Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Viongozi wanne wa Chama cha Wananchi CUF Wafariki baada ya kupata ajali usiku wa kuamkia leo

$
0
0
Watu watatu wamefariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa baada ya gari aina ya Toyota Noah kugongana na lori eneo la Ubena Zomozi mkoani Pwani usiku wa kuamkia leo.

Naibu mkurugenzi wa ulinzi na usalama wa CUF, Masoud Mhina akizungumzia ajali hiyo, amesema waliokufa ni wanachama wa chama hicho mkoani Tanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga amesema ajali hiyo ilitokea saa 8:30 usiku wa kuamkia leo Septemba 6 baada ya Toyota Noah lililokuwa likitokea Dodoma kuhama njia na kugongana na lori.

Lyanga amesema lori hilo lilikuwa likiendeshwa na Yassin Hamad mkazi wa Dar es Salaam.

Amesema waliokufa katika ajali hiyo ni Uledi Salumaa (32) ambaye alikuwa dereva wa Toyota Noah, Mary Komba (40) na mwingine aliyetambuliwa kwa jina moja la Isack, wote wakazi wa Muheza mkoani  Tanga.

Kamanda Lyanga amewataja majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni Juma Nindi, Chausiku Hassan na Esther Masie ambao pia ni wakazi wa Muheza.

Amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Tumbi mjini Kibaha na majeruhi walipelekwa kwa matibabu katika Kituo cha Afya Chalinze.

Kamanda Lyanga ametoa wito kwa madereva kuacha kuendesha kwa mwendo wa kasi na hasa usiku kwa kuwa madhara yake huwa makubwa.

“Niwatake madereva wote wanaoendesha magari usiku, ukijihisi umechoka weka gari pembeni pumzika. Ukilazimisha utakuwa kama huyu ambaye alihama upande wake na kugongana na lori,” amesema.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Raila Odinga kugoma kushiriki uchaguzi wa marudio Kenya

$
0
0
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raia Odinga amesema kuwa hatoshiriki katika uchaguzi mkuu wa marudio uliopangwa kufanyika Oktoba 7 mwaka huu kama michakato muhimu ya kikatiba na kisheria haitawekwa sawa.

Raila Odinga alisema mbali na michakato hiyo ambayo hakuiweka bayana alisema pia lazima mabadiliko ndani ya Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC) yafanyike ili kuondolewa kwa maafisa ambao walisababisha kuharibika kwa uchaguzi mkuu uliopita.

“Tunajua ambacho tume ya uchaguzi ilifanya, ndio sababu tunasema kuwe na mabadiliko kwani tukirudia uchaguzi na watu hao hao matokeo yatakuwa yale yale,”  alisema Odinga.

Mapema juma lililopita Mahakama ya Juu nchini Kenya ilitangaza kuwa uchaguzi mkuu wa Agosti 8 ni batili kutokana na kukumbwa na kasoro nyingi.

Katika uchaguzi uliopita, Rais Kenyatta alitangazwa mshindi kwa kupata 54%  huku akifuatiwa na Odinga aliyepata 45%.

Akizungumza na waandishi wa habari Odinga alisema kuwa, uchaguzi wa marudio unatakiwa kufanyika katika mazingira ambayo kila kilichokosewa katika uchaguzi uliopita kitaweza kurekebishwa.

Jumatatu Tume ya Taifa ya uchaguzi nchini Kenya ilitangaza kwamba uchaguzi mpya wa urais nchini humo utafanyika tarehe 17 Oktoba, 2017.

Mwenyekiti wa tume, Wafula Chebukati alisema uchaguzi huo utashirikisha wagombea wawili pekee wa urais, Rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga.

Taarifa mpya ya Tume ya Uchaguzi Kenya kuhusu Uchaguzi wa marudio

$
0
0
Muda mfupi  baada ya kiongozi wa upinzani Kenya Raila Odinga kutangaza kutoshiriki katika marudio ya Uchaguzi Mkuu mpaka Tume ya Uchaguzi ifanyiwe mabadiliko, Tume hiyo imetangaza kundi la watu sita ambalo litasimamia uchaguzi huo.

Walioteuliwa ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo Ezra Chiloba, Naibu wake Betty Nyabuto, Mkurugenzi wa Usajili wa wapiga kura pamoja na Mkuu wa Operesheni za Uchaguzi Immaculate Kasait, Naibu wake Mwaura Kamwati, Mkuu wa Operesheni za Tume na Mkuu wa Teknolojia James Muhati.

Uchaguzi wa marudio Kenya umepangwa kufanyika October 17, 2017 kutokana na ruhusa ya Mahakama ya Juu nchini humo kufuatia kesi ya kupinga matokeo iliyofunguliwa na Odinga.

Breaking News: CCM Yamvua Udiwani Yusuf Manji

$
0
0
Mfanyabiashara Yusuf Manji amepoteza sifa ya kuwa Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu kutokana na kutohudhuria vikao zaidi ya sita na vikao vya kamati vya maendeleo ya halmashauri ya Temeke zaidi ya vitatu.

Meya wa Manispaa ya Temeke, Abdallah Chaurembo amesema hayo leo Jumatano katika mkutano na waandishi wa habari.

Kutokana na hilo wamemuondoa Manji kwenye nafasi hiyo kutokana na kukosa sifa

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhanisi ya Septemva 7

Kimenuka Tena......Ripoti ya Madini ya Tanzanite Yaibua UOZO Mzito Ukiwahusisha Mawaziri wa Sasa na Wa Zamani

$
0
0
Uko uwezekano mkubwa wa Baraza la Mawaziri kutikisika baada ya mawaziri kadhaa waliopo na wale walioondolewa kutajwa mara kadhaa katika taarifa za kamati maalumu za bunge kuchunguza biashara ya Tanzanite na almasi.

Aidha taarifa zote mbili ziliwataja kwa majina watu kadhaa wakiwemo mawaziri waliopo katika baraza la sasa kwa kujihusisha moja kwa moja katika maamuzi yaliyopindisha sheria na kukiuka utaratibu.

Kamati zote mbili zilizungumzia kwa undani hasara kubwa zilizopatikana kutokana na ushauri mbovu na usimamizi dhaifu katika mkataba wa kuuza hisa katika kampuni ya almasi mwaka 1994 ambao hazikusaidiwa na pia ubia wa Stamico na Tanzanite One Mining Limited (TML) ambapo unaelezwa uliharakishwa na Waziri George Simbachawene.

Pia, Stamico ilionekana kutofuatilia mikataba yote huku baadhi ya watendaji wa sasa wakibariki ubia huo na kusema kwamba ulikuwa ni msaada mkubwa kwa Stamico. 

Pia imeelezwa kuwa hakuna taarifa sahihi kuhusu uzalishaji na uuzaji wa tanzanite ingawa duniani mauzo ni dola trilioni 8.582 katika miaka 12 iliyopita huku takwimu za Tanzania zikionesha kwamba mauzo ni bilioni 454 tu kwa kipindi hicho.

Imeelezwa kuwa ni asilimia 20 ya uuzaji wa tanzanite unajulikana nchini lakini 80 husafirishwa kwa njia ya panya.

 Aidha, katika uchunguzi uliofanywa na kamati hizo ulibaini kwamba baraka zilizotolewa kwa Sky zilikuwa kinyume kwani kampuni hiyo haina usajili nchini wala haitambuliki brela.

Waziri mkuu anena 
Taarifa za kamati maalumu za Bunge zilikabidhiwa jana kwa Spika wa Bunge kabla ya yeye naye kukabidhi kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye naye alisema kwamba anazifikisha kwa Rais John Magufuli leo saa nne na nusu kwa hatua zaidi.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa hizo Waziri Mkuu alishukuru kazi njema iliyofanywa na kamati hizo na kuahidi kwamba yote yaliyozungumzwa yatafanyiwa kazi katika kipindi kifupi kijacho.

Alisisitiza kuwa serikali ya awamu ya tano kamwe haitamwacha mtu ambaye anakiuka katiba kwa kuacha kulinda maliasili za taifa huku akikariri Ibara ya 27 ya katiba ya mwaka 1977 kama muhuri tosha kwa kila Mtanzania.

“27 (1) kila mtu ana wajibu wa kulinda mali asilia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mali ya Mamlaka ya Nchi na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na Wananchi na pia kuiheshimu mali ya mtu mwingine.

“(2) Watu wote watatakiwa na Sheria kutunza vizuri mali ya Mamlaka ya nchi na pamoja vita aina zote za uharibifu na ubadhilifu na kuendesha uchumi wa Taifa na kuendesha uchumi wa taifa kwa makini kama watu ambao ndiyo waamuzi wa hali ya baadaye ya taifa lao.” Alisema serikali itaendelea na jitihada za kuleta mageuzi katika madini ili rasilimali hizo zinufaishe Watanzania wote.

Pamoja na hatua za haraka kuchukuliwa alisema kwamba sheria ya madini, petrol, kodi ya mapato zitafanyiwa marekebisho ili kuimarisha mifumo ya kusimamia madini na rasilimali nyingine za taifa.

Alisema ni lazima kuchukua hatua kali kwa wahusika wote na kuwataka Watanzania kwenda pamoja katika vita hiyo iliyoanzishwa na Rais John Magufuli. 

Mmoja wa mawaziri aliyetajwa mara kadhaa kwa ni George Simbachawene ambaye kwa sasa ndiye Waziri katika Ofisi ya Rais Tamisemi ambaye alishawahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini. 

Waziri huyo alitajwa kuhusiana na biashara ya Tanzanite ambaye aliridhia mabadiliko katika mauzo ya kampuni uchimbaji Tanzanite na utoaji wa leseni kinyume na utaratibu.

Aidha Naibu Waziri Edwin Ngonyani naye ametajwa hasa kuhusiana na kadhia ya kuzuia serikali kununua mgodi wa almasi kwa dola milioni 10 na kuikosesha serikali zaidi ya dola milioni 300, fedha ambazo zilienda kwa kampuni iliyonunua hisa.

 Aidha kamati hiyo ilihoji namna ambavyo walioshiriki kukataa serikali kununua mgodi huo wa almasi walivyopata bahati ya kuchaguliwa katika bodi ya waliouziwa hisa.

Aidha taarifa zote mbili zimehoji tabia iliyooneshwa na watendaji mbalimbali wa kutochukua maamuzi na kuishia kusema kwenye mahojiano kwamba waliona ni upuuzi na wizi mtupu kuendelea kufuatia masuala ya ndani yanayogusa mikataba na uendeshaji.

Kitendo cha Eliakim Maswi kusema kwamba alipatwa na hasira baada ya kutoka katika mgodi huo wa almasi na kujionea madudu na kuapa kutokanyaga tena kulielezwa na kamati hizo kuwa moja ya sababu ya watendaji kuacha mambo yakiharibika.

Aidha aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo alitajwa kupindisha mambo kadhaa na kufanya maamuzi bila kushirikisha bodi zinazotakiwa na hivyo kusababisha hasara kubwa.

Watu wengine waliotajwa katika taarifa zote mbili ni pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu Nishati na Madini, Eliakim Maswi, aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngereja, mwanasheria wa zamani George Werema

Pamoja na kuelezwa kuwa serikali imepata hasara ya matrilioni kutokana na mikataba mibovu, na kukosekana kwa uaminifu miongoni mwa watendaji na watumishi wa umma, pia kuna makampuni yanachimba almasi na kuuza bila kufuata utaratibu. Makampuni yaliyotajwa ni matatu yakiwemo Caspian na Midwest.

Mikataba iliyozungumzwa na kuambiwa ina walakini mkubwa ni pamoja na umiliki wa Mwadui na mkataba wa Stamico na Tanzanite One Mining Limited, mkataba ambao ulizaa migogoro ya madeni makubwa kwa upande wa Stamico na kuiacha ikiwa hoi na deni la dola milioni 4. Spika Job Ndugai alisema kutojipanga kwa watu wa Stamico kumefanya kampuni hiyo kuingia katika hasara kubwa huku sera zikiwa hazifuatwi wala sheria.

Ukiukaji wa kitaasisi Kuwepo kwa ukiukaji wa taratibu na kanuni za kitaasisi na kiutendaji pia zilielezwa kutoa mwanya wa kampuni ndani ya mgodi wa almasi wa Mwadui kufanya wanachotaka, huku takwimu za uzalishaji na mauzo za TMA na Wizara ya Nishati na madini zikipishana.

Aidha hata akiba ya almasi iliyopo imeelezwa kuwa si ya uhakika kutokana na serikali kutojua akiba hiyo ikitegemea taarifa zaidi kutoka kampuni ya Mwadui ambayo kwa muda sasa wanasema wametengeneza hasara na hivyo kutolipa kodi Kampuni ya Mwadui imekuwa hailipi kodi kuanzia mwaka 2007 hadi 2017 kwa kisingizio kwamba wamepata hasara, hali ambayo haiendi sambamba na uwekezaji mkubwa unaoendelea hadi mwaka 2023.

Kamati ilisema usahihi wa takwimu ndiyo msingi wa kufanya biashara, lakini wakati Williams wanazo takwimu na wanazitumia taasisi za serikali na serikali yenyewe takwimu zake zinagongana huku nyingine zikionekana ‘kupikwa’ kutokana na kuwiana wakati sheria na muda ni tofauti.

Aidha takwimu hizo zimekuwa haziendi kwenye uhalisia wa kipindi cha sheria na maagizo ya kisheria yaliyopo. Tofauti kubwa inayooneshwa katika takwimu za wizara na taasisi ya TMAA za uzalishaji na pia na TRA katika mauzo.

Katika maelezo yote kamati ya Zungu ilihoji fedha kiasi cha Sh bilioni 7 na milioni 700 ambazo hazijaingia serikalini wakati inajulikana pia kwamba almasi ya Tanzania ndiyo ghali lakini inauzwa kwa bei ya kutupwa katika soko.

Aidha kumezuka sintofahamu ya akaunti ya mrabaha kutoka kampuni ya almasi ambapo inadaiwa ilifunguliwa akaunti NMB ambayo hata katibu mkuu alikuwa haifahamu, huku suluhu ya kibenki ikiwa haitumiki kuoanisha takwimu za mapato.

“Mrabaha wa bilioni 100 ulivyopokelewa na kuhamishwa katika kaunti haueleweki,” inasema taarifa hiyo ikionesha kuwapo na ubadhirifu mkubwa wa fedha kutokana na kukosekana kwa uwajibikaji na ufuatiliaji.

Pamoja na mikataba mibovu kuna shida ya uangalizi wa almasi yenyewe ambapo hata watendaji wa serikali (walinzi) hawapo katika maeneo nyeti kama katika x ray na chumba maalumu cha hifadhi; huku Williamson wakiuweka mgodi wa almasi rehani kufuatia madeni ambayo kiukweli hayajapitishwa wala kuhakikiwa na Benki Kuu kwa mujibu wa sheria.

Kwa mujibu wa taarifa za takwimu Tanzania kwa namna ilivyo sasa imeweka rehani almasi yenye thamani ya trilioni 80 na milioni 800. Ilielezwa kuwa kuna deni la dola milioni 238 ambalo halijahakikiwa na benki kuu wala halijulikani limefikia hapo kwa namna gani ni muhimu kuangaliwa.

Ushauri wa kamati Kwa upande wa kamati ya Dk Bitego iliyochunguza tanzanite kuna haja ya kuwawajibisha wote waliohusika kuliingiza taifa hili katika mikataba mibovu isiyokuwa na tija na kuleta hasara.

Aidha wametaka watumishi waliotajwa wote kuhojiwa tumefikaje hapa huku wakitaka kutungwa sheria maalumu kuhusiana na madini hayo yanayopatikana Mererani pekee duniani kote.

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli anapokea taarifa hiyo ya uchunguzi wa madini kutoka kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, Ikulu Dar es Salaam leo.

Aliyeongoza kamati ya Makinikia akumbwa katika kashfa ya Almasi na Tanzanite

$
0
0
Wakati kumbukumbu za ripoti za uchunguzi wa usafirishaji wa mchanga wa madini (makinikia) nje ya nchi zikiwa bado zinawatafuna watanzania walio wengi kuhusu hatma ya nchi yetu katika sekta ya madini baada ya taarifa kuonyesha tumeibiwa sana, kidonda hicho kimetonyeshwa upya jana  baada ya kamati mbili za bunge kuwasilisha ripoti kuhusu biashara ya madini ya Almasi na Tanzanite.

Kamati ya iliyochunguza biashara ya madini ya Almasi imeongozwa na Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu huku Kamati ya Tanzanite ikiongozwa na Mbunge wa Bukombe, Doto Mashaka Biteko.

Wakati wenyeviti wa kamati zote wakiwasilisha ripoti zao mbele wa Spika wa Bunge na viongozi wengine waandamizi wa serikali na vyombo vya ulinzi, wameonyesha namna serikali inavyopata hasara kutokana na kusainiwa kwa mikataba mibovu, rushwa, biashara za kupendeleana, maamuzi ya kukurupuka lakini pia na uzembe wa viongozi walioaminiwa kulinda rasilimali hiyo adimu.

Moja ya jambo lililowashtua watu wengi na pengine kuleta mfadhaiko, ni baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Almasi, Mussa Azzan alipokuwa akieleza moja ya sababu zilizosababisha serikali kupata hasara na kubambikiwa madeni ni kiongozi aliyekuwa akihusika na uhakiki wa madeni hayo kutokuwa makini.

Zungu alisema, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ukaguzi wa Madini Nchini, Profesa Abdulkarim Hamis Mruma amelisababishia taifa hasara kwa kuruhusu madini yapotee kwa uzembe.

Prof. Mruma ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kwanza ya Makinikia iliyoundwa na Rais Magufuli alipohojiwa sababu za kusababisha hasara hiyo na serikali kubambikiwa madeni ambayo si halali alisema, nyaraka hizo za madini alizisaini bila kusoma.

Kamati ilipohoji kwanini kiongozi wa ngazi ya juu kama yeye anasaini nyaraka bila kuzisoma alisema kuwa alikuwa ametingwa na kukosa muda wa kusoma ripoti zilizoletwa kwake, lakini pia alikuwa anawaamini waliokuwa wakizileta ndio sababu hakusita kuzisaini.

Prof. Mruma alijizolea sifa nyingi alipowasilisha ripoti ya uchunguzi wa makinikia ambapo yeye na wajumbe wengine wa kamati walikuwa wakichunguza aina  ya madini iliyokuwa katika mchanga huo. Katika ripoti yake alionyesha namna taifa linavyopoteza matrilioni fedha kutokana na usafirishwaji wa mchanga wa madini nje ya nchi.

Wengine walionaswa na kamati hizo ni waliokuwa Mawaziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. Muhongo na William Ngeleja ambao wao kwa nyakati tofauti inadaiwa walitoa leseni za uchumbaji madini kwa kampuni mbalimbali mfano Tanzanite One kinyume na sheria.

Aakieleza zaidi Zungu alisema, kuna leseni moja ya madini ambayo serikali ilishauriwa na kamati nyingi kutoitoa, lakini Prof. Muhongo siku chache baada ya kuingia madarakani alitoa leseni hiyo.

Mwingine anayetuhumiwa kuisababishia serikali hasara ni pamoja na Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Edwin Ngonyani wakati akifanyakazi katika Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) ambapo kamati imeeleza kuwa alishindwa kusimamia wajibu wake vizuri na kulisababishia taifa hasara.

Aidha, miongoni mwa mapendekezo yaliyotolewa na kamati hizo, ni serikali kuwachukulia hatua watumishi wote waliohusika kwa namna moja ama nyingine katoka kulisababishia taifa hasara.

Lakini pia kamati zimependekeza kupitiwa kwa mikataba ya kampuni za uchimbaji madini kwani biashara hiyo imekumbwa na rushwa na uongo, hali inayosababisha serikali kupata hasara.

Rais Magufuli akutana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Chakula Duniani

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Chakula Duniani (FAO) Bw. Jose Graziano da Silva amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Shirika hilo lipo tayari kushirikiana na Tanzania kufanya mageuzi katika kilimo kwa kuwezesha uzalishaji wa mazao na viwanda vya mazao hayo.

Bw. Jose Graziano da Silva amesema hayo jana tarehe 06 Septemba, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya kufanya mazungumzo na Mhe. Rais Magufuli na kumshukuru kwa ushirikiano mzuri ambao shirika hilo limeupata kwa kipindi cha miaka 40 ya uwepo wake hapa nchini.

Akitoa mfano wa nchi yake ya Brazil Bw. Jose Graziano da Silva amesema Tanzania inaweza kupata manufaa makubwa ya kuongeza uzalishaji wa chakula, kuuza nje ya nchi, kuzalisha ajira na kukuza pato la Taifa kupitia mapinduzi yatakayotokana na kuunganisha kilimo na viwanda vikiwemo vya kusindika nyama na samaki kwa kuwa fursa zipo nyingi.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Bw. Jose Graziano da Silva kwa kuja nchini na amemhakikishia kuwa Serikali itaendeleza na kuimarisha zaidi ushirikiano wake FAO, huku akitilia mkazo dhamira yake ya kutaka ushirikiano huo uelekezwe katika ujenzi wa viwanda vya kuzalisha bidhaa zitokanazo na mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi.

“Tanzania ina maziwa mengi, ina ukanda wa bahari wenye urefu wa kilometa 1,422 na ina mito mingi ambayo inaweza kuwekezwa viwanda vya samaki, inashika nafasi ya pili kwa mifugo Barani Afrika, hivyo tunahitaji kujenga viwanda vya nyama.

“Asilimia 75 ya nguvu kazi ya Taifa ni vijana ambao wanauwezo wa kuzalisha mazao mengi ya kilimo tunahitaji viwanda, uchumi wetu ni mzuri na unakua kwa wastani wa asilimi 7.1 na mengine mengi, kwa haya yote tunahitaji wadau ikiwemo FAO tushirikiane kutumia fursa hizi” alisema Mhe. Rais Magufuli na kuahidi kuwa Serikali yake imejipanga kusimamia miradi yoyote itakayoletwa nchini ili itekelezwe kwa uadilifu na ubora wa hali ya juu.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli alifanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Mzee Joseph Butiku Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Baada ya mazungumzo hayo Mzee Butiku amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya kuongoza Serikali ambapo katika kipindi kifupi amesimamia vizuri nidhamu, watu kufanya kazi, kupiga vita rushwa, ulipaji wa kodi na amemtaka asirudi nyuma kwa kuwa nchi inakwenda vizuri.

“Mimi nimefanya kazi hapa Ikulu kwa miaka 23, Mwl. Nyerere alijenga misingi mizuri, lakini huyu Rais Magufuli ameisimamia vizuri sana, unapofanya mambo kama haya, lazima hapa nyumbani na huko nje kutakuwa na maneno, mazuri sikiliza, ya hovyo achana nayo” alisisitiza Mzee Butiku.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais Magufuli ameagana na Balozi wa China hapa nchini anayemaliza muda wake Mhe. Dkt. Lu Youqing na kumshukuru kwa kazi kubwa na nzuri aliyoifanya katika kipindi cha miaka mitano aliyokuwepo hapa nchini.

Mhe. Rais Magufuli amesema katika kipindi chake Mhe. Dkt. Lu Youqing ametoa mchango mkubwa katika kuendeleza na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano kati China na Tanzania, uliofanikisha kuongeza uwekezaji katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu, elimu, kilimo, afya na kukuza biashara ambapo wafanyabiashara wengi wa China wamekuja kuwekeza nchini, mambo ambayo yamezalisha ajira na kukuza pato la nchi.

Mhe. Dkt. Magufuli amemuomba Mhe. Dkt. Lu Youqing kuendelea kuitangaza vyema Tanzania nchini China, ambako anakwenda kushughulikia masuala ya uchumi na kwamba anaamini atatumia nafasi hiyo kuhimiza wawekezaji na wafanyabiashara wengi zaidi wa China kuja kuwekeza hapa nchini.

“Mhe. Balozi Dkt. Lu Youqing Watanzania hatutakusahau kwa mchango wako, wewe ni ndugu na rafiki yetu, tunakushukuru sana kwa yote uliyoifanyia nchi yetu, naomba nikuhakikishie kuwa kazi nzuri uliyoifanya tutaiendeleza na tutashirikiana na Balozi mpya atakayekuja kuendeleza pale ulipoachia” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Kwa upande wake Mhe. Dkt. Lu Youqing amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa ushirikiano alioupata kwa kipindi chote alichokuwepo hapa nchini na ameahidi kuwa ataendelea kuwa Balozi mzuri wa kuinadi Tanzania huko nchini China.

“Mhe. Rais Magufuli nakushukuru sana, hapa Tanzania ni nyumbani kwangu na nipo tayari wakati wote kutoa ushirikiano pale nitakapohitajika kufanya hivyo kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini China ama kutoka Serikalini hapa Tanzania” Alisema Dkt. Lu Youqing.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Rais Magufuli Kupokea Ripoti ya Madini ya Almasi Leo Saa Nne Asubuhi

$
0
0
LEO  Tarehe 07 Septemba, 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli atapokea taarifa ya uchunguzi wa madini ya Tanzanite na Almasi uliofanywa na kamati maalum mbili zilizoundwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai.

Taarifa hiyo itakabidhiwa kwa Rais Magufuli na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Hafla ya kukabidhiwa kwa taarifa hiyo itarushwa moja kwa moja na vituo vya redio na televisheni kuanzia saa 4:00 Asubuhi.

Wananchi wote mnaombwa kufuatilia matangazo hayo kupitia vyombo vya habari na tovuti rasmi ya Ikulu ambayo ni www.ikulu.go.tz

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Mtekaji akiri kuua watoto 2, kuwatumbukiza shimoni

$
0
0
Mtuhumiwa  wa mauaji ya watoto wawili, Moureen David (6) na Ikram Salum (3), amekiri kuwateka watoto hao, kuwaua na kuwatumbukiza ndani ya shimo la maji taka.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, mtuhumiwa Samson Peter (18), alipomaliza kuwateka watoto hao na wengine kuwaachia, alikimbilia mkoani Geita ambako alikamatwa Septemba 2 mwaka huu kisha kuletwa jijini Arusha, Septemba 4, mwaka huu.

Kamanda Mkumbo alisema baada ya mahojiano, Peter alikiri kuwateka watoto hao na wengine kuwaachia kisha kukiri kuwaua Ikram na Moureen na kuwatumbukiza ndani ya shimo la maji taka lililopo katika nyumba ambayo haishi mtu na haijamalizwa kujengwa iliyopo eneo la Mtaa wa Olkerian katika Kata ya Olasiti. Alisema askari baada ya kufika eneo hilo huku wakiwa na mtuhumiwa huyo, waliikuta miili ya watoto hao ikiwa inaelea juu ya maji yaliyopo ndani ya shimo hilo.

Aliongeza kuwa licha ya matukio hayo mawili, mtuhumiwa huyo Agosti 28, mwaka huu saa 11:45 jioni eneo la Kwamrombo, aliwateka watoto wawili ambao ni Ayub Fredy mwenye umri wa miaka mitatu na miezi minne na Bakari Suleiman mwenye umri wa miaka mitatu na miezi miwili na baada ya juhudi za Jeshi la Polisi na wananchi, walifanikiwa kuwapata watoto hao siku hiyo hiyo muda wa saa 2:00 usiku.

Alisema polisi kwa sasa wanaendelea kumhoji mtuhumiwa huyo ambaye anatarajia kufikishwa mahakamani muda wowote mara upelelezi utakapokamilika. 

Awali, Mwenyekiti wa Mtaa wa Olkerian, Daudi Safari alisema wazazi wa watoto hao wanasubiri uchunguzi wa kitaalamu wa madaktari ili waruhusiwe kuchukua miili hiyo na kwenda kuizika kwani imeharibika vibaya na kusisitiza kuwa mtoto Ikram atazikwa muda wowote leo baada ya kukamilika kwa taratibu hizo za kiuchunguzi.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Msimamo wa CUF ya Maalim Seif baada ya Wabunge wa Lipumba kuapishwa

$
0
0
Chama cha Wananchi (CUF) upande wa Maalim Seif kimetangaza misimamo yake baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai kuwaapisha wabunge viti maalumu saba walioteuliwa na Baraza Kuu la Uongozi linalomuunga mkono Mwenyekiti anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba.

Wakati akitangaza misimamo ya CUF mbele ya Wanahabari, Naibu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa chama hicho, Mbarala Maharagande amesema Baraza Kuu la Uongozi la Taifa CUF haliwatambui wabunge hao walioapishwa Septemba 5.

Mbarala amesema CUF haitokubali kutumiwa kutengeneza upinzani bandia wa kisiasa wa kuendelea kuisaidia CCM kubaki madarakani, na kudai kwamba haiko tayari kushirikiana na wabunge hao kwa kuwa wameteuliwa kwa ajili ya kuisaidia CCM Bungeni.

“Jana tumeshuhudia jinsi wafuasi wa Lipumba walivyopokelewa na wabunge wa CCM Dodoma na kuandaliwa dhifa ya kusherehekea ushindi wa hujuma dhidi ya CUF. Hii ni mara ya kwanza kaa wanaoitwa wabunge wa Upinzani kuingia bungeni kuapishwa na kusindikizwa na wabunge wa CCM,” amesema.

“Kwa hakika spika amepoteza sifa na haiba ya kuongoza Bunge ambalo ni mhimili wa dola na ambao ulipaswa kuwa alama ya uadilifu katika nchi, lilipaswa kuwa chombo muhimu cha watanzania katika kuisimamia serikali ili wananchi wapate maendeleo, lilipaswa kuwa huru chenye kujisimamia na kuacha kutumiwa kukandamiza upinzani. Ajitathimini aone kwamba anahitaji watanzania wamkumbuke kwa jambo lipi baada ya kuondoka katika nafasi hiyo,” amesema.

Wakizungumza katika mkutano huo baadhi ya wabunge waliovuliwa ubunge wao, wamezitaka baadhi ya taasisi za serikali kutoshiriki katika kuhujumu mfumo wa demokrasia.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Riziki Ngwali amesema anasikitishwa na kitendo cha Bunge kuwaapisha wabunge hao kwa madai kwamba kimelenga kuugandamiza mfumo wa demokrasia.

“Inasikitisha, nchi ambayo ni ya kidemokrasia imeweka sheria na taratibu za kusimamia mifumo ya demokrasia, halafu taasisi zinashiriki kuuharibu mfumo huo. Sikutegemea kama ofisi ya msajili ingefanya hivyo, ni muendelezo wa njama na hujuma,” amesema na kuongeza.

“Nilimtahadharisha msajili kwamba anachokifanya kinahatarisha usalama, CUF ni chama chenye nguvu hasa upande wa Zanzibar. Hivi vilio vya kila mara haviwezi vikaisha kimya kimya. Kuna mwisho na kikomo, hujuma haisaidii, mkinya haki watu wataitafuta.”

Kwa upande wake Savelina Mwijage amesema

“Sisi hatulilii kuvuliwa kwetu ubunge, tunalilia kuathirika kwa chama chetu. Sisi ni wanadamu hatuwezi kusema lolote Mungu ataamua na mahakama pia itaamua, Spika anachuki na CUF si vingine,” amesema.

Uhuru Kenyatta Awakataa Maofisa wa Tume ya Uchaguzi (IEBC)

$
0
0
Chama cha Jubilee cha Rais Uhuru Kenyatta kimewakataa maofisa wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ambao wanatarajiwa kusimamia uchaguzi mpya wa Urais mwezi ujao Oktoba 17.

Chama hicho kimetoa orodha ya majina ya maofisa hao, ambao kimesema wanawafahamu kuwa wanapendelea wapinzani.

Siku moja iliyopita Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati alitangaza maofisa saba watakaoongoza maandalizi ya uchaguzi utakaofanyika Oktoba 17  ambapo miongoni mwa maofisa hao ni Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) na msimamizi wa kituo cha Taifa cha kujumlishia matokeo.

Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) limesema "Tuna habari za kuaminika kwamba kwenye orodha ya maofisa hao kuna watu wanaofahamika wazi kuegemea upande fulani."

Leo Rais Uhuru amekutana na viongozi wa kidini ikulu ambapo amesema tarehe iliyotangazwa inafaa ili kutovuruga kalenda ya mitihani ya taifa ambayo imepangiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Oktoba.

Mahakama ya Juu nchini Kenya Septemba Mosi ilifuta matokeo ya Urais  kwa kudai ulikuwa na dosari ambapo katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Agosti 8 ambao Rais Kenyatta alitangazwa mshindi.

Katika uchaguzi wa Agosti 8, Kenyatta alitangazwa mshindi kwa kupata kura 8,203,290 sawa na asilimia 54.27, huku mpinzani wake Odinga akipata kura 6,762,224 sawa na asilimia 44.74.

Hivi karibuni Muungano wa National Super Alliance (NASA), ambao mgombea wake ni Raila Odinga, ulidai mabadiliko makubwa kwenye IEBC kabla ya uchaguzi mpya kufanyika.

Bashe ataka kinga ya Rais iondolewe

$
0
0
Mbunge wa Nzega kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Hussein Bashe amefunguka na kutaka katiba ya nchi kubadilika ili ikiwezekana kinga ya Rais iondolewe kwenye katiba kwa kuwa kinga hizi zinawafanya viongozi hao kufumbia macho baadhi ya vitu.

Bashe amesema hayo jana mjini Dodoma baada ya kamati za bunge kutoa ripoti juu ya biashara za madini ya Tanzanite na Almasi ambapo katika ripoti hizo baadhi ya mawaziri wa serikali mbalimbali wametajwa kuhusika katika kufanya maamuzi ambayo yamelitia hasara taifa kwa maslahi yao binafsi.

"Umeona maamuzi yaliyofanywa na mawaziri waliotajwa kwenye hizo ripoti unatakiwa kujiuliza swali la msingi hivi maamuzi yote yale ya kuvunja sheria yaliyofanywa na mawaziri hivi Marais waliokuwa madarakani walikuwa hawajui? 

"Leo Rais Magufuli asingekuwa tu amesukumwa na moyo wake kufanya haya anayofanya kwenye uwekezaji wa madini tungeyajua haya? Umefika wakati kama nchi wa kuangalia uwezekano kufanya mabadiliko ya katiba, tuangalie mabadiliko ya sheria tuangalie tunapowapa marais hawa kinga haya mambo ndiyo hutokea" alisema Bashe

Bashe anaamini kuwa maamuzi ambayo hufanywa na mawaziri hao ili kufanya mabadiliko makubwa katika baadhi ya mikataba ambayo imeigharimu serikali na nchi kiujumla kuwa ni lazima viongozi wao wa juu ambao ni Marais walikuwa wakitambua mambo hayo.

Waziri Mkuu Atoa Maagizo Mazito Wizara ya Kilimo

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi pamoja na Bodi ya Korosho Tanzania zifanye tathimini ya maandalizi ya msimu ujao kwa wakati na zimpatie taarifa mara moja ili kama yapo matatizo yatatuliwe kwa muda.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo  wakati akizungumza na wadau wa zao la korosho kwenye kikao alichokiitisha ofisini kwake mjini Dodoma kujadili mwenendo wa zao la korosho na ununuzi wa pembejeo.

"Lipo tatizo la tathmini ya maandalizi ya msimu kutofanyika kwa wakati na kusababisha matatizo kutotatuliwa kwa wakati. Bodi na Wizara zitoe tathimini ya maandalizi ya msimu ujao kuhusu vyama vya ushirika vilivyojipanga, upatikanaji wa vifaa kama magunia na nyuzi, maghala, masoko, mizani, minada, malipo na mfumo wake," alisema.

Aidha Mh Majaliwa amesema tangu serikali iamue kusimamia mazao makuu matano ya pamba, chai, kahawa, korosho na tumbaku hajapata muda wa kukaa na kuongea na wadau wote.

 "Serikali imeamua kufuatilia usimamizi wa mashamba; kusimamia upatikanaji wa mbegu, miche na pembejeo; kufuatilia uvunaji na mfumo wa masoko ya korosho na pia kufuatilia mfumo wa ushirika katika baadhi ya mazao. Kwa sasa zao la korosho linalimwa katika wilaya 50 kwenye mikoa 11 ya Dodoma, Iringa, Lindi, Mbeya, Morogoro na Mtwara. Mingine ni Njombe, Pwani, Ruvuma, Singida na Tanga. Ameongeza

Ameongeza kwamba "Katika msimu wa mwaka 2016/2017 zao la korosho lilikuwa ni moja kati ya mazao ya kibiashara yenye tija na faida nyingi kwa kuliingizia Taifa fedha za kigeni kiasi cha dola za Marekani milioni 346.6," alisema na kuongeza kuwa katika msimu wa mwaka 2017/2018 watendaji hawana budi kujipanga vizuri ili zao la hilo liendelee kuliingizia Taifa dola nyingi zaidi kwa kuwa Serikali imetoa viatilifu bure. 

 "Ninasisitiza eneo hili kwa sababu tumebaini kuwa korosho inachangia zaidi ya asilimia 50 ya mapato kwenye Halmashauri zinazolima kwa wingi zao hilo. Kwa kuwa zao hili ni la kimkakati, naitaka Wizara inipatie taarifa sahihi na kwa wakati," alisisitiza.

Mwanasheria Amtaka Rais Magufuli Asaini Hukumu ya Kumnyonga Hadi Kufa Kijana Aliyeteka Watoto na Kuwaua

$
0
0

Mwanasheria wa kujitegemea hapa nchini Alberto Msando, amemtaka Rais Magufuli kusaini hukumu ya kunyongwa hadi kufa kwa mtuhumiwa wa mauaji ya watoto waliotekwa mkoani Arusha Bw. Samson Peter ili iwe somo kwa wengine.

Kwenye Ukurasa wake wa Instagram Alberto Msando ameandika ujumbe wa kusikitisha kuhusu vifo vya watoto hao waliotekwa na miili yao kukutwa kwenye shimo la choo mkoani Arusha, na kusema kwamba tukio alilolifanya mtuhumiwa huyo ni la ukatili wa hali ya juu, na kwamba kesi yake iendeshwe kwa haraka iwezekanavyo ili ahukumiwe na kumpa adhabu kali ikiwemo kunyongwa hadi kufa.

"Samson Peter Mungu akuadhibu, yaani huyu wala siyo wa kukaa zaidi ya miezi sita na kesi ya utekaji na mauaji!! Hii iishe hata kesho!! Na Rais asaini adhabu ya kunyongwa mpaka afe!! Naomba akihukumiwa tu Mh. Rais atengeneze historia ya kusaini kunyongwa kwake!!!", aliandika Alberto Msando.

Mwanasheria huyo machachari na maarufu Tanzania aliendelea kwa kuwataka wakazi wa Arusha kujitokeza kwa wingi katika shughuli ya mazishi ya watoto hao, ili kuwapa faraja wafiwa.

Watoto waliofariki Moureen David na Ikram Salim miili yao iliokotwa jana katika shimo la choo ambako walitelekezwa, baada ya kutekwa na mtu aliyejulikana kwa jina la Samson Peter ambaye kwa sasa anashikiliwa na polisi, kwa tamaa za fedha

A post shared by Msando Alberto (@albertomsando) on

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Breaking News: Mtekaji Wa Watoto Arusha Auawa Kwa Kupigwa Risasi

$
0
0
Mtuhumiwa wa utekaji wa watoto Arusha, Samson Peter amefariki dunia kwa kupigwa risasi wakati akijaribu kuwakimbia Polisi alipokuwa amekwenda kuwaonyesha washirika wenzake wa utekaji eneo la Muriet Mkoni Arusha.

Akithibitisha kutokea kwa kifo chake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Charles Mkumbo amesema kuwa mtuhumiwa huyo wa utekaji alipigwa risasi ya mguuni kama onyo la kujaribu kumtoroka Askari aliyekuwa ameongozana naye majira hayo ya saa 5:30 usiku.

Kamanda Mkumbo amesema kuwa baada ya tukio hilo la kumjeruhi  mtuhumiwa Samson Peter kwa nia ya kumuadhibu alifikishwa Hospital ya Mt. Meru lakini alifariki kutokana na kuvuja damu nyingi kwenye jeraha la mguu.

"Ni kweli mtuhumiwa amefariki. Ambapo jana usiku wakati alipokuwa amesindikizwa na polisi kuwaonyesha waashirika wenzake alitaka kutoroka, lakini katika hatua ya kumuadhibu kwa kitendo chake hicho ndipo akapigwa risasi ya mguuni ambapo ilimpelekea kuvuja damu nyingi na alifariki baada ya kufikishwa hospitali" amesema Kamanda Mkumbo.
 
Hata hivyo Kamanda Mkumbo amesema msako zaidi wa kuunasa mtandao huo bado unaendelea na iwapo wakipatikana wote watakumbana na mkono wa sheria.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images