Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jalada La Kesi La Mkurugenzi Wa Nida Liko Kwa DPP

0
0
Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu  jana imeelezwa kuwa jalada la kesi ya uhujumu uchumi dhidi ya aliyekiwa Mkurugenzi Mkuu Wa Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu,  lipo kwa DPP.

Mwendesha Mashtaka, wakili wa serikali, Peter Vitalis alieleza hayo mbelw ya Hakimu Mkazi Respicius Mwijage.

Alidai kuwa shauri hilo jana lilikuja kwa ajili ya kutajwa lakini jalada halisi la kesi hiyo liko kwa DPP na pia upelelezi bado haujakamilika, hivyo likirejeshwa ndipo itafahamika upelelezi umefikia wapi.

Hata hivyo, Hakimu Mwijage alisema kesi hiyo ina mwaka mmoja na upelelezi haujakamilika, hivyo wakamilishe ambapo  ameahirishwa kesi hadi September 28/2017.

Katika kesi hiyo, mshtakiwa Maimu na wenzake, wanakabiliwana mashtaka ya 27 yakiwemo ya kutumia madaraka vibaya, kula njama, kutumia nyaraka za uongo kumdanganya mwajiri na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh 1,169,352,931.

Mbali ya Maimu, washtakiwa wengine  Ni aliyekiwa Meneja Biashara Wa NIDA, Avelin Momburi, Mkurugenzi wa TEHEMA, Joseph Makani. Kaimu Mhasibu Mkuu wa NIDA, Benjamin Mwakatumbula, Mkurugenzi wa Kampuni ya Aste Insurance Brokers,  Astery Ndege, Ofisa Usafirishaji,  George Ntalima, Mkurugenzi wa Sheria, Sabina Raymond naXavery Kayombo.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Mawakili kesi ya Kitilya na wenzake walalamikia upelelezi......Wataka Kesi Ifutwe

0
0
Upande wa utetezi umeiomba Mahakama kuulazimisha upande wa mashtaka kuifuta kesi ya utakatishaji fedha, inayomkabili aliyekuwa Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya na wenzake.

Wakili wa utetezi, Majura Magafu ametoa ombi hilo  jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Mbele ya Hakimu Mfawidhi Cyprian Mkeha wakati kesii hiyo ilipokuja kwa kutajwa.

Aliiomba mahakama kuwa, upande wa mashtaka ulazimishwe kesi ifutwe ama waiondoe mahakamani kwa sababu washtakiwa awali walikuwa chini ya dhamana na wakiripoti kila walipohitajika Takukuru.

Wakili wa utetezi, Majula Magafu alidai kuwa sasa imefikia wakati mahakama ihakikishe maelekezo inayoyatoa yanaheshimiwa

"Mahakama inaweza kuifuta kesi ili ushahidi ukikamilika waletwe tena, kwa sababu imebaki hadithi kila wakija wanasema wanasubiri vielelezo kutoka Ulaya na miaka inaenda tu,".

Akijibu hayo, wakili wa serikali, Constantine Kakula alidai upelelezi wa kesi hiyo unashindwa kukamilika kwa sababu inahusisha uchunguzi unaovuka mipaka.

Alidai, siyo kama jamhuri imelala bali inafanya mawasiliano na upande wa pili, kwa sababu hatuwezi kumlazimisha anayetuma nyaraka za upelelezi kutoka Ulaya.

Hakimu Mkeha akautaka upande wa mashtaka kuhakikisha unakamilisha upelelezi.

 Kitilya na wenzake, aliyekuwa Miss Tanzania mwaka 1996, Shose Sinare na Sioi Solomon wanashtakiwa kwa utakatishaji wa fedha dola milioni 6. Kesi hiyo imeahirishwa hadi September 8/2017.

Zitto Kabwe Aeleza Kwa Nini Yeye Hakamatwi na Polisi Licha ya Kuikosoa Serikali

0
0
Mbunge wa jimbo la Kigoma Mjini Mh. Zitto Zuberi Kabwe, amesema pamoja na kuwa ni mwanasiasa na upinzani na miongoni mwa watu wanaokosoa serikali, atahakikisha anafanya hivyo pasipo kukamatwa na jeshi la polisi.

Akiwajibu wananchi kwenye ukurasa wake wa twitter ambao walikuwa wanashangaa kwa nini yeye hasumbuliwi na polisi licha ya kuongea maneno ya kuikosoa serikali kama inavyotokea kwa wengine, Zitto Kabwe amesema hataki na hapendi kufanyiwa hivyo, na atajitahidi kukwepa kitendo hicho.

“Sitaki na sipendi kukamatwa, itokee kwa kuwa imebidi, lakini kama ipo ndani ya uwezo wangu kukwepa kukamatwa nitahakikisha sikamatwi”, aliandika Zitto Kabwe.

Zitto Kabwe aliendelea kutoa maelezo ya suala hilo akitolea mfano wa viongozi mbali mbali wa Afrika ambao walikuwa wanaharakati na wanasiasa waliokuwa wakikososa serikali, lakini hawakuwahi kusumbuliwa kisheria mpaka ndoto zao zilipotimia.

“Kagame alikuwa mpiganaji na leo yupo madarakani kwa kuwa hakutaka kukamatwa, Meles mpiganaji dhidi ya The Derg akiwa na umri mdogo wa miaka 19 mpaka 36 akawa Rais wa Ethiopia 39 hakukamatwa”, aliandika Zitto Kabwe.

Hivi karibuni mwanasiasa na mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu alikamatwa na polisi kwa kile kilichoelezwa kutoa taarifa za uchochezi.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Tembo Avamia Kijiji......Aua Mtu Mmoja Kwa Kumkanyaga na Kujeruhi Mwingine

0
0
Kijana Emmanuel Ernest wa kitongoji cha Ilolo, Mvumi Misheni wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma, amefariki dunia baada ya kukanyagwa na tembo huku mwingine akijeruhiwa vibaya baada ya tembo huyo kuvamia mashamba ya zabibu.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema tembo huyo alikuwa akitafuta maji majira ya alfajiri hivyo baadhi ya wanakijiji baada ya kumuona walikusanyika na kupiga mayowe, kitendo kilichomfanya mnyama huyo kukasirika na kuanza kuwafukuza kabla ya kumkuta marehemu Emanuel akiwa na mdogo wake wakichimba mitaro ya mizabibu na kumkanyaga kifuani na kumvunja mbavu nne na kusababisha kifo chake.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mvumi Misheni, Peter Songoro, amethibitisha kupokea majeruhi wawili, akiwemo marehemu na mdogo wake Amani Joseph ambaye alikanyagwa mgongoni na kisha utumbo kutoka nje, kabla ya Emmanuel kufariki baadaye wakati akipatiwa matibabu.

Ofisi za Mawakili Fatma Karume na Lawrence Marsha Zimeteketea kwa Moto

0
0
Ofisi ya IMMMA House inazomilikiwa na wanasheria kadhaa akiwepo Fatma Karume na Lawrence Masha   zimeungua moto usiku wa kiamkia leo ambapo chanzo cha moto huo bado hakijafahamika.

Wakili Fatma Karume kwa siku za hivi karibuni alisikika sana alipokuwa akimtetea Tundu Lissu mara baada ya kukamatwa uwanja wa ndege alipokuwa akisafiri kwenda Rwanda.

Taarifa za awali ambazo hazijathibitishwa na Jeshi la Polisi kutoka kwa majirani wa eneo hilo wamedai kuwa walisikia mlio mithili ya bomu wakati wa usiku.

Itazame Hapa Video Mpya ya WCB Wakiongozwa na Diamond....ZILIPENDWA

0
0
Wasanii wanaofanya kazi chini ya lebo ya muziki ya WCB Wasafi, pamoja na boss wa lebo hiyo Diamond Platnumz na wasanii wake Rayvanny, Harmonize , ,Lavalava , Queen Darleen, Rich Mavoko na msanii wa zamani wa Yamoto Band Marombosso ‘Mbosso’, wameachia video mpya ya wimbo unaitwa ‘Zilipendwa’, 

==Tazama hapo chini

Kikwete Awatetea Wapinzani......Ataka Wasichukuliwe kama Maadui

0
0
Rais mstaafu wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amevitaka vyama tawala barani Afrika kutovichukulia vyama vya upinzani kama maadui wa serikali badala yake vionekane kama moja ya nguzo muhimu katika kutimiza utawala wa sheria.

Aidha, Rais Kikwete amewataka wabunge wa vyama tawala pamoja na viongozi wengine, kuvikosoa vyama vyao pale vinapokwenda mrama badala ya kuwa waoga na kuunga mkono mambo yote.

Rais Kikwete ambaye ni maarufu Tanzania kwa jina la JK ameyasema hayo alipokuwa katika mkutano wa masuala ya uongozi barani Afrika wa mwaka 2017 (African Leadership Forum 2017) ambao umefanyikia nchini Afrika Kusini.

Viongozi wengine waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na Rais mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa, Rais mstsaafu wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki na Rais mstaafu wa Malawi, Bakili Muluzi.

Akizungumza katika kongamano hilo la siku mbili lililomalizika Agosti 25, 2017, JK alisema kuwa, kuvichukulia vyama vya upinzani au wanasiasa wa upinzani kama maadui, ni kutengeneza uadui ambao hauna ulazima katika nchi za Afrika.

Kikwete alisema kuwa vyama vya upinzani katika nchi nyingi za Afrika vina kazi kubwa ya kuhakikisha vinanadi sera zao kwa wananchi ili viweze kufahamika zaidi kwa vingi ni vichanga. Hii itasaidia wananchi kuwa na uelewa wa sera pamoja na mipango yao inapofika wakati wa uchaguzi wakiomba dhamana ya kuongoza nchi, alisema JK.

Mbali na wito huo kwa watawala, Rais Kikwete alivitaka vyama vya upinzania pia kukubali matokeo ya uchaguzi endapo umefanyika katika mazingira ya haki, uhuru na uwazi.

Kazi ya vyama vya upinzani ni kuhakikisha kuwa serikali inakuwa macho muda wote kutekeleza majukumu yake, lakini na wao wasiwe watu wa kupinga au kukataa kila jambo.

Kauli hii ya Rais Kikwete imekuja wakati ambao vyama vya upinzani nchini vinalalamika kuhusu kuzuiwa kwa mikutanao ya kisiasa, maandamano, pamoja na kukamatwa mara kwa mara kwa viongozi wa vyama vya upinzani.

Kwa upande wake Rais Mzee Mkapa, alivitaka vyombo vya habari na waandishi wa habari kuwa wazalendo kwa nchi zao wanapofanya kazi na waandike habari zitakazochochea maendeleo ya wananchi pamoja na kuzikosoa serikali kwa nia ya kujenga.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Polisi Yaanza Kuchunguza Mlipuko Ulioteketeza Ofisi za Mawakili Fatma Karume na Lawrence Marsha

0
0
Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya amethibitisha kushambuliwa ofisi za wanasheria za IMMMA saa 8 usiku wa kuamkia leo Jumamosi, Agosti 26.

Mkondya amesema polisi wanafanya uchunguzi kujua ni nini kilihusika katika tukio hilo la mlipuko.

“Tupo hapa eneo la tukio, uchunguzi unaendelea na ukikamilika tutawapa taarifa zaidi, ila hatujajua kama bomu limehusika,” amesema Mkondya.

Ameeleza hadi sasa hakuna watu wanaoshikiliwa kuhusika na tukio hilo.

Mmoja wa viongozi wa Kampuni ya IMMMA, Sadock Magai amesema hakuna wizi ambao umefanyika katika mali zilizokuwa ndani.

“Tuwaachie Jeshi la Polisi wafanye kazi yao,” amesema Magai.

Ofisi za wanasheria wa kampuni hiyo zipo Barabara ya Umoja wa Mataifa eneo la Upanga jijini hapa.

Miongoni mwa wamiliki wa kampuni hiyo ni Fatma Karume, ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.

Alikiba Na Diamond Waendelea Kuchuana Vikali YOUTUBE

0
0
Wimbo mpya wa Alikiba ‘Seduce Me’ ulioachiwa Ijumaa hii unaendelea kutrend kupitia mtandao wa video wa YouTube huku nafasi ya pili ukifuatiwa na wimbo mpya wa WCB, Zilipendwa.

Video ya muimbaji huyo wa RockStar400 mpaka sasa ina views 540,320 ikiwa ni video ya kwanza kuachiwa kabla ya WCB iliyoachiwa jioni yake.

Video ya WCB ‘Zilipendwa’ mpaka sasa ina views 222,962 ikiwa ina saa 12 toka iachiwe kupitia YouTube.

Kitendo cha WCB kuachia video ya wimbo huo muda mchache baada ya Alikiba kuachia Seduce Me, kumewafanya mashabiki wa wasanii hao kushindanisha project hizo mbili ambazo bado zinashindana kupitia mtandao wa YouTube.

Wawili hao kila mmoja anaonyesha bado ana hasira na mwenzake kwani kila mmoja anamtishia mwenzake ataachia ngoma nyingine.

Alikiba anadaiwa kutweet kwamba wimbo ‘Secude Me’ alikuwa anatesh mitando huku akidai ngoma kamili inakuja.

Kwa upande wa Diamond naye kupitia meneja wake Sallam amedai kwamba baada ya ‘Zilipendwa’ wataachia wimbo mpya ambao Diamond ameshirikiana na msanii mkubwa wa kimataifa.

==>Itazame  ZILIPENDWA  ya  Diamond

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya August 27

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya August 28

Tundu Lissu Aitisha Mgomo wa Mawikili Nchi Nzima

0
0
Baraza la Uongozi wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) limewataka mawakili nchi nzima kutokwenda mahakamani Jumanne na Jumatano kama njia ya kupinga Kampuni ya Immma Advocate kuvamiwa.

Akizungumza jana Jumapili, Rais wa TLS, Tundu Lissu alisema uamuzi huo umefikiwa jana na kikao cha baraza la uongozi la chama hicho.

Alisema mawakili wote wanaotetea wananchi kwenye mahakama na kwenye mabaraza wasifanye kazi siku hiyo.

Alisema baraza hilo linafahamu kwamba wateja wao wataathirika siku hizo lakini usalama wa mawakili ni muhimu zaidi.

Lissu alisema baraza la uongozi linavitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwahakikishia ulinzi mawakili wa Immma Advocate dhidi ya vitisho vinavyoweza kuhatarisha usalama wao.

Alisema baraza hilo linafanya jitihada za haraka za kukutana na Mkuu wa Jeshi la Polisi na Idara la usalama ili kujadiliana kuhusu shambulio hilo.

Lissu aliwataka wananchi kuhakikisha wanalinda usalama,uhuru na heshima ya wanasheria na mawakili ili waweze kutekeleza wajibu wao wa kuwatetea wananchi.

==>Lisome Tamko Zima hapo chini

CCM Yatangaza Kufuta Uchaguzi Kata 41

0
0
Chama  Cha Mapinduzi (CCM) kimeanza kupeleka salamu kwa wagombea wa nafasi mbalimbali, wanaokiuka Katiba na Kanuni za Uchaguzi, baada ya kufuta uchaguzi wa ndani ya chama hicho katika kata 41 kati ya kata 4,420 zinazoshiriki katika uchaguzi huo, kutokana na kubaini mchezo mchafu na kuagiza mchakato kurejewa upya.

Hayo yalibainishwa jana Dar es Salaam na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole alipozungumza na waandishi wa habari. 

“Hii ni awamu ya kwanza tunapeleka ujumbe kwa sababu wanaCCM wanataka CCM mpya inayosimamia haki, haya ni maelekezo na yanapaswa kuzingatiwa ili kurejesha hali ya uchaguzi katika eneo husika katika namna inayoheshimu Katiba na Kanuni ya Uchaguzi na Uongozi na Maadili,” alifafanua Polepole.

Polepole alibainisha kuwa kufutwa kwa uchaguzi huo ni agizo la viongozi wa juu wa chama hicho akiwemo Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais John Magufuli na Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana baada ya kusikiliza kwa kina kero na malalamiko ya kiuchaguzi ya wanachama wa CCM.

Akifafanua kuhusu suala hilo, alisema baada ya kusikiliza malalamiko hayo, Dk Magufuli alimuelekeza Kinana kuchukua hatua na kwa mamlaka aliyopewa, ameagiza kufutwa na kurejewa upya hivyo wanachama na viongozi wanatakiwa kufuata maagizo hayo.

Alizitaja kata hizo ambazo ni 20, ni za Mkoa wa Dar es Salaam na nafasi zinazotakiwa kurejewa katika mabano ni Kata ya Buguruni (Mwenyekiti na Katibu), Kata ya Liwiti (Katibu), Kata ya Kariakoo (Mwenyekiti, Katibu na Katibu Mwenezi), Kata ya Manzese (Mwenyekiti, Katibu na Katibu Mwenezi), kata za Makuburi, Mabibo na Kigamboni.

Nyingine ni Kiburugwa, Mchafukoge, Gerezani, Segerea (Mwenyekiti na Katibu), Pugu Stesheni (Mwenyekiti, Katibu na Katibu Mwenezi), Kata ya Mianzini, Kata ya Pugu (Katibu Mwenezi), Kata ya Ndugumbi, Kata ya Kilungule, Kata ya Makumbusho, Kata ya Kitunda (Katibu na Katibu Mwenezi), Kata ya Ukonga na Kata ya Msasani.

Polepole alieleza kuwa kata nyingine ni kutoka mikoa mingine ni 18 kutoka kata zote za Wilaya ya Simanjiro Mkoa wa Manyara, Kata ya Seria kwa vijana Wilaya ya Kondoa Mjini Mkoa wa Dodoma nafasi ya Katibu pamoja na Kata ya Mapinga wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

Alizitaja changamoto zilizojitokeza katika maeneo hayo na kusababisha uchaguzi huo kufutwa ni: Kuwepo kwa wanachama wanaoendeleza makundi yaliyokuwepo wakati wa Uchaguzi Mkuu, ambao wamekuwa wakipanga safu za uongozi na kuamua nani atakuwa kiongozi wa chama, jambo ambalo halikubaliki.

Pia alisema wapo viongozi ambao walishindwa kutoa usimamizi mzuri wa mali za chama na kusababisha upotevu mkubwa wa fedha na mali, lakini wamerejea katika nafasi hizo, jambo ambalo pia halikubaliki.

Aidha, alisema wapo wanachama waliokiuka misingi ambayo inamtaka mgombea kuwa mkazi wa eneo ambao unaomba dhamana ya uongozi, lakini kama siyo mkazi wa eneo hilo hupaswi kugombea, lakini wapo ambao si wakazi wameomba dhamana katika maeneo hayo, jambo ambalo halikubaliki.

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi CCM aliongeza kuwa katika uchaguzi huo, pia kumebainika kuwepo kwa vitendo vya uonevu na kutokutenda haki katika mchakato wa uchaguzi, kama ambavyo Katiba ya CCM inavyosema kuwa haki ni asili ya chama hicho.

Alisema changamoto nyingine ni kukiukwa kwa Katiba na Kanuni, baada ya maeneo mengine kutokutoa taarifa sahihi kuhusu wagombea, jambo ambalo limetajwa kama kupotosha vikao.

Machi mwaka huu, Rais Magufuli alionya kuwa mwanachama yeyote atakayebainika kutumia rushwa kwenye uchaguzi wa ndani wa chama hicho, jina lake halitarudi. Aliwataka wanachama wa chama hicho, bila ya kujali uwezo wao kifedha, wajitokeze kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali.

Alisema chama kitafuatilia kwa ukaribu mchakato wa uchaguzi wote kuanzia ngazi ya chini ili kujihakikishia kuwa watakaoshiriki kwenye vitendo vya rushwa, watachukuliwa hatua kali kwa mujibu wa Katiba, Kanuni za Uchaguzi na Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM.

Polisi, Jaji Mkuu Watoa ONYO Kuhusu Mgomo wa Mawaikili Nchini

0
0
Kaimu  Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma na Jeshi la Polisi nchini, wamelionya Baraza la Uongozi la Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), kutoingilia vyombo vya uchunguzi na upelelezi, vinavyochunguza tukio la mlipuko, uliotokea kwenye ofisi za Kampuni ya Mawakili ya IMMMA usiku wa kuamkia juzi jijini Dar es Salaam.

Profesa Juma jana  alisema TLS hawana haki ya kutoa agizo kwa mawakili, kutohudhuria mahakamani na kwenye mabaraza mengine, kwa kuwa kila wakili ana mkataba binafsi na mteja wake.

Profesa Juma alisema uhuru wa mahakama ni pamoja na kuheshimu mamlaka nyingine za nchi zinapokuwa zinafanya kazi zake. 

Alisema kwa kuwa tukio la kulipuliwa kwa ofisi za Mawakili wa Immma ni tukio la kihalifu, hivyo wanasheria waiache Polisi na vyombo vingine vya upelelezi kufanya kazi yao.

“Kama kutatokea wateja watakaolalamika kuwa mawakili wao hawakufika mahakamani siku ya Jumanne na Jumatano, hatua za kisheria dhidi ya mawakili hao zitachukuliwa ikiwemo kuwapeleka kwenye Kamati ya Maadili ya Mawakili,” alieleza Kaimu Jaji Mkuu.

Kwa upande wao, Jeshi la Polisi limesema liachwe liendelee na kazi ya uchunguzi, badala ya kulihusisha na tukio hilo.

Msemaji wa Jeshi hilo Makao Makuu, Kamishina Msaidizi Barnabas Mwakalukwa alisema Jeshi la Polisi ndicho chombo chenye mamlaka ya kufanya uchunguzi na hivyo kama kuna mtu yeyote mwenye taarifa yoyote kuhusu tukio hilo, anatakiwa kuzitoa polisi badala ya kuzungumza na vyombo vya habari.

Kauli hizo za Polisi na ya Kaimu Jaji Mkuu, zimekuja baada ya Rais wa TLS, Tundu Lissu kuwaeleza waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuwa Baraza lao la Uongozi lina taarifa kuwa kikundi cha watu wenye silaha za moto, wakiwa wamevalia sare za Jeshi la Polisi, kiliwateka nyara walinzi binafsi wa Kampuni ya IMMMA na kuingia ndani ya eneo la ofisi hizo.

Lissu alidai watu hao baada ya kuingia ndani, walitega milipuko na madumu manne ya mafuta ya petroli katika maeneo kadhaa ya jengo la ofisi hizo. 

Alidai muda mfupi baadaye, milipuko hiyo ililipuka na kusababisha uharibifu mkubwa wa jengo la ofisi za IMMMA Advocates zilizoko Upanga pamoja na majengo jirani.

“Kama Lissu ana hizo taarifa alitakiwa azilete polisi kwa kuwa ndicho chombo cha uchunguzi badala ya kuzungumza na vyombo vya habari. 

"Kazi ya polisi ni kufanya uchunguzi wa kina na ndiyo maana Kaimu Kamanda wa Kanda Maalumu alisema atatoa taarifa uchunguzi ukikamilika, hivyo watu wanapaswa kusubiri taarifa kamili, nje ya hapo tunakuwa tunafanya kazi nje ya utawala wa sheria,” alieleza Msemaji wa Jeshi la Polisi, Mwakalukwa.

Mwakalukwa alivitaka vyombo vya habari, kuwatafuta walinzi hao ambao Lissu alidai walitekwa na watu wanaodhaniwa kuwa polisi ili waeleze tukio lilivyokuwa na ikibidi walinzi hao kutoa taarifa za kutekwa kwao polisi.

Alisema jambo hilo siyo dogo, hivyo watu waviache vyombo vya uchunguzi, viendelee na kazi yake kwani uchunguzi pekee ndiyo utakaobaini chanzo na wahusika. 

Ili kuonesha mshikamano, Baraza la Uongozi la TLS limewataka mawakili wote ambao ni wanachama wao nchini, wasuse kuhudhuria mahakamani na kwenye mabaraza ya aina zote kwa siku mbili, kesho na keshokutwa.

Polisi Singida waua mtu mmoja akidaiwa kuwa jambazi

0
0
Mkazi wa kijiji cha Shiponga, Hanang Mkoani Manyara anayedaiwa kuwa jambazi, Hamisi Athumani (32), amefariki dunia baada ya kupigwa risasi kiunoni na askari polisi wakati akiwa katika harakati ya kutoroka.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani hapa, ACP Debora Magiligimba, amesema tukio hilo limetokea Agosti 25 mwaka huu saa nane mchana, huko katika kijiji cha Mgori tarafa ya Ngimu wilaya ya Singida.

Amefafanua kuwa Hamisi (marehemu) alipigwa risasi na askari polisi wakati akijaribu kuwatoroka mara baada kuonyesha bunduki aina ya rifle yenye namba 7358 na risasi zake tano.

Amesema bunduki hiyo iliyokuwa imekatwa mtutu na risasi zake tano zilikuwa zimefichwa kwenye soksi, vitu hivyo vilikuwa vilihifadhiwa kwenye mfuko wa sandarusi, na kufichwa chini ya jiwe.

ACP Magiligimba amesema Agosti 23 mwaka huu, mtuhumiwa alikamatwa na wananchi wa kijiji cha Ngamu, na kufikishwa katika kituo cha polisi cha kijiji hicho kwa tuhuma ya kujihusisha na matukio ya ujambazi.

“Kesho yake mtuhumiwa alihojiwa na kukiri kujihusisha na matukio ya ujambazi wa kutumia silaha katika mikoa mbalimbali. Pia aliahidi kuwapeleka askari kuwaonyesha mahali alikoificha silaha anayoitumia kwenye matukio hayo ya ujambazi,” amesema ACP Magiligimba.

Kamanda huyo amesema Agosti 25 mwaka huu saa sita mchana, askari polisi wakiwa na mtuhumiwa, walikwenda katika pori la kijiji cha Mgori mahali alipokuwa ameficha bunduki hiyo aina ya rifle.

“Mara tu baada ya kuwaonyesha askari hao silaha hiyo na wakati askari wanaendelea kufanya upekuzi katika eneo hilo, mtuhumiwa alijaribu kutoroka askari kwa kukimbia” amesema na kuongeza.

“Askari mmoja alifyatua risasi tatu hewani akimtaka asimame, lakini hakutii. Ndipo alipompiga risasi moja iliyompata sehemu ya kiunoni”.

Amesema jereha hilo la risasi lilisababisha mtuhumiwa Hamisi avuje damu nyingi, na hivyo kufariki dunia wakati akikimbizwa hospitali ya mkoa kwa matibabu.

“Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linaendelea kutoa wito kwa wananchi waote kutoa taarifa zitakazosaidia kubaini wahalifu katika maeneo yao ili hatua ziweze kuchukuliwa kudhibiti vitendo vya kihalifu,” amesema kamanda huyo.

Waziri Nchemba aliagiza Jeshi la Polisi kuwakamata wasiovaa kofia ngumu

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ameliagiza Jeshi la Polisi nchini kuwakamata wamiliki wapikipiki ambao watashindwa kuwa na kofia ngumu za pikipiki maarufu kama bodaboda.

Waziri Mwigulu ameyaongea hayo akiongea na madareva wa pikipiki wa wilaya ya shinyanga ambao wanapatiwa mafunzo ya usalama barabarani mkoani humo, Waziri Mwigulu amesema Polisi sasa wakiwakamata madereva wa pikipiki wakiwa hawana kofia ngumu wawaulize mmiliki wa pikipiki ni nani naye akamatwe aulizwe kwanini hana kafia ngumu awekwe ndani

Waziri Mwigulu amesema pia kama abiria naye akikataa kuvaa kofia ngumu na wakati pikipiki ina kofia hizo basi naye akamatwe na dereva pikipiki achiwe aendelee na biashara kwani kila mtu lazima atimize wajibu wake hivyo anatoa mwezi mmoja madereva wote wa pikipiki na wamiliki wahakikishe wanakofia ngumu mbili za pikipiki.

Naye mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini Steven Masele amesema zamani palikuwa na msugaono mkubwa sana kati ya madereva wa pikipiki na askari wa jeshi la polisi hali iliyopelekea kutokuwa na mahusiano mazuri kati yao lakini kwasasa hivi kuna uhusiano mzuri uliojengwa na RPC mpya.

Kamanda wa polisi mkoa wa shinyanga ACP Simon Haule amesema mafunzo hayo ni utekelezaji wa maagizo na mkuu wamkoa baada ya wananchi wengi kutojua au kutokutumia sheria ya matumizi ya barabara hasa katika mzunguko (roundabout).

Naye mmoja wa madereva wa pikipiki wilaya ya shinyanga ameeleza kwasasa changamoto kubwa wanayokutana ni mfumo usiorafiki wa upatika wa leseni ya udereva hivyo kufanya madereva wengi wapikipiki kutokuwa na leseni kwani ni zaidi ya miezi sita tangu alipie kupata leseni hiyo. Waziri Mwigulu amesema anachukua hilo watalifanyia kazi

Tanzania Kufungua Ubalozi nchini Cuba

0
0
Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Cuba, Gladys Bejarano na kumhakikishia ufunguzi wa ofi si za ubalozi wa Tanzania nchini humo.

Amesema Tanzania inayatambua na kuyathamini mahusiano mazuri ya kidiplomasia, kisiasa, kiuchumi, kielimu, kiafya na kiutamaduni kati yake na Cuba, hivyo inatarajia kufungua ubalozi nchini humo ili kurahisisha utendaji wa kazi za kibalozi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Majaliwa alikutana na Bejarano juzi jioni wakati alipokuwa akihitimisha ziara yake ya kikazi nchini Cuba. Malengo ya ziara yalikuwa ni kuimarisha na kudumisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

“Tunatambua uhusiano mzuri uliopo kati Tanzania na Cuba, ambao ulikuwepo kuanzia Serikali ya Awamu ya kwanza chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, hivyo lazima tufungue ofisi za ubalozi na tutamleta balozi wetu hapa,” alieleza Majaliwa.

Pia Waziri Mkuu aliishukuru Serikali ya Cuba kwa ujenzi wa kiwanda cha dawa za kuulia vijidudu vya malaria pamoja na ufadhili wa masomo ya udaktari, inaoutoa kwa wanafunzi wa Tanzania wanaosoma katika vyuo mbalimbali nchini humo.

Aliiomba serikali hiyo iendelee kutoa ufadhili wa masomo kwa madaktari hao hadi ngazi ya Shahada ya Uzamili kwa sababu Serikali ya Tanzania inawahitaji madaktari bingwa wengi kwani walioko nchini ni wachache.

Kwa upande wake, Bejarano alimshukuru Waziri Mkuu kwa kufanya ziara nchini Cuba na alimhakikishia kwamba uhusiano wa serikali yake na Serikali ya Tanzania utaendelea kuimarishwa kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.

Alisema Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais John Magufuli, inafanya jitihada kubwa za kuhakikisha uchumi wake unakua kwa kasi jambo ambalo ni tofauti na mataifa mengine.

Makamu huyo wa Rais alisema Serikali ya Cuba itaendelea kushirikiana na Tanzania katika uboreshaji wa sekta za afya, utamaduni, kilimo, uchumi na elimu. Kuhusu ombi la kuongeza ufadhili wa shahada ya uzamili kwa madaktari, alisema amelip
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images