Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

ACT Wazalendo kudai mikutano ya hadhara mahakamani

$
0
0
Chama cha ACT-Wazalendo kimepanga kufungua shauri Mahakama Kuu kupinga amri ya kuzuia mikutano ya hadhara ya kisiasa kwa wale ambao hawakushinda kwenye uchaguzi katika majimbo husika.

Chama hicho kimefikia uamuzi huo kupitia Mkutano Mkuu wa Kidemokrasia wa pili uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita.

Taarifa ya mkutano huo iliyotolewa kwa vyombo vya habari imeeleza kuwa chama hicho kimeamua kufungua shauri hilo kudai haki ya kufanya mikutano ya hadhara ambayo ni shughuli halali za vyama vyote vya siasa kwa mujibu wa katiba.

Aidha, taarifa hiyo imeeleza kuwa mbali na kufungua shauri hilo, wameazimia kumuandikia barua Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kumuomba atengue zuio la kufanya mikutano ya hadhara ya kisiasa.

“Maazimio haya yote yatapelekwa kwenye idara husika za chama kwa ajili ya kutekeleza mara moja. Pia, viongozi wa chama wataendelea kuipigania misingi ya kidemokrasia,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

ACT Wazalendo walishinda jimbo moja pekee la ubunge la Kigoma Mjini ambapo kwa mujibu wa masharti ya kufanya mikutano ya hadhara ndilo jimbo pekee ambalo chama hicho kinaweza kufanya mkutano wa hadhara wa jimbo.

Zitto Kabwe ambaye ni Kiongozi Mkuu wa chama hicho ndiye mbunge pekee anayekiwakilisha bungeni.

Kutana na Mtabibu wa Nyota za Binadamu.........Anafungua Kizazi, Pete za Bahati na Kusafisha Nyota

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika

Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). 


Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.


Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.


Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls +255 710 279 458
+255 710 279 458


Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Darasa la 7 Wamponza Godbless Lema ........Apigwa marufuku kufanya Mkutano

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Arusha limepiga marufuku mikutano ya mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema iliyokuwa ianze jana  kwa maelezo kuwa kuna maandalizi ya mtihani wa darasa la saba na mbio za Mwenge wa Uhuru.

Taarifa kutoka Ofisi ya Mkuu wa polisi, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) E.Tille wilayani Arusha, amesema katika barua yake iliyothibitishwa na Kamanda wa polisi Arusha, Charles Mkumbo imesema kuwa Mhe. Lema amezuiwa kufanya mikutano iliyokuwa imepangwa kuanzia  jana hadi Septemba Mosi.

“Ofisi ya Mkuu wa Polisi Wilaya ya Arusha inakutaarifu kuwa imezuia mikutano yako yenye ratiba kuanzia Agosti 27 hadi Septemba 1 kwa ajili ya kupisha maandalizi ya kuhitimisha mtihani wa darasa la saba na Mwenge wa Uhuru,” Sehemu ya barua hiyo ilinukuliwa.

Kamanda Mkumbo alisema sababu ya kuzuia mikutano hiyo ni polisi kuhitajika kwa ulinzi, hivyo haiwezekani kupata wa kulinda mikutano na kushiriki masuala ya mitihani na Mwenge.

“Haya ni mambo ya kitaifa, hivyo ndiyo sababu OCD amesitisha mikutano ya mbunge na mambo haya yakimalizika ataendelea na mikutano yake,” alisema.

Hospitali ya Kairuki Yashitakiwa Kwa Kufanya Opareshen na Kisha Kusahau Vitu Tumboni

$
0
0
Mkazi  wa jijini Dar es Salaam, Khairat Omary, ameishtaki Hospitali ya Kairuki na kudai fidia ya Sh milioni 155 kwa kumsababishia matatizo katika mfuko wa uzazi yaliyofanya aondolewe kizazi.

Khairat kupitia Kampuni ya Uwakili ya Jonas amefungua kesi ya madai namba 184 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na imepangwa kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Katika madai hayo, mdai anadai alikuwa akihudhuria kliniki wakati wa ujauzito katika hospitali hiyo na Desemba 15 mwaka jana alijifungua kwa upasuaji, akaruhusiwa Desemba 17 mwaka huo na kutakiwa kurudi tena Desemba 21.

Mdai akiwa nyumbani alianza kusikia maumivu ikiwamo kutapika, ilipofika Desemba 21 alirudi hospitali akaeleza maumivu anayopata kwa daktari ambaye alielekeza afanyiwe kipimo cha Ultra Sound.

Majibu yalipotoka daktari akampatia dawa za kutuliza maumivu na kumtaka apumzike hali itaendelea kuimarika.

“Akiwa nyumbani hali iliendelea kuwa mbaya, alisikia maumivu makali ya kichwa na alianza kubadilika rangi ambapo alikimbizwa hospitali ya jirani, walipompima wakaelekeza apelekwe Regency Hospital kwa matibabu zaidi.

“Regency walimfanyia vipimo na kubaini kuna tatizo katika mfuko wa uzazi na kumuhamishia Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako pia walimfanyia vipimo na kubaini wakati alipofanyiwa upasuaji kuna vitu vilibakia kama pamba ambavyo vimesababisha mfuko wa uzazi kuharibika,” ilisema sehemu ya hati hiyo ya madai.

Anadai ili kuokoa maisha yake alishauriwa kuondolewa kizazi, hata hivyo licha ya kuondolewa alibakia na tatizo la fístula lililosababishwa na pamba zilizoachwa wakati anajifungua.

Mdai anadai kutokana na uzembe huo wa kutokuwa makini wakati wa kumzalisha anaomba mahakama iamuru alipwe Sh milioni 20 gharama za matibabu, Sh milioni 25 fidia kwa kukosa kipato wakati anaumwa, Sh milioni 80 gharama za adhabu na Sh milioni 30 fidia.

Wadaiwa wanatakiwa kupeleka utete wao mahakamani na kesi hiyo itatajwa Agost 31, mwaka huu.

Kesi ya Kupinga Ushindi wa Uhuru Kenyatta Yaanza Kusikilizwa Kenya

$
0
0
Mahakama Kuu nchini Kenya imeanza kusikiliza kesi ya kupinga ushindi wa Rais wa Kenya,Uhuru Kenyata, iliyotakiwa kuanza kusikilizwa jana.

Kesi hiyo ilitakiwa kuanza jana   jioni baada ya kumalizika kwa hatua ya kwanza iliyofanyika juzi kwa pande zote tatu yaani upande wa NASA, Jubilee na Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Mipaka nchini humo(IEBC) kuwasilisha mahakamani hoja zao za maandishi.

 Msajili wa Mahakama hiyo, Esther Nyaiyaki akinukuliwa na  gazeti la Kiingereza la Standard nchini humo bila kueleza mabadiliko hayo alisema itasikilizwa leo.

Kesi hiyo inatokana na uamuzi wa Muungano wa vyama vya upinzani NASA chini ya mgombea wake Raila Odinga kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais wa Agosti 8, wakidai kuwa haukuwa wa haki na huru.

Odinga amepinga  matokeo yaliyotangazwa Agosti 11, mwaka huu na Tume hiyo yakimtambua Rais Uhuru Kenyatta wa Muungano wa Jubilee kuwa mshindi wa kiti cha urais katika ungwe ya pili akipata kura 8, 203, 290 sawa na asilimia 54.27 huku mpinzani wake mkuu, mgombea wa Muungano wa upinzani wa NASA, Raila Odinga akIpata kura milioni 6,762,224 sawa na asilimia 44.74.

Odinga hakukubaliana na matokeo hayo hadharani na aliamua kuwasilisha stakabadhi zake mahakamani hapo ikiwa ni saa nane kabla ya tarehe ya mwisho. Baadaye, Agosti 24, mwaka huu, Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto kwa upande wao, pia waliwasilisha stakabadhi zao kuhusiana na kesi hiyo.

Odinga ambaye alikuwa ni miongoni mwa wagombea nane wa kiti hicho cha urais, alilalamika pia kuwapo hujuma za Rais Uhuru Kenyatta kutumia mamlaka yake vibaya katika kuingilia mfumo wa tume hiyo.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Ripoti ya Mkemia wa Serikali kuhusu sampuli ya mkojo wa Agness Masogange Yapokelewa Mahakamani....Pingamizi Latupwa

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo August 28, 2017 imepokea taarifa ya Mkemia kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali iliyoonesha kuwa sampuli ya mkojo wa Agnes Gerald maarufu kama Masogange una chembechembe za dawa za kulevya.

Taarifa hiyo imepokelewa baada Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kutoa uamuzi wake ambapo amesema Mahakama imepokea taarifa hiyo na pingamizi la utetezi limetupiliwa mbali.

Pingamizi la upande wa utetezi ni kwamba fomu zilizopelekwa kwa Mkemia Mkuu hazikufuata sheria.

Hakimu Mashauri amesema Mkemia huyo Elia Mulima ambaye ni Shahidi wa kwanza ana haki ya kuandaa ripoti, kupima sampuli na kutoa ripoti Mahakamani.

Kuhusu hoja ya kuwasilishwa maombi ya kupimwa mkojo Masogange, Hakimu amesema ni wazi Polisi walipeleka maombi kwa Mkemia na mshtakiwa alienda akiwa chini ya askari wawili, ambapo walipatiwa kontena kwa ajili ya kuweka sampuli ya mkojo wa Masogange.

Watu 7 Wafariki kwa Ajali

$
0
0
Picha sio ya tukio
 
Watu saba wamefariki katika ajali mbili tofauti ambapo ajali ya kwanza watu wawili wa familia moja wamepoteza maisha na wengine sita kujeruhiwa katika ajali ya gari dogo aina ya Kluger iliyotokea eneo la Masaki mkoani Pwani leo.

Majeruhi sita wa ajali ya gari ndogo iliyotokea mkoani Pwani wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani na taratibu zinafanyika ili kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi kutokana na hali zao kuwa mbaya.

Aidha watu wengine watano wamefariki dunia na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha lori la mzigo lililokuwa limebeba abiria mkoani Singida.

Ajali zote mbili zimesababisha vifo vya watu saba huku wengine 26 wakiwa ni majeruhi.

Ali Kiba Ataja Sababu ya Wimbo Wake Mpya Kupokelewa Vizuri

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva Nchini Ali Kiba amefunguka juu ya siri inayomfanya awe anapata mapokezi makubwa kwa mashabiki wake  kila anapotoa kazi mpya kuwa ni kazi nzuri ambazo amekuwa akizifanya.

Akizungumza Juma tatu hii ndani ya ‘Planet Bongo’ya East Africa Radio,Ali Kiba  alifunguka kuwa kazi nzuri ndio zinazomfanya awe anapata mapokeo makubwa sana kutoka kwa mashabiki wa muziki wake na wala si kitu kingine kama ambavyo imezoeleka kwa baadhi ya wasanii walio wengi kutumia ‘kiki’ kwa ajili ya kupata mapokeo makubwa ya kazi zao.

‘’Mi nafanya kazi nzuri ndio mana mapokeo ya kazi zangu kwa mashabiki yanakuwa makubwa na sio kitu kingine ninacho kifanya katika kazi yangu zaidi ya kufanya kazi nzuri’’alisema Ali kiba.

Ali Kiba ameanza rasmi kufanya ziara katika vyombo mbali mbali vya habari kwa ajiri ya kuutambulisha wimbo wake mpya ‘Seduce Me’ ambao unatamba sana kwa sasa huku akiongozana na mtayarishaji wa kazi hiyo ‘Man Walter’ kutoka katika studio za Combination Sound.

Polisi Watoa Majibu ya Uchunguzi Ofisi za Mawakili wa IMMMA Kulipuliwa Bomu

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, leo limesema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa watu wasiojulikana utambulisho wao na idadi yao walifika katika ofisi za Mawakili wa IMMMA Advocates wakiwa katika magari mawili na kujifanya ni maaskari na kuwarubuni walinzi na kuondoka nao katika gari mojawapo kabla ya kulipua jengo hilo.

Walinzi hao wanadaiwa kukutwa baadaye maeneo ya Kawe wakiwa hawajitambui.

Imedaiwa kuwa kundi lililobaki liliingia katika ofisi hizo hilo na kuweka vilipuzi vilivyotengenezwa kienyeji, ambavyo vililipuka muda mfupi baada ya watu hao kuondoka eneo hilo na kusababisha uharibifu wa wa mali na jengo la ofisi hiyo pamoja na majengo ya jirani.

Jeshi hilo limesema kuwa linaendelea kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini watu waliofanya tukio hilo na kujua dhamira yao ili wafikishwe katika vyombo vya sheria kwani wajibu wa jeshi la polisi ni kulinda raia na mali zao na kamwe haliwezi kuhujumu maisha ya watu na mali za wananchi

Aidha, jeshi hilo limewaomba waathirika wa tukio hilo na wananchi kwa ujumla kuwa watulivu wakati vyombo vya dola vikiendelea na upelelezi wa tukio hilo

Bulaya Aruhusiwa Kutoka Muhimbili

$
0
0
Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (Chadema) ameruhusiwa kutoka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa takribani wiki moja.

Bulaya alikimbizwa Muhimbili kutoka tarime mkoani Mara baada ya kupata tatizo la kupumua baada ya kuzidiwa akiwa mahabusu ya kituo cha polisi mjini Tarime. Alikuwa amelazwa wodi namba 18 katika jengo la Sewahaji akipatiwa matibabu.

Mbunge huyo wa Chadema, leo Agosti 28 ameruhusiwa kutoka hospitali na amewashukuru madaktari wa Muhimbili kwa kumpatia matibabu ya kina.

Amesema afya yake imetengemaa lakini amepewa maelekezo kadhaa.

“Kwanza nitapumzika kwa siku 10, hivyo ndivyo nilivyoagizwa na nitatakiwa kurudi tena hospitalini kwa ajili ya kuangaliwa afya yangu zaidi. Kwa sasa nitapumzika kabla ya kurudi jimboni kuendelea  na shughuli za maendeleo,” amesema Bulaya.

Bulaya aliwekwa rumande Agosti 18 baada ya kukamatwa na polisi akidaiwa kuingia jimbo la Tarime kufanya shughuli za kisiasa kwa kutoa msaada wa mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu katika shule za msingi kwa mwaliko wa mbunge mwenzake Esther Matiko.

Rais Magufuli Atoa MAAGIZO Mazito TAKUKURU

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewataka viongozi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kutokuwa na kigugumizi cha kuchukua hatua pale wanapokuwa na ushahidi dhidi ya watu wanaojihusisha na vitendo vya rushwa.

Mhe. Rais Magufuli ametoa kauli hiyo  tarehe 28 Agosti, 2017 alipotembelea na kuzungumza na wafanyakazi wa TAKUKURU katika ofisi za makao makuu ya taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam.

“Kuna mambo mengi ya hovyo yanafanyika, tumehakiki pembejeo za ruzuku na kubaini madai ya Shilingi Bilioni 48 ni hewa, tumebaini wafanyakazi hewa zaidi ya 19,500, tumebaini kaya masikini hewa 56,000 zilizopaswa kupata fedha TASAF, tumebaini wanafunzi hewa 5,850 waliotakiwa kupata mkopo, kuna vichwa vya treni 11 vimeletwa bila kuwepo mkataba na mengine mengi, haya yote yanafanyika kwa rushwa, nataka kuwaona mnachukua hatua stahiki” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amesema ana imani na TAKUKURU na amewataka wafanyakazi wa taasisi hiyo kufanya kazi kwa kuzingatia weledi, uzalendo na uadilifu mkubwa na kwamba Serikali itafanyia kazi changamoto zinazowakabili.

Katika mkutano huo Mhe. Rais Magufuli amepokea masuala mbalimbali kutoka kwa wafanyakazi wa TAKUKURU na amewaahidi kuwa Serikali itayafanyia kazi ili kuboresha maslahi yao na mazingira ya kazi.

Mkutano huo umehudhuriwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Anjellah Kairuki, Katibu Mkuu Dkt. Laurian Ndumbaro na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Valentino Mlowola.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi na wataalamu wanaosimamia utekelezaji wa miradi mikubwa ikiwemo ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stieglers’ Gorge Hydropower Project), ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) na ujenzi wa barabara mbalimbali nchini, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Katika Mkutano huo, Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Matogolo Kalemani ametoa taarifa ya maandalizi ya awali ya kuanza kwa ujenzi wa mradi wa umeme wa Stiegler’ Gorge na kwamba zabuni ya kuanza kwa ujenzi huo itatangazwa tarehe 30 Agosti, 2017.

Mhe. Rais Magufuli amesema fedha za kuanza kwa ujenzi wa mradi huo mkubwa utakaozalisha Megawatts 2,100 zitakazoingizwa katika gridi ya Taifa zipo.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

28 Agosti, 2017

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya August 29

Wafungwa Kupatiwa Kazi Magereza kwa Mikataba Maalumu

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ameliagiza jeshi la Magereza na idara zingine zenye mashirika ya uzalishaji ambazo zipo chini ya wizara yake zifanye uzalishaji mali pamoja na kuwatumia wafungwa katika kufanya kazi ndani ya jeshi.

Waziri Nchemba ameongea hayo akiwa katika ufunguzi wa nyumba tano za maaskari wa jeshi la magereza mkoa wa Arusha nyumba zilizojengwa kwa kutumia fedha za shirika la magereza la uzalishaji mkoani humo.

Mh. Nchemba ametoa rai kwa jeshi hilo kuona kama inawezekana jeshi hilo kutumia wafungwa ambao wamemaliza mafunzo yao na wakaona wamerekebika kitabia na kuwachukua waendelee kufanya kazi kwa mkataba katika mashirika hayo kwani itarahisisha kupunguza wahalifu zaidi kuliko kwenda uraiani wakiwa hawana uwezo wakufungua biashara na kurudia makosa.

Naye mkuu wa Magereza Tanzania Dr Juma Malewa amewataka wananchi na mashirika ya umma na serikali kutumia jeshi la Magereza nchini katika shughuli za ujenzi kwani gharama zake ni nafuu sana lakini zenye ubora zaidi.

Kwa upande wa Mkuu wa Jeshi la Magereza mkoa wa Arusha, Hamis Nkabasi amesema nyumba hizo zimetumia gharama ndogo za ujenzi kwasababu rasilimali watu wametumia askari wenye ujuzi wa ujenzi na wafungwa ambapo imegharimu milioni 50 kila nyumba na itaweza kuchukua askari 12 ambapo zote zitachukua askari 60 na kama wangechukua kampuni kujenga basi ingegharimu fedha nyingi zaidi.

Korea Kaskazini Yarusha Kombora Zito Katika Anga la Japani........Ni Siku Chatu Baada ya Japani Kudai Inauwezo wa Kuyatungua Hayo Makombora

$
0
0
Korea kaskazini imerusha makombora yake ambayo yalipita Japan kabla ya kudondokea baharini.

Makombora hayo yalisafiri kuelekea mashariki karibu kilomita elfu moja juu ya kisiwa cha Japan cha Hokkaido.

Tukio hilo limechochea tahadhari ya hatari ambayo watu walielekezwa kujificha katika maeneo yaliyo chini ya ardhi ama kwenye majengo yaliyo imara.

Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe amesema urushwaji huo wa makombora ambao haujawahi kutokea , umeleta kitisho kikubwa kwa taifa lake.

Hakuna juhudi zilizofanywa na Japan kulitengua kombora hilo licha ya hapo awali kudai kuwa ilikuwa na uwezo huo, na badala yake  ilitoa onyo la kiusalama ikiwaambia raia wake katika eneo la Hokkaido kujificha chini ya majumba yaliojengwa ardhini.

Wanajeshi wa Marekani na Japan wanafanya zoezi la pamoja katika eneo hilo la Hokkado.

Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in ameagiza uwezo wa utumiaji  nguvu ili kujibu shambulio hilo.Ndege nne za Korea Kusini zilifanya zoezi la kurusha makombora jana.

Bwana Abe alisema kuwa amezungumza na rais wa Marekani Donald Trump na kwamba wote wamekubaliana kuiongezea vikwazo  Korea Kaskazini.

Katika mfululizo wa majaribio yake ya makombora ya hivi karibuni Korea kaskazini haijawahi kurusha makombora yaliyopita juu ya ardhi ya nchi hiyo, hivyo tukio hili la sasa limeleta wasiwasi mkubwa.

Katika siku za hivi karibuni, Korea Kaskazini  ilijaribu kombora lake lililopata mafanikio kutokana na uwezo wake wa kuweza kuifikia Marekani na kuonyoa kuwa inasimamia mipango yake ya kushambulia kwa makombora eneo la Marekani la Guam, kilomita elfu mbili kusini mashariki mwa Japan.

Matangazo ya Nafasi za Kazi 1083 Kutoka Taasisi Mbalimbali

$
0
0
Matangazo ya Nafasi za Kazi 1083  Kutoka Taasisi Mbalimbali

Nikiteuliwa na Rais Magufuli nitakataa

$
0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema kuwa hatokubali endapo Rais Dkt Magufuli atamteua kushika nafasi yoyote ya uongozi kwani hatakuwa na fursa ya kukijenga chama chake ili kiwe tayari kushinda uchaguzi na kushika dola.

Zitto ambaye chama anachotoka tayari kimetoa viongozi wawili ambao ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Prof. Kitila Mkumbo na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Elisha Mghwira alisema endapo atateuliwa, atamshukuru Rais na kukataa uteuzi huo.

Zitto Kabwe ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini aliyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na gazeti la Mwananchi wakati akijibu swali kuhusu uteuzi wa viongozi wa chama chao ambao mmoja alikuwa mshauri wa chama na mwingine alikuwa mwenyekiti wa chama hicho kichanga Tanzania.

“Sitakubali uteuzi kwa sababu jukumu langu na viongozi wengine wa ACT- Wazalendo ni kujenga chama ili kupata ushawishi  na kuungwa mkono na umma na hatimaye kushika dola,” alisema Zitto.

“Kukubali uteuzi utakaoniondoa na kuniweka kando kwenye jukumu na malengo hayo ni kufifisha matumaini ya maelfu ya wana-ACT Wazalendo,” aliongeza Zitto.

Akizungumzia sababu za chama kuridhia uteuzi wa Prof. Mkumbo, Zitto alisema kwamba hapo hali ilikuwa ni tofauti kwa sababu kabla na baada ya uteuzi wa Mkumbo, yeye ni mtumishi wa umma, hivyo uteuzi wake haukushtua.

“Mama Anna Mghwira alikuwa ni mwanasiasa kwa nafasi yake ya uenyekiti Taifa, ndio maana tulimuondoa ili kumpa fursa kutumikia serikali.”

Je, Una Tatizo La Nguvu Za Kiume, Kukosa Hamu Ya Tendo, Kushindwa Kurudia Tendo Au Maumbile Madogo ? Soma Hapa

$
0
0
JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇 
 
      Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

   UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
      @natural beauty pro. Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 7.5 @140,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @140,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
5.DISCREET.Ni dawa ya kuondoa mvi milele na zisiludi tena @130,000/=
    KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
       @natural2162
       @natural2162
       @natural2162
   Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0759029968 na 0659618585
    NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
      Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

                     < WELCOME ALL>

Kutana na Mtabibu wa Nyota za Binadamu.........Anafungua Kizazi, Pete za Bahati na Kusafisha Nyota

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika

Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). 


Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.


Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.


Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls +255 710 279 458
+255 710 279 458


Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images