jitihada kumpeleka Tundu Lissu Marekani zagonga Mwamba

0
0
Mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu ambaye amekuwa akifuatilia kwa ukaribu matibabu ya mbunge mwenzake wa Singida Mashariki Tundu Lissu, ameweka wazi kwamba jitihada za kumpeleka Lissu Marekani kutibiwa kwa sasa zimegonga mwamba.

Lazaro Nyalandu ametoa taarifa hiyo kwenye ukurasa wake wa facebook ambapo amendika ujumbe kuhusu kauli ya madaktari wanaomtibu Tundu Lissu jijini Nairobi Kenya, na kueleza kwamba madaktari hao wamesema hawawezi kuruhusu Tundu Lissu asafirishwe kupelekwa Marekani kutokana na hali yake jinsi ilivyo.

“Kwa sasa mipango ya kumsafirisha Mheshimiwa Tundu Lissu nje itasimama kutokana na ushauri wa madaktari wa hospitali ya Nairobi, ili kuruhusu kukamilishiwa huduma za tiba ambazo tayari ameanzishiwa hadi hapo itakavyoshauriwa au vinginevyo, ama endapo kutatokea umuhimu wa kufanya hivyo katika siku zijazo”, ameandika Lazaro Nyalandu.

Hapo jana Lazaro Nyalandu alitoa taarifa kwamba wanafanya jitihada za kumpeleka Tundu Lissu Marekani kwa ajili ya matibabu zaidi, huku wakisubiria ripoti ya madaktari wa hospitali ya Nairobi ambako mbunge huyo anatibiwa, na ndipo ilipokuja taarifa hiyo kwamba haitowezekana kumsafirisha kwa sasa.

Ikumbukwe  kuwa Mbunge Tundu Lissu alipigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 mjini Dodoma majira ya mchana, na usiku wa siku hiyo hiyo alikimbizwa jijini Nairobi kwa ajili ya matibabu zaidi, kutokana na hali yake kutokuwa nzuri.

==>>Huu ni ujumbe alioundika Lazaro Nyalandu
TUNAFAHAMU kwamba, tangu Alhamisi, Septemba 7, siku ambayo Mh #TunduLissu, Mb., (Singida Mashariki-CHADEMA) alishambuliwa kwa kupigwa risasi mjini DODOMA, Watanzania wengi wamesononeshwa na kulia sana, na kubwa zaidi, WOTE wameungana katika kuomba Sala na Dua kwa ajili ya Mh #TunduLissu, ili mkono wa Mkombozi, aliye MUNGU wetu, upate kumgusa tena na kumponya dhidi ya majeraha, maumivu na mateso anayoyapitia.

MAPEMA leo, baada ya kutembelea #NairobiHospital asubuhi, nimefanya mazungumzo mchana wa leo na Mh #FreemanMbowe, ambapo kwa pamoja tumeelezwa kuwa MADAKTARI #NairobiHospital wameendelea na kumtibu Mh #TunduLissu, ikiwa ni pamoja na kuanza upasuaji, na huduma zingine za Kitabibu walizomwanzishia tangu awasili Nairobi siku ya Alhamisi, Septemba 7. IMEELEZWA vilevile kuwa kwa sasa Mh #TunduLissu ataendelea na TIBA hospitalini hapo kutokana na kile kilichoelezwa kuwa hali yake bado ni "Critical but stable", na KWAMBA mwili wake unaendelea kuitikia vema matibabu lukuki anayofanyiwa kwa wakati mmoja.

KWA SASA, mipango ya kumsafirisha Mh #TunduLissu NJE itasimama, kutokana na ushauri wa MADAKTARI #NairobiHospital, ili kuruhusu kukamilishiwa huduma za TIBA ambazo tayari ameanzishiwa, hadi hapo itakavyoshauriwa vinginevyo, ama endapo kutatokea umuhimu wa kufanya hivyo katika SIKU zijazo.
AIDHA, SOTE tuzidi KUMWOMBEA MUNGU na kushiriki katika CHANGIZO za kusaidia gharama za matibabu yake.

NI DHAHIRI kwamba Wana Singida, na Watanzania WOTE tumeumia, tumekwazwa, na tumesononeshwa sana kwa uonevu na dhuluma aliyotendewa ndugu yetu Mh #TunduLissu. Kitendo hiki hakikubaliki mbele za MUNGU na mbele za wanadamu.

Tunaiomba Serikali yetu iendeleze juhudi zake na kuchukua hatua za haraka kuwasaka, kuwakamata, na kuwatia mbaroni watu wote waliohusika kupanga na kutekeleza shambulio hili la kigaidi dhidi ya Mh #TunduLissu. Aidha, shambulio hilo walilolifanya watu wasiojulikana limedhalilisha taifa, na kudhoofisha taswira ya kukomaa kwa demokrasia inayoruhusu kuvumiliana na kuheshimiana licha ya tofauti zetu za kiitikadi na mitazamo ya kisiasa.

HALIKADHALIKA, kwetu sote kama TAIFA, huu ni wakati wa Watanzania wote kuwa wamoja, bila kujali tofauti zetu za kiitikadi, kidini, wala kikabila, tuungane na kulaani kitendo hiki na vitendo vyote vya uonevu na kuumizana. TANGU zamani, IMEANDIKWA: Haki HUINUA Taifa.

Lazaro S Nyalandu, Mb.
Singida Kaskazini-CCM
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (TAIFA)

PCCB: Vitendo vya Rushwa Vyazidi Kupungua Nchini

0
0
Na. Paschal Dotto- MAELEZO
Serikali ya Awamu ya Tano chini ya  uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza vitendo vya rushwa katika ofisi za Serikali, taasisi na mashirika ya umma na kuweka usawa katika  upatikanaji wa huduma kwa jamii.
 
Hayo yamesemwa  Jijini Dar es Salaam  na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Brigedia Jenerali John  Mbungo wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kuhusu rushwa katika taasisi na mashirika ya umma kilichofanyika jana  jijini Dar es Salaam. 
 
 Brigedia Jenerali Mbungo alisema kuwa lazima watumishi wajifunze kuwa waadilifu, kwa hiyo kile watakachokipata kutoka katika mkutano huo kikafanye kazi kuleta haki kwa wananchi wakati wa kupata huduma katika ofisi zao ili kuendana na sera ya Awamu ya Tano ya kutokuvumilia vitendo vya rushwa nchini.
 
“Tumieni fursa katika kikao hiki ili kuweza kupata elimu itakayosaidia wananchi kuelimika juu ya vitendo vya rushwa na kupata haki zao za msingi wanapopata huduma katika ofisi zenu”,alisema Brigedia Jenerali Mbungo.
 
Kikao kazi hiki ni cha kwanza ambacho kinafuatia mkakati wa awamu wa tatu  utakaokuwa wa miaka mitano kuanzia  Julai, 2017 unaolenga kuanzia ngazi za vijiji, wilaya, mkoa, mpaka taifa ili kudhibiti uadilifu, nidhamu na utendaji kazi wenye kuzingatia haki katika ofisi mbalimbali nchini.
 
Aidha Brigedia Mbungo alisema kuwa kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na serikali, hali ya rushwa nchini imepungua kwa kiasi kikubwa kwani malalamiko yamepungua katika ofisi, taasisi na mashirika ya umma.
 
“Hali ya rushwa sasa hivi imepungua kwa sababu Serikali kwa kutumia juhudi  mbalimbali imedhibiti hali hii, Tanzania ina viwango vya chini sana vya rushwa ikilinganishwa na nchi nyingine za maziwa makuu kwa hiyo naweza kusema kiwango kimepungua sana hususani kwa Jiji la Dar es Salaam ambapo vitendo hivi vilishamiri sana, hivyo katika awamu hii ya tatu ya mkakati huu tunatarajia viwango vitashuka zaidi”, alisisitiza Brigedia Jenerali Mbungo.
 
Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Bi.Theresia Mmbando alisema kuwa katika mkoa wa Dar es Salaam hali ya vitendo vya rushwa imepungua kwa kiasi kikubwa na sasa wananchi wanapata huduma pasipo kuwa na dalili zozote za rushwa.
 
“Hali ya rushwa katika mkoa wetu wa Dar es Salaam inapungua siku hadi siku kwa kuwa watu wanaendelea kupata elimu ya haki zao za msingi na kuhudumiwa pasipo kutoa rushwa, wala kuwepo dalili za rushwa”, alisema Bi. Mbando.
 
Kwa upande wake Mkuu wa TAKUKURU,  kanda maalum ya Dar es Salaam Bw.Juventus Baitu ameeleza kuwa wamefanikiwa kuweka sawa  mkakati huo kwa kutoa elimu kwa wananchi na kwa sasa kumekuwa na mwamko wa kuripoti matukio ya rushwa katika ofisi yake.
 
Aliongeza kusema kuwa katika kitengo cha Dawati la Uchunguzi wamepokea malalamiko yapatayo 665 kwa mkoa wa Dar es Salaam huku kitengo hicho kikifungua majalada ya kesi 40 kwa Mwendesha Mashtaka (DPP) na kusikilizwa kesi 26 ambapo taasisi  hiyo ilifanikiwa kushinda kesi 14 na kuokoa kiasi cha pesa kisichopungua shilingi milioni 791,443,984 katika kesi mbalimbali za rushwa.
 
Aidha TAKUKURU kupitia dawati la elimu ya rushwa imeweza kufungua vilabu 94 vipya katika shule mbalimbali mkoani Dar es Salaam, kuendesha semina 91 kwa watumishi wa taasisi na mashirika ya umma pamoja na maonesho 12 yanayohusu vitendo vya rushwa ikiwemo kuwahabarisha wananchi kupitia vipindi vya televisheni 14 kuanzia mwaka 2016 pamoja na kutoa taarifa kwenye vyombo vya habari kwa kutoa vitini 19 kuhusu mapambano dhidi ya rushwa.
 
“Tumeweza kutoa elimu kupitia matamasha mbalimbali zaidi ya 16 katika taasisi na mashirika ya umma ambapo matamasha 7 yalikuwa na lengo la kutoa mazimio kwa taasisi na mashirika ya umma kuhusu kwa vitendo vya rushwa”,alisisitiza Bw.Baitu.
 
Mkakati huo kwa awamu ya tatu ulizinduliwa rasmi, Desemba 10, 2016 wakati wa maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu duniani  na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan ambapo utekelezaji wake ulianza tarehe 1, Julai, 2017.

Waziri Mkuu: Serikali Kumaliza Kero Zote za Maji

0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kumaliza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na huduma ya umeme katika maeneo mbalimbali nchini zikiwemo wilaya za Chemba na Kondoa mkoani Dodoma.

Amesema serikali kupitia kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo, itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini watapata huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao.

Waziri Mkuu ameyasema hayo wakati  akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa wilaya ya Chemba na Kondoa waliomsimamisha katika maeneo ya Chemba, Kalema, Bicha na Bereko akiwa njiani kuelekea mkoani Arusha kwa shughuli za kikazi.

Alisema kwa sasa Serikali imeendelea na uchimbaji wa visima virefu, vifupi pamoja na kuweka mtandao wa mabomba ya kusamba maji katika maeneo mbalimbali nchini yakiwemo na ya wilaya hizo ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo karibu na makazi yao

Kufuatia hali hiyo Waziri Mkuu aliwaagiza watendaji wawachukulie hatua watu wote watakaokutwa wakiendesha shughuli mbalimbali kama za kilimo, ujenzi wa makazi na uchungaji wa mifugo ndani ya vyanzo vya maji kwa kuwa zinasababisha ukame.

Aidha Mh. Majaliwa ameagiza wakandarasi wamalize maeneo yaliyosalia katika REA awamu ya pili ndipo waendelee na awamu ya tatu. Alisema Serikali imetenga sh. trilioni moja kwa ajili ya kusambaza umeme katika vijiji 8,000 ambavyo bado havijaunganishiwa nishati hiyo.

"Rais wetu Dkt. John Magufuli anajali sana wananchi wake, hivyo ametenga fedha nyingi zitakazotosheleza kusambaza umeme katika vijiji vyote vikiwemo na vya wilaya za Chemba na Kondoa. Gharama za kuunganishiwa umeme huo ni sh. 27,000 tu" amesema.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 22


Jaji Mku: Hatupo Tayari Kuzungumza Lolote Kuhusu Tundu Lissu

0
0
Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma amesema shambulio alilofanyiwa Tundu Lissu ni uhalifu mkubwa lakini majaji hawawezi kuzungumza juu ya tukio hilo kwani kanuni haziwaruhusu kutoa maoni au kuzungumzia jambo ambalo wanaona litakwenda mahakamani

Jaji Mkuu amesema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam na kusema amekuwa akiona watu wakitaka kusikia maoni yao juu ya tukio hilo na kuendelea kusema hawawezi kutoa maoni yao juu ya sakata hilo la Tundu Lissu kwa sababu wao mahakamani wana kanuni ambazo zinawazuia kutoa maoni au kuongelea jambo ambalo wanaona litakwenda mahakamani.

"Kwenye mitandao mmekuwa mkijaribu kutuvuta tutoe maoni sisi hatutasema kitu, tuache sheria zifanye kazi yake ila pale tutakapoona kwamba waliopewa jukumu la kukusanya ushahidi wanashindwa kufanya hivyo ndiyo tupige kelele. Kitu cha kwanza ni kukusanya ushahidi na huo ushahidi utakusanywa hapa hapa Tanzania asikudanganye mtu kwamba mtu kutoka nje ndiyo atakuwa na uwezo wa kukusanya ushahidi hapa nyumbani bali ushahidi unakusanywa hapa hapa" alisema Jaji Mkuu wa Tanzania

Mbali na hilo Jaji Mkuu wa Tanzania amesema siku za karibuni kuna moja ya hakimu alishambuliwa na kuuwawa lakini wao kama majaji hawakuwahi kulalamika, au kusema jambo lolote, au kulaani jambo hilo wala kuwataka watu walaani kitendo hicho kwa kuwa kanuni zao haziwaruhusu kufanya hivyo.

Jaji Mkuu alimaliza kwa kuwataka Watanzania kuacha sheria ifanye kazi yake na kuwataka kuwa na imani ya Mahakama kwa kuwa ni muhimili wake unaojitegemea na hauwezi kuingiliwa.

Majibu Aliyoyatoa Zitto Kabwe Baada ya Kukamatwa na Kupelekwa Kamati ya Maadili ya Bunge

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Ruyagwa Kabwe jana amefikishwa kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kama ilivyotakiwa na Spika wa Bunge Job Ndugai, kujibu tuhuma za kutoa kauli za kulidhalilisha bunge.

Kwenye Kamati hiyo ambayo alifikishwa chini ya ulinzi wa Polisi, Mbunge Zitto Kabwe amekiri kwamba kauli hiyo ni kweli aliitoa na kueleza haya.....

Uhuru Wangu wa Maoni Ulilenga Kulinda Uhuru, Haki, Hadhi na Heshima ya Bunge

Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati,

Mnano tarehe 13 Septemba, 2017 nilipata wito wa kufika mbele ya Kamati yako kutoa ushahidi wa masuala mbalimbali. Nilipata wito husika saa nane na dakika 40 mchana, nikitakiwa kufika mbele ya kamati yako, hapa Dodoma saa saba mchana siku hiyo hiyo.

Nililetewa wito huo na RCO Mkoa wa Kigoma nikiwa kwenye kikao cha Baraza la Madiwani la Manispaa ya Kigoma Ujiji. Sikuweza kufika, isingewezekana katika mazingira hayo niwe na uwezo wa kusafiri kutoka Kigoma na kufika mbele ya kamati yako hapa Dodoma. Kwanza muda ulishapita, lakini hata taratibu za kiusafiri pamoja na umbali kati ya Kigoma na Dodoma hazikuwezesha Jambo hilo.

Siku iliyofuata nilipata ajali, ambapo nyumba yangu iliwaka moto wakati nikiwa njiani kwenda Nairobi kumuona mbunge mwenzetu mgonjwa, ndugu Tundu Lissu. Jana tarehe Septemba 20, 2017 nikiwa natokea Kigoma ili kuja kwenye Kamati nilikamatwa na Polisi ili kufikishwa mbele ya Kamati yako.

Leo nimefika mbele yenu na nitajibu wito wenu kama ifuatavyo:

A: Kwamba maoni yangu kwenye mtandao wa Twitter kuwa "Bunge siku hizi ni Idara ya Tawi la Utawala" yanadhalilisha Mhimili Wa Bunge.

Maneno hayo ni ya kwangu na nimeyatoa kama raia wa Tanzania. Ninaamini kwa dhati kuwa Bunge la Kumi na Moja limekuwa likifanya kazi kwa kuingiliwa na Serikali chini ya ndugu Rais John Pombe Magufuli.

Maneno na vitendo vya Rais yanaashiria kuwa Bunge halina Uhuru wake, na mimi kama Mbunge nina wajibu wa kuonyesha kutopendezwa kwangu na hali hiyo. Nina mifano kumi (10) kuthibitisha maelezo yangu hayo kama ifuatavyo:
  1.     1. Kuzuiwa kwa "Bunge Live" kwa kisingizio cha kupunguza gharama za uendeshaji wa mhimili wa Bunge, wakati Mikutano yote ya mhimili wa Serikali, hasa ya Rais ikirushwa live (mubashara) ni dalili ya wazi ya kufifisha sauti ya Bunge na kupandisha sauti ya serikali. Hata vituo binafsi ambavyo vilipanga kurusha bunge Live bila malipo (na hivyo kutokuwa na gharama) vilizuiwa, lakini vinarusha Live mikutano ya Rais.
  2.      Kitendo cha Uongozi wa Bunge kurudisha serikalini shilingi Bilioni 6 bila ridhaa ya wabunge kwa kisingizio kwamba zimebaki kutokana na kubana matumizi. Hii ni dalili ya wazi ya Bunge "kujipendekeza" kwa serikali. Wakati Uongozi wa Bunge ukirejesha kiwango hicho cha Fedha, kuna taarifa kwamba kamati nyingi za Bunge zinashindwa kutekeleza wajibu wake kwa sababu ya ukata.
  3.      Maelekezo ya mhimili wa Serikali kwa mhimili wa Bunge, kupitia maagizo ya Rais Magufuli kwa Spika Ndugai kuwa "Awashughulikie wabunge" (kwa kuwafukuza bungeni) aliowaita "waropokaji" ili waje wazungumze nje ya Bunge na yeye Rais (Serikali) apate nafasi ya kuwashughulikia. Kauli hii ya Rais aliyoitoa wakati akipokea Ripoti ya Prof. Osoro kuhusu Mikataba ya Madini, Juni 12, 2017 inaonyesha picha iliyo dhahiri kuwa Bunge linapokea Maelekezo kutoka Serikalini ya kuwadhibiti wabunge hasa wanaoiwajibisha serikali. Na hatuwahi kuliona Bunge likiyakana maelekezo hayo ya Rais kwa Spika.
  4.      Kitendo cha Bunge kuhariri hotuba za kambi ya upinzani kwa kushinikiza kuondolewa kwa vipengele vinavyoikosoa Serikali. Mathalani, Wakati wa Bunge la Bajeti, hotuba ya Msemaji wa Kambi ya upinzani wa Wizara ya Mambo ya Ndani, ndugu Godbless Lema, iliamriwa kuondolewa maneno yanayohusu kashfa ya Mkataba wa Lugumi, kumhusisha Rais na kuuzwa kwa nyumba za Serikali, Mauaji ya wanasiasa, pamoja na Bunge kulinda wahalifu.
  5.      Kauli ya Rais Magufuli ya Novemba 4, 2016 akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari kuwa "mzizi wa mhimili wa serikali ni mrefu zaidi kuliko mihimili mingine" mara baada ya kuulizwa juu ya matumizi ya Serikali Nje ya Bajeti iliyoidhinishwa na bunge, unaonyesha dhahiri fikra ya Rais na Serikali yake juu ya ukuu wa mhimili wa Serikali dhidi ya Bunge.
  6.      Kitendo cha Ripoti ya Kamati ya Bunge ya Tanzanite na Almasi kusomwa nje ya Bunge na kuwasilishwa kwa Waziri Mkuu na Rais bila kuwasilishwa na kujadiliwa Bungeni ili kuwekewa azimio la Bunge. Kitendo hiki kinaifanya Kamati hiyo kuonekana kuwa ya Serikali badala ya Kamati ya Bunge.
  7.      Kauli ya Rais kuwa Spika alimpigia simu kumuuliza juu wajumbe wa kuwaweka kwenye Kamati za Bunge za Tanzanite na Almasi inaonyesha dhahiri kuwa Spika anafanya kazi kwa maelekezo ya Rais. Na Bunge na Spika hawajawahi kuikana kauli hii ya Rais.
  8.     Kwa mara ya kwanza kwenye Historia ya Nchi yetu tumeshuhudia Mbunge akishambuliwa kwa risasi wakati Mkutano wa Bunge ukiwa unaendelea. Haijapata kutokea katika historia ya Bunge letu, Wabunge kukamatwa hovyo mbele ya mageti ya Bunge na kusafirishwa usiku usiku bila hata Spika kujulishwa kama taratibu za Mabunge ya Jumuiya ya Madola zinavyotaka. Kitendo cha 'Watu Wasiojulikana' kummiminia risasi zaidi ya thelathini Mbunge wa Singida Mashariki, ndugu Tundu Lissu, wakati akitokea Bungeni, tena kwenye makazi yake, ambayo kwa mujibu wa sheria ni sehemu ya Bunge, ni dharau ya hali ya juu kwa Mhimili huu. Ni tukio linalolenga kuliziba mdomo Bunge. Makala yangu ya Nani alitaka kumwua Tundu Lissu (kwa lugha ya Kiingereza) naiambatanisha katika maelezo yangu haya.
  9.     Kitendo cha Serikali kutowasilisha 'Taarifa za Utendaji wa Robo Mwaka' kwenye Kamati ya Bunge ya Bajeti kama inavyotakiwa kwa mujibu wa Sheria ya Bajeti ya mwaka 2014 ni dharau kubwa kwa Mhimili wa Bunge. Ni dharau zaidi kwamba Serikali ilileta Muswada wa sheria kuondoa kifungu kinacholazimisha Waziri wa Fedha kutoa Taarifa hizo, na Bunge kupitisha kuwa Sheria, hivyo kuondoa kabisa Uwajibikaji wa kibajeti wa Serikali ndani ya Bunge, hivyo kudunisha hadhi ya bunge.
  10.     .Bajeti ya Bunge kutowekwa kwenye Mfuko wa Bunge kwa mujibu wa sheria, na Spika kutakiwa kuomba vibali vya safari za Wabunge kwa Mkuu wa Tawi la Utendaji (Serikali) ni maelezo tosha kuwa Bunge ni Tawi la Utendaji na sio Mhimili unaojitegemea.
Ninayo mifano mingine mingi tu ya kuonyesha kama ushahidi wa jambo hili, kwa sasa hiyo 10 naomba itoshe.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nchi yetu ina mihimili mikuu mitatu ya dola ambayo ni Serikali, Bunge na Mahakama. Katiba na Sheria mbalimbali za nchi zimewekwa kuhakikisha kila mhimili unafanya kazi kwa uhuru bila kuingiliwa na mhimili mwingine. Kikatiba, mbali na wajibu wake wa kutunga sheria, Bunge lina wajibu wa kuisimamia serikali. Kwa lugha nyingine, katika utekelezaji wa majukumu yake, Bunge ni "Kiranja" wa kuibana na kuisimamia Serikali.

Tangu kuingia madarakani kwa serikali ya awamu ya tano, kumekuwepo na kauli na matendo ya viongozi wa serikali na Bunge yanayoashiria uelekeo wa serikali kuminya na kuingilia uhuru wa Bunge. Baadhi ya vitendo hivi vimefanywa hata na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa kutambua wajibu wangu katika kulinda heshima, uhuru, hadhi, haki, ufanisi na madaraka ya Bunge katika kutekeleza majukumu yake, mara kadhaa nimekumbusha na ilipobidi kuonya ndani na nje ya Bunge dhidi ya vitendo hivi.

Maoni yangu yaliyonifanya niitwe hapa, pamoja na Mifano kumi (10) niliyoitoa hapo juu vinaonyesha wazi nia yangu njema ya kuonya na kutaka kulindwa kwa hadhi, heshima, haki na madaraka ya Bunge letu tukufu. Naamini bunge lilipaswa kunipongeza ni kunishajiisha kwa kazi hiyo, na si kinyume chake ninapotuhumiwa na kuletwa mbele ya Kamati yako kuwa nimelidhalilisha bunge pamoja na spika wa bunge. Jambo hili litavunja morali ya wabunge kutetea hadhi ya bunge letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti (Mzee George Huruma Mkuchika),

Wewe ni miongoni mwa wazee ninaowaheshimu sana hapa nchini, nilivyo sasa kwa kiasi kikubwa ni sehemu ya malezi yako kwangu hapa bungeni, umeshiriki kunifinyanga niwe mbunge imara kwa busara na hekima zako, pamoja na kunipa ujasiri wa kuisimamia kutokana na uzoefu wako. Nakutambua kama muumini wa Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, iliyotangazwa kupitia Azimio la Arusha. Napenda ninukuu sehemu ya Azimio la Arusha kuhusu Uhuru wa mawazo. Azimio linasema "kwamba TANU inaamini: kila Raia wa Tanzania ana haki ya Uhuru wa Mawazo..."

Napenda kusisitiza kuwa kama Mtanzania ninao Uhuru wa Mawazo na Maoni, hiyo ni kwa mujibu wa Katiba yetu, Ibara ya 18. Kitendo cha mimi kuitwa mbele ya Kamati yako kwa maoni yangu haya, naamini ni mwendelezo wa kufinywa kwa haki na uhuru wa mawazo na maoni ya raia.

Mimi kama mtanzania ninaruhusiwa kuwa na maoni yangu, na pia nina haki ya kutoa maoni yangu hayo. Kunituhumu kwa maoni yangu binafsi kuwa yanavunja heshima, hadhi, haki na mamlaka ya bunge, na kuwa maoni yangu hayo ni kulidhalilisha Bunge na Spika si sahihi kabisa, ni uonevu dhidi yangu, ni ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni kinyume na Haki za Binadamu, hasa kwa kuwa mifano hiyo 10 niliyoitoa imeonyesha usahihi wa maoni yangu hayo.

Maoni yangu yalilenga kulinda hadhi, haki, heshima na madaraka ya bunge letu tukufu. Ni maoni yaliyolenga kulinda heshima ya spika, ili azitumie nguvu alizonazo kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Bunge kulinda heshima na hadhi ya Bunge isiporomoke, ni maoni yaliyolenga kuonyesha imani niliyokuwa nayo juu yake (Spika), ni maoni yaliyolenga kulizindua Bunge juu ya hali ya kukosa mshawasha/msisimko ambao Watanzania wameuzoea.

Tafsiri kuwa maneno yangu kuwa Spika hajafikia viwango vya Maspika waliotangulia kabla yake kuwa ni kumdharau si sahihi. Maoni yangu hayakulenga kuonyesha dharau, bali yalilenga kutaka Bunge liyalinde yale mambo mazuri yaliyosimikwa na Maspika hao wa nyuma katika kuisimamia Serikali.

Jambo hili (la kutaka kuendelezwa na kulindwa kwa mambo mazuri ya maspika wa nyuma yaliyoimarisha hadhi ya Bunge) ni ahadi ya Spika wetu, ndugu Ndugai, wakati wa kikao maalum cha Bunge cha msiba wa Spika wa Bunge la 9, ndugu Samuel John Sitta. Hivyo ni dhahiri, mimi kukumbushia ahadi hiyo ya Spika mwenyewe haiwezi kwa namna yoyote ile kuwa ni kudhalilisha Bunge na kumdhalilisha Spika, bali kitendo cha kuitwa hapa mbele ya kamati yako kwa maoni yangu binafsi nje ya bunge, maoni yaliyolenga tu kukumbushia ahadi husika, hakika kinalidhalilisha Bunge na Spika wa Bunge

Kuona mawazo huru haya yangu kuwa ni kudhalilisha Bunge si sawa. Ni kinyume kabisa na misingi ya TANU iliyoasisi Utaifa wetu, ni kinyume na Utanzania wetu. Wananchi wangapi wataletwa mbele ya Kamati yako kuhojiwa kwa kutoa maoni yao juu ya hadhi ya mhimili wa Bunge?

Imani yangu ni kuwa, Hadhi, Heshima, Haki na Madaraka ya Bunge haitotokana na kuhoji wanaotoa maoni juu ya mwenendo wa bunge, kutumia maguvu ya Jeshi la Polisi, wala vitisho vya Kiongozi wa Mhimili wetu huu dhidi ya wabunge, bali ni mwenendo wake wa kuisimamia Serikali mbele ya umma ndio utakaojenga hadhi, heshima, haki na madaraka ya Bunge kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti
Iwapo Bunge litaendelea kuwa 'paraded ' Ikulu kila wakati na kupewa maelekezo na wakati mwengine kusimangwa na Serikali, kupitia Rais, umma utaona sio Bunge lao bali ni Tawi tu la Serikali, na kamati yako itakuwa na kazi ya kuita maelefu ya Watanzania.

Nawashukuru sana kwa kunisikiliza.

Naomba Kuwasilisha.
Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto
Mbunge, Kigoma Mjini - ACT Wazalendo
Dodoma

Septemba 21, 2017

Naibu Waziri afunga Machimbo Mkuranga Pwani

0
0
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina amefunga machimbo ya mchanga katika kijiji cha Kolangwa Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani.

Waziri Mpina amefikia uamuzi huo kutokana na uharibifu wa mazingira unaofanywa na wachimbaji wa mchanga katika machimbo hayo.

Mpina ametoa agizo la kufungwa kwa machimbo hayo akiwa kwenye ziara ya ukaguzi wa mazingira mkoani Pwani ambapo amebaini uharibifu huo umechangiwa na Taasisi za Serikali ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Idara ya Madini na Baraza la Taifa na Usimamizi wa Mazingira NEMC.

Waziri amebaini kuwa uchimbaji huo umefanyika bila wananchi kushirikishwa na haukuzingatia miundombinu na sheria ya Mazingira pia makazi ya watu.

Kufuatia mapungufu hayo, Mpina ameagiza Taasisi hizo za Serikali kufuatilia uharibifu huo uliofanywa kwa muda wa wiki mbili.

JWTZ Waanza Kutekeleza Agizo la Rais Magufuli la Kujenga Ukuta Katika Madini ya Tanzanite

0
0
Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania JWTZ limeanza kutekeleza agizo la Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli la kujenga ukuta na kuweka kamera katika eneo linalopatikana madini ya Tanzanite huko Mererani.

Meja Jenerali Michael Isamuyo ametua Mererani, Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara kwa Helkopta na kukagua maeneo ambayo ukuta utaanza kujengwa mara moja. Wachimbaji na wananchi wa Manyara wamefurahia na kuahidi ushirikiano.

Rais Magufuli alitoa agizo hilo juzi alipokuwa akiwahutubiwa wananchi wa Simanjiro kabla ya kufungua barabara ya KIA – Mererani yenye kilomita 26.

Tamko la Serikali Kuhusu Matibabu ya Tundu Lissu

0
0
Baada ya kushutumiwa kwamba imekaa kimya katika suala la matibabu ya Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, Serikali imejitokeza na kueleza kwamba iko tayari kugharamia tiba yake popote pale ikiwa itaombwa na familia au kwa ushauri wa madaktari.

Lakini wakati Serikali ikisema hayo Lazaro Nyalandu ambaye amekuwa akifanya mipango ili Lissu apelekwe kutibiwa ng’ambo, amesema madaktari wa Nairobi alikolazwa wamesema hawezi kusafirishwa katika kipindi hiki.

Jana akiwa Tanga, Waziri wa Afya, Ummy Mwaimu aliitisha mkutano na wanahabari na kusisitiza kuwa Serikali haijashindwa kuchangia gharama za matibabu ya Lissu huku akisema tangu mwanzo wa tukio la kushambuliwa kwake kwa risasi Septemba 7 huko Dodoma, viongozi wamekuwa wakishirikiana na familia katika kunusuru maisha yake.

Alisema amesikitishwa na namna ya suala la matibabu ya Rais huyo wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), linavyochukuliwa kisiasa huku akitahadharisha kwamba michango inayoendelea kuhamasishwa kusaidia kumtibu inaweza kutumiwa na matapeli kuwaibia wanaochanga.

“Serikali ina mpango wake katika kushughulikia matukio kama hayo, njia hiyo ndiyo iliyofanyika awali baada ya mbunge huyo kushambuliwa. Alifikishwa hospitalini na baadaye kukawepo na mpango wa kumpeleka Muhimbili,” alisema Ummy.

Baada ya shambulio hilo, Lissu alipelekwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa matibabu ya awali kabla ya kusafirishwa kwa ndege ya kukodi hadi Nairobi, Kenya anakoendelea na matibabu.

Kabla ya kupelekwa Nairobi, Serikali kupitia Bunge ilieleza kwamba kwa utaratibu wake, mgonjwa anapopata rufaa hupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili na ikishindikana anahamishiwa Apollo, India na si kinyume cha hapo.

 Utaratibu huo ulipingwa na viongozi wa Chadema ambao wakiongozwa na mwenyekiti wake, Freeman Mbowe waliamua kumpeleka Nairobi kwa walichoeleza kuwa ni kwa usalama wa mgonjwa.

Tangu alipopelekwa huko, Chadema imekuwa ikisema kwamba Serikali haijachangia chochote katika matibabu hayo ambayo tayari kiasi cha Sh160 milioni kimeshatumika ambazo zimetoka katika chama hicho na michango ya wananchi.

Lakini jana, Waziri Ummy alisema Serikali inasubiri familia iseme nini inataka kifanyike na wapi inataka mgonjwa wao akatibiwe na kwamba itakuwa nayo bega kwa bega kuhakikisha anatibiwa popote duniani na kwa gharama yoyote ile na si kwa michango ya wasamaria wema.

Alisema lengo la Serikali ni kuondoa dhana kwamba imejitenga katika matibabu ya Lissu hadi jukumu hilo kuonekana kuwa limebebwa na jamii na jambo linaloweza kuleta taswira mbaya ndani na nje ya nchi kutokana na ukweli kuwa aliyehusika ni kiongozi na Mtanzania.

Pamoja na hayo, aliwashukuru watu wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine wakiwamo madaktari na wahudumu wa Hospitali ya Dodoma kutoa huduma kwa Lissu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images