Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli aifumua Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 23 Agosti, 2017 amemteua Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi kuwa Kamishna wa Operesheni wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya.

Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi anachukua nafasi ya Bw. Mihayo Msikela ambaye amerejeshwa Makao Makuu ya Polisi.

Uteuzi wa Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi unaanza mara moja.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amezungumza na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa Kulevya Bw. Rogers William Siyanga ambaye amemhakikishia kuwa kazi ya kukabiliana na tatizo la biashara na matumizi ya dawa za kulevya inaendelea vizuri.

Bw. Rogers William Siyanga amesema tatizo la dawa za kulevya lilikuwa kubwa na ametaja dawa za kulevya ambazo Mamlaka inapambana nazo kuwa ni bangi, heroine, cocaine, kemikali bashirifu na kwamba kwa sasa imeanza kukamata na kuharibu mashamba ya bangi na bangi iliyovunwa.

Amebainisha mikakati mitatu inayotumika katika mapambano dhidi ya tatizo hilo kuwa ni kuzuia dawa za kulevya zisiingie nchini, kutoa elimu kuanzia shule za msingi, sekondari, vyuo na kwenye jamii ili watu waache kutumia dawa za kulevya na kutoa tiba kwa watu walioathirika na dawa za kulevya, na pia ametoa wito kwa watu wenye waathirika wa dawa za kulevya kuwapeleka katika mamlaka hiyo ili watibiwe.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

23 Agosti, 2017

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Uingereza yatoa Tsh 1.007 trilioni kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania.

Waziri Mwijage Aivaa TRA.....Aitaka Isimfanye Akatumbuliwa na Rais

$
0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage ameitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutomfukuzisha kazi kwa uzembe wao uliopelekea nchi kupigwa na kupata hasara kutokana na watu kuingiza cement kutoka nje ya nchi wakidai ni krinka.

Waziri Mwijaga alisema hayo jana kupitia kipindi cha HOTMIX na ambapo alitumia nafasi hiyo kupiga marufuku Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kukagua krinka yoyote kutoka nje ya nchi.

"Mtu anatengeneza Krinka anauza Kenya, sasa kama mtu anatengeneza Krinka Tanga anauza Kenya wewe unafuata nini Pakistan? Hakuna krinka inatoka nje ya nchi ile ni Cement iliyokamilika TRA wanashindwa kufanya kazi yao, narudia kusema hakuna krinka inaingia nchini kutoka nje ile ni Cement kamili na anayepinga aje aniambie mimi, na kuanzia leo TBS wasikague krinka yoyote kutoka nje ya nchi waingize ndani ya nchi bila TBS kukagua, TBS ipo chini yangu sasa kama mimi naambiwa sitoshi na wa TBS ajiangalie" alisema Mwijage

Aidha Waziri Mwijage alidai kuwa watu wa Cement walikubaliana na DR Meru kununua hizo Krinka hapa hapa nchini

"Watu wa Cement walikubaliana hapa na Dr. Meru, Twiga Cement ananunua Krinka, Simba Cement ....mwingine nani ananunua krinka nyingine kutoka wapi, watu wanaleta cement iliyokamilika wanasema Krinka sasa kuanzia leo TBS hawezi kukagua krinka yoyote kutoka nje ya nchi, mpaka mamlaka iliyopo juu yangu sasa kama TRA walizembea tukapigwa juu yao kwanini wanataka kuniharibiana kazi, eti bwana wanataka kuniharibia kazi mimi" alisisitiza Waziri Mwijage

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya August 24

Chadema yapata pigo tena, yakimbiwa na madiwani wengine

$
0
0
Madiwani watatu wa Chadema Manispaa ya Iringa wameamua kuachia nafasi zao kwa madai ya mwenendo mbaya wa chama.

Madiwani hao walichukua uamuzi huo baada ya kumwandikia barua ya kujiuzulu mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa. Madiwani ambao wamechukua uamuzi huo ni Baraka Kimata wa Kata ya Kitwiru na wawili wa viti maalumu; Husna Ngasi na Leah Mlelewa.

Wakizungumzia uamuzi huo, viongozi hao walisema kuwa wameamua kufanya hivyo baada ya kuchoshwa na mwenendo wa chama hicho.

Kimata alisema anaendelea na kazi zake nje ya siasa na kwamba, hatabaki na nafasi yoyote ndani ya chama hicho.

Alisema kuwa ushirikiano mdogo kati yake na mbunge wa jimbo hilo umemsukuma kuachia nafasi yake hiyo.

Kwa upande wake, diwani mwingine ambaye alikuwa katibu wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Mlelewa alisema hatabaki na nafasi yoyote ndani ya chama hicho kama ilivyo kwa Kimata.

Madiwani wengine wa Chadema ambao walijiuzulu kutoka Jimbo la Arumeru Mashariki ni Anderson Sikawa, Emmanuel Mollel, Greyson Isangya na Josephine Mshiu pamoja na diwani wa Murieti, Credo Kifukwe.

Dalala Lagonga Treni Morogoro Na Kuua Watu Kadhaa

$
0
0

Watu ambao idadi yake haijaweza kufahamika mara moja, wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa, baada ya daladala waliyokuwa wakisafiria kugonga treni mkoani Morogoro.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Urich Matei, amesema ajali hiyo imetokea leo asubuhi na imehusisha gari aina ya daladala yenye amba za usajili T 438 ADR iliyokuwa inakwenda Mvumi kwenye njia panda inayoingilia treni ndipo ikagonga treni hiyo, na kuburuzwa takribani mita 200.

Kamanda Matei amesema chanzo cha ajali hiyo ni daladala kuingia kwenye njia ya treni bila kusimama ili kuangalia kama kuna treni inakuja, ndipo treni hiyo ikaburuza gari hiyo kwa umbali mrefu na kusababisha maafa hayo.

Idadi rasmi ya majeruhi bado haijafahamika rasmi mpaka sasa na majeruhi wamepelekwa hospitali ya mkoa wa Morogoro


Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Mrithi wa Jamal Malinzi TFF aanza kufanya mageuzi

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Wallace Karia amewateua Makamu wa Rais wa zamani wa TFF, Athuman Nyamlani na Ahmed Mgoyi kuwa Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF. Rais Karia ameteua kwa kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo katika Katiba ya TFF ikiwa ni wiki moja baada ya kupatikana kwa viongozi wa shirikisho katika uchaguzi mkuu uliofanyika Agosti 12, mwaka huu.

Rais Karia aliwatambulisha viongozi hao kwenye Kikao cha Kamati ya Utendaji iliyofanyika Jumanne Agosti 22, mwaka huu jijini Dar es Salaam. Katika kikao hicho pia Rais Karia alitumia fursa hiyo kutangaza viongozi wa kamati mbalimbali za TFF zikiwamo za kinidhamu na kisheria.

Kamati ya Nidhamu: Mwenyekiti Tarimba Abbas, Makamu Mwenyekiti, Peter Hella wakati wajumbe ni Boniface Lyamwike, Dk. Bill Haonga na Kassim Dau.

Kamati ya Rufani za Nidhamu: Mwenyekiti ni Wakili Rahim Zuber Shaban; Makamu Mwenyekiti, Stella Mwakingwe wakati Wajumbe ni Abbas Mtemvu, Amani Mulika na Siza Chenja.

Kamati ya Maadili: Mwenyekiti ni Wakili Hamidu Mbwezeleni, Makamu Mwenyekiti ni Wakili Steven Zangira wakati Wajumbe ni Glorious Luoga, Walter Lungu na Amin Bakhressa.

Kamati ya Rufaa ya Maadili: Mwenyekiti ni Wakili Ebenezer Mshana; Makamu Mwenyekiti ni DCP. Mohammed Mpinga na wajumbe  ni Wakili Benjamin Karume, George Mayawa na ASP. Benedict Nyagabona.

Kamati ya Uchaguzi: Mwenyekiti ni Revocatus Kuuli; Makamu Mwenyekiti ni Wakili Mohammed Mchengerwa; Wakili Edwin Mgendera; Wakili Kiomoni Kibamba na Wakili Thadeus Karua.

Kamati ya Rufani ya Uchaguzi: Mwenyekiti ni Kenneth Mwenda; Makamu Mwenyekiti ni Jabir Shekimweri na Wajumbe ni Wakili Rashid Sadalla, Irene Kadushi na Mohammed Gombati.

Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji: Mwenyekiti ni Elias Mwanjala; Makamu Mwenyekiti ni Wakili Malangwe Mchungahela wakati Wajumbe ni Zakaria Hanspope, Robert Selasela, Goodluck Moshi, Mhandisi Issa Batenga na Hamis Semka.

Kamati ya Fedha na Mipango: Mwenyekiti ni Michael Wambura; Makamu Mwenyekiti ni Francis Ndulane na Wajumbe ni Almas Kasongo, Pascal Kihanga, Maximillian Tabonwa, Paul Bilabaye na Farid Abeid.

Kamati ya Mashindano: Mwenyekiti ni Ahmed Mgoyi; Makamu Mwenyekiti ni James Mhagama wakati Wajumbe ni Kenneth Pesambili, Shafii Dauda, Fortunatus Kalewa na Mhandisi Andrew Makota.

Kamati ya Ufundi: Mwenyekiti ni Vedastus Lufano; Makamu Mwenyekiti ni Issa Bukuku na wajumbe ni Sarah Chao, Ally Mayay, Michael Bundala, Omar Abdulkadir na Israel Mujuni.

Kamati ya Soka la Vijana: Mwenyekiti ni Khalid Abdallah; Makamu Mwenyekiti ni Lameck Nyambaya na Wajumbe ni Mohammed Aden, Ramadhani Nassib, Salim Kibwana na Vicent Majili.

Kamati ya Mpira wa Wanawake: Mwenyekiti ni Amina Karuma; Makamu Mwenyekiti ni Rose Kissiwa na Katibu wa Kamati hiyo ni Somoe Ng’itu wakati Wajumbe ni Zena Chande, Beatrice Mgaya, Sofia Tigalyoma, Zuhura Kapama na Nia Mjengwa.

Kamati ya Waamuzi: Mwenyekiti ni Saloum Chama; Makamu Mwenyekiti Joseph Mapunda wakati Wajumbe ni Nassib Mabrouk, Leslie Liunda na Soud Abdi.

Kamati ya Habari na Masoko: Mwenyekiti ni Dunstan Mkundi; Makamu Mwenyekiti ni Mbasha Matutu wakati Wajumbe ni Imani Kajura, Mgaya Kingoba, Godfrey Dilunga na Samson Mbamba.

Kamati ya Ukaguzi wa Fedha: Mwenyekiti ni Yahya Hamad; Makamu Mwenyekiti ni Athuman Nyamlani na Wajumbe ni Khalifa Mgonja, Japhary Kachenje, Jackson Songoro na Benesta Rugora.

Kamati ya Tiba: Mwenyekiti ni Dkt. Paulo Marealle; Makamu Mwenyekiti ni Dkt. Fred Limbanga Wakati wajumbe ni Dkt. Norman Sabun, Dkt. Lisobina Kisongo, Dkt. Eliezer Ndalama, Dkt. Elson Maeja na Violet Lupondo.

Kamati ya Futsal na Beach Soccer: Mwenyekiti ni Ahmed Mgoyi; Makamu Mwenyekiti ni Hussein Mwamba na Wajumbe ni Blassy Kiondo, Isaac Munisi, Didas Zimbihile na Aaron Nyanda.

Kamati ya Ajira: Mwenyekiti ni Issa Bukuku; Makamu Mwenyekiti ni Saloum Chama wakati Wajumbe ni Athuman Kihamia, Mtemi Ramadhani, Noel Kazimoto na Hawa Mniga.

Kamati ya Leseni za Klabu: Mwenyekiti ni Wakili Lloyd Nchunga; Makamu Mwenyekiti Wakili Emmanuel Matondo wakati Wajumbe ni Profesa Mshindo Msolla, Hamisi Kissiwa na David Kivembele.

Kamati ya Rufaa za Leseni: Mwenyekiti Wakili Dk. Damas Ndumbaro; Makamu Mwenyekiti ni Wakili Alex Mngongolwa Wajumbe ni Meneja wa zamani wa Uwanja wa Taifa, Charles Matoke, Tumainiel Mlango na Ahmed Menye.

Majaliwa awakaribisha wafanyabiashara kutoka Cuba

$
0
0
Serikali imewakaribisha wawekezaji kutoka nchini Cuba waje kuwekeza kwakuwa kuna fursa nyingi hapa Tanzania na kama zitatumika vizuri basi zitawezesha uchumi kuendelea kukua kwa kasi.

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Havana nchini Cuba mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Cuba, Lucas Domingo Polledo, ambapo amewakaribisha wafanyabiashara wa Cuba kuja kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vya dawa.

Amesema kwa sasa Serikali ya Tanzania inaagiza dawa kutoka nje ya nchi jambo ambalo linasababisha kutumia fedha nyingi, hivyo uwepo wa kiwanda utasaidia katika kupunguza gharama.

Majaliwa ameongeza kuwa Serikali imedhamiria kuendeleza sekta ya viwanda nchini kama mkakati wa kukuza uchumi na kufikia uchumi wa kati, hivyo wafa

IGP Simon Sirro afanya Mabadiliko Makubwa Ya Jeshi la Polisi

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Nyakoro Sirro amefanya mabadiliko ya makamanda wa polisi mikoani.

Taarifa ambayo imetolewa na msemaji wa Jeshi la Polisi   Barnabas Mwakalukwa  imesema kwamba  Sirro amemteua Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Juma Yusuf Ally kuwa Kaimu Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Uteuzi huo unafuatia kustaafu kwa aliyekuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar Kamishna Hamdani Omari Makame kwa mujibu wa sheria baada ya kutimiza umri wa miaka sitini (60).

Kabla ya uteuzi huo DCP Juma alikuwa ni Mkuu wa Utawala na Fedha Makao Makuu ya Polisi Zanzibar.

IGP Sirro pia amemteua Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi  (SACP) Lazaro Mambosasa kuwa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam.

Kabla ya uteuzi huo, SACP Mambosasa alikuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.

Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Kaimu Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi  (SACP) Neema Mwalimu Mwanga anakwenda Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam.

IGP Sirro pia amemteua aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Gilles Bilabaye Mroto kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma na  Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Emmanuel Lukula kwenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke.

Kabla ya uteuzi huo, ACP Lukula alikuwa Ofisa Mnadhimu wa Polisi mkoa wa Mbeya.

Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi wote kuendela kushirikiana na Jeshi hilo kwa kufichua taarifa za uhalifu na wahalifu ili kwa pamoja tuendelee kuiweka Tanzania salama.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Maswa 22 Ambayo Mkuu wa Wilaya Hai Aliwauliza Walimu Kabla ya Kuamuru Mwalimu Mmoja Akamatwe Baada ya Kushindwa Kutaja Jina Lake

$
0
0
Wakati sakata la Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gelasius Byakanwa kumsweka mahabusu mwalimu wa sekondari kwa kushindwa kutaja jina lake likiendelea kuzua mjadala, imedaiwa kuwa siku hiyo aliwauliza walimu aliokuwa na kikao nao maswali 22.

Tukio hilo la Byakanwa kudaiwa kuamuru kukamatwa na kuwekwa mahabusu mwalimu huo wa Shule ya Sekondari Lerai, Erasto Mhagama, ndilo limekuwa gumzo katika mitandao ya kijamii.

Mbali na kubamba mitandao ya kijamii, walimu katika mijumuiko mbalimbali na kupitia Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na makundi ya WhatsApp ya walimu, tukio hilo ndilo linalojadiliwa zaidi katika mitandao hiyo.

Inadaiwa baada ya mwalimu huyo kushindwa kuandika jina la mkuu wa wilaya, kiongozi huyo alimtaka achague mojawapo ya adhabu kati ya kupiga pushup 20  au kwenda mahabusu ya polisi.

Mwalimu huyo alimweleza mkuu huyo wa wilaya kuwa asingeweza kupiga pushup kwa kuwa ana matatizo ya kiafya, ndipo mkuu wa wilaya alipoita polisi na kumpeleka mahabusu.

Ilielezwa kuwa katika kikao hicho na walimu wa shule mbili za sekondari Boma na Lerai, mkuu huyo wa wilaya alianza kwa kugawa karatasi na kuwauliza walimu kama kuna anayemfahamu.

Alipowauliza swali hilo walimu wa Shule ya Lerai, ni mmoja tu aliyesema anamfahamu ndipo alipowataka wengine wote kuandika jina lake kwenye karatasi.

Baadaye alimsimamisha mwalimu mmoja baada ya mwingine akitaka waende ubaoni kuandika maneno au kuweka majibu ya maswali atakayowauliza na maswali hayo yalikuwa kama ifuatayo:

1.Nani ambaye ananifahamu?

2. Kila mmoja aaandike jina langu kwenye hiyo karatasi

3. Waziri mkuu wa awamu ya tatu ni nani?

4. Nitajie kirefu cha CDF (Chief of Defence Forces)

5. Nitajie Waziri wa Nishati na Madini

6. Andika kirefu cha DC (District Commissioner)

7. Andika neno IGP na kirefu chake

8. Andika neno CDF na kirefu chake

9. Andika CUF na kirefu chake

10. Andika CAF na kirefu chake

11. Andika neno Tanu na kirefu chake.

12. Andika TLP na kirefu chake

13. Agronomy means what?

14. Nani ni viongozi wakuu wa CUF. Baada ya kujibiwa ni Profesa Ibrahim Lipumba na Maalim Seif Sharifu Hamad akauliza mkutano wao mkuu wa mwisho ulikuwa lini?

15. Nani ni kiongozi wa CAF (Confederation of African Football)

16. Nitajie IGP (Inspekta Jenerali wa Polisi) ni nani na CDF (mkuu wa majeshi) ni nani kwa majina

17. Mwenye cheo cha CDF ni nani

18. Mwamunyange mnamfahamu? Ni Nani

19. Baada ya kustaafu Mwamunyange akaja nani?

20. Mkuu wa Majeshi kwa Kiingereza anaitwaje?

21. Rais wa CAF ni nani?

22. Andika pale ubaoni Chief of Defence Forces

TFF yaomba radhi kwa makosa ya kiuandishi kwenye Ngao ya Jamii Waliyopewa Simba Jana

$
0
0
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limeomba radhi wanafamilia wote wa mpira wa miguu nchini kutokana na makosa ya kiuandishi yaliyoonekana kwenye utambulisho wa Ngao ya Jamii iliyotolewa Jumatano Agosti 23, 2017 kwa klabu ya Simba.

Ngao hiyo ilitolewa mara baada ya mchezo uliokutanisha timu za Simba SC na Yanga SC zote za Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo, Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 dhidi ya Yanga na kutwaa ngao hiyo.

Makosa yaliyoonekana katika ngao hiyo ya jamii ni kukosewa kuandikwa kwa neno “SHIELD” ambapo liliandikwa “SHEILD” na hivyo kupoteza maana yake ya msingi.

Katika taarifa ya TFF iliyotolewa leo Agosti 24 wamesema kwamba “Watanzania hususani wanafamilia ya mpira wa miguu popote pale, TFF hatujapokea vizuri mwonekana wenye makosa kwenye Ngao hiyo ya Jamii kama ambavyo wadau hawajapokea vema suala hili.”

Kuonyesha kukerwa na uzembe huo uliofanywa na baadhi ya viongozi wake, Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, tayari amechukua hatua za kinidhamu kwa watumishi waliohusika.

Mbali na hilo, kiongozi huyo amewasiliana na uongozi wa Simba SC kuirejesha ngao hiyo ili kufanyiwa marekebisho yatakayobaki kwenye kumbukumbu sahihi.

Uongozi wa TFF umesisitiza kuwa hatutegemei tukio kama hili kujirudia tena.

Kilichoendelea Leo Mahakamani Baada ya Jamali Malinzi Kufikishwa Mahakamani

$
0
0
Upande wa utetezi katika kesi inayomkabili aliyekuwa Rais wa TFF, Jamal Malinzi na wenzake umeiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu itoe maelekezo mahususi kwa upande Serikali kuharakisha upelelezi, kinyume na hapo Mahakama iwasikilize na iwaachiwe.

Wakili wa utetezi, Domician Rwegoshora amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Wilfred Mashauri kwamba wanautaka upande wa mashtaka uharakishe upelelezi kwa sababu kesi hiyo haina dhamana, hivyo washtakiwa wakiendelea kukaa ndani wanateseka.

"Mahakama itoe maelezo mahususi kwa upande wa mashtaka kwa muda mfupi, au washtakiwa wasikilizwe ikiwezekana Mahakama iwaachie.”  Amesema Wakili  Domician Rwegoshora.

Baada ya kueleza hayo, Wakili wa Serikali, Vitalis akaeleza kuwa upelelezi upo katika hatua ya mwisho na muda si mrefu itaanza kusikilizwa.

Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi September 9, 2017 huku akiutaka upande wa Serikali kuharakisha na ikiwezekana katika tarehe hiyo watoe taarifa kuhusu upelelezi.

Mahakama yaijia juu Tanroads kwa kubomoa nyumba iliyozipa kinga

$
0
0
Baada ya Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kubomoa baadhi ya nyumba zilizowekewa kinga ya muda, Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi imesema hilo ni kosa la kuupuza amri ya mahakamana na kueleza hatua ambazo waathirika wanapaswa kuzichukua.

Msajili wa mahakama hiyo, Frank Mahimbali jana alisema kuwa wanachoweza kufanya waathirika ni kwenda mahakamani kuomba iwaite waliohusika na ubomoaji huo ili wajieleze ni kwa nini wasifungwe kwa kupuuza amri ya mahakama.

Mahimbali alisema mtuhumiwa akitiwa hatiani anaweza kufungwa jela.

Ijumaa iliyopita, mahakama hiyo ilitoa amri ya zuio la muda la ubomoaji kwa nyumba 286 zilizoko katika operesheni ya bomoabomoa maeneo mbalimbali kati ya Ubungo Maji na Kiluvya, zilizojengwa ndani ya umbali wa mita 121.5 kutoka katikati ya Barabara ya Morogoro.

Amri hiyo ilitolewa na Jaji Leila Mgonya baada ya maombi ya dharura yaliyowasilishwa na wakazi 286 wa maeneo hayo, wakiomba mahakama itoe zuio nyumba zao zisibomolewa kusubiri kesi yao ya msingi itakapoamuriwa.

Hata hivyo, juzi Tanroads ilibomoa nyumba tatu katika eneo la Kimara Stop Over, ambazo ni kati ya hizo 286. Nyumba hizo zilizobomolewa ni pamoja na Nicomed Leo na ya Aisha Juma.

Wakati mahakama ikitoa msimamo na maelekezo hayo kwa waathirika wa bomoabomoa hiyo ambao nyumba zao zimewekewa kinga hiyo, wakili wao Benedicto Mandele alisema jana kuwa tayari wameshamwandikia barua Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kueleza malalamiko yao na hatua wanazopanga kuzichukua.

Wakili Mandele alisema katika barua hiyo ambayo pia nakala yake imetumwa kwa Jaji Mgonya, Meneja wa Tanroads Mkoa wa Dar es Saalam, Ofisa Mtendaji wa Tanroads, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na Kamanda wa Polisi Kinondoni, wateja wake wameeleza kusikitishwa kwao na kitendo hicho wakati kuna amri ambayo ilibandikwa kwenye nyumba hizo.

“Tayari barua hiyo imepokewa leo (jana) saa nne na sasa hapa ninaandaa maombi kwa ajili ya kumuita meneja wa mkoa wa Tanroads afike mahakamani kujieleza ni kwa nini asifungwe jela kama mfungwa wa kesi ya madai kwa kupuuza amri ya mahakama,” alisema Wakili Mandele na kuongeza kuwa maombi hayo dhidi ya meneja huyo wa Tanroads atapeleka mahakamani leo baada ya wateja wake kuweka saini.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

LHRC walaani TANROADS Kupuuza Amri ya Mahakama

$
0
0
Kituo cha Sheria na haki za Binadamu (LHRC) kimelaani vikali vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu vinavyoendelea nchini.

Pia wamelaani  kitendo cha Wakala wa barabara nchini (Tanroads) kuidharau mahakama na kuminywa kwa haki za wanasiasa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho, Hellen Kijo-Bisimba amesema wameshangazwa na uamuzi wa Tanroads wa kubomoa nyumba za wananchi wa Kimara hadi Kiluvya wakati wanapingamizi la Mahakama.

"Tunalaani kitendo hiki na tunaona ilichofanya Tanroads ni kuidharau Mahakama ambapo kwa lugha ya kisheria tunaita Contempt of Court(kuiingilia Mahakama) "amesema 

Mkurugenzi huyo pia amesema wanalaani kitendo cha kukamatwa ovyo kwa wanasiasa na kusema kitendo hicho ni kuminywa kwa haki za kisiasa.

"Hali hii imejitokeza sana kwa kuwanyanyasa wabunge wa vyama vya upinzani bila kufuata misingi ya kisheria na haki za binadamu "amesema 

Amesema  ukamatwaji wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Bunda mjini Ester Bulaya aliyekamatwa akiwa hotelini kwa tuhuma za kutaka kuhudhuria mkutano nje ya jimbo lake na kudai kuwa huo ni ukiukwaji wa haki na kunyimwa uhuru wa vyama vya upinzani kufanya kazi yake.

Rais aeleza kitu kimoja kinachomkera kuhusu utendaji wa TAKUKUR

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 24 Agosti, 2017 amemuapisha Brigedia Jenerali John Julius Mbungo kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Hafla ya kuapishwa kwa Brigedia Jenerali John Julius Mbungo imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Mcheche Masaju, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Anjellah Kairuki, Waziri wa Sheria na Katiba Mhe. Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi na Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Pamoja na kula kiapo cha kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali John Julius Mbungo amekula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Mstaafu Harold Nsekela.

Akizungumza mara baada ya kiapo Mhe. Rais Magufuli amewataka viongozi wote nchini kushirikiana katika jukumu la mapambano dhidi ya rushwa ili kuepusha madhara ya tatizo hilo katika uchumi na ustawi wa jamii.

“Ukiangalia mambo makubwa tunayopambana nayo yanasababishwa na rushwa iliyosambaa kila mahali, watumishi hewa chanzo ni rushwa, dawa za kulevya ndani yake kuna rushwa, vyeti feki ndani kuna rushwa, mikataba mibovu ndani kuna rushwa, pembejeo za ruzuku ndani kuna rushwa na huko mahakamani nako ni rushwa tu” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli ameipongeza TAKUKURU kwa kazi iliyoanza kuifanya lakini ametaka juhudi zaidi ziongezwe ili watu wote wanaojihusisha na vitendo vya kutoa na kupokea rushwa washughulikiwe kwa mujibu wa sheria.

Hata hivyo Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutoridhishwa kwake na taratibu za uchunguzi na uendeshaji wa mashitaka ya rushwa zinavyochukua muda mrefu na ametoa wito kwa viongozi wa TAKUKURU kufanyia kazi eneo hilo ili vita dhidi ya rushwa ionekane ikizaa matunda haraka.

“Tukifanikiwa kupunguza rushwa kwa angalau asilimia 80, nchi yetu itafanikiwa kutatua matatizo mengi, na ni vema mtambue kuwa hatua hizi tunazochukua zimeanza kuwavutia wafadhili wengi na wawekezaji.

“Na mimi nikiwa kiongozi wenu nimeamua kupambana na rushwa kikwelikweli, na ninawaomba nyote mshirikiane kuondoa rushwa katika maeneo yenu ya kazi” amefafanua Mhe. Rais Magufuli.

Kabla ya Mhe. Rais Magufuli kuzungumza, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Brigedia Jenerali John Julius Mbungo ameshukuru kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo na ameahidi kufanya kazi kwa ushirikiano na viongozi wengine wa TAKUKURU katika mapambano dhidi ya rushwa.

Nae Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Mstaafu Harold Nsekela amewataka viongozi wote wa umma kuhakikisha wanajaza fomu za tamko la mali kwa wakati na pia amewataka kutoa ushirikiano kwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma pale inapochukua hatua ya kufanya uhakiki wa taarifa zilizojazwa katika fomu hizo.

Kwa upande wake Waziri Anjellah Kairuki na Mkurugenzi wa Utawala wa TAKUKURU Bw. Alex Mfungo wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumteua Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU na wamemhakikishia kuwa wataendelea kufanya kazi kwa bidii.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

24 Agosti, 2017

Dereva Aliyegonga Treni Morogoro na Kuua Watatu Atiwa Mbaroni

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro linamshikilia dereva wa basi lenye namba za usajili T 438 ADR Charles Diamond, kwa kusababisha ajali iliyopoteza uhai wa watu mkoani Morogoro na kusababisha majeraha kwa baadhi ya watu.

Akitoa taarifa ya ajali hiyo iliyotokea leo asubuhi Kamanda wa Polisi mkoani humo Urlich Matei, amesema mpaka sasa idadi kamili ya watu waliofariki kutokana na ajali hiyo ni watu watatu, ambapo wawili ni wanawake na mmoja ni mwanaume, huku mmoja wao akiwa ni mwanafunzi.

Majeruhi wa ajali hiyo ni 27 ambao wamepelekwa hospitali ya mkoa wa Morogoro, lakini suala la utambuzi wa miili ya marehemu bado halijafanyika mpaka pale uchunguzi utakapofanyika.

Ajali hiyo imetokea leo asubuhi iliyohusisha gari aina ya daladala ikielekea Mvumi kugonga treni iliyokuwa ikipita kwenye njia yake, kulikopelekea kuburuzwa kwa gari hiyo na kusababisha vifo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images