Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Yaingiza Tani 55,000 za Mbolea Ili Kudhibiti Mfumuko wa Bei

$
0
0
Na. Eliphace Marwa – Maelezo
Serikali imeingiza nchini jumla ya tani elfu 32 za mbolea ya kukuzia pamoja na tani elfu 23 za mbolea ya kupandia kupitia mfumo mpya wa uagizaji wa mbolea kwa pamoja, lengo likiwa ni kudhibiti bei kwa kuzingatia bei elekezi.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam wakati zoezi la upakuaji wa mbolea hiyo likiendelea Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Udhibiti wa Ubora wa Mbolea Tanzania(TFRA) Bw. Lazaro Kitandu amesema kuwa mpaka sasa jumla ya tani elfu 55 za mbolea zimewasili nchini.

Hii ni awamu ya kwanza ya kuingiza mbolea nchini kupitia mfumo mpya ya uagizaji mbolea kwapamoja ambapo kampuni ya OCP S.A ya nchini Morocco imeingiza jumla ya tani elfu 23 za mbolea ya kupandia na Kampuni ya Premium Agro Chem imeingiza tani elfu 32 za mbolea ya kukuzia.

“Mpaka sasa zoezi la kupakua mbolea ya kupandia (DAP) tani elfu 23 linaendelea vizuri na mara baada ya kumaliza kupakua mbolea hii tutaanza zoezi la kupakua mbolea ya kukuzia (UREA) ambayo ni tani elfu 32,” alisema Bw. Kitandu.

Kitandu aliongeza kuwa Mheshimiwa Waziri wa kilimo juzi alipokuwa anaongea na waandishi wa habari mjini Dodoma na akasisitiza bei ambazo zimetolewa zisimamiwe na kila ngazi kwasababu taasisi peke yake haiwezi kuwa na watu kila mahali hivyo Tawala za mikoa, Serikali za mitaa mpaka Kijiji zitasaidia kusimamia bei ambazo zimetolewa.

Pia Kitandu aliongeza kuwa kuhusiana suala la bei ya mbolea hiyo itatangazwa kupitia vyombo vya habari kama vile magazeti na televisheni na hivyo kutoa onyo kwa mawakala kujipangia bei kwa kuuza mbolea nje ya bei elekezi ya Serikali kwamba watachukuliwa hatua za kisheria kama kunyang’anywa leseni, kufungwa, faini au vyote kwa pamoja.

Aidha Kitandu alisisitiza kuwa mbolea hizi siyo mbolea za ruzuku kwani wakulima wengi wamekuwa wakichanganya mbolea hizi na mbolea za ruzuku na amefafanua kuwa mbolea hii imefanyiwa utaratibu wa kudhibiti toka kule inapotoka na hivyo serikali itahakikisha mbolea hii inauzwa kwa kulingana na bei ya soko la dunia.

Aidha Bw. Kitandu  aliwahakikishia wakulima kuwa  mbolea itasafirishwa mpaka vijijini kwa kutumia treni na malori kwa sehemu ambapo treni haiwezi kufika, na amewatoa hofu wakulima kuwa msimu unaoanza mwezi huu wameingiza tani 23,000 kwa mbolea ya kupandia (DAP) na tani 32,000 kwa mbolea ya kukuzia (UREA) ambapo watakuwa wanaagiza kwa awamu kwa miezi miwili miwili.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Serikali Yawasilisha Bungeni Mkataba wa Kimataifa wa Mradi wa Ujenzi wa Bomba la mafuta ghafi

$
0
0
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO, DODOMA
Serikali imewasilisha Mkataba wa Kimataifa wa Mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Uganga.
 
Akiwasilisha Mkataba huo kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe amesema kuwa Tanzania na Uganda ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo malengo yake ni pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi wanachama kwenye maeneo ya kisiasa, kiuchumi, kijamii kiteknolojia , utafiti, ulinzi na masuala ya Kisheria.
 
Dkt. mwakyembe amesema kuwa Serikali ya Uganda kupitia kampuni za Kimataifa za TOTAL, TULLOW NA CNOOC iligundua uwepo wa mafuta ghafi takribani mapipa bilioni 6.5 katika eneo la Albertine nchini Uganda.
 
” Kufuatia ugunduzi huo, Serikali ya Uganda ilianza kutafuta njia ya kusafirisha mafuta hayo kwenda kwenye soko la kimataifa ambapo iliaanisha njia takribani tatu ikiwemo ile ya kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania” amesema Dkt. mwakyembe.
 
Aidha Dkt. mwakyembe amebainisha baadhi ya faida zitokanazo na Mkataba huo ikiwemo kuongezeka kwa mapato ya Serikali kutokana na Kodi ya zuio na Kodi ya Mapato ya Kampuni zitakazotozwa wakati wa ujenzi na uendeshaji wa Mradi.
 
Vilevile amesema kuwa Serikali ya Tanzania itanufaika katika kuongezeka kwa mapato ya Serikali kwa takribani Dola za Marekani 12.2 kwa kila pipa la mafuta ghafi litakalosafirishwa kupitia Bandari ya Tanga kulingana na kiwango cha Hisa za Serikali ya Tanzania.
 
” kuimarika kwa mahusiano ya kidiplomasia, ulinzi na usalama kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uganda pamoja na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ujumla sambamba na kuimarika kwa huduma mbalimbali katika bandari ya Tanga kutokana na shughuli za Mradi na miundombinu itakayojengwa” aliongeza Dkt. Mwakyembe
 
Pia ongezo kwa fursa za  ajira kwa Watanzania ambapo takribani watanzania 10, 000 wataajiriwa wakati wa ujenzi na ajira zipatazo 1,000 wakati wa uendeshaji, Amesema Dkt. Mwakyembe.
 
Kwa upande wake Deogratius Ngalawa akimuwakilisha  Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ameishauri Serikali kuhakikisha inasimamia utekelezaji wa mkataba huo kwa kuzingatia mustakabali wa manufaa ya kiuchumi kwa Taifa.
 
” Napenda kutoa pongezi za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa juhudi zake na umahiri aliouonesha katika kuhakikisha Tanzania inapata fursa ya mradi huu mkubwa wa ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania” Amesema Ngalawa.
 
Akiongea kwa niaba ya Msemaji Mkuu kambi Rasmi ya Upinzani Wizara ya Nishati na Madini Mhe. Devota Minja amesema kuwa bomba hilo la kusafirisha mafuta ilikuwa na kazi iliyohusu zaidi ushawishi mpana kwani kulikuwa na ushindani mkubwa utoka kwa nchi jirani.

Ofisi ya Wakili wa Yusuf Manji, Hudson Ndusyepo Yavamiwa na watu wasiojulikana na Kutoweka na kabati la kutunzia nyaraka

$
0
0
Watu wanane wanaodaiwa kuwa ni wahalifu wamevamia jengo la Prime House lililopo Mtaa wa Tambaza  na kufanya uharibifu wa mali za wapangaji.

Jengo la Prime House lina ghorofa tano lipo jirani na ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wilayani Ilala.

Mwandishi  ameshuhudia barabara ya kuingia eneo hilo ikifungwa kwa muda na polisi ambao walitumia magari yao kuziba njia na kuweka uzio wa  utepe wa rangi ya njano.

Jengo la Prime House lina ofisi za kampuni mbalimbali, zikiwemo za mawakili  wa Yusuf Manji ambazo zimevamiwa na wameondoka na nyaraka muhimu, duka la dawa na sehemu ya kufanya mazoezi gym.

Mmoja wa mawakili ambao wana ofisi katika jengo hilo, ambaye  hakutaka kutaja jina lake alisema  kwamba watu hao walipofika walimfunga mlinzi kwa kamba na kisha kuingia ndani kwa nguvu.

"Mlinzi ameniambia baada ya kuingia walipokuwa wakifanya upekuzi walikuwa wakisikika wakisema si huku tutazame ghorofa linalofuata si hili,” wakili huyo amemkariri mlinzi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni amethibitisha tukio hilo akisema limetokea kati ya saa nane na saa tisa usiku wa kuamkia leo.

Ripoti: Tanzania Yaporomoka kwa Ukarimu Duniani

$
0
0
Tanzania imeporomoka nafasi sita katika utafiti wa ukarimu duniani ikiwa ni mwaka mmoja baada ya kufanya vizuri, jambo linaloonyesha Watanzania wameanza kuwa na mkono wa birika katika kuchangia wenye uhitaji.

Ripoti mpya ya ukarimu ya mwaka 2017 iliyotolewa mwishoni mwa wiki iliyopita inabainisha sasa Tanzania inashika nafasi ya 63 duniani kutoka 57 mwaka jana, nyuma ya majirani Kenya na Uganda katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Katika ripoti hiyo ya kila mwaka inayoandaliwa na asasi ya kiraia ya kimataifa kutoka Uingereza ya Charities Aid Foundation (CAF), inaonyesha Tanzania imeanguka katika vipengele viwili kati ya vitatu ambavyo hutumika kupima ukarimu wa watu wa nchi husika.

Mwaka jana, Tanzania ilifanya vyema katika utafiti huo katika vipengele vyote vya kumsaidia usiyemjua, kuchangia fedha na kujitolea muda kwa ajili ya kuwasaidia wale wenye uhitaji.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya nane, ni rahisi kwa Mtanzania kukupatia fedha lakini si kupoteza muda wa kukusaidia au kukuhudumia iwapo hakufahamu.

Katika ripoti ya mwaka huu, Tanzania inashika nafasi ya 110 katika kipengele cha kujitolea muda kwa wenye uhitaji na nafasi ya 60 kati ya 138 zilizofanyiwa utafiti duniani katika kipengele cha kusaidia wageni wasiofahamika.

Ni kipengele kimoja tu cha kujitolea fedha ambacho Tanzania imepaa kwa nafasi 13 kutoka nafasi ya 49 mwaka jana hadi nafasi ya 36 mwaka huu ikiwa juu ya Uganda, Rwanda na Sudan Kusini.

Hii ni kinyume cha Kenya ambao wanashikilia nafasi ya pili duniani katika kipengele cha kujitolea muda kwa wenye uhitaji na nafasi ya nne kwa kumsaidia mgeni wasiyemjua. Kenya ni nchi ya tatu duniani kwa ukarimu.

Hata hivyo, ripoti ya utafiti huo uliofanywa mwaka jana inabainisha kuwa, licha ya ukarimu kushuka kwa jumla duniani mwaka jana, bado Afrika imefanya vyema baada ya wastani wa ukarimu kupanda kwa kila kipengele.

“Afrika mwaka huu imeenda kinyume cha mwenendo wa dunia na ndiyo Bara pekee lililoshuhudia kupanda kwa tabia ya kujitolea katika vipengele vyote vitatu itakapolinganishwa na wastani wa ukarimu kwa miaka mitano,” inaeleza ripoti hiyo.

Myanmar ndiyo nchi yenye ukarimu zaidi duniani kwa mwaka wa nne mfululizo ikifuatiwa na Indonesia na Kenya.

Utafiti huo ulifinyika katika nchi 138. Baadhi ya watu walioteuliwa kuwa sampuli waliulizwa ni mara ngapi huwasaidia watu wasiowajua, kuchangia fedha na kujitolea muda wao kwa wasiojiweza ili kupima kiwango cha ukarimu wao.

“Ili kuongeza tabia ya kujitolea miongoni mwa watu duniani, Serikali zote zinatakiwa kuhakikisha asasi za kiraia zinadhibitiwa kwa haki na kwa uwazi, zirahisishe mazingira ya watu kujitolea na kutoa motisha pale inapobidi,” inasema ripoti hiyo.

Ripoti inaeleza, “Serikali pia, zihamasishe uwepo wa asasi za kiraia kama sauti huru za maisha ya watu na kuheshimu haki za taasisi zinazojiendesha pasipo kupata faida kuzungumzia masuala ya msingi ya kitaifa.”

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Tamko la Baraza la Habari Tanzania kuhusu kupigwa risasi Tundu Lissu

$
0
0
Baraza la Habari Tanzania ‘MCT’ limesema limesikitishwa na jaribio hilo la mauaji dhidi ya Mbunge na Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kupitia kwa Katibu Mtendaji Kajubi Mkajanga September 11, 2017 Baraza hilo linaungana na wapenda amani na wadau wa habari na wa haki ya kujieleza na kutoa maoni kulaani kitendo hicho.

==>Isome hapo chini 

Mwanafunzi Aliyenusurika Ajali Lucky Vicent Kutoa Ushahidi Mahakamani

$
0
0
Mwanafunzi   Wilson Tarimo, aliyenusurika katika ajali ya basi iliyoua wanafunzi 32 wa Shule ya Msingi Lucky Vincent ni miongoni mwa mashahidi 15 wa upande wa Jamhuri kwenye kesi inayomkabili mmiliki wa shule hiyo, Innocent Moshi.

Moshi anakabiliwa na tuhuma za makosa ya usalama barabarani ikiwamo kusafirisha wanafunzi bila kuwa na vibali muhimu.

Katika kesi hiyo namba 78 ya mwaka huu, Moshi pamoja na Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo, Longino Nkana, jana walisomewa hoja za awali katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Desderi Kamugisha, Wakili wa Jamhuri, Khalili Nuda, alidai Jamhuri inatarajia kuwa na mashahidi 15 katika kesi hiyo, pamoja na vielelezo 12.

Mashahidi wengine ni Ofisa Kazi Mfawidhi wa Idara ya Kazi Mkoa wa Arusha, Wilfred Mdemi, Mohamed Matumula kutoka Kampuni ya Bima ya Zanzibar Insurance, Songoyi Jilala (askari wa usalama barabarani Arusha), Koplo Hamad (Karatu), Inspekta Shukrani (askari wa usalama barabarani Arusha), Koplo Saada (trafiki Arusha) na E.4312 PC Mugobe (trafiki Arusha).

Wengine ni Mkuu wa Polisi wa Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha (RTO), Nuru Suleiman, G 4130 PC Mwita (askari wa usalama barabarani Karatu), Ignatus Paul(Karatu), Leonidas Gerald (Morombo) na Hamis Omary mkazi wa Sombetini.

Wakili Nuda alitaja vielelezo hivyo kuwa ni kadi ya gari  namba  T 871 BYS, mkataba wa ununuzi wa gari, Barua ya RTO kwenda Sumatra ya Mei 8 mwaka huu, barua ya RTO kwenda Zanzibar Insurance ya Mei 8, mwaka huu na  taarifa ya Zanzibar Insurance ya Mei 9 mwaka huu.

Vingine ni taarifa ya Sumatra ya Mei 9 mwaka huu, taarifa ya idara ya kazi, taarifa ya ukaguzi wa gari, ramani ya eneo la tukio, maelezo ya mshitakiwa wa kwanza na maelezo ya mshitakiwa wa pili.

Wakili huyo aliiomba mahakama hiyo kutoa wito kwa mashahidi hao.

Akiwasomea hoja hizo za awali, Wakili Nuda alidai  katika shitaka la kwanza linalomkabili Moshi, ni kufanya biashara ya usafirishaji abiria bila kuwa na leseni ambapo kati ya Desemba 12 mwaka jana hadi Mei 6 mwaka huu, alitumia gari katika barabara ya umma  aina ya Mitsubishi Rossa T. 871 BYS, kubeba wanafunzi.

Alidai shitaka la pili ni kuruhusu gari hilo kutumika bila kuwa na bima kati ya Desemba 16 mwaka jana na Mei 6 mwaka huu.

Shitaka  la tatu ni kushindwa kuingia mkataba na mwajiriwa wake kati ya Juni Mosi mwaka jana hadi Mei 6, mwaka huu akiwa mmiliki  wa gari hilo alishindwa kuingia mkataba wa ajira kinyume na sheria za ajira na dereva wake, Dismas  Gasper ambaye kwa sasa ni marehemu.

Katika shitaka  la nne, Moshi anadaiwa kubeba na kuzidisha  abiria  13 ambako Mei 6, mwaka huu akiwa Mmiliki wa Kampuni ya Lucky Vincent, katika maeneo ya Kwa Morombo, aliruhusu gari hilo kubeba abiria 38 badala ya abiria 25.

Katika kesi hiyo, Nkama anakabiliwa na shitaka moja ambalo ni kuzidisha abiria katika chombo cha usafiri  ambako akiwa mwandaaji wa safari hiyo ya wanafunzi aliruhusu abiria zaidi ya 13 kupanda katika gari hilo ambalo lilipaswa kuwa na abiria 25.

Baada ya kusomewa maelezo hayo Moshi alikiri gari hilo kwenda Karatu likiwa halina bima huku Mwalimu Mkuu Msaidizi akikiri kuwa alizidisha abiria katika safari hiyo.

Tamko la Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Baada ya Rais Magufuli Kugoma Kuwanyonga Wafungwa

Katibu Mkuu CHADEMA Asimulia Alichohojiwa na Polisi Sakata la Tundu Lissu Kupigwa Risasi

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Vincent Mashinji amehojiwa na polisi kuelezea namna anavyowafahamu watu waliofanya shambulio la risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Akizungumza jana baada ya kutoka katika mahojiano hayo na maofisa wa polisi, Dk. Mashinji alisema maofisa hao walimtaka kuelezea alichowaambia waandishi wa habari katika mkutano wake nao mara baada ya kutokea kwa tukio hilo ambapo alionyesha dalili ya kuwafahamu waliohusika na tukio hilo.

“Niliwataka kurejea kwenye yale mazungumzo ili kuangalia kama nilionyesha dalili ya kuwafahamu watu hao au la.

“Baada ya kuwaambia hivyo walirejea kwenye mazungumzo hayo na kubaini kuwa katika kauli zangu sikuonyesha kama nilikuwa nawajua watu hao bali niliwataka wananchi kufufua polisi jamii ambayo itasaidia kuimarisha ulinzi,” amesema.

Dk. Mashinji amesema kutokana na hali hiyo, maofisa hao wa polisi walitaka kujua kama anazo taarifa zozote kuhusiana na tukio hilo ambapo alijibu hana taarifa hizo ila aliwataka polisi kuhakikisha waliofanya tukio hilo wanakamatwa na kufikishwa kwenye mikono ya sheria.

Mahojiano hayo ya polisi na Dk. Mashinji, yanatokana na wito wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto ambaye alimtaka kiongozi huyo kufika kwenye Ofisi ya Polisi ya Mkoa wa Dodoma au Ofisi ya DCI kwa ajili ya mahojiano.

Siku tano baada ya Lissu kushambuliwa Dodoma, mwingine apigwa risasi Dar

$
0
0
Ikiwa ni siku tano tu zimepita tangu Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake Area D, Dodoma, tukio lingine kama hilo limetokea Dar es Salaam ambapo watu wanaodhaniwa kuwa majambazi wamemshambulia kwa risasi Meja Jenerali Vincent Mritaba.

Tukio hilo limetokea jioni ya September 11, 2017 wakati Meja Jenerali Mritaba akiwa anaingia getini nyumbani kwake Tegeta ambapo alivamiwa na watu wasiojulikana na kupigwa risasi tumboni, begani na mguuni.

Hadi usiku wa jana Madaktari walikua wanaendelea na upasuaji kutoa risasi tatu tumboni na kushughulikia majeraha mengine.

Rais Amtembelea Meja Mstaafu Aliyepigwa Risasi

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 12 Septemba, 2017 ametembelea hospitali ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Lugalo, Jijini Dar es Salaam na kumjulia hali Meja Jen. Mstaafu Vincent Mritaba aliyelazwa hospitalini hapo baada ya kushambuliwa na watu wenye silaha wakati akiingia nyumbani kwake Ununio, Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

Meja Jen. Mstaafu Mritaba alishambuliwa kwa risasi jana tarehe 11 Septemba, 2017 majira ya mchana na kisha kukimbizwa katika hospitali ya Jeshi Lugalo kwa matibabu.

Mkuu wa kituo cha tiba cha hospitali hiyo na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo Brigedia Jenerali Paul Massawe amemueleza Mhe. Rais Magufuli kuwa Meja Jen. Mstaafu Vincent Mritaba anaendelea vizuri baada ya madaktari kufanikiwa kutoa risasi alizopigwa mkononi, kiunoni na tumboni.

Meja Jen. Mstaafu Mritaba amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumjulia hali na kumuombea dua ili apone haraka.

Mhe. Rais Magufuli aliyeongozana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jen. Venance Mabeyo pia ametembea wodi ya majeruhi na kuwajulia hali wagonjwa wanaotibiwa katika wodi hiyo na baadaye akawasalimu wananchi waliofika hospitali hapo kwa ajili ya kupata matibabu.

Mhe. Dkt. Magufuli amewapongeza Madaktari wa hospitali ya jeshi Lugalo kwa huduma za matibabu wanazotoa kwa askari na wananchi wengine na amewahakikishia kuwa Serikali itaendelea kufanyia kazi changamoto mbalimbali zinazowakabili katika utekelezaji wa majukumu yao.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
12 Septemba, 2017

Wabunge WA Upinzani Wagoma tena

$
0
0
Mapema leo Septemba 12, 2017  umetokea mgomo mwingine Bungeni kutoka kwa wabunge wa upinzani wakigomea kuapishwa kwa wabunge wateule wa Chama cha Wananchi CUF.

Huu unakuwa ni mwendelezo wa mgomo ule wa awali Septemba, 5 mwaka huu ambapo wabunge wa upinzani walitoka nje ya ukumbi wa bunge wakieleza kutounga mkono kitendo cha kuapishwa kwa wabunge Saba wa CUF.

Wabunge wa Upinzani hususani wale wanaotoka vyama vinavyounda Ukawa wametoka nje ya Ukumbi wa Bunge leo wakipinga kuapishwa kwa mbunge mmoja wa CUF upande wa Lipumba aliyekuwa amebaki kati ya wale Saba walioapishwa Septemba 5 mwaka huu.

Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA Suzan Lyimo amesema wameamua kutoka nje baada ya kuona 'Order Paper' ikionyesha kuna Mbunge wa CUF anaapishwa.Lyimo amesema wataendelea kususia tukio lolote linalohusisha wabunge hao wapya wa CUF.

Kumekuwepo na mgogoro ndani ya CUF hali iliyopelekea kuwepo kwa makundi mawili moja likiwa ni kundi linalilomuunga mkono Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa vyama vya siasa Profesa Lipumba, huku kundi lingine likiwa ni upande wa Katibu Mkuu wa CUF taifa Maalim Seif.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Spika aagiza Kubenea asakwe, Zitto afikishwe mbele ya kamati

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amemuagiza kutafutwa kwa namna yoyote Mbunge wa Ubungo(Chadema), Saed Kubenea apelekwe kesho kwenye Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama ili ahojiwe kuhusu kauli aliyoitoa ya kumtuhumu Spika kuwa amedanganya idadi ya risasi alizopigwa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema),  Tundu Lissu.

Pia  Spika Ndugai ameagiza Kubenea na Mbunge wa Kigoma Mjini(ACT Wazalendo), Zitto Kabwe kupelekwa katika Kamati ya Bunge ya Maadili na Madaraka kwa tuhuma mbili tofauti                      

Zitto anatuhumiwa kutamka kuwa Bunge limewekwa mfukoni na muhimili fulani, wakati Kubenea ni kwa kumtuhumu Spika kusema uongo wa idadi ya risasi alizopigwa Lissu.

Spika Ndugai ametoa maagizo hayo bungeni mjini Dodoma leo Jumanne.

Katibu Mkuu CHADEMA Asimulia Jinsi Tundu Lissu Alivyo Vunjwavunjwa kwa Risasi

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji amesema mwanasheria mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu ameumizwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili wake na kwamba alipigwa risasi nyingi tofauti na risasi tano zilizoelezwa.

Dk Mashinji amesema Lissu amevunjwa miguu yake, nyonga na mkono wa kushoto, jambo ambalo linawapa madaktari kazi kubwa na kuimarisha afya yake.

Kiongozi huyo amesema jana asubuhi Lissu alianza kusumbuliwa na kifua, jambo lililowalazimu madaktari kumwekea mashine za kumsaidia kupumua, hata hivyo anasema walizitoa baadaye na leo Jumanne ameamka salama.

"Bado najisikia uzito wa kuelezea jamii ya Watanzania hali ya kiongozi wetu Tundu Lissu, najua nina jukumu kubwa kama mtendaji wa chama kutaarifu umma juu ya hali ya Lissu inavyoendelea. Ni majonzi makubwa sana na kama kuna mtu katika taifa hili alifanya hicho kitendo anatakiwa ajitafakari sana. Mpaka jana asubuhi ameenza kupatwa na matatizo ya kifua kutokana na kulala kitandani muda mrefu, na kwa sababu mguu wake wa kulia umevunjwa vunjwa kwa risasi, nyonga yake pia mkono wake umevunjwa kwa risasi lakini 'inshallah' kama nilivyosema awali kuwa Mwenyezi Mungu ndiye anayeamua kuchukua roho ya nani na aache ya nani", amesema Mashinji..

Amesema Lissu ameongezewa damu nyingi akiwa Dodoma na bado anaendelea kuongezewa huko Nairobi. Amesema madaktari wanajitahidi kuokoa maisha yake na kwamba ana imani kwamba watafanikiwa.

"Waswahili wanasema hujafa hujaumbika, kwa kweli wamemuumiza kwa hiyo ndugu zangu hiyo hali ya Lissu jana ilikuwa mbaya mpaka wakamuwekea mipira ya kupumulia lakini ilipofika wakati wa mchana hali yake ilikuwa inaendelea vizuri. Tunasafari ndefu ya kuhakikisha Lissu anapona, sasa hivi wamemtibu zile sehemu za ndani ambazo zingeweza kuhatarisha maisha yake kwa zile risasi zilizopita tumboni na sehemu nyingine", amesema Mashinji.
 
"Mhe. Lissu ni kweli tuliambiwa alipigwa risasi tano katika mwili wake lakini kulingana na hali ya mwili ulivyobomolewa yawezekana zilizidi. Leo ni siku ya tano akiwa anatibiwa hospitali na mpaka sasa hivi ameshafanyiwa oparesheni tatu nadhani itabidi kuzisitisha kidogo ili kumpa ahueni aweze kupumzika na yeye. Tulitegemea ingekuwa suala la kawaida tu yeye kwenda kutibiwa na kurudi lakini imekuwa tofauti. Msilie wala kusononeka kwa sababu Lissu bado yupo hai anaendelea kupigana na sisi, kuhakikisha kwamba anapona na kurudi kuendeleza ukombozi Watanzania ili kufikia uhuru wa kweli na mabadiliko ya kweli", amesisitiza Mashinji.

Kwa upande mwingine, Mashinji amesema wanajiandaa kisaikolojia kumpokea Lissu na hali ambayo atarudi nayo kwa kuwa hiyo ndiyo zawadi waliyopewa na Mwenyezi Mungu.

Mwanasheria Mkuu wa serikali amzungumzia Lissu

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju amefunguka kuhusu sakata la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kupigwa risasi na watu wasiojulikana na kusema kuwa kwa sasa jambo hilo waachiwe polisi na vyombo vya usalama.

Akiongea leo bungeni George Masaju alianza kwanza kwa kutoa pole kwa Mbunge Tundu Lissu kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana na kusema serikali inalaani vikali kitendo hicho alichofanyiwa Tundu Lissu.

"Naomba kutoa pole kwa Tundu Lissu kwa majeraha aliyopata kutokana na kupigwa risasi na watu wasiojulikana sisi kama serikali tunalaani vikali jambo hili, kwa kuwa sasa jambo hili lipo kwa jeshi la polisi, tuviachie vyombo vya usalama naamini watafanya upelelezi kwa haraka" alisema George Masaju

Mbunge Tundu Lissu kwa sasa yupo nchini Kenya akipatiwa matibabu kufuatia kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 mjini Dodoma.

Zitto Kabwe 'Ampa Makavu' Spika Job Ndugai

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Zitto Kabwe amefunguka na kumjia juu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai na kusema kuwa anamsikitikia sana kama haoni jinsi  heshima ya Bunge inavyoshuka.

Zitto Kabwe amesema hayo leo kupitia mitandao yake ya kijamii baada ya Spika wa Bunge Job Ndugai kuagiza na kuwataka wabunge Zitto Kabwe pamoja na Saed Kubenea wa Ubungo kufika kwenye Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge kuhojiwa kutokana na kauli zao ambazo wamezitoa hivi karibuni.

Kufuatia wito huo Zitto Kabwe amesema yeye atafika kwenye kamati hiyo ya maadili na Madaraka ya Bunge kama ambavyo Spika wa Bunge Job Ndugai ameagiza na kusema kuwa spika huyo kama angeweza kujua nguvu yake wala asingehaika na wabunge ambao wanakosoa kwa staha.

"Spika Ndugai anajua ninavyomheshimu kama imefikia haoni heshima ya Bunge inavyoporomoka namsikitikia. Nitakwenda Kamati ya Maadili, Ndugai amekuwa Spika wa kwanza katika historia ya nchi yetu kushuhudia mbunge anapigwa risasi mkutano wa bunge ukiendelea wabunge wazoefu tulikuwa na matumaini makubwa na spika Ndugai tulimpigania dhidi ya njama za kumhujumu kutoka Ikulu anatuangusha angejua nguvu aliyonayo kukabili udikteta unaonyemelea nchi yetu asingehangaika na ukosoaji wenye staha tunaoufanya" alisema Zitto Kabwe

Aidha Zitto Kabwe amesema kuwa Ndugai alitamani kufikia japo robo marehemu Sitta katika kuongoza shughuli za bunge lakini ameshindwa kufikia hata asilimia ya Anna Makinda.

"Kwenye mazishi ya Spika wa watu Mzee Sitta, Ndugai aliomba afike japo robo ya Sitta. Hajafika hata 10% ya Anna Makinda miaka 2 sasa hatujawahi kuwa na Spika anayedhalilishwa na Rais kwamba aliuliza wajumbe gani awaweke Kamati za uchunguzi za Bunge" alisema Zitto Kabwe





Breaking News: Jeshi la Polisi Lakanusha Kutuma Makachero Kumfuatilia Tundu Lissu Nchini Kenya

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Katika siku za karibuni kumejitokeza vitendo vya baadhi ya watu kutumia majina ama picha za watu na kuwahusisha na matukio ya kihalifu au matukio yanayohusiana na uhalifu kwa lengo la kujipatia umaarufu, kuwachafua watu hao au kuwakosanisha na jamii inayowazunguka.

Mnamo tarehe 11.09.2017 kupitia mitandao ya kijamii kulisambaa picha ya askari wa Jeshi la Polisi akihusishwa na muendelezo wa tukio la kujeruhiwa kwa risasi kwa Mhe. Tundu Lissu (MB) ambapo taarifa hiyo ilimtambulisha askari huyo kuwa ni kachero wa Kitengo cha Interpol na kwamba yupo jijini Nairobi nchini Kenya akifuatilia taarifa za Mhe. Lissu.
 
Jeshi la Polisi linapenda kukanusha taarifa hizo kuwa si za kweli na ni za uongo zenye lengo la kumchafua askari huyo na Jeshi la Polisi kwa ujumla. 

Askari huyo hayupo Nairobi kama ilivyoenezwa na picha iliyotumika ilipigwa hapa nchini tarehe 07.01.2017 kwenye sherehe ya mahafali ya mtoto wa kaka yake.

Kuhusiana na safari ya Nairobi, askari huyo alikuwa nchini Kenya kwa kozi ya kimafunzo kuanzia tarehe 04.09.2017 na kurejea tarehe 08.09.2017, huku Mhe. Lissu akipatwa na mkasa wa kujeruhiwa kwa risasi Tarehe 07.09.2017 na kusafirishwa kwenda Nairobi usiku wa kuamkia tarehe 08.09.2017.

Jeshi la Polisi linakemea vikali kitendo hiki chenye lengo la kumharibia maisha yake askari wetu, na linawataka wale wote waliohusika kusambaza au kutajwa katika taarifa hizo kuripoti kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kwa ajili ya mahojiano. 

Vilevile tunatoa onyo kwa wote wanaofikiri kuwa wanaweza kukaa na kupika habari ili waweze kuivuta jamii iwe upande wao na kuchafua upande wa serikali.

Suala hili la Mhe. Lissu lipo chini ya uchunguzi ili kuwabaini wote waliohusika na tukio hili na hatimaye kuwafikisha mahakamani. 

Ni vema wananchi na wanasiasa wakaliacha Jeshi la Polisi liweze kufanya kazi yake bila kuliingilia ili kuweza kupata ukweli wa jambo hili.

Jamii itambue kuwa Jeshi la Polisi linafanyakazi kwa mujibu wa Sheria, kanuni na taratibu za Nchi na kamwe halifanyi kazi kwa kuvizia. 

Endapo mtu yeyote anahitaji taarifa, tunayo mifumo yetu rasmi inayotuwezesha kupata taarifa tuzitakazo kupitia uhusiano tulionao ndani na nje ya nchi.

Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha upelelezi wa makosi ya mitandao (Cyber Crime Investigation Unit) linaendelea na uchunguzi ili kuwabaini wote waliohusika na kusambaa kwa taarifa hizi za uongo ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Jeshi la Polisi linatoa rai kwa wananchi kuacha kutumia mitandao ya kijamii vibaya na badala yake mitandao hii itumike kwa ajili ya kuelimisha na kuihabarisha jamii juu ya masuala mbalimbali ya kimaendeleo.

Imetolewa na:
Barnabas David
Mwakalukwa – ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi 
Makao Makuu ya Polisi.

CHADEMA: Hatuna Imani na Uchunguzi wa Polisi Dhidi ya Tundu Lissu

$
0
0
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara na Wakili wa kujitegemea Tanzania. Prof Abadallah Safari amesema wao kama CHADEMA hawana imani na uchunguzi utakaofanywa na jeshi la polisi au serikali kuhusu shambulio la kujaribu kumuua Mbunge Tundu Lissu.

Akizungumza na wanahabari wakati wakitoa taarifa ya kamati kuu kupitia kikao walichokaa mwishoni mwa wiki iliyopita, Prof. Safari amesema kuwa wao hawana nia mbaya ya kutaka uchunguzi kufanywa na wachunguzi wa mambo ya nje lakini hii ni kutokana jinsi tukio lilivyotokea.

"Hatuna nia mbaya lakini sisi kama CHADEMA hatuna imani na serikali pamoja na jeshi lake la polisi katika uchunguzi wa jaribio la mauaji ya Mbunge wetu. " alisema Prof Safari.

Pamoja na hayo Prof. Safari amedai anamshangaa sana Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini , IGP Simon Sirro, kwa kauli yake ya kwamba Tundu Lissu hakufika kuripoti tukio la kufuatiliwa na watu asiowajua na kusema kuwa huko ni kutojua sheria ya mmwenendo wa makosa ya jinai.

Amesema kuwa Sheria hiyo inaeleeza namna jeshi lapolisi linavyotakiwa kufanya kazi zake na kwamba jeshi la polisi kazi yake ni kufuatilia  na kufanya upelelezi juu ya taarifa kwani wao ni walinzi wa amani na kuongeza kwamba Lissu tayari alieleza kila kitu lakini polisi hawakujali.

"Hatuamini kama walikuwa hawajui kama kuna taarifa Lissu alizitoa kuhusu yeye kufuatiliwa au waliamua tuu kutotilia maanani"  alisisitiza Prof. Safari.

Mbali na hayo Katibu Mkuu wa Chama hicho Dkt. Vicent Mashinji ameeleza kwamba kwa sasa wanachohakikisha ni kwamba hospitali aliyopo Lissu inazidi kuimarishwa ulinzi lakini pia hatoweza kuzungumzia hali yake kwa undani kutokana pia na kuwepo watu wasiokuwa na nia njema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images