Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Usikubali Kuaibika.......Pata Tiba ya Nguvu za Kiume Utunze Heshima Yako

$
0
0
Tatizo la kukosa hamu ya tendo la ndoa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote.

   UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
      @natural beauty pro. Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 7.5 @140,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
5.DISCREET.Ni dawa ya kuondoa mvi milele na zisiludi tena @130,000/=
    KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
       @natural2162
       @natural2162
       @natural2162
   Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0759029968 na 0659618585
    NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
      Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

                 < WELCOME ALL>

Ugonjwa wa Manji selo waahirisha kesi yake

$
0
0
Mfanyabiashara Yussuf Manji (41) anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi pamoja na wenzake watatu, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu anaumwa na amepewa mapumziko ya siku mbili.

Hayo yameelezwa jana Ijumaa, Agosti 18 na Wakili wa Serikali, Esterzia Wilson  mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mwambapa.

Wakili Wilson alidai mahakamani hapo kuwa alipata taarifa hizo za kuwa Manji anaumwa na amepewa mapumziko ya simu mbili toka kwa askari Magereza.

Hata hivyo, alidai kuwa kesi hiyo ilipangwa kwa kutajwa na upelelezi wake hadi sasa bado haujakamilika. Kesi imeahirishwa hadi Agosti 25, 2017.

Manji na  wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba chini ya sheria ya uhujumu uchumi na usalama wa Taifa kwa kukutwa na vitambaa vya kushonea sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania vyenye thamani ya zaidi ya Sh200 milioni na mihuri.

Washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Deogratius Kisinda (28), Abdallah Sangey (46) na Thobias Fwere (43).

Ufafanuzi wa Taarifa za kuwepo tozo za ukiukwaji ukomo wa mwendokasi barabaran

$
0
0
Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa zinazozua mkanganyiko kwenye mitandao ya kijamii kuhusu faini zinazotoshwa na Wakala wa Usimamizi wa Barabara Tanzania (TANROADS) kwa madereva wanaozidisha mwendo wa magari au kufanya makosa mengine ya barabarani.

Kufuatia mkanganyiko huo, Balozi wa Usalama Barabarani (RSA) ambao hujitolea kutoa elimu ya usalama barabarani kuhakikisha watumiaji wote wa barabara wanakuwa salama.

Katika ufafanuzi huo uliotolewa na RSA, kwanza walianza kujibu swali ambalo liliulizwa na wengi kama TANROADS ina mamlaka ya kupiga faini kwa kosa la mwendokasi.

TANROADS kama mamlaka ya usimamizi wa barabara chini ya Sheria ya Barabara (ROADS ACT 2007) inayo mamlaka ya kuwaadhibu wale wote wanaokiuka mwendo uliooneshwa kwenye alama za barabarani au kadiri ya maelekezo yao.

Mamlaka haya wanayapata kwa mujibu wa kifungu cha 32(2) cha Sheria ya Barabara, Na.13 ya mwaka 2007. Hata hivyo, ili mtu atozwe faini chini ya sheria hiyo ni hadi atiwe hatiani.

Inayotia mtu hatiani ni mahakama, hivyo ukikamatwa na TANROADS unatakiwa kufikishwa mahakamani na huko ukipatikana na hatia uweze kutozwa kiasi cha shilingi 200,000 au jela mwaka 1, na sio vinginevyo.

Jambo jingine lilitotolewa ufafanuzi baada ya kuzua maswali ni kama kweli faini za barabarani zinazotozwa kwa kosa la mwendokasi sasa ni sh 200,000 na inagawanyika mara tatu yaani kiasi cha shilingi 90,000 kinaenda SUMATRA, Shilingi 30,000 kinaenda Polisi na inayobaki ni ya TANROADS.

RSA wameeleza kwamba, madai hayo ni upotoshaji. Faini ya chini ya sheria ya barabara ni shilingi 200,000 kwa kuzidisha mwendo kinyume na kifungu cha 32(2) na haigawanyiki.

“Haiwezekani kutozwa faini zaidi ya moja kwa kosa hilo hilo. Kwani sheria inasema mtu hataadhibiwa mara mbili kwa kosa hilo hilo alilolitenda mara moja. Iwapo mtu ameadhibiwa mara mbili adhabu hiyo ya pili ni batili. Ndio kusema kwamba, hata mamlaka zote 3 ziwepo pamoja, ukikamatwa umezidisha mwendo utaadhibiwa mara moja tu na mamlaka ile iliyokukamata.”

Mabalozi hao walilazimika kulielezea hilo baada ya kuwepo swali kama inawezekana mtu mmoja akaadhibiwa na mamlaka zote tatu kwa pamoja endapo zitakuwa barabarani kwa wakati mmoja eneo moja zinafanya operesheni.

Kuhusu uwepo wa sheria 3 kwa jambo hilo hilo moja la kuzidisha mwendo, imeelezwa kwamba kila sheria ilitungwa kipindi tofauti na nyingine na kila sheria inasimamiwa na mamlaka yake bila mamlaka moja kuiingilia nyingine.

SUMATRA anasimamia Transport licensing Act Cap 317 na kanuni zake, ambapo faini ni kati ya shilingi 200,000 na 500,000. TANROADS inasimamia Roads Act 2007 pamoja na kanuni zake za mwaka 2009, ambapo faini ni shilingi 200,000 huku Polisi wakisimamia Sheria ya Usalama Barabarani (Road Traffic Act Cap 168) ambapo faini yake ya papo kwa papo ni shilingi 30,000 bila kujali ukubwa au udogo wa kosa.

Kila mamlaka inasimamia sheria yake na kwamba mamlaka moja mfano Polisi hawawezi kukuandika faini kwa kutumia sheria ya TANROADS. Kama watataka kufanya hivyo watalazimika kukukabidhi kwa mamlaka hiyo.

Washirikishe na wenzako waweze kupata elimu ya usalama barabarani.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Wanafunzi Wawili Wafariki wakichimba mchanga

$
0
0
Wanafunzi wawili wa Shule ya Msingi Chikomo Tarafa ya Nalasi, Wilaya ya Tunduru Mkoa wa Ruvuma wamefariki baada ya kuangukiwa na kifusi wakati wakichimba mchanga wa kujengea darasa walipokuwa kwenye mafunzo ya vitendo.

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa mkoani Rukwa SACP Gemini Mushi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba  wanafunzi waliofariki ni Selina Selemani Kazembe (12) wa darasa la tatu pamoja na Sofia Sillo (9) darasa la tatu kwa kusema kuwa watoto hao waliangukiwa kwa kufunikwa na ukuta wa shimo la mchanga ambao ulikuwa ukitumika kujengea darasa.

Kamanda Mushi amefafanua kwamba "Kwa mujibu wa taarifa tulizopewa na uongozi wa shule hiyo wanafunzi hao walikuwa katika mafunzo ya vitendo yajulikanayo kama elimu ya Kujitegemea (EK).

Pamoja na hayo Kamanda huyo amesema jitihada zilizofanyika ni kuwakimbiza watoto hao katika hospitali ya Mbesa lakini kwa bahatI mbaya wakati watoto hao wanafikishwa hospitali walikuwa wameshakata roho.

Kwa mujibu wa Kamanda Mushi amesema jukumu la mazishi familia hizo zimeachiwa.

Uamuzi pingamizi kesi ya Wema Sepetu kutolewa Agosti 31

$
0
0
Uamuzi wa kupokea au kutopokea   kielelezo cha ushahidi cha msokoto mmoja wa bangi na vipisi viwili vya bangi katika kesi inayomkabili mlimbwende wa Tanzania 2006, Wema Sepetu utatolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mwisho wa mwezi huu.

Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba amesema uamuzi huo ulipaswa autoe jana, lakini bado kuna tafiti anazifanya, hajakamilisha hivyo aliuahirisha hadi Agosti 31,2017.

Hata hivyo, baada ya kutolewa kwa uamuzi huo shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka ataendelea kutoa ushahidi wake katika kesi hiyo. Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa Septemba 12 na 13, 2017.

Uamuzi huo umefuatia baada ya shahidi huyo ambaye ni mkemia kutoka ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Elias Mulima ambaye alipima msokoto mmoja na vipisi viwili vinavyodaiwa kukutwa nyumbani kwa Wema na kugundua ni bangi, kuomba kuvitoa mahakamani hapo kama kielelezo cha ushahidi.

 Mulima kupitia wakili wa Serikali, Costantine Kakula aliomba kuitoa bahasha iliyofungwa juu yenye muhuri, saini ya shahidi huyo na namba ya maabara 291 ya 2017  ambayo ndani yake kulikuwa na msokoto na vipisi viwili vya bangi mahakamani hapo kama kielelezo cha ushahidi.

Hata hivyo wakili wa Wema, Tundu Lissu alipinga kisipokewe kama kielelezo cha ushahidi kwa sababu ndani ya bahasha hiyo kuna vitu zaidi ya msokoto mmoja na vipisi viwili vinavyodaiwa kuwa ni bangi.

Kutokana na hoja hizo, Hakimu Simba alisema Agosti 18, 2017 atatoa uamuzi juu ya hoja hizo na kesi hiyo pia inaendelea kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka.

Baba Mzazi wa Diamond amshauri Kuoa wake wawili, Zari na Hamisa Mobetto

$
0
0
Baba Mzazi wa Msanii Diamond Platinum, Abdul Naseeb amefunguka kuhusu tetesi zinazoendelea za mtoto wake kutajwa kuwa ndiye mzazi halali wa mtoto wa mlimbwende Hamisa Mobeto anayetambulika kwa jina la Abdul Naseeb ambalo ndiyo jina la baba yake na Diamond.

Akizungumza katika kipindi cha SHILAWADU cha Clouds TV Ijumaa hii, Baba Diamond ameeleza kuwa kama Diamond ameamua kumpa mtoto huyo jina lake ni upendo na inaonesha thamani kwake.

Baba Diamond amesema hawezi kumlaumu mwanaye Diamond kwa kilichotokea kwani yeye ni msanii mkubwa anakumbana na vishawishi mbalimbali, hivyo cha kufanya asiendekeze zinaa awaoe wanawake aliozaa nao (Hamisa Mobeto na Zarina Hassan) na awatendee haki kwa kutoa huduma sawa.

Kuhusu wajuukuu zake, Mzee Abdul ameeleza kuwa yeye anawapenda wote ingawa hajawahi kumuona hata mmoja.

Alhamisi hii Diamond aliandika maneno makali mtandaoni yaliyohusishwa kwenda Mobetto ambaye siku chache zilizopita alitangaza jina mwanaye kuwa Abdul Naseeb. Hatua hiyo iliwafanya mashabiki wengi ambao walitaka kumjua baba wa mtoto huyo wa Mobetto kuwa ni Diamond.

Hata hivyo mpaka sasa mkali huyo wa wimbo Eneka hajawahi kutoa neno lolote juu ya mtoto huyo licha ya mama yake pamoja na dada yake Esma kuonekana mara kadhaa wakimtembelea mrembo huyo wakati alipojifungua katika hospitali moja jijiji Dar es salaam.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Polisi Waapa Kuwasaka na Kuwanasa Waliomuua Wayne Lotter Ambaye Ndiye Aliyefanikisha Kukamatwa kwa Malkia wa Meno ya Tembo

$
0
0
Jeshi la Polisi limesema linafanya uchunguzi kuhakikisha linawatia mbaroni watu waliompiga risasi na kumuua Mkurugenzi na Mwanzilishi-Mwenza wa Shirika lisilo la kiserikali la PAMS Foundation, Wayne Lotter jijini Dar es Salaam juzi.

Lotter ndiye aliyefanikisha kukamatwa kwa mfanyabiashara kinara wa meno ya tembo, Yang Feng Glan maarufu kama ‘Malkia wa Meno ya Tembo’ hivi karibuni baada ya mhalifu huyo kusakwa kwa muda mrefu katika mataifa mbalimbali duniani.

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema linafanya upepelezi wa hali ya juu ili kuhakikisha kuwa linawatia mbaroni wahusika wa mauaji hayo huku Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe akieleza kusikitishwa na tukio hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Kamanda Kanda Maalumu, Lucas Mkondya alisema tukio hilo lilitokea Agosti 16, saa tano maeneo ya makutano ya barabara ya Haile Selassie na Kaole eneo la Masaki.

Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema Lotter (51), alipigwa risasi katika maeneo hayo ya Masaki, wakati akitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) ambapo teksi aliyopanda ilisimamishwa na gari lingine kabla ya watu wawili kutelemka na kumpiga risasi.

Lotter alikuwa Mkurugenzi na Mwanzilishi-Mwenza wa PAMS Foundation, Shirika lisilo la Kiserikali ambalo linajihusisha na masuala ya kupinga ujangili ambalo lilianza shughuli zake Tanzania mwaka 2009.

Imeelezwa kuwa Lotter amekufa huku akiwa amepanga kufanya mikakati mbalimbali ya kukabiliana na ujangili wa tembo ikiwemo kuzindua vilabu vya kupinga ujangili, kufunga vifaa vya GPS kwa tembo wote nchini, pia alikuwa msaada kwa serikali kupitia miradi mbali mbali kama vile kufanikisha kumkamata malkia wa ndovu aliyekuwa anatafutwa Dunia nzima ambaye alikamatwa nchini miezi michache iliyopita.

Pia alianzisha vikosi vya ulinzi (game rangers) ambao aliwalipa ili kusaidia ulinzi wa tembo kwenye mbuga mbalimbali nchini. 

Alifadhili pia filamu ya The Ivory Game iliyochezewa Tanzania na China, ambayo ilizinduliwa Hollywood, Marekani ikionesha ujangili unavyofanyika na pia alisaidia magari ya doria kwa Jeshi la Polisi na Wizara ya Maliasili na Utalii.

Kamanda Mkondya alisema wauaji hao wanaodhaniwa kuwa ni majambazi mbali na kumuua mkuregenzi huyo, walipora kompyuta mpakato tatu, simu moja aina ya Nokia na nyaraka mbalimbali 

Alisema marehemu alikuwa akitokea mkoani Arusha akiwa amepanda gari ya kukodi yenye namba za usajili T 499 DEV aina ya Toyota Sienta pamoja na mfanyakazi mwenzake, Christine Clarkl (40) raia wa Afrika Kusini.

Mkondya alisema raia hao walikuwa wanaelekea Bawbaw Apartment zilizoko maeneo ya barabara ya mwaya Masaki kwa ajili ya mapumziko ambapo wakiwa njiani alitokea mtu mmoja akiwa na gari na kuwaziba kwa mbele akiwa amevaa koti jeusi na baadaye alifyatua risasi mbili akidai apewe dola ambapo risasi ilimjeruhi marehemu mdomoni na baadaye alifariki dunia akiwa anapelekwa Hospitali ya Sami iliyopo Masaki kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Makamu Wa Rais Ahudhuria Mkutano Wa Troika Mbili Mjini Pretoria,nchini Afrika Kusini

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassana , jana tarehe 18 Agosti 2017 amehudhuria Mkutano wa Troika Mbili za Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC na Troika ya SADC kwa ajili ya kujadili hali ya Siasa , Ulinzi na Usalama katika Kanda.

Mkutano huu umejadili zaidi hali ya Siasa nchini Lesotho na namna ya kuisaidia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambayo inatarajiwa kufanya Uchaguzi Mkuu.

Taarifa kamili ya Mkutano huu itawasilishwa kesho Jumamosi tarehe 19 Agosti 2017, katika Mkutano wa 37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC.

Double Troika inahusisha nchi wanachama Sita ambao kwa sasa ni Swaziland, Tanzania, Afrika Kusini, Angola, Botswana na Msumbiji.

Imetolewa na

Ofisi ya Makamu wa Rais
Pretoria, Afrika Kusini
18 Agosti, 2017.

Maalim Seif Amjibu kuhusu sakata la kufukuzwa uanachama wanachama 7 na Kutomtambua

$
0
0
Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad amemjibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Mhe. Jaji Francis S.K.Mutungi kuhusu sakata la kufukuzwa uanachama wanachama saba wa CUF na kuhusu kutomtambua yeye kama Katibu wa CUF.

Maalim Seif amedai kuwa wao kama CUF hawakubaliani na maamuzi ya Jaji Mutungi kumtambua Profesa Lipumba kama Mwenyekiti wa CUF kwa kuwa wao tayari walishamfukuza uanachama hivyo si mwanachama wa CUF na wala hana sifa ya kuwa kiongozi katika chama hicho.

"Mheshimiwa Msajili unafahamu fika kuwa Profesa Ibrahim H. Lipumba mwenyewe aliamua kujiuzuilu uenyekiti wa taifa wa Chama cha CUF. Pamoja na kuniandikia mimi nikiwa Katibu Mkuu na pia Katibu wa Mamlaka iliyomchagua (Mkutano Mkuu wa Taifa) kunijulisha kuwa amejiuzulu, pia alikwenda kwenye mkutano na waandishi wa habari akatangaza hadharani kuwa amejiuzulu

"Hatimaye Mkutano Mkuu wa Taifa wa CUF ukaitishwa na Katibu Mkuu akatoa taarifa ya kupokea barua ya kujiuzulu kwa Profesa Ibrahim Lipumba nafasi yake ya Uenyekiti wa Taifa wa Chama. Nikaisoma barua yake mbele ya Mkutano Mkuu wa Taifa, na baada ya mjadala wa kina maamuzi yakachukuliwa kwa mujibu wa matakwa ya Katiba ya CUF ya 1992 (Toleo la 2014) kwa kupiga kura. Wajumbe 437 wakakubali kujizulu kwa Profesa Lipumba dhidi ya Wajumbe 14 waliokataa. Hivyo Profesa Ibrahim H. Lipumba kuanzia siku aliyojiuzulu si Mwenyekiti wa Taifa wa CUF. Profesa Lipumba hana mamlaka ya kukiongoza Chama chetu" alisisitiza

Aidha Maalim Seif anasema kutokana na maamuzi hayo ya CUF baadaye Profesa Lipumba alikuwa akilalamika kwa Msajili wa Vyama Vya Siasa kufuatia maamuzi hayo na baadaye Msajili alitoa msimamo wake kuwa anamtambua Lipumba kama Mwenyekiti wa Taifa wa CUF ingawa Katibu Mkuu wa CUF anasema msajili hana uwezo huo wa kumrudisha Lipumba kama Mwenyekiti wa CUF

"Najua kuwa alikulalamikia, ukaniletea barua zake za malalamiko na ukataka maoni ya Chama. Nikakujibu kwa maandishi. Kwenda na kurudi ukatoa kile ulichokiita Msimamo wa Msajili juu ya kadhia iliyokikumba Chama! Huo ni Msimamo sio hukumu. Maana kama ni hukumu ningetarajia katika huo ulioita msimamo ungeeleza kuwa kwa uwezo uliopewa na kifungu Na. kadhaa cha Sheria ya Vyama vya Siasa Na.5 ya 1992, au kwa mujibu wa uwezo uliopewa na Katiba ya CUF ya 1992 (Toleo la 2014) katika kifungu Na. kadhaa umeamua kumrudisha Profesa Ibrahim Lipumba kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CUF. Lakini hukuweza kuonyesha uwezo wako wa kisheria au kikatiba kumrudisha Profesa Lipumba kuwa Mwenyekiti wa Taifa CUF kwa sababu huna uwezo huo kwa mujibu wa sheria za nchi wala kwa mujibu wa Katiba ya CUF" alisema Maalim Seif

Katibu Mkuu wa CUF amesema wao wanazidi kumshangaa msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Mutungi kuendelea kushirikiana na Profesa Lipumba hata katika mambo ambayo yanatia aibu kama kutaka kutoa ruzuku za chama na kumpa Lipumba na genge lake.

"Tunaloshuhudia ni kila kukicha unaendelea kumuunga mkono Profesa Lipumba hata katika mambo ya aibu ya kula njama na Profesa Lipumba kumuwezesha atoe ruzuku ya CUF kinyume na matakwa na taratibu zilizowekwa katika Katiba ya CUF ya 1992 (Toleo la 2014). Narudia kusema kuwa Prof. Lipumba si Mwenyekiti wa Taifa wa CUF. Lakini kutokana na vitendo vyake vya kukosa nidhamu katika kusababisha vurugu katika kikao cha dharura cha Mkutano Mkuu wa Taifa wa chama chetu, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa, kwa uwezo lillonao kwa mujibu wa masharti ya Katiba ya CUF, lilimfukuza Profesa Ibrahim Lipumba uanachama wa CUF. Taarifa hiyo pia nilikuletea, lakini umeamua kuitia kapuni ili kutimiza matakwa yako binafsi. Ikiwa Profesa Ibrahim H. Lipumba sio mwanachama wa CUF, hawezi kabisa kuwa kiongozi wa Chama, hasa nafasi ya juu kabisa katika Chama. Kinachotokea kikiongozwa nawe na Ofisi yako ni ubabe, kutojali sheria za nchi wala Katiba ya Chama chetu ilimradi mufikie lengo lenu" alisema Maalim

Mbali na hilo Maalim Seif aliweka msimamo wake kuwa Chama Cha Wananchi CUF hakiendeshwi na hisia za mtu wala hakiwezi kupangiwa kiongozi na kudai ni CUF ni taasisi inayoongozwa na sheria za nchi na Katiba na si vinginevyo.

"Mheshimiwa Msajili napenda utambue kuwa CUF ni taasisi, tena Taasisi makini. Kinaendeshwa na kuongozwa kwa mujibu wa sheria za nchi na Katiba ya Chama hicho pamoja na Kanuni ambazo hutungwa na mamlaka husika kila inapohitajika. Sisi viongozi wa CUF tunajitahidi kuongozwa na sheria za nchi, Katiba ya Chama na Kanuni zake katika kukiendesha chama. Hatuongozwi na matakwa ya mtu yeyote, hata kama mtu huyo ni Msajili wa Vyama vya Siasa. Ninavyofahamu Msajili hana mamlaka ya kupandikiza watu anaowataka kuwa viongozi wa chama chetu. Msajili hana uwezo wa kuingilia maamuzi halali ya vikao halali vya Chama chetu. Viongozi huchaguliwa /kuteuliwa na wanachama wenyewe/viongozi halali wa chama" alisisitiza Maalim Seif

Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR; Anauwezo wa kutabiri nyota yako na kukuletea mafanikio makubwa katia biashara yako, kazini na malengo yako ya maisha.Pia anatoa pete ya bahati yenye uwezo wa kukuletea mafanikio makubwa na kutimiza ndoto zako.

Je, Umedhurumiwa? unamdai na hakulipi?...Njoo upatiwe dawa ulipwe haraka. Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

Tundu Lissu adai kufuatwa na usalama wa Taifa kila anapokwenda

$
0
0
Rais wa chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Tundu Lissu amefunguka kwa kuwataka wakuu wa vyombo vya usalama nchini wawaelekeze watumishi wao kazi za kufanya na siyo kupoteza muda na rasilimali za nchi.

Lissu amesema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliyoitishwa na CHADEMA wenye lengo la kuzungumzia namna nchi inavyoenda kufilisika na ndipo alipomtaka Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Kamanda Modestus Francis Kipilimba na Mkuu wa Majeshi Tanzania, IGP Simon Sirro kuwapa uweledi mzuri wa kufanya kazi vijana wao.

"Mkuu wa TISS au IGP wale vijana mliowatuma wiki tatu mfululizo kunifuata kila nilipo, niliowakaba Kanisani St. Peter, muwaambie wakubwa wawaelekeze watumishi wao kutumia muda na rasilimali za nchi kupambana na wahalifu na si kuhangaika na raia wanaotimiza wajibu wao kikatiba kuwawajibisha viongozi serikalini,”  alisema Lissu.

Pamoja na hayo, Lissu ameendelea kwa kusema "Wafanye kazi ya kupambana na wahalifu na siyo kupoteza muda wao na pesa za walipa kodi kuhangaika na raia ambao wanatimiza uhuru wao wa kuiwajibisha serikali iliyoko madarakani".

Kwa upande mwingine, Lissu amemtaka Kamanda Sirro pamoja na Kamanda Kipilimba kupamba na wahalifu na wamuachie yeye kazi ya kuwajibisha waliyoko madarakani kwa mujibu wa sheria za nchi.

Ukomo wa matumizi ya mashine za EFD zilizoanza kutumika kati ya mwaka 2010-2013

Lipumba akwama kufuta kesi inayomzuia kupewa ruzuku ya CUF

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imekataa maombi ya Mwenyekitti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba na wenzake, ya kufuta kesi namba 28/2017 inayomzuia kupata ruzuku ya chama hicho.

Kupitia taarifa yake kwa umma aliyotoa  Agosti 17, 2017, Naibu Mkurugenzi wa Habari, Mawasiliano na Umma CUF, Mbarala Maharagande amesema Jaji wa Mahakama Kuu, Wilfred Ndyansobera anayesimamia kesi hiyo, amekataa maombi hayo ya Lipumba ambaye ni mshitakiwa kwenye kesi hiyo.

Kwa mujibu wa Maharagande, kufuatia maamuzi hayo ya mahakama, Prof. Lipumba na wenzake watakosa kiasi cha shilingi bilioni 1.4 ambazo zilikuwa ruzuku ya chama hicho mpaka mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu.

Kesi hiyo ilifunguliwa na Bodi ya Wadhamini ya CUF inayomuunga mkono Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Shariff Hamad baada ya Lipumba kupewa ruzuku ya chama hicho na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Ambapo Bodi hiyo inadai kuwa uamuzi huo ulikuwa kinyume cha sheria kwa madai kuwa Lipumba si kiongozi halali wa chama hicho.

Jipatie ofa ya kitabu cha PRESIDENT WIFE....Ni Riwya Kali ya Kusisimua

$
0
0
WEEKEND YAKO KWA NINI IWE MBAYA. OFA HIZI ZA VITABU VINAKUHUSU WEWE MSOMAJI WANGU WA NGUVU.

Jipatie ofa ya kitabu cha PRESIDENT WIFE(Shadow of D.F.E) kwa sh 5000 kupitia mitandao ya Whatsapp 06570725588 na Email eddazariaM@gmail.com 
 
Pia unaweza kusoma kitabu cha SORRY MADAM season one pamoja na SHE IS MY WIFE kila kimoja utakipata pia kwa sh 5000/=.
 
HIZI NI BAADHI YA STORY NILIZO ZIANDIKA NA ZINAPATIKANA
1. AIISSII U KILL ME(Hi inauzwa kila episode moja sh 250)
2. AM NOT A DOCTOR sh 10000/=
3. MY LIFE sh 10000/=
4.HARD DAY sh 4000/=
5. SEX DEALERS sh 3000/=
6. MY MOM'S FRIEND sh 7000/=
7. SORRY MADAM- 5000/=
8. SHE IS MY WIFE- 5000/=
9. Story MPYA ambazo POWER na AIISSII U KILL ME LEGACY nazo zipo sokni. Unachelewa nini, huu ni wakati wako mpenzi msomjai wa hadithi zangu za kusisimua,
 
NA NYINGINE NYNGI. KARIBUNI SANA NA NINAOMBA MUZIDI KUENDELEA KUNIUNGA MKONO KATIKA KIPAJI CHANGU HICHI CHA UANDISHI. 
WASILIANA NAMI 0657072588 AU 0768516188 
 
KARIBUNI SANA TENA SANA

Wapigadebe 150 kufikishwa mahakamani

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limetangaza kukamata watu wapatao 150 kuanzia Agosti 14 hadi 17 mwaka huu, kwa makosa ya kuwabughuzi abiria katika maeneo mbalimbali ya jiji katika vituo vya mabasi.

Wakati akizungumza na wanahabari jana  jijini Dar es Salaam, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamanda Lucas Mkondya, alisema watuhumiwa hao walikamatwa kufuatia misako na operesheni kali iliyofanywa na polisi, na kwamba watafikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayowakabili.

“Stendi ya mabasi ya Ubungo walikamatwa 39, Posta 12, Ferry 7, Tegeta 12, Tandika 16, Mnazimmoja 6, Stesheni 5, Manzese 12, Bunju 8 na Stereo 7,” amesema.

Katika hatua nyingine, Kamanda Mkondya alisema Jeshi la Polisi katika nyakati tofauti ilikamata watuhumiwa 167 kwa makossa mbalimbali ya kihalifu ikiwemo kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya, unyang’anyi wa kutumia sialaha na utapeli, kucheza kamali na kuuza pombe haramu ya gongo.

“Katika operesheni hii kali ambayo ni endelevu, jumla ya kete 96 za dawa ya kulevya, misokoto ya bangi 107, gongo lita 60 zilikamatwa. Tunaomba raia wema kuendelea kutoa taarifa za wahalifu ili tuwakamate na hatua kali za kisheria zifuatwe dhidi yao,” alisema.

 Alisema watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa kulingana na makossa yao na kwamba upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria zaidi.

Tundu Lissu afichua kilichochelewesha Bombadier kufika

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu amedai kuwa ndege aina ya Bombardier Q 400-Dash 8 iliyonunuliwa na Serikali, imezuiwa nchini Canada kutokana na Serikali kudaiwa fidia.

Ndege hiyo ilitakiwa iwasili nchini mwezi uliopita, lakini hadi sasa hakuna taarifa kuhusu ujio wake.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Lissu aliyekuwa ameongozana na Freeman Mbowe, ambaye ni mwenyekiti wa Chadema na Frederick Sumaye (mwenyekiti wa Kanda ya Pwani), alisema ndege hiyo inashikiliwa na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd inayoidai Serikali dola 38.7milioni sawa na Sh87bilioni.

Alisema kutokuja kwa ndege hiyo kama ilivyopangwa licha ya kukamilika, kunatokana na maamuzi yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Nne, wakati huo Rais John Magufuli akiwa Waziri wa Ujenzi, wa kuvunja mkataba wa kampuni hiyo ya Canada iliyokuwa ikijenga barabara ya Tegeta Wazo-Bagamoyo.

Lissu, ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki, alisema baada ya uamuzi huo, Stirling ilifungua kesi Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi, ikidai kukiukwa kwa mkataba na ilipofika Juni 2010, mahakama hiyo ilitoa tuzo ya ushindi kwa kampuni hiyo, ikiitaka Serikali ilipe fidia ya dola 25 milioni za Kimarekani, huku deni hilo likiwekewa riba ya asilimia nane.

Kwa madai ya Lissu, Serikali ilikataa kulipa fidia hiyo hadi Juni 30 mwaka huu wakati mahakama hiyo ilipoipa Stirling kibali cha kukamata mali zote za Tanzania zitakazokuwa katika nchi za Ufaransa, Uholanzi, Uingereza, Ubelgiji, Uganda na Canada.

Lissu ameibua tuhuma hizo miezi mitatu baada ya Serikali kutangaza kuwa ndege hiyo mpya ingewasili Julai.

Akizindua safari za Kampuni ya Usafiri wa Anga la Tanzania (ATCL), Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani alisema ndege hiyo aina ya Bombadier Dash 8-Q 400 imenunuliwa kuimarisha huduma za shirika hilo la Serikali.

Alisema hatua hiyo itaiweza ATCL kufikisha ndege nne na hivyo kupanua mtandao wa huduma zake na kufikia masoko ya nchi jirani kama Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Malawi, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Lakini kutowasili kwa ndege hiuyo kumeibua maswali na katikati ya wiki, mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe aliandika katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii akihoji mustakabali wa chombo hicho cha usafiri wa anga.

Chini ya swali hiyo, mchangiaji anayeonekana kwa jina la Mbarawa amejibu kuwa kulikuwa na matatizo kidogo yaliyochelewesha na kuahidi kuwa ndege hiyo itawasili mapema.

Akizungumzia suala hilo, Lissu alidai kuwa hata Waziri wa Mambo ya Nje, Profesa Augustine Mahiga alienda Canada kushughulikia suala hilo.

“Waziri Mahiga akatae kama hakuwa Canada Agosti 3 mwaka huu kimyakimya katika mkutano wa maridhiano na kampuni hiyo ili waachie ndege iletwe Tanzania. Wameikamata hadi wapewe dola 12.5milioni,” alisema Lissu.

Alipoulizwa kuhusu madai ya kushikiliwa kwa ndege hiyo, Ngonyani alisema anachofahamu makubaliano ya manunuzi na kampuni inayotengeneza hiyo yamekwamishwa na ratiba za kampuni hiyo yenye zabuni nyingi za kuzalisha ndege.

“Mimi sina taarifa ya kushikiliwa kwa ndege hiyo, ila ninachojua ndege itakuja. Katika makubaliano ilitakiwa ifike Julai, lakini ratiba zao kwa miezi miwili ijayo hadi Oktoba, ndege itakuwa tayari na itakuwa imeshakamilika,” alisema.

“Unajua Bombardier sasa hivi kwenye soko la ndege ndiyo ‘talk of the day (gumzo). Nchi nyingi zinahitaji, kwa hiyo oda ni nyingi na foleni inakuwa kubwa.

“Lissu ni mwanasiasa anayeweza kuzungumza lolote, ila ukweli utajulikana baadaye. Wasipoleta watakuwa wame-breach contract (wamekiuka mkataba) na sidhani kama watafanya hivyo maana wana kazi zetu nyingi.”

Alipoulizwa kuhusu maagizo ya mkataba wake, alisema kwa sasa yuko nje ya ofisi na asingeweza kueleza kwa undani makubaliano ya mkataba huo katika masharti na muda wa matengenezo itakuwaje.

“Hapa sina details zake, nikirudi kutoka safari nitafute,” alisema.

Kuhusu madai ya kampuni hiyo ya Stirling, Ngonyani alisema serikali kudaiwa si jambo la kushangaza. Alisema tangu Serikali ilipoingia madarakani mwaka 2015, wizara hiyo ya ujenzi ilikuwa inadaiwa Sh1.12 trilioni, lakini hadi Julai, tayari limepungua hadi Sh900 bilioni.

“Mimi sina taarifa kuhusu deni hilo ila kikubwa Serikali kudaiwa si big deal (jambo la kushangaza), ila tunafanyaje katika kuyalipa madeni, pengine inawezekana deni hilo likawa ni sehemu ya madeni tunayodaiwa,” alisema.

 

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Serikali Yamjibu Tundu Lissu Sakata la Ndege Kushikilia Canada kisa Madeni

$
0
0
Serikali kupitia kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu Idara ya Habari, Zamaradi Kawawa imejibu hoja zilizotolewa na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Tundu Lissu kuhusu kushikiliwa kwa ndege ya Tanzania aina ya Bombadier Q-400 Dash 8 nchini Canada.

Zamaradi Kawawa amekiri kuwa ni kweli ununuzi wa ndege hizo umeingiliwa na mgogoro na kukiri kuwa ndege hiyo Q-400 Dash 8 inashikiliwa nchini Canada kwa madai ya kuwa ndege hiyo imeshikiliwa kwa mgogoro wa kutengeneza na wanasiasa wa Tanzania wasioitakia mema nchi ya Tanzania.

"Ununuzi wa ndege ya 3 ya Bombadier umeingiliwa na mgogoro uliotengenezwa na wanasiasa na watu wasioitakia mema Tanzania, Wanasiasa waliotengeneza mgogoro huo wanahujumu maendeleo ya nchi na usalama wa raia" alisema Zamaradi Kawawa

Aidha Zamaradi Kawawa amesema kuwa ndege ya tatu ambayo ilikuwa inatarajiwa kuingia nchini mwezi Julai amedai kuwa itaingia muda si mrefu na kuwataka Watanzania waiamini serikali ya Tanzania iliyopo chini ya Rais John Pombe Magufuli

"Ndege ya 3 ya Bombadier ipo na inakuja kwahiyo wananchi waiamini Serikali yao ila serikali imesikitishwa na ushiriki wa wanasiasa na baadhi ya watu kuhujumu maendeleo ya nchi, Watanzania tuwe wazalendo kulinda, kutetea na kukabiliana na hujuma zozote zinazorudisha nyuma maendeleo ya Nchi, tuunge mkono jitihada za Rais Magufuli  katika kuleta maendeleo bila kujali itikadi ya chama, kabila au dini" alisisitiza Zamaradi Kawawa

Mbali na hilo Kawawa amesema kuwa serikali imeanza kuchukua hatua kadhaa kuhusiana na mgogoro wa ununuzi wa ndege hizo

"Kuhusiana na mgogoro wa ununuzi wa ndege hatua za Kidiplomasia na sheria zimeanza kuchukuliwa ili kumaliza jambo hili" alisema Zamaradi Kawawa

Hapo Jana Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia Na maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu katika taarifa yake kwa vyombo vya habari alisema ndege hiyo imeshindwa kuwasili nchini kufuatia kesi ya madai iliyofunguliwa dhidi ya Serikali ya Tanzania nakupelekea kukamatwa kwa Ndege hiyo mali ya Tanazania. 
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images