Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Hussein Bashe: Amani Imepoteza, Hakuna Aliye na Uhakika na Maisha Yake

$
0
0
Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe amefunguka na kuomba muongozo wa Spika kuhusu hali ya usalama wa nchi, kwa kuwa matukio ambayo yanaendelea kutokea ya kihalifu hayana hitimisho yake.

Bashe amesema hayo wakati akiomba muongozo ndani ya bunge kwa kumtaka Spika wa bunge Job Ndugai kukubali ombi la kamati ya usalama ya bunge likutane na vyombo vya usalama ili yaweze kupatikana majibu ya matukio yanayoendelea kutokea.

"Mhe. Spika katika taifa letu katika kipindi cha muda mrefu kumekuwa yakitokea matukio mbalimbali ambayo sisi kama wawakilishi wa wananchi tuna wajibu wa kupata taarifa sahihi juu ya muendelezo wa matukio hayo ambayo hayana hitimisho", amesema Bashe.

Pamoja na hayo, Bashe aliendelea kwa kusema "sisi tunawawakilisha Watanzania milioni 50 lakini matukio haya yanayotokea yanaharibu heshima ya taifa letu ningekuomba kama utaridhia na wabunge wataniunga mkono, uitake kamati yako ya ulinzi na usalama ya bunge tukufu ikutane na vyombo vya ulinzi na usalama ili tuweze kupata taarifa kamili juu ya mambo haya yanayoendelea katika taifa letu, ili Watanzania na sisi wabunge tuwe na uhakika kwa sababu hali inavyoendelea hakuna mtu mwenye uhakika na maisha yake ya kesho. Dhamana tuliyopewa sisi dhamana ya kusimamia mali, usalama pamoja na raia wa nchi hii", amesisitiza Bashe.

Kwa upande wake Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai alikubali hoja iliyotolewa na mbunge Bashe na kutoa amri  kwa kamati ya ulinzi na usalama ya bunge iende kukutana ili wapange ni jinsi gani ya kulishughulikia jambo hilo na watakapokuwa tayari kabla bunge kuhairishwa siku ya Ijumaa wiki ijayo warudishe majibu kwa bunge juu ya walichoamua.

Gwajima Kumuomea Tundu Lissu

$
0
0
Mchungaji Mchungaji Josephat Gwajima  wa kanisa la Ufufuo na Uzima amefunguka na kusema kuwa siku ya Jumapili atafanya maombezi maalum kwa afya ya Mbunge Tundu Lissu ambaye juzi alipigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa Dodoma nyumbani kwake.

Mchungaji Gwajima amesema kuwa atatumia misa hiyo kulaani vikali kitendo cha kinyama alichofanyiwa Tundu Lissu na watu hao wasiojulikana ambao waliweza kupiga gari lake zaidi ya risasi 30 huku risasi tano ndizo ziliweza kumjeruhi Mbunge huyo.

"Jumapili hii  Septemba 10, 2017 nitaongoza maombi maalumu ya kuombea Afya ya Mhe. Tundu Lissu na kulaani Vikali kitendo cha Kikatili na Kinyama alichofanyiwa. Maombi haya yatafanyika katika Kanisa la Ufufuo na Uzima, Ubungo Dar es Salaam tunawakaribisha wote watakaopenda kuungana nasi katika maombi haya" aliandika mchungaji Gwajima kupitia ukurasa wake wa facebook

Mchungaji Gwajima amekuwa akilaani mambo mbalimbali ambayo huwa yanatokea katika nchi kupitia misa mbalimbali ambazo huwa anafanyia katika kanisa lake hilo ikiwa pamoja na kuombea taifa amani na usalama. 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Septemba 10

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Maneno aliyosema Tundu Lissu baada ya kuzinduka

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa (CHADEMA) Tundu Lissu ambaye anapatiwa matibabu nchini Kenya kufuatia kujeruhiwa kwa risasi na watu wasiojulikana siku Septemba 9, 2017 amezinduka na kutoa neno kwa Mwenyekiti wa CHADEMA.

Katika ujumbe amboa umewekwa na Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa unasema kuwa kiongozi huyo alipopata fahamu aliweza kutoa maneno machache akimtaka Mwenyekiti kuendeleza mapambano.

Tundu Lissu kwa sasa amelazwa nchini Kenya akipatiwa matibabu jijini Nairobi kufuatia kupigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa Makao Makuu ya nchi mjini Dodoma siku ya Alhamis saa saba na nusu 

Waziri Mkuu Atoa Maagizo Mazito Kwa Wakuu wa Mikoa

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewaagiza wakuu wa mikoa 10 inayolima pamba nchini kusimamie zao hilo kwa karibu ili kuinua uzalishaji wake na kuwaongezea kipato wananchi.

Majaliwa alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza na wakuu hao wa mikoa kwenye kikao alichokitiisha mjini Dodoma, kujadili mbinu za kufufua zao hilo.

Wakuu wa mikoa waliohudhuria kikao hicho ni kutoka Shinyanga, Singida, Kagera, Tabora, Morogoro, Mara, Mwanza, Simiyu, Katavi na Geita.

“Serikali imeamua kufufua mazao makuu matano ya biashara ambayo ni pamba, chai, kahawa, korosho na tumbaku na leo (jana) nimetaka nianze na ninyi wakuu wa mikoa ili mwende mkawasimamie watu wenu tunapokaribia kuanza msimu mpya,” alisema.

Majaliwa alisema Serikali imeamua kusimamia kilimo cha pamba kuanzia maandalizi ya shamba, kupanda, matumizi ya pembejeo na dawa, kuvuna na kutafuta masoko na akawataka wasimamie katika maeneo yao ili kilimo cha zao hilo kiweze kubadilika.

“Kama hajafanya kazi hiyo, usiridhike kuwa na ofisa kilimo wa aina hiyo,” alisema Majaliwa na kuongeza:

“Lazima kila mmoja awe na mpango kazi, ausimamie na atoe matokeo ya kuwa zao hili limefanikiwa katika eneo lake. Tunataka zao hili lichukue nafasi yake ya namba moja. Heshima ya “Dhahabu Nyeupe” lazima irudi lakini pia ni vyema mkumbuke kuwa zao la pamba ni uchumi, zao la pamba ni siasa katika mikoa yenu.”

Wakulima wa pamba wamekuwa wakilalamikia bei kubwa ya pembejeo ambazo husambazwa na mawakala, huku wakipewa baada ya mavuno wakipewa bei ambayo hailingani na gharama za uzalishaji.

Pia, wamekuwa wakilalamikia kuuziwa mbegu ambazo hazioti na hakuna fidia ambayo hulipwa.

Serikali Yataifisha Almasi ya Mabilioni Iliyokuwa Inatoroshwa Kwenda Ughaibuni

$
0
0
Almasi zenye uzito wa kilogramu 29.5 za thamani ya zaidi ya Sh bilioni 64, ambazo zilibakiza dakika tano tu kutoroshwa kutoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam (JNIA) kwenda ughaibuni, zimetaifi shwa na serikali.

Aidha, watumishi wa serikali na maofisa wa Mgodi wa Almasi wa Williamson wa Mwadui Shinyanga, waliohusika na uthaminishaji wa awali wa almasi hizo na kudanganya kuwa zilikuwa na uzito wa kilogramu 14 tu, watachunguzwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa akipokea ripoti ya timu ya wataalamu, iliyoundwa kuchunguza upya uzito na thamani halisi ya almasi hizo baada ya kuzikamata katika uwanja huo wa JNIA Agosti 31, mwaka huu.

Uthamini uliofanywa awali kwa almasi hiyo, iliyokuwa mbioni kupakiwa ndani ya ndege kutoroshewa nchini Ubelgiji, ulieleza kuwa ilikuwa na thamani ya chini ya Sh bilioni 32, huku ikielezwa pia kuwa na kilogramu 14, taarifa zilizogundulika kuwa zilikuwa ni za uongo.

Jana Waziri Mpango alipokea maelezo ya almasi hiyo kutoka kwa Kiongozi wa Jopo la Wataalamu waliofanya uthamini mpya, Profesa Abdulkarim Mruma na wasaidizi wake. 

Baada ya kuridhika na maelezo, yaliyodhihirisha kuwepo kwa kiwango cha juu cha udanganyifu kuhusu uzito na gharama za almasi hiyo, kwa lengo la kuliibia taifa, Waziri Mpango aliagiza almasi hiyo yote kutaifishwa, kupigwa mnada na fedha zitakazopatikana kuingia serikalini.

Aliagiza pia kuwajibishwa kwa maofisa wa serikali waliohusika katika udanganyifu huo kwa wahusika hao kukamatwa, kuchunguzwa mali zao ikiwemo majumba, mashamba, magari kuona kama vinaendana na mishahara yao na baadaye kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Alisema, Watanzania wamechoshwa kuona mali zao zikiibiwa kila kukicha huku serikali ikikosa mapato makubwa kutokea katika rasilimali hizo. 

Pia, aliagiza kuandaliwa kwa wataalamu wa madini na wapelekwe kwenye migodi haraka, kukabiliana na wizi wa aina hiyo, huku akivitaka vyombo vya ulinzi na usalama kukabiliana na wizi wa aina hiyo.

Waziri Mpango aliagiza pia upimaji wa madini kufanyikia kwenye eneo la migodi, na pia kununuliwa kwa mashine za kupimia madini kwenye maeneo ya migodi, baada ya kuelezwa na Profesa Mruma kuwa ukosefu wa vifaa vya kupimia ni chanzo cha udanganyifu huo.

“Kazi nzuri sana umefanya Professa Mruma na wenzako na kwa sasa ninaagiza haya madini tuliyokamata hapa, kulindwa kuanzia hapa hadi pale yatakapoingizwa sokoni, pia ninamtaka Gavana wa Benki Kuu (Profesa Benno Ndulu) kuanza kuhifadhi madini ya vito na si fedha peke yake.

“Inashangaza kuona maofisa wa juu wa Wizara ya Nishati na Madini waliokuwa na jukumu la kuthaminisha madini haya wamedanganya huku wale walio chini yao wametoa tathmini ya kweli, sasa huu ndiyo uzalendo unaotakiwa,” aliongeza Dk Mpango.

Kwa upande wa Mgodi wa Williamson Diamond LTD, Waziri Mpango alisema kutokana na kubainika kujihusisha na udanganyifu, huku kampuni hiyo ikieleza kupata hasara kila mwaka, kuanzia mwaka huu itawajibika kutoa gawio serikalini na alimuagiza Profesa Mruma kuijulisha Bodi ya Kampuni hiyo agizo hilo la serikali mara moja.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salam, Lazaro Mambosasa akizungumzia agizo hilo, alisema kuwa hakuna mtuhumiwa ambaye hatoshughulikiwa katika kosa hilo.

Alisema sheria itafuata mkondo na kuwa kila mtu ambaye ameshiriki kwa namna moja au nyingine, atakamatwa kuanzia wale waliopo mgodini hadi wale walioshiriki katika kutaka kutorosha madini hayo.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Polisi Wamsaka Dereva wa Tundu Lissu na Katibu Mkuu wa CHADEMA

$
0
0
Wakati  Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan jijini Nairobi, Kenya, Jeshi la Polisi limemtaka dereva wake, Adam na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Vincent Mashinji kuripoti Polisi Dodoma au Makao Makuu ya Upelekezi Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, SACP, Giless Muroto alisema jeshi hilo linamtaka devera wa Lissu na Katibu Mkuu wa Chadema kuripoti polisi ili kufanya mahojiano nao. 

“Popote alipo dereva wa Lissu, Adam ajitokeze na afike Polisi Dodoma na Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam ili kutoa maelezo kuhusiana na tukio kwani ndiye alikuwa pamoja na majeruhi,” alisema.

Kamanda alisema kitendo cha kutoweka kwa dereva huyo na kujificha ni kosa la jinai na kama kuna mtu au watu wanaomficha, wanatenda kosa la jinai, wamfikishe Polisi mara moja bila kukosa kwa kuwa ni shahidi muhimu katika upelelezi.

Kuhusu Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Mashinji, naye anatakiwa kuripoti kituo cha polisi kutokana na hotuba aliyotoa juzi, ambayo iliwahamasisha wanachama wa chama hicho popote walipo, kuwa wanatakiwa kuchangia damu, kitendo ambacho ni uchochezi, na kinaamsha mshituko katika jamii.

Akizungumzia upepelezi kuhusu Lissu kushambuliwa na risasi kati ya 28 hadi 32 na tano kumdhuru, Kamanda alitoa mwito kwa wananchi kuendelea kuwa watulivu wakati Jeshi la Polisi likiendelea na upelelezi.

Kamanda Muroto alisema Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na timu ya upelelezi kutoka Makao Makuu ya Upepelezi kutoka Dar es Salaam, linaendelea kufanya upelelezi wa kina ili kuwabaini waliohusika na tukio hilo.

“Pia taarifa zimetolewa mapema katika wilaya na mikoa jirani ili kufanya misako na ufuatiliaji kulingana na taarifa zilizopo ndani ya jeshi hilo,” alisema. 

Wakati upelelezi ukiendelea, aliwataka wananchi kuendelea kushirikiana na jeshi hilo kwa kutoa taarifa sahihi ili kufanikisha kuwabaini watu waliohusika na tukio hilo la kumshambulia Lissu na matukio mengine.

Kamanda pia aliwaonya wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii kwa kuandika habari za upotoshaji, uchochezi dhidi ya taasisi za serikali na baadhi ya viongozi wa dola kuhusu tukio hilo, kuacha mara moja.

Alitoa angalizo kwamba wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii, wanatenda kosa kisheria waanze kuchukua tahadhari wasije tumbukia mikononi mwa sheria.

 Aliwataka wale wote wenye taarifa sahihi kuhusu tukio hilo la kushambuliwa Lissu wajitokeze na watoe taarifa kwa Jeshi la Polisi au kwa viongozi wa serikali walipo na taarifa hizo zitafanyiwa kazi ili kukomesha vitendo hivyo.

Aidha alisema jeshi hilo limeyakamata magari manane aina ya Nishani Patrol na yanafanyiwa uchunguzi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na taasisi nyingine kuhusiana na kuhusishwa na tukio la kujeruhiwa kwa risasi Mbunge Lissu.

Lissu ambaye ni Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alishambuliwa kwa risasi Septemba 7, mwaka huu saa 7.30 Area D katika maghorofa ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) katika Manispaa ya Dodoma.

Uchunguzi wa awali kuhusu tukio hilo, ambalo watu walioshambulia hawajulikani, Kamanda Muroto alisema unaonesha kuwa wahalifu walikuwa na silaha ya SMG/SAR kutokana na maganda ya risasi yaliyokutwa eneo la tukio.

Lugumi Apoteza Nyumba ya Kwanza......Magorofa Mawili Yakoa Wanunuzi

$
0
0
Kampuni ya udalali ya YONO  imesimamia shuguli za kuuzwa kwa mnada gorofa lililopo upanga mali ya kampuni ya Lugumi Enterprises Limited na kununuliwa na kampuni ya Al-Naeen Enterprises kwa shilingi Milioni 700.

Mnada huo wa magorofa hayo na majengo mengine mawili  ambayo yamekosa wateja kutokana na bei zake kuwa juu ukilinganisha na ukubwa wa jengo bado hayajapatiwa wateja.

Akizungumza wakati wa mnada huo, Mkurugenzi wa kampuni ya YONO Scolastica Kevela amesema kuwa Nyumba ambazo zimekosa wateja zinauzwa Shilingi Milioni 460 na zinapatikana eneo la Mbweni JKT Wilaya ya Kinondondi jijini Dar es Salaam.

Kampuni ya Lugumi Enterprises Limited inahusishwa na kashfa ya ubadhirifu wa fedha za serikali pamoja na kudaiwa kodi na TRA masuala ambayo yamepelekea kuuzwa kwa majengo hayo na kulipia kodi TRA.

Ma IGP Wastaafu Wampa Mbinu Mpya Kamanda Sirro

$
0
0
IGP Simon Sirro amefunguka na kusema kuwa viongozi wastaafu wa jeshi la polisi nchini wamempa ushauri namna ambavyo anapaswa kuendesha jeshi hilo na kudai viongozi hao wameona mapungufu mbalimbali ndani ya jeshi hilo ambayo yanatakiwa kufanyiwa kazi.

Akiongea na waandishi wa habari IGP Sirro jana baada ya kumaliza mkutano na wastaafu hao alisema mambo kadhaa ambayo alishauriwa na viongozi hao ambayo jeshi la polisi linatakiwa kulifanyia kazi.

"Jambo kubwa ambalo walikuwa wanasisitiza ni suala la weledi kwamba wanapokuwa kule wanatuangalia sisi ambao tuko jeshini tunahudumia Watanzania wanaona kuna mapungufu katika baadhi ya utendaji wa askari wetu, kwa hiyo walikuwa wanasisitiza sana katika suala la weledi, lakini la pili viongozi hawa wanazungumzia sana suala la mafunzo kwamba kila askari anapaswa kuwa na mafunzo mbalimbali" alisema IGP Sirro

Baadhi ya maafisa wastaafu wa jeshi la polisi walioshiriki katika kikao hicho ni pamoja na IGP Mstaafu Ernest Mangu, saima Mwema, Omari Maita pamoja na makamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam Suleman Kova na Afred Tibaigana

Msigwa Ampinga IGP Sirro Sakata la Tundu Lissu Kupigwa Risasi

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini (CHADEMA) Mchugaji Peter Msigwa amefunguka na kuonyesha kutoridhishwa na kauli ya  Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Nyakoro Sirro kusema Tundu Lissu hakuwahi kutoa taarifa juu ya watu wanaomfuatilia.

Mbunge Msingwa ambaye sasa yupo nchini Kenya kwenye matibabu ya Tundu Lissu ameonyesha kusikitiswa na taarifa hiyo ya IGP ambayo aliitoa Septemba 8, 2017 katika mkutano wa waandishi wa habari na kusema kiongozi huyo hakuwahi kutoa taarifa yoyote polisi juu ya gari ambalo lilikuwa likimfuatilia kabla ya kupatwa na shambulizi hilo la kupigwa risasi.

"Kamanda Sirro Ulitaka Lissu atoe taarifa gani zaidi? Sisi wengine ni wanasiasa, hatuna mafunzo ya kijeshi, Polisi wala Kikachero. Silaha yetu kubwa ni kipaza sauti (microphone), kazi yetu ni kupaza sauti , hoja inapaswa kujibiwa kwa hoja! Siyo kwa mabomu ya machozi, sio kwa virungu na bunduki. Inaonyesha jeshi letu la polisi uwezo wake mkubwa ni kupambana na vyama vya siasa hasa CHADEMA na CUF kuwalinda wakuu wa wilaya na mikoa" aliandika Mchungaji Msigwa

Aidha Msigwa anasema anaumia kuona Tundu Lissu akiteseka kwa ajili ya kutetea haki na Demokrasia ya taifa la Tanzania na kusema alichofanyiwa Tundu Lissu kinampa ujasiri wa kusonga mbele.

"Mungu anakataza kumwaga damu isiyo na hatia! machozi yanitoka kuona rafiki yangu Tundu Lissu akiteseka kwa kutetea  haki na demokrasia ya taifa letu, amewakosea nini? Inanipa ujasiri wa kusonga mbele, sitanyamaza, tunakupenda Lissu wewe ndiye shujaa wetu" aliandika Msigwa 

Askofu Gwajima Awashangaa Viongozi wa Dini Kufumbua Maovu Yayoendelea Nchini

$
0
0
Mchungaji Mchungaji Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima amefunguka na kudai anawashangaa viongozi wa kiroho wanaokaa kimya na kuacha masuala ya uhalifu yakiendelea katika nchi bila ya kusema lolote juu ya hilo.

Mchungaji Gwajima amesema hayo akiwa Kanisa kwake leo Jumapili ambapo aliahidi kumfanyia ibada maalum ya kumuombea mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu baada ya kupigwa risasi na watu wasiofahamika akiwa nyumbani kwake Dodoma siku za hivi karibuni.

"Naona huruma sana kwa watu wanaofanya uhalifu katika nchi kwa sababu unapomwaga damu ya mtu na wewe yako itamwaga na mwingine bila ya kujarisha umemwaga kwa sababu zipi. Damu imekuwa ikimwagika sana katika nchi hii kuanzia kule Kibiti. Nashangaa sijui imekuwaje viongozi wa kiroho walikuwa kimya, mimi sikuwepo. Viongozi wa kiroho ni lazima waseme", amesema Gwajima.

Aidha, Mchungaji Gwajima katika maombi yake amewataka watu wanaofanya vitendo vya uhalifu nchini wafanye hima kutubu dhambi zao juu ya wanachokifanya na endapo hawatafanya hivyo basi watambue yatawafika yale yale ambayo walikuwa wakiwatendea wenzao.

"Mambo ya kiuhalifu tunatakiwa kuyakemea bila ya kuwa na uoga wa aina yeyote wala kuangalia upande wowote ule na hivyo ndivyo Mungu anavyotaka, unasema unachotakiwa kusema kama hiki hakipo sawa. Tundu Lissu ana baba, mama, watoto pamoja na mke anatakiwa kuishi", amesisitiza Gwajima.

Kwa upande mwingine, Gwajima amesema hakuna jambo baya kama kuwepo katika nchi halafu hutambui inaeleka wapi.

Rais Magufuli ateua Jaji Mkuu wa Tanzania

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 10 Septemba, 2017 amemteua Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Uteuzi huu unaanza leo tarehe 10 Septemba, 2017.Kabla ya uteuzi huo Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amechukua nafasi ya Mhe. Jaji Mstaafu Mohamed Chande Othman ambaye amestaafu.

Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma ataapishwa kesho tarehe 11 Septemba, 2017 saa 4:00 Asubuhi, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
10 Septemba, 2017

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Septemba 11


Tamko la Maaskofu kuhusu kushambuliwa kwa Tundu Lissu

$
0
0
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), limelaani shambulizi la hivi karibuni lililotekelezwa na watu wasiojulikana dhidi ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Mbunge huyo aliyejeruhiwa Septemba 7 kwa kupigwa risasi tano mjini Dodoma, hivi sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan, jijini Nairobi nchini Kenya.

Baraza pia limeungana na Watanzania kulaani kwa nguvu zote matendo yote ya vurugu, mauaji na uvunjifu wa amani nchini.

Tamko la baraza hilo lililosainiwa na Makamu wa Rais wa TEC, Askofu Beatus Kinyaiya limetolewa baada ya kikao cha kawaida cha baraza kilichofanyika kwa siku mbili Septemba 9 na 10 jijini Dar es Salaam.

“Katika Taifa letu sasa tunashuhudia matendo ya mauaji ya watu wasio na hatia kama ilivyokuwa kule Mkuranga, Rufiji na Kibiti, utekwaji wa watu na kuteswa, utekaji wa watoto, ulipuaji wa ofisi za watu na hivi karibuni shambulio la mbunge Lissu,” limesema baraza katika tamko hilo.

Imeelezwa vurugu na mashambulizi ya aina yoyote ile yanalifedhehesha Taifa kwa kuwa matendo hayo ni dhambi, uhalifu na si utamaduni wa Mtanzania, hivyo vyombo vinavyohusika havina budi kuyakomesha mara moja.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya Septemba 12

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0
Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Mwili wa mtoto waokotwa mferejini Arusha

$
0
0
Mwili wa mtoto ambaye anakadiriwa kuwa na umri wa siku moja umeokotwa kwenye mfereji wa kupitisha maji machafu katika eneo la Mtaa wa Ali Nyanya kata ya Ungalimited jijini Arusha.

Kichanga hicho kimeonekana kutekelezwa na mama yake mzazi mara tu baada ya kujifungua na kupelekea kupoteza maisha, baadhi ya wananchi wa eneo hilo wamelaani kitendo hicho cha kinyama na kikatili kinachofanywa na baadhi ya wanawake wasiokuwa na hofu ya Mungu ndani yao ambao wanakatisha uhai wa watoto hao ambao hawana hatia.

Mwenyekiti wa Mtaa huo Omari Shehe naye amelaani kitendo hicho na kuahidi kushirikiana na vyombo vya dola kuhakikisha wanamtafuta muhisika ambaye amefanya tukio hilo la kinyama ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia hizo za kufanya uovu na ukatili huo.

Vitendo vya watu kutekeleza watoto vimekuwa vikishamiri katika maeneo mbalimbali ya nchi huku wengi wakionekana kufanya ukatili huo kutokana na baadhi ya wanaume kukataa watoto au ujazito jambo ambalo hata hivyo halikubaliki.

Waziri Mkuu Atoa Msaada Wa Sh. Milioni 10

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa msaada wa sh. milioni 10 ili kumuwezesha Bw. Ernest Masenga kutatua changamoto zinazomkabili.

Bw. Masenga alikuwa msanii wa muziki wa dansi ambaye sasa anasumbuliwa na maradhi ya miguu. Pia makazi anayoishi si salama yanahitaji kukarabatiwa.

Waziri Mkuu ametoa msaada huo jana (Jumatatu, Septemba 11, 2017) katika makazi ya Waziri Mkuu Oysterbay jijini Dar Es Salaam.

Ametoa msaada huo baada ya kuguswa na hali ya maisha ya msanii huyo aliyemuona kupitia kipindi maalumu kilichoonyeshwa na TBC Sempemba, 5, 2017. Kipindi hicho kiliongozwa na Bw. Godfrey Nago.

“Nawaomba Watanzania wenzangu tumsaidie mwezetu ili aweze kuishi vizuri kwa sababu sanaa yake imesaidia katika kuelimisha na kuburudisha umma .”

Kwa upande wake Bw. Nago ambaye amepokea msaada huo kwa niaba ya Bw. Masenga amesema atahakikisha anasimamia vizuri fedha hizo ili zitumike kama ilivyokusudiwa.

Pia Bw. Nago amesema anamshukuru Waziri Mkuu kwa kuwaunga mkono na kutoa msaada huo kwa sababu ameonesha kwamba Serikali inawajali wananchi wake na TBC itaendelea kuwaomba wadau mbalimbali wajitokeze na kumsaidia msanii huyo.

Naye Mjomba wa msanii huyo Bw. Kanuti Mloka ambaye ameiwakilisha familia amemshukuru Waziri Mkuu kwa msaada huo kwa kuwa familia imeshindwa kumsaidia Bw. Masenga kutokana hali duni ya maisha waliyonayo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, SEPTEMBA 11, 2017.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images